Category Archive Uncategorized @sw-tz

Tarishi au Matarishi ni akina nani  kwenye biblia?

Tarishi ni mtu aliyeajiriwa kwa kazi ya kusafirisha na kuwasilisha barua au nyaraka mahali pengine. Katika biblia watu ambao walikuwa wanatumwa kusambaza barua za wafalme kwa watu wa mji, au viongozi  waliitwa Matarishi.

Kwa mfano katika habari hii, utaona enzi zile za wafalme kulikuwa na  Mfalme aliyeitwa Hezekia ambaye alikusudia kurejesha tena sikukuu zilikuwa zimesahauliwa katika Israeli kwa miaka mingi, Hivyo ili adhma yake iweze kufanikiwa  ilimbidi awaandae hawa wajumbe (matarishi) ili wamsaidie kulipeleka hili agizo lake kwa watu wote waliokuwa Israeli wapande Yerusalemu kwenda kumfanyia Mungu sikukuu ya pasaka..

2Nyakati 30:5 “Basi wakafanya amri kupiga mbiu kati ya Israeli yote, toka Beer-sheba mpaka Dani, ya kwamba watu waje wamfanyie pasaka Bwana, Mungu wa Israeli, huko Yerusalemu; maana tangu siku nyingi hawakuifanya kama vile ilivyoandikwa.

6 Wakaenda MATARISHI wenye nyaraka za mfalme na wakuu wake, kati ya Israeli yote na Yuda, na kwa amri ya mfalme, kusema, Enyi wana wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, apate kuwarudia waliosalia wenu waliookoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru”.

Utaona tena, kipindi kile, cha Mfalme Ahasuero, Amri ilipotolewa na Mfalme kuwa wayahudi wote wanapaswa wauliwe ndani ya siku moja, utaona agizo hilo lilisambazwa katika miji yote kwa mikono ya  hawa matarishi.

Esta 3:13 “BARUA ZIKAPELEKWA KWA MIKONO YA MATARISHI mpaka majimbo yote ya mfalme kuwaangamiza Wayahudi wote, na kuwaua, na kuwafisha, vijana kwa wazee, watoto wachanga na wanawake pia, siku moja, yaani, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili ndio mwezi wa Adari; na kuyachukua mali yao kuwa nyara”.

Neno hilo utalisoma pia katika vifungu hivi..

Esta 8:10 “Akaandika kwa jina la mfalme Ahasuero, na kutia muhuri kwa pete ya mfalme, akazipeleka barua kwa MATARISHI, wamepanda farasi, wamepanda wanyama wepesi sana waliotumika kwa huduma ya mfalme, ndio waliozalishwa katika zizi la mfalme”.

Ayubu 9:25 “Basi siku zangu zina mbio kuliko TARISHI; Zakimbia, wala hazioni mema”.

Yeremia 51:31 “TARISHI mmoja atapiga mbio kumlaki mwingine, Na mjumbe mmoja atapiga mbio kumlaki mwenziwe, Ili kumpasha habari mfalme wa Babeli, Ya kuwa mji wake umetwaliwa kila upande”.

Soma pia 2Nyakati 30:10, Esta 8:14

Lakini swali la kujiuliza na sisi je  ni matarishi wa habari gani? Je Ni habari za Kristo, au habari za watu mitaani?. Sote tunawajibu wa kuwa matarishi wa Kristo, tuwe wepesi kwenda kuwahubiria wengine habari njema za msalaba, ili waokolewe, kuliko habari nyingine zozote. Bwana anatazamia, vinywa vyetu, mikono yetu, maisha yetu,  vyote vitumike katika kuutangaza ufalme.

Je, mimi na wewe tunafanya hivyo?. Majibu tunayo mioyoni mwetu,

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Mharabu ni nani katika biblia?

Matuoni ni nini katika biblia?

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

Rudi nyumbani

Print this post

Neno Buruji lina maana gani katika biblia?

Buruji ni aina ya mnara ambao ulijengwa  zamani mahususi kwa ajili ya kuvamia kambi za maadui zilizojengwa kwa kuta ndefu.

Kwa namna ya kawaida ilikuwa ni ngumu kuvamia ngome za namna hiyo..kwani askari walikaa juu ya kuta hizo ndefu wenye mishale ya moto na mawe mazito..kwahiyo kama nyinyi mtakwenda kushindana nao kwa njia za kawaida kwa pale chini. Kitakachokuwa kinaendelea ni kifo tu.

Hivyo iliwabidi wabuni njia nyingine za kuwashambulia maadui waliojizungushia boma juu ya kuta..ndipo hapo sasa yakagunduliwa  haya maburuji..ambayo kwa chini yalikuwa na matairi manne..na urefu wake ulilingana na zile kuta za maadui zao au zaidi kidogo..hivyo askari walikuwa wanapanda mpaka juu kabisa mwa maburuji hayo…mahali ambapo watakuwa usawa mmoja na wale maadui zao..kisha wanaanza kuwashambulia..huku wanazidi kuusogelea ukuta wa mji kidogo kidogo.

Na wakishafanikiwa kufika kwenye ukuta wanashusha ngazi zao..kisha wanashuka kutokea huko huko juu na kuingia katika mji na kuanza kuwashambulia. 

Tazama picha juu uone jinsi zilivyotengenezwa

Kwa kuwa buruji hizo zilikuwa zinajengwa kwa mbao..sasa ili kuzuia moto kutupwa kuziteketeza..walizizungushia chuma au ngozi za wanyama kiasi kwamba mishale ya moto hata ikitupwa haikuweza kuleta madhara.

Isaya 23:13

  • [13]Tazama, nchi ya Wakaldayo; watu hao hawako tena; Mwashuri ameiweka tayari kwa hayawani wa jangwani; WAMESIMAMISHA BURUJI ZAO ZA VITA, wameyaharibu majumba yake ya enzi, akaufanya kuwa uharibifu.

Pia kibiblia minara yote ya maficho iliyokuwa ndani ya ngome iliitwa kwa jina hili

Vifungu hivi vinaelezea neno hilo.

Waamuzi 9:46

[46]Kisha watu wote waliokaa katika ile buruji ya Shekemu waliposikia habari hiyo wakaingia ndani ya ngome ya nyumba ya El-berithi.

2 Mambo ya Nyakati 26:15

[15]Akafanya katika Yerusalemu mitambo ya vita, iliyobuniwa na watu wastadi, iwekwe juu ya 

na juu ya buruji, ili kutupa mishale na mawe makubwa. Jina lake likaenea mbali sana; kwa kuwa alisaidiwa mno ajabu, hata akapata nguvu.

Soma pia Waamuzi 9:47,49 Yeremia 31:38, Sefania3:6 Wimbo 8:9 Nehemia 3:8

Halikadhalika pia kiroho zipo kuta nzito adui yetu ibilisi ameziweka mbele yetu.. lakini Tukimtumainia Bwana yeye mwenyewe ndio atakuwa buruji letu. Hatuhitaji nguvu za mwilini kupambana naye..bali zile za Rohoni..Wana wa Israeli walimwamini Mungu na wakafuata maagizo yake kwa ukamilifu..na walipokutana na zile kuta za Yeriko, sote tunafahamu ni nini kilitokea..ni kwamba zilizama chini zote..pakawa tambarare kama vile hakujawahi kuwa na kuta au ngome..

Halikadhalika na sisi tunahitaji kumwamini Mungu na kuishi sawasawa na njia zake. Na hayo mengine ya vita vya ibilisi yeye atayashughulikia mwenyewe kirahisi kabisa.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka?Je umepata uhakika kama ukifa leo utakwenda wapi?..una habari kuwa hili ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia? Na kwamba zile dalili zote za kuja kwa Yesu zimeshatimia tunachongojea sasa ni Unyakuo tu?

Unangojea nini? Tubu mrudie muumba wako katika hizi dakika za lala salama.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Rudi nyumbani

Print this post

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

Ukiona unahubiriwa juu ya hukumu ya Mungu, au juu ya habari ya siku za mwisho halafu unachukia au unakwazika, lakini wakati huo huo ukiambiwa habari za mafanikio na mema ndio unafurahia, basi fahamu kuwa upo karibu sana kupotea.

Kwasababu kitengo hicho ndicho kitengo-mama cha shetani kuwadanganyia watu, Embu fikiria pale Edeni Mungu hakuwaficha chochote bali aliwaeleza Adamu na hawa madhara ya dhambi, akawaambia mkila matunda la ujuzi wa mema na mabaya hakika MTAKUFA..

Lakini shetani akaibuka na mahubiri yake laini, kinyume na yale Mungu aliyowaangiza, na kuwaambia hakika HAMTAKUFA,…Unaona? Hawa aliposikia habari za mema zimekuja, habari za mafanikio, habari za uzima wakati wote, habari za kuwa juu tu, haijalishi kuwa utamkasirisha Mungu kiasi gani, haijalishi kuwa utazini kiasi gani, atatoa mimba nyingi namna gani,  maadamu ni ya kutakiwa mema, basi akayachukua tu na kuyadharau yale ya Mungu, akayashilia yale ya shetani akayaamini kwelikweli kuwa hatakufa, bali ataishi naye atayasimulia matendo ya Bwana.

Ndugu yangu hizi ni siku za mwisho, ambazo biblia ilizitabiri kuwa kutatokea wimbi kubwa la manabii wa uongo, ambao kimsingi kazi yao kubwa itakuwa ni hiyo..kuwahubiria watu maneno laini, haijalishi watakuwa hawajaokoka, au la, hilo haliwahusu, kazi yao ni kuwatabiria mafanikio tu na uzima, na mema, lakini madhara ya dhambi hawataambiwa.. Kama alivyofanya shetani kwa Hawa pale Edeni.

Isaya 30:9 “Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya Bwana;

10 wawaambiao waonaji, Msione; na manabii, Msitoe unabii wa mambo ya haki, TUAMBIENI MANENO LAINI, HUBIRINI MANENO YADANGANYAYO;

Kwa  hawa manabii, na waalimu wa uongo kamwe hutasikia Neno ‘ukizini hakika utakufa’, na kwenda jehanamu, huwezi kusikia maneno kama hayo, kwasababu shetani anataka wewe uendelee kubakia hivyo hivyo katika ujinga, ili ufe ghafla ujikute kuzimu uanze kujuta kwanini sikufahamu haya yote.

Angalia shida tunazozipitia duniani leo hii, ni kwasababu ya wazazi wetu kusikiliza injili laini za shetani,  Inasikitisha kuona pale mtu unapoambiwa kuhusu dhambi zako, unaona kama vile unahukumiwa. Mama yetu  Hawa aliona kama Mungu anamtamkia mabaya, akafanya makosa yale..Na sisi vivyo hivyo tukipuuzia injili ya kuambiwa ukweli, injili za kukemewa dhambi, injili za ziwa la moto. Tujue kuwa tunajiandaa kwa majuto ya milele.

Mara nyingi wana wa Israeli waliingia katika makosa kama haya mpaka wakapelekwa utumwani Babeli kwasababu ya kuwasikiliza manabii wa uongo waliokuwa wanawatabiria amani tu muda wote, bila kushughulika na dhambi zao, ambazo ndio kiini cha matatizo yao.

Soma vifungu hivi;

Ezekieli 13:16 “yaani, manabii wa Israeli, watabirio habari za Yerusalemu, na kuona maono ya amani katika habari zake; wala hapana amani, asema Bwana MUNGU”.

Yeremia 6:14 “Wameiponya jeraha ya watu wangu kwa juu juu tu, wakisema, Amani, Amani, wala hapana amani”.

Unaona yaliyokuwa yanaendelea kale ndiyo yanayoendelea sasa.

Leo swali linakuja kwako, Je unaufungaje mwaka wako?, mwaka huu wa 2020 ndio unapita, unakuja mwingine mpya wa 2021, kumbuka kwa jinsi miaka inavyosogea ndivyo tunavyoyakaribia mambo mawili makuu mbele yetu, la kwanza Ni Unyakuo. Na la pili ni Kifo chako. Maelfu ya watu kila sekunde wanakufa duniani, vilevile na wewe hujui siku yako itakuwa ni lini, pengine ni kesho, au mwanzoni mwa mwaka ujao, Jiulize ukifa leo ghafla huko utakapokwenda utakuwa ni upande gani?

Vilevile jiulize ikiwa unyakuo utapita leo usiku halafu ukaachwa, utakuwa kwenye hali ya namna gani..Kumbuka ni siku kama hizi  ndizo Bwana atakazorudi, watu watakuwa wakila na kunywa, wakipanda na kujenga, wakisherehekea, ndipo huo mwisho utakapokuja..Jiulize utakuwa wapi wakati huo ukikujia kwa ghafla.

Ukijifunza kuyatafakari hayo, hutaishi maisha ya ilimradi tu hapa duniani, bali utajiangalia sana mwenendo wako, ili siku ile isije ikakunasa kama mtego.

Hivyo, tubu dhambi zako mgeukie Muumba wako, usikubali uanze mwaka mpya na viporo vya dhambi vya mwaka huu, mgeukie Yesu Kristo leo hii, akusafishe dhambi zako.

Ikiwa upo tayari kutubu sasa, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako. Mahali popote ulipo, tafuta sehemu ya utulivu, piga magoti, kisha kwa kumaanisha kabisa kutoka katika moyo wako sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE, NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Basi kwa sala hiyo fupi, Mungu ameshakusamehe, kilichobakia kwako ni kubatizwa, ikiwa hukubatizwa, na kudumu katika neema na utakatifu siku zote za maisha yako.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya kiroho, basi tutafute kwa namba hizi +255693036618

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

KUMTUMIKIA MUNGU, KUNAWEZA KUWE KINYUME NA MATARIJIO YAKO.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Rudi nyumbani

Print this post

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

Shalom, karibu tujifunze Neno la Mungu, ambalo ndio cha kweli cha roho zetu.

Kawaida ya Mungu ni huwa hatoi agizo juu ya agizo. Yaani kwa mfano leo akikupa agizo fulani ulitelekeze, haundi agizo lingine juu yake kulibatilisha hilo la kwanza, Atafanya hivyo endapo tu lile la kwanza litakuwa limeisha muda wake.

Mara nyingi tunakuwa tukiacha yale maagizo ya kwanza ya Mungu, na hiyo inatupelekea aidha kukutana na hukumu yake, au kushindwa kutekeleza mipango yetu  kwa wakati.

Kwamfano utakutana na nabii mmoja katika biblia enzi za wafalme, ambaye alipewa maagizo na Mungu ya kwenda kumtolea unabii Mfalme mwasi Yeroboamu, akaambiwa akishamaliza kazi yake asile wala asinywe chochote katika mji huo, wala asilale au kupumzika na njia atakayoipita asiirudie tena hiyo hiyo. Lakini huyu nabii alipomaliza kweli kazi ya huduma alianza safari ya kuondoka. Lakini akiwa njiani alikutana na nabii mwingine mzee, akamshurutisha, aende kulala nyumbani kwake. Lakini yeye akamwambia Bwana amenionya nisikae mahali popote kwenye mji huu.

Sasa yule nabii mzee alipoona kuwa kijana huyu hataki, akamtungia habari za uongo na kumwambia, Bwana ameniambia ameghahiri, mpango wake, hivyo anataka uje ule upumzike nyumbani kwangu. Na yule kijana pasipo kufikiria ni kwanini Mungu awe kigeugeu, saa hiyo hiyo akamwamini, kwasababu  tu ni nabii mwenzake tena mzee, anauzoefu wa mambo ya kinabii, akaenda kukaa kwake.  Kitu kilichomtokea hatuna haja ya kueleza, sote tunajua alikuja kuliwa na simba, kwa kuyaasi maagizo ya Mungu (Soma 1Wafalme 13)

Tunamwona Mtu mwingine anaitwa, Balaamu, naye pia mwanzoni Mungu alimuonya asiende kuwalaani Israeli, lakini baadaye akawa analazimisha mawazo yake kwa Mungu, kilichofuata ilikuwa ni Mungu kumwambia haya nenda nitakuwa pamoja nawe..kumbe hakujua tayari njia Mungu alikuwa ameshamuandalia malaika wake amuue, na kama sio yule punda kumsaidia habari yake tusingeisoma leo hii kwenye biblia (Soma Hesabu 22).

Hiyo yote ni kutozingatia agizo la kwanza Mungu alilokupa, Siku zote agizo linalokuja juu ya agizo lile la mwanzo huwa halitokani na Mungu.

Tukisoma tena habari nyingine maarufu katika biblia ile ya Wana wa Israeli walipokuwa wanatoka  Babeli utumwani, baada ya kukaa kule miaka 70. Biblia inatuambia Mungu alimuamsha moyo mfalme Koreshi wa uajemi, ili atoe amri kuwa watu wote waondoke kwenye makoloni yake, waende Yerusalemu kumjengea Mungu nyumba, kufuatana na unabii uliotolewa na Yeremia zamani.

Tunaona baada ya hapo Mfalme aliwapa zawadi nyingi sana, Hivyo waliondoka kwa moyo mkunjufu  wakijua kabisa Mungu kaitimiza ahadi yake ya kwenda kumjengea nyumba Yerusalemu. Lakini walipofika kule na kuanza kutia msingi wa nyumba ya Mungu, maadui zao wakaanza kunyanyuka hilo likawadhoofisha, na kama hiyo haitoshi wakaandika waraka wa uchongezi wakampelekea mfalme mwingine wa uajemi ambaye alikuja kutawala baada ya Koreshi, aliyeitwa Dario,  mfalme alipousoma, akatoa amri nyingine, kuwa usiendelee ujenzi wowote Yerusalemu, wa nyumba ya Bwana. Na mtu yeyote atakayefanya vile ilikuwa ni kifo.

Wayahudi waliposikia, juu waraka huo mpya, wote wakavunjika moyo, wakaacha kuijenga nyumba ya Mungu ambayo ilikuwa tayari katika hatua nzuri, Hivyo ikapelekea nyumba hiyo kubakia hivyo hivyo kwa muda wa miaka mingi sana..Kila mtu akarudi kuendelea na shughuli zake kila siku.

Wakasau kuwa ni Mungu ndiye aliyewapa maagizo kuwa wakamjengee nyumba yeye, hawakujiuliza sasa haya maagizo mengine yanatoka wapi?

Mpaka baadaye sana, tunaona manabii wawili yaani Hagai na Zekaria wanatokea, wanawatabiria na kuwauliza kwanini mnaacha kujenga nyumba ya Mungu, wakidai kuwa huu sio wakati wa kumjengea Mungu? Kwa muda wako soma kitabu chote cha Hagai utaona mambo hayo.

Unaona, walisikiliza sauti ya pili, wakaicha ile ya kwanza, na hiyo ikawapelekea kucheleweshwa kwa huduma yao waliyokuwa wameshaianza,.. Siku zote sauti ya pili ni ya shetani, na sio ya Mungu.

Vilevile katika agano jipya kuna agizo ambalo tayari Mungu alishatupa.

Marko 16:15-16 Inasema..

“Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Hili ni agizo ambalo Kristo alishatoa kibali, kufanya.. Lakini dunia ya sasa shetani ameshaiingilia, kiasi kwamba, sehemu nyingine watu hawaruhusiwi kuhubiri kabisa, sheria za nchi zao zimekataza..Sasa wewe kama mkristo ukiogopa sheria ya wanadamu, ukasema pengine huu sio wakati wa kufanya hivyo, ujue kuwa utafanana na wana wa Israeli walipokuwa wanalijenga hekalu la pili, utasubiria wee, na kamwe hiyo siku ambayo unayoina itafaa haitafika, Mungu atakachofanya ni kukumbusha tu, uliacha agizo la kwanza.

Sio hilo tu yapo maagizo mengine madogo madogo, yanakubana kiasi kwamba yanakufanya ushindwe hata kuiendeleza kazi ya Mungu, mpaka uwe na hiki au kile, au ukamilishe hiki au kile..Hayo yote hatupaswi kuyazingatia sana, mengine yana agenda ya shetani nyuma yake kukumwisha tu, bali tuzingatie lile agizo kuu la mwanzo ambalo Kristo ametupa enendeni ulimwenguni kote.

Mwingine atasema familia yangu iko hvi au vile..hupaswi kuangalia hayo yote

Safari ya imani, si mteremko muda wote, kuna wakati itasumbuliwa na mambo mengi, lakini hatupaswi kuyaogopa kwasababu Mungu ameshaahidi atakuwa na sisi katika hayo yote. Kama tu vile alivyokuwa kwa mababa zetu katika mapito yao.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

BWANA AYAGANGE NA MACHO YETU PIA.

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Rudi nyumbani

Print this post

MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.

Shalom, karibu tujifunze maneno ya uzima.. Lipo swali ambalo linaulizwa na watu wengi, kwamba kama Mungu anajua kuna jambo litakwenda kutokea mbeleni ambalo litanisababishia mauti, kwanini basi asinizuie kwenda kulifanya badala yake ananiacha mpaka naingia, na mwisho wa siku napotea na kwenda kuzimu? Mbona kama vile atakuwa sio Mungu wa upendo?

Kama na wewe swali hili lipo ndani yako basi tuzidi kutafakari pamoja somo letu la leo,

Kitabu cha Mithali kinasema..

“Kwa kuwa mtego hutegwa BURE, Mbele ya macho ya ndege ye yote”.( Mithali 1:17).

Embu jiulize, mtu anayetega mtego wa kumshika ndege kwa ajili ya kitoweo chake, Je! Unadhani Mungu hampendi ndege yule? Au unadhani Mungu hajampa uwezo wa kuwakimbia maadui zake kiwepesi?

Au mtu anayetega mtego wa kunasa panya, unadhani Mungu anawachukia panya, na hivyo kawaondolea uwezo wa kuwakimbia adui zao?

Au mtu anayetega ndoano kuvua samaki, unadhani Mungu hawapendi samaki wake,?

Sikuzote mpaka umeona kitu fulani kinaundiwa mitego, basi ujue kuwa kitu hicho kilishashindikana  kukamatika kwa njia rahisi, au ya kawaida, hivyo kimetafutiwa njia mbadala, kwamfano leo hii unaweza kumuona ndege katua hapo pembeni yako, hatua kadhaa tu pembeni, lakini embu kajaribu kwenda kumkamata kwa mikono yako kama utaweza,? Au umwone panya anakatiza kwenye kona ya nyumba, au store, halafu fanya mazoezi ya kwenda kumkata kwa mikono kama vile unavyokamata chura uone kama itakuwa ni kazi rahisi kwako.

Au umwone samaki anaelea juu ya maji, hivyo unatakwenda kwenda kumchota haraka kwa mikono yako, jaribu zoezi hilo kama litakuwa rahisi. Huwezi kuwapata kwasababu Mungu tayari kashawekea uwezo ndani yao wa kujiangua kutoka kwa maadui zao kivyepesi sana.. na wenyewe wanajua kabisa maadui zetu ni ngumu kutushika kwasababu hawana wepesi tulionao sisi, au hawana uhodari tulionao sisi wenyewe.. Na  sisi tunaowawinda tunajua kuwa ili waendelee kuwa salama ni wajibu wao, kutotuamini sisi kwa kitu chochote siku zote za maisha yao hapa duniani, haijalishi tutawavutia kwa vitu vingi kiasi gani wanavyovipenda.

Vivyo hivyo na sisi wanadamu, Mungu ameshatupa uwezo mkubwa sana ndani yetu wa kumshinda adui yetu shetani, na yeye analijua hilo, hawezi kuja na kukukamata hivi hivi kama anavyotaka, hana uwezo huo, anajua kabisa hawezi kukupata, lakini anachokifanya ni kijiundia mitego yake mbalimbali, ambayo hiyo  ikishakunasa, basi  hapo ndipo anakuwa na uwezo wa kukufanya chochote anachotaka ikiwemo hata kukuua.

Kwamfano mtego mmojawapo maarufu , ni uasherati, shetani anaweza kukuletea kahaba, ili mkazini, lengo lake sio ukutane na kahaba au uzini tu halafu basi, hapana, bali  ni ukosane na Mungu wako kwa kitendo hicho, ili apate nafasi ya kuyaachilia mapepo yake yaingie katika maisha yako kukuharibu kirahisi katika kila nyanja, ikiwemo upate na magonjwa ya zinaa kama vile ukimwi ili ufe kabla ya wakati wako.

Lakini hayo anajua hayawezi kuja hivi hivi, ni mpaka akuwekee mtego, ndipo hapo   anakuletea kahaba mzuri, au mwanaume mwenye pesa, anakulaghai na wewe bila kufikiri kuwa ule ni mtego umewekwa mbele yako unakwenda kuuva, ukidhani kuwa Mungu atakuepusha nao.. Hilo Mungu hawezi kulifanya ndugu yangu.

Kwa nafasi yako soma kitabu cha Mithali sura ya 7 yote, uone jinsi, kijana mpumbavu aliyetegwa na mwanamke mzinzi, na hatma yake inavyokuwa; hatuwezi kusoma vyote lakini vile vifungu vya mwisho mwisho vinasema..

Mithali 7:21 “Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.

22 Huyo akafuatana naye mara hiyo, KAMA VILE NG’OMBE AENDAVYO MACHINJONI; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;

23 Hata mshale umchome maini; KAMA NDEGE AENDAYE HARAKA MTEGONI; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.

24 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.

25 Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake.

26 Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, JUMLA YA WALIOUAWA NAYE NI JESHI KUBWA.

27 Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.

Ndege anayenaswa kwenye mtego ni kajitakia mwenyewe na sio kwamba alikuwa ni dhaifu, tamaa zake ndizo zilizompeleka pale,. Leo hii, unapojikuta kwenye matatizo mazito, ambayo unajua kabisa ni kwasababu ya dhambi Fulani uliyoifanya ndio yakakukuta, usianze kumlaumu Mungu ni kwanini hakukuepusha nayo hapo kabla. Mungu alishakupa uwezo huo tangu zamani,  Na Mungu naye hawezi kumlaumu shetani, kwasababu shetani naye analo la kujitetea, anasema mimi sikumuita mtu aje kwenye mtego wangu, wala sikumlazimisha mtu, kufuata kile nilichokiweka kwenye mtego, ni yeye mwenyewe alinifuata, ni ndio hapo akanasikia akaangamia, ilikuwa ni wajibu wake kuchukua tahadhari anapoishi duniani.

Na ndio maana biblia inasema..

Hosea 4: 6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa;..”

 Tukikosa maarifa ya kuzijua njama za shetani, au kuyajua mafumbo ya shetani, tutajikuta tunaingia katika matatizo ambayo tutajiuliza ilikuwaje kuwaje tumejikuta hapa,

Ufunuo 2:24 “Lakini nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, wo wote wasio na mafundisho hayo, WASIOZIJUA FUMBO ZA SHETANI, kama vile wasemavyo, Sitaweka juu yenu mzigo mwingine.

25 Ila mlicho nacho kishikeni sana, hata nitakapokuja”.

Hivyo kila mmoja anao wajibu wa kupata maarifa sahihi ya kuitambua mitego ya adui. Na maarifa hayo utayapata kutoka katika Neno la Mungu tu basi, biblia imejaa siri za kuepukana na hila za adui. Na ndio maana shetani hapendi watu waisome.

Kuwa msomaji wa biblia kila siku, tafakari , usiisome kama gazeti, hiyo tu ndio itakayokuwa nuru yako katika zama hizi za kumalizia, kumbuka mitego ni mingi, vishawishi ni vingi, na ipo ya aina tofauti toauti, uwezo umepewa, pengine umepungukiwa tu na maarifa. Hivyo ni wajibu wako kuyatafuta maarifa hayo, ambayo utayapata katika Neno la Mungu. Yaani BIBLIA.

Hakuna jaribu lolote linalotendeka leo hii, ambalo halijawahi kuandikwa katika biblia na njia ya kuepukana nalo., Hivyo jijengee desturi ya kusoma Neno la Mungu. Ili usiwe wa kumlaumu Mungu, kwanini hiki, kwanini kile, wakati ni wewe mwenyewe uliyakataa maarifa, hivyo ukanasika kirahisi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.

Rudi nyumbani

Print this post

Mlima wa Mizeituni  unaumuhimu gani kwetu?

Mlima wa Mizeituni ni moja ya milima saba ambayo inauzunguka mji wa Yerusalemu kule Israeli . Mlima huu upo upande  wa Mshariki mwa mji huo,  umbali usiozidi kilometa moja, mpaka kuuingia mjini Yerusalemu. Hivyo haupo mbali sana.

Umeitwa mlima wa Mizeituni, kutokana na kuwa na sifa ya kuzungukwa na miti mingi ya mizeituni pembezoni mwa mlima huo.

Mlima huu umetajwa mara mbili katika agano la kale, mara ya kwanza ni siku ile Daudi alipokuwa anafukuzwa na mwanawe Absalomu, biblia inatuambia aliupanda mlima huu akiwa analia peku, akiambatana na wale watu aliokuwa nao kwenye ufalme.(2Samweli 15:30).

Sehemu nyingine ni katika kitabu cha Zekaria ambacho kinaeleza unabii wa masihi siku atakaposhuka mara ya pili hapa duniani, kwamba atashukia kwanza juu ya mlima huu;

Zekaria 14:3 “Hapo ndipo atakapotokea Bwana, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita.

4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini”.

Lakini katika agano jipya mlima huu umetajwa mara nyingi kidogo;

Lakini cha kufahamu zaidi ni kuwa habari zote ambazo  Yesu Kristo alizitaja kuhusiana na siku za mwisho na kurudi kwake mara ya pili duniani, alizizungumzia juu ya mlima huu wa mizeituni. Utasoma hayo katika (Mathayo 24, Marko 13, Luka 21)

Hata  siku ile Yesu alipoulilia mji wa Yerusalemu, juu ya maangamizi yake yaliyo mbeleni, alikuwa amesimama juu ya mlima huu.(Luka 19:37-44)

Na juu ya mlima huu, ndio aliopaa kutoka ulimwenguni, mara ya mwisho  alipokutana na wanafunzi wake baada ya siku zile 40 na kuwapa maagizo ya kuhubiri injili, na kuingojea ahadi ya Roho Mtakatifu..

Matendo 1:9 “Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.

10 Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,

11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni”.

JE! MLIMA HUU UNAO UMUHIMU WOWOTE KWETU? NA JE! NI SAHIHI KWENDA KUOMBA JUU YA MLIMA HUU?.

mizeituni, mlima,

Ni wajibu wetu kujua kuwa huu ndio mlima ambao Kristo atashukia siku ile atakaporudi mara ya pili kuuhukumu ulimwengu na kutawala kama mfalme. Na kama tulivyosoma katika unabii wa Zekaria ni kwamba siku hiyo atakapokuja, mlima huu utagawanyika katikati, upande wa Mashariki, na Upande wa Magharibi, na hapo katikati kutakuwa na bonde kubwa sana. Siku hiyo  atauwa waovu wote watakaokuwepo duniani kwa wakati huo.. Kipindi hichi ndio kile biblia inasema  kila jicho litamwona, na mataifa yote watamwombolezea, watu watatamani milima iwaungukie kwasababu watauliwa na Kristo mwenyewe. (Mambo hayo watakutana nao wale watakaoukosa unyakuo)

Kwa urefu wa somo hilo fungua hapa >>WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA;

Na baadaye akishawamaliza waovu wote ataingia  mji wa Yerusalemu, na kisha atatawala kama Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana, juu ya dunia nzima kwa muda wa miaka 1000,

Ataitengeneza upya hii dunia, kutakuwa na amani ya milele isiyoelezeka. Dunia itakuwa kama paradiso. Na wakati huo upo karibuni sana. Hivyo ni wajibu wetu sisi sote kujua mambo yatakayoendelea Israeli katika siku za mwisho, ikiwemo juu ya mlima huu wa mizeituni, ili tujue  leo hii tunasimama wapi. Tusiishi tu kama watu wengine wa ulimwengu, wasioona mambo ya mbeleni.

Lakini sasa tukirudi kwenye sehemu ya pili ya swali letu  je! Ni Sahihi kwenda kuomba juu ya mlima huu?

Watu wengi wamekuwa wakienda Yerusalemu, kupeleka maombi yao, wakidhania kuwa mahali pale ndipo Mungu atawasikia vizuri zaidi kuliko huku walipo, wengine wamekuwa wakikesha kwenye ule ukuta wa maombolezo, wengine juu ya mlima huu wa Mizetuni, wengine kwenye mto Yordani n.k..

Lakini ukweli ni kwamba kufanya hivyo ni kukosa maarifa ya kutosha juu ya agano tulilo nalo leo hii. Bwana Yesu alimwambia Yule mwanamke;..

Yohana 4:21 “Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu….

4.23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

Agano la Damu ya Yesu, ni agano la kimbinguni, kiasi kwamba mtu yeyote mahali popote atasikiwa na Mungu ikiwa tu ataingizwa katika agano hilo lililo bora. Na Mtu ataingia ndani ya agano hilo, kwanza kwa kumwamini Yesu Kristo, kisha kutubu dhambi zake, na baada ya hapo kuwa tayari kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. Akikamilisha hatua hizo anakuwa ameshaokoka.

Na mtu kama huyo maombi yake yanasikiwa, ziadi hata mtu aliyekwenda kuomba juu ya mlima huu.

Je! Wewe umeingizwa kwenye agano hili?. Je! Una habari kuwa Yesu Kristo yupo mlangoni kurudi? Na unabii huo upo mlangoni kutimia? Unasubiri nini usimkaribishe Kristo moyoni mwako. Bado unatangatanga na ulimwengu ili siku ile ikujie ghafla?.  Mambo yatakayoendelea huku duniani kwa watakaoukosa unyakuo hayaelezeki ndugu yangu, Ni heri leo ukayakabidhi maisha yako kwa Yesu. Kama moyo wako leo hii upo tayari kufanya hivyo. Basi uamuzi huo ni wa busara sana. Hivyo fungua hapa kwa ajili ya kupata maelekezo ya sala ya Toba.  >>> SALA YA TOBA

Na Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UFUNUO: Mlango wa 20

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

Biblia inaziorodhesha bahari kuu nne, tuzisome;

1 ) Bahari ya shamu: Kwa sasa inajulikana kama bahari nyekundu, (Kwa kiingereza red sea). Hii ni ile bahari ambayo wana wa Israeli waliivuka baada ya Mungu kuipasua pale walipokuwa wanafuatiliwa na maadui zao, ambapo tunaona baadaye walikuja kumezwa na bahari ile.

bahari ya shamu

Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji”.

2) Bahari kubwa , au bahari ya Wafilisti, (Kutoka 23:31): Kwasasa inajulikana kama habari ya Mediteranea. Ipo upande wa Magharibi wa taifa la Israeli. Hii ndio bahari kubwa kuliko zote zinazoorodheshwa kwenye biblia.

bahari kubwa, ya wafilisti, au mediterenia

Hesabu 34:6 “Kisha mpaka wenu wa upande wa magharibi mtakuwa na bahari kubwa na mpaka wake; hii ndiyo mpaka wenu upande wa magharibi”.

Soma pia Yoshua 9:1, 15:47, 23:4, Ezekieli 47:19

3) Bahari ya Galilaya; Au kwa jina lingine Bahari ya Tiberia, au ziwa la Genesareti au Bahari ya Kinerethi Yoshua 12:3, 13:27, 34:11. Hii ndio ile bahari ambayo Bwana Yesu alitembea juu ya maji.

bahari ya galilaya

Luka 5:1 “Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,”

Mathayo 4:18 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi”.

4) Bahari ya chumvi: Hii ni habari ndogo sana, ambapo ipo chini ya mto Yordani, maji yake ni ya chumvi nyingi sana, jambo ambalo linaifanya bahari hiyo isiwe na kiumbe wa kuishi ndani yake kama samaki, sehemu nyingine wanaiita ‘bahari mfu’(Dead Sea)

bahari ya chumvi

 Hesabu 34:3 “ndipo upande wenu wa kusini utakuwa tangu bara ya Sini kupita kando ya Edomu, na mpaka wenu wa kusini utakuwa tangu mwisho wa Bahari ya Chumvi kuelekea mashariki”;

 Kumbukumbu 3:17, Yoshua 15:2.

Shalom, tazama maeneo mengine mbalimbali ya biblia chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?

Sharoni ni nini au ni wapi kibiblia?(1Nyakati 5:16)

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kikoto ni nini?(Yohana 2:15)

Kikoto ni nini?


Kikoto ni aina ya kiboko mfano wa mjeledi. Tazama picha juu.

Tunaweza kuona wakati ule Yesu alipokwenda Hekaluni na kukuta watu wameigeuza nyumba yake kuwa pango la wanyang’anyi, tendo alilolifanya ni kuunda aina hii ya mjeledi, kwa kuusokota kwa kamba mbeleni. Ili awaadhibu vizuri wale watu waliokuwa wanasitiri maovu yao kule, waliokuwa wanafanya biashara zao mule ndani , pamoja na mifugo yao.

Yohana 2:13 “Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu akakwea mpaka Yerusalemu.

14 Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng’ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi.

15 Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao;

16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara”.

Ili kujua Bwana Yesu alimaanisha nini kusema msiigeuze nyumba ya Baba yangu kuwa pango la wanyang’anyi fungua hapa>> USIIGEUZE NYUMBA YA MUNGU KUWA PANGO LA WANYANG’ANYI.

Hiyo ni kutuonyesha kuwa wivu wa Mungu sikuzote unaleta adhabu.

Na adhabu hii ipo kwenye makundi mawili;

Kundi la kwanza: Ni kwa wale watu wanaolinajisi hekalu lake leo hii (yaani Kanisa), kwa kufanya mambo ambayo hayana misingi ya kiimani. Mfano kuigeuza kazi ya Mungu kama biashara, kuabudu masanamu, kwenda nusu uchi kanisani, n.k.

Na kundi la pili: Ni lile la watu wanaolinajisi hekalu lake (yaani Miili yao) kwa kufanya mambo ambayo hayampendezi. Kama vile uzinzi, uuaji, ulevi, n.k. Kwani biblia inasema;

1Wakorintho 6:18 “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.

19 Au hamjui ya kuwa MWILI WENU NI HEKALU LA ROHO MTAKATIFU aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.

Na inasema tena;

1Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi”.

Unaona? Na kikoto hichi tayari kipo mkononi mwa Bwana. Hivyo tujichunguze na sisi tumelitunzaje hekalu lake?  Kama tumekuwa tukiliharibu, ni heri tumgeukie kwa Bwana sasa, kabla ya wakati wa kuharibiwa haujafika. Kwasababu ukishafika na tukakutwa katika hali kama hizo, tujue kuwa hakuna neema tena.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya uvuvio?.

Nini maana ya kuabudu?

MOJA YA HIZI SIKU TUTAONA MABADILIKO MAKUBWA SANA.

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

MADHARA YA KUPUUZIA MAAGIZO YA MSINGI MUNGU ANAYOKUPA.

Mataifa ni nini katika Biblia?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Sinagogi la Mahuru ni lipi? na lilimaanisha nini(Matendo 6:9)

Neno hilo italisoma katika ile habari ya Stefano alipokuwa anatumiwa na Mungu kufanya ishara na maajabu yasiyokuwa ya kawaida katika kanisa lake.

Lakini baadhi ya wayahudi wa masinagogi mbali mbali walipoliona hilo wakamchukua kuja kujadiliana naye, na baada ya kuona kuwa wameshindwa waliingiwa wivu na kufanya mambo ambayo huwezi kudhani dhehebu la dini linaweza kufanya. Sasa moja ya sinagogi hilo lilikuwa ndio hilo lililoitwa Sinagogi la Mahuru; kulikuwa na mengine pia tusome.

Matendo 6:8 Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.

9 Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa sinagogi la Mahuru, na la Wakirene, na la Waiskanderia, na la wale wa Kilikia na Asia, wakaondoka na kujadiliana na Stefano;

10 lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye.

11 Hata wakashawishi watu waliosema, Tumemsikia mtu huyu akinena maneno ya kumtukana Musa na Mungu.

12 Wakawataharakisha watu na wazee na waandishi, wakamwendea, wakamkamata, wakampeleka mbele ya baraza.

13 Wakasimamisha mashahidi wa uongo waliosema, Mtu huyu haachi kusema maneno ya kufuru juu ya mahali hapa patakatifu na juu ya torati;

Sasa ni kwanini liitwe kwa jina hilo?

Biblia haijaeleza chochote kuhusu chimbuko la sinagogi hilo mpaka wakajiita hivyo, lakini inaaminiwa na baadhi ya wanazuoni kuwa kulikuwa na kundi la wayahudi ambao walikuwa ni watumwa wa dola ya Ki-Rumi, Na baadaye wakafanywa kuwa huru, na ndipo hapo wakawa na sinagogi lao, wakaliita Sinagogi la mahuru. Yaani sinagogi la watu waliofanywa kuwa huru.

Hivyo hata kama chimbuko la jina hilo lingekuwa ni tofauti na hiyo, lakini bado jina lake ni nzuri, “Mahuru”.  Lakini shida inakuja ni pale ambapo mioyo yao haiakisi jina hilo.  Ni wazi kuwa watu hawa hawakuwekwa huru moyoni, kwasababu kama wangewekwa huru wasingekuwa na wivu, na wasingemzushia Stefano habari za uongo. Hiyo ni kuonyesha kuwa walikuwa ni watu walio mbali na wokovu kuliko hata watu wasiomjua Mungu kabisa.

Tunajifunza nini?

Hatushangai hata sasa kuona yapo makanisa mengi, na mikusanyiko mingi, yenye majina mazuri ya rohoni,  yenye misalaba mingi, yenye kila aina ya mapambo mazuri ya rohoni. Lakini  ndani yake wanazipinga nguvu za Roho Mtakatifu kama walivyompinga Stefano.

Biblia ilishatabiri  katika kitabu cha 1Timotheo 3 kuwa katika nyakati za mwisho watatokea watu wengi wa namna hiyo

2Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

2 Maana watu watakuwa……….

5 wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao”.

Unaona watakuwa wenye mfano wa utauwa lakini wanazikana Mungu za Mungu.

Huu si wakati wa kujivunia dhehebu au dini ndugu, ni wakati wa kujivunia Kristo ndani yako. Unaweza ukawa na dhehebu zuri kweli, kubwa kweli, lakini Mungu amelikataa, wewe litakufaidia nini? Tunapaswa tuutafute utakatifu kwa bidii kwasababu hatuwezi kumwona Mungu tusipokuwa nao(Waebr 12:14).

Tunapaswa tujichunge tusifanane na hawa wa sinagogi la mahuru ambao wana jina zuri lakini ni wapinga-Kristo ndani yao.

Bwana atusaidie.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Nini Maana ya Hosana?

Mataifa ni nini katika Biblia?

UFUNUO: Mlango wa 18

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mount Gerizim and Mount Ebal: Their Meaning and Spiritual Significance

Introduction

In the heart of ancient Israel’s journey into the Promised Land lie two significant mountains: Mount Gerizim and Mount Ebal. Located in Samaria and facing each other directly, these two mountains were not just geographical landmarks but served as vivid illustrations of the covenant between God and His people. Through them, God presented the Israelites with a life-altering choice—blessing for obedience and curse for disobedience.

This symbolic moment reveals a deep theological truth: God’s covenant demands a response, and the results of that response echo through our lives, both physically and spiritually.


The Biblical Account

While still in the wilderness, Moses gave Israel a prophetic instruction from God. After crossing the Jordan River into Canaan, the Israelites were to hold a covenant-renewal ceremony at Mount Gerizim and Mount Ebal.

“And when the Lord your God brings you into the land that you are entering to take possession of it, you shall set the blessing on Mount Gerizim and the curse on Mount Ebal.”
Deuteronomy 11:29, 

They were to build an altar (on Ebal), write the entire Law on large stones, and divide the tribes into two groups. Half of the tribes would stand on Mount Gerizim to pronounce blessings, while the other half would stand on Mount Ebal to declare curses. In the valley between stood the Levitical priests with the Ark of the Covenant, representing God’s presence and authority.

“And half of them shall stand on Mount Gerizim to bless the people, and half of them on Mount Ebal for the curse…”
Deuteronomy 27:12–13

Later, Joshua fulfilled this exact command after leading the Israelites across the Jordan:

“And all Israel, sojourner as well as native born, with their elders and officers and their judges, stood on opposite sides of the ark before the Levitical priests… Half of them in front of Mount Gerizim and half of them in front of Mount Ebal…”
Joshua 8:33

This dramatic gathering was a powerful reminder: God’s covenant involves both promise and responsibility.


Theological Significance

  1. Covenant Relationship and Free Will
    Mount Gerizim and Ebal represent the dual outcomes of the covenant—blessing and curse—which depend on human response to God’s Word. This reflects the theological principle of human responsibility in divine covenant. God initiates relationship, but we are called to respond in obedience.

    “I call heaven and earth to witness against you today, that I have set before you life and death, blessing and curse. Therefore choose life…”
    Deuteronomy 30:19

  2. Symbol of Judgment and Grace
    Mount Ebal (where the altar was built) is where the Law and the sacrifices met—highlighting that even under judgment, God provided a way of forgiveness through sacrifice. This points forward to Jesus Christ, the ultimate sacrifice for our sins.

    “For the law was given through Moses; grace and truth came through Jesus Christ.”
    John 1:17

  3. Foreshadowing the Gospel
    Though these mountains aren’t often mentioned in the New Testament, Jesus indirectly referenced Mount Gerizim during His encounter with the Samaritan woman:

    “Our fathers worshiped on this mountain, but you say that in Jerusalem is the place where people ought to worship.”
    John 4:20

    The Samaritans still honored Mount Gerizim as sacred. But Jesus responded with a revelation of New Covenant worship:

    “The hour is coming when neither on this mountain nor in Jerusalem will you worship the Father… true worshipers will worship the Father in spirit and truth.”
    John 4:21, 23

    In Christ, physical locations give way to spiritual realities. True blessing is not tied to geography but to relationship with God through Jesus.


Spiritual Application for Believers Today

Even today, Mount Gerizim and Mount Ebal stand as spiritual metaphors. Every believer faces a similar choice: to walk in obedience and receive God’s blessings (Gerizim), or to reject His Word and suffer the spiritual consequences (Ebal).

God’s Word is clear—those who walk in His ways will experience the fruit of obedience:

“Blessed is the man who walks not in the counsel of the wicked… but his delight is in the law of the Lord.”
Psalm 1:1–2

But those who reject His truth will find themselves cut off from His blessing:

“But they refused to pay attention… therefore great wrath came from the Lord of hosts.”
Zechariah 7:11–12


Conclusion

Mount Gerizim and Mount Ebal are more than historical sites—they are enduring symbols of the choices we make daily in our walk with God. The Law, blessings, curses, sacrifice, and grace all intersect on those slopes. Through Christ, the curse is broken, and the blessing is fulfilled in those who believe and obey.

We now live not under the shadow of the Law, but in the reality of grace. Yet the principle remains: our lives are shaped by our response to God’s Word.

Will you choose the path of Gerizim or Ebal? The mountain of blessing or the mountain of judgment?

Shalom.

 

Print this post