Title 2021

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

Nakusalimu katika jina kuu sana la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuyatafakari maandiko maadamu siku ile inakaribia.

Tukitazama matukio yaliyokuwa yanaendelea pale msalabani yapo mambo kadha wa kadha tunaweza kujifunza. Kwamfano siku ile utaona walimvua  nguo zake zote, wakazigawanya mafungu manne, kila askari fungu lake. Hii ikiwa na maana kuwa Bwana Yesu alisulibiwa akiwa uchi kabisa, hakutuonea haya sisi, iweje sisi tumwonee haya  yeye?

Lakini wale askari walipofika kwenye Kanzu yake nayo, kwasababu ilikuwa ni ya Tano, na wenyewe walikuwa ni wanne, na kila mmoja alitaka apate sehemu ya vazi lile..Wakaona njia rahisi ni kuligawanywa, walau kila mtu apate kipande chake.

Lakini lile vazi lilikuwa ni la kitofauti sana, lilikuwa halijashonwa kwa kuunganishwa vipande mbalimbali hapana.Bali Lote tokea juu hadi chini lilikuwa ni vazi moja, kiasi kwamba kulikuwa hakuna sehemu lilikuwa na kipande kilichojitegemea kikaunganishwa nalo hapana. Unaweza kutazama mfano wa vazi hilo kwenye picha juu.

Hivyo wale askari walipotafuta walau, maungio ya vazi lile ili wawezi kukata wagawane kila mtu kipande chake hawakuona. Pengine walitafuti kwenye mikono hawakuona, kwenye kola hawakuona, kwenye mfuko hawakuona. Mwishoni wakaona ni heri walipigie tu kura, ili liwe la mmojawapo.

Yohana 19:23 “Nao askari walipomsulibisha Yesu, waliyatwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu.

24 Basi wakaambiana, Tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani. Ili litimie andiko lile linenalo, Waligawanya nguo zangu, Na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari”.

Lakini tunaposoma habari hiyo ni jambo gani Mungu anataka tujue? Je! Ni mambo ya mavazi yake tu kupigiwa kura tu au ni nini?

Ujumbe mkuu Mungu anataka tuone hapo  ni  kwamba VAZI LA YESU HALIGAWANYI.. Kwasababu halija ungwaungwa, kama mengine yalivyo. Kama utalihitaji ni sharti ulichukue lote, au uliharibu kabisa, hakuna namna..

Hata sasa, mtu yeyote anayeamua kuwa mkristo, hana budi alivae vazi hili. Ambalo haliungwi ungwi.. Ndilo linalojulikana kama VAZI LA WOKOVU, Tunalolisoma katika

Isaya 61:10 “Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana AMENIVIKA MAVAZI YA WOKOVU, AMENIFUNIKA VAZI LA HAKI, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu.

Unapolivaa vazi hili ni  lazima UUISHI wokovu wote, huwezi kuyakwepa maisha ya utakatifu.. Wakristo wengi wanatafuta kuligawanya vazi la wokovu wawe nalo kwa sehemu tu, hawataki kujitoa kikamilifu kwa Mungu pale wanapookoka. Wanataka waitwe wanakwaya, lakini bado waendelee na uzinzi kwa chini chini, wanataka waitwe vijana waliokoka, lakini waendelee kwenda disco, wavae vimini, na milegezo, na viduku, Wanadhani, hilo jambo linawezekana katika wokovu. Ni kweli litawezekana kwenye dini zao, na madhehebu yao, lakini kwa KWA YESU hilo jambo halipo.

Ndugu, watakaokwenda kwenye UNYAKUO, watakuwa wale tu walio tayari kulichukua vazi lote la Yesu, hao ndio wanaojulikana kama BIBI-ARUSI wa Kristo. Lakini tukijidanganya kuwa tumeokoka, halafu bado tupo nusu nusu, hatueleweki sisi ni wa upande upi, ipo wazi kuwa wakati ule tatabaki tu hapa duniani kwenye dhiki kuu ya mpinga-Kristo, na kama hutakuwa hai, basi utaendelea kubakia makaburini mpaka siku ile ya ufufuo itakapofika uhukumiwe uende motoni.

Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; KWA MAANA KITANI NZURI HIYO NI MATENDO YA HAKI YA WATAKATIFU”.

Naamini utakuwa unatambua kuwa tunaishi katika kanisa la Laodikia, na uvuguvugu na tabia ya kanisa hili ni kuwa lipo Vuguvugu, tofauti na  yale mengine. Hivyo Bwana atuepushe na uvuguvugu huu uliopo duniani leo.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Wanefili walikuwa ni watu gani?

Wanefili tunawasoma kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Mwanzo 6:4, Tusome..

Mwanzo 6:4 “Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana; HAO NDIYO WALIOKUWA WATU HODARI ZAMANI ,WATU WENYE SIFA.

5 Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.”

Sasa tafsiri ya wanefili ni “watu wakubwa”.. yaani watu wenye maumbo makubwa. Hivyo wanefili walikuwa ni watu wenye miili makubwa sana.. Na biblia inaendelea kusema kuwa walikuwa ni WATU HODARI na WENYE SIFA. Maana yake walikuwa ni watu wenye uwezo mkubwa wa kiakili na vile vile walikuwa ni watu wenye sifa (maaana yake maarufu na wanaojulikana sana). Hivyo hawakuwa tu wakubwa kama tembo halafu hawana akili, hapana! Walikuwa wakubwa na vile vile walikuwa na uwezo mkubwa wa kiakili, ambao uliwafanya wawe maarufu.

Sasa asili ya hawa wanefili ilianzia kwa Kaini. Ikumbukwe kuwa Kaini baada ya kumuua ndugu yake, alilaaniwa na Mungu, na baada ya ile laana, Mungu alimtia alama Kaini ili yeyote atakayemwona asimuue.

Mwanzo 4: 13 “Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.

  14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.

 15 Bwana akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. BWANA AKAMTIA KAINI ALAMA, MTU AMWONAYE ASIJE AKAMPIGA.

 16 Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni”

Umeona hapo? Kaini anatiwa alama na Mungu, ili kila atakayemwona asimpige!.. Sasa alama hiyo aliyotiwa na Mungu sio mchoro Fulani katika mwili, hapana bali ni UKUBWA WA MWILI NA AKILI, hiyo ndiyo alama aliyowekewa Kaini na Mungu, ambayo itakuwa kwake kama ulinzi, kila atakayemwona na kujaribu kumdhuru aogope!..  kwa kawaida ni ngumu kujaribu kupambana na mtu aliyekuzidi ukubwa!

Kwahiyo Uzao wa Kaini, Mungu aliupa akili na ukubwa, ingawa ulikuwa umelaaniwa..Laana ile ilimfanya Kaini na uzao wake kuacha kazi zao za ukulima, kwasababu walishalaaniwa, na kuanza kufanya kazi nyingine za ufugaji na utengenenezaji wa bidhaa..Ndio maana ukiendelea mbele kidogo kusoma utaona wana wa Kaini wanajishughulisha na utengenezaji wa vyuma na shaba na bidhaa nyingine, kama vifaa vya muziki n.k. (Mwanzo 4:22)

Hivyo kwa shughuli hizo zikawafanya wawe watu maarufu sana duniani na hodari, wakajenga miji mikubwa, na wakawa na ustaarabu wao, wakazaliana wao kwa wao, na wakafanyiana biashara wao kwa wao kwa hizo bidhaa zao na hivyo wakawa na ngome kubwa duniani…

Kutokana na ngome yao kuwa kubwa, na ukubwa wa teknolojia yao, maana ndio watu wa kwanza kugunudua vyuma, shaba na madini mengine yote,  na zana zote za kazi, ni wazi kuwa jamii nyingine za watu ziliwaogopa.. (ili litimie neno la Bwana kwamba kila atakayemwona Kaini asimuue) na pengine walijiwekea sheria ya kwamba yeyote atakayemuua mtu yeyote wa jamii ya uzao wa Kaini adhabu yake ni “kulipiziwa kisasi mara saba”, kwasababu wao ndio walikuwa hodari na wenye nguvu kuliko wengine wote. Ni sawa na wakati wana wa Israeli wapo Misri utumwani, ni wazi kuwa ilikuwa ni kosa kubwa sana kwa mwisraeli aliye mtumwa kumuua Mmisri, pengine adhabu yake ilikuwa ni kubwa sana!. Au wakati wa kipindi cha ukoloni,barani Afrika, inawezekana ilikuwa ni adhabu kubwa sana, mtu mweusi kumuu mtu mweupe!, kutokana na nguvu walizokuwa nazo watu weupe!.. Ndicho kilichokuwa kinaendelea katika dunia ya wakati wa Nuhu.

Lakini wakati huo huo uzao wa Sethi ambao Mungu aliuweka ili kuziba pengo la Habili, ulikuwa ni wa watu wakawaida wakulima na vile vile wafugaji. Uzao huu haukulaaniwa, ndio WANA WA MUNGU tunaowasoma katika Mwanzo 6:2. Na walikuwa ni watu wenye Miili ya wastani, (kwaufupi ni watu wa kawaida tu), na hawakuwa hodari kama hawa Wana wa Kaini (Wanefili).. uzao wa Kaini ndio ulioitwa WANA WA WANADAMU na wanawake wao Binti za Wanadamu (Mwanzo 6:2)

Hivyo wana wa Mungu walipowatamani hao binti za wanadamu na kuwaoa, jambo hilo likamchukiza Mungu, kwasababu ni dhahiri kuwa waliwageuza mioyo, wakapunguza au wakaacha kabisa kumtumainia Mungu wa mbingu na nchi. Hivyo dunia ikajaa dhuluma, kukawa hakuna tena watu wanaomcha Mungu..

Kwahiyo wanefili walikuwa ni wanadamu, ambao ni uzao wa Kaini, na si (mchanganyiko wa wanadamu na malaika), biblia inasema Malaika hawaoi wala hawaolewi (Marko 12:25).

Lakini hata leo hawa wanefili wapo!. Wanaweza wasiwe wakubwa kimwili lakini ni wakubwa kiulimwengu!. Watu wenye sifa na hodari, ambao wanaweza kutengeneza ala za miziki ambazo zinaweza kuiteka dunia nzima, ambao wanaweza kutengeneza filamu na ikakomba watu wengi, ambao wanaweza kutunga mitindo wa mavazi ikaharibu mamilioni ya wanawake, ambao wanaushawishi mkubwa wa kimawazo ambayo ni kinyume na mapenzi ya Mungu, hao ndio wanefili wa kipindi hichi…

Na biblia inasema kama zilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa siku za kuja kwake mwana wa Adamu (Luka 17:26). Siku za Nuhu wana wa Mungu waliwatamani binti za wanadamu.. kadhalika siku hizi wana wa Mungu (wakristo) wanawatamani binti za wanadamu (wanawake wa kiulimwengu), na wanawake wa kikristo wanawatamani wana wa ulimwengu huu, na kujitafutia wanaume wanaowataka!, pasipo hata kujali vigezo vya kibiblia. Jambo ambalo ni machukizo mbele za Mungu kwasababu watawageuza mioyo na kuwafanya wamwache Mungu. Ndicho kilichotokea wakati wa Nuhu.

Binti wa Mungu, jiepushe na tamaa za ulimwengu huu.. Furaha pekee ya maisha utaipata kwa Yesu na si kutafuta kuoelewa na mtu asiyemcha Mungu, huyo atakugeuza moyo wako umwache Mungu, maandiko yanasema hivyo. (1Wafalme 11:2-4)

Kijana uliyemwamini Yesu, jiepushe na wanawake wa kidunia, usiitamani mitindo yao, wala mionekano yao…hao watakugeuza moyo, kama walimgeuza Sulemani aliyekuwa na Hekima kuliko watu wote, hawatakushindwa wewe!!. Hivyo Kabla ya kukimbilia kuoa, ni heri ukambadilisha kwanza ampokee Yesu Yule Yule uliyempokea wewe, na awe na imani ile ile uliyonayo wewe, na ubatizo ule ule ulionao wewe, na Roho Mtakatifu Yule Yule uliyenaye wewe (Waefeso 4:5). Vinginevyo utakuwa unajiharibia mwenyewe.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba wanefili walikuwa ni majitu, hawakuwa na habari na Mungu isipokuwa mambo ya ulimwengu huu!. Walikuwepo wakati wa Nuhu, na baada ya Nuhu walikuwepo na hata leo wapo!

Bwana atubariki na kutulinda.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

MUNGU HAONI SHIDA KUMUHAKIKISHIA MWOVU ULINZI.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?

SWALI: Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”. Kwanini isingesema tu mara moja saba, mpaka ianze sita,halafu tena saba?


JIBU: Ni lugha ya zamani, iliyotumika kuwekea msisitizo kitu hususani kile cha mwisho, yaani, kama inadhaniwa ni sita, basi kipo na cha saba ambacho ndio zaidi.

Kwa mfano ukisoma ile Mithali 6:16  inayozungumzia mambo sita ambayo Mungu anayachukia utaona anaongezea na kingine cha saba, ambacho  ni “kupanda mbegu ya fitina katika ya ndugu” ikiwa na maana hicho ndio kibaya zaidi..

Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.

17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;

18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;

19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu”.

Ukisoma pia  Mithali 30:18 “utaona Sulemani anasema tena kati ya mambo ambayo yanamshangaza mienendo yao, yapo matatu lakini lile la nne ndio zaidi, ambalo ni mwendo wa kijana pamoja na msichana.

Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.

19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana”.

Vivyo hivyo, ukisoma Mithali 30:29, Sulemani anasema pia vipo vitu vitatu vyenye mwendo wa kupendeza lakini akakiongezea na cha nne chenye mwendo wa kupendeza zaidi nacho ni mfalme asiyehasika.

Mithali 30:29 “Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote;

31 Jimbi aendaye tambo; na beberu; Na mfalme ambaye haasiki”.

Soma, pia vifungu hivi;

Mithali 30:15 “Mruba anao binti wawili, Waliao, Nipe! Nipe! Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!

16 Kuzimu; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!”

Ayubu 5:19 “Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.

Amosi 1:3 “Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Dameski, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya kupuria vya chuma”;

Soma pia Amosi 1:4.

Na hata sasa, katika mambo saba(7) ambayo  biblia inasema yanamkamilisha mwanadamu, lipo la nane(8) ambalo ndio kuu zaidi linaloitwa UPENDO.

Tusome.

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,

6 na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa,

7 na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, UPENDO.

8 Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.

Ni vizuri tukawa na hayo mengine yote, lakini tukikosa upendo wa Ki-Mungu, basi bado hatujakamilishwa.

Je! Upendo wa AGAPE upo ndani yako?

Ili kufahamu tunaupate upendo wa namna hii, fungua link hii>>

https://wingulamashahidi.org/2020/12/21/nitaupataje-upendo-wa-ki-mungu-ndani-yangu/ 

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

UFUNUO: Mlango wa 1

Je! kuna madhara kuchukiwa na kila mtu kwasababu huna mali?. Kama biblia inavyosema katika Mithali 14:20?.

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Rudi nyumbani

Print this post

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

Adui yetu shetani, ni kama simba angurumaye akitafuta mtu wa kummeza (1Petro 5:8), hivyo usiku na mchana anatupigana vita ili mradi, atuangushe au atwae vile tulivyo navyo.

Leo tutaingalia njia moja anayoitumia kutunyang’anya baraka zetu.

Shetani akishajua kuna Baraka Fulani umeahidiwa na Mungu, moja kwa moja anaanza kutafuta njia ya kukupokonya hiyo, sasa tofauti na wengi wanavyodhania kuwa adui yetu shetani anatunyang’anya baraka zetu kwa kutuloga, au kututumia wachawi!.. La! Hakuna uchawi wowote unaweza kubatilisha Baraka za Mungu alizotuahidia kwa kinywa chake.

Wengi wanapoteza nguvu nyingi na muda mwingi kushughulika na wachawi na washirikina wakidhani wao ndio wanaozuia Baraka Mungu alizowaahidia juu ya maisha yao kumbe sio!. Shetani anajua kabisa hawezi kamwe kutupokonya kile Mungu alichotuahidia, hizo nguvu hana!. Mungu akisema nitakupa hiki au kile, shetani hawezi kubatilisha hilo jambo..hivyo hatumii uchawi, wala uganga!.. Anachotumia ni kutafuta tu njia ya kumkosesha mtu na Mungu wake ili Mungu aibatilishe ile ahadi aliyomuahidia… Huo ndio uchawi mkubwa wa shetani, wala si mwingine!.

Kwamfano umekwenda katika njia za haki, umekuwa mnyenyekevu mbele za Mungu, umemtumikia na Mungu akapendezwa na wewe sana, hata akakupa ahadi kama alivyompa Ibrahimu, pengine  labda ya kuishi miaka mingi, au hata ya kupata mtoto au jambo lingine lolote zuri..na pengine akakuonyesha kabisa hata katika maono, au hata akamtuma malaika wake kukupa huo ujumbe.

Anachofanya shetani baada ya kujua kuwa umepewa ahadi kabambe kama hiyo, si kukutumia wachawi wakuloge au wachukue nyota yako.. la! Hawezi kufanya hivyo kwasababu anajua atakuwa anapoteza muda..atakachokifanya ni kuhakikisha wewe unaitumainia ile haki yako ya kwanza, na kuanza kukufanya upoe kuendelea kutenda haki.. ili Mungu achukizwe na wewe, na aiondoe ile ahadi aliyokuahidia…

Utauliza je! Mungu huwa anabatilishaga ahadi zake? Jibu ni ndio!.. Endapo mtu akiacha njia yake ya haki na kurudia uchafu, Mungu huwa anazighairi zile ahadi zote alizomwahidia mtu, haijalishi alimtuma malaika wake kumpelekea ujumbe, au alimtokea yeye mwenyewe, lakini mwisho ataibatilisha tu… Utauliza ni wapi katika maandiko tunasoma hilo…

Ezekieli 33:13 “Nimwambiapo mwenye haki, ya kwamba hakika ataishi; KAMA AKIITUMAINIA HAKI YAKE, AKATENDA UOVU, basi katika matendo yake ya haki, hata mojawapo halitakumbukwa; bali katika uovu wake alioutenda, atakufa katika uovu huo”.

Bwana akikupa ahadi ya kuishi miaka mingi, ukikengeuka na kuacha haki yako, utakufa kabla ya kutimiza miaka yako, japokuwa alishakuonyesha kuwa utaishi miaka mingi.

Dada, unayemcha Mungu sasa, Bwana akikuonyesha kuwa umebeba mtoto siku za mbeleni, au atakutumia kwa viwango vikubwa mbeleni na wewe ukakengeuka, na kuanza kufanya uasherati, ukaanza kuvaa kama wanawake wa kidunia wanavyovaa, ukaanza kuwa msengenyaji n.k, hiyo ahadi utaisahau.. Utabaki kujiuliza kama kweli ni Mungu alizungumza na wewe siku ile au la!.. Utatanga tanga huku na kule.. Na jambo hilo halitatimia kwako, na mwisho utakata tamaa na kusema Mungu ni mwongo!. Si mwongo, tayari shetani kashaitwaa Baraka yako siku nyingi sana, na wala hajaitwaa kwa uchawi!.. Ameitwaa kwa kukufarakanisha wewe na Mungu wako.

Kumbuka siku zote kuwa, Bwana akikupa ahadi ya jambo Fulani haimaanishi kuwa hilo jambo ndio tayari umeshalipata!. (Hilo usilitoe katika akili yako)

Inawezekana na wewe leo hii shetani kashakunyang’anya taji yako, au ahadi yako nzuri ambayo Mungu alishakupa…shetani ameshakurudisha kwenye ulimwengu, ndio maana huoni tena dalili ya ile ahadi  Mungu aliyokupa kutimia, alikuonyesha maono ya kwamba utakuja kumtumikia, na tena kwa viwango vikubwa.. lakini mpaka sasa huoni chochote unajiuliza ni Mungu kweli alikuonyesha yale maono au ni kitu gani!..

Ndio ni Mungu mwenyewe ndiye aliyekuonyesha, na wala hakukudanganya, isipokuwa ni  wewe ndio umemruhusu shetani kuitwaa taji yako…. Ulisahau kuwa ahadi za Mungu zinatimia juu yetu, endapo tu tukidumu katika mapenzi yake, tunapotoka katika mapenzi yake hakuna ahadi yoyote ya Mungu itakayotimia juu yetu.

 Lakini habari nzuri ni kwamba tumaini bado lipo, hata kama shetani kakuibia Baraka yako, upo uwezekano wa wewe kuirudisha tena, na zile Baraka zote zilizofutwa juu yako zikakurudia…

Ezekieli 33:15 “kama mtu mwovu akirudisha rehani, na kumrudishia mtu mali yake aliyomnyang’anya, akizifuata sheria za uzima, asitende uovu wo wote; hakika ataishi, hatakufa.

16 Katika dhambi zake zote alizozitenda, hata mojawapo haitakumbukwa juu yake; ametenda yaliyo halali na haki; hakika ataishi.”

Unachopaswa kufanya sasa, ni kutubu!..na kumrudia Bwana kwa moyo wako wote!.. sio umrudie kwasababu tu unataka Baraka!. Bali urudi kwasababu kweli umejua wewe ni mkosaji, njia zako ni mbovu, kama ulikuwa unaiba unaacha wizi, na unarudisha vile ulivyoiba kama bado vipo katika uwezo wa mikono yako, kama ulikuwa ni mzinzi unaacha uzinzi, kama ulikuwa ni mlevi unaacha ulevi kwa vitendo, kama ulikuwa unavaa vibaya, (Ni mwanamke lakini unavaa suruali, vimini, wigi, hereni, unapaka lipstick n.k) yote hayo unaacha, mwanaume kama ulikuwa unanyoa mitindo ya kidunia, na ulikuwa unavaa nguo za kidunia unaacha..na mambo mengine yote yasiyofaa.. Na baada ya kuacha yote hayo, na kutubu hatua inayofuata ni ubatizo, kumbuka ubatizo ndio unaokamilisha wokovu kwa mtu (Marko 16:16). Na ubatizo sahihi ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo.

Na baada ya hapo Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yako, atakuongoza na kukutia katika kweli yote. Na yeye mwenyewe atazirejeza zile Baraka zote na ahadi zote zilizokuwa zimefutwa juu yako. Utaziona zinatimia mbele ya macho yako.

Hiyo ndiyo njia rahisi ya kurejesha Baraka zako na Ahadi zako, wala huhitaji kuombewa na mtu.. Na wewe tu kurejesha mahusiano yako na Mungu, ambayo yalikuwa yamevurugwa..na Baraka zako zote utaziona..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni vitu vipi hivyo viwili visivyoweza kubadilika? (Ebr 6:18)

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

Ni vitu vipi hivyo viwili visivyoweza kubadilika? (Ebr 6:18)

Rudi nyumbani

Print this post

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo litukuzwe milele. Karibu tujifunze Neno la Mungu.  Kuna wakati sisi wenyewe ndio tunakuwa kikwazo cha Kristo kujifunua kwetu katika utimilifu wake wote, na hiyo yote ni kwasababu tuna mioyo miwili miwili kwake. Leo tutaangalia makundi mawili ya watu. Moja ni wale mafarisayo, na la pili ni mitume wa Yesu likiongozwa na Nathanieli.

Kuna wakati mafarisayo walimwomba Yesu awaonyeshe Ishara itokayo juu ili waamini zaidi, Lakini Yesu akawaambia kamwe hawatapewa Ishara yoyote, isipokuwa ile ishara ya Yona.Akiwa na maana Ishara ya hukumu.

Mathayo 12:38 “Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.

39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi”.

Ili kufahamu kwa urefu alikuwa anamaanisha nini, juu ya hiyo  ishara ya Yona unaweza kufungua link hii kusoma >>> https://wingulamashahidi.org/2019/05/13/madhara-ya-kutafuta-ishara/ 

Lakini Bwana hakuwa na nia ya kutojifunua kwao zaidi, isipokuwa ile mioyo yao, ya kutokuamini, ya unafki, ndio iliyowapelekea kutoona utukufu wa Mungu mkubwa zaidi ya yale waliyoyaona, akiyafanya.

Lakini kulikuwa na wakati ambao Yesu yeye mwenyewe aliwathibitishia wale waliomwamini kuwa wataona mambo makubwa zaidi ya yale waliyomjua kwayo. Lakini hiyo yote ilihitaji kwanza watu hao kutokuwa na “HILA” ndani yao kama Nathanieli alivyokuwa.. Tusome..

Yohana 1:43 “Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate.

44 Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro.

45 Filipo akamwona Nathanaeli, akamwambia, Tumemwona yeye aliyeandikiwa na Musa katika torati, na manabii, Yesu, mwana wa Yusufu, mtu wa Nazareti.

46 Nathanaeli akamwambia, Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone.

47 Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, HAMNA HILA NDANI YAKE.

48 Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona.

49 Nathanaeli akamjibu, Rabi, wewe u Mwana wa Mungu, ndiwe Mfalme wa Israeli.

50 Yesu akajibu, akamwambia, Kwa sababu nilikuambia, Nilikuona chini ya mtini, waamini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.

51 Akamwambia, Amin, amin, nawaambia, Mtaziona mbingu zimefunguka na malaika wa Mungu wakikwea na kushuka juu ya Mwana wa Adamu”.

Kama tunavyoweza kusoma hapo, Nathanieli alipokutana na Filipo hakuona shaka ndani yake, juu ya habari njema alizoletewa, japokuwa zilikinzana na kile alichokifahamu hapo kabla..Lakini alikuwa radhi kwenda kufuatilia, kwasababu nia yake ilikuwa ni kupata jambo jema, na sio kitetea dini..

Leo hii ni watu wachache sana, wanaweza kuwa tayari kusikia au kufuatilia lile jambo linalokinzana na imani yao, au dhehebu lao, hata kama watajua ni kweli kiasi gani, bado watapuuzia tu, wakiambiwa katika maandiko hakuna ubatizo wa vichanga, wanadhani wanapelekewa dini mpya, ukiwaeleza habari za kuokoka watakuambia dhehebu lao haliamini hilo.. Unaona, hizo ni HILA zilizondani ya mtu. Lakini Nathanieli hakuwa hivyo? Yeye alipoelezwa tu habari za MASIHI, Akauliza, Je! Inawezekana kweli jambo jema kutokea Nazareti mji ambao haujaandikiwa chochote? Lakini yeye hakuacha kwenda kutazama, ajihakikishie.

Na matokeo yake Yesu alipomwona, hakuhitaji kujieleza mbele zake, Yeye mwenyewe alimtamkia habari zake. “Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake”. Hakuwa na wingu la udhehebu wala udini kama mafarisayo walivyokuwa..Yeye alikuwa radhi kwenda kutazama, mahali ambapo hata hapana uelekeo wa kutokea Kristo.

Na matokeo yake ikawa ni Yesu kuwaambia wataona makubwa zaidi ya yale.. Yaani atajifunua kwao kwa katika viwango vingine vya juu sana, kwasababu walikuwa tayari kumwamini na kumfuata. Na ndio utaona ni hao peke yao ndio walioweza kumwona Yesu mpaka hatua ya mwisho ya kupaa kwake.

Hata na sisi leo hii, tukumbuke kuwa Yesu ni yeye Yule jana na leo na hata milele. (Waebrania 13:8).  Yupo tayari kutuonyesha makubwa zaidi ya haya tunayoyajua, lakini ufarisayo wetu, uvuguvugu wetu, ndio unaotukwamisha tusimjue Kristo katika viwango vingine vya utukufu.

Tunadhani Yesu ni ile sura yake tu basi, hapana, Yesu ni Ufunuo wa Mungu mwenyewe. Na huwa hajifunui kwa watu wote sawasawa. Na ndio maana alivyotembea na mitume haikuwa sawa na alivyotembea na makutano, vilevile sio yote aliyowafunulia mitume aliwafunulia makutano au waandishi. Na sio kila mahali alipopita watu wote walijua. Hapana.

Hiyo yote ni kuonyesha kuwa anajifunua na kutembea katika viwango.

Hata sasa,  yatupasa tumwamini Yesu, tuiamini biblia, tuondoe HILA mioyoni mwetu. Tuwe tayari kutii kile ambacho biblia inatufundisha hata kama kitakinzana vipi na madhehebu yetu, tukiona maandiko yanatuambia tubatizwe kwa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, tutii, tukiambiwa sanamu ni machukizo kwa Mungu, tutii, tukiambiwa hakuna njia nyingine yoyote ya kutufikisha mbinguni isipokuwa ya Yesu tu peke yake, na sio mtume mwingine fulani tuamini hilo, hata kama dini zetu zimetufundisha hivyo tangu tulipozaliwa kuwa kuna mtume mwingine.

Tukizingatia mambo kama hayo, ambayo ni maagizo ya Yesu mwenyewe kwenye BIBLIA yake. Basi tujue kuwa tupo kwenye daraja kubwa sana, na kumwona yeye katika viwango vingine vya tofauti sana, vya mbingu kufunguka juu yetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

BIRIKA LA SILOAMU.

RABI, UNAKAA WAPI?

Rudi nyumbani:

Print this post

Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?

SWALI: Nini maana ya hii mistari?

Isaya 42:19 “Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu? Au aliye kiziwi, kama mjumbe wangu nimtumaye? Ni nani aliye kipofu, kama yeye aliye na amani? Naam, kipofu kama mtumishi wa Bwana?

20 Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake ya wazi, lakini hasikii”.


JIBU: Maneno hayo hayamaanishi kuwa watumishi wa Mungu wote ni vipofu na viziwi kwamba wanaona mambo mengi lakini hawayatilii maanani, hapana.

Bali Isaya kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu aliandika kwa wayahudi, Ambao  hao ndio waliokuwa kwanza kumjua Mungu, kufahamu sheria zake, kuona miujiza yake na matendo yake makuu, tangu zamani, na ndio maana akawafananisha na watumishi / wajumbe wake. Lakini kinyume chake wao ndio wakawa wa kwanza kukimbilia kuabudu miungu mingine, na kufuata mambo maovu, kuliko hata mataifa ambayo hayamjui Mungu.

Jambo kama hilo liliendelea mpaka kipindi cha kutokea kwa Masihi duniani(Yesu Kristo), mafarisayo na waandishi ambao ndio wangepaswa wawe wa kwanza kumtambua Kristo wao, na kumwamini, kutokana na kuwa walishajua unabii wake katika torati tangu zamani, lakini kinyume chake ndio waliokuja kumpinga, na kumuua.

Na ndio maana Bwana Yesu akawaambia maneno haya..

Yohana 9:39 “Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.

40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu?

41 Yesu akawaambia, Kama mngekuwa vipofu, msingekuwa na dhambi; lakini sasa mwasema, Twaona; basi dhambi yenu inakaa”.

Unaona? Hata sasa, inasikitisha kuona baadhi ya watu wanaojiita ni watumishi wa Mungu ni vipofu rohoni. Kwasababu kama tutashindwa kujua kiini cha Kristo kuja hapa duniani ni nini. matokeo yake tunaigeuza injili ya Kristo kuwa sehemu ya biashara, na mahali pa kutafutia tu mafanikio, na sio wokovu tena, hakuna cha kukemewa dhambi, wala mafundisho ya mbinguni. Huo ni upofu wa hali ya juu sana.

Tunakuwa hatuna tofauti na wale mafarisayo na masadukayo, na wale watumishi wa mishahara ambao Bwana Yesu aliwataja katika. Yohana 10:12-13

Bwana atusaidie sana, tusiwe vipofu na viziwi, kwa kubaki katika misingi ya Neno la Mungu..

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

WANA WA MAJOKA.

WAPE WATU WANGU RUHUSA ILI WAPATE KUNITUMIKIA.

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

TAFAKARI SANA KABLA YA KUAMUA HATIMA YAKO.

Mharabu ni nani katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Makuruhi ni nini, kama tunavyosoma katika biblia?

Makuruhi; Ni neno linalomaanisha “kuchukiza kuliko pitiliza”, Kwa mfano mtu akisema mabeberu ni makuruhi kwa waafrika. Anamaanisha kuwa mabeberu ni watu wanaochukiza sana/ au ni harufu mbaya sana kwa waafrika, hawapendwi hata kidogo. Na hiyo yote ni kwasababu ya maumivu ambayo pengine walishawahi kuyapata kutoka kwao enzi za utumwa.

Vivyo hivyo neno hili katika biblia utalisoma katika mstari huu;

1Samweli 13:4 “Waisraeli wote wakasikia habari ya kwamba Sauli ameipiga hiyo ngome ya Wafilisti, na ya kwamba Waisraeli wamepata kuwa MAKURUHI kwa Wafilisti. Basi hao watu wakakusanyika pamoja kumfuata Sauli huko Gilgali.

5 Nao Wafilisti wakakusanyana ili wapigane na Waisraeli, magari thelathini elfu, na wapanda farasi sita elfu, na watu kama mchanga ulio ufuoni mwa bahari kwa wingi wao; wakapanda juu, wakapiga kambi yao katika Mikmashi, upande wa mashariki wa Beth-aveni”.

Habari hiyo ni baadaya ya Israeli kuwavamia kambi mojawapo ya wafilisti na kuipiga, na kisha kujigamba baada ya hapo, Hivyo wafilisti walivyosikia hivyo ikawabidi wawachukie Israeli kupitiliza, mpaka ikawabidi wafilisti wote waungane na idadi yao ikawa kama mchanga wa bahari ili waifutilie Israeli mbali, hiyo yote ni  kwasababu tayari wameshafanyika kuwa makuruhi kwao.

Lakini kama tunavyoijua habari ni kuwa, walikuja kuuliwa wote, na waisraeli kwa msaada wa Mungu.

Jambo kama hili linajirudia leo hii, Vita kati ya Israeli na Palestina.  Wapalestina (ambao ndio wafilisti wa kipindi kile), sasa wanawachukia wayahudi kupitiliza, Israeli imekuwa harufu mbaya kwao, na hiyo yote ni kutimiza maandiko. Ili baadaye Mungu aje kujichukulia utukufu kutoka katika vita ambavyo vitakavyopiganwa siku za hivi karibuni pale Israeli ( Soma Ezekieli 38 &39).

Na sio tu ni makuruhi kwa  wapalestina peke yao. Hapana bali wataendelea kuwa hivyo, mpaka kwa dunia nzima. Ili kutimiza unabii wa vita ile kuu ya Har Magedoni ambayo itapiganwa pale Israeli, siku za mwisho. Vita hiyo itakuwa kati ya Israeli na mataifa yote duniani.

Zekaria 12:3 “Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake”.

Kwa urefu wa vita hiyo na mambo hayo yatakayotokea fungua link hii > https://wingulamashahidi.org/2018/07/17/siku-ya-bwana-inayotisha-yaja/

Hivyo ndugu, unapoona migogoro inayoendelea Israeli leo hii, usidhani ni ishara nzuri kwako wewe mwenye dhambi. Hiyo ni ishara ya Israeli kurudiwa na Mungu. Na moja ya hizi siku tutaona mabadiliko ya ghafla katika hii dunia. Na mabadiliko hayo yakishatokea tujue kuwa Unyakuo utakuwa umeshapita wakati huo, kanisa lipo mbinguni kwenye karamu ya mwana-kondoo.

1Wathesalonike 5:3 “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Jiulize, mabadiliko hayo yakitokea leo, wewe utakuwa wapi?

Majibu yote yapo moyoni mwako.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Ufunuo 12 inaelezea vita vya wakati upi?

NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Rudi nyumbani

Print this post

MUNGU ATAKUUA UKIWA MBAYA MACHONI PAKE.

Mwanzo 38:6 “Yuda akamwoza mke Eri, mzaliwa wake wa kwanza, na jina lake huyo mke ni Tamari.

7 Naye Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mbaya machoni pa Bwana; na Bwana akamwua”.

Lazima tukumbuke kuwa Mungu anatazama matendo ya kila mmoja wetu katika hii dunia, Na pale yanapovuka mipaka yake aliyoiweka tujue kuwa tunayahatarisha maisha yetu sisi wenyewe.

Vifuatavyo ni vitu ambavyo, havimpendezi Mungu, na kama vipo ndani yako, basi hakikisha vinaondoka mapema sana. Tulishajifunza huko nyuma lakini ni vizuri tujikumbushe tena, ili visiondoke mioyoni mwetu. Tunavisoma katika..

Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.

17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;

18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;

19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.

MACHO YA KIBURI:

Kiburi ni kujiona wewe ni bora kuliko wengine, upo juu wa wengine wote, hivyo unawadharau , hutaki kurekebishwa, hutaki kuonywa, hutaki kuwasaidia wengine. watu wa namna hii, ni machukizo mbele za Mungu, katika biblia kulikuwa na mtu aliyeitwa Nabali, ni mfano wa mtu aliyekuwa na kiburi, japokuwa alisaidiwa na Daudi kuangaliwa mifugo yake, lakini bado alimdharau na kumtukana, kisa tu ana mali, na mafanikio, na mwisho wa siku Mungu akamuua. (1Samweli 25:1-38)

Kiburi pia kinachozungumziwa hapo ni kiburi cha uzima. Kisa una afya, ni mzuri, una nguvu, una mafanikio, basi ukielezwa habari za Mungu, wewe ni kudharau, na kudhihaki, na kukebehi, unasema watu wanaomtafuta Mungu ni watu wajinga, wavivu, hawana akili. Kama wewe ni mmoja wapo wa hili kundi la watu, jirekebishe mapema sana, upo hatiani kuuliwa na Mungu.

ULIMI WA UONGO: 

Kilichomfanya shetani apewe adhabu ya kutupwa katika ziwa la moto, ni pamoja na uongo aliokuwa nao tangu mwanzo. Bwana Yesu alisema..

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; KWA SABABU YEYE NI MWONGO, NA BABA WA HUO”.

Embu fikiria na wewe pale unapokuwa mwongo mwongo kwa kila jambo, unadhani Mungu atapendezwa na wewe? Hawezi kinyume chake unajitafutia kifo tu na hukumu. Uongo unaharibu mahusiano ya mtu na Mungu kwa kiasi kikubwa sana. Tuziponye ndimi zetu.

MIKONO IMWAGAYO DAMU ISIYO NA HATIA:

Kundi lingine ambalo Mungu halipendi kabisa, ni la wauaji. Wengi wanadhani kuwa muuaji ni mpaka utimilize  tendo lenyewe. Hapana, kitendo tu cha kusema nashika silaha,nashika kisu, panga, n.k. na kwenda kuvamia kuiba, tayari wewe ni muuaji, kwasababu hiyo silaha uliyobeba tayari ulishawaza kichwani mwako, endapo ikitokea shida utaitumia kujihamu, ikiwezekana hata kuua. Mambo kama hayo, yanavuta kifo chako cha kiroho na kimwili kwa haraka sana.(Mathayo 5:21-22). Acha matendo yenye harufu za uuaji nyuma yake. Zitakupunguzia maisha yako hapa duniani.

MOYO UWAZAO MAWAZO MABAYA:

Ni moyo ambao hauna fikra chanya kwa Mungu, au katika kuuendeleza ufalme wa Mungu. Badala yake ni moyo ambao unawaza uzinzi wakati wote, unafikiria mbinu ambazo unaweza kupata pesa ukatumie katika anasa. Moyo ambao unaamka asubuhi unafikiri ukafanye kazi ile baadaye ukamalizie siku yote baa.

Moyo ambao unafikiria utapeli, uporaji, dhulma, hauna nafasi hata mara moja kufikiria hatma ya maisha yake ya baadaye, haumfikirii muumba wake, haufikirii kumtolea Mungu, haufikirii kuifanya kazi ya Mungu. Watu kama hawa Mungu anawaua mapema sana, aidha rohoni au mwilini.

MIGUU ILIYO MYEPESI KUKIMBILIA MAOVU;

Kwa kawaida mwanadamu yoyote ni lazima aone ugumu Fulani, katika kutekeleza jambo ambalo sio la haki, ni lazima ashtuke pale anapoletewa habari ya kwenda kuzini na mke wa mtu, anapoambiwa tule rushwa n.k. Lakini kama wewe ni mwepesi wa kukimbilia maovu, mtu anakwambia twende Disko na wewe unakurupuka kuongozana naye, twende tukaibe, unakurupuka kuenda, twende tukazini mume wangu kasafiri, na wewe unaenda, Ujue mwisho wako utakuwa ni mbaya sana, kwasababu miguu hiyo ni mepesi kukimbilia maovu. (Mithali 1:16 , 7:5-27)

SHAHIDI WA UONGO ASEMAYE UONGO;

Huyu ni zaidi ya mtu anayesema uongo. Huyu anaushuhudia kabisa uongo  kuwa ni kweli. Kipindi kile Yezebeli aliajiri watu wamshuhudie uongo Nabothi kwamba amemkufuru Mungu, ili watu wampige mawe afe ili arithi kiwanja chake 1Wafalme 21:1-16

Hata leo hii, wapo watu ni hodari wa kushuhudia uongo, wanafundishwa kusema uongo ili wasitiri dhambi zao, au za wengine, hilo ni jambo baya sana, ambalo linamchukiza Mungu. Bwana atusaidie tusifanyike mashahidi wa uongo.

NAYE APANDAYE MBEGU ZA FITINA KATI YA NDUGU:

La mwisho ndio hili, unatunga uchonganishi katikati ya ndugu wanaomwamini Mungu, ili wachukiane, wagombane, wasiongee, unavunja umoja wao na upendo wao, ambao Bwana Yesu aliwaombea wawe nao katika Yohana 17. Lakini wewe furaha yako ni kuona hivyo. Jambo hilo linamchukiza sana Mungu.

Wakati Mungu anasema,Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu. Wewe unakuwa mchonganishi..kinyume chake ni kuwa utaitwa mwana wa Ibilisi.

Hivyo tunapoishi hapa duniani tuwe watu wenye Hofu ya Mungu. Tusiishi kana kwamba Mungu hatuoni.. Anatuona, na tunavyozidi kuwa wabaya ndivyo tunavyoyaweka maisha yetu hatarini. Ni wazi kuwa mtoto wa Yuda, alifanya mojawapo ya dhambi hizo na ndio maana Mungu akamuua. Vivyo hivyo na sisi tujichunguze kama mambo hayo yapo basi tuyaweke mbali na sisi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

TABIA KUU TATU ZA WAHUBIRI WALIORUDI NYUMA NA KUMWACHA MUNGU.

VIKAANGUKA MACHONI PAKE VITU KAMA MAGAMBA.

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani:

Print this post

Je! kuna madhara kuchukiwa na kila mtu kwasababu huna mali?. Kama biblia inavyosema katika Mithali 14:20?.

Jibu: Tusome,

Mithali 14:20 “Maskini huchukiwa hata na jirani yake; Bali tajiri ana rafiki wengi”.

Na  pia

Mithali 19:4 Inasema  “Utajiri huongeza rafiki wengi; Bali maskini hutengwa na rafiki yake”.


Hizi ni Mithali ziliyoandikwa na Mfalme Sulemani, kwa hekima alizopewa na Mungu, na zipo Mithali nyingine nyingi alizoandika kwa mafunzo na maonyo. Lakini tofauti na inavyodhaniwa na wengi, Kuwa kila Mithali Sulemani aliyoiandika ilikuwa ni agizo! Hapana!. Sio kila mithali tunayoisoma katika kitabu cha Mithali ilikuwa ni agizo!. Mithali nyingi Sulemani alizoziandika zilikuwa zinahusu uhalisia wa jambo Fulani, na si agizo la jambo Fulani.

Kwamfano mimi leo nikisema “Watu wengi walio wapole wanaonewa na kudhulumiwa”. Hapo sijatoa agizo kwamba wapole wasiendelee kuwa wapole tena, waanze kuwa wakali na wakorofi. bali nimezungumza “uhalisia, jambo fulani ambalo lipo!”. Na huo umetokana na mimi kuchunguza mpaka nikaja na jawabu hilo.

Kadhalika Mithali nyingi Sulemani alizoziandika hazikuwa ni maagizo, bali ni uhalisia wa mambo fulani, ambayo yapo!!!  na huo unatokana na uchunguzi alioufanya!..Na mfano mmojawapo alioutoa ambao ulikuwa ni uhalisia na si agizo ndio huu tunaousoma..

Mithali 14:20 “Maskini huchukiwa hata na jirani yake; Bali tajiri ana rafiki wengi”.

Sasa hapa sio kwamba Sulemani, alitoa agizo kwamba.. “kuwa maskini watafute utajiri ili wawe na marafiki wengi”. Hapana hakumaanisha hivyo, Kwasababu ingekuwa ndivyo mbeleni asingekuja kusema tena haya maneno..

Mithali 28:6 “Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotofu wa njia angawa ni tajiri”

Umeona! alisema maneno kwasababu alichunguza na kuona kuwa Walikuwepo Maskini wenye busara na hekima, ambao katika haki yao yote bado hawakupendwa, walichukiwa… Na hapo hapo akaona walikuwepo matajiri wengi ambao katika udhalimu wao walipendwa na wengi. Jambo ambalo ni kawaida hata sasa, mtu aliye na mali hata kama ni mali za haramu atapata marafiki wengi!..(lakini ni marafiki wasiofaa)

Hebu tusome tena mahali pengine Sulemani alipochunguza jambo kama hilo..

Mhubiri 9:14 “Palikuwa na mji mdogo, na watu ndani yake walikuwa wachache; akaja mfalme mkuu juu yake, akauhusuru, akajenga ngome kubwa ili kuupiga.

15 Basi, kulionekana humo MTU MASKINI MWENYE HEKIMA, naye kwa hekima yake akauokoa mji ule lakini hata hivyo HAPAKUWA NA MTU YE YOTE ALIYEMKUMBUKA YULE MTU MASKINI.

16 NDIPO NILIPOSEMA, BORA HEKIMA KULIKO NGUVU; walakini hekima ya maskini hudharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi.

17 Maneno ya wenye hekima yanenwayo taratibu husikiwa, Zaidi ya mlio wake atawalaye katikati ya wapumbavu.

18 Hekima NDIYO BORA KUPITA SILAHA ZA VITA; Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi”

Umeona hapo?.. Sulemani anamsifu Maskini mwenye hekima, ambaye kwa hekima yake ameuokoa mji, anasema “Bora hekima kuliko nguvu, na hekima ni bora kuliko silaha za vita”.

Mithali 16:16 “Si afadhali kupata hekima kuliko dhahabu? Naam, yafaa kuchagua ufahamu kuliko fedha.

Na japokuwa anamwona maskini huyo hakumbukwi, wala hatapendwa na wengi, wala marafiki wengi, wala hakuna mtu aliyemkumbuka.. Lakini kwa hekima yake ameuokoa mji, na hivyo ipo thawabu yake baada ya maisha haya…

Mhubiri 4:13 “Heri kijana maskini mwenye hekima Kuliko mfalme mzee mpumbavu”.

Kwahiyo  ni vizuri kuzichambua vyema hekima za Sulemani na kuzielewa, kwasababu si kila kitu kilichoandikwa kule ni agizo!..

Tukirudi katika ukristo pia hatujaahidiwa kwamba tukimpokea Yesu tutakuwa na marafiki wengi, au ndio tutapendwa na watu wengi..la! kinyume chake ndio tutachukiwa.. Na kuchukiwa huko sio laana!, bali ndio muhuri wa wito wetu.

Luka 21:16  “Nanyi mtasalitiwa na wazazi wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu.

17  Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu”

Vile vile hatujaahidiwa kuwa tunapozaliwa mara ya pili ndio hatutapitia dhiki za hapa na pale.. vipindi vya dhiki vitakuwepo, lakini Bwana ameahidi kuwa atakuwa na sisi hatatuacha.

Bwana Yesu alisema maneno haya..

Ufunuo 2:9 “Naijua dhiki yako NA UMASKINI WAKO, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.

10  Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima”

Mathayo 16:2  “Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi”.

Bwana atubariki na kutusaidia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine


Mada Nyinginezo:

TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

Mego ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Mithali 17:1)

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

Rudi nyumbani

Print this post

Ni yupi aliyekuwa mkwe wa Musa kati ya Reueli na Yethro?

JIBU: Ukisoma katika kitabu cha Kutoka, utaona kuna habari kama inajichanganya kuhusiana na baba-mkwe halisi wa Musa, Kwamfano Kutoka 2:18 Inasema aliitwa Reueli, lakini sehemu nyingine zote zilizosalia kama vile Kutoka 3:1,4:18, inamtaja kama ni Yethro. Je  kuna makosa ya kiuandishi?

Embu tusome baadhi ya vifungu hivyo;

Kutoka 2:15 “Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani; akaketi karibu na kisima.

16 Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la baba yao.

17 Wachungaji wakaja wakawafukuza; lakini Musa akasimama, akawasaidia, akalinywesha kundi lao.

18 Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo?

19 Wakasema, Mmisri mmoja alituokoa katika mikono ya wachungaji, tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi.

20 Akawaambia binti zake, Yuko wapi basi? Mbona mmemwacha mtu huyo? Mwiteni, ale chakula.

21 Musa akawa radhi kukaa kwake mtu yule, naye akampa Musa binti yake, Sipora.

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu”.

Jibu ni kuwa hakuna hitilafu, yoyote ya kiuandishi isipokuwa zamani ilikuwa ni jambo la kawaida mtu mmoja kuwa na jina zaidi ya moja, Kwamfano tukimtazama Yakobo, Mungu alimwambia utaitwa Israeli, Hivyo majina yake yote mawili utayakuta yakiandikwa sehemu mbalimbali katika biblia Lakini mtu ni Yule Yule mmoja.

Vivyo hivyo na Yethro mkwewe Musa, aliitwa pia Reueli, na kwasababu alikuwa ni kuhani, hatushangai kuona akiwa na majina mawili, moja la kwake la asili na lingine la kikuhani.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Rudi nyumbani

Print this post