SWALI: Ayubu alipopata yale majaribu, alimwambia mkewe;
Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Swali ni je! Mambo mabaya yanatoka pia kwa Mungu?
JIBU:
Ayubu 2:10
[10]Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.
Ukweli ni kwamba Mungu hatoi mabaya, bali sikuzote hutoa mema…mabaya huwa yanatoka kwa adui..
Isipokuwa katika kuyapokea mema ya Mungu, yapo mapito ambayo (mbele ya macho yetu), tunayaona kuwa ni mabaya lakini kiuhalisia ni njia tu ya kufikia Mema yetu Mungu aliyotuandalia..wala hakuna lolote linaloharibika..
Angalia mwisho wa Ayubu…kumbe Mungu alitaka kumpatia mara dufu, ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzo, na ndio maana ilinpasa vile vya mwanzo viondoke…
Tengeneza picha miaka mingi baadaye labda tuseme miaka 30 baada ya lile pito, akiwa na watoto wake wapya ambao ni mashuhuri wenye hadhi na nguvu za Mungu..Tena Akiwa Mwenye utajiri mwingi na heshima kuliko mwanzoni..bila shaka huwenda alipokumbuka zile nyakati ambazo alikuwa analia na kusema “ilaaniwe siku ile niliyozaliwa” alikuwa anacheka na kusema Mungu Nisamehe nilikuwa sijui nitendalo!
Yakobo 5:11
[11]Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.
Mungu hutujenga katika nyakati zote nyakati za furaha lakini pia nyakati za mateso.Ukishalitambua hili kama mwana wa Mungu hutasumbuliwa na tufani..Bali utamtukuza Mungu katika mazingira yote,, ukijua kuwa kusudi la Mungu linatimia katika mazingira yote…Wala hakuna lolote linalo haribika..
Nyakati tuzionazo mbaya huleta baraka..majeshi ya washami yalipowazunguka Israeli, mwisho wake ulikuwa ni kuziachilia nafaka na mali kwao, Samsoni alipokutana na Simba, kumbe ni asali aliletewa..mwanamke apatapo na utungu hawezi kusema ni mabaya anapitia, kwasababu anajua kuwa hiyo ni njia tu ya kupata kiumbe kipya duniani.
Vitu kama Saburi, unyenyekevu, upole Mungu anavijenga ndani ya watoto wake katika nyakati kama hizi (ambazo sisi tunaziita ni mbaya)…
Hivyo jifunze kuliona kusudi la Mungu katika nyakati zako zote.
Kwa hitimishi ni kuwa Ayubu aliposema ‘Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya?’
Alimaanisha nyakati za huzuni..ambazo zinatimiza kusudi la Mungu….lakini sio mabaya mfano wa mabalaa na vifo, ambayo mwisho wake ni uharibifu. Mungu kamwe haleti uharibifu kwa mtoto wake, hawezi kutupatia samaki na wakati huo huo kutupatia nyoka.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Print this post
Jibu: Tusome..
Warumi 12:11 “kwa BIDII, si walegevu; mkiwa na JUHUDI katika roho zenu; mkimtumikia Bwana”
“Bidii” ni hamasa/msukumo wa ndani wa kufanya jambo fulani… na mtu anaweza kuwa na bidii lakini asiwe na juhudi.
Kwamfano mtu anaweza kwa na bidii kubwa katika kupanga mambo, lakini katika utekelezaji akashindwa.
Lakini “Juhudi” yenyewe inakwenda mbali zaidi katika utekelezaji kwa vitendo, kwamfano mtu anaweza kuwa na bidii ya kuweka mikakati ya kilimo na mipango, na baadaye akafanya juhudi katika kilimo kwa kuingia shambani na kulima.
Mtu anaweza kuwa na bidii ya kununua vitabu vingi vya imani vya kumsaidia kukua kiroho na akaonyesha “juhudi” ya kuvisoma vile vitabu na akazalisha kitu katika maisha yake ya kiroho… au mtu anaweza kuwa na bidii nyingi kujua mafundisho ya upendo, imani, maombi au wokovu lakini kama hatakuwa na “juhudi” ya kuishi au kukitenda kile anachojifunza au kikosoma “bidii” yake ni bure..
Biblia inatufundisha kuwa na bidii na juhudi pia katika mambo yote..
Usiwe na bidii na kukosa Juhudi kwani Juhudi ni ngazi ya msingi sana kufikia lengo la kiroho..
Tito 2:14 “ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale WALIO NA JUHUDI KATIKA MATENDO MEMA”.
Kwahiyo sio tu BIDII katika kusoma, bali pia na JUHUDI katika kutenda, ndivyo Biblia inavyotufundisha..
1Petro 3:13 “Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?”
1Petro 4:8 “Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi”.
Bwana atusaidie.
Mafundisho mengine:
Ipi tofauti ya Kukemea na kukaripia? (2Timotheo 4:2)
Ipi Tofauti ya Agano jipya na Agano la Kale?.
Ipi tofauti ya utakatifu na utukufu?
Ipi tofauti ya Falme, Mamlaka na Wakuu wa giza (Waefeso 6:12)
Ipi tofauti ya Hasira na Ghadhabu ya MUNGU?.
WhatsApp
Jibu: Turejee…
2Wakorintho 6:15 “Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na BELIARI? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?”
Neno Beliari ni muunganiko wa maneno mawili ya kiebrania, ambayo ni “Beliy-ya’al” lenye maana ya “Asiyefaa kitu” na Neno lingine la “Baradhuli”
Sasa hapo kwenye 2Wakorintho 6:15 inaweza kusoma hivi kwa Kiswahili kirahisi… “Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na mtu asiye na maana? ”
Kibiblia mtu asiyefaa kitu ni mtu asije mcha Mungu, asiye na hofu ya Mungu, mwenye roho ya ibilisi ndani yake, kwaufupi ni Baradhuli, mfano wa Beliari/baradhuli ni wale tunaowasoma katika 2Nyakati 13:7..
2Nyakati 13:7 “Wakamkusanyikia watu mabaradhuli, WASIOFAA KITU, waliojitia nguvu juu ya Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana na wa moyo mwororo, asiweze kuwazuia”.
Waamuzi 19:22 “Hapo walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, tazama, watu wa mji huo, watu mabaradhuli wakaizingira hiyo nyumba pande zote, wakagonga mlango; wakasema na huyo mwenye nyumba, huyo mzee, na kumwambia, Mlete nje mtu yule aliyefika nyumbani kwako, ili tupate kumjua”.
Soma pia Kumbukumbu 13:13, Waamuzi 11:3, Waamuzi 20:13, 2Samweli 6:20 na Ayubu 11:11.
Na kama maandiko yanavyosema hakuna mapatano au ulinganifu kati ya Kristo na Beliari, maana yake Kristo hawezi kuchanganywa na uchafu, wala hawazi kutembea na Mabeliari au Mabaradhuli, hivyo hatuna budi kujitakasa na uchafu wote wa mwilini na rohoni, ili tutembee na Kristo.
2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.
Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?
WATU WASIOJIZUIA.
HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE
Watu wenye kuvunja maagano ndio watu wa namna gani? (Warumi 1:31)
Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)
Shalom.. Karibu tujifunze Biblia pamoja.
Zipo nyakati Ngumu ambazo kama mkristo utazipitia, ni nyakati za dhiki, na vilio wakati mwingine…na nyakati hizo haimaanishi kuwa Mungu kakuacha, hapana!, ni iko namna hiyo tu.… maana maandiko yanasema tumewekewa hizo, ingawa ni za kitambo tu.
1Wathesalonike 3:3 “mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo. 4 Kwa kuwa tulipokuwapo kwenu tulitangulia kuwaambia kwamba tutapata dhiki, kama ilivyotukia, nanyi mwajua”.
1Wathesalonike 3:3 “mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.
4 Kwa kuwa tulipokuwapo kwenu tulitangulia kuwaambia kwamba tutapata dhiki, kama ilivyotukia, nanyi mwajua”.
Sasa inapotokea umekutana na dhiki, au majaribu na huku ukijitazama upo sawa kiimani, na wala hujarudi nyuma, ni nini cha kufanya?
Jambo ni moja tu, nalo ni kusimama na kuendelea mbele na si kuendelea kulia (USIKATE TAMAA)…… Machozi yapo kweli, lakini hayawezi kukusaidia sana wakati wa majaribu, bali ujasiri na kusimama ndio kuendelea mbele ndio Nguvu ya kuvuka huo wakati.
Tujifunze kwa habari ya Daudi kabla hajawa mfalme. Maandiko yatuambia, kuna siku alirudi mjini mwake akakuta mji umevamiwa na Waamaleki na wake zake wamechukuliwa mateka pamoja na mali zao, ilikuwa ni kilio kikubwa cha uchungu mkubwa, na Daudi pamoja na wenzake walilia sana..
1Wafalme 30:1 “Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Siklagi siku ya tatu, hao Waamaleki walikuwa wameshambulia Negebu, na Siklagi, nao wameupiga Siklagi, na kuuchoma moto; 2 NAO WAMEWACHUKUA MATEKA WANAWAKE WALIOKUWAMO WAKUBWA KWA WADOGO; HAWAKUWAUA WO WOTE, ILA WAKAWACHUKUA, WAKAENDA ZAO. 3 Basi Daudi na watu wake walipoufikilia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, waume kwa wake, wamechukuliwa mateka. 4 Ndipo Daudi na watu waliokuwa pamoja naye WAKAINUA SAUTI ZAO NA KULIA, HATA WALIPOKUWA HAWANA NGUVU ZA KULIA TENA 5 Na hao wake wawili wa Daudi walikuwa wamechukuliwa mateka, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, aliyekuwa mkewe Nabali, wa Karmeli ”.
1Wafalme 30:1 “Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Siklagi siku ya tatu, hao Waamaleki walikuwa wameshambulia Negebu, na Siklagi, nao wameupiga Siklagi, na kuuchoma moto;
2 NAO WAMEWACHUKUA MATEKA WANAWAKE WALIOKUWAMO WAKUBWA KWA WADOGO; HAWAKUWAUA WO WOTE, ILA WAKAWACHUKUA, WAKAENDA ZAO.
3 Basi Daudi na watu wake walipoufikilia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, waume kwa wake, wamechukuliwa mateka.
4 Ndipo Daudi na watu waliokuwa pamoja naye WAKAINUA SAUTI ZAO NA KULIA, HATA WALIPOKUWA HAWANA NGUVU ZA KULIA TENA
5 Na hao wake wawili wa Daudi walikuwa wamechukuliwa mateka, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, aliyekuwa mkewe Nabali, wa Karmeli ”.
Sasa baada ya Daudi na wenzake kulia mpaka machozi yalipoisha ni kitu gani kilitokea….tuendelee…
6 Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE. 7 Kisha Daudi akamwambia Abiathari, kuhani, mwana wa Ahimeleki, Tafadhali niletee hapa hiyo naivera. Naye Abiathari akamletea Daudi naivera huko. 8 Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote…………….. 16 Na hapo alipokuwa amewaongoza chini, tazama, hao walikuwa wametawanyika juu ya nchi yote, wakila na kunywa, na kufanya karamu, kwa sababu ya hizo nyara kubwa walizochukua katika nchi ya Wafilisti, na katika nchi ya Yuda. 17 Naye Daudi akawapiga tangu ukungu wa jioni hata jioni ya siku ya pili; hakuna aliyeokoka, ila vijana mia nne waliopanda ngamia na kukimbia. 18 DAUDI AKAWAPOKONYA WOTE WALIOKUWA WAMECHUKULIWA NA WAAMALEKI; NAYE DAUDI AKAWAOKOA WAKEZE WAWILI. 19 Wala hawakupotewa na kitu, mdogo wala mkubwa, wana wala binti, nyara wala cho chote walichojitwalia hao; Daudi akavirudisha vyote”.
6 Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.
7 Kisha Daudi akamwambia Abiathari, kuhani, mwana wa Ahimeleki, Tafadhali niletee hapa hiyo naivera. Naye Abiathari akamletea Daudi naivera huko.
8 Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote……………..
16 Na hapo alipokuwa amewaongoza chini, tazama, hao walikuwa wametawanyika juu ya nchi yote, wakila na kunywa, na kufanya karamu, kwa sababu ya hizo nyara kubwa walizochukua katika nchi ya Wafilisti, na katika nchi ya Yuda.
17 Naye Daudi akawapiga tangu ukungu wa jioni hata jioni ya siku ya pili; hakuna aliyeokoka, ila vijana mia nne waliopanda ngamia na kukimbia.
18 DAUDI AKAWAPOKONYA WOTE WALIOKUWA WAMECHUKULIWA NA WAAMALEKI; NAYE DAUDI AKAWAOKOA WAKEZE WAWILI.
19 Wala hawakupotewa na kitu, mdogo wala mkubwa, wana wala binti, nyara wala cho chote walichojitwalia hao; Daudi akavirudisha vyote”.
Unapofika wakati umeishiwa nguvu, huo ndio wakati wa KUJITIA NGUVU!.. kwasababu maandiko yanatufundisha kuwa “tulipo dhaifu, ndipo tulipo na nguvu (2Wakorintho 12:10)”
Laiti Daudi angeendelea kulia pale bila kuchukua hatua yoyote, wale watu wangempiga mawe, au hata wasingempiga kwa mawe, bado asingewapata wake zake na mali zake, lakini ALIPOJITIA NGUVU KWA BWANA ndipo nguvu ikaongezeka kwake na Bwana akamsaidia.
Ukipitia majaribu ya afya jitie nguvu endelea mbele na maombi, pia ishi kwa ujasiri kana kwamba huumwi, na utaona maajabu makuwa….
Ukipitia majaribu ya familia jitie nguvu kwa Bwana endelea na maombi na kutafuta masuluhisho Bwana atakuwa nawe,
Ukipitia majaribu ya watoto au ndoa jitie nguvu kwa Bwana,
Ukipitia majaribu ya huduma jitie nguvu kwa Bwana songe mbele,
Ukipitia majaribu ya kipato vile vile jitie nguvu kwa Bwana songe mbele, zidi kumwomba Bwana wala usikate tamaa, njia itaonekana tu na milango itafunguka, haijalishi umeshapita muda gani… na magumu mengine yote fahamu kuwa ni ya kitambo, lakini ujasiri wako kwa Bwana unahusika sana huo wakati.
JIPE MOYO MKUU.
USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.
NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?
Kwanini kuna mrudio wa uumbaji kwenye Mwanzo sura ya pili?
LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.
Mungu huwa anasema nasi mara nyingi mioyoni mwetu, lakini huwa hatuzingatii na mwisho wake tunaingia katika matatizo.
Matokeo ya kutozingatia sauti ya Mungu ni makubwa, hebu tujifunze kwa mwana mpotevu, aliyeomba urithi kwa Baba yake.
Luka 15:11 “Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; 12 yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake. 13 Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati”. 14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. 15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe. 16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. 17 ALIPOZINGATIA MOYONI MWAKE, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. 18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako”
Luka 15:11 “Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili;
12 yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake.
13 Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati”.
14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji.
15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.
16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu.
17 ALIPOZINGATIA MOYONI MWAKE, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa.
18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako”
Nataka tuone huo mstari wa 17, unaosema.. “ALIPOZINGATIA MOYONI MWAKE”.
Maana yake tayari sauti ya MUNGU ilikuwa imeshaanza kumsemesha muda mrefu sana moyoni mwake, kwamba njia anayoiendea sio sahihi, mambo anayoyafanya ni mabaya na hivyo ageuke, lakini hakuwa ANAZINGATIA hiyo sauti.
Na kwa kadiri alivyokuwa anaipuuzia ndivyo mambo yalivyozidi kuwa mabaya, mpaka siku alipoamua kuizingatia.
Inawezekana sauti ya MUNGU inasema nawe moyoni mwako muda mrefu (dhamiri inakushuhudia), usiiendee hiyo njia, usiendelee kufanya hayo unayoyafanya, lakini huzingatii, leo anza kuzingatia sauti ya MUNGU, na geuka acha hiyo njia, mrudie Baba yako, mpe Mungu moyo wako…
Mithali 23:26 “Mwanangu, nipe moyo wako; Macho yako yapendezwe na njia zangu”.
Zingatia sauti inayokuambia UOMBE, zingatia sauti inayokuambia ufunge, Zingatia sauti inayokuambia usome Neno, zingatia sauti inayokuambia Usamehe, zingatia sauti inayokuambia mtumikie MUNGU, wakati mwingine zingatia hata sauti unayokuambia uhame hapo ulipo…
Matokeo ya kuikaidi hiyo sauti ni mabaya, ni kama hayo ya Mwana mpotevu na yale ya Yona.
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.
MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;
SAA INAKUJA NA SASA IPO.
SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.
DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?