USINIPITE MWOKOZI

USINIPITE MWOKOZI

Usinipite Mwokozi wangu..

Mwanzo 18:1 “Bwana akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari.

2 Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi,

3 akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba USINIPITE SASA MIMI MTUMWA WAKO.

4 Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu.

5 Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema”.

Hapo Ibrahimu Ibrahimu, alitokewa na watu watatu na hakujua kuwa..mmojawapo wa wale watatu alikuwa ni ELOHIMU (MUNGU) mwenyewe na wale wengine wawili waliosalia walikuwa ni malaika watakatifu. Ambao baadaye ndio waliokwenda nchi ya Sodoma na Gomora..Lakini Elohimu ambaye ndiye aliyekuwa mnenaji mkuu alibaki na Ibrahimu nyuma kuzungumza naye..Na Bwana Mungu akamfunulia siri kubwa sana ya jambo analokwenda kulifanya Sodoma na Gomora. Na alipomfunulia siri hizo ndipo akaenda zake.

Hapa Mungu aliamua kujidhihirisha kimwili mbele ya Ibrahimu lakini kwasasa anatembea kwa Roho.

Bwana anatabia ya kutembea huku na huko duniani kote..Sio lazima aonekane kwa macho kama alivyoonekana kwa Ibrahimu…lakini anatembea kwa namna ya Roho..Yaani Roho yake inazunguka duniani kote, inapita Taifa kwa Taifa, inapita mkoa kwa mkoa, mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyuma, inakatiza mpaka vichochoro vyote na kona zote ambazo hata watu hawajafika…inakwenda mpaka katikati  ya mbuga za wanyama na mapori ya ndani, inaingia mpaka kwenye migodi mikubwa na inamfikia mpaka mtu wa mwisho ambaye anapumua ulimwenguni…Ipo inawapeleleza wanadamu kila siku na inafikisha ripoti kwa Mungu. Roho hiyo imejigawanya mara saba (yaani Inatenda kazi kwa namna saba na nyakati saba) na ndio macho ya Mungu.

Zekaria 4:10 “…. hizi saba ndizo macho ya Bwana; yapiga mbio huko na huko duniani mwote”

Na tena biblia inasema katika Ufunuo juu ya Roho hiyo ya Mungu..

Ufunuo 5.6 “Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na macho saba, ambazo ni ROHO SABA ZA MUNGU ZILIZOTUMWA DUNIANI KOTE.

Sasa hii Roho ya Mungu ndiyo inayoZURU watu..kumbuka ni KUZURU na sio KUDHURU..Kudhuru ni kuharibu kitu lakini KUZURU ni KUTEMBELEA KITU.  Hivyo Roho ya Bwana yenyewe inatuZURU (Tembelea) sisi kila siku. Ipo ndani yetu kila siku kila saa, lakini ipo nje inatembea huko na huko kama Mtu atembeavyo. Inatenda kazi kwa namna nyingi.

Sasa inapopita na kukutana na anayestahili Baraka basi anabarikiwa, ikimkuta asiyestahili baraka basi inampita.

Kwahiyo tunaposali ni vizuri pia kuomba…Ee Bwana UNAPOZURU WENGINE kuwapatia Mema…USINIPITE MWOKOZI.

Na pia ni wajibu wetu kujiweka katika usafi, kwasababu kwasababu Mungu ni mwenye haki, hawezi kamwe kumpa mtu asiyestahili haki, ampatie haki…hilo halipo kwa Mungu..vinginevyo atakuwa sio Mungu wa Haki…Ili awe Mungu wa haki ni lazima ampatie mtu kile anachostahili na sio kile asichostahili..Hivyo akikuzuru na kukukuta unafanya uasherati hawezi kukubariki..akikukuta unakula rushwa vile vile hawezi kukubariki…akiyazuru maisha yako na kukukuta unaishia na mwanamume/mwanamke ambaye hamjafunga ndoa atakupita..

Lakini yote katika yote usilisahau Neno hilo katika sala…USINIPITE MWOKOZI, unapozuru wengine…unapowapa wengine thawabu usinipite…Ibrahimu alimwambia Mungu USINIPITE MWOKOZI..Na pia hakumwambia tu kwa midomo bali kwa vitendo kwani tunaona alimtayarishia chakula..Na wewe na mimi ni wajibu wetu kuhakikisha tunamfanya Bwana asitupite kwa lazima..Kwa matendo yetu mema na kwa utoaji wetu tunamwambia Bwana usitupite mwokozi, kama yule mtunzi wa Tenzi alivyoandika.

Ubarikiwe.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

TENZI ZA ROHONI

SALA YA ASUBUHI

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

USIKIMBILIE TARSHISHI.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Yeremia 33:3 (NIITE NAMI NITAKUITIKIA)

Katika kitabu cha Yeremia 33:3 biblia inasema maneno haya…..”Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua”.

Maneno haya ni Mungu aliyazungumza kwa kinywa cha Yeremia, alipokuwa katika gereza alilokuwa amefungwa, wakati huo Mji wa Yerusalemu ulikuwa umeshazungukwa na majeshi ya Nebukadneza, na ndani ya mji kuna njaa kali. Na tayari Bwana alikuwa ameshawaambia penda wasipende watakwenda Babeli tu..utumwani kutokana na maovu yao yasiyokuwa na toba, japokuwa wameonywa miaka mingi watubu lakini wamekataa.

Lakini kama biblia inavyosema “Mungu hatamtupa mtu hata milele (Maombolezo 3:31)”. Maana yake ni kwamba kutakapotokea mitikisiko hata mtu akageuka na kumwacha Mungu na mtu yule akaadhibiwa katika dhambi zake, na mtu yule akatubu mbele za Mungu…Basi Mungu hataishikilia adhabu yake juu ya huyo mtu milele..Itafika kipindi atamrehemu tu…ooh ni Mzuri kiasi gani huyu Mungu wetu?.

Sasa katikati ya kipindi hicho cha kujeruhiwa na Bwana, katikati ya kipindi hicho cha kuumizwa na Bwana kutokana na makosa uliyoyafanya..katikati ya kipindi hicho Bwana alichokuadhibu baada ya kuonywa mara nyingi juu ya uasherati wako, juu ya wizi wako, juu ya ujambazi wako, juu ya ubaya wako wote..upo kipindi unaitumikia Adhabu ya Mungu wako kwa makosa uliyoyafanya..kipindi ambacho maji yapo shingoni..

Ikiwa unatafuta bangili. Kuna kitu kinachofaa kila mwonekano, https://www.swisswatch.is/product-category/rolex/ kutoka kwa kukumbatiana kwa mwili hadi kwa muundo, kutoka kwa cuffs hadi mnyororo na cuffs.Kipindi hicho ndicho anachomwambia Nabii Yeremia kwamba awaambie watu wake..wafikiapo kipindi kama hicho “wamwite Mungu naye atawaitikia”.

Upo taabuni kwa sababu ya dhambi zako..Tubu leo kwa kumaanisha na kiri kuwa umekosa…na wala usione umeonewa wala usijihesabie haki..kubali umestahili adhabu hiyo, kutokana na makosa yako..na Bwana amekuzuia kila kona kila pembe, unaona mauti tu..

Zaburi 107:10 “Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma,

11 Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, Wakalidharau shauri lake Aliye juu.

12 Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa wala hakuna msaidizi.

13 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao”

Baada ya kutubu..Leo hii hili ni Neno lako.

Yeremia 33:3 “Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua”.

Japokuwa umemwasi Bwana kama wana wa Israeli lakini bado lipo tumaini la kuonyeshwa MAMBO MAKUBWA. Japo kuwa unaona umeshakwisha na kupotea kabisa lakini Bwana atakuonyesha MAMBO MAGUMU pia usiyoyajua.

Lakini anachokihitaji kutoka kwako na kwangu..Ni toba kamili kutoka moyoni..Ndio maana amekushusha hivyo lakini yeye moyoni mwake hapendi kuwatesa wanadamu wala kuwahuzunisha kama alivyosema mwenyewe katika Maombolezo 3:33.

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.

MKUU WA ANGA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NI NANI ALIYEWALOGA?

Ni nani aliyewaloga?..Je! nini maana ya kulogwa? na je! wewe nawe umelogwa?

Unaweza kujiuliza swali je! watu wa Mungu wanalogwa?..Jibu ni Ndio! Biblia inasema hivyo wanalogwa..Sasa ni kwa namna gani wanalogwa? Leo tutajifunza ni kwa namna gani wanalogwa.

Kulogwa kwa watu wa Mungu ni tofauti na kule kunakotafsiriwa na watu wa kidunia…Leo ukizungumzia neno kulogwa au kuloga moja kwa moja tafsiri yake ya kwanza inayodhaniwa ni “uchawi ” unahusika….Mtu ambaye hana fedha ni rahisi kudhaniwa kuwa kalogwa kwa nyakati zetu hizi, mtu ambaye ana ugonjwa unaodumu muda mrefu kulingana na kizazi cha sasa ni amelogwa, mtu ambaye ana tatizo la akili huyo kalogwa moja kwa moja, mtu ambaye ana udhaifu fulani ni lazima atakuwa amelogwa n.k

Lakini leo tututazama maana kuu ya neno “kulogwa” kibiblia..yaani kulogwa hasaa ni kupi?

Tusome..

Wagalatia 3:1 “Enyi Wagalatia msio na akili, NI NANI ALIYEWALOGA, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?

2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?

3 Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?”

Ukisoma kitabu hicho cha Wagalatia karibia chote utaona Mtume Paulo kwa uweza wa Roho alikuwa akiwakemea sana wakristo hawa waliokuwepo huko Galatia..KUHUSU MWENENDO WAO WA KUIACHA IMANI, NA KUCHUKULIWA NA MAFUNDISHO MENGINE MAGENI…Wagalatia hawa walianza vizuri na Mungu, walianza kwa kumwabudu Mungu na kushika mafundisho ya kweli ya kumhusu Yesu Kristo, kama walivyofundishwa na Mitume..Lakini baadaye kidogo ghafla wakaanza kuingiliwa na mafundisho mageni na kuyaamini, na kuacha Imani ya kwanza ya kweli ya neno la Kristo.

Hivyo hiyo tabia ya kuiacha Imani ya kwanza na kugeukia mafundisho yadanganyayo ndiyo inayofananishwa na “kulogwa” kibiblia….Na hakuna kulogwa bila mlogaji…Hivyo waliokuwa wanawaloga wakristo hawa waliokuwa Galatia ni waalimu wao wa uongo waliokuwa wanazuka, waliokuwa wanalipindua Neno la Mungu, na kuwafanya watu waenende kidini Zaidi badala ya kuenenda katika kweli ya Neno la Mungu, wanawafundisha watu waishike torati kidini, mambo ambayo ni kinyuma na misingi ya imani iliyo katika Kristo Yesu…hawa ndio wale Mtume Paulo aliwazungumzia katika..

Wafilipi 3:18 “Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;

19 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.

20 Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;

21 atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake”

Watu hawa Mtume Paulo alisema kwa uweza wa Roho kwamba wamelaaniwa ukisoma mwanzoni kabisa mwa kitabu hichi cha Wagalatia..

Wagalatia 1:6 “NASTAAJABU KWA KUWA MNAMWACHA UPESI HIVI YEYE ALIYEWAITA KATIKA NEEMA YA KRISTO, NA KUGEUKIA INJILI YA NAMNA NYINGINE.

7 Wala si nyingine; lakini WAPO WATU WAWATAABISHAO NA KUTAKA KUIGEUZA INJILI YA KRISTO.

8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, NA ALAANIWE.

9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe”

Umeona maana ya kulogwa?..Je na wewe umeiacha Imani na kuigeukia injili ya namna nyingine inayokuambia hakuna kuokoka duniani?..Je umeiacha Imani na kuigeukia injili inayokuambia Mungu haangalii jinsi mtu anavyovaa bali anaangalia moyo wake? Je umeiacha injili inayokuambia pasipo huo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu (Waebr.12:14), na kuigeukia injili inayokuambia bila kuwa mshirika wa dhehebu fulani huwezi kuingia mbinguni?, Je! Umeiacha injili inayokuambia Waasherati, walevi, waabudu sanamu, walawiti, wezi sehemu yao ni katika lile ziwa la moto na kuigeukia injili inayokuambia Mungu hawezi kuwateketeza watu aliowaumba katika ziwa la moto?..

Je umeiacha injili inayokuambia baada ya kifo ni hukumu (Waebr.9:27) na kuigeukia injili inayokuambia kuna nafasi ya pili baada ya kufa na kwamba kunauwezekano wa marehemu kuombewa baada ya kufa ili utoke kwenye mateso ya kuzimu?.

Je! Umeiacha injili inayokuambia mpatanishi katika ya Mungu na wanadamu ni mmoja tu, Yesu Kristo na umegeukia injili nyingine inayokuambia wapo wapatanishi wengine, pembezoni mwa Yesu kama vile bikira Mariamu n.k., au yupo nabii mwingine ambaye ameteuliwa na Mungu kuwa ndiye atakayewapeleka wanadamu mbinguni..

Ndugu mpendwa kama umeacha hayo yote na mengine Zaidi ya hayo yaliyokweli ya Neno la Mungu na umegeukia mambo ambayo hayapo kwenye biblia basi UMELOGWA na Mhubiri huyo!, umelogwa na kanisa hilo!, umelogwa na kikundi hicho cha imani!. Toka upesi, anza kuisoma biblia.

Mahubiri yoyote ambayo baada ya kumaliza kuyasikiliza yanakufanya ujisikie hamu ya kufanya mambo ya kidunia Zaidi ya kulipenda Neno na kulitafuta kulisoma…Muhubiri huyo ni Mchawi, na analoga watu, hata kama hana tunguli nyumbani kwake, anafanya kazi ya kichawi madhabahuni….Mahubiri yoyote yasiyokupa Morali yoyote ya kumfuata Yesu na kuzidi kuyasafisha Maisha yako badala yake unapata morali zaidi ya kumchukia mwingine, kumlaani mwingine, kutafuta kisasi kwa mwingine, kumwacha mke/mume wako, kufanya uasherati, n.k…basi fahamu kuwa umelogwa na hayo mahubiri.

Uchawi mkubwa shetani anaoweza kumfanyia mtu sio kumfunga asipate kazi, au kumfunga asifanikiwe, au kumfunga asipate mtoto..hiyo ni ngazi ndogo sana ya uchawi wa shetani…Uchawi mkubwa anaoufanya ni KUWAFANYA WATU WASIMJUE KRISTO KWA MAARIFA YOTE!, kuwafanya watu wawe vuguvu katika Imani, kuwafanya watu waabudu sanamu na kumkosea Mungu. Huo ndio uchawi shetani kila siku anaoufanya kuuloga ulimwengu.

Na watumishi wake wa ngazi za juu, anaowahitaji na kuwaheshimu sana..si wachawi, wala waganga wa kienyeji…hao wanaloga vitu vidogo vidogo tu…Yeye jeshi lake kubwa linalofanya kazi yake kubwa ni MANABII WA UONGO! Wapinga-Kristo..Wanaoligeuza Neno la Mungu kuwa uongo..Hao ndio watumishi wake wa ngazi za juu kuliko wote. Ndio maana biblia haikusema nyakati za mwisho kutatokea waganga wa kienyeji wengi, au washirikina wa uongo wengi, au wachawi wengi…bali ilisema kutatokea “manabii wa uongo wengi”..Maana yake hao ndio shetani anawatumia kufanya maangamizi makubwa sana ya roho za watu .

Hawa ni watumishi Dhahiri kabisa wa shetani, wanaojigueza kuwa kama manabii wa kweli..Manabii hao wa uongo kazi yao ni kutoa unabii tu siku zote, lakini hawamshuhudii Yesu hata kidogo…Yohana Mbatizaji ambaye alikuwa ni nabii aliyetokea kuwa mkuu kuliko wote “YEYE ALIMSHUHUDIA YESU KWA NGUVU SANA” kwasababu alijua hakuna uzima nje ya Yesu. Na manabii wengine wote walikuwa wanaushuhuda wa Yesu…

Kama biblia inavyosema katika Ufunuo 19:10b “…….KWA MAANA USHUHUDA WA YESU NDIO ROHO YA UNABII”.

Hivyo tunapaswa tujihadhari sana. Hizi ni nyakati za mwisho.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

JUMATANO YA MAJIVU NI TENDO LA KIMAANDIKO?

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

SWALI : Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?

SAA YA KUHARIBIWA IIJIAYO ULIMWENGU WOTE.

KUOTA UMETUMBUKIA SHIMONI.

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

RABI, UNAKAA WAPI?

Swali muhimu kwa Bwana wetu (Rabi unakaa wapi)?.

Yohana 1:35 “Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake.

36 Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!

37 Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

38 Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?

39 Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi”.

Kipindi kifupi kabla ya Bwana Yesu kuianza huduma yake duniani, Yohana mbatizaji alitokea kuzishuhudia habari zake, alihubiri karibu kila mahali akieleza habari za ujio wa mwokozi wa ulimwengu. Na alipokuwa akihubiri aliwaeleza kuwa huyo mwokozi tayari yupo katikati ya wayahudi lakini hawamtambui(Yohana 1:26)..Hiyo iliwafanya watu wengi wawe na maswali mwengi, ni nani huyo, na anaishi wapi? ..

Yohana aliwaambia watu wote kuwa hata yeye mwenyewe hamjui lakini Mungu alimweleza kuwa Yule ambaye atamwona Roho Mtakatifu anashuka juu yake kama hua basi huyo ndiye. Hivyo baadhi ya wanafunzi wake wakawa makini sana kusubiria wakati wa kufunuliwa kwa tukio hilo..

Na kweli siku zilipofika, Yesu alipoongozwa na Roho kwenda kubatizwa kwa Yohana, wakati tu akiwa pale majini anabatizwa kama mtu mwingine wa kawaida tu, saa hiyo hiyo Yohana akaonyeshwa yale maono aliyoambiwa kuwa Yule ambaye Roho atashuka juu yake huyo ndiye…Na wakati huo huo Yohana akamtangaza kuwa huyu ndiye mwokozi wa ulimwengu, watu wote waliokuwa pale wakasikia..

Lakini baada ya Yesu kubatizwa aliondoka zake, wala hawakujua alipokwenda..Kwa bahati nzuri siku ya pili yake, Yohana alipokuwa na wawili kati ya wanafunzi wake anawafundisha, ambaye mmojawapo alikuwa ni Andrea, pengine wakiwa wanamuuliza habari za kuja kwa mwokozi ambaye jana alitoa habari zake..mara ghafla, huyo hapo wanamwona Bwana Yesu akipita karibu yao mahali walipokuwepo akiendelea katika safari yake…Yohana alipomuona tena, akawaambia wale wanafunzi…mtazameni! Mwanakondoo wa Mungu!!..

Muda huo huo wanafunzi wale wawili, hawakukawia wakamwacha Yohana na kuanza kumfuata Bwana Yesu kwa nyuma kisiri-siri..Na lengo lao lilikuwa ni moja tu wajue makao yake yalipo, wajue anapoishi hilo tu, na hayo mengine yatafuata baadaye..

Ndipo Yesu alipogundua kuwa kuna watu wanamtafuatilia tokea mbali akageuka na kuwaulizia Mnatafuta nini??

Hili ni swali ambalo hata leo hii..Bwana Yesu anatuuliza sisi tunaodai tunamfuata..Je! tunatafuta nini? Tunataka nini?

Lakini vijana wale wawili, hawakumwambia Rabi, tunaumwa tuombee, wala hawakumwambia tunaomba utuwekee mikono utubariki, wala hawakuomba wakae wafundishwe pale pale barabarabani, wala hawakuomba wafanyiwe miujiza,La! Badala yake walimuuliza Rabi, unakaa wapi?..Tunahitaji kujua unapoishi ili tujue tunakupataje hata ikitokea umepotea machoni petu tujue tunakupatia wapi..Tuna mengi ya kujifunza kwako, tunahitaji tukae chini tuzungumze na wewe, huku barabarani tu hakutoshi kutatuliwa matatizo yetu yote, na kutumiza haja zetu zote…ambapo tukishamaliza mazungumzo ndio basi tena hatutaonana tena.

Ndipo Yesu aliposikia hivyo akawapeleka nyumbani kwake.wakapaona..Hilo liliwafanya wale wanafunzi wawe na amani kuanzia huo wakati na muda si mrefu labda baada ya siku moja, Andrea ambaye alikuwa ni mmojawapo wa wale wanafunzi akaenda kumuita ndugu yake ambaye ndio Petro aje kwa Yesu..

Sasa embu fikiria kama asingeyafahamu makao ya Yesu, angemwelekezaji ndugu yake sehemu ya kumpata Yesu.?

Hata sasa, watu wengi wanamfuata Yesu, lakini hawaulizii anakaa wapi.. Nataka nikuambie ukimfuata Yesu, tambua kuwa atakuuliza nawe hili swali kama aliowauliza mitume wake, UNATAFUTA NINI?..Ukisema ninatafuta uponyaji, basi atakupa uponyaji wako na habari yenu itakuwa imeishia hapo hapo..Ukisema ninatafuta nyumba na magari atakupa nyumba na magari lakini habari yako na yeye itakuwa imeishia hapo njiani, ukisema ninatafuta mchumba atakupa mchumba lakini mkataba wenu utakuwa umeishia hapo…Lakini ukisema BWANA UNAKAA, WAPI? Hapo ndipo atakapokupeleka na kukukaribisha na kupaona anapokaa..

Anapokaa utapata kila kitu, zaidi ya yote ukimuhitaji muda wowote, unajua ni wapi utamkuta, hata mtu mwingine akihitaji kumjua huyo Yesu unayemfuata itakuwa ni rahisi kumwelekeza ni wapi alipo kwasababu anapajua nyumbani kwake….Na nyumbani kwake si pengine zaidi ya kwenye NENO LAKE.

Watu wengi wasasa wanalikimbia Neno la Mungu, wanatafuta njia za mkato za kumfikia Kristo..Na ndio maana Bwana hawawi wa kudumu ndani yao kwasababu wanakutana naye njiani tu kama habati, akikunja kona tu basi hawamuoni tena..na wala wao hawana habari naye tena..kwasababu wameshapata haja ya mioyo yao.

Unapolikimbia Neno la Mungu, hutaki kumjua Kristo katika Neno lake halafu unamtafuta katika maombezi, au maji upako, au miujiza hapo ni sawa na unamkimbia Kristo, kwasababu yeye mwenyewe ni NENO. Mhubiri yeyote anayekuletea habari njema za Yesu Kristo ni mfano wa Yohana mbatizaji..anakuelekeza kwa Kristo, hivyo ni jukumu lako wewe mwenyewe kujua unapomfuata una malengo gani na yeye.. Kama ni wa muda tu, wa kukutimizia mahitaji yako kisha basi, au kwamba ni wa kudumu..Kama ni wa kudumu basi taka kujua anapoishi…

Neno la Kristo likikaa kwa wingi ndani yako, basi ujue upo karibu sana na Yesu kuliko mtu mwingine yoyote kama ilivyokuwa kwa mitume, ambao walikuwa ni zaidi ya makutano mengi yaliyokuwa yanamfuata Kristo..walizijua siri nyingi kumhusu Yesu ambazo makutano wengine walikuwa hawazifahamu…Ikiwa utaishikilia tu dini yako, au dhehebu lako, ukadhani Kristo yupo huko na huku huna habari ya biblia, Hujawahi kutenga muda kukisoma angalau kitabu kimoja cha injili chote peke yako pasipo kusubiri kusimuliwa na mtu au mhubiri fulani…nataka nikuambie bado hujampata Yesu.

Na wakati mwingine anakuwa anapita akitembea huko na huko na kukutana na wewe katika safari yako ya Maisha…kama wale watu wa Emau, waliokuwa wanatembea na ghafla njiani Yesu akaungana nao pasipo wenyewe kujua kama ni Yesu…na kama ukisoma pale kwa makini utaona baada ya Yesu kuzungumza nao wakiwa kule kule njiani, akataka kama kuendelea mbele na safari yake..mpaka wale watu wawili walipomshurutisha aingie ndani kwao ale nao..na alipoingia ndani kwao na kula nao ghafla macho yao yakafumbuliwa na kumtambua ni Yesu, na akatoweka mbele yao.(Luka 24:13-32)

Hali kadhalika leo hii unapoisikia injili kama hii ambayo inakufikia hapo ulipo bure, ni Yesu anapita karibu na wewe hakikisha unamkaribisha nyumbani mwako (yaani aingie moyoni mwako kama wale watu wa Emau)..na kisha akishaingia kwako usikubali aondoke bila na yeye kukupeleka kwake (yaani katika Neno lake) kama wale wanafunzi wawili wa Yesu walivyofanya.

Ni maombi yangu kuwa Leo, usimwache Yesu akawa MPITAJI NJIANI TU KWAKO, anza kuchukua hatua ya kudumu kwenda nyumbani kwake (kwenye Neno lake), upate pumziko la kweli..na yeye aingie kwako…Penda kulitafakari Neno la Mungu kwa kadiri uwezavyo, na Yesu Kristo atakuwa na wewe kila wakati…Atakuita RAFIKI kama alivyowaita MITUME.  Mwulize leo unakaa wapi? Na atakufunulia mambo ambayo hata wanadamu wengine hawajui kwasababu upo sikuzote nyumbani kwake na yeye yupo nyumbani mwako.

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

UMUHIMU WA YESU KWETU.

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

IMANI NI NINI?

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BWANA HUWAJUA HAO WAMKIMBILIAO.

Nahumu 1:7 “Bwana ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao”.

Nataka nikuambie wewe uliyemfanya Mungu kuwa sehemu yote ya Maisha yako bila unafki, ujue kuwa Mungu anakuona, wewe ambaye umemfanya kuwa tegemeo lako la mwisho, Mungu anakuona, wewe ambaye muda wote unatenga kumuwaza yeye, kuzifikiria habari zake, unajishughulisha kuifanya kazi yake, bila kuangalia mazingira uliyopo, wewe ambaye unajibidiisha kutafuta maarifa yake bila kuchoka, japo wengine watakuona kama umerukwa na akili au unapoteza muda…Ujue Mungu anakujua vyema sana.

Haijalishi ulimwengu utakuona umepotea kiasi gani, au ndugu wamekukataa vipi, au marafiki wamejitenga nawe mbali kiasi gani…Hilo halimfanya Mungu asikuone.. Anakuona sana, kuliko hata wewe unavyodhani..

Nyakati hizi za mwisho. Ni rahisi kuona hata mlevi, au mzinzi, au mvaaji vimini anasema Mungu ndiye kimbilio langu,..ni mshirika mzuri wa kanisani anaimba kwaya, au ni kiongozi wa vijana, au wa wakina mama, lakini ni mtazamaji pornography na mzinzi naye pia anasema Mungu ndiye kimbilio langu..kila mtu atasema hivyo maadamu ni rahisi tu kulitamka hilo neno..Lakini Mungu anasema..mimi nawajua wanikimbiliao.

Haihitaji kukaa chini na kumsimulia, au kumweleza katika maombi, au kumwimbia nyimbo nzuri na kumwambia wewe Mungu ni kimbilio langu, au kumueleza kila mtu jambo hilo..hilo halikupi tiketi ya Mungu kukuona kuwa umemkimbilia..Bali matendo yako kwake yatazungumza, Kwake hakuna siasa..

Lakini nataka nikuambie ipo faida kubwa sana, na thawabu kubwa uliyowekewa wewe unayemtafuta Mungu kwa nguvu zako zote..Ipo siku ukiwa hapa hapa duniani utaburudishwa sana, kabla hata ya kwenda mbinguni kama usipozimia moyo..

Zaburi 31: 19 “Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako Ulizowawekea wakuchao; Ulizowatendea wakukimbiliao Mbele ya wanadamu!

20 Utawasitiri na fitina za watu Katika sitara ya kuwapo kwako; Utawaficha katika hema Na mashindano ya ndimi”.

Hivyo usikate tamaa. Yeye siku zote huwajua hao wamkimbiliao

Mungu akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

Mpagani ni nani?

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

MPINGA-KRISTO

JIWE LA KUKWAZA

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA?.Mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?

Je! mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?…(1Wakorintho 11:21 “kwa maana kila mmoja hutangulia kutwaa chakula chake katika kule kula; hata huyu ana njaa, na huyu AMELEWA.

22 Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA? Au mnalidharau kanisa la Mungu, na kuwatahayarisha hao wasio na kitu? Niwaambieni? Niwasifu? La! Siwasifu kwa ajili ya hayo.”)


JIBU: Watu wengi hususani wale wanaohalalisha ulevi katika makanisa yao ndio wanaoushikilia wakidhani kuwa Paulo alihalalisha ulevi kwamba waumini wakitaka kunywa mpaka walewe basi waende wakalewee majumbani kwao na sio kanisani.

Lakini Hebu tafakari huu mfano… “Watu wawili wamegombana katika nyumba ya Mungu (kanisani)…mpaka kufikia kupigana..Mhudumu wa kanisa akawakuta..na kwa hasira akawaambia “mmekosa sehemu za kupigania mpaka mnapigania kanisani”…Je! Kwa sentensi hiyo Mhudumu huyo atakuwa amehalalisha mapigano?…Jibu ni la! Hajayahalalisha hata kidogo…bali kwasababu anaiheshimu nyumba ya Mungu ikamlazimu yeye kusema vile. Kwamba nyumba ya Mungu sio ulingo wa mapambano..sio sehemu ya kufanyia dhambi wala mapambano…kama wameshindwa kuiheshimu nyumba ya Mungu na kutaka kuendelea kupigana basi wakapiganie sehemu nyingine huko lakini si nyumbani kwa Mungu.

Na hapa Mtume Paulo ndio anawaambia kwa ukali watu ambao wanaigeuza nyumba ya Mungu sehemu au vituo vya ulevi na ulafi. Watu ambao hawaiheshimu nyumba ya Mungu wala meza ya Bwana watu waovu, wana wa ibilisi. Hao ndio anaowaauliza je hawana nyumba za kunywea pombe zao?…maana yake wasiigeuze nyumba ya Mungu kuwa Bar… Kama tu Bwana alivyowafukuza wale watu hekaluni na kuwaambia wasiigeuze nyumba ya Baba yake kuwa pango la wanyang’anyi.

Picha kamili ya kinachoendelea katika kanisa la leo…watu wanakwenda kanisani ni walevi, wengine wanapafanya ni sehemu ya kunywea pombe kabisa rasmi bila aibu, wakitumia maandiko machache machache ya uongo waliyoyageuza kama walivyoligeuza hili…wengine  wanapageuza kanisani ni mahali pa kwenda kutafuta wachumba wa kufanya nao uasherati, wengine wanapageuza mahali pa kwenda kupata burudani za nyimbo na mahubiri ya kuwachekesha n.k..

Hivyo tunaonywa vikali kwamba tumheshimu Mungu..kanisani sio sehemu ya kwenda kujiuza..wala si sehemu ya kwenda kutafuta makahaba…Unapovaa vimini na suruali na kuingia navyo kanisani ni unakwenda kupageuza pale danguro (ni sawa na unakwenda kujiuza pale)..na hivyo ni kujitafutia laana badala ya Baraka..

Kama umeamua kuwa hivyo ulivyo huna mpango na Mungu basi upo huru kuishi maisha unayoyataka wewe na  unayoyachagua wewe..Toka kanisani nenda disko na nguo zako hizo, kule ni sehemu sahihi kwa mavazi hayo, nenda bar kule ni sehemu sahihi ya kulewa pombe lakini si katika nyumba ya Mungu. Nyumba ya Mungu ni nyumba takatifu ya sala, na ya kumwabudu Mungu, na ya Mungu muumba wa mbingu na nchi kwenda kukutana na sisi. Hivyo iheshimu.

Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

AMANI YA BWANA /AMANI YA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

Kuota mtu amekufa au ndugu amekufa.


Wakati mwingine unaweza ukaota umefiwa na mzazi, au kaka au dada, au mtu wako wa karibu sana. Na ndoto hizi huwa zinakuja kwa uzito sana, kiasi kwamba unaposhtuka huamini kama kweli ilikuwa ni ndoto, kwasababu unaona kama tukio hilo lilikuwa ni halisi kabisa..unabaki kuishia  kumshukuru Mungu na kusema asante  kwa kuwa ilikuwa ni ndoto tu..

Ndoto kama hizi huwa zinawapata watu wengi, na kama haijawahi kukutokea, basi itakuja kukupata siku moja katika maisha.. Lakini fahamu kuwa ni Mungu  hapo anakukumbusha hatma ya maisha yako na ya ndugu zako itakavyokuwa..kwamba siku moja wataondoka duniani, sio lazima wafe kwa njia hiyo hiyo uliyoiona kwenye ndoto hapana bali inaweza ikaja kwa njia yoyote lakini lakini kitendo ni kile kile kifo..

Vilevile inaweza ikawa ni hivi karibuni, au isiwe hivi karibuni pengine baada ya miaka 5 au 10 au hata 50 lakini ujumbe ni ule ule, kifo kinakuja.

Hivyo ni wajibu wako kufanya mambo mawili makuu juu ya maisha ya ndugu zako angali wakiwa bado hai,

  • Kwanza: Ni kwa kuwahubiria habari njema za wokovu, wamrudie Mungu kama hawajaokoka..
  • Na pili: Ni kuwaombea maisha yao hapa duniani yawe ni ya kumcha Mungu na Mungu awaepusha na njama za Yule adui.

1Samweli 12:23 “Walakini mimi, hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka.”

Unaona Nabii Samweli hakuacha kuiombea Israeli japokuwa ilikuwa inamchukiza Mungu kwa sanamu zao, lakini alikuwa akidumu katika kuwaombea..aliwaombea kwa bidii sana, na akahesabu kwamba ni dhambi kuacha kuwaombea ndugu zake,…na pia akawa anawaonya..hata Musa naye kule jangwani ni mara nyingi Mungu alitaka kuwaangamiza wana wa Israeli kwa matendo yao maovu lakini kwa maombi ya Musa Mungu alighahiri mabaya yao.

Hivyo na wewe ikiwa upo ndani ya Kristo ni rahisi Mungu kusikia maombi yako na Mungu akawaweka katika mstari sahihi ikiwa utaendelea kuomba kwa bidii juu yao bila kukata tamaa, na vile vile Mungu atawaepusha na mabaya na njama nyingi za ibilisi ziliyopangwa kinyume chao, ikiwemo vifo ambavyo sio vya wakati.

Lakini kama upo nje ya Kristo, hakuna dua yoyote itakuwa rahisi kwa ndugu zako. Hivyo nakushauri umpe Bwana Yesu maisha yako leo, tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha na kuwa tayari kumfuata yeye kwa moyo wako wote ili Bwana akuokoe kwanza wewe, ndipo iwe rahisi kusikia maombi yako kwa wengine.. Yesu sio wa watu wa dini Fulani tu, hata kama wewe ni muislamu, kimbilio lako ni YESU tu, wala hakuna mwingine..Yeye ndiye anayekuahidi uzima wa milele, yeye pekee ndio anayetoa faraja ya kweli ukiwa kwanza hapa duniani, na hata utakapofika kule..

Hivyo Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi hapo

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa kuukamlisha wokovu wako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312 jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Au jiunge Whatsapp hapa

https://chat.whatsapp.com/GBX2lWIcoCq8zmlnXJgaWQ

https://chat.whatsapp.com/GBX2lWIcoCq8zmlnXJgaWQ

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

KUOTA UPO UCHI.

Kuota unafanya Mtihani (Upo shuleni).

KUOTA UNAPAA.

USIKIMBILIE TARSHISHI.

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

Kwaresma ni nini?..Je! Kwaresma ipo katika Maandiko?..Na je ni lazima kufunga Kwaresma?, ni dhambi kuikatisha kwaresma? na je! ni dhambi kuishika kwaresma?


Neno Kwaresma limetokana na Neno la kilatini (Quadragesima) lenye maana “YA AROBAINI “… Kwahiyo siku ya 40 ndiyo inayoitwa Kwaresma..Kulingana na mapokeo ya, Madhehebu ya kikristo wanalitumia neno hilo kama kuwakilisha kipindi cha siku 40 cha mfungo kabla ya Pasaka.

Madhumini ya Mfungo huo ni kuwaandaa wakristo katika maombi, toba na kujinyenyekeza kwa ajili ya Pasaka ambayo itakuja baada ya siku hizo 40. Mfungo huo kulingana na mapokeo yao ni wa siku 40, lakini kiuhalisia ni zaidi ya siku 46..Kwasababu siku za jumapili huwa hazihesabiwi katika mfungo huo..Kwahiyo zinakuwepo jumapili 6 katika mfungo mzima..na kufanya Idadi ya siku za mfungo kuongezeka mpaka kufikia 46.

Mfungo huo pia unahusishwa na Bwana alivyofunga siku 40, akiwa jangwani, akijaribiwa na Ibilisi. Hivyo na wakristo wana jukumu la kufunga siku 40 kama Bwana alivyofunga.

JE KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

Jibu ni La! Hapana sehemu yoyote katika maandiko kuna sharti la kuitimiza Kwaresma..Hayo ni mapokeo..Na mapokeo yapo yaliyo mazuri na yaliyo mabaya..Mazuri ni yale ambayo hayakinzani na Neno la Mungu na mabaya ni yale yanayokinzana na Neno la Mungu na kuwafanya watu wawe wa kidini zaidi, kuliko kuwa wa Kiroho.

JE NI DHAMBI  KUISHIKA KWARESMA.

Katika Biblia ni wajibu wa kila Mkristo “kufunga na kusali”..Mambo hayo yanakwenda pamoja huwezi kusema unasali siku zote halafu hufungi hata mara moja, na pia huwezi kusema unafunga siku zote na husali hata siku moja. Kwahiyo Mfungo ni sharti kwa kila mwamini. Iwe ni mfungo wa wiki moja, wiki 2, siku 30, siku 40 au 50…Ni jambo la sharti. Na mfungo huo mtu auite kwa jina lolote iwe Kwaresma, jubilee, baragumu, au jina lolote lile ambalo mtu atapenda kuliita sio dhambi…

Kikubwa na cha msingi..Tendo lolote la kufunga halipaswi kuchukuliwa kidini..Kwamba mtu anafunga tu ili kutimiza sheria za dini yake, kama inavyofanyika leo. Haipaswi mtu kufunga halafu asiwe mwombaji…Wengi wanafunga lakini hata siku moja hawajawahi kutenga kusali hata lisaa limoja…huko ni kufunga kwa kidini ambako kuna matokeao madogo sana au kunaweza kusiwe na matokeo yoyote kabisa ikawa ni bure.

Hali kadhalika wakati wa Mfungo sio wakati wa kujichanganya na mambo ya kidunia, ni wakati wa kuwa katika utulivu wa roho na kujitesa nafsi, wakati wa kutubu kikweli kweli na wakati wa kuomba kwa bidii..Ni wakati wa kuongeza bidii sana katika mambo ya kiroho zaidi ya kimwili..Ndio maana unafunga kula..si wakati wa kuupendeza mwili ni wakati wa kuutiisha mwili.

Kwahiyo Mfungo huo unaoitwa Kwaresma kama hautafanyika kidini basi una matokeo makubwa sana kwa mhusika.

JE NI DHAMBI KUIKATISHA KWARESMA?

Mfungo mara nyingi ni kama Nadhiri, kabla ya kuanza kufunga mtu unaweka nadhiri kwamba unafunga siku 40, lakini ukisema unafunga halafu ndani ya mfungo huo unakuwa sio mwaminifu,  utakuwa unajipotezea muda tu wewe mwenyewe..Kama umeamua kufunga sharti umalize siku zote na kama huwezi basi usifunge…Maana utakuwa hujafunga kwa Imani, na biblia imesema tendo lolote lisilotokana na Imani ni dhambi (Warumi 14:23)

JE NI LAZIMA KUFUNGA KWARESMA?

Jibu ni la!..sio lazima kufunga wakati huo unaoitwa Kwaresma…lakini ni wajibu wa kila Mkristo kufunga..Kama hutafunga msimu huo ambao ni rahisi kueleweka na watu wengi…basi hakikisha unatafuta kipindi kingine katikati ya mwaka ambacho utafunga. Na kama ni mkristo kikweli kweli na si wakidini, basi utafunga nawe siku hizo hizo 40 au zaidi. Kwasababu ukilijua lile neno linalosema..

Matendo 5:20 “Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”

Kwasababu kama mtu unayemwita wewe wa kidini anakushinda idadi ya siku za kufunga…hapo ni nani wa kidini?…wewe au yeye?..Jibu ni wewe?..kwasababu huwezi kufanya hata anachokifanya yeye..na bado unamwita wa kidini. Sharti ufanye kama yeye tena vizuri zaidi umpite ili uwe na sababu ya kumrekebisha, lakini kama huwezi kumzidi, yeye ndio anayepaswa akurekebishe wewe.

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JUMATANO YA MAJIVU NI TENDO LA KIMAANDIKO?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

YESU KWETU NI RAFIKI

MTINI, WENYE MAJANI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JUMATANO YA MAJIVU NI TENDO LA KIMAANDIKO?

Jumatano ya majivu, ni mojawapo ya mapokeo ya kanisa katoliki..ambapo Ni kipindi cha mwanzo wa mfungo wa siku 40… Siku hii yanachukuliwa “matawi ya Mitende” na kuchomwa mpaka yawe jivu. Na kisha lile jivu linachukuliwa na kwenda kupakwa katika paji la uso la mwamini,  ishara kama ya msalaba.

Na wakati mhudumu anampaka mwamini majivu yale anakuwa anayasema maneno haya “kumbuka u mavumbi wewe na mavumbini utarudi”.. Na baada ya hapo ndipo muumini ataanza mfungo wa siku 40

Je Tendo hilo la Jumatano ya Majivu ni la kimaandiko?

Jibu ni la! si la kimaandiko hata kidogo. Hakuna mahali popote katika biblia wakristo walikuwa wanadesturi za kufanya hayo mapokeo ya jumatano ya majivu. Ni mapokeo tu yaliyoanzishwa na wanadamu. Ingawa Tendo la Mfungo ni la kimaandiko, ambalo kila mwamini anapaswa alitekeleze pia, lakini jumatano ya majivu sio ya kimaandiko.

Kwahiyo hakuna ulazima wowote wa mkristo kushika hiyo siku ya “jumatano ya majivu” kana kwamba ni siku takatifu isiposhikwa au kuenziwa ni dhambi mbele za Mungu. Na kwamba yale majivu yana nguvu fulani ya kiMungu, kana kwamba ukipakwa au ukipaka kuna jambo fulani la kiroho linaongezeka kwa msharika. Hapana, vilevile Mtu anaweza kuanza kufunga siku alizozipanga yeye pasipo huo utaratibu.

Kwahiyo hayo sio mambo ya msingi hata kidogo na wala hayamwongezei chochote Muumini, zaidi ya kumfanya awe wa kidini kuliko kuwa wa kiroho kuamini kuwa kuna kitu cha kipekee kinaongezeka ndani yake anapopakwa yale majivu.

Mambo ya lazima na ya sharti kuyafanya tuliyoagizwa na Roho Mtakatifu sisi wakristo yapo manne nayo ni…. 1)KUUMEGA MKATE,  2)KUKUSANYIKA PAMOJA,  3)KUDUMU KATIKA FUNDISHO LA MITUME (yaani kudumu katika Neno la Mungu) na 4) KUSALI. (Matendo 2:42). Hayo ndio mambo manne na ya muhimu na ya lazima kufanya kwa kila Mwamini. Na sio kushika sikukuu ya majivu wala ijumaa kuu. Na hilo la Nne la kusali linajumuisha pia KUFUNGA..Kwasababu kufunga na kusali vinakwenda pamoja.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

AMEFUFUKA KWELI KWELI.

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Siku zote Mungu akitaka kumuokoa mtu neema yake huwa anaizidisha sana kwa kiwango cha juu kiasi kwamba kwa nje ni rahisi kuona kama anatumia nguvu, au analazimisha ndivyo ilivyokuwa kwa Lutu na mke wake na watoto wake… Wale malaika wawili walipoona wanachelewa chelewa, wanakawia kawia waliwashika mikono yao na kuwavuta mpaka nje ya mji kwa nguvu kwa jinsi Mungu alivyowahurumia…

Mwanzo 19: 15 “Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu.

16 Akakawia-kawia; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, kwa jinsi Bwana alivyomhurumia, wakamtoa wakamweka nje ya mji.”

Lakini tendo hilo la kushikwa mikono halikuendelea milele walipofikishwa tu nje ya ule mji, wameshajua sasa yawapasayo kufanya jambo lililofuata waliambiwa..jiponyeni nafsi zetu msigeuke nyuma..Lakini Mke wa Lutu alijiharibia.

Mwanzo 19:17 “Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea”.

Ndugu, picha hii inatuonyesha kuwa wokovu ni tendo la neema kubwa sana, kiasi kwamba hakuna mtu anayeweza kujiokoa mwenyewe kwa nguvu zake…Na ndio maana Mungu aliona malaika hawatoshi kuja kutuokoa sisi na hukumu hiyo kubwa inayokuja huko mbele, badala yake akaamua kumtuma mwanawe kabisa , YESU KRISTO, ili aje kutuvuta sisi mbali na ile hukumu ya siku za mwisho na ziwa la moto…Yeye ndiye anayetushika mkono na kutuvusha kutoka katika ulee mji wa mauti na kutupeleka sehemu salama..

Lakini ikiwa ameshatuweka sehemu salama mbali na dunia, ni wajibu wa kila mmoja kuuthamini wokovu ule kwa kukimbia mbali zaidi na dhambi kama ilivyokuwa kwa Lutu na watoto wake..Ikiwa tulishaona mkono wa Mungu ulivyotuepua kutoka katika dhambi, hatupaswi kujilegeza tena, kusubiria tena neema itutoe kwenye dhambi tunazozitenda kwa uzembe wetu.. Tukishafikia hii hatua ni wakati wa kuziponya nafsi zetu…

Lakini embu tumtafakari mke wa Lutu ambaye ni mfano wa wale waliookolewa ambao mioyo yao bado ipo ulimwenguni, yeye alipogeuka nyuma alikuwa nguzo ya chumvi, unaweza kujiuliza ni kwanini awe nguzo ya chumvi na sio kitu kingine chochote labda tuseme nguzo ya mti, au ya chuma, au ya udongo?..Chumvi ni kiungo cha kipekee sana ambacho huwa kinadumu milele, yaani ukiihifadhi chumvi vizuri leo kwenye chupa mtu anatakaye kuja kuzaliwa miaka milioni moja mbele ataitumia na ikawa na ubora ule ule..

Na ndio maana Mungu sehemu nyingine alikuwa analifananisha Agano aliloingia na Daudi pamoja na wana wa Israeli kama agano la Chumvi, ikimaanisha kuwa ni agano la milele soma..

2Nyakati 13:5 “je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi?”

Soma tena Hesabu 18:19..

Hivyo lile lilikuwa ni agano la kukataliwa milele kati yake na mke wa Lutu.. Hata sisi leo hii, ikiwa Bwana Yesu alishatuokoa, halafu tunauchezea wokovu wetu, leo tunaenda mbele, kesho tunarudi nyuma…hatuthamini ondoleo la dhambi tulilopewa siku ile tulipotubu bure, ..na wema wake wote Mungu aliotutenda, hatuoni kama kuokolewa kule ni jambo la bahati sana ambapo sio watu ulimwenguni wanaweza kupewa neema hiyo badala yake mguu mmoja kwa Kristo na mguu mwingine kwa shetani Tujue tu tupo hatarini kuwa MAWE YA CHUMVI katika roho..

Yaani Mungu kuingia na sisi agano la rohoni la milele kuwa hatukustahili kuokolewa na yeye, na matokeo yake ni kuwa safari yetu ya wokovu inakuwa imeishia pale pale, tunakuwa tumekufa,japo kwa nje tunaonekana tupo hai..Kumbuka hilo ni agano la milele, maana yake ni kuwa Mungu hatakaa akupokee wewe tena milele kwasababu ile nguvu ya kukuvuta kwake inakuwa haipo tena…utaendelea na ubaridi wako, mpaka siku unakufa ili uishie katika ziwa la moto..mifano hiyo ipo duniani leo hii, utakuta mtu alianza vizuri na Bwana, wengine hata walitokewa kabisa na malaika, wengine walisikia sauti ikizungumza nao, wengine wakaonyeshwa maono, wengine Mungu akawa anawapa chochote waombacho katika hatua za awali kabisa za wokovu wao, wengine wakaepushwa na hatari nyingi kimiujiza, wakajua kabisa sasa hapa safari imeanza..Lakini kwa tabia zao za kuyarudia rudia yale yale machafu ya nyuma kwa kipindi kirefu hiyo ikawafanya wageuke kuwa mawe ya chumvi..Ambao ndio hao leo hii huwezi kuamini hata kama walishawahi kumjua Kristo…

Wokovu sio jambo la kujaribu, na ndio maana biblia inatuambia..

Wafilipi 2:12 “………..utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.

2 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.

Ikiwa ni wewe mmojawapo ndugu yangu unayesoma haya, na ndani yako bado kuna kanuru kadogo ambacho kanakaribia kuzima… basi usikubali izime kabisa…ni vizuri ukatubu kwa kumaanisha kabisa mbele za Mungu sasahivi, na kuacha kwa moyo wako wote mambo maovu yote unayoyafanya kwa vitendo, na kumfuata Kristo, neema hii bado ipo juu yako na ndio maana unasikia ndani yako kuhukumiwa unaposoma haya,….huyo ni Roho Mtakatifu anakuvuta kwake tena, anza kugeuka na kupiga hatua mbele, usipoitii hiyo sauti itafika kipindi hutaisikia tena ndani yako, utakuwa ukipita mahali na kukutana na maneno kama haya utaishia kudhihaki na kukejeli, lakini sasa kuna hofu ndani yako kiasi kwamba unaogopa hata kusema neno lolote la kejeli, hiyo hofu ni ya thamani na ya muhimu sana, na ndio inayokuvuta utubu,

Hivyo Tubu leo acha kwenda disko, acha ulevi, mrudie mke/mume wako, acha wizi, acha rushwa, acha kila aina ya dhambi unayoifanya maishani mwako na wala usigeuke nyuma kama mke wa lutu..…hizi ni siku za mwisho..Siku yoyote unyakuo unapita, na hii dunia inakwenda kuwa jivu, Maisha yatasimama…kilichosalia kwako sasa ni nini kama sio kuyasalimika maisha yako kwa Bwana Yesu ayaokoe, naye atakupokea kwasababu anakupenda na kukuhurumia…dini yako ya kiislamu haitakupeleka popote, dini ya kikristo haitakupeleka popote, dhehebu lako mashuhuri halitakupeleka popote bali YESU KRISTO pekee ndiye atakayekupeleka sehemu salama..

Hivyo Ikiwa upo tayari leo hii kuanza tena upya na Bwana..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako.

Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Zingatia hayo na Bwana atakuwa pamoja na wewe daima. Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

USIKIMBILIE TARSHISHI.

NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.

YEZEBELI ALIKUWA NANI

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

Ni nani anayetawala dunia kati ya Mungu na shetani?

Rudi Nyumbani:

Print this post