Title 2020

Siku ya uovu ndio siku gani hiyo?

SWALI: ‘Siku ya uovu’  inayozungumziwa katika Waefeso 6:13 Ni ipi? Waefeso 6:13 “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.


JIBU: Ikiwa umedumu katika wokovu kwa muda mrefu utaelewa, si wakati wote mambo yatakwenda sawa kama unavyotaka wewe,

 Bwana Yesu aliweka wazi kabisa juu ya suala hilo..akasema..

Mathayo 18:7 “Ole ni wa ulimwengu kwa sababu ya mambo ya kukosesha! Maana hayana budi kuja mambo ya kukosesha…

Unaona anasema, hayana budi kuja..Hiyo haijalishi wewe ni mtakatifu au la!. Si wakati wote shetani atakuwa anakuangalia ukiufurahia wokovu wako kwa kwa amani na utulivu, kuna wakati atapanga mashambulizi ya kukuangamiza, au kukufanya utetereke kwenye imani, au ya kukuudhi, kipindi hicho ukikipitia  basi ujue  hiyo ndio “siku ya uovu” inayozungumziwa hapo.

Kwahiyo kama siku hiyo ikikukuta halafu ulikuwa hujajiweka tayari, ni ngumu sana kumshinda shetani, ni rahisi kupoa au kuurudia ulimwengu kabisa, katika eneo lolote ulilopo hata katika utumishi wako, anaweza kukuletea vitisho visivyo vya kawaida, anaweza kukuletea majaribu, anaweza kukuletea magonjwa, anaweza kukuletea mashahidi wa uongo, anaweza kukubambikizia hata kesi, anaweza kukujia kwa njia yoyote ile, lengo ni kukuangusha, yalimkuta Yusufu, yalimkuta Danieli, yalimkuta Ayubu, yakamkuta Bwana wetu Yesu Kristo, yakawakuta mitume, mimi na wewe ni nani yasitukute?. Hivyo usipojua namna ya kukabiliana na mitego hiyo inapokuja kwa ghafla, utaanguka mara moja.

Na ndio maana mtume Paulo anatoa suluhisho baada ya mstari huo, anasema;

Waefeso 6:13 “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote”

Umeona, vigezo vimeshatolewa hapo juu, ili kumshinda shetani wakati wote, kusema tu umeokoka haitoshi, na huku hujijengei desturi ya kuwa mwombaji wa mara kwa mara, husomi Neno, huifanyi kazi ya Bwana kwa jinsi Mungu alivyokupa karama, Ukiwa ni mkristo wa dizani hiyo ni ngumu kustahimili vishindo vya adui siku ya uovu ikifika,  maana ni lazima ije.

Ni sawa na mtu anayejisifia nyumba yake kubwa ya kisasa yenye mali nyingi za thamani, lakini ndani amekosa vifaa vya uokozi kama vile zima moto, au waya wa Earth.  Anaweza kuifurahia kweli nyumba yake nzuri kaijenga na kuipamba kwa muda mrefu, lakini siku janga kama la moto  litakapotokea kwa ghafla na kuteketeza mali zake zote, pamoja na nyumba yake yote, au umeme unapozidi ndani ya nyumba au radi itakapopiga nyumba, ndipo atakapojua kuwa alikosa vifaa muhimu sana ndani ya nyumba yake.

Vivyo hivyo, tukitaka na sisi tuwe wakristo tuliokamilika, ni lazima tuzingatie vigezo tajwa vyote hapo juu. Tuyafanye maombi kuwa sehemu ya maisha yetu kama tahadhari, Neno la Kristo likae kwa wingi ndani yetu kutuongezea imani, na tutumie karama zetu kuwapelekea na wengine habari njema.

Bwana atutie nguvu.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MWANANCHI WA UFALME WA MBINGUNI

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA.

KUOTA UPO KANISANI.

FAIDA ZA MAOMBI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Yakobo alikuwa na watoto wangapi?

Yakobo alikuwa na watoto wangapi?


Yakobo, mjukuu wa Ibrahimu, alipewa neema na Mungu ya kuwa na Watoto 13, Kati ya hao 12 ni wa kiume na 1 wa kike aliyejulikana kama Dina.

Yakobo alikuwa na wake wawili, Na hao wake zake kila mmoja alikuwa na kijakazi wake mmoja, ambao baadaye walikuja kufanyikiwa kuwa masuria wa Yakobo.

Mke wa kwanza aliitwa Lea, Na mke wa pili aliitwa Raheli. Kijakazi wa Lea aliitwa  Zilpa Na kijakazi wa Raheli aliitwa, Bilha.

Wafuatano ni Watoto wa Yakobo waliozaliwa na Lea.

  1. Rubeni
  2. Simeoni
  3. Lawi
  4. Yuda
  5. Isakari
  6. Zabuloni
  7. Dina(wa kike)

Wafuatao ni Watoto wa Yakobo waliozaliwa na Raheli.

  1. Yusufu
  2. Benyamini

Wafuatao ni Watoto wa Yakobo waliozaliwa na Zilpa (Suria)

  1. Gadi
  2. Asheri

Wafuatao ni Watoto  waliozaliwa na Bilha (Suria)

  1. Dani
  2. Naftali

Habari yote ya uzao wao utaipata katika kitabu cha Mwanzo, kuanzia sura ya 29 na kuendelea.

Mwanzo 29:31 “Bwana akaona ya kwamba Lea hakupendwa, naye akafungua tumbo lake; bali Raheli alikuwa hazai.

32 Lea akapata mimba akazaa mwana, akampa jina lake, Reubeni, maana alisema, Kwa kuwa Bwana ameona teso langu; sasa mume wangu atanipenda.

33 Akapata mimba tena akazaa mwana, akasema, Kwa kuwa Bwana amesikia ya kwamba mimi sikupendwa, amenipa na huyu; akamwita jina lake Simeoni.

34 Akapata mimba tena, akazaa mwana, akasema, Basi wakati huu mume wangu ataungana nami, kwa sababu nimemzalia wana watatu. Kwa hiyo akamwita jina lake Lawi.

35 Akapata mimba tena, akazaa mwana. Akasema, Mara hii nitamsifu Bwana; kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; akaacha kuzaa…………..”

Bwana akubariki.

Angalia Habari za watakatifu wengine wa kale chini.

Pia kama utapenda mafundisho ya biblia yawe yanakufikia kila mara kwa njia ya whatsapp basi utatumie ujumbe kwa namba hii : +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Nuhu alikuwa na watoto wangapi?

Israeli ipo bara gani?

Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

Nimrodi ni nani?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

Kuota unaolewa/ unaoa kunamaanisha nini?


Zipo ndoto zenye maana katika Maisha yetu, na pia zipo ndoto zisizo na maana yoyote katika Maisha yetu,.

Hizi zisizo na maana ni ndoto ambazo, ubongo wetu unajiundia wakati tunapokuwa tumelala kutoka katika mazingira yetu yanayotuzunguka, au mambo ambayo tulikuwa tunayawaza au tunayafanya mara kwa mara, Na ndio maana biblia inasema;

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi..”

Hivyo asilimia kubwa ya ndoto tunazoziota kila siku, zinaangukia katika hili kundi. Kama wewe ni  mshonaji, basi tarajia asilimia kubwa ya ndoto utakazokuwa unaota mara kwa mara zitakuwa ni za namna hiyo,..Vilevile ndoto kama Kuota unaolewa/unaoa, wazo hilo pengine si geni katika kichwa chako,kwamba siku moja umekuwa ukifikiria kuwa utakuja kuoa au utaolewa, Hususani pale unapokuwa umefikia umri huo, lakini bado haijawa hivyo kwako.

Au inakuja kutokana na kuwa umekuwa ukihudhuria mazingira ya harusi mara kwa mara, Hivyo ubongo wako ukayachukua hayo matukio na kuyarudia hivyo hivyo au kwa namna nyingine unapokuwa umelala.

Lakini pia ndoto za namna hii zinaweza kuwa ni za rohoni, hivyo kubeba maana Fulani,

Kwa mfano ikiwa ulikuwa katika kumwomba Mungu, akupe mume/mke, ukiota upo katika ndoa, basi ujue jambo hilo lipo mlangoni kwako.

Lakini unachopaswa kufanya ili Mungu akupe sawasawa na chaguo lake.

  • Kwanza unapaswa uwe katika utakatifu,
  • Vilevile unapaswa uwe mwombaji,

Lakini ukiwa ni mzinifu, unatanga tanga na kila mwanaume, au mwanamke,  au unaishi mtu ambaye  hamjaona, sahau Mungu kulitekeleza hilo, na kama likifanikiwa basi ujue huyo utakayempata hujachaguliwa na Mungu.

Ili kufahamu njia sahihi ya kumpa mweza wa Maisha fungua hapa;

>>> NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

Lakini hayo yote ni lazima uwe katika wokovu, ukimpata Kristo, umepata vyote, Ukimkosa yeye, umepoteza vyote mpaka uzima wako. Hivyo kama leo hii unahitaji kumkaribisha Bwana Yesu maishani mwako, basi uamuzi huo ni mzuri kwako..Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, basi fungua link hii, kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Pia kama utahitaji kujiunga katika magroup yetu ya Whatsapp unaweza ukabofya hapa chini>>

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

KUOTA UNA MIMBA.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

Shalom, mtu wa Mungu..karibu tujifunze Biblia…

Katika kisiwa cha Patmo, Bwana Yesu alimtokea Yohana alipokuwa ametelekezwa kule na kumwambia maneno mengi sana kama tunavyoyasoma katika kitabu cha Ufunuo. Na moja ya maneno aliyomwambia ni haya.

Ufunuo 1:17 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu”

Mtu aliye na funguo maana yake yeye ndie mwenye uwezo wa kuingia na kutoka, au ana uwezo wa kumruhusu mtu mwingine aingie au atoke. Ana uwezo pia wa kumfungia mtu nje au akamfungia ndani. Vilevile huwezi kuzungumzia funguo bila mlango.

Sasa kuna Malango makuu matatu katika maisha 1)  Lango la  MAUTI  na 2) Lango la KUZIMU na 3) Lango la UZIMA WA MILELE

  1. Lango la MAUTI.

Lango la mauti ni hatua ile ya mwisho kabisa mtu anapouacha mwili na kufa..Anakuwa anaingia katika upeo mwingine, ambao sio wa maisha haya ya duniani. Huko anakwenda kukutana na vitu vipya ambavyo havipo hapa duniani aidha vizuri au vibaya. Katika huu mlango au geti kabla ya agano jipya ilikuwa haiwezekani mtu aliyeenda huko arudie tena huku ulimwenguni. Ukifa hakuna kurudi, wanaoingia mautini wanakuwa wamefungiwa huko huko milele. Lakini baada ya Kristo na kuzitwaa funguo za Mauti, ndipo ukazaliwa uwezekano mpya wa wafu kurudia tena uhai… Na huo ulianza na Yesu mwenyewe kutoka kaburini na kurudia uhai, na siku ile tu alipokufa wapo wengine waliotoka makaburini Pamoja naye, wale waliokufa katika haki wakati wa agano la kwanza.

  1. Lango la Kuzimu.

Lango hili mtu analiingia baada ya kifo, Mtu aliyekufa katika dhambi, pasipo kutubu..anapokufa baada ya kuvuka lango la kwanza la Mauti, anaingia lango la pili la kuzimu. Huko ni sehemu mbaya isiyofaa. Na huko nako kuna malango mengine madogo madogo kumtenganisha mwovu na mwovu..hatutaingia huko sana. Lakini katika lango hili kuu la kuzimu, waliokuwa wamekufa katika uovu katika agano la kale, ilikuwa haiwezekani kutoka huko milele. Lakini Kristo alizitwaa funguo, na siku moja wafu waliopo kuzimu watatolewa huko kwaajili ya hukumu na wakiisha hukumiwa watatupwa katika ziwa la moto. 

Yohana 5:27  “Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. 

28  Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. 

29  Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.

Hivyo hata wafu waliopo kuzimu siku moja watatolewa huko kwaajili ya hukumu. Ufunuo 20:13  “Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”. Ufufuo huu sio mzuri kabisa kwasababu ni wa hukumu.

Na roho ya malango ya kuzimu inafanya kazi hata kabla ya mauti, roho hiyo ndiyo inayowavuta watu wengi waiendee njia iliyopotea, shetani na majeshi yake wanafanya kazi kwa nguvu sana kuhakikisha ni kundi kubwa linataingia kuzimu.

  1. Lango la UZIMA WA MILELE:

Lango hili ni ndio la lenye maana  kwetu wanadamu, kwasababu ndio lango la uzima wa milele. Tofauti na malango hayo mengine ambayo yanahitaji kifo ndipo uyaingie.. Lango hili la uzima wa milele halihitaji mtu ufe, linaanzia hapa hapa duniani..wakati huu huu mtu anapumua na kuishi katika mwili wake. Lango hili ni bure kuingia lakini linahitaji kupambana sana, kwasababu yupo mwingine adui yetu ambaye hatamani hata mmoja wetu aingie.

Lango hili ni lile Bwana Yesu alilolisema katika kitabu cha Luka..

Luka 13:24  “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze. 

25  Wakati mwenye nyumba atakaposimama NA KUUFUNGA MLANGO, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako; 

26  ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu. 27  Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu. 

28  Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Kama tunapenda uzima wa milele basi lango hili lipo wazi mbele yetu leo, Bado Bwana Yesu hajalifunga na tunaingia ndani ya lango leo hili kwa kuyatii maneno yake yanayohubiriwa katika biblia takatifu na yanayohubiriwa na watumishi wake. Lakini tukiyakataa maneno yake basi mlango huu utafungwa mbele yetu.

Wapo watu wanaoishi hapa duniani ambao tayari wameshafungiwa mlango huu.(kwamfano watu waliomkufuru Roho Mtakatifu tayari wameshafungiwa, hao kamwe hawawezi kusamehewa tena kadhalika na watu baadhi ambao wameisikia injili kwa muda mrefu sana, wamepigiwa kelele sana, injili imerudiwa na kurudiwa masikioni mwao lakini hata kujigusa hawajigusi, wengi wameshafungiwa huu mlango hivyo kamwe hawataweza kusikia tena ile hamu ya kutubu na kuvutwa kwa Mungu).

Yesu ndiye mwenye funguo za hili lango na funguo hizo pia amewapa watumishi wake..Hebu tusome maandiko yafuatayao ili tuelewe Zaidi..

Yohana 20:21  “Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. 

22  Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. 

23  Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa”.

Umeona hapo? Wale waliotumwa na Yesu kuhubiri wamepewa amri ya kuwafungia watu dhambi..Na hawawafungii kwa kutamka mdomoni kwamba “Fulani nakufungia dhambi” hapana hiyo sio tafsiri yake..Tafsiri ya kuwafungia watu dhambi iliyozungumziwa hapo ni hii >>

Mathayo 10:14  “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu.

15  Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.

Kwahiyo mtu anaposikia injili na kuidharau tena kuikejeli..Yule mtumishi wa Mungu Roho Mtakatifu anapomwongoza aondoke mahali pale..hao waliosalia hapo nyuma, ndio Habari yao imeisha!..hawatapata tena neema kamwe, wataendelea katika njia hiyo hiyo! Mlango umefungwa tayari. Hali kadhalika wanapoikubali na kuitii, basi wanafunguliwa mlango ambao malango ya kuzimu hayataiweza..maana yake hao watu watakaoitii injili inayohubiriwa na mtu yule aliyetumwa na Mungu..basi ni ngumu sana kupotea…Watakuwa wana ulinzi Fulani wa daima ambao hata wakirudi nyuma kidogo nguvu ya Mungu itawarudisha kwenye mstari kwasababu tu! Waliitii injili ya Kristo. Bwana Yesu alimwambia maneno haya Petro.

Mathayo 16:18  “Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. 

19  Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”

Petro ni mfano wa watu wote waliothibitishwa na Mungu na kuwekwa wakfu kwa ajili ya kazi yake.

Hivyo dada/kaka unayesikia maneno haya. Kama unapenda kuishi Maisha yasiyo na mwisho…miaka milioni kwa mamilioni yasiyo na shida wala taabu, wala uchungu…Njia ni moja tu, nayo ni Yesu. Yeye ndiye mwenye funguo za Uzima wa Milele, na funguo hizo amewapa watumishi wake pia..Ukitaka kuishi, ukitaka uzima..Mkubali Yesu. Ukimkubali Yesu malango ya kuzimu yatakukwepa..kuna nguvu fulani itaachiliwa juu yako ambayo atakuweka katika mstari uliyoonyooka..Lakini kama hutaki kuishi milele, basi malango ya Mauti na kuzimu yanakungoja, hivyo chagua chaguo jema, Yesu ndiye lango na anakupenda!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KUZIMU ni mahali pa namna gani, Je! huko wanaishi watu wakifa na kwenda kupata mateso au ni vinginevyo?

USIUZE URITHI WAKO.

HASIRA YA MUNGU KUKUWAKIA, KWA KUTOMZUNGUZIA TU MUNGU IPASAVYO.

FAHAMU MAJIRA ULIYOPO NA NINI UNAPASWA UWE NACHO.

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

NI KITU GANI PETRO NA YOHANA WALIKIGUNDUA KABURINI?

UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?

Mwezi wa Abibu ni upi?


Huu ni mwezi wa kwanza kwa kalenda ya Kiyahudi. Ambao kwa kalenda yetu hii ya ki-gregory unaangukia katikati ya mwezi Machi, na Aprili, kutegemeana na mwaka wenyewe jinsi ulivyokuja.

Upo mwaka ambao mwezi huu wa Abibu unaanza katikati ya  mwezi wa tatu, na upo mwaka, unaanza mwanzoni mwa mwezi wa nne.

Mwezi huu ni mwezi muhimu sana kwa wayahudi, kwasababu ndio mwezi wa kumbukizi yao ya kutoka katika nchi ya Misri(Nchi ya Utumwa).

Kutoka 13:4 “Ninyi mwatoka leo katika mwezi wa Abibu”.

Ndani ya mwezi huu, Siku ya 14 walikuwa wanasheherekea sikukuu iliyojulikana kama sikukuu ya pasaka, Na kuanzia tarehe 15-21, walisheherekea sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu.

Kumbukumbu 16:1 “Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka Bwana, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku Bwana; Mungu wako.

2 Nawe umchinjie pasaka Bwana, Mungu wako, katika kundi la kondoo na la ng’ombe, mahali atakapochagua Bwana apakalishe jina lake”.

Mwenzi wa Abibu ulijulikana kwa jina lingine kama  mwezi Nisani.

Esta 3:7 “Basi mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari”.

Soma pia. Nehemia 2:1

Sasa wayahudi kila wanapoiungia huu mwezi wa Abibu/Nisani, huwa wanakumbuka siku ya kutolewa kwao utumwani..

Lakini swali linakuja kwako wewe mkristo, Siku yako ya Nisani ni ipi?

Abibu/Nisani yetu ni pale tunapookoka, siku tunapoamua kuacha dhambi na kumfuata Kristo, na kwenda kubatizwa, basi kuanzia siku hiyo nasi pia tunakuwa tumejumuishwa katika kalenda ya ki-Mungu. Hivyo rohoni tunaonekana kuwa tumeshauanza mwezi wa Abibu/Nisani.

Na faida yake ni kuwa, kuanzia huo wakati unakuwa unaanza kutembea  katika mpango wa Mungu wa kimbinguni, wewe unakuwa sio mwana-haramu tena, Mungu anaanza kutenda kazi zake ndani ya maisha yako, kipindi kwa  kipindi, Na hilo utalishuhudia mwenyewe, kwa jinsi siku zitakavyokuwa zinakwenda. Utaona tofauti yako ya mwezi uliopita na mwezi huu, utaona tofauti yako ya  mwaka ule uliookoka, na ile mingine iliyopita nyuma.

Lakini kama upo katika dhambi, wewe bado kalenda ya ki-Mungu haijaanza kuhesabiwa kwako. Na hivyo Mungu anakuwa hana mpango wowote na wewe, unakuwa ni kama mwana haramu tu. Shetani atajiamulia kufanya lolote atakalo katika maisha yako, atakuharibia maono yako, atafanya chochote ajisikiacho na mwisho wa siku utapotea na kwenda kuzimu. Na kuishia katika majuto ya milele

Lakini ukitubu dhambi zako, leo na ukawa tayari kuanza maisha mpya na Kristo, basi ni uhakika kuwa utaanza kutembea katika huo mpango wa Mungu. Hivyo bila kupoteza muda Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki,

pia fungua vichwa vingine  vya masomo chini, upate mafundisho mengine ya rohoni.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

Israeli ipo bara gani?

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

 MAVUNO NI MENGI

KRISIMASI (CHRISTMAS) NI NINI? JE IPO KATIKA BIBLIA?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nimrodi ni nani?

SWALI: Nimrodi ni nani? Na je! Alikuwa ni mtumishi wa Mungu?

Nimrodi ni kitukuu cha Nuhu kwa kupitia  uzao wa Hamu,

Biblia inatuambia alianza kuwa mtu Hodari, na sio Hodari tu, bali alikuwa ni Hodari wa kuwinda mbele za Bwana, Mpaka enzi hizo ukatungwa msemo maarufu kwa jina lake (Soma Mwanzo 10:9),  

Hivyo aliendelea na huo uhodari wake mpaka akafikia hatua ya kuwa na nguvu nyingi za kuanza kujenga miji mikubwa, ikiwemo Babeli na Ninawi.

Mwanzo 10:8 “Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.

9 Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za Bwana. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za Bwana.

10 Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.

11 Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;

12 na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa”

Lakini japokuwa alikuwa ni Hodari, alikuwa ni mwovu katika fikra zake na matendo yake, nakala nyingi za kale zinaonyesha, hata nia yake ya kutaka kuujenga mnara wa Babeli ilikuwa ni kumlipizia Mungu kisasi, kwamba kwanini aliwaua mababu zake, hivyo akaunyanyua mnara ule juu sana kuelekea mbinguni kiasi kwamba hata Mungu akileta tena mafurukio mengine asiweze kuwaangamiza.

Lakini jitihada zake hazikufika mbali, tunajua kilichotokea ni nini baada ya pale, ni kwamba walichafuliwa lugha zao na semi, ndoto zao zote zikayeyukia palepale, Kwasababu Mungu hadhihakiwi.

 Lakini Pamoja na hayo bado tunakuja kuona Babeli iliendelea kuwepo kwa miaka mingi mbeleni, mpaka ikaja kuwa  kitovu cha machafuko yote duniani, Na ndio  hawa wababiloni baadaye wakaja kulichukua taifa la Israeli utumwani tena. Kama ulikuwa hujui ni kwamba chimbuko la ibada zote za sanamu na miungu, ilianzia huko, Hii miungu ya Rumi ya kuabudu mungu mke na katoto chake (ambayo kwa sasa wameipachika majina ya watakatifu kama Mariamu ) chimbuko lake lilikuwa ni huko,

Na ndio maana Babeli hiyo mpaka siku hizi za mwisho bado inaonekana kuishi, isipokuwa safari hii inatenda kazi  rohoni. Katika kivuli cha dini.

Sasa muhasisi wa hayo yote alikuwa huyu Nimrodi.

Biblia inasema..

Mithali 1:32 “Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”

Usifurahie mafanikio ya kipumbavu hata kama utasifiwa na ulimwengu mzima, shetani naye alikuwa ni Hodari hivyo hivyo kabla ya kuasi, lakini ulikuwa ni uhodari unaokwenda kinyume na mapenzi ya Mungu.

Ezekieli 28:14 “Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto.

 15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako.

16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto.

 17 Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama.

18 Kwa wingi wa maovu yako, katika uovu wa uchuuzi wako, umepatia unajisi patakatifu pako; basi nimetokeza moto kutoka ndani yako, nao umekuteketeza, nami nimekufanya kuwa majivu juu ya nchi, machoni pa watu wote wakutazamao.

  19 Wote wakujuao kati ya kabila za watu watakustaajabia; umekuwa kitu cha kutisha, wala hutakuwapo tena hata milele”.

Nasi pia tusiige mifano hiyo, tuwe wanyenyekevu kwa Mungu, tuishi kwa kuyafanya mapenzi yake, Hilo tu linatosha Sio kila jambo linalofanywa na watu Hodari wa mataifa yaliyoendelea na sisi tuigee, Ni heri tubakie na ushamba wetu kuliko tuige utukanaji, ushoga, au upagani, au uvaaji wa mavazi yasiyo na heshima mbele za Mungu na wanadamu.

Imemfaidia nini Nimrodi kuupata ulimwengu mzima, halafu amepata hasara ya roho yake?

Bwana atusaidie.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

YEREMIA

Kuungama ni nini?

Je! msalaba kaburini una umuhimu wowote?

UMEFUMBULIWA MACHO YAKO YA KIROHO?

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

FAIDA ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Je! Unazijua faida za kufunga na kuomba?


Embu isome Habari ifuatayo kwa makini;

Mathayo 17:18  “Yesu akamkemea pepo, naye akamtoka; yule kijana akapona tangu saa ile.

19  Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa?

20  Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

21  [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga”.

Mstari wa 21 unasema.. “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga”

Hii ikiwa na maana kuwa yapo mambo ambayo mtu atashindwa kuyafanya, haijalishi yeye ni mkristo au la, haijalishi  yeye ni mtakatifu au la! kama hafungi na kuomba, basi atashindwa kufanya mambo mengi sana.

Embu tuzitazame faida za kufunga na kuomba..

Tukianza na kufunga:

1)   Pale mtu unapofunga, ina maana kuwa  hali chakula, au hanywi maji, kwa wakati Fulani, Na hiyo inampelekea mtu kuwa katika uhitaji mkubwa, Sasa uhitaji huo ndio unaoutesa mwili na kufanya mates ohayo yapenye mpaka  kwenye nafsi ya mtu. Nafsi ya mtu ikishapokea mabadiliko hayo inaifanya roho ya mtu kuwa na mwitikio wa tofauti sana katika mambo ya rohoni. Tofauti na mtu ambaye hajafunga kabisa.

Kufungu kunakwenda sambamba na magonjwa, kwamfano mtu aliye katika hali nzito ya kuumwa au kuugua mwilini, mateso yale huwa yanashuka mpaka kwenye nafsi ya mtu, na ndio hapo utaona wagonjwa wengi wapo karibu na Mungu kuliko watu walio na afya zao,

Sasa turudi katika kufunga, pale unapofunga hata maombi yako yanakuwa na uzito wa tofauti ukilinganisha na siku nyingine ambazo ulikuwa hufungi, (jaribu hilo utalithibitisha) kama ulikuwa katika kuyatafakari maandiko, uelewa wako unakuwa wa ndani Zaidi tofauti na siku nyingine ambazo ulikuwa hufanyi hivyo .

Na kwa jinsi atakavyozidi kuenendelea kufunga kwa siku nyingi, ndivyo utakavyozidi kuwa mwepesi katika mambo ya rohoni.

Musa alifanikiwa kufunga siku 40 asiku na mchana bila kula, na sote tunajua ni nini alipata kule mlimani..Mungu alizungumza naye uso kwa uso, na kumpa zile Amri 10, Vivyo hivyo hata kwa Eliya naye alipofunga siku 40, Mungu alisema naye kwenye ule ule mlima wa Musa..

Halikadhalika na kwa Bwana wetu Yesu Kristo, yeye pia alifunga siku 40 usiku na mchana bila kula chochote, mpaka ibilisi akatokea kumjaribu na kushindwa na aliposhuka kule mlimani alishuka na nguvu nyingi za Roho Mtakatifu ndipo akaanza kuhubiri injili na kuponya wangojwa katika Israeli yote.

Hivyo mifungo ya muda mrefu inafaa sana.

2) Faida nyingine ya kufunga inakusaidia kushusha chini matamanio ya mwili. Kwa kuwa chakula kinakuwa hakina sehemu kubwa katika mwili kwa wakati huo, hivyo hata kazi za uzalishaji wa  homoni, zinapungua na hivyo inamfanya yule mfungaji awe katika hali ya utulivu Zaidi katika kumtafuta Mungu.

Biblia inatuambia pia, ukifunga, Mungu anakupa thawabu, Hiyo ni kuonyesha kuwa Mungu anathamini kujitesa kwetu kwa ajili yake.

Mathayo 6:16  “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.

17 Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;

18  ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

 

Kuomba.

Lakini pia unapaswa kujua kuwa kufunga kokote ni lazima kuambatane na kuomba..hivi ni vitu viwili vinavyokwenda sambamba, ni sawa na chai na sukari, unapobandika chai jikoni, inamaanisha kuwa  sukari ni lazima iwepo chini pale inaongojea chai iepuliwe, vinginevyo haitaitwa chai.

Vivyo hivyo na  Katika kufunga, hupaswi kufunga tu, unaamka asubuhi, unarudi jioni, halafu hufanyi lolote, unarudia tena hivyo kesho, na kesho kutwa,..hapo ni sawa na kufanya “diet” tu , Lakini unapofunga ni lazima uwe na malengo ya rohoni kwanini unafanya hivyo.

Hapo ndipo hapo sasa suala la kuomba lazima lijitokeze; Danieli alipofunga alikuwa mwombaji, vivyo hivyo na watu wote katika biblia..

Danieli 9:3 “Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. 

4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake; 

5 tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na hukumu zako”;

Ukizingatia vigezo hivyo basi faida za kuomba ni kama zifuatazo;

  • Kwanza Mungu anakuepusha na majaribu;

Mathayo 26:40 “ Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?

41  Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”

  • Pili Mungu anakupa thawabu

Mathayo 6:5  “Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao

6  Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

  • Tatu unafungua milango ambayo ilikuwa ni migumu kufunguka.

Kama tulivyoona katika mistari ya mwanzoni juu, Bwana aliwaambia wanafunzi wake, pale waliposhindwa kutoa mapepo, kuwa namna ile haitoki isipokuwa kwa kufunga na kusali. Hata wewe unapojijengea ustaarabu wa kuwa mwombaji mzuri, basi unapokea mamlaka kubwa Zaidi ya kuamrisha nguvu za giza ziwatoke watu.

  • Na nne unarejesha furaha ya wokovu;

Siri nyingine ya maombi ni kuwa, kwa jinsi unavyodumu kwenye kuomba ndivyo unavyoukaribisha uwepo wa Mungu ndani yako..Na matokeo yake ni kuwa  ile furaha ya wokovu inajengeka ndani yako.

Usipokuwa mwombaji, ni ngumu sana kuufurahia wokovu wako, utaona kama Mungu yupo mbali na wewe kila siku, utakosa ujasiri wa Imani yako, lakini ukiwa mwombaji amani Fulani utaipata na ujasiri.

Hivyo kama wewe, ulikuwa unalega lega, au ulikuwa hujua faida za kufunga, basi anza leo kufanya hivyo, pia hakikisha unajijengea utaratibu wa kuomba, saa moja kila siku, hicho ndio kiwango cha chini tulichopewa na Bwana Yesu.Kama ukifanya hivyo  hakika utaona matokeo makubwa katika Maisha yako..

Utaona tofauti yako ya leo na jana.

Bwana akubariki.


Ikiwa utatamani kujua Zaidi juu ya faida za kufunga, basi tazama masomo mengine yaliyoorodheshwa chini hapa.

Lakini Kama hujaokoka, na unatamani kuokoka leo, Basi uamuzi huo ni mzuri sana, hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>>>

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

Namna ya kuomba

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

KIAMA KINATISHA.

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

SABATO TATU NI NINI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

SABATO TATU NI NINI?

Swali: Sabato tatu ni nini? Kama tunavyosoma katika Matendo 17:2

Jibu: Tusome,

Matendo 17:1 “Wakiisha kupita kati ya Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalonike, ambapo palikuwa na sinagogi la Wayahudi.

2 Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko SABATO TATU,

3 akiyafunua na kuwaeleza ya kwamba ilimpasa Kristo kuteswa, na kufufuka katika wafu; na ya kwamba, Yesu huyu ninayewapasha ninyi habari zake ndiye Kristo”.

Mstari huo haumaanishi kwamba kuna aina tatu za sabato au sabato zipo tatu. Hapana, bali unamaanisha Sabato tatu mfululizo.

Kwamfano tafakari hii sentensi.. “Yohana baada ya kuokoka alihudhurua kanisani JUMAPILI TATU mfululizo za mwezi uliopita”. Sasa hapo simaanishi jumapili zipo za aina tatu, bali namaanisha ni jumapili za majuma matatu. Ndivyo Paulo alichomaanisha hapo katika sabato tatu. Maana yake kwa sabato tatu mfululizo aliingia hekaluni kuhojiana nao kwa maneno ya maandiko.

Sasa unaweza kuuliza je! kwa mantiki hiyo na sisi tunapaswa tuishike sabato?

Jibu ni la! Sabato halisi katika agano jipya sio siku moja maalumu, bali ni kila siku ya maisha yetu tunayoishi, sasa kwanini hapo Paulo aingie kuhojiana nao wakati wa sabato?. Ni kwasababu kwa wakati huo wayahudi (yaani waisraeli), walikuwa bado wana desturi ya kuishika sabato. Hivyo siku pekee  ya kuweza kukutana nao ni siku ya sabato katika masinagogi yao, siku nyingine zozote wasingeweza kupatikana ndio maana hapo Paulo alikwenda kukutana nao katika siku yao ya kuabudu.

Ni sawa leo utafute namna ya kuwapata watu wa dini Fulani kuhojiana nao kuhusu imani, huwezi kuwapata nje na ile siku yao wanayokutana kuabudu. Kama ni ijumaa, au jumamosi au jumapili, au siku nyingine yoyote ile, sasa kitendo cha wewe kuwafuata ili uwashuhudie katika siku yao ya Ibada haimaanishi kwamba na wewe umeihalalisha siku ile.

Kufahamu zaidi kuhusu Sabato halisi ni ipi, mwisho wa somo hili chini kabisa utaona orodha ya mada hizo zinazohusiana na sabato, zifungue uzisome.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

Je! “majira na sheria” mpinga-kristo atakayokuja kubalisha ni kupindua siku ya sabato na kuwa jumapili?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

KIAMA KINATISHA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

IPELEKE SADAKA YAKO MAHALI SAHIHI,ILI UBARIKIWE.

Karibu tujikumbushe mambo machache, ambayo yanaonekana ni madogo lakini ni ya umuhimu sana, katika mapambano ya Imani.

Kuna tofauti ya sadaka na msaada. Unapomsaidia maskini huo ni msaada, na una thawabu zake mbele za Mungu..lakini sadaka ina matokeo makubwa zaidi kuliko msaada.

Sadaka ni nini?

Sadaka ni matoleo yoyote yanayohusisha madhababu!.. Katika agano la kale, sadaka iliyokuwa inakubalika kwa Mungu ni ile iliyokuwa inapelekwa mbele ya madhabahu ya Mungu katika nyumba ya Mungu…iwe ni kafara ya kondoo, au sadaka ya mazao au chochote kile. Vigezo ni lazima ipelekwe katika hema ya kukutania au katika nyumba ya Mungu.

Usipeleke sadaka yako kwa maskini, ukifanya hivyo utakuwa hujatoa sadaka bali umetoa msaada, utabarikiwa kwa ulichotoa lakini si kama ungeitoa kama sadaka. Sadaka ni lazima ihusishe madhabahu ya ki-Mungu.

Hata watu wanaokwenda kwa waganga huwa wanapewa masharti ya kupeleka sadaka..Na ile sadaka wanapewa maagizo ya kuiacha pale kwenye madhabahu zao, ili ilete matokeo wanayoyataka, kama ni kuku ataambiwa ampeleke hapo wamchinjia hapo hapo na kumwacha pale pale…Huwezi kusikia wanapewa maagizo na waganga na kuambiwa wakachinje jogoo mweusi nyumbani halafu wakawape maskini, au wakaipeleke kwa mganga mwingine,! Huwezi kusikia hicho kitu!.watakuambia leta hapa (kwenye hii madhabahu) hiki au kile kama sadaka yako, kwasababu ili kitu kiwe sadaka ni lazima kihusishwe na madhabahu.

Kwahiyo hakuna sadaka pasipo madhabahu.

Bwana Yesu alisema maneno haya katika

Mathayo 23:18 “Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga”.

Maneno hayo yanaelezea uhusiano uliopo kati ya sadaka na madhababu.

Kwahiyo kama wewe ni mkristo, sadaka yako peleka kanisani na mahali unapokuzwa kiroho (kwamfano kwenye mikutano ya injili, semina n.k), ndipo utakapobarikiwa Zaidi… Bila kusahau kusaidia maskini na wenye uhitaji ambako pia kuna thawabu kubwa kutoka kwa Mungu. Lakini sadaka ina nguvu mara nyingi Zaidi ya hiyo, endapo utaelewa ufunuo wake!.. Ongeza bidii sana katika kutoa sadaka kuliko kupeleka michango yako sehemu nyingine.

Kuna fikra mbaya sana ambayo shetani kaisambaza kwenye akili za watu wengi, ambayo imewasababishia watu wengi kukosa baraka zao. Na hicho ni saikolojia ya kwamba ukiipeleka sadaka kanisani basi ni kuwatajirisha wale wachungaji na watumishi!, na hivyo ni afadhali kuipeleka kwa maskini, Hiyo ni saikolojia ya Adui, usikubali ikutawale.

Bwana Yesu alisema pia maneno haya..

Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,

24  iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”.

Mambo haya yanaonekana ni madogo machoni pa wengi, lakini yana umuhimu mkubwa sana. Hivyo ni muhimu sana kuyafahamu na kuyazingatia. Zaka yako ipeleke nyumbani kwa Bwana, Sadaka zako za shukrani vilevile ipeleke nyumbani kwa Bwana.

Mungu akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 693036618/ 0789001312

Mada Nyinginezo:

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Ubatizo wa moto ni upi?

MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

JE KUVAA PETE NI DHAMBI?

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNALIA/UKIOTA UNALIA KWA UCHUNGU.

Kuota unalia kwa uchungu/Ukiota unalia maana yake ni nini kibiblia?.


Zipo ndoto zenye maana, na pia zipo ndoto zisizo na maana yoyote katika maisha ya mtu, hizi za pili ni ndoto ambazo zinatengenezwa na ubongo wako tu wenyewe, kwa kuchukua matukio ambayo aidha ulishawahi kuyafanya au kuyapitia huko nyuma, au mazingira unayoishi sasa, au mambo unayoyafanya mara kwa mara.

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi…;”

Kwamfano kama wiki iliyopitia ulikuwa unahudhuria sana kwenye sherehe, tarajia moja ya ndoto unazoziota kila siku kuwa za namna hiyo.. Vivyo hivyo na ndoto hii ya kuota unalia/ukiota unalia kwa uchungu, inaweza kuja kutokana na mazingira yako ya nyuma, Wengine walifiwa na jamaa zao wa karibu kipindi sio kirefu, wengine walikuwa misibani.n.k..Hivyo ubongo unachukua matukio hayo na kuyarudia rudia kwenye ndoto zetu za kila siku.


Lakini pia ndoto ya namna hii inaweza  kuja kwa namna ya kitofauti sana, pengine hujafiwa siku za hivi karibu, au hujapitia matatizo yoyote mazito ya kukufanya uwe katika huzuni kubwa..Lakini unashangaa usiku umeota unalia kwa uchungu mwingi, bila kujua sababu ya kulia kwako ni nini. Unalia tu, unalia tu,

Ukiona hivyo basi lipo jambo unapaswa ulijue rohoni..

Ndugu unayesoma ujumbe huu, fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho, na Yesu anakaribia kuja kulinyakua kanisa lake. Mwisho wa dunia upo karibu sana.

Kuota unalia kwa uchungu, Ni Mungu anakuonyesha kuwa jinsi hali itakavyokuja kuwa huko mbeleni ikiwa utaachwa katika unyakuo, na watu wote watakavyokuwa..Haijalishi wewe ni muislamu, ujumbe huu unakuhusu pia wewe, kiama kipo karibu, watu wataomboleza, kwa kilio na uchungu usioeleza,  kwa hayo mambo ya kutisha ambayo Mungu atayaleta katika hii dunia,

Biblia inasema hivi;

Sefania 1:14 “Hiyo siku ya Bwana iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya Bwana; SHUJAA HULIA KWA UCHUNGU MWINGI HUKO!

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,

16 Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.

17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.

18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha”.

Unaona, hali itakavyokuwa kwa watu hata wale wanaojiona mashujaa leo, watalia kwa uchungu mwingi..

Isaya 33:7 “ANGALIA, MASHUJAA WAO WANALIA NJE, WAJUMBE WA AMANI WANALIA KWA UCHUNGU.

8 Njia kuu zimeachwa, msafiri amekoma; ameyavunja maagano, ameidharau miji, hamjali mtu.

9 Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani”.

Ni mambo ya kutisha sana, ikiwa leo Yesu amerudi, na umeachwa, kitakachokuwa kinaendelea kwako, ni zaidi ya ulichokiona katika ndoto..

Yeremia 4:8 “Kwa sababu hiyo jifungeni nguo za magunia; ombolezeni na kulia kwa uchungu; kwa maana hasira kali ya Bwana haikugeuka na kutuacha.

9 Na katika siku hiyo itakuwa, asema Bwana, moyo wa mfalme utapotea, na moyo wa wakuu wake; na makuhani watastaajabu, na manabii watashangaa”.

Mathayo 13:41 “Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,

42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, NDIKO KUTAKUWAKO KILIO NA KUSAGA MENO”.

Yapo maandiko mengi yanayoelezea maombolezo yatakayokuwa yanaendelea katika kipindi hicho lakini hatuwezi kuiorodhesha yote hapa, Kama utapenda kufahamu kwa marefu juu ya siku hiyo ya mwisho itakavyokuwa basi fungua hapa usome.>>> MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Hivyo Kama wewe hujaokoka, na unajijua kabisa unaishi katika maisha ya dhambi, basi ni vema ukamgeukia Kristo leo, ayaokoe maisha yako, Kukutana na ujumbe huu sio bure, Umeoteshwa ndoto hiyo ni kwasababu Mungu ana mpango na wewe. Hivyo usifanye moyo wako mgumu, mkabidhi Yesu maisha yako leo aanze kutembea na wewe na hakika utamwona kwa namna ambayo hukuwahi kumtazamia, na atahakikisha kuwa mabaya hayo yote hayatakukuta ikiwa atarudi leo..

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki sana.

Pia angalia vichwa vya masomo mengine chini, fungua upitie naamini vitakutoa sehemu moja kiroho hadi nyingine.

 Ikiwa utapenda kupata mafundisho ya Neno la Mungu ya kila siku kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwa namna hii: +255 789001312

Au jiunge kwa kubofya hapa chini;

Group la whatsapp  Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Mada Nyinginezo:

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

SIKU ILE NA SAA ILE.

MAONO YA NABII AMOSI.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

FAHAMU MAJIRA ULIYOPO NA NINI UNAPASWA UWE NACHO.

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

Rudi Nyumbani:

Print this post