Watu baadhi kutoka nchi mbalimbali wamenitumia ujumbe wanasema, mtumishi huku kwetu hali sio nzuri hatuwezi kwenda kanisani kama tulivyozoea, hatuwezi kufanya chochote isipokuwa tu ni kukaa nyumbani, na wala hakuna dalali ya jambo hilo kuisha hivi karibuni…Tufanye nini?
Shalom, ndugu,
Ipo Habari moja katika biblia tunapaswa tujue na tujifunze kama wakristo katika wakati huu ambao dunia ipo katika taharuki kubwa, Tukisoma kitabu cha matendo ya Mitume, kuna wakati ambapo mitume wa Bwana walipitia kipindi fulani cha ukimya mkubwa sana, jambo ambalo liliwapasa wasifanye kitu kingine Zaidi ya kwenda kujifungia gorofani. Kwanini walilazimika kuwa vile, ni kwasababu ni kipindi ambacho, Sio YESU tu peke yake ambaye walizoea kumwona na kutembea naye kila siku hakuwa nao, bali pia Roho Mtakatifu ambaye walisikia habari zake alikuwa bado hajashuka juu yao.. walikuwa katikati ya pengo, kama vile mayatima fulani..
Kitu pekee kilichowafanya wawezi kukivuka hicho kipindi kifupi cha ukimya, ilikuwa ni ile AHADI TU, waliopewa na Bwana Yesu siku ile aliyokuwa anapaa..
Hiyo ndio iliyokuwa salama yao kwa wakati huo waliokuwa wanapitia..Kumbuka hawakujua ahadi hiyo itatimia lini, lakini maaadamu wana Neno la Ahadi, basi hiyo iliwafanya wapate nguvu siku baada ya siku, wavumilie hicho kipindi cha mpito mbele yao wakitumai kuwa siku si nyingi itatimia, na AHADI yenyewe ilikuwa ni kungojea YERUSALEMU, mpaka wakatakapopokea kipawa cha Roho Mtakatifu..Basi.
Matendo 1:3 “wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.
4 Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu;
5 ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache”.
Hivyo baada ya ile siku ya 40, hawakumwona, wala hawakusikia chochote, wala hawakuoona uwepo wowote, wala hawakuwa na shughuli nyingine yoyote ya kuhubiri, au kushuhudia kama pale mwanzo, au kuzunguka huku na huko kuhubiri..Bali iliwagharimu kwenda kukaa tu sehemu moja..na zaidi ya yote biblia inasema nje kulikuwa na hofu ya wayahudi.
Lakini biblia inatuonyesha ahadi hiyo haikuchelewa, bali ndani ya siku 10 mbeleni ilitimia, ambayo ndio iliyokuwa siku ya Pentekoste, Roho Mtakatifu aliwashukia mitume wake kwa nguvu ya ajabu, na hapo ndipo Mungu akaleta uamsho mwingine tena ambao uliitikisa dunia nzima katika historia..
Sasa swali ni Je ndani ya kipindi kile cha mpito ambacho hakukuwa na sapoti yoyote ya kimbinguni mitume walikuwa wanafanya nini ndani, Je! walikuwa wamelala tu au wameacha wakovu wao sasa wafikirie mambo yao ya kale, au walikuwa wamekaa wanapiga tu story na kuzungumzia Maisha ya wengine, au wanaangalia movie, au wanachat whatasapp kila wakati au wanacheza magemu, au wanafanya nini??
Embu Tusome..
Matendo 1:10 “Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,
11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
12 Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.
13 Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.
14 Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja KATIKA KUSALI, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake”.
Unaona, biblia inasema hapo walikuwa WAKIDUMU KWA MOYO MMOJA KATIKA KUSALI,..
Ndugu, wakati huu wa LOCKDOWN, na kuwa karantini kutokana na janga la Corona, nchi yoyote uliyopo. Wakati huu Wa kuzuiwa kufanya ibada, au kuzunguka huku na huko, wa kuzuiwa kwenda mtaani kuhubiri kama ulivyokuwa unafanya hapo mwanzoni, wa kuzuiwa kuitishi mikutano ya injili, wa kuzuiwa kwenda kumwabudu Mungu kanisani, kwenda kwenye masomo ya biblia, kila baada ya siku mbili, sio wakati wako wa wewe kuwa na kisingizio cha kuacha kumtafuta Mungu, na kurudi nyuma kwenye ulimwengu ulipokuwepo, wa kurudi kuanza sasa kutokusoma biblia yako,..bali huu ndio unapaswa uufanye muda wakati wako wa kudumu katika KUSALI kwa bidii ukiingalia ahadi ya Mungu iliyo mbele yako, kwamba hivi karibuni atakwenda tena kutuachilia, lakini hatatuachilia hivi hivi, bali atatuachilia na UAMSHO MKUBWA WA ROHO ambao haujawahi kutokea..kama ilivyokuwa katika kipindi cha Pentekoste.
Hivyo huu sio wakati wa kuzimia mioyo, wala sio wakati wa kuogopa maadamu tupo ndani ya Kristo, badala yake ndio tuongeze kutazama juu, tukiziangalia Ahadi za Bwana ndani ya kipindi hichi cha mpito, tukiongeza viwango vyetu vya kujisomea biblia nyumbani, na kusali sana tena Zaidi ya pale tulipokuwa mwanzoni, ikiwezekana kufunga, na kila wakati kumtafakari Mungu kweli kweli..
Sisi hatujapitia kipindi cha kuachwa na mbinguni kwa Muda kwa ilivyokuwa kwa mitume, lakini wao hawakuiacha Imani, badala yake walidumu katika kusali tena walipanda OROFANI, juu kabisa mahali ambapo hapana usumbufu wa watu kuingia na kutoka, ili wamtuafakari Mungu vizuri na kusali..
Vivyo hivyo huu ni wakati wa wewe, kupanda OROFANI (mahali penye utulivu), Umtafute Mungu peke yako, kwasababu UAMSHO MKUU SANA, Unakwenda kuzuka duniani kote hivi karibuni. Kipindi cha nyuma pengine ulikuwa na visingizio vya kutokusali, kwamba upo bize kutafuta riziki na shughuli leo hii mazingira yanakulazimisha kukaa nyumbani, na tena kuna agizo limetolewa la kuomba, hivyo isiwe sababu ya wewe kuhukumiwa siku ile kwa kutokuomba sasahivi…Unayo sababu inayoeleweka kidunia ya wewe kutozurura zurura mtaani, basi kaa nyumbani kuomba…utajitetea vipi siku ile??..Utasema ulikosa muda? Utasema serikali ilikuzuia kuomba? Leo hii imekutangazia wewe kuomba?.. Utasema sikuomba kwasababu mazingira yalikuwa hayaruhusu?..jibu unalo.
Hivyo nakutia moyo wewe mkristo ambaye umeathiriwa na hali hii ya sasa duniani, Fahamu kuwa ni kipindi kifupi tu cha Siku 10 rohoni kinapita ambacho ni Mungu mwenyewe kakiruhusu..hivyo kuwa na akili, kujua nyakati na majira, ongeza viwango vyako vya utakatifu kama vile hukuwahi kuishi hivyo hapo kabla, ni wakati wa kutubu (kutubu maana yake ni kuacha yale uliyokuwa unayafanya yasiyo mpendeza Mungu) ili hiyo PENTEKOSTE itakapokuja kwa watu wa Mungu duniani, uwe na wewe ni mmojawapo..
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Karibu tujifunze biblia na kujikumbusha mambo yale yale ambayo tumekwisha kujifunza huko nyuma kupitia sehemu mbalimbali..
Wengi wanajiuliza je ubatizo ni wa muhimu?..Jibu ni NDIO ni wa muhimu sana na si kidogo. Shetani hapendi wengi wajue siri iliyopo katika ubatizo sahihi kwasababu anajua madhara yake.
Wakati wana wa Israeli wanatoka Misri, Farao bado alikuwa anawafuatilia fuatilia..lakini walipovuka tu bahari ya shamu na majeshi ya Farao yote kuzama kwenye ile bahari ya shamu ndio ikawa mwisho wa Farao na majeshi yake kuwafuatilia wana wa Israeli.
Kutoka 14:26 “Bwana akamwambia Musa, Nyosha mkono wako juu ya bahari, ili maji yarudi tena juu ya Wamisri, juu ya magari yao, na juu ya farasi zao.
27 Musa akaunyosha mkono wake juu ya bahari, na kulipopambazuka, bahari ikarudi kwa nguvu zake; Wamisri wakakimbia mbele yake; na Bwana akawakukutia mbali hao Wamisri kati ya bahari.
28 Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja.
29 Lakini wana wa Israeli wakaenda katika nchi kavu katikati ya bahari; na hayo maji yalikuwa ni kuta upande wao wa kuume, na upande wao wa kushoto.
30 Ndivyo Bwana alivyowaokoa Israeli siku ile mikononi mwa Wamisri; Waisraeli wakawaona Wamisri ufuoni kwa bahari, wamekufa”.
Sasa siri ilikuwa ni nini mpaka Mwisho wa Farao ukawa kwenye hiyo bahari ya Shamu?..Jibu ni rahisi: Ni huo ubatizo wana wa Israeli waliobatizwa kwa kupita katikati ya bahari hiyo.
Utauliza je!..ina maana wana wa Israeli walibatizwa katika bahari ya Shamu?..Jibu ni ndio!..
1Wakorintho 10:1 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;
2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;”
Unaona hapo?..kitendo cha Wana wa Israeli kupitishwa katika yale maji ya Shamu, pasipo kupatikana na madhara ndiko kunakofananishwa na ubatizo. Hivyo ule ubatizo ndio uliohitimisha kazi ya shetani na majeshi yake kuwafuatilia, haijalishi kuwa tayari walishapewa ruhusu huko nyuma ya kuondoka.
Hali kadhalika, ubatizo sahihi wa maji mengi sasa unafanya kazi hiyo hiyo. Unapoingia katika yale maji na kubatizwa katika jina la Yesu na kutoka katika yale maji…wewe utatoka salama ukiwa na furaha, na amani lakini nyuma yako yale majeshi ya mapepo wabaya yaliyokuwa yanakufuatia yanakufa na maji huko nyuma.
Hivyo maji ni ishara ya wokovu kwako na maangamizi kwa shetani na majeshi yake. Ndio maana Bwana Yesu alisema katika Roho kwamba pepo amtokapo mtu hupitia mahali pasipo maji(maana yake mahali ambapo hapana maji) ili apumzike na akirudi na kukuta nyumba yake imefagiliwa anakwenda kuwachukua pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye, na hali ya mwisho ya Yule mtu inakuwa mbaya kuliko ya kwanza.
Maana yake ni kwamba pepo likimtoka mtu na Yule mtu kama hatachukua uamuzi wa kuukamilisha wokovu wake ikiwemo kubatizwa ubatizo sahihi wa kuzama mwili mzima kulingana na maandiko na kudumu katika usafi..Mtu huyo yupo hatarini kurudiwa na zile zile nguvu za giza zilizomwacha hapo kwanza. Hivyo ubatizo sahihi ni wa muhimu sana…Na ubatizo sio dini mpya bali ni maagizo ya Bwana wetu Yesu…na kwa faida yetu kama ilivyokuwa kwa faida kwa wana wa Israeli wakati wanatoka Misri, kama sio yale maji Farao angeendelea kuwafuatilia daima.
Shetani na mapepo yake yataendelea kumfuata Yule mtu ambaye hajakamilisha wokovu wake…Na Bwana alishatuambia katika Neno lake, kwamba “aaminiye na kubatizwa ataokoka”..maana yake mambo hayo mawili yanakwenda pamoja, hayaachani, vinginevyo ni ngumu sana kuokoka na mkono wa Adui.
Kama unakumbuka kile kisa cha Yule mtu aliyekuwa na mapepo yaliyojitambulisha kama JESHI. Mtu Yule aliingiwa na mapepo, na mapepo yale yalipomtoka yaliwaingia nguruwe…Jinsi wale Nguruwe walivyokwenda kuangamia majini ni mfano wa Farao na majeshi yake yalivyozama majini…Kwahiyo unaweza kuona kuna uhusiano mkubwa sana wa maji na majeshi ya Adui. Hivyo ubatizo ni wa muhimu sana. Pale tu mtu anapoamini na kutubu anapaswa akabatizwe bila kuchelewa…
Itakuwa ni jambo la kushangaza, mtu utasema umeokoka, halafu miezi inapita, miaka inapita, bado hujabatizwa, unaishi kwa kanuni ipi ya wokovu?
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.
JINA LA MUNGU NI LIPI?
KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.
USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.
KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.
HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM
Kabla Mungu hajaleta maangamizi katika dunia, huwa anawatuma kwanza malaika zake wapelelezi kwenda kuhakiki hicho kilichomfikia kuwa ni kweli au La, na ikithibitika kuwa ni kweli basi hatua inayofuata saa hiyo hiyo ni wale malaika kutekeleza hukumu ya Mungu juu ya watu hao au Mji huo. Kwananini anawaagiza malaika hawa kwanza kupeleleza, je ni kwasababu yeye mwenyewe hajui kiwango cha maasi na haki yaliyomo ulimwenguni?..jibu ni hapana!..anajua kila kitu pasipo hata kutegemea malaika zake, wala mwanadamu..lakini anafanya hivyo ili pawepo na mashahidi ya kile kinachoendelea…Kama biblia inavyosema “Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa.(2Wakorintho 13:1)”
Ndicho kilichotokea kipindi kifupi kabla ya miji ya Sodoma na Gomora kuangamizwa. Mungu aliwatuma malaika zake wawili, kwenda kuipeleleza miji ile, na kama tunavyoifahamu habari, malaika wale walipofika jioni ile, wakakutana na Lutu, Lutu naye akawalazimisha kuingia nyumbani kwake, mwanzoni walikataa, lakini baadaye wakafika, na walipofika tu kumbe huku nyuma, walikuwepo pia wapelelezi wengine wanawafuatilia malaika wale, na hao si wengine zaidi ya watu wa miji ile..
Hivyo sio malaika tu waliokuwa wanapeleleza, na wao pia walikuwa wanapelelezwa, jambo ambalo linaendelea sasa katika roho..
Sasa walipoona hatma yao ni wapi, kuwa ni ile nyumba ya Lutu, hawakufanya chochote, bali walisubiri mpaka usiku ulipoingia ndipo wakakusanyika wote wakaizingira ile nyumba ya Lutu na kumwambia Lutu, awatoe hao watu ili wapate kulala nao..Embu fikiria hali yao ilivyokuwa mbaya..Sasa kama ukichunguza pale utaona, wale malaika hawakuchukua hatua yoyote kwanza, ni kama walikuwa wanawasikiliza walichokuwa wanamueleza Lutu pale nje, na mashindano yao pale mlangoni..Na baadaye ilipoonekana Lutu anashindwa, wakawa wanakaribia kuuvunja mlango, ndipo wakanyanyuka wakamvuta Lutu ndani, kisha wakawapiga upofu wale watu waliokuwepo pale mlangoni..
Hiyo ilisababisha ripoti yao ya upelelezi iwe imekamilika, kwamba Sodoma kumeoza na wao ni mashahidi, kilichobakia kwao ni kumuhimiza Lutu kwa haraka aondoke Sodoma kwa sababu miji ile wanakwenda kuiteketeza. (Soma Mwanzo 19 yote)
Ndugu yangu, dalili kubwa inayotutambulisha kuwa tunaishi katika wakati wa upelelezi wa malaika hawa, Sio kuzuka kwa vitendo vya Ushoga na usagaji tu peke yake, hapana, kwani hivyo vilikuwepo tangu zamani..lakini ni kuzuka kwa vitendo vya Ushoga na Usagaji katika nyumba ya Mungu…Tunavyoona leo hii ushoga unafungishwa katika nyumba ya Mungu, basi tujue hiyo ni dalili mbaya, ni sawa na kutaka kuzini na malaika wa Mungu walio katika kanisa lake..
Malaika hao wameshapita na wameshaona kile ambacho kilitokea wakati wa sodoma na Gomora ndicho kinachotokea na sasa hivi, hivyo wanachokifanya sasa ni kuwapiga watu upofu kwa kasi sana, ili wasione mlango wa neema tena ambao wenyewe wanauvunjia heshima, na kinachobakia kwa watu hao ni maangamizi tu..
Unapojiona wewe ni mtazamaji wa Pornography, ujue kuwa wewe ni kundi moja na hawa wanaoufanya ushoga nyumbani mwa Mungu, isipokuwa wewe tu ni mfuasi wa nyuma, lakini adhabu yenu ni moja,,..na hivi sasa unapigwa upofu, ambao hutakaa uuone mlango wa neema kamwe kama hutatubu. Ukiona unazini, na kwako wewe zinaa ni kama kitu cha kawaida na huku unajiita ni mkristo bado, ujue upofu unaendelea sasahivi duniani, ukiona unajihusisha na mambo yote ya kizinzi (iwe ni kujichua, au ulawiti) ujue upo katika kundi hilo la kupigwa upofu na malaika hawa wapelelezi wa Bwana.
Wanapopita na kuangalia makundi mengi ya watu, leo hii yapo kwenye simu zao mikononi, kutwa kuchwa ku-download video za pornography na kutazama video hizo, na miziki ya kidunia..ujue kuwa hao watu wanapigwa upofu, na malaika hao waliotumwa na Mungu kuipepeleza dunia, kabla ya kwenda kuangamizwa dunia hii kwa moto siku hizi za mwisho.
Wakati huu ni wakati wa hatari nyingi, ikimbie dhambi, unaweza kuona inavutia leo machoni pako, na ndivyo ilivyo dhambi siku zote ni ya kuvutia lakini mwisho wake ni majuto ya milele. Mungu tayari ameshakikasirikia kizazi hiki, kinachoichezea madhabahu yake mpaka kufikia hatua ya kufanya mambo ya ajabu kama hayo madhabahuni pake..Utasema ni hao sio mimi, kumbuka kile kikundi kichache kilichokuwa kinacheza mlangoni mwa Lutu ndicho kilichouwashia moto mji mzima wa Sodoma na Gomora..ikasababisha hata wengine walio mbali wasiojua chochote ambao wanafanya mambo kama hayo mwisho wao kufika. Kwahiyo uovu unapoendelea katika nyumba ya Mungu ni jambo la kuomboleza kwa wote.
Hivyo na sisi Bwana atusaidie tusiwe wamoja wapo, bali tuchukue hatua ya kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kabisa kumgeukia yeye, katika huu wakati mfupi wa kumalizia kabla ya unyakuo kupita. Kwasababu tusidhani kuwa yaliyowakuta wale, hawayawezi kutukuta na sisi.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA?.Mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?
SWALI: Je! Mtume Paulo alikuwa anamwabudu malaika wake aliyekuwa anatembea naye kama tunavyosoma katika Matendo 27:23?
JIBU: Tuusome huo mstari..
Matendo 27:23 “Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,”
Mstari huu ukisomwa kwa haraka haraka ni rahisi kutafsiri kwamba Mtume Paulo alimaanisha kusema kwamba anamwabudu Malaika wake..Lakini ukiurudia tena taratibu utaona kwamba hapo Mtume Paulo hakumaanisha kuwa anamwabudu Malaika bali ni Mungu..
Sasa tunaweza kuiweka vizuri sentensi hiyo kama ifuatavyo; “Kwa maana usiku wa leo Malaika wa Mungu alinijia”…..sasa swali ni Mungu yupi?…ndio anaendelea kusema…Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye…
Hivyo ukirudia kusoma kwa namna hiyo huo mstari utapata tafsiri kamili.
Hivyo Pamoja na hayo tunazidi kujifunza kwamba tunapaswa kuzidi kuyachunguza maandiko, ili tupate kulielewa Neno la Mungu kama yeye Mungu wetu anavyotaka tulielewe..kwasababu ipo mistari mingi na Habari nyingi katika maandiko matakatifu ambazo wakati mwingine ni ngumu kuzielewa lakini tunapokaa chini na kutaka kumwuliza Roho Mtakatifu yeye ni mwaminifu na atatufulia, kwasababu tusipopata tafsiri kamili kwa msaada wa Roho Mtakatifu shetani anaweza kuitumia mistari hiyo hiyo kutukosesha na kutuhalalisha uovu wake…kama alivyoitumia baadhi ya mistari kuwadanganya watu kuhalalisha ulevi, zinaa, ndoa za mitara na hata ameshautumia mstari huu kwa baadhi ya watu kuhalalisha ibada za kuabudu malaika na ibada za sanamu.
Bwana atusaidie na kutubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?
Je! Shetani alitolea wapi uovu?
Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?
Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
Kwanini Musa alipewa mbao mbili za mawe na sio moja au zaidi
Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;
35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima”
Shalom, Jina kuu la mwokozi wetu Yesu libarikiwe daima.
Wengi tunayafahamu maneno hayo ya Bwana, lakini hatujui ni ulevi na ulafi wa namna gani unaozungumziwa katika Habari hiyo mpaka siku hiyo iwajilie ghafla, kama mtego unasavyo..
Ili kupata picha embu tutazame mfano mmoja halisi kabisa wa kwenye biblia na jinsi walivyolemewa na ulafi na ulevi wa kipekee mpaka, mwisho wao ulipowakuta kwa ghafla..
Sasa kama tukisoma kile kitabu cha Danieli sura ya 5, tunamwona mfalme mmoja aliyejulikana kwa jina la Belshaza, huyu alikuwa ni mtoto wa Nebukadreza, kama wengi tunavyoifahamu Habari, ni mtu ambaye alibahatika kuona mambo yote ambayo Baba yake aliyoyapita na jinsi alivyoadhibiwa kutokana kiburi chake na ukatili wa kutesa watu wasiokuwa na hatia na wengine kuwatupa katika matanuru ya moto, kama sio kuwachinja, lakini baadaye Mungu alikikomesha kiburi chake, kwa kumng’oa katika ufalme wake, akawa anaishi misituni kama sokwe Fulani tu, mpaka miaka 7 ilipoisha, na pale alipogundua kuwa Mungu ndiye anayetawala dunia nzima, na kwamba yeye ndio anatakiwa aogopwe ndipo akatubu na kumgeukia Mungu na Mungu akamrehemu na akamrejeshea enzi yake kupita kiasi hata kuliko pale alipokuwepo mwanzo.
Sasa huyu mtoto wake aliyeitwa Belshaza, alikuwa anayaona hayo yote, na alikuwa ameshapata somo kamili ambalo haikumpasa yeye tena alipitie kwasababu babayake tayari ameshafanyika mfano..Kama tu vile sisi, watu wa kizazi hiki, tayari mifano mingi ilishatangulia mbele yetu huko nyuma, mfano ile ya watu wa Nuhu, na Watu wa sodoma na Gomora, jinsi walivyoangamizwa kwa maovu yao, lakini sasa tunaona na kuzipuuzia, na kuzichukulia tu kama Habari zilizopitwa na wakati kama tu huyu mtoto wa Nebukadreza.
Yeye alipuuzia yale yote ambayo Baba yake aliyotendewa na Mungu.. Na kibaya Zaidi akaamua kuchukua hatua nyingine mbaya kuliko zote, ambayo ndiyo iliyompelekea hata Mungu kumwangamiza kwa ghafla na kwa haraka sana..Na hicho ndicho wote tunachopaswa tujifunze leo hii.
Alichofanya ni kuchukua vile vyombo vya hekaluni, ambavyo baba yake alivichukua kutoka Yerusalemu, alipouteketeza mji na hekalu, na kuvihifadhi asivitumie kwa kitu chochote kwasababu vilikuwa ni vitakatifu, lakini yeye (huyu Belshaza), akawa mlevi, na mlafi wa kupindukia, akawa anafanya karamu, akaona kuwa haitoshi kunywea vyombo vyake mwenyewe, chupa zake za vilabu vyake, na kutumia visu vyake vya kifalme kuchinjia nyama zake, na hata sahani zake akaona hazitoshi kuzitumia kuwekea vyakula vyake haramu…
hivyo akaenda kwenye hazina ya baba yake, na kupekua pekua na kuvikuta vile vyombo vya hekaluni ambavyo vilikuwa vimefunga na kuhifadhiwa visitumike, yeye akavichukua vile vyombo vitakatifu vya Mungu, akaanza kuvinywea na kuvilia yeye Pamoja na wakuu wake, na makahaba wake..Unaweza kuona Ni uvunjifu wa heshima kiasi gani.?? Hayo ndio mambo yanayoendelea katika roho sasa hivi..
Na alipomaliza kufanya vile tu, saa hiyo hiyo kiganja cha mkono kikatokea, kikasogea mpaka ukutani mahali ambapo mwanga ulikuwa unapiga, akaona kikiandika maneno yale, MENE, MENE, TEKELI NA PERESI.. Kama tunavyoijua habari maneno yale yalikuwa ni Hukumu, kwamba mwisho wake umeshafika, ufalme wake ndio umeishia pale..
Sasa huyu Belshaza, utaona tena aliposikia vile badala atubu, ndio kwanza anafikiria kumpandisha Danieli cheo, na kumfanya awe mkuu, unajua ni kwanini?.. Ni kwasababu alidhani, jambo hilo haliwezekani kutokea kwake, na hata kama likiwezekana basi litakuwa ni jambo la baadaye sana, kwasababu mji wake wote ameshauzungushiwa kuta kubwa sana pande zote, ambazo juu yake wapo walinzi wamekaa wakiangalia malango yake usiku na mchana yenye askari waliobebea wenye sifa dunia nzima, (kwasababu kipindi hicho Babeli ndio iliyokuwa inatawala dunia nzima)..
Hivyo Habari hizo za Danieli hazikumwogopesha hata kidogo, akiangalia kuwa hayo mataifa ambayo ameambiwa yatakuja kuuchukua ufalme wake, yaani umedi na uajemi ni vitaifa vidogo, visivyokuwa na nguvu, hivyo akawa hana hofu tena..
Lakini ndivyo alivyojidanganya..Biblia inasema usiku ule ule, alivamiwa na kuuliwa, na ufalme wake kuchukuliwa kirahisi na Wamedi na Waajemi, ni jambo la ghafla sana..utajiuliza wale watu walitokea wapi asipate Habari siku zote..
Ili kufahamu ukirudi katika historia inasema, ule mji wa Babeli ulikuwa na mto mkubwa ambao ulikuwa unaingiza maji katika mji, sasa kwa namna ya kawaida, maji yanayoingia katika mji hayawezi kuwekewa kuta, hivyo pale pale kwenye maingilio ya mto ule ndipo hapo hapo Wamedi walipokuja kuingilia usiku ule, walichokifanya ni kuupindisha ule mto mbali sana hivyo maji yakapungua ndipo walipopatia nafasi ya kuuingia mji, na kuwaua watu wale kwa ghafla sana na haraka usiku ule..wakati walinzi wa mji wanaendelea kulinda mageti makubwa kule..kumbe huku kwa njia ya chini ya watu wameshaingia mjini na kuanza kuangamiza watu.
Hata leo, Kanisa la sasa limeshalemewa na ulafi na ULEVI WA ROHONI, ni heri ungekuwa ni ulevi wa kawaida, lakini ni ulevi unaotumia vyombo vya hekaluni mwa Bwana na hiyo ndiyo inayoleta ghadhabu.. Yaani watu wanapomchanganya MUNGU NA DUNIA..leo wapo kanisani, kesho disko, leo wanamwimbia Mungu, kesho shetani, leo wanashiriki meza ya Bwana, kesho wanakwenda kuzini, yaani hayo yamekuwa mambo ya kawaida kabisa, mtu kusema ameokoka, na huku, anakunywa pombe kisirisiri, anazini nje ya ndoa, anajichua, anatazama picha za ngono ni mambo ya kawaida, anakula rushwa, ana honga..
Huo ndio ulevi na ulafi Bwana Yesu aliokuwa anauzungumzia pale..
Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;
35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima”
Moja ya hizi siku, dunia nzima itaingia katika mtego huo, wakati watu wakiwa katika vilele vya amani, katika furaha, ndipo mambo yatakapobadilika kwa ghafla. Hivyo ndugu, huu ni wakati wa kutengeneza uhusiano binafsi na Mungu..Dunia hii imeshaandikiwa MENE, MENE, TEKELI na PERESI..Ukizidi kung’ang’ania kwenda nao, mwisho wa siku itakuchukua kama ilivyomchukua Belshaza, Leo hii tubu itii injili, uokolewa, Usafishwa Maisha yako, Na Bwana atakusaidia kwa yale yaliyobakia.
Ubarikiwe sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
RABI, UNAKAA WAPI?
KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?
ANGALIA USIJE UKANG’OA NGANO KATIKATI YA MAGUGU.
MUNGU AKIKUPITA LEO, HAIMAANISHI KUWA HAJAKUCHAGUA.
HATA NA BARNABA PIA AKACHUKULIWA NA UNAFIKI WAO!!
Chukua tahadhari juu ya neema ya Mungu.
Hakuna ulinzi mkubwa ambao mwanadamu anaweza kuupata kama ulinzi wa kuwa ndani ya Yesu..Kama wengi wetu tunavyojua au tulivyosikia kwamba watu wote waliompokea Yesu Kristo uhai wao unakuwa umefichwa pamoja na Kristo.(Wakolosai 3:3). Kiasi kwamba tunalindwa dhidi ya nguvu za giza na mipango yote ya Ibilisi.
Wengi wetu tunaifurahia neema hii na kutamani kuingia ndani yake lakini hatujui kuwa ikichukiliwa isivyopaswa ina madhara makubwa kuliko kitu kingine chochote tunachoweza kukijua.
Neema ya Mungu inafananishwa na nyumba ya karamu, yenye mlango…Mathayo 7:13. Sasa kama tujuavyo nyumba yoyote ile ya muhimu kama Ikulu au ukumbi wa sherehe ya muhimu sana ina mlango na vile vile ina uzio…na mara nyingi kuta zake zinakuwa zimezungushiwa uzio mwingine ambao ni wa umeme..Na kama ni nyumba yenye umuhimu mkubwa zaidi ya hayo inakuwa na walinzi wanaotembea tembea wenye silaha kuizunguka, lengo ni kuzuia watu wa wasiruke ukuta na kuingia ndani…Na ikitokea mtu akijaribu kukiuka na kuusogelea ukuta kutaka kuruka aingie ndani ndipo anaweza akajikuta kapigwa risasi au kapigwa shoti ya umeme, na hivyo hata kuweza kujisababishia kifo…Lakini ulinzi huo haujawekwa kwaajili ya kuangamiza watu, bali kulinda usalama.
Na Neema ya Mungu ni hivyo hivyo…Ipo nguvu ya ziada iwalindao wale watu walioingia ndani ya Neema ya Kristo..Nguvu hiyo ndiyo inayotulinda dhidi ya nguvu zote za giza, dhidi ya shetani na majeshi yake (mapepo na wachawi) na kila mpango mwovu wa Ibilisi..Hivyo yoyote anayejaribu kuingia kutaka kuwaharibu watu wa Mungu walio chini ya neema ya Mungu basi atakuwa anajitafutia matatizo yeye mwenyewe..
Lakini jambo lingine la kuogopesha ni kwamba ikitokea mtu aliyeko ndani ambaye tayari kashaingia ndani ya jengo hilo, akatoka na kwenda kupanda ukuta na kurukia zile nyaya za umeme zilizouzunguka ukuta, yeye naye atajeruhiwa vile vile kama sio kufa kabisa. Maumivu yale yale atakayoyasikia Yule anayetaka kuruka ukuta na kuingia ndani ndio hayo hayo atayapata Yule anayetaka kuruka na kutoka nje.
Madhara atakayoyapata mchawi anayetaka kuwadhuru watu wa Mungu, ndio hayo hayo atakayoyapata mkristo anayeuacha wokovu na kuurudia ulimwengu. Mkristo ambaye ameshaonja kipawa cha Mungu na kuburudika na neema ya Mungu, na ghafla anarudia uasherati wake, anarudia wizi wake, anarudia matusi yake, anarudia mauaji yake, usagaji wake, utoaji mimba wake, mambo ambayo alikuwa ameshayaacha machafu anayarudia tena…akidhani kwamba mkono wa Mungu ni kinyume cha wale waliopo nje pasipo kujua hata waliopo ndani ambao wanataka kutoka vile vile mkono wa Mungu upo kinyume chao.
Wengi wetu hatupendi kusikia mambo kama haya kwasababu hatupendi kuumizwa mioyo, hatupendi kusikia habari mbaya, lakini fahamu kuwa tahadhari siku zote sio habari njema, lakini zina umuhimu sana katika maisha hususani katika siku za baadaye…hata vidonge tupewacho na wataalamu wa afya ambavyo vinatumika kwa tiba, bado vina tahadhari zake…lengo la tahadhari zile sio kuwatisha watumiaji wala kuwakatisha tamaa bali kuwanufaisha zaidi.
Vivyo hivyo Neema ya Kristo inayo tahadhari…Na ni lazima kila mtu aijue tahadhari hiyo, wahubiri wengi hawaifundishi kwasababu watakosa waumini, na wao bado wanatafuta waumini…Lakini sikia leo hii mtu wa Mungu tahadhari, ili baadaye tusije kujuta, na tahadhari hii haikuhusu wewe unayesoma tu, hapana hata mimi ninayeandika inanihusu. Biblia inasema..
Waebrania 10:26 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;
27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.
28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.
29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”
Kama umeamua kumfuata Yesu basi umfuate kweli kweli..usiusogelee kabisa ukuta wa Neema..uwe ndani au nje ni upanga ukatao kuwili..Neno la Mungu linasema usizini…hizo ni kuta!..neno linasema usiibe, usiue hizo ni kuta..ukipanda na kuzivuka nguvu ya Mungu utakumaliza..ambayo hiyo Mungu hakuiweka kwaajili ya kuua watu, bali kwaajili ya kuwalinda watu wake.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?
USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.
MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?
NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.
Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?
SWALI: Shalom, nimekuwa na shida usiku nakuwa kama nimeganda siwezi kusogeza mkono au mguu au kuongea lakini akili nakuwa bado ninayo huwa nakemea inachukua muda kidogo naachiwa nashindwa kujua tatizo ni nini naomba nisaidie.
JIBU: Ndoto yoyote ambayo inakuja, na unajikuta katika mazingira ya kupambana na hali Fulani na huku unatumia jina la Yesu, ambapo mwanzoni inaonekana kuleta upinzani Fulani lakini baadaye inakuja kuachia kwa jinsi unavyozidi kuendelea kukemea ni ndoto yenye ujumbe kutoka kwa Mungu..
Wengine wanaota wanashindana na wachawi, na wale wachawi mwanzoni ni kama wanataka kumshinda lakini baadaye anawashinda kwa jina la YESU, wengine wanaota wamekutana na roho za mapepo, halafu kila alipolitaja jina la Yesu sauti, haitoki, lakini kwa jinsi alivyokuwa anaendelea kulitaja mwisho wa siku sauti inatoka na anayashinda.. Mwingine hata sio mapepo bali hali fulani ya udhaifu, kama hiyo ya kwako, unajikuta umeganda huwezi kusogeza kiungo chako hata kimoja, kila unapojaribu unashindwa, unajikuta unahitaji msaada kwa kulitaja jina la Yesu, na unapofanya hivyo mwanzoni ni kama inashindakana lakini baadaye inaachia hali hiyo inaisha ghafla..
Zote hizo ni ndoto zenye ujumbe mmoja,..Ambao ni Mungu tu anakuonyesha SILAHA pekee ambayo inayoweza kukupa ushindi dhidi ya adui yako shetani, na silaha hiyo tayari umeshaijua ambayo ni jina la YESU. Hivyo ni kuongeza bidii ili uwe na mamlaka kamili juu ya jina hilo kuu.. (Kumbuka mamlaka hayaji kwa kulitamka tu kama ulivyoona kwenye ndoto, bali yanakuja kwa kumwelewa Yesu Kristo katika Neno lake, ndipo kutamka kwako kuwe na nguvu).
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.
Unaona hakuna lolote litakalokushinda, ikiwa maneno ya Mungu yatakuwa ndani yako kwasababu utakuwa umepewa mamlaka kamili na Kristo mwenyewe ya kushinda mambo yote..
Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru’’.
Hivyo jitahidi kumjua Kristo zaidi, au ongeza bidii, ili upokee mamlaka hayo kamili..Ndio ujumbe mkuu unaopewa hapo.
Vile vile sababu nyingine ya pembeni, ambayo unapaswa ujue katika ndoto kama hizo za kujikuta umeganda kitandani na huwezi kufanya chochote, ambapo wengine zinakuja katika uhalisia kabisa kana kwamba sio ndoto, bali ni kitu halisi na wanajiona hawawezi kusogeza kiungo chao chochote kitandani, na anatamani hata mtu amsaidie kusogeza mkono wake lakini hawezi kumwambia, na wengine wanasema amekufa lakini yeye anajiona bado ..Ni kwamba hapo Mungu anakuonyesha, hali halisi ya jinsi watu wanavyokufa, na Kwamba yapo maisha baada ya kufa, sio kama wengine wanavyodhani, ukifa huelewi chochote, La, ukifa roho yako inaendelea kuishi inaondolewa katika mwili wako na kupelekwa mahali pengine..(Mhubiri 12)..
Hivyo siku ya kufa, kila mtu atajiona jinsi anavyotoka katika mwili wake na kwenda sehemu nyingine, na ataona pia wanaomzunguka jinsi anavyowaacha!.
Hivyo tunapaswa tujiulize , je! tumejiandaaje huko tuendako? Jibu lipo katika maisha ya kila mmoja jinsi anavyoishi.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)
Kama watu wamefunga ndoa ya serikali na wakaachana, wanaweza kuoa au kuolewa tena na watu wengine?
JIBU: Shalom, Ndoa iliyofungwa kiserikali, au kwa namna yoyote ile…ambayo imehusisha makubaliano ya pande zote mbili na taratibu zote ikiwemo mahari na kutangazwa mbele ya jamii kuwa watu hao wawili wamekuwa mume na mke…kwa namna yoyote ndoa hiyo haipaswi kuvunjwa kwasababu imetangazwa tayari mbele ya mashahidi, hivyo hiyo tayari ni ndoa (ingawa sio ya kikristo)..
Na endapo ikitokea wawili hao wamefunga ndoa hiyo ya kiserikali na wakaachana, basi mbele za Mungu watakuwa na hatia…(Na kumbuka ndoa ya kiserikali hawafungi na wakristo, yaani maana yake mtu ambaye tayari ameshamjua Yesu Kristo na kumwamini, hawezi kwenda kufungishwa ndoa ya kiserikali, mkristo anayefunga ndoa ya kiserikali ni mwasherati), wanaofungishwa ndoa hizo za kiserikali ni wale ambao bado hawajamjua au kumwamini Yesu Kristo, au kwa namna nyingine wapagani, mfano wa ndoa hizo ni kama ile ya Herodia ambayo alimwacha mumewe aliyeitwa Filipo na kwenda kuolewa na ndugu ya mume wake, sasa ndoa hiyo ya Herodia na Filipo haikuwa ya kikristo, pengine ilikuwa ya kiserikali au ya kitamaduni za taifa lao au ya kidini yao lakini maadamu ilikuwa imeshahalalishwa na jamii yao au serikali yao basi ilikuwa ni dhambi kwa Herodia kumwacha mume wake huyo na kwenda kuolewa na ndugu ya mume wake (kasome kisa hicho katika Marko 6:17-18).
Lakini ikitokea mmoja wa waliofungishwa ndoa ya namna hiyo /kiserikali kaamini na kuwa mkristo na mwenzake hataki kuishi naye kwasababu tu kawa mkristo na akaamua kumuacha..hapo huyu aliyeachwa kwasababu ya Imani yake ya kikristo atakuwa huru kuolewa/kuoa na mtu mwingine ambaye ni mkristo mwenzake tu, lakini kama hata baada ya kuokoka kwake mwenziye ambaye anaishi naye hataki kuokoka lakini bado anataka kuendelea kuishi naye..huyu hana budi kuendelea kuishi naye hata kama hajaokoka..na endapo akimwacha kwasababu tu hataki kuokoka atakuwaa na hatia mbele za Mungu..Na akimwacha na kwenda kuoa/kuolewa na mwingine atakuwa anazini.
Sasa wapo watu huko nyuma kabla ya kuokoka walifunga ndoa ya kiserikali, na baada ya kuokoka wanapojaribu kuwashawishi wake zao/waume zao nao pia waokoke kama wao, wanapowaona wanakataa basi wanakusudia kuwaacha..ingawa bado wanapedwa na hao wenza wao na hawajaachwa..lakini wao kwasababu wameokoka hawataki tena kuishi na wale waume zao/wake zao ambao hawajaokoka..Ndugu usifanye hivyo ni dhambi kubwa sana!..Mume wako/mke wako uliyefunga naye ndoa hata kama ni mlevi lakini hataki kukuacha, basi hupaswi kumuacha…na hiyo ni kulingana na Biblia kasome..1Wakorintho 7:10-15.
Na pia ikitokea wote wawili hapo kwanza walikuwa wamefunga ndoa ya kiserikali na sasa wameokoka na kuifahamu neema ya Kristo, Hawa wote wawili wanapaswa kwenda kanisani kuifanya ndoa yao iwe ya kikristo. Kwasababu ilipofungwa kiserikali haikumhusisha Kristo wala maagizo yake, Wanapaswa kwenda kuahidiana upya mbele za Mungu na wanadamu kwamba wataishi kwa uaminifu pasipo kuachana, na kifo ndicho kitakachowatenganisha, na kwamba watakuwa kielelezo kwa watakatifu wengine wowote kwa kuishi katika ndoa ya kikristo ya mume mmoja na mke mmoja, na mambo mengine ambayo watayaahidi mbele ya kanisa la Mungu na mbele ya Kristo mwenyewe. Baada ya hapo ndoa yao itabarikiwa na Mungu, na kuwa ya kikristo na zile baraka zote za wanandoa zitafuatana nao.
Sasa kuna kundi lingine ambalo linajiita ni wanandoa…Hili ni lile ambalo walikutana tu na kuamua kuishi Pamoja, pasipo utaratibu wowote…ni ile watu wawili wamekutana tu kijana na binti na kuwekana ndani, hakuna cha mahari, hakuna imani. Hawa kibiblia wanafanya uasherati (NI WAASHERATI).
Na endapo ikitokea mmoja kaamini katika hali hiyo waliyopo ya kukaa Pamoja (maana yake katubu na kuwa Mkristo). Moja kwa moja yule aliyeamini anapaswa avunje hayo mahusiano, kwasababu ni uasherati ndio aliokuwa anaufanya..Anapaswa avunje hayo mahusiano hata kama wameshazaa Watoto, arudi kwa wazazi wake, au akaishi peke yake kwa kujitegemea na wanawe… mpaka huyo mwenzake naye atakapotubu kama yeye na kuwa mkristo na kwenda kufunga ndoa kanisani. Lakini endapo huyo mwingine kakataa kutubu katakata na kujisalimisha kwa Yesu Kristo, basi huyu aliyetubu yupo huru kuolewa/kuoa mtu mwingine lakini aliye mkristo kama yeye tu!…(hapaswi kwenda kuoa/kuolewa na mtu ambaye sio mkristo)
Kumbuka tena mtu ambaye ameshamjua Yesu Kristo, na kufahamu kuwa ndoa halali ni ile ya kikristo (mfano wa mimi na wewe ambao tumeshajua sasa) na ameshafahamu kuwa inapaswa ifungwe mbele ya kusanyiko la Kristo, akienda kufunga ndoa yoyote ile kinyume na hiyo, akaenda kufunga ndoa aidha ya kimila au ya kiserikali au akijichukulia tu mke/mume na kuishi naye ndani…pasipo kwenda kuifungisha ndoa yake kanisani BASI ANAFANYA UASHERATI!!…Na waasherati wote biblia inasema hawataurithi ufalme wa mbinguni (1Wakoritho 6:9).
Na pia maana halisi ya neno ndoa ni Muunganiko wa MUME na MKE na sio muunganiko wa mume na mume au mke na mke…Hivyo hicho kinachoitwa ndoa ya jinsia moja hakipaswi kiitwe hivyo…kinapaswa kiitwe “uasherati wa jinsia moja”…na sio “ndoa ya jinsia moja”..Hivyo serikali inayohalalisha “uasherati wa jinsia moja” Huo Mungu kaukataa na ni machukizo makubwa mbele za Mungu..kasome Walawi 20:13.
Je umemwamini Yesu Kristo?, kama bado unasubiri nini?, hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo karibuni kulichukua kanisa lake, je utakuwa miongoni mwa watakaonyakuliwa, Unafahamu kuwa kanisa hili tunaloishi ndio kanisa la mwisho, hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hapa?
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?
Kama kuna majira ambayo si ya kufanya mchezo na masuala ya wokovu wetu hata kidogo basi ni haya. Kwani moja ya hizi siku tutashuhudia mabadiliko makubwa sana na ya ghafla katika kanisa la Kristo,..wakati ambao Bwana Yesu anakwenda kuchukua hatua ambayo hakuwahi kuichukua tangu aondoke hapa duniani.. Na hatua yenyewe ni Kuingia na kuufunga mlango wa hekalu lake.
Hayo mambo pengine utayashuhudia kwa macho yako siku si nyingi,..Kumbuka biblia inalifananisha kanisa la Kristo na hekalu lake (Waefeso 2:19-22)..Sasa ukisoma kitabu cha Ezekieli utaona anaonyeshwa matukio yanayoambata na hakalu la Mungu, Na utaona akionyeshwa malango mengi ya hekalu yakiwa wazi, lakini ukisoma ile sura ya 44 utaona Ezekieli anaonyeshwa ghafla lango la mashariki likiwa limefungwa..Na anaambiwa halitafunguliwa tena, wala mtu awaye yote hataingia kwa kupitia lango hilo.
Ndipo Ezekieli akaambiwa sababu ya lango hilo kufungwa, na sababu yenyewe ilikuwa ni hii..tusome..
Ezekieli 44:1 “Kisha akanirudisha kwa njia ya lango lile la nje, la mahali patakatifu lililoelekea upande wa mashariki; nalo lilikuwa limefungwa.
2 Bwana akaniambia, Lango hili litafungwa, halitafunguliwa, wala mtu awaye yote hataingia kwa lango hili, kwa maana Bwana, Mungu wa Israeli, ameingia kwa hilo; basi kwa sababu hiyo litafungwa”.
Unaona, sababu ni kuwa Bwana, Mungu wa Israeli (KRISTO), ameingia kwa lango hilo.. Hii ni kuonyesha kuwa mlango huo uliwekwa mahususi kwa ajili yake na si mwingine, yeye ndiye aliyekuwa amewekewa wazi mlango huo mpaka atakapofika,. Hivyo wale waliokuwa wanaingia kabla ya hapo ni neema tu, lakini haukuwekwa wazi kwa ajili yao..
Hivyo Habari hiyo jambo kwa sehemu limetimia lakini ni unabii wa siku za mwisho, wakati ambao Mlango wa Neema utafungwa.
Ndugu, huu mlango ambao tunauita wa neema tulio nao leo hii, Mungu kauacha wazi si kwasababu yetu, bali kwasababu ya Yesu Kristo, Ni mlango wa Kristo Yesu mwenyewe na sio wetu, na moja ya siku hizi, hivi karibuni atasimama, kisha ataupita, na akishaingia, basi utafungwa na ukishafungwa, Habari imeishia hapo hautafunguliwa tena milele..
Mambo yatakayokuwa yanaendelea humo ndani ni siri yake na wale watakaokuwa humo.. Kwahiyo usione unahubiriwa injili, usione unapigiwa kilele utubu dhambi ukadhani Mungu anakuangalia wewe sana, hilo jambo halipo! Mungu anamtazama Kristo tu!, achukue hatua yake, na akishaichukua, hapo ndipo kutakuwa na kilio na kusaga meno kama alivyosema, hakutania alimaanisha kweli wapo watu watalia kweli kweli wakitamani hata nusu saa nyuma lirudi watengeneze mambo yao lakini watakuwa wameshachelewa.
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu. 27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno…”
Kumbuka hatua hiyo sio ya unyakuo, hapo unyakuo bado, mambo hayo yatatendeka hapa hapa duniani, kwasababu wakati huo utatamani umjue Kristo, lakini hutaweza tena, kwasababu anayewavuta watu kwa Kristo sasa ni Roho Mtakatifu na sio mtu mwenyewe..Hivyo Roho Mtakatifu akishaondoka juu yako huwezi tena kumfuata Mungu hata iweje..(Yohana 6:44)
Sasa muda mfupi baada ya huo wakati, Unyakuo ndio utapita, na wewe ambaye humtaki Kristo sasa…utaendelea kubaki hapa hapa duniani ambacho kitakachofuata ni dhiki kuu kabla hujafa na kuingia katika jehanamu ya moto. Kama tunavyoona mambo yalivyo sasa, ni tunaishi katika muda wa nyiongeza tu.., hii dunia ingepaswa iwe imeshaisha tangu zamani kulingana na unabii wa kibiblia, lakini dalili zote zinaonyesha sasa wakati wowote, mambo yatabadilika kwa ghafla sana. Na Mlango utafungwa na watu watatamani kuingia watashindwa..
Soma Habari hii kulithibitisha hilo tena..uone jinsi wanawali wale wapumbavu waliporudi na kukuta mlango umefungwa, ufananishe na hali itakavyokuwa wa wakristo wengi vuguvugu waliopo leo duniani..
Mathayo 25 : 1-13 “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.
2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.
3 Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao; 4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.
5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.
6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.
7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. 9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.
10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.
12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.
13 Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa”.
Je! Na wewe bado nje ya mlango huo hujaingia tu ndani mpaka sasa?..Kumbuka tena jambo hili lango hilo likishafungwa mara moja, halitafunguliwa tena milele..(Na Yesu ndiye lango) Ni heri ukatubu dhambi zako leo ikiwa hujafanya hivyo..Ili Mungu atakusamehe na kukupa uzima wa milele bure.
Ufunuo 22:17 “Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.”
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Adamu aliwasaliana na Mungu kwa lugha ipi pale bustanini?
Katika maisha kila mwanadamu ambaye ameumbwa na Mungu mkuu, ni lazima ameumbiwa kitu kinachoitwa huzuni ndani yake. Maana yake ni kwamba ni lazima atapitia vipindi vya huzuni na vile vile atapitia vipindi vya furaha. Kila mwanadamu hata kama ni mtumishi wa Mungu ni lazima atapitia hivyo vipindi..Bwana wetu Yesu Kristo ambaye alikuwa ni mkamilifu asilimia zote alivipitia si zaidi sisi tusiokuwa wakamilifu?..Ni lazima tuvipitie. Na huzuni ni kama ugonjwa ukiwekwa katika mazingira Fulani inazidi na pia ikiwekwa katika mazingira Fulani unapungua.
Na huzuni inaweza kuja aidha kutokana na kupata taarifa mbaya, au umepatwa na jambo baya..au unakwenda kupatwa na jambo baya…au wakati mwingine inakuja pale linapotokea jambo ambalo hukulitegemea au hukulipanga, au hukutamani liwe hivyo lilivyo.
Mtu anapofikia hali kama hiyo anajikuta anazama katika dimbwi kubwa la mawazo, na kukosa hamu ya kufanya jambo lolote lile..hata hamu ya kula inatoweka, wakati mwingine hata hamu ya kuishi.
Siku ile ambayo Bwana ndio alikuwa anakwenda kusulibiwa, Huzuni kubwa iliwaingia wanafunzi wake, baada ya kuwaambia kwamba muda si mrefu atakwenda kusulibiwa, na ataondoka atakwenda zake kwa Baba..
Yohana 16:5 “Lakini sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi?
6 Ila kwa sababu nimewaambia HAYO HUZUNI IMEJAA MIOYONI MWENU.
7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.
Na zaidi ya yote walipoambiwa kwamba mmoja wao atamsaliti..Ndio kabisa moto wote ukakata ndani yao..Wakati wanadhani kwamba Kristo atazidi kuendelea kuwepo, yeye anawapa taarifa za msiba, kwamba anakwenda kusulibiwa..wakawa wanawaza kwanini hayo yote yampate Bwana wao, sasa maisha yatakuwaje baada ya yeye kuondoka.
Na hata Bwana alipowachukua usiku ule kwenda kusali naye hata nguvu zilikuwa zimewaisha kabisa, hawakusali sana wakalala kwasababu ya huzuni nyingi..Tusome..
Luka 22:45 “Alipoondoka katika kuomba kwake, akawajia wanafunzi wake, AKAWAKUTA WAMELALA USINGIZI KWA HUZUNI.
46 Akawaambia, Mbona mmelala usingizi? Ondokeni, mkaombe, msije mkaingia majaribuni”.
Lakini katika hali kama hiyo, Bwana aliuona udhaifu wa mioyo yao kwamba wamechoka na wanahuzuni nyingi. Lakini aliwaambia waamke waombe..kwasababu roho i radhi lakini mwili ni dhaifu…Hivyo wanapaswa waishinde hali hiyo ya huzuni..kwasababu wana huzuni, lakini siku chache baadaye watakuwa na furaha. Hivyo alijaribu kuwaasa kwamba wajaribu kuishinda huzuni ambayo ilipelekea udhaifu wa mwili wasimame waombe kwasababu majaribu hayo ni ya siku chache tu..siku mbili baadaye watakuwa na furaha isiyo na kifani. Kwasababu aliwaambia bado kitambo kifupi hawamwoni (yaani atakufa na kuzikwa)..na tena bado kitambo kidogo watamwona tena (yaani siku atakapofufuka)..wataendelea kumwona mpaka Pentekoste na watakuwa na furaha kuu.(Soma Yohana 20:20).
Katika wakati huu unaoitwa wa pasaka miongoni mwa mambo mengi tunayojifunza basi ni muhimu kulijua hili pia…USIHUZUNIKE..Pengine umepitia shida Fulani, au umepata usumbufu Fulani, au huzuni Fulani, au tabu Fulani, au taarifa Fulani, au jambo lolote lile ambalo limekuletea huzuni kubwa moyoni hata umekata tamaa ya kila kitu na ya kuendelea mbele katika imani…Huo sio wakati wa kuzidi kuipalilia huzuni kwa kukata tamaa na kuiacha Imani, sio wakati wa kulala usingizi kwa huzuni..Bali ni wakati wa kusimama na KUOMBA kwa nguvu…ni wakati wa kuzidi kuendelea mbele kwasababu huzuni hiyo ni ya kitambo tu!. Baada ya siku chache itaondoka na furaha itakurudia kama mwanzo na utajuta kwanini siku chache nyuma ulikuwa unahuzunika…utajuta kwanini ule muda ambao ulikuwa na huzuni usingeutumia hata kuomba au kumsifu Mungu.
Hivyo simama sasa mtu wa Mungu, huu sio wakati wa kupalilia huzuni bali ni wakati wa kuomba..Mitume wa Yesu huzuni yao iligeuka furaha pale walipomwona Bwana kafufuka…nawe pale utakapoona kile kilichokuwa kimekufa kimefufuka, siku sio nyingi furaha yako itarudi. Hivyo usihuzunike..simama uombe, simama uendelee mbele kwasababu hatua zilizobakia mbele yako ni chache kuliko ulizoziacha nyuma. Hivyo sio wakati wa kunyongonyea ni wakati wa kuomba.
Bwana akubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo: