Safari ya mbinguni.

Safari ya mbinguni.

Safari ya kwenda mbinguni ni safari isiyo na siku ya kupumzika. Kama vile moyo unavyodunda bila kusimama kwa miaka na miaka…Ndivyo safari ya Mbinguni ilivyo.. Ni mwendelezo kila kukicha, tukilala, tukiamka tupo safarini.

Hivyo ni lazima kulikumbuka hilo. Na safari ya kwenda mbinguni ni ngumu kuliko ya kwenda kuzimu.  Hata katika hali ya kawaida, kupanda juu ni kugumu kuliko kushuka… Ukitaka kushuka kilima unaweza kujiachia tu ukaserereka mpaka ukafika chini, pasipo kutumia nguvu yoyote. 

Lakini upandapo kilima huwezi kujiachia, ni lazima kupambana na kutumia nguvu nyingi ili kufika juu. Na safari ya kwenda mbinguni ipo hivyo hivyo. Kila hatua ni ya kujishika usianguke.  Kwasababu ipo nguvu itakayotuvuta chini  tusipojishika vizuri.

1Wakorintho 10:12 “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Hivyo ni lazima tujiangalia sana! kwasababu kubomoa ni rahisi kuliko kujenga, mahali tunapoishi, mahali tunapofanyia kazi, mazingira tunayoishi n.k Ni lazima kuhakikisha hayaharibu imani yetu na wala hayakwamishi safari yetu ya kwenda mbinguni.

Mbingu ipo! na Kristo Mwana wa Mungu anarudi!. 

Bwana akubariki.


Mada Nyinginezo:

IPELEKE SADAKA YAKO MAHALI SAHIHI,ILI UBARIKIWE.

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments