Kwa namna ya kawaida fedha haina ubaya wowote, ni nyezo ambayo Mungu aliiruhusu iwepo na itumiwe ili kuendesha kushughuli zote za kijamii.
Mhubiri 19:19 “…Na fedha huleta jawabu la mambo yote”.
Lakini kitendo cha kupenda fedha, hicho ndicho Mungu amekikatazata, na katika biblia kimekemewa sana, ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu, na roho ya kupenda fedha ipo ndani yako, basi upo hatarini sana, kuzama katika maovu mengi..biblia inasema hivyo..
1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”
Ndio maana biblia inawaasa sana watoto wa Mungu na kuwaambia..
Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”.
Mungu ametoa ahadi ya kuwahudumia watoto wake, kiasi kwamba hawatapungukiwa kabisa, hawatakosa kabisa ikiwa tu watakuwa watulivu katika shughuli zao.
Mtu mwenye tabia ya kupenda fedha ni rahisi kuhonga, ili upate fursa Fulani,ni rahisi kufanya biashara haramu kisa tu ameona zinamwingizia fedha nyingi, mwingine atakuwa radhi hata kujiuza mwili wake kisa fedha, wengine wanakwenda kwa waganga, wengine wapo tayari kuikana imani,..n.k.n.k. hapo ndipo unajua ni kwanini biblia inasema kupenda fedha ni shina la mabaya yote ulimwenguni. Wengine wapo tayari hata kuua watu, ili walipwe au waibe.
Mithali 1:19 “Ndivyo zilivyo njia za kila mwenye tamaa ya mali; Huuondoa uhai wao walio nayo”.
Na dalili mojawapo ambayo biblia inasema itatutambulisha kuwa tunaishi katika siku za mwisho, ni kuibuka kwa wimbi kubwa la watu wanaopenda fedha.
2Timotheo 3:1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,”
2Timotheo 3:1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.
2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,”
Mpaka sasa, imefikia hatua huduma za rohoni kutolewa kwa fedha,
1Timotheo 6: 5 “na majadiliano ya watu walioharibika akili zao, walioikosa kweli, huku wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida”.
Hiyo yote ni matokeo ya wanadamu kupenda fedha..Bwana Yesu alisema..
Mathayo 6:24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali”.
Shetani alijua hapa ndipo wanadamu wengi wanapoweza kunaswa, hivyo, akatumia njia hiyo hiyo kumjaribia pia Yesu, akamwambia nitakupa milki zote za ulimwenguni, nitakupa fedha zote na majumba yote ikiwa utanisujudia tu. Lakini Bwana Yesu alimkemea akamwambia utamsujudia Bwana Mungu wako tu.. Kwasababu alijua kupenda fedha ni kuupenda ulimwengu.
1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake”.
Kama hiyo haitoshi Wenye mali, bado biblia inawapa nafasi ndogo sana ya kuurithi ufalme wa mbinguni;
Mathayo 19:23 “Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni. 24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”.
Mathayo 19:23 “Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.
24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”.
Vifungu vipo vingi sana kwenye biblia vinavyozungumzia hatari za kupenda fedha., hatuwezi kuviweka vyote hapa, lakini kwa hivyo vichache kama na wewe ni mmojawapo, basi geuka haraka sana, uridhike na vile Mungu anavyokupa, kwasababu biblia inasema..
Mhubiri 5:10 “Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili”.
Na pia inasema.
Zaburi 37:16 “Kidogo alicho nacho mwenye haki ni bora Kuliko wingi wa mali wa wasio haki wengi”.
Chuma kidogo kidogo utafanikiwa..
Mithali 13:11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”.
Lakini kama wewe hujaokoka, ukweli ni kwamba hii roho ya kupenda fedha haiwezi kuondoka ndani yako, hata iweje, itaondoka, ikiwa tu utamruhusu Bwana Yesu aingie ndani yako aibadilishe Nia yako..
Akishakubadilisha hapo ndipo Roho ya kuridhika na ya utulivu itaingia ndani yako, na hapo hapo Mungu ataanza kukufundisha njia sahihi na yenye Baraka ya kukusanya..mpaka mwisho wa siku atakufikisha pale anapotaka uwepo. Na zaidi ya yote utaurithi uzima wa milele.
Hivyo kama upo tayari leo hii kutubu dhambi zako, unahitaji kuokoka, uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana basi, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
YONA: Mlango 1
UNYAKUO.
UTAWALA WA MIAKA 1000.
EPUKA MUHURI WA SHETANI
Rudi Nyumbani:
Print this post
Luka 16:16 “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.
Nataka uone hicho kifungu cha mwisho, “ Na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”..
Bwana Yesu alipotoa habari hiyo, kulikuwa na sababu kubwa kwanini alianza kwanza na habari za agano la kale(Torati na manabii) kisha akaja kwenye agano jipya, na kumalizia kwa kusema, tangu huo wakati kila mtu atakawa anajiingiza kwa nguvu.
Alisema hivyo kuonesha kuwa hapo kabla, kulikuwa hakuhitaji bidii yoyote, au jasho lolote, au nguvu yoyote, kuijua torati, lakini kuanzia wakati wa Yohana, injili ya kweli ambayo inaleta ondoleo la dhambi, ilipoanza kuhubiriwa, injili ya kumfanya mtu awe na maarifa kamili kumuhusu Mungu ilipoanza kuhubiri, injili inayomfungua mtu kweli kweli, basi vipingamizi vikubwa sana vitanyanyuka kiasi kwamba, mpaka mtu aipate ni lazima atumie nguvu nyingi sana kuingia, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo.
Kwamfano utaona wakati ule tu, kulikuwa na mafarisayo na waandishi, ambao wamesimama hapo, katikati kuhakikisha kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu hadharani, moja kwa moja atatengwa na sinagogi, (Yohana 9:22)
Na kutengwa kwa zamani sio kama sasa, zamani ukitengwa na sinagogi ni jamii nzima ya Israeli imekutenga mpaka familia yako. Hata misaada ya kijamii ulikuwa hupati, Hivyo suala la kutengwa lilikuwa ni jambo zito sana.
Hivyo haikuwa ni rahisi, hata kidogo, ilibidi watu walazimishe, mambo kwa nguvu, wawe radhi kutengwa tu, wawe tayari kupoteza mahusiano yao tu, lakini wasiukose ufalme wa mbinguni.
Mambo hayo hayo hata sasa, yanaendelea, kuupata ufalme wa mbinguni, ni kujiingiza kwa nguvu nyingi, wapo viongozi wako wa dini wanakuzuia usiokoke, kisa tu imani yao haimini kile biblia inachosema, pengine Imani yao inafundisha kusujudia sanamu, haiamini katika karama za Roho, ndugu usiwaangalie hao, wewe jiingize kwa nguvu katika ufalme wa Mungu,.
Hao ni wale wana-sheria wa dini, ambao Bwana Yesu anasema, kazi yao ni kusimama pale mlango kushikilia funguo, kuwazuia watu wasiingie, na wao wenyewe hawauingii, wanataka mkae wote katika giza la milele pamoja..
Luka 11:52 “Ole wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa maarifa; wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia”.
Hivyo usiwaangalie hao hata kidogo, achana na mapokeo ya dini, tubu dhambi uokoke, tafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, na sio ule wa kunyunyiziwa ambao haupo katika maandiko.
Jiingize kwa nguvu, hata kama ndugu zako hawakuelewi, Jiingize kwa nguvu hata kama marafiki zako watakuona mshamba, jipenyeze kwa nguvu hata kama dunia itakuona umerukwa na akili..Iokoe roho yako, wakati huu jiepushe na mtu ambaye unaona kabisa anaizuia njia yako ya wokovu.
Wenyewe hawawezi kuona hilo, kwasababu bado wapo gizani, lakini wewe umeiona nuru, usijifananishe na wao, zidi jenga uhusiano wako binafsi ya Yesu. Hizi ni nyakati za mwisho na unyakuo upo karibu sana,
Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka. 13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana”.
Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana”.
Isiishi kwa kuwapendezesha watu na huku umelisahau Neno, kwasababu kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe (Wagalatia 6:5). Dakika hizi za majeruhi, zinafananishwa na Sodoma na Gomora, ambazo tunajua ni watu 3 tu kati ya mamilioni waliokuwa katika miji ile ndio waliopona….Ndivyo itakavyokuwa siku hizi, litavuka kundi dogo tu, lililoweza kujiingiza kwa nguvu katika ufalme wa mbinguni bila kujali vizuizi vya mpito vya ibilisi.
Unadhani shetani, hajui kuwa mtu akiupata ufalme wa Mungu, amepata kitu cha thamani kubwa sana, anajua hilo, na ndio maana lazima akuletee ugumu ili usijaribu kuuingia, ubakie kwenye giza huko huko..Hivyo vitisho kutoka kwa viongozi wako wa dini na ndugu na marafiki, visikufanye usichukue uamuzi wa kumpokea Yesu.
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga. 35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu; 36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake. 37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. 38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. 39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.
Kama bado hujafanya uamuzi huo basi anza sasahivi, wokovu unapatikana bure, lakini si rahisi si rahisi lakini inahitaji nguvu kujiingiza kwa huo, hivyo jiingize kwa nguvu bila kujali, na huko huko Bwana Yesu atajifunua kwako kwa namna ambayo hukuwahi kumjua hapo kabla, ndipo utakapomjua Mungu, na ndipo atakapotembea na wewe.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
USIUZE URITHI WAKO.
Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?
KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.
JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.
MWANANCHI WA UFALME WA MBINGUNI
USIISHI BILA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KABISA..
WhatsApp
Jukumu moja na kuu tulilonalo sisi ni KUMJUA SANA YESU KRISTO. Wengi wanalikwepa jukumu hili. Na Zaidi wanapenda sana kutafuta kuwajua watumishi wa Yesu kuliko ya Yesu mwenyewe.
Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”.
Jitathmini ukiona kuna mahali unamjua mtumishi, zaidi ya Bwana wake mwenyewe ambaye ni Yesu, basi kuna tatizo mahali na pia una laana.(1Wakorintho 16:22)
Kama mtumishi wa Kristo akizungumziwa vibaya inakuuma Zaidi ya Yesu akifanyiwa mzaha, basi kuna tatizo katika uhusiano wako na Yesu.
Kama comedy za kumtania Mwokozi Yesu hazikuhuzunishi sana kama za kumtania mchungaji wako, au mwalimu wako, basi kuna tatizo mahali.
Kama unakuwa mkali dini yako inapozungumziwa vibaya, au dhehebu lako au mwalimu wako anayekufundisha Neno la Mungu kanisani, na wakati huo huo unakutana na comedy inayomkebehi Kristo waziwazi na wala haikuhumizi sana Zaidi inakuchekesha!, hebu jitafakari tena, inawezekana humjui kabisa Yesu, wala hayupo maishani mwako.
Kama Maisha yako ya binafsi ya siri, hujawahi kukaa ukazungumza na mwokozi wala kumshukuru, basi kuna shida.
Dada/kaka usitumie nguvu nyingi kutafuta kumpendeza mtumishi, wala usiwe mshabiki wa dini, wala usiwe mshabiki wa mtumishi wa Mungu.
Tafuta kumjua Yesu, na kumjua Yesu sio kuhama na kubadilisha kanisa…Ni hapo hapo ulipo tu!..Unachopaswa kukifanya baada ya kumpokea Kristo ni kukinunua kitabu kinachoitwa Biblia. Usitegemee ile ya ku-download kwenye simu yako.. Ya kudownload ni nzuri baada ya kuwa na ya KITABU chenye kurasa za karatasi.
Hivyo kinunue hichi kitabu kinachoitwa Biblia. Ukishakipata! Anza kukisoma mwenyewe!..Mungu kakupa macho, kakupa na uwezo wa kusoma, hawezi kukunyima uwezo wa kuelewa!..
Kinachosababisha wengi wasiielewe biblia ni kusoma kwa kutimiza wajibu tu!..na sio kwa kutoka ndani ya mioyo yao, wanasoma tu kwasababu wameambiwa wasome, au kwasababu tu wanahisi ndio wanampendeza Mungu, na anasoma kwa mwezi mara moja…Hivyo biblia inakuwa ni kitabu kigumu sana kwao kukielewa. Na pia wanasoma mstari mmoja kisha wanarukia mwingine…Hawapendi kusoma mwanzo wa kitabu hadi mwisho.
Hivyo soma biblia mwenyewe kwa macho yako mawili. Ukikutana na jambo gumu kuna nguvu Fulani ya asili ambayo Mungu kaiweka ndani yetu itakayokupeleka katika kuutafuta ukweli Zaidi, hapo ndipo kitakuja kitu cha kutafuta msaada Zaidi kwa mahubiri ya watumishi wa Mungu, utaona kuna kitu kinakusukuma kwenda sehemu Fulani labda kanisa Fulani, au kwenye semina Fulani, au katika mahubiri Fulani.. ambapo utaona utapata majibu ya maswali yako, au utakwenda kusoma jumbe Fulani ambazo utaona zitakufaidisha roho yako. Na kwa njia hiyo ndipo mafunuo ya Roho yanapokuja.
Lakini huwezi kusema naondoka kanisa hili nahamia lile kama hujapata sababu yoyote ya kimaandiko ya kufanya hivyo.. Wengi wanahama kanisa kwasababu tu wameambiwa ukweli..hivyo ule ukweli unawauma na kuishia kuhama, wengine kwasababu wamesikia wakisengenywa, wengine kwasababu wameona kanisani kumepungua watu hivyo na wao wanaondoka…mambo ambayo hayana mashiko kabisa!..Mtu wa namna hiyo hajaongozwa na Mungu, bali kafuata akili zake mwenyewe.
Lakini mtu wa kweli ambaye anaongozwa na Roho, huwa anaondoka sehemu moja hadi nyingine, ni kwasababu anatafuta uelewa wa maandiko Zaidi, anatamani kumjua Yesu zaidi na kukua kiroho.. huyo ndiye anayeongozwa na Roho. Anaona kuna umuhimu wa kutafuta kujifunza Neno Zaidi, kutafuta kufunga Zaidi na kusali. Na si kwasababu kasikia kasengenywa, au kasemwa, au kaudhiwa.
Hivyo siku zote usilisahau hili ndugu yangu mpendwa.. MJUE SANA YESU. Huyo ndio ndiye Mkuu wa Uzima, na ndiye mwenye funguo za Uzima, na ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na Duniani..Tunavyozungumza sasa yupo anaishi! Na atarudi tena kulichukua kanisa lake, Ana nguvu nyingi sana, yeye hadhihakiwi sio yule unayemwona kwenye picha, sio unayemwona kwenye Tv, Yesu ni Mungu, akijifunua kwetu kikamilifu, hata hapa duniani tunaweza tusitamani kuendelea kuishi, Hivyo tumjue yeye kila siku, tujinyenyekeze mbele zake, ajifunue kwetu zaidi na zaidi. Anatamani kujifunua kwetu sana, ni sisi tu.
Bwana atubariki sana.
JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?
Kuna haja gani ya kumwamini Yesu aliyezaliwa kama sisi?
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.
MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.
RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.
Isaya 24:3 “Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo. 4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika. 5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele. 6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.
Isaya 24:3 “Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo.
4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.
5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele.
6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.
Nabii Isaya alipotabiri juu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo na bikira (Isaya 7:14), miaka 700 kabla ya Masihi kuja duniani, wapo watu pengine walioona kuwa hizo ni hadithi tu za kufikirikika… Alipotabiri tena juu ya mateso yake yatakayoompata (Isaya 53), nazo pia zikaonekana pengine ni habari tu, lakini wakati ulipofika, hayo yote kutimia kwa ufasaha wote, ndipo wakajua kuwa Neno la Mungu huwa halipiti.
Isaya huyo huyo aliyetabiri ujio wa Kristo kwa uvuvio wa Roho, ni huyu huyu alioonyeshwa pia hatma ya huu ulimwengu utakavyokuja kuwa siku za mwisho, na habari zake kaziandika sehemu nyingi sana kwenye kitabu hicho chenye sura 66, alionyeshwa jinsi hii dunia itakavyokwenda kuwa utupu, na kuharibiwa kabisa, jinsi jua litakavyotiwa giza, jinsi watu watakavyoadimika kama dhahabu duniani, na kibaya zaidi alionyeshwa fedha ya mtu wakati huo haitafanya kazi yoyote, umaarufu wa mtu utakuwa hauna maana, biashara za mtu zitakuwa ni kama takatakata, elimu ya mtu haitafanya kazi..tajiri na maskini wote watakuwa wakiomboleza sawa.
Na nyakati zenyewe ndio hizi tunazoishi mimi na wewe, kila mtu analijua hilo, hata ukimuuliza mtoto mdogo atakuambia, hizi ni nyakati za mwisho, watu wengi wanaposikia maneno haya wanapuuzia wakidhani hichi ni kama kile kipindi cha mitume..Ndugu hichi sio kipindi cha mitume.. Fuatilia mambo yanayoendelea duniani hata kupitia mitandao ndipo utakapojua kuwa tunaishi nyakati nyingine.
Bwana Yesu alisema hivi..
“Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu; 33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni. 34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia” (Mathayo 24:32).
“Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;
33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.
34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia” (Mathayo 24:32).
Sasa kama wewe ni msomaji wa Biblia utajua kuwa Mtini unafananishwa na Taifa la Israeli (Yeremia 24), na wakati ule Israeli ilikuwa bado haijachipua (yaani haijawa taifa), ilipitia miaka zaidi ya 2,500 tangu wachukuliwe utumwani Babiloni, na ulipofika mwaka 1948, Israeli ikachipuka tena na kuwa taifa kwa mara ya kwanza,..Na tunajua kabisa agenda ya Mungu ya wokovu itamalizia tena na Israeli pale Yerusalemu.
Hivyo tangu huo wakati Bwana alisema kizazi hiko, (yaani kilichoshuhudia Israeli kuchupuka tena), hakitapita mpaka hayo yote, kutimia,..Mambo yote aliyoyazungumzia katika Mathayo 24, hadi kurudi kwa pili kwake,..Na kizazi huwa hakizidigi miaka 120, sasa piga hesabu hapo, tunaishi katika wakati gani.. (Hatujui siku wala saa lakini tunayajua majira).
Sikuzote, kiwango chako cha maarifa kuhusu Mungu, ndio kinachoelezea maisha ya kiroho unayoishi sasa hivi, kama jicho lako bado halioni kuwa tunaishi katika majira ya unyakuo, na kwamba huu ndio ule wakati ambapo watu watadhanishia mbona ni amani, na salama, na kumbe ule uharibifu unakuja kwa ghafla (1Wathesalonike 5:3)..Kama ilivyokuja Corona kwa ghafulani pasipo ulimwengu kujiandaa…Ndicho kitakachoitokea dunia kipindi sio kirefu.
Sijui kama hilo unalijua ndugu yangu, kanisa hili linaitwa Laodikia, (Sio dhehebu linaloitwa Laodikia! Hapana!..Bali ni hali ya kanisa kwa ujumla inayofananishwa na Kanisa la Laodikia la Nyakati za kwanza, kasome Ufunuo 3:14), na ndio kanisa la mwisho la 7, na hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hili, niambie ni dalili ipi ambayo haijatimia Yesu aliyoirodhesha kwenye Mathayo 24.
Internet imeweza kurahisisha mambo, siku hizi haihitaji mtu aende tena kwenye mikutano ya Injili asikie mahubiri, pale pale alipo hata kama ni kijijini akiwa chumbani mwake Injili inamfikia, utasema Injili haijahubiriwa dunia nzima leo?..
Shetani anataka watu waendelee kufikiria hivyo hivyo, kwamba bado sana, anataka watu waangalie upepo wa dunia unavyokwenda, lakini wasiangalie biblia inasema nini kuhusu siku hizi. Usipokuwa mvivu kusoma biblia ndipo utakapojua ni kwa jinsi gani tunaishi katika nyakati za hatari kushinda zote ambazo zilishawahi kupita katika historia.
Hivyo huu ni wakati wa kuamka usingizini..
Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza”.
Kama bado hujaokoka, au umeokoka lakini bado mguu mmoja nje mwingine ndani, Embu anza, kuyaangalia upya maisha yako ya rohoni ndugu, Je! Yesu amekuokoa kweli kweli? Kama sio, basi huu ndio wakati, na sio kesho, unachopaswa kufanya ni kuamua kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha na kutozifanya tena, na kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 3:38,8:16 na 10:48 Upate ondoleo la dhambi zako.(Maagizo hayo ni muhimu sana!). Na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.
Na kuanzia hapo, anza kuishi maisha ya kama mtu unayemngojea Bwana Yesu kwasababu nyakati hizi, sio za kubembeelezewa wokovu tena, ni kubutuka haraka na kuishindania Imani.
KUOTA UNAKOJOA KITANDANI.
MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.
NI WAKATI WA KUJIPIMA, WEWE KAMA MTUMISHI WA MUNGU!
NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME
MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.
MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe!.
Karibu tujifunze Biblia.
Ndege tunazozipanda zinazoruka angani, hazijaundwa na mtu mmoja, kuna jopo kubwa sana la watu wamechangia maarifa katika kuiunda ile.. Utaona aliyegundua injini ya ndege ni mwingine, aliyegundua mfumo wa hewa ndani ya ndege ni mwingine, aliyebuni umbile na mwonekano wa ndege ni mwingine, aliyegundua sayansi ya kuifanya iruke ni mwingine, aliyegundua mfumo wa umeme ndani ya ndege ni mwingine, aliyegundua Mafuta ya ndege ni mwingine, aliyegundua kona ya ndege ni mwingine, aliyebuni matairi ya ndege ni mwingine n.k.
Sasa hao wote kila mmoja akiandika kitabu chake kidogo cha maelezo kuhusu mchango wake huo na vitabu hivyo vikakusanywa Pamoja bila shaka tunaweza kujikuta tuna kitabu kimoja kikubwa kama Biblia au hata Zaidi ya biblia, kilichojaa elimu kuhusu ndege. Maana yake ni kwamba mtu atakayejifunza hicho na kukielewa anaweza naye pia kutengeneza ndege yake.
Hivyo basi kama ilikuwa ni mpango wa Mungu kwamba wanadamu siku moja waruke angani, waende mbali sana kule juu Zaidi ya Tai..kumbe mpango wake haukuwa wa kumpa mtu mmoja maarifa hayo, bali aligawanya ujuzi huo kwa watu tofauti tofauti wanaojulikana kama wanasayansi..ambao katika hao kila mmoja alipochangia ujuzi wake na uvumbuzi wake ndipo kitkapoumbwa kitu kinachoitwa Ndege.
Kama ulikuwa ni mpango wa Mungu siku moja tusafiri kutoka bara moja hadi lingine kwa muda mfupi kwa kutumia ndege, na tena kama ulikuwa ni mpango wa Mungu siku moja turuke mbali sana Zaidi ya mawingi hata kuufikia mwezi kwa kutumia roketi…Basi pia upo mpango mwingine wa Mungu ulio mkubwa Zaidi ya huo, ambao utatufanya tupae Zaidi ya mawingu na mwezi na Zaidi ya nyota… Na huo si mwingine Zaidi ya ule wa kutupeleka mbinguni yeye alipo.
Na kama vile maarifa ya uvumbuzi wa kifaa kinachoitwa ndege au roketi, yalivyogawanyika katikati ya watu tofauti tofauti, vivyo hivyo maarifa ya kwenda mbinguni wamefunuliwa Mitume na Manabii mbalimbali wa kwenye biblia…Wakina Yeremia, Danieli, Musa, Ezekieli,…Wakina Petro, Paulo, Yohana n.k Hao kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu kila mmoja kaandika siri za ufalme wa Mbinguni kwa jinsi alivyojaliwa…ambazo sisi kama wakristo, tunajifunza leo katika kitabu kinachoitwa biblia, na kama tukifuzu kukielewa vyema basi tunaweza kupaa juu Zaidi ya yale mawingu. Tunaweza kutengeneza roketi na kuingia ndani yake na kuruka Zaidi ya yale mawingu, na ndege yetu hiyo au Roketi ni YESU KRISTO.
Yesu ndiye NJIA, KWELI na UZIMA…Mtu hawezi kufika kwa Baba mbinguni isipokuwa kwa Njia yake yeye (Soma Yohana 14:6).
Teknolojia inahubiri injili, ukiona wakati tunaoishi inawezekana kusafiri hewani, basi jua kuna safari kubwa kuliko zote inakaribia. Lakini hayo yote hayaji pasipo maarifa.
Ndugu dada/kaka usiache kusomana kujifunza kamwe biblia, Hakuna sehemu yoyote utaweza kupata maarifa ya kumjua Yesu nje ya biblia. Usiposoma biblia kwa kujifunza utachukuliwa na kila aina ya upepo wa uongo.
Usipende kusubiria tu kufundishwa biblia, Jifunze kuisoma mwenyewe!.. Hata mwanafunzi anayefanikiwa masomoni ni yule kwanza anayependa kujisomea mwenyewe…Na anapokutana na maswali magumu ndipo anapokwenda kuuliza kwa mwalimu wake!..Lakini mwanafunzi anayependa kufundishwa tu! Na wala hana muda wa kujisomea yeye mwenyewe..kamwe hawezi kufanya vizuri..Na ndivyo hivyo hata sisi, Mungu anataka tuisome biblia wenyewe!.
Kumbuka pia hajayarekodi maneno yake kwa njia ya Audio, kayaweka kwenye kitabu…Ukiona kitu kimewekwa kwenye kitabu maana yake anayekisoma anahitaji kuketi chini mahali pasipo na usumbufu, akiwa na kalamu yake na daftari..Biblia hatuisomi kama gazeti, tunajifunza na ndivyo Roho Mtakatifu anataka tuwe hivyo ili aweze kutufunulia siri zake..
Je unataka kwenda mbinguni?..Mimi nataka sijui wewe?..kama wewe nawe unataka basi Ni lazima tuifahamu biblia sana.
Bwana akubariki
Maran atha!
WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.
ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.
MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.
USIRUHUSU MUNGU AWEKE UADUI KATI YAKO NA WATU WAKO.
Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?
Bawabu (kwa kiingereza -Doorkeeper/Porter) ni nani katika biblia?
Bawabu maana yake ni msimamzi wa mlangoni, anayefunga na kufungua, na anayeruhusu na kutoruhusu mtu au vitu kuingia, Hawa wanakuwa hususani katika mageti ya kuingilia miji mikubwa na kwenye majumba ya kifalme na mahekalu,
2Samweli 18:26 Kisha huyo mlinzi akaona mtu mwingine anapiga mbio; mlinzi akamwita bawabu, akasema, Angalia, mtu mwingine anakuja mbio peke yake. Mfalme akasema, Huyu naye analeta habari.
Soma pia 2Wafalme 7:10,11
1Nyakati 9:23 “Basi watu hao na wana wao walikuwa na usimamizi wa malango ya nyumba ya Bwana, yaani, nyumba ya maskani, kwa zamu…. 27 Nao wakalala kandokando nyumbani mwa Mungu, kwa kuwa ulinzi wake ulikuwa juu yao, nayo ilikuwa kazi yao kuyafungua malango asubuhi baada ya asubuhi.”.
1Nyakati 9:23 “Basi watu hao na wana wao walikuwa na usimamizi wa malango ya nyumba ya Bwana, yaani, nyumba ya maskani, kwa zamu….
27 Nao wakalala kandokando nyumbani mwa Mungu, kwa kuwa ulinzi wake ulikuwa juu yao, nayo ilikuwa kazi yao kuyafungua malango asubuhi baada ya asubuhi.”.
Kazi hii ni kazi iliyokuwa inaonekana kama nyonge kuliko kazi zote kwenye utumishi wa Majumbani au kwenye ulinzi, hata sasa ndivyo zinavyoonekana..
Lakini Daudi alisema..
Zaburi 84:10 “Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu”.
Daudi alitumia kazi yenye cheo cha chini kabisa, katika jumba kubwa akasema kama na kwa Mungu ipo hivyo, basi angependelea walau apate hata kazi hiyo ndogo tu, maadamu ni ya Mungu, kuliko kupata cheo kikubwa na kibali katika mambo ya kidunia.
Akasema tena siku moja nyuani kwa Bwana ni bora kuliko siku elfu penginepo..
Alijua faida ya kazi ya Mungu, hata kama ni ndogo kiasi gani, alijua akipoteza siku moja kuitenda kazi ya Mungu ni sawa zaidi ya siku elfu kujisumbua na shughuli nyingine za kidunia..Firikia siku elfu ni karibia na miaka 3, Hivyo miaka 3 yako wewe kwenye masumbufu yako ni siku moja kwa mtu anayedeki choo cha kanisa.
Hivyo na wewe jiulize kazi yako ni nini kwenye nyumba ya Mungu? Mchango wako wa kusambaza kazi ya Mungu ni ipi? Nguvu zako za kifedha unazimalizia wapi ndugug? Au kwako kazi ya Mungu haina faida yoyote..
Daudi anasema ni heri “Ni heri niwe bawabu nyumbani mwa Mungu..”
Shalom.
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara katika email yako au Whatsapp yako basi tutumie ujumbe kwenye namba hii :+255 789001312
Bwana alimaanisha nini kusema JIKANE mwenyewe?(Mathayo 6:24)
JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?
Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?
Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?
MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.
Behewa kwa jina lingine ni UA, ni eneo la wazi lililokuwa limezungushiwa fensi mbele ya Hema ya kukutania , kwa ajili ya makuhani kutoa sadaka za kuteketezwa, na kufanya shughuli za kikuhani tazama picha juu..
Lakini baadaye Hekalu lilipokuja kutengenezwa na Sulemani pale Yerusalemu, eneo la behewa/Ua lilizungushiwa ukuta, na pakawa na behewa kuu mbili, 1) ya ndani 2) na ya nje, ili ya ndani ikabakia kuwa ya makuhani tu, kufanya mambo ya upatanisho na sadaka za kuteketezwa, Na ile ya nje ikabakia kuwa ya Wayahudi wote kukutanika kuabudu..Tazama picha chini..
Lakini pia behewa, kwenye biblia haikumaanisha tu ni lazima iwe mbele ya hema ya kukutania au mbele ya Hekalu la Mungu, biblia inayonyesha pia, zilikuwa pia kwenye majumba ya kifalme na ya kikuhani.
1Wafalme 7:1 “Naye Sulemani alikuwa katika kuijenga nyumba yake mwenyewe miaka kumi na mitatu, akaimaliza nyumba yake yote….11 Na juu kulikuwa na mawe ya thamani, mawe ya kuchongwa, sawasawa na cheo, na mierezi.12 Na behewa kubwa pande zote ilikuwa na safu tatu za mawe ya kuchongwa, na safu moja ya mihimili ya mierezi; mfano wa behewa ya ndani ya nyumba ya Bwana, na ukumbi wa nyumba”.
1Wafalme 7:1 “Naye Sulemani alikuwa katika kuijenga nyumba yake mwenyewe miaka kumi na mitatu, akaimaliza nyumba yake yote….11 Na juu kulikuwa na mawe ya thamani, mawe ya kuchongwa, sawasawa na cheo, na mierezi.
12 Na behewa kubwa pande zote ilikuwa na safu tatu za mawe ya kuchongwa, na safu moja ya mihimili ya mierezi; mfano wa behewa ya ndani ya nyumba ya Bwana, na ukumbi wa nyumba”.
Mathayo 16:3 “Wakati ule wakuu wa makuhani, na wazee wa watu, wakakusanyika katika behewa ya Kuhani Mkuu, jina lake Kayafa”;
Lakini pia katika kitabu cha ufunuo tunasoma, kuwa wakati wa mwisho, behewa/ua iliyo nje ya hekalu ambalo litakuja kujengwa na Wayahudi pale Yerusalemu siku za mwisho, litamilikiwa na watu wa mataifa kwa muda wa miezi 42..
Ufunuo 11:1 “Nikapewa mwanzi kama fimbo; na mmoja akaniambia, Inuka, ukalipime hekalu la Mungu, na madhabahu, na hao wasujuduo humo.2 Na behewa iliyo nje ya hekalu uiache nje wala usiipime, kwa maana Mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili”.
Ufunuo 11:1 “Nikapewa mwanzi kama fimbo; na mmoja akaniambia, Inuka, ukalipime hekalu la Mungu, na madhabahu, na hao wasujuduo humo.
2 Na behewa iliyo nje ya hekalu uiache nje wala usiipime, kwa maana Mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili”.
Ili kufahamu habari kamili, sababu na maana yake rohoni ya mambo hayo fungua vichwa vingine vya masomo tulivyovirodhesha chini.
Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye namba hizi: +255789001312/ +255693036618
Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo
Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?
NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA
Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?
Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.
Kuna wakati ulifika Nabii Nahumu alifunuliwa juu ya hatma ya mji mmoja ulioitwa Ninawi, Mji huu ndio uliokuwa mji mkuu waTaifa la Ashuru, ulikuwa mji wa kwanza kwa ukubwa kuliko mji yote iliyokuwa ulimwengu kwa wakati ule. Baadaye ndio ikaja kutokea miji mwingine ulioitwa Babeli ..Sasa katika mambo aliyoongozwa Nabii Nahumu kuandika ni pamoja na uvumilivu wa hasira ya Mungu, pamoja na ukali wa hasira ya Mungu. Maneno hayo utayaona mwanzoni kabisa mwa kitabu cha Nahumu..
Nahumu 1:1 “Ufunuo juu ya Ninawi. Kitabu cha maono aliyoyaona Nahumu…. 2 Bwana ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; Bwana hujilipiza kisasi, NAYE NI MWINGI WA HASIRA; Bwana hujilipiza kisasi juu ya adui zake, huwawekea adui zake akiba ya hasira. 3 BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, ana uweza mwingi….”
Nahumu 1:1 “Ufunuo juu ya Ninawi. Kitabu cha maono aliyoyaona Nahumu….
2 Bwana ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; Bwana hujilipiza kisasi, NAYE NI MWINGI WA HASIRA; Bwana hujilipiza kisasi juu ya adui zake, huwawekea adui zake akiba ya hasira.
3 BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, ana uweza mwingi….”
Unaona, sasa unaweza ukajiuliza ni kwanini Mungu azungumze maneno hayo mawili kwa wakati mmoja?
Utakumbuka kuwa mji huu wa Ninawi ndio ule mji ambao Nabii Yona alitumwa kwenda kuwahubiria juu ya dhambi zao kwamba watubu..Kama tunavyoijua ile habari, watu wale walisikia injili ya Yona, na walipotubu Mungu aliwarehemu japokuwa walikuwa sio wakamilifu ipasavyo.. hiyo ilimfanya mpaka Yona amkasirikie Mungu kwanini hajawaangamiza wale watu waovu..Ndipo Mungu akamwambia Yona maneno yafuatayo;
Yona 4:11 “na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi ya mia na ishirini elfu, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufugwa wengi sana?”
Unaona huruma za Mungu jinsi zilivyokuwa nyingi?.. Japokuwa walikuwa ni waabudu miungu, wapagani, lakini Mungu aliwahurumia tu pale walipotubu dhambi zao na kugeuka…Lakini tunavyozidi kusoma biblia tunaona, mambo hayakuwa hivyo siku zote ulifika wakati mji huo wa Ninawi ulirudia mambo yale yale ya kale, uovu ukaendelea kama ulivyokuwa pale mwanzo kipindi Yona anatumwa, wakasahau kuwa walinusurika kuwa jivu mfano wa Sodoma na Gomora.
Matokeo yake ndio tunakuja kuona Nabii Nahumu akitokea na kutoa unabii juu ya mwisho wa Taifa hilo..Pengine wakati Nahumu anatoa unabii huu waliona kama ni utani tu, kwamba watatubu tu kama kipindi kile cha Yona?..Wakawa wanasema tunajua Mungu siku zote si mwepesi wa hasira, Mungu ni wa rehema, anaghahiri mabaya..Hata hivyo hawezi kuliangamiza Taifa kubwa kama hili duniani (Ashuru) na mji wetu huu Ninawi ulio msaada wa mataifa mengi ulimwenguni.
Ndivyo walivyodhania, wakapumbazwa, wakajisahau kabisa, tena na jinsi walivyoona wamefanikiwa kuwachukua wayahudi utumwani, (yale makabila 10), ndio wakadhani kuwa Mungu amewapendelea..
Lakini Nabii Nahumu akatoa unabii juu ya mji huo..akisema.
Nahumu 3:7 “Hata itakuwa, wote wakutazamao watakukimbia, wakisema, Ninawi umeharibika; ni nani atakayeuhurumia? Nikutafutie wapi wafariji”?
Hayo maneno aliyoyasema nabii Nahumu yalikuja kutimia kama yalivyo, ni kwa vile tu, biblia haiwezi kuandika kila kitu, na kila historia, kama ingekuwa ni hivyo vitabu visingetosha duniani vya biblia. Lakini historia ipo wazi kabisa inaonyesha, ulipofika mwaka wa 612 KK, Wababiloni pamoja na wamedi waliunganisha nguvu, na kuizunguka Ninawi mji mkuu wa Ashuru, na kuuteka na kuungamiza, na hapo ndipo ikawa mwisho wa Taifa linaloitwa ashuru na mji wa Ninawi mpaka leo hii tunavyozungumza ni miaka zaidi ya 2,500, ni vipande vya mawe tu vimesimama pale kaskazini mwa Iraq. Na taifa la Babeli ndipo lilipopatia nguvu hapo, ambalo nalo baadaye lilikuja kuangamizwa hivyo hivyo.
Nahumu 3:19 “Jeraha yako haipunguziki; jeraha yako ni nzito sana; wote wasikiao habari zako wapiga makofi juu yako; kwa maana ni nani ambaye uovu wako haukupita juu yake daima”?
Biblia inasema Ninawi ni mji uliokuwa umekaa pasipo kufiri, upo upo tu, ukidhani wenyewe ndio wenyewe, ulipokuwa unashinda vita vingi, na unafanikiwa kuchukua mateka mataifa mengi, lakini siku yao ilipofika, yalikuwa ni majuto yasiyoelezeka..
Sefania 2:13 “Naye atanyosha mkono wake juu ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza Ashuru; naye ataufanya Ninawi kuwa ukiwa, kuwa mahali pakavu kama jangwa….. 15 HUU NDIO MJI ULE WA FURAHA, ULIOKAA PASIPO KUFIKIRI, ULIOSEMA MOYONI MWAKE, MIMI NIKO, Wala hapana mwingine ila mimi. Jinsi ulivyokuwa ukiwa, Mahali pa kulala pa wanyama wa bara! Kila mtu apitaye atazomea, Na kutikisa mkono wake”.
Sefania 2:13 “Naye atanyosha mkono wake juu ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza Ashuru; naye ataufanya Ninawi kuwa ukiwa, kuwa mahali pakavu kama jangwa…..
15 HUU NDIO MJI ULE WA FURAHA, ULIOKAA PASIPO KUFIKIRI, ULIOSEMA MOYONI MWAKE, MIMI NIKO, Wala hapana mwingine ila mimi. Jinsi ulivyokuwa ukiwa, Mahali pa kulala pa wanyama wa bara! Kila mtu apitaye atazomea, Na kutikisa mkono wake”.
Ezekieli 32:22 “Ashuru yuko huko, na watu wake wote jamii; makaburi yake yamzunguka; wote pia wameuawa, wameanguka kwa upanga”
Ni nini Bwana anataka tujue?
Hiyo ni kuonyesha kuwa japokuwa Mungu si mwepesi wa Hasira, lakini hasira yake inapofika kilele basi ni MWINGI WA HASIRA..yaani haipoi kwa haraka, inadumu milele kama sio kwa kipindi kirefu sana..
Na ndio maana leo hii watu wengi wanaposoma yale mapigo yaliyoandikwa kwenye kitabu cha ufunuo wanaona kama hayafikirikiki kwa akili za kibinadamu, ni kweli unaweza kudhani hivyo lakini ndugu yale mapigo unavyoyaona pale ndivyo yatakavyokuwa.. Ziwa la moto unavyolisikia ndivyo lilivyo. Ukienda kule, hutatamani hata adui yako afike huko kwa mateso yaliyo kule yasiyoelezeka.. “Mungu si mwepesi wa hasira, lakini ni mwingi wa hasira”
Kama leo unalikataa Neno lake, na unaona hakuna chochote kinachotokea au kitakachoweza kutokea juu yako, pengine Mungu amekuambia utubu mara nyingi, lakini unafanya hivyo leo, kesho unarudia mambo yale yale ya kidunia.. Upo wakati utafananishwa na Ninawi..Utakatwa na kupotea moja kwa moja, wakati huo ukifika hata uombeje, hata ulieje, hakuna rehema tena juu yako.
Mambo haya sio uongo!..yaliwatokea watu wa Ninawi kama yalivyo..kasome katika Historia baada ya kukataa maonyo, na pia yaliwatokea wana wa Israeli vile vile kwa kukataa maonyo, na hata kusababisha Mungu kukataa kuwasamehe. Soma mistari ifuatayo utathibitisha..
2Nyakati 36: 15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake; 16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya. 17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake”.
2Nyakati 36: 15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake”.
Mathayo 3:10 “Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.
Kama hujampokea Yesu, fanya hivyo sasa..
AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.
YONA: Mlango wa 4
JE KUVAA PETE NI DHAMBI?
JE! KUBET NI DHAMBI?
HAPANA HATA MMOJA ATAKAYEIONJA KARAMU YANGU.
Ni vizuri kufahamu kwanza maana ya uwanda, Uwanda ni sehemu iliyowazi iliyonyooka. Hivyo uwanda wa Dura ni sawa na kusema eneo la Dura lililo wazi.
Eneo hilo lilikuwepo Babeli na ndilo Nebukadneza mfalme alilichagua kuwa sehemu ya sanamu yake ya dhahabu aliyoitengeneza kwa ajili ya watu wa ulimwengu mzima kuisujudia. Eneo hilo la uwanda wa dura lilikuwa zuri kwa sanamu kuonekana vizuri na watu wengi kukusanyika.
Danieli 3:1 “Nebukadreza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita; akaisimamisha katika uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli. 2 Ndipo Nebukadreza akatuma watu kuwakusanya maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, ili wahudhurie wakati wa kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha”.
Danieli 3:1 “Nebukadreza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita; akaisimamisha katika uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli.
2 Ndipo Nebukadreza akatuma watu kuwakusanya maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, ili wahudhurie wakati wa kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha”.
Je! unafahamu ile sanamu inafunua nini siku hizi za mwisho?
Je! unajua chapa ya mnyama ndio itakuja kwa namna hiyo? Ili kufahamu hayo kwa upana fungua vichwa vya masomo tulivyoviorodhesha chini.
DANIELI: Mlango wa 3
UFUNUO: Mlango wa 13
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Shushani ngomeni ni sehemu gani kwasasa?
Mji wa shushani/Susa kwasasa upo eneo linaloitwa Shush katika nchi ya Iran.
kabla wamedi na waajemi kuiangusha Babaeli, Shushani ulikuwa ni mji mkuu wa Elamu, ambao tunaona Danieli akiuzungumzia katika.
Danieli 8:1 “Katika mwaka wa tatu wa kumiliki kwake mfalme Belshaza maono yalinitokea mimi, naam, mimi Danieli, baada ya hayo yaliyonitokea hapo kwanza. 2 Nami naliona katika maono; ilitukia, nilipoona, nalikuwako huko Shushani ngomeni, katika wilaya ya Elamu; nikaona katika maono, nami nalikuwa karibu na mto Ulai”.
Danieli 8:1 “Katika mwaka wa tatu wa kumiliki kwake mfalme Belshaza maono yalinitokea mimi, naam, mimi Danieli, baada ya hayo yaliyonitokea hapo kwanza.
2 Nami naliona katika maono; ilitukia, nilipoona, nalikuwako huko Shushani ngomeni, katika wilaya ya Elamu; nikaona katika maono, nami nalikuwa karibu na mto Ulai”.
Lakini baada ya wamedi na waajemi kuuchukua ufalme, mji huu ulikuja kugeuzwa kuwa mji wa kifalme wa wafalme wa Uajemi na Umedi.
Katika biblia tunaona Esta aliishi sehemu kubwa ya umalkia wake katika mji huu wa kifalme Shushani.
Esta 1:1 Zamani za Ahasuero; naye huyu Ahasuero alimiliki toka Bara Hindi mpaka Kushi, juu ya majimbo mia na ishirini na saba; 2 siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;
Esta 1:1 Zamani za Ahasuero; naye huyu Ahasuero alimiliki toka Bara Hindi mpaka Kushi, juu ya majimbo mia na ishirini na saba;
2 siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;
Unaweza kusoma pia, (Esta 2:3,5,8 Esta 3:15, Esta 4:8,16, Esta 8:14, Esta 9:6,11,12,13.)
Vilevile Nehemia naye alipokuwa mnyweshaji wa mfalme wa kiajemi alikuwa katika mji huu, huu wa Shushani..
Nehemia 1:1 “Habari za Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa katika mwezi wa Kisleu, mwaka wa ishirini, nilipokuwapo Shushani ngomeni, 2 Hanani, mmoja wa ndugu zangu, akanijia, yeye na watu wengine waliotoka Yuda; nami nikawauliza habari za Wayahudi waliopona, hao watu wa uhamisho waliosalia; na habari za Yerusalemu”.
Nehemia 1:1 “Habari za Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa katika mwezi wa Kisleu, mwaka wa ishirini, nilipokuwapo Shushani ngomeni,
2 Hanani, mmoja wa ndugu zangu, akanijia, yeye na watu wengine waliotoka Yuda; nami nikawauliza habari za Wayahudi waliopona, hao watu wa uhamisho waliosalia; na habari za Yerusalemu”.
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia ya mara kwa mara kwa njia ya whatsapp au email yako, basi tutumie ujumbe kwa kupitia namba hii: +255 789001312
MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?
Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?
Israeli ipo bara gani?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.