Title April 2020

Pakanga ni nini?

Pakanga ni mmea fulani mchungu uliokuwa unajulikana enzi za kale za biblia, ulikuwa ni mmea unaoota sehemu kame na ulikuwa ni mchungu sana..Hivyo kutokana na sifa ya mmea huo, chochote kile ambacho kingeleta uchungu mkali zamani kiliitwa jina la pakanga Kwa mfano kwenye biblia tunaona neno hilo likitumika sehemu mbali mbali…

Yeremia 23:15 “Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote”.

Soma tena..

Mithali 5:3 “Maana midomo ya malaya hudondoza asali, Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta; 4 Lakini mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga; Ni mkali kama upanga wa makali kuwili”.

Yeremia 9:14 “bali wameenenda katika ushupavu wa mioyo yao wenyewe, na kuandamana na Mabaali, kama walivyofundishwa na baba zao.

15 Basi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitawalisha pakanga, naam, watu hawa, nami nitawapa maji ya uchungu wayanywe.

16 Nami nitawatawanya kati ya mataifa, ambao wao hawakuwajua; wala baba zao, nami nitatuma upanga nyuma yao, hata nitakapowaangamiza kabisa”

Ufunuo 8:10 “Malaika wa tatu akapiga baragumu, nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, iliyokuwa ikiwaka kama taa, ikaanguka juu ya theluthi ya mito, na juu ya chemchemi za maji. 11 Na jina lake ile nyota yaitwa Pakanga; theluthi ya maji ikawa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kwa maji hayo, kwa kuwa yalitiwa uchungu”.

Soma pia (Maombolezo 3:15,19), (Amosi 6:12), utaliona Neno hilo..

Hivyo biblia inapotumia hili Neno pakanga, inamaanisha uchungu mkali usio wa kawaida utakaowapata watu wanaotenda dhambi.. kama vile uasherati, uabuduji sanamu, utoaji wa unabii wa uongo n.k..

Hata leo Maisha yetu Mungu anaweza kuyatia pakanga, ikiwa tutaendelea kuishi Maisha ya kutokujali..Tuombe Bwana atuepushe na hayo mambo, huku tukikaa mbali na dhambi..Magonjwa haya tuyaonayo leo hii ni sehemu tu ndogo ya Pakanga, Ukilishangaisha ni hiyo itakayokuja kuachiliwa siku za mwisho ambapo watu watasaga ndimi, wakitamani vifo viwafikie, lakini mauti itawakimbia.. mambo hayo yatakuja baada ya unyakuo kupita.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

NDUGU,TUOMBEENI.

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

TIMAZI NI NINI

Rudi Nyumbani:

Print this post

NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?

Karibu tujifunze Biblia.

Tukio la Ibrahimu kukubali kumtoa mwanawe kuwa sadaka ya kuteketezwa lilikuwa ni jambo gumu na la kishujaa sana…Kiasi kwamba ilihitajika kuwa mtu mwingine ndipo moyo huo mtu uweze kuwa nao.

Hebu jiulize leo itokee ni wewe umeambiwa hivyo kwamba ukamtoe mwanao wa kwanza wa kiume kuwa sadaka ya kuteketezwa..Kumbuka kwa wakati ule sadaka ya kuteketezwa ilikuwa ni unamkamata mbuzi au kondoo unamchinja, kisha unamkata kata nyama zake vipande vipande, kisha unamweka juu ya madhabahu ambayo ilikuwa inatengenezwa kwa mawe na kuni..halafu unawasha moto na kuichoma ile nyama mpaka iteketee kabisa kuwa jivu…harufu inayotoka ni kama ya nyama choma..Sasa piga mahesabu ni mwanao ndio unamfanyia hivyo, unamshika unamchinja akiwa mzima, anakuuliza baba ni nini unataka kufanya…halafu ghafla unaona machozi yanaanza kumshuka mashavuni.. kisha unamkata vipande vipande bila huruma na kuweka vipande vile juu ya kuni..na kuwasha moto…na kuichoma nyama yake mpaka iteketee kabisa…huku unatazama huku unaisikia ile harufu ya nyama ya mwanao. Utakuwa katika hali gani?

Bila shaka ni jambo gumu…lakini kwa Ibrahimu lilikuwa ni rahisi…Kwanini lilikuwa ni rahisi? Leo tutajifunza siri iliyomfanya Ibrahimu iwe rahisi kwake kutaka kumchinja mwanawe..

Na siri hiyo tunaipata katika kitabu cha Waebrania..

Waebrania 11:17 “Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee;

18 naam, yeye aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa,

19 AKIHESABU YA KUWA MUNGU AWEZA KUMFUFUA HATA KUTOKA KUZIMU; akampata tena toka huko kwa mfano”.

Umeona hapo mstari wa 19?…Siri ndio ipo hapo…Kwamba Ibrahimu alihesabu kuwa hata baada ya kumchinja mwanawe na kuwa jivu…Mungu huyo huyo aliyempa mtoto kimiujiza jiza wakati umri wake ukiwa umeshakwenda sana…anaweza kufanya muujiza wa kumtoa mwanawe kule kuzimu alipokwenda, na kuligueza lile jivu lililochomwa juu ya zile kuni kurudi kuwa vile vipande vya nyama, kisha akavirudisha vile vipande vya nyama vilivyokatwa katwa na kuwa mtu kamili na kuirudisha ile damu iliyomwagika kuwa mtu tena na hata anauwezo wa kulifuta lile wazo kwa mwanawe kwamba alikuwa anakwenda kutolewa sadaka..na Mungu kumpa tena mwanawe akiwa mzima bila dhara lolote kama alivyokuwa mwanzo…

Kwa Imani hiyo ya kumwamini Mungu kuwa anaweza kufanya hayo…ndiyo iliyomfanya Ibrahimu asipate shida kumtoa mwanawe kuwa sadaka ya kuteketezwa….alijua hata kama mwanawe atateketea, ndani ya dakika tano Mungu anaweza kumrudisha tena akawa wake…kwahiyo akahesabu kumtii Mungu ni bora kuliko kusikiliza hisia zake..

Na siri hiyo hiyo ndiyo itakayotufanya na sisi tuweze kumtolea Mungu wetu vilivyo bora pasipo kuangalia hasara tutakazozipata…Tutaweza kumtolea Mungu vilivyo vikubwa ambavyo vinatugharimu tukifahamu kuwa japokuwa tumevipoteza vyote kwa ajili ya Mungu…lakini Mungu bado ana uwezo kuturudishia vile vitu kufumba na kufumbua kama vilivyo…

Sio hilo peke yake…pia tunapomwamini Kristo na kujitwika misalaba yetu na kumfuata ni sawa na tumeyatoa maisha yetu kuwa sadaka kwake…Maana yake ni kwamba tunaishi Maisha ya kujitoa kwa Kristo na kuzipoteza nafsi zetu kwa ajili yake na hata kuifia imani tukiamini kuwa japokuwa tumezipoteza nafsi zetu katika ulimwengu huu kwa ajili yake, lakini bado Mungu wetu anao uwezo wa kutufufua na kutufanya upya tena na kuturudishia uhai wetu na kutupa Maisha marefu na mazuri kuliko haya tuliyonayo hapa duniani…Lakini tusipoamini kwa namna hiyo, kamwe hatuwezi kuyatoa Maisha yetu kwa Kristo kikamilifu. Tutaanza kusema aah..kuna faida gani kumtumikia Mungu…kuna faida gani kuyatoa Maisha yangu kwake na kuishi kuzishika amri zake..

Biblia inasema..

Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.

25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.

26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?”

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

MOJA YA HIZI SIKU TUTAONA MABADILIKO MAKUBWA SANA.

SIKU ILE NA SAA ILE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

SWALI: Habari mtumishi, naomba kujifunza habari hii ya kwamba, agano la kale ni kivuli cha agano jipya.., sasa ile habari ya Yusufu ilikua ina ufunuo gani kwa agano jipya?


JIBU: Ni kweli kabisa agano la kale ni kivuli cha mambo yanayoendelea katika agano jipya biblia inatuambia hivyo katika (Waebrania 10:1, Wakolosai 2:17)

Kwa msingi huo basi ipo habari iliyojificha nyuma ya maisha ya Yusufu ambayo tukiijua tutafungua siri nyingi za Mungu zinazoendelea katika wakati huu wa sasa wa agano jipya.

Maisha ya Yusufu ni mfano wa Maisha ya Bwana wetu Yesu Kristo kabisa tangu alipozaliwa hadi anakufa na hadi atakapokuja tena kuwaokoa wayahudi..

Kama tunavyofahamu, Yusufu mara baada ya kuwaeleza ndugu zake, kuhusu zile ndoto kuwa atakuja kuwatawala, mambo yalikuwa tofauti badala ya kumpenda walimchukia, na mwishowe wakamuuza kwa watu wa mataifa..

Mfano hai wa Bwana wetu Yesu alipokuja duniani, alikuja kwa watu wake(wayahudi), lakini walio wake hawakumpokea (Yohana 1:11), kinyume chake ndipo walipozidi kumchukia pale alipowaambia kuwa yeye ni mfalme, hivyo walichokifanya wakamweka mikononi mwa mataifa ili auawe,..

Na kama vile, Yusufu, alivyokwenda kuuzwa, Misri, na matokeo yake baada ya kutoka gerezani akavikwa mavazi ya kifalme na kuketi mkono wa kuume wa Farao na kukubalika na wamisri wote, akawa mkubwa sana, kule Misri, akajulikana sana na kuwa mkuu,..Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, alipokataliwa na ndugu zake, wayahudi, akauzwa, na kuuawa na kuzikwa na kuwekwa katika kifungo cha kaburi kwa siku tatu…alipotoka kaburini kama vile Yusufu alivyotoka gerezani, hakuwa dhaifu tena…Bwana wetu Yesu aliketi mkono wa kuume wa Mungu baba kama vile Yusufu alivyoketi mkono wa kuume wa Farao.

Na kama vile mataifa yote ulimwenguni yalivyokuja kumwangukia Yusufu, na Bwana Yesu baada ya kufufuka kwake mataifa yote ulimwenguni yanamwangukia yeye sasa..Nafaka yote inatoka kwake mkuu wa uzima Yesu Kristo.

Hivyo kitendo cha Wayahudi kumkataa Yesu kimekuwa neema kwetu. ambapo mpaka sasa sisi tunaifurahia neema hiyo.. (Matendo 13:46-52)

Lakini wakati ulipofika wa Njaa kuipiga dunia na ndugu zake Yusufu kuona umuhimu wa kwenda kutafuta chakula cha uzima, ikawabidi washuke Misri kununua huko, ndipo wakakutana na ndugu yao Yule Yule ambaye walimuuza zamani..

Ndivyo ilivyo sasa, wayahudi wengi bado hawamwamini Bwana Yesu Kristo kama ndiye Yule masihi wao aliyetabiriwa atakayewaokoa, Leo hii ukiwaeleza habari za Yesu, wanaweza hata wakakupiga na hiyo yote ni kwasababu Mungu aliwapiga upofu kwa makusudi kabisa ili sisi watu wa mataifa tupate wokovu biblia inasema hivyo katika (Warumi 11:11-27)..Lakini utafika wakati ambao sasa upo karibuni, njaa ya kiroho itakuwa kali sana kwao…kiasi kwamba watahitaji maji ya uzima..na siku hiyo watamrudia Kristo naye atajifunua kwao tena kwa namna isiyokuwa ya kawaida, nao watamwamini..

Lakini jambo moja la kujifunza katika habari ile ya Yusufu ni kuwa, ule wakati ambao anataka kujifunua mbele ya ndugu zake, aliwaondoa kwanza watu wote wa nyumbani kwake, akiwemo mke wake, walipelekwa mbali na pale,..ndipo akajifunua mbele za ndugu zake..

Tusome..

Mwanzo 45:1 “Hapo Yusufu hakuweza kujizuia mbele yao wote waliosimama karibu naye. Akapiga kelele, na kusema, Mwondoeni kila mtu mbele yangu. Wala hakusimama mtu pamoja naye, Yusufu alipojitambulisha kwa nduguze.

2 Akapaza sauti yake akalia, nao Wamisri wakasikia. Watu wa nyumba ya Farao nao wakasikia”.

Vivyo hivyo kabla Kristo hajajifunua kwa watu wake wayahudi, litatangulia kwanza tukio la UNYAKUO, Kristo atamwondoa kwanza bibi-arusi wake kwanza, na ndipo atakapojidhihirisha kwa wayahudi..

Na ndio huo wakati wayahudi watalia sana,na kumwombolezea waliyemchoma kama tunavyosoma katika Zekaria 12:10-14..kutakuwa na maombolezo makubwa Yerusalemu, wayahudi watatubu dhambi zao kwa kumaanisha.., Na ndio huo wakati Mungu ataipigania Israeli kama ilivyokuwa zamani.. huo wakati hakutakuwa na neema tena kwa watu wa mataifa,..Kitakachobakia ni dhiki tu..

Hivyo tunaweza kuona, ni muda mfupi kiasi gani tumebakiwa nao..Hii neema hivi kwetu sisi watu wa mataifa ipo karibuni inaondoka kwetu na kurudi kwa waliokusudiwa kupewa tangu zamani, lakini sisi bado tunauchezea wokovu. Biblia inatufundisha wazi kabisa mambo yatakayoendelea huko mbeleni ni ya kutisha, hizi ni siku za mwisho.. Na leo hii tunayashuhudia, hivyo huu sio wakati wa mtu kubembelezewa wokovu, ni wakati wako sasa wewe uliyelala kuamka na kumgeukia Kristo katika hichi kipindi kifupi tulichonacho.

Maran Atha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

YONA: Mlango 1

UFANYE NINI KAMA MKRISTO WAKATI HUU WA JANGA LA CORONA?

SAUTI NI SAUTI YA YAKOBO, LAKINI MIKONO NI YA ESAU.

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

HISTORIA YA ISRAELI.

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

SWALI: Shalom, naomba msaada wenu kuna sehemu zimenichanganya.. Kutoka 1:15-20 ..wale wazalishaji wa kimisri.. wanatumia uongo na Mungu anawabariki… swali langu .. Je busara ya uongo inaweza tumika na isiwe kikwazo mbele ya mtu wa Mungu…


JIBU: Kama ulivyosema busara ya uongo..maana yake kuna uongo wa busara na usio wa busara…Wenye busara ni ule wenye nia ya kujenga na usio wa busara ni ule wenye nia ya kuharibu ambao ni wa Adui shetani.

Tuchukue mfano…mtoto mdogo wa miaka 5 anakuuliza mama/Baba eti Watoto wachanga wanatokea wapi?…sasa si busara kumweleze hatua zote za mtoto kuzaliwa..kwamba kuna vitendo vya kama kukutana kimwili vinahusika…kwa umri wake ule hastahili kufahamu hayo mambo..kwahiyo utamwambia tu kama tulivyokuwa tunaambiwa sisi tulivyokuwa wadogo kwamba “wanapatikana kwenye maua mazuri tu”..Huo ni uongo wa busara…na si dhambi.

Hali kadhalika ndugu yako amekuja kuomba msaada kwako na akakueleza siri zake za ndani sana na amekuomba tafadhali sana usimwambie mtu…na baada ya kutoka hapo..baadhi ya watu wanakufuata na kukuambia uwaambie Habari za ndugu yako yule (yaani maana yake wanataka habari za kumzungumzia kutoka kwako)..Sasa hapo ili kuizuia dhambi ya umbea na usengenyaji..na dhambi ya kumwumiza mwingine kwa kutoa siri zake nje…utawaambia tu wale watu waliokuja kutafuta umbea kutoka kwamba “sifahamu mengi sana kuhusu huyo mtu labda mngeenda kumwuliza mwenyewe”…Sasa hapo umetumia Uongo kuwadanganya kwamba hujui mengi kuhusu yule mtu, ili hali unafahamu mengi..Lakini kwasababu umetumia busara kumfichia ndugu yako aibu yake..basi hujafanya dhambi na Mungu atakubariki.

Lakini ukasema kwamba mimi sio mwongo ni mkweli…na kuwaambia wale watu ndio nafahamu kila kitu wacha nianze kutiririka…japokuwa yote utakayoyasema yatakuwa ni ukweli kuhusu yule mtu lakini mbele za Mungu una dhambi.

Au umepishana na mtu mbaya anatafuta Albino, na anakuuliza hivi mtaa huu kuna mtu ambaye ni Albino nataka tufanye dili, na wewe hapo moyoni ukijua kuwa huyu ni mwalifu, na huku unaona kabisa hapo mtaani kwenu yupo mtu wa namna hiyo..na kwa busara ukamwambia yule mtu hakuna mtu wa namna hiyo mtaani kwetu..hapo utakuwa umetumia uongo lakini uongo wa busara wa kuokoa Maisha ya wengine wasio na hatia hivyo, Bwana atakubariki…lakini ukaanza kueleza kila jambo hapo umesema ukweli lakini ukweli wenye dhambi nyuma yake…Na wengi hawafahamu kuwa shetani japokuwa ni baba wa uongo lakini wakati mwingine pia anazungumza ukweli….lakini ukweli wake anaouzungumza ni ukweli unaopotosha…Kwahiyo upo uongo unaojenga na ukweli unaopotosha vile vile…(Kufahamu juu ya ukweli unaopotosha unaweza kututumia ujumbe tutakutumia somo hilo).

Kwahiyo ndio maana Mungu pia aliwabariki hawa wazalishaji wa ki-Misri kwa busara walizotumia…Ingawa walitumia uongo lakini ulikuwa ni kwa lengo la kuokoa Maisha ya Watoto wasio na hatia.

Na kuna mifano mingi katika biblia watu walitumia uongo unaojenga na Mungu akawabariki…kasome Habari za Yaeli katika Waamuzi 4:17-24, na jinsi alivyobarikiwa kuliko wanawake wote katika Waamuzi 5:24, Hali kadhalika kasome Habari za Elisha katika 2Wafalme 6:19-20, na kasome pia Habari za Rahabu yule kahaba katika Yoshua 2:3-7 n.k

Lakini hiyo haifungua fursa ya kuzungumza uongo kila mahali kwa kisingizio kwamba ni busara tunatumia…Sio unaulizwa wewe ni mkristo unajibu la! Kwa kuogopa kufa..kwa kisingizio kwamba unatumia uongo kwa busara kujiokoa Maisha yako!, hiyo siyo busara bali ni kumkana Kristo, na Biblia inasema tuwe tayari hata kuutoa uhai wetu kwa ajili yake na alisema pia anikanaye mimi nami nitamkana mbele ya Baba yangu na malaika zake siku ile. (Mathayo 10:33)…

Vivyo hivyo sio unaona mtu ni mwasherati kanisani unamfumbia macho na kusema unatumia busara kumhifadhi…watu wote wanaofanya uasherati kanisani kwa makusudi baada ya kuijua kweli na Neno la Mungu, biblia imesema waondolewe, wasifichwe..(kasome 1Wakorintho 5). Hali kadhalika na wauaji, watukanaji, waizi na walevi kanisani…

Hali kadhalika hatupaswi kuambiana uongo kwa sababu nyingine yoyote, Ndugu yako anakuuliza upo sehemu fulani wewe unamwambia sipo hapo, kwasababu tu hutaki aje..huo ni uongo wa yule adui, Unaulizwa leo umesali unasema ndio..na wakati hujasali huo ni uongo wa adui..

Bwana atusaidie tuwe na busara.

Maran atha.

Mada Nyinginezo:

UKWELI UNAOPOTOSHA.

NITAPOKEAJE NGUVU YA KUSHINDA DHAMBI?

Mahuru ndio nini?

KUMBUKA, VIVUKO VYA YORDANI VINAKUNGOJA MBELENI.

MOJA YA HIZI SIKU TUTAONA MABADILIKO MAKUBWA SANA.

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

Nilikuwa naomba kujua utofauti kati ya DHAMBI, UOVU na KOSA kibiblia.asante!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

Fukuza tai wote..

Shalom, Jina la mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe daima,.

Karibu tujifunze Neno la Mungu..

Lipo jambo naamini utaongeza katika Habari hii nzuri ya Ibrahimu ambaye tunamwita baba wa Imani, nasi leo tuige hii Imani yake..Embu tusome sasa..

Mwanzo 15:7 “Kisha akamwambia, Mimi ni Bwana, niliyekuleta kutoka Uru wa Wakaldayo nikupe nchi hii ili uirithi.

8 Akasema, Ee Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi?

9 Akamwambia, Unipatie ndama wa miaka mitatu, na mbuzi mke wa miaka mitatu, na kondoo mume wa miaka mitatu, na hua, na mwana njiwa.

10 Akampatia hao wote, akawapasua vipande viwili, akaweka kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege hakuwapasua.

11 Hata tai walipotua juu ya mizoga Abramu akawafukuza.

12 Na jua lilipokuwa likichwa usingizi mzito ulimshika Abramu, hofu ya giza kuu ikamwangukia”.

Kama tunavyosoma Habari hiyo, kuna wakati Ibrahimu alimwomba Mungu amthibitishie kuwa alichomwahidia ni kweli, kama Gideoni alivyofanya..hivyo Mungu akampa maagizo Ibrahimu juu ya sadaka atakayomwandalia ili aitoe, Hivyo Pengine Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema sana, na kwenda mbali kabisa na maeneo ya watu porini, kisha akaindaa akaiweka juu ya kuni, labda kwenye saa moja moja hivi asubuhi alikuwa ameshamaliza shughuli yote ya kuindaa, kinachofuata kwake ni kusubiria sasa aone hatua Mungu anayoichukua..Lakini kilichotokea kwake kilikuwa ni nje ya matarajio yake, alitazamia Mungu angeshuka kwenye muda ule ule, au saa mbili mbili hivi, lakini hakuona chochote,

Akasubiria tena labda kwenye saa nne nne, au saa tano, hakuona chochote, anaingalia tu ile sadaka, aone ni kitu gani Mungu atakwenda kufanya lakini hakuna chochote kilichotokea muda wote huo, mpaka Jua la saa saba linaanza kuwa kali, anaona sasa asogee pembeni kidogo kwenye mti wenye kivuli aendelee kuikodolea macho ile sadaka yake aliyoitoa mapema asubuhi lakini hakuona chochote, mchana kutwa mpaka inafika alasiri, bado akiwa huko porini mwenyewe haoni chochote, akiingalia tu ile nyama, ikianza kukakamaa na mainzi kuongezeka, mpaka sasa wale tai wa angani ambao kazi yao ni kupita porini kutafuta mizoga, wanaiona ipo pale kwa muda mrefu wakidhani pengine ni simba aliila na kuiacha, wakaanza kushuka sasa waile..

Lakini Ibrahimu hakukata tamaa na kuwaachia Tai wale waile sadaka yake aliyoitaabikia tangu asubuhi, japokuwa hamwoni Mungu akimjibu kwa lolote, badala yake kila walipojaribu kutua aliondoka pale kichakani alipokuwa amekaa, na kwenda kuwafukuza..

Aliendelea kufanya hivyo mpaka jua linaanza kuchwa(yaani kuzama), biblia inatuambia, hofu ya giza kuu ikaanza kumwangukia, ni wazi kuwa eneo lile halikuwa eneo lenye makazi ya watu, ni pori nene, hata sadaka yake akawa haioni tena vizuri, ni kama vile Mungu kaitelekeza, au pengine hajairidhia, au pengine alimkosea, lakini katikati ya hofu ile na mashaka yale, muda huo huo alipitiwa na usingizi mzito,..Na ndani ya usingizi ule Mungu akaanza kuzungumza naye, na kumwambia mambo yanayokuja kutokea mbele yake yeye na uzao wake na kumpa ahadi na kumbariki na kumwonyesha nchi atakayompa..

Na alipoamka tu, akashangaa kuona moto umetokea katikati ya ile Sadaka yake, na tayari umeshakwisha kuiteketeza..Ni furaha kiasi gani.kuona unajibiwa maombi yako wazi wazi na Zaidi ya yote Mungu anazungumza na wewe.

Lakini ni nini Mungu anataka tujue ndani ya Habari hiyo?

Wengi wetu, tunakuwa na moyo wa kumtolea Mungu sana katika siku za mwanzoni, na tukishamaliza huwa tunatazama ni wapi Mungu atatubariki, Labda utakuta mtu zamani, alikuwa anatoa ZAKA kwa wakati mbele za Mungu, alikuwa ni mwaminifu kutoa kile alichomwahidia Bwana,..Lakini baadaye alipoona mwezi wa kwanza, na wa pili, na wa tatu, unapita na bado haoni badiliko lolote, au haoni faida yoyote aliyoipata tangu aanze kumtolea Mungu, Zaidi ndio hali inazidi kuyumba hapo ndipo anapokata tamaa na kuacha kuendelea kumtolea Mungu..

Wengine, wanaweza kuwa na nia ya kuendelea kweli kumtolea Mungu, lakini sadaka zao wanaziruhusu zidokolewe na TAI, tofauti na pale mwanzoni wanasema moyoni moyoni aah! Mwaka mzima huu ninatoa fungu la 10, na sioni baraka zozote wacha mwezi huu niiongezee kwenye karo ya shule ya Watoto, kisha mwenzi ujao nitatoa, wengine wanasema, aah, dharura hii imenipata Rafiki yangu anaomba nimtolee mchango wa harusi ngoja mwezi huu nisitoe zaka yangu kwa Mungu..

Ndugu Ibrahimu, hakuruhusu, sadaka yake idokolewe na TAI, japokuwa hakumwona Mungu kwa wakati alioutegemea, lakini aliilinda sadaka yake, kuhakikisha kuwa kile alichoagizwa ndicho atakachokitoa kikiwa kamili hadi dakika ya mwisho muda wote,haijalishi Mungu atawahi au atachelewa.

Lakini tunaona kabla ya Ibrahimu kuingia katika giza kuu, Mungu alimjia na kumtokea, na kuiteketeza sadaka yake..Na kumbariki..

Ndivyo hivyo hata sisi, hatupaswi kuangalia na kusema, tangu nilipoanza kumtolea Mungu, sikuwahi kuona baraka yoyote, wewe endelea kumtolea kwa uaminifu, tu, usiruhusu, sadaka yako imegwe megwe na mambo yasiyokuwa na maana..Haijalishi huoni mabadiliko yoyote kwa miezi au miaka sasa..Lakini endelea kuwa mwaminifu na Mungu aliyemwaminifu Zaidi ya waaminifu, upo wakati ameuweka wa kushusha moto juu ya sadaka yako.. Ukifika huo wakati wewe mwenyewe hutahitaji kusema huyu ni Mungu, kwani mambo yatakuwa wazi mbele ya macho yako.

Tunaona mfano wa Kornelio katika agano jipya, jinsi sadaka zake, zilivyogeuzwa na kuwa ukumbushombele za Mungu (Matendo 10), Jambo lililomfanya sio awe mkristo, lakini hadi sasa tunaisoma Habari yake, katika maandiko.

Vivyo hivyo na sisi, wakati mwingine Mungu anaujaribu uaminifu wetu..Hivyo unapoona huoni faida yoyote sasa katika kumtolea Mungu, usiwe mjinga ukaacha kumtolea au ukaruhusu sadaka zako kudonolewa donolewa, na sababu zisizokuwa na maana yoyote, nataka nikuambie mwisho wa siku hutaambulia chochote, kwasababu Mungu hapokei sadaka kilema.(Malaki 1:14)

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNATEMBEA JUU YA MAJI.

Nini maana ya Kuota unatembea juu ya maji ?.


Kama tunavyojua stori ya mtu mmoja  katika biblia ambaye alirekodiwa kutembea juu ya maji, ni Bwana wetu Yesu Kristo peke yake.

Lakini swali la kujiuliza, ni kwanini aamue kufanya vile? Kulikuwa na umuhiimu gani wa yeye usiku  ule kutembea juu ya maji? Je, ni kwasababu alikuwa anawahi mahali fulani, au alikuwa anawaonyesha tu wanafunzi wake ukuu wake..

Tunafahamu kuwa kila jambo alilolifanya Bwana Yesu, lilikuwa na somo la kutufundisha sisi, na wala sio kutuburudisha..Hata kitendo cha kupaa kwake tu, kilibeba ujumbe mzito kwetu sisi.

Ukifahamu hilo utajua pia sababu ya kwanini wewe unaota ndoto za mara kwa mara unatembea juu ya maji.

Sasa kabla Bwana Yesu usiku ule kutembea juu ya maji utaona alitumia masaa mengi sana kule mlimani katika kusali, hakutembea kwanza bila kuwepo uweponi mwa Bwana muda mrefu..ndipo baadaye sana, akaondoka kuwafuata wanafunzi wake mle baharini, na  alipoikaribia boti walimwona kwa mbali wakaogopa lakini Petro akajitia ujasiri akaomba amfuate kule alipo. Bwana hakumkatalia, akamwambia Njoo, ndipo Petro akaanza kutembea, akapiga hatua kadhaa, akadhani ni rahisi kama anavyofikiria, Lakini wimbi lilipomjia akaogopa akaanza kuzama..

Lakini Bwana Yesu alimwambiaje?, Embu Tusome..

Mathayo 14:25  “Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.

26  Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu.

27  Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope.

28  Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.

29  Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu.

30  Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.

31  Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka”?

Sasa kama ukiitafakari hiyo Habari kwa karibu utagundua somo Kristo alilokuwa anawafundisha wanafunzi wake, ni kuwa YOTE YAWEZEKANA KWA MTU ASIYEKUWA NA SHAKA..

Lakini sasa hayo mashaka mtu anayaondoaje..ndipo baadaye alikuja kuwaambia wanafunzi wake.. jinsi ya kuondoa shaka rohoni..

Mathayo17:21  [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.

Na ndio maana kabla ya tukio lile Bwana alikuwa katika sala muda mrefu..

Hivyo uotapo ndoto za wewe unatembea juu ya maji, au unakimbia juu ya maji au unapaa wakati mwingine.. Ujue ni Mungu anakukumbusha Habari ile ya Kristo kuwa yote yanawezekana..Lakini haiwezekani kirahisi rahisi tu bali kwa kufunga na kuomba (yaani kwa  kujiweka karibu na Mungu kwa wakati mwingi uwezavyo.)

Sasa ikiwa wewe ni mwenye dhambi, hakuna lolote litakalowezekana kwako lile ambalo haliwezekani kibinadamu..Ikiwa Kristo yupo mbali na wewe (yaani hujamkabidhi Maisha yako)..Huwezi kufanya kila kitu..

Vilevile ikiwa umeokoka, na huna muda Mungu, yaani hata huwezi kujitengea muda kusali hata lisaa limoja kwa siku, husomi Neno, huna bidii ya kuishi maishi yampendezayo Mungu,..kamwe huwezi kutenda yale yasiyowezekana kwa macho ya kibinadamu.

Hivyo kama hujaokoka, ujumbe huu ni wako, mkaribishe Yesu maishani mwako leo..Hapo ulipo dhamiria kwanza kuacha mienendo yako yote ya dhambi, kisha ndio uje uombe rehema Mungu akusamehe, kama hujadhamiria basi ni heri usimwombe Mungu msamaha, kwasababu utakuwa unamdhihaki..Geuka kivitendo, ndipo umwomba Mungu rehema na yeye atakusamehe,..

Uthibitisho kuwa amekusamehe, ni ile amani atakayoileta ndani yako..Na kuanzia hapo anza kuishi maisha ya kikristo..nenda kabatizwe ikiwa hujafanya hivyo, na Roho Mtakatifu atakuja juu yako kukusaidia kutimiliza yale ambayo yatakuwa yamesalia.

Vilevile ikiwa wewe ulikuwa tayari ndani ya Kristo lakini ulizembea zembea wakati wako ndio huu wa kuyatengeneza upya, ukizingatia hizi ni nyakati za mwisho..ongeza viwango vyako vya maombi, funga, jifunze biblia sana, kuliko kitu kingine uwezacho kujifunza, pia ongeza viwango vyako vya Maisha ya utakatifu..Na wewe mwenyewe utaona jinsi utakavyoweza kufanya visivyowezekanika kirahisi sana.

Mambo ambayo kwa namna ya kawaida yaliyonekana hayawezaniki kwa mtu kama wewe kuyafanya lakini ukiitii hiyo kanuni ya Kristo hapo ndipo watu watakaposhanga kukuona ukifanya..ndio tafsiri ya ndoto yako..lakini kumbuka tena neno hili..

 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga. (Mathayo17:21) shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

KUOTA AJALI, KUNAMAANISHA NINI?

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

KUOTA UNAKOJOA KITANDANI.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NI WAKATI WA KUJIPIMA, WEWE KAMA MTUMISHI WA MUNGU!

Fuatilia kisa hii,

Binti mmoja akiwa bado mdogo wa miaka 9 aliwauliza wazazi wake, Je! Wazazi wangu Niishi maisha gani ili nifanikiwe,

Wazazi wake wakamwambia, mwenetu, wewe huihtaji kwenda shule kupata elimu, wala huna haja ya kujua jambo lingine lolote kwa wakati huu wewe tafuta pesa kwa namna yoyote ile utakayoona ni rahisi, ukishazipata basi maisha yako yatakuwa sawa..

Ndipo Yule msichana akalizingatia hilo akaendelea kukua, hakujali elimu yoyote ya maisha mpaka alipofikisha umri wa miaka 12 akajiingiza mtaani, Na kule mtaani alikutana na makahaba wakamshawishi ajiingize katika shughuli kama za kwao za kujiuza, atapata fedha kirahisi..Ndipo Yule msichana kwasababu alishauriwa hivyo hivyo pia na wazazi wake, akaona ni ushauri mzuri na yeye pia akajiingiza kwenye biashara hiyo na kweli akaanza kupata fedha, na alipowaletea wazazi wake fedha zile, na kuwaeleza jinsi alivyozipata, basi wale wazazi wake, hawakumuonya kwa lolote japo walijua madhara ya vitendo vile, wakamwacha aendelee, ili awe anawaletea fedha nyingine nyumbani..

Na Yule binti aliendelea kuifanya ile kazi kwa bidii kwasababu aliwaonea huruma pia wazazi wake wasije wakaishi maisha ya shida,..aliendelea hivyo kwa miaka, mpaka akabobea katika hiyo kazi, Na kila mwisho wa mwezi anawapelekea wazazi wake fedha nyingi sana..

Lakini siku moja alianza kuumwa ghafla , hali yake ikabadilika sana, wazazi wake walivyoona vile walijua kabisa mwanao kwa dalili zile lazima atakuwa amesha athirika, lakini kwa hofu hawakumshauri akapime afya yake, bali walimfariji tu, wakimwambia hiyo itakuwa ni hali ya magonjwa ya kawaida tu, uwe unakunywa pain-killer hali itakuwa sawa…endelea tu kutafuta fedha mwenetu..(wakisema hivyo kuogopwa binti asije kujua akaacha hiyo kazi ya kuwaletea fedha).

Lakini Yule binti hali yake ilipozidi kuwa mbaya, mpaka akawa hawezi hata kutembea, ikabidi yeye mwenyewe siku moja, ajiamulie kwenda hospitali kupima, na alipopima afya yake,akagundulika kuwa ana virusi vya ukimwi..

Baada ya hapo akaanza kulia sana, akajutia maisha yake,akitazama na umri wake, ingawa mwenyewe mwenyewe tu alishasikia sikia kuhusu gonjwa hilo lakini hakulitilia maanani sana, kama angelisikia kutoka kwa wazazi wake waliomzaa…akaenda kuwaeleza wazazi wake, akiwahadithia sababu zilizomfanya apate ugonjwa ule, alizoelezwa na daktari, ndipo Akawauliza wazazi wake, kama je walijua kazi ile ingeweza kumletea madhara makubwa kama yale huko mbeleni.. ndio walikiri waziwazi ndio tulijua kuwa utaathirika, lakini tuliogopa kukwambia..Mtoto akasema nyie kama wazazi ulikuwa ni wajibu wenu kunionya mimi kama mtoto madhara yake kwani mimi nilikuwa ni bado sijajitambua, mmesubiri mpaka mimi mwenyewe nimejigundua mpaka dakika hii hali imekuwa mbaya,..Je! ni kweli mlikuwa mnanipenda au mlikuwa mnanitumia tu?

Habari hiyo inatufundisha nini?

Tukiona mpaka leo hii, Mkuu wa nchi anatangaza watu WATUBU DHAMBI ZAO, kwasababu wamemkosea Mungu, na wananchi pia wanafanya hivyo..Halafu sisi tunaojiita ni manabii na mitume, na watumishi, na waalimu hatukuwahi kuwaonya watu kabla ya mambo haya, kuwa ni sababu ya dhambi zetu, mpaka wamegundua wao wenyewe..basi tujue tuna dhambi kubwa mbele za Mungu..

Watu wasiomjua Mungu leo hii wanagundua tatizo, ni nini?.. kuwa ni DHAMBI lakini sisi, miaka nenda rudi, tunawahubiria tu injili za mafanikio, na huku tunajua dhambi bado ipo mioyoni mwao, tunawahubiria amani tu, hatuwaonyi dhambi zao, kisa tunaogopa hawataleta zaka, hawataleta sadaka…Ni nani aliyekuambia utumishi wa Mungu ni zaka tu na sadaka?.

Tujue kuwa watu wanapokwenda kumtafuta Mungu, wanamaanisha kweli kutafuta uzima wa nafsi zao, lakini wewe unapowaelekeza kwenye biashara, na mafanikio, na mwisho wa siku wanagundua kuwa hayawezi kutatua matatizo yao..Wanakuonaje wewe nabii, au mtume au mwalimu?

Hutaki kuwaonya watu kuwa hii dunia inakwenda kuisha na siku si nyingi unyakuo utapita na mpinga-Kristo atanyanyuka, na ataleta dhiki kubwa duniani ambayo hajiwahi kutokea kwa watu ambao watakuwa wameachwa,..kinyume chake sisi tunawahubiria mwaka huu watakwenda China kufanya biashara, na watashusha makontena, watabarikiwa..Hayo makontena wanayokwenda kushusha China mwaka huu yako wapi?.

Hatuwahubirii kuwa yapo mapigo ya vitasa saba, ambayo Mungu atayaleta juu ya dunia nzima kipindi sio kirefu kwa wale wote wasiomcha Mungu, kiasi kwamba magonjwa haya tunayoyaona leo hii, yatakuwa si kitu kulinganisha na hayo yanayokuja huko mbeleni..Ili watu watu watubu leo waache dhambi,tupone!..lakini sisi Tupo busy kuwatabiria tu majumba na magari. Ni nani aliyekuambia mioyo yao ipo kwenye magari na majumba?

Hutaki kujua hali za watu rohoni kuwa mtu akifa leo kama hajaokoka, atakwenda kuzimu, matokeo yake tuwasisitize watengeneze mambo yao na Mungu hata ikitokea wamekufa ghafla, basi wanakuwa upande salama, upo bize, kuanzia mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka, kuwatabiria mema, angali wapo bado katika dhambi. (Mbaya zaidi ni kwamba tunaujua ukweli lakini hatutaki kuwaambia watu). Tafakari ingekuwa ni dada yako wa damu, au ndugu yako..

Na wewe pia unayehubiriwa jiulize, Kristo akirudi leo, utakuwa katika upande upi? Usiridhishwe tu na mahubiri ya vichekesho, na burudani, ndugu ijali roho yako, siku hizi ni za mwisho. Haya tuyaonayo sasa ni mwanzo wa utungu tu…Yanakuja mengine makubwa zaidi na ya kutisha kuliko haya biblia imeshatabiri.

Lakini wakati unafika, ambao Mungu ataleta hukumu juu ya manabii wote wa Uongo, na Watumishi wote, wanaolitumia jina la Mungu isivyopasa..wakati huo unafika, nao upo karibu sana..

Yeremia 23:14 “Katika manabii wa Yerusalemu nimeona neno linalochukiza sana; hufanya zinaa; huenenda katika maneno ya uongo, HUTIA NGUVU MIKONO YA WATENDAO MAOVU, HATA IKAWA HAPANA MTU AREJEAYE NA KUUACHA UOVU WAKE; wote pia wamekuwa kama Sodoma kwangu, na wenyeji wake kama Gomora.

15 Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, TAZAMA, NITAWALISHA PAKANGA, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote”.

Siku zote tujifunze kuiogopa ghadhabu ya Mungu na tujiepushe nayo na wengine pia.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

ANGALIA UZURI WAKO, USIGEUKE KUWA KITANZI CHAKO.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

Shalom karibu tujifunze Biblia, kwasababu Neno la Mungu ndio mwanga wa njia zetu na taa iongozayo miguu yetu.

Ni wapi mahali sahihi pa kulipa zaka je ni kanisani, au kwa mayatima au kwa wajane?..Hili ni swali linaloulizwa na wengi..Leo kwa neema za Bwana tutajifunza..

Andiko linalofahamika na wengi wetu lihusulo mahali sahihi pa kulipa zaka ni hili..

Kumbukumbu 26:12 “Utakapokwisha kutoa zaka, katika zaka zote za maongeo yako mwaka wa tatu, ambao ndio mwaka wa kutolea zaka, umpe zile zaka Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane, wapate kula ndani ya malango yako na kushiba;”  

Sasa kabla ya kuingia kwa undani kulielezea andiko hili..ni muhimu kwanza kufahamu mambo machache yafuatayo..

Kwa mtu aliyeokoka na kuitambua Neema ya Yesu kikweli kweli, Zaka ni jambo la lazima ingawa sio la sheria.(Mathayo 23:23)

Ipo michango mingine tofauti na Zaka..ambayo ni ya muhimu pia kwa kila aliyebadilishwa na kuwa mkristo kuitoa…na michango hiyo ni CHANGIZO, na SADAKA…Hii miwili ni tofauti na Zaka…Zaka ni sehemu ya Kumi ya Mapato…Changizo ni chochote ambacho mtu anaweza kumtolea Mungu kama mchango, (hakina sheria, wala kiwango maalumu)..na sadaka ni dhabihu mtu anayomtolea Mungu wake, inaweza kuwa sadaka ya shukrani, ya malimbuko, au ya ombi ya kutimiziwa hitaji fulani.(Warumi 15:26, 1Wakorintho 16:1 )

Jambo la tatu la kufahamu ni kwamba..Zaka/fungu la 10…Ndiyo sadaka inayopaswa ichukuliwe kuwa ya kiwango cha chini kuliko hizo nyingine zote… haipaswi kuchukuliwa kama ni adhabu wala kitu kikubwa kuliko vingine…(maana yake changizo na sadaka zinaweza kuzidi mara nyingi sana Zaidi ya zaka).

Sasa tukirudi kwenye swali letu..Je! zaka inapaswa itolewe wapi..JIBU NI RAHISI INAPASWA ITOLEWE KANISANI TU!!…Na si penginepo!..Michango mingine inaweza kwenda kwa masikini, kwa wasio jiweza ambayo hiyo inaweza ikawa hata ni nyingi sana kuliko zaka..Kwa mfano mtu aliyepata mapato ya laki moja, maana yake hapo zaka ni elfu 10..kilichosalia ana uhuru nacho kusaidia kiwango chochote kwa wasiojiweza na masikini wa mitaani, kama atawapa elfu 50 au Zaidi ya hapo ni mapenzi yake mwenyewe..na tena ni vizuri Zaidi…Kwasababu ndivyo atakavyojiwekea daraja zuri Zaidi la kubarikiwa kama maandiko yanavyosema heri kutoa kuliko kupokea, lakini ZAKA ni kanisani tu!.

Sasa swali linakuja..kwanini hapo juu kwenye Kumbukumbu la Torati, maandiko yanasema zaka iliwe na maskini, mjane, yatima na Mlawi?.

Jibu rahisi ni kwamba katika Agano la kale…Kanisa la Mungu lilikuwa ni jamii nzima ya wana wa Israeli…Wote waliovuka bahari ya shamu hilo ndilo lililokuwa kanisa la kwanza yaani uzao wa Ibrahimu…Hivyo Zaka zililihusu kanisa hilo lote kwa ujumla…ambapo ilikuwa inawekwa kwa utaratibu maalumu kwamba walio wajane kweli kweli ambao hawana watu wa kuwasaidia, Pamoja na walawi(yaani makuhani na uzao wao) ambao hawa hawakuwa na shughuli yoyote Zaidi ya kuhudumu katika nyumba ya Mungu…pamoja na mayatima wasio na ndugu wala wazazi na wageni walio wayahudi..Kwa utaratibu maalumu Zaka waligawanyiwa wao.

Hivyo kwa ujumla hilo ndilo lililokuwa kanisa la Mungu la kwanza…Utauliza ni wapi wana wa Israeli walijulikana kama ni kanisa…Soma, Matendo 7:37-38. Hivyo zaka ziliwahusu wana wa Israeli tu.. yaani maskini, walawi, wajane, na mayatima na wa Israeli tu..hazikuwahusu maskini waliokuwepo Babeli, wala wajane wa Ashuru.

Na katika Agano jipya…Zaka zinalihusu kanisa la Kristo peke yake…na si penginepo…Yaani maana yake ni kwamba (wajane,yatima, maskini, na walawi ambao kwasasa wanawakilisha wachungaji, waalimu,manabii, mitume na wote wanaohudumu madhahabuni, au wanaoifanya kazi ya Mungu kwa ujumla wake)..Hao ndio wanaopaswa kunufaika na zaka zitolewazo…na si wajane wa mitaani, au maskini tunaopishana nao barabarani…hao wanaweza kupewa michango ambayo mtu anaweza kutoa kama apendavyo..na pia inaweza ikazidi hata kiwango cha zaka..sio dhambi….lakini zaka ni kwa KANISA TU!. Maana yake kwa wajane ambao ni wakristo waliopo pale kanisani ambao ni wajane kweli kweli, wamedumu katika utakatifu na kuosha watakatifu miguu kama maandiko yanavyosema katika…1Timotheo 5:9-16,..Na mayatima ni hivyo hivyo…wale ambao ni wakristo au wazazi wao walikuwa ni wakristo walioshuhudiwa na kanisa.

Sasa swali linakuja..je nikipata zaka nimtafute Yatima fulani au mjane fulani pale kanisani nimpe, au nimtafute mchungaji pale kanisani au nabii nimpe kwa siri, nitakuwa tayari nimeshalipa Zaka??…Jibu ni hapana!..hupaswi kwenda kumpa mchungaji binafsi zaka yako, wala yatima binafsi, wala mjane..Kama unataka kufanya hivyo basi unaweza kufanya kama mchango tu kwao, yaani ukawatafuta wao binafsi kwa fedha yako ukawapa lakini zaka usifanye hivyo…

Tayari tumeshapewa utaratibu katika biblia wa namna ya kulipa zaka..

Tusome…

Matendo 4: 32 “ Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika. 

33  Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote. 

34  Wala hapakuwa na mtu mmoja miongoni mwao mwenye mahitaji; kwa sababu watu wote waliokuwa na viwanja au nyumba waliviuza, wakaileta thamani ya vitu vile vilivyouzwa, 

35  wakaiweka miguuni pa mitume; kila mtu akagawiwa kwa kadiri ya alivyohitaji”.

Umeona hapo?..wote walipeleka sadaka zao na zaka zao miguuni mwa mitume…Na ndipo Mitume wakawa wanawagawia kila mtu kama alivyohitaji (maana yake kila mkristo mwenye mahitaji, na sio maskini wa barabarani), Hivyo wenye mahitaji walikuwa wanachunguzwa kwanza wenye vigezo vya kimaandiko vya kupewa ndipo wanapewa sio tu kila mtu ambaye anashida anapewa tu hapana!..palikuwa na utaratibu…Na kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utakuja kuona kuwa hata bado huo mfumo ulikuwa ni ngumu kuusimamia mitume..mpaka wakaweka watu wengine 7 wenye hekima Zaidi, ambao wataweza kujua na kusimamia ni nani anastahili Zaidi na nani hastahili, na ni nani anapaswa apate Zaidi na nani asipate, Ndio wakapatikana wakina Stefano huko huko ambao ndio walikuwa mashemasi…Sasa Mashemasi kazi yao ndio hiyo kusimamia bajeti ya kanisa na kuigawanya kwa watu kulingana na katiba ya kimaandiko.

Kwahiyo kwa hitimisho katika Agano la kale na agano jipya…hakuna mahali popote zaka walipelekewa watu wa nje ya kanisa…na kulikuwa na utaratibu maalumu. Hivyo kama kuna mtu umemwona ana uhitaji labda umekutana naye barabarani, au mtaani au popote pale nje ya kanisa mpe kwa kadiri uwezavyo lakini si zaka..zaka yako peleka katika kanisa lako unaloshiriki(hiyo inawahusu watakatifu)…Huko kama ni kanisa la kweli la Kristo wanaujua utaratibu wa kimaandiko wa namna ya kuigawanya.

Bwana akubariki..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UFANYE NINI KAMA MKRISTO WAKATI HUU WA JANGA LA CORONA?

UFUNUO:Mlango wa 6-( Maelezo ya Muhuri saba)

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Kutubu sio kuomba rehema kwa Mungu!.


Jina la Bwana libarikiwe.

Ipo tofauti kati ya kutubu na kuomba rehema…Wengi tunaomba rehema lakini hatutubu…Ndugu, Rehema bila Toba ni bure!.

Kuomba rehema hakuna tofauti na kuomba msamaha…Unapomwomba Mtu msamaha hapo ni umemwomba rehema…(akurehemu), Lakini Toba haiombwi, toba ni inafanywa na wewe.

Sasa Toba/kutubu ni nini?

Toba maana yake ni KUGEUKA NA KUCHA KILE ULICHOKUWA UNAKIFANYA. Ulikuwa unakwenda mbele ghafla ukaghairi ile njia uliyokuwa unaiendea na kugeuka nyuma na kurudi ulikotoka au kuiendea njia nyingine kutokana labda na sababu fulani ambazo unazijua wewe….sasa hicho kitendo cha kugeuka na kughairi ndicho kinachoitwa Toba. Lakini kuomba msamaha sio kutubu.

Ili kuelewa tofauti Zaidi tofauti ya vitu hivi viwili..tafakari mfano ufuatao.

Mzazi kamwita mwanawe ili amtume mahali, lakini yule mtoto akamfanyie jeuri mzazi wake yule na kumtusi na akaenda kuendelea na michezo…Wakati yupo njiani anaelekea kwenye michezo njiani, dhamiri ikamchoma akagundua amefanya kosa…Hivyo akaghairi safari yake ya kwenda kwenye michezo, akarudi kwa mzazi wake..akampigia magoti akamwambia nisamehe Mama kwa jeuri yangu nimekosa, nipo tayari kwenda kule ulikonituma.

Sasa mtoto huyo pale alipokuwa njiani na kughairi njia yake na kugeuka na kurudi kwa Mama, Hapo ndipo alipotubu…Na hatua ya pili kwenda kumwomba mama yake msamaha kwa jeuri yake ile pale ndipo alipoomba Rehema. Hivyo umeona tofauti ya mambo hayo mawili?…Hauwezi ukasema umeomba rehema na huku hujatubu…Toba inaanza ndipo ndipo kuomba rehema kunafuata.

Ndio mfano ambao Bwana Yesu aliutoa juu ya wale wana wawili..Tusome

Mathayo 21:28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.

29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.

30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.

31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili…”

Wakati huu wa matatizo haya yaliyoikumba dunia..sio wakati wa kuomba rehema…ni wakati wa kutubu, maana yake ni wakati wa kuacha dhambi…kughairi mabaya tunayoyafanya…kughairi rushwa tulizokuwa tunakula na tunazoendelea kuzila sasa, ni wakati wa kuacha uasherati kabla ya kumkaribia Mungu wetu kumwomba rehema…ni wakati wa kutupa na kuchoma vimini…niwakati wa kutupa mahereni, mabangili, na kuondoa make-up na kutuacha kuwa asili kama Mungu alivyotuumba, na baada ya hapo ndipo tunamwambia Baba tumeacha sanamu zote hizi tunaomba uturehemu..Ni wakati wa kuwarudishia watu vitu tulivyowarusha au kuwatapeli, ni wakati wa kuwasamehe waliotukosea, ni wakati wa kupatana na ndugu zetu ambao tulikuwa tumewachukia mpaka tukawawekea  vinyongo, Ni wakati wa kuacha kutukana kabisa, ni wakati wa kuacha kuwaseng’enya jirani zetu na kuwatakia shari, Ni wakati wa kuacha ULEVI, na kwenda Disko, ni wakati wa kuacha starehe za kidunia na kumgeukia Mungu..

Tukiyafanya hayo, mbele za Mungu wetu ndio tutakuwa tumetubu..kwasababu tutakuwa tumegeuka na kuziacha njia zetu mbaya..na hivyo akiona Toba yetu hiyo ndipo hata pasipo kutumia nguvu nyingi kuomba rehema..yeye mwenyewe ataturehemu kwasababu ni mwingi wa rehema…Lakini tukienda na lipstick zetu midomoni, mbele zake kumwomba rehema, tukienda na zinaa zetu mbele yake kumwomba aturehemu, tukienda na nguo zetu za nusu uchi mbele zake na kumwomba msamaha…Ni sawa na kijana anayekwenda huku amelewa pombe na huku ana sigara mdomoni mbele za Baba yake na kumwambia Baba naomba unisamehe kwa ulevi wangu. Hapo atakuwa anamdhihaki mzazi wake. Na ndivyo tunavyoonekana mbele za Mungu wetu tunapokwenda kumwomba rehema huku bado hatujadhamiria kuacha dhambi zetu tunazozifanya kwa siri au kwa wazi.

Wakati huu tunayo nafasi ya kuomba rehema kwaajili ya nchi Pamoja na nafsi zetu na ndugu zetu…Ni wakati wa kutanguliza TOBA kwanza kabla ya REHEMA. Na hilo linatosha kabisa kupata rehema bila hata ya sisi kutumia nguvu nyingi…Kama Habari ile ya mwanampotevu..alipoghairi Maisha yake yale na kugeuka kuamua kurudi kwa Baba..hata alipokuwa mbali Baba yake alimwona na kumpokea..hakutumia nguvu nyingi sana Kupata rehema kutoka kwa Baba yake.

Bwana akubariki, kama hujampa Yesu Kristo Maisha yako..unangoja nini?..Wewe ni shahidi wa nyakati hizi tunazoishi na majira haya..bado makubwa zaidi ya haya unayoyaona yanakuja huko mbeleni kwa wote ambao wapo nje ya Kristo. Hivyo tubu leo na Bwana atakurehemu na kukupa Roho wake Mtakatifu kwasababu anatupenda sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

MTINI, WENYE MAJANI.

JE MOYO WAKO NI MNYOFU MBELE ZA MUNGU

JE UNAMTHAMINI BWANA?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini kabila la Dani limeondolewa kwenye Ufunuo 7?

SWALI: Hujambo ndugu.Nina ulizo kuhusu kabila 12 ya Yakobo (Israeli) katika mwanzo 49 tunaona kabila la DANI lipo, lakini katika ufunuo 7 kabila la Dani halipo badala yake lipo manase. Kwanini?


JIBU: Katika kitabu cha Ufunuo sura ya 7, kabila la Dani halionekani miongoni wa watu wale watakaoitiwa muhuri siku ya mwisho ili kuiamini Injili itakayokuja kuhubiriwa pale Israeli..Sasa Mungu hakulisahau kabila hilo, hapana bali aliliondoa kwa makusudi kabisa pale na kuliweka hilo la manasae.

Lakini ni kwanini Mungu afanye vile?.. Tukijua jambo hilo jinsi laana za Mungu zilizo kali basi na sisi hatutauchezea wokovu wetu tuliopewa sasa na Mungu wetu.. Kwasababu neema ikishaondoka imeondoka kweli kweli.

Sasa tukisoma kwenye biblia Mungu alishatoa angalizo hili tangu zamani…

Kutoka 20:2 “Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.

3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.

4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”

Unaona Mungu alisema kabisa katika amri zake, kuwa yeye ni Mungu mwenye wivu, na pia anapatiliza maovu yao hata kizazi cha tatu na cha nne..ikiwa na maana kuwa ukifanya dhambi ya makusudi baada ya kuujua ukweli mapatilizo yake yanaweza kuendelea hata kwa vizazi vya wanao huko mbele.

Na tena alisema katika kitabu cha Mambo ya walawi..

Walawi 18:27 “(kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;)

28 ili kwamba hiyo nchi isiwatapike na ninyi pia, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu.

29 Kwani mtu awaye yote atakayefanya machukizo hayo mojawapo, NAFSI HIZO ZITAKAZOYAFANYA ZITAKATILIWA MBALI NA WATU WAO”.

Sasa kabila la DANI lilikuwa ni kabila mojawapo la makabila ya Israeli, na kwamba kabila hili lingetakiwa lionyeshe kielelezo kwa watu wa Mataifa kuwa Mungu wa Israeli ndio Mungu na ndiye pekee anayepaswa kuabudiwa,..Lakini lilifika wakati hilo kabila lenyewe likaamua kumuacha Mungu na kwenda kusimamisha SANAMU katika mji wake, na kuiabudu na kuitolea kafara..Ni kabila pekee katika biblia nzima liliokuwa na ujasiri wa kufanya jambo kama hilo..Habari yote hiyo unaweza kuisoma mwenyewe katika kitabu cha Waamuzi sura ya 17 na 18

Sasa jambo hilo lilimfanya Mungu, alifute katika mpango wake wa wokovu..(sawasawa na Neno lake alilolisema) na ndio maana hapo tunaona katika kitabu cha ufunuo ambacho kinazungumzia habari za siku za mwisho, wakati ambapo wana wa Israeli watarejeshewa tena neema hii ya wokovu tuliyonayo sisi, kabila hilo la Dani halitakuwepo katika hesabu hiyo.

Hiyo inatukumbusha na sisi, tusipoizingatia neema hii ya wokovu, tukawa tunaifanyia mzaha, tunajiweka hatarini kwa Mungu kutuacha na kwenda kwa wengine.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Kwanini kabila la Dani na Efraimu hayaonekani yakiorodheshwa miongoni mwa yale makabila 12 ya Israeli katika Ufunuo 7?

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

KITABU CHA UZIMA

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

MIHURI SABA

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

Rudi Nyumbani:

Print this post