MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.

MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.

Muonekano mpya wa yesu baada ya kufufuka, unabeba somo gani?


Bwana Yesu alipokuwa bado anaishi duniani, ilikuwa ni rahisi kumtambua, kwani kwa sura yake tu watu waliweza kumtambua kuwa huyu ndiye. Lakini mara baada ya kufufuka kwake, mambo yalikuwa tofauti kabisa, haikuwezekana kumtambua tena Bwana Yesu kwa sura yake..Ilihitaji kipimo kingine tofauti..

Hilo tunalithibitisha sehemu kadha wa kadha, wengine walipomwona walidhani ni mtunza bustani makaburini, wengine walidhani ni mpita njia tu, na wengine walidhani ni mzee Fulani tu anapunga upepo beach..Na kama wangekikosa hicho kipimo kingine ndani yao cha kumtambua Yesu basi wasingekaa wamjue daima haijalishi huko nyuma waliishi naye na kutembea naye na kulala naye muda mrefu kiasi gani..kamwe wasingemjua.

Kwamfano embu tumwangalie Mariamu Magdalene, yeye ile siku ya kwanza ya juma, siku Yesu aliyofufuka, ndio aliyekuwa wa kwanza kufika pale makaburini, lakini alipomkosa Bwana, akidhania kuwa ameibiwa, alikwenda kuwaambia mitume, nao walipokwenda hawakukuta mtu kaburini.. wakaamua kuondoka zao, Sasa wakati Mariamu akiwa pale kaburini analia, kulikuwa na mtu yupo pale muda mrefu tu, anazunguka zunguka, pengine wakina Petro walimwona wakadhani ni watu wale wasio na shughuli wanaozunguka makaburini, lakini Mariamu alipokaa pale muda kidogo akiwa analia, ndipo Huyu mtu ambaye alimwona kama mtunza bustani akamfuata na kumuuliza unatafuta nini?.

Mariam akasema: ikiwa ni wewe ndio umemuiba Bwana wangu niambie..Kumbe hakujua anayezungumza naye ni YESU mwenyewe..Ndipo Yesu akalitaja jina lake Mariamu!..Na alipolitaja tu, Hapo hapo Mariamu akaitambua sauti ile, ni ile sauti yake yenye uweza, sauti ile ile iliyomwita Lazaro atoke makaburini kipindi kile kule nyuma, sasa imemwingia na yeye mpaka kwenye vilindi vya moyo wake ikampa uhakika kuwa huyu ndiye BWANA….Haikujalisha sauti ilikuwa ni ya mtu mwingine,inayofanana na mtu wa taifa lingine, lakini uweza tu wa ile sauti ulimpa uhakika kwamba huyu ndiye Bwana..(Soma..Yohana 20:1-18).

Lakini kama Mariamu asingekuwa na ushuhuda huo huko nyuma, basi ingekuwa ni rahisi kumpoteza Yesu..

Vivyo hivyo wale watu wawili ambao walikuwa wanakwenda katika kile Kijiji cha Emau, nao pia walipokuwa wanatembea njiani, Yesu alikutana nao isipokuwa katika sura nyingine..Na akaanza kuzungumza nao habari za kutabiriwa kwake, kuja kwake, na kufufuka kwake..Wale watu waliposikia tu yale maneno, jinsi yalivyokuwa yenye nguvu kwa namna ile ile waliyokuwa wanamsikia Bwana akifundisha makutano akiwa bado hai, hawakumuacha aondoke hivi hivi, wakamkaribisha nyumbani kwao, ndipo baada tu ya kuumega mkate na kuwapa, wakafumbuliwa macho wakatambua kuwa alikuwa ni YESU. Na saa hiyo hiyo akatoweka mbele ya macho yao.(Luka 24:13-33)..Lakini kama wasingetilia maanani uweza uliokuwa unatoka ndani ya maneno yale..wasingekaa wamtambue Kristo.

Mwisho kabisa Petro na wenzake, walipokuwa wanakwenda kuvua samaki, baada ya kuhangaika usiku kucha hawajapata kitu..Asubuhi yake kwa mbali walimwona mtu kama mzee akiwa pwani, mwenye sura wasioijua, mtu yule akawauliza wanangu mmepata kitoweo, wakasema hapana Bwana, akawaambia, tupeni jarife upande wa pili, wakidhani ni mzee tu wa kawaida anawashauri, wajaribu bahati yako, ..Na walipotupa tu jarife, wakapata samaki wengine..Mwanafunzi mmoja alipoiona ile ishara, akatambua kuwa hii ni ishara ile ile aliyotufanyia Bwana kipindi kile akiwa hapa duniani..Ndipo Yule mwanafunzi akamwambia Petro aliyetupa maagizo haya ni Bwana Yesu..Petro kusikia hivyo muda huo huo akapiga makasia kumfuata Pwani..

Biblia inatuambia walipomwona Bwana japo aliwatokea katika sura nyingine tofuati kabisa..Lakini hakuna hata mmojawao aliyetaka uthibitisho kama yeye ni Bwana kweli au la, Wote walipata uhakika ule, kwa ule uweza wake mkuu , na yale maneno aliyokuwa anazungumza nao akiwa pale ufukweni..(Yohana 21:1-25)..Lakini kama wasingeyaona matendo makuu kama yale Bwana aliyowahi kuwafanyia huko nyuma, kamwe wasingejua hata kama yule ni YESU. Wangedhani ni mzee Fulani tu amewapa dili la kazi.

Hivyo ndivyo Kristo alivyochagua kujidhihirisha kwa watu baada ya kufufuka kwake..Mpaka ikawafanya hata wengine wamtilie shaka..Hao ndio wale ambao walioukosa ushuhuda wake ndani yao..ndio wale waliokuwa wanalitazama umbo la Yesu, lakini hawayatafakari matendo yake, na ishara zake.

Mathayo 28:16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu. 17 Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka”.

Sasa kwa mabadiliko hayo, mitume kuanzia huo wakati wakatoa akili zao kabisa katika kuitegemea sura ya YESU, kama kipimo cha kumtambua Kristo mpaka kuutegemea ushuhuda wa YESU Maishani mwao.

Hivyo sura ya Yesu ikawa haina umuhimu tena kwao..Na ndio maana utaona Mitume mahali popote hawakuwahi kujisifia umbile la Yesu au Sura yake, au sauti yake..Bali ule Ushuhuda wa YESU uliokuwa ndani yao, ndio uliowafanya wamjue na kumtambua Yesu.

Vivyo hivyo leo hii KRISTO yupo kila mahali, lakini kama umeukosa ule ushuhuda wake ndani yako, utamwona tu kama mtunza bustani, utamwona tu kama mpita njia, utamwona tu kama mzee Fulani..

Ndio maana kuna umuhimu sisi tunaojiita wakristo, kujifunza biblia sana..kwasababu wakati utafika Kristo atajidhihirisha kwako, lakini hutamtambua kwasababu huujui ule ushuhuda wake alipokuwa hapa duniani ulivyokuwa.

Kwamfano Injili ya Kristo inapohubiriwa kwako, na unaona kabisa imekuja kwa ukali, na uzito, na kwa nguvu, labda inakutaka wewe ufanye jambo Fulani.. Sasa kwa kuwa wewe huna ushuhuda wa Yesu ndani yako, unaokushuhudia hata katika maandiko kuwa kulikuwa na watu wawili wa Emau, ambao neno la Kristo liliwajia kwa uzito kama huo, wakachukua hatua ya kusikiliza mpaka mwisho..Wewe unapuuzia, Unadhani ni mlokole Fulani anahubiri, au mchungaji tu Fulani, au kijana tu Fulani anauhibiri..kumbe hujui unampuuzia Kristo mwenyewe.

Na wakati huo huo unakesha kuomba kwamba Bwana akutokee, unataka akutokee vipi? Unataka umwone kavaa mavazi meupe, mwenye nywele ndefu, ndio umtambue?. Hilo wazo na ufute. YESU ameshafufuka, haji kwetu kwa muonekano ule tena.

Huu ni wakati wa kumjua yeye kwa ushuhuda wake.Hapo ndipo tutakapomwona akitembea katika Maisha yetu kila siku. Na hiyo inakuja pale tu Neno la Kristo linapokaa kwa wingi ndani yetu.

Vingenevyo tutamtilia shaka tu sikuzote, hata akitokea kwa sura ipi, kama wale wengine walivyomtilia shaka kule Galilaya, na wewe utamtilia shaka hivyo hivyo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye boksi la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

TULICHUNGUZE UMBO LA YESU NA MWENENDO WAKE.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ni dhambi kuchukua riba?

Biblia inasema tusikopeshe kwa riba, je! Wanaowakopesha watu kwa riba wanafanya dhambi?


JIBU: Biblia imezuia kutozana riba ndugu kwa ndugu tu..lakini kwa wengine nje ya ndugu sio dhambi kuwatoza riba.

Kumbukumbu 23:19 “Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;

20 mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki”.

Kwa mfano ndugu yako unamwona anayoshida, anaomba umkopeshe fedha kidogo, halafu wewe unatumia ile fursa kumwambia aongeze na kiwango kingine cha fedha juu yake(riba), kama faida yako, Hiyo ni dhambi, akikopa, basi arudishe kile kile alichokopa..Usigeuze shida za ndugu yako kuwa mtaji..

Katika hali ya kawaida hata bila kuambiwa na mtu au kufundishwa, ukiwa na nyumba ya biashara, halafu ndugu yako wa karibu amekuja kukaa hapo kwa kipindi fulani tu.. Huwezi kumwambia alipie kodi kamili kama watu wengine, anaweza kulipia tu zile gharama za kawaida ndogo ndogo lakini sio kulipia kila kitu..hakuna mtu mwenye utu anaweza kumfanyia hivyo ndugu yake.

Hali kadhalika katika Ukristo, wote tuliomwamini Yesu Kristo tunafanyika kuwa ndugu..Upendo wa Kristo unatuunganisha pamoja.tunakuwa tunapendana bila masharti..Upendo huo unatufanya kusiwepo hata na hamu ya kutaka faida kutoka kwa ndugu zetu katika Imani kama vile ilivyo katika ndugu zetu wa mwili. Ndio hapo biblia inatuasa kwamba tusitozane riba sisi kwa sisi. Lakini kwa mtu mwingine nje na ndugu zetu wa kimwili na kiimani, tunaweza kuwatoza ili tupate faida katika tunavyovifanya..kwasababu riba ndio inayokifanya kile kitu au ile shughuli ile iendelee mbele zaidi.

Lakini tukiwatoza ndugu zetu kwa lengo la kupata faida hapo upendo wa Kristo haupo ndani yetu, na hivyo tunafanya dhambi na kumkosea Mungu.

Ezekieli 22:12 “Ndani yako wamepokea rushwa ili kumwaga damu; umepokea riba na faida; nawe kwa choyo umepata mapato kwa kuwadhulumu jirani zako, nawe umenisahau mimi, asema Bwana MUNGU.

 Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEACHWA NA GARI.

Kuota umeachwa na gari, Maana yake ni nini?


Hii ni ndoto inayowapata watu wengi sana.Hususani wale ambao walishaokoka, lakini mambo mengine ya kidunia yanawasonga sasa hivi..Au walisharudi nyuma kabisa na kuacha wokovu

Ndogo hii inakuja katika maumbile tofuati tofauti wengine wanaota wameachwa na ndege, wengine wanaota wameachwa na wenzao ambao walikuwa wanakwenda pamoja,  lakini wengi wao wanaota wameachwa na gari walilokuwa wanasafiria.

Kwa mfano mtu mmoja alinihadhithia ndoto hii, ambayo rafiki yake aliiota ikawa inamsumbua sana..

Aliota alikuwa kwenye basi anasafiri, sasa lile basi likafika mahali kwenye foleni, na yeye baada ya kuona vile limesimama pale,  akaamua kushuka kidogo, na aliposhuka tu lile gari likaanza safari, anasema akaanza kulikimbilia, kumbe wakati analikimbilia kulikuwa na watu wengi nao wanalikimbilia lile gari, mchanganyiko wamama, watoto, na watu wengine n.k. Lakini baadaye yeye akajitahidi kwa nguvu sana kuliwahi akafanikiwa kuingia lakini kwa shida sana, na alipofika ndani akakuta siti yake imeshakaliwa na mtu mwingine..Ikimbidi ajikalie tu mwenyewe pale pembeni, lakini baada ya muda mfupi mzee mmoja akatokea akamsukuma atoke hata pale alipokuwa amekaa, akiwa hana sehemu ya kukaa kwa bahati nzuri akaona siti moja ipo wazi pembeni yake akaenda kuikalia na muda huo huo akashtuka..

Nilipo hoji nikagundua kuwa mtu huyo alikuwa ameokoka lakini baadaye alirudi nyuma, amesongwa na mambo ya ulimwengu huu..Na pale Mungu alikuwa anamwonyesha mwenendo wake jinsi ulivyo alipoona anakawia kukipata kile alichokuwa anakitafuta katika njia yake ya wokovu akaamua kwenda kukitafuta katika mambo ya ulimwenguni..Na hiyo itamgharimu kwasababu upo wakati atatamani kurudi lakini itakuwa ngumu sana kwake kwasababu wokovu sio safari ya kujaribu jaribu kama yule mke wa Lutu alivyofanya, aligeuka mara moja tu, na saa hiyo hiyo akageuka kuwa jiwe la chumvi.

Ikiwa na wewe ni mfano wa mtu kama huyu umeota ndoto ya namna hii umeachwa na basi ujue huo ni ujumbe kamili kutoka kwa Mungu, kuwa unaupoteza wokovu wako, na kuwa ukiendelea katika hali hiyo inayoendelea sasahivi ya kujitenga na wokovu, au kusongwa na mambo ya ulimwengu basi hautaupata tena daima na nafasi yako atapewa mwingine..

Lakini kama wewe hujaokoka kabisa yaani Bwana YESU hajayabadilisha maisha yako, wala huna habari na Mungu.. wewe umekuwa mkristo jina tu, au Muislamu, au huna dini kabisa..Hapo ni Mungu anakuonyesha jinsi gani inavyoogopesha na inavyosikitisha mtu unapoachwa safarini..Sasa jiulize, kwa mtu ambaye haujaanza kabisa safari, yeye atakuwa katika hofu nyingi kiasi gani?..Ndivyo ilivyo hali yako wee Upo katika dhambi, upo mautini, mbingu ipo mbali na wewe.

Sikia sauti ya Kristo, inayokuambia njoo kwangu leo.. Uanze naye safari njema ya kuelekea ufalme wa mbinguni. Kukutana na ujumbe kama huu si bure, Ni Mungu anazungumza na wewe.

Yesu anasema..

Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.(Yohana 14:6)..

Ikiwa unataka na wewe kwenda mbinguni basi YESU ndiye njia..wala hakuna mwingine.

Vile vile biblia inasema..

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo”.

Dunia hii inapita na mambo yake..Utauhangaikia huu ulimwengu mpaka lini, Ukifa leo, ni nani atakuwa mgeni wako huko uendako?. Ni nani atakayekupokea, utaulizwa safari yako ilikuwa ya kuelekea wapi, utajibu nini..Kwanini leo usichukue tiketi yako mkononi, uanze maisha mapya na Bwana Yesu..Kwasababu ni kweli atayabadilisha maisha yako na wewe mwenyewe utaona ni jinsi gani umeianza safari njema, ya uhakika na yenye matumaini..Ulevi, uzinzi, starehe, sema leo ni mwisho ninaamua kumgeukia Kristo.

 Ikiwa unataka kufanya hivyo leo.

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

Maswali na Majibu

KUOTA UPO UCHI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

USHUHUDA WA RICKY:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya huu mstari “sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”

Swali: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema.. “sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”? Ni kwa namna gani atatupwa nje? Na ni kwanini atupwe nje na sio chini?


JIBU: Tusome huo mstari…

Yohana 12:31 “Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo; sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.

32 Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu. ”

Kama ukichunguza vizuri hapo utaona anatumia neno “ATA” na si “ALI”.. yaani atatupwa na sio alitupwa au anatupwa..Ikionyesha kuwa ni kitendo kijacho ambacho bado hakijatokea..

Kumbuka tena hapo anasema atatupwa NJE, na sio atatupwa CHINI.. Shetani alishatupwa chini zamani sana, Kile kitendo cha yeye kuasi kule mbinguni biblia inasema kilimsababishia atupwe chini yeye pamoja na malaika zake (soma Ufunuo 12:7-10), Hivyo akawa ameganda tu hapa duniani kwenye giza nene, bila shughuli yoyote, wala tumaini lolote, akisubiria siku yake ya maangamizo ifike,apotee.. Mpaka sisi tunakuja kuumbwa, yeye alikuwa bado yupo hapa hapa anatazama tu, mwanadamu akimilikishwa kila kitu..

Lakini Adamu alipoasi, ndipo shetani akapata nafasi ya kuingia ndani ya ufalme ambao ulikuwa ni milki ya mwanadamu tu, Adamu akaiuza ile hati yake ya umiliki kwa shetani..Na tangu huo wakati shetani akapata nguvu akawa na mamlaka juu ya mambo mengi sana katika huu ulimwengu, akawa na uwezo hata wa kuwaendea wafu waliokufa(ikiwemo watakatifu) na kuzungumza nao kama alivyofanya kwa Samweli, akawa na uwezo hata wa kuzuia maombi ya watakatifu, yasimfikie Mungu …Yaani kwa ufupi japo watakatifu walikuwa wanalindwa na Mungu..lakini bado shetani alikuwa na uwezo fulani juu yao..

Sasa wakati ulipofika wa Mungu kuirudisha ile hati ya umiliki kwake, Ndipo akamletea mwanadamu aliyefanana na Adamu, ndiye Bwana wetu YESU KRISTO.. yeye alikuja kufanya kazi moja, na kazi yenyewe ilikuwa ni KUMFUKUZA SHETANI atoke ndani ya milki ya wanadamu..

Lakini si kwa wanadamu wote, bali wale tu watakaomwamini na kumpokea..

Na ndio maana sasa utaona Bwana Yesu anasema hapo.. sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”? Ikiwa na maana bado kitambo kifupi tu atakwenda kutupwa nje ya milki ya utawala wa watakatifu..Na tukio hilo lilikuja kutimia siku ile, pale KALVARI Bwana Yesu alipokufa na kuchukua funguo zote za uzima, pia na za kuzimu na mauti (Ufunuo 1:18).

Sasa tangu huo wakati hali yake shetani ikarudia kama mwanzoni alipokuwa pale Edeni kabla ya Adamu kuasi, akawa hana nguvu yoyote kwa wale watu waliomwamini Yesu na kuoshwa kwa damu yake, akawa hawezi kujiamulia tena kitu chochote juu yao, hawezi kuwaendea wafu na kuzungumza nao tena, hawezi kumdhuru mtu yoyote wa Mungu, ikiwa Mungu hajaruhusu.

Hivyo leo hii mtu aliyeokoka, hahitaji kuogopa wachawi, hahitaji kuogopa mapepo au majini, hahitaji kuwa na wasiwasi labda shetani atamuua, hahitaji kuwa na hofu labda maombi yake yamezuiliwa sehemu fulani hapo juu ya wakuu wa anga kama Danieli.. Sasa hivi shetani hawezi kufanya hivyo kwa mtu aliyeokoka kweli kweli.

Lakini kama upo nje ya Kristo..basi Maisha yako yapo hatarini..Wewe unapaswa uwe na hofu ya kila kitu, hukosei kuwaogopa wachawi, au majini, au wanadamu..kwasababu huna ulinzi wowote wa Mungu na shetani bado yupo ndani ya maisha yako, kila siku akikupangia njama za kukuangamiza..hivyo upo sahihi kabisa kuwaogopa kikweli kweli.

Ni neema za Mungu tu zinakushikilia ili utubu ndio maana upo hai.. Mpe Kristo Maisha yako kama hujampa, Uwe salama.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001312.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Mapambano dhidi ya shetani.

Katika vita siku zote wanaopambana ni wanajeshi dhidi ya wanajeshi..na si raia dhidi ya wanajeshi…Na ndio maana vita huwa vinakuwa ni vigumu sana na vikali…hiyo yote ni kwasababu mwanajeshi anafundishwa kwenda kupambana na mwanajeshi mwenzake ambaye anautaalamu kama yeye, ambaye ni mjuzi wa silaha kama yeye, ambaye anavaa dirii ya kuzuia risasi kifuani kama yeye anavyovaa..ambaye anavaa chepeo kichwani ambayo ni ngumu isiyoweza kuingia risasi kama yeye anavyovaa…ambaye anasilaha na vifaa vya kijeshi kama vya kwake…

Ndio maana unaweza kuona Taifa moja linajiongezea uwezo wa silaha za kijeshi kila kukicha ni kwanini?….Ni kwasababu wanajeshi wanapokwenda vitani wanakwenda kupambana na watu wanaotumia vifaru kama wao…wanakwenda kupambana na watu wenye ujuzi kama wao…Kwa ufupi wanakwenda kupambana na watu wanaofanana na wao karibia kila kitu..na hawaendi kupambana na raia.

Na wakishafanikiwa kumaliza jeshi la maadui basi huwa hawana muda ya kuwaua raia,.. wanachokifanya ni kuchukua tu rasilimali zao, na kuwachukua raia mateka au kuwafanya watumwa wao basii…hawana muda wa kuwaua…kwasababu vile vifaru walivyokuwa wanavitumia vitani havikuwa kwaajili yao bali kwaajili ya wanajeshi wao…

Sasa na sisi wakristo tunafananishwa na wanajeshi waendao vitani…na Biblia inatuambia “Tutwae silaha zote za Mungu”

Waefeso 6:11  “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani

12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15  na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16  zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17  Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

18  kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;”

Kumbuka na sisi hatuendi kupigana na watu wa shetani…bali tunakwenda kupambana na Adui yetu Shetani mwenyewe na mapepo yake. Na kama sisi tulivyo ndivyo na yeye alivyo…kama na sisi tulivyo na upanga mkononi na yeye anao upanga mkononi..kama sisi tulivyo na ngao na yeye pia anayo ngao ya kuzuia mishale kutoka kwetu..kama sisi tulivyo na chepeo kichwani mwetu na yeye ni hivyo hivyo anayo ya kwake…Kwahiyo hapo vita ni lazima viwe vikali tu..kinachohitajika ni kuwa na uwezo wa kuutumia upanga kuliko yeye, kuwa na uwezo wa kuitumia ngao kuliko anavyoitumia yeye, kuwa na uwezo wa kutumia chepeo kuliko anavyoitumia yeye..hiyo ndio njia tu ya kumshinda Adui shetani. Lakini kama yeye anauwezo mkubwa wa kutumia silaha zake kuliko wewe basi atakushinda tu, haijalishi una upanga mkononi, au ngao au chepeo….

Sasa Kwanini tunashika upanga wa Roho mkononi ambao ni Neno la Mungu?..Ni kwasababu Adui yetu na yeye ameshika upanga mkononi…kutupinga sisi…Ndugu usifikiri shetani halijui Neno?…. Analifahamu vizuri sana..na kama biblia inavyosema Neno la Mungu ni upanga ukatao kuwili…maana yake adui akiupata anaweza kuutumia kukuua hata wewe…Hivyo shetani naye ameshikilia upanga wa Neno la Mungu akipambana dhidi yetu…

Kama alivyopambana na Bwana Yesu akiwa kule jangwani…alimwambia Bwana Yesu “imeandikwa hivi katika maandiko”…Na Bwana akawa anamjibu “tena imeandikwa hivi”..Katika ulimwengu wa roho hapo ni pambano kati ya Bwana Yesu na shetani…shetani anaurusha upanga dhidi ya Bwana na Bwana anauzuia na kwa ushapu anamkata na upanga wake ulio mkononi..

Lakini endapo Bwana angekuwa halijui Neno..shetani angemkata kwa Neno hilo hilo..Lakini kwasababu alikuwa analijua kulitumia Neno vizuri aliweza kumshinda shetani..

Kwahiyo ukienda kupambana na Adui shetani na mapepo yake..kama hulijui neno na namna ya kulitumia ipasavyo hakika atakumaliza, kwasababu na yeye kaushikilia upanga unaofanana na wako….(Mapambano dhidi ya shetani  yatakuwa makali sana kwako)

Katika siku hizi za mwisho biblia imetabiri kuwa upendo wa wengi utapoa…Upendo unaozungumziwa hapo ni upendo wa kumpenda Mungu…na si wa kumpenda mwanamke/mwanamume. Watu wengi watakuwa hawana habari ya Neno la Mungu. Leo utamwuliza mtu mara ya mwisho kujifunza mwenyewe binafsi biblia ni lini? Bila kusubiri kutafsiriwa na mtumishi Fulani?..atakuambia ni muda mrefu sana..na hata akisoma, anasoma sura moja mbili kamaliza…Nyakati hizi mbaya tulizopo sio nyakati za kusoma sura moja ya biblia na kutulia baada ya wiki ndio unasoma nyingine…hapo shetani hashindani na wewe anakuona tu kama raia ambaye huna madhara kwake hivyo anakuchukua mateka tu, kama wanajeshi wanavyowachukua raia mateka..

Sasa siku hizi za mwisho, shetani kashawachukua wengi mateka…inawezekana hata wewe umeshachukuliwa lakini hujijui tu, (kwasababu huna silaha yoyote mkononi mwako ya kumwogopesha)…sasa choropoka leo anza kuzifaa silaha chini chini kwa kuanza kujifunza Neno, na baadaye utoke upambane naye ili ukiisha mshinda uwafungue mateka wale wote aliokuwa amewateka kwa uongo wake na kuwafanya kuwa mateka yake kwa uongo wake… wewe wageuze wawe mateko wa Kristo wote aliowateka yeye, kwa elimu yako ya uongo na tabu zake… Kama biblia inavyotuambia..

2 Wakorintho 10:3  “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4  (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII KRISTO;

6  tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”

Na silaha hiyo ni NENO LA MUNGU..Ukilifahamu Neno la Mungu, Bwana atakutumia kumnyang’anya shetani mateka…na yeye atabaki hana kitu..na jeshi la Bwana litakuwa kubwa zaidi kuliko lake.

Sasa utawezaje kuanza kujivika silaha hizo.?

Kwanza tubu, mpe Yesu Kristo maisha yako kama hujaokoka..kisha jikane nafsi na beba msalaba wako..Halafu anza kupunguza mizigo katika maisha yako ya kila siku, ondoka kwenye magroup yote ya kidunia katika mitandao, Kanunue biblia leo kama huna… “Biblia ya maandishi sio ya kwenye simu”,..kila siku tenga muda mrefu wa kusoma Neno, na unaposoma zima simu na pia kaa sehemu ya utulivu..kisha yasome maandiko na utaona mambo Bwana atakayokufunulia ambayo ulikuwa huyajui…usisome kimstari kimoja au sura moja…Soma angalau kitabu kizima…kwasababu ufunuo wa Roho unaachiliwa pale unapolielewa Neno katika msingi wake, lakini ukisoma kijimstari kimoja hutaelewa chochote na hutapata ufunuo wowote. Soma kitabu cha Injili ya Mathayo uone ni vitu vingapi ulikuwa huvijui na jinsi gani likuwa vinakupita tu na shetani alivyokuwa anakudanganya.

Wakolosai 3: 16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote..”

Na siku zote kumbuka, mapambano dhidi ya shetani hayajaisha.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine, na pia kama utapenda kuyapata masomo haya kwa njia ya whatsapp au email au inbox yako ya facebook basi utatutumia ujumbe mfupi, hali kadhalika unaweza kuyapata bure kwa njia ya internet, tembelea website yetu hii kwa masomo Zaidi /www wingulamashahidi org/.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JILINDE NA UNAJISI, UNA MADHARA MAKUBWA.

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

RABI, UNAKAA WAPI?

Shetani ni nani?

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

2Wakorintho 5.17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Kuwa kiumbe mpya sio kuwa “mtu mpya”…Mtu ni yule yule isipokuwa tabia zinabadilishwa….Mtu wa tabia za asili anania mambo ya ulimwengu huu…Furaha yake ni kula na kunywa  na anasa kama mnyama tu. Mnyama kamwe hawezi kufikiri kwamba akifa ataenda wapi, na wala hajali chochote isipokuwa watoto wake tu…

Kikubwa katika maisha ya wanyama wanachokijua ni kula, kunywa, kuzaliana, kulea watoto wao na kujiburudisha katika mazingira tofauti tofauti. yanayopatikana katika mazingira ya ulimwengu huu basii…Hali kadhalika hali yake mtu ambaya hajazaliwa mara ya pili..vitu vya pekee vinavyoutawala ufahamu wake ni kuwa na maisha bora katika kiulimwengu huu, aoe/aolewe…awe na nyumba nzuri, awe na mali na maisha bora…na baada ya hapo afe.

Hakuna chochote kinachomhimiza afikiri kuwa kuna maisha baada ya hapa. Fungu lake lipo katika ulimwengu huu.

Lakini mtu aliyezaliwa mara ya pili..biblia inasema anakuwa amevuka kutoka mautini kuingia uzimani, na anakuwa amefanyika kiumbe kipya…akili yake inakuwa imebadilishwa na kuwa akili ya kimbinguni..mawazo yake yanaelekea mbinguni tu…

Vitu vya ulimwengu huu avipate au asivipate hiyo inakuwa haimsumbui sana kwasababu anajua anao utithi wa mbingu zilizo tajiri kuliko mamlaka zote na falme zote duniani.

Je ya kale yamepita kwako? je umefanyika kiumbe kipya?

Kama bado unasubiri nini usiingie ndani ya Yesu leo?..Mkabidhi Yesu maisha yako uokolewe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Ubatizo wa moto ni upi?

NITAPOKEAJE NGUVU YA KUSHINDA DHAMBI?

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

AMANI YA BWANA /AMANI YA MUNGU.

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

CHEMBE YA NGANO ISIPOANGUKA KATIKA NCHI, IKAFA,

Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi”.


Shalom, Jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze maneno ya Mungu yanayobubujisha uzima wa milele ndani yetu.

Kama tunavyosoma katika biblia kuna wakati ambao huduma ya Bwana wetu Yesu Kristo ilifika katika kilele chake, yaani habari zake zilivuma karibia kila mahali, sehemu zote habari zake zilikuwa zinazungumziwa,..Mpaka watu kutoka mataifa mbali mbali wakawa wanakuja kutaka kumwona YESU. Na kuja kwao hakukuwa kwa ajili ya kufuata miujiza tu hapana, bali kwa lengo la kupata wokovu aliokuwa nao.

Mpaka ikafikia wayunani nao wakawa wanatafuta kumwona Yesu..

Yohana 12:20 “Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.

21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu”.

Unaona?? Lakini Bwana alipoona mazingira yale, na mwitikio ule mkubwa wa watu wengi na wengine kutoka mataifa mbalimbali, aliwaambia wanafunzi wake maneno haya..

Yohana 12:24 “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi”.

Aliwapa mfano huo ulio hai wa chembe ya ngano, ili kuwafundisha watu ni kwanini Mungu ampokee, kwanini Mungu amtukuze kiasi kile, ambapo sisi watu wa kizazi hiki ndio tunaojua ni kwa namna gani Mungu amemtukuza Bwana wetu YESU kwa namna isiyokuwa ya kawaida, leo hii mtu aliye maarufu kuliko wote duniani kwa wakati wote ni YESU KRISTO, na mtu anayezungumziwa sana, kwa kila dakika na kila sekunde moja ni YESU, na jina linalotajawa mara nyingi Zaidi kulingana na takwimu za dunia ni YESU KRISTO, haijalishi ni watu wangapi maarufu watapita hapo katikati lakini yeye atabakia kuwa mtu asiye karibiwa hata kwa nukta moja kwa sifa, na umaarufu duniani kwa wakati wote…

Lakini siri ya yeye kuwa hivyo, ndio ilikuwa katika ule mfano wa chembe (mbegu) ya ngano..akawaambia kama ngano isipotupwa ardhini, ikachimbiwa chini sehemu chafu, ikaoza, na mwisho wa siku ikafa kabisa, basi haiwezi kuzaa na kutoa mazao, na kuletea faida yoyote ulimwenguni.. itaendelea kubakia tu palepale ghalani, katika hali ile ile kwa miezi na miezi na miaka kwa miaka.. Hiyo ni kanuni ya asili kabisa, inajulikana hata kwa mbegu nyingine zote.

Bwana Yesu alikubali kufa kwanza, na kuonekana sio kitu, kwa ulimwengu, soma

(Isaya 53:3 “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.”),

Unaona? ulimwenguni wote ulimchukia kwa maisha yake ya kuchukia dhambi, alionekana kama mtu baki duniani,na hiyo ilimfanya aonekana pia kama amerukwa na akili soma..(Marko 3:21)

Yohana mbatizaji alisema alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea (Yohana 1:11).. Alikiri kabisa kwa ndugu zake, kuwa ulimwengu hauwezi kuwachukia wao, bali unamchukia yeye kwasasabu anazishuhudia kazi zake kuwa ni mbovu (Yohana 7:7)..

Embu mwangalie jinsi alivyojikana nafsi,..Jinsi alivyokubali kuoza kwa habari ya ulimwenguni..Lakini hapa sasa Mungu anamtukuza, anamletea mataifa, waje wamsujudie, wanadhani ilitokea tu juu juu.. Ndipo anapowaambia wanafunzi wake..

Yohana 12:24 “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.

25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.

26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu”.

Hata na sisi leo hii ni kwanini wokovu wetu unaonekana umekwama mahali Fulani..yaani tangu tuliposema tumeokoka hadi leo, hatuoni badiliko lolote katika roho zetu..ni kwasababu hatukujikana nafsi..Hatukukubali kuoza ardhini kwa habari ya ulimwengu..

Tulipookoka tulikuwa bado tunataka tuonekana ni wa kisasa, kwamba na sisi tunajua kwenda na wakati, na fashion za kiulimwengu, tuvae na sisi vimini vyetu kama zamani, tuvae suruali zetu kama zamani tusiwe tofauti na wale wanenguaji..tuendelee kuhudhuria katika kumbi za starehe..tuendelee kulewa vilabuni, tuendelee kukaa na watu wanaozungumza maneno ya mizaha muda wote,..tuendelee na biashara zetu haramu..tuzidi kuwa wakidunia..tusipende kujifunza maneno ya Mungu marefu, tupende mafundisho mepesi mepesi, tunayotutabiria mafanikio..n.k.

Kwa namna hiyo Bwana Yesu anatuambia..tutabaki katika hali hiyo hiyo katika roho..miaka nenda miaka rudi..hutaona badiliko lolote katika roho yako, hutaona Bwana akikupigisha hatua nyingine rohoni..utakuwa unakwenda kanisani unarudi, unahudhuria madarasa ya biblia kila siku..Lakini maisha yako hayana ushuhudu wowote..

Yaani kwa kifupi ukiulizwa tangu siku uliposema umeokoka hadi leo, ni jambo gani Mungu kakuongezea ndani ya maisha yako, utasema sijaona.. Hatuzungumzii masuala ya fedha, kwasababu si kila mwenye fedha amebarikiwa, japo Baraka zinaweza kuambata na fedha..lakini fedha si lazima ziambatane na Baraka..Tunachozungumzia ni mafanikio yako ya rohoni..Je! Roho yako imenufaishwa na huo wokovu kiasi gani tangu uliposema umeokoka?..

Damu ya YESU imeleta badiliko gani jipya katika maisha yako? Je! Zile chemchemi za maji ya uzima zinabubujika ndani yako? Je! Roho Mtakatifu anakushuhudia ndani yako kuwa wewe ni mwana wa Mungu?, Je! Siku kwa siku unamwona akitembea katika maisha yako,

Je! Wokovu wako ulishawahi kuwa faida kwa wengine nao pia wakaupokea?..Je! ndani yako dhambi imekuwa mbali na wewe kiasi gani?..Je utakatifu ni mrahisi kwako? N.k

Kama ni La! Basi ujue mbegu yako haijaoza..na ndio maana huna matunda yoyote..

Kama unafikiria kutubu dhambi zako..basi ujue kuwa toba inaambatana na kitendo cha kujikana nafsi, mahali ambapo unasema msalaba mbele dunia nyuma..Unakuwa tayari kuchekwa kwa ajili ya wokovu wako..Unakuwa tayari kuonekana ni mshamba kwa ajili ya wokovu wako, unakuwa tayari kuonekana umerukwa na akili kwa ajili ya kukubali kwako kuishi maisha matakatifu..

Hapo ndipo unapooza…mbinguni unaonekana umeipoteza nafsi yako,..mpaka unakufa kabisa kwa habari ya ulimwengu..Sasa baada ya hapo, Mungu ndipo anapokuhuisha na kuanza kukuchipua tena kutoka ardhini, na kidogo kidogo anakukuza, anakutoa hatua moja hadi nyingine, unaanza kumwona Mungu katika viwango vya tofauti na pale mwanzo, unauhisi ule uhalisia wa wokovu ndani yako yako..

Na ghafla utashangaa anakufikisha mahali ambapo, wewe mwenyewe hukudhania kama ungeweza kufika kwa wakati huo..na hata yale uliyoyapoteza Mungu anakurudishia kwa wakati wake ukifika..Mwisho wa siku unakuwa na matunda kote kote…

Hivyo ndugu, kama hujaubeba msalaba, basi tujikane nafsi leo mfuate Yesu..maana huko ndipo yeye anapotungojea wote. Ili na sisi tubarikiwe kama yeye, tusibaki katika hali ile ile rohoni siku zote.

Shalom. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

NI NANI ALIYEWALOGA?

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

MAONO YA NABII AMOSI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Mungu anapotaka kumtoa mtoto wake sehemu moja kwenda nyingine anakuwa kama anamrudisha kwanza nyuma ili ampandishe juu katika hatua nyingine…Vitu vya asili pia vinatufundisha, ili Mshale uweze kwenda mbali Zaidi ni lazima uvutwe nyuma kwa nguvu kwa kadiri iwezekanavyo kutoka katika ule uta..ukiuvuta kidogo utakwenda mbali kidogo, ukiuvuta nyuma sana, utakwenda mbali zaidi, vivyo hivyo katika mkuki, au manati. Kila kitu ili kufike mbali ni lazima kirudishwe nyuma kidogo. Kwasababu nguvu ya kwenda mbali Zaidi inaanzia nyuma zaidi.

Baada ya Mungu kuona ukamilifu wa Ayubu, jinsi anavyomcha yeye na anavyojiepusha na uovu…aliona anastahili kubarikiwa baraka mara mbili Zaidi..na ulipofika wakati wa kumbariki alimshusha kwanza chini na kumnyang’anya vile vyote alivyokuwa navyo…na baada ya kumnyang’anya ni sawa na mshale uliovutwa nyuma unaojiandaa kuachiwa uende mbali zaidi , Na,tunaona baadaye Ayubu alipoachiliwa alikuja kupata vitu mara mbili Zaidi.

Mungu alipoona uaminifu wa Danieli katika nafasi yake ya uwakili wa Uajemi aliowekwa kwamba hali-rushwa wala haibi na kwamba ni mwaminifu siku zote katika nafasi yake…ulipofika wakati wa kumpandisha cheo cha ju Zaidi alikuwa hana budi kushushwa kwenye nafasi ile ya chini kabisa mpaka kupelekwa kwenye tundu la simba kuuawa…hapo alikuwa ni sawa na upinde uliovutwa nyuma, na ulipoachiwa alipanda juu Zaidi..akawa mkuu zaidi ya maliwali wote (Danieli 6:28)

Mungu alipoona uaminifu wa Mordekai katika geti la Mfalme kwamba ni mwaminifu, hali rushwa, na katika nafasi yake hajawa mnafiki wala mtu mwenye nia mbaya na mfalme, Zaidi ya yote alimwokoa mfalme na mauti ya watu wabaya, aliokuwa anafanya nayo kazi..Mungu alipoona huo moyo wake mwema na mkamilifu na alipotaka kumpandisha juu…Mordekai alikuwa hana budi kwanza kuvutwa chini, kwani tunaona alitengenezewa visa vya kuuawa mpaka Adui yake mkubwa akaenda kuchonga mti mrefu ili amtundike Mordekai kwa ruhusa ya Mfalme..na Mordekai alikuwa yupo hatarini kufa kama alivyokuwa Danieli…

Lakini Mungu alimwokoa Mordekai na kumpandisha cheo cha juu Zaidi na kuwa mkuu wa majemedari wa Uajemi..Kutoka kuwa mlinzi mpaka kuwa mkuu wa majeshi…Lakini ilikuwa ni lazima kwanza ashushwe chini kiwango cha kukaribia na kufa.

Na ipo mifano mingi katika biblia ya namna hiyo ambapo kabla ya Bwana kumpandisha mtu kutoka ngazi moja kwenda nyingine…anakuwa anamrudisha kwanza ngazi moja chini ili apande juu Zaidi. Hakuna njia ya mkato.

Kwahiyo usiogope unapoona umepoteza kitu fulani unachoona cha muhimu katika Maisha yako, labda kazi au mali kwasababu ya haki unazozifanya…Ukiona umepoteza vyote hivyo na kufikia hatua upo hatarini hata kupoteza Maisha yako, au heshima yako basi fahamu kuwa ni Bwana amekupenda na anataka kukunyanyua juu Zaidi na pale ulipokuwepo…katika hatua kama hiyo usiache uaminifu wako kwasababu ameiona haki yako na hivyo anataka kukupandisha juu Zaidi kama alivyomfanyia Danieli. Lakini njia ya kupandishwa ndio kama hiyo aliyotumia kwa watumishi wake katika biblia..(unatikiswa kwanza kidogo)

Ukiona hata umefungwa kwa kesi ambayo ni ya kusingiziwa au kwa jinsi isivyo haki, ukiona umefilisika kwa sababu hufanyi biashara za magendo na umekataa biashara zisizo halali..hiyo isikusumbue hata kidogo upo katika kipindi cha kuvutwa chini ili upande juu Zaidi..Ni jambo la muda tu!..

Ukiona unamcha Mungu na hapo kwanza mambo yako yalikuwa yanaenda vizuri.. lakini ghafla mambo yameharibika kunatokea visa hivi na vile…kunatokea maadui wengi sana, hatua kama hiyo unapofikia usimchukie mtu bali ujue kuwa upo katika kipindi cha kushushwa ili upandishwe. Hivyo ndivyo Mungu anavyofanya ili kumpandisha mtu kutoka ngazi moja kwenda nyingine.

Lakini kama umepoteza vyote kwasababu ulikuwa mwasherati, au kwasababu umekamatwa unakula rushwa, au fisadi au kwasababu ya wizi au jambo lolote baya ukafungwa au ukafilisika…hapo ni Bwana amekurudi ili utubu…uache wizi wako, uache uasherati wako, uache rushwa zako, uache mambo yote mabaya unayoyafanya na umgeukie yeye kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote. Na baada ya kufanya hivyo ndipo atakufanyia hayo mengine. Lakini usipotubu hakuna lolote litakalotokea la kukunufaisha. Kwasababu hapo Mungu hajakushusha ili akupandishe juu, bali ili utubu kwanza!

Lakini kama unamcha Bwana, umeokoka, umejitenga kweli kweli na ulimwengu..usiogope! tena majaribu yanapokuja ya namna hiyo unapaswa ufurahi kwasababu ndio wakati wa kukumbukwa kwako.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

BWANA HUWAJUA HAO WAMKIMBILIAO.

RABI, UNAKAA WAPI?

UFUNUO: Mlango wa 1

CHAPA YA MNYAMA

Rudi Nyumbani:

Print this post

WEWE U MWALIMU WA ISRAELI,NA MAMBO HAYA HUYAFAHAMU?

Maneno haya aliambiwa Nikodemo, mwalimu wa torati, Farisayo aliyemfuata Bwana Yesu kwa siri usiku na kumweleza mambo ambayo mafarisayo mwenzake wanayajua juu yake..alikiri na kusema kuwa sisi mafarisayo tunajua kabisa wewe umetoka kwa Mungu.(Lakini walikuwa wanampinga).. Lakini kabla hajafika mbali Bwana Yesu alimkatiza na kuanza kumweleza habari za kuzaliwa mara ya pili..

Yohana 3:1 “Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.

2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, TWAJUA ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.

3 Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”.

Lakini ukiendelea utaona Nekodemo anaanza kushangaa juu ya habari hizo mpya, inawezekanijae mtu kuzaliwa mara ya pili.. Wakati anastaajabia hayo..Kumbe Bwana naye akawa anamshangaa, huyu ni mwalimu wa torati, mtu aliyebobea katika masuala ya Imani halafu halijui jambo hili wala hata hajawahi kulisikia?..akamwambia..

Yohana 3:10  Yesu akajibu, akamwambia, Je! Wewe u mwalimu wa Israeli, na mambo haya huyafahamu?

Hata sasa baadhi yetu sisi wahubiri, Bwana anatushangaa sana.. Tunafundisha Neno la Mungu, tunahubiri, tunajiita wachungaji, tunajiita manabii, tunajiita mitume, tunajiita waalimu..Lakini habari za watu kuzaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho hatuzijui?, na hata kama tunazijua basi hatuzifundishi wala kushughulika nazo..

Bwana alimwambia Nikodemo kigezo cha kuingia mbinguni, ni sharti mtu azaliwe mara ya pili.. Hivyo na sisi kama hatutawaambia watu juu toba, na umuhimu wa kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu kamwe watu hao hawatakaa wauone(wauelewe), na wauingie ufalme wa mbinguni kwa namna yoyote ile, haijalishi watafunga kiasi gani, watafanyiwa maombezi mengi kiasi gani..watatoa sadaka nyingi kiasi gani, wataponywa kiasi gani..Kama hawajazaliwa mara ya pili basi wajue kuwa hakuna wokovu wowote ndani yao.

Je! Mtu anazaliwaje mara ya pili?

Tunazaliwa kwa maji na kwa Roho, hayo mambo mawili lazima yaende pamoja, pale mtu unapotubu kwa kumaanisha kabisa kuziacha dhambi zako, kwa vitendo, anapokusudia kuacha uasherati, rushwa, wizi, utukunaji n.k na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamwishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO.

Basi hapo anakuwa amepokea ondoleo la dhambi zake sawasawa na Matendo 2:38, Na anapokuwa amesamehewa dhambi zake, kinachofuata kwake si kingine Zaidi ya Roho Mtakatifu kuja juu yake wakati huo huo. Hivyo akitii maagizo hayo yote kwa kumaanisha kabisa kuanza Maisha mapya ndani ya Kristo na kwamba kuanzia huo wakati na kuendelea atamwishia Kristo kwa gharama zozote zile, na kukubali kwenda kubatizwa haraka iwezekanavyo, basi wakati huo huo Roho wa Mungu anaingia ndani yake, Na Hivyo anakuwa ameshazaliwa mara ya pili.

Jina lake linakuwa limeandikwa katika kitabu cha uzima mbinguni. Lakini endapo ukisema mimi nimeokoka, halafu unaukwepa ubatizo ni wazi kuwa bado hujamaanisha kuokoka, na kwa namna hiyo Roho Mtakatifu hawezi kuja juu yako, na ndio maana dhambi kuishinda inakuwa na nguvu juu yako.. kwasababu bado haujazaliwa mara ya pili. Hivyo tendo la ubatizo sio tendo la kulazimishwa au la kushurutishwa, au la kubembelezwa au kusukumwa sukumwa..Ni wewe mwenyewe uliyeona umuhimu wa kwenda mbinguni unautafuta kwa bidii zako binafsi, hata ikikugharimu kusafiri kwenda kutafuta ubatizo mahali mbali na ulipo unafanya hivyo kwasababu ni kwa faida yako mwenyewe.. Na ukifanya hivyo ndivyo utakavyomvutia Roho Mtakatifu kuja kufanya makao yake ndani yako kwa haraka sana, kwasababu anaona ni jinsi gani una kiu ya kuutaka uzima wa milele..Lakini kama utakuwa unavutwa vutwa, ni uthibitisho kubwa bado hujadhamiria kuwa upande wa Kristo, na bado hujaelewa umuhimu wa hicho kitu.

Ubatizo sio dini mpya, agizo la ubatizo halijatolewa na mwanadamu yeyote..Bali limetolewa na Bwana Yesu mwenyewe. Alisema..

Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Unaona wokovu wako haukamilishwi na kuamini tu peke yake..bali pia na kubatizwa. Hivyo wewe mwenye kiu ya kuzaliwa mara ya pili, baada ya kutubu kwako, tafuta binafsi kwa bidii ubatizo. Na ubatizo sio dini mpya wala dhehebu jipya..na maagizo ya Bwana Yesu mwenyewe… Na ubatizo sahihi wa kimaandiko ni ule wa kuzamwishwa katika maji mengi sawasawa na (Yohana 3:23), na uwe kwa JINA LA YESU KRISTO sawasawa na (Matendo 2:38, 8:16, 10:48, na 19:5). Ikiwa ulibatizwa nje ya hapo au utotoni ni vema ukabatizwe tena.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

https://wingulamashahidi.org/2018/07/17/uzao-wa-nyoka/

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

KIWANGO CHA TATU CHA IMANI.

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?

Wengi wetu, tunapoisoma habari ya mwana mpotevu, macho yetu yote yanamwelekea yule mwana wa mwisho..kwasababu sehemu kubwa ya mfano ule ulikuwa unamzungumzia yeye.

Lakini pia ipo siri nyingine imejifichwa kwa yule mwana mkubwa ambayo tukiijua basi, lile wazo la kufiria kumwacha Mungu ovyo ovyo tu litafutika katika vichwa vyetu..

Leo tutajifunza kwa ufupi ni nini tunapaswa tujifunze kwa watoto wote wawili..Sasa kabla hatujaanza nao, embu tuisome tena habari yenyewe jinsi ilivyo kisha tuendelee..

Luka 15:11  “Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili;

12  yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake.

13  Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.

14  Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji.

15  Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.

16  Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu.

17  Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa.

18  Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako;

19  sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.

20  Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.

21  Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena.

22  Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;

23  mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;

24  kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.

25  Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo.

26  Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini?

27  Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima.

28  Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi.

29  Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu;

30  lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.

31  Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako.

32  Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana”.

Sasa ukisoma hapo kwa makini utagundua kuwa kila mmoja alikuwa tayari ameshaandaliwa urithi wake, na wote walikuwa wameshajua kuwa urithi wao utakuwa ni nini..Na ndio maana yule mdogo(ambaye ndiye mwana mpotevu) alikuwa na ujasiri wa kutosha wa kumwambia baba yake amgawie sehemu ya mali inayomuangukia…

Huyu Mwana mpotevu hakuwa mvumilivu..Mfano tu wa baadhi ya watoto wa Mungu leo hii, wakishaona urithi wao mbinguni unachelewa wanakuwa tayari, kuachana na habari za wokovu na kugeukia mambo ya kidunia, wanauuza  urithi wao kama vile Esau alivyouza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa ndugu yake..

Sasa huyu mwana mpotevu akagaiwa urithi wake kama alivyoomba akaenda zake, akawa hana sehemu yoyote ya urithi katika nyumba ya baba yake..Lakini hilo halikumfanya asiwe kabisa mtoto wa Baba.

Lakini yule mkubwa alikuwa mvumilivu, alistahimili yote baba yake aliyokuwa anamfanyia kwa kujibana bana, japokuwa baba yake alikuwa tajiri lakini hakuwahi hata sikumoja kumfanyia karamu yoyote…Na hivyo ndivyo Mungu anavyofanya kwa watoto wake wote anaowapenda  leo hii duniani…Wewe kama ni mwana wake ukiona maisha yako ni ya kawaida tu..usivunjike moyo hiyo haimaanishi kuwa urithi wako ni wa kawaida tu au wewe ni maskini au Mungu anakuchukia..bali fahamu kuwa sehemu yako ni kubwa mbinguni..

Sasa yule mwana mkubwa alipoona ndugu yake amezingatia kurudi kwa baba yao, baada ya ulimwengu kumshinda..Hilo halikumfanya ajisikie vibaya..Bali lililomfanya ajisikie vibaya ni kuona jinsi alivyopokelewa kwa shangwe nyingi na karamu kubwa aliyofanyiwa… Hata leo hii Mungu huwa anawafanyia karamu kubwa sana wale watoto wake ambao wanazingatia kurudi kwake.., Hivyo ikiwa umepotea leo hii mrudie Bwana kwasababu hajakuchukia bado anakupenda sana..

Sasa turudi kwa yule mwana mkubwa alipoona vile alipomwambia baba yake, maneno haya;

‘ mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu;   lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona’.

Sasa sikiliza kwa makini kitu Baba yake alichomjibu…

‘Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, NA VYOTE NILIVYO NAVYO NI VYAKO’.

Nataka uzingatie hilo Neno la mwisho. NA VYOTE NILIVYO NAVYO NI VYAKO… Hilo ndilo lililotuliza moyo wake..

Leo hii ukiwa mtiifu, usipokuwa na haraka ya kumkimbia Mungu, unakuwa mwaminifu hata kufa, unakuwa tayari kuonekana hupendi raha, hupendi maisha kama huyu mwana mkubwa alivyokuwa..anatumika tu kama mtumwa..lakini urithi wote ulikuwa ni wa kwake.

Na wewe ndivyo ilivyo baada ya maisha haya, ikiwa tangu siku ulipookoka hukuwahi kuwa  kiguu na njia, leo huku kesho kule..basi URITHI WOTE Mungu aliotuandalia katika huo ulimwengu unaokuja ni wa kwako..Usizimie tu moyo..Hiyo ndio thawabu yako.

Lakini kama wewe ni mfano wa mwana mpotevu, au bado upo katika dhambi na umenaswa katika mitego mibaya ya shetani, umeingia katika ushirikina na huku ulikuwa unajua kabisa ni makosa, umeua watu, umefanya uzinzi, umetoa mimba, umekula rushwa, umedhulumu watu, umetoka nje ya ndoa, umemkufu Mungu, umeiharibu kazi ya Mungu, ni msagaji, ni mfiraji, na muuzaji wa dawa za kulevya, ni mlevu, n.k. unajijua kabisa wewe ni mwenye dhambi..

Leo hii Mungu anakuita tena umrudie yeye..Anataka uanze upya tena naye. Anataka uwe na moyo wa kujiachilia kama wa mwana mpotevu.. Usiogope atakufikiriaje..Yeye hayupo hivyo..anakusamehe na kusahau unaanza upya tena kana kwamba hujawahi kutenda dhambi..Na urithi atakupa sawa sawa na yule mwana wake wa kwanza kwasababu ulifanya hivyo kwa kutokujua lakini kama utakuwa tayari kuanzia leo kumfuata kwa moyo wako wote..

Leo hii Amani ya Kristo itaingia ndani ya moyo wako kwa namna isiyokuwa ya kawaida, ikiwa upo tayari kuufungua moyo wako, na kudhamiria kutubu kweli kweli..

Na  umeamua saa hii maisha yako yaandikwe kwenye kitabu cha Uzima

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

NI NANI ALIYEWALOGA?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

Print this post