Title March 2022

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele.

Utajiuliza, ni kwanini wengi wa mitume wa Bwana Yesu walikuwa ni wavuvi? Tukiachilia mbali wale wanne (yaani Petro, Yakobo, Yohana, na Andrea, ambao kazi yao rasmi ilikuwa ni uvuvi), Kulikuwa na wengine watatu, ambao walikuwa wanaifanya pia hii kazi, kama sio kuwa na uzoefu nayo (Soma Yohana 21:1-3). Hivyo tunaweza kusema, si chini ya mitume saba (7), walikuwa ni wavuvi.

Utajiuliza Ni kwanini Bwana alipendelea sana wavuvi, na sio watoza ushuru wengi, ni kwasababu kazi yake ya kuokoa watu ilifanana na hiyo, na ndio maana akamwambia Petro tangu sasa nitakufanya kuwa mvuvi wa watu, hakumwambia nitakufanya kuwa muhubiri wa watu, hapana bali mvuvi wa watu. Kuonyesha kuwa maarifa ya uvuvi, yana mchango mkubwa sana, katika kuokoa roho za watu.

Sasa tabia mojawapo ya mvuvi, ni kuwa hachagui cha kuvua pindi anapotupa nyavu yake baharini, huwa kichani pake anajua kabisa, vitakavyokuja juu, sio  Samaki tu peke yake, bali pia na viumbe vingine vingi vya majini, Pamoja na takataka nyingi.

Ndio maana Bwana Yesu alitoa mfano huu, akasema;

Mathayo 13:47 “Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;

48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa”.

Umeona? Samaki waliovuliwa, inaweza ikawa ni asilimia 20 tu, lakini 80 yote iliyobakia, ni konokono, kobe, nyoka, magugu, minyoo n.k.

Hivyo akishafika ufukweni, kazi yake inakuwa ni kukusanya Samaki, lakini hao wengine anawatupa, kesho tena anaendelea na uvuvi wake huo huo, anatoa tena vitu kama hivyo. Lakini hilo halimfanyi akate tamaa. Kwasababu Neti/Nyavu yake ndio ilivyotengenezwa, kuvua kila kitu.

Anajua ndio hali halisi ilivyo.

Kuonyesha kuwa na sisi kama wavuvi wa rohoni, tunaowahubiria watu Habari njema ili waokoke, si kazi yetu, kuchunguza chunguza kama huyu ni wa Mungu kweli au sio, ukifanya hivyo, utakata tamaa mapema. Watu mia, utakaowahubiria Kristo, pengine ni kumi tu, wakawa na matokeo unayoyatazamia.

Kinyume chake wengine ndio wanakuwa mwiba kwako, badala ya faraja. Bwana Yesu alipochagua mitume wake, mmoja wao alikuwa mwizi na msaliti, Lakini hiyo haikumaanisha kuwa hakuwa makini katika uchaguzi wake, au alifanya hitilafu. Hapana, neti yake ilikuwa bora kabisa.

Vivyo hivyo na wewe ndugu, ikiwa upo katika kazi ya uvuvi wa watu wa Mungu, basi leweke akilini, hilo, utumishi wa kweli wa Mungu hauchagui, cha kuvua. Si kila utakayemshuhudia, atapokea ujumbe wako, hivyo usikate tamaa ukadhani kuwa kuna dosari katika utumishi wako, hapana, bali, ndivyo uvuvi ulivyo. Endelea kuwashuhudia wengine, ukijua kabisa kati ya mia hutakosa wachache watakaoponyeka. Na hao ndio Samaki.

Bwana alitaka hilo likae katika vichwa vya mitume wake,kabla ya kazi kuanza, ili wasikatishwe tamaa katika shamba la Bwana, pindi wakutanapo na wasivyovitarajia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Juya ni nini kwenye biblia? (Mathayo 13:47)

TENGENEZA  NYAVU ZAKO, OSHA NYAVU ZAKO.

CHAMBO ILIYO BORA.

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

Nini maana ya kuokoka katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

TATIZO LA VISIGINO KUUMA KIBIBLIA

Tatizo la visigino kuuma ni ishara ya nini kibiblia?..Au visigino kuwaka moto?.

1) Visigino kuuma.

Kama unafanya shughuli yenye kuhusisha miguu, kwamfano kulima au kutembea umbali mrefu, au michezo..basi ni jambo la kawaida visigino kuuma, au visigino kuwaka moto.

Suluhisho la tatizo hilo ni kupunguza shughuli hizo zinazohusisha miguu, na miguu itarudia hali yake.

Lakini kama huna shughuli zozote unazozifanya na umeenda hospitali na hujapata suluhisho, na hujui sababu, na pengine umeshafanyiwa hata na maombezi, na tatizo bado lipo palepale..

Basi suluhisho la tatizo hilo,linaweza kuwa la kimaandiko,na maandiko yafuatayo yatakufungua…

Yeremia 13:22 “Nawe ukisema moyoni mwako, Mbona mambo haya yamenipata mimi? Ni kwa sababu ya WINGI WA UOVU WAKO, marinda yako yamefunuliwa, na visigino vya miguu yako vimeumia”.

Jiangalie maisha yako ni wapi hapako sawa na Mungu..tubu makosa yako kwa Mungu kwa kumaanisha kuyaacha.

Angalia mahali unapofanyia kazi, au mahali unapoishi, jinsi unavyoenenda, tafakari mawazo ya mioyo yako, je yanampendeza Mungu?..

Je unao upendo?, Wewe ni mvumilivu, ni mtu wa kusamehe au wa vinyongo?, Je ni mtu unayemcha Mungu na kumwogopa?.

Kama sio basi hiyo ndio sababu kwanini visigino vyako vinauma, au vinawaka moto, na umekosa ufumbuzi kila mahali.

Litafakari sana hilo na Mungu akusaidie, yeye ni mwaminifu tukiungama dhambi zetu kwa lengo la kuziacha kabisa, anatusamehe na kuponya magonjwa yetu na majeraha yetu, kwasababu lengo lake sio sisi tuteseke, bali tuwe na furaha na tupate mema, ndio maana saa nyingine anaruhusu vitu fulani vitutokee ili tutubu, na mwishoni atubariki zaidi.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

WITO WA MUNGU

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

Rudi nyumbani

Print this post

FANYA KAMA UONAVYO VEMA.

Moja ya mambo ambayo yanadhoofisha karama, au yanamchelewesha mtu kuifanya kazi ya Mungu, ni tabia ya kusubiria Mungu amwambie jambo Fulani, au Mungu amwoneshe jambo kwanza.

Watu wengi sana leo hii wamekuwa watu wa kungojea ngojea!.. Utamwuliza mtu kwanini huanzi kuifanya  kazi ya Mungu?.. Jibu atakalokupa ni “nangojea wakati wa Bwana” au “Nangoja Bwana aniambie kwanza au anioneshe kwanza”. Na ilihali kashamwamini Yesu na kupokea Roho Mtakatifu.

Leo nataka nikuambie ndugu yangu.. Usiendelee kungoja!!.. Nenda kaanze kumtumikia Bwana, maadamu umeshamwamini Bwana Yesu, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, usisubiri maono, wala sauti ikuambie nenda kanitumikie!.. “Hiyo utaingoja sana”.. Anza sasa.

Utauliza nitaanzaje anzaje sasa?

Usiogope, Roho Mtakatifu aliye ndani yako atakufundisha na kukuongoza!.. hutaanza katika ukamilifu wote lakini utaishia katika ukamilifu, kwasababu Roho Mtakatifu yu Pamoja nawe, kukufundisha cha kusema au cha kufanya, anachosubiri kutoka kwako ni wewe tu kuchukua hatua ya kuanza.

Luka 12:11 “Na watakapowapeleka ninyi mbele ya masinagogi na maliwali na wenye mamlaka, msifadhaike kwa kuwaza maneno yenu jinsi mtakavyojibu au kusema;

12 kwa kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha saa ile ile yawapasayo kuyasema”.

Hakikisha unamtumikia Mungu tu! Katika Neno lake, hayo mengine mwachie yeye!.

Sasa utazidi kuuliza ni kwa namna gani??..kama sipaswi kungoja kusikia sauti, nitasemaje au nitafanyaje?..

Jibu ni rahisi, kama tayari umeshampokea Roho Mtakatifu, Songa mbele, FANYA KAMA UONAVYO VYEMA!

1. Kama unaona ni vema wewe kumwimbia Mungu, Basi fanya hivyo kwa bidii.. usisubiri uambiwe au uone maono, au Malaika akutokee.

 2. Kama unaona ni vema wewe kuhubiri, basi anza kufanya hivyo hata kama unajiona huna ujasiri, Bwana atakupa ujasiri pale tu utakapotia nia ya kuanza kuwahubiria watu.

 3. Kama unaona ni vema wewe kuishikilia kazi ya Mungu kwa maombi au michango!, usingoje uwekewe mikono, au Roho Mtakatifu akuambie, wewe fanya na Bwana atakuwa na wewe, na kukupa kibali.

 4. Kama unaona ni vema wewe kuwafundisha Watoto, basi usingoje ngoje, anza kufanya kazi hiyo,. Kwasababu ni Roho Mtakatifu kaliweka hilo ndani yako.

 5. Kama unaona ni vema wewe kuhubiri mitaani, au mitandaoni, usisubiri utokewe na Bwana, wala usiseme ngoje, wakati Fulani ufike ndio uanze!, anza sasa!

 6. Kama unaona vema kuandaa Makala mbali mbali au kuchapisha vitabu vya mahubiria au mafundisho, basi fanya hivyo usingoje ngoje, usizidi kupoteza muda, kwasababu Muda haukungoji wewe. Na mambo mengine yote!, usingoje.. FANYA KAMA UONAVYO VEMA.

Ili tujifunze Zaidi, hebu tuutazame wito wa Mfalme Sauli, jinsi Mungu alivyompaka mafuta, na jinsi alivyoagizwa namna ya kuuongoza ufalme aliopewa!.

Sauli baada ya kupakwa mafuta na nabii Samweli ya kuwa mfalme wa kwanza wa Israeli, alikuwa anajiuliza uliza atawezaje kutawala, atafanyaje fanyaje!. Lakini Nabii Samweli alimpa maneno makubwa sana yaliyompatia Mwanga!.. na maneno hayo ni kwamba.. “BAADA TU YA KUPOKEA ROHO, BASI AFANYE KAMA AONAVYO VEMA”.

Tusome,

1Samweli 10:1 “Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta, akayamimina kichwani pake, akambusu, akasema, Je! Bwana hakukutia mafuta [uwe mkuu juu ya watu wake Israeli? Nawe utamiliki watu wa Bwana, na kuwaokoa na mikono ya adui zao; kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa Bwana amekutia mafuta] uwe mkuu juu ya urithi wake.

2 Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na wanaume wawili karibu na kaburi la Raheli, katika mpaka wa Benyamini huko Selsa; nao watakuambia, Punda hao uliokwenda kuwatafuta wameonekana; na tazama, baba yako ameacha kufikiri habari za punda, anafikiri habari zenu, akisema, Nifanye nini kwa ajili ya mwanangu?

3 Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na kufika kwa mwaloni wa Tabori, na hapo watu watatu watakutana nawe, wanaokwea kumwendea Mungu huko Betheli, mmoja anachukua wana-mbuzi watatu, na mwingine anachukua mikate mitatu, na mwingine anachukua kiriba cha divai;

4 nao watakusalimu na kukupa mikate miwili; nawe utaipokea mikononi mwao.

5 Baada ya hayo utafika Gibea ya Mungu, hapo palipo na ngome ya Wafilisti; kisha itakuwa, utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakishuka kutoka mahali pa juu, wenye kinanda, na tari, na kinubi, na filimbi mbele yao, nao watakuwa wakitabiri;

6 na roho ya Bwana itakujilia kwa nguvu, nawe utatabiri pamoja nao, nawe utageuzwa kuwa mtu mwingine.

7 Basi, hapo ishara hizi zitakapokutukia, FANYA KAMA UONAVYO VEMA; KWA KUWA MUNGU YU PAMOJA NAWE”.

Umeona hapo mstari wa 7??.. Samweli hakuendelea kumpa maagizo kwamba, baada ya ishara hizo, aende akatwae jeshi, au aende akatawale watu kwa namna hii au ile, bali alimwambia tu maneno haya machache… “hapo ishara hizi zitakapokutukia, FANYA KAMA UONAVYO VEMA; KWA KUWA MUNGU YU PAMOJA NAWE”.

Maana yake jinsi ya kutawala, afanye jinsi aonavyo, kwasababu Mungu yu Pamoja naye..hataruhusu ajikwae wala akose, atamlinda na mashauri ya adui, hivyo yeye kile kijacho kichwani mwake maadamu ni cha kujenga, basi akifanye asiogope!, asianze kusubiri maono na ishara!.

Hali kadhalika na wewe leo!… Umeshamwamini Bwana Yesu, umeshabatizwa na tena umepokea Roho Mtakatifu.. unachosubiria ni nini???..Ishara ya mwisho ya Roho Mtakatifu imeshatimia juu yako unachosubiri ni nini??...HARAKA SANA FANYA UONAVYO VEMA, KWASABABU ROHO MTAKATIFU HAKUDHARAU.

Lakini kama bado hujampokea Yesu usifanye lolote kwanza!!..kwasababu utaharibu badala ya kujenga!.. Mpokee Yesu kwanza, na ubatizwe kwa ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la BWANA YESU KRISTO (Matendo 2:38). Baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukuongoza katika kweli yote!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

JIBU: Hakuna mahali popote katika biblia inamtaja Mikaeli kuwa ndiye Bwana Yesu. Kinyume chake, maandiko yanamtofautisha Yesu na Malaika hata kwa asili aliyoitwaa,  Biblia inasema.

Waebrania 2:16 “Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu”.

Ikiwa na maana, kudhihirishwa kwa Bwana Yesu kwa mara ya kwanza, kulikuwa ni katika asili ya mwanadamu na sio Malaika. Na ndio maana utaona, Malaika nao, walimwona na kumtambua kwa mara ya kwanza, siku ile alipozaliwa katika mwili.

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Ni kweli Mikaeli ni mmoja wa Malaika wakuu mbinguni,na pengine Zaidi ya wote, Lakini hana sifa yoyote ya kudhaniwa kuwa yeye ndiye Kristo, kwani  biblia inatuambia kuwa Kristo anaabudiwa sio tu na wanadamu, bali pia na malaika wote mbinguni(Waebrania 1:6), Lakini  hakuna Malaika yoyote anayeabudiwa.

Pia Kristo alikuwa na mamlaka ya kusamehe dhambi, Pamoja na kukemea pepo kwa uweza wake,lakini Malaika (akiwemo Mikaeli), hawana uwezo huo, wanajiona hawastahili mpaka wanasema Bwana mwenyewe na awakemee mashetani (Yuda 1:9)..

Na mwisho biblia inasema, hakuna mahali popote, Mungu alimwita Malaika yoyote “Mwanangu”, bali hao ni watumishi wake, watumikao kuwahudumia watakatifu, lakini kwa Bwana Yesu, Mungu alimwita mwana, kumtofautisha yeye na Malaika zake.

Waebrania 1:5 “Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?

Hivyo, Mikaaeli ni Malaika wa Bwana na atabakia kuwa hivyo. Lakini ikiwa utatamani kujua Zaidi aina za Malaika wa Mungu, na kazi zao na idadi zao, Fungua hapa >> Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

Swali Je! Unatambua kuwa Mungu ameshawaweka tayari Malaika zake kwa ajili ya mapigo ya siku hizi za mwisho? Una Habari kuwa unyakuo upo karibuni sana kutokea, kuliko unavyoweza kudhani?

Kumbuka paraparanda ya Mungu ikilia leo, basi, Malaika hao wa mapigo, Mungu atawaachilia ulimwenguni mwote, wataipiga dunia kwa kwa zile baragumu saba, na vitasa saba. Wakati huo kutakuwa ni nyakati za shida sana ulimwenguni. Soma Ufunuo 8 &16, ujionee mpendwa. Ni Malaika mahususi wa kuleta mabaya duniani.

Zaburi 78:49 “Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya”.

Usitamani uwepo wakati huo ndugu yangu, Ni heri leo ukatubu na kumrudia muumba wako. Upokee uhakika wa kuurithi uzima wa milele. Ikiwa utataka kusoma juu ya mapigo hayo, fungua link hii>>

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

UNYAKUO.

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

Jina la Bwana, Yesu libarikiwe.

Kuna tofauti ya Marhamu na Manukato, kujua tofauti yake fungua hapa >> Marhamu na manukato ni nini?.

Lakini kwaufupi ni kwamba Marhamu ni pafyumu.

Sasa maandalio ya wayahudi kabla ya kuzika, ilikuwa ni desturi ya kumpaka maiti Marhamu kichwani, kisha Manukato yanafungiwa katika sehemu nyingine ya mwili. Na manukato hayakuwa katika mfumo wa kimiminika.

Lakini tunaona Bwana Yesu alipokufa, Yusufu yule mtu Tajiri Pamoja na Nikodemo waliandaa tu Manukato!, bila Marhamu na kwenda kuyafungia ndani ya mwili wa Bwana Yesu.

Yohana 19:38 “Hata baada ya hayo Yusufu wa Arimathaya, naye ni mwanafunzi wa Yesu, (lakini kwa siri, kwa hofu ya Wayahudi), alimwomba Pilato ruhusa ili auondoe mwili wake Yesu. Na Pilato akampa ruhusa. Basi akaenda, akauondoa mwili wake.

39 Akaenda Nikodemo naye, (yule aliyemwendea usiku hapo kwanza), AKALETA MACHANGANYIKO YA MANEMANE NA UUDI, YAPATA RATLI MIA.

40 Basi wakautwaa mwili wake Yesu, wakaufunga sanda ya kitani pamoja na YALE MANUKATO, kama ilivyo desturi ya Wayahudi katika kuzika”.

Lakini desturi ni kwamba, Maiti lazima apakwe pia Marhamu.. Lakini hapa tunaona hawakufanya hivyo!. Na utaona wale wanawake  walipanga kurudia hilo zoezi la kuupaka uso wa Bwana Marhamu siku ya kwanza ya juma baada ya sabato kuisha!…wangeupaka siku ile ile lakini tayari sabato, ilikuwa imeshaingia na kulingana na desturi za wayahudi, ilikuwa si ruhusa kufanya shughuli yoyote siku ya sabato!, hivyo ikawapasa wasubiri mpaka jumapili asubuhi.

Lakini chaajabu ni kwamba asubuhi walipokwenda wakiwa na Marhamu zao, Pamoja na manukato mengine hawakumkuta Bwana kaburini..Hivyo Marhamu zao zikawa hazina kazi tena!.

Luka 23:54 “Na siku ile ilikuwa siku ya Maandalio, na sabato ikaanza kuingia.

55 Na wale wanawake waliokuja naye toka Galilaya walifuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa.

56 Wakarudi, wakafanya tayari MANUKATO NA MARHAMU. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa.

Luka 24:1 “Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari.

2 Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi,

3 Wakaingia, wasiuone mwili wa Bwana Yesu”.

Umeona hapo?.. wenyewe walikuja kwa lengo la kuupaka uso wa Bwana Yesu  marhamu na  mwili wake kuufungia manukato!, lakini hawakumkuta!..walikuwa wamechelewa.. Kumbe nafasi ya kumpaka Marhamu kichwani ilikuwa ni kipindi yupo hai!, si kipindi amekufa kama wafu wengine wanavyofanyiwa..

Na utaona yule mwanamke wa kwanza alipata huo ufunuo, na akawahi kumpaka Bwana Marhamu ya thamani kichwani mwake, na Bwana Yesu akawaambia watu “AMEFANYA VILE KUMWEKA TAYARI KWA MAZIKO YAKE”..Na popote injili itakapohubiriwa.. itahubiriwa kwa kumbukumbu lake!.

Mathayo 26:6 “Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,

7 MWANAMKE MWENYE KIBWETA CHA MARHAMU YA THAMANI KUBWA ALIMKARIBIA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE ALIPOKETI CHAKULANI.

8 Wanafunzi wake walipoona, wakachukizwa, wakasema, Ni wa nini upotevu huu?

9 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa fedha nyingi wakapewa maskini.

10 Yesu akatambua akawaambia, Mbona mnamtaabisha mwanamke? Maana ni kazi njema aliyonitendea mimi.

11 Kwa maana siku zote mnao maskini pamoja nanyi; lakini mimi hamnami siku zote.

12 MAANA KWA KUNIMWAGIA MWILI WANGU MARHAMU HIYO, AMETENDA HIVYO ILI KUNIWEKA TAYARI KWA MAZIKO YANGU.

13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.

Na kwa heshima yake, utaona Bwana Yesu alipofufuka, vile vitambaa vya sanda vilifunguliwa na kuachwa pale, lakini ile LESO ya kichwani, maandiko yanasema “ilizongwa zongwa pembeni (Yohana 20:7)”.. maana yake ilikunjwa vizuri na kuwekwa pembeni..

Sasa kwanini ikunjwe na kuwekwa pembeni?, ni kuonesha uthamani wa leso ile, kwamba isitupwe, bali iwekwe ije itumike tena!!..kwasababu bado inafaa kwa matumizi, na kufaa huko ni kutokana pia na ile Marhamu yule Mwanamke aliyompaka Bwana siku chache nyuma kabla ya kufa kwake!

Nini tunajifunza hapo?

Kuna wakati unaofaa wa kumfanyia jambo Bwana, na pia upo wakati usiofaa!!.. Ukipata nafasi ya kumtolea Bwana fedha zako, au mali zako, au muda wako.. Mtolee sasa usingoje siku Fulani mbeleni ifike. Huo muda unaoungoja ukifika, utakapokwenda kumfanyia Bwana huduma utakuwa sio muda unaofaa..

Akina Mariamu Magdalene na wenzake, ni kweli walikuwa wana nia nzuri ya kwenda kumpaka Bwana Marhamu lakini walikuwa wamechelewa, Bwana havihitaji tena hivyo vitu kwa wakati huo!!…

Aliwaambia wale watu, “maskini mnao siku zote, lakini mimi hamnami siku zote”.

Ndugu, Watoto wako unao siku zote, ndugu zako wenye shida unao siku zote, Rafiki zako wenye matatizo unao siku zote, lakini kazi ya Bwana haipo kwako siku zote!, mfanyie Bwana kitu leo usingoje kesho.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

Naivera ni nini? Kwanini Daudi aliihitaji alipomtafuta Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

1) Marhamu ni nini?

Marhamu kwa lugha ya kiingereza ni “perfume”..kwa lugha ya kiswahili iliyozoeleka ni “pafyumu”. Pafyumu inatengenezwa kutoka katika mimea mbali mbali na inakuwa katika mfumo wa kimiminika, matumizi yake ni kukifanya kitu kiwe  chenye kutoa harufu nzuri, na kufukuza wadudu na baadhi ya viumbe viharibifu, Viwango na ubora wa pafyumu (marhamu) unatofautiana.

Zipo Marhamu za gharama kubwa, ambazo hazipungui nguvu yake ya harufu haraka! (Mfano wa hizo ndio zile Bwana Yesu alizopakwa kichwani na yule mwanamke, kipindi yupo nyumbani mwa Simoni, mkoma).

Mathayo 26:6 “Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,

7 mwanamke mwenye KIBWETA CHA MARHAMU YA thamani kubwa alimkaribia akaimimina kichwani pake alipoketi chakulani.

8 Wanafunzi wake walipoona, wakachukiwa, wakasema, Ni wa nini upotevu huu?

9 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa fedha nyingi wakapewa maskini”.

Na zile akina Mariamu, Magdalene walizoziandaa kwaajili ya kumpaka Bwana siku ile ya kwanza ya juma

Luka 23:56 “Wakarudi, wakafanya tayari manukato na MARHAMU. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa”.

Lakini pia zipo Marhamu za gharama ndogo!, ambazo hazidumu sana katika mwili wa mtu.

Kwa urefu juu ya Marhamu Mwanamke aliyompaka Bwana kichwani na ujumbe wake kiroho unaweza kufungua hapa>> MARHAMU KICHWANI MWA BWANA

2) Manukato ni nini?

Manukato ni viungo ambavyo havipo katika mfumo wa kimiminika, ambavyo vikichomwa, au kupikwa au kuwekwa mahali basi vinatoa harufu Fulani inayovutia, au inayowakilisha jambo Fulani. Mfano wa manukato ni UDI, UVUMBA, na MANEMANE.. Kwasasa kuna maelfu ya aina za Manukato!

Kwa maelezo marefu kuhusu Manukato aina ya UVUMBA, na jinsi wakuhani walivyofukiza uvumba na ujumbe wake kiroho unaweza kufungua hapa >> KUVUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

MUNGU HATAZAMI MOTO WA KIGENI,KUWA MAKINI!

Ratli/ Ratili ni nini katika biblia?

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Rudi nyumbani

Print this post

Moabu ni nchi gani kwasasa?

 1) Moabu ni nchi gani kwasasa? 2) Wamoabu walikuwa ni akina nani? 3) Na waamoni walikuwa ni watu gani na wa nchi gani?


1) Moabu ni nchi gani kwasasa?

Moabu ni Mji uliokuwepo maeneo ya nchi ya YORDANI kwasasa. Yordani ni nchi iliyopakana na Nchi ya Israeli kwa upande wa Mashariki.

2) Wamoabu walikuwa ni akina nani?

Asili ya Wamoabu na Waamoni ni kutoka kwa LUTU, aliyekuwa ndugu yake Ibrahimu (Baba wa imani). Mabinti wawili wa Lutu, walilala na Baba yao na kila mmoja kubeba mimba, Watoto hao waliozaliwa mmoja aliitwa MOABU na wa PILI aliitwa AMONI.

Mwanzo 19:30 “Lutu akapanda kutoka Soari akakaa mlimani, na binti zake wawili pamoja naye, kwa sababu aliogopa kukaa katika Soari. Akakaa katika pango, yeye na binti zake wawili.

31 Yule mkubwa akamwambia mdogo, Baba yetu ni mzee, wala hakuna mtu mume katika nchi atuingilie kama ilivyo desturi ya dunia yote.

32 Haya, na tumnyweshe baba yetu mvinyo, tukalale naye, ili tumhifadhie baba yetu uzao.

33 Wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka huyo mkubwa akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.

34 Ikawa siku ya pili, mkubwa akamwambia mdogo, Tazama, nimelala jana na baba yangu, tumnyweshe mvinyo tena usiku huu, ukaingie ukalale naye.

35 Wakamnywesha tena baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka mdogo akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.

36 Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.

37 Yule mkubwa akazaa mwana, akamwita jina lake Moabu; huyo ndiye baba wa Wamoabi, hata leo.

38 Na yule mdogo naye akazaa mwana akamwita jina lake Benami; huyo ndiye baba wa Waamoni hata leo”.

3) Na waamoni walikuwa ni watu gani na wa nchi gani?

Kama tulivyosoma hapo Mwanzo 19:38, kwamba walikuwa ni kutoka uzao wa Lutu.

Taifa la Moabu ni moja ya mataifa yaliyolisumbua sana Taifa la Israeli, hususani katika safari yao ya kutoka Misri, utakumbuka Mfalme wa Moabu alimwajiri BALAAMU MCHAWI ili awalaani Israeli (yaani awaloge!).. lakini mpango huo ulishindikana!.

Bwana hakupendezwa na Taifa hilo, na alililaani.

Kwa maelezo marefu kuhusu Balaamu na uchawi wake unaweza kufungua hapa >> Balaamu mchawi

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Babeli ni nchi gani kwasasa?

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?

Marko 3:16 “Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;

17 na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo”.

Wana wa Zebedayo (yaani Yakobo na Yohana), walipewa jina hilo la Boarnege kwasababu ya ukaribu wao kwa Bwana.

Ikumbukwe kuwa ni wanafunzi watatu tu! Peke,e ndio waliobadilishwa majina na Bwana, na hao ni Petro, Yohana na Yakobo, Ambao biblia inawataja kama NGUZO! (Soma Wagalatia 2:9). Wakati Bwana akienda mlimani kusali hawa nao walikuwa Pamoja naye! (Soma Mathayo 17:1)..hawa walimpenda Bwana sana kuliko wale wanafunzi wengine 9 waliosalia.

Yakobo na Yohana ulifika wakati walikwenda kumwomba Bwana awaketishe mkono wa kuume na wa kushoto katika ufalme wake siku ile.

Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.

21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.

22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.

23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu”.

Umeona?

Hivyo hawa wana wa Zebedayo Pamoja na Petro siku zote walikuwa wanatamani kumsogelea Bwana sana, na Bwana aliijua mioyo yao!.

Kutokana na mapenzi hayo kwa Bwana, walikuwa ni watu wasiopenda kuona Bwana anakataliwa mahali popote!.. Utaona Petro, alimkata mtumwa wa kuhani mkuu sikio, kipindi ambacho walikwenda kumkamata Bwana. Halikadhalika Yohana na Yakobo walitaka Bwana ashushe moto kuwaangamiza watu wa Samaria kipindi kile walichomkataa.

Luka 9:51 “Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;

52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.

53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.

54 wanafunzi wake YAKOBO NA YOHANA walipoona hayo, walisema, BWANA, WATAKA TUAGIZE MOTO USHUKE KUTOKA MBINGUNI, UWAANGAMIZE; [KAMA ELIYA NAYE ALIVYOFANYA]?

55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.

Umeona hapo?.. Tabia hiyo ya “kutaka Moto ushuke kutoka mbinguni” ni tabia za KUNGURUMA.. Moto hauwezi kushuka kabla mbingu hazijanguruma, sauti ya Ngurumo ni sauti ya Hukumu iliyokaribu au ya adhabu!.

Hivyo Bwana aliiona tabia hiyo ndani yao, kwamba siku za mbeleni baada ya kuondoka kwake, watakuja kunguruma juu ya kazi zote za shetani, na kuziteketeza!.. kipindi hicho watakuwa hawafanyi vita juu ya damu ya nyama, kama walivyotaka kufanya juu ya hawa watu wa Samaria,(kutaka kuwaua kwa moto) bali wakati huo, watanguruma juu ya kazi zote za shetani katika ulimwengu wa roho na kuzichoma na kuwaacha watu wa Bwana huru!.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

NGURUMO SABA NI NINI?

KAMA VILE UMEME UTOKAVYO MASHARIKI UKAONEKANA HATA MAGHARIBI.

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

UFUNUO: Mlango wa 1

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

SWALI: Naomba kuelewa kwa undani Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?


JIBU:

Mbinguni,

Sehemu nyingi Biblia inaposema mbinguni, huwa inamaanisha moja kwa moja kule Mungu alipo Pamoja Malaika zake, Kule ambako Bwana Yesu alikwenda kutuandalia makao. Mahali ambapo sisi kama watakatifu bado hatujafika hata mmoja.

Ndio mbingu ya Tatu, ambayo Mtume Paulo alinyakuliwa kuonyeshwa baadhi ya vitu vilivyopo kule vipo kule ambavyo havielezeki kibinadamu, kwasababu upeo wetu ni mdogo. (2Wakorintho 12:1-4)

Ni juu sana, ambako, hatuna maelezo ya kutosha kupaelezea, mpaka tutakapofika.

2Nyakati 6:18 “Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga!”

Peponi/Paradiso:

Ni mbingu ya mangojeo, ambayo sio makazi yetu ya kudumu. Mtakatifu anayekufa sasa hivi anakwenda mahali panapoitwa Peponi/Paradiso, akisubiria, siku ya unyakuo ifike, arudi kaburini achukue mwili wake, kisha aungane Pamoja na wale watakatifu watakaokuwa hai wakati huo, na moja kwa moja safari ya kwenda mbinguni ianze, kule Bwana Yesu alipo.

Yule mwizi pale msalabani, Bwana alimwambia maneno hayo;

Luka 23:42 “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.

Wengine wanaiita mbingu ya pili, lakini vyovyote vile iitwavyo, bado ni mahali pa mangojeo pa watakatifu, Ndio kifuani pa Ibrahimu, yule maskini Lazaro alikwenda (Luka 16:19-31), ndio kule ambazo zile Roho zilizo chini ya madhahabu zilikuwa zinalia, zikiomba zilipiziwe kisasi kwa watesi wao.

Ufunuo 6:9 “Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.

10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?

11 Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao”.

Vilevile huku ndio kule wale wafu waliofufuka na Bwana Yesu walipoelekea kwa mara ya kwanza. (Mathayo 27:52-53)

Hivyo leo, hii ukifa katika Kristo, basi unakwenda katika eneo hili la mbingu, ambalo ni lizuri sana. Ukisubiri ufufuo wa mwisho.

Kuzimu:

Kuzimu kibiblia ni Neno lililomaanisha makao ya wafu  Au kaburini. Ambapo, waovu na wema walikuwa wanakwenda kabla ya Kristo kuja duniani, kuwatenganisha moja kwa moja kimakao,

Ayubu anasema

Ayubu 14:13 “Laiti ungenificha kuzimuni, Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!”

Daudi pia alipazungumzia, (Zaburi 16:10), kwamba Bwana hatomwacha huko milele.

Lakini baada ya Bwana Yesu kuja, wakatifu walitoka huko  makaburini, na kwenda peponi/ Paradiso. Mahali pa raha Zaidi pa juu na si makaburini tena. Hivyo wanaobakia makaburini au kuzimu ni waovu.

Jehanamu:

Ni mahali pa mangojeo pa waovu, ni mahali pa mateso, kama vile Paradiso palivyo mahali pa raha pa mangojeo kwa watakatifu, vivyo hivyo jehanamu nako, ni mahali pa mangojeo pa watu waovu wanaokufa sasa. Wanaadhibiwa huko, wakingojea siku ile ya hukumu ya mwisho ifike. Ili wapewe hukumu yao, katika hukumu ya kile kiti cheupe cha enzi cha mwanakondoo, kisha wakatupwe kwenye lile ziwa la moto, ambalo ndio mauti ya pili ilipo.

Ni sawa na mhalifu anayekamatwa sasa hivi, kabla ya kuhukumiwa kifungo, huwa anawekwa kwanza mahabusu, akisubiria siku ya kupandishwa kizimbani ifike, ahukumiwe kisha akatumikie kifungo chake Jela, Ndivyo ilivyo kwa watu waovu wanaokufa sasa, na waliokufa zamani. Wanakwenda katika sehemu hii ya mateso, ambayo si ya kawaida.

Bwana Yesu alisema..

Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [

46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”

Je! Wewe ni wa makao yapi?

Swali, la kujiuliza ni Je! Tukifa leo, au Unyakuo ukitukuta leo, mimi na wewe tutakuwa wa upande upi? Katika mambo ambayo hupaswi kuyachukulia juu juu tu, basi ni mambo ya Maisha yako ya milele. Kwasababu ukishakufa hakuna nafasi ya pili tena. Kama umestahili Jehanamu basi utaendelea kuishi humo milele.

Ni heri ukamgeukie Kristo, maadamu muda mchache bado unao. Acha kutazama, mambo ya ulimwengu, kwani huwa yanapumbaza sana, kukufanya usione kama kuna mabaya yanakuja mbele, Moja ya hizi siku utajutia Maisha yako, uliishije endapo hukumpa Kristo Maisha yako leo.

Tubu dhambi zako, maanisha kumfuata Yesu.

Bwana atusaidie, kuyafahamu haya.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

MILANGO YA KUZIMU.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post

Babeli ni nchi gani kwasasa?

Eneo ambalo mji wa Babeli ulikuwepo, ni maeneo ya nchi ya IRAQ kwa sasa, Mji huu ndio uliokuwa maarufu kwa kuwa na “bustani zinazoelea”, lakini kwasasa mji huu haupo tena, wala maajabu yake hayapo!!,

kwasababu mji huo ulikuwa mji wa kishetani na ulifanya dhambi nyingi, na Mungu akauadhibu.. mahali ulipokuwepo pamebakia tu mbuga!!, sawasawa na unabii Mungu alioutoa juu ya mji huo.

Isaya 13:19 “Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.

20 Hautakaliwa na watu tena kabisa, wala watu hawatakaa ndani yake tangu kizazi hata kizazi. Mwarabu hatapiga hema yake huko, wala wachungaji hawatalaza makundi yao huko.

21 Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini watacheza huko.

22 Na mbwa-mwitu watalia ndani ya ngome zake; na mbweha ndani ya majumba ya anasa; na wakati wake u karibu kufika, na siku zake hazitaongezeka”..

Kwahiyo leo hii hakuna kilichosalia pale!, pamebakia tu kuwa sehemu ya makumbusho ya kale.

Kumbuka shetani aliinyanyua Babeli ya kwanza, ambayo Mungu aliiharibu kwa kuchafua lugha za wajenzi wao!, na kazi ya ujenzi ikaishia pale! (Mwanzo 11), Lakini hakukata tamaa bali aliitengeneza Babeli nyingine, ambayo ndiyo iliyokuja kuangushwa na falme za Umedi na Uajemi, ikawa jaa!!

Lakini sasa shetani katengeneza Babeli nyingine ambayo ni ya KIROHO, hii iliyopo sasa ndio mbaya kuliko mbili zilizotangulia, na ndio kitovu cha machukizo na machafuko yote yan chi (sawasawa na Ufunuo 17).

Kwa urefu juu ya Babeli hiyo ya rohoni iliyopo sasa, fungua hapa >>> BABELI YA ROHONI.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

JE WEWE NI LAZARO YUPI, WA KWANZA AU WA PILI?

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Rudi nyumbani

Print this post