Category Archive maswali na majibu

Yaya ni nani? (Mwanzo 24:59).

Swali: Huyu yaya aliyeenda na Rebeka ni nani kama tunavyomsoma katika Mwanzo 24:59?

Jibu: Turejee…

Mwanzo 24:59 “Ndipo wakampeleka Rebeka ndugu yao, na YAYA wake, na mtumishi wa Ibrahimu, na watu wake”.

Yaya maana yake ni muuguzi (yaani mwangalizi wa mtu aliye katika udhaifu fulani au ugonjwa)...kwa kiswahili kingine chepesi ni NESI.

Kwahiyo Rebeka wakati anachukuliwa ili apelekwa kwa Isaka…aliambatana na Nesi wake huyo(Yaya).

Sasa biblia haijaelezea kwa undani sababu za kwenda naye, kwamba ni kwasababu za ugonjwa Rebeka aliokuwa nao (ambao pia haujatajwa) au labda kwa dharura endapo angepata shida fulani katika njia anayoiendea basi apate msaidizi kwani safari ile ilikuwa ni ndefu sana….

Au labda alimuhitaji yaya mbeleni katika maisha yake ya ndoa, baada ya kujifungua n.k hakuna anayejua, biblia imesema tu alienda na Yaya wake.

Neno hili pia limeonekana sehemu nyingine katika biblia..

2 Samweli 4:4 “Naye Yonathani, mwana wa Sauli alikuwa na mwana aliyekuwa na kilema cha miguu. Alikuwa amepata miaka mitano, habari za Sauli na Yonathani zilipofika Yezreeli, na yaya wake akamchukua akakimbia ikawa, alipokimbia kwa haraka, huyo mtoto akaanguka, akawa kilema. Na jina lake aliitwa Mefiboshethi”

Soma pia 2Nyakati 22:11 utaona pia  neno hilo.

Naam kiroho YAYA wetu ni YESU KRISTO, tuwapo wadhaifu au katika dhiki au hali za kuishiwa nguvu na kuhitaji msaada, ni YESU KRISTO tu pekee awezaye kututunza na kututoa katika hizo hali.

Lakini Bwana hawezi kuwa mlezi wetu ikiwa hatutamruhusu awe hivyo, lakini tukiruhusu aingie maishani mwetu, na pia tukimheshimu na kuzishika amri zake hakika hatatuacha katika mateso sawasawa na ahadi zake.

Zaburi 41:3 “BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani. Katika ugonjwa wake umemtandikia”

Je unaye YESU moyoni, na je maisha yako yanaakisi wokovu wa kweli?.

Kama bado upo nje ya YESU tafuta msaada mapema kwa YESU kabla mambo hayajaharibika zaidi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kwanini Mwanadamu hakuumbwa kwa Neno tu kama viumbe wengine?

Swali: Katika kitabu cha Mwanzo tunaona viumbe vyote viliumbwa na Mungu kwa kutamka tu Neno!, lakini kwa mwanadamu haikuwa hivyo, alimwumba kwa mikono yake, je sababu ni nini?


Jibu: Turejee

Mwanzo 1:19 “Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya nne.

 20 MUNGU AKASEMA, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.

 21 MUNGU AKAUMBA nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. 

22 Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi. 

23 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tano.

24 MUNGU AKASEMA, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo

25 MUNGU AKAFANYA mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.”

Hapa tunasoma kwamba MUNGU AKASEMA, na kisha MUNGU AKAFANYA..  Kwahiyo kumbe MUNGU alianza kwanza kwa kusema ndipo “akafanya”..Naam hata wewe unaweza kusema “utajenga nyumba” ikawa ni kauli, na wakati utakapofika ukaanza kukusanya malighafi na kuitengeneza ile nyumba.. Kwahiyo kuna “KUSEMA” na “KUFANYA” ndiyo kanuni Bwana MUNGU aliyoenda nayo pia.

Sasa biblia haijaeleza kwa urefu alifanyaje fanyaje, kwenye huo udongo wakatokea wanyama, na viumbe..Kwamba ile kauli ya kinywa chake ndio ilienda kubadili ule udongo na kuwa Twiga, na Simba, na Tembo, au kwamba baada ya kusema alienda kuchukua udongo kwa vidole vyake na kufanya wanyama wale wote hakuna anayejua, lakini tunachojua ni kwamba wanyama walitokea ardhini kwa neno lake hilo.

Lakini tukiendelea na mstari wa 26 alipomwumba mtu, tunaona jambo jipya.. MUNGU ANASEMA, na kisha ANAUMBA kwa maelezo  marefu zaidi tofauti na ilivyokuwa kwa wanyama.

Mwanzo 1:26 “MUNGU AKASEMA, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 

27 MUNGU AKAUMBA mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.

Soma tena Mwanzo 2:7 na Isaya 45:12 utaona maelezo ya ziada juu ya uumbaji wa mtu.

Kwa wanyama Bwana MUNGU hakuelezea kawaumba kwa mfano wa kitu gani, na kwa sura ya kitu gani, huenda labda waliumbwa kwa mfano wa baadhi ya viumbe vya mbinguni (kwani kuna malaika mbinguni wenye uso kama wa tai, na wengine wenye uso kama wa simba na ndama, na pia mbinguni kumetajwa uwepo wa farasi, soma Ezekieli 1:10, Ufunuo 4:7 na Ufunuo 19:11), lakini hiyo yote biblia haijaeleza, ni makisio tu..

Lakini alipoumbwa mwanadamu, biblia imetoa maelezo ya wazi kabisa ziada kaumbwa kwa mfano wa MUNGU, na kwa sura  ya MUNGU, kuonyesha umaalumu wake na utofauti wake na viumbe vingine vyote.

Na kama jinsi MUNGU alivyo Mkuu mbinguni na tena anatawala mbinguni, hali kadhalika na yule aliyetengenezwa kwa mfano wake duniani, atakuwa na nguvu na utawala kama wa kwake duniani.

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”.

Lakini pamoja na kwamba Adamu aliumbwa ili atawale duniani, bado alimwuzia shetani nafasi yake hiyo, lakini habari njema ni kwamba YESU KRISTO alishinda na kuirejesha nafasi ya mwanadamu ya utawala..

Na wote wamwaminio Bwana YESU wanatawala naye si tu duniani, bali hata mbinguni.. kwani tumeketi naye mbinguni katika ulimwengu wa roho.

Waefeso 2:5 “ hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.

6  Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu”

Lakini ukiwa nje ya Kristo, huna mamlaka yoyote, kwani shetani ndiye anayekutawala..Mpokee leo KRISTO na upande viwango vingine vya kiroho.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kufuatana na ile habari ya Tajiri na Lazaro, ingewezekanikaje Nabii Samweli kupandishwa juu?

Swali: Katika ile habari ya Tajiri na maskini Lazaro (katika Luka 16: 27-31) tunasoma kuwa haikuwezekana kwa Lazaro kurudishwa duniani kuwahubiria ndugu watano wa yule Tajiri, ijapokuwa yule Tajiri alimsihi sana baba Ibrahimu amtume Lazaro, lakini haikuwezekana…

Lakini tukirudi nyuma katika 1Samweli 28:12-14….. tunasoma kuwa iliwezekana kumrudisha nabii Samweli aliyekuwa amekufa na kusema na Mfame Sauli ambaye alikuwa anaishi..je hii imekaaje, na ili hali tunajua Ibrahimu alikuwepo kabla hata ya Samweli na Sauli?.


Jibu: Awali turejee habari ya maskini Lazaro na Tajiri.

Luka 16:27 “Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,

28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.

29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.

31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu”

Hapa biblia inaonyesha kuwa ni kweli haikuwezekana Lazaro kutumwa duniani na kusema na ndugu watano wa yule Tajiri…

Lakini tusome tena ile habari ya nabii Samweli na Sauli alipokwenda kwa yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi.

1 Samweli 28:12 “Hata yule mwanamke alipomwona Samweli alilia kwa sauti kuu; na yule mwanamke akamwambia Sauli, akasema, Mbona umenidanganya? Kwa kuwa wewe ndiwe Sauli.

13 Mfalme akamwambia Usiogope; waona nini? Yule mwanamke akamwambia Sauli, Naona mungu anatoka katika nchi.

14 Naye akamwuliza, Ni mfano wa nini? Akajibu, Ni mzee anazuka; naye amefunikwa vazi. Basi Sauli akatambua ya kwamba ndiye Samweli mwenyewe, akainama uso wake mpaka nchi, akasujudia

15 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Mbona umenitaabisha mimi, hata kunipandisha juu? Sauli akajibu, Mimi nimetaabika sana; kwa kuwa hao Wafilisti wananifanyia vita, naye Mungu ameniacha; hanijibu tena, wala kwa manabii, wala kwa ndoto; kwa hiyo nimekuita wewe, ili wewe unijulishe nifanyeje”

Hapa tunaona Samweli aliyekufa akipandishwa juu, sasa swali la msingi ni hili; ingewezekanikaje jambo hilo na ilihali ile habari ya Lazaro na Maskini inakataa uwezekano wa jambo hilo?..je biblia inajichanganya?

Jibu ni la! biblia haijichanganyi, kwani maneno yake yote yamethibitika na wala haijakosewa mahali popote..

Sasa iliwezekanikaje nabii Samweli kuzungumza na Sauli aliye hai na ishindikane kwa Lazaro kurudi kuwahubiria walio hai?.

Fumbo lipo kwa huyo mwanamke mwenye pepo, alichokifanya mwanamke mwenye pepo si kumfufua nabii Samweli na kumrudisha juu, hiko kitu kisingewezekana….alichokifanya mwanamke mwenye pepo ni kuwasiliana na wafu.. na kutoa taarifa za wafu na kuwapa walio hai.

Hivyo Sauli hakumwona Samweli kwa macho, ndio maana alimwuliza yule mwanamke; anayezuka anaonekanaje na yule mwanamke akamtajia kuwa ni mzee mwenye mvi, ikimaanisha kuwa Sauli hakuwa anamwona Samweli, bali alikuwa anasubiria taarifa kutoka kwa yule mwanamke.

Kwahiyo kilichokuwa kinaendelea pale ni kwamba Sauli alikuwa anaongea na Samweli kupitia kinywa cha yule mwanamke, (kama tu vile mtu anavyoongea na roho za mapepo, kupitia kinywa cha yule aliyepagawa na pepo).

Lakini katika ile habari ya Luka, yule Tajiri alitaka Lazaro atoke kule kwa wafu (yaani afufuke) arudi katika mwili aseme na walio hai, jambo ambalo lisingewezekana..

Sasa utauliza je mpaka leo inawezekana mtu kuwasiliana na wafu kama huyu mwanamke mwenye pepo alivyofanya?.

Jibu ni La! Baada ya Bwana YESU kufufuka alizitwaa funguo za mauti na kuzimu, na kuwamiki wote walio hai na walio kufa, kwahiyo hakuna yoyote hata shetani mwenye uwezo wa kuwasiliana na mfu, au kutoa habari za wafu.

Mwenye uwezo huo ni BWANA YESU PEKE YAKE!!.

Mapepo yanaweza kujigeuza na kuchukua sauti na umbile la mtu aliyekufa na kuigiza kama yule mtu, na kuwatokea watu yakidai ni watu halisi waliokufa… yanaweza kufanya hivyo kwani maandiko yanathibitisha hilo.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Nabii Samweli hakumtokea Sauli na kusema naye, bali alizungumza naye kupitia kinywa cha yule mwanamke mwenye pepo, na jambo hilo kwasasa haliwezekani tena kwani Kristo ndiye mwenye funguo hizo peke yake.

Kwa urefu kuhusiana na roho za waliokufa na mizimu fungua hapa 》》》Mizimu ni nini?

Bwana akubariki…

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Nini tofauti kati ya kileo na divai ?

1Samweli 1:5 Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi  sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za Bwana.

Divai na kileo ni vinywaji vya kulewesha, na vyote vilitumika zamani katika Israeli, ambavyo hata sasa vinatumika.

Tofauti kati ya Divai na kileo ni hii;

DIVAI:

Divai, ilichachushwa kutoka katika matunda ya zabibu tu.

Kwa wayahudi divai ilikuwa kama kinywaji cha kitamaduni kilichotumika sana sana katika karamu mbalimbali za kijamii,  tunaona mfano wa sherehe ile aliyoalikwa Bwana Yesu kule Kana,  katikati ya sherehe walitindikiwa Divai, ndipo Yesu akaenda kuyageuza yale maji kuwa divai. Kuonyesha kuwa divai ilikuwa ni kinywaji kilichoruhusiwa kitamaduni Israeli, katika karama. (Yohana 2)

 Lakini pia ilikuwa kama kinywaji cha kiibada, katika karamu za kidini, kwa mfano sikukuku za pasaka, wana wa Israeli walikunywa  divai pamoja na mikate isiyotiwa chachu. Tunaona hilo Kristo alilidhihirisha kipindi kile cha pasaka alipoketi na wanafunzi wake akawapa mkate na divai, kama ishara ya mwili wake na damu yake, imwagikayo kwa ajili ya ondoleo la dhambi za watu wengi. (Mathayo 26.27-29)

Lakini pia divai ilisimama kama kiashiria cha furaha, au baraka.

Zaburi 104: 15 Na divai imfurahishe mtu moyo wake. Aung’aze uso wake kwa mafuta, Na mkate umburudishe mtu moyo wake.

MVINYO:

Mvinyo ulitengenezwa kwa  ngano, shayiri, makomamanga, au tende tofauti na divai iliyozalishwa katika zabibu tu.

Mvinyo ulikuwa na kilevi kikali kuliko divai, na matumizi yako hayakuwa rasmi Israeli, Ilitumika sana sana katika karamu za ulafi na ulevi, lakini sio katika shughuli zozote za kijamii au kidini.

Makuhani hawakuruhusiwa kuinywa walipokuwa wakihudumu katika hema (Walawi 10:9)

Lakini maandiko yanasema nini kuhusu ulevi?

Mithali 20:1 Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.

Katika andiko hilo tunaona Hana, aliposhutumiwa na Eli kuhusu ulevi, yeye akamwambia mimi sikunywa divai wala kileo. Kuonyesha kuwa alitilia umakini ibada yake na sala zake kwa Mungu.

Hata leo, ni vema tufahamu kuwa hatulewi tena kwa mvinyo, bali kwa Roho Mtakatifu tuliyepewa ndani yetu (Waefeso 5:18), Yeye ndiye divai yetu na mvinyo yetu.

Hivyo ni wajibu wa mwamini yoyote kudumu katika Maombi, kutafakari Neno, na ibada, ili ajazwe vema Roho.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Paulo alimwambia Timotheo atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lake, Je! tunaruhusiwa na sisi pia kutumia pombe?

Je! mabalasi Bwana Yesu aliyoyatumia kugeuzia maji kuwa divai, yalitumika tu kwa kazi hiyo?

Kwanini Bwana YESU ageuze maji kuwa Divai? Na ni ujumbe gani tunapata?

Print this post

Je Bwana YESU alikuwa na amri ya kumwingiza mtu katika ufalme wa MUNGU au hakuwa nayo?

Swali: Kwenye Mathayo 20:20-25 Mke wa Zebedayo anamwendea YESU na wanawe akimuomba wakae pande zote za YESU na awape mamlaka alizonazo ila YESU akamwambia hana amri juu ya jambo hilo lakini huku kwenye Luka 23:39 anamwambia mmoja wa wale wanyang’anyi leo hii utakuwa na mimi peponi, naomba ufafanuzi wa mwingiliano huo wa maandiko….Je biblia inajichanganya kwa maneno hayo???…

Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.

21  Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.

22  Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.

23  Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.

24  Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili”.

Hapa tunaona Bwana anatamka kuwa “Hana amri ya kuwaketisha vijana hao upande wa kuume na kushoto katika ufalme wake”

Tusome tena Luka 23:39

Luka 23:39 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.

40  Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

41  Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

42  Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43  YESU AKAMWAMBIA, AMIN, NAKUAMBIA, LEO HIVI UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI.”

Sasa swali ni kwanini KRISTO awe na amri juu ya huyu mhalifu na asiwe amri juu ya wale Vijana wa Zebedayo?.

Jibu ni kwamba “walichokiomba wana wa Zebedayo ni tofauti na alichokiomba huyu mhalifu”.. Wana wa Zebedayo wenyewe waliomba nafasi za ukubwa ndani ya ufalme wa mbinguni (kwamba watakapofika mbinguni wakawazidi wengine wote ikiwemo akina Petro na mitume wengine na hata sisi watu wa kizazi hiki)…

Lakini huyu Mhalifu yeye hakuomba ukubwa wowote ndani ya ufalme wa mbinguni kwamba akawe nani huko anakokwenda bali aliomba tu nafasi ya kuuingia ule ufalme wa mbinguni, (habari za kwenda kuwa nani huko aendako hilo hakujali, alichokitamani na kuuingia tu ule ufalme).

Na KRISTO alimpa hiyo nafasi kwani hiyo AMRI anayo kwa watu wote watakaokiri makosa yao Ikiwa na kumwamini Bwana YESU kama alivyofanya huyu Mhalifu. (Na KRISTO alimwambia vile kwasababu alijua hatakengeuka tena, kwani maisha yake ndio yalikuwa yanaenda kuisha, alikuwa amebakisha masaa machache tu ya kuishi).

Lakini wana wa Zebedayo, tayari walikuwa wameshajiwekea hakika wa kuuingia ufalme wa mbinguni, kwasababu walishamwamini Bwana YESU na kutubu kitambo kirefu….na hivyo wakaenda mbali zaidi si kuomba kuuingia ufalme wa mbinguni, bali kuomba nafasi za juu katika huo ufalme wa mbinguni watakaouingia… Jambo ambalo KRISTO asingeweza kuwaahidia.

Ni sawasawa na mwanafunzi anayemwomba mwalimu ampe zawadi ya nafasi ya kwanza darasani na ilihali bado hajafanya mtihani.. Ni wazi kuwa mwalimu hawezi kumpa hiyo zawadi, kwani bado hajafanya/kumaliza mtihani…Matokeo yatakapotoka ndio yatakayoeleza kama anastahili hiyo zawadi ya nafasi ya kwanza au la!.

Na KRISTO hakuwa na amri ya kuwapa hizo nafasi walizokuwa wanazitaka kwani vita vya imani bado walikuwa hawajavimaliza, na ule mwisho bado haujafika, ambapo kazi ya kila mtu itakapopimwa na kupewa thawabu,

Siku ile kama watakuwa wamefanya bora kuliko wengine wote watapata hiyo nafasi waliyoiomba (ya kuketi mkono wa kuume na kushoto), lakini kama watatokea wengine watakaofanya vema kuliko wao, basi wataikosa na nafasi hizo watapewa wengine.

Je umeokoka?

Je unajua kuwa YESU KRISTO anarudi!… na dalili za kurudi kwake karibia zote zimeshatimia?..Je unafahamu kuwa kuishi maisha ya uvuguvugu ni laana? Soma Ufunuo 3:14, leo unaenda kanisani kesho unaenda bar, asubuhi unaimba kwaya, jioni miziki ya kidunia, kwenye kabati una nguo za heshima, na nguo za kikahaba.. Huo wote ni uvuguvugu ambao Bwana YESU alisema matokeo yake ni kutapikwa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kwanini Ayubu ailaani siku aliyozaliwa?

Swali: Kuna uhusiano gani kati ya aina ya maisha anayoishi mtu na ile siku aliyozaliwa?.. Kwanini Ayubu anailaani ile siku aliyozaliwa na ule usiku ilipotungwa mimba? (Ayubu 3:1-6).

Jibu: Turejee..

Ayubu 3:1 “Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake. 

2 Ayubu akajibu, na kusema; 

3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba. 

4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie. 

5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe. 

6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi”.

Sababu kuu ya Ayubu kuilaani siku aliyozaliwa ni kutokana na majaribu aliyoyapitia!.. Ya kupoteza mali zake pamoja na watumwa wake, lakini pia ya kupoteza watoto wake na zaidi sana kupatwa na magonjwa.

Hali hiyo ya mapito magumu ndiyo iliyomfanya Ayubu ailaani siku yake ya kuzaliwa… Maana ya kulaani hapo “ni kutotamani kuzaliwa”, kwamba ni “kosa kubwa limefanyika yeye kuzaliwa/kuja duniani”.

Lakini pamoja na kwamba Ayubu aliilaani siku yake ya kuzaliwa bado hakumlaani MUNGU, wala kumwazia mabaya.. ndio maana hapo anasema… “Siku hiyo (ya kuzaliwa) Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie”.. kitendo hiko cha kumhusisha MUNGU katika kauli yake hiyo ni kuonyesha Ayubu alimheshimu MUNGU.

Lakini swali ni Je! jambo hilo  Ayubu alilolifanya ni sahihi? Na Je na sisi pia tunaweza kuzilaani siku zetu tulizozaliwa ikiwa tutapitia majaribu yanayofanana au kukaribia kufanana na ya Ayubu?..

Jibu ni hapana! hatupaswi kuzilaani siku zetu tulizozaliwa, vile vile  Ayubu hakufanya jambo lililo jema machoni pa BWANA kwa kauli ile!.. kwani tunaona ijapokuwa Ayubu hakumlaani MUNGU kwa kinywa chake lakini kitendo pia cha kuilaani siku yake ya kuzaliwa kilikuwa ni kosa, wala haikuwa ni busara kusema vile, bali alinena pasipo maarifa, ingawa nia yake ya ndani haikuwa ovu kama ile ya mke wake..

Ayubu 35:16 “Ndiposa Ayubu hufunua kinywa chake kwa ubatili; Huongeza maneno pasipo maarifa”.

Kwahiyo alinena hayo maneno pasipo maarifa, ndio maana mwishoni tunaona baada  ya kutokewa na MUNGU katika upepo wa kisulisuli na kusahihishwa alitambua makosa yake ya kuwa maneno aliyoyatoa yalikuwa yana kasoro (yasiyo na maarifa) na alitubu..

Ayubu 42:1 “Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema. 

2 Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika. 

3 Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? KWA MAANA, NIMESEMA MANENO NISIYOYAFAHAMU, MAMBO YA AJABU YA KUNISHINDA MIMI, NISIYOYAJUA. 

4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie. 

5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. 

6 KWA SABABU HIYO NAJICHUKIA NAFSI YANGU, NA KUTUBU Katika mavumbi na majivu”.

Umeona hapo?, Ayubu anakiri makosa aliyoyafanya ya kusema maneno asiyoyajua, na anamaliza kwa kutubu. Ikimaanisha kuwa nasi hatupaswi kusema maneno kama hayo. Kukosoa siku uliyozaliwa bado kwa namna moja au nyingine ni kumkosoa MUNGU, Hata kama hatutalihusisha jina la  MUNGU katika kukosoa kwetu huko, bado hatupaswi kulaani, kwasababu kila kitu kinakuja kwa makusudi..

Ikiwa unaona unapitia majaribu mazito usiojua mwanzo wake wala mwisho wake, suluhisho si kuikimbilia siku uliyozaliwa na kuilaani, au kujijutia kuzaliwa!.. hiyo haisaidii kitu, kwani hiyo siku imeshapita na haiji tena mbeleni,.. zaidi sana badala ya kulaani, ni vizuri kutafuta kujua chanzo cha majaribu hayo ni nini, kwa kujinyenyekeza mbele za MUNGU.

Na MUNGU kwakuwa ni mwaminifu kwetu na mwenye upendo, hawezi kamwe kutuacha muda mrefu katika mitihani mkubwa wa kutokuelewa sababu ya majaribu yanayotukabili, ni lazima tu ataonyesha njia na kutufunulia sababu ya mapito tupitayo….hivyo ni suala la kujinyenyekeza tu na kumngoja BWANA, Na si kulaani…

Laiti Ayubu angejua kuwa muda mchache tu umebaki wa MUNGU kwenda kumrudishia vile alivyovipoteza mara dufu, asingesema yale maneno ya laana,… lakini tunajua alisema vile pasipo maarifa ili baadaye na sisi pia tuje kujifunza.. ma ndio maana baadaye alitubu na MUNGU akamsamehe..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kujihudhurisha mbele za Bwana ndio kufanyaje (Ayubu 2:1).

Swali: Maana ya kujihudhurisha mbele za MUNGU kulingana na Ayubu 2:1 ndio kufanyaje?.


Jibu: Turejee…

Ayubu 2:1 “Tena kulikuwa na siku hao wana wa Mungu walipokwenda KUJIHUDHURISHA mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao, ili kujihudhurisha mbele za BWANA”.

Kujihudhurisha ni kitendo cha kujisogeza mbele za MUNGU.. Neno hili msingi wake ni “kuhudhuria”… Kama vile askari anavyohudhuria kituoni kila siku, ni hivyo hivyo pia kwa hawa wana wa MUNGU kibiblia.

Sasa katika biblia kuna mahali Malaika wanatajwa kama wana wa Mungu na kuna mahali wanadamu (wanaomcha MUNGU) wanatajwa kama wana wa MUNGU. (Mfano. Wote waliomwamini Bwana YESU ni wana wa MUNGU, soma Yohana 1:12).

Makundi haya yote mawili, huwa yanajihudhurisha mbele za MUNGU kwa malengo mbalimbali kwa ufupi tuangalie jinsi yanavyojihudhurisha mbele za MUNGU.

   1. MALAIKA

Malaika wanajihudhurisha (yaani wanajisogeza) mbele za MUNGU kupeleka taarifa zetu njema, wao ni mawakili wema kwetu, wakati shetani na majeshi yake yanajihudhurisha kupeleka mashitaka juu yetu kwa Mungu, malaika watakatifu wenyewe wanapeleka taarifa njema.

Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”.

Soma pia Yuda 1:9 na Waebrania 1:14, utaona huduma za hawa Malaika watakatifu kwetu, na soma pia Ufunuo 12:10 na 1Petro 5:8 utaona huduma ya shetani juu yetu kuwa ni mashitaka tu (anajihudhurisha mbele za MUNGU kutushitaki usiku na mchana).

Na ndicho kilichotokea hapa kwa Ayubu, wakati Malaika watakatifu (wamejihudhurisha kwa MUNGU) kupeleka taarifa njema za watakatifu waliopo duniani, shetani naye alijihudhurisha kuwachafua..

Ndio maana utaona baada ya Bwana kumwuliza umetoka wapi na baada ya kumwuliza habari za Ayubu, hakuanza kumtetea Ayubu badala yake kumchochea kwa MUNGU..

Ayubu 2:3 “BWANA akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu”.

Umeona hapo hapo shetani alimchochea MUNGU ili.amwangamize Ayubu (kwani yeye ni mshitaki tu siku zote).

  2. WANADAMU.

Kama Malaika (watakatifu na walioasi) wanavyojihudhurisha mbele za MUNGU, na hali kadhalika wanadamu wanaweza kujihudhurisha mbele za MUNGU.

Njia zifuatazo ndizo mtu anaweza kuzitumia kujihudhurisha mbele za BWANA.

     1. Maombi.

Maombi binafsi ni njia ya kwanza ya mtu kujihudhurisha mbele za  MUNGU.

Mathayo 6:6 “Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”

Mtu anapoomba katika roho anajisogeza mbele za MUNGU, Zile hoja anazozipeleka zinamfikia MUNGU katika kiti chake cha enzi, sawasawa tu na Malaika wanavyomfikia MUNGU na kusema naye.

   2. Kukusanyika na wengine.

Mkusanyiko pamoja na wengine unahusisha watu zaidi ya mmoja ikiwemo kanisani.

Mathayo 18:20 “Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao”.

Kama Bwana YESU yupo katikati ya mahali walipokusanyika watu wawili au zaidi, maana yake hiyo ni sehemu sahihi ya kujihudhurisha mbele za MUNGU, na sehemu hiyo ni rahisi kupokea majibu ya maombi kwani alisema wawili wenu wakipatana jambo lolote na kumwomba Baba wa mbinguni watatendewa.

Mathayo 18:19 “Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni”.

Pamoja na hayo yapo mambo ambayo pia hayatuhudhurishi mbele za Bwana sawasawa na 1 Wakorintho 8:8.

1 Wakorintho 8:8 “Lakini chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu; maana, tusipokula hatupunguziwi kitu, wala tukila, hatuongezewi kitu”

Kwa urefu kuhusiana na kitu kisichotuhudhurisha kwa Bwana fungua hapa >>>

Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

Mwisho: Je wewe unajihudhurisha mbele za Bwana?..unaomba?, unakusanyika na wengine katika Bwana?..

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je kuna haja gani ya kuamini biblia iliyoandikwa na watu?

Swali: Biblia imeandikwa na watu, (kama Paulo, Petro, Musa, Daudi na wengineo) je tutaamini vipi kitu kilichoandikwa na wanadamu kuwa ni kweli,? vipi kama wametoa tu kwenye akili zao, kwanini tukiamini kitabu cha namna hiyo, chenye mikono ya wanadamu?

Jibu: Kabla ya kujibu swali hili, tusome kwanza maandiko yafuatayo…

Yohana 14:11 “Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, SADIKINI KWA SABABU YA KAZI ZENYEWE”

Hapa Bwana YESU anatoa njia za sisi kumwamini yeye, kwamba kama hatutamwamini kwa yeye kutuambia kwa mdomo wake mwenyewe, basi tumwamini kupitia zile kazi anazozifanya ambazo ni ishara na miujiza.

Hiyo hakika ni hekima kuu sana!… kwamba kama sisi ni kazi sana kumwamini yeye kwa maneno ya kinywa chake, basi tuzipime zile kazi anazozifanya ikiwa ni halisi na za kweli, basi tumwamini kwahizo pasipo hata maneno yake.

Vile vile na hata kuhusiana na waandishi wa Biblia, kama hatuwaamini kuwa wameandika mambo waliyovuviwa na MUNGU, basi kupitia matokeo ya kazi hizo, (jinsi yanavyobadilisha watu wengi leo, na kuponya watu wengi) basi tuamini.

Labda hujaelewa vizuri, tafakari tena mfano huu.

Umeletewa kitabu cha Fizikia, ambacho kimsingi kimeandikwa na watu wengi, ambapo ndani ya kitabu hiko waandishi wameeleza kanuni/fomula za kuunda ndege inayoruka juu sana, sasa kitabu kama kitabu kinakuambia kuwa kwa kupitia kanuni hii inawezekana kutengeneza chombo na kuruka juu mawinguni..(hayo ni maneno ya waandishi wa kitabu, ambao ni wanasayansi).

Sasa kwa maneno yao hivyo tu, hatuwezi kuamini, au tuseme ni ngumu kuamini!, kwamba huwenda yakawa ni maneno ya kutunga tu, au ya watu waliorukwa na akili… lakini anapotokea mtu na kutengeneza chombo kinachoruka angani kupitia kanuni za wanasayansi hao walizoziandika kwenye kitabu chao hiko, basi ndipo tunaweza kuamini kuwa waliyokuwa wanayasema ndani ya kitabu ni kweli, kwani tumeona kabisa ndege ikiruka kupitia kanuni walizoziandika kupitia kile kitabu.

Vile vile tunaweza tusiyaamini maneno ya Paulo, au ya Petro au ya Daudi au ya Mtume mwingine yoyote ndani ya biblia, lakini tutakapoyaona yametumiwa na wengine na kuleta matokeo kama waliyoyasema ndani ya kitabu cha biblia tutawaamini.

Sasa maneno yao (Paulo, Petro, Daudi na wengineo) yamewekwa katika matendo na majaribio ya mamilioni ya watu, na yameleta matokeo yale yale waliyoyasema hao Mitume ndani ya biblia, hicho ndicho kinachotufanya tuwaamini kuwa waliyokuwa waliyoyaandika ni kweli, na uzuri ni kwamba hata mimi na wewe tumepewa nafasi ya kuyatafiti maneno hayo kama ni kweli au uongo..

Walisema na kuandika ndani ya kitabu (biblia) kuwa kwa jina la YESU pepo wanatoka, leo tumejaribu na tumeona ni kweli, na maelfu ya watu wamejaribu na kuona ni kweli, hivyo basi maneno yao ndani ya biblia ni kweli!.

Mitume waliandika kuwa Aminiye na kubatizwa atapokea zawadi ya Roho Mtakatifu (Matendo 2:38), jambo hilo tumelihakiki wenyewe kuwa ni kweli, na wewe unaweza kulihakiki kuwa ni kweli, sasa kuna sababu gani ya kutoaiamini biblia, ijapokuwa imeandikwa na watu?.. kama watu wanaishuhudia kweli, basi kinachofuatwa ni ile kweli wanaousema na si watu.

Ukiona mtu anasema mwanasayansi aliyetoa kanuni ya kuunda ndege ni mwongo na katunga, na huku ndege zinaonekana zikiruka, basi mtu huyo anayepinga huwenda anamatatizo ya afya ya akili, na anahitaji msaada, vile vile ukiona mtu anapinga elimu inayotolewa na mitume wa kwenye biblia na huku matokeo ya elimu hiyo yanaonekana wazi kwa macho, basi mtu huyo huwenda anayo matatizo pia ya afya ya akili za rohoni au hata ya mwilini, anahitaji msaada.

2Petro 1:20 “Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.

21  Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, WAKIONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU”.

Biblia si kitabu kilichoandikwa kwa fikra za watu, kama ulikuwa unafikiri hivyo, basi leo hii anza kubadili mtazamo wako na fikra zao, anza kuisoma Biblia kwa mtazamo mwingine na utamwona MUNGU na si Mtu, kwa msaada wa njia bora ya kusoma biblia tutafute inbox.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?

Jibu: Mpaka kufikia mwaka 2024 biblia imetafsiriwa kwa lugha 756, hivyo kuna tafsiri Zaidi ya 756 mpaka sasa duniani kote.

Sasa kwa asili biblia iliandikwa kwa lugha kuu tatu, ambazo ni KIEBRANIA (Agano la Kale), lugha ya KIARAMU (Sehemu za Agano la kale na jipya) pamoja na lugha ya KIYUNANI AU KIGIRIKI (Agano jipya), Hizo ndizo lugha kuu tatu zilizoandikia biblia ya kwanza, na haikuandikwa kwa lugha ya kiingereza wala Kiswahili, wala lugha nyingine yoyote tofauti na hizo tatu.

Sasa kuna tafsiri nyingi za biblia siku hizi za leo kwasababu kadhaa, na sababu hizo zipo tatu (3)..

1)Tofauti za lugha, 2) Maendeleo ya Lugha 3) Mitazamo ya kidhehebu.

Hizo ndizo sababu kuu tatu,.. hebu tutatame moja baada ya nyingine.

1. Tofauti za Lugha

Kwasababu biblia kwa asili iliandikwa kwa lugha ya Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Zipo jamii za watu zisizozungumza lugha hizo, na kwasababu ni lazima watu wote, ulimwenguni kote walisikie Neno la Mungu, ni lazima tafsiri iwepo,….na watalisikiaje na kulielewa wasipolisikia kwa lugha yao na kulisoma kwa lugha yao?..

Hiyo ndiyo ikawa sababu ya Biblia ya kwanza yenye lugha hizo tatu, kutafsiriwa kwa lugha nyingine mbali mbali ikiwemo lugha yetu ya Kiswahili, Hebu tafakari laiti isingetafsiriwa kwa lugha yetu, biblia kwetu ingekuwa ngumu kiasi gani leo?.. Hivi ilivyo tu tayari ni ngumu!… vipi kama tungekuwa tunaisoma kwa lugha nyingine?? Si hali ingekuwa mbaya Zaidi??…kwasababu ingetupasa tukajifunze kwanza lugha hizo tatu, jambo ambalo lingekuwa gumu sana kwa wengi!.

Kwasababu ya shida hiyo, ndipo Bwana MUNGU wetu kupitia Roho wake Mtakatifu alitangulia kuachilia uwezo wa lugha na tafsiri zake ile siku ya Pentekoste, (soma Matendo 2) kuonyesha kuwa sasa Neno linapaswa lihubiriwe kwa watu wote na lugha zote, na ndipo zikaja tafsiri hizo.

 2. Maendeleo ya Lugha.

Hii ni sababu ya pili ya uwepo wa tafsiri nyingi, utaona tayari kuna tafsiri moja ya lugha husika, tuchukue mfano lugha ya Kiswahili, halafu baada ya muda unaona kuna tafsiri nyingine zinaongezeka tofauti na hiyo ya kwanza na tena kwa lugha hiyo hiyo ya Kiswahili.

Sasa hiyo inatokana na kukua kwa lugha, kwani lugha siku zote inakuwa (inaongezeka misemo na maneno), na kwasababu hiyo basi tafsiri nyingi zinatokea na bado zitaendelea kutokea,

3. Mitazamo ya Kidhehebu na Theolojia

Kutokana na ongezeko la Madhehebu mengi yenye itikadi zinazotofautiana, imechangia pakubwa kutokea kwa tafsiri mpya kila siku kulingana na misimamo ya dhehebu husika. Kwani tafsiri nyingine zinaegemea mapokeo ya dhehebu hilo, kwamfano utaona dhehebu la katoliki linatumia biblia yenye vitabu vingine vya Deuterokanoni, ambavyo vinafanya jumla ya vitabu 72, tofauti na Biblia ya asili yenye vitabu 66.

Zipo na sababu nyingine ndogo ndogo ikiwemo mbinu za kutafsiri, kwamba wengine wanatafsiri neno kwa neno, na wengine wanatafsiri sentensi nzima na kuleta maana ya ujumla, na sababu nyingine ni mapendekezo ya lugha laini kwaajili ya watoto, zenye kutumia tafsida na zisizotumia lugha za ukali na kuogopesha. Hizi zote ndizo zinazochangia ongezeko la tafsiri za biblia kila siku.

Lakini swali je! Ni tafsiri ipi iliyo sahihi na isiyo na sumu kwa mkristo?

Mara nyingi kitu cha asili kinakuwa ni bora kuliko kile kilichochujwa Zaidi.. Tafsiri iliyo bora na yenye kufaa kuliko zote ni ile yenye lugha tatu (Kiebrania, Kiaramu na kiyunani), lakini kwasababu ni ngumu sisi kukijua kiyunani, na kiebrania kifasaha, basi tafsiri inayofuata kwa Ubora ni ile ya kwanza kabisa iliyotafsiriwa katika yetu lugha husika, kwamfano kwa sisi tunaozungumza Kiswahili, tafsiri ya kwanza kabisa na bora kwa lugha yetu ni ile ya SWAHILI UNION VERSION (SUV), ambayo ndiyo inayotumika sasa kwa wingi, inayoanza na…

Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.”

Hiyo ndiyo tafsiri iliyo bora, tafsiri nyingine zinazofuata baada ya hapo faida yake inakuwa ni ndogo ukilinganisha na hasara…kwani zinabadilishwa maana na zinatengenezwa kwa kuegemea dini Fulani, na katika lugha nyingine ni hivyo hivyo, ile ya kwanza ni bora Zaidi kuliko zilizoendelea kufuata.

Kwahiyo kwa hitimisho, Tafsiri sahihi yenye kumfaa mtu ni ile ya kwanza (yenye kiebrania, kiyunani na kigiriki) ikiwa mtu atakuwa ana uwezo wa kuzielewa lugha hizo, lakini kama hana uwezo basi ile tafsiri ya kwanza kabisa iliyotafsiriwa kwa lugha yake, ni bora Zaidi.

Je umempokea Bwana YESU kikweli kweli?

Je unajua kuwa tunaishi katika siku za kurudi kwa pili kwa Bwana YESU na unyakuo upo karibu?, Je unajua kuwa kama huna Roho Mtakatifu huwezi kuiona mbingu (Warumi 8:9).. sasa kama bado hujaokoka unasubiri nini?,

Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini

12  Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.

13  Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.

14  Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake”.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?

SWALI: Naomba kufahamu Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?


JIBU: Kazi ya jina sio tu kumtambulisha au kumtofautisha mtu mmoja na mwingine. Bali jina linasimama pia kueleza Wasifa wa mtu,

Hivyo jina la mtu linapobadilika, aidha Wasifa pia hubadilika.

Kwamfano Ibrahimu alipobadilishwa jina kutoka Abramu na Kuwa Ibrahimu ni kwasababu alikuwa anaenda kuwa Baba wa mataifa mengi.(Mwanzo 17:5)

Vilevile Sarai kuitwa Sara. Ni kwasababu anaenda kuwa mama wa mataifa mengi..(Mwanzo 17:15)

Sauli kuwa Paulo kwasababu anaenda kuwa mtume kwa mataifa.(Matendo 13:9)

Vivyo hivyo tunaona Mungu katika maandiko Akijitambulisha kwa majina mbalimbali, lengo sio kuonyesha uzuri au upekee wa majina yake hapana bali kutambulisha wasifa wake.

Kwamfano alipojitambulisha kama Yehova rafa, alisimama kama Mungu mponyaji..Yehova yire Mungu atupaye, Yeshua(Yesu), kama Mungu atuokoaye.

Tukirudi kwa wakati wa sasa Biblia Inatuonyesha kuwa Kristo atakaporudi mara ya pili atakuja na jina lingine jipya. Ambalo ndio tunangojea kuona utukufu wake, mamlaka yake na nguvu zake.

Ufunuo wa Yohana 3:12

[12]Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.

Jina hili halitakuwa Yesu,tulitumialo sasa ambalo linawasifa wa wokovu, lililojikita katika kiwakomboa na kuwafungua wanadamu katika mauti na vifungo vya kila namna.

Lakini hilo linalokuja litakuwa ni jina lenye uweza Mwingi, la kifalme, la kiutawala zaidi. Wakati huo Kristo hataonekana tena kama mwanakondoo mpole, asimamaye kutuombea kwa Baba N.k..hapana ataonekana katika taswira mpya kabisa ya kifalme, na zaidi ya hapo (Ufunuo 19:11-16), sawasawa na hilo jina lake litakavyokuwa.

Ndio maana kuna umuhimu sana kuokoka sasa, angali neema na msamaha upo katika jina la YESU, kwasababu atakaporudi mara ya pili,na jina jipya hatajua kusamehe ni nini, bali mambo mengine mapya yatakuwa wanaendelea..Usipookoka leo hakuna wokovu siku ya mwisho.

Vilevile wale watakaoshinda Kristo ana ahidi kuwapa majina mapya ya kipekee, ambayo yatawanafisisha kipekee mbele ya Kristo.

Ufunuo wa Yohana 2:17

[17]Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.

Ndugu Utukufu Unaokuja wa Kristo ni mkuu sana, ni heri ukose vyote sasa, lakini usikose mbingu Mpya na nchi mpya na ile Yerusalemu mpya ishukayo kutoka kwa Baba mbinguni.

Siku hizi ni za mwisho, unyakuo umekaribia sana. Mambo ya umilele yanakaribia kuanza. Bado unaendelea kung’ang’ana na ya kidunia? tubu leo mgeukie Kristo.

Bwana akubariki.

Amen.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

JE NI LAZIMA KUBADILISHA JINA BAADA YA KUOKOKA?


Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?

Print this post