Title June 2021

Zunga ni nini? (Walawi 12:3, Kutoka 4:24)

Neno hilo utalisoma kwenye vifungu hivi katika biblia;

Walawi 12: 3 Siku nane mtoto atatahiriwa govi ya zunga lake.

Kutoka 4:24 “Ilikuwa walipokuwa njiani mahali pa kulala, Bwana akakutana naye akataka kumwua.

25 Ndipo Sipora akashika jiwe gumu na kuikata govi ya zunga la mwanawe, na kuibwaga miguuni pake akasema. Hakika wewe u bwana arusi wa damu kwangu mimi”.

Zunga ni kipande cha govu kilicho mbele ya maumbile  ya mwanaume. Pale anapotahiriwa kipande hichi cha nyama ndicho kinachoondolewa. Hicho ndicho kinachojulikana kama Zunga.

Mungu alitoa maagizo kwa Ibrahimu na wazao wake wote, kuwa watahiriwe, kwa kukatwa zunga zao. Na kwamba hiyo ndio itakuwa dalili ya agano aliloingia nao, siku zote za maisha yao.

Mwanzo 17:9 “Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada yako.

10 Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa.

11 Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi.

12 Mtoto wa siku nane atatahiriwa kwenu, kila mwanamume katika vizazi vyenu, mzaliwa nyumbani, na mnunuliwa kwa fedha, kila mgeni asiyekuwa wa uzao wako”.

Mwanzoni Ibrahimu wala wa Israeli hawakuelewa ufunuo wa Mungu kuwaambia wafanye vile. Lakini sisi tuliomwamini Kristo leo hii ndio tunaofahamu kuwa. Kumbe kila mwanadamu anazaliwa na zunga lake la asili(yaani dhambi ya asili) rohoni. Na kwamba linapaswa litoke, kwa kukatwa. Na linaondolewa kwa kumwamini tu Yesu Kristo, ambapo kunaambatana na kubatizwa katika ubatizo sahihi.

Wakolosai 2:11 “Katika yeye mmetahiriwa kwa tohara isiyofanyika kwa mikono, kwa kuuvua mwili wa nyama, kwa tohara ya Kristo.

12 Mkazikwa pamoja naye KATIKA UBATIZO; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu”.

Unaona, usipotahiriwa moyo wako, wewe huna agano na Mungu. Hivyo kwasasa tohara yetu sio tena ya mwilini, bali rohoni, Na kila mmojawetu ni sharti awe nayo.

Wafilipi 3:3 “Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili”.

Swali ni Je! Umeokoka? Je! Umebatizwa ipasavyo?. Kumbuka ubatizo sahihi ni muhimu katika ukristo wako, na tohara yako ya rohoni kama tulivyosoma hapo juu. Yakamilishe maagizo yote ya Bwana Yesu, kwasababu hatuokoki kwa kukiri tu bali pia na kwa kubatizwa, na ubatizo ni sharti uwe wa kuzamishwa kwenye maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, 8:16:, 10:48, 19:5

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

JE! ULEVI NI DHAMBI?.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

WAPE WATU WANGU RUHUSA ILI WAPATE KUNITUMIKIA.

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

MAVUNO YAMESHAKWISHA  SHAMBANI.

Mathayo 24:14 “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja”.

Bwana Yesu asifiwe ndugu mpendwa..

Ukitaka kujua kuwa mambo yote sasa yameshakamilika, kinachongojewa ni UNYAKUO tu, angalia hali ya mavuno shambani mwa Bwana. Embu fananisha watu waliokuwa wanamjia Kristo kipindi cha mitume, na watu wanaookoka sasa  katika kipindi chetu hichi.

Kipindi kile injili ilipokwenda kuhuburiwa mahali kwa mara ya kwanza, mwitikio wa watu  wa kumgeukia Kristo ulikuwa ni wa kustaajabisha sana, utakumbuka baada ya Pentekoste tu, kanisa lilikuwa likijiongeza  kwa idadi ya maelfu, kwa injili ndogo sana. Na ndio maana kwa kipindi kifupi sana, ukristo ulienea ulimwenguni kote, na sio kuenea tu, badi kuhubiriwa (Wakolosai 1:6, 1Wathesalonike 1:8).Hiyo ni kuonyesha kuwa kweli ule ulikuwa ni wakati wa mavuno.

Lakini angalia sasa,  mambo ni tofauti hakuna mtu asiyeifahamu injili, au kuzijua habari za Kristo, wote tunazifahamu, lakini jiulize kwanini, watu hawataki kuokoka, kinyume chake ndio wanakwenda mbali kabisa na Ukristo..Hiyo ni kuonyesha kuwa mavuno yameshakwisha shambani, kilichobaki ni magugu tu.

Na hiyo imepelekea sasa injili kubadilika sio tena ya kuwavuta watu, bali ni ya ushuhuda. Unapoona, injili imekufikia hapo ulipo kitandani kwako ukiwa umeishika simu yako na kusoma, ujue hiyo sio ya kukuvuta wewe, hiyo ni ya ushuhuda tu, ukiona injili imekufikia hapo sebuleni kwako unapotazama tv na familia yako, injili inakufikia kwenye hivyo vipeperushi unavyovisoma huko mitaani. Unapewa biblia bure ya kwenye simu yako, mambo ambayo hata zamani hayakuwepo. Basi ujue hiyo sio injili ya kukuvuta tena kwa Kristo ndugu. Ni injili ya USHUHUDA Tu. Ili utakapokufa katika dhambi zako, usiwe na sababu ya kusema sikuwahi kusikia, au kuona, au kuambiwa.

Wewe jiulize tu, ni kwanini pamoja na mahubiri yote hayo uliyohubiriwa na kuyasikia siku zote za maisha yako, na bado huna badiliko lolote ndani yako. Unadhani ni jambo la kawaida? Hapana, kwa kawaida Neno moja tu lingetosha kukufanya uwe mtakatifu sawasawa na Waebrania 4:12.  Lakini hujageuka kwasababu  wewe sio Ngano bali ni gugu tu.

Kilichosalia sasa hivi ni Mungu anatazama walau kama yatakuwepo masalia salia machache ayaokoe. Lakini nataka nikuambie, moja ya hizi siku ambazo zinahesabika, tutashuhudia mabadiliko makubwa sana duniani. Tutashuhudia tendo kuu la Unyakuo wa kanisa.

Ndio yale maneno ambayo Bwana Yesu alisema, .(Mathayo 24:40-42) yatatimia hapo. Usiku huo wawili watakuwa wamelala mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa. Wanawake wawili watakuwa wanasaga(ikimaanisha watakuwa katika biashara zao), mmoja atatwaliwa mmoja ataachwa. Wale watakaoachwa, huku duniani kitakachokuwa kinaendelea ni vilio na kusaga meno. Wakijuta kwanini kipindi kile hawakuitii sauti ya Mungu, ilipokuwa inawavuta kwake kwa upole. Watalia na kuomboleza, kweli kweli, ndugu usiwe mmojawapo.

Lakini watakaokuwa wamenyakuliwa, moja kwa moja wataelekea mbinguni wakiwa na miili yao ya utukufu, katika ile karamu ya mwana-kondoo.  Kwenye raha isiyokuwa na kifani. Wakifutwa machozi kwa taabu zao walizokuwa wanapitia huku duniani kwa ajili ya Kristo.

Ndugu mambo haya unaweza kuona kama ni hadithi, au mambo yatakayotokea miaka elfu 5 mbeleni, usijidanganye. Yesu aliposema TUBUNI, kwa maana ufalme wa mbinguni UMEKARIBIA. Alikuwa hasemi uongo. Ni kweli ufalme wa mbinguni  ulikuwa umekaribia, jiulize  sisi wa sasa hivi tusemeje?.

Maanisha kugeuka, unaposikia injili kwa wakati huu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

UFUNUO: Mlango wa 14

Kuwiwa maana yake nini katika biblia?

Je watu ambao hawajasikia kabisa injili watahukumiwa?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kuoatama katika biblia?

Kuoatama ni lugha ya zamani, inayomaanisha “kwenda haja kubwa”

Kumbukumbu 23:13 “nawe uwe na jembe dogo katika silaha zako; napo uotamapo nje uchimbe kwa lile jembe, na kugeuka na kukifunika kikutokacho;

 14 kwa kuwa Bwana. Mungu wako, yuatembea katika kituo akuokoe, na kukutolea adui zako mbele yako; kwa hiyo na kiwe kitakatifu kituo chako; asije akaona kitu kwako kisichokuwa safi, akageuka na kukuacha”.

Wana wa Israeli walipewa maagizo na Mungu, waweke mazingira yao yanayowazunguka katika hali ya safi!.. Kwamba watu wasafishe mazingira ya maeneo wanayoishi, wasikae katika uchafu, mtu anapokwenda haja kubwa, angalau ahakikishe uchafu wake hauachi juu, bali aufukie.

Na hiyo ni kwasababu Bwana Mungu anapita katikati ya mazingira yao, ili kuwapigania..Hivyo apitapo na kuona au kukuta uchafu (mf. Kinyesi n.k), atageuka na kuwaacha!.

Hiyo ni kuonyesha kuwa Mungu haangalii roho tu, bali pia anaangalia pia Mwili na mazingira. Kama Mungu anaweza kuwaacha tu wana wa Israeli kwasababu ya kinyesi kilichozagaa juu ya ardhi, ataachaje kumwacha binti anayevaa nusu uchi?, ataachaje kumwacha binti anayevaa vimini au nguo zinazobana na kuchora maungo yake, ataachaje kumwacha kijana aliyejichora mwili wake?.

Ndugu, mahubiri ya kusema kwamba Mungu haangalii mwili anaangalia tu roho! Ni ya kutoka kuzimu!!, jihadhari nayo, ni ya adui shetani asilimia mia. Tunawajibu wa kujitunza miili yetu, kwasababu biblia inasema miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na vile vile tunawajibu wa kujiweka safi katika mazingira pia ya nje, kwasababu Mungu wetu pia ni Mungu wa usafi na si uchafu. Kama anayatazama mazingira ya nje, na kutoa hukumu, hatashindwa kutazama mwili wako na kutoa hukumu.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

]https://wingulamashahidi.org/2020/11/26/lango-limebadilika/

Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

Rudi nyumbani

Print this post

NI SAHIHI KABISA, HUU SI WAKATI WA TINI!

Katika ukristo ogopa sana ile kauli ya kusema “Huu si wakati”… “Bado kidogo”…. “Wakati wake utafika tu siku moja”… Ogopa sana kauli kama hizo, tena ziogope kuliko  ukoma.

Kwanini ninakuambia hivyo? Ni kwasababu wakati ambapo unafikiria majira yake bado, huo ndio wakati Kristo anatazamia kuona matunda kwako. Jambo ambalo ni kinyume kabisa na asili. Hana tabia ya kutafuta matunda wakati wa msimu. Haongozwi na misimu.

Embu kitafakari vizuri kitendo alichokifanya siku ile alipokuwa anakwenda Yerusalemu kutokea Bethania, alipokutana na ule mtini njiani, alifanya nini!. Utaona alikwenda moja kwa moja na kutafuta matunda juu yake, Na alipokosa akaulaani na kunyauka saa ile ile , pasipo kujali kuwa ule haukuwa hata msimu wake wa kuzaa..

Marko 11:12 “Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.

13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; MAANA SI WAKATI WA TINI.

14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia”.

Hili ni jambo ambalo watu wengi hawalifahamu, wanapoangalia mazingira Fulani, wanaona kama vile wakati wake bado, pale mtu unapomuambia biblia inasema “saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubalika kuokoka ni leo (2Wakorintho 6:2 )” yeye atasema, ngoja kwanza, siku moja nitaokoka tu!, ngoja nimalize chuo, ngoja nioe kwanza, ngoja nipate kazi, ngoja nitoke kwanza kwa wazazi wangu..Ngoja nijenge nyumba yangu kwanza..

Huku akitazamia kweli siku moja akishavipata hivyo vitu  ndio atatulia afikirie sasa kumtumikia Mungu. Lakini hajui wakati amekaa akiungojea huo wakati  ufike Kristo anatokea ghafla kwenye maisha yake, kutafuta matunda, anayakosa, hatua inayofuata kwake ni KULAANIWA MILELE.

Maana yake ni kuwa kamwe asahau WOKOVU katika maisha yako, na ndio maana watu kama hao ambao wana tabia ya kusubiri, subiri, kujivuta vuta, mwisho wa siku unawakuta mpaka wanakufa hawajaokoka haijalishi kuwa wameshapata kila kitu. Sio kwamba kulikuwa na ugumu wowote. Hapana lakini kwasababu walishalaaniwa na Yesu tangu zamani, walipotazamiwa wamzalie Kristo matunda wakashindwa.

Hivyo ndugu, tambua kuwa jicho lako sio jicho la Yesu. Wewe unatazama misimu, Yesu hajui msimu. Wewe unatazama nyakati, Kristo hajui nyakati. Wakati wowote anataka ajapo akukute, ukiwa na matunda. Akukute unamzalia matunda ya Roho. Lakini ukiwa ni mtu wa kusubiria siku Fulani ifike ndio ufanye maamuzi. Upo katika hatari kubwa sana ya kulaaniwa.

Wana wa Israeli, kuna wakati nao pia walijibunia utaratibu kama huo, wakati ambapo Mungu alishawapa tamko la kwenda kumjengea nyumba, Lakini walipopokea vitisho kutoka kwa mfalme aliyefuata kwamba waache ujenzi, wao nao wakasikiliza sauti yake kweli wakaacha. Ukisoma pale utagundua kuwa Kilichofuata ni Mungu kuwalaani, akawapiga kwa umaskini na shida zisizokuwa za kawaida. Mpaka siku walipogundua kosa lao, na kwenda kumjengea tena Mungu nyumba, walijutia mawazo yao.

Hagai 1:2 “Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya Bwana.

3 Ndipo neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema,

4 Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika”?

Leo hii, mtu akishazuiwa na wazazi wake, au boss wake, au mume wake, basi hiyo ndio inakuwa tiketi ya yeye kuukimbia kabisa wokovu au utumishi wa Mungu, akijitetea kuwa pengine haukuwa wakati sahihi na ndio maana vikwazo kama hivyo vimetokea. Nataka nikuambie, ondoa hayo mawazo kuanzia leo, kwasababu hata kwa Yesu hayapo, utalaaniwa.

Upokee wokovu leo, tubu dhambi zako leo, kuwa tayari kubatizwa katika ubatizo sahihi  leo, anza kuishi maisha matakatifu yampendezayo Mungu, bila kujali mazingira, watu, hali, au msimu,..Na baada ya hapo yeye mwenyewe atakupokea na kukujalia kuzaa matunda wakati huu huu, unaoonekana kama haufai kwako.

Kumbuka hizi ni siku za mwisho, wakati wa mavuno umekaribia sana, dalili zote zinaonyesha kizazi chetu tunachoishi kitashuhudia tukio halisi la kurudi kwa Bwana Yesu duniani mara ya pili, kulinyakua kanisa lake. Jiulize Ikiwa atarudi leo usiku utakuwa na lipi la kujitetea, ikiwa hukumpa maisha yako? Au ukifa leo utamweleza nini huko uendako kama Yesu si mwokozi wa maisha yako.

Usizifiche dhambi zako, ikiwa upo tayari kuokoka leo, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako. Basi popote pale kama utahitaji msaada huo wasiliana nasi kwa namba hizo hapo chini, au tafuta kanisa la kiroho lililo karibu na wewe, wakusaidie kupokea wokovu.

Kisha hakikisha unatafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi, na kwa jina la YESU KRISTO (Zingatia sana hilo), kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako. Na yeye mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

AINA TATU ZA WAKRISTO.

UFUNUO: Mlango wa 22

JE UNAYAFANYA MAPENZI YA MUNGU?

Mlima wa Mizeituni  unaumuhimu gani kwetu?

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

Rudi nyumbani

Print this post

UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.

Kuna silaha ambazo nataka ufahamu shetani anazozitumia kwa watu ambao wanakaribia kuokoka, au waliookoka lakini bado ni wachanga katika imani. Silaha hizo, zimewafanya watu wengi waishi katika hofu, na misongo mikubwa ya mawazo, mimi nikiwa mmojawapo kabla sijaokoka.

Nataka nikuambie mawazo haya yakikujia, yakatae kwa nguvu zako zote, kwasababu ni vita vya kifikra ambavyo shetani na majeshi yake ya mapepo wanavyoleta ili kukuangusha uiche imani, au usisonge mbele. Narudia tena usiruhusu hata kidogo mawazo hayo yakutawale;

     1)  Umemkufuru Roho Mtakatifu:

Hii ndiyo silaha ya ibilisi ya kwanza ; Anakuletea mawazo kuwa wewe huwezi kusamehewa, kwani dhambi yako ni ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Na anaweza kukurushia mpaka hayo mawazo ya namna hiyo ili ujione wewe tayari dhambi yako imeandikwa kwa kalamu ya chuma.

Nataka nikuambie, huo ni uongo tu, dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu haiji hivyo. Na kamwe mtu aliyemkufuru Roho hata hofu na Mungu hana ndani yake, ni mfano wa mafarisayo na masadukayo ambao walikuwa wanazipinga kazi za Roho Mtakatifu wazi wazi na kuzishuhudia hadharani kuwa ni za mapepo wakati wanaujua kabisa ukweli kwamba na Roho Mtakatifu ndiye aliyekuwa anafanya kazi zile (Mathayo 12:24-32).

Sasa jiulize wewe ni lini ulishawahi kwenda kuzipinga kazi za Roho Mtakatifu huku ukajua kabisa ndio yeye, halafu ukatoa maneno ya kufuru  na kusema zile ni kazi ya mapepo..Ulishawahi kufanya jambo kama hilo mbele ya kadamnasi? Ni wazi kuwa hujawahi kufanya.. Sasa hayo mawazo ya wewe umemkufuru Roho Mtakatifu yametoka wapi kama sio kwa shetani?

Watu wengi, nimewasiliana nao, wamekuwa wakisumbuliwa na mawazo mkandamizo kama hayo, Lakini leo nataka nikuambie Usiogope, hiyo ni ishara kuwa Mungu yupo karibu na wewe sana, unachopaswa kujua ni kufahamu ile kweli, ili ikuweke huru kweli kweli.

   2) Bado hujaokoka: 

Unaweza ukawa umetubu kweli dhambi zako kwa kudhamiria kuziacha, na ukabatizwa katika ubatizo sahihi, na baada ya hapo ukaanza kuishi maisha yanayompendeza Mungu, Lakini kipindi fulani kikapita shetani akakuletea mawazo kwamba bado hujaokoka, wanaookoka hawawi kama wewe. Mawazo kama haya, yakatae, Bwana Yesu alisema, “Hakuna mtu anayeweza kwenda kwake, kama Baba yake hajamvuta kwake (Yohana 6:44)” Hivyo mpaka wewe umefikia hatua ya kutubu, na kubatizwa na kuanza kuonyesha bidii ya kuishi sawasawa na mapenzi yake, haikuwa kwa akili zako, bali ni Yesu mwenyewe alikuvuta.

Hivyo songa mbele, zidi kujitakasa siku baada ya siku, mpaka kuufikia ukamilifu kwasababu Yesu yupo pamoja na wewe.

  3) Umeshachelewa:

Hili ni jambo lingine ambalo, limewadhoofisha wengi. Wanadhani elimu ya kidunia ni sawa na elimu ya ufalme wa mbinguni. Elimu ya kidunia, ukishakuwa mtu uzima na hujaenda shule, unaweza ukaonekana kama umeshachelewa. Duniani ukifikisha umri fulani hujaolewa, au hujapata kitu fulani umeshachelewa. Lakini kwa Mungu haiendi hivyo, maadamu pumzi ya uhai ipo ndani yako bado hujachelewa kumtumikia yeye.

Mungu anakutazama, ufanye vizuri isipokuwa tu uonyeshe bidii, ili ufanye vizuri kuliko hata wale ambao walikuwepo tangu zamani. Embu mkumbuke mtume Paulo, hakuwa miongoni mwa wale 12, wala siku ile ya Pentekoste hakuwepo. Lakini alikuja kufanya kazi kubwa kuliko wote waliomtangulia.

Ukumbuke pia ule mfano wa mwajiri na waajiriwa ambao Bwana Yesu aliutoa, akasema kulikuwa na wengine ambao walikutwa jioni kabisa hawana kazi yoyote, wakaambiwa waende shambani, na kule shambani walipomaliza shughuli yao, wakalipwa sawa sawa na wale wengine, ambao walikuwa tangu asubuhi shambani.(Mathayo 20:1-16). Na ndio maana Bwana Yesu akamalizia na kusema “wapo walio wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wale wa kwanza watakuwa wa mwisho”.

Vivyo hivyo na wewe, ikiwa umeitwa kwenye miaka ya 20, au 30 au 40 au 50 au 80. Hujachelewa  popote pale. Mtumikie Bwana kwa moyo wako wote na kwa uaminifu. Na thawabu yako inaweza kuwa kubwa kama tu ile ya mitume.

   4) Mungu hawezi kupendezwa na wewe:

Haya mawazo yanakuja hususani pale ambapo pengine hukutumiza wajibu wako fulani uliloambiwa na Mungu ufanye, au ulifanya dhambi fulani ambayo ilikuwa ni ya makusudi kabisa kwa Mungu, pengine ulivunja viapo vya ndoa yako ukaenda kuzini, au uliua mtu, au uliiba n.k..

Nataka nikuambie kama umetubu tayari kwa kumaanisha kutoka katika moyo wako. Basi usiruhusu tena hayo mawazo yawe ndani yako, kukutawala. Mrudie Mungu wako, mtumikie kwa bidii, kwani kumpendeza tena kunawezekana, na akawa rafiki yako, zaidi hata ya pale mwanzo kama utatii. Daudi alizini ni mke wa Uria, lakini alitubu, hata baada ya kuadhibiwa na Mungu, aliendelea kumtafuta Mungu wake, na mwisho wa siku bado akawa mtu ambaye ameupendeza moyo wa Mungu.

    5) Fulani ni bora kuliko wewe mbele za Mungu:

Haya ni mawazo mengine ya ibilisi, kukukandamizi tu usipige hatua, kwamba fulani ni zaidi yako wewe mbele za Mungu. Hilo jambo halipo, Mungu hana utaratibu huo wa kulinganisha watu.Yeye huwa anasimama katika utaratibu wake. Ni sawa na mwalimu anayesahihisha mitihani, hasahishi kwasababu fulani ni machachari kuliko wengine, hapana, bali kwasababu amejibu sawasawa na alichotaka.

Ndivyo ilivyo kwa Mungu, hana habari na sura ya mtu, ikiwa wewe utatembea katika njia zake, basi atakuwa rafiki kwako, wala hakulinganishi na mtu mwingine aliye juu yako au aliye chini yako, na Yule mwingine hamlinganishi na wewe, bali wote anawalinganisha na Neno lake, kila mmoja kivyake.

Hivyo na wewe tembea katika njia yako, na Mungu wako, acha kujilinganisha na fulani, jilinganishe na biblia. Vinginevyo shetani atakuletea mikandamizo ya mawazo ukashindwa kumtumikia Mungu kwa ufanisi, kwa kumwona fulani tayari ni mtiwa mafuta wa Bwana, wewe huwezi kumfikia yeye.

Mawazo kama hayo yakatae.

Kumbuka, kuingia katika wokovu ni kurahisi sana, lakini kudumu kunakuwa kugumu, na hiyo yote inasababishwa na shetani na mapepo yake, Na dawa ya shetani sio tu kuomba, bali pia kulijua NENO. Nikisema Neno, sio kukariri vifungu vya biblia hapana, bali kupata ufunuo wa Neno la Mungu katika maisha yako ya kila siku.

Bwana Yesu alimshinda shetani kwa Neno kule jangwani, vivyo hivyo na wewe. Mungu anaweza akawa ameshakupa uhuru, lakini kama hutakuwa na maarifa ya kutosha ya kuupigania uhuru wako, bado ibilisi atakusumbua hata kama umeokoka. Maombi ya kufunguliwa pekee hayawezi kukufanya kuwa huru.. Kama ni hivyo Bwana Yesu asingesema..Mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru” (Yohana 8:32)Umeona kinachokamilisha uhuru wa mtu ni KWELI, na KWELI ni Neno la Mungu. (Yohana 17:17)

Hivyo jitahidi sana, uwe mtafakariji wa Neno. Ili ujue nafasi yako kwa Mungu ni ipi, wakati huu ni wakati wa vile VITA vikali ambavyo, Danieli alionyeshwa, katika (Danieli 10:1). Si vita tena vya kimwili, bali vita vya kifikra vinavyoletwa na ibilisi na mapepo yake.

Kama hujatubu, nafasi bado unayo. Tubu sasa mgeukie muumba wako, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako, ikiwa hukufanya hivyo. Na baada ya hapo Mungu atakupa Roho wake Mtakatifu atakayekusaidi kuifahamu kweli yote ili uwe huru (Yohana 16:13).

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

Nakusalimu katika jina kuu sana la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuyatafakari maandiko maadamu siku ile inakaribia.

Tukitazama matukio yaliyokuwa yanaendelea pale msalabani yapo mambo kadha wa kadha tunaweza kujifunza. Kwamfano siku ile utaona walimvua  nguo zake zote, wakazigawanya mafungu manne, kila askari fungu lake. Hii ikiwa na maana kuwa Bwana Yesu alisulibiwa akiwa uchi kabisa, hakutuonea haya sisi, iweje sisi tumwonee haya  yeye?

Lakini wale askari walipofika kwenye Kanzu yake nayo, kwasababu ilikuwa ni ya Tano, na wenyewe walikuwa ni wanne, na kila mmoja alitaka apate sehemu ya vazi lile..Wakaona njia rahisi ni kuligawanywa, walau kila mtu apate kipande chake.

Lakini lile vazi lilikuwa ni la kitofauti sana, lilikuwa halijashonwa kwa kuunganishwa vipande mbalimbali hapana.Bali Lote tokea juu hadi chini lilikuwa ni vazi moja, kiasi kwamba kulikuwa hakuna sehemu lilikuwa na kipande kilichojitegemea kikaunganishwa nalo hapana. Unaweza kutazama mfano wa vazi hilo kwenye picha juu.

Hivyo wale askari walipotafuta walau, maungio ya vazi lile ili wawezi kukata wagawane kila mtu kipande chake hawakuona. Pengine walitafuti kwenye mikono hawakuona, kwenye kola hawakuona, kwenye mfuko hawakuona. Mwishoni wakaona ni heri walipigie tu kura, ili liwe la mmojawapo.

Yohana 19:23 “Nao askari walipomsulibisha Yesu, waliyatwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu.

24 Basi wakaambiana, Tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani. Ili litimie andiko lile linenalo, Waligawanya nguo zangu, Na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari”.

Lakini tunaposoma habari hiyo ni jambo gani Mungu anataka tujue? Je! Ni mambo ya mavazi yake tu kupigiwa kura tu au ni nini?

Ujumbe mkuu Mungu anataka tuone hapo  ni  kwamba VAZI LA YESU HALIGAWANYI.. Kwasababu halija ungwaungwa, kama mengine yalivyo. Kama utalihitaji ni sharti ulichukue lote, au uliharibu kabisa, hakuna namna..

Hata sasa, mtu yeyote anayeamua kuwa mkristo, hana budi alivae vazi hili. Ambalo haliungwi ungwi.. Ndilo linalojulikana kama VAZI LA WOKOVU, Tunalolisoma katika

Isaya 61:10 “Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana AMENIVIKA MAVAZI YA WOKOVU, AMENIFUNIKA VAZI LA HAKI, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu.

Unapolivaa vazi hili ni  lazima UUISHI wokovu wote, huwezi kuyakwepa maisha ya utakatifu.. Wakristo wengi wanatafuta kuligawanya vazi la wokovu wawe nalo kwa sehemu tu, hawataki kujitoa kikamilifu kwa Mungu pale wanapookoka. Wanataka waitwe wanakwaya, lakini bado waendelee na uzinzi kwa chini chini, wanataka waitwe vijana waliokoka, lakini waendelee kwenda disco, wavae vimini, na milegezo, na viduku, Wanadhani, hilo jambo linawezekana katika wokovu. Ni kweli litawezekana kwenye dini zao, na madhehebu yao, lakini kwa KWA YESU hilo jambo halipo.

Ndugu, watakaokwenda kwenye UNYAKUO, watakuwa wale tu walio tayari kulichukua vazi lote la Yesu, hao ndio wanaojulikana kama BIBI-ARUSI wa Kristo. Lakini tukijidanganya kuwa tumeokoka, halafu bado tupo nusu nusu, hatueleweki sisi ni wa upande upi, ipo wazi kuwa wakati ule tatabaki tu hapa duniani kwenye dhiki kuu ya mpinga-Kristo, na kama hutakuwa hai, basi utaendelea kubakia makaburini mpaka siku ile ya ufufuo itakapofika uhukumiwe uende motoni.

Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; KWA MAANA KITANI NZURI HIYO NI MATENDO YA HAKI YA WATAKATIFU”.

Naamini utakuwa unatambua kuwa tunaishi katika kanisa la Laodikia, na uvuguvugu na tabia ya kanisa hili ni kuwa lipo Vuguvugu, tofauti na  yale mengine. Hivyo Bwana atuepushe na uvuguvugu huu uliopo duniani leo.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Wanefili walikuwa ni watu gani?

Wanefili tunawasoma kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Mwanzo 6:4, Tusome..

Mwanzo 6:4 “Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana; HAO NDIYO WALIOKUWA WATU HODARI ZAMANI ,WATU WENYE SIFA.

5 Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.”

Sasa tafsiri ya wanefili ni “watu wakubwa”.. yaani watu wenye maumbo makubwa. Hivyo wanefili walikuwa ni watu wenye miili makubwa sana.. Na biblia inaendelea kusema kuwa walikuwa ni WATU HODARI na WENYE SIFA. Maana yake walikuwa ni watu wenye uwezo mkubwa wa kiakili na vile vile walikuwa ni watu wenye sifa (maaana yake maarufu na wanaojulikana sana). Hivyo hawakuwa tu wakubwa kama tembo halafu hawana akili, hapana! Walikuwa wakubwa na vile vile walikuwa na uwezo mkubwa wa kiakili, ambao uliwafanya wawe maarufu.

Sasa asili ya hawa wanefili ilianzia kwa Kaini. Ikumbukwe kuwa Kaini baada ya kumuua ndugu yake, alilaaniwa na Mungu, na baada ya ile laana, Mungu alimtia alama Kaini ili yeyote atakayemwona asimuue.

Mwanzo 4: 13 “Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.

  14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.

 15 Bwana akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. BWANA AKAMTIA KAINI ALAMA, MTU AMWONAYE ASIJE AKAMPIGA.

 16 Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni”

Umeona hapo? Kaini anatiwa alama na Mungu, ili kila atakayemwona asimpige!.. Sasa alama hiyo aliyotiwa na Mungu sio mchoro Fulani katika mwili, hapana bali ni UKUBWA WA MWILI NA AKILI, hiyo ndiyo alama aliyowekewa Kaini na Mungu, ambayo itakuwa kwake kama ulinzi, kila atakayemwona na kujaribu kumdhuru aogope!..  kwa kawaida ni ngumu kujaribu kupambana na mtu aliyekuzidi ukubwa!

Kwahiyo Uzao wa Kaini, Mungu aliupa akili na ukubwa, ingawa ulikuwa umelaaniwa..Laana ile ilimfanya Kaini na uzao wake kuacha kazi zao za ukulima, kwasababu walishalaaniwa, na kuanza kufanya kazi nyingine za ufugaji na utengenenezaji wa bidhaa..Ndio maana ukiendelea mbele kidogo kusoma utaona wana wa Kaini wanajishughulisha na utengenezaji wa vyuma na shaba na bidhaa nyingine, kama vifaa vya muziki n.k. (Mwanzo 4:22)

Hivyo kwa shughuli hizo zikawafanya wawe watu maarufu sana duniani na hodari, wakajenga miji mikubwa, na wakawa na ustaarabu wao, wakazaliana wao kwa wao, na wakafanyiana biashara wao kwa wao kwa hizo bidhaa zao na hivyo wakawa na ngome kubwa duniani…

Kutokana na ngome yao kuwa kubwa, na ukubwa wa teknolojia yao, maana ndio watu wa kwanza kugunudua vyuma, shaba na madini mengine yote,  na zana zote za kazi, ni wazi kuwa jamii nyingine za watu ziliwaogopa.. (ili litimie neno la Bwana kwamba kila atakayemwona Kaini asimuue) na pengine walijiwekea sheria ya kwamba yeyote atakayemuua mtu yeyote wa jamii ya uzao wa Kaini adhabu yake ni “kulipiziwa kisasi mara saba”, kwasababu wao ndio walikuwa hodari na wenye nguvu kuliko wengine wote. Ni sawa na wakati wana wa Israeli wapo Misri utumwani, ni wazi kuwa ilikuwa ni kosa kubwa sana kwa mwisraeli aliye mtumwa kumuua Mmisri, pengine adhabu yake ilikuwa ni kubwa sana!. Au wakati wa kipindi cha ukoloni,barani Afrika, inawezekana ilikuwa ni adhabu kubwa sana, mtu mweusi kumuu mtu mweupe!, kutokana na nguvu walizokuwa nazo watu weupe!.. Ndicho kilichokuwa kinaendelea katika dunia ya wakati wa Nuhu.

Lakini wakati huo huo uzao wa Sethi ambao Mungu aliuweka ili kuziba pengo la Habili, ulikuwa ni wa watu wakawaida wakulima na vile vile wafugaji. Uzao huu haukulaaniwa, ndio WANA WA MUNGU tunaowasoma katika Mwanzo 6:2. Na walikuwa ni watu wenye Miili ya wastani, (kwaufupi ni watu wa kawaida tu), na hawakuwa hodari kama hawa Wana wa Kaini (Wanefili).. uzao wa Kaini ndio ulioitwa WANA WA WANADAMU na wanawake wao Binti za Wanadamu (Mwanzo 6:2)

Hivyo wana wa Mungu walipowatamani hao binti za wanadamu na kuwaoa, jambo hilo likamchukiza Mungu, kwasababu ni dhahiri kuwa waliwageuza mioyo, wakapunguza au wakaacha kabisa kumtumainia Mungu wa mbingu na nchi. Hivyo dunia ikajaa dhuluma, kukawa hakuna tena watu wanaomcha Mungu..

Kwahiyo wanefili walikuwa ni wanadamu, ambao ni uzao wa Kaini, na si (mchanganyiko wa wanadamu na malaika), biblia inasema Malaika hawaoi wala hawaolewi (Marko 12:25).

Lakini hata leo hawa wanefili wapo!. Wanaweza wasiwe wakubwa kimwili lakini ni wakubwa kiulimwengu!. Watu wenye sifa na hodari, ambao wanaweza kutengeneza ala za miziki ambazo zinaweza kuiteka dunia nzima, ambao wanaweza kutengeneza filamu na ikakomba watu wengi, ambao wanaweza kutunga mitindo wa mavazi ikaharibu mamilioni ya wanawake, ambao wanaushawishi mkubwa wa kimawazo ambayo ni kinyume na mapenzi ya Mungu, hao ndio wanefili wa kipindi hichi…

Na biblia inasema kama zilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa siku za kuja kwake mwana wa Adamu (Luka 17:26). Siku za Nuhu wana wa Mungu waliwatamani binti za wanadamu.. kadhalika siku hizi wana wa Mungu (wakristo) wanawatamani binti za wanadamu (wanawake wa kiulimwengu), na wanawake wa kikristo wanawatamani wana wa ulimwengu huu, na kujitafutia wanaume wanaowataka!, pasipo hata kujali vigezo vya kibiblia. Jambo ambalo ni machukizo mbele za Mungu kwasababu watawageuza mioyo na kuwafanya wamwache Mungu. Ndicho kilichotokea wakati wa Nuhu.

Binti wa Mungu, jiepushe na tamaa za ulimwengu huu.. Furaha pekee ya maisha utaipata kwa Yesu na si kutafuta kuoelewa na mtu asiyemcha Mungu, huyo atakugeuza moyo wako umwache Mungu, maandiko yanasema hivyo. (1Wafalme 11:2-4)

Kijana uliyemwamini Yesu, jiepushe na wanawake wa kidunia, usiitamani mitindo yao, wala mionekano yao…hao watakugeuza moyo, kama walimgeuza Sulemani aliyekuwa na Hekima kuliko watu wote, hawatakushindwa wewe!!. Hivyo Kabla ya kukimbilia kuoa, ni heri ukambadilisha kwanza ampokee Yesu Yule Yule uliyempokea wewe, na awe na imani ile ile uliyonayo wewe, na ubatizo ule ule ulionao wewe, na Roho Mtakatifu Yule Yule uliyenaye wewe (Waefeso 4:5). Vinginevyo utakuwa unajiharibia mwenyewe.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba wanefili walikuwa ni majitu, hawakuwa na habari na Mungu isipokuwa mambo ya ulimwengu huu!. Walikuwepo wakati wa Nuhu, na baada ya Nuhu walikuwepo na hata leo wapo!

Bwana atubariki na kutulinda.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

MUNGU HAONI SHIDA KUMUHAKIKISHIA MWOVU ULINZI.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?

SWALI: Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”. Kwanini isingesema tu mara moja saba, mpaka ianze sita,halafu tena saba?


JIBU: Ni lugha ya zamani, iliyotumika kuwekea msisitizo kitu hususani kile cha mwisho, yaani, kama inadhaniwa ni sita, basi kipo na cha saba ambacho ndio zaidi.

Kwa mfano ukisoma ile Mithali 6:16  inayozungumzia mambo sita ambayo Mungu anayachukia utaona anaongezea na kingine cha saba, ambacho  ni “kupanda mbegu ya fitina katika ya ndugu” ikiwa na maana hicho ndio kibaya zaidi..

Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.

17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;

18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;

19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu”.

Ukisoma pia  Mithali 30:18 “utaona Sulemani anasema tena kati ya mambo ambayo yanamshangaza mienendo yao, yapo matatu lakini lile la nne ndio zaidi, ambalo ni mwendo wa kijana pamoja na msichana.

Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.

19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana”.

Vivyo hivyo, ukisoma Mithali 30:29, Sulemani anasema pia vipo vitu vitatu vyenye mwendo wa kupendeza lakini akakiongezea na cha nne chenye mwendo wa kupendeza zaidi nacho ni mfalme asiyehasika.

Mithali 30:29 “Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote;

31 Jimbi aendaye tambo; na beberu; Na mfalme ambaye haasiki”.

Soma, pia vifungu hivi;

Mithali 30:15 “Mruba anao binti wawili, Waliao, Nipe! Nipe! Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!

16 Kuzimu; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!”

Ayubu 5:19 “Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.

Amosi 1:3 “Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Dameski, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya kupuria vya chuma”;

Soma pia Amosi 1:4.

Na hata sasa, katika mambo saba(7) ambayo  biblia inasema yanamkamilisha mwanadamu, lipo la nane(8) ambalo ndio kuu zaidi linaloitwa UPENDO.

Tusome.

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,

6 na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa,

7 na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, UPENDO.

8 Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.

Ni vizuri tukawa na hayo mengine yote, lakini tukikosa upendo wa Ki-Mungu, basi bado hatujakamilishwa.

Je! Upendo wa AGAPE upo ndani yako?

Ili kufahamu tunaupate upendo wa namna hii, fungua link hii>>

https://wingulamashahidi.org/2020/12/21/nitaupataje-upendo-wa-ki-mungu-ndani-yangu/ 

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

UFUNUO: Mlango wa 1

Je! kuna madhara kuchukiwa na kila mtu kwasababu huna mali?. Kama biblia inavyosema katika Mithali 14:20?.

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Rudi nyumbani

Print this post

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

Adui yetu shetani, ni kama simba angurumaye akitafuta mtu wa kummeza (1Petro 5:8), hivyo usiku na mchana anatupigana vita ili mradi, atuangushe au atwae vile tulivyo navyo.

Leo tutaingalia njia moja anayoitumia kutunyang’anya baraka zetu.

Shetani akishajua kuna Baraka Fulani umeahidiwa na Mungu, moja kwa moja anaanza kutafuta njia ya kukupokonya hiyo, sasa tofauti na wengi wanavyodhania kuwa adui yetu shetani anatunyang’anya baraka zetu kwa kutuloga, au kututumia wachawi!.. La! Hakuna uchawi wowote unaweza kubatilisha Baraka za Mungu alizotuahidia kwa kinywa chake.

Wengi wanapoteza nguvu nyingi na muda mwingi kushughulika na wachawi na washirikina wakidhani wao ndio wanaozuia Baraka Mungu alizowaahidia juu ya maisha yao kumbe sio!. Shetani anajua kabisa hawezi kamwe kutupokonya kile Mungu alichotuahidia, hizo nguvu hana!. Mungu akisema nitakupa hiki au kile, shetani hawezi kubatilisha hilo jambo..hivyo hatumii uchawi, wala uganga!.. Anachotumia ni kutafuta tu njia ya kumkosesha mtu na Mungu wake ili Mungu aibatilishe ile ahadi aliyomuahidia… Huo ndio uchawi mkubwa wa shetani, wala si mwingine!.

Kwamfano umekwenda katika njia za haki, umekuwa mnyenyekevu mbele za Mungu, umemtumikia na Mungu akapendezwa na wewe sana, hata akakupa ahadi kama alivyompa Ibrahimu, pengine  labda ya kuishi miaka mingi, au hata ya kupata mtoto au jambo lingine lolote zuri..na pengine akakuonyesha kabisa hata katika maono, au hata akamtuma malaika wake kukupa huo ujumbe.

Anachofanya shetani baada ya kujua kuwa umepewa ahadi kabambe kama hiyo, si kukutumia wachawi wakuloge au wachukue nyota yako.. la! Hawezi kufanya hivyo kwasababu anajua atakuwa anapoteza muda..atakachokifanya ni kuhakikisha wewe unaitumainia ile haki yako ya kwanza, na kuanza kukufanya upoe kuendelea kutenda haki.. ili Mungu achukizwe na wewe, na aiondoe ile ahadi aliyokuahidia…

Utauliza je! Mungu huwa anabatilishaga ahadi zake? Jibu ni ndio!.. Endapo mtu akiacha njia yake ya haki na kurudia uchafu, Mungu huwa anazighairi zile ahadi zote alizomwahidia mtu, haijalishi alimtuma malaika wake kumpelekea ujumbe, au alimtokea yeye mwenyewe, lakini mwisho ataibatilisha tu… Utauliza ni wapi katika maandiko tunasoma hilo…

Ezekieli 33:13 “Nimwambiapo mwenye haki, ya kwamba hakika ataishi; KAMA AKIITUMAINIA HAKI YAKE, AKATENDA UOVU, basi katika matendo yake ya haki, hata mojawapo halitakumbukwa; bali katika uovu wake alioutenda, atakufa katika uovu huo”.

Bwana akikupa ahadi ya kuishi miaka mingi, ukikengeuka na kuacha haki yako, utakufa kabla ya kutimiza miaka yako, japokuwa alishakuonyesha kuwa utaishi miaka mingi.

Dada, unayemcha Mungu sasa, Bwana akikuonyesha kuwa umebeba mtoto siku za mbeleni, au atakutumia kwa viwango vikubwa mbeleni na wewe ukakengeuka, na kuanza kufanya uasherati, ukaanza kuvaa kama wanawake wa kidunia wanavyovaa, ukaanza kuwa msengenyaji n.k, hiyo ahadi utaisahau.. Utabaki kujiuliza kama kweli ni Mungu alizungumza na wewe siku ile au la!.. Utatanga tanga huku na kule.. Na jambo hilo halitatimia kwako, na mwisho utakata tamaa na kusema Mungu ni mwongo!. Si mwongo, tayari shetani kashaitwaa Baraka yako siku nyingi sana, na wala hajaitwaa kwa uchawi!.. Ameitwaa kwa kukufarakanisha wewe na Mungu wako.

Kumbuka siku zote kuwa, Bwana akikupa ahadi ya jambo Fulani haimaanishi kuwa hilo jambo ndio tayari umeshalipata!. (Hilo usilitoe katika akili yako)

Inawezekana na wewe leo hii shetani kashakunyang’anya taji yako, au ahadi yako nzuri ambayo Mungu alishakupa…shetani ameshakurudisha kwenye ulimwengu, ndio maana huoni tena dalili ya ile ahadi  Mungu aliyokupa kutimia, alikuonyesha maono ya kwamba utakuja kumtumikia, na tena kwa viwango vikubwa.. lakini mpaka sasa huoni chochote unajiuliza ni Mungu kweli alikuonyesha yale maono au ni kitu gani!..

Ndio ni Mungu mwenyewe ndiye aliyekuonyesha, na wala hakukudanganya, isipokuwa ni  wewe ndio umemruhusu shetani kuitwaa taji yako…. Ulisahau kuwa ahadi za Mungu zinatimia juu yetu, endapo tu tukidumu katika mapenzi yake, tunapotoka katika mapenzi yake hakuna ahadi yoyote ya Mungu itakayotimia juu yetu.

 Lakini habari nzuri ni kwamba tumaini bado lipo, hata kama shetani kakuibia Baraka yako, upo uwezekano wa wewe kuirudisha tena, na zile Baraka zote zilizofutwa juu yako zikakurudia…

Ezekieli 33:15 “kama mtu mwovu akirudisha rehani, na kumrudishia mtu mali yake aliyomnyang’anya, akizifuata sheria za uzima, asitende uovu wo wote; hakika ataishi, hatakufa.

16 Katika dhambi zake zote alizozitenda, hata mojawapo haitakumbukwa juu yake; ametenda yaliyo halali na haki; hakika ataishi.”

Unachopaswa kufanya sasa, ni kutubu!..na kumrudia Bwana kwa moyo wako wote!.. sio umrudie kwasababu tu unataka Baraka!. Bali urudi kwasababu kweli umejua wewe ni mkosaji, njia zako ni mbovu, kama ulikuwa unaiba unaacha wizi, na unarudisha vile ulivyoiba kama bado vipo katika uwezo wa mikono yako, kama ulikuwa ni mzinzi unaacha uzinzi, kama ulikuwa ni mlevi unaacha ulevi kwa vitendo, kama ulikuwa unavaa vibaya, (Ni mwanamke lakini unavaa suruali, vimini, wigi, hereni, unapaka lipstick n.k) yote hayo unaacha, mwanaume kama ulikuwa unanyoa mitindo ya kidunia, na ulikuwa unavaa nguo za kidunia unaacha..na mambo mengine yote yasiyofaa.. Na baada ya kuacha yote hayo, na kutubu hatua inayofuata ni ubatizo, kumbuka ubatizo ndio unaokamilisha wokovu kwa mtu (Marko 16:16). Na ubatizo sahihi ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo.

Na baada ya hapo Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yako, atakuongoza na kukutia katika kweli yote. Na yeye mwenyewe atazirejeza zile Baraka zote na ahadi zote zilizokuwa zimefutwa juu yako. Utaziona zinatimia mbele ya macho yako.

Hiyo ndiyo njia rahisi ya kurejesha Baraka zako na Ahadi zako, wala huhitaji kuombewa na mtu.. Na wewe tu kurejesha mahusiano yako na Mungu, ambayo yalikuwa yamevurugwa..na Baraka zako zote utaziona..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni vitu vipi hivyo viwili visivyoweza kubadilika? (Ebr 6:18)

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

Ni vitu vipi hivyo viwili visivyoweza kubadilika? (Ebr 6:18)

Rudi nyumbani

Print this post

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo litukuzwe milele. Karibu tujifunze Neno la Mungu.  Kuna wakati sisi wenyewe ndio tunakuwa kikwazo cha Kristo kujifunua kwetu katika utimilifu wake wote, na hiyo yote ni kwasababu tuna mioyo miwili miwili kwake. Leo tutaangalia makundi mawili ya watu. Moja ni wale mafarisayo, na la pili ni mitume wa Yesu likiongozwa na Nathanieli.

Kuna wakati mafarisayo walimwomba Yesu awaonyeshe Ishara itokayo juu ili waamini zaidi, Lakini Yesu akawaambia kamwe hawatapewa Ishara yoyote, isipokuwa ile ishara ya Yona.Akiwa na maana Ishara ya hukumu.

Mathayo 12:38 “Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.

39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi”.

Ili kufahamu kwa urefu alikuwa anamaanisha nini, juu ya hiyo  ishara ya Yona unaweza kufungua link hii kusoma >>> https://wingulamashahidi.org/2019/05/13/madhara-ya-kutafuta-ishara/ 

Lakini Bwana hakuwa na nia ya kutojifunua kwao zaidi, isipokuwa ile mioyo yao, ya kutokuamini, ya unafki, ndio iliyowapelekea kutoona utukufu wa Mungu mkubwa zaidi ya yale waliyoyaona, akiyafanya.

Lakini kulikuwa na wakati ambao Yesu yeye mwenyewe aliwathibitishia wale waliomwamini kuwa wataona mambo makubwa zaidi ya yale waliyomjua kwayo. Lakini hiyo yote ilihitaji kwanza watu hao kutokuwa na “HILA” ndani yao kama Nathanieli alivyokuwa.. Tusome..

Yohana 1:43 “Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate.

44 Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro.

45 Filipo akamwona Nathanaeli, akamwambia, Tumemwona yeye aliyeandikiwa na Musa katika torati, na manabii, Yesu, mwana wa Yusufu, mtu wa Nazareti.

46 Nathanaeli akamwambia, Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone.

47 Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, HAMNA HILA NDANI YAKE.

48 Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona.

49 Nathanaeli akamjibu, Rabi, wewe u Mwana wa Mungu, ndiwe Mfalme wa Israeli.

50 Yesu akajibu, akamwambia, Kwa sababu nilikuambia, Nilikuona chini ya mtini, waamini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.

51 Akamwambia, Amin, amin, nawaambia, Mtaziona mbingu zimefunguka na malaika wa Mungu wakikwea na kushuka juu ya Mwana wa Adamu”.

Kama tunavyoweza kusoma hapo, Nathanieli alipokutana na Filipo hakuona shaka ndani yake, juu ya habari njema alizoletewa, japokuwa zilikinzana na kile alichokifahamu hapo kabla..Lakini alikuwa radhi kwenda kufuatilia, kwasababu nia yake ilikuwa ni kupata jambo jema, na sio kitetea dini..

Leo hii ni watu wachache sana, wanaweza kuwa tayari kusikia au kufuatilia lile jambo linalokinzana na imani yao, au dhehebu lao, hata kama watajua ni kweli kiasi gani, bado watapuuzia tu, wakiambiwa katika maandiko hakuna ubatizo wa vichanga, wanadhani wanapelekewa dini mpya, ukiwaeleza habari za kuokoka watakuambia dhehebu lao haliamini hilo.. Unaona, hizo ni HILA zilizondani ya mtu. Lakini Nathanieli hakuwa hivyo? Yeye alipoelezwa tu habari za MASIHI, Akauliza, Je! Inawezekana kweli jambo jema kutokea Nazareti mji ambao haujaandikiwa chochote? Lakini yeye hakuacha kwenda kutazama, ajihakikishie.

Na matokeo yake Yesu alipomwona, hakuhitaji kujieleza mbele zake, Yeye mwenyewe alimtamkia habari zake. “Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake”. Hakuwa na wingu la udhehebu wala udini kama mafarisayo walivyokuwa..Yeye alikuwa radhi kwenda kutazama, mahali ambapo hata hapana uelekeo wa kutokea Kristo.

Na matokeo yake ikawa ni Yesu kuwaambia wataona makubwa zaidi ya yale.. Yaani atajifunua kwao kwa katika viwango vingine vya juu sana, kwasababu walikuwa tayari kumwamini na kumfuata. Na ndio utaona ni hao peke yao ndio walioweza kumwona Yesu mpaka hatua ya mwisho ya kupaa kwake.

Hata na sisi leo hii, tukumbuke kuwa Yesu ni yeye Yule jana na leo na hata milele. (Waebrania 13:8).  Yupo tayari kutuonyesha makubwa zaidi ya haya tunayoyajua, lakini ufarisayo wetu, uvuguvugu wetu, ndio unaotukwamisha tusimjue Kristo katika viwango vingine vya utukufu.

Tunadhani Yesu ni ile sura yake tu basi, hapana, Yesu ni Ufunuo wa Mungu mwenyewe. Na huwa hajifunui kwa watu wote sawasawa. Na ndio maana alivyotembea na mitume haikuwa sawa na alivyotembea na makutano, vilevile sio yote aliyowafunulia mitume aliwafunulia makutano au waandishi. Na sio kila mahali alipopita watu wote walijua. Hapana.

Hiyo yote ni kuonyesha kuwa anajifunua na kutembea katika viwango.

Hata sasa,  yatupasa tumwamini Yesu, tuiamini biblia, tuondoe HILA mioyoni mwetu. Tuwe tayari kutii kile ambacho biblia inatufundisha hata kama kitakinzana vipi na madhehebu yetu, tukiona maandiko yanatuambia tubatizwe kwa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, tutii, tukiambiwa sanamu ni machukizo kwa Mungu, tutii, tukiambiwa hakuna njia nyingine yoyote ya kutufikisha mbinguni isipokuwa ya Yesu tu peke yake, na sio mtume mwingine fulani tuamini hilo, hata kama dini zetu zimetufundisha hivyo tangu tulipozaliwa kuwa kuna mtume mwingine.

Tukizingatia mambo kama hayo, ambayo ni maagizo ya Yesu mwenyewe kwenye BIBLIA yake. Basi tujue kuwa tupo kwenye daraja kubwa sana, na kumwona yeye katika viwango vingine vya tofauti sana, vya mbingu kufunguka juu yetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

BIRIKA LA SILOAMU.

RABI, UNAKAA WAPI?

Rudi nyumbani:

Print this post