Title August 2020

HASIRA YA MUNGU KUKUWAKIA, KWA KUTOMZUNGUZIA TU MUNGU IPASAVYO.

Shalom, karibu tena tujifunze maneno ya uzima ya Mungu wetu YEHOVA.

Kuna wakati Mungu anaweza kukaa kimya na kuruhusu mambo Fulani yatokee, ili aone watu wake watamzungumziaje kuhusu jambo hilo, Na hapo ndipo tunapopaswa tuwe makini, kwasababu mtu akikosa kujua makusudi ya Mungu ni nini, halafu akamzungumzia tu kutokana na mawazo yake au uonavyo yeye, anaweza kujisababishia hasira yake iwake juu yako.

Kuna jambo moja la namna hiyo ambalo lipo hasaa kwetu sisi watu wa kanisa la Laodikia, ambalo tunamzunguzia Mungu isivyopasa. Kosa hilo lilifanywa na watu wa kale na sisi bado tunataka kulirudia Na leo hii tutaliona katika biblia.

Kosa lenyewe lilifanywa na wale marafiki watatu Ayubu (yaani Elfazi, Sofari na Bildadi). Mawazo yao yalianzia pale, walipoona Mungu kamletea Ayubu majanga makubwa kama tunavyoyasoma katika biblia.. Walipoona ghafla mali za Ayubu zimepukutika, baadaye tena familia yake ikaondoka, na zaidi ya yote, magonjwa ya mauti yakawa yanamwandama…

Hivyo hawa marafiki zake watatu ambao walikuwa ni wenye hekima kweli kama yeye, na wakati mwingine wenye upendo, kiasi kwamba kufunga safari toka mbali kuja kumfariji Rafiki yao, na kulia naye, ni jambo la upendo mwingi..Lakini walikosa kujua kitu kimoja..Wao walidhani kigezo pekee cha mtu kukubaliwa na Mungu ni kuwa na mali, na utajiri, na mafanikio na Maisha mazuri basi…

Hivyo watu wote waliokuwa wanawaona barabarani kama matajiri, na wenye mali, walihitimisha kuwa ni marafiki wa Mungu wakubwa, Halikadhalika wale wanaopatwa na matatizo na shida, wanatumika chini ya laana kubwa ya Mungu..Hilo tu ndilo lilikuwa kikwazo kwao, lakini mengine yote hawakuwa na hatia..

Sasa ulipofika wakati wa Rafiki yao kipenzi Ayubu kukutwa na majanga kama yale, ndipo wakahitimisha kuwa Ayubu sasa kuna mahali alimkosea Mungu, tena mahali pakuwa sana, na hivyo ni lazima akiri, na atubu makosa yake, wakawa wanamshurutisha kwa nguvu, wakijaribu kushuhudia mabaya yake kwa kila namna..kwa kumwambia maneno kama haya:

Ayubu 4:7 “Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi?

8 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.

9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika”.

Ayubu 8:3 “Je! Mungu hupotosha hukumu? Au, huyo Mwenyezi hupotosha yaliyo ya haki?

4 Kwamba watoto wako wamemfanyia dhambi, Naye amewatia mkononi mwa kosa lao;

5 Wewe ukimtafuta Mungu kwa bidii, Na kumsihi huyo Mwenyezi;

6 Ukiwa wewe u safi na mwelekevu; Hakika yeye sasa angeamka kwa ajili yako, Na kuyafanya makazi ya haki yako kufanikiwa.

7 Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, Lakini mwisho wako ungeongezeka sana.

Ayubu 15:34 “Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, Na moto utateketeza mahema yenye rushwa”.

N.k n.k, hatuwezi kuorodhesha mistari yote hapa, lakini soma kitabu cha Ayubu kuanzia sura ya 4-25, utaona, msimamo wao hao watu jinsi ulivyokuwa mkali na ule ule, Kwamba Ayubu kupatwa na misiba ile ni matokeo ya uovu wake aliomtendea Mungu, Pamoja na familia yake..

Lakini kwasababu Ayubu alikuwa anamjua Mungu vizuri, hakuhitimisha kuwa kupitia shida, au mtu kuwa maskini au kupungukiwa ni kwamba Mungu amekukataa, badala yake alianza kuwaeleza siri ambayo walikuwa hawaijui akawaambia, wapo watu ambao wamemkataa Mungu, ambao hawaamini hata uweza wa Mungu, lakini Mungu huyo huyo anawapa, afya, amebariki kazi za mikono yao, amewafanikisha kwa kila kitu watakacho, na zaidi ya yote wamepewa Maisha marefu, lakini mwisho wa siku watakufa na watashuka kuzimu kwa ghafla…Hivyo kigezo cha kufanikiwa sio kigezo kuwa Mungu amekukubali..

Ayubu 21:7 “Mbona waovu wanaishi, Na kuwa wazee, naam, na kuongezeka kuwa na nguvu?

8 Kizazi chao kinathibitika nao machoni pao, Na wazao wao mbele ya macho yao.

9 Nyumba zao zi salama pasina hofu, Wala fimbo ya Mungu haiwapigi.

10 Fahali wao huvyaza wala hapungukiwi na nguvu; Ng’ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba.

11 Huwatoa kama kundi watoto wao. Na watoto wao hucheza.

12 Huimba kwa matari na kwa kinubi, Na kuifurahia sauti ya filimbi.

13 Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula.

14 Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee; Kwani hatutaki kuzijua njia zako.

15 Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie? Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?

16 Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao; Mashauri ya waovu na yawe mbali nami.

17 Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimishwa? Na msiba wao kuwajilia? Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake?

18 Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo, Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba”?

Unaona? Hata baada ya kuelezwa maneno hayo, hilo halikuwafanya marafiki wa Ayubu wabadilishe mitazamo yao, msimamao wao bado ulikuwa ni ule ule, kwamba Ayubu kakosea mahali!, ndio maana yale yote yamempata…Mungu kamwe hawezi kuruhusu mabaya kama yale yamkute mja wake..hilo haliwezekani,

Lakini mwisho kabisa mwa kitabu cha Ayubu tunaona Mungu anasimama na kuanza kuzungumza sasa, akamwambia Ayubu maneno yafuatayo..

Ayubu 42:7 “Basi ikawa, baada ya Bwana kumwambia Ayubu maneno hayo, Bwana akamwambia huyo Elifazi Mtemani, HASIRA ZANGU ZINAWAKA JUU YAKO, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi HAMKUNENA YALIYO SAWA KATIKA HABARI ZANGU, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.

8 Basi sasa, jitwalieni ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba, mkamwendee mtumishi wangu Ayubu, mjisongezee sadaka ya kuteketezwa; na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi; kwa kuwa nitamridhia yeye, nisiwatende sawasawa na upumbavu wenu; kwani ninyi HAMKUNENA MANENO YALIYONYOKA KATIKA HABARI ZANGU, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu”

Ni lipi tunafundishwa?

Kwa bahati mbaya, hata sasa mawazo kama haya mabovu yapo vichwani mwa baadhi yetu (Hususani wahubiri wa leo). Tunamwazia Mungu katika utajiri tu na mafanikio? Na mahubiri yetu kila siku ni hayo, na tunatumia mistari baadhi baadhi ya kusimami, kama walivyofanya wakina Bildadi, Sofari na Elfazi.

Ndugu unayosoma ujumbe huu, ikiwa na wewe unamnenea Mungu maneno kama hayo, ikiwa na wewe unamuhubiri Mungu kwa njia hiyo tu, ikiwa biblia unayoisoma unaona mistari tu kufanikiwa kimwili, na unawafundisha wengine hivyo..angalia sana..Hasira ya Mungu isije ikawa juu yako.

Kumbuka: (Sio kwamba tusihubiri mafanikio, la! Kwa Mungu yapo mafanikio, makubwa sana! lakini usihubiri kwamba wote ambao hawajafanikiwa na maskini wamepungukiwa na kitu kwa Mungu wao, hapo utakuwa hujamzungumzia Mungu vizuri). Hata ufanyaje huwezi elewa njia zote za Mungu, hivyo epuka kulazimisha kila jambo, na kutaka liwe kama wewe unavyotaka liwe. Sio kila mtu mwenye ulemavu ana laana!, sio wote wenye magonjwa ya muda mrefu yasiyopona kafungwa na nguvu za giza!..sio vipofu wote unaowaona au viziwi ni laana inawafuata… Wengine Mungu karuhusu wawe hivyo kwa makusudi yake yeye (kasome Yohana 9:1-3)

Yakobo 2:4 “ Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?”

1Wakoritho 10:11 “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Jehanamu ni nini?

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/FgA1HWRFZWH4IqqLunFGcs

Mistari ya biblia kuhusu ndoa  ni ipi?


Ndoa ni tendo ambalo Mungu aliliumba kwa makusudi kabisa, ili kumpa mwanadamu picha ya jinsi ndoa yake halisi itakavyokuwa kati ya yeye na watu wake, baada ya ulimwengu huu kuisha. 

Uhusiano walio nao mke na mume, ni mfano mdogo sana wa uhusiano atakaokuwa nao Mungu na watu wake watakaoshinda, katika mbingu mpya na nchi mpya.

Hivyo tutaitazama mistari michache ihusuyo ndoa za kibinadamu, na vilevile tutaitazama mistari michache ihusuyo ndoa ya ki-mbinguni(yaani Kristo na kanisa lake).

NDOA YA MKE NA MUME

Mwanzo 2:24 “Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja”

Waefeso 5:25  “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake”;

Waefeso 5:33  “Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe”

Mithali 5:18 “…. Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako”

Waefeso 4:2  “kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; 3  na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani”.

Marko 10:9  “Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe”

Wimbo 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu. 

7 Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa”.

Waebrania 13:4  “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu”.

Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu. 

19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana”.

Mithali 31:10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani”.

Mhubiri 4:9 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao. 

10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua! 

11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto”?

Mathayo 19:6  “Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe”

1Petro 3:7  “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe”

Malaki 2:16 “Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli…”

Ruthu 1:16 “Naye Ruthu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu; 

17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe nami”.

Yohana 13:34  “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo”.

1Wakorintho 13:4  “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5  haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya”;

Malaki 2:14 “Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako. 

15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana”.

Mistari ya biblia kuhusu ndoa ya;

KRISTO NA KANISA LAKE.

Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

Isaya 54:5 “Kwa sababu Muumba wako ni mume wako; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote”.

2Wakorintho 11:2  “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi”.

Ufunuo 19:9  “Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

Ufunuo 21:1  “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2  Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe”.

Luka 14:24  “Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.

Luka 5:34 “ Lakini Yesu akawaambia, Je! Mwaweza kuwafanya wafunge walioalikwa arusini, akiwapo bwana arusi pamoja nao”?

Ufunuo 21:9 “…Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo”.

Mathayo 25:1  “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.

2  Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.

3  Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;

4  bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.

5  Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.

6  Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.

7  Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.

8  Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.

9  Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.

10  Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.

11  Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.

12  Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.

13  Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.

Ufunuo 22:17  “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.

Hivyo ni wajibu wetu mimi na wewe kuhakikisha kwa gharama zozote hatuikosi hii karamu ya mwana-kondoo mbinguni, Kumbuka kama tunavyojua huwa kinaanza ndoa kisha baadaye karamu,.vivyo hivyo na kwa Mungu pia, inaanza kwanza ndoa, ambayo Kristo anafunga na watakatifu wake hapa hapa duniani, na baadaye atawanyakua kwenda nao kula naye karamu kule mbinguni.

Kwa mapana na marefu juu ya somo hili la karamu ya mwanakondoo, angalia somo lililoorodheshwa chini baada ya hili; Lakini kikubwa zaidi, ni kuwa tuhakikishe na sisi ni bibi-arusi ambao wapo tayari kumkojea Bwana wao aje waende karamuni.

Na tunakuwa bibi-arusi kwa kumwamini Yesu, na kubatizwa, na kuishi maisha yampendezayo.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda tukuunge kwenye group la mafundisho ya biblia,Whatsapp: basi utatutumia ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

https://wingulamashahidi.org/mafundisho-ya-ndoa/

UTAWALA WA MIAKA 1000.

MJI WENYE MISINGI.

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MIHURI SABA

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.

Historia ya nyimbo KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili~ Tis So Sweet to Trust in Jesus.


Wimbo huu uliandikwa na mwanamke mkristo wa kiingereza aliyeitwa, Louisa M. Stead, Mnamo mwaka 1882, Ni wimbo unaoeleza furaha mtu anayoweza kuipata katika kumtegemea Kristo, Lakini nyuma ya uandishi wa wimbo huu, imelala historia nzito ya Maisha aliyopitia Louisa M stead,

Ilikiwa ni siku moja Louisa na mumewe Pamoja na mtoto wao wa kike aliyeitwa Lily, walipanga safari ya kwenda matembezi, wakiwa ufukweni mwa kisiwa kimoja ghafla walisikia  sauti kama ya mtu inapiga kilele za kuzama, kwenda kukimbia kuangalia wakamwona kijana mmoja, hilo lilimfanya mume wa Louisa, ajaribu kwenda kumwokoa, lakini katika jitihada zake za kufanya hivyo kwa bahati mbaya wote wawili wakazama, wakafa (kijana Pamoja na mume wake), mbele ya macho ya Louisa na binti yake.

Maisha yao baada ya hapo yalianza kuporomoka, Maisha yakawa magumu, Lakini wakagundua kuwa Mungu hakuwaacha katika hali zao, aliwatimizia mahitaji yao, hapo ndipo Louisa na binti yake walijifunza kumtegemea Mungu, na ndipo akauandika wimbo huu;

Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa;
Kukubali Neno lake,
Nina raha moyoni.
 
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.
 
Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa,
Kuamini damu yake,
Nimeoshwa kamili.
 
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.
 
Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa;
Kwake daima Napata,
Uzima na amani.
 
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.
 
Nafurahi kwa sababu,
Nimekutegemea
Yesu,Mpendwa na Rafiki,
Uwe nami dawamu.
 
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.

*****

Baadaye Louisa na binti yake wakasafiri kwenda Afrika kusini kwa kazi ya umishionari.

Lakini ni nini tunajifunza katika wimbo huu na uandishi wake?

Mimi na wewe tunaweza tukawa hatujapitia katika hali ngumu kama aliyopitia yeye, lakini yeye aliyeyapitia amemwona Mungu akimpigania, mpaka anaimba na kusema, “Nimemwona thabiti”..Hiyo ni kuonyesha kuwa hata wewe ukimwamini Yesu na kumtegemea, ..Utamwona thabiti/hakika akiwa na wewe katika maisha yako haijalishi leo unapitia mahali pagumu kiasi gani.

Imba wimbo huu ukikumbuka matendo yote makuu aliyokutendea nyuma. Na hakika utausikia uwepo wake nafsi mwako.

Bwana akubariki.

Tazama chini historia za nyimbo nyingine za Tenzi.

Tafadhali share na wengine.

Mada Nyinginezo:

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

MWAMBA WENYE IMARA

USINIPITE MWOKOZI Lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya Shalom na Maran atha

Utauwa umewahi kusikia maneno haya mawili yakitamkwa miongoni mwa wakristo. (Shalomu na Maranatha) Lakini pengine huelewi maana yake!.

Nini maana ya Shalomu?

Shalomu au Shalom ni neno la kiebrania lenye maana ya “AMANI” Kwa kiingereza “PEACE”. Hivyo wayahudi pamoja na wakristo wa kanisa la kwanza walipokutana walisalimiana na kwa salamu ya neno hilo “Shalomu”.

Pia Mungu wetu jina lake ni YEHOVA-SHALOMU, maana yake “Mungu wa amani”

Waamuzi 6:22 “Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gideoni akasema, Ole wangu, Ee Bwana MUNGU! Kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso.

23 Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa.

24 Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri”.

Kasome pia Warumi 15:33, Warumi 16:20, Wafilipi 4:9, 1Wathesalonike 5:23, Waebrania 13:20

Na Bwana wetu Yesu anajulikana kama Mfalme wa Amani (kasome Isaya 9:6, Waebrania 7:2).

Hivyo kama Mungu wetu ni Mungu wa Amani na mwana wake wa pekee Yesu Kristo ni Bwana wa Amani, Basi na sisi pia tunapaswa tuwe watu wa Amani na watu wote ili tufanane na yeye, na sio Amani ya midomo tu! bali ya vitendo. Neno Shalom litokapo vinywani vyetu liwe ni udhihirisho wa kitu kinachoendelea katika maisha yetu kwamba tunayo Amani na watu wote. Na lisiwe linatoka tu vinywani na huku mioyoni mwetu kuna unafiki, shari na chuki. Ukitamka tu! na huku moyoni mwako kuna vinyongo na hasira, na shari basi utakuwa hujaelewa nini maana ya shalomu.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”

1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.

11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana“.

Maana ya Maran atha

Ni neno la kiebrania hivyo hivyo lenye maana ya “Bwana wetu anakuja” ni neno la Faraja kwa wakristo wote wanaomgonja Bwana....1Wakorintho 16:23

Bwana atubariki.

Shalom.


Tafadhali washirikishe na wengine na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Maana ya watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.

SWALI: Nini maana ya hili Neno “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa” (Hosea 4:6).


JIBU: Maarifa yanayozungumziwa hapo sio maarifa ya darasani.. ingawa hata hayo ya shuleni pia ni maarifa na yana nafasi yake katika maisha, lakini yaliyozungumziwa hapo sio hayo..

Maarifa yanayozungumziwa hapo ni maarifa ya kumjua Mungu.

Mithali 1:7 “Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu”

Hali kadhalika biblia inaposema “Mkamate sana Elimu, usimwache aende zake, maana yeye ndio uzima wako (Mithali 4:13)”.. Tafsiri ya kwanza ya mstari huo sio Elimu ya kidunia, bali ni elimu ya Ufalme wa Mbinguni.

Mathayo 13:51  “Yesu aliwauliza, Mmeyafahamu hayo yote? Wakamwambia, Naam.

52  Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye ELIMU YA UFALME WA MBINGUNI amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale”

Kasome pia (Yohana 7:15-17, Marko 1:27,1Timotheo 6:3-5, Matendo 17:18-34), Na pia kuna somo tuliloliandikwa lenye kichwa “Fahamu majira tuliyopo na nini unapaswa uwe nacho”, upatapo nafasi lipitie utapata kuelewa Zaidi.

Kwahiyo mbele za Mungu mtu asiye na Elimu ni yule asiyezijua siri za ufalme wa Mbinguni ikiwemo uweza wa Mungu, na mtu asiye na maarifa ni yule asiyeyajua maarifa ya kimbinguni (maana yake hajui chochote kuhusu Mungu), haijalishi atakuwa na Elimu ya kidunia kubwa kiasi gani; awe profesa, awe dokta awe waziri au awe mtu yeyote yule mwenye elimu kubwa..kama hana Elimu na Maarifa ya ufalme wa mbinguni, basi mbingu inamwona ni hana Elimu wala maarifa yoyote…Na hivyo Ataangamizwa.

Ikiwa uko kwenye soko, swisswatch.is jukwaa letu ni chaguo lako bora! Duka kubwa zaidi la ununuzi!

Sasa tukirudi kwenye huo mstari wa Hosea kuna kitu cha kujifunza Zaidi..Hebu tuusome tena kwa makini..

Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako”

Ukisoma kwa makini hapo inasema “watu wangu wanaangamizwa!” na sio “wanaangamia”..Maana yake ni kwamba mtu akikosa maarifa ya kimbinguni kuna kitu cha nje kitamwangamiza. Hataangamia tu peke yake..La! bali kuna kitu kitakuja kumwangamiza.

 Kwa lugha nyepesi ni kwamba maarifa ni kama “ULINZI”. Unapokuwa na maarifa mengi ya kumjua Mungu basi ni ngumu kushambuliwa na Adui yetu shetani na majeshi yake.

Mithali 1:26 “Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu, Nitadhihaki hofu yenu ifikapo; 

27 Hofu yenu ifikapo kama tufani, Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli, Dhiki na taabu zitakapowafikia.

 28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.

  29 KWA KUWA WALICHUKIA MAARIFA, WALA HAWAKUCHAGUA KUMCHA BWANA. 

30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote. 

31 Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.

 32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza. 

33 Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya”.

Kwahiyo ni jukumu letu kila mmoja kuyatafuta Maarifa ya Mungu kwa bidii ili tusiangamizwe!..Ukikosa maarifa ya ki-Mungu, utawaogopa wachawi, ukikosa maarifa ya ki-Mungu hutajua tunaishi siku gani hizi, na hivyo utapotea katika hiki kizazi, na mwisho kwenda kuangamizwa katika moto wa milele.

Bwana atubariki.

Mada Nyinginezo:

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

MSHIKE SANA ELIMU.

CHEMBE YA NGANO ISIPOANGUKA KATIKA NCHI, IKAFA,

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.

KUMCHA MUNGU NI NINI? NA MTU ANAMCHAJE MUNGU?

DAKIKA MOJA TU, INAKUFANYA UMWAMINI SHETANI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.

Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate ‘Neno la siku’ kila asubuhi. Na mistari mingine mingi ya faraja ..kwa link hii >>>> https://chat.whatsapp.com/LO2BncRILtiAlnRYfZWG2V

Mistari ya biblia ya uponyaji.


Inawezekana wewe ni mgonjwa na pengine unapitia katika hali ya kukata tamaa kabisa ya kupona, au unao ugonjwa usioponyeka mfano Ukimwi au Kansa, lakini nataka nikuambie jambo moja, kwa mwanadamu ni kweli haiwezekani lakini kwa Mungu hakuna linaloshindikana,

Hapo kabla nilikuwa ninasikia tu shuhuda za watu wengine kuponywa, nikadhani pengine mimi sistahili, lakini nilipokuwa katika dhambi siku moja Yesu Kristo aliniponya ugonjwa wangu wa sikio uliokuwa unanisumbua kwa muda mrefu, Na hapo ndipo ulipokuwa mwanzo wa kumtazama Kristo kwa sura nyingine, na kuendelea hapo aliniponya mara kadhaa tena katika vipindi tofauti tofauti nilipougua..Kama alinifanyia mimi niliyekuwa na dhambi, atakufanyia na wewe pia.

Kwa maana Yesu mwenye upendo yeye mwenyewe alituambia hivi..

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.

Hivyo nawe pia unapoitafakari mistari hii, nakuombea kwa Mungu ikafanyike Uponyaji mkubwa ndani ya mwili wako na maisha yako kwa ujumla, katika jina la YESU KRISTO.

Ifuatayo ni mistari ya biblia ya uponyaji:

Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.

Zaburi 30:2 “Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya”.

Ufunuo 21:4 “Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita”.

2Wafalme 20:5 “Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa Bwana”.

Zaburi 146:8 “Bwana huwafumbua macho waliopofuka; Bwana huwainua walioinama; Bwana huwapenda wenye haki”;

3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”.

Yeremia 17:14 “Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu”.

Zaburi 118:17 “Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana”.

Zaburi 119:50 “Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imenihuisha”.

Mathayo 8:17 “ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu”.

Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake,

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Mathayo 14:14 “Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao”.

Yeremia 30:17 “Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye”.

Isaya 57:18 “Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia. 19 Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema Bwana; nami nitamponya”.

1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.

Mathayo 9:35 “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina”.

Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana

Yakobo 5:14 “Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana”.

Zaburi 6:2 “Bwana, unifadhili, maana ninanyauka; Bwana, uniponye, mifupa yangu imefadhaika”.

Mathayo 8:1 “Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.

2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.

3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika”.

2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwafuraha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu”.

Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao,

Zaburi 107:19 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao,

21 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.”.

Zaburi 103:2 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote.

3 Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote”

Kumbukumbu 7:15 “Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako maradhi yo yote mabaya uyajuayo ya Misri, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao”.

Hosea 14:4 “Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha”.

na kwa kupigwa kwake mliponywa

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;

3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

*****

Amini!, Endelea kuamini, uponyaji wako hakika umekufukia.

Tafadhali Share, na kwa wengine ujumbe huu wa faraja,.

Pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya biblia kwa njia ya email au  kwa Whatsapp tutumie ujumbe kwa namba hii: +255693036618 / +255789001312

Mada Nyinginezo:

YESU MPONYAJI.

Aponywa Ukimwi.

Ameponywa kansa iliyokuwa katika hatua ya Nne.

RABI, UNAKAA WAPI?

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

MWAMBA WENYE IMARA

Rudi Nyumbani:

Print this post

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. Na mistari mingine mingi ya faraja ..kwa link hii >> https://chat.whatsapp.com/LO2BncRILtiAlnRYfZWG2V

Mistari ya biblia kuhusu upendo.


Upendo ndio nguzo ya kwanza katika Ukristo. Unaweza ukawa na vyote, lakini ukikosa upendo wewe mbele za Mungu  si kitu kabisa,

Biblia inazungumza juu ya  upendo wa aina 4:

  • Upendo wa kuwapenda wengine.
  • Upendo wa mke na mume
  • Upendo kwa maadui
  • Upendo wa ki-Mungu

Mistari ya Upendo wa kwa wengine:

1 Wakorintho 13:1-8

1 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.

4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.

Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo. (1Yohana 4:8)

Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.(1Petro 4:8)

Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.

35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi. (Yohana 13:34-35)

Kuchukiana huondokesha fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote.  (Mithali 10:12)

Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. (1Yohana 4.11)

Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.(1Wakoritho 16:14)

 

Mistari ya upendo kwa walio katika mahusiano (Mke na Mume)

Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana. Ninyi waume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao.(Wakolosai 3:18-19)

Kitambo kidogo tu nikiisha kuwaondokea, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena, Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu, Chumbani mwake aliyenizaa. (Wimbo 3:4)

Mkono wake wa kushoto ungekuwa chini ya kichwa changu, Nao wa kuume ungenikumbatia. (Wimbo 8:3)

Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu.( Wimbo 8: 6)

Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.

Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.

Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe. (Marko 10:6-9)

 

Mistari ya kuwapenda maadui zako.

Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi,

wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.

 Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang’anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.

 Mpe kila akuombaye, na akunyang’anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.( Luka 6:27-30)

Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu. (Mathayo 5:43-48)

Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake. (Warumi 12:20-21)

Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.(Warumi 12:21)

 

Mistari ya Upendo wa Mungu.

Upendo huu ndio upendo wa hali ya juu kuliko yote (Agape), upendo wa kujitoa wakfu, usiojali hali, usiojali uzuri au ubaya wa mtu, usio na chembe yoyote ya mapungufu, Upendo wa Mungu.

Ikiwa uko kwenye soko la superclone, https://www.swisswatch.is/product-category/richard-mille/rm-022/ Super Clone Rolex ndio mahali pa kwenda! Mkusanyiko mkubwa zaidi wa Rolex bandia hutazama mtandaoni!

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (Yohana 3:16)

Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye.

Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.

Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.

Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu. (1Yohana 4:9-12)

Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza. (1Yohana 4:19)

Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi.

Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. (Yohana 15:12-13)

Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu; (Kumbukumbu 7:9)

*****

Hivyo mimi na wewe ili Upendo wa namna hii uingie ndani yetu, Ni sharti kwanza tumpende yeye mwenye Upendo huo.

Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. (1Yohana 4:16)

Hiyo ndilo kusudi la kwanza la sisi kuwepo hapa duniani..Kumpenda Yeye.

Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. (Marko 12:29-30)

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUMCHA MUNGU NI NINI? NA MTU ANAMCHAJE MUNGU?

Kumcha Mungu ni kukoje?


Kumcha Mungu ni Neno la jumla, linalomaanisha kujishughulisha na mambo yote yanayompendeza Mungu ikiwemo; kumpenda, kumtii, kumwogopa, kuchukia uovu, kumtumikia yeye, kufanya mapenzi yake, kumwabudu, kumfanyia ibada n.k. hiyo ndio maana ya kumcha Mungu..Ni tendo la jumla linalomaanisha kufanya mambo yote anayotaka wewe uyafanye.

Na ni  jukumu la kila mwanadamu chini ya jua kumcha Mungu. Na biblia imetoa faida nyingi za kufanya hivyo.

Tutaziorodhesha faida chache hapa, naamini kwa kuzijua hizo itakusaidia na wewe ambaye bado hujajua faida za kumtii Mungu, kukupa hamasa na wewe uanze kufanya.

  1. Faida ya kwanza kabisa ni kuwa unapata uzima wa milele.

Mithali 14:27 “Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti”.

Unaona unapokusudia kusema leo, naanza kumtafuta Mungu, basi hapo hapo tayari unafungua mlango wa chemchemi za uzima wa milele kububujika ndani yako.

    2. Kumcha Mungu unafungua mlango wa maarifa:

Mithali 1:7 “Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu”.

Leo hii ukachagua kumtafuta Mungu katika maisha yako, ukajinyima kufuatana na njia za ulimwengu, basi Mungu anakupa zawadi nzuri sana ijulikanayo kama  maarifa..Maarifa hayo mtu mwingine yoyote hawezi kupewa, Ukiwa unaendelea tu kuishi maisha ya kumpendezesha Mungu, kuna kipindi kitafika utaanza kuona mabadiliko  fulani ndani yako ambayo yatakutofautisha ki-uelewa wewe na Mtu mwingine.

Mfano tunamwona Danieli na Wenzake watatu (Shedraki, Meshaki, na Abednego), wao walipoitwa na mfalme walichagua fungu la kumcha Mungu kuliko kujifurahisha na vyakula najisi vya kifalme..Na hiyo ikawapelekea baadaye mwishoni walipokuja ku-dahiliwa na mfalme, wakaonekana wao ni bora mara 10 zaidi ya wale wenzao waliokuwa wanajifurahisha katika vyakula vya kifalme.

Danieli 1:17 “Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieli naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto.

18 Hata mwisho wa siku zile alizoziagiza mfalme za kuwaingiza, mkuu wa matowashi akawaingiza mbele ya mfalme Nebukadreza.

19 Naye mfalme akazungumza nao; na miongoni mwao wote hawakuonekana waliokuwa kama Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria; kwa hiyo wakasimama mbele ya mfalme.

20 Na katika kila jambo la hekima na ufahamu alilowauliza mfalme, akawaona kuwa walifaa mara kumi zaidi ya waganga na wachawi waliokuwa katika ufalme wake”.

Hivyo na wewe ukiamua leo kumcha Mungu, yaani kutafuta kuyatenda mapenzi yake yapo maarifa mengine yatokayo mbinguni yataingia ndani yako kukutofautisha na ulimwengu wote.

      3.Kumcha Mungu, unapata hekima;

Zaburi 111:10 “Kumcha Bwana ndio mwanzo wa hekima, Wote wafanyao hayo wana akili njema, Sifa zake zakaa milele”.

Sulemani alichagua kwanza kumcha Mungu, ndipo akapata hekima ambayo  iliwazidi watu wote ulimwengu..Hekima inakusaidia kupambanua mambo, inakusaidia kuelewa hata maandiko..Leo hii unaweza kusoma biblia usiielewe, lakini ukiwa ni mtu wa kutafuta kumjua Mungu na kuzidi kutaka kujifunza kutenda mapenzi yake, hekima hiyo Mungu anaileta ndani yako, na kujikuta unapata ufahamu wa kuyaelewa maandiko, na kupambanua mambo.

4.Kumcha Mungu kunaongeza siku za kuishi.

Mithali 10:27 “Kumcha Bwana kwaongeza siku za mtu; Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa”.

Kama ulidhani ni kuwaheshimu tu wazazi ndio kunaongeza siku za kuishi..Basi leo ujue kuwa ukiishi kwa kumpendeza Mungu nako pia kunazidisha siku zako za kuishi duniani. Mwangalie Ibrahimu, mwangalie Ayubu, mwangalie Yakobo n.k. hawa wote walikuwa ni wacha Mungu, na Mungu akawapa maisha marefu.

  5.Kumcha Mungu ni ulinzi kwa watoto wako.

Mithali 14:26 “Kumcha Bwana ni tumaini imara; Watoto wake watakuwa na kimbilio”.

Ukijibidiisha wewe kumtumikia Mungu, faida zake haziishi tu kwako, bali mpaka wa watoto wako,utakapokuwa haupo duniani,  ndivyo ilivyokuwa kwa watoto wa Ibrahimu, na watoto wa Yakobo na watoto wa Yusufu,

   6. Kumcha Bwana ni utajiri.

Mithali 22:4 “Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha Bwana Ni utajiri, na heshima, nayo ni uzima”.

Kama ukijibidiisha kuifanya kazi yake, Mungu anakupa na utajiri pia juu yake, wakati wake ukifika..

Bwana Yesu alisema..

Marko 10:29 “Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,

30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele”.

Hizo zote ni faida zitokanazo na mtu Yule anayejishughulisha na mambo ya Mungu.

Lakini utawezaje kuishi maisha ya kumcha Mungu?

Ikiwa wewe umeokoka tayari, ni biblia pekee ndio itakayokuwa msaada wako wakati wote.Ukiwa msomaji wa Biblia itakayokusaidia kulifanya lile joto la kumcha Bwana liendelee kudumu ndani yako.. Lakini ukiwa sio msomaji wa biblia, yaani ni mivivu, ni rahisi kulipunguza kama sio kuacha kabisa kuyafanya mapenzi ya Mungu, biblia ni mwanga hiyo pekee ndio inatoa faraja, inatoa tumaini, inatia nguvu, inaonya, inakumbusha, inaongoza, inashauri..Hivyo ikiwa wewe ni msomaji mzuri wa biblia ni rahisi kwako kuishi maisha ya kumcha Mungu sikuzote..

Na ndio maana Mungu aliwapa wana wa Israeli, mpaka na wafalme maagizo haya kujifunza torati daima;

Kumbukumbu 17:18 “.. ajiandikie nakala ya torati hii katika chuo, kufuata hicho kilicho mbele ya makuhani Walawi;

19 na awe nayo, asome humo siku zote atakazoishi; ili apate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wake, ayashike maneno yote ya torati hii na amri hizi, kwa kuyafanya;

Hivyo nawe pia jifunze biblia kwa muda mwingi uwezavyo. Na pia jitenge na mambo maovu

Mithali 8:13 “Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia’.

Kwa kufanya hivyo faida zote tulizo zihorodhesha hapo juu zitakuja juu ya maisha yako.

Lakini kama hujaokoka,  na unataka leo uanze safari yako na Mungu, basi uamuzi, huo ni mzuri, hapo ulipo Bwana anaweza kukusamehe na kukuokoa kabisa..Ikiwa tu utakuwa tayari kutubu kwa kumaanisha..Hivyo kama  upo tayari kufanya hivyo basi bofya hapa, kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe: +255 789001312

Mada Nyinginezo:

RABI, UNAKAA WAPI?

WEWE NI BWANA UNIPONYAYE.

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

MANENO ALIYOWEZA KUTAMKA YESU TU PEKE YAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

FAHAMU MAJIRA ULIYOPO NA NINI UNAPASWA UWE NACHO.

Kiwango cha uelewa kuhusu wokovu au Mungu waliokuwa nacho Kiwango cha uelewa, hutupaswi tuwe nacho sisi kwa wakati huu, tunapaswa tuende zaidi ya pale, Hata mambo ya kidunia yanatufundisha, elimu ya kidato cha 4 aliyokuwa nayo mtu wa mwaka 1960, Si sawa na elimu ya kidato cha 4 aliyonayo mtu wa sasa hivi.

Wakati ule, elimu hiyo ilimtosha mtu kupata kazi hata ngazi za juu katika mashirika makubwa, lakini kwa sasahivi elimu hiyo haina thamani yoyote japokuwa ni elimu ile ile.

Ndivyo ilivyo hata katika ukristo, wakati mwingine unajiuliza ni kwanini hauisikii nguvu ya wokovu ndani yako, japokuwa utasema umeokoka, na umefuata vigezo vyote vya kuokoka kama tu watu wa kale walivyofanya, lakini bado huoni ndani yako moto kama waliokuwa nao wale, Ni kwasababu tunataka tuishi kama watu wa zamani, kama kipindi cha mitume, kama kipindi cha Martin Luther, kwamba ukimkiri Yesu kwa kinywa ya kuwa ni Bwana na tena ukaamini kwamba alikufa akafufuka utaokoka (Warumi 10:9)..Hilo tu basi!..

Kwa kudhani kwamba hilo tu linatosha kutufanya tuimalize hii safari salama. Ndugu hilo lilitosha kwa wakati wao, ambao kwanza hawakupata neema ya kuwa na mikusanyiko ya vitabu vyote vya maandiko kama tulivyonavyo sisi, Au kama walikuwa navyo basi hawakuruhusiwa kuvisoma (Fuatilia historia utaona), hiyo ni moja, pili, shetani alikuwa hafanyi kazi kwa nguvu kama anavyofanya sasa hivi.

Ikiwa hutaki kuongeza maarifa yako kuhusu Mungu katika nyakati hizi, na umeng’ang’ana tu kusema mimi nilishaokoka basi, nataka nikuambie kuwa ukristo wa namna hiyo safari hii hautakufikisha popote. Hilo pekee halitoshi kukufikisha popote, wala kutufikisha popote!.

Hili ndio kanisa pekee linaloonekana lina makundi mawili ya wakristo (yaani Wanawali werevu na Wanawali wapumbavu. Math.25). Ikiwa na maana kutakuwa na wakristo wenye bidii ya kupata maarifa, na wakristo ambao hawatakuwa na ujuzi wowote mioyoni mwao, na biblia inaonyesha  wale werevu tu ndio watakaoenda kwenye unyakuo. Jambo hilo halikuwahi kuonekana katika vipindi vyote vya kanisa huko nyuma..

Na katika wakati ambao ni mgumu kuliko wakati wote uliowahi kutokea katika historia ya dunia basi ni huu!, kwasababu hili ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, “ndio tonge la mwisho linalokomba mboga yote” na shetani analijua hilo, huu ndio wakati wake wa kufanya kazi kwa nguvu zaidi ili kuwaangusha wengi, Hivyo wewe na mimi tunaojiita mkristo tusipojua ni nini tunapaswa tuwe nacho kwa majira haya, ndugu basi tumekwisha!.

Ukisoma kitabu cha Ufunuo, utaona wapo wale wenye uhai 4, wanaosimama mbele ya kiti enzi cha Mungu, mmoja akiwa na uso kama wa Simba, mwingine wa Ndama, mwingine kama wa mwanadamu na Mwingine kama wa Tai (Ufu 4:7).

Sasa hizo nyuso zao na mionekanayo yao sio urembo tu, hapana bali zilikuwa zinafunua nguvu za Roho Mtakatifu katika nyakati tofauti tofauti za kanisa..Sasa mwenye uhai wa kwanza hadi yule wa Tatu, walifanya kazi kwa vipindi vya makanisa 6 ya mwanzo, kwa urefu wa Habari hiyo fungua hapa >> UFUNUO: Mlango wa 4

Lakini yule mwenye uhai wa 4 ambaye ndiye mwenye uso wa Tai, alianza kutenda kazi katika kanisa la 7 na la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, ambalo ndio tunaishi mimi na wewe, na kanisa hili lilianza mwaka 1906, (hilo linajulikana na wanazuoni  wote na wana theolojia wote duniani, sio jambo la kutengeneza)..

Sasa kama tulivyosema, Sio kwamba huyo mwenye uhai wa 4 ndio anayetenda kazi hapana, bali Ni Roho ya Mungu yenye tabia ya Tai ndio iliyoachiwa kwa kanisa la Mungu tangu huo wakati na kuendelea (Mwaka 1906- Pentekoste ya mwisho ilipoanza)

Hivyo mimi na wewe tunaishi katika  Upako huo wa Roho ya Tai.

Sasa ni kwanini iwe ni Tai na sio wale wengine, labda simba, au ndama, au mwanadamu?.

Ni kwasababu kanisa la sasa hivi linahitaji wakristo wenye jicho la TAI,..Kumbuka tai ni ndege anayeona tokea mbali kuliko kiumbe kingine chotechote duniani, Tai anaona kwa umbali ambao wewe mwenyewe huwezi kumwona angani. Anaweza kuona vitu vya mbali sana, vidogo sana,..tofauti na ndege wengine kama kuku, kuku yeye anaona hapa chini tu, lakini kile kinachotokea maili mbili mbele hawezi kukiona.

Hivyo jicho hilo la Tai ni jicho la kinabii, Kwamba wakristo wote waliopo duniani leo hii Roho hii inapaswa iwepo juu yao, ili wawezi kuushinda ulimwengu huu wa sasa, vinginevyo watakachukuliwa tu maji..Na ndio maana kusema tu Umeokoka, hilo halitoshi kwa majira haya..Ni lazima uwe na jicho la kinabii.. Na jicho la kinabii sio kuona maono usiku, wala wachawi, wala kutabiri…Bali ni utashi wa kujua wakati tuliopo, na kuona mambo yajayo, ambayo bado hayajafika yatakayoupata ulimwengu, na hivyo kuchukua tahadhari mapema.

Mungu alijua kabisa wakati huu udanganyifu utakuwa mkubwa duniani, na watu watamsahau Mungu kupindukia kama alivyosema watu watakuwa wa kupenda anasa kuliko kumpenda Mungu (2Timotheo 3:4), alijua kabisa kutatokea mapinduzi makubwa ya kiteknolojia, alijua kabisa kutakuwa na mwingiliano mkubwa wa watu na wa-kiutamaduni katikati ya mataifa, alijua kabisa dini nyingi zitaongezeka duniani, kiasi kwamba mpaka sasa duniani zipo dini Zaidi ya 4,300, ukristo ni mmojawapo na madhehebu yasiyoweza kuhesabika.

Alijua kabisa lile wimbi kubwa la makristo wa uongo, na manabii wa uongo, alilolitabiri zamani halitatokea wakati mwingine wowote, bali katika wakati wetu huu wa siku za mwisho.

Alijua kabisa wale watu wa kudhahaki, wale wanatakaosema yupo wapi huyo Yesu mnayemngojea mbona harudi, watazaliwa katika wakati wetu, (2Petro 3:3-4) mambo ambayo hapo nyuma hayakuwepo.

Alijua kabisa ile siri ya kuasi itakuwa inatenda kazi kwa nguvu, katikati ya ukristo, kiasi kwamba watu wengi watazombwa na nguvu hiyo..

Na ndio maana katika kizazi hichi chetu aliiachilia Roho ya Tai, Ili kukabiliana na udanganyifu uliopo sasa hivi. Na ni lazima kila mtu awe nayo, kwasababu ni kwaajili yetu.

Sasa dalili za mtu ambaye hana Roho hiyo ni ipi?

Ukiona hupendi kuongeza maarifa na kutaka kujifunza kitabu cha Ufunuo kinachozungumzia mambo yajayo, na vitabu vingine vya manabii, basi ujue Roho huyo bado hajaanza kutenda kazi ndani yako. Watu wengi tunadhani Mungu hana agenda yake ya kutimiza mambo, tunadhani tupo tu tunangojea siku Fulani ya unyakuo ifike halafu tuondoke kana kwamba hapa katikati Mungu hafanyi kazi yoyote.

Kama ulikuwa hufahamu Bwana Yesu alisema, kabla ya kurudi kwake atamtuma Eliya, ili kuigeuza mioyo ya wana iwaelekee baba zako, kwa kanisa letu Mungu alishaanza kutimiza hiyo agenda, na bado ataendelea kuitimiza,..Zipo ngurumo saba, ambazo zimezungumziwa katika Ufunuo 10:4. Ambazo hazijaandikwa kabisa katika maandiko, na hizo ni sharti zije zifunuliwe katika siku za mwisho kabla Kristo hajarudi, hapo ndipo Mungu atakapoitimiza siri yake yote (Ufu 10:7), kwasasa hivi siri ya Mungu bado haijatimizwa yote.

Hatujui sauti za ngurumo hizo 7 zitakuwa ni nini, Lakini siku zitakaposemwa duniani, wale wanawali wapumbavu hawataelewa chochote. Hata leo hii Mungu anasema, lakini usipokuwa na jicho la Tai huwezi kuona..Huwezi kuona hizi ni siku zenyewe, kwasababu macho yako yanaona tu ya ulimwengu huu, wapo ambao hata Ugonjwa wa Corona wanaona kama ni ugonjwa wa kibailojia tu, umetengenezwa na watu!. Huwajui kuwa hizi ndizo tauni Yesu alizozizungumzia zitatokea siku za mwisho (Luka 21:11).

Yapo mambo mengi, ya kujifunza wakati huu, Hivyo usiridhike na dini yako tu, au dhehebu lako tu, Chukua biblia yako, itafakari, na huko huko Roho Mtakatifu atakufundisha siri zake nyingi, na mipango yake, ukiwa msomaji wa biblia mzuri, itakuwa ni rahisi kuzijua hila za ibilisi kwa haraka, na kutokupotezwa na udanganyifu wa shetani wa siku hizi za mwisho.

Na zaidi sana kumwomba Mungu azidi kutuongezea jicho hilo la Tai ndani yetu kila siku. Kwasababu pasipo kuwa nalo hilo, hakuna Unyakuo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KWANINI UKATE TAMAA?

Ulokole ni nini? Na kwanini wakristo waliookoka wanaitwa walokole?

UTAWALA WA MIAKA 1000.

FAIDA ZA MAOMBI.

SHUKURU KWA KILA JAMBO.

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Biblia. Huu ni mwendelezo wa vitabu vya biblia ambao tumeshatazama vitabu 17 vya mwanzo..Ikiwemo kitabu cha Ezra na Yeremia. Hivyo leo kwa Neema za Bwana tutaendelea na kitabu kimoja mbele ambacho ni kitabu cha Ezekieli. Kama hujapitia vitabu vya nyuma nakushauri ukavipitia kwanza wewe binafsi taratibu na kwa utulivu, ili hapa iwe ni sehemu ya kujiongezea vitu vichache juu ya vile ambavyo unavifahamu.

Kitabu cha Ezekieli ni kitabu cha 26 katika orodha ya vitabu vya Biblia na kina sura 48. Mwandishi wa kitabu hichi ni Ezekieli mwenyewe…na tafsiri ya jina Ezekieli ni “Mungu atatia nguvu”. Kitabu hichi kinakadiriwa kuandikwa kati ya mwaka 593-570 KK. Kiliandikwa kwa miaka isiyopungua 20. Na kilianzwa kuandikwa wakati wa lile kundi la pili la wayahudi kupelekwa Babeli.

Kumbuka hatuna za kupelekwa Babeli kwa wana wa Israeli ziligawanyika katika makundi matatu.

  1. Kundi la kwanza: ndio lile lililokuwa chini ya Mfalme, Yehoyakimu, ambalo Danieli alikuwa miongoni mwao.
  2. Kundi la Pili: lilikuwa chini ya huyu Mfalme Yekonia/Yehoyakini, ambapo Nabii Ezekieli ndio alikuwa ndani ya kundi hili.
  3. Na kundi la tatu Na la mwisho: lilikuwa ni la mfalme Sedekia, ambaye huyu alionyesha kiburi kwa Nebukadneza ikamfanya mpaka atobolewe macho, na kusababibishia kundi kubwa sana la wa-Yuda kuchukuliwa utumwani. Na ndio ikawa mwisho wa Wayahudi kuwepo katika nchi yao ya Ahadi. 

Sasa ukisoma vitabu vya nyuma vya Mambo ya nyakati na Wafalme, na kitabu cha Yeremia utaona ni jinsi gani Nabii Yeremia alivyowalilia wana wa Israeli juu ya kuamishwa kwao, lakini hawakusikia mpaka walipotolewa wote kwenye nchi ya ahadi na kupelekwa Babeli.

Sasa wakina Danieli, Shedraka, Meshaki na Abednego walichukuliwa wakiwa vijana wadogo sana katika kundi la kwanza na kutangulia Babeli..Tutakuja kuona Habari zao vizuri katika mfululizo wetu  baada ya kitabu hichi. Lakini kipindi kifupi tu baada ya wao kufika Babeli likatolewa kundi lingine la pili ambalo ndilo Ezekieli alikuwepo ndani yake. Wakiwa njiani kuelekea Babeli kijana mdogo Ezekieli alianza kuona maono. Hatuwezi kuyaandika haya maono yote aliyoyaona hapa (unaweza kuyasoma binafsi katika kitabu hicho cha Ezekieli 1 na 2).

Lakini kwa ufupi tu ni kwamba aliona Mbingu zimefunguka kama Nabii Isaya na Mtume Yohana walivyoona, na akaona makerubi na kiti cha enzi cha Mungu.

Ezekieli 1:1“Ikawa katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa pamoja na watu waliohamishwa, karibu na mto Kebari, mbingu zilifunuka, nikaona maono ya Mungu”.

Akiwa katika maono hayo Mungu alimpa “gombo” alile (Ezekieli 2:9).. Na gombo lile lilikuwa limeandikwa nje na ndani. Sasa tafsiri ya gombo hapo sio kitu Fulani mfano wa chakula, hapana bali ni aina Fulani ya vitabu vya kale ambavyo vinaandikwa kwa kuviringishwa. Hivyo ni kitabu ndicho alichopewa akile, na sio chakula..Sasa utauliza alikulaje kulaje kitabu?..Hatujui!..kama kiligeuka na kuwa mkate hilo hatujui..lakini mwisho  ni kwamba tunajua alikula kile kitabu alichopewa.

Na kile kitabu kilikuwa kimendikwa maneno nje na ndani.. Na maneno yalioandikwa humo yalikuwa yanahusiana na MAOMBOLEZO, VILIO NA OLE.

Sasa Huduma/ kusudi la Mungu kumwita Ezekieli lilikuwa ni lipi?

Tusome kidogo mistari ifuatayo ndipo tutajua Zaidi..

Ezekieli 3:1 “Akaniambia, Mwanadamu, kula uonacho; kula gombo hili, kisha enenda ukaseme na wana wa Israeli.

 2 Basi nikafunua kinywa changu, naye akanilisha lile gombo.

 3 Akaniambia, Mwanadamu, lisha tumbo lako, ulijaze tumbo lako kwa hili gombo nikupalo. Ndipo nikalila, nalo kinywani mwangu lilikuwa tamu, kama utamu wa asali. 

4 Akaniambia, Mwanadamu, haya! Waendee wana wa Israeli ukawaambie maneno yangu. 

5 Maana wewe hukutumwa kwa watu wa maneno mageni, ama wa lugha ngumu, bali kwa nyumba ya Israeli;

  6 si kwa watu wa kabila nyingi wenye maneno mageni, na lugha ngumu, ambao huwezi kufahamu maneno yao. Bila shaka, kama ningekutuma kwa watu hao, wangekusikiliza”

Umeona hapo? Ezekieli alitumwa  kwa watu wa Israeli…Hususani kwa lile kundi la mwisho..ambalo bado limebaki nyuma, halijafika bado Babeli..Kile kitabu alicholishwa ni lugha ya rohoni inayofunua KULISHWA MANENO YA MUNGU,  Na maneno hayo ni  Kuwaonya (yaani OLE), kuwaombolezea kwa yatakayowapata wasipotubu, na kuwatabiria vilio vitakavyowakuta kipindi kifupi kama hawatatubu.

Baada tu ya kula hicho kitabu katika maono…Roho ya Mungu ilimshukia kwa nguvu na kuanza kuwatabiria wana wa Israeli yatakayowakuta. Wakati huo Sedekia akiwa mfalme wa waisraeli, alikuwa ni mbishi na mwenye kiburi, hakutaka kuamini kwamba atachukuliwa utumwani kwenda Babeli, Nabii Yeremia alikuwa bado yupo hai kipindi hicho na alikuwa anamwonya aache njia zake mbaya na ajinyenyekeze, lakini hakusikia…Ikiwa bado imesalia miaka michache Mji wote uchomwe moto Ezekieli naye huko anaona maono na maneno kama yale yale ya Yeremia ya kuwaonya juu ya hukumu ile ile. Kwa hiyo huko Israeli yupo Yeremia na huku njiani kuelekea Babeli yupo Ezekieli..Wote wanazungumza kitu kimoja!.

Hivyo kuanzia Sura ya 1 hadi ya 24 ya kitabu cha Ezekieli.. Inaelezea Unabii juu ya kuangamizwa kwa Yerusalemu, kwa lile kundi lililobakia. Na maono hayo yalikuja kutimia vile vile kama alivyosema.

Baada ya Yerusalemu kuteketezwa na hilo kundi la tatu kufikishwa utumwani, Bwana alianza kumpa Ezekieli maono mengine..juu ya mataifa mengine yaliyobaki kama Misri na mengine yaliyo kando kando, kwamba nayo pia yatachukuliwa utumwani kwenda Babeli. Jambo ambalo Nabii Yeremia pia alilitabiri.

Hivyo kuanzia Sura ya 25-32. Bwana anampa Ezekieli maono juu ya kuangamizwa kwa mataifa mengine yaliyosalia, kwani nayo pia yalikuwa yamemwasi Mungu.

Na baada ya mataifa hayo yote kupitia kile yalichokipitia Israeli (yaani yote kuangamizwa na watu wao kupelekwa utumwani Babeli). Bwana akaanza kumpa Ezekieli tena maono mengine ya kuwaonya Wana wa Israeli watubu sana.. kwasababu anawazia kuwafanyia mema mwishoni. Katika Sura ya 33 utaona wito huo Mungu anaowaita wana wa Israeli.

Na mwisho kabisa baada ya wito huo kuanzia Sura ya 34-48. Bwana anampa Ezekieli maono mengine ya mwisho kabisa…Maono ni juu ya  kujengwa upya Yerusalemu katika siku za mwisho..Na baadhi ya maono hayo bado hayajatimia mpaka sasa…kwani kuna Hekalu la Tatu la mwisho ambalo limezungumziwa humo kwamba litatengenezwa siku za mwisho bado halijatimia…Ingawa mpaka sasa vifaa vyote vya ujenzi vipo tayari, vinasubiriwa nyakati na majira tu yaliyoamriwa na mbingu…ambapo siku moja isiyokuwa na jina Hekalu litaanza kujengwa kwa haraka sana na kwa kipindi kifupi kutimiza huo unabii wa Ezekieli.

Hivyo huo ndio ufupisho wa kitabu cha Ezekieli ..(katika Sura hizo zote zimejaa, maonyo mengi sana, na tabiri nyingi sana zihusuzo siku za mwisho, na ole nyingi na maombolezo),  na ole nyingine zinatuhusu hata sisi!..Ndani yake Bwana aliwaonya manabii wote wa Uongo vikali, na kuwalaani….kwamfano hebu soma ole hii..

Ezekieli 13:1 “Kisha neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, tabiri juu ya manabii wa Israeli wanaotabiri, uwaambie wanaotabiri kwa mioyo yao wenyewe, Lisikieni neno la Bwana; 

3 Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao manabii wajinga, wanaoifuata roho yao wenyewe, wala hawakuona neno lo lote!”

Unaona, yapo mafunzo mengi na maonyo, ambayo Roho Mtakatifu anatamani kumfunulia kila mtu atakayekisoma kitabu hiki. (Ndani ya kitabu cha Ezekieli utajifunza ni jinsi gani Mungu hapendi ibada za sanamu, utajifunza ni jinsi gani Mungu hapendezwi na maovu, na kusema kila nafsi itendayo dhambi itakufa! Kasome Eze.18:4,18:20). Pia ndani ya kitabu hichi utajifunza madhara ya kutokuifanya kazi ya Mungu, maana yake ni kwamba Mungu anapokuambia kitu ili ukawaonye watu na wewe hutaki kwenda kuwaonya basi wakifa katika dhambi zao bila wewe kuwaonya, damu yao itakuwa juu yako.

Ezekieli 33:7 “Basi wewe, mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli; basi ulisikie neno hili kinywani mwangu, ukawape maonyo yangu. 

8 Nimwambiapo mtu mbaya, Ewe mtu mbaya, hakika utakufa, nawe husemi neno la kumwonya mtu huyo, aiache njia yake, mtu mbaya huyo atakufa katika uovu wake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako. 

9 Walakini ukimwonya mtu mbaya kwa sababu ya njia yake, kusudi aiache; wala yeye asiiache; atakufa huyo katika uovu wake, lakini wewe umejiokoa roho yako”.

Hivyo sio kufurahia kusikia tu…bali tunaposikia injili au maonyo ya Mungu yanageuka kuwa deni kwetu kwenda kuwaonya wengine. Ndio maana Ezekieli baada ya kula lile gombo, kinywa aliliona litamu lakini tumboni lichungu..

Ndani ya kitabu hichi, utajifunza juu ya vita kubwa ambayo itakuja kupigwana pale Israeli, ambapo mataifa yanayoizunguka nchi ile yataongozwa na nchi ya magogu (Urusi kwa sasa),ili kupigana nao, Vita hiyo Israeli itashinda, pengine mimi na wewe tunaweza kuishuhudia vita hiyo katika kizazi chetu.

Hivyo tenga muda wa kukisoma chote wewe binafsi, usiridhike na haya yaliyoandikwa  hapa, na kujitumainisha kwamba tayari umeshakielewa! Huu ni muhtasari tu wa kukupa dira!,..kila kitu kipo kule!..

Biblia haijaeleza kifo cha Ezekieli, lakini ni wazi kuwa alifia huko huko Babeli..Na sehemu kubwa ya maono yake inafanana na maono aliyoyaona Mtume Yohana katika kisiwa cha Patmo..tutakapofika kitabu cha Ufunuo wa Yohana, tutaelewa Zaidi.

Mwisho kabisa…Kumbuka hizi ni siku za mwisho!..tunaishi katika kanisa la Mwisho lijulikanalo kama kanisa la Laodikia…Kanisa la Laodikia sio dhehebu linaloitwa Laodikia, au shirika Fulani la dini hapana!…Bali ni hali ya kanisa ya dunia nzima inavyoonekana mbele za Mungu, kwamba inafananishwa na kanisa la saba kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Ufunuo 3:14. Ni kanisa vuguvugu, ambalo Kristo alisema atalitapika. Na hakutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili. Hivyo Kristo anatuita kwasababu ule mwisho umekaribia, na hataki hata mmoja wetu apotee.

Hivyo kama hujaokoka kikamilifu, kama hujaacha ya ulimwengu..kama ni mwasherati bado, kama ni mzinzi, kama ni mtazamaji wa pornography kama ni mtukanaji, tubu leo..kwasababu wokovu ni bure, na atakusamehe na kukutengeneza upya. Na kusudia kuacha yote mabaya unayoyafanya na Bwana atakupa Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi na kukuongoza katika kuijua kweli yote.

Bwana akubariki.

Kama utahitaji uchambuzi wa vitabu vya nyuma basi utatumia ujumbe inbox. Kitabu kitakachofuata kitakuwa ni kitabu cha Danieli hivyo usikose mwendelezo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

DANIELI: Mlango wa 1

Je! Ni ipi tarehe sahihi Evil-merodaki alimtoa Yekonia gerezani?

UFUFUO TUNAOUSUBIRIA UTAHITIMISHA YOTE.

 

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Wafilisti ni watu gani.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post