Ikimbie dhambi.
Shalom.
Karibu tujifunze biblia, na kujikumbusha yale ambayo tumeshajifunza. Kitu pekee ambacho watu wa Mungu tunapaswa tukiogope kuliko vyote kwa nyakati zetu hizi sasa ni dhambi…Wala hatupaswi kuogopa mapepo wala wachawi wala shetani mwenyewe. Tunachopaswa kukiogopa cha kwanza ni dhambi.
Kwasababu dhambi ndio mlango wa mambo hayo mengine yote.
Hivyo kwa nguvu zote na kwa jitihada zote tunapaswa tujiepushe na dhambi..Na tunajiepusha na dhambi kwa kuikimbia dhambi..maana yake unaiacha kwa gharama zozote zile..Roho Mtakatifu biblia inamwita MSAIDIZI, (Yohana 14:16), unaelewa maana ya msaidizi?..Msaidizi ni mtu anayekusaidia wewe kufanya jambo Fulani ambalo tayari umeshachukua hatua ya kulifanya…yeye sio mfanyaji..bali ni mwongezeaji nguvu kile ambacho umeshaanza kukifanya…
Hivyo tunapookoka na kumpokea Roho Mtakatifu ndani yetu…kazi yake sio KUTUZUIA KWA NGUVU TUSIFANYE DHAMBI!..Hapana hiyo sio kazi yake hata kidogo…Kazi yake ni kutusaidia namna ya kuishinda dhambi!..anatupa mashauri, anatupa kila sababu kwanini sasa hatupaswi kufanya jambo hili baya na tufanye hili jema..Hivyo tunapomtii mashauri yake ndani yetu ile kiu ya kufanya dhambi inakufa ghafla, ndipo hapo tunajikuta tunakaa bila kutenda dhambi. Na kwa jinsi unavyozidi kujizoeza kumtii ndani yako ndivyo zile dhambi zinazidi kufa ndani yako. Ni kawaida kitu usipokifanyia mazoezi muda mrefu unakisahau na unapoteza uzoefu wa hicho kitu (kitendo cha kupoteza uzoefu wa kile ulichokuwa unakifanya ndio kufa katika hicho kitu)…kadhalika unapopoteza uzoefu katika kutenda dhambi ambazo ulikuwa unazitenda hapo kwanza, unapomtii Roho Mtakatifu ndani yako..ule uzoefu unapungua na hatimaye unaisha kabisa na unakuwa UMEKUFA KWA HABARI YA DHAMBI!…Unakuwa hata iweje huwezi kufanya uasherati, huwezi kutukana, huwezi kuiba, huwezi kula rushwa, huwezi kumchukia mtu n.k
Sasa tatizo kubwa linalokuja kwa wengi wetu ni kutoelewa kazi ya Roho Mtakatifu ndani yetu, na hivyo tunadhani Roho anapokuja ndani yetu kama dikteta, ambaye ataziharibu na kutuzia kwa nguvu tusifanye dhambi. Na kutokana na watu kufikiria hivyo wanajikuta wanapopokea Roho na kujiachia ndipo wanajikuta wanashindwa na dhambi na hivyo kuendelea na maisha ya dhambi..na kujiuliza wengine wanawezaje na wao wanashindwa.
Nataka nikuambie ukishaamua kumfuata Bwana Yesu kwa kutubu dhambi zako, ambazo Roho kakushuhudia ndani yako kwamba umepotea kwa hizo na hivyo uziache..Hatua inayofuata baada ya hapo ni kumtii. Na humtii kwa kusema maneno tu mdomoni kwamba “NIMEKUTII BWANA”. Hapana huo ni mwanzo tu wa kutii..Unapaswa umtii kwa VITENDO. Maana yake ni kwamba kama ulikuwa unafanya dhambi Fulani UNAIACHA kwa lazima!…Hutafuti ushauri kwa yeyote Yule, unaiacha kwa kutumia akili zako zote, nguvu zako zote, na roho yako yote. Wala hapo huhitaji kuombewa..
Kwamfano tuchukue mfano mmoja namna ya kuiacha dhambi ya uasherati kisha tutahitimisha. Dhambi ya uasherati ambayo ndani yake inajumuisha uzinzi, ulawiti, ufiraji, na usagaji na hata utazamaji wa picha cha ngono na kujichua, na masturbation…Dhambi hii haimtoki mtu kwa Kuombewa!!..Usimfuate mtumishi wa Mungu na kumwambia niombee niache dhambi hii au dhambi ile..Hakuna maombi ya namna hiyo!..Nakuambia hivyo kwasababu na sisi wengine tulikuwa namna hiyo hiyo..tukadhani kuombewa ndio suluhisho..tukafunga muda mrefu na kujiombea na hakuna kilichobadilika ndani yetu, mpaka tulipoyasoma maandiko, tukaifahamu kweli nayo hiyo kweli ikatuweka huru. Hivyo ndugu mpendwa usipoteze muda kufanya utafiti ambao tayari umeshasaidiwa kuufanya utazunguka na kuzunguka na mwisho wa siku utarudi pale pale.
Suluhisho la kuacha dhambi ya uasherati ni KUUKIMBIA!..Kuukimbia maana yake ni kuondoka bila HIARI ya huo uasherati. Maana yake ni kwamba kama ulikuwa unaishi na mwanamke/mwanamume ambaye mnafanya naye uasherati ni KUMKIMBIA GHAFLA! Na Kukata mazoea!…Akikutafuta kwenye simu mwambie mara moja tu kwamba umeokoka na hivyo tunapaswa tutubu kwa yote tuliyokuwa tunayatenda na kumrudia Mungu. Ukiona hakuelewi wewe jiokoe nafsi yako usitazame nyuma wala usiwe na huruma, usipokee simu zake, …Usianze kushauriana naye huku bado mnakutana kutana na kuzungumza zungumza, akikutafuta kwenye simu usijibu meseji yake hata moja, hata akilia kwa machozi ya damu kwamba mrudiane usiwe na huruma jiokoe nafsi yako na yake, kwa kuukimbia uasherati ikiwezekana block hiyo namba …Usizungumze naye hata kidogo. Mfano wa Yusufu. Mke wa Potifa alimtamani na Yusufu baada ya kulijua hilo, aliacha kuongea na mke wa Potifa..
Mwanzo 39:10 “Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, wala aongee naye”.
Utasemaje unataka kuacha uzinzi na bado unaongea na unajibu meseji za watu unaozini nao?..utasemaje unataka kuacha uasherati na huku unamazoea zoea na wanawake wa mtaani na wanaume wa mtaani?, na huku bado unafuatilia vitamthilia na vi-movie vya kipepo vyenye maudhui ya kizinzi ndani yake kwenye Tv yako vinavyochochea uzinzi tu na wala si kitu kingine?..utasemaje unataka kuacha kutazama picha za ngono na huku kwenye simu yako bado zipo?, bado umejiunga whatsapp na facebook makundi ya mambo hayo?, utasemaje unatamani kuacha pombe na wakati kuna chupa za bia ndani mwako, na bado unakula meza moja na kampani zako za walevi?. Na dhambi nyingine zote ni hivyo hivyo…dawa ya kuziacha ni KUZIKIMBIA!!…Ondoka! Dhambi nyingine ili uweze kuziepuka zinakugharimu kuhama hata hapo ulipo, hama hata mtaa..hamia mwingine..Hizo ndio gharama za kuacha dhambi!..Hizo ndizo gharama za kumtii Roho Mtakatifu.
Usipotaka kuzikimbia namna hiyo na kutafuta kuombewa, au kuwekewa mikono, kirahisi rahisi tu hivyo…Utajikuta unaombewa na kila mtu na hata kuwekewa maroho mengine mabaya hata kuliko hayo uliyonayo sasa. Hali yako kila siku itazidi kuwa mbaya kwasababu umekosa maarifa ya kutosha!.
Ndugu umeyasikia/umeyasoma haya..hutasema siku ile hukuambiwa…kama hutamtii Roho Mtakatifu leo, basi yeye mwenyewe atahakikisha anakusaidia kuyatimiza maazimio yako..lakini pia kama hutatii uamuzi ni wako. Lakini natumaini utatii, na Bwana akusaidie. Hivyo kama hujaokoka au kama wewe ni vuguvugu, upo hatarini kutapikwa hivyo kabla hujatapikwa hebu fanya mageuzi haraka..Mtii leo Roho Mtakatifu kwa kuacha dhambi kwa Lazima.. baada ya kuziacha, nenda katafute ubatizo sahihi wa kuzama mwili wote katika maji na kwa jina la Bwana Yesu kulingana na Matendo 2:38, na Yule Roho Mtakatifu ambaye aliishaianza kazi njema moyoni mwako atakusaidia kufanya yale ambayo peke yako ilikuwa ni ngumu kuyatimiza, na dhambi kwako itakuwa sio kitu kigumu kukishinda kwasababu Nira ya Kristo siku zote ni laini na utapata furaha, na amani isiyoelezeka, na utaona siku zote ulikuwa wapi kuingia ndani ya Kristo…kwa raha utakayoipata na furaha..wala dhambi haitakuwa ni kitu kinachokusisimua hata kidogo.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?
Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?
TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.
KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.
NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.
MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.
SWALI: Chapa zake Yesu ni nini? Kama tunavyosoma katika Wagalatia 6:17?
JIBU:
Wagalatia 6:17 “Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.”
Kuna mambo machache ya kuzingatia hapo. 1) jambo la kwanza ni chapa 2) mahali Inapochukuliwa.
Chapa ni alama..Chochote kilichopigwa chapa maana yake kimewekwa alama inayokitambulisha kitu hicho kuwa ni milki ya kitu kingine. Kila bidhaa inayouzwa lazima ina chapa ya kampuni husika, au anayeizalisha. Sasa katika mstari huu Mtume Paulo anasema “tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.”..Maana yake ni kwamba “anachukua alama za Yesu katika mwili wake”..zingatia hilo Neno “mwilini mwake”..maana yake alama alizokuwa nazo Yesu na yeye anazichukua..kama uthibitisho wa kuwa milki ya Yesu.
Sasa kwanini Mtume Paulo alizungumza Sentensi hiyo kwamba TANGU SASA MTU ASINITAABISHE?
Ukianza kusoma kuanzia juu kidogo mstari wa 12 wa kitabu hicho cha Wagalatia utaona kuwa Mtume Paulo alikuwa anawazungumzia wayahudi ambao walikuwa wanawafundisha watu kuwa KUTAHIRIWA ndio uthibitisho au alama ya ki-Mungu…Kwamba alama au chapa pekee katika mwili ya kuonyesha kwamba wewe ni mtu wa Mungu ni KUWA UMETAHIRIWA, kama hujatahiriwa basi wewe huna chapa ya kiMungu au alama ya kiMungu. Hivyo wakawa wanawahubiria watu wengi mafundisho hayo potofu na hivyo kuwataabisha watu wengi hususani watu wa Mataifa. Sasa Paulo ndio akawa analisahihisha hilo na kusema, watu hao nia yao ni kutafuta kuona fahari au kupata wafuasi juu ya watu ambao watatahiriwa, lakini mioyoni mwao hata hawana mpango na Mungu..Na hapo ndio Paulo akasema mpaka sasa “tangu sasa mtu asinitaabishe kwa maana ninachukua katika mwili wangu chapa zake Kristo”..maana yake alama za Kristo kama uthibitisho wa kuwa Mkristo..
Sasa alama katika mwili wa Yesu ni zipi?..si nyingine Zaidi ya zile za Mateso, makovu ya misumari katika mwili wake, makovu ya viboko katika mgongo wake, uso uliotemewa mate, msalaba juu ya mwili wake n.k. Hizo ndizo alama au chapa za Yesu. Na hapa Mtume Paulo anasema naye pia anazichukua katika mwili wake…maana yake hizo ndizo zitakazomthibitisha kwamba yeye ni milki ya Yesu. Na sio KUTAHIRIWA.
Ndio maana utaona Paulo alijikana nafsi katika viwango vikubwa sana. Kama Bwana Yesu alivyochapwa viboko vingi, Paulo naye alichapwa idadi ya viboko 39 mara 5..
2Wakorintho 11:23 “Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.
24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.
25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;
26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;
27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi”.
2Wakorintho 4:8 “Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa;
9 twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi;
10 siku zote twachukua katika mwili kuuawa kwake Yesu, ILI UZIMA WA YESU NAO UDHIHIRISHWE KATIKA MIILI YETU.
11 Kwa maana sisi tulio hai, siku zote twatolewa tufe kwa ajili ya Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu ipatikanayo na mauti”
Hizo ndizo chapa za Yesu ambazo Mtume Paulo na mitume wengine walizozichukua katika miili yao. Hawakujisifia kutahiriwa kama wayahudi, wala hawakujisifia mavazi marefu na meupe katika miili yao kama alama ya kuwa watu wa Mungu, wala vyakula bali mateso katika Imani ndio iliyokuwa alama yao kuwa wao ni watu wa Mungu.
Je ni wao tu waliopaswa kuzichukua chapa za Yesu katika miili yao au pia ni kwa watu wote?
Jibu ni kwamba kila mtu aliyeokoka ni lazima azitwae chapa hizi..wengi hatupendi kusikia hivi kwasababu tunafikiri Ukristo ni kupata tu raha na burudani katika haya Maisha…Bwana Yesu alisema mtu yoyote akitaka kunifuata sharti ajitwike msalaba wake na ajikane nafsi yake ndipo amfuate…Maana yake huo msalaba atakaojitwika ndio utakaompeleka msalabani… msalaba alioubeba Bwana ulimpeleka kufa pale Kalvari kifo cha mateso…wewe na mimi ni misalaba gani tunayoibeba ambayo mwisho wa siku itatupekea kuifia Imani, au kuteswa kwa ajili ya Imani?..Misalaba unayovaa shingoni ni urembo tu.
Soma maandiko machache yafuatayo..ambayo yatakusaidia kujua kuwa Ni wajibu wetu wote kubeba chapa zake Yesu katika miili yetu..
Wafilipi 1:29 “Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake; 30 mkiwa na mashindano yale yale mliyoyaona kwangu, na kusikia kwamba ninayo hata sasa.”
1Wathesalonike 3: 3 “mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo”.
Warumi 5: 3 “Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;”
2Wathesalonike 1:4 “Hata na sisi wenyewe twaona fahari juu yenu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya saburi yenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na dhiki mnazostahimili.
5 Ndiyo ishara hasa ya hukumu iliyo haki ya Mungu, ili mhesabiwe kuwa mwastahili kuuingia ufalme wa Mungu, ambao kwa ajili yake mnateswa”
Je umebeba msalaba wako na kumfuata Yesu?..kumbuka kubeba msalaba sio kuvaa mkufu wa msalaba shingoni bali ni kuukataa ulimwengu kama Yesu, kuishikilia Imani bila kuangalia ni nani anakubaliana na wewe au hakualiani na wewe…Kwa ufupi kama tukio lile lile lililotokea kwa Bwana nasi pia linapaswa lijirudie katika Maisha yetu.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.
WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.
UKADHANI YA KUWA MIMI NI KAMA WEWE.
MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.
NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.
Kwanini Ibrahimu analitaja jina la YEHOVA wakati Musa anasema hakujifunua kwa jina hilo kwao?
Shalom, Naomba kufahamu kitendo cha kupiga miayo mara kwa mara hususani wakati wa maombi, Je! Ishara ya kuwa na mapepo au nguvu za giza?.
JIBU: Kwa namna ya kawaida kupiga miayo ni ishara ya mambo mawili makuu katika mwili, 1) Ya kwanza ni njaa, 2) Ya pili ni usingizi.
Hivyo tukirudi katika masuala ya maombi mkristo hapaswi kufikiria kuwa kupiga miayo ni kitendo cha mapepo au nguvu za giza, hapana bali ni mwitikio wa mwili wake mwenyewe, ukimwambia kuwa huu sasa ni wakati wa kwenda kupumzika umechoka, sio wakati wa kusali..Na ndio maana utagundua ni wakati tu wa kusali, au wa kusikiliza Neno watu ndio wanasikia uchovu wa hali ya juu, lakini wakitoka hapo hiyo hali inapotea yenyewe, utajiuliza ni kwa nini?
Ni kwasababu Biblia inatufundisha kuwa mwili ni adui wa mambo ya rohoni sikuzote, wakati roho yako ipo tayari hata kuzama muda mrefu kwenye maombi mwili wako utaanza kutoa sababu nyingi, mara umechoka, unapaswa ukapumzike, utakuletea mpaka hivyo viashiria vya miayo mingi, ili tu kukuthibitishia, na tena kama utakuwa unafikiria chakula muda wa maombi ndio kabisa utakuletea mpaka miayo ya njaa, mpaka utatetemeka wakati ni muda mfupi tu nyuma hapo ulitoka kula.
Wagalatia 5:17 “Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka’’.
Hivyo, hali kama hiyo ikikujia, hupaswi kukemea mapepo, bali ni wakati kushindana na mwili wako mpaka ukutii wenyewe, na habari njema ni kuwa kwa jinsi utakavyozidi kuzama katika maombi, ndivyo hiyo hali itakavyokuwa inatoweka yenyewe ndani yako kidogo kidogo, mpaka mwishoni utajikuta unaweza kwenda muda mrefu mpaka utajiuliza ule usingizi mwanzoni ulitokea wapi.
Kwahiyo njia rahisi ni kuhakikisha wakati unaposali, peleka mawazo yako yote na fikra zako zote kwenye maombi na sio katika mambo mengine, ndivyo utakavyoweza kuushinda mwili kirahisi, na kama ni usiku unasali toka katika mazingira ya kitanda.
Mwisho, fahamu kuwa kama mkristo huwezi kuishi bila maombi.
Kwahiyo shindana na mwili wako mpaka uushinde, vinginevyo hutadumu muda mrefu katika imani au kama utaendelea kuwepo basi ujue maisha yako yatakuwa ni ya majaribu kila kukicha ambayo yangeweza kuepukika tu kwa maombi..
Mathayo 26:41 “ Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?
Mathayo 7:6 “Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua”.
Maneno hayo yalizungumzwa na Bwana wetu Yesu. Akifunua kuwa sio kila neno/kitukinawafaa baadhi ya watu. Hivyo tuwe na hekima tunapotoa au tunaposema vitu vyetu vilivyo vya thamani mbele za watu, kwasababu unaweza ukasema kitu ukadhani kitakuwa na manufaa kwa yule unayemwambia badala yake kitu kile kikageuka kuwa matatizo kwako.
Tutajifunza mfano mmoja muhimu katika biblia kisha kupitia huo tutapata kuelewa Zaidi kiini cha somo letu.
Wakati Mungu anamtokea Musa na kuzungumza naye kwa mara ya kwanza katika kile kijiti kilichokuwa kinawaka moto lakini hakiteketei…Alimwambia maneno haya..
Kutoka 3:6 “Mimi ni Mungu wa baba yako Ibrahimu, Isaka na Yakobo….
7 Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
10 Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.”
Baada ya Mungu kumwambia maneno haya ya ahadi na ya Faraja..alimwambia akawaambie habari hizo wana wa Israeli…Kwamba wamejiliwa na wanakwenda kutolewa katika nchi ya Misri ya utumwa na kupelekwa nchi ya Ahadi. Hivyo Musa akaenda kuwaambia wana wa Israeli habari hizo nao wakafurahi.
Lakini jambo la kipekee ni kwamba Mungu alipomwambia Musa aende kwa Farao…alimwambia amwambie Farao maneno mengine tofauti na hayo…Tusome..
Kutoka 3:16 “Enenda, ukawakusanye wazee wa Israeli pamoja, ukawaambie, Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenitokea, akaniambia, Hakika nimewajilieni, tena nimeyaona mnayotendewa huko Misri;
17 Nami nimesema, Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali.
18 Nao watakusikia sauti yako; nawe utakwenda, wewe na wazee wa Israeli kwa mfalme wa Misri, na kumwambia, BWANA MUNGU WA WAEBRANIA, AMEKUTANA NASI; BASI SASA TWAKUOMBA, TUPE RUHUSA TWENDE MWENDO SIKU TATU JANGWANI, ILI TUMTOLEE DHABIHU BWANA MUNGU WETU.
19 Nami najua ya kuwa huyo mfalme wa Misri hatawapa ruhusa mwende zenu, la, hata kwa mkono wa nguvu”.
Sasa unaweza kujiuliza kwanini Mungu hakumwambia Musa amwambie Farao kwamba “Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo nimeona mateso ya watu wangu jinsi gani unavyowatumikisha hivyo wape ruhusa waondoke waende nchi ya ahadi niliyowaahidia?”…Badala yake Mungu hakumruhusu Musa kumwambia Farao habari zozote kuhusu Ibrahimu, wala kuhusu mahali wanapokwenda..badala yake ni kama Mungu alimdanganya Farao kwamba wanakwenda tu kumtolea Mungu dhabihu jangwani kisha watarudi…kumbe ndio walikuwa wanakweda kutokomea huko.
Hivyo Farao akadanganyika akajua kuwa wana wa Israeli wanataka tu kwenda kumtolea Mungu wao dhabihu jangwani siku tatu na kisha watarudi kumbe nyuma yake kulikuwa na mpango mwingine wa wana wa Israeli kutokomea huko huko na kutokurudi tena…
Sasa japokuwa Farao alikuwa anajua ni kitendo tu cha kwenda na kurudi lakini alikuwa mgumu vile hebu tafakari laiti angejua kuwa wale watu ndio wamepanga wanaondoka kabisa kabisa hali ingekuwaje?..bila shaka vingeamka tena vita vingine visivyokuwa na maana.
Sasa Kwanini Mungu alifanya vile?, Ni kwasababu aliwazuilia wana wa Israeli wasitupe lulu zao mbele za nguruwe wasije wakazikanyaga mbele ya miguu yao na kugeuka na kuwararua.
Hivyo wana wa Israeli mpaka wanaondoka Misri…Farao alikuwa anajua kuwa ni wanakwenda tu na kurudi.. Hebu tusome mistari kadhaa kulithibitisha hilo..
Kutoka 5:2 “Farao akasema, Bwana ni nani, hata niisikilize sauti yake, na kuwapa Israeli ruhusa waende zao? Mimi simjui Bwana, wala sitawapa Israeli ruhusa waende zao.
3 Wakasema, Mungu wa Waebrania amekutana nasi; twakuomba, tupe ruhusa twende safari ya siku tatu jangwani, tumtolee dhabihu Bwana, Mungu wetu; asije akatupiga kwa tauni, au kwa upanga”.
Soma tena..
Kutoka 8:25 “Farao akawaita Musa na Haruni akawaambia, Endeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu ndani ya nchi hii.
26 Musa akasema, Haitupasi kufanya hivyo; kwa kuwa tutamchinjia sadaka Bwana, Mungu wetu, na hayo machukizo ya Wamisri; je! Tutachinja sadaka ya hayo machukizo ya Wamisri mbele ya macho yao, wasitupige kwa mawe?
27 La, tutakwenda safari ya siku tatu jangwani, tumchinjie dhabihu Bwana, Mungu wetu, kama atakavyotuagiza.
28 Farao akasema, Mimi nitawapa ruhusa mwende, ili mmchinjie dhabihu Bwana, Mungu wenu, jangwani; lakini hamtakwenda mbali sana; haya niombeeni”.
Umeona hapo Farao anawaambia “lakini hamtakwenda mbali sana”…maana yake alikuwa anafikiri kwamba watarudi baada ya kutoka kule…na sehemu nyingine utaona Farao anawaambia waende tu huko jangwani watu walio wazee lakini Watoto wabaki na mifugo (soma kutoka 10:24)…Hivyo ikabakia kuwa siri ya Musa na wana wa Israeli kwamba siku yao ya kutoka Misri kikabisa kabisa imefika…Farao na waMisri hawakuijua hiyo siri, walidhani wanakwenda tu jangwani watarudi baada ya siku chache watakapomaliza kutoa sadaka zao hizo, watarudi na kuendelea kuwatumikisha.
Farao alikuja kushtuka kuwa kalaghaiwa na wale watu, wamekimbia na hawana mpango wa kurudi tena siku alipokuja kupata taarifa kuwa wale watu hawaelekea ile njia ya jangwa bali waligeuka na kurudi kuikabili bahari…Ndipo alipoelewa kuwa wamefanya makosa makubwa kuwaachilia waondoke.. Tusome
Kutoka 14:5 “Mfalme wa Misri aliambiwa ya kuwa wale watu WAMEKWISHA KIMBIA; na moyo wa Farao, na mioyo ya watumishi wake, iligeuzwa iwe kinyume cha hao watu, nao wakasema, Ni nini jambo hili tulilotenda, kwa kuwaacha Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?”
Ndugu katika safari ya wokovu… si kila kitu kizuri Bwana anachokuambia ni cha kwenda kuwaambia watu kama kilivyo…Bwana amekuahidia au amekupa ufunuo fulani wa jambo lako zuri linalokuja mbele usikurupuke na kwenda kusimulia simulia huku na huko…kwa kufanya hivyo utakuwa umempa adui nafasi na mlango mzuri wa kuyaharibu maono yako uliyopewa..
Hali kadhalika Bwana anapokutoa leo katika ulimwengu(yaani katika dhambi)…ambao inafananishwa na Misri yetu…sio kila kitu ambacho Mungu kakufunulia ni cha kukieleza mbele za watu wa kidunia…Unatakiwa uondoke katika dhambi kwa njama kama hizo za wana wa Israeli..
Kwamfano Ulikuwa unauza Bar…na majirani zako wanauza bar kama wewe, sasa umempokea Yesu na Roho Mtakatifu amekushuhudia ndani yako kwamba, biashara hiyo ni ya utumwa wa dhambi na itakupeleka kuzimu…sasa wewe anza kuifunga hiyo haraka sio lazima uwaambie wale wanaokuzunguka sababu ya kuifunga, wewe jiponye nafsi yako kwanza huo sio wakati wa kuanza kuwahubiria….baada ya kuifunga na kuhakikisha marago yako yote umeyatoa Misri, ndipo uwaambie mimi nimeokoka na hiyo kazi siirudii tena….lakini ukiwahi kuwaambia kwamba nimeokoka na Kesho au Kesho kutwa nitaifunga hiyo Bar, au nitaacha hii kazi ya kujiuza, au nitaacha haya madili haramu tunayoyafanya, au nitaacha uvaaji wa nguo hizi na vimini hivi, au nitaacha dansi..ukianza kumwambia huyo mpenzi wako unayefanya naye uasherati kwamba sasa umeokoka hivyo kuanzia Kesho nakuacha…nataka nikuambie kwamba utakuwa umejiweka kupitia vita visivyokuwa na lazima…mwache kwanza huyo unayefanya naye uzinzi, ikiwezekana mtoroke baadaye akikuuliza kwanini umeondoka bila kuniambia mwambie ni kwasababu nimeokoka na siwezi tena kuishi Maisha ya uasherati…lakini ukimwambia huku bado upo naye nyumba moja….nakwambia shetani atakupelekesha kweli kweli na unaweza kujikuta huwezi kumwacha wala kuuacha ulimwengu….Utapitia vita visivyokuwa na sababu..
Vita vinatakiwa vianze baada ya wewe kuondoka katika ulimwengu..Ulimwengu unatakiwa ujue kwamba wewe umeokoka baada ya kuondoa marago yako yote ulimwenguni na sio wakati ambao wewe bado upo katika ulimwengu…kama vile wana wa Israeli walivyoondoa majeshi yao ndipo Farao akabutuka na kujua kuwa wale watu hawakwenda safari ya kwenda na kurudi..bali walipanga kupotelea moja kwa moja..ndipo akapanga majeshi kumfuatilia.
Hivyo kama hujaokoka leo? Huu ndio wakati wako sasa..Tubu mpokee Yesu, kutubu maana yake ni kugeuka na kuacha yale uliyokuwa unafanya mwanzo…na njia ni hiyo hiyo, fungasha marago yako yote na kimbia kimya kimpya!…usitoe taarifa kamili kwanini utatoka mpaka utakapotoka Misri…Toka Misri leo kwa njama zozote zile uwezazo…Toka kwenye ulevi, toka kwenye ulimwengu wa starehe za kidunia,miziki, toka kwenye huo mtandao wa wala rushwa, wizi, , utapeli, usengenyaji, uasherati, ulawiti,ufisadi…
Kwa mwanzo igiza hata unaumwa ili wakupe ruhusa utoke katika kampuni yao hiyo ya bia..na baadaye wakikuuliza mbona hurudi waambie mimi nimeokoka na huko sirudi tena..Igiza hata unakwenda kusalimia nyumbani ili tu huyo mtu unayeishi naye ambaye mnafanya naye uasherati akupe ruhusa uondoke na huko akiona hurudi akikuuliza vipi mwambie nimeokoka huku huku na Maisha hayo siyaishi tena. Jiponye nafsi yako kwa gharama zozote…
Dunia inapita na mambo yake yote..Bwana Yesu alisema itakufaidia nini upate ulimwengu mzima na upate hasara ya nafsi yako?…Ikimaanisha kuwa nafsi ni kitu cha kulinda kuliko kitu kingine chochote…hivyo kwa gharama zozote na njama zozote jiokoe nafsi yako na huu ulimwengu.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Ni sahihi kwa mkristo kufikiria hivi?..
Jaribu kufikiria mfano huu..
Mtu mmoja alitamani sana kujua afya ya mwili wake, hivyo akakusudia kweli kwenda hospitali kupima afya yake kama ameathirika na Ukimwi au La, Hivyo akafanikiwa kwenda kuonana na daktari akachukuliwa vipimo vyote, Lakini alipomaliza kuchukuliwa tu vipimo akaondoka zake akarudi nyumbani kwake, daktari alipomaliza uchunguzi wake wa vipimo akarudi sasa ili ampe majibu yake, na kumpa ushauri nasaha lakini alipofika hakumwona..
Sasa akiwa kule nyumbani, siku zikapita, miezi ikapita, miaka ukapita, akawa anaishi Maisha ya furaha na ya amani kabisa, siku moja watu wakamuuliza vipi kuhusu afya yako, tunatumai sasa ipo njema kwasababu siku ile tayari ulishakwenda kuonana na Daktari..
Ndipo yeye akajibu, ndio! Natumai itakuwa ni njema!..Watu waliposikia vile wakashangaa kwa jibu lile, unatamai vipi tena? Wakati ulishapata uhakika kwa Daktari,..Lakini yeye akawajibu, ndio nilishaonana na daktari akanichukua vipimo vyote, ila majibu anayo yeye mwenyewe, mimi sijui kingine Zaidi ya hapo, Hivyo yeye Mungu ndiye anayejua kuwa mimi ni muathirika au La!. Hilo ni jukumu lake kama daktari, mimi sihitaji kujua sana kwasababu mimi sio daktari..
Fikiria mtu kama huyo wale watu walimwonaje? Ni Dhahiri kuwa watasema huyu atakuwa amerukwa na akili, alikwenda hospitali kufanya nini sasa kama hakupata majibu ya afya yake, ambayo yangempa uhakika wa afya yake kuwa ni njema au la!.
Na ndivyo ilivyo hata leo kwa mtu ambaye hajapata bado uhakika wa wokovu wake..Watu wengi ukiwauliza Je! Umeokoka watasema ndio, nilishaokoka zamani sana, mpaka nikabatizwa,..Ukizidi tena kuwauliza, sawa Je unaouhakika hata ukifa leo au Yesu Kristo akirudi leo utakwenda naye mbinguni.. hapo ndipo watakapokuambia ninatumai hivyo, wengine watakuambia hilo ni Mungu ndio analolijua..mimi siwezi kujua hukumu zake, na mwingine atakwambia,nikisema hivyo nitakuwa ninajihesabia haki, na kujiona mimi ni kitu fulani mbele za Mungu..wakati bado sijafika lolote linaweza kutokea.
Ndugu Neno WOKOVU ni Neno lenye msingi wa UHAKIKA chini yake, mfano huwezi kusema umeokolewa kwenye moto, na huku bado unajihisi kama upo bado mule mule motoni, vinginevyo hiyo itakuwa ni ndoto tu au bumbuazi fulani limekushika, lakini mfano ukiokolewa kutoka motoni na mtu fulani, utajiona kabisa jinsi unavyohama kutoka ulipokuwepo kwenye mateso na kwenda sehemu nyingine salama..Hivyo ni jambo la uhakika..
Na ndio maana biblia inaweka wazi kabisa kwa kutuambia…
2Wakorintho 13:5 “Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa”
Unaona, ukiwa mkristo huendi tu ilimradi, huwi tu kama mshabiki fulani, bali kila hatua inajipima je! Mpaka sasa Kristo yupo pamoja nami au La!, Na je ikitokea leo hii safari yangu ya Maisha imekwisha ghafla Je nitakuwa upande wa haki au hukumu?
Sasa, swali unaloweza kujiuliza ni Je utaupataje Uhakika huo wa wokovu ndani yako?
Unapaswa uangalie mambo mawili la kwanza Ni Je! Tangu uliposema umeokoka, kuna badiliko lolote lililotokea ndani yako?..Je yale matunda ya Roho yamezalika ndani yako?
Sawasawa na Wagalatia 5:22 inayosema..
“Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
Hivyo kama hayo yapo ndani yako, basi hiyo ni hatua ya kwanza ya kukupa uhakika ndani yako.
Na jambo la pili, Je! Tangu ulipoubeba msalaba wako na kumfuata Kristo, Je! Ulipitia vipingamizi vyovyote katika hilo?..Kupitia majaribu sio sifa kwamba ni jambo jema, lakini shetani hawezi kukuangalia umeacha rushwa, akakuvumilia, umeacha ulevi na kuuza pombe kwenye biashara yako akakuangalia tu, umeacha kampani za marafiki wabaya na disko asikuletee udhia, umeacha ulimwengu kwa ujumla wake na mambo yake yote asikuletee dhihaka, umekatisha ghafla yale madili haramu uliyokuwa umepanga wewe na wenzako kwenda kuyafanya shetani akabaki anakutazama tu!..Umekatisha hayo mahusiano ya kiasherati ghafla anakutazama tu…wakati mwingine utapitia kupigwa au kutengwa, n.k. Sasa kama haya hayakuonekana ndani yako basi uhakika huo kuupata ni ngumu, Kristo na mitume wake waliyapitia hayo, vilevile na wewe utakumbana nayo kwa sehemu fulani katika safari yako ya wokovu.
Sasa Ikiwa hayo mambo mawili makuu yameonekana ndani yako, basi uhakika wenyewe wa kama upo katika njia sahihi ya wokovu utatokea wenyewe ndani yako, wala hautahitaji kuulizia bali Roho Mtakatifu mwenyewe atakushuhudia kuwa wewe ni mwana wa Mungu na umeokoka..
Sawasawa na Warumi 8:16 “Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;
Hivyo ndugu, kama bado mpaka sasa hujapata uhakika huo, Ujue tu, mbinguni hutakwenda haijalishi utasema niliongozwa sala ya toba, au nilibatizwa, au nilikuwa ninahudhuria kwenye maombi..Hutakwenda kwasababu suala la wokovu sio suala la kubahatisha au kuhisi hisi tu bali ni uhakika Mungu anaompa mtu akiwa bado hapa hapa duniani..Na kuwa na uhakika wa kwenda mbinguni sio kujihesabia haki..
Biblia inasema…
2Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”.
Ukisoma kwenye tafsiri nyingine hususani zile za kiingereza(kjv) Hilo Neno “jitahidini zaidi kufanya imara” linasema hivi..
“brethren, give diligence to make your calling and election sure…”
Neno SURE, linaamisha uhakika, maana yake ujitahidi kuufanya kuitwa kwako na uteule wako uwe wa uhakika..
Hivyo na wewe pia hujachelewa, ndani ya kipindi hichi kifupi cha maisha yako uliyobakiwa nayo hapa duniani, na kabla Bwana hajarudi, anza kuuthibitisha tena wokovu wako, kusudia kweli kuanzia leo kumfuata Kristo, anza kuzaa hayo matunda ya Roho, na kuwa tayari kuubeba msalaba wako..Na Bwana mwenyewe atauweka uhakika huo ndani yako. Nawe utaishi Maisha ya amani kila siku, ambapo hata wimbi lolote likisimama mbele yako, hata bunduki ikiwekwa mbele yako, huna wasiwasi kwasababu unajua ukifa tayari moja kwa moja utakuwa mbinguni kwa Baba.
Bwana akubariki sana.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Mkaribie Bwana.
Shalom, karibu tujifunze Neno la Mungu..
Miongoni mwa watu waliokuwa wanamfuata Bwana Yesu kulikuwa na makundi manne..1) Makutano 2)Wanafunzi 3)Mitume 12 na 4) Nguzo.
Kundi la kwanza ambalo ni makutano, hawa walikuwa tu wanakusanyika kusikiliza mahubiri ya Bwana Yesu ambao mara zote Bwana alikuwa anazungumza nao kwa mifano, na kuwaponya magonjwa yao..baada ya hapo walikuwa wanarejea katika shughuli zao na maisha yao ya kawaida.
Kundi la pili ambalo lilikuwa ni la wanafunzi wa Yesu, hawa walikuwa wapo kama 70 hivi au zaidi kidogo..Kundi hili ni lile ambalo lilikuwa linamfuata Bwana Yesu lakini si kila mahali…Ni baadhi ya watu ambao waliamua kujitoa kumtumikia Yesu sehemu zote alizokuwa anakwenda…na hawa pia Bwana alikuwa anawatuma kuhubiri injili kila mahali ambapo Bwana alipokuwa anataka kwenda. (Soma Luka 10:1).
Kundi la tatu lilikuwa ni Mitume…Mitume hawa walikuwa 12 tu, na waliteuliwa na Bwana Yesu kati ya lile kundi la wanafunzi 70 waliokuwa wanamfuata Yesu.
Luka 6: 13 “Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume”
Kundi la mitume ndio lilikuwa linamkaribia sana Bwana kuliko wale wanafunzi 70 na makutano..Hawa kila mahali Bwana alipokuwa na wao walikuwepo, walikula nae na kunywa naye…na mbele za Bwana ni kama vile walipendelewa zaidi kuliko wanafunzi wengine kwasababu kila mfano ambao Bwana aliokuwa anawafundisha makutano usioeleweka wao ndio walikuwa wanapata fursa ya kwenda kumwuliza akiwa peke yake, maana ya mifano hiyo, nafasi ambayo makutano wala wale wanafunzi wengine hawakuipata.
Lakini lilikuwepo kundi la mwisho ambalo ni la kipekee sana..ambalo hilo lilikuwa karibu sana na Bwana zaidi ya makundi hayo matatu yaliyotangulia…na kundi hilo lilitwaliwa kutoka miongoni mwa wale wanafunzi 12…Na hao walikuwa watatu tu ambao ni (Petro, Yohana na Yakobo)..Hawa watatu walijulikana kama NGUZO.
Wagalatia 2:9 “tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; YAKOBO, na KEFA na YOHANA, WENYE SIFA KUWA NI NGUZO, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;”
Kefa ni jina lingine la Petro(soma Yohana 1:42). Hawa watatu walijulikana kama nguzo…Maana yake walikuwa wanauhusiano wa kipekee na Bwana zaidi ya mitume wote, zaidi ya wanafunzi wote na zaidi ya makutano yote.
Utaona hawa watatu kila mahali ambapo Bwana alitaka kwenda peke yake (labda mlimani kusali, au kuwafunulia siri za ndani sana) aliwachukua hawa watatu tu Yohana, Yakobo na Petro, na si mitume wengine waliosalia..Hebu tuangalie mifano michache kulithibitisha hili..
Luka 9:27 “Nami nawaambia kweli, Wapo katika hawa wanaosimama hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata wauone kwanza ufalme wa Mungu.
28 Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa PETRO NA YOHANA NA YAKOBO, AKAPANDA MLIMANI ILI KUOMBA.
29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.
30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni Musa na Eliya”
Unaona hapo walikuwepo mitume wote lakini Yesu aliwachagua tu hao watatu kwenda nao mlimani..kusali na huko akawafunulia ufunuo mkubwa namna ile, na wakaisikia sauti ya Mungu ikisema huyu ni mwanangu mteule wangu, msikieni Yeye. Ufunuo huo waliouona tu hawa watatu, na Bwana aliwaambia wasimwambie mtu mwingine yoyote mpaka atakapofufuka katika wafu. Maana yake ni kwamba wanafunzi hawa walikuwa na siri nyingi ambazo Bwana aliwafunulia ambazo mitume wengine hawakuzijua.
Tutazame mfano mwingine tena..
Mathayo 26:36 “Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe.
37 Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka.
38 Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami.
39 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.
40 Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?”
Hapo utaona Bwana alitenga makundi mawili..kundi la kwanza ambalo ndilo lile la mitume 9 aliliacha kule kwenye bustani ya Gethsemane….hakuenda nalo kuomba usiku ule, badala yake akawachukua Petro, na wale wana wawili wa Zebedayo ambao ni (Yohana na Yakobo), hao ndio akaenda nao kusali..na hao ndio aliowaambia wakeshe waombe pamoja na yeye wasije wakaingia majaribuni..kwasababu shetani ndio aliokuwa anawawinda zaidi kwasababu walikuwa na Bwana zaidi..Na kama wewe ni msomaji wa biblia utagundua kuwa wakiwa kule waliona tena ishara nyingine wakati Yesu akiwa anaomba jasho lake lilikuwa kama matone ya damu, na pia waliona malaika wakija kumtia nguvu…
mambo hayo mitume wengine waliosalia hawakuyaona…
Na hawa watatu, hata wakati wa Pentekoste na kuendelea ndio mitume Bwana alitembea nao kwa viwango vikubwa sana..mpaka watu wote wakawaita kuwa ni NGUZO YA KANISA. Kitabu cha Ufunuo wa Yohana, ambacho kimebeba siri nyingi za ufunuo wa siku za mwisho, na ujio wa Bwana Yesu kimendikwa na Yohana huyu…ambaye ndiye mmoja wao wa wale watatu.
Sasa kwanini wanafunzi hawa watatu waliteuliwa na Bwana kuwa karibu zaidi na yeye kuliko wengine wote?
Jibu ni kwamba, kwasababu walimpenda Bwana zaidi..Mungu hana upendeleo hata kidogo..kila dakika, kila muda walikuwa wanamtafakari Bwana, wanamfikiria yeye, wanamtumikia yeye, na wamejikana nafsi na kusema lolote liwalo tutamfuata Yesu Bwana wetu popote aendapo, kwa moyo huo Bwana akawapenda zaidi na hivyo kuwakaribisha wamsogelee zaidi kuliko wengine…Kama ni mwanafunzi wa Biblia utamjua Petro alivyokuwa anampenda Bwana…ilifika wakati akamwambia Bwana wajapochukizwa wote kwaajili yako mimi sitachukizwa..ijapokuwa alikuwa ni dhaifu lakini angalau hata alikuwa anaujasiri wa kusema hivyo tofauti na wengine…
Hali kadhalika Yohana na Yakobo ni hivyo hivyo,..walimpenda Bwana mpaka ikafikia wakati wakamwendea Bwana wao na kumwomba katika ufalme wake waketi mmoja mkono wake wa kuume na mwingine wa kushoto…(walimpenda Bwana mno na hivyo Bwana akawapenda zaidi). Yohana ilifika wakati akawa anaegemea kifuani mwa Yesu kila mahali…na ilifika kipindi Bwana akawaambia wazi wazi kuwa mmoja wao atamsaliti..na kila mmoja akawa anawasiwasi ni nani amtajaye..na Bwana akamfunulia Yohana peke yake kwamba ni Yuda kwa sauti ya chini, wengine hawakusikia.. kwasababu alikuwa karibu sana na yeye kifuani mwake…
Yohana 13:23 “Na palikuwapo mmoja wa wanafunzi wake, ameegama kifuani pa Yesu, ambaye Yesu alimpenda.
24 Basi Simoni Petro akampungia mkono, akamwambia, Uliza, ni nani amtajaye?
25 Basi yeye, hali akimwelekea Yesu kifua chake, akamwambia, Bwana, ni nani?
26 Basi Yesu akajibu, Ndiye mtu yule nitakayemtowelea tonge na kumpa. Akatowelea tonge, akalitwaa akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote”.
Tabia ya hawa watatu kuwa tayari chochote Bwana alichowaambia ndizo zilizowafanya kuwa karibu zaidi na Bwana kuliko wengine, Bwana alipotaka kwenda kuomba walikuwa tayari kutaka na wao kwenda kuomba..walikuwa hawaonyeshi dalili za uvuvi ingawa walikuwa na madhaifu, walijinyima kila kitu ili tu wampendeze Yesu.
Vivyo hivyo Neno la Mungu linasema..Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.
Unapojikana nafsi na kumpenda Mungu zaidi, na kumfanya yeye ndio wakwanza kila mahali, hapo ndipo unapojitengenezea daraja zuri la Mungu kukukaribia zaidi..ndipo unapoongeza daraja zuri la Mungu kukupenda zaidi ya wengine, kukufunulia siri nyingi zaidi ya wengine…kukutumia na kukubariki. Unapoutafa uso wa Mungu kwa kusali, kufunga, kutenda mema zaidi ya wengine..mema yako yanapimwa mbele za Mungu kila siku na yanapoonekana yamezidi ya wengine wengi ndipo na wewe thamani yako inapanda mbele za Mungu, lakini kama leo ukiambiwa tu usali..hata dakika mbili humalizi, kusoma tu neno ni mara moja kwa wiki, na hata ukisoma unasoma tu mistari na sio mada nzima..hapo utafanyikaje NGUZO mbele za Mungu.?
Hivyo tusiridhike na uhusiano wetu na Mungu..Tuzidi kumkaribia Bwana..kutoka kuwa wanafunzi wake, hata mitume wake hata Nguzo..
Ufunuo 3: 12 “Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa NGUZO katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya”.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Maran atha!
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Shalom, karibu tujifunza Neno la Mungu..
Matendo 13:46 “Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa milele, angalieni, twawageukia Mataifa.
47 Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, Upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.
48 Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini.
49 Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote”.
Ni jambo la kuogopesha kusikia kuwa wapo watu waliokusidiwa uzima wa milele, na wapo ambao hawajakusudiwa uzima wa milele. Na hilo linatupa picha kuwa suala la wokovu sio jambo la kubabaisha bali ni mpango wa Mungu mkamilifu ambao ulishapangwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu..alishakuwa na Idadi kamili ya watakaokolewa na akawaandika katika kitabu chake cha uzima..
Ufunuo 17:8 “ Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama…”
soma pia Waefeso 1:4
Na ndio maana Bwana Yesu alisema..
Yohana 6:44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.
Ikimaanisha kuwa tendo la kumwamini tu Kristo na kumfuata kwa uaminifu wote sio jambo la mtu tu kujiamulia, bali ni jambo ambalo Mungu alishalipanga kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu na hivyo akamchagua mtu huyo, kisha akamwekea mwiitikio huo ndani yake na ndio maana akamwamini na kumfuata bila kigugumizi chochote..
Na ndio maana hata wakati mwingine utamwona yupo ambaye kazaliwa katika ukristo, kalelewa katika mambo ya imani maisha yake yote, amekuwa akihudhuria kanisani miaka mingi na kwenye mikutano mbali mbali lakini bado suala la wokovu lisiwe ni jambo la muhimu sana katika maisha yake..Lakini wakati huo huo, utaona tena mtu mwingine ambaye amezaliwa katika mazingira yasiyomjua Mungu, au pengine muislamu, au mbudha hajui vizuri masuala ya wokovu, lakini siku moja akasikia tu mahali Fulani Kristo anahubiriwa, na muda huo huo akachomwa moyo, akaacha kila kitu na kumfuata Yesu kwa kutokujali kuwa ndugu zake watamchukuliaje..
Sasa Hapo unajiuliza inakuwaje?..Ni kwasababu yeye alikusudiwa uzima wa milele, na huyu mwingine hakukusudiwa.
Angalia tena sehemu nyingine biblia inasema..
2Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu”.
SASA UTAJITAMBUAJE KUWA WEWE NI MMOJA WA WALE WALIOKUSUDIWA UZIMA WA MILELE, AU LA..
Kama tulivyosoma hapo juu anasema wote walioakusudiwa uzima wa milele WALIAMINI..Unaona? Waliamini kile walichohubiriwa wakati ule ule, maana yake wakaenda kubatizwa, wakadumu katika imani, na utakatifu, wakawa kila siku wanalitendea kazi lile Neno walilokuwa wanafundishwa na mitume..
Lakini wale wengine ambao hawakukusudiwa ambao walikuwa wanajiona wao ni watu wa dini, watu waliozaliwa katika imani hao ndio Mungu aliowakataa, matokeo yake wakabaki vile vile,..Na ndivyo ilivyo hata leo, Ukiona umeshahubiriwa injili, miaka nenda rudi, lakini ndani yako hakuna badiliko lolote, au wokovu unauchukulia kama jambo lisilokuwa la maana sana kwako, fahamu kuwa wewe hujakusudiwa uzima wa milele..Kwasababu ungekuwa umesudiwa uzima wa milele, usingepambana au kushindana na habari njema za Yesu Kristo, pale unapoambiwa utubu dhambi.
Biblia inasema njia ile ni nyembamba iendayo uzimani,..Pengine Ni Mungu anasema na wewe leo, ili umgeukie, pengine wewe ni mmojawapo wa waliokusudiwa uzima wa milele, na ndio maana unasikia Roho Mtakatifu akiugua ndani yako..Basi kubali wito huo haraka na kumpokea Yesu kwa moyo wako wote siku ya leo, ili uwe mmojawapo wa wale ambao majina yao yalishaandikwa katika kitabu cha uzima kabla hata ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu.
Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo hii, Kumkabidhi Yesu Kristo maisha yako.
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako ili kuukamilisha wokovu wako.
Ubarikiwe sana
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?
MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.
UCHAWI WA BALAAMU.
YULE JOKA WA ZAMANI.
KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
Basi tuendelee kumjua mungu, naye atatujilia kama mvua ya vuli.
Ndugu, mmoja aliniuliza, akasema, Ni faida gani unapata katika kumtumikia Mungu?..Nikamwambia ni nyingi tu, akasema mimi niliokoka tangu zamani, na niliamua kweli kumfuata Mungu, mpaka ikafika hatua ya mke wangu kunikimbia kutokana na hali yangu, nikawa ninamwomba Mungu sana, ninafunga, ninahudhuria semina mbalimbali, ninahudhuria maombi ya mikesha sana tena sana, nikawa ninamwomba Mungu anikumbuke katika hali yangu ya kiuchumi, lakini kwa jinsi nilivyozidi kuendelea ndivyo mambo yangu yalivyozidi kuwa mabaya,..
Ndugu huyu Kwa jinsi alivyokuwa anaongea na mimi alikuwa anaonyesha kuwa tayari ameshakata tama na ameshaachana na wokovu..Mwisho kabisa akaniambia “Huoni kuwa kuna tatizo fulani na huyu Mungu tunayemtumikia”?
Neno hilo lilinishtua kidogo, nikamwambia kwangu mimi sijaona tatizo lolote katika kumtumikia, sijajua uhusiano wako na Mungu upoje kwa upande wako, Nikamwambia Daudi alisema katika biblia kuwa yeye tangu ujana wake mpaka amekuwa mzee hajawahi kuona mwenye haki ameachwa na Mungu…
Nilipomwambia vile nikisubiri anijibu, Yule mtu hakunijibu tena akaondoka..
Ndugu yangu, lipo jambo ambalo sisi kama wakristo tulioamaaisha kweli kumfuata Mungu tunapaswa tulijue Daudi japokuwa alizungumza maneno hayo, lakini haikumaanisha kuwa ni muda wote na wakati wote mambo yalikuwa yanakwenda kama alivyotaka.. Zipo nyakati nyingi alimwona Mungu kama amemwacha, Kama alikuwa hamsikii, au haoni shida zake anazozipitia dhidi ya hali yake na maadui zake lakini alijipa moyo akisema, Bwana yupo pamoja nami,gongo lake na fimbo yake vyanifariji na alizidi kujipa moyo kumshukuru na kumsifu Mungu..akijua kuwa hata katika mateso yake Mungu hawezi kumwacha.
Sikiliza maneno haya ya Daudi..
Zaburi 13:1 “Ee Bwana, hata lini utanisahau, hata milele? Hata lini utanificha uso wako?
2 Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Hata lini adui yangu atukuke juu yangu?
3 Ee Bwana, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.
4 Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.
5 Nami nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.
6 Naam, nimwimbie Bwana, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu”.
Zaburi 42:9 “Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?
10 Watesi wangu hunitukana mithili ya kuniponda mifupa yangu, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako?”
Unaona, upo wakati aliomba lakini haoni majibu, alitamani lakini hakupata, alikuwa akihuzunika akikumbuka kuna wakati alimpiga Goliathi, na wafilisti wote wakawa wanamuogopa lakini wakati mwingine haoni msaada wowote mpaka anaenda kuomba hifadhi kwa hao hao wafilisti ambao walikuwa adui zake, walau wampe eneo la kuipumzisha nafsi yake..mpaka unafika wakati tena wafilisti wanakwenda kupigana na ndugu zake Wayahudi na yeye pia anataka kujumuika nao ili tu awaridhishe wafilisti wasimwone kuwa ni msaliti..Wengi wetu hatujui kuwa Daudi tunayemsoma kuna wakati alilikimbia taifa lake na kwenda kutafuta msaada kwa wafilisti (maadui wa Israeli)..
Sasa kwa namna ya kawaida ungeweza kusema Daudi alishaachwa na Mungu tangu zamani, kuna tatizo na huyo Mungu anayemtukia,..Lakini pamoja na mateso hayo yote alizidi kuzishilia ahadi za Mungu, akimshukuru yeye, na kumwimbia siku zote..Mpaka wakati ulipofika wa yeye kustareheshwa ulipofika, na kufanywa mfalme wa Israeli nzima, mpaka leo hii tunamsoma Daudi kama mtu aliyeupendezesha moyo wa Mungu, haikuwa safari rahisi, ya kudhani kuwa kila alichokiomba kilikuwa kinakuja kwa ghafla tu..
Baadaye Daudi anakuja kusema..
Zaburi 66:19 “Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu.
20 Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake”.
Hata na sisi wakati huu, Bwana Yesu alituambia, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtaona, bisheni nanyi mtafunguliwa, hakumaanisha kuwa tuombapo yatakuja wakati huo huo kwa ghafla, inaweza pia ikawa hivyo lakini si wakati wote,..Ni kuamini, na kungoja na kuwa na saburi…Na ndio maana Bwana wetu huyo huyo sehemu nyingine alisema maneno haya..
Luka Luka 18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.
2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.
3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.
4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,
5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.
6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.
7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?
8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”
Unaona, maandiko hayo yanatuonyesha kabisa, kuombwa kwetu kunapaswa kusiwe kwa kukata tamaa kama vile kulivyokuwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo na kwa Daudi. Kwasababu ni uhakika kwamba mwisho wa siku tutajibiwa, iwe isiwe, majibu yatakuja tu kama tulivyomwomba, kwasababu Mungu ni mvumilivu kwetu. Na anatuhurumia na anapendezwa na dua zetu.
Hivyo wewe uliyemfuata Kristo kwa moyo wako wote, nataka nikuambie usikatishwe tamaa, kuona hakuna dalili yoyote leo, majira yako yatafika, nawe utasema kama Daudi “Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu”.
Zidi tu kuonyesha bidii kumtafuta yeye leo ,wacha kuangalia hali yako ya sasa..Wakati wa kukujilia kama mvua ya vuli utafika kama hautautupa utakatifu wako na wokovu wako.
Hosea 6:3 “Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini [HAKIKA] kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi”.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.
https://wingulamashahidi.org/mafundisho-ya-ndoa/
SAA YA KUHARIBIWA IIJIAYO ULIMWENGU WOTE.
KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.
KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.
UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.
SWALI: Hujambo mpendwa,naomba nieleweshwe hili tafadhali katika mwanzo 22:14 utaona Ibrahimu alipaita mahali pale YEHOVA-YIRE ambapo alimtoa yule kondoo kuwa sadaka, badala ya Isaka, lakini ukisoma tena katika Kutoka 6:2-3 Mungu anamwambia Musa kwamba hakuwai kujidhihirisha kama YEHOVA kwa Ibrahimu ,Isaka, na Yakobo, bali Mungu mwenyezi. Je! Biblia inajipinga? Asante sana.
JIBU: Kumbuka vitabu vitano vya mwanzo vimeandika na mtu mmoja ambaye ni MUSA (Ambavyo ni Mwanzo, kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na kumbukumbu la Torati ).. Na kama tunavyojua Musa aliviandika vitabu hivi alipokuwa jangwani (yaani akiwa njiani kuelekea nchi ya Ahadi).. Na katika kitabu cha Mwanzo ambacho ndicho tunapata huko habari za Ibrahimu…wakati anaziandika habari hizo akiwa jangwani tayari alikuwa ameshafunuliwa jina hilo jipya la Mungu yaana YEHOVA. Hivyo mahali popote ambapo alisoma habari za Ibrahimu, akimtaja Mungu kwa jina lolote lile yeye Musa ni lazima angeliandika kwa jina YEHOVA, kadhalika mahali popote ambapo Nuhu angemtaja Mungu kwa jina lolote lile yeye Musa angesahihisha katika maandishi yake na kuandika jina YEHOVA badala yake..na hivyo hivyo kwa Lutu, Yakobo, Isaka, Yusufu na wengineo.
Sasa utauliza mbona kila mahali katika vitabu hivyo vitano vya kwanza vya Musa kila mahali Mungu katajwa kama BWANA, na si hilo YEHOVA ??
Kumbuka Katika biblia yetu ya Kiswahili na ya kiingereza na ya lugha nyingine zote…kila mahali ambapo leo hii tunapasoma pameandikwa neno BWANA, Kwa asili hapakupaswa paandikwe hivyo…Sehemu nyingi katika agano la lake unapopaona pameandikwa neno BWANA, kwa asili pangepaswa paandikwe neno YEHOVA. Musa nyingi alizitafsiri kama Yehova..kwa mfano katika
Mwanzo 2:7 biblia inasema
“ Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”…Mstari huu Musa aliuandika hivi “Yehova Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai ”
Lakini sasa watafsiri wa kwanza biblia waliona ili kuliheshimu zaidi hilo jina la Mungu si vyema kuandika jina hilo Tukufu na kuu kama lilivyo…Hivyo kwa hekima ya Roho ndipo likawekwa jina BWANA badala ya YEHOVA..Kitu ambacho ni kizuri!..kama tu vile isivyo hekima wala heshima kumwita mzazi wako jina lake halisi na badala yake unamwita jina lake la cheo “BABA”..huwezi kusema shikamoo Joseph badala yake utasema shikamoo Baba. Hivyo si dhambi kumwita Mungu BWANA kama inavyochukuliwa leo na ndugu zetu mashahidi wa Yehova wakidhani kuwa kumuita Mungu BWANA ni kumvunjia heshima..
Biblia zote, pale kwenye utangulizi, zimechapishwa na angalizo hilo pale mwanzoni kabisa.. Kuwa BWANA lilimaanisha YEHOVA.
Kwahiyo kitabu cha Mwanzo kimetaja Yehova na kitabu cha Kutoka kwasababu mwandishi ni huyo huyo mmoja, na aliviandika vitabu hivyo akiwa tayari ameshalijua jina la Mungu kamilifu yaani Yehova.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?
KWANINI BWANA YESU ALISULUBIWA NA WEZI WAWILI?
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.
13 Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.
14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.
15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.
16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.
17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama JUU YA MCHANGA WA BAHARI”.
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, kama ukisoma mistari iliyotangulia kabla ya hiyo, utaona kuwa shetani kuna majira alijaribu kufanya vita katika mbingu, lakini alishindwa kama biblia inavyotuambia akatupwa chini na mahali pake hapakuonekana tena mbinguni kuanzia huo wakati.
Lakini biblia inatuambia pia alipotupwa, hakukaa katika eneo la nchi peke yake, au hakwenda baharini moja kwa moja , hapana, bali alikwenda kusimama juu ya mchanga wa bahari….Kwa namna nyingine alikwenda kusimama ufukweni mahali ambapo nchi na bahari vinakutana.
Shetani alifahamu kuwa, hivyo ndivyo vitu viwili vinavyoikamilisha dunia, hakuegemea tu upande mmoja afanye makao yake huo hapana..badala yake alisimama pale ufukweni ili aweze kuyaona na kuyatawala yale yanayotoka katika nchi na yale yanayotoka katika bahari. Na ndio maana baada ya pale biblia inasema “Ole wa nchi na bahari”, Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu..
Unaona? haituambii nchi tu peke yake, au bahari peke yake, hapana bali vyote viwili, kwasababu ndipo alipopania kuwanasa wanadamu.
SASA NCHI NA BAHARI KIBIBLIA VINAWAKILISHA NINI?
BAHARI: au sehemu yenye maji mengi, biblia imeshatupa majibu yake,.Tusome.
Ufunuo 17:15 “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha”.
Kumbe maji yanawakilisha jamaa, na makutano na mataifa na lugha…Yaani kwa ufupi watu wengi.
Vilevile, tunaweza kuona jambo lingine, pale Bwana Yesu alipochagua mitume wake, wengi wao aliwachagua kutoka katikakati ya wavuvi, akifunua kuwa watakuja kufanya kazi ya uvuvi wa watu wengi, yaani jamaa, na mataifa la Lugha, kama alivyomwambia Petro na Andrea katika (Mathayo 4:19)..
Hivyo Bahari inawakalisha watu wengi, kwahiyo shetani tangu alipoona ameshindwa hawezi tena kupigana yeye kama yeye aliamua sasa kuelekeza macho yake katikati ya watu ili apate nguvu, na chombo kikubwa anachokitumia ili kupata ufuasi mkubwa wa watu ni kupitia kitu kinachoitwa DINI, penye dini ndipo palipo na watu wengi, sio katika siasa au makabila..
Hivyo mpaka sasa yupo katika kilele cha kuzikutanisha dini zote na madhehebu yake yote ambayo tangu zamani yalishautupilia mbali uongozo wa Roho Mtakatifu na kufuata mapokeo yao ya kibinadamu, ili zikubaliane katika kitu kimoja.
Na ndio maana ukisoma ile sura inayofuata ya 13, utaona Yule joka aliposimama tu pale kwenye mchanga wa bahari, wakati huo huo wanyama wawili walitokea, mmoja alitokea baharini, na mwingine akatokea nchi kavu (Soma ufunuo sura ya 13 yote utaona)..Sasa Yule aliyetokea habarini ndiyo huyu atakayepata nguvu ya kuwa na wafuasi wengi sana duniani kwa kupitia dini…
NCHI: NI Hifadhi ya kimwili, tangu mwanzo, Mungu alipomuumba Adamu alimpa ardhi ailime na kuitunza kwasababu huko ndipo alipomchipulia chakula chake kitakachomfanya aishi hapa duniani.
Ayubu 28:5 “Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula;…”..
Hata sasa chakula na utajiri vipo katika ardhi..Hivyo kwa lugha ya sasa nchi tunaweza kusema inawakilisha Uchumi,..Fedha, biashara, hazina, vitu vinavyoweza kumpatia mwanadamu Rizki ili aishi hapa duniani n.k…
Kwahiyo shetani kuona hivyo, alisimama pia katika eneo hilo.. tangu huo wakati akajikita kudhibiti mihimili hiyo miwili mikuu, Watu, na uchumi.. nchi na bahari..
Kwanza Ili awapate Watu anatumia kivuli cha dini, ambapo hivi karibu anaenda kutimiza adhma yake ya kuzileta dini zote zilizopoteza uongozo wa Roho Mtakatifu pamoja, zikiongozwa na ile dini mama ya Rumi, na cha ajabu biblia inatuambia watu wote na mataifa yote ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu wataufurahia huo utawala na mfumo mzima wa ibilisi ..
Na sasa ili kuwalazimisha watu wote waufuate huo mfumo wa mpinga-Kristo, shetani atamnyanyua mnyama mwingine ambaye atakuwa na nguvu ya kiuchumi sana,(taifa kubwa) ambalo hilo litayahimiza mataifa mengine yote yapokee maagizo kutoka kwa huo umoja wa dini duniani, na mtu yoyote atakayekataa kuupokea hataruhusiwa kununua wala kuuza, wala kufanya biashara yoyote, wala kuajiriwa mahali popote.. Unaona Jinsi hali itakavyokuwa mbaya.. Ni nani atapona hapo.
Haya ni mambo ambayo tunaweza kuyashuhudia siku za hivi karibuni wala tusidhani bado miaka mingi, jaribu kufikiria jinsi ugonjwa huu wa Corona ulivyozuka tu ghafla, na athari yake ndogo tu inawafanya watu wasiweze kutembea hata nje katika baadhi ya nchi, na imetokea tu ndani ya kipindi kifupi cha miezi mitatu tu, hakuna ambaye angeamini kuwa dunia ingeweza kuwa namna hii, dunia ambayo inashamra shamra za kila namna..Lakini mambo yamekuwa hivyo barabara zipo wazi..Hata matajiri na wana wa wafalme, na watu mashuhuri na fedha zao haziwasaidii wakati huu. Ndivyo mambo yatakavyobadilika ghafla tu wakati huo ukifika.
Shetani ameshajidhatiti vya kutosha, na ghafla tu, dini zote zitafikia muafaka mmoja zikiongozwa na dini ile mama ya Rumi, watafikia muafaka mmoja, watapata sapoti kutoka katika kila pembe ya dunia, watakuwa na kiongozi wao mmoja ambaye ndio atakuwa mpinga-Kristo..Huyo ataishawishi dunia iwe na ustaarabu mpya, Lakini lengo lake ni kuihimiza ile chapa ya mnyama ili awanase wanadamu wote.. Sasa kwa kuwa yeye amejikita katika masuala ya kiimani sana, kama tulivyosema atapata msaada mwingine kutoka katika taifa lenye nguvu ya kiuchumi duniani, ili kuyalazimisha mataifa mengine yote yamtii yeye kwa shuruti.
Mpaka wakati huo umefika ujue unyakuo tayari umeshapita ndugu yangu, sijui utakula nini wewe unayemkataa Yesu leo, wewe ambaye utakuwepo ulimwenguni wakati huo, pona yako itakuwa ni kufia njaa ndani, kama utakuwa hujakamatwa na kuuliwa kwa mateso yasiyokuwa ya kawaida.. Hakuna mtu yoyote atayevumiliwa na mtu au chombo chochote cha dola ambaye ataonekana hajapokea chapa hiyo ya mnyama.. usifikiri utapona..Ni ngumu sana ndugu, usidhani akaunti yako ya benki itakusaidia wakati huo, hilo jambo halitakuwepo, usidhani utakimbilia mafichoni, ondoa hayo mawazo, usidhani elimu yako itakusaidia kupata ajira wakati huo, acha kufikiria hivyo..Chapa utaipokea tu.
Hizi ni nyakati za hatari tunazoishi, ole wa nchi na bahari!…Kimbilio pekee ni Kristo tu saa hii..Ikiwa upo bado nje ya Kristo, basi fanya uamuzi wa Busara leo hii, tubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, omba toba kwa Mungu, nenda kabatizwe ikiwa bado hujafanya hivyo. huu ni wakati sasa wa kuamka usingizini.
Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini”.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
UFUNUO: Mlango wa 13
UCHAWI WA BALAAMU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
DANIELI: Mlango wa 7
MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?
Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko miaka elfu”?