MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

Mkaribie Bwana.

Shalom, karibu tujifunze Neno la Mungu..

Miongoni mwa watu waliokuwa wanamfuata Bwana Yesu kulikuwa na makundi manne..1) Makutano 2)Wanafunzi 3)Mitume 12 na 4) Nguzo.

Kundi la kwanza ambalo ni makutano, hawa walikuwa tu wanakusanyika kusikiliza mahubiri ya Bwana Yesu ambao mara zote Bwana alikuwa anazungumza nao kwa mifano, na kuwaponya magonjwa yao..baada ya hapo walikuwa wanarejea katika shughuli zao na maisha yao ya kawaida.

Kundi la pili ambalo lilikuwa ni la wanafunzi wa Yesu, hawa walikuwa wapo kama 70 hivi au zaidi kidogo..Kundi hili ni lile ambalo lilikuwa linamfuata Bwana Yesu lakini si kila mahali…Ni baadhi ya watu ambao waliamua kujitoa kumtumikia Yesu sehemu zote alizokuwa anakwenda…na hawa pia Bwana alikuwa anawatuma kuhubiri injili kila mahali ambapo Bwana alipokuwa anataka kwenda. (Soma Luka 10:1).

Kundi la tatu lilikuwa ni Mitume…Mitume hawa walikuwa 12 tu, na waliteuliwa na Bwana Yesu kati ya lile kundi la wanafunzi 70 waliokuwa wanamfuata Yesu.

Luka 6: 13 “Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume”

Kundi la mitume ndio lilikuwa linamkaribia sana Bwana kuliko wale wanafunzi 70 na makutano..Hawa kila mahali Bwana alipokuwa na wao walikuwepo, walikula nae na kunywa naye…na mbele za Bwana ni kama vile walipendelewa zaidi kuliko wanafunzi wengine kwasababu kila mfano ambao Bwana aliokuwa anawafundisha makutano usioeleweka wao ndio walikuwa wanapata fursa ya kwenda kumwuliza akiwa peke yake, maana ya mifano hiyo, nafasi ambayo makutano wala wale wanafunzi wengine hawakuipata.

Lakini lilikuwepo kundi la mwisho ambalo ni la kipekee sana..ambalo hilo lilikuwa karibu sana na Bwana zaidi ya makundi hayo matatu yaliyotangulia…na kundi hilo lilitwaliwa kutoka miongoni mwa wale wanafunzi 12…Na hao walikuwa watatu tu ambao ni (Petro, Yohana na Yakobo)..Hawa watatu walijulikana kama NGUZO.

Wagalatia 2:9 “tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; YAKOBO, na KEFA na YOHANA, WENYE SIFA KUWA NI NGUZO, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;”

Kefa ni jina lingine la Petro(soma Yohana 1:42). Hawa watatu walijulikana kama nguzo…Maana yake walikuwa wanauhusiano wa kipekee na Bwana zaidi ya mitume wote, zaidi ya wanafunzi wote na zaidi ya makutano yote.

Utaona hawa watatu kila mahali ambapo Bwana alitaka kwenda peke yake (labda mlimani kusali, au kuwafunulia siri za ndani sana) aliwachukua hawa watatu tu Yohana, Yakobo na Petro, na si mitume wengine waliosalia..Hebu tuangalie mifano michache kulithibitisha hili..

Luka 9:27 “Nami nawaambia kweli, Wapo katika hawa wanaosimama hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata wauone kwanza ufalme wa Mungu.

28 Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa PETRO NA YOHANA NA YAKOBO, AKAPANDA MLIMANI ILI KUOMBA.

29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.

30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni Musa na Eliya”

Unaona hapo walikuwepo mitume wote lakini Yesu aliwachagua tu hao watatu kwenda nao mlimani..kusali na huko akawafunulia ufunuo mkubwa namna ile, na wakaisikia sauti ya Mungu ikisema huyu ni mwanangu mteule wangu, msikieni Yeye. Ufunuo huo waliouona tu hawa watatu, na Bwana aliwaambia wasimwambie mtu mwingine yoyote mpaka atakapofufuka katika wafu. Maana yake ni kwamba wanafunzi hawa walikuwa na siri nyingi ambazo Bwana aliwafunulia ambazo mitume wengine hawakuzijua.

Tutazame mfano mwingine tena..

Mathayo 26:36 “Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe.

37 Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka.

38 Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami.

39 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.

40 Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?”

Hapo utaona Bwana alitenga makundi mawili..kundi la kwanza ambalo ndilo lile la mitume 9 aliliacha kule kwenye bustani ya Gethsemane….hakuenda nalo kuomba usiku ule, badala yake akawachukua Petro, na wale wana wawili wa Zebedayo ambao ni (Yohana na Yakobo), hao ndio akaenda nao kusali..na hao ndio aliowaambia wakeshe waombe pamoja na yeye wasije wakaingia majaribuni..kwasababu shetani ndio aliokuwa anawawinda zaidi kwasababu walikuwa na Bwana zaidi..Na kama wewe ni msomaji wa biblia utagundua kuwa wakiwa kule waliona tena ishara nyingine wakati Yesu akiwa anaomba jasho lake lilikuwa kama matone ya damu, na pia waliona malaika wakija kumtia nguvu…

mambo hayo mitume wengine waliosalia hawakuyaona…

Na hawa watatu, hata wakati wa Pentekoste na kuendelea ndio mitume Bwana alitembea nao kwa viwango vikubwa sana..mpaka watu wote wakawaita kuwa ni NGUZO YA KANISA. Kitabu cha Ufunuo wa Yohana, ambacho kimebeba siri nyingi za ufunuo wa siku za mwisho, na ujio wa Bwana Yesu kimendikwa na Yohana huyu…ambaye ndiye mmoja wao wa wale watatu.

Sasa kwanini wanafunzi hawa watatu waliteuliwa na Bwana kuwa karibu zaidi na yeye kuliko wengine wote?

Jibu ni kwamba, kwasababu walimpenda Bwana zaidi..Mungu hana upendeleo hata kidogo..kila dakika, kila muda walikuwa wanamtafakari Bwana, wanamfikiria yeye, wanamtumikia yeye, na wamejikana nafsi na kusema lolote liwalo tutamfuata Yesu Bwana wetu popote aendapo, kwa moyo huo Bwana akawapenda zaidi na hivyo kuwakaribisha wamsogelee zaidi kuliko wengine…Kama ni mwanafunzi wa Biblia utamjua Petro alivyokuwa anampenda Bwana…ilifika wakati akamwambia Bwana wajapochukizwa wote kwaajili yako mimi sitachukizwa..ijapokuwa alikuwa ni dhaifu lakini angalau hata alikuwa anaujasiri wa kusema hivyo tofauti na wengine…

Hali kadhalika Yohana na Yakobo ni hivyo hivyo,..walimpenda Bwana mpaka ikafikia wakati wakamwendea Bwana wao na kumwomba katika ufalme wake waketi mmoja mkono wake wa kuume na mwingine wa kushoto…(walimpenda Bwana mno na hivyo Bwana akawapenda zaidi). Yohana ilifika wakati akawa anaegemea kifuani mwa Yesu kila mahali…na ilifika kipindi Bwana akawaambia wazi wazi kuwa mmoja wao atamsaliti..na kila mmoja akawa anawasiwasi ni nani amtajaye..na Bwana akamfunulia Yohana peke yake kwamba ni Yuda kwa sauti ya chini, wengine hawakusikia.. kwasababu alikuwa karibu sana na yeye kifuani mwake…

Yohana 13:23 “Na palikuwapo mmoja wa wanafunzi wake, ameegama kifuani pa Yesu, ambaye Yesu alimpenda.

24 Basi Simoni Petro akampungia mkono, akamwambia, Uliza, ni nani amtajaye?

25 Basi yeye, hali akimwelekea Yesu kifua chake, akamwambia, Bwana, ni nani?

26 Basi Yesu akajibu, Ndiye mtu yule nitakayemtowelea tonge na kumpa. Akatowelea tonge, akalitwaa akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote”.

Tabia ya hawa watatu kuwa tayari chochote Bwana alichowaambia ndizo zilizowafanya kuwa karibu zaidi na Bwana kuliko wengine, Bwana alipotaka kwenda kuomba walikuwa tayari kutaka na wao kwenda kuomba..walikuwa hawaonyeshi dalili za uvuvi ingawa walikuwa na madhaifu, walijinyima kila kitu ili tu wampendeze Yesu.

Vivyo hivyo Neno la Mungu linasema..Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.

Unapojikana nafsi na kumpenda Mungu zaidi, na kumfanya yeye ndio wakwanza kila mahali, hapo ndipo unapojitengenezea daraja zuri la Mungu kukukaribia zaidi..ndipo unapoongeza daraja zuri la Mungu kukupenda zaidi ya wengine, kukufunulia siri nyingi zaidi ya wengine…kukutumia na kukubariki. Unapoutafa uso wa Mungu kwa kusali, kufunga, kutenda mema zaidi ya wengine..mema yako yanapimwa mbele za Mungu kila siku na yanapoonekana yamezidi ya wengine wengi ndipo na wewe thamani yako inapanda mbele za Mungu, lakini kama leo ukiambiwa tu usali..hata dakika mbili humalizi, kusoma tu neno ni mara moja kwa wiki, na hata ukisoma unasoma tu mistari na sio mada nzima..hapo utafanyikaje NGUZO mbele za Mungu.?

Hivyo tusiridhike na uhusiano wetu na Mungu..Tuzidi kumkaribia Bwana..kutoka kuwa wanafunzi wake, hata mitume wake hata Nguzo..

Ufunuo 3: 12 “Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa NGUZO katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Maran atha!

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

YULE JOKA WA ZAMANI.

KUOTA UNAANGUKA .

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

Shalom, karibu tujifunza Neno la Mungu..

Matendo 13:46 “Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa milele, angalieni, twawageukia Mataifa.

47 Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, Upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.

48 Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini.

49 Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote”.

Ni jambo la kuogopesha kusikia kuwa wapo watu waliokusidiwa uzima wa milele, na wapo ambao hawajakusudiwa uzima wa milele. Na hilo linatupa picha kuwa suala la wokovu sio jambo la kubabaisha bali ni mpango wa Mungu mkamilifu ambao ulishapangwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu..alishakuwa na Idadi kamili ya watakaokolewa na akawaandika katika kitabu chake cha uzima..

Ufunuo 17:8 “ Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama…”

soma pia Waefeso 1:4

Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Yohana 6:44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.

Ikimaanisha kuwa tendo la kumwamini tu Kristo na kumfuata kwa uaminifu wote sio jambo la mtu tu kujiamulia, bali ni jambo ambalo Mungu alishalipanga kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu na hivyo akamchagua mtu huyo, kisha akamwekea mwiitikio huo ndani yake na ndio maana akamwamini na kumfuata bila kigugumizi chochote..

Na ndio maana hata wakati mwingine utamwona yupo ambaye kazaliwa katika ukristo, kalelewa katika mambo ya imani maisha yake yote, amekuwa akihudhuria kanisani miaka mingi na kwenye mikutano mbali mbali lakini bado suala la wokovu lisiwe ni jambo la muhimu sana katika maisha yake..Lakini wakati huo huo, utaona tena mtu mwingine ambaye amezaliwa katika mazingira yasiyomjua Mungu, au pengine muislamu, au mbudha hajui vizuri masuala ya wokovu, lakini siku moja akasikia tu mahali Fulani Kristo anahubiriwa, na muda huo huo akachomwa moyo, akaacha kila kitu na kumfuata Yesu kwa kutokujali kuwa ndugu zake watamchukuliaje..

Sasa Hapo unajiuliza inakuwaje?..Ni kwasababu yeye alikusudiwa uzima wa milele, na huyu mwingine hakukusudiwa.

Angalia tena sehemu nyingine biblia inasema..

2Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu”.

SASA UTAJITAMBUAJE KUWA WEWE NI MMOJA WA WALE WALIOKUSUDIWA UZIMA WA MILELE, AU LA..

Kama tulivyosoma hapo juu anasema wote walioakusudiwa uzima wa milele WALIAMINI..Unaona? Waliamini kile walichohubiriwa wakati ule ule, maana yake wakaenda kubatizwa, wakadumu katika imani, na utakatifu, wakawa kila siku wanalitendea kazi lile Neno walilokuwa wanafundishwa na mitume..

Lakini wale wengine ambao hawakukusudiwa ambao walikuwa wanajiona wao ni watu wa dini, watu waliozaliwa katika imani hao ndio Mungu aliowakataa, matokeo yake wakabaki vile vile,..Na ndivyo ilivyo hata leo, Ukiona umeshahubiriwa injili, miaka nenda rudi, lakini ndani yako hakuna badiliko lolote, au wokovu unauchukulia kama jambo lisilokuwa la maana sana kwako, fahamu kuwa wewe hujakusudiwa uzima wa milele..Kwasababu ungekuwa umesudiwa uzima wa milele, usingepambana au kushindana na habari njema za Yesu Kristo, pale unapoambiwa utubu dhambi.

Biblia inasema njia ile ni nyembamba iendayo uzimani,..Pengine Ni Mungu anasema na wewe leo, ili umgeukie, pengine wewe ni mmojawapo wa waliokusudiwa uzima wa milele, na ndio maana unasikia Roho Mtakatifu akiugua ndani yako..Basi kubali wito huo haraka na kumpokea Yesu kwa moyo wako wote siku ya leo, ili uwe mmojawapo wa wale ambao majina yao yalishaandikwa katika kitabu cha uzima kabla hata ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo hii, Kumkabidhi Yesu Kristo maisha yako.

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako ili kuukamilisha wokovu wako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

 

UCHAWI WA BALAAMU.

YULE JOKA WA ZAMANI.

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Basi tuendelee kumjua mungu, naye atatujilia kama mvua ya vuli.


Ndugu, mmoja aliniuliza, akasema, Ni faida gani unapata katika kumtumikia Mungu?..Nikamwambia ni nyingi tu, akasema mimi niliokoka tangu zamani, na niliamua kweli kumfuata Mungu, mpaka ikafika hatua ya mke wangu kunikimbia kutokana na hali yangu, nikawa ninamwomba Mungu sana, ninafunga, ninahudhuria semina mbalimbali, ninahudhuria maombi ya mikesha sana tena sana, nikawa ninamwomba Mungu anikumbuke katika hali yangu ya kiuchumi, lakini kwa jinsi nilivyozidi kuendelea ndivyo mambo yangu yalivyozidi kuwa mabaya,..

Ndugu huyu Kwa jinsi alivyokuwa anaongea na mimi alikuwa anaonyesha kuwa tayari ameshakata tama na ameshaachana na wokovu..Mwisho kabisa akaniambia “Huoni kuwa kuna tatizo fulani na huyu Mungu tunayemtumikia”?

Neno hilo lilinishtua kidogo, nikamwambia kwangu mimi sijaona tatizo lolote katika kumtumikia, sijajua uhusiano wako na Mungu upoje kwa upande wako, Nikamwambia Daudi alisema katika biblia kuwa yeye tangu ujana wake mpaka amekuwa mzee hajawahi kuona mwenye haki ameachwa na Mungu…

Nilipomwambia vile nikisubiri anijibu, Yule mtu hakunijibu tena akaondoka..

Ndugu yangu, lipo jambo ambalo sisi kama wakristo tulioamaaisha kweli kumfuata Mungu tunapaswa tulijue Daudi japokuwa alizungumza maneno hayo, lakini haikumaanisha kuwa ni muda wote na wakati wote mambo yalikuwa yanakwenda kama alivyotaka.. Zipo nyakati nyingi alimwona Mungu kama amemwacha, Kama alikuwa hamsikii, au haoni shida zake anazozipitia dhidi ya hali yake na maadui zake lakini alijipa moyo akisema, Bwana yupo pamoja nami,gongo lake na fimbo yake vyanifariji na alizidi kujipa moyo kumshukuru na kumsifu Mungu..akijua kuwa hata katika mateso yake Mungu hawezi kumwacha.

Sikiliza maneno haya ya Daudi..

Zaburi 13:1 “Ee Bwana, hata lini utanisahau, hata milele? Hata lini utanificha uso wako?

2 Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Hata lini adui yangu atukuke juu yangu?

3 Ee Bwana, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.

4 Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.

5 Nami nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.

6 Naam, nimwimbie Bwana, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu”.

Zaburi 42:9 “Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?

10 Watesi wangu hunitukana mithili ya kuniponda mifupa yangu, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako?”

Unaona, upo wakati aliomba lakini haoni majibu, alitamani lakini hakupata, alikuwa akihuzunika akikumbuka kuna wakati alimpiga Goliathi, na wafilisti wote wakawa wanamuogopa lakini wakati mwingine haoni msaada wowote mpaka anaenda kuomba hifadhi kwa hao hao wafilisti ambao walikuwa adui zake, walau wampe eneo la kuipumzisha nafsi yake..mpaka unafika wakati tena wafilisti wanakwenda kupigana na ndugu zake Wayahudi na yeye pia anataka kujumuika nao ili tu awaridhishe wafilisti wasimwone kuwa ni msaliti..Wengi wetu hatujui kuwa Daudi tunayemsoma kuna wakati alilikimbia taifa lake na kwenda kutafuta msaada kwa wafilisti (maadui wa Israeli)..

Sasa kwa namna ya kawaida ungeweza kusema Daudi alishaachwa na Mungu tangu zamani, kuna tatizo na huyo Mungu anayemtukia,..Lakini pamoja na mateso hayo yote alizidi kuzishilia ahadi za Mungu, akimshukuru yeye, na kumwimbia siku zote..Mpaka wakati ulipofika wa yeye kustareheshwa ulipofika, na kufanywa mfalme wa Israeli nzima, mpaka leo hii tunamsoma Daudi kama mtu aliyeupendezesha moyo wa Mungu, haikuwa safari rahisi, ya kudhani kuwa kila alichokiomba kilikuwa kinakuja kwa ghafla tu..

Baadaye Daudi anakuja kusema..

Zaburi 66:19 “Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu.

20 Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake”.

Hata na sisi wakati huu, Bwana Yesu alituambia, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtaona, bisheni nanyi mtafunguliwa, hakumaanisha kuwa tuombapo yatakuja wakati huo huo kwa ghafla, inaweza pia ikawa hivyo lakini si wakati wote,..Ni kuamini, na kungoja na kuwa na saburi…Na ndio maana Bwana wetu huyo huyo sehemu nyingine alisema maneno haya..

Luka Luka 18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”

Unaona, maandiko hayo yanatuonyesha kabisa, kuombwa kwetu kunapaswa kusiwe kwa kukata tamaa kama vile kulivyokuwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo na kwa Daudi. Kwasababu ni uhakika kwamba mwisho wa siku tutajibiwa, iwe isiwe, majibu yatakuja tu kama tulivyomwomba, kwasababu Mungu ni mvumilivu kwetu. Na anatuhurumia na anapendezwa na dua zetu.

Hivyo wewe uliyemfuata Kristo kwa moyo wako wote, nataka nikuambie usikatishwe tamaa, kuona hakuna dalili yoyote leo, majira yako yatafika, nawe utasema kama Daudi “Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu”.

Zidi tu kuonyesha bidii kumtafuta yeye leo ,wacha kuangalia hali yako ya sasa..Wakati wa kukujilia kama mvua ya vuli utafika kama hautautupa utakatifu wako na wokovu wako.

Hosea 6:3 “Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini [HAKIKA] kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

MAFUNDISHO YA NDOA.

SAA YA KUHARIBIWA IIJIAYO ULIMWENGU WOTE.

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Ibrahimu analitaja jina la YEHOVA wakati Musa anasema hakujifunua kwa jina hilo kwao?

SWALI: Hujambo mpendwa,naomba nieleweshwe hili tafadhali katika mwanzo 22:14 utaona Ibrahimu alipaita mahali pale YEHOVA-YIRE ambapo alimtoa yule kondoo kuwa sadaka, badala ya Isaka, lakini ukisoma tena katika Kutoka 6:2-3 Mungu anamwambia Musa kwamba hakuwai kujidhihirisha kama YEHOVA kwa Ibrahimu ,Isaka, na Yakobo, bali Mungu mwenyezi. Je! Biblia inajipinga? Asante sana.


JIBU: Kumbuka vitabu vitano vya mwanzo vimeandika na mtu mmoja ambaye ni MUSA (Ambavyo ni Mwanzo, kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na kumbukumbu la Torati ).. Na kama tunavyojua Musa aliviandika vitabu hivi alipokuwa jangwani (yaani akiwa njiani kuelekea nchi ya Ahadi).. Na katika kitabu cha Mwanzo ambacho ndicho tunapata huko habari za Ibrahimu…wakati anaziandika habari hizo akiwa jangwani tayari alikuwa ameshafunuliwa jina hilo jipya la Mungu yaana YEHOVA. Hivyo mahali popote ambapo alisoma habari za Ibrahimu, akimtaja Mungu kwa jina lolote lile yeye Musa ni lazima angeliandika kwa jina YEHOVA, kadhalika mahali popote ambapo Nuhu angemtaja Mungu kwa jina lolote lile yeye Musa angesahihisha katika maandishi yake na kuandika jina YEHOVA badala yake..na hivyo hivyo kwa Lutu, Yakobo, Isaka, Yusufu na wengineo.

Sasa utauliza mbona kila mahali katika vitabu hivyo vitano vya kwanza vya Musa kila mahali Mungu katajwa kama BWANA, na si hilo YEHOVA ??

Kumbuka Katika biblia yetu ya Kiswahili na ya kiingereza na ya lugha nyingine zote…kila mahali ambapo leo hii tunapasoma pameandikwa neno BWANA, Kwa asili hapakupaswa paandikwe hivyo…Sehemu nyingi katika agano la lake unapopaona pameandikwa neno BWANA, kwa asili pangepaswa paandikwe neno YEHOVA. Musa nyingi alizitafsiri kama Yehova..kwa mfano katika

Mwanzo 2:7 biblia inasema

“ Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”…Mstari huu Musa aliuandika hivi “Yehova Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai ”

Lakini sasa watafsiri wa kwanza biblia waliona ili kuliheshimu zaidi hilo jina la Mungu si vyema kuandika jina hilo Tukufu na kuu kama lilivyo…Hivyo kwa hekima ya Roho ndipo likawekwa jina BWANA badala ya YEHOVA..Kitu ambacho ni kizuri!..kama tu vile isivyo hekima wala heshima kumwita mzazi wako jina lake halisi na badala yake unamwita jina lake la cheo “BABA”..huwezi kusema shikamoo Joseph badala yake utasema shikamoo Baba. Hivyo si dhambi kumwita Mungu BWANA kama inavyochukuliwa leo na ndugu zetu mashahidi wa Yehova wakidhani kuwa kumuita Mungu BWANA ni kumvunjia heshima..

Biblia zote, pale kwenye utangulizi, zimechapishwa na angalizo hilo pale mwanzoni kabisa.. Kuwa BWANA lilimaanisha YEHOVA.

Kwahiyo kitabu cha Mwanzo kimetaja Yehova na kitabu cha Kutoka kwasababu mwandishi ni huyo huyo mmoja, na aliviandika vitabu hivyo akiwa tayari ameshalijua jina la Mungu kamilifu yaani Yehova.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?


Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

KWANINI BWANA YESU ALISULUBIWA NA WEZI WAWILI?

Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?

Rudi Nyumbani:

Print this post

OLE WA NCHI NA BAHARI.

Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.

13 Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama JUU YA MCHANGA WA BAHARI”.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, kama ukisoma mistari iliyotangulia kabla ya hiyo, utaona kuwa shetani kuna majira alijaribu kufanya vita katika mbingu, lakini alishindwa kama biblia inavyotuambia akatupwa chini na mahali pake hapakuonekana tena mbinguni kuanzia huo wakati.

Lakini biblia inatuambia pia alipotupwa, hakukaa katika eneo la nchi peke yake, au hakwenda baharini moja kwa moja , hapana, bali alikwenda kusimama juu ya mchanga wa bahari….Kwa namna nyingine alikwenda kusimama ufukweni mahali ambapo nchi na bahari vinakutana.

Shetani alifahamu kuwa, hivyo ndivyo vitu viwili vinavyoikamilisha dunia, hakuegemea tu upande mmoja afanye makao yake huo hapana..badala yake alisimama pale ufukweni ili aweze kuyaona na kuyatawala yale yanayotoka katika nchi na yale yanayotoka katika bahari. Na ndio maana baada ya pale biblia inasema “Ole wa nchi na bahari”, Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu..

Unaona? haituambii nchi tu peke yake, au bahari peke yake, hapana bali vyote viwili, kwasababu ndipo alipopania kuwanasa wanadamu.

SASA NCHI NA BAHARI KIBIBLIA VINAWAKILISHA NINI?

BAHARI: au sehemu yenye maji mengi, biblia imeshatupa majibu yake,.Tusome.

Ufunuo 17:15 “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha”.

Kumbe maji yanawakilisha jamaa, na makutano na mataifa na lugha…Yaani kwa ufupi watu wengi.

Vilevile, tunaweza kuona jambo lingine, pale Bwana Yesu alipochagua mitume wake, wengi wao aliwachagua kutoka katikakati ya wavuvi, akifunua kuwa watakuja kufanya kazi ya uvuvi wa watu wengi, yaani jamaa, na mataifa la Lugha, kama alivyomwambia Petro na Andrea katika (Mathayo 4:19)..

Hivyo Bahari inawakalisha watu wengi, kwahiyo shetani tangu alipoona ameshindwa hawezi tena kupigana yeye kama yeye aliamua sasa kuelekeza macho yake katikati ya watu ili apate nguvu, na chombo kikubwa anachokitumia ili kupata ufuasi mkubwa wa watu ni kupitia kitu kinachoitwa DINI, penye dini ndipo palipo na watu wengi, sio katika siasa au makabila..

Hivyo mpaka sasa yupo katika kilele cha kuzikutanisha dini zote na madhehebu yake yote ambayo tangu zamani yalishautupilia mbali uongozo wa Roho Mtakatifu na kufuata mapokeo yao ya kibinadamu, ili zikubaliane katika kitu kimoja.

Na ndio maana ukisoma ile sura inayofuata ya 13, utaona Yule joka aliposimama tu pale kwenye mchanga wa bahari, wakati huo huo wanyama wawili walitokea, mmoja alitokea baharini, na mwingine akatokea nchi kavu (Soma ufunuo sura ya 13 yote utaona)..Sasa Yule aliyetokea habarini ndiyo huyu atakayepata nguvu ya kuwa na wafuasi wengi sana duniani kwa kupitia dini…

NCHI: NI Hifadhi ya kimwili, tangu mwanzo, Mungu alipomuumba Adamu alimpa ardhi ailime na kuitunza kwasababu huko ndipo alipomchipulia chakula chake kitakachomfanya aishi hapa duniani.

Ayubu 28:5 “Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula;…”..

Hata sasa chakula na utajiri vipo katika ardhi..Hivyo kwa lugha ya sasa nchi tunaweza kusema inawakilisha Uchumi,..Fedha, biashara, hazina, vitu vinavyoweza kumpatia mwanadamu Rizki ili aishi hapa duniani n.k…

Kwahiyo shetani kuona hivyo, alisimama pia katika eneo hilo.. tangu huo wakati akajikita kudhibiti mihimili hiyo miwili mikuu, Watu, na uchumi.. nchi na bahari..

Kwanza Ili awapate Watu anatumia kivuli cha dini, ambapo hivi karibu anaenda kutimiza adhma yake ya kuzileta dini zote zilizopoteza uongozo wa Roho Mtakatifu pamoja, zikiongozwa na ile dini mama ya Rumi, na cha ajabu biblia inatuambia watu wote na mataifa yote ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu wataufurahia huo utawala na mfumo mzima wa ibilisi ..

Na sasa ili kuwalazimisha watu wote waufuate huo mfumo wa mpinga-Kristo, shetani atamnyanyua mnyama mwingine ambaye atakuwa na nguvu ya kiuchumi sana,(taifa kubwa) ambalo hilo litayahimiza mataifa mengine yote yapokee maagizo kutoka kwa huo umoja wa dini duniani, na mtu yoyote atakayekataa kuupokea hataruhusiwa kununua wala kuuza, wala kufanya biashara yoyote, wala kuajiriwa mahali popote.. Unaona Jinsi hali itakavyokuwa mbaya.. Ni nani atapona hapo.

Haya ni mambo ambayo tunaweza kuyashuhudia siku za hivi karibuni wala tusidhani bado miaka mingi, jaribu kufikiria jinsi ugonjwa huu wa Corona ulivyozuka tu ghafla, na athari yake ndogo tu inawafanya watu wasiweze kutembea hata nje katika baadhi ya nchi, na imetokea tu ndani ya kipindi kifupi cha miezi mitatu tu, hakuna ambaye angeamini kuwa dunia ingeweza kuwa namna hii, dunia ambayo inashamra shamra za kila namna..Lakini mambo yamekuwa hivyo barabara zipo wazi..Hata matajiri na wana wa wafalme, na watu mashuhuri na fedha zao haziwasaidii wakati huu. Ndivyo mambo yatakavyobadilika ghafla tu wakati huo ukifika.

Shetani ameshajidhatiti vya kutosha, na ghafla tu, dini zote zitafikia muafaka mmoja zikiongozwa na dini ile mama ya Rumi, watafikia muafaka mmoja, watapata sapoti kutoka katika kila pembe ya dunia, watakuwa na kiongozi wao mmoja ambaye ndio atakuwa mpinga-Kristo..Huyo ataishawishi dunia iwe na ustaarabu mpya, Lakini lengo lake ni kuihimiza ile chapa ya mnyama ili awanase wanadamu wote.. Sasa kwa kuwa yeye amejikita katika masuala ya kiimani sana, kama tulivyosema atapata msaada mwingine kutoka katika taifa lenye nguvu ya kiuchumi duniani, ili kuyalazimisha mataifa mengine yote yamtii yeye kwa shuruti.

Mpaka wakati huo umefika ujue unyakuo tayari umeshapita ndugu yangu, sijui utakula nini wewe unayemkataa Yesu leo, wewe ambaye utakuwepo ulimwenguni wakati huo, pona yako itakuwa ni kufia njaa ndani, kama utakuwa hujakamatwa na kuuliwa kwa mateso yasiyokuwa ya kawaida.. Hakuna mtu yoyote atayevumiliwa na mtu au chombo chochote cha dola ambaye ataonekana hajapokea chapa hiyo ya mnyama.. usifikiri utapona..Ni ngumu sana ndugu, usidhani akaunti yako ya benki itakusaidia wakati huo, hilo jambo halitakuwepo, usidhani utakimbilia mafichoni, ondoa hayo mawazo, usidhani elimu yako itakusaidia kupata ajira wakati huo, acha kufikiria hivyo..Chapa utaipokea tu.

Hizi ni nyakati za hatari tunazoishi, ole wa nchi na bahari!…Kimbilio pekee ni Kristo tu saa hii..Ikiwa upo bado nje ya Kristo, basi fanya uamuzi wa Busara leo hii, tubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, omba toba kwa Mungu, nenda kabatizwe ikiwa bado hujafanya hivyo. huu ni wakati sasa wa kuamka usingizini.

Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini”.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 21

UCHAWI WA BALAAMU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

DANIELI: Mlango wa 7

MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UCHAWI WA BALAAMU.

Hesabu 23:23 “Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli”

Wengi tunalifahamu hili andiko na tunalitumia, pale tunapohisi roho za kichawi zinatunyemelea…Na tunapolitumia kwa Imani linaleta majibu hakika kwasababu ni pumzi ya Mungu…Lakini hebu leo tuingie kwa undani kidogo kujifunza juu ya Neno hili ili tupate faida mara mbili Zaidi.

Siku zote tunashauriwa tujifunze biblia na sio tuisome tu…tukichukua tu kipengele cha mstari wa biblia na kukitumia hicho bila kutafuta maana ya mstari huo, kwanini mwandishi aliandika hivyo, na Mungu alikuwa anamaanisha nini juu ya mstari huo..hapo tutakuwa hatujajifunza bali tumesoma tu..ambapo matokeo yake ni madogo kuliko kama tungeketi chini na kujifunza kuanzia juu chanzo cha mstari huo na dhima, na maudhui ya huo mstari ukoje.

Sasa tukirudi katika mstari huo hapo juu, kama ukianza kusoma kitabu hicho cha Hesabu kuanzia sura zilizotangulia kabla ya hiyo ya 23, utaona inahusu safari ya wana wa Israeli (au wana wa Yakobo), walipokuwa wanatoka Misri kuelekea nchi yao ya Ahadi,

Wakiwa njiani jangwani walikutana na kikwazo, Ilikuwa kwamba ili waendelee na safari yao iliwapasa wakatize katika nchi ya watu fulani ambao walijulikana kama wamoabu.

Nchi hiyo ilikuwa na mfalme na huyo mfalme akawakatalia wasikatize katika nchi hiyo, na hakukuwa na njia nyingine ya karibu isipokuwa kukatiza katika nchi hiyo..Ijapokuwa waliwaomba sana na kuwaahidi kwamba watalipia gharama zote za uharibifu wowote kama ukijitokeza katika kukatiza kwao lakini wenyeji wa mji ule walikataa katakata wakiongozwa na mfalme wao..Na kwa hofu Mfalme wao hakuishia tu kuwazuia bali alipanga pia kwenda kupigana nao, hivyo akatafuta pia namna ya kuwalaani(au kwa lugha rahisi kuwaloga) ili atakapokwenda kupigana nao aweze kuwashinda kirahisi bila kutumia nguvu nyingi.

Katika harakati za kutafuta mtu mashuhuri wa kuloga, akampata mtu anayeitwa Balaamu mchawi (Hesabu 24:1), huyu alikuwa ni mchawi wa viwango vya juu sana na aliyejulikana kwa kuloga hata mataifa, ambaye alitumia nguvu za giza, na alikuwa anauwezo wa kuisikia pia sauti ya Mungu..na kabla ya kuloga alikuwa anauwezo wa kupima kiwango cha kiroho mtu alichopo kabla ya kumwangusha…na sio hilo tu, alikuwa anazo mpaka mbinu mbadala zisizo za kuweza kumwangusha mtu bila kutumia uchawi wowote…(na huo ndio mbaya Zaidi ambao ndio alioutumia kuwaangusha wana wa Israeli).

Sasa alipoitwa kama wengi wetu tunavyoijua habari…haraka sana aliwajua wana wa Israeli ni watu gani…alijua ni watu wa Mungu na wamezungukwa na ukingo wa Mungu pande zote…hakuna namna ya kuweza kuwaingia kwa njia ya uganga wala uchawi (hakuna namna yoyote vibuyu na dawa za miti shamba zinaweza kufanya kazi juu yao)..hata hivyo alinusurika kifo njiani wakati anajaribu kutaka kwenda kuwalaani…Ili litimie lile neno la kwanza (akulaaniye atalaaniwa, na akubarikiye atabarikiwa).

Hivyo Balaamu alilijua hilo na alipofika kwa mfalme wa MOABU akamwambia wazi kabisa kwamba “HAKIKA HAPANA UCHAWI JUU YA YAKOBO, WALA HAPANA UGANGA JUU YA ISRAELI”.

Hiyo ndiyo asili ya Neno hilo…Ni mchawi Balaamu ndiye aliyeyasema maneno hayo sio Mungu kama wengi wetu tunavyodhani. Balaamu alikiri kabisa..Hivyo akaacha kujaribu kuwaloga/kuwalaani Israeli ambaye ndiye Yakobo, kinyume chake akawabariki, kwasababu alijua endapo angetaka kuwaalaani ni kujitafutia laana na kifo..hivyo akaamua kuhamia kwenye Mbinu yake ya pili ambayo ndiyo KUBWA NA KUU.

Hesabu 24:1 “Basi Balaamu alipoona ya kuwa ilimpendeza Bwana kuwabariki Israeli, hakwenda, kama hapo kwanza, ili kutafuta uchawi, bali alielekeza uso wake jangwani”

Mbinu hiyo siyo ya kutumia vitunguli tena/wala vibuyu/ wala ya kuwatamkia maneno mabaya..Mbinu hii ya pili ambayo ndio UCHAWI HASAA ni ya kuwakosesha wana wa Israeli na Mungu wao..Ili Mungu awakasirikie na kuwaadhibu yeye mwenyewe…kwasababu kuwaangusha kwa njia ya uchawi imeshindikana sasa dawa ni kuwachonganisha na Mungu wao..Hivyo akamfundisha Mfalme wa Moabu namna ya kuwakosesha wana wa Israeli ili wapigwe na Mungu wao..

Akamfundisha na kumwambia wawaalike wana wa Israeli baadhi katika sadaka za miungu yao na kuwapa wanawake wao walio wazuri na warembo, hivyo Wana wa Israeli watakapoona hivyo wataingia tamaa na kuzini na wanawake hao katika karamu hizo za miungu na hasira ya Mungu itawaka juu ya wana wa Israeli..Tusome

Hesabu 25:1 “Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu;

2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.

3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli”.

Ukiendelea kusoma utaona Mungu aliwakasirikia na aliwaua kwa pigo watu elfu 24. Kama sio mtu mmoja kwenda kurekebisha Israeli wote wangeisha siku hiyo mbele ya ghadhabu ya Mungu..Hivyo japokuwa Yule mchawi balaamu hakuwaloga kwa uchawi wa uganga na vibuyu lakini aliwaloga kwa kuwakosesha na Mungu wao.

Jambo hilo hilo linaendelea hata sasa katika nyakati hizi za agano jipya. Ni kweli hakuna uganga wala uchawi juu yako, umelindwa na kuzungukwa na kingo za moto pande zote, katika afya yako, katika kazi zako, katika familia yako, mpaka una ujasiri wa kusema Bwana ndiye anisaidiaye sitaogopa mabaya, wala uchawi wala uganga..Ndio shetani analijua hilo na wala hawezi kukuloga kwa vitunguli, wanaokuendea kwa waganga ni kweli wanapoteza muda..nataka nikuambie shetani akishalijua hilo wala hapotezi muda wake kukutumia watu kutafuta kukuloga wewe…kwasababu hawezi kulaani kilichobarikiwa…hviyo acha kufikiri kwamba wachawi wanakuwinda wewe uliyeokoka kweli kweli, walishaacha siku nyingi wakati ule walipogundua tu unazungukwa na jeshi la mbinguni…

Shetani anachofanya sasa juu yako ni kutafuta njia ya kukukosesha wewe na Mungu wako, ili Mungu akuadhibu…na anatumia watu mfano wa Balaamu..wanaoonekana nje ni watu wa Mungu kumbe ndani ni mbwa-mwitu wa kali…Hao watakwambia kuoa mke wa pili si dhambi, watakwambia kuziangukia sanamu na kuzibusu na kuzipa heshima sio kuzisujudia.

Na biblia imeshatabiri nyakati hizi za mwisho watu wengi wataangukia katika kosa hili la Balaamu..

Yuda 1:11 “Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya Kora”.

Watakwambia kufanya matambiko ya ukoo sio dhambi, watakuwambia kuishi na mwanamke/mwanamume ambaye hamjaoana hakuna tatizo, watakuwambia kuzini ni mapungufu ya kila mtu, watakuweka katika kila kishawishi cha wewe kufanya dhambi, , Zaidi sana watakufariji katika dhambi na watakukemea katika kuwa mtakatifu…lengo na madhumuni ni kukukosesha wewe na Mungu wako ili Mungu akukasirikie na kukuangamiza (Huo ndio uchawi mkubwa shetani anaowalogea watu wa Mungu kuliko hata ule wa vibuyu)..

Bwana Yesu alisema maneno hayo Dhahiri katika Ufunuo.

Ufunuo 2:14 “Lakini ninayo maneno machache juu yako, kwa kuwa unao huko watu washikao mafundisho ya Balaamu, yeye aliyemfundisha Balaki atie ukwazo mbele ya Waisraeli, kwamba wavile vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na kuzini”.

Je! Na wewe umedanganyika na uchawi huo wa Balaamu? Nabii wa uongo?..Unadhani shetani anahangaika na bati lako usiku na kundi lake la wachawi?..usidanganyike!..anahangaika sasa kukukosesha na Mungu wako. Hataki ulifahamu neno na anafanya juu chini ufe katika dhambi zako ili siku ile uingia katika adhabu ya hasira ya Mungu katika ziwa la moto. Hivyo mwache aende peke yake huko yeye na mabalaamu wake, sisi tujitenge na yeye kwa kutubu leo na kushika amri za Mungu na Neno lake, kwa kujitenga na uasherati wote, wizi, rushwa, anasa, tamaa mbaya, wivu, matusi, na mambo yote machafu na kuzidi kujitakasa kila siku, na kuishi katika utakatifu ndipo tutakapojiepusha na ghadhabu ya Mungu na kupata baraka zote alizozikusudia katika Maisha yetu. Hatuna haja ya kuogopa wachawi wa vibuyu kwasababu huko waliko wanakiri kwamba hakuna uchawi wala uganga kwa waliokoka..

Sisi tupambane kujilinda na dhambi ndilo jukumu tulilolonalo sasa.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

NENO NI LILE LILE, LAKINI UJUMBE NI TOFAUTI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

JINA LA MUNGU NI LIPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UKADHANI YA KUWA MIMI NI KAMA WEWE.

Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima..

Kwanini mara nyingine tunakuwa ni wepesi kufanya dhambi, ni wepesi kuwasengenya majirani zetu, ni wepesi kwenda kuzini, licha ya kwamba tunasema tumeokoka, au tupo karibu na Mungu, lakini bado ni wepesi kutazama picha chafu mitandaoni na kufanya masturbation….

Ni kwasababu tunamdhania Mungu yeye ni kama sisi, kwamba anaelewa tu! Ni madhaifu ya kawaida ya mwili..Na kibaya Zaidi pale tunapoona Mungu hachukui hatua yoyote ya adhabu katika ouvu tulioufanya, pengine pale tulipoenda kutazama picha chafu mitandaoni halafu Mungu akakaa kimya, halafu kesho yake tena tukarudia jambo hilo hilo na bado akawa yupo vilevile, hakuna lolote baya amelifanya katika Maisha yetu, kesho kutwa tena tukaenda kuzini, jambo likawa vilevile, kanisani tunahudhuria, kwaya tunaimba, maombi tunafanya, wala hakuna shida yoyote, wiki ijayo tukaanza kuwazungumizia vibaya majirani zetu, tulikuwa hatuli rushwa wala hututoi rushwa lakini tulipoanza kula rushwa na tukaona hakuna jambo lolote baya lililotukuta basi ndio ikawa desturi yetu kufanya hivyo, licha ya kuwa unasema ni mkristo.

Imekuwa hivyo hivyo miaka nenda miaka rudi, unawaza moyoni na kusema “hata Mungu anaelewa mambo haya”, ndio maana haniadhibu kwa lolote, Unadhani yeye ni kama wewe, Unadhani anavyowaza juu ya maovu ni kama wewe unavyowaza, unamchukulia kama mtu mwenzako asiyeweza kujali mambo madogo madogo kama hayo, unadhani kuwa hawezi kukuacha, wala kukuadhibu kwa vitu kama hivyo..

Lakini leo sikiliza Neno la Mungu linavyosema..

Zaburi 50:16 “Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia, Una nini wewe kuitangaza sheria yangu, Na kuliweka agano langu kinywani mwako?

17 Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.

18 Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, Ukashirikiana na wazinzi.

19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako watunga hila.

20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.

21 NDIVYO ULIVYOFANYA, NAMI NIKANYAMAZA; UKADHANI YA KUWA MIMI NI KAMA WEWE. Walakini nitakukemea; Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.

22 Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane mwenye kuwaponya”

Angalia tena ule mstari wa 21 anasema.. “Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza; ukadhani ya kuwa mimi ni kama wewe”…Unaona, Mungu anapokaa kimya kutokana na dhambi zako unazozifanya kwa siri, usidhani yeye anakufurahia tu!.. Unasema umeokoka na huku unayo mambo yako ya siri ambayo unajua kabisa ni machukizo kwa Mungu, lakini Mungu hakusemeshi kwa lolote na wewe umestarehe tu, unadhani Mungu ni kama wewe, ataendelea na wewe hivyo siku zote..La! Anasema atakurarua na asipatikane mtu wa kukuponya..

Hasemi atakupiga tu, halafu basi au atakuadhibu, hapana anasema atakurarua..Na unajua anayerarua ni mnyama mkali kama vile simba, maana yake ni kuwa atakuharibu vibaya sana, kiasi cha kwamba hutaweza kusimama tena baada ya hapo, hata uombeweje, au uhubiriweje, hutaweza tena kusimama…Ndio maana anasema hapo “asipatikane mtu wa kukuponya”

Na ujumbe huo Mungu anausema kwa wale wote wanaomsahau..Inamaanisha kuwa hapo mwanzo walishawahi kuwa wake, lakini wakamzoelea wakamwona kama yeye ni kama wao, wakawa hawaogopi tena kufanya dhambi mbele zake..

Ndugu ikiwa wewe ni mmojawapo, Basi wakati wako wa kutubu kwa kumaanisha ndio huu, pengine umebakisha kipindi kifupi sana kukumbana na makucha hayo ya Mungu (Usitafute kuujua upande wa pili wa ghadhabu ya Mungu, kwasababu inatisha sana).. Ikiwa unafanya dhambi kisirisiri za kujirudia rudia ambazo hazimpendezi Mungu, na umekuwa ukizifanya kwa muda mrefu sasa na Mungu amekaa kimya tu, ni heri usiendelee kuzifanya, kwasababu kwa kukaa kwake kimya hivyo usidhani yeye ni kama wewe..

Hivyo chukua hatua sasa ya kuuimarisha wokovu wako, na Mungu atakusamehe na kuiahirisha ghadhabu yake kwako.

Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho, hakuna haja ya kuthibitishiwa tena kuwa tunaishi katika majira ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hali halisi yenyewe inaonekana kwa mambo yanayoendelea sasa hivi duniani, hivyo huu si wakati wa kuweka mguu mmoja kwa Kristo na mwingine nje, huu ni wakati wa kuzama moja kwa moja kwa Bwana, kwasababu UNYAKUO sasa ni wakati wowote.

2Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

 

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

KRISIMASI (CHRISTMAS) NI NINI? JE IPO KATIKA BIBLIA?

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

Rudi Nyumbani:

Print this post

PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA (2026)?

Pasaka ni nini kibiblia?, na je tunaruhusiwa kusheherekea pasaka sisi wakristo kama wayahudi?

Pasaka ni neno la Kiswahili ambalo limetokana na neno la kigiriki “pascha” ambalo tafsiri yake kwa lugha ya kiingereza ni “passover” kwa Kiswahili  ni “pita juu”. Hivyo pasaka kwa Kiswahili tunaweza kusema tafsiri yake ni “pita juu au vuka upite”.

Asili ya Neno hili ni siku ile wana wa Israeli walipokuwa wanatolewa kutoka Misri, usiku ule ambao ndio walikuwa wanatoka Misri, Bwana Mungu aliwaagiza wasitoke kwenye nyumba zao kwamba mpaka watakapomchinja yule Mwanakondoo na damu yake kuipaka katika miimo miwili ya Milango…ili wakati yule malaika ambaye alitumwa kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza wote wa wanadamu na wanyama waliokuwepo katika Misri nzima..atakapopita katika kila nyumba na kuiona damu hiyo ya mwanakondoo kwenye miimo ya mlango basi hataingia katika nyumba hiyo kumharibu mzaliwa wa kwanza wa nyumba hiyo “ATAVUKA JUU, AU ATAPITA JUU” Kuendelea na nyumba nyingine…na atakapofika katika nyumba nyingine na kukuta damu juu ya miimo ya mlango kama nyumba ya kwanza vile vile ATAPITA JUU na kuendelea mpaka atakapokuta nyumba ambazo hazina damu hiyo, ndipo ataingia na kuangamiza.

Kutoka 12:12 “Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi Bwana.

13 Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, NITAPITA JUU YENU, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu, nitakapoipiga nchi ya Misri”.

Hivyo hicho kitendo cha kuvuka na KUPITA JUU ndicho kinachoitwa Passover, kwa kigiriki Pascha, kwa Kiswahili PASAKA.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

pasaka ni nini

Sasa katika Agano jipya damu ya mwanakondoo yule ndio inayofanananishwa na damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, Sisi tuliokuwa dhambini tulipotolewa dhambini (yaani Misri yetu) na tunapoelekea nchi yetu ya ahadi mbinguni…Damu ya Yesu ndiyo iliyotuokoa na laana ya Mungu dhidi ya watu wote walio katika dhambi..Na damu ya Yesu ni ishara ya Agano kwamba kwa kupitia damu yake tunalindwa na hukumu ya Mungu..Hukumu ya Mungu inapoachiliwa au itakapoachiliwa tutakuwa tumefunikwa chini ya damu ya Yesu na Malaika yule wa hukumu ATAPITA JUU YETU, na tutanusurika na hukumu ya Mungu.

Swali ni Je tunaruhusiwa kusheherekea pasaka kama watu wengine?

Tafsiri ya kusheherekea kibiblia ni tofauti na tafsiri ya kusheherekea kama inavyotafsiriwa na ulimwengu. Tafsiri ya sherehe kwa ulimwengu ni kula, na kunywa na kulewa, na kwenda kujiburudisha, kujifurahisha, kufanya uasherati, kujisisimua na kufanya anasa na kufanya kila aina ya mambo ya kimwili.

Lakini kibiblia tafsiri ya kusheherekea sio hiyo…Hata wayahudi hawakusheherekea Pasaka kwa hivyo…Kibiblia, kusheherekea ni kujiweka katika ibada, na ibada sio kwenda kanisani tu..bali kujinyenyekeza na kujishusha chini ya uwepo wa Mungu, kwa kuomba, kusali, na kuzidi kujitakasa mbele zake huku tukikumbuka kuwa kwa tukio kama hili lililowahi kutokea miaka mingi iliyopita Bwana alitupa wokovu kwa kupitia damu yake pale Kalvari. Hivyo ni wakati wa kumwekea Bwana nadhiri,  wakati wa kuishiriki meza ya Bwana katika vigezo vya kimaandiko, ni wakati wa kusamehe Zaidi (sio kwamba sasa hatupaswi kusamehe mpaka siku ya pasaka ifike, hapana! tunasamehe kila siku, siku hiyo ikifika ni kumalizia tu kuvisafisha vile vidogo ambavyo tulikuwa hatujavimalizia), kwasababu utakatifu sio tu siku ya pasaka hapana bali kila siku!, siku hiyo ni kumalizia tu kuvisafisha vile vichache ambavyo vilikuwa vimesalia. Hivyo hiyo ndiyo tafsiri ya sherehe. Tukisheherekea kwa namna hiyo kuna amani fulani na furaha ya ajabu ambayo Mungu anaimimina ndani yetu..

Lakini tukisheherekea kidunia kwamba ndio siku ya kutafuta kwenda disko, ndio siku ya kwenda kulewa, ndio siku ya kuvaa nguo za nusu-uchi na kutembea nazo barabarani, kwamba ndio siku ya kwenda kwenye dansi,  n.k..Tutakuwa tumejitafutia laana badala ya Baraka..Tutakuwa tumeshirikiana na shetani asilimia mia kuudhihaki na kuuzalilisha msalaba wa Kristo, na damu yake ya thamani. Hivyo tutakuwa tumejiharibia wenyewe. Lakini tukisheherekea kibiblia tutapata baraka.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

(Pasaka ni nini)

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo

Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)

Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

Ijumaa kuu ni nini? Na kwanini iitwe kuu?

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

HAPANA MFUPA WAKE UTAKAOVUNJWA.

JE! UTATOA HESABU YA NINI KATIKA SIKU ILE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

SWALI: Nini maana ya  “Tusitweze unabii”?


JIBU: Tusome..

1Wathesalonike 5:19 “Msimzimishe Roho;

20 msitweze unabii;

21 jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;

22 jitengeni na ubaya wa kila namna”.

Maana ya neno “kutweza” ni kudharau au kupuuzia jambo fulani…Hivyo biblia inaposema msitweze unabii maana yake ni “msiudharau/msiupuuzie unabii”..Na unabii unaozungumziwa hapo ambao haupaswi kutwezwa (maana yake haupaswi kudharauliwa/kupuuziwa)..ni unabii wa kurudi kwa Bwana mara ya pili.. ambao Mtume Paulo aliwaonya Wakristo hao waliopo Thesalonike mwanzoni kabisa mwa sura hiyo ya tano(5). Tusome..

1 Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Huu ndio unabii wa kwanza ambao haupaswi kupuuziwa hata kidogo, na haukuandikwa kwa Wathesalonike tu peke yao, bali hata kwetu sisi, kwasababu ndio tunaoishi ukingoni mwa nyakati kabisa kuliko vizazi vyote vilivyotangulia. Ukisoma sura yote ya 5 hiyo ambayo ndio ya mwisho kabisa ya kitabu hicho cha 1Wathesalonike utaona jinsi biblia inavyotuonya kwa msisitizo mkubwa kujiweka tayari na siku hiyo ya kurudi kwa pili kwa Kristo, Kwamba siku hiyo inakuja kama mwivi na tusilale usingizi kama wengine walalavyo, na TUSIUUPUUZIE WALA KUUDHARAU HUO UNABII…Kwasababu ni kweli siku hiyo yaja na Mungu hawezi kusema uongo…wote wanaoudharau huo unabii siku hiyo itawajia kama mwivi na kutakuwa na maombolezo makubwa na majuto makubwa, watatamani warudishwe dakika tano nyuma warekebishe mambo yao, lakini itashindikana.

Na hautwezwi kwa midomo tu bali matendo pia…Mtu ambaye hajajiweka tayari kwa kumwamini Yesu Kristo na kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kuziacha, na kuishi kulingana na Neno la Mungu, ingawa kila siku anasikia injili lakini anapuuzia mtu huyo ANAUTWEZA UNABII, hali kadhalika mtu ambaye kila siku anasikia habari za kurudi kwa Kristo mara ya pili na anadhihaki na kudharau na kuwaona wanaomgoja Bwana ni watu waliorukwa na akili, na wanaopoteza muda wao, au wamepoteza dira ya Maisha, huyu naye anafanya dhambi hiyo hiyo ya kuutweza unabii ambapo siku moja atajuta majuto makuu na hatapata nafasi ya kurekebisha mambo yake, na mambo hayo yatakuwa hivi karibuni, moja ya hizi siku hii dunia itakuwa si dunia tena..

Vilevile Na unabii mwingine wowote wa kwenye biblia sio wa kuudharau kabisa, kwasababu kila alilolisema Bwana lazima litatimia.

Hivyo kama hujaokoka, saaa wokovu ni sasa, sio baadaye wala kesho..Tubu sasa na Kristo atakusamehe bure kama alivyoahidi.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MWACHE YESU, NDIO AWE WA  KWANZA KUKUHURUMIA.

Siku zote mwache Yesu, ndio awe wa  kwanza kukuhurumia!.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo.

Ni jambo la kawaida kila mmoja wetu kuijali kwanza hali yake binafsi, na si dhambi kufanya hivyo, japo hilo halitufanyi tuonekane kuwa wa maana sana mbele za Mungu.. Kuna wakati Bwana Yesu aliitisha mkutano mkubwa sana, pengine eneo la mjini lilikuwa ni dogo la kuuketisha umati mkubwa wa watu, au pengine palikuwa na usumbufu fulani ambao ungewafanya watu wasimsikilize vizuri, Hivyo akaamua kuwaitisha eneo la mbali kidogo na mji, mahali ambapo hapana makazi ya watu, eneo la nyika tupu,..mahali ambapo hakuwaandalia mahema ya kukutania wala hakuwachagulia penye miti mingi, ambapo walau wangekaa chini yake wapate uvuli, bali alichagua eneo la jangwa lenye nyika tupu.

Na mkutano huo ulikuwa ni Mkutano wa siku tatu..

Lakini biblia inatuambia wengi waliposikia habari ile wakatoka mbali sana, wakaenda eneo hilo la jangwa ili kwenda kuyasikiliza maneno ya uzima ya Bwana Yesu,..Watu wale walifikia pengine asubuhi sana na mapema, wakijua kuwa siku zote tatu zitakuwa ni siku za kufunga, za kumsikiliza tu Bwana Yesu si vinginevyo, hivyo walifika mahali pale wakilijua hilo asubuhi sana, wakakaa chini kwenye jua lile, kuanzia asubuhi mpaka jioni,..

Jaribu kutengeneza picha, masaa 12 ya mchana wanamsikiliza tu Bwana Yesu akiwafundisha, na usiku vivyo hivyo.. siku ya kwanza, siku ya pili, mpaka siku  tatu zinakwisha, wamekaa tu pale, nyikani wakimsikiliza Bwana Yesu kwa makini bila kuondoa miguu yao, huku njaa zikiwauma, lakini waliona kile wanachokisikiliza ni Zaidi ya chakula cha mwilini.. Walijua mtu hawezi kuishi kwa mkate tu, bali kwa kila Neno linalotoka katika kinywa cha Bwana..

Embu tengeneza tena picha Bwana alikuwa anajua kabisa watu wale, walikuwa katika hali ngumu kweli kweli katika eneo lile la ukame na jua kali, alijua kabisa walikuwa hawajala kwa muda wa masaa mengi sana, alijua kabisa hali zao zinakaribia kuwa mbaya..lakini aliendelea kuwafundisha bila kuwahudumia kwa lolote, kwasababu aliona utayari wao wa kumsikiliza yeye bila kuchoka, mpaka siku tatu kamili zilipokwisha..

Lakini siku ile alipomaliza kuwafundisha, biblia inatuambia Bwana Yesu hakuwaacha hivi hivi waondoke waende zao katika hali zile za njaa bali aliona umaskini wao, aliona njaa zao, aliona mateso yako, aliona kiu yao, aliona mahitaji yao na pale pale  maandiko yanatuambia AKAWAHURUMIA ..embu tusome:

Marko 8:1 “Katika siku zile, kwa vile ulivyokuwa mkuu tena ule mkutano, nao wamekosa kitu cha kula, akawaita wanafunzi wake, akawaambia,

2  NAWAHURUMIA MKUTANO kwa sababu yapata siku tatu wamekaa nami, wala hawana kitu cha kula;

3  nami nikiwaaga waende zao nyumbani kwao hali wanafunga, watazimia njiani; na baadhi yao wametoka mbali.

4  Wanafunzi wake wakamjibu, Je! Ataweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani?

5  Akawauliza, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba,

6  Akawaagiza mkutano waketi chini; akaitwaa ile mikate saba, akashukuru, akaimega, akawapa wanafunzi wake wawaandikie; wakawaandikia mkutano.

7  Walikuwa na visamaki vichache; akavibarikia, akasema wawaandikie na hivyo pia.

8 Wakala, wakashiba, wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba.

9  Na watu waliokula wapata elfu nne. Akawaaga”.

Unaona hapo?..Walipaswa waondoke vile vile, lakini kwa jinsi alivyoona “WAMEKAA NAYE” siku zote tatu bila kuondoka uweponi mwake, bila kwenda kuhangaika hangaika kuyajali maisha yao, familia zao, biashara zao, miradi yao, ili wapate chakula wao na Watoto wao, badala yake wamedumu pamoja naye kwa siku kadhaa bila kuchoka..basi tukio hilo lilimfanya Bwana Yesu AWAHURUMIE hata kwa yale mengine waliyoyakosa..

Na kama tunavyosoma kitu gani kilifuata.. Wote walishibishwa mikate wakiwa pale nyikani, wakapata na ya kuondokea, mpaka ikabaki na wale samaki vivyo hivyo…Sasa unaweza ukafikiri Bwana Yesu aliwashibisha pale tu…La! Alikuwa anawadhihirishia kuwa baada ya pale na Maisha yao pia yatabarikiwa kwa mfano ule ule wa vikapu, na wala hawatapungukiwa kabisa…Lakini hiyo yote ilikuwa ni kwasababu ya yale maneno ya uzima waliokuwa wanayasikia bila kuchoka ndio yakazaa vikapu vile vya mikate na baraka walizoziendea baada ya pale.

Na sisi tujiulize Je tunaweza kufikia hatua kama hii ya hawa watu?…Je tunaweza kuwa tayari kufunga kutokula kwa ajili tu ya kuutafuta uso wa Bwana kwa kipindi kirefu?, Je tunaweza Kufunga mihangaiko yetu, na shughuli zetu tukatenga wakati wa kuhudhuria ibada na semina ndefu za Neno la Mungu?..kwa kutokujali eneo lenyewe, kutokujali mazingira yanaruhusu kiasi gani, kutokujali umbali, kutokujali hata uzima wako na afya yako?.. Ikiwa tu tutaalikwa mahali ambapo tumewekewa mahema, chini kuna vivuli, lakini bado hatutakwenda ikiwa tunayo makanisa mazuri tena mengine yana feni lakini hatuwezi kukaa hata masaa 2, Je tutawezaje ikiwa tutalikwa mahali penye njika tupu kama pa hawa watu?..Na wakati huo huo bado tunataka Bwana Yesu azihurumie hali zetu,?

Mungu anatuambia tumkaribie yeye na yeye atatukaribia sisi (Yakobo  4:8)..Hivyo tukiwa hatupo tayari kujinyima nafsi zetu na kujitesa katika kuutafuta uso wa Mungu kwa bidii, katika kuutafuta ufalme wake na haki yake, basi tujue itakuwa shida sana kuyaona matendo makuu ya Mungu maishani mwetu.

Usikazane kutafuta kujihurumia kwanza wewe unapoutafuta uso wa Mungu, subiri kwanza mwache Yesu akuhurumie yeye..jukumu letu ni kuutafuta uso wa Mungu kwa bidii mengine tumuachie yeye, kwasababu anajua shida zetu, na mahitaji kabla hata sisi hatujamwambia. (Mathayo 6:32).

Bwana atusaidie katika hilo. Na atujalie tuchukue hatua zinazostahili katika hilo.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

MUNGU AKIKUPITA LEO, HAIMAANISHI KUWA HAJAKUCHAGUA.

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

Rudi Nyumbani:

Print this post