TUYASHIKE SANA MAUNGAMO YETU.

TUYASHIKE SANA MAUNGAMO YETU.

Waebrania 4:14  “Basi, iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu

Kuungama maana yake ni kukiri kwa wazi jambo fulani mbele ya wote… Katika ukristo tunaungama kwa “kukiri kwa vinywa vyetu kuwa Yesu ni Bwana na mwokozi wa maisha yetu, na kukiri kwa vinywa vyetu kuwa sisi ni wenye dhambi, na kutubu!”.. sawasawa na Warumi 10:10.

Warumi 10:9 “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.

Biblia inazidi kutufundisha kuwa ni lazima TUYASHIKE MAUNGAMO YETU, maana yake tusikiri tu kwa vinywa na kusahau, bali yale tuliyoyakiri mbele za Mbingu na Nchi, hayo TUYAISHI siku zote za maisha yetu.

Sasa swali tunayashikaje/tunayaishije Maungamo yetu?.

Tusome 1Timotheo 6:12.

1Timotheo 6:12 “PIGA VITA VILE VIZURI VYA IMANI; SHIKA UZIMA ULE WA MILELE ULIOITIWA, ukaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi wengi

 13  Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato”.

Kumbe tunayashika Maungamo yetu kwa kuvipiga vita vya Imani, na kushika ule uzima wa milele tulioitiwa!. Hebu tutazame moja baada ya lingine.

1.PIGA VITA VYA IMANI.

Vita vipo vingi, lakini kama wakristo tumeagizwa kupigana vita vya aina moja tu!, NAVYO NI VILE VYA IMANI!. Na vita hivyo hatupambani na wanadamu wenzetu, bali na roho za mapepo na falme zao katika ulimwengu wa roho…

Waefeso 6:11  “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”.

Kwa maelezo marefu kidogo kuhusiana na vita hivi vya Imani na jinsi ya kupambana fungua hapa >>> TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.

 2) SHIKA UZIMA WA MILELE.

Yohana 17:2 “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.

3 Na uzima wa milele ndio huu, WAKUJUE WEWE, MUNGU WA PEKEE WA KWELI, NA YESU KRISTO ULIYEMTUMA”.

Uzima wa milele maana yake ni “kumjua sana Mungu na Yesu Kristo aliyemtuma”… Hivyo tunavyodumu katika kutafuta kumjua Mungu na siri iliyopo ndani ya mwanae Yesu Kristo ndivyo uzima wa milele unavyozidi kudumu ndani yetu. Lakini tutakapopunguza kumtafuta Mungu, ndivyo ule uzima wa milele unavyozidi kufifia ndani yetu.

Je unayashika Maungamo yako?.

Bwana atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

VITA DHIDI YA MAADUI

USIMPE NGUVU SHETANI.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Kuungama ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments