Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >> https://chat.whatsapp.com/GRri9BATojl2FNGbOJpjC6
Masomo mbalimbali ya Neno la Mungu.
Awali ya yote nakupa hongera kwa kupenda kutafuta kujifunza Neno la Mungu, lipo kusudi la Mungu kukufikisha hapa, biblia inatuambia..
1Timotheo 4:13 “…ufanye bidii katika kusoma…”
Ni wachache sana katika wengi wanaozunguka mitandaoni kutafuta mambo ya msingi kama wewe.
Na unajua nini? bidii yako sio bure, Bwana Yesu alisema,
Mathayo 7:8 “kwa maana kila..atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa”.
Na pia alisema..
Mathayo 5:6 “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa’.
Kwahiyo unachokitafuta Bwana atakupatia, na pengine hata zaidi ya kile ulichokuwa unakitazamia,
Mahali hapa utakutana na masomo mbalimbali ya Neno la Mungu, zaidi ya 1,000, na maswali mengi ya biblia yaliyojibiwa. Kuanzia kitabu cha Mwanzo hadi kitabu cha ufunuo.
Ili kuingia katika horodha ya masomo ya mbalimbali ya Neno la Mungu, fungua hapa>>> MASOMO MAPYA
Ili kusoma maswali ya biblia yaliyoulizwa na kujibiwa fungua hapa >>> MASWALI NA MAJIBU YA BIBLIA
Ili kusoma shuhuda za Mashahidi wa Imani wa kale fungua hapa >>> WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
Je! ulishawahi kujiuliza Unyakuo ni nini, na utakuwaje? Na kwanini Bwana Yesu alisema, Amin! Amin! Nawaambia kizazi hiki hakitapita hata hayo yote yatakapotokea, kusema kule kulimaanisha nini? Tazama hapa >> AMIN, NAWAAMBIA, KIZAZI HIKI HAKITAPITA,
Je! Unafahamu kuwa kanisa tunaloishi mimi na wewe ndio kanisa la Mwisho lijulikanalo kama Laodikia? Tayari makanisa 6 yalishapita, na sasa tupo katika kanisa la mwisho? >>> AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.
https://www.high-endrolex.com/16
Je unafahamu Historia ya nyimbo mbalimbali za Tenzi>> TENZI ZA ROHONI
Je! Unajua Sadaka ni nini? Na umuhimu wake kwetu>> NGUVU YA SADAKA.
Je! Unajua aina za upendo, na upi tunapaswa tuwe nao?>> UPENDO NI NINI ?
Fahamu juu ya chukizo la uharibifu lililozungumziwa na Danieli na Bwana Yesu >> CHUKIZO LA UHARIBIFU
Ijue siku ya Bwana itakuwaje>> KIAMA KINATISHA.
Kwanini shetani aitwe nyoka wa zamani >> YULE JOKA WA ZAMANI.
Mbinguni ni wapi? Na je kuna aina ngapi za mbingu>> MBINGUNI NI WAPI?
Kuna siri gani katika kitabu cha Ruthu, kwanini kiandikwe na wakati yeye hakuwa mwanamke wa Kiyahudi, >>> MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:
Ni siri gani imelala katika kitabu cha Esta juu ya Kristo na kanisa lake? >>> ESTA: Mlango wa 1
Mfahamu Melkizedeki, Je! alikuwa ni nani? Na kwanini awe hana baba wala mama, wala mwanzo wa siku wala mwisho? >>HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?
Utawala wa miaka 1000 ni utawala gani? >>> UTAWALA WA MIAKA 1000.
Kitabu cha Danieli kina maudhui gani? Je naweza kupata uchambuzi wake tangu mwanzo hadi mwisho? >>> DANIELI: Mlango wa 1
Ubatizo sahihi ni upi? Kulingana na maandiko. >> UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?
Nahitaji kuokoka je nifanyaje?. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Kama utapenda masomo haya yawe yanakufikia kwa njia ya email/ whatsapp tutumie ujumbe katika namba hii :+255693036618 / +255 789001312
Print this post
kuota unatoka damu ya hedhi inamaanisha nini kibiblia?
Yapo mambo mawili;
Jambo la kwanza unapaswa ujue asilimia kubwa ya ndoto tunazoziota kila siku, si zote zina tafsiri ya rohoni kukusaidia, naweza kusema asilimia hata 90 ya unavyoviota kila siku vinatokana na ubongo wako wenyewe.
Ubongo wako Mungu kauumba kwa namna ambayo unaweza kuhifadhi kumbukumbu ya mambo unayofanya karibu kila siku, au mambo ambayo ulishawahi kuyapitia au mazingira ambayo ulishawahi kuyoana au kuwepo..
Kwahiyo katikati ya hayo yote, Ubongo wako utajiundia matukio na kuyachezesha akilini mwako wakati ukiwa umelala.
Biblia inasema hivi..
Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;….”
Umeona? Kwamfano ikiwa wewe kazi yako ni uvuvi na mara nyingi huwa unakesha baharini kuvua, kuota ndoto unajiona unavua au unatengeneza nyavu, itakuwa ni kitu cha kawaida kwako kujirudia rudia mara kwa mara, halikadhalika kwa mpishi, au mwalimu, au mjenzi, kuota anafanya mojawapo ya ujuzi wake, litakuwa ni jambo la kawaida sana.
Vilevile katika hizo zipo ndoto ambazo zinaotwa na jinsia husika tu, kwamfano kuota unajifungua, hizi ndoto huwezi sikia zikiotwa na mwanaume, vivyo hivyo na kuota unatoka damu ya hedhi ni ndoto zinazowahusu wanawake peke yao, mwanaume hawezi kuota hivyo kwasababu jambo kama hilo hajawahi kulipitia katika Maisha yake yote,
Kwahiyo ndoto kama hii ikikujia isikusumbue sana. Elewa ni ndoto itokanayo na mazingira unayopitia.
Lakini pia jambo la pili ni kuwa.. Mungu anaweza kuzungumza na sisi, pia kwa njia hizo hizo za ndoto za mazingira yetu ya kila siku.
Kwamfano katika biblia utaona kulikuwa na wafungwa wawili waliokuwa gerezani na Yusufu, mmoja alikuwa anafanya kazi ya kumnywesha mfalme, na wa pili alikuwa ni mpishi. Siku moja wote wawili wakaota ndoto, na ndoto walizoota zililandana na mazingira yao ya kazi.. Lakini zilikuwa zimebeba ujumbe mzito kutoka kwa Mungu.
Mwanzo 40:5 “Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. 6 Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika. 7 Akawauliza hao maakida wa Farao, waliokuwa pamoja naye katika kifungo, nyumbani mwa bwana wake, akisema, Mbona nyuso zenu zimekunjamana leo? 8 Wakamwambia, Tumeota ndoto wala hapana awezaye kuifasiri. Yusufu akawaambia, Kufasiri si kazi ya Mungu? Tafadhalini mniambie. 9 Mnyweshaji mkuu akamhadithia Yusufu ndoto yake; akamwambia, Katika ndoto yangu nimeota, uko mzabibu mbele yangu. 10 Na katika mzabibu mlikuwa na matawi matatu, nao ulikuwa kana unamea, unachanua maua, vishada vyake vikatoa zabibu zilizoiva. 11 Na kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, nikampa Farao kikombe mkononi mwake. 12 Yusufu akamwambia, Tafsiri yake ndiyo hii. Matawi matatu ni siku tatu. 13 Baada ya siku tatu Farao atakiinua kichwa chako, atakurudisha katika kazi yako; nawe utampa Farao kikombe mkononi mwake, kama desturi ya kwanza, ulipokuwa mnyweshaji wake…….. 16 Mkuu wa waokaji alipoona ya kwamba hiyo tafsiri ni ya mema, akamwambia Yusufu, Mimi kadhalika nilikuwa katika ndoto yangu, na tazama, ziko nyungo tatu za mikate myeupe juu ya kichwa changu. 17 Na katika ungo wa juu, mlikuwa na kila namna ya chakula kwa Farao, kazi za mwokaji; ndege wakavila katika ungo juu ya kichwa changu. 18 Yusufu akajibu, akasema, Tafsiri yake ndiyo hii Nyungo tatu ni siku tatu..
Mwanzo 40:5 “Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani.
6 Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika.
7 Akawauliza hao maakida wa Farao, waliokuwa pamoja naye katika kifungo, nyumbani mwa bwana wake, akisema, Mbona nyuso zenu zimekunjamana leo?
8 Wakamwambia, Tumeota ndoto wala hapana awezaye kuifasiri. Yusufu akawaambia, Kufasiri si kazi ya Mungu? Tafadhalini mniambie.
9 Mnyweshaji mkuu akamhadithia Yusufu ndoto yake; akamwambia, Katika ndoto yangu nimeota, uko mzabibu mbele yangu.
10 Na katika mzabibu mlikuwa na matawi matatu, nao ulikuwa kana unamea, unachanua maua, vishada vyake vikatoa zabibu zilizoiva.
11 Na kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, nikampa Farao kikombe mkononi mwake.
12 Yusufu akamwambia, Tafsiri yake ndiyo hii. Matawi matatu ni siku tatu.
13 Baada ya siku tatu Farao atakiinua kichwa chako, atakurudisha katika kazi yako; nawe utampa Farao kikombe mkononi mwake, kama desturi ya kwanza, ulipokuwa mnyweshaji wake……..
16 Mkuu wa waokaji alipoona ya kwamba hiyo tafsiri ni ya mema, akamwambia Yusufu, Mimi kadhalika nilikuwa katika ndoto yangu, na tazama, ziko nyungo tatu za mikate myeupe juu ya kichwa changu.
17 Na katika ungo wa juu, mlikuwa na kila namna ya chakula kwa Farao, kazi za mwokaji; ndege wakavila katika ungo juu ya kichwa changu.
18 Yusufu akajibu, akasema, Tafsiri yake ndiyo hii Nyungo tatu ni siku tatu..
Ukiendelea kusoma pale utaona ni kweli, mambo hayo yaliwakuta vilevile kama Yusufu alivyowatafsiria.
Unaona sasa “point” hapo ni kuwa walichoota kiliendana na kazi zao au mazingira yao ya kila siku, yule wa kwanza alikuwa ni mnyweshaji wa mfalme akajiona anaweka divai mezani pa mfalme, kutoka katika mzabibu, ..Yule mwingine ni mpishi, aliona mikate kichwani pake.
Vivyo hivyo na wewe kuota unatoka damu ya hedhi, mara mara, na tena kama ndoto hiyo inakujia kwa uzito Fulani basi ujue upo ujumbe mzito Mungu wa Mungu nyuma yake.. Na ujumbe huo unatoka kwenye biblia.
Sasa ipo Habari moja ambayo pengine ulishawahi kuisikia, lakini leo hii nataka uifuatilie tena kwa ukaribu. Habari yenyewe ni kuhusu yule mwanamke aliyekuwa anatokwa na damu kwa muda mrefu wa miaka 12. Tusome;
Luka 8:43 “Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote, 44 alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma. 45 Yesu akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana, Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya wanakuzunguka na kukusonga. 46 Yesu akasema, Mtu alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka. 47 Yule mwanamke, alipoona ya kwamba hawezi kusitirika akaja akitetemeka, akaanguka mbele yake, akamweleza mbele ya watu wote sababu yake ya kumgusa, na jinsi alivyoponywa mara. 48 Akamwambia Binti, imani yako imekuponya; enenda zako na amani”.
Luka 8:43 “Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote,
44 alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.
45 Yesu akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana, Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya wanakuzunguka na kukusonga.
46 Yesu akasema, Mtu alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka.
47 Yule mwanamke, alipoona ya kwamba hawezi kusitirika akaja akitetemeka, akaanguka mbele yake, akamweleza mbele ya watu wote sababu yake ya kumgusa, na jinsi alivyoponywa mara.
48 Akamwambia Binti, imani yako imekuponya; enenda zako na amani”.
Umeona mwanamke huyu, tatizo lililomsumbua kwa muda mrefu, lilimgharimu pesa nyingi, kwa waganga, halikuweza kutatuliwa na mtu mwingine yeyote isipokuwa YESU TU PEKE YAKE.
Jiulize kwanini liwe ni kutokwa na damu, na si kingine?
Wewe unaota kutokwa na damu, jiweke katika nafasi ya huyo mwanamke, na ujue leo ni mahali gani sahihi pa kukimbilia.
Kama wewe hujaokoka, na unadhani dunia itakuwa ni jibu la Maisha yako, au utatuzi wa matatizo yako, leo hii ujue Mungu anasema na wewe kuwa UMEMWACHA YESU APITE.
Mungu anakuonyesha YESU tu ndio jibu la Maisha yako, haijalishi wewe ni muislamu, au dini gani,..Ni Yesu tu pekee ndiyo kila kitu kwako. Na anachotaka tu ni ushike pindo la vazi lake, aiponye roho yako.
Maana ya Kushika pindo la vazi lake, ni kuonyesha kuwa unahitaji msaada, hivyo hapo ulipo kama Maisha yako yapo dhambini, basi tubu leo, mpe Bwana Yesu Maisha yako. Na atakupokea na ataiponya roho yako, na hata mwili wako ikiwa una matatizo.
Hivyo ikiwa upo tayari kutubu leo na kutaka akufanye kuwa kiumbe kipya, akuponye misiba yako, akupe tumaini jipya, hata kama wewe ni muislamu, basi uamuzi huo ni wa busara sana. Hivyo fungua hapa Kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Jiunge na kundi la whatsapp kwa kubofya chini;
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tazama masomo mengine chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au kwa namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
JE! DAMU INA UMUHIMU WOWOTE KATIKA MAISHA?
DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?
MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.
KUOTA NYOKA.
Rudi Nyumbani:
WhatsApp
Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/FgA1HWRFZWH4IqqLunFGcs
Mistari ya biblia kuhusu ndoa ni ipi?
Ndoa ni tendo ambalo Mungu aliliumba kwa makusudi kabisa, ili kumpa mwanadamu picha ya jinsi ndoa yake halisi itakavyokuwa kati ya yeye na watu wake, baada ya ulimwengu huu kuisha.
Uhusiano walio nao mke na mume, ni mfano mdogo sana wa uhusiano atakaokuwa nao Mungu na watu wake watakaoshinda, katika mbingu mpya na nchi mpya.
Hivyo tutaitazama mistari michache ihusuyo ndoa za kibinadamu, na vilevile tutaitazama mistari michache ihusuyo ndoa ya ki-mbinguni(yaani Kristo na kanisa lake).
Mwanzo 2:24 “Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja”
Waefeso 5:25 “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake”;
Waefeso 5:33 “Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe”
Mithali 5:18 “…. Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako”
Waefeso 4:2 “kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; 3 na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani”.
Marko 10:9 “Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe”
Wimbo 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu. 7 Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa”.
Wimbo 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu.
7 Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa”.
Waebrania 13:4 “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu”.
Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu. 19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana”.
Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.
19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana”.
Mithali 31:10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani”.
Mhubiri 4:9 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao. 10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua! 11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto”?
Mhubiri 4:9 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto”?
Mathayo 19:6 “Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe”
1Petro 3:7 “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe”
Malaki 2:16 “Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli…”
Ruthu 1:16 “Naye Ruthu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu; 17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe nami”.
Ruthu 1:16 “Naye Ruthu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu;
17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe nami”.
Yohana 13:34 “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo”.
1Wakorintho 13:4 “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya”;
1Wakorintho 13:4 “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya”;
Malaki 2:14 “Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako. 15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana”.
Malaki 2:14 “Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako.
15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana”.
Mistari ya biblia kuhusu ndoa ya;
Isaya 54:5 “Kwa sababu Muumba wako ni mume wako; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote”.
2Wakorintho 11:2 “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi”.
Ufunuo 19:9 “Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.
Ufunuo 21:1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe”.
Ufunuo 21:1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.
2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe”.
Luka 14:24 “Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.
Luka 5:34 “ Lakini Yesu akawaambia, Je! Mwaweza kuwafanya wafunge walioalikwa arusini, akiwapo bwana arusi pamoja nao”?
Ufunuo 21:9 “…Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo”.
Mathayo 25:1 “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.3 Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.13 Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.
Mathayo 25:1 “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.
2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.
3 Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;
4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.
5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.
6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.
7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.
9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.
10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.
12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.
13 Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.
Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.
Hivyo ni wajibu wetu mimi na wewe kuhakikisha kwa gharama zozote hatuikosi hii karamu ya mwana-kondoo mbinguni, Kumbuka kama tunavyojua huwa kinaanza ndoa kisha baadaye karamu,.vivyo hivyo na kwa Mungu pia, inaanza kwanza ndoa, ambayo Kristo anafunga na watakatifu wake hapa hapa duniani, na baadaye atawanyakua kwenda nao kula naye karamu kule mbinguni.
Kwa mapana na marefu juu ya somo hili la karamu ya mwanakondoo, angalia somo lililoorodheshwa chini baada ya hili; Lakini kikubwa zaidi, ni kuwa tuhakikishe na sisi ni bibi-arusi ambao wapo tayari kumkojea Bwana wao aje waende karamuni.
Na tunakuwa bibi-arusi kwa kumwamini Yesu, na kubatizwa, na kuishi maisha yampendezayo.
Ikiwa utapenda tukuunge kwenye group la mafundisho ya biblia,Whatsapp: basi utatutumia ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
KARAMU YA MWANA-KONDOO.
MAFUNDISHO YA NDOA.
UTAWALA WA MIAKA 1000.
MJI WENYE MISINGI.
NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.
HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MIHURI SABA
Historia ya nyimbo KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili~ Tis So Sweet to Trust in Jesus.
Wimbo huu uliandikwa na mwanamke mkristo wa kiingereza aliyeitwa, Louisa M. Stead, Mnamo mwaka 1882, Ni wimbo unaoeleza furaha mtu anayoweza kuipata katika kumtegemea Kristo, Lakini nyuma ya uandishi wa wimbo huu, imelala historia nzito ya Maisha aliyopitia Louisa M stead,
Ilikiwa ni siku moja Louisa na mumewe Pamoja na mtoto wao wa kike aliyeitwa Lily, walipanga safari ya kwenda matembezi, wakiwa ufukweni mwa kisiwa kimoja ghafla walisikia sauti kama ya mtu inapiga kilele za kuzama, kwenda kukimbia kuangalia wakamwona kijana mmoja, hilo lilimfanya mume wa Louisa, ajaribu kwenda kumwokoa, lakini katika jitihada zake za kufanya hivyo kwa bahati mbaya wote wawili wakazama, wakafa (kijana Pamoja na mume wake), mbele ya macho ya Louisa na binti yake.
Maisha yao baada ya hapo yalianza kuporomoka, Maisha yakawa magumu, Lakini wakagundua kuwa Mungu hakuwaacha katika hali zao, aliwatimizia mahitaji yao, hapo ndipo Louisa na binti yake walijifunza kumtegemea Mungu, na ndipo akauandika wimbo huu;
*****
Baadaye Louisa na binti yake wakasafiri kwenda Afrika kusini kwa kazi ya umishionari.
Lakini ni nini tunajifunza katika wimbo huu na uandishi wake?
Mimi na wewe tunaweza tukawa hatujapitia katika hali ngumu kama aliyopitia yeye, lakini yeye aliyeyapitia amemwona Mungu akimpigania, mpaka anaimba na kusema, “Nimemwona thabiti”..Hiyo ni kuonyesha kuwa hata wewe ukimwamini Yesu na kumtegemea, ..Utamwona thabiti/hakika akiwa na wewe katika maisha yako haijalishi leo unapitia mahali pagumu kiasi gani.
Imba wimbo huu ukikumbuka matendo yote makuu aliyokutendea nyuma. Na hakika utausikia uwepo wake nafsi mwako.
Tazama chini historia za nyimbo nyingine za Tenzi.
Tafadhali share na wengine.
NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics
MWAMBA WENYE IMARA
USINIPITE MWOKOZI Lyrics
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
CHA KUTUMAINI SINA lyrics
UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.
UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.
NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?
Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate ‘Neno la siku’ kila asubuhi. Na mistari mingine mingi ya faraja ..kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/GRri9BATojl2FNGbOJpjC6
Mistari ya biblia ya uponyaji.
Inawezekana wewe ni mgonjwa na pengine unapitia katika hali ya kukata tamaa kabisa ya kupona, au unao ugonjwa usioponyeka mfano Ukimwi au Kansa, lakini nataka nikuambie jambo moja, kwa mwanadamu ni kweli haiwezekani lakini kwa Mungu hakuna linaloshindikana,
Hapo kabla nilikuwa ninasikia tu shuhuda za watu wengine kuponywa, nikadhani pengine mimi sistahili, lakini nilipokuwa katika dhambi siku moja Yesu Kristo aliniponya ugonjwa wangu wa sikio uliokuwa unanisumbua kwa muda mrefu, Na hapo ndipo ulipokuwa mwanzo wa kumtazama Kristo kwa sura nyingine, na kuendelea hapo aliniponya mara kadhaa tena katika vipindi tofauti tofauti nilipougua..Kama alinifanyia mimi niliyekuwa na dhambi, atakufanyia na wewe pia.
Kwa maana Yesu mwenye upendo yeye mwenyewe alituambia hivi..
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.
Hivyo nawe pia unapoitafakari mistari hii, nakuombea kwa Mungu ikafanyike Uponyaji mkubwa ndani ya mwili wako na maisha yako kwa ujumla, katika jina la YESU KRISTO.
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. 2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. 3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.
Zaburi 30:2 “Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya”.
Ufunuo 21:4 “Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita”.
2Wafalme 20:5 “Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa Bwana”.
Zaburi 146:8 “Bwana huwafumbua macho waliopofuka; Bwana huwainua walioinama; Bwana huwapenda wenye haki”;
3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”.
Yeremia 17:14 “Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu”.
Zaburi 118:17 “Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana”.
Zaburi 119:50 “Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imenihuisha”.
Mathayo 8:17 “ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu”.
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Mathayo 14:14 “Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao”.
Yeremia 30:17 “Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye”.
Isaya 57:18 “Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia. 19 Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema Bwana; nami nitamponya”.
1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.
Mathayo 9:35 “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina”.
Yakobo 5:14 “Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana”.
Zaburi 6:2 “Bwana, unifadhili, maana ninanyauka; Bwana, uniponye, mifupa yangu imefadhaika”.
Mathayo 8:1 “Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. 2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa. 3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika”.
Mathayo 8:1 “Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.
2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.
3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika”.
2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwafuraha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu”.
Zaburi 107:19 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao, 21 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.”.
Zaburi 107:19 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao,
21 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.”.
Zaburi 103:2 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote. 3 Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote”
Zaburi 103:2 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote.
3 Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote”
Kumbukumbu 7:15 “Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako maradhi yo yote mabaya uyajuayo ya Misri, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao”.
Hosea 14:4 “Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha”.
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. 2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; 3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
Amini!, Endelea kuamini, uponyaji wako hakika umekufukia.
Tafadhali Share, na kwa wengine ujumbe huu wa faraja,.
Pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya biblia kwa njia ya email au kwa Whatsapp tutumie ujumbe kwa namba hii: +255693036618 / +255789001312
YESU MPONYAJI.
Aponywa Ukimwi.
Ameponywa kansa iliyokuwa katika hatua ya Nne.
RABI, UNAKAA WAPI?
MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.
Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. Na mistari mingine mingi ya faraja ..kwa link hii >> https://chat.whatsapp.com/GRri9BATojl2FNGbOJpjC6
Mistari ya biblia kuhusu upendo.
Upendo ndio nguzo ya kwanza katika Ukristo. Unaweza ukawa na vyote, lakini ukikosa upendo wewe mbele za Mungu si kitu kabisa,
Biblia inazungumza juu ya upendo wa aina 4:
1 Wakorintho 13:1-8 1 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. 4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
1 Wakorintho 13:1-8
1 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo. (1Yohana 4:8)
Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.(1Petro 4:8)
Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. 35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi. (Yohana 13:34-35)
Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi. (Yohana 13:34-35)
Kuchukiana huondokesha fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote. (Mithali 10:12)
Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. (1Yohana 4.11)
Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.(1Wakoritho 16:14)
Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana. Ninyi waume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao.(Wakolosai 3:18-19)
Kitambo kidogo tu nikiisha kuwaondokea, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena, Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu, Chumbani mwake aliyenizaa. (Wimbo 3:4)
Mkono wake wa kushoto ungekuwa chini ya kichwa changu, Nao wa kuume ungenikumbatia. (Wimbo 8:3)
Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu.( Wimbo 8: 6)
Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe. (Marko 10:6-9)
Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.
Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe. (Marko 10:6-9)
Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi, wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi. Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang’anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu. Mpe kila akuombaye, na akunyang’anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.( Luka 6:27-30)
Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi,
wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.
Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang’anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.
Mpe kila akuombaye, na akunyang’anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.( Luka 6:27-30)
Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo? Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu. (Mathayo 5:43-48)
Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu. (Mathayo 5:43-48)
Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake. (Warumi 12:20-21)
Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.(Warumi 12:21)
Upendo huu ndio upendo wa hali ya juu kuliko yote (Agape), upendo wa kujitoa wakfu, usiojali hali, usiojali uzuri au ubaya wa mtu, usio na chembe yoyote ya mapungufu, Upendo wa Mungu.
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (Yohana 3:16)
Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye.
Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu. (1Yohana 4:9-12)
Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.
Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.
Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu. (1Yohana 4:9-12)
Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza. (1Yohana 4:19)
Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. (Yohana 15:12-13)
Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi.
Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. (Yohana 15:12-13)
Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu; (Kumbukumbu 7:9)
Hivyo mimi na wewe ili Upendo wa namna hii uingie ndani yetu, Ni sharti kwanza tumpende yeye mwenye Upendo huo.
Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. (1Yohana 4:16)
Hiyo ndilo kusudi la kwanza la sisi kuwepo hapa duniani..Kumpenda Yeye.
Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja; nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. (Marko 12:29-30)
Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;
nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. (Marko 12:29-30)
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?
Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?
YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.
Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..
Kuota upo kanisani inamaanisha nini kimaandiko?
Hiyo ni ndoto njema itakayo kwa Mungu. Kamwe shetani hawezi kukuotesha ndoto ya namna hiyo..
Kama umeota ndoto hii kuna mawili. La kwanza ikiwa wewe ni mkristo uliyeokoka na umesimama imara, Hapo ni Mungu anakuonyesha kuwa upo katika njia sahihi, hivyo endelea kumtafuta Bwana kwa bidii Zaidi kwasababu Upo uweponi mwake..Daudi alisema..
Zaburi 122:1 “Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana”.
Kwasababu huko ndipo Mungu alipo. Kanisani na nyumbani mwa Bwana, kwahiyo ukiota upo kanisani ni ishara kuwa inaishi kwa Mungu.
Lakini ikiwa umeiota ndoto hii upo kanisani, na huku nyuma unajijua kabisa hauna mahusiano yoyote na Mungu, au hata kanisani huendi, Maisha yako ni ya dhambi..
Basi ujue hiyo ni sauti ya Mungu, anayokuvuta kwake,..Anakuonyesha kuwa hapo ndipo unapopaswa uwepo, hapo ndipo nyumbani kwako.. Wewe sio wa ulimwengu huu.
Hivyo itii sauti ya Mungu, mgeukie yeye, kwasababu huwezi jua ni kwanini afanye hivyo kwako leo… Kumbuka duniani hapa sisi ni wapitaji pengine kesho inayodhani itakuwepo inaweza isiwe yako.
Hivyo fanya uamuzi haraka wa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuucha ulimwengu moja kwa moja, na ukifanya hivyo YESU atakusamehe, Fahamu hiyo ndoto inatoka kwa kwa Mungu kabisa hivyo usiipuuzie. Mungu huwa anazungumza na watu wakati mwingine hata Zaidi ya mara moja.
Ayubu 33: 14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. 15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani”;
Ayubu 33: 14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani”;
Pengine Mungu alishazungumza na wewe kwa njia mbalimbali utubu dhambi zako umgeukie. Leo hii usiifanye shingo yako kuwa ngumu.
Kama upo tayari kuokoka na kuanza Maisha mapya na Yesu Kristo basi huo utakuwa ni uamuzi wa busara sana kwako..Unaweza kusema mimi mboni ni muislamu, haijalishi wewe ni nani, Mungu anakuita, kwasababu amekuchagua wewe na anakupenda, na anataka kukuokoa upate uzima wa milele..Hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Na hayo mengine yaliyosalia Bwana atakusaidia kuyashinda.
NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?
KUOTA UPO UCHI.
Hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge.(Ufu 21:27)
FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.
Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?
Kuota umechomwa kisu au Kuota umepigwa risasi kuna maanisha nini?
Awali, ni vyema kujua kuwa si kila ndoto aotayo mtu, ina maana katika maisha yake, Hilo ni vizuri ukalifahamu, Ndoto nyingi tunazoziota kila siku zinatokana na shughuli zetu za kila siku (Mhubiri 5:3), au mazingira yanayotuzunguka, au mambo ambayo tunayawaza mara kwa mara, au tulishawahi kuyaona, au kuyapitia sehemu Fulani katika maisha yetu (Isaya 29:8)..
Naweza kusema asilimia 90 ya ndoto tunazoziota kila siku zinaangukia katika kundi hili,.Hapo ndipo watu wengi wanaposhindwa kuelewa, wanataka kila ndoto wapate tafsiri ya rohoni, au maishani, hilo jambo halipo, utaishia kudanganywa, au kujidanganya mwenyewe, Kumbuka kinachoweza kueleza hatma ya maisha yetu kwa ufasaha wote, sio ndoto tunazoziota usingizini, bali Neno la Mungu tunaloliishi kila siku.
Mungu anaziita ndoto kama makapi ukifananisha na Neno lake(Yeremia 23:28-29). Akiwa na maana kuwa mtu Yule anayeishi kwa kulishika Neno lake, Ni bora kama ngano, kuliko yule anayetafuta maana za ndoto zilizofananishwa na makapi.
Ni mara chache, ndoto zinabeba ujumbe, ili kutambua ndoto yako inatoka kwa Mungu au kwa shetani, au kwako mwenyewe, basi fungua hapa usome kwanza>>> Nitajuaje kama ndoto ni ya Mungu au ya Shetani?
KUOTA UMECHOMWA KISU/KUOTA UMEPIGWA RISASI.
Hivyo ukiwa umeshasoma, na unao uhakika kabisa kuwa ndoto uliyoota, si ya kawaida, imekujia kwa uzito mwingine wa kitofauti, imekushtua sana, imeonekana kama ni jambo la halisi kabisa, basi upo ujumbe wa rohoni.
Sasa kwa namna ya kawaida, ukishaona mpaka mtu amefikia hatua ya kukuchoma kisu, au amekupiga risasi ni wazi kuwa kuna jambo ulilifanya, au unalifanya sasa hivi, ambalo limemchukiza sana, kiasi cha kufikia uamuzi wa kuona kufa kwako ni bora kuliko kuishi.
Vivyo hivyo katika ndoto ukiona umepigwa risasi, au umechomwa kisu, au upanga, au mkuki,au kitu chenye ncha kali, hiyo ni ishara kuwa maishani mwako, lipo jambo ambalo unalifanya, halifurahiwi na wengine, aidha ni zuri au baya,
Katika biblia tunasoma habari ya mtu mmoja, aliyeitwa Egloni mfalme wa Boabu, huyu, aliwatumikisha Israeli kwa muda wa miaka 18, na hiyo yote ilikuwa ni kutokana na makosa yao wenyewe(Israeli)..Lakini walipomlilia Mungu, awaokoe kutoka katika utumwa na mateso ya mfalme huyu, Mungu akawasikia ndipo akawapelekea mwokozi aliyeitwa Elihu.
Huyu Elihu alijifanya kama mjumbe, aliyeituwa na Israeli, kumbe hila zake zilikuwa ni kwenda naye katika chumba cha siri, ili wakiwa wao wawili peke yao achomoe upanga wake na kumchoma tumboni, Tusome kidogo..
Waamuzi 3:20 “Basi Ehudi akamwendea; naye alikuwa anaketi peke yake katika chumba chake cha baridi. Ehudi akasema, Mimi nina ujumbe utokao kwa Mungu kwako wewe. Basi akainuka katika kiti chake. 21 Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake; 22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma. 23 Ndipo Ehudi akatoka nje barazani, akamfungia milango ya hicho chumba na kuifunga kwa ufunguo. 24 Basi alipokuwa amekwisha toka nje, hao watumishi wake wakaenda; wakaona, na tazama, hiyo milango ya chumba ilikuwa imefungwa kwa ufunguo; nao wakasema, Hapana budi amejifunika miguu yake ndani ya chumba cha baridi. 25 Wakangoja hata wakatahayari; na tazama, hakuifungua milango ya chumba; basi wakatwaa ufunguo, na kuifungua; na tazama, bwana wao alikuwa ameanguka nchi, naye amekufa”.
Waamuzi 3:20 “Basi Ehudi akamwendea; naye alikuwa anaketi peke yake katika chumba chake cha baridi. Ehudi akasema, Mimi nina ujumbe utokao kwa Mungu kwako wewe. Basi akainuka katika kiti chake.
21 Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake;
22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma.
23 Ndipo Ehudi akatoka nje barazani, akamfungia milango ya hicho chumba na kuifunga kwa ufunguo.
24 Basi alipokuwa amekwisha toka nje, hao watumishi wake wakaenda; wakaona, na tazama, hiyo milango ya chumba ilikuwa imefungwa kwa ufunguo; nao wakasema, Hapana budi amejifunika miguu yake ndani ya chumba cha baridi.
25 Wakangoja hata wakatahayari; na tazama, hakuifungua milango ya chumba; basi wakatwaa ufunguo, na kuifungua; na tazama, bwana wao alikuwa ameanguka nchi, naye amekufa”.
Umeona? Sasa huyu Elgoni alichomwa kutokana na makosa yake, lakini, pia wapo wengine waliochomwa kutokana na haki zao, mfano mmojawapo ni Bwana wetu YESU KRISTO..Yeye alichomwa mkuki pale msalabani, sio kwasababu alikuwa mwovu hapana.
Hivyo na wewe jiangalie ni wapi katika maisha yako, pana vita kwa wengine, wewe umesimama, Ikiwa upo ndani ya Kristo basi, ujue maadui wa imani wapo, lakini huna haja ya kuogopa, Kwasababu Mungu atakupigania, kikubwa unachopaswa ufanye ni kuzidi kuwa mwombaji.
Lakini kama upo nje ya Kristo, ukweli ni kwamba, licha tu kuzungukwa na hatari za maadui, lakini, maisha yako ya rohoni yapo hatarini.. Mungu anaweza kweli kukuepusha na hatari za mwilini, lakini zile za rohoni za ibilisi hawezi kukuzuia kutokana na kwamba wewe ni milki ya ibilisi.
Jiulize ukifa leo ghafla katika dhambi utakuwa mgeni wa namna huko uendako?
Hivyo ndugu ikiwa unahitaji kumpa leo YESU maisha yako..Basi uamuzi huo utakuwa ni busara sana kwako, Kama upo tayari kufanya hivyo, moja kwa moja fungua hapa, kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Na hayo mengine yaliyosalia Mungu atakujalia rehema zake.
Kwa mafundisho zaidi ya Neno la Mungu.
Whatsapp: +255 789001312
Kuota unafanya Mtihani.
KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.
HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?
NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.
ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.
Kuabudu Sanamu ni nini? Na ibada za sanamu ni zipi?
Kuabudu sanamu: Katika agano la kale ni kitendo chochote cha kwenda kuabudu au kusujudia, au kutumika kitu kingine chochote, tofauti na Mungu mkuu mmoja aliye hai (YEHOVA).
Moja ya amri 10 Mungu alizowapa wana wa Israeli, ilikuwa ni pamoja na kujiepusha na ibada za sanamu za aina yoyote..
Amri ya pili inasema hivi..
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.
Hivyo mtu akikigeuza kitu chochote, kuwa mbadala wa Mungu, huko ni sawa na kuabudu sanamu, ukiweka mdoli nyumbani kwako na kwenda kumpigia magoti na kumwomba kana kwamba ni Mungu, ujue hapo unafanya ibada za sanamu..
Ukitengeneza kinyago chenye sura ya mtakatifu Fulani labda Mariamu, au Bwana Yesu akiwa pale msalabani, kisha ukakihusianisha na mambo ya ibada kwa mfano kukisujudia, au kukiabudu, au kuombea dua zako kwa kupitia hicho, tayari hiyo ni ibada za sanamu,
Ukining’iniza picha ukutani ya mtu Fulani maarufu, au mnyama , au kitu Fulani kwa lengo la kukifanya kama kipatanishi chako na Mungu, au kitu chako kinachoweza kukupa bahati Fulani, hiyo tayari ni ibada za sanamu.
Hata ukipanda mti, au Ua fulani, ukiamini kuwa linaweza kukulinda, au kueleza hatma ya maisha yako, tayari hiyo nayo ni ibada za sanamu.
Kumbukumbu 16:21 “Usipande mti uwao wote kuwa Ashera kwako kando ya madhabahu utakayofanya ya Bwana, Mungu wako.”
Na ni machukizo makubwa sana mbele za Mungu, yanayomtia wivu kiasi cha Mungu kukupatilizia maovu hata ya baba zako, uone ni jinsi gani kitendo hicho kinavyomuudhi Mungu..
Ipo mifano mingi sana katika biblia, ya watu walioadhibiwa kwa makosa kama haya..Kumbuka hili ndilo lililowafanya wana wa Israeli wengi wasiione Kaanani, kadhalika hili ndilo lililochangia wana wa Israeli tena baadaye kuchukuliwa utumwani Babeli.
Hivyo kuhusianisha kitu chochote na Ibada ni hatari sana, Ibada zako zote zinapaswa zimwelekee Mungu peke yake.
JE! KUABUDU SANAMU/IBADA ZA SANAMU KATIKA AGANO JIPYA KUKOJE?.
Tukirudi katika agano jipya, kuabudu sanamu sio tu kwenda kusujudia vinyago tu peke yake n.k., hapana ni Zaidi ya hapo, biblia inasema..
Waefeso 5:5 “Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu”.
Unaona, mtu yeyote ambaye ni mchafu, mbele za Mungu ni mwabudu sanamu, Mtu yeyote aliye na tamaa mbele za Mungu huyu naye ni mwabudu sanamu.
Hawa wote biblia inasema hawana urithi katika ufalme wa Mungu.
Hivyo mimi na wewe tunapaswa tujiepushe na Ibada zote mbili, yaani sanamu za nje, Pamoja na zile Sanamu za ndani. Ili Mungu atupokee tukaurithi uzima wa milele aliyotuandalia tumpendao.
Ikiwa hujaokoka na unataka kufanya hivyo leo, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara kwako. Fungua hapa kwa ajili ya sala ya toba.>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ubarikiwe.
Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?
USIABUDU SANAMU.
CHAPA YA MNYAMA
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
NEEMA YA MZALIWA WA PILI.
Usinipite mwokozi Lyrics| Swahili, – “Pass me not, O Gentle Savior”
Historia ya nyimbo Usinipite mwokozi.
Wimbo huu uliandikwa mwaka 1868, na mwanamke wa kimarekani aliyeitwa Fanny Crosby. Mwanamke huyu mkristo alizaliwa akiwa mzima lakini wiki 8 baada ya kuzaliwa kwake alipatwa na opofu, ambao ulidumu mpaka kufa kwake, lakini katika maisha yake yote aliyoishi hapa duniani (yaani miaka 94), haikuwa bure kwa Mungu wake, alifanikiwa kuandika nyimbo zaidi ya 8,000..Hivyo hiyo ikamfanya apate umaarufu na kumfanya ajulikane kwa jina la “mtunzi-kipofu-wa-nyimbo-za-tenzi”, na “Malkia wa nyimbo za Injili”.
Lakini siku moja alipokuwa amealikwa kwenda kuzungumza na wafungwa wa mji, na alipokuwa akitembea kule gerezani alimsikia mfungwa mmoja akisema “Bwana mwema usinipite, usinigeuzie mgongo wako,unikumbuke”,
Fanny anasema aliguswa sana na maneno yale, jambo ambalo halikuondoka kwenye kichwa chake mpaka alipofika nyumbani. Na huko ndipo alipoandika beti zote nne za wimbo ujulikanao kama USINIPITE MWOKOZI.
Alipomaliza kuuandika akampa muhusika wa kuweka midundo, na mwaka, 1870 wimbo huo, ulizinduliwa rasmi katika machapisho..
Na kwa kipindi kifupi` sana ukapata umaarufu mkubwa duniani kote.
Jambo hili tunaliona kwa wale kipofu wawili waliomsikia Yesu anapita..
Mathayo 9:27 “Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, UTUREHEMU, MWANA WA DAUDI. 28 Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana. 29 Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate”.
Mathayo 9:27 “Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, UTUREHEMU, MWANA WA DAUDI.
28 Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana. 29 Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate”.
Na itakuwa hivyo na kwako:
Ikiwa wewe umeokoka, na unaona unapita katika hali ngumu, ambayo unaona kwa namna ya kawaida huwezi kutoka, basi wakumbuke watu kama hawa, wakutie nguvu,..Zidi kumwita Yesu, atakuonekania kwa wakati wake. Kwasababu yeye anatupenda na kutujali, na yote yanawezekana kwake.
Lakini kama hujaokoka, basi ni vizuri leo ukamwita kwanza mwokozi akuokoe maisha yako, usiruhusu akupite, anapokwenda kuwapa wengine uzima wa milele, sema na mimi leo nauhitaji huo uzima, hivyo kama upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa, kwa ajili ya Sala ya Toba..>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki..
Tazama historia ya nyimbo nyingine za Tenzi chini.
TENZI ZA ROHONI
Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?
MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.
UNYAKUO.