Shalom, Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya Bwana wetu.
Katika mambo ya uvuvi, zipo kanuni za uvuvi za kufuatwa, wengi wetu tunadhani, kazi ya mvuvi ni ya kwenda tu kutupa nyavu baharini, kukusanya samaki, kisha kuwatoa nje, halafu basi analala, anaamka tena kesho na nyavu yake hiyo hiyo, anakwenda kuitupa habarini na kuvua samaki wengine tena.. Ndugu Kama umekuwa ukifikiria hivyo basi umekosea.. Vinginevyo kazi ya uvuvi ingekuwa ni rahisi sana.
Kwa kawaida, wavuvi ni sharti, kila wamalizapo uvuvi mmoja, wazioshe nyavu zao kama sio kuzitengeneza, Kwasababu wanapokwenda kuvua sio tu samaki peke yake wanajinasa kwenye nyavu, bali pia kunakuwa na takataka nyingine nyingi zinakwama kwenye neti, sana sana magugu ya baharini, masalia ya magamba ya viumbe , na matope, kiasi kwamba nyavu zile zikiachwa, siku kadhaa bila kuoshwa, vinavundisha nyavu.
Na si hilo tu, kunakuwa na samaki waliokufa, katikati ya neti, nao pia wakaachwa kipindi kifupi sana wanaozesha , na hiyo inapelekea kukaribisha panya kula neti, na kuifanya iwe dhaifu sana, hususani kwenye kamba zake,
Na bado wanasema, ili samaki wawezi kukamatwa kiwepesi, ni sharti ni yenyewe iwe kama vile haionekani itupwapo habarini ,lakini kama inauchafu mwingi, wanasema samaki wakiona, wanaogopa na kukimbia.
Pia nyavu hiyo hiyo inapaswa itengenezwe/au ifanyiwe ukarabati, kwasababu wakati mwingine, kunakuwa ni miamba yenye ncha kali chini inayochana nyavu, au samaki wenye miiba mikali ambao wakipita mara moja tu katikati wanachana nyavu. Hivyo kama mvuvi kila unapoliza kuvua ni sharti ukague neti yako kama inamatundu uizibe.
Hivyo suala la kusafisha na kukarabiti neti ni lazima kwa mvuvi yeyote kila anapomaliza kuvua, haijalishi siku hiyo amepata samaki au hajapata. Haijalishi atakuwa amechoka au hajachoka, Ni lazima aisafishe, kwasababu ni lazima tu itakuwa na uchafu.
Na ndio maana wakati ule Bwana Yesu alipokuwa anapita pwani aliwaona akina Petro, wametoka kuvua samaki, na hawajapata chochote usiku kucha, lakini kanuni ilikuwa ni lazima wazioshe nyavu zao, haijalishi walipata au hawakupata.
Luka 5:1 “Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti, 2 akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, LAKINI WAVUVI WAMETOKA, WANAOSHA NYAVU zao. 3 Akaingia katika chombo kimoja, ndicho chake Simoni, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni. 4 Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki. 5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu”.
Luka 5:1 “Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,
2 akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, LAKINI WAVUVI WAMETOKA, WANAOSHA NYAVU zao.
3 Akaingia katika chombo kimoja, ndicho chake Simoni, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.
4 Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.
5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu”.
Umeona, sasa soma tena vifungu hivi, uone kuna wakati pia walizitengeneza nyavu zao, na sio kuosha tu peke yake.
Marko 1:19 “Akaendelea mbele kidogo, akamwona Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, nao pia walikuwa chomboni, WAKIZITENGENEZA NYAVU ZAO. 20 Mara akawaita, wakamwacha baba yao Zebedayo ndani ya chombo pamoja na watu wa mshahara, wakaenda, wakamfuata.
Marko 1:19 “Akaendelea mbele kidogo, akamwona Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, nao pia walikuwa chomboni, WAKIZITENGENEZA NYAVU ZAO.
20 Mara akawaita, wakamwacha baba yao Zebedayo ndani ya chombo pamoja na watu wa mshahara, wakaenda, wakamfuata.
SASA MAMBO HAYO KATIKA ROHO YANAFUNUA NINI?
Sisi kama wahubiri, sisi kama watumishi wa Mungu tunaofanya kazi ya kuwavua watu kwa Kristo, huwa tunajisahau sana na kudhani kuwa kuhubiri tu kunatosha, Au kufundisha tu, au kushuhudia tu. Hatujui kuwa tunapaswa kila siku TUSAFISHE na kutengeneza NYAVU zetu, tunazozitumia kuvulia.
TUNATENGENEZAJE NYAVU ZETU?
Na tunazitengeneza kwa NENO LA MUNGU. Ikiwa na maana tunapaswa Neno la Mungu likae kwa wingi ndani yetu, tusome Neno, tujue misingi na kanuni za uvuvi Kristo anazozitaka, tujue ni nini tunapaswa tufundishe, na nini tusifundishe kwa wakati husika, ujumbe upi tutoe, na upi tusitoe kwa watu fulani. Vinginevyo tukipuuzia, tutajikuta samaki watapenya kwenye nyavu zetu, tukawakosa, kwasababu zina matundu matundu.
TUNAOSHAJE NYAVU ZETU?
Vile vile, Kuosha nyavu zetu. Ni kwa kujitakasa maisha yetu. Maana yake kuishi maisha yanayompendeza Mungu, maisha ya ushuhuda, maisha matakatifu. Ikiwa tuna ushuhuda mbaya katika mazingira yanayotuzunguka, na huku bado tunahubiri injili ni kuonyesha kuwa NYAVU zetu ni chafu. Hivyo Samaki watatukimbia wanapoona uchafu huo kwetu. Na ndio maana pale tunapovua hatuona matunda yoyote, kumbe ushuhuda wetu ndio unaowakimbiza mbali na sisi.
Hivyo ni wajibu wetu, sisi kama wahubiri kuzingatia hayo mambo mawili kila siku. Kwasababu wavuvi nao wanafanya hivyo kila siku. Nasi tuifuate kanuni hiyo rohoni. Na hakika tutamletea Kristo matunda mengi.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
MIUJIZA YA KRISTO, HAITEGEMEI KANUNI ZA KIBINADAMU.
Je ni sahihi kuweka walinzi kulinda mali zetu?
Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?
MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?
APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.
Rudi nyumbani
Print this post
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha sasa tuzidi kuyatafakari maneno matukufu ya Mungu wetu, Maadamu katujalia kuiona leo.
Kwanini leo hii imekuwa ngumu sana kuipeleka injili kwa watu walio nje, ili wamwamini Yesu Kristo (Tukisema walio nje, tunamaanisha watu wa kidunia, au watu walio katika dini nyingine), Tunaweza kusema Mungu anawajua walio wake, ni kweli, lakini hicho sio kisingizio, ipo sababu nyingine ambayo tumeikosa sisi kama kanisa na sababu yenyewe ni kukosa UMOJA.
Tukiupata huo kama kanisa basi hatutamia nguvu nyingi sana kuulezea ulimwengu uzuri wa Yesu, bali huo umoja wenyewe tu utauaminisha ulimwengu yeye ni nani.
Bwana Yesu alilizungumza hilo katika..
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Umeona, kumbe ulimwengu unaweza kumwamini Yesu, kuwa ndiye mwokozi wa ulimwengu, ikiwa tu tutajitengeneza sisi kwanza katika umoja. Lakini tunapaswa tujue si kila umoja, ni umoja sahihi unaotokana na Mungu..Hapo Bwana hazungumzii umoja wa kichama au umoja wa kidini, au umoja wa kimadhehebu, kama unaoendelea sasa hivi ulimwenguni.. bali umoja anaouzungumzia hapo ni umoja wa Roho,. Kwasababu haiwezekani watu wawili wanaamini vitu viwili tofauti, halafu wawe na umoja, huo sio umoja utakuwa ni umoja wa kimaslahi tu, lakini sio wa Roho.
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.
Umeona vifungu hivyo? Agizo mojawapo ni kwamba tuutambue ubatizo mmoja na sahihi ni upi, kisha wote tuwe nao, ambao ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5, kisha wote tumpokee Roho mmoja, ambaye ndiye Roho Mtakatifu, tuwe na Bwana mmoja ambaye ni YESU KRISTO jiwe kuu la pembeni, na sio mtume mwingine, au mtakatifu mwingine pembeni yake hapana,.. Na vilevile tuwe na Imani moja, ambayo mzizi wake na shina lake ni BIBLIA TAKATIFU na sio dini au dhehebu.
Tukizingatia hayo, kisha tukashirikiana na ulimwengu ukatuona, basi hatutatumia nguvu kubwa kuwaamishi Kristo kwao, kwani huo umoja wenyewe tu utawahubiria watu uzuri wa Kristo. Lakini tukizidi kuupoteza umoja huo, kila mtu na imani yake, dhehebu lake,. Ni ngumu sana kuugeuza ulimwengu. Hivyo ni wajibu wetu sisi, kama kanisa la Kristo tujipime, je! Umoja huu uliosahihi upo ndani yetu? Kama haupo, basi ipo kasoro. Tujitahidi sana tuunde kwa bidii zote, ili Bwana aaminiwe katikati ya mataifa, matunda mengi yaje kwake..
Hilo ni agizo la Bwana, na sio la mwanadamu.
“Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Shalom.
Maran atha.
MADHARA YA KUFUATA MAMBO YAKO TU!
Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?
ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.
KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Jibu: Shalom.
Neno “Amali” maana yake ni “kazi ngumu” hususani ile inayohusisha mwili, kama vile kazi ya kibarua cha kulima au kukata mti.
Katika biblia neno hilo limeonekana mara nne..
Mhubiri 4: 4 “Tena nikafikiri AMALI ZOTE, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.
Mistari mingine inayoainisha neno hilo ni pamoja na Mhubiri 4:8, Mhubiri 5:19, na Mhubiri 8:15.
Neno “Ijara” maana yake ni “mshahara anaolipwa mtu kwa siku”. kumbuka mshahara anaolipwa mtu kwa mwezi hauitwi Ijara, Ijara ni mshahara wa siku tu, mara nyingi unawahusu vibarua.
Walawi 19:13 “Usimdhulumu jirani yako, wala kumnyang’anya mali yake; IJARA YAKE aliyeajiriwa isikae kwako usiku kucha hata asubuhi”.
Isaya 3:11 “Ole wake mtu mbaya; shari itakuwa kwake, kwa maana atapewa IJARA ya mikono yake”
Isaya 40: 10 “Tazameni, Bwana Mungu atakuja kama shujaa, Na mkono wake ndio utakaomtawalia; Tazameni, thawabu yake i pamoja naye, Na ijara yake i mbele zake”.
Mistari mingine inayoanisha neno hilo ni 2Nyakati 15:7, Mhubiri 4:9, Mhubiri 9:5, Isaya 5:23, Mika 1:7, Zekaria 8:10, na 2Wakorintho 5:10.
Hivyo hakuna Amali isiyo na Ijara. Vile vile kazi ya Mungu ina ujira wake, kama Bwana alivyosema katika kitabu cha Ufunuo..
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo. 13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.
Maran atha!
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.
JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?
Maana Ya Maneno Katika Biblia.
WhatsApp
Mbu ni mdudu ambaye endapo akitua juu ya mwili wa mtu, kama hatasumbuliwa kwa namna yoyote ile, basi atanyonya damu na mwisho wa siku tumbo lake litajaa sana mpaka kupasuka akiwa pale pale ananyonya!..na hapo ndio unakuwa mwisho wa maisha yake!.
Utafiti unaonyesha, kuwa wakati mbu ananyonya damu, mfumo wa taarifa wa tumbo lake na ufahamu wake unakatika, hivyo hajijui kuwa kama hapa kashiba au bado, yeye ile njaa ya kwanza ipo pale pale, anaendeleo kunyonya tu, mpaka anafia pale pale..
Biblia inasema pia katika Mhubiri 5:10 kuwa..
Mhubiri 5:10 “APENDAYE FEDHA HATASHIBA FEDHA, Wala apendaye wingi hatashiba nyongeza. Hayo pia ni ubatili. 11 Mali yakiongezeka, hao walao nao waongezeka na mwenyewe hufaidiwa nini, ila kuyatazama kwa macho yake tu?”
Mhubiri 5:10 “APENDAYE FEDHA HATASHIBA FEDHA, Wala apendaye wingi hatashiba nyongeza. Hayo pia ni ubatili.
11 Mali yakiongezeka, hao walao nao waongezeka na mwenyewe hufaidiwa nini, ila kuyatazama kwa macho yake tu?”
Sio vibaya kutafuta fedha, ni jambo la muhimu, lakini lisiwe jambo linalotawala maisha kiasi kwamba, unapoangalia kushoto, au kulia unaona fedha, au unawaza fedha!. Ukiwa katika hali kama hiyo, nataka nikuambie “kupenda fedha kupo ndani yako hata kama hutakiri kwa kinywa”.
Hekima ya ulimwengu huu inatuambia na kutufundisha, kuwa muda wote tuwaze fedha, tufikiri fedha, tuziishi fedha, tuzitafute lakini hekima ya Mungu haisemi hivyo.. hekima ya kiMungu inasema hivi…
Waebrania 13:5 “MSIWE NA TABIA YA KUPENDA FEDHA; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”.
Hekima hii kwa ulimwengu inaonekana ni upumbavu!, lakini kwa watu wa Mungu ni nguvu ya Mungu.
Hekima ya kiMungu pia inasema, shina moja la mabaya yote ni kupenda fedha!
1Timotheo 6:10 “Maana SHINA MOJA LA MABAYA YA KILA NAMNA NI KUPENDA FEDHA; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.
Mtu anayependa fedha anakuwa hashibi fedha siku zote, akipata elfu hashukuru wala haridhiki, atatamani tena laki, akipata laki hali yake ni ile ile, atataka milioni, akipata milioni atataka milioni 100, wala hutaona badiliko lolote kwake, hashukuru wala hatosheki..ni kama mbu anayenyonya damu, pasipo kujijua kuwa tayari tumbo lake limeshajaa na linakaribia kupasuka, yeye anaendelea tu!, mwisho wa siku anapasuka matumbo!.
Ndicho kilichomtokea Yuda, alianza kupenda fedha kidogo kidogo, na kwasababu kupenda fedha ni roho!, ikampelekea asitosheke kuiba fedha iliyokuwa inapatikana katika mfuko wa Bwana!, akapiga hatua nyingine ya kutamani hata apate fedha nyingi zaidi, kwa kumsaliti Bwana Yesu! Pasipo kujua kuwa tayari tumbo lake limejaa na linakaribia kupasuka!, yeye aliendelea kuzisaka fedha kwa nguvu, na ulipofika wakati matumbo yake yalipasuka kama maandiko yanavyosema…
Matendo 1:18 “(Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka. 19 Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.)”
Matendo 1:18 “(Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka.
19 Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.)”
Biblia inatuonya tusiwe na tabia ya kupenda fedha.., haijatukataza kufanya kazi!, bali tusiwe watu wa kupenda fedha!…unaweza kuipenda kazi unayoifanya lakini usiwe na tamaa ya kupenda fedha katika hiyo!, kiasi kwamba upate kingi au kidogo!, moyo wako hauutaabiki!!, maadamu umetoa huduma iliyo bora, furaha yako inakuwa ni ule uaminifu katika kazi yako, yaani siku ukiona hujafanya kazi kwa uaminifu ndio moyo wako unauma, na sio siku umeona hujapata faida nyingi!… Na wengi wanaoipenda kazi zao kuliko faida na fedha, ndio wanaofanikiwa kuliko wale ambao kipaumbele chao ni fedha tu!.. Hao wapo tayari mwingine alie ili wao wapate faida, au mwingine adhurike wao wapate fedha, kama Yuda!, wapo radhi wakuuzie hata sumu, au wafanye biashara haramu ilimdari tu matumbo yao yajae…
Ndio maana wanafananishwa na mbu anayenyonya damu!.. mbu ananyonya uhai wa mtu, ambayo ni damu yake..ndio maana mwisho wake unakuwa ni kupasuka matumbo!..
Bwana atusaidie, tuwe watu wa kumpenda yeye zaidi ya kupenda fedha!.
Mathayo 6:33 “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”
KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.
ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.
BWANA AYAGANGE NA MACHO YETU PIA.
MAMA UNALILIA NINI?
Leo hii dunia imekuwa na sikukuu nyingi sana za maonyesho. Na sikukuu hizo Mungu ameruhusu makusudi kabisa ziwepo ili kutupa picha halisi ya jinsi sikukuu yake kubwa ya maonyesho itakavyokuwa mbinguni.
Kwamfano kipindi hiki, kwa taifa kama la Tanzania, lipo katika sikukukuu ya maonyesho ya wafanyabiashara maarufu kama saba saba (7’7). Na mwezi ujao kutakuwa na maonyesho mengine makubwa ya wakulima yajulikanayo kama nane nane (8’8). Kama ulishawahi kutembelea maonyesho haya, au yanayofanana na haya nadhani utakuwa unaelewa ni nini hasaa kinaendelea kule.
Kwa ufupi ni kwamba utakutana na mabanda mengi sana, na kila banda lina onyesho lake la kipekee, kiasi kwamba mpaka utakapomaliza mabanda yote, hutatoka kama ulivyo. Utakutana na mambo mengi sana usiyoyajua, ni jinsi gani vitu vinatengezwa, ni technolijia gani inafanya kitu kiwe hivi au vile n.k.
Sasa, mambo hayo na kwa Bwana Yesu pia yapo. Ipo siku kubwa sana ya maonyesho, ambayo itafanyika huko mbinguni, Sikukuu hiyo biblia inatuonyesha tumeandaliwa sisi, mahususi ili kuuona utukufu wa Yesu aliopewa na Baba yake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kwa ajili yetu sisi.
Yohana 17:24 “Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, WAPATE NA KUUTAZAMA UTUKUFU WANGU ULIONIPA; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu”.
Umeona hapo? Anasema, lengo la yeye kutaka tuwepo na yeye popote alipo ni kusudi kwamba tuutazame utukufu wake aliopewa… Ndugu hadi sasa Bwana Yesu ameshajiandaa kutuonyesha ukuu wake, huko mbinguni.. Tengeneza picha jinsi siku hiyo itakavyokuwa, tutakapotembezwa katika mabanda ya mbinguni(tukitumia lugha ya kibinadamu).. Tunatoka sehemu moja anatuonyesha nchi nzuri ya dhahabu, tukidhani ndio basi, tunatoka hapo anatupeleka kwingine anatuonyesha makasri mazuri ya kifalme, halafu anasema hayo yote ni ya kwenu, niliyokuja kuwaandalia huku kwa miaka 2000, kama nilivyowaambia katika Yohana 14
Yohana 14:1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. 2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. 3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”.
Yohana 14:1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”.
Anatoka hapo anatupeleka tena katika banda lingine, anatuonyesha viumbe wa kimbinguni, ambao hutujawahi hata kuwaona huku duniani, anakuambia hawa watawatumikia nyinyi.. Tunatoka hapo anawapeleka na kwa malaika zake wote, anatutambulisha kwa mmoja baada ya mwingine, kisha Bwana anasema hawa nao watawahudumia siku zote.. Tunatoka hapo tunakwenda kuonyeshwa vyombo vizuri za muziki, ambavyo kwa hivyo tutakuwa tunamwimbia Mungu daima. Mnaenda sehemu nyingine mahali pa mafunzo mnaambia hapa mtafundishwa jinsi ya kuwa na uwezo wa kiroho kama wa malaika, mnatoka hapo mnapelekwa tena kwingine kuonyeshwa mambo ya ajabu, ambayo kimsingi hatuwezi kuyaeleza hapa, kwasababu ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala, sikio kusikia, wala halijawahi kuingia katika moyo wa mwanadamu yoyote.
1Wakorintho 2:9 “lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao”.
Siku hiyo ndiyo tutakapojua Bwana Yesu ni mkuu namna gani. Leo hii huwezi kujua lolote, kwasababu wakati wa yeye kudhihirisha utukufu wake haujafika, lakini siku si nyingi, atatunyakua na kutupeleka huko aliko. Tukauone utukufu wake aliopewa na Baba yake.
Tutaona mambo mengi sana, kila mahali tutakapokuwa tunapelekwa tutabakia kutoa macho tu, kwasababu tutasema hiki nacho tumepewa sisi? Hata hiki? Hata kile? Na Yesu atasema NDIO niliwaandalia nyinyi haya yote..Kama hatujaelewa Tutauliza maswali, na yote yatajibiwa, tutatembea katika maonyesho hayo makuu kwa muda wa miaka saba mfululizo.
Kwakweli tukose vyote sasa lakini sio hilo. Tukose mali sasa, tukose umaarufu, tukose vya kidunia, tusikose karamu kuu ya mwanakondoo, mbinguni. Lakini kwa bahati mbaya ni kuwa watu wengi watayakosa maonyesho hayo makuu, kwasababu kama mpaka leo hii, mtu akiambiwa aokoke kwa kumaanisha kabisa kumfuata Yesu, anaona kama analetewa habari za kilokole, unategemea vipi mtu huyo, ataingia kwenye karamu hiyo na maonyesho hayo?
Hatakwenda popote,atabaki tu hapa duniani, hata akifa leo, hiyo siku yenyewe ikifika, hatoweza kufufuliwa aende katika UNYAKUO. Ndugu huo ndio wakati ambao kutakuwa na kilio na kusaga meno kama Bwana Yesu alivyosema.. Hutalia kwasababu inaingia kwenye dhiki kuu tu, bali utalia sana kwasababu umekosa tendo hilo kuu la karamu ya Bwana Yesu, ambayo itaambatana na MAONYESHO hayo MAKUBWA SANA.
Maneno hayo ni lazima yatimie. Haleluya.
Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?
Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?
TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.
Je! Mfalme Abiya na Mfalme Asa walikuwa ni ndugu?
Jibu: Ni vizuri kufahamu kuwa kuna vitu vimeumbwa na Mungu na kuna vitu vimeumbwa na viumbe wa Mungu.
Kwa mfano Mungu hajaumba gari, wala treni, wala pikipiki. Gari tunaloendesha limeumbwa na wanadamu, vile vile hajaumba ndege, wala kiti, mambo hayo yote ni sisi wanadamu ndiyo tuliyoyatengeneza… tumeichukua malighafi hii iliyoumbwa na Mungu, tukaichanganya na malighafi ile, tukatengeneza gari. N.k
Vile vile Mungu hajaumba chapati tunazokula wala maandazi, wala pilau.. alichokiumba ni malighafi hizo, yaani unga, mafuta, chumvi na maji.. Kwa utashi wetu sisi wanadamu, ndio tukachukua malighafi hizo na kuzichanganya pamoja na kuzichoma ndipo vikatokea vyakula hivyo tunavyokula kama maandazi au chapati au chakula kingine chochote.
Kadhalika Mungu hajaumba dhambi, wala matatizo wala shida.. Mambo hayo ni sisi tumeyatengeneza wenyewe, kupitia malighafi au vitu ambavyo Mungu kaviumba. Tunapochukua ukweli na kuuchanganya na vitu vingine na kuugeuza hapo ndipo unapozaliwa uongo!.. Ndio DHAMBI YENYEWE!!
Kitendo cha kukutana kimwili si kibaya lakini kinapofanyika wakati usio sahihi, au na mtu asiyesahihi kinageuka kuwa uzinzi au uasherati, Hivyo uasherati ni kitu sahihi kilichochanganywa na muda usio sahihi na mtu asiyesahihi. Kwahiyo Mungu hajaumba uasherati, bali ni watu ndio walioumba uasherati.
Hivyo dhambi zote zimeumbwa na wanadamu pamoja na shetani na malaika zake. Na si Mungu aliyeziumba kwasababu yeye ni mtakatifu, na wala hachangamani na uchafu. Ndio maana anaichukia dhambi.. Kwasababu ingekuwa ni yeye kaiumba asingeichukia.. Mtu hawezi kuchukia kitu alichokitengeneza yeye mwenyewe..
Na kila siku dhambi zinaendelea kuumbwa na wanadamu.. Ndio maana biblia inasema siku za mwisho maasi yataongezeka, maana yake kila siku maovu mapya yanazaliwa..Ndio maana katika kilele cha maovu haya Bwana lazima aiangamize hii dunia.
Hivyo hatuna budi kukaa mbali na dhambi, kwasababu Mungu wetu ni mtakatifu na wala hachangamani na dhambi.
Mathayo 5:48 “Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Na hatuwezi kuishinda dhambi tukiwa nje ya agano la mwanae mpendwa Yesu. Tunaishinda dhambi na kuacha kuiumba kwa kuungama dhambi zetu zote, kwa kumaanisha kutozitenda tena, na kisha kwenda kubatizwa ubatizo sahihi na kupokea Roho Mtakatifu.
Nini maana ya “Bwana Yesu ni mzaliwa wa kwanza wa waliokufa?”(Ufunuo 1:5)
SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.
Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni ipi?
Maswali na Majibu
JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?
Ipo faida ya kufuata mambo yako na kutojishughulisha na mambo ya wengine!.. Lakini pia ipo hasara kubwa ya kutojishughulisha na mambo ya wengine na kufuata mambo yako tu!. Faida ya kufuata mambo yako ni kwamba utakuwa huru katika mambo yako, na hautaishi kwa wasiwasi wala hofu!…kwasababu utakuwa hufuatilii mambo ya wengine, na wala hushirikiani nao, hivyo hutakuwa na mtu wa kushindana naye wala kujilinganisha naye..Kwahiyo utaishi maisha ya uhuru sana..
Lakini pamoja na hayo kuna hatari kubwa sana ya kuishi maisha ya namna hiyo, Maana yake yanapozidi sana, kiasi kwamba unakuwa umefunga milango yote, umejitenga na hutaki kufuatilia chochote cha nje! Ipo hatari!!
Leo tutajifunza kupitia biblia, mojawapo ya hatari ya maisha ya namna hiyo..
Katika maandiko tunausoma mji mmoja ulioitwa Laisha, mji huu ulikuwepo kaskazini mwa Taifa la Israeli, kabla haujatwaliwa na Israeli, ulikuwa unaitwa hivyo Laisha, lakini mji huu ulikuwa ni wa kipekee sana, kwanza ulikuwa ni mji ambao umejitenga, upo mbali sana na miji mingine, na pili ulikuwa ni mji ambao haukushirikiana na miji mingine, hivyo watu wake walikuwa wanafuata mambo yao tu!, wanafanya kazi kwaajili ya kuuendeleza mji wao, na wala hawakuwa na shughuli na mataifa mengine.. Hiyo ikawafanya wafanikiwe sana, kwasababu mambo yao yote hawakuyaendesha kwa hofu wala kwa mashindano.. Na zaidi ya yote, wakajiwekea utaratibu kuwa watu wote ni sawa katika ile jamii, hakuna wa kumtawala mwenzake wala kunyanyasana..
Lakini biblia inatuambia uharibifu wake ulikuja ghafla bila wao kutegemea..na mji mzima uliangamizwa pasipo msaada, kwasababu walikuwa mbali na miji mingine ambayo pengine ingewasaidia, na vile vile haikuwa na mahusiano na mji wowote ule.. ni wao kama wao..
Tusome habari hiyo kidogo katika maandiko.. (Zingatia vipengele vilivyoainishwa kwa herufi kubwa)
Waamuzi 18:7 “Ndipo hao watu watano wakaenda zao, WAKAFIKA LAISHA, wakawaona wale watu waliokuwamo ndani yake, jinsi walivyokaa salama salimini kwa mfano wa walivyokaa hao Wasidoni, WENYE STAREHE NA HIFADHI, kwa maana hapakuwa na mtu katika nchi hiyo aliyekuwa na amri, aliyeweza kuwatweza katika neno lo lote, nao walikuwa wa mbali na hao Wasidoni, WALA HAWAKUWA NA SHUGHULI NA MTU YE YOTE. 8 Kisha wakawarudia ndugu zao huko Sora na Eshtaoli; ndugu zao wakawauliza; Haya, mna habari gani? 9 Wakasema, Haya, inukeni, twende tukapigane nao; KWA MAANA TUMEIONA HIYO NCHI NAYO NI NCHI NZURI sana; nanyi, je! Mwanyamaa tu? Msiwe wavivu kwenda, na kuingia, ili mpate kuimiliki nchi hiyo. 10 Hapo mtakapokwenda mtawafikilia WATU WAKAAO SALAMA SALIMINI, na hiyo nchi nayo ni kubwa; kwa kuwa Mungu ameitia mikononi mwenu; ni mahali ambapo hapana kupungukiwa na kitu cho chote kilicho duniani. 11 Basi wakatoka hapo watu mia sita waliovaa silaha za vita, wa jamaa ya Wadani, kutoka Sora, na kutoka Eshtaoli…………………………………… 27 Nao wakakitwaa hicho alichokuwa amekifanya Mika, na kuhani aliyekuwa naye nao wakafikilia Laisha, KWENYE WATU WALIOKUWA WENYE STAREHE NA HIFADHI, wakawapiga kwa makali ya upanga; wakaupiga moto mji wao. 28 WALA HAKUWAKO MWOKOZI, KWA SABABU HUO MJI ULIKUWA NI MBALI SANA NA SIDONI, NAO HAWAKUWA NA SHUGHULI NA MTU AWAYE YOTE; na mji huo ulikuwa katika hilo bonde lililo karibu na Bethrehobu. Nao wakaujenga huo mji na kukaa humo. 29 Wakauita mji jina lake Dani, kwa kuliandama jina la baba yao Dani, aliyezaliwa kwake Israeli; lakini jina la mji huo HAPO KWANZA ULIKUWA UKIITWA LAISHA”.
Waamuzi 18:7 “Ndipo hao watu watano wakaenda zao, WAKAFIKA LAISHA, wakawaona wale watu waliokuwamo ndani yake, jinsi walivyokaa salama salimini kwa mfano wa walivyokaa hao Wasidoni, WENYE STAREHE NA HIFADHI, kwa maana hapakuwa na mtu katika nchi hiyo aliyekuwa na amri, aliyeweza kuwatweza katika neno lo lote, nao walikuwa wa mbali na hao Wasidoni, WALA HAWAKUWA NA SHUGHULI NA MTU YE YOTE.
8 Kisha wakawarudia ndugu zao huko Sora na Eshtaoli; ndugu zao wakawauliza; Haya, mna habari gani?
9 Wakasema, Haya, inukeni, twende tukapigane nao; KWA MAANA TUMEIONA HIYO NCHI NAYO NI NCHI NZURI sana; nanyi, je! Mwanyamaa tu? Msiwe wavivu kwenda, na kuingia, ili mpate kuimiliki nchi hiyo.
10 Hapo mtakapokwenda mtawafikilia WATU WAKAAO SALAMA SALIMINI, na hiyo nchi nayo ni kubwa; kwa kuwa Mungu ameitia mikononi mwenu; ni mahali ambapo hapana kupungukiwa na kitu cho chote kilicho duniani.
11 Basi wakatoka hapo watu mia sita waliovaa silaha za vita, wa jamaa ya Wadani, kutoka Sora, na kutoka Eshtaoli……………………………………
27 Nao wakakitwaa hicho alichokuwa amekifanya Mika, na kuhani aliyekuwa naye nao wakafikilia Laisha, KWENYE WATU WALIOKUWA WENYE STAREHE NA HIFADHI, wakawapiga kwa makali ya upanga; wakaupiga moto mji wao.
28 WALA HAKUWAKO MWOKOZI, KWA SABABU HUO MJI ULIKUWA NI MBALI SANA NA SIDONI, NAO HAWAKUWA NA SHUGHULI NA MTU AWAYE YOTE; na mji huo ulikuwa katika hilo bonde lililo karibu na Bethrehobu. Nao wakaujenga huo mji na kukaa humo.
29 Wakauita mji jina lake Dani, kwa kuliandama jina la baba yao Dani, aliyezaliwa kwake Israeli; lakini jina la mji huo HAPO KWANZA ULIKUWA UKIITWA LAISHA”.
Umeona?.. Laiti mji huo ungekuwa na mahusiano na miji mingine, labda wangepata mwokozi, na wangeokoka na maangamizi hayo, kwani ingekuwa ni rahisi wao kusaidiwa na majirani zao, lakini maadui zao walipowasoma udhaifu wao kuwa ni watu wanaojiona kuwa hawawezi kuhitaji msaada kutoka kwa mwingine yeyote, ni watu ambao wapo wenyewe wenyewe, ndipo wakapata nguvu!, kwani walitambua hata watakapowavamia hakuna atakayekuja kuwasaidia. Na siku ya maangamizi yao ilipofika, wakaangamia wote!, pamoja na utajiri wao, na fedha zao, na mali zao na kila kitu chao, waliopotea wote.
Hiyo inatufundisha nini?
Umoja ni ulinzi, biblia inasema katika Mhubiri….
Mhubiri 4:12 “ Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi.”
Wakati mwingine unaweza kufikiri kuwa peke yako ndio afya, lakini kinyume chake ndivyo unavyodhoofisha ulinzi wako! Na usalama wako!.. Ni vizuri kutojishughulisha na mambo ya wengine na kufuata mambo yako!.. lakini isizidi sana, kiasi kwamba hata hutaki kuwa na mahusiano na wengine!, hutaki kujifunza kutoka kwao, hutaki kusaidiwa na wao, hutaki kuwasaidia, hutaki kujinyenyekeza kwao, ni wewe kama wewe tu! n.k
Kwasababu huo ubinafsi wako ambao unadhani ni ulinzi kumbe ndio nguvu ya adui yako shetani. Yeye anatamani uendelee kukaa hivyo hivyo bila kuwa na shughuli na mtu mwingine yeyote ili siku atakapokuletea madhara!, ukose msaada. Ni kweli ubinafsi wako utakupa uhuru!, hata unaweza kukupa utajiri, lakini siku ya hautakusaidia siku ya maangamizi..
Hata katika kanisa kitu cha kwanza shetani anachokiua ni Umoja!.. kwasababu anajua ni ngumu kulishambulia kundi kubwa kuliko mtu mmoja mmoja!.. hivyo anachokifanya kwanza ni kuhakikisha analitenganisha kundi, na kutenga mtu mmoja mmoja, hivyo anahakikisha anaweza roho ya kila mtu kufuata mambo yako, na kutojishughulisha na mambo ya wengine.. Na akishafanikiwa hilo, ndipo anaanza kuwamaliza mmoja mmoja.
Ndugu! Usikimbie vikundi vya maombi, na kutafuta kuomba mwenyewe mwenyewe kila mara, ukidhani ndio salama!… Tenga muda wako mwingi wa kusali mwenyewe lakini usiache kukusanyika na wengine katika maombi.
Vile vile usijione kuwa una hekima kwa wewe kutokwenda kanisani kukusanyika na wengine!, kwasababu tu ya vikasoro vidogo vidogo unavyoviona pale!..na huku ukijitumainisha katika kusali mwenyewe ! Bali kinyume chake uogope!… kwasababu upo katika rada ya shetani!!.. Hutadumu muda mrefu, utapotea kabisa..
Yohana 17: 21 “WOTE WAWE NA UMOJA; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. 22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ILI WAWE NA UMOJA KAMA SISI TULIVYO UMOJA. 23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ILI WAWE WAMEKAMILIKA KATIKA UMOJA; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Yohana 17: 21 “WOTE WAWE NA UMOJA; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ILI WAWE NA UMOJA KAMA SISI TULIVYO UMOJA.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ILI WAWE WAMEKAMILIKA KATIKA UMOJA; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Bwana atubariki.
Kama hujampokea Yesu, mlango wa neema bado upo wazi!.. ila hautakuwa hivyo siku zote, hivyo mpokee Yesu leo akuoshe dhambi zako na kukupa uzima wa milele.
Maashera na Maashtorethi ni nini?
KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.
WAOMBEENI WANAOWAUDHI.
Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?
Neno Ahera limeonekana mara tatu tu katika biblia, limeonekana katika kitabu cha 1Wafalme 2:6 na 9 na katika kitabu cha Wimbo ulio bora 8:6, mara zote hizi Neno hilo limetumika likimaanisha “kaburi”. Hivyo Ahera maana yake ni kaburi.
1Wafalme 2:5 “Na zaidi ya hayo, umejua alivyonitenda Yoabu, mwana wa Seruya, yaani, alivyowatenda majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri, mwana wa Neri, na Amasa, mwana wa Yetheri, ambao aliwaua, na kuimwaga damu ya vita wakati wa amani, akautia damu ya vita mshipi uliokuwa viunoni mwake, na viatu vilivyokuwa miguuni mwake. 6 Kwa hiyo ufanye kama ilivyo hekima yako, wala usimwachie mvi zake kushukia AHERA KWA AMANI”.
1Wafalme 2:5 “Na zaidi ya hayo, umejua alivyonitenda Yoabu, mwana wa Seruya, yaani, alivyowatenda majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri, mwana wa Neri, na Amasa, mwana wa Yetheri, ambao aliwaua, na kuimwaga damu ya vita wakati wa amani, akautia damu ya vita mshipi uliokuwa viunoni mwake, na viatu vilivyokuwa miguuni mwake.
6 Kwa hiyo ufanye kama ilivyo hekima yako, wala usimwachie mvi zake kushukia AHERA KWA AMANI”.
Ahera inatukumbusha kuwa kuna mwisho wa maisha haya… hivyo hatuna budi kutengeneza maisha yetu, kabla hatujaingia kaburini… Kwasababu baada ya kifo kitakachokuwa kimebakia kwetu ni hukumu..
Waebrania 9:27 “Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu”.
Bwana atujalie tuishi maisha yanayompendeza yeye, angali bado tunaishi.
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
NYAKATI HIZI NI ZA MWISHO, HII DUNIA INAKWENDA KUISHA.
MUNGU ATAKUUA UKIWA MBAYA MACHONI PAKE.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu katika kuyatafakari maandiko.
Je! Umewahi kujiuliza kwanini biblia inasema upendo una nguvu kama mauti?.
Wimbo ulio bora 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana UPENDO UNA NGUVU KAMA MAUTI, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu”
Upendo wa Mungu kwetu! Unafananishwa na upendo wa Mtu kwa mpenzi wake. Jinsi mwanaume anavyompenda mke wake ndivyo Kristo anavyotupenda sisi. Na mtu anapozama sana katika upendo huwa anakitu kingine kinachofuatana na huo mpendo, na hicho si kingine zaidi ya Wivu!.. hivi vitu viwili ni Pacha!.. vinakwenda pamoja..
Kadhalika Kristo naye analipenda kanisa na sio tu analipenda bali pia analionea wivu. Endapo watu wake aliowapenda wakikengueka na kujitenga naye, basi wivu wake unawaka!, na kuweza kufanya lolote, kama vile mtu aliyesalitiwa na mke wake.
Lakini leo tutajifunza ni kwa namna gani upendo wa Kristo ulivyo na nguvu!.
Hapo biblia inasema “Upendo una nguvu kama mauti”. Maana yake tukiielewa nguvu ya mauti, basi tutaielewa nguvu ya upendo wa Kristo kwetu.
Kama tunavyojua Mtu anayekumbwa na Mauti, anakuwa haishi tena, anakuwa amepotea moja kwa moja, kumbukumbu lake linapotea duniani, hawezi kutenda jambo lolote wala shughuli yoyote ya huu ulimwengu.
Kadhalika mtu anayeingia na kuzama katika pendo la Kristo, ule upendo wa Kristo unamuua na mambo yote ya kidunia.. unamfanya anakufa kwa habari ya dhambi, anapotea kabisa kwenye dira ya mambo ya ulimwengu huu, anakuwa katika umoja na Kristo, ambao hakuna mtu anayeweza kuukaribia.. na hakuna kitu chochote kinachoweza kumtenga yeye na Kristo..
Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. 34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. 35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?”
Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?”
Je na wewe leo umeingia katika pendo la Mwana wa Mungu??..
Kumbuka huwezi kuushinda ulimwengu kama hutakufa kwa habari za uliwengu.
Yohana 15:9 “Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu. 10 Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. 11 Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe”.
Yohana 15:9 “Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu.
10 Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
11 Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe”.
Ni kwanini leo hii huwezi kushinda ulevi?, ni kwasababu pendo la Kristo halijaingia ndani yako, ambalo lingeweza kuua nguvu yote ya ulevi, vile vile kwanini leo huwezi kuacha uzinzi, ukahaba, wizi, uuaji n.k?.. ni kwasababu bado Pendo la Kristo halijamiminwa ndani yako, ambalo lingekufanya ufe kwa habari ya dhambi ndio maana bado ulimwengu una nguvu juu yako.
Lakini habari njema ni kwamba, Kristo mpaka sasa yupo hai na anaokoa!.. utakapompokea kwa kumaanisha kutubu na kuacha dhambi, basi ataingia moyoni mwako, na lile pendo lake litaua kazi zote za ibilisi ndani yako, na kukuacha huru, na hutaona uzito wala ugumu katika kuishi maisha yanayompendeza Mungu. Kumbuka “UPENDO UNA NGUVU KAMA MAUTI”.
Hivyo ukitaka mauti katika kazi zote za ibilisi juu ya maisha yako, zama katika pendo la Kristo. Kwasababu Kristo mwenyewe hawezi kuruhusu wewe usumbuliwe na mambo ya ulimwengu huu!, hivyo lazima aue kazi zote za ibilisi ndani yako..
Kama hujaingia katika pendo hili, basi tubu leo kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako zote, na kisha tafuta ubatizo sahihi, ambao ni ule wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo. Na kwasababu Kristo ni mwenye upendo, atakuingiza katika pendo lake na kukupa uzima wa milele.
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.
NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?
JE UPENDO WAKO UMEPOA?
WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.
Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibu tena tuyatafakari maneno ya uzima.
Kuna wakati Mtume Paulo alifunuliwa siri nyingi sana zimuhusuzo Bwana wetu Yesu Kristo, hususani zile zinazomlinganisha yeye na Melkizedeki. Na hamu yake ilikuwa ni kanisa zima lifahamu siri hizo, lakini alikumbana na kipingamizi kikubwa, ambacho kilimfanya asiweze kuzieleza zote, na kipingamizi chenyewe ni ule UVIVU WA WATU KUSIKIA.
Waebrania 5:10 “kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki. 11 Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia”.
Waebrania 5:10 “kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.
11 Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia”.
Embu tengeneza picha kama Paulo angeendelea, kumwelezea Melkizedeki kama alivyokuwa anamwelezea katika sura hizo chache za kitabu cha waebrania, ungefahamu mangapi ya ziada yamuhusuyo Bwana Yesu, kuliko hayo unayoyajua sasa hivi, Lakini asingeweza kuwaeleza kwasababu hata yale ya mwanzo machache tu, bado watu walikuwa ni wavivu wa kufuatilia..Hivyo kama mwalimu asingeweza kufundisha hesabu za maumbo wakati hesabu kujumlisha na kutoa bado watu hawazijui.
Hata sasa tabia hii, ipo miongoni mwa watakatifu. Ni rahisi kusikia mkristo fulani akisema tena kwa ujasiri, “Aah huu ujumbe ni mrefu siwezi kusoma” lakini wakati huo huo anaweza kumaliza vitabu vitatu vya hadithi, na asione shida. Anaweza kusikiliza mahubiri dakika 10, lakini muvi za kidunia, akakesha nazo usiku kucha.. Anaweza akatumia dakika 2 kutazama video ya ki-Mungu, lakini akatumia saa 6 kuchat Instagramu, na Facebook. Huyo ni mkristo, hatuzungumzii mpagani. Na bado atagemea Mungu atajidhihirisha kwake zaidi ya hicho kiwango anachomjua.
Ndugu, kila siku Bwana anataka tujae maarifa, ili tuweze kuishi kulingana na viwango anavyovitaka yeye kwetu. Mtume Paulo japokuwa alipewa mafunuo makubwa sana yamuhusuyo Mungu, na kule mbinguni, mpaka Mungu akamwekea mwiba maishani mwake ili asijisifu kupita kiasi kwa wingi wa mafunuo hayo (2Wakorintho 12:7).. Lakini bado hakuwa mvivu wa kusoma Neno la Mungu, na kutaka kujua habari za Mungu, Na ndio maana utaona mpaka dakika yake ya mwisho anamwagiza Timotheo ambebee vile vitabu vya ngozi (torati na manabii) ampelekee.
2Timotheo 4:12 “Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso. 13 Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi”.
2Timotheo 4:12 “Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.
13 Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi”.
Sisi tumekuwa kikwazo cha Mungu kujifunua kwetu katika utimilifu wote, Kwasababu ya uvivu wetu wa kusikia/kusoma. Leo hii Bwana atusaidie tuzidishe bidii, kumtafuta Mungu. Ili Bwana ajifunue kwetu zaidi. Bwana Yesu alisema..
Yohana 3:12 “Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni”?
Kumbe alitamani pia kuwaeleza watakatifu wa kipindi kile mambo ya mbinguni, lakini kwa ajili ya uvivu wao wa kutamani kujifunza, hawakuambiwa. Ndugu yangu Leo hii ua TV unazoangalia muda wote, ua huo muda unaokesha Instagramu, na facebook, kutazama video ambazo hazikujengi. Usipokuwa na instagramu, hupungukiwi chochote, si lazima uwe nayo, Muda utakuwa nao mwingi sana na wa kutosha,wa kusikiliza habari za Mungu, na kusoma, kama utaacha mitandao ya kijamii ikupite.
Kumbuka, Mungu anatazamia kile mkristo akue siku baada ya siku.
KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!
Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.
Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika..
BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?