Adui yetu shetani, usiku na mchana anatafuta kutumeza, kama biblia inavyosema katika..1Petro 5:8 “ Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzungukazunguka, AKITAFUTA MTU AMMEZE”.
Hivyo anazo njia nyingi za kummeza mtu, na kila siku anabuni njia mpya…Lakini anayo moja maarufu anayoitumia ambayo ni ya MAWAZO.Anachofanya ni kupanda mbegu Fulani mbaya ndani ya mtu, ambayo hiyo mbegu inavyozidi kukuwa ndani yake inamletea kukata tamaa na mwisho kuanguka kabisa. Sasa yafuatayo ni baadhi ya Mawazo ambayo, ukiona yanakuja ndani yako, fahamu kuwa ni mawazo ambayo yamebuniwa na ibilisi, hivyo Yakatae na kuyapuuza.
Hii ni silaha moja maarufu ya adui shetani kwa watu wa Mungu. Anayatengeneza mawazo haya ndani ya mtu, na kumfanya aishiwe nguvu ya kuendelea kumtafuta Mungu na kuwa na amani.
Hivyo wazo lolote linalokuja ndani yako kwamba tayari umemkufuru Roho Mtakatifu, kwasababu pengine ulishawahi kusema maneno Fulani wakati Fulani, kuikejeli injili. Au ulifanya dhambi Fulani kubwa sana, ambayo haielezeki, au ulirudi nyuma baada ya wokovu wako, na sasa unataka kutubu uanze upya, Ukiona hilo wazo linakuja ndani yako, kukuambia kuwa ulishamkufuru Roho Mtakatifu, Fahamu kuwa hilo ni wazo la ibilisi asilimia 100, hivyo lipuuzie usilipe nafasi hata kidogo. Hakuna mwanadamu aliyemkufuru Roho Mtakatifu na bado ana hofu ya Mungu..Lakini usipolipuuzia hili wazo na kuendelea kukaa nalo moyoni, litazidi kukua na mwishowe litakufanya usiendelee kumtafuta Mungu, na litakufanya uwe unakosa amani na furaha kila wakati.
Hii ni silaha nyingine ya shetani, kuharibu watu wa Mungu..Ukiona upo kwenye hili tatizo kwamba unaona kama Mungu anakuchukia, hakupendi anawapenda tu baadhi ya watu Fulani, au watumishi wake..Jua tayari upo katika shambulizi la adui yako shetani, tayari upo katika anga
zake anakuharibu kidogo kidogo. Fahamu kuwa Mungu hamchukii mtu yeyote yule hata yule mwovu kuliko wote, ingekuwa anakuchukia sidhani kama angekuumba uishi katika hii dunia, mpaka umejiona umetokea kwenye hii dunia, jua ni kwaajili ya upendo wake kwako. Hivyo hilo wazo la kujiona hupendwi ni kutoka kwa adui.
Mungu anasikia maombi ya kila mwanadamu..kama kilio cha dhambi tu kinamfikia mbinguni, kwanini maombi yasimfikie?. Yanamfikia isipokuwa majibu ya maombi yanatofautiana mtu na mtu. Wapo ambao watapeleka maombi yao watajibiwa kama walivyoomba na wapo ambao hawatajibiwa, sasa wale ambao hawatajibiwa maombi yao, ipo sababu, na Mungu wa upendo atahakikisha wanaijua hiyo sababu kwa njia yeyote ile, ili warekebishe wapokee majibu ya maombi yao.. Kamwe hawezi kumwacha mtu yeyote hewani tu!, bila kumpa sababu ya kwanini hajapokea majibu ya maombi yake..Kinachowakwamisha wengi ni kukata tamaa
kirahisi…Unapokata tamaa tayari umekatisha safari yako ya kupokea baraka zako ukiwa katikati.
Kwa mfano, mtu anaweza kwenda kumwomba Mungu naomba unipe mume bora, au mke bora..lakini ukimwangalia ni kahaba, hivyo Mungu mwema hawezi kumpa kitu kizuri kabla hajamtengeneza kwanza…Kwahiyo wakati anasubiria majibu ya maombi yake, Mungu anamletea mhubiri, ambaye atamhubiria wokovu, na njia bora ya kuishi Maisha ya kumpendeza Mungu, anapotii na kukubali kubadilika na kuacha njia zake mbaya..Mungu ndipo anamletea jibu la
maombi yake aliyomwomba, analetewa mwenzi mwema wa Maisha, ambaye hatamsumbua na aliye mcha Mungu kama yeye. Lakini kama hatatii bado anataka kuendelea kukaa na ukahaba wake ndio atakaa hivyo hivyo kwa muda mrefu mpaka siku atakapofunguka akili, atarudia kuomba yale yale maneno lakini hataona majibu…
Hizo tu ndizo sababu za Mungu kuchelewesha majibu, lakini si kwamba Mungu hasikii maombi… Anayasikia, isipokuwa katika ujubuji wake ndio suala lingine.
Hivyo ukikosa kujiamini na kufikiri Mungu hajawahi kusikia maombi unayoomba chumbani kwako, au barabarani unapotembea, au kazini unapofanyia kazi…basi jua umeshambuliwa rohoni na adui shetani. Kazana kujua kwanini hujapata majibu lakini usifikiri kwamba hujasikiwa kabisa. Tayari umeshasikiwa, na uliloliomba limeshafanyiwa kazi, wewe fuatilia ombi lako lipo katika hatua gani sasa.
Marko 11:24 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu”.
Ndugu ukifikiri kwamba unaweza kufikia kiwango cha utakatifu kiasi kwamba huna kosa kabisa..basi fahamu kuwa hutaweza kamwe kumtumikia Mungu, kumbuka bado tunaishi duniani,
na lazima tutakuwa na kasoro nyingi, ambazo nyingi hatuzijui kama tunakosea…Sasa kama Mungu angezihesabu hizo biblia inasema hakuna mtu angesimama. Baada ya kuokoka ukiamka asubuhi usianze kukaa kuhesabu makosa yako, ukifanya hivyo kamwe hutaweza kumtumikia Mungu, na shetani atakusumbua sana na kila dakika atakuletea mawazo wewe ni mbaya, wewe hustahili, wewe hufai, wewe umeshamkosea Mungu, hufai, hufai n.k
Ukiamka asubuhi anza kuhesabu ni mazuri mangapi umemfanyia Mungu wako, na kama hujafanya kabisa ndipo uhuzunike, na tafuta kufanya, na jioni ukirudi..Mwambie Bwana asante kwa hichi kizuri ulichoniwezesha kukufanyia siku ya leo, na pia naomba nisamehe makosa yangu
yote niliyokukosea wewe pasipo kujua siku ya leo. Na kama unayakumbuka baadhi uliyoyafanya hakikisha kesho unayarekebisha, na ukishatubu tu usianze kujilaumu laumu!..Ukifanya hivyo utaruhusu mashambulizi ya shetani kukuvamia na kukuletea mawazo yale yale kwamba Mungu
alichukizwa na wewe jana, hivyo hawezi kuendelea kutembea na wewe leo…Kwahiyo siku zote Vaa ngao ya Imani, ili uweze kuizima hiyo mishale ya adui. Mungu wetu wa upendo hakai huko mbinguni na karatasi na kalamu akitiki mabaya tunayoyafanya baada ya sisi kuokoka…hafanyi hivyo, yeye yupo kutazama mema yetu, maadamu tumeshaokoka na
kumwamini na tumeweka mbali Maisha ya dhambi. Basi tunakuwa tunahesabiwa haki kwa Neema na si kwa matendo. Na hivyo kidogo kidogo anatutakasa mpaka unafika wakati tunakuwa wakamilifu kabisa kwake.
Hivyo hizo ni silaha 4 za adui yetu shetani. Sasa kama hizi Habari ni mpya kwako, na kama zimekufungua macho, basi ni dalili ya kwamba ulikuwa huna Ngao mkononi mwako, hivyo
ulimfungulia shetani nafasi ya kukushambulia ndio maana husongi mbele kiimani, na hiyo ni kutokana na kwamba pengine nafasi ya kutafuta kumjua Mungu Zaidi katika Maisha yako ni ndogo, au ulikuwa umesongwa na hivyo kulifahamu Neno imekuwa ngumu kwako, kwahiyo nakushauri mtu wa Mungu usiruhusu tena kusongwa..Neno hili wakristo wote waliofanikiwa ambao umeona wamesimama na hawapelekwi ni kwasababu, wana ngao za Imani mikononi
mwao, ni kwasababu Hivyo vipengele 4 hapo juu wamevishinda tangu zamani. Hivyo ni wewe peke yako umebaki.
Anza kumtafuta Mungu kwa bidii, anza kusoma Neno kwa bidii, usipitishe siku bila kushika biblia, na usomapo usisome kwa kutimiza wajibu, Ukilisoma Neno la Mungu na kulielewa ndivyo linavyokaa ndani yako, na linakupa Imani na maarifa, na ndivyo linavyokuweka huru, Ukilikosa hilo kamwe usitegemee kumshinda shetani, na wala kamwe usitegemee kama utaweza kumtumikia Mungu. Kwasababu shetani hawezi kuruhusu umtafute Mungu kirahisi rahisi hivyo, ni lazima akuletee hivyo vita vya kimawazo, akishinda hivyo atakuletea na vya nje, sasa ni wajibu wetu kufahamu kuwa tupo vitani. Ni lazima upambane kumjua Mungu.
Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”
Bwana akubariki.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)
KWANINI LEO HII KUNA KUNDI KUBWA LA WAKRISTO WALIORUDI NYUMA?
NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.
FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.
JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?
Rudi Nyumbani:
Print this post
Kabari ni nini?
Kabari ni ni kipande kikubwa cha kitu Fulani aidha mbao, chuma, dhahabu, shaba n.k.. (donge)
Katika biblia tunaona wana wa Israeli walipoingia nchi ya ahadi na kuwepo maagizo kuwa vitu vyote vya thamani watakavyovikuta kule vitatolewa wakfu kwa Bwana(Yoshua 6:19), lakini tunaona walipofika kulikuwa na mtu mmoja aliyeitwa Akani, mwana wa Karmi, huyu alipofika tu aliyeingiwa na tamaa, pale alipoona vitu vya thamani, ikiwemo hizi kabari (vipande) vya dhahabu, hakuvithaminisha kwa Bwana, bali alikwenda kuvificha(Yoshua 7:11).
Akasababisha mpaka taifa zima la Israeli kupigwa na kufadhaishwa mbele ya maadui zao. Hiyo ikawafanya wapepeleze tatizo ni nini, ndipo walipogundua kuwa ni huyu Akani ameficha baadhi ya vitu vya thamani walivyovikuta kule, hivyo wakamkamata na kumuua.
Yoshua 7:21 “Nilipoona katika nyara joho nzuri ya Babeli, na shekeli mia mbili za fedha, na kabari YA DHAHABU, uzani wake shekeli hamsini, basi nalivitamani nikavitwaa; tazama, vimefichwa mchangani katikati ya hema yangu, na ile fedha chini yake….. 24 Kisha Yoshua, na Israeli wote pamoja naye, wakamtwaa Akani, mwana wa Zera, na ile fedha, na Lile joho, na ile KABARI YA DHAHABU, na wanawe, na binti zake, na ng’ombe zake, na punda zake, na kondoo zake, na hema yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta juu hata bonde la Akori”.
Yoshua 7:21 “Nilipoona katika nyara joho nzuri ya Babeli, na shekeli mia mbili za fedha, na kabari YA DHAHABU, uzani wake shekeli hamsini, basi nalivitamani nikavitwaa; tazama, vimefichwa mchangani katikati ya hema yangu, na ile fedha chini yake…..
24 Kisha Yoshua, na Israeli wote pamoja naye, wakamtwaa Akani, mwana wa Zera, na ile fedha, na Lile joho, na ile KABARI YA DHAHABU, na wanawe, na binti zake, na ng’ombe zake, na punda zake, na kondoo zake, na hema yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta juu hata bonde la Akori”.
Hiyo inatufundisha nini? Inatufundisha kuwa tusiwe na tamaa ya mali ikiwa sisi ni watoto wa Mungu, kwani haitatugharimu maisha yetu tu, bali itagharimu kama sio kuathiri na maisha ya wengine pia. Na ndio maana biblia inasema,
1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.
Bwana atusaidie, tupende kujikusanyia zaidi kabari za ufalme wa mbinguni kuliko hizi za hapa duniani..Kwani za hapa duniani ni za kitambo tu, lakini zile zinadumu milele.
Shalom.
Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)
Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?
FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.
JIEPUSHE NA UNAJISI.
Kuna tofauti ya kumpa Mungu utukufu na kumshukuru Mungu. Mungu anapokufanyia jambo zuri, lakukupa faraja na furaha, na moyoni ukafurahi, ni kawaida ya kila mwanadamu mwenye moyo wa shukrani, huwa anakwenda kupiga magoti na kumshukuru Mungu wake kwa alilomtendea aualiyomtendea, na zaidi sana huwa anaambatanisha hata na sadaka yake ya shukrani.
Sasa hilo ni jambo moja ambalo linampendeza sana Mungu wetu, pale tunapomshukuru, lakini lipo lingine linalompendeza pia ambalo litatufungulia milango ya baraka mara mbili. Na jambo hilo si lingine zaidi ya KURUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.
Kurudi kumpa Mungu utukufu, ni kitendo cha kurudi na kutangaza kwa wazi, yale yote Mungu aliyokufanyia.. Hivyo Mungu wako anakuwa anatukuzwa katikati ya watu.
Ni jambo linalodharaulika na wengi lakini ni la umuhimu sana. Kurudi kumpa Mungu utukufu…Je umeshawahi kurudi kumpa Mungu utukufu kwa jambo lolote jema alilokufanyia?
Hebu tusome hichi kisa maarufu kwenye biblia..
Luka 17:11 “Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria naGalilaya. 12 Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali, 13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu! 14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakiendawalitakasika. 15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, HUKU AKİMTUKUZA MUNGU KWA SAUTİ KUU; 16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria. 17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi? 18 JE! HAWAKUONEKANA WALİORUDİ KUMPA MUNGU UTUKUFU İLA MGENİ HUYU? 19 Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa”
Luka 17:11 “Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria naGalilaya.
12 Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakiendawalitakasika.
15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, HUKU AKİMTUKUZA MUNGU KWA SAUTİ KUU;
16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?
18 JE! HAWAKUONEKANA WALİORUDİ KUMPA MUNGU UTUKUFU İLA MGENİ HUYU?
19 Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa”
Waliponywa wote kumi lakini ni huyu mmoja tu ndiye Aliyepaza sauti yake, kwa sauti kuu, akitangaza jinsi alivyoponywa njia nzima, mpaka alipofika kwa Bwana Yesu..Pengine wale 9 walikwenda kutoa sadaka zao za shukrani tu!..Lakini hawakumtukuza Mungu, walakutangaza waliyofanyiwa kwa wazi, kwasababu zao wenyewe, labda waliona aibu, au waliogopa kutengwa, au kuonekana wa kikale…Lakini huyu hakujali hayo, alitangaza kwa watu lililomtokea kuanzia mwanzo hadi mwisho..
Na hivyo likawa ni jambo jema mbele za Mungu..
Je na wewe ulishawahi kurudi kumpa Mungu utukufu?… Bwana alipokuponya ugonjwa ambao ilikuwa ni ngumu kupona, je! Ulishawahi kusimama na kutangazia watu wawili au watatu mambo makuu Mungu aliyokufanyia?..au uliishia kuwatukuza madaktari tu! Kwamba walikupambania lakini hukuwahi kumtaja Mungu maneno yasiyozidi mawili?..Kama ndivyo basi badilika leo.
Je ulishawahi kumpa Mungu utukufu kwa huyo mtoto uliyempata ambaye ulihangaika miaka mingi bila kupata mtoto?..Ni kweli pengine ulitoa sadaka ya shukrani, hiyo ni vizuri…lakini bado haitoshi…Mungu wako anapaswa atukuzwe mbele za watu kwa hicho alichokufanyia.. Inapaswa watu wamwonapo mwanao aliyekupa Mungu, wamfikirie Mungu wako na si daktari wako wala jitihada zako.
Nyumba Mungu aliyokupa, mali alizokupa, afya aliyokupa, uzima anaokupa, cheo alichokupa, elimu aliyokujalia, nguvu alizokupa n.k…Je Mungu wako anatukuzwa katika huo? Au jitihada zako?..Watu wanapaswa wakitazama cheo chako wanakumbuka ushuhuda uliowasimulia wa jinsi Mungu alivyokuweka pale kimiujiza, na sio wanakumbuka jinsi ulivyopambana…Watu wanapokuona leo umesimama ni mzima, wanapaswa wakumbuke ushuhuda uliowaambia jinsi ulivyokuwa hatiani kupona na ukamwomba Mungu na Mungu akakufungulia mlango wa uponyaji… ili Mungu wako atukuzwe kwao.
Watu wanapokuona una hiki au kile..wanapaswa wautafakari uzuri wa Mungu wako, na utukufu wake, kwa utukufu uliomrudishia wakati unavipata hivyo…kila kitu wajue ni Mungu kakusaidia na si nguvu zako.
Na hatumpi Mungu wetu utukufu kwa yale aliyotutendea kwa kuwawekea watesi wetu CD za mipasho!.. Kwasababu siku hizi zipo nyimbo za dini ambazo hazina tofauti na nyimbo za kidunia (Taarabu)..zimejaa maneno ya kiburi na ushindani. Kwamba Mungu kanitendea hichi ili maadui
zangu waone waumie moyo…Hapana! mpango wa Mungu sio maadui zetu waumie moyo na waone Mungu alichotufanyia halafu basi!. Mungu hatupiganii ili awachome watu mioyo, bali ili awageuze nia zao wamgeukie yeye.
Hivyo ukimpa Mungu utukufu mbele za watu, jinsi inavyopaswa, kwa kutangaza kwa kina ulipotoka na ulipo sasa, na jinsi gani Mungu alivyokuokoa, kwa neema…Wale wanaokusikiliza akili zao zitahama kutoka kushindana na wewe, na kuhamia kumtafakari Mungu wako, na hivyo nao pia wamtamtamani Mungu wako aliyekutendea mambo makuu namna hiyo. Na watakuuliza “nami nifanyaje Mungu anitendee kama alivyokutendea wewe”
Lakini ukianza kuwawekea mipasho, watakuchukia na hawatavutiwa na unachokiamini, hivyo utakuwa nawe pia unaifanya kazi ya ibilisi ya kuwapeleka watu mbali na Mungu, na moyoni ukidhani umemtukuza Mungu kwa nyimbo zako hizo za kiburi na majivuno kumbe ndio unaenda kinyume na mapenzi ya Mungu.
Hivyo Usiache kamwe kurudi kumpa Mungu utukufu kwa jambo lolote lile analokutendea, hata liwe dogo kiasi gani…Nenda kalitangaze kanisani, kalitangaze kwa rafiki zako, kalisimulie kwa ndugu, kalisimulie kwa yoyote yule ambaye utapata nafasi ya kumsimulia..hakikisha tu lengo lako ni Mungu atukuzwe na si wewe utukuzwe, au kujisifu.
JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?
Mavu ni nini katika biblia?(Kutoka 23:28, Kumb 7:20)
UTAWALA WA MIAKA 1000.
CHAPA YA MNYAMA
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.
Mtu akikufanyia fadhila ya hali ya juu, ni wazi kuwa nafsi yako haitatulia mpaka na wewe utakapohakikisha umemrudishia naye pia fadhila..hiyo ni hali ya kawaida ya kibinadamu kabisa, hata kama hakitafikia kile alichokufanyia walau utaonyesha shukrani kwa kumwombea dua kwa Mungu.
Hata sisi tunapookoka, tunapogundua kuwa kumbe kuna mtu alitupenda upeo, kumbe kuna mtu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu na kama asingekufa leo hii sisi tungekuwa ni wa kuzimu.
Ni dhahiri kuwa kama tumeithamini fadhila hiyo ya kipekee basi na sisi ni lazima tutaonyesha kurudisha kitu Fulani kwake, ni kweli hatuwezi kumrudishia fadhila za matendo yetu mema kama yeye aliyotufanyia, kwasababu mpaka hapa tulipo tulishamkosea Mungu mara nyingi sana. Lakini fadhili tunayoweza kumrudishia ni kuupeleka Upendo wake, uwafikie na wengine, ambao bado haujawafikia, ili nao pia waokolewe kama sisi. Na hiyo ndio inayotufanya tuwahubirie injili na wengine, na kuwaombea.
Mtume Paulo alisema maneno haya;
2Wakorintho 5:14 “MAANA, UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote”;
Unaona? Vivyo hivyo na sisi, huu upendo wa ajabu wa Yesu kutoa maisha yake kwa ajili yetu sisi bure, ugeuke na kuwa deni kwetu,..Huu ndio utupe sababu ya kuwapelekea watu wengine habari njema, tusiuchukulie bure tu..
2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure. 2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”.
Kama wewe umeokolewa mshukuru Mungu sana kwa neema hiyo , lakini kumbuka wapo watu wengi wanaohitaji kuokolewa kama wewe, swali tujiulize tangu tumeokoka Je viungo vyetu vimeleta faida yoyote kwa Kristo? Je kilishamleta mmoja katika neema ya wokovu au la? Kama karama yako haijawahi kufanya hivyo, badala yake imetumika kuwaburudisha tu watu, basi ujue karama hiyo ni feki, haijatoka kwa Mungu.
Hivyo kwa pamoja sote, tuufanye upendo wa Kristo kama deni kwetu. Huo utubidiishe kumtumikia Mungu, kwa karama zetu na kwa tulivyonavyo, ili neema ya Mungu iwafikie na wengine kama sisi nao pia waufurahie wokovu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
Kilichoawafanya mitume waupindue ulimwengu kwa wakati wao, ni kwasababu kwa pamoja waliutambua Upendo wa Kristo, hivyo ukageuka kuwa deni kwao, wakamtumikia Mungu kwa vyote walivyokuwanavyo, na ndio maana na hapo wanasema Upendo wa Kristo watubidiisha, vivyo hivyo na sisi, tuugeuze Upendo huu kuwa deni.
Na Bwana atatuonekania katika maisha yetu.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?
Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?
LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.
Ni wajibu wa kila mkristo kutambua kuwa kuna vita vikubwa sana katika kuyafanya mapenzi ya Mungu, na mapenzi ya Mungu ni Neno la Mungu..Mtu anapolisoma Neno la Mungu na kulielewa na kulifanya au kulitenda kama lilivyoandikwa, hapo anakuwa anafanya mapenzi ya Mungu.
Leo tutakwenda kutazama kipengele kimoja cha Neno la Mungu ambacho huwa shetani anakiua kwa watu wengi. shetani huwa hapendi watu walishike Neno la Mungu, kwasababu Neno la Mungu ndio ufunguo wa mafanikio yote.
Kwamfano Neno la Mungu linasema tuwe watu wa kuomba (Wakosai 4:2, Wafilipi 4:6, Yakobo 5:16, Yuda 1:20) na pia kuomba/kusali ndio ngao pekee ya kujilinda na majaribu ya yule Adui Marko 14:38. Hivyo mtu anayeomba, kamwe shetani hawezi kumshinda kwa majaribu..Na njia mojawapo shetani anayoitumia kuangusha watu ni kwa njia ya majaribu.
Utauliza majaribu kwa namna gani?
Unapopanga kwenda kanisani halafu linatokea jambo la kukukwamisha, hilo tayari ni jaribu, unapopanga kwenda kutenda wema lakini kinatokea kitu cha kuvuruga huo mpango hilo tayari ni jaribu..Sasa majaribu kama hayo yanaweza kuepukika kama ukiwa mtu wa kuomba.
Ukiwa mtu wa kuomba utaona kila unalolipanga linakwenda kama ulivyolipanga…Ulipanga jumapili uende kanisani, unaona siku hiyo inafika hakuna vikwazo vyovyote vinavyojitokeza kuanzia asubuhi mpaka jioni, umepanga uende ukahubiri unaona ratiba zinakwenda kama ulivyopanga n.k.
Sasa turudi kwenye somo letu, lenye kichwa kinachosema je! Kuna uchawi katika kutenda mema?
Ndugu hakuna uchawi wowote katika kutenda wema/mema. Shetani amekuwa akiwatishia watu wengi kuwa ukifanya kitu fulani kwa mtu fulani unaweza kujikuta unalogwa!. Hivyo ni vitisho vya shetani kuwazuia watu wasibarikiwe. Kwasababu anajua funguo mojawapo ya kubarikiwa ni kuwa mtoaji..Bwana wetu Yesu alitufundisha hiyo siri ambayo tulikuwa hatuijui alisema..
Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.
Sasa shetani hataki tufanikiwe! Anachotaka tuendelee kuwa jinsi tulivyo..Na ili kuhakikisha hilo linafanikiwa anakimbilia kuligeuza hili neno la Bwana wetu Yesu, linalosema wapeni watu vitu nanyi mtapewa…yeye (shetani) analigeuza na kusema (usimpe mtu usiyemjua kitu usimpe nguo zako, atazipeleka kwa mganga na mwisho wa siku utajikuta wewe ndio unakuwa maskini, atakwambia usisaidie watu barabarani wengine ni wachawi, chuma ulete, utajikuta nyota yako inahamishwa).
Hayo ndiyo mahubiri ya shetani, ya kuwazuia watu wasibarikiwe. Na kwasababu inakuja na vitisho vikali, watu wengi inawaogopesha na hivyo inawafanya wasidhubutu kusaidia saidia hovyo!!. Nimewahi kuona filamu fulani inaonyesha mtu kapita barabarani akakutana na mtu anaomba msaada, na katika kuomba kwake akamsaidia kwa kumpa fedha, ghafla yale matatizo ya yule mtu yakahamia kwake huyo aliyetoa msaada.
Ndugu usidanganyike na injili hiyo ya kuzimu!..(kumbuka kulishika Neno la Mungu ni vita!)..lazima upambane hiyo vita na uishinde..na huishindi kwa maneno tu! Bali kwa kulijua Neno la Mungu vizuri, vinginevyo ni rahisi kwenda na maji..kwasababu shetani anavitisho vya kutosha kuhakikisha hulitendi neno la Mungu. Kila jambo kwako atakuundia picha ya kulogwa tu.
Hivyo ni uongo kwamba ukifanya wema utalogwa, au utafungua mlango kwa shetani kuyadhuru maisha yako…Huo ni uongo
Sasa unaweza kuuliza hata kama “yule fulani namjua ni mchawi, au anaamini ushirikina, au ni mganga wa kienyeji” akija kuniomba fedha au chochote kile nimpe??..je hatanidhuru?..Jibu ni ndio mpe..hutapatikana na madhara yoyote badala yake ndio utabarikiwa…hata kama ni mchawi kaja kukuomba na umeona ni kweli anahitaji msaada mpe usifikiri mara mbili mbili…kwasababu hakuna uchawi katika kutenda mema!..
Mithali 25:21 “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; 22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu”..
Utasema hilo ni agano la kale, vipi katika agano jipya? Kasome Warumi 12:20.
Sasa hapo anasema “Adui yako” na si rafiki yako, maana yake ni kwamba “yule mtu ambaye unaona anaweza kukuletea madhara”.. Huyo ndiye msaidie kwa kumpa chakula au chochote kile, kwasababu hakuna chochote kitakachokupata wewe cha kukuletea madhara unapomsaidia, badala yake hicho ulichompa ndio kitakuwa chachu ya kumponya yeye, na Mungu atakubariki wewe kwa kufanya hivyo.
Ndugu kuna vita kali katika kulishika Neno, tena si ndogo…Hilo Neno la Bwana Yesu kulisoma ni rahisi, lakini ukilileta katika maisha halisi linavita vingi, limejaa vitisho vya shetani ndani yake, limewafanya hata watu wakiona mtu kalala barabarani, kaishiwa nguvu wampite tu! Bila kutoa msaada wowote..wakihofia kwamba endapo wakimsaidia ndio nyota zao zitakwenda hivyo..kumbe kwa kumpita yule ndio wanazipita baraka zao hivyo hivyo.(kasome Luka 10:32-36).
Na kuna mahubiri siku hizi yanayofundisha kinyume cha hilo Neno zuri la Bwana wetu Yesu Kristo, “neno lililojaa upendo wa ajabu”…lakini wanahubiri na kulitukuza neno la Adui shetani lililojaa chuki na vitisho!. Tangu lini Mungu aliye na upendo akamkataza mwanadamu wake kuwa na upendo?.
Unataka kupata fursa? Unataka kupata vitu? Unataka kubarikiwa?..Njia ni hiyo (wapeni watu vitu nanyi mtapewa), na sio tu fedha, au chakula.. bali hata faraja..wafariji wanaohitaji kufarijiwa nawe pia siku ya kupata mashaka na masononeko, Bwana atamtuma mtu wa kukufariji, watie moyo wanaohitaji kutiwa moyo ili itakapofika siku ambayo utakuwa umekaribia kukata tamaa, uwe na deni kwa Mungu wako la wewe kufarijiwa pia n.k n.K.
Mathayo 5:42 “Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo. 43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; 44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, 45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. 46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo? 47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? 48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”
Mathayo 5:42 “Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.
43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”
Bwana akubariki, na Bwana atubariki wote.
NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!
KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.
UPONYAJI WA ASILI
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Baradhuli ni nani/ ni nini kama lilivyotumika kwenye biblia?
Kibiblia Baradhuli ni mtu asiyefaa, mpumbavu sana, aliyevuka mipaka
Ipo mistari kadha wa kadha inayoeleza tabia za watu wabaradhuli. Kwa mfano:
Wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji angali wanajua kabisa wanachokifanya ni kinyuma na mapenzi ya Mungu, wanaofanya uchawi, wanaofanya matambiko n.k. Hao ni mabaradhuli kibiblia.
Kumbukumbuku 13:12 Ukisikia yasemwa habari ya miji yako mmojawapo, akupayo Bwana, Mungu wako, ukae humo, ukiambiwa, 13 Kumetoka katikati yako MABARADHULI kadha wa kadha, wamewapotoa wenyeji wa mji wao, wakisema, Twendeni tukaabudu miungu mingine msiyoijua; 14 ndipo nawe uulize na kutafuta, ukiuliza kwa bidii; nawe angalia, ikiwa kweli, na jambo lile halina shaka, kwamba machukizo mfano wa haya yafanyika katikati yako; 15 hakika yako uwapige wenyeji wa mji ule kwa makali ya upanga, kwa kuwaangamiza kabisa, pamoja na vitu vyote vilivyomo, na wanyama walio humo, kwa makali ya upanga.
Kumbukumbuku 13:12 Ukisikia yasemwa habari ya miji yako mmojawapo, akupayo Bwana, Mungu wako, ukae humo, ukiambiwa,
13 Kumetoka katikati yako MABARADHULI kadha wa kadha, wamewapotoa wenyeji wa mji wao, wakisema, Twendeni tukaabudu miungu mingine msiyoijua;
14 ndipo nawe uulize na kutafuta, ukiuliza kwa bidii; nawe angalia, ikiwa kweli, na jambo lile halina shaka, kwamba machukizo mfano wa haya yafanyika katikati yako;
15 hakika yako uwapige wenyeji wa mji ule kwa makali ya upanga, kwa kuwaangamiza kabisa, pamoja na vitu vyote vilivyomo, na wanyama walio humo, kwa makali ya upanga.
Ukisoma kitabu cha Waamuzi utaona Gideoni alikuwa na watoto sabini na wawili, lakini baada ya Gideoni kufa, mtoto wake mmoja aliingiwa na tamaa kutawala sehemu ya Gideoni hivyo akaamua kuwaua ndugu zake wote waliosalia ili yeye afanywe muamuzi badala yake, Ndipo biblia inatuambia alikwenda kuwaajiri watu Mabaradhuli ili kutekeleza adhma yake hiyo ya uuaji,..Hao watu wakashirikiana naye kuwaua ndugu zake wote siku moja juu ya jiwe. (Waamuzi 9:1-5).
Ukisoma tena kitabu cha Waamuzi 19 utamwona Yule mlawi ambaye alikuwa na suria wake, aliyekwenda kufanya ukahaba, kitendo ambacho kilimpelekea amrudishe nyumbani kwa baba yake, hivyo akakaa kule kwa muda wa miezi 4, ndipo baadaye akaghahiri akaamua amfuate surua wake amrudishe kwake, sasa alipokuwa njiani mji mmoja wa ugenini, alikaribishwa na mzee mmoja wa mji ule. Lakini usiku mambo yalibadilika kwani wale watu wa mji ule wa Benyamini, waliizingira nyumba wakataka wapewe hao wageni walale nao..Kama tunavyoijua habari Yule mlawi akaona ni heri amtoe suria wake wamfanye waliyotaka kumfanya..Wakafanya hivyo mpaka asubuhi baadaye Yule Suria akafa..
Waamuzi 19:22 “Hapo walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, tazama, watu wa mji huo, watu MABARADHULI wakaizingira hiyo nyumba pande zote, wakagonga mlango; wakasema na huyo mwenye nyumba, huyo mzee, na kumwambia, Mlete nje mtu yule aliyefika nyumbani kwako, ili tupate kumjua”.
Soma sura yote ya 19,20 na 21, upate picha kamili, na nini kiliendelea baada ya pale..
Watu wanaoshikamana na viongozi waasi, au waliokosa heshima katika jamii.
2Nyakati 13:7, Waamuzi 11:3.
Je mpaka sasa mabaradhuli wapo?
Unapaswa ujiulize je! tabia mojawapo ya hizo unazo?
Kumbuka kuwa waovu wote, sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Ikiwa wewe ni muuaji, wewe ni baradhuli, ikiwa wewe ni mchawi(unakwenda kwa waganga) wewe ni baradhuli, n.k.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Lakini tumaini lipo kwa Yesu tu peke yake. Yeye peke yake ndiye anayeweza kuyageuza maisha yako na kukusaheme kabisa kabisa. Na kukufanya kuwa mwana wake.
Je! unahitaji kuokoka leo?
Unahitaji Yesu ayabadilishe maisha yako leo?
Unahitaji kupokea Roho Mtakatifu?
Biblia inasema..
Isaya 1:18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. 19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi”;
Isaya 1:18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.
19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi”;
Kama ndivyo basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?
Arabuni maana yake ni nini?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
SWALI: Ibada ni nini, Na je ili ibada ikamilike inapaswa iwe na nini na nini? Na je ni siku gani maalumu ya kufanya ibada?
Ibada ni kitendo chochote kifanywacho kuonyesha unyenyekevu wa hali ya juu, utiifu, heshima, shukrani, na utukufu, aidha kwa Mungu au kitu kingine, na hiyo inaambata na mambo kadha wa kadha, ikiwemo kusifu, kuabudu, kusujudu, kuimba, kufunga, kutoa sadaka, na kushiriki maagano ya imani, Na vilevile kujitoa mwili wako kuvitumikia, hiyo nayo ni ibada kamili.
Kibiblia kuna ibada za aina tatu
Hizi, ni zote tuzifanyazo aidha kanisani au manyumbani kwetu wenyewe, tunapokutana kumwimbia na kumwabudu Mungu, au kumshukuru, au kushiriki meza ya Bwana, hiyo tayari ni ibada kwa Mungu.
Matendo 13:2 “Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia”.
Na kama tulivyosema awali hata kujitoa mwili wako kwa ajili ya kutenda matendo yote yampendezayo Mungu ni ibada kamili tayari..
Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana”.
Hizi kwa jina lingine ndio ibada za sanamu. Ambazo biblia imezikemea sehemu nyingi sana katika biblia. Unapokwenda kuisujudia sanamu yoyote ile, iwe na mfano wa mtakatifu Fulani mbinguni, tayari hiyo ni ibada kamili ya sanamu.. Inayomtia Mungu wivu wa kukuangamiza haraka sana.
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.
1Wakorintho 10:14 “Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu”.
Lakini kama hilo halitoshi, unaweza pengine ukawa husujudii masanamu, lakini mwili wako unafanya maasi, hiyo nayo ni ibada kamili ya sanamu sawasawa na kusujudia vinyago.
Wakolosai 3:5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu”;
Hizi ni ibada ambazo, hazitokani na Mungu wala shetani, bali zinatokana na watu wenyewe, wamejitungia wakidhani kuwa wanamfanyia Mungu, kumbe wanafanya kimakosa..
Wakolosai 2:20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani, 21 Msishike, msionje, msiguse; 22 (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu? 23 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, KATIKA NAMNA YA IBADA MLIYOJITUNGIA WENYEWE, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
Wakolosai 2:20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,
21 Msishike, msionje, msiguse;
22 (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?
23 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, KATIKA NAMNA YA IBADA MLIYOJITUNGIA WENYEWE, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
Na zina madhara yake makubwa, kwasababu wakati mwingine zinasababisha hata watu waue watu wengine wakidhani kuwa ndio wanampendeza Mungu, kama tu walivyokuwa wanafanya Warumi na Wayahudi kwenye kanisa la kwanza, na jinsi zinavyofanywa na baadhi dini leo hii duniani kuchinja watu. Zote hizo ni ibada ambazo watu wamejitungua lakini hazitokani na Mungu.
Yohana 16:2 “Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa ANAMTOLEA MUNGU IBADA.
Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa, ibada halisi ni moja tu, nayo ni kwa Mungu muumba wa mbingu na nchi (YEHOVA), na Kristo wake aliyesulibiwa kwa ajili ya dhambi zetu sisi wanadamu. Na maagizo pekee ya ibada hiyo halisi yanapatikana katika biblia tu.. Ibada nyingine yoyote tofauti na hiyo, ni machukizo makubwa kwake.
Na pia tunaikamilisha kwa miili yetu kama biblia inavyotufundisha, kwa kuishi maisha yampendezayo Bwana, ndio ibada yenye maana, ikiwa tutakuwa tunahudhuria kanisani kila siku, tunamwabudu Mungu usiku na mchana, tunamtolea matoleo mengi, tunashiriki meza ya Bwana kila wiki halafu matendo yetu, au miili yetu tumeiuza kwa shetani, ibada zetu bado ni batili..Zinakuwa ni ibada za sanamu, au ibada tulizojitungia tu sisi wenyewe.
Lakini kama utayakamilisha yote ya rohoni na mwilini, basi ibada hiyo inafaa sana mbele za Mungu, na inathawabu nyingi sana. Wanaomfanyia Mungu ibada kamili wanakuwa marafiki wa karibu sana Mungu.
Na pia hakuna siku maalumu ya kumfanyia Mungu ibada, kwani ibada yetu halisi ipo rohoni, hivyo wakati wowote na muda wowote uwapo na nafasi inaingia uweponi mwa Mungu, kumsifu, kumshukuru, kumwabudu, kumtolea dhabihu za shukrani n.k.. Lakini pia ipo ibada ya watakatifu wote, ambayo inafanyika kila juma, hivyo ikiwa ni jumapili au Jumamosi, inapaswa ifuatwe. Kama tulivyoambiwa tusiache kukutanika pamoja..
Bwana wetu atusaidie sote, tuweze kuyakamilisha hayo.
USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.
Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?
JE KUVAA PETE NI DHAMBI?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, karibu tujifunze biblia.
Imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo.. Je! Una uhakika wa mambo yatakayokuja ambayo bado hujayaona wala kuyafikia?..Na kama ndio, je kwa kiwango gani?.
Ili Imani yako ionekane kuwa kubwa ni lazima uwe na uwezo wa kuamini vitu visivyoweza kuaminika. Yaani uwe na kila sababu itakayokufanya kuwa na uhakika kwamba jambo Fulani lazima litokee.
Kwamfano ukizungumza na mtu kwenye simu, aliye umbali Fulani akakwambia panda gari (daladala) unifuate mahali nilipo baada ya lisaa limoja…bila shaka kama utakuwa na fedha ya kutosha mfukoni mwako, hutakuwa na wasiwasi wa kufika pale alipo…kwasababu unajua hata Ukikosa daladala utatafuta tax, na hata ukikosa hiyo bado unaweza kupanda pikipiki ukafika pale alipo katika muda ule ule. Hivyo huo uwezo wa kuwa na kila sababu ya kufika pale kwa muda unaotakiwa ndio unaoitwa IMANI (una uhakika wa mambo yatarajiwayo yatafanikiwa asilimia 100).
Lakini kama huna fedha kabisa au unafedha kidogo tu ya daladala, utakuwa na wasiwasi, utasema itakuwaje endapo nikikosa gari? itakuwaje endapo gari nitakalopanda likiharibikia njiani?..si nitachelewa n.k Hivyo unakuwa huna uhakika sana wa mambo yatarajiwayo..Hapo inahesabika kuwa Imani yako ya kufika unakotaka kwenda kwa muda unaotakiwa ni ndogo au huna kabisa.
Sasa tukirudi katika Biblia ni hivyo hivyo..Ili uweze kuhesabika kuwa na Imani kubwa ya kutosha ya kuweza kupata kile unachokihitaji kwa Asilimia zote, ni lazima uwe na Hazina ya kutosha ya UELEWA WA MAANDIKO, ili uweze kukipata kile kitu. Kumbuka hapo ninasema ni UELEWA WA MAANDIKO, na si IDADI YA MAANDIKO. Mtu mwenye idadi kubwa ya maandiko pasipo kuyaelewa huyo ni sawa redio yenye idadi kubwa ya sauti na nyimbo zinazotoka ndani yake, lakini yenyewe haielewi chochote.
Hivyo kinachojalisha kwetu ili tuhesabike kuwa na Imani ya kuweza kupokea jambo lolote lile ni HAZINA YA KUYAELEWA MAANDIKO NA KUYACHAMBUA.
Hebu tujifunze mfano mmoja kwenye biblia ya Mtu aliyekuwa na hazina na uwezo wa kuyaelewa maandiko vyema na kuyagawanya..
Mathayo 15:22 “Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. 23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. 24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli 25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie. 26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. 27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao. 28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.
Mathayo 15:22 “Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.
27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.
Unaweza kuona hapo, anakatishwa tamaa kwa maneno ya YESU, na kama tunavyojua maneno ya Yesu ni Neno la Mungu. Lakini kwa maneno hayo hayo, mwanammke anayafafanua vizuri kwa Bwana, na hatimaye anapata haki yake.. “ni kweli si vyema kutwaa chakula cha watoto kuwatupia mbwa, lakini hata mbwa wanakula makombo yaangukayo chini ya meza za Bwana zao”…Maana yake ni kwamba sistahili kweli kupewa hichi ninachokitafuta, (ni kweli mimi ni kama mbwa).. Lakini kuna vile vidogo vichache vinavyobakigi..ipo neema kidogo inakuwepo kwa Mungu kwa wale wasiomcha yeye…Hiyo ndio ninayoihitaji mimi!..Ni kweli Mungu hasikii maombi ya waovu, lakini bado Mungu huyo huyo anawanyeshea mvua waovu na wema…anawaangazia jua lake wenye haki na wasio haki..
Ni kweli mimi sio mkamilifu mbele zake, lakini bado wale waovu kuliko mimi anahakikisha wanafikiwa na miale ya jua, anahakikisha upepo mwanana unawaburudisha, anahakikisha wanapata hewa safi ya oksijeni kila dakika..hivyo kwa rehema hizo, ni lazima na mimi na mimi lazima nipone, lazima nibarikiwe na kufanikiwa katika yote..Mungu hana mbaraka mmoja tu!.
Hebu tujifunze Zaidi kisa cha Esau na Yakobo.
Tusome..
Mwanzo 27: 33 “Isaka akatetemeka tetemeko kuu sana, akasema, Ni nani basi yule aliyetwaa mawindo akaniletea? Nami nimekwisha kula kabla hujaja wewe, nikambariki; naam, naye atabarikiwa. 34 Esau aliposikia maneno ya babaye, akalia kilio kikubwa cha uchungu sana, akamwambia babaye, Nibariki na mimi, mimi nami, Ee babangu. 35 Akasema, Nduguyo amekuja kwa hila, akauchukua mbaraka wako. 36 Akasema, Je! Hakuitwa Yakobo kwa haki, maana amejitia mahali pangu mara mbili hizi? Alichukua haki yangu ya mzaliwa wa kwanza, na sasa amechukua mbaraka wangu. Akasema, Je! Hukuniwekea na mimi mbaraka? 37 Isaka akajibu, akamwambia Esau, Tazama, nimemfanya awe bwana wako, na ndugu zake wote nimempa kuwa watumishi wake; kwa nafaka na mvinyo nimemtegemeza, nami nikufanyie nini sasa, mwanangu? 38 ESAU AKAMWAMBIA BABAYE, UNA MBARAKA MMOJA TU, BABANGU? Unibariki mimi, mimi nami, Ee babangu. Esau akapaza sauti yake, akalia. 39 Isaka, baba yake, akajibu, akamwambia,Angalia,penye manono ya nchi patakuwa makao yako,Na penye umande wa mbingu unaotoka juu”.
Mwanzo 27: 33 “Isaka akatetemeka tetemeko kuu sana, akasema, Ni nani basi yule aliyetwaa mawindo akaniletea? Nami nimekwisha kula kabla hujaja wewe, nikambariki; naam, naye atabarikiwa.
34 Esau aliposikia maneno ya babaye, akalia kilio kikubwa cha uchungu sana, akamwambia babaye, Nibariki na mimi, mimi nami, Ee babangu.
35 Akasema, Nduguyo amekuja kwa hila, akauchukua mbaraka wako.
36 Akasema, Je! Hakuitwa Yakobo kwa haki, maana amejitia mahali pangu mara mbili hizi? Alichukua haki yangu ya mzaliwa wa kwanza, na sasa amechukua mbaraka wangu. Akasema, Je! Hukuniwekea na mimi mbaraka?
37 Isaka akajibu, akamwambia Esau, Tazama, nimemfanya awe bwana wako, na ndugu zake wote nimempa kuwa watumishi wake; kwa nafaka na mvinyo nimemtegemeza, nami nikufanyie nini sasa, mwanangu?
38 ESAU AKAMWAMBIA BABAYE, UNA MBARAKA MMOJA TU, BABANGU? Unibariki mimi, mimi nami, Ee babangu. Esau akapaza sauti yake, akalia.
39 Isaka, baba yake, akajibu, akamwambia,Angalia,penye manono ya nchi patakuwa makao yako,Na penye umande wa mbingu unaotoka juu”.
Hebu tafakari Esau, angenyamaza asingelia kuomba na yeye abarikiwe, hebu tafakari angeishia kuondoka kwa majonzi leo hi angeishia kuwa kama Kaini, asingekuwa na baraka yoyote….Lakini japokuwa aliikosa ile Baraka kuu, lakini alilia kwa baba yake..akamwambia baba yake nibariki na mimi, kwani una mbaraka mmoja tu??? Na mwishowe akabarikiwa akaambiwa palipo na manono ya nchi patakuwa mahali pake, ingawa Mungu alimchukia Esau(Warumi 9:13)… lakini bado alimbariki alikuwa na mali nyingi hata Zaidi ya Yakobo kasome (kasome Mwanzo 33:9)
Na sisi ni hivyo hivyo, (simaanishi kuwa tuwe waovu, Mungu atusaidie), nachomaanisha ni kuwa ikiwa wewe ni mkristo hupaswi kukata tamaa hata kama inaonekana mambo yameshashindikana…Tujue tu! Mungu hana mbaraka mmoja tu!, usijiangalie ukamilifu wako!..Esau Mungu alimchukia lakini kwa kupambana akambariki hivyo hivyo…
Ukiona jambo Fulani katika Maisha kama haliwezekani, basi jua huo ndio uthibitisho kwamba linawezekana….kibiblia kutokuwezekana ndio uthibitisho wa kuwezekana kwa jambo. Amini tu! Amini tu.. usiache kumwamini Mungu kamwe.
Mwisho kabisa kama tulivyosema… “kubarikiwa wakati mwingine sio uthibitisho wa kumpendeza Mungu”..Esau hakumpendeza Mungu lakini alibarikiwa, na wengine wengi katika biblia…na hata leo Mungu ni yule yule…anawanyeshea mvua waovu na wema…Kwahiyo kuzimu watakuwepo matajiri sana, na mbingu pia watakuwepo maskini, hivyo lililo la Muhimu sana ni kutafuta kuyatenda mapenzi ya Mungu, ambayo hiyo inakuja kwa kutubu na kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa Maisha yako na kutafuta ubatizo sahihi wa kimaandiko (Matendo 2:38), na kupokea Roho Mtakatifu, hilo ndio jambo la muhimu na la kwanza, mengine yatafuata. Lakini kama unahitaji jambo lolote…Mwombe Mungu kwa bidii na kumwamini, utaona majibu…
Bwana anakupenda, Bwana anatupenda, na Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.
JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.
Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?
BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.
2Wakorintho 13:14 “Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote”.
Hii ni salamu ya kumalizia ambayo mtume Paulo aliwaandikia wakorintho, na watu wote watakaousoma waraka huo (ikiwemo mimi na wewe).
Maneno haya, yamegusa Nyanja zote tatu za Kusudi la Mungu kwetu sisi wanadamu.
> Paulo anaanza kwa kusema, Neema ya Bwana Yesu Kristo, ikae nasi; Akiwa na maana kuwa mpaka sisi tukamilike, mpaka sisi tushinde, tunaihitaji hii neema ya Yesu Kristo wakati wote itembee na sisi, tukipungukiwa neema, basi ni ngumu kuweza kuushinda ulimwengu. Na neema hii inaanza kutembea juu ya mtu kwa mara ya kwanza pale anapookoka.
> Anasema tena, Pendo la Mungu likae nasi: Ni kwa njia ya upendo Mungu alitukuomboa (Yohana 3:16). Hivyo na sisi tukiukosa Upendo, haijalishi tutakuwa washirika wazuri kiasi gani, haijalishi tutafanya miujiza mingi kiasi gani, tutanena kwa lugha za malaika nyingi kiasi gani, bado sisi tutabakia kuwa si kitu. Hivyo Pendo la Mungu linapokaa ndani yetu basi Mungu anakuwa karibu na sisi. Na pendo la Mungu ndio lile linalozungumziwa katika 1Wakorintho 11:1-8
Na ndio huo Paulo alikuwa analiombea kanisa ukae ndani yao.
> Anamalizia na kusema pia Ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote; Hii ikiwa na maana palipo na Roho Mtakatifu pana ushirika.. Sisi kama wakristo tuliookoka ni jukumu letu kuutunza ushirika wa Roho tukinia mamoja, tukiifanya kazi ya Mungu..
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. 4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. 5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. 6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.
Mambo haya matatu yakienda pamoja na sisi, basi Mungu naye ataenda pamoja na sisi, lakini tukipungukiwa kimoja wapo, aidha neema, au Upendo, au Ushirika, ni ngumu kusimama kama Kanisa.
Hivyo mimi na wewe tujitathmini ni wapi, hatujakamilisha, kisha tukamilishe, Na Bwana atusaidie.
UNYAKUO.
KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?
JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?
ADAM NA EVA.
Jiunge na channel yetu ya Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/GWxBOH2GXncIc0pwVIhnch
Unaweza ukawa unapitia wakati mgumu, mateso, majaribu, jangwa, au shida. Kama mkristo, imani yako inaweza kujaribiwa. Lakini Biblia peke yake ndiyo inayoweza kukupa faraja ya kweli. Haijalishi maneno elfu kumi ya faraja kutoka kwa wanadamu, Biblia peke yake inaweza kukupa utulivu wa kweli.
“Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.
“Usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”.
“Bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.
“Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana Bwana, Mungu wako, yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha”.
“Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo”.
“Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili”.
“Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza”.
“Kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi”.
“Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana Bwana YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu”.
“Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”.
“Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani”?
“Iweni hodari, mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja Bwana”.
“Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele”.
“Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani”.
“Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.
“Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu”.
“YEHOVA, aliye Bwana, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka”.
“Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.
“Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu”.
“Kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu”.
“Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.
“Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu”.
“Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini”.
“Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.
Mada zaidi zinazohusu Faraja: FARAJA FORUMS
Inawezekana hujaokoka, lakini leo hii unataka Yesu asikupite bila kuyaokoa maisha yako. Ikiwa umeamua kumgeukia Mungu kwa moyo wako wote, yeye mwenyewe anasema:
“Kila ajaye kwangu sitamtupa Nje kamwe”.
Leo hii Yesu ataingia ndani ya maisha yako kama umeamua kweli kumfuata. Fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa Sala ya Toba: KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ikiwa unataka, naweza pia kuunda meta description na SEO keywords zinazofaa ili chapisho hiki kionekane vizuri kwenye Google, bila kubadilisha maneno.
Je, nifanye hivyo pia?
NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.
RABI, UNAKAA WAPI?
MAONO YA NABII AMOSI.