Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..Ni neema Bwana katujalia kuliona jua tena siku ya leo, karibu tuyatafakari maandiko Pamoja..
Kama tunavyojua tunaishi katika siku za mwisho, na kila dakika inayosogea mbele ndivyo tunavyozidi kuusogelea ule mwisho…Hivyo leo tu tayari tumeshapunguza siku nyingine moja, kati ya zile chache zilizobakia mbele yetu, kuufikia ule mwisho.
Lakini Pamoja na hayo biblia inatuonya kuwa mojawapo ya dalili za kurudi kwa pili kwa Kristo ni kuongezeka kwa MAASI NA MAARIFA. Leo hatutazungumzia sana juu ya kuongezeka kwa maarifa, kama utapenda kufahamu juu ya hilo basi utatutumia ujumbe inbox tukutumie somo lake. Lakini leo tutaangalia juu ya kuongezeka kwa MAASI,(Mathayo 24:12) ambapo tutajifunza kitu cha muhimu sana. Na pia nakushauri kabla ya kusoma somo hili, tenga muda pitia somo fupi lililotangulia kabla ya hili lenye kichwa kinachosema “Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo?” kwasababu linamahusiano mkubwa sana na hichi tutakachokwenda kujifunza leo.
Ukiyatafakari Maisha ya leo unaweza kusema, ni afadhali na jana na juzi kuliko leo kwa jinsi maasi yanavyozidi kuongezeka…Upendo wa wengi unapoa, mauaji yanaongezeka, chuki zinaongezeka, visasi, ubinafsi, wizi, uasherati na kila aina ya uchafu, unazidi kuongezeka…
Hiyo yote ni ishara ya kurudi kwa pili kwa Kristo, Lakini swali la kujiuliza ni je!.. kwanini ishara ya mabaya ndio iwe dalili ya kurudi kwa Yesu, na si Ishara ya mazuri, yaani kwanini Bwana Yesu asingesema kabla ya kurudi kwake Mema yataongezeka sana?.
Jibu ni kwamba…wakati wa Kristo kurudi, (yaani kipindi kifupi kabla ya kutokea mawinguni) Kiwango cha utakatifu cha watakatifu kitakuwa kipo juu sana.. Na ishara mojawapo ya kuwa kiwango cha utakatifu kimekuwa kikubwa ni kiwango cha maovu kuwa kikubwa.
Ndugu unapoona dhambi zimezidi mipaka, jua kuwa sehemu Fulani mema yamezidi sana… Inaweza isiwe ni watu wengi wanatenda hayo mema, lakini hata kama ni mmoja tu! Basi atakuwa anatenda mema kwa kiwango kikubwa..
Wengi hawalioni hili wakifikiri kwamba kwasababu dhambi ni nyingi katika kipindi hichi basi hakuna kabisa watu wanaompendeza Mungu. Usilisahau hilo siku zote (Maovu kuwa juu ni ishara ya utakatifu pia kuwa juu). Ukiona kuna maasi makubwa sana katika mji fulani jua upande mwingine katika mji huo huo kuna wakamilifu au mkamilifu wa kiwango kikubwa sana.
Wakati Mungu amechukizwa na maasi ya Sodoma na Gomora, wakati huo huo Mungu alikuwa amependezwa sana na mtu mmoja aliyeitwa Ibrahimu, ambaye tunamwita sasa Baba wa Imani, Hivyo Ishara ya maasi kuongezeka Gomora ni ishara ya wema kuongezeka kwa mtu Fulani wa Mungu mahali fulani. Ukiona dunia inazidi kuoza sasa, jua ni ishara kuwa kuna watakatifu mahali Fulani wanazidi kujitakasa sana.
Ukiona sasa hivi kuna wanawake wengi wanaotembea nusu uchi barabarani, na hata wanaingia makanisani wakiwa hivyo… usifikiri ni wote wapo hivyo…Hiyo ni ishara ya kuiogopa sana, kwasababu ni ishara kuwa kuna mwanamke/wanawake mahali Fulani wanaojiheshimu na kujisitiri sana, na kumheshimu Mungu kwa viwango vya kimbinguni..
Unapoona kuna wimbi la manabii wa uongo..ni jambo la kuogopa wala sio la kucheka na kudharau, kwasababu hiyo ni ishara kwamba kuna kuna watumishi wa Mungu wa kweli. Biblia inasema katika siku za mwisho magugu na ngano vyote vitakomaa.. hivyo ukiona shambani magugu yamekomaa jua na ngano pia zimekomaa…Ndio maana mavuno yanakuja.
Hata Maisha ya kawaida yanatufundisha..Ijapokuwa miaka hii watu wanaonekana duniani kuwa dhaifu, na magonjwa kuongezeka na uwezo kupungua…lakini ukifuatilia rekodi, utagundua kuwa bado zinavunjwa kila mwaka.
Mtu mwenye mbio kuliko wote anaishi miaka yetu hii hii ambayo watu wanakula vibaya, watu wana magonjwa sana n.k. kumbe katikati ya kizazi ambacho watu ni wadhaifu watakuwepo watu ambao ni Hodari kuliko wote katika historia?.
Na katika Imani ni hivyo hivyo…Katikati ya maovu ya dunia yaliyokithiri, Bwana anao watu wake walio waaminifu, wakati wa mfalme Ahabu ambapo Yezebeli mke wake aliifanya Israeli kuwa nchi ya kichawi kiasi kwamba manabii wote waliouliwa, lakini mahali Fulani alikuwepo Eliya Mtishbi, na kama hiyo haitoshi walikuwepo pia manabii wengine 7000 ambao hakupigia goti baali katika mji, Bwana aliojisazia.. Hivyo ndugu huu sio wakati wa kusema aaah! dunia imeharibika yote, hivyo na mimi lazima niwe mwovu…au aaah siku hizi hakuna watakatifu hivyo hakuna haja ya mimi pia kujitakasa..n.k Usikubali kuusikiliza huo ni uongo wa shetani ambao upo kama KILEVI, shetani anawalevya watu wote wa ulimwengu, wafikiri kwamba hali inafanana kila mahali na kwa kila mtu.
Likumbuke hili neno.. Mhubiri 7:10 “Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo”.?
Bwana atusaidie tufumbuke macho..na tuzidi kujitakasa. Maadamu wakati siku ile inakaribia.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MAONO YA NABII AMOSI.
Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?
YONA: Mlango wa 4
UFUNUO: Mlango wa 3 part 3
SWALI: Ibada ni nini, Na je ili ibada ikamilike inapaswa iwe na nini na nini? Na je ni siku gani maalumu ya kufanya ibada?
Ibada ni kitendo chochote kifanywacho kuonyesha unyenyekevu wa hali ya juu, utiifu, heshima, shukrani, na utukufu, aidha kwa Mungu au kitu kingine, na hiyo inaambata na mambo kadha wa kadha, ikiwemo kusifu, kuabudu, kusujudu, kuimba, kufunga, kutoa sadaka, na kushiriki maagano ya imani, Na vilevile kujitoa mwili wako kuvitumikia, hiyo nayo ni ibada kamili.
Kibiblia kuna ibada za aina tatu
Hizi, ni zote tuzifanyazo aidha kanisani au manyumbani kwetu wenyewe, tunapokutana kumwimbia na kumwabudu Mungu, au kumshukuru, au kushiriki meza ya Bwana, hiyo tayari ni ibada kwa Mungu.
Matendo 13:2 “Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia”.
Na kama tulivyosema awali hata kujitoa mwili wako kwa ajili ya kutenda matendo yote yampendezayo Mungu ni ibada kamili tayari..
Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana”.
Hizi kwa jina lingine ndio ibada za sanamu. Ambazo biblia imezikemea sehemu nyingi sana katika biblia. Unapokwenda kuisujudia sanamu yoyote ile, iwe na mfano wa mtakatifu Fulani mbinguni, tayari hiyo ni ibada kamili ya sanamu.. Inayomtia Mungu wivu wa kukuangamiza haraka sana.
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.
1Wakorintho 10:14 “Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu”.
Lakini kama hilo halitoshi, unaweza pengine ukawa husujudii masanamu, lakini mwili wako unafanya maasi, hiyo nayo ni ibada kamili ya sanamu sawasawa na kusujudia vinyago.
Wakolosai 3:5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu”;
Hizi ni ibada ambazo, hazitokani na Mungu wala shetani, bali zinatokana na watu wenyewe, wamejitungia wakidhani kuwa wanamfanyia Mungu, kumbe wanafanya kimakosa..
Wakolosai 2:20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,
21 Msishike, msionje, msiguse;
22 (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?
23 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, KATIKA NAMNA YA IBADA MLIYOJITUNGIA WENYEWE, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
Na zina madhara yake makubwa, kwasababu wakati mwingine zinasababisha hata watu waue watu wengine wakidhani kuwa ndio wanampendeza Mungu, kama tu walivyokuwa wanafanya Warumi na Wayahudi kwenye kanisa la kwanza, na jinsi zinavyofanywa na baadhi dini leo hii duniani kuchinja watu. Zote hizo ni ibada ambazo watu wamejitungua lakini hazitokani na Mungu.
Yohana 16:2 “Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa ANAMTOLEA MUNGU IBADA.
Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa, ibada halisi ni moja tu, nayo ni kwa Mungu muumba wa mbingu na nchi (YEHOVA), na Kristo wake aliyesulibiwa kwa ajili ya dhambi zetu sisi wanadamu. Na maagizo pekee ya ibada hiyo halisi yanapatikana katika biblia tu.. Ibada nyingine yoyote tofauti na hiyo, ni machukizo makubwa kwake.
Na pia tunaikamilisha kwa miili yetu kama biblia inavyotufundisha, kwa kuishi maisha yampendezayo Bwana, ndio ibada yenye maana, ikiwa tutakuwa tunahudhuria kanisani kila siku, tunamwabudu Mungu usiku na mchana, tunamtolea matoleo mengi, tunashiriki meza ya Bwana kila wiki halafu matendo yetu, au miili yetu tumeiuza kwa shetani, ibada zetu bado ni batili..Zinakuwa ni ibada za sanamu, au ibada tulizojitungia tu sisi wenyewe.
Lakini kama utayakamilisha yote ya rohoni na mwilini, basi ibada hiyo inafaa sana mbele za Mungu, na inathawabu nyingi sana. Wanaomfanyia Mungu ibada kamili wanakuwa marafiki wa karibu sana Mungu.
Na pia hakuna siku maalumu ya kumfanyia Mungu ibada, kwani ibada yetu halisi ipo rohoni, hivyo wakati wowote na muda wowote uwapo na nafasi inaingia uweponi mwa Mungu, kumsifu, kumshukuru, kumwabudu, kumtolea dhabihu za shukrani n.k.. Lakini pia ipo ibada ya watakatifu wote, ambayo inafanyika kila juma, hivyo ikiwa ni jumapili au Jumamosi, inapaswa ifuatwe. Kama tulivyoambiwa tusiache kukutanika pamoja..
Bwana wetu atusaidie sote, tuweze kuyakamilisha hayo.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.
Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?
JE KUVAA PETE NI DHAMBI?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
CHAPA YA MNYAMA
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.
SWALI: Nini maana ya huu mstari.. Mhubiri 7:10 “Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo? “
JIBU: Mstari huo kwa lugha ya kueleweka zaidi ni sawa na kusema, “Usiseme mbona siku za kale, au nyakati za zamani zina afadhali kuliko siku hizi au nyakati hizi nilizopo mimi? Kwani kusema hivyo hujatumia hekima kufikiri.”
Msemo huu, ni maarufu hata sasa, tunaona kama wale watu wa zamani walikuwa ni watu wa ki-Mungu sana kushinda sisi, Au Watu wa zamani walikuwa wanaishi kwa raha kuliko watu wa sasahivi..Tukiwa tunafikiri hivyo ni ishara kuwa tumeshindwa kuyatimiza majukumu yetu ya msingi tuliyokabidhiwa sasa na Mungu, kwa kisingizio kuwa majira yamebadilika.
Ukweli ni kwamba hata hao watu wa kale ungewafuata na kuwauliza, nao pia wangekuambia heri watu wa kale kuliko sisi wa kipindi chetu.. Hivyo sisi sote tumepewa nafasi sawa, biblia inaposema hakuna jipya chini ya jua, fahamu kuwa unachokipitia sasa, ndicho walichokipitia watu wa kale, unayoyaona sasa ndiyo waliyoyaona wale, kama maovu yalikuwepo, tena pengine mengi kuliko unayoyaona wewe leo, mpaka wengine wakafikia hatua ya kugharikishwa na wengine kuteketezwa na moto.
Hivyo kama unaona wengi wao walikuwa karibu na Mungu, basi ni katika shida kama ulizonazo wewe, ni katikati ya maovu kama unayoyapitia wewe. Hivyo kusema heri siku za zamani kuliko hizi, ujue kuwa hutumii hekima kuuliza hivyo.
Ikiwa tunaukataa wokovu sasa au unakataa kuitenda kazi ya Mungu kwa kisingizio kuwa shughuli zinatusonga nyakati hizi zimebadilika, sio kama zamani, tujue kuwa hiyo sio hoja mbele za Mungu.
Ikiwa hatujizuii na mambo ya ulimwenguni, kwa kisingizio kuwa tunaishi katika majira ya dhambi kuliko mengine yote, kisa tunazo Internet, na simu, basi tujue kuwa hizo bado sio hoja mbele za Mungu.
Biblia inasema wapo watakaoshinda ulimwengu vizuri katika siku za mwisho, kuliko hata wale wa kwanza,
Luka 13:29 “Nao watakuja watu toka mashariki na magharibi, na toka kaskazini na kusini, nao wataketi chakulani katika ufalme wa Mungu.
30 Na tazama, wako walio wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, na wa kwanza watakaokuwa wa mwisho”.
Kwahiyo mimi na wewe tusiwe na sababu za kulaumu nyakati na majira tuliyopo..Ni wakati wa kuyafahamu majukumu yetu na kuyatimiza katika huu wakati mfupi tuliobakiwa nao hapa duniani. Ili na sisi tufanye vizuri zaidi kuliko wale, tupokee taji lililo bora. Hivyo tubadilishe hii mitazamo,
Mwisho Bwana atubariki sote, tuliozaliwa nyakati hii ya Laodikia.. Kwasababu tukishinda thawabu yetu ni kuwa kuliko za wengine wote..Kwasababu sisi tumeahidiwa kuketi pamoja na Mfalme mwenyewe (Bwana Yesu Kristo) katika kiti chake cha enzi, katika ufalme wake unaokuja, hakuna kanisa lingine lolote lililoahidiwa thawabu nono kama hii (kasome Ufunuo 3:21-22).. Hivyo Tukaze mwendo tusiikose.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/sala-ya-baba-yetu-sala-ya-bwana/
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, karibu tujifunze biblia.
Imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo.. Je! Una uhakika wa mambo yatakayokuja ambayo bado hujayaona wala kuyafikia?..Na kama ndio, je kwa kiwango gani?.
Ili Imani yako ionekane kuwa kubwa ni lazima uwe na uwezo wa kuamini vitu visivyoweza kuaminika. Yaani uwe na kila sababu itakayokufanya kuwa na uhakika kwamba jambo Fulani lazima litokee.
Kwamfano ukizungumza na mtu kwenye simu, aliye umbali Fulani akakwambia panda gari (daladala) unifuate mahali nilipo baada ya lisaa limoja…bila shaka kama utakuwa na fedha ya kutosha mfukoni mwako, hutakuwa na wasiwasi wa kufika pale alipo…kwasababu unajua hata Ukikosa daladala utatafuta tax, na hata ukikosa hiyo bado unaweza kupanda pikipiki ukafika pale alipo katika muda ule ule. Hivyo huo uwezo wa kuwa na kila sababu ya kufika pale kwa muda unaotakiwa ndio unaoitwa IMANI (una uhakika wa mambo yatarajiwayo yatafanikiwa asilimia 100).
Lakini kama huna fedha kabisa au unafedha kidogo tu ya daladala, utakuwa na wasiwasi, utasema itakuwaje endapo nikikosa gari? itakuwaje endapo gari nitakalopanda likiharibikia njiani?..si nitachelewa n.k Hivyo unakuwa huna uhakika sana wa mambo yatarajiwayo..Hapo inahesabika kuwa Imani yako ya kufika unakotaka kwenda kwa muda unaotakiwa ni ndogo au huna kabisa.
Sasa tukirudi katika Biblia ni hivyo hivyo..Ili uweze kuhesabika kuwa na Imani kubwa ya kutosha ya kuweza kupata kile unachokihitaji kwa Asilimia zote, ni lazima uwe na Hazina ya kutosha ya UELEWA WA MAANDIKO, ili uweze kukipata kile kitu. Kumbuka hapo ninasema ni UELEWA WA MAANDIKO, na si IDADI YA MAANDIKO. Mtu mwenye idadi kubwa ya maandiko pasipo kuyaelewa huyo ni sawa redio yenye idadi kubwa ya sauti na nyimbo zinazotoka ndani yake, lakini yenyewe haielewi chochote.
Hivyo kinachojalisha kwetu ili tuhesabike kuwa na Imani ya kuweza kupokea jambo lolote lile ni HAZINA YA KUYAELEWA MAANDIKO NA KUYACHAMBUA.
Hebu tujifunze mfano mmoja kwenye biblia ya Mtu aliyekuwa na hazina na uwezo wa kuyaelewa maandiko vyema na kuyagawanya..
Mathayo 15:22 “Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.
27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.
Unaweza kuona hapo, anakatishwa tamaa kwa maneno ya YESU, na kama tunavyojua maneno ya Yesu ni Neno la Mungu. Lakini kwa maneno hayo hayo, mwanammke anayafafanua vizuri kwa Bwana, na hatimaye anapata haki yake.. “ni kweli si vyema kutwaa chakula cha watoto kuwatupia mbwa, lakini hata mbwa wanakula makombo yaangukayo chini ya meza za Bwana zao”…Maana yake ni kwamba sistahili kweli kupewa hichi ninachokitafuta, (ni kweli mimi ni kama mbwa).. Lakini kuna vile vidogo vichache vinavyobakigi..ipo neema kidogo inakuwepo kwa Mungu kwa wale wasiomcha yeye…Hiyo ndio ninayoihitaji mimi!..Ni kweli Mungu hasikii maombi ya waovu, lakini bado Mungu huyo huyo anawanyeshea mvua waovu na wema…anawaangazia jua lake wenye haki na wasio haki..
Ni kweli mimi sio mkamilifu mbele zake, lakini bado wale waovu kuliko mimi anahakikisha wanafikiwa na miale ya jua, anahakikisha upepo mwanana unawaburudisha, anahakikisha wanapata hewa safi ya oksijeni kila dakika..hivyo kwa rehema hizo, ni lazima na mimi na mimi lazima nipone, lazima nibarikiwe na kufanikiwa katika yote..Mungu hana mbaraka mmoja tu!.
Hebu tujifunze Zaidi kisa cha Esau na Yakobo.
Tusome..
Mwanzo 27: 33 “Isaka akatetemeka tetemeko kuu sana, akasema, Ni nani basi yule aliyetwaa mawindo akaniletea? Nami nimekwisha kula kabla hujaja wewe, nikambariki; naam, naye atabarikiwa.
34 Esau aliposikia maneno ya babaye, akalia kilio kikubwa cha uchungu sana, akamwambia babaye, Nibariki na mimi, mimi nami, Ee babangu.
35 Akasema, Nduguyo amekuja kwa hila, akauchukua mbaraka wako.
36 Akasema, Je! Hakuitwa Yakobo kwa haki, maana amejitia mahali pangu mara mbili hizi? Alichukua haki yangu ya mzaliwa wa kwanza, na sasa amechukua mbaraka wangu. Akasema, Je! Hukuniwekea na mimi mbaraka?
37 Isaka akajibu, akamwambia Esau, Tazama, nimemfanya awe bwana wako, na ndugu zake wote nimempa kuwa watumishi wake; kwa nafaka na mvinyo nimemtegemeza, nami nikufanyie nini sasa, mwanangu?
38 ESAU AKAMWAMBIA BABAYE, UNA MBARAKA MMOJA TU, BABANGU? Unibariki mimi, mimi nami, Ee babangu. Esau akapaza sauti yake, akalia.
39 Isaka, baba yake, akajibu, akamwambia,Angalia,penye manono ya nchi patakuwa makao yako,Na penye umande wa mbingu unaotoka juu”.
Hebu tafakari Esau, angenyamaza asingelia kuomba na yeye abarikiwe, hebu tafakari angeishia kuondoka kwa majonzi leo hi angeishia kuwa kama Kaini, asingekuwa na baraka yoyote….Lakini japokuwa aliikosa ile Baraka kuu, lakini alilia kwa baba yake..akamwambia baba yake nibariki na mimi, kwani una mbaraka mmoja tu??? Na mwishowe akabarikiwa akaambiwa palipo na manono ya nchi patakuwa mahali pake, ingawa Mungu alimchukia Esau(Warumi 9:13)… lakini bado alimbariki alikuwa na mali nyingi hata Zaidi ya Yakobo kasome (kasome Mwanzo 33:9)
Na sisi ni hivyo hivyo, (simaanishi kuwa tuwe waovu, Mungu atusaidie), nachomaanisha ni kuwa ikiwa wewe ni mkristo hupaswi kukata tamaa hata kama inaonekana mambo yameshashindikana…Tujue tu! Mungu hana mbaraka mmoja tu!, usijiangalie ukamilifu wako!..Esau Mungu alimchukia lakini kwa kupambana akambariki hivyo hivyo…
Ukiona jambo Fulani katika Maisha kama haliwezekani, basi jua huo ndio uthibitisho kwamba linawezekana….kibiblia kutokuwezekana ndio uthibitisho wa kuwezekana kwa jambo. Amini tu! Amini tu.. usiache kumwamini Mungu kamwe.
Mwisho kabisa kama tulivyosema… “kubarikiwa wakati mwingine sio uthibitisho wa kumpendeza Mungu”..Esau hakumpendeza Mungu lakini alibarikiwa, na wengine wengi katika biblia…na hata leo Mungu ni yule yule…anawanyeshea mvua waovu na wema…Kwahiyo kuzimu watakuwepo matajiri sana, na mbingu pia watakuwepo maskini, hivyo lililo la Muhimu sana ni kutafuta kuyatenda mapenzi ya Mungu, ambayo hiyo inakuja kwa kutubu na kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa Maisha yako na kutafuta ubatizo sahihi wa kimaandiko (Matendo 2:38), na kupokea Roho Mtakatifu, hilo ndio jambo la muhimu na la kwanza, mengine yatafuata. Lakini kama unahitaji jambo lolote…Mwombe Mungu kwa bidii na kumwamini, utaona majibu…
Bwana anakupenda, Bwana anatupenda, na Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.
HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.
JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.
Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?
BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
Shalom, kila mahali biblia inatuasa juu ya kujiweka tayari, wakristo wengi tunadhani wokovu ni suala la kuotea tu kwamba nitaokoka au tutaokoka siku yoyote, au baada ya kuokoka leo basi hakuna haja ya kuyakamilisha yale mapungufu niliyonayo..Hatujui kuwa wokovu ni process, ni mchakato endelevu,. ni jambo lenye maandalizi, maana yake ni kuwa mpaka unyakuliwe ni lazima uwe umekidhi vigezo vyote vya kuwa bibi-arusi kamili wa Kristo, na sio suria.
Kama tunavyoijua ile habari ya wanawali 10 katika Mathayo 25. Ni habari ambayo inatupa picha halisi ya kitakachotokea muda mfupi kabla ya Yesu kurudi, ambapo tunaona 5 wao walikuwa werevu na 5 wao walikuwa wapumbavu, Lakini wote hawa walikuwa wanadai wanamngojea Bwana wao aje waende karamuni, mfano tu makundi yaliyochanganyikana ya wakristo leo kanisani, kila mtu anadai anamngojea Bwana, hata Yule mzinzi kanisani naye pia madai yake ni hayo hayo.. Lakini tunasoma wale werevu walikuwa wamejiandaa kwa kila kitu, mpaka na mafuta ya ziada katika chupa zao, lakini wale wengine hiyo kwao haikuwa na umuhimu hata kidogo, japokuwa walijua kuwa taa zao hazitadumu, lakini hawakulizingatia hilo, waliendelea kubahatisha hivyo hivyo tu, wakidhani maadamu wameshafika mahali pa kumsubiria Bwana basi hiyo inatosha..Lakini kilichotokea ni kwamba, ghafla tu usiku wa manane, pakawa na kelele..
Wote wakashtuka kuna nini? Wakaambiwa Bwana wao anakuja,..wale werevu wakawasha taa zao, lakini wale wengine ndio wakaanza mchakato wa kuzichochea taa zao, wakawa wanaona zinazima, wakaanza kuwaomba wenzao wawapunguzie kidogo, Lakini hilo halikuwezekana ikabidi wakajinunulie ya kwao (kwasababu Roho Mtakatifu hatolewi kwa mwanadamu bali kwa Mungu..Na waliporudi wakakuta mlango umeshafungwa..
Mathayo 25:6 “Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.
7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.
9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.
10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.
12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi”.
Ni jambo gani nataka tuone hapo; kabla mlango haujafungwa, palitangulia kwanza na sauti za kelele ili kuwaamsha wote..Yaani maana yake ni kuwa wote walipewa muda mfupi sana wa neema kutengeneza mambo yao kabla Bwana hajawasili.. Lakini muda huo haukuwa si muda wa kwenda tena kununua mafuta, ulikuwa ni muda wa kuwasha tu taa.
Ndivyo ilivyo katika siku hizi za mwisho,.Tunapozidi kuukaribia ule mwisho, wakati wa unyakuo, kabla parapanda haijalia, kutatangulia kwanza sauti za kelele, sauti hizo zitakuwa ni mahubiri maalumu ambayo yatahubiriwa katika ulimwengu mzima, hayo ni mahususi kwa ajili ya kuwaweka tayari watakatifu wote waliomwamini Yesu kwa ajili ya tukio la unyakuo ambalo linakwenda kutokea ndani ya kipindi kifupi sana.
Lakini wakati huo ukifika, na wewe ulikuwa hauuthamini wokovu wako, ulikuwa unaishi hoe hae tu, vuguvugu, mguu mmoja nje, mwingine ndani..usidhani siku hiyo itakuwa ni ngumu kuivuka.. Hata iweje, Ni kweli utajua kabisa Unyakuo umefika, na utaanza michakato ya kuyatengeneza mambo yako kwa Mungu, lakini hilo halitakamilika, ghafla tu utashangaa wenzako uliokuwa unashiriki nao kanisani hawapo ndipo utakapokuwa katika kilio cha kusaga meno.
Wokovu ni maandalizi..Kwenda katika unyakuo, ni kukamiliza vigezo vyote, sio kusema tu nimeokoka, halafu basi, wale wanawali wapumbavu nao pia walikuwa wameokoka, lakini kumbuka kwa Mungu hatufiki kwenye muda wenyewe tuliopangiwa, hapana bali tunafikia ndani ya Muda….Kwa mfano mtu akikuambia tuonane saa 8 kamili..na wewe ukafika pale muda huo huo wa saa 8, hapo ni sawa na umefika kwenye muda wenyewe..Lakini ukifika saa 7 na nusu, hapo umefika ndani ya muda, na ndio Mungu anachotaka kwetu.. Kwa Mungu ukifika saa 8 umeshachelewa..
Kwasababu, kabla haujamfikia huwa kunakuwa na maandalizi rasmi. Na ndio maana hata ukisafiri huwa unawekewa kabisa muda wa kuwasili(reporting time) na Muda wa kuondoka(departing time), Kama ukisema mimi nitafika ule muda wa kuondoka..Ujue tayari umeshachelewa, kwasababu zipo hatua za kufuata ambapo mpaka ukamilishe zote, tayari ule muda wa kuondoka utakuwa umeshapita..
Hivyo, katika hichi kipindi cha mwisho, wewe kama mkristo unaishi ukristo wa kubahatisha, ule wa kusema tu mimi nimeokoka, halafu, hakuna mabadiliko katika maisha yako, siku zinakwenda siku zinarudi haujiweki sawa kwa ajili ya kurudi kwa pili kwa Kristo. Ndugu yangu nataka nikuambie, Unyakuo utakupita, mbele ya macho yako hivi hivi ukiona ikiwa wakati huo utakuwa hai. Na kama utakuwa umekufa hutafufuliwa, kuungana na walio hai kwenda mbinguni.
Huu wakati wa mwisho ni wa ajabu kwasababu biblia inatoa maelezo kuwa kutakuwa na makundi mawili ya wakristo wakristo wanaomngojea Bwana, na sio kundi moja kama inavyopaswa iwe, ndio hao wanawali werevu na wapumbavu. Sasa swali la kujiuliza mimi na wewe je! tupo katika kundi lipi?
Sio kila staili unayoiona kwa watu Fulani wanaoitwa wakristo ni ya kuiiga..
Sio kila maisha unayoona anaishi mtu Fulani anayejiita mkristo ni ya kuyaiga.
Sio kila mahubiri na mafundisho ni ya kuyasikiliza, ni lazima uyachuje.
Sio kila sauti inayosema ndani yako ni ya kuifuata.
Huu ni wakati wa kuitengeneza taa yako wewe mwenyewe binafsi, na kuwa na uhakika kuwa hata leo mambo ya kibadilika ghafla ninaweza kwenda kumlaki Bwana mawinguni.
2Wakorintho 13:5 “Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa”.
Naamini sisi sote tutaanza kuishi kama wanawali werevu. Na Bwana atusaidie.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe. Ni neema za Mungu tumeiona siku nyingine, hivyo nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko, ambayo ndio chakula cha roho zetu.
Watu wengi tumekuwa tukitafuta msaada kutoka kwa Mungu wetu, jambo ambalo ni zuri sana, kwasababu hakuna pengine popote ambapo tunaweza kupata msaada, shetani kazi yake ni kutuharibu na si kutupa msaada.
Hivyo basi zipo njia nyingi za kupata msaada kutoka kwa Mungu katika jambo lolote lile unalopitia au unalohitaji.
Njia ya kwanza na ya Muhimu kuliko zote, ni wewe binafsi kupiga magoti na kumwomba Mungu. Kama Maovu na dhambi zote zinazoendelea leo ulimwenguni zinamfikia Mungu, si Zaidi maombi yetu!. Mungu wetu anasikia hata sauti ya mapigo ya mioyo yetu, kila sekunde yanapodunda, hata ile sauti ya jogoo anayewika alfajiri inamfikia, Si zaidi sana maneno yanayotoka katika vinywa vyetu.
Kwahiyo njia ya kwanza na bora ni ile ya kupiga magoti binafsi na kumwomba Mungu hitaji la moyo wako huku ukiamini kwamba anakusikia na atakifanya hicho ulichomwomba kikiwa ni sawasawa na mapenzi yake.
Njia ya Pili, ambayo ndio kiini cha Somo letu, ni ile ya KUWATUMIA WATUMISHI WA MUNGU.
Njia hii sio bora kuliko hiyo ya kwanza lakini ni Njia halali, ambayo imehalalishwa na Mungu mwenyewe. Upatapo shida, au upitiapo jambo lolote..watafute watumishi wa Mungu wa ukweli. Hao Bwana amewapa neema ambayo huwezi kuipata mahali pengine. Watakapokuombea au kukushauri ni rahisi kupata majibu au matokeo yaliyo sahihi kabisa.
Ipo mistari mingi kujifunza juu ya neema waliyopewa watumishi wa Mungu, lakini leo napenda tujifunze mistari ifuatayo ili tupate kuelewa Zaidi.
Marko 6:34 “Naye aliposhuka mashuani, akaona mkutano mkuu, akawahurumia; kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji; akaanza kuwafundisha mambo mengi.
35 Hata zilipopita saa nyingi za mchana, wanafunzi wake walimwendea, wakasema, Mahali hapa ni nyika tupu, na sasa kunakuchwa;
36 uwaage watu hawa, ili waende zao mashambani na vijijini kandokando, wakajinunulie chakula.
37 Akajibu, akawaambia, WAPENI NINYI CHAKULA. Wakamwambia, Je! Twende tukanunue mikate ya dinari mia mbili ili tuwape kula?
38 Akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Nendeni mkatazame. Walipokwisha kujua wakasema, Mitano, na samaki wawili.
39 Akawaagiza wawaketishe wote, vikao vikao, penye majani mabichi.
40 Wakaketi safu safu, hapa mia hapa hamsini.
41 Akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akashukuru, akaimega ile mikate, AKAWAPA WANAFUNZI WAKE WAWAANDIKIE; na wale samaki wawili akawagawia wote.
42 Wakala wote wakashiba.
43 Wakaokota vipande vilivyomegwa vya kuweza kujaza vikapu kumi na viwili; na vipande vya samaki pia.
44 Na walioila ile mikate wapata elfu tano wanaume”.
Katika mistari hiyo kuna mambo kadhaa nataka tujifunze.
Jambo la kwanza Bwana aliwahurumia makutano lakini hakuwapa yeye ile mikate. Badala yake aliwaambia wanafunzi Ndio wawape wao chakula (soma mstari wa 37).
Jambo la Pili, ni kwamba muujiza ule haukufanyika mkononi mwa Bwana, bali mikononi mwa Wanafunzi wake. Utaona kuwa Bwana alishukuru kisha akaimega ile mikate mitano na samaki wawili na kuwapa wanafunzi… Na wala hakuimega mikate elfu tano na kuwapa wanafunzi. Hapana! Maana yake ni kwamba miujiza ilitendeka mikononi mwa wanafunzi na si mkononi mwa Bwana Yesu. Hivyo likatimia neno Bwana alilowaambia “wapeni nyinyi chakula”, na wanafunzi wakawapa chakula.
Kwahiyo kwa ufupi ni kwamba muujiza ule ulifanywa na Bwana Yesu, kwa kupitia mikono ya mitume wake (watumishi wake). Bwana hakushindwa kufanya yeye, lakini ndivyo ilivyompendeza yeye kuwatumia watumishi wake kutimiza kusudi lake la kuwahudumia watu wake wenye kuhitaji msaada.
Hivyo upatapo tatizo, na hujui pa kuanzia msaada wa kwanza piga magoti mwombe Mungu binafsi, na kama bado unaona una mashaka mashaka, au bado kuna mambo unaona bado hayajakaa sawa..basi watafute watumishi wa Mungu wa kweli…watakusaidia, kwasababu Bwana anafanya kazi kupitia wao. Na Mungu anao watumishi wake karibia kila mahali, kwasababu anajua watu wake wengi wanahitaji msaada.
Kama unahitaji ushauri wa kimaisha, wa kiroho, au una ugonjwa, au jambo lolote lile, mtafute mchungaji wako, au askofu, mweleze usimfiche kwasababu tatizo unalodhani wewe peke yako ndio wa kwanza unalipitia, kumbe hujui kuna wengi waliotangulia kuwa nalo na likatatulika..hivyo usikubali shetani akutengenezee hofu, na kusema haiwezekani..Chukua hatua kawatafute, na jaribu kueleza kwa kina, kama unavyomweleza daktari unapokwenda hospitali..Ukifanya hivyo ni rahisi kupata msaada kwa haraka sawasawa tu na kama Kristo mwenyewe angekuwepo hapo kukuhudumia…
Na pia nakushauri!..Usiende mikono mitupu!..na wala usiende na saikolojia kwamba anahitaji fedha yako..nenda kama vile unaenda kukutana na Kristo, na kwamba huwezi kuondoka bila kuacha chochote cha kumshukuru Mungu. Ukifanya hivyo utaona matokeo makubwa sana.
Na pia kama wewe ni mtumishi wa Mungu wa kweli, utawahurumia wenye matatizo kama hawa wanafunzi walivyofanya, hata kufikia kupeleka hoja zao mbele ya Kristo. Wanafunzi wa Yesu, hawakuona fursa ya fedha bali waliona matatizo ya watu.. Ingawa walijua wale watu walikuwa na fedha zao mifukono mwao, ndio maana walimwambia Bwana awape ruhusua wakajinunulie chakula, hilo neno kujinunulia linaonyesha kabisa kwamba wale watu ingawa walikuwa na matatizo lakini walikuwa na fedha mifukoni mwao!..
Lakini mitume walihurumia matatizo yao na hawakutamani fedha zao. Na nani ajuaye pengine baada ya kupokea ile miujiza ya kula mikate na kushiba, zile fedha walizokuwa nazo walizitoa pale kama sadaka!!!..pengine walitoa kwasababu katika hali ya kawaida hakuna mtu ambaye anaweza kuponywa na kufanyiwa kitu cha kimiujiza na asiguswe kabisa kutoa chochote.
Na pia tunajifunza kitu kingine kuwa wanafunzi waliwaketisha watu kwa SAFU, watu hamsini na sehemu nyingine watu mia. Pengine yalitengwa makundi ya wanawake na wanaume kivyao, hali kadhalika ya wazee kivyao na Watoto kivyao..hawakuchanganywa wote kwa Pamoja.
Hiyo ni kutufundisha watumishi kuwa ni lazima katika kuwahudumia watu Utaratibu uwepo.. Mungu wetu ni Mungu wa utaratibu, mahali pasipo na utaratibu basi Mungu hafanyi kazi. Na utaratibu ni Pamoja na kuwaheshimu watu, kujua jinsi gani ya kushughulika na marika..Huwezi kumhudumia mzee kama unavyomhudumia mtoto, huwezi kuzungumza na mzee kama unavyozungumza na kijana. Hekima na heshima lazima viwepo, ndipo Bwana ataachilia miujiza yake.
1Wakorintho 14: 40 “ Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu”
Hivyo ni kwa njia gani utapata msaada kutoka kwa Mungu? Ni kwa kuwatumia pia watumishi wa Mungu, na sio tu msaada wa kimwili, bali pia msaada wa kiroho ambao ni Neno la Mungu.
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU
Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?
Mafuta yanayozungumziwa kwenye Yakobo 5:14, ni mafuta gani?
Nyamafu ni nini?
HUDUMA YA WALE MASHAHIDI WAWILI.
BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.
Nyamafu ni nini?
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima. Karibu tujifunze Maneno ya uzima.
Siku zote tunavyolijua Neno la Mungu ndivyo tunavyozidi kuwa na amani na ujasiri zaidi wa kusonga mbele kwasababu biblia inasema.. Neno lake ni taa ya miguu yetu, Na mwanga wa njia zetu (Zab 119:105).
Leo kwa neema za Bwana tutajifunza tena kisa cha Yohana Mbatizaji,. Kama tunavyoijua habari yake Yohana alikuwa ni mkuu zaidi ya nabii yeyote aliyewahi kutokea kulingana na maneno ya Bwana wetu Yesu, na kwamba tangu wakati wake, kurudi nyuma hakuna nabii yote aliyemzidi kwa ukuu mbinguni, si Eliya, si Isaya, si Yeremia, si Musa wala si mwingine yeyote yule.
Lakini pamoja na ukuu wake wote, kuna wakati alimtilia shaka Bwana Yesu..Japokuwa aliisikia kabisa sauti kutoka mbinguni ikimshuhudia kuwa Yesu ndiye mwana pekee wa Mungu, aliyependezwa naye..Japokuwa alimwona Roho Mtakatifu akishuka juu yake kama hua, kumtia mafuta..Lakini kuna wakati alifikia kumtilia shaka..
Japokuwa aliwashuhudia wanafunzi wake, na watu wengine kuwa Yule kweli ni mwana wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu, mpaka baadhi ya waliokuwa wanafunzi wake wakamwacha, wakafuatana na Yesu, lakini alikuja kumtilia shaka wakati fulani.
Hiyo ilitokea siku moja akiwa gerezani akawatuma wanafunzi wake, kumfuata Yesu ili kumuuliza, je! yeye kweli ni Yule mwokozi wa ulimwengu waliyekuwa wanamsubiria au wamtazamie mwingine..?
Jaribu kutafakari maneno hayo, mtu ambaye maisha yake yote amekuwa akimshuhudia, na ambaye ndiye aliyetiwa mafuta na Mungu kumtengenezea njia leo hii, anauliza tena kana kwamba alikuwa hana uhakika kuwa yeye ndiye..
Mathayo 11:1 “Ikawa Yesu alipokwisha kuwaagiza wanafunzi wake kumi na wawili, alitoka huko kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
2 Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza,
3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?
4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona;
5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
6 NAYE HERI AWAYE YOTE ASIYECHUKIZWA NAMI.
Unadhani ni kwanini Yohana alisema vile? Alisema vile kwasababu “alimtazamia zaidi ya matazamio yenyewe kwa wakati ule”, Pengine alitazamia Bwana Yesu atakwenda kukaa kama mfalme awaokoe Israeli na maadui zao, kama maandiko yanavyosema, lakini akashangaa, mbona havutiwi hata na mambo ya ufalme wa duniani hii!!..Alitazamia atakaa kuwahukumu Israeli kwa mkono wa Mungu kama maandiko yanavyosema!, lakini yeye anamwona ndio kwanza anawahubiria wenye dhambi na maskini habari njema..Alitazamia atakuwa tajiri kwasababu ya ufalme wake, lakini anamsikia analala kwenye milima, hana hata kibanda n.k..
Unaona? Si kwamba matazamio yake yalikuwa ni uongo hapana, yalikuwa ni kweli lakini si katika wakati husika.
Ndipo Yesu aliposikia hivyo, akawatuma wale watu kumrudishia ujumbe juu ya kazi alizokuwa anazifanya..Na mwisho kabisa akamalizia na kuwaambia “Heri awaye yote asiyechukizwa nami”
Au kwa namna nyingine heri mtu Yule asiyekwazwa na haya niyafanyayo sasa..
Ndivyo ilivyo hata leo, mawazo kama hayo yapo miongoni mwetu kanisa la leo, si watumishi, si washirika.. wote.
Tunasema Yesu wewe ni mkuu, ni tajiri, nimempokea siku nyingi, nimesoma shuhuda zake, na mambo yake makuu aliyoyafanya kwenye biblia, na aliyowafanyia watu wengine, lakini mbona sioni akinibadilisha maisha yangu, na uchumi wangu.? Huyu ni Yule kweli wa kwenye biblia, au nimtazamie mwingine?
Bwana anasema.. Heri awaye yote asiyechukizwa nami.
Ndugu yangu, usivunjwe moyo ukamwacha Yesu, kisa tu hajakuponya ugonjwa wako ulionao kwa muda mrefu..
Usichukizwe na Yesu kisa tu hajayajibu maombi yako uliyokuwa unamwomba kwa muda mrefu.. Si kila jambo ni lazima ujue sababu yake leo, wewe endelea kumwamini tu..Anasema heri mtu Yule asiyechukizwa nami.
Hujui kesho kakupangiaje.. Wale walioweza kumvumilia Bwana Yesu mpaka dakika za mwisho ndio waliokuja kumjua yeye vizuri alikuwa ni nani, walijua kuwa kumbe itampasa aje mara mbili, kumbe mara ya kwanza ilikuwa ni kwa lengo la kuwaokoa watu dhambi zao, na mara ya pili ndio itakuwa ni ya kuketi kama Mfalme wa Wafalme na kuwahukumu mataifa, na kutawala pamoja na watakatifu wake..Na kwamba yeye ndiye atakayeshika utajiri wote wa mataifa. Lakini wao waliokuwa wanataka yatokee yote kwa wakati mmoja, hapo ndipo walipokosa shabaha.
Kumbuka upo ufalme Bwana Yesu alikwenda kutuandalia mbinguni, ambapo sisi tutakaoshinda, sisi ambao hatukuchukizwa na yeye tukiwa hapa duniani, tutaurithi huo, nasi tutawala naye kama wafalme na makuhani, wakati huo, ndio tutajua kuwa Mungu alikuwa anatuwazia mawazo mazuri.
Kwahiyo ukiona mambo hayaendi kama ulivyoyatazamia leo, ndio kwanza zidi kumpenda Yesu. Usimtilie shaka, Yesu ni Mungu. Siku zote anatuwazia mawazo mazuri, Na kesho yetu ipo mikononi mwake, tusichukizwe naye hata kidogo, pale ambapo hajibu maombi yetu kama tulivyotazamia..Kila jambo lina majira yake na wakati wake.
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani”.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
JIBU: Nyamafu ni nyama ya mnyama aliyekufa (kibudu) bila kuuliwa kwa asili (yaani kuchinjwa). Mungu aliwakataza wana wa Israeli katika agano la kale wasile nyama ya mnyama yoyote aliyekufa bila kuchinjwa..
Walawi 17: 15 “Tena kila mtu atakayekula NYAMAFU, au nyama aliyeraruliwa na wanyama, kama ni mzalia, kama ni mgeni, atafua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni; ndipo atakapokuwa safi.
16 Lakini kwamba hazifui, wala haogi mwili, ndipo atakapochukua uovu wake”.
Mistari mingine ya biblia inayozungumzia maagizo kama hayo ni kama ifuatavyo (Kumbukumbu 14:21, Walawi 22:8, Ezekieli 4:14, Ezekieli 44:31)..Unaweza ukaipitia binafsi upatapo muda.
Lakini Mungu aliwakataza wasile nyamafu kwasababu ni nyama ambayo ina damu ndani yake..
Utauliza kwani kuna nyama isiyo na damu na ambayo ina damu?
Jibu ni ndio!..Ipo tofauti kati ya nyama ya mnyama aliyechinjwa na damu yake kutoka na ile ya Mnyama ambaye hajachinjwa na wala damu yake haijatoka..wanjichaji wanajua zaidi. Sasa sio kwamba nyama ya mnyama aliyechinjwa itakosa damu kabisa, itakuwa na damu lakini sio kiwango cha kama ile ambayo haijachinjwa.
Sasa Bwana Mungu aliwakataza wana wa Israeli wasile nyama na damu yake, ndio maana akawapa maagizo ya kuwachinja Wanyama na damu yao waimwage juu ya nchi..
Mwanzo 9: 3 “Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa mboga za majani, kadhalika nawapeni hivi vyote. 4 Bali nyama pamoja na uhai, yaani, damu yake, msile”
Ezekieli 33:25 “Basi, waambie, Bwana MUNGU asema hivi; MNAKULA NYAMA PAMOJA NA DAMU YAKE, na kuviinulia vinyago vyenu macho yenu, na kumwaga damu; je, mtaimiliki nchi hii”
Na pia sio usafi kumla mnyama ambaye kafa mwenyewe!.. hata katika hali ya kawaida Mwili unakataa wenyewe! Hata hamu haipo!, hiyo ni kuonyesha kwamba sio kitu cha kufaa kula, kwasababu hujui mnyama kafaje kafaje, pengine kwa kula sumu au.
Hivyo hiyo ndio maana ya nyamafu (Ni nyama ya mnyama aliyejifia mwenyewe bila kuchinjwa).
Lakini katika kumnjicha mnyama ni kitu gani cha rohoni tunajifunza?
Ilikuwa ili mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo uweze kukubalika na kuleta matokeo makubwa ya ukombozi, ilipaswa naye pia auawe, na damu yake imwagike!, ndipo ilete uhai kwetu sisi.. Hivyo mwili wa Kristo ni chakula cha ulimwengu, ambaye ni mfano wa kondoo aliyechinjwa na kuandaliwa vyema na si nyamafu. Kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
Yohana 6:31 “Baba zetu waliila mana jangwani kama vile ilivyoandikwa, Aliwapa chakula cha mbinguni ili wale.
32 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Siye Musa aliyewapa chakula kile cha mbinguni, bali Baba yangu anawapa ninyi chakula cha kweli kitokacho mbinguni
33 Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.
34 Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.
35 Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.”
Je na wewe leo umekipata hichi chakula halali kilichoshushwa kutoka mbinguni? Au unakula nyamafu?..Nyamafu ni kitu chochote ambacho hakikufa kwa kumwaga damu yake kwa ajili yako, hakijachinjwa kwaajili yako.
Kuutumainia ulimwengu ni kujilisha nyamafu, kuzitumainia fedha zako, au umaarufu wako, au kumtumainia mwanadamu yoyote ambaye hajui hata mapigo ya moyo wako yanadundaje ni kujilisha nyamafu na hivyo ni machukizo kwa Mungu.
Mtegemee Yesu, Mwamini Yesu, HUYO PEKE YAKE NDIYE CHAKULA KILICHOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI, Mwanakondoo halisi aliyechinjwa Kalvari kwaajili yetu, (na si kibudu), huyo pekee ndiye anayeweza kutupa uzima.
Kama hujampokea, Leo anakuita, unachotakiwa kufanya ni kukiri tu wewe ni mwenye dhambi, hicho tu! (Anahitaji rehema na si sadaka)..ndicho anachokitafuta kutoka kwetu..Baada ya kukiri na kukubali, basi unaomba msaada kutoka kwake, kwamba akurehemu na kukusaidia, na ukiisha kumwomba rehema..thibitisha ulichokiomba kwa kuyaacha mabaya yote uliyokuwa unayafanya yasiyompendeza yeye..kama ulikuwa mlevi, mwizi, mzinzi n.k yaache yote.
Na yeye ni mwaminifu, kwasababu kabla hata hujamaliza kusema Amen, katika sala yako hiyo ya toba tayari atakuwa ameshakusamehe na kuingia moyoni mwako, kwasababu anakupenda upeo, na anatupenda wote. Na atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu ambaye atakusaidia kukuongoza katika kuijua kweli yote ya biblia. Pia unahitaji kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38, Kama utakuwa tayari kufanya hivyo, basi wasiliana na sisi Inbox, tutakuongoza ni wapi utabatiziwa.
Usikubali kula au kulishwa nyamafu wakati chakula halisi kipo!
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618/ +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?
Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)
Huyu Azazeli ni nani tunayemsoma katika(Walawi 16:8)
Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?
Orodha ya wafalme wa Israeli.
Kabla ya Israeli kugawanyika sehemu mbili kulikuwa na wafalme wakuu watatu waliotawala Israeli
Baada ya kugawanyika. Na kuwa mataifa mawili,.. lile kubwa lilichukua makabila 10 hivyo likaendelea kuitwa jina hilo hilo Israeli, na lile dogo lilibakiwa na kabila moja tu,la Yuda, na lenyewe pia likaendelea kuchukua jina la kabila hilo hilo Yuda (1Wafalme 11:35-36). Ikumbukwe kuwa kabila la 12 la Lawi lenyewe halikuwa na urithi, walitawanywa katikati ya makabila 11 yote ya Israeli.
Jumla ya wafalme wote waliotawala upande wa Israeli (iliyogawanyika) walikuwa ni 19.
Jumla ya wafalme wote waliotawala Yuda ilikuwa ni wafalme 19, malkia 1.
Shalom.
Tazama mada nyingine chini.
Pia Kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Israeli ipo bara gani?
MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?
Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
CHAPA YA MNYAMA
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
SWALI: Yakobo 5:14 inasema, wazee wa kanisa wakitaka kumwombea mgonjwa wampake mafuta, je! yale ni mafuta ya upako au?. Na kama sio, ni mafuta gani yanayozungumziwa pale?.
Yakobo 5:14 “Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana”.
JIBU: Kabla hutujaona ni mafuta gani yanayozungumziwa pale..Tuutazame kwanza kwa ukaribu mstari huo, ukiungalia vizuri utaona umegawanyika katika vipengele viwili.. utaona baada ya hao wazee wa kanisa kuitwa, hatua ya kwanza ni wanamuombea, (hicho ni kipengele cha kwanza kilichotenganishwa na alama ya mkato), na hatua ya pili inayofuata sasa baada ya hapo ni kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
Watu wengi hawalioni hilo, wanayaunganisha hayo maneno mawili pamoja, na ndio hapo wanadhani, mafuta Fulani ya chupa ndio maombezi yenyewe, .. Jambo ambalo si sahihi?. Kilichomaanishwa pale ni kuwa maombi yakishakwisha, kinachofuata ni kupakwa mafuta…Ukisoma biblia kwa haraka haraka ni rahisi kupoteza shabaha ya maandiko mengi.
Sasa tukirudi kwenye swali ni mafuta gani yale yaliyomaanishwa?..
Biblia inasema..
1Yohana 2:20 “Nanyi mmepakwa mafuta na Yeye aliye Mtakatifu nanyi mnajua nyote”.
Roho Mtakatifu ndiye anayepaka watu mafuta, na mafuta yenyewe ni Neno lake (Yohana 16:13). Hivyo mtu aliye na Neno la Mungu kwa wingi ndani yake, mtu huyo ana mafuta mengi sana ya kumsaidia.
2Wakorintho 1:21 “Basi Yeye atufanyaye imara pamoja nanyi katika Kristo, na kututia mafuta, ni Mungu.
22 naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu.”
Sasa mitume na wazee wa kanisa kwa kujua mafuta hasaa na halisi ni yapi, ilikuwa ni desturi yao mara baada ya kuwaombea wagonjwa, jambo linalofuata na kuwaimarisha kwa Neno, ,Kwasababu walijua hicho ndicho kinachoweza kumfanya mtu asimame na kuweza kufanya mambo yote mwenyewe, hata baada ya kutoka pale.
1Yohana 2:27 “Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake”.
Vivyo hivyo, na sasa, tunapaswa tuendeleze desturi hiyo, si kuwaombea tu wagonjwa matatizo yao, sio kufanyia tu kuwafanyia maombi ya ukombozi peke yake halafu hakuna cha ziada baada ya hapo, bali pia, tuwapake mafuta ya Roho wa Bwana..Tuwape chakula cha uzima..ambacho hata wakitoka pale, wanaweza kusimama wao wenyewe, pindi wanapokumbana na matatizo kama hayo na hata kumshinda shetani.
Huo ndio uponyaji hasaa, Lakini kama mtu atatolewa mapepo kwa kuombewa, halafu hatiwi mafuta,(Yaani hufundishwi au ajifunzi maneno ya uzima), akitoka pale, ataendelea na dhambi zake, na yale mapepo yatamrudia baada ya kipindi kifupi, tena yenye nguvu mara saba zaidi, na hali yake ya mwisho itakuwa mbaya kuliko ile ya kwanza kama biblia inavyosema. Na kazi inakuwa ni bure, Hivyo jitathmini na wewe kama mhubiri je unafanya hivyo?.
Kwahiyo mafuta yanayozungumziwa pale, sio mafuta ya chupa, bali ni Neno la Mungu, linalomiminwa na Roho Mtakatifu mwenyewe ndani ya mtu..
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?