Title 2020

Mkomamanga ni nini? Na katika biblia unawakilisha nini?

Mkomamanga ni nini?


Komamanga ni tunda lenye mbegu ndogo ndogo nyingi ndani yake, ambalo linaliwa kwa kumumunywa mumunywa mbegu zake mpaka utamu wote uishe, au kwa kukamuliwa juisi, ni tunda lenye ladha nzuri sana, na kisayansi linavirutubisho vingi sana mwilini, kama hukuwahi kulifahamu tunda hili tazama picha juu.

Katika biblia tunda hili linawakilisha mfanikio, au uzuri wa aidha taifa, au kitu au mtu.

Kwamfano ukisoma mstari huu;

Kumbukumbu 8:6 “Nawe uzishike amri za Bwana, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.

7 Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima;

8 nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali”;

Utaona Mungu akilitaja tunda hili pamoja na mizabibu, na mitini, kuonyesha uzuri wa nchi ya ahadi ambayo Mungu aliwaambia wana wa Israeli wataiingia, kuonyesha ni jinsi gani nchi hiyo itakavyokuwa nzuri na yenye mafanikio makubwa..

Na ndio maana utaona hata sehemu nyingine, walipoasi, Mungu alitumia miti hii hii ya matunda kama mfano kuonyesha, alivyowafunguia milango ya Baraka na mafanikio katika mambo yao maovu, soma.

Hagai 1:18 “Tafakarini, nawaomba; tangu siku hii ya leo na siku zijazo; tangu siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kenda, naam, tangu siku hiyo ulipowekwa msingi wa hekalu la Bwana tafakarini haya.

19 Je! Mbegu ingali ghalani? Naam, huo mzabibu, wala mtini, wala mkomamanga, wala mzeituni, haikuzaa kitu; tangu siku hii ya leo nitawabariki”.

Soma tena;

Yoeli 1:12 “Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu”.

Pia tunda hili, linawakilisha mafanikio ya kazi za mtu.

Wimbo 6:11 “Nalishukia bustani ya milozi, Ili kuyatazama machipuko ya bondeni; Nione kama mzabibu umechanua, Kama mikomamanga imetoa maua”.

Wimbo 8:1 Laiti ungekuwa kama ndugu yangu, Aliyeyanyonya matiti ya mamangu! Kama ningekukuta huko nje, Ningekubusu, asinidharau mtu.

2 Ningekuongoza nyumbani mwa mamangu, Naye angenifundisha; Ningekunywesha divai iliyokolea,Divai mpya ya mkomamanga wangu.

Soma pia 1Samweli 14:2,

Hivyo kwa ujumla, tunda hili, limetumika kuwakilisha hali ya mafanikio ya taifa, mtu au kitu.

Lakini pamoja hayo ipo nchi ya mikomamanga halisi, kuliko ile ya Kaanani, ambayo wana wa Israeli waliingia lakini bado waliugua, walikufa, waliteseka n.k. , Nchi hiyo si nyingine  zaidi ya Yerusalemu mpya. Huko hakuna shida, wala njaa, wala magonjwa, wala vifo, wala ajali, wala dhiki, lakini  swali ni je! wewe na mimi tunayo nafasi humo?

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

MADHABAHU NI NINI?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Wafilisti ni watu gani.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

Adui yetu shetani, usiku na mchana anatafuta kutumeza, kama biblia inavyosema katika..1Petro 5:8 “ Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzungukazunguka, AKITAFUTA MTU AMMEZE”.

Hivyo anazo njia nyingi za kummeza mtu, na kila siku anabuni njia mpya…Lakini anayo moja maarufu anayoitumia ambayo ni ya MAWAZO.Anachofanya ni kupanda mbegu Fulani mbaya ndani ya mtu, ambayo hiyo mbegu inavyozidi kukuwa ndani yake inamletea kukata tamaa na mwisho kuanguka kabisa. Sasa yafuatayo ni baadhi ya Mawazo ambayo, ukiona yanakuja ndani yako, fahamu kuwa ni mawazo ambayo yamebuniwa na ibilisi, hivyo Yakatae na kuyapuuza.

  1. Mawazo ya kwamba Umemkufuru Roho Mtakatifu, au una dhambi isiyosameheka:

Hii ni silaha moja maarufu ya adui shetani kwa watu wa Mungu. Anayatengeneza mawazo haya ndani ya mtu, na kumfanya aishiwe nguvu ya kuendelea kumtafuta Mungu na kuwa na amani.

Hivyo wazo lolote linalokuja ndani yako kwamba tayari umemkufuru Roho Mtakatifu, kwasababu pengine ulishawahi kusema maneno Fulani wakati Fulani, kuikejeli injili. Au ulifanya dhambi Fulani kubwa sana, ambayo haielezeki, au ulirudi nyuma baada ya wokovu wako, na sasa unataka kutubu uanze upya, Ukiona hilo wazo linakuja ndani yako, kukuambia kuwa ulishamkufuru Roho Mtakatifu, Fahamu kuwa hilo ni wazo la ibilisi asilimia 100, hivyo lipuuzie usilipe nafasi hata kidogo. Hakuna mwanadamu aliyemkufuru Roho Mtakatifu na bado ana hofu ya Mungu..Lakini usipolipuuzia hili wazo na kuendelea kukaa nalo moyoni, litazidi kukua na mwishowe litakufanya usiendelee kumtafuta Mungu, na litakufanya uwe unakosa amani na furaha kila wakati.

  1. Mawazo ya kujiona kama Mungu anakuchukia:

Hii ni silaha nyingine ya shetani, kuharibu watu wa Mungu..Ukiona upo kwenye hili tatizo kwamba unaona kama Mungu anakuchukia, hakupendi anawapenda tu baadhi ya watu Fulani, au watumishi wake..Jua tayari upo katika shambulizi la adui yako shetani, tayari upo katika anga

zake anakuharibu kidogo kidogo. Fahamu kuwa Mungu hamchukii mtu yeyote yule hata yule mwovu kuliko wote, ingekuwa anakuchukia sidhani kama angekuumba uishi katika hii dunia, mpaka umejiona umetokea kwenye hii dunia, jua ni kwaajili ya upendo wake kwako. Hivyo hilo wazo la kujiona hupendwi ni kutoka kwa adui.

  1. Mawazo ya kujiona kwamba Mungu hasikii maombi yako:

Mungu anasikia maombi ya kila mwanadamu..kama kilio cha dhambi tu kinamfikia mbinguni, kwanini maombi yasimfikie?. Yanamfikia isipokuwa majibu ya maombi yanatofautiana mtu na mtu. Wapo ambao watapeleka maombi yao watajibiwa kama walivyoomba na wapo ambao hawatajibiwa, sasa wale ambao hawatajibiwa maombi yao, ipo sababu, na Mungu wa upendo atahakikisha wanaijua hiyo sababu kwa njia yeyote ile, ili warekebishe wapokee majibu ya maombi yao.. Kamwe hawezi kumwacha mtu yeyote hewani tu!, bila kumpa sababu ya kwanini hajapokea majibu ya maombi yake..Kinachowakwamisha wengi ni kukata tamaa

kirahisi…Unapokata tamaa tayari umekatisha safari yako ya kupokea baraka zako ukiwa katikati.

Kwa mfano, mtu anaweza kwenda kumwomba Mungu naomba unipe mume bora, au mke bora..lakini ukimwangalia ni kahaba, hivyo Mungu mwema hawezi kumpa kitu kizuri kabla hajamtengeneza kwanza…Kwahiyo wakati anasubiria majibu ya maombi yake, Mungu anamletea mhubiri, ambaye atamhubiria wokovu, na njia bora ya kuishi Maisha ya kumpendeza Mungu, anapotii na kukubali kubadilika na kuacha njia zake mbaya..Mungu ndipo anamletea jibu la

maombi yake aliyomwomba, analetewa mwenzi mwema wa Maisha, ambaye hatamsumbua na aliye mcha Mungu kama yeye. Lakini kama hatatii bado anataka kuendelea kukaa na ukahaba wake ndio atakaa hivyo hivyo kwa muda mrefu mpaka siku atakapofunguka akili, atarudia kuomba yale yale maneno lakini hataona majibu…

Hizo tu ndizo sababu za Mungu kuchelewesha majibu, lakini si kwamba Mungu hasikii maombi… Anayasikia, isipokuwa katika ujubuji wake ndio suala lingine.

Hivyo ukikosa kujiamini na kufikiri Mungu hajawahi kusikia maombi unayoomba chumbani kwako, au barabarani unapotembea, au kazini unapofanyia kazi…basi jua umeshambuliwa rohoni na adui shetani. Kazana kujua kwanini hujapata majibu lakini usifikiri kwamba hujasikiwa kabisa. Tayari umeshasikiwa, na uliloliomba limeshafanyiwa kazi, wewe fuatilia ombi lako lipo katika hatua gani sasa.

Marko 11:24 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu”.

  1. Mawazo ya kufikiri kwamba Siwezi kumpendeza Mungu wala kuwa mtakatifu:

Ndugu ukifikiri kwamba unaweza kufikia kiwango cha utakatifu kiasi kwamba huna kosa kabisa..basi fahamu kuwa hutaweza kamwe kumtumikia Mungu, kumbuka bado tunaishi duniani,

na lazima tutakuwa na kasoro nyingi, ambazo nyingi hatuzijui kama tunakosea…Sasa kama Mungu angezihesabu hizo biblia inasema hakuna mtu angesimama. Baada ya kuokoka ukiamka asubuhi usianze kukaa kuhesabu makosa yako, ukifanya hivyo kamwe hutaweza kumtumikia Mungu, na shetani atakusumbua sana na kila dakika atakuletea mawazo wewe ni mbaya, wewe hustahili, wewe hufai, wewe umeshamkosea Mungu, hufai, hufai n.k

Ukiamka asubuhi anza kuhesabu ni mazuri mangapi umemfanyia Mungu wako, na kama hujafanya kabisa ndipo uhuzunike, na tafuta kufanya, na jioni ukirudi..Mwambie Bwana asante kwa hichi kizuri ulichoniwezesha kukufanyia siku ya leo, na pia naomba nisamehe makosa yangu

yote niliyokukosea wewe pasipo kujua siku ya leo. Na kama unayakumbuka baadhi uliyoyafanya hakikisha kesho unayarekebisha, na ukishatubu tu usianze kujilaumu laumu!..Ukifanya hivyo utaruhusu mashambulizi ya shetani kukuvamia na kukuletea mawazo yale yale kwamba Mungu

alichukizwa na wewe jana, hivyo hawezi kuendelea kutembea na wewe leo…Kwahiyo siku zote Vaa ngao ya Imani, ili uweze kuizima hiyo mishale ya adui. Mungu wetu wa upendo hakai huko mbinguni na karatasi na kalamu akitiki mabaya tunayoyafanya baada ya sisi kuokoka…hafanyi hivyo, yeye yupo kutazama mema yetu, maadamu tumeshaokoka na

kumwamini na tumeweka mbali Maisha ya dhambi. Basi tunakuwa tunahesabiwa haki kwa Neema na si kwa matendo. Na hivyo kidogo kidogo anatutakasa mpaka unafika wakati tunakuwa wakamilifu kabisa kwake.

Hivyo hizo ni silaha 4 za adui yetu shetani. Sasa kama hizi Habari ni mpya kwako, na kama zimekufungua macho, basi ni dalili ya kwamba ulikuwa huna Ngao mkononi mwako, hivyo

ulimfungulia shetani nafasi ya kukushambulia ndio maana husongi mbele kiimani, na hiyo ni kutokana na kwamba pengine nafasi ya kutafuta kumjua Mungu Zaidi katika Maisha yako ni ndogo, au ulikuwa umesongwa na hivyo kulifahamu Neno imekuwa ngumu kwako, kwahiyo nakushauri mtu wa Mungu usiruhusu tena kusongwa..Neno hili wakristo wote waliofanikiwa ambao umeona wamesimama na hawapelekwi ni kwasababu, wana ngao za Imani mikononi

mwao, ni kwasababu Hivyo vipengele 4 hapo juu wamevishinda tangu zamani. Hivyo ni wewe peke yako umebaki.

Anza kumtafuta Mungu kwa bidii, anza kusoma Neno kwa bidii, usipitishe siku bila kushika biblia, na usomapo usisome kwa kutimiza wajibu, Ukilisoma Neno la Mungu na kulielewa ndivyo linavyokaa ndani yako, na linakupa Imani na maarifa, na ndivyo linavyokuweka huru, Ukilikosa hilo kamwe usitegemee kumshinda shetani, na wala kamwe usitegemee kama utaweza kumtumikia Mungu. Kwasababu shetani hawezi kuruhusu umtafute Mungu kirahisi rahisi hivyo, ni lazima akuletee hivyo vita vya kimawazo, akishinda hivyo atakuletea na vya nje, sasa ni wajibu wetu kufahamu kuwa tupo vitani. Ni lazima upambane kumjua Mungu.

Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

KWANINI LEO HII KUNA KUNDI KUBWA LA WAKRISTO WALIORUDI NYUMA?

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

SWALI: Nini maana ya huu mstari? Mhubiri 10:2 “Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume; Bali moyo wake mpumbavu upo mkono wa kushoto”.


JIBU: Mstari huo unatuonyesha wazi kuwa kumbe moyo wa mwanadamu unao upande wa kukaa, haupo tu hewani bila una makao, ni aidha ukae upande wa mkono wa kuume, au upande wa mkono wa kushoto. Kumbuka moyo unaozungumziwa hapo sio huu wa nyama, bali ni ule wa rohoni ambao unaeleza tabia ya mtu.

Kama tunavyojua mkono wa kuume ni mkono wa heshima, mkono wa kuonyesha kujali, na usafi, tofauti na mkono wa kushoto, na ndio maana ukikutana na mtu yeyote mahali fulani huwezi kutoa salamu kwa mkono wa kushoto, bali utampa mkono wa kulia kuonyesha heshima, na kujali.

Vivyo hivyo na mioyo yetu, ikiwa haionyeshi Heshima, na usafi na kujali kwa Mungu na kwa wanadamu, rohoni inaonekana ipo upande wa kushoto. Na siku ile ya hukumu Mungu atatuweka upande wa mkono wake wa kushoto. Lakini tukiwa wasafi rohoni, na tunamjali Mungu na watu(hususani ndugu katika imani), siku ile Bwana atatuweka upande wa mkono wake wa kuume ambapo moyo upo.

Vifungu hivi vinaeleza wazi tabia zilizo upande wa mkono wa kuume na ule wa kushoto, Tusome;

Mathayo 25:31 “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;

32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;

33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.

34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;

35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.

Umeona, hivyo Bwana atujalie tuwe na hekima, kuhakikisha kuwa mioyo yetu haipo upande wa kushoto, kwa tabia zilizoorodheshwa hapo juu.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

Shetani ni nani?

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

JE UNAMTHAMINI BWANA?

UFUNUO: Mlango wa 1

YAKINI NA BOAZI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

PALE AHADI ZA MUNGU ZINAPOKUJARIBU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha tuzidi kuyatafakari maneno ya uzima maadamu siku ya ukombozi wetu inazidi kukaribia.

Mungu anapotupa Neno la ahadi, huwa haiishii hapo tu, bali kuna majira yanafika, hizo ahadi zinatujaribu, Utamwona Yusufu pindi alipopewa maono ya kuwa utafika wakati baba yake na mama zake na ndugu zake watamwinamia, (yaani kwa ufupi atakuwa mkuu), tendo lile alidhani lingetokea tu papo kwa papo, Lakini kama tunavyojua habari mambo ndio yalikuwa kinyume na matarajio yako, kwanza aliuzwa na ndugu zake, akaenda kuwa mtumwa Misri.

Na alipofika kwenye ile nyumba ya Potifa kama mtumwa walau akaanza kuona unafuu pale alipofanywa kuwa msimamizi wa mali na kazi za bosi wake, pengine akadhani Mungu kashaanza kumkumbuka, lakini mambo yakabadilika tena baada ya kukutana na mke wa Potifa na kumsababishia apelekwe gerezani, akafungwa  huko muda mrefu, tena lile gereza la wafungwa wa wafalme ambao hao hawana mdhamana, wanasubiria siku yoyote tu kuuawa.

Sasa mambo hayo yote Yusufu aliyoyapitia, hayakuletwa na shetani, bali ni Mungu aliyeruhusu ayapitie, zilikuwa ni ahadi za Bwana zikimjaribu kwa wakati ule. Aone kama Je! bado atashikamana na utimilifu wake kabla ya kuzipokea zile ahadi zenyewe?

Zaburi 105:17 “Alimpeleka mtu mbele yao, Yusufu aliuzwa utumwani.

18 Walimwumiza miguu yake kwa pingu, Akatiwa katika minyororo ya chuma.

19 Hata wakati wa kuwadia neno lake, AHADI YA BWANA ILIMJARIBU”.

Jambo kama hilo, tunaliona kwa Ibrahimu pia, Mungu alimuahidia kuwa atamfanya kuwa baba wa mataifa mengi, na uzao wake utakuwa mwingi kama nyota za mbinguni, lakini jambo hilo hakulipata siku hiyo hiyo, hakulipata mwezi huo huo, hakulipata mwaka huo huo..Bali ilipita miaka mingi, zaidi ya 25,akiwa mzee wa miaka karibu 100, ndipo dalili zinaanza kuonekana onekana kwa kumpata Isaka.

Lakini ghafla naye tena dalili hizo zinaenda kuzimwa, pale Mungu anapomwambia, amchukue Isaka akamtoe kafara mbele zake, kwa namna ya kawaida ni rahisi kusema huyu sio Mungu, lakini Ibrahimu alitii kwasababu alijua ni wakati wa Ahadi za Bwana kumjaribu. Akapanda na Isaka kule mlimani,  akijua kabisa tayari hana mtoto, wazo la kuwa Mungu ataghahiri halikupita katika akili yake hata kidogo.

Mwanzo 22:1 “Ikawa baada ya mambo hayo MUNGU ALIMJARIBU IBRAHIMU, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.

2 Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.

3 Ibrahimu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu.”

Umeona, agano la kale ni kivuli cha agano jipya.

Na sisi kama kanisa, Mungu ametupa ahadi zilizo kubwa zaidi ya akina Ibrahimu na Yusufu, tumepewa maono makubwa sana, na maono yenyewe ni kuurithi ufalme wa mbinguni, ahadi za kuketi pamoja na Yesu katika kiti chake cha enzi kule mbinguni, ahadi za kufanywa nguzo, ahadi za kuwa wafalme wa makuhani wa Bwana katika ile Yerusalemu mpya itakayoshuka kutoka mbinguni kwa Baba ambayo njia zake ni za dhahabu,

Unategemea vipi ahadi hizi zisitujaribu?

Zitatujaribu tu wakati mwingine, Mungu anafanya hivyo ili aone je! ni kweli tumemaanisha kwenda mbinguni au la? .Hivyo wewe na mimi tukipitia mazingira ya upingamizi, usifikiri kuwa ahadi ya Mungu ya kuwa mfalme na kuhani imebatilika kwetu…La! Haijabatilika hata kidogo..ipo pale pale.

Kupitia vikwazo vya namna mbalimbali kwa ajili ya imani yako, usitetereke hata kidogo, wala usikufuru, macho yako yasiache kuzitazama ahadi Mungu alizokuwekea mbele kama Ibrahimu na Yusufu. Hata kama hakuna dalili inayoonekana leo, fikiri juu ya uzuri wa mbinguni, Kwasababu moja ya hizi siku, parapanda italia, wafu watafufuliwa, kisha kwa pamoja tutaicha hii dunia kwa mara ya kwanza, tutakwenda mbinguni katika karamu tuliyoandaliwa na Bwana Yesu, tutaisheherekea hiyo kwa kipindi cha kirefu, tutazuru mitaa yote ya mbinguni, tutaona mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, hapo tukiwa na miili ya utukufu, isiyoumwa, isiyozeeka, isiyougua, kisha tutarudi hapa duniani kutawala na Bwana Yesu kwa kipindi cha miaka 1000 kama wafalme, na baada ya hapo tutaingia katika ile Yerusalemu mpya, ambapo Makao ya Mungu yatakuwa pamoja na sisi wanadamu milele.

Mambo tuliyoandaliwa huko, hayajawahi kuingia katika moyo wa mwanadamu yoyote, biblia inatuambia hivyo. Kwahiyo tusichoke kumngojea Mungu, tusichoke kuzingojea ahadi za Bwana za milele. Utaona pamoja na kwamba Ibrahimu na Yusufu na Ayubu walipitia katika mapito yote yale, lakini mwisho wao ulikuwa ni mzuri, wa kufundisha na wa kuokoa na sio wa kukomoa, Yusufu kuuzwa utumwani ni kwasababu njaa ilikuwa mbele, hivyo alihitajika kwenda Misri kuwaandalia ndugu zake makao, na chakula, Ibrahimu kumtoa kafara mwanawe, ilikuwa ni ujumbe kwa kanisa juu ya dhabihu ya Yesu Kristo. N.k.

Vivyo hivyo na sisi tuliookoka, tusipozimia mioyo ahadi zetu zitatufikia.

Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;

31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Maran Atha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

MADHABAHU NI NINI?

JE KUVAA PETE NI DHAMBI?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?

Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

Biblia inasema shetani ni Baba wa uongo Yohana 8:44, Maana yake kazi yake ni kusema uongo, na uongo sio wa kudanganya watumishi wake, hao siku nyingi tayari ni wa kwake…anachokifanya ni kuwafundisha watumishi wake uongo, ili wakadanganye wengine…Ndio maana anaitwa Baba wa uongo.

Na uongo wake unakaribia sana kufanana na ukweli…ili hela bandia iweze kuwadanganya wengi ni lazima ikaribiane sana kufanana na hela halali…kwahiyo jinsi uongo unavyozidi kukaribiana na ukweli ndivyo unavyokuwa na nguvu zaidi..

Kwahiyo shetani anajua kabisa Neno la Mungu ndio KWELI…Kwahiyo ili atengeneze uongo wenye nguvu kubwa ni lazima autengeneze unaokaribiana sana kufanana na Kweli ya Neno la Mungu…maana yake ni kwamba atatumia maandiko/biblia kuupotosha ukweli katika utashi wa hali ya juu kiasi kwamba ni ngumu kugundua kama Neno hilo limepotoshwa…Huo ndio uongo wa shetani unaozungumziwa katika biblia…

Kama unakumbuka wakati anamjaribu Bwana kule jangwani, utaona alikuwa anatumia maandiko yaani neno la Mungu…hakuwa anatumia kitabu cha sayansi au mithali za wahenga…bali alikuwa anatumia Neno la Mungu kwamba imeandikwa hivi au vile…kiasi kwamba kama Bwana asingekuwa mtu wa Rohoni wa kulielewa Neno sana, na kufananisha maandiko vyema angenaswa na mtego wa Ibilisi na angeusikiliza uongo wake.

Na hadi leo mbinu ya shetani ni hiyo hiyo, ya kuligeuza Neno la Mungu la kweli kuwa uongo….

Kama wengi wetu tunavyojua Mungu alimwagiza Musa kutengeneza “Yule nyoka wa shaba” ambaye aliambiwa amnyanyue juu ili kila amtazamaye ambaye kaumwa na nyoka aweze kupona, andiko hilo linapatikana katika kitabu cha Hesabu 21:6-9.

Sasa kupitia andiko hili shetani kawadanganya watu kuwa Ni halali kutengeneza sanamu ya nyoka, au ya mtu Fulani katika biblia, au ya kitu na kuitazama, na kuisujudia au kuiheshimu na hata kuiabudu ili kupata faida Fulani kutoka katika hiyo, labda uponyaji au Baraka.

Sasa tukirudi katika habari hiyo ya nyoka wa shaba..utaona kuwa Mungu hakuwaambia wana wa Israeli waiabudu, wala waiangukie, wala waipe heshima yoyote, wala haikuwekwa pale kama kitu kitakatifu…bali Mungu aliiweka pale kwa lengo la kuwatafakarisha upumbavu wao walioufanya na wanaoufanya wa kumnung’unikia Mungu..na hivyo Mungu akawaonyesha kwamba amewachapa kwa kiboko cha nyoka (Ndio maana utaona ni fimbo iliyozungushiwa nyoka)..Ili watafakari, na kutubia uovu wao…na waliotazama na kutafakari ndio waliopona.

Kama wewe ni msomaji wa biblia utakuja pia kuona kuna wakati wafilisti walilichukua sanduku la Agano kutoka Israeli na Mungu akawapiga kwa majipu mabaya na tauni…ndipo wafilisti wakatengeneza sanamu za majibu na za panya kuzipeleka Israeli kuonyesha kwamba wametambua wamefanya kosa na wametambua kwamba Mungu kawaadhibu kwa majibu na Tauni ambayo inatokana na panya..na hivyo wanatubu..na walipofanya hivyo ndipo Mungu akaacha kuwapiga….kasome 1Samweli 6:1-11.

Sasa wafilisti hawakutengeneza hizo sanamu kwa lengo la kuziabudu, wala kuzipa heshima, wala kuzitumikia…bali kwa lengo la kutubu (kwamba wametafakari makosa yao na kujua mkono wa Mungu umekua juu yetu kama mfano wa hayo majibu)..

Kwahiyo hata wana wa Israeli Mungu aliwaambia waitengeneze sanamu ile ili iwatafakarishe, na ili wamwogope Mungu..kwamba wakimuudhi Mungu wao..anaweza kuwachapa kwa fimbo ya kitu chochote kile, inaweza kuwa fimbo ya nyoka, fimbo ya wanyama wengine wakali, fimbo ya magonjwa au chochote kile, na hivyo wamweshimu na kuzishika amri zake. Na wachache waliotii na kuelewa ujumbe walipona lakini wengine walikufa…na hata baada ya janga hilo kuisha kuna wachache ambao bado walikuwa hawajamwelewa Mungu wakaihifadhi sanamu ile na kuanza kuiabudu na kuifanya ni chombo cha ibada…pasipo kujua kuwa wanamchukiza Mungu kwa kuiabudu ile fimbo ya nyoka wa shaba…Mungu akawa anawaadhibu kwa kuiabudu lakini bado wakawa na shingo ngumu kutoivunja vunja ile fimbo ya nyoka wa shaba. Sanamu ile ilikuja kuendelea kupata umaarufu, hadi kufikia Israeli wengi kuiabudu.

Mpaka siku ilipofika alipotokea mtumishi wa Mungu, Mfalme Hezekia, alipoona Taifa linapotea kwa ibada za sanamu, kwa kuiabudu hiyo sanamu ya nyoka wa shaba…ndipo aliponyanyuka na kwenda kuivunja vunja na kuitowesha kabisa, na Mungu akambariki kwa kufanya hivyo.. Tusome..

2Wafalme 18:1 “Ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea, mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Hezekia, mwana wa Ahazi, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.

2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Abiya, binti Zekaria.

3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, mfano wa yote aliyoyafanya Daudi, baba yake.

4 Alipaondoa mahali pa juu, akazibomoa nguzo, akaikata hiyo Ashera; AKAIVUNJA VIPANDE VIPANDE ILE NYOKA YA SHABA ALIYOIFANYA MUSA; MAANA HATA SIKU ZILE WANA WA ISRAELI WALIKUWA WAKIIFUKIZIA UVUMBA; NAYE AKAIITA JINA LAKE NEHUSHTANI

5 Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israeli; hata baada yake hapakuwa na mfano wake katika wafalme wote wa Yuda, wala katika hao waliomtangulia.

6 Maana alishikamana na Bwana, hakuacha kumfuata, bali alizishika amri zake Bwana alizomwamuru Musa”.

Umeona hapo mstari wa 4 ???…Aliivunja vunja maana yake ni kwamba, halikuwa agizo la Mungu kuiabudu, wala kuitolea uvumba, wala kuipa heshima yoyote ile…ni machukizo makubwa!.
Na sanduku la Agano ni hivyo hivyo, Mungu alitoa maagizo kwa Musa litengenezwe lakini hakuna mahali popote Mungu aliagiza liabudiwe…hata hivyo wana wa Israeli wakati Fulani walipojaribu kuligeuza kuwa ni chombo cha Ibada, liliwaletea laana badala ya Baraka kasome 1Samweli 4:1-11. Hakuna kitu chochote kile kwenye biblia nzima agano la kale wala agano jipya kinachoitwa sanamu ambacho Mungu alitoa maagizo kiabudiwe wala kitukuzwe. Ni uongo wa shetani ambao lengo lake ni kuugeuza ukweli wa Neno la Mungu.

Hivyo ndugu..usidanganywe na uongo wa shetani ambao unakaribia sana kufanana na ukweli..usidanganyike na kuabudu sanamu, usidanganyike na kuisujudia sanamu ya bikira Maria wala ya Petro, wala inayojulikana kama sanamu ya Bwana Yesu, wala usiisujudie misalaba, wala kitu chochote kile…Ni machukizo makubwa…biblia inasema..

Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

Na pia inasema..

Ufunuo 21:7 “Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao?

NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!

WAKATI WA BWANA KUKUVUSHA, NI LAZIMA ARUHUSU JESHI LA ADUI KUNYANYUKA.

MIJI YA MAKIMBILIO.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

Rudi Nyumbani:

Print this post

“Bonde la vilio” ni nini katika biblia?(Zaburi 84:6)

“Bonde la vilio” ni nini katika biblia?(Zaburi 84:6)


Neno hili linaonekana mara moja tu katika biblia, tunalitosoma katika mistari hii;

ZABURI 84:4 “Heri wakaao nyumbani mwako, Wanakuhimidi daima.

5 Heri ambaye nguvu zake zatoka kwako, Na njia ziendazo Sayuni zimo moyoni mwake.

6 WAKIPITA KATI YA BONDE LA VILIO, Hulifanya kuwa chemchemi, Naam, mvua ya vuli hulivika baraka 7 Huendelea toka nguvu hata nguvu, Huonekana Sayuni kila mmoja mbele za Mungu”.

Ukianzia kusoma juu Zaburi yote hiyo ya 84 utaona inazungumzia uheri wa watu wale, wanaopenda kwenda nyumbani kwa Bwana kumtafakari yeye daima,kumuhimidi yeye, kumwabudu yeye, kusikiliza maneno yake, unazungumzia juu ya watu wale wanaopenda wakati kuwa uweponi mwa Mungu, nyumbani mwake kumtafakari yeye,..

Biblia inasema, watu wa namna hiyo hata ikifika wakati wakapita katika bonde la vilio, Mungu ataligeuza bonde hilo kuwa chemchemi ya maji, na  kulinyeshea mvua ya vuli.

Kibiblia yapo mabonde mengi, kama vile lilivyo bonde la uvuli wa mauti, ambalo tafsiri yake ni sehemu ambayo mtu atapita haoni tumaini la kuishi tena, inaweza ikawa ni maadui wanamwinda, au magonjwa yanamsumbua kama vile Kansa,Ukimwi n.k., au kesi za mauaji zinamkabili, au sehemu za hatari sana anazipitia sasa n.k..Hilo ndio bonde la Mauti ambalo Daudi alisema nijapopita hapo, sitaogopa mabaya kwa maana Bwana atakuwa pamoja nami (Zab 23:4).

Vivyo hivyo Bonde la vilio nalo lipo, bonde hili ni bonde la ukame, kiu na njaa, bonde la kutokuwa na kitu, na kupungukiwa kabisa, lakini kwa mtu Yule ambaye amekuwa akipenda kuwepo nyumbani mwa Bwana daima kumuhimidi, kumshukuru, kumsujudu, kumwabudu..Mungu anasema bonde hilo kwake litageuzwa na kuwa chemchemi ya vijito vya maji, na mvua ya vuli italinyeshea.

Wana wa Israeli walipita katika bonde hili walipokuwa jangwani , wakalia sana kwa kukosa maji, lakini Mungu aliwapasulia miamba maji yakatoka kama mto wakanywa wakafurahi.(Kutoka 17:1-7, Hesabu 20:1-8) Vivyo hivyo na mtu Yule ambaye Nyumbani kwa Mungu (Kanisani) na sehemu yeyote ile Mungu ambayo Mungu anakaa ndio mahali pake pa kustarehe. Mungu anasema hata ajapopitia wakati mgumu Mungu atakuwa mvua yake ya vuli.

Na ndio maana mtunzi wa Zaburi akamalizia na kusema..

Zaburi 84:10 “Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu”.

Bwana atujalie na sisi tuone umuhimu wa kuwepo nyumbani mwake wakati mwingi.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko miaka elfu”?

FAIDA ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

BONDE LA KUKATA MANENO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao?

SWALI: Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao au kwa watu wote wa mataifa..Maana yeye mwenyewe alisema katika Mathayo 10:5, kwamba wasihubiri kwa watu wa Mataifa.


JIBU: Tusome..

Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie.

6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”

Ni kweli Bwana aliwaagiza wanafunzi wake wasiende kuhubiri Injili kwa watu wa mataifa kipindi yupo nao, bali wawaendee kwanza wayahudi (yaani waisraeli). Sasa kwanini awazuie wasiende kuwahubiria watu wa Mataifa?

Jibu ni rahisi: Ni kwasababu wakati wa Mataifa kwenda kuhubiriwa injili ulikuwa bado hujafika. Tunaweza kujifunza katika mfano wa kawaida wa Maisha. Unapotengeneza bidhaa yako mpya na kuipeleka sokoni, huwa huanzi na soko kubwa, badala yake utawaambia wale wasambazaji wako, msiende mbali kwanza, hakikisheni kwanza hapa mtaani kwetu au mkoani kwetu bidhaa zetu zimefika.

Kwa sentensi hiyo, haimaanishi kwamba..bidhaa yako huna mpango wa kuivukisha mipaka siku za mbeleni…

Bali ni umefanya hivyo ni kwasababu unataka kazi imalizike hapa kwanza, ndipo iende pengine…Mahitaji ya hapa yakishajitosheleza kwamba watu wameikubali au wameikataa ndipo utanue na kwenda kuitangaza mahali pengine mbali Zaidi.. hiyo ndiyo hekima na akili.

Ndicho Bwana alichowaambia wanafunzi wake, kwamba kwa wakati ule waanze Injili kwa WaIsraeli kwanza, na ndipo wengine watafuata, wasirukie kwenda pengine, muda wa kwenda huko bado.. Ili tuelewe vizuri zaidi hebu tukisome tena kile kisa maarufu tunachokijua cha yule mwanamke mkananayo ambaye hakuwa Mwisraeli.

Mathayo 15: 22 “Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24 Akajibu, akasema, SIKUTUMWA ILA KWA KONDOO WALIOPOTEA WA NYUMBA YA ISRAELI. 25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie”.

Sasa tuishie hapo, na kisha twende tena tukakirudie kisa hiki hiki katika Injili ya Marko, ili tupate kuelewa Zaidi…

Marko 7:24 “Akaondoka huko, akaenda zake hata mipaka ya Tiro na Sidoni. Akaingia katika nyumba, akataka isijulikane na mtu; lakini hakuweza kusitirika.

25 Ila mara mwanamke, ambaye binti yake yuna pepo mchafu, alisikia habari zake, akaja akamwangukia miguuni pake.

26 Na yule mwanamke ni Myunani, kabila yake ni Msirofoinike. Akamwomba amtoe pepo katika binti yake.

27 Akamwambia, WAACHE WATOTO WASHIBE KWANZA; maana si vizuri kukitwaa chakula cha watoto, na kuwatupia mbwa.

28 Naye akajibu, akamwambia, Naam, Bwana, lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya Watoto”.

Ukiusoma hapo kwa makini huo mstari wa 27?…utaona Bwana Yesu anamwambia huyo Mwanamke ambaye sio mwisraeli, anamwambia waache Watoto washibe KWANZA… Sasa kama wewe unaelewa Kiswahili vizuri, utakuwa pia unaelewa nini maana ya neno “KWANZA”… Neno kwanza maana yake, kinaanza hichi, halafu ndipo kifuate kingine.

Ndicho Bwana alichomaanisha hapo, kwamba waache Waisraeli wale KWANZA(yaani wapokee baraka hizi za rohoni kwanza), ndipo nyie watu wa mataifa mtafuata baadaye..Ndio maana mwishoni kabisa

mwa Injili yake, siku ile baada ya kufufuka kwake, aliwapa wanafunzi wake ruhusa sasa ya kwenda kote ulimwinguni kuhubiri injili, kwasababu wakati wa mataifa umeshafika…

Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

47 na kwamba MATAIFA YOTE watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, KUANZA TANGU YERUSALEMU.

48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

49 Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu”

Mstari huo wa 47, umehitimisha jibu la swali letu.. Kwahiyo Injili ni kwa watu wote na mataifa yote, Ilianzia Yerusalemu (yaani kwa waisraeli)..na sasa inahubiriwa kwenye mataifa yote..na imeshafika kila Taifa duniani, mpaka mataifa ambayo ni ngumu kufikiwa, lakini imeshapenya…anasubiriwa tu yule kondoo wa Mwisho kuingia ndani ya Neema, ule mwisho ufike, kama alivyosema..Marko 13: 10 “Na sharti Injili ihubiriwe kwanza katika mataifa yote” na Mathayo 24:14 “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja”

Je umetubu dhambi zako na kumpokea Kristo?..Kama bado unasubiri nini..Ni wapi leo injili haihubiriwi?..unadhani tunaishi nyakati gani hizi?…Dunia inaisha na Zaidi ya yote ibilisi anafanya kazi kwa nguvu sana nyakati hizi za mwisho, kuwapotosha watu, na kuwaaminisha kwamba hakuna Mungu , wala mwisho wa dunia, Mkabidhi leo Kristo Maisha yako kama hujafanya hivyo bado, na ukabatizwe na kupokea Roho Mtakatifu, ili upate kuokoka.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.

Tofauti kati ya Myunani, Farisayo na Sadukayo ni ipi?

JIEPUSHE NA UNAJISI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

AKIJUA YA KUWA ANA WAKATI MCHACHE TU”.

Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”.

Shalom, katika mistari hiyo biblia inatuonyesha kuwa shetani naye anayo kalenda ya muda kichwani pake. Aishi hoe hae tu, kuna kipindi alifanya kazi zake akijua bado kuna muda, lakini kuna wakati ulifikia kwa jinsi mambo yanavyokwenda, na mabadiliko aliyoyaona akajua kabisa kweli  hana  muda tena hapo wa kuchezea, muda aliobakiwa nao ni mchache.

Na sikuzote mtu mwenye majira ya muda kichwani, hata utendaji kazi wake unatofautiana kulingana na majira husika, Kwamfano, wanariadha, pale wanaposikia kengele imelia ya “mzunguko”  wa mwisho, utaona badala wapunguze mwendo kwasababu wamechoka,  kinyume chake utaona ndio wanaongeza kasi, kana kwamba ndio wameanza riadha, kwasababu wanajua hicho ndicho kipindi cha lala salama.

Mwanafunzi ambaye amebakisha wiki moja au mbili mpaka afanye mtihani wake wa kuhitimu, utaona hata usomaje wake katika kipindi hicho unabadilika, ataanza kuzingatia masomo, atakuwa tayari kukesha kila siku kwenye kusoma, mambo ambayo huko nyuma alikuwa hayafanyi kwa nguvu hizo.

Wachezaji mpira, utaona zinapokaribia dakika 5 mpira kuisha, utaona aina ya uchezaji wao nao unabadilika kwa pande zote mbili, ule upande uliofungwa utaona ndio unaongeza mashambulizi zaidi hata Yule kipa ambaye anakaa pale golini muda wote, ataondoka kwenda kuongeza mashambulizi kwa  upande wa pili, ili tu kuhakikisha wanarudisha magoli waliyofungwa.

Halikadhalika, ule upande uliofunga nao, utaacha kupeleka mashambulizi upande wa pili, utaona kwanza kikosi chote kinarudi nyuma, ili kulinda ushindi wao, adui zao wasirudishe magoli. (Sasa huo ni mfano tu, haimaanishi kila kinachofanyika kwenye hiyo michezo kipo sawa).

Ndivyo ilivyo kwa shetani wakati huu wa siku hizi chache alizobakiwa nazo, anaelewa hakuna muda tena wa kuchezea, hivyo kama ni mpira anaucheza kwa nguvu zote, ikiwa umemfunga (yaani umeokoka), atahakikisha mashambulizi atakayokuletea ni mazito, Na kama wewe ni mwenye dhambi,(hapo ni sawa na amekufunga) basi atahakikisha ulinzi atakaoweka ili usiufikie wokovu unakuwa ni mkubwa sana.

Ndugu, vizuizi shetani alivyonavyo leo, watu wasimfikie Mungu ili watubu dhambi zao, sio kama alivyokuwa navyo zamani, na hiyo yote ni kwasababu anajua muda wake ni mchache sana, anajua hivi karibuni mambo yote yanakwenda kuisha, atashikwa na kutupwa katika lile ziwa la moto..Na ndio maana anakusonga uwe busy ni mambo ya kidunia usipate muda wa kumtafakari Mungu,

Anakusonga na Ma-movie na Ma-series kutwa kuchwa uyawaze hayo,  ili muda wako wote uyawaze hayo usipate nafasi ya kuyatafakari maandiko, mwisho ukukute kwa ghafla, ufe uende kuzimu, au uukose unyakuo.

Anakusonga kwenye anasa na starehe, na pombe, na simu, na magroup ya kidunia, ili muda wako mwingi uumalizie huko, usahau kuwa muda uliobakiwa nao ni mchache, kwamba ni wajibu wako sasa kwa muda uliobakiwa nao hapa duniani ni kuhakikisha mbingu huikosi.

Shetani anajua huu ni  muda wa nyongeza tu, dakika 90 zenyewe zilishaisha, lakini sisi tunaishi kama vile ndio tupo dakika za 5 za kwanza, tunasubiria dalili zipi tena ndio tuamini kuwa Yesu yupo mlangoni? Mapigo kama haya ya Corona ndio zile tauni ambazo zilitabiriwa zitaipiga dunia  siku za mwishoni kabisa (Luka 21:11),  na cha kuogopesha zaidi biblia inasema, pale watakaposema mbona kama kuna Amani, ndipo hapo uharibifu utakapowajia kwa ghafla,

Siku moja utaamka asubuhi, utaiona dunia ni nzuri, jua linachomoza kama kawaida, jua linazama, uchumi wa nchi unaimarika, mikataba ya amani inasainiwa, sayansi inazidi kusitawi na kufanya maisha kuwa marahisi zaidi,  una afya njema, una amani, lakini usiku huo huo, kumbe ndio unyakuo unapita..

Hapo ndipo wengi wataanza kujutia muda wao wameutumiaje hapa dunia. Hivyo tunapoina neema ya Kristo inalia ndani yetu leo, tujitahidi tuipokee, kwasababu muda uliobakia kweli ni mchache, Bwana Yesu alisema hivyo, shetani naye anasema hivyo moyoni mwake, na anataka iwe ni siri yake peke yake, ili atushambulie chap chap atumalize aishinde yeye. Lakini sisi tunapaswa tumshinde kwa kuutafuta wokovu kwa bidii.

Hivyo kama wewe  ni mwenye dhambi, leo fanya uamuzi, Tubu dhambi zote kwa kumaanisha kuziacha, kisha, tafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, kisha baada ya hapo utapokea Roho Mtakatifu, ambaye ndio muhuri wa Mungu kwako (Waefeso 4:30), kukulinda, kukuongoza, kukufariji, na kukufundisha, hata siku ya unyakuo itakapofika.

Bwana akubariki sana.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

HERODE NA PILATO, MAADUI WAWILI WAPATANA.

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

Juya ni nini kwenye biblia? (Mathayo 13:47)

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

KALAMU YA CHUMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuota unachimba viazi, mihogo,madini n.k Kuna maanisha nini?

Kuota unachimba viazi, mihogo, vitunguu, karoti, madini n.k Kuna maanisha nini?


Inategemea na maisha unayopitia sasa, ikiwa shughuli zao za mara kwa mara ni za migodini au mashambani hususani katika kazi hizo za kulima viazi, au vyakula vya ardhini, basi ndoto kama hizo kujirudia rudia  ulalapo litakuwa ni jambo la kawaida sana kwasababu biblia inasema ndoto huja kutokana na shughuli nyingi Mhubiri 5:3,

Hivyo kama upo katika mazingira hayo, basi ndoto hiyo usiitilie maanani sana kwasababu haibebi ujumbe wowote wa rohoni, zaidi sana hizo ni ndoto za mwili.

lakini ikiwa sivyo na imekujia kwa namna ya kipekee, yaani kwa uzito Fulani, basi inaweza ikawa ishara ya kuwa Mungu anakufungulia milango ya rizki mbeleni.

Biblia inasema.

Ayubu 28:5 “Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula; …”.

Unaona, hivyo ikiwa utakaa katika hali ya kuyatenda mapenzi ya Mungu, basi ipo milango mingi sana, Mungu kakuwekea mbele yako, kwa hicho unachokifanya, na hata zaidi ya hapo. Ni wewe tu kuishi maisha yampendezayo Mungu wako.

Kwa muda wako soma, Kumbukumbuku la Torati sura ya 28 yote uone Baraka Mungu alizowawekea wale wote watakaoyashika maagizo yake kwa bidii.

Hivyo ili na wewe ndoto hizo ziwe kweli, hakikisha kwanza Kristo yupo ndani yako, kama hujaokoka hakikisha una mkabidhi Kristo maisha yako leo, na pia kuanzia huu wakati unaishi maisha kulingana na yeye anachotaka kulingana na Neno lake, baada ya hapo kuwa tayari kwa wema wake kujidhihirisha maishani mwako, lakini nje ya hapo, hilo linaweza lisikufikie kabisa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Au jiunge moja kwa moja whatsapp kwa kubofya chini.

Group la whatsapp  Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAJIFUNGUA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Konde la Soani ni nini? (Zaburi 78:12,43)

Konde la Soani ni nini?


Soani/konde la Soani ni mji uliokuwa Misri, upande wa mashariki mwa bonde la mto Nile, tazama picha juu. Hili ndio eneo ambalo Musa alionyesha miujiza yote ya Mungu kwa Farao, pale alipomtaka awaaachie huru wana wa Israeli akakataa.

Hivi ni  baadhi ya vifungu vinavyoelezea Neno hilo.

Zaburi 78:11 “Wakayasahau matendo yake, Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.

12 Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu, Katika nchi ya Misri, konde la Soani.

13 Aliipasua bahari akawavusha; Aliyasimamisha maji mfano wa chungu”.

 

Zaburi 78:42 “Hawakuukumbuka mkono wake, Wala siku ile alipowakomboa na mtesi.

43 Alivyoziweka ishara zake katika Misri, Na miujiza yake katika konde la Soani.

44 Aligeuza damu mito yao, Na vijito wasipate kunywa”.

 

Hesabu 13:22 “Wakapanda katika Negebu, wakafika Hebroni; na Ahimani, na Sheshai, na Talmai, wana wa Anaki, walikuwako huko. Nao Hebroni ulijengwa miaka saba kabla ya Soani wa Misri”.

Vifungu vingine ni Isaya 19:11,13, Ezekieli 30:14.

Tazama chini maana ya maeneo mengine katika biblia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

WAKATI WA BWANA KUKUVUSHA, NI LAZIMA ARUHUSU JESHI LA ADUI KUNYANYUKA.

PARAPANDA ITALIA.

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

UFUNUO: Mlango wa 19

Rudi Nyumbani:

Print this post