Title 2021

Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio?

SWALI: Je! Mwandishi wa kitabu cha Warumi alikuwa ni Paulo au Tertio? kulingana na mstari huu;

Warumi 16:22 “Mimi Tertio, niliyeandika waraka huu, nawasalimu katika Bwana”.


JIBU: Paulo katika maneno yake ya utangulizi alishatupa  mwangaza kuwa yeye ndiye aliyekiandikia kitabu hicho, kiwaelekee watakatifu wote waliokuwa Rumi. Tusome;

Warumi 1:1 “PAULO, MTUMWA WA KRISTO YESU, ALIYEITWA KUWA MTUME, NA KUTENGWA AIHUBIRI INJILI YA MUNGU;

2 ambayo Mungu amekwisha kuiahidi kwa kinywa cha manabii wake katika maandiko matakatifu;

3 yaani, habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili,

4 na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu;

5 ambaye katika yeye tulipokea neema na utume ili mataifa yote wapate kujitiisha kwa imani, kwa ajili ya jina lake;

6 ambao katika hao ninyi mmekuwa wateule wa Yesu Kristo;

7 KWA WOTE WALIOKO RUMI, WAPENDWAO NA MUNGU, WALIOITWA KUWA WATAKATIFU. Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo”.

Lakini baadaye karibia na mwishoni mwa waraka huu tunakuja kumwona mtu mwingine aliyeitwa Tertio akijitokeza na kusema ameuandika waraka ule. Sio kwamba mtume Paulo hakuhusika hapana, Jibu ni kwamba Tertio alikuwa ni mwandishi wa mtume Paulo, aliyekuwa anamwandikia nyaraka zake. Aidha kwa kuandika kile alichokuwa anaambiwa au kwa kunakili kile alichoandikiwa na Paulo, japo hakuna sehemu nyingine katika biblia Tertio anaonekana akitajwa.

Na kulikuwa na sababu ya mtume Paulo kutokutumia mkono wake mwenyewe kuandikia waraka huu, pengine Tertio alikuwa ni mwandishi  mwaminifu anayejulikana sana  na watakatifu waliokuwa Rumi kwa umahiri na ufanisi wa kazi zake zilizothibitishwa. Hivyo mtu akiona waraka ulionakiliwa na yeye, basi ilikuwa ni rahisi kuamini uhalisia wa yule mwandishi husika. Kwasababu wakati huo walikuwepo pia watu waliojifanya ni mitume, na kutoa kopi zao wakidai kuwa ni za mitume, ili tu kuwachanganganya watu.

Na ndio maana mtume Paulo ili kuthibitisha nyaraka zake, sehemu nyingine alikuwa anatia sahihi yake mwishoni, soma(2Wathesalonike 3:17), na pia na hapa aliona  ni vema amtumie huyu Tertio kuuandika kwa warumi, iwe kama sahihi yake.

Hivyo waraka huu uliandikwa na Paulo, lakini aliyeunakili ni Tertio.

Hii ni kutufundisha kuwa, si kila kazi ya Mungu, hata kama tutaiona  ni nyepesi kiasi gani, tuifanye sisi mwenyewe, wakati mwingine tutahitaji tushirikiane na viungo vingine vya Kristo, ili kuleta ufanisi Zaidi wa kazi hiyo kwa watu wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

Kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe.

Rudi nyumbani

Print this post

JIFUNZE KUSEMA NA MUNGU KATIKA HALI ZOTE.

Kumbuka Mungu yupo katika masumbufu, Na pia Mungu yupo katika utulivu. Katika majira yote na wakati wote jifunze kuzungumza na kuisikia sauti ya Mungu.

Unaweza ukajiuliza ni kwanini Mungu alimtokea Ayubu katika upepo wa kisulisuli na kuzungumza naye, (Ayubu 38:1), lakini Eliya alimtokea katika mazingira ya utulivu mkuu?.(1Wafalme 19:11-13)

Jibu ni kuwa sio kwamba alikuwa anataka kumtisha Ayubu hapana bali alikuwa anataka kumuonyesha kuwa katikati ya misukosuko, katikati ya tufani za Maisha, katikati ya dhiki, katikati ya shida, katikati ya magonjwa, na umaskini yeye yupo hapo kuzungumza naye na kumsaidia. Biblia inasema..

Nahumu 1:3b “..Bwana ana njia yake katika kisulisuli na tufani,…”

Vilevile alipojifunua kwa Eliya katika sauti ya upole na utulivu, alikuwa hamwonyeshi kuwa yeye anajua kuongea kwa utulivu sana, na upole hapana, lakini alikuwa anamwonyesha kuwa katikati utulivu na amani yeye pia yupo kuzungumza na watu wake.

Mwanzoni Ayubu alidhani Mungu amemwacha kwa dhiki alizokuwa anazipitia ,alidhani hastahili tena mbele za Mungu, hata Mungu alipokuwa anasema naye kwa kinywa cha Elihu mwana wa Barakeli, hakutambua, alidhani Mungu kakaa mbali naye, mpaka akadhubutu kusema laiti kama Mungu angekuja nihojiane naye (Ayubu 13:3) akidhania kuwa Mungu yupo mbali naye.

Kumbe hakujua Mungu alikuwa karibu naye kuliko alivyokuwa anadhani. Leo hii lipo kundi kubwa la wakristo, linadhani pale palipo na amani tu, pale palipo na mafanikio tu ndio Mungu yupo hapo katikati yao, pale wanapopitia raha, wanapokuwa katika afya na mafanikio katika biashara zao, pale wanapopata heshima  hapo ndipo wanaweza kukaa chini na kuzungumza na Mungu.

Lakini pale mambo yanapoharibika kwa ghafla, tufani na upepo kidogo wa kusulisuli unapovuma juu yao wanamtupa Mungu nyuma yao, wanasema Mungu hawezi kuwepo hapa ameniacha, wanapopitia dhiki kidogo utaona ni rahisi kupoa kama sio kuuacha wokovu kabisa, wanapougua, hawategi sikio tena kusikia chochote kuhusu Mungu. Wanachofanya ni kukimbilia kutafuta njia mbadala kwa ajili ya suluhu za shida zao.

Kumbuka biblia inasema.. Nahumu 1:3b “..Bwana ana njia yake katika kisulisuli na tufani,…”

Unaona, sio tu katika mahali pa utulivu, lakini pia katikati ya Tufani na kisulisuli. Wakati mwingine Mungu atakujilia kwa njia hii. Hivyo uonapo hayo ikiwa wewe ni mkristo, usiogope.

Kuna wakati mtume Paulo alipitia njaa mara nyingi lakini hakumwacha Bwana. Kuna wakati alipitia kutajirika sana lakini bado aliendelea na Bwana.. mpaka akadhubutu kusema ninayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Wafilipi 4:12 “Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.

13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.

Je na sisi  tunaweza kusimama kwa ujasiri na  kuzungumza na Mungu katika tufani ? Bwana atusaidie tuyatambue na hayo ili tusiiache Imani, kwasababu maadamu tupo duniani, Mambo ya ghafla yanaweza kututokea, lakini hatupaswi kumtupa Mungu nyuma.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho

Mada Nyinginezo:

Mtu mwenye “kitango” ni mtu wa namna gani kibiblia?

Shubaka ni nini kibiblia? (Mithali 7:6)

USIISHI KWA NDOTO!

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Tusome,

Yohana 5:45  “Msidhani kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba; yuko anayewashitaki, ndiye Musa, mnayemtumaini ninyi.

46  Kwa maana kama mngalimwamini Musa, mngeniamini mimi; kwa sababu yeye aliandika habari zangu.

47  Lakini msipoyaamini maandiko yake, mtayaamini wapi maneno yangu?”

Mstari huo haumzungumzii Musa kama Musa, kwamba yupo mahali Fulani mbinguni, anawashitaki watu..hapana!! bali unazungumzia maneno ya Musa (yaani mahubiri yake). Hayo ndiyo yanawashitaki watu sasa, na yatakayowashitaki watu siku ya hukumu, ndio maana hapo katika mstari wa 47 unamalizia kwa kusema.. “Lakini msipoyaamini maandiko yake, mtayaamini wapi maneno yangu?”.

Sasa Ni kwa namna gani maneno ya Musa yanawashitaki watu sasa?, tutakuja kuona mbele kidogo, lakini sasa tuangalie kwa ufupi ni jinsi gani yatawashitaki watu siku ya hukumu…

Bwana Yesu alisema mahali Fulani maneno haya..

Yohana 12:47  “Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu

48  Yeye anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, ANAYE AMHUKUMUYE; NENO HILO NILILOLINENA NDILO LITAKALOMHUKUMU SIKU YA MWISHO.

49  Kwa sababu mimi sikunena kwa nafsi yangu tu; bali Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema.”

Umeona? hapo Bwana Yesu anasema..”Neno analolihubiri ndilo litakalohumu siku ya mwisho”.

Hivyo hata Musa naye, hasimami kumhukumu mtu, bali injili yake ndiyo itakayohukumu watu siku ya mwisho..Kama Musa alitabiri kwamba “Atakuja Masihi”, na Masihi alipokuja kweli kulingana na huo unabii, watu wakamkataa Masihi huyo, basi siku ile ya hukumu, Unabii ule alioutoa kwa uwezo wa Roho utawahukumu wale watu, waliomkataa Masihi. Kwasababu Musa alisema kitu alichoonyeshwa na Mungu, na wala si kwa nafsi yake.

Na si maneno ya Musa tu peke yake, bali na ya Mitume wote wa Mungu na Manabii katika biblia takatifu.

Kwamfano utaona mahali Fulani Mtume Paulo alisema maneno yafuatayo kwa uwezo wa Roho…

1Wakorintho 6:9  “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? MSIDANGANYIKE; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”

Na mtu akausikia mstari huo aliouzungumza Paulo kwa ufunuo wa Roho, lakini akaudharau, na kuona kama kasema hayo kwa akili zake, siku ile ya hukumu, Maneno hayo ya Mtume Paulo yatamhukumu. Ndio maana Mtume Paulo mwenyewe alisema tena maneno yafuatayo..

Warumi 2: 16 “katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, SAWASAWA NA INJILI YANGU, kwa Kristo Yesu”.

Hapo anasema “sawasawa na Injili yangu”.. maana yake tutahukumiwa kulingana na Injili ya Paulo, na mitume wengine kwenye biblia, ndio maana nyaraka za Mitume, Roho Mtakatifu kazifanya leo kuwa ni Neno lake.  Chochote kilichozungumzwa na Mtume Paulo katika biblia, au Mtume Petro, au Yohana, au Mathayo kimekuwa ni NENO LA MUNGU KAMILI, na wala si la huyo mtume, na ndicho siku ile ya hukumu, kitakacho hukumu watu.

Mtume Paulo alisema  kwa ufunuo wa Roho…“  Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika kama sina upendo mimi si kitu”. Maana yake kama hatutatafuta upendo kwa bidii, na kujitumainisha kwa karama tulizo nazo, kama lugha au unabii,  siku ile hatutaurithi uzima wa milele, kwasababu Neno hili litasimama kutuhukumu, kwamba tulipaswa tuwe na upendo na si karama tu peke yake.

Lakini pamoja na hayo, Maneno yote ya Watumishi wa Mungu waliopo katika Biblia, yanasimama pia kutuhukumu leo, Maana yake ni kwamba Injili ya Musa, Paulo, Petro, Yohana, na wengine wengi katika biblia, yapo yanatuhukumu wakati huu.

Sasa yanatuhukumu kwa namna gani?

Jibu ni rahisi, kwa njia ya MASHITAKA!.

Mtu anayejiita ameokoka, na huku anajua kabisa katika biblia Mtume Paulo aliandika kwa uwezo wa Roho katika..

1Wakorintho 6:16  “Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja”

Na kwa kulijua hili neno, akakaidi na kwenda kufanya uasherati makusudi, moja kwa moja Shetani analichukua hili andiko na kwenda nalo mbele za Mungu, kumshitaki mtu huyo, atakachosema ni hichi>> “Bwana Mungu Yule mtu, anayesema amekupokea wewe, tazama anafanya uzinzi na kahaba makusudi na ilihali anajua kabisa katika maandiko yako umesema, yeye ajiunganishaye na kahaba ni mwili mmoja naye,”.

Kwa mashitaka kama hayo, shetani anashinda hoja juu yako, na hivyo unahesabika kuwa na hatia juu ya hilo andiko… Ni heri ungekuwa hujaokoka halafu unafanya hayo, shetani asingekuwa na hoja nyingi juu yako, lakini unasema umempokea Yesu lakini unafanya uasherati, hapo ndipo unakabidhiwa shetani na Adui yako shetani anaweza kukufanya lolote kuhakikisha kuwa unakuwa mwili mmoja na Yule unayezini naye… Maana yake matatizo yake yote na laana anazobeba huyo unayezini naye, zinakuja kwako (kwasababu mmeshakuwa mwili mmoja), hata kama anamapepo basi na wewe ni rahisi kuyashiriki. Ndio maana kuna hatari kubwa sana ya kulipuuzia Neno la Mungu, hata tukiwa hapa duniani, kabla hata ya kufika siku ya hukumu.

Hivyo ni muhimu sana kulifuata na kulishika Neno la Mungu, na wala si la kulidharau, kwasababu  ndilo tutakalohukumiwa nalo siku za Mwisho na ndilo linalotushitaki sasa kupitia adui yetu shetani. Na neno la Mungu linapatikana katika kitabu kimoja tu! Kinachoitwa Biblia yenye vitabu 66, na si kwenye kitabu kingine chochote.

Kama hujampokea Yesu leo, huu ndio wakati wako, shetani hakupendi kama unavyodhani, anachokitaka kwako ni ufe katika dhambi zako, siku ile ukahukumiwe na kutupwa katika lile ziwa la Moto. Huko tumwache aende peke yake, lakini sisi tujiokoe roho zetu kwa kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo, na kutubu dhambi zetu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu, na kupokea Roho Mtakatifu, ili tujiweka salama na tuwe na uhakika wa uzima wa milele.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho


Mada Nyinginezo:

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

MMESIKIA KWAMBA IMENENWA?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya usimfunge ng’ombe kinywa apurapo nafaka!.(Kumbukumbu 25:4)

Jibu: Neno kupura maana yake ni “kutenganisha mbegu ya nafaka kutoka katika suke lake”. Kwamfano tunapozitoa punje za ngano, au mchele kutoka katika masuke yake, hapo tunakuwa tumezipura hizo nafaka, tunapotoa maharage kutoka katika yale maganda yake, hapo tumepura maharage.

Sasa zipo njia nyingi za namna ya kupura nafaka,  zamani njia maarufu  zilizokuwa  zinatumika ni aidha kutumia watu au wanyama. Lakini katika zama zetu hizi, zipo mashine za kufanya hivyo.

Kwahiyo njia hiyo ya kwanza ya kutumia watu, ni pale watu wanapoyatwaa masuke makavu na kuyatwanga au kuyachapa na kitu mfano wa fimbo nzito, njia hii ilikuwa ni ya kuchosha kidogo kwasababu ilihitaji nguvu na watu, na ilikuwa inachukua muda mrefu. Lakini pia ilikuwepo njia ya wanyama, ambapo mnyama kama ng’ombe analazimishwa kupita juu ya  masuke ya nafaka hizo kavu, na anapozikanyaga, zile mbegu zinatengana na masuke yake. Hivyo njia hii ilikuwa ni rahisi, kwasababu ilikuwa haitumii nguvu, na ilikuwa ni ya muda mfupi!. Ni sawa na kilimo cha mkono na kile cha kutumia ng’ombe. Kile cha ng’ombe ni rahisi Zaidi kuliko cha mkono.

Sasa wakati wa kupura kulikuwa na tabia ya watu kuwafunga ng’ombe midomo wakati wa kuzipura nafaka!, ili wasizile zile nafaka. Kwahiyo mtu yupo tayari kumfanyisha ng’ombe kazi ya kupura tani kadhaa za nafaka, lakini hataki hata aonje katika kile kidogo, wakati anazipura. Sasa kwa tabia hiyo ndipo Mungu akawapa amri wana wa Israeli kwamba wakati wa kupura nafaka wasiwafunge ng’ombe vinywa, maana yake wawaache na wenyewe wale katika hizo nafaka zinazopurwa.

Kumbukumbu 25: 4 “Ng’ombe apurapo nafaka usimfunge kinywa”.

Sasa kwanini Mungu aliitoa hiyo sheria?. Ni kwasababu ng’ombe hata iweje hawezi kumaliza tani nzima ya nafaka, atakula kidogo tu atashiba!, hiyo nyingine ataacha, hivyo haiwezi kuleta athari yoyote wala hasara yoyote kwa mzigo ule wote wa nafaka. Kwasababu mpaka umeamua kutumia ng’ombe kupuria na si mkono wako, maana yake mzigo wa nafaka ulio nao ni mwingi. Kwahiyo kumnyima ng’ombe chakula kidogo tu katika hicho, ambacho ni anakila tu hapo hapo, na wala hakipeleki ghalani, ni kukosa utu na huruma.

Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.

Sasa ufunuo wa mstari huo ni nini?..Mtume Paulo kwa uweza wa Roho alitoa ufafanuzi

Tusome, 1Wakorintho 9:9, (zingatia vipengele vilivyoainishwa kwa herufi kubwa)

1Wakorintho 9:9 “Kwa maana katika torati ya Musa imeandikwa, USIMFUNGE KINYWA NG’OMBE APURAPO NAFAKA. JE! HAPO MUNGU AANGALIA MAMBO YA NG’OMBE?

10 Au yamkini anena hayo kwa ajili yetu? Naam, yaliandikwa kwa ajili yetu; kwa kuwa alimaye nafaka ni haki yake kulima kwa matumaini, naye apuraye nafaka ni haki yake kutumaini kupata sehemu yake.

11 IKIWA SISI TULIWAPANDIA NINYI VITU VYA ROHONI, JE! NI NENO KUBWA TUKIVUNA VITU VYENU VYA MWILINI?

12 Ikiwa wengine wanashiriki uwezo huu juu yenu, sisi si zaidi? Lakini hatukuutumia uwezo huo; bali twayavumilia mambo yote tusije tukaizuia Habari Njema ya Kristo.

13 HAMJUI YA KUWA WALE WAZIFANYAO KAZI ZA HEKALUNI HULA KATIKA VITU VYA HEKALU, NA WALE WAIHUDUMIAO MADHABAHU HUWA NA FUNGU LAO KATIKA VITU VYA MADHABAHU?

14 NA BWANA VIVYO HIVYO AMEAMURU KWAMBA WALE WAIHUBIRIO INJILI WAPATE RIZIKI KWA HIYO INJILI”.

Katika mfano huo, ng’ombe kafananishwa na Mtumishi yeyote wa kweli wa Mungu, au anaweza kuwakilisha kanisa la Kristo, maana yake ni kwamba kama kuna sehemu unanufaika kiroho aidha kanisani au kupitia mtumishi wa Mungu, kwamba kupitia yeye au hilo kanisa, pamechangia pakubwa sana kupata mafanikio yako ya kiroho na kimwili, hupaswi kuzuia chochote katika vile Mungu alivyokubariki, yaani kumbariki yule mtumishi au lile kanisa, au ile huduma. KWASABABU HATAKULA CHOTE!, ni kidogo tu.. Ng’ombe anapokusaidia kupura tani zako za nafaka, anachotaka kutoka kwako kama ujira wake, ni kile chakula cha siku tu!..wala hahitaji ghala lako zima, utakuwa usiye na utu kama utamnyima hata hicho!!. Kwasababu hicho ndicho kitakachompa nguvu ya yeye kuendelea kukusaidia kuzipura hizo nafaka.

Kadhalika utakuwa ni mtu wa ajabu sana, kama utakuwa unanufaika na Baraka za kimbinguni kupitia watumishi wa Mungu, halafu hujigusi hata kidogo!!!.. Ni biblia ndio inasema hivyo, kwamba  hao wahubirio injili, wapate riziki kupitia hiyo. Lakini kama utaona ni sawa wewe kunufaika kiroho lakini si sawa kuchangia chochote!.. Hapo unajipunguzia thawabu zako tu! Za rohoni na mwilini. Biblia inasema wewe ni mkatili! Na mwovu! (Mithali 12:10).

Ametumia mfano mrahisi tu! Wa ng’ombe apurapo nafaka!… ili tuweze kuelewa ni jinsi gani ilivyo ni jambo la kikatili, kuzuilia fedha yako au chochote Mungu anachokubariki,  katika kuipeleka kazi ya Mungu mbele, na ilihali unanufaika na hicho kitu kwa asilimia kubwa.

Unaweza kusoma tena juu ya jambo hilo hilo katika 1Timotheo 5:18.

Je! Wewe ni miongoni mwa wanaowafumba vinywa ng’ombe zao wapurapo nafaka?..wewe ni mmoja wao wa watu wakatili na waovu??. Kama ni mmoja wao basi tubu!..kwasababu ulikuwa unafanya dhambi, na anza kuwa mwenye huruma, na mtu unayejali. Mtolee Mungu kwa moyo pasipo kulazimishwa, kwasababu pumzi unayovuta hulipii chochote, uzima ulionao anakupa bure!, injili unayoipata kila siku hautozwi chochote, sasa kwanini na wewe usijali pasipo kuambiwa, wala kulazimishwa.

Bwana akubariki.

Kumbuka Kristo anarudi, na dalili zote zimeshatimia, hivyo kama hujampokea Yesu, ni vizuri ukafanya hivyo leo na wala si kesho!.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara”

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho


Mada Nyinginezo:

NGUVU YA SADAKA.

MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe.

SWALI: Mtume Paulo alikuwa na maana gani kusema kwa herufi gani hii kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe?

Wagalatia 6:11 “Tazameni ni kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe”!


JIBU: Ili tufahamu vizuri ni vema tukatazama maudhui ya kitabu cha Wagalatia ilikuwa ni nini, Kitabu hichi Mtume Paulo aliwaandikia wagalatia, kanisa ambalo alilizaa yeye mwenyewe katika Kristo. Kulingana na kitabu kuna wakati ambapo aliondoka, lakini akiwa huko mbali alipata taarifa kuwa Wagalatia wameiacha Imani aliyowaachia hapo mwanzo na kuigeukia injili ya namna nyingine, Ambayo kimsingi ililetwa na baadhi ya wayahudi waliotoka Yerusalemu.

Wagalatia 1:6 “Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine.

7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo”.

Wayahudi waliowashurutisha watu wa mataifa waliokoka, kuwa ni lazima watahiriwe kama sheria ya Musa inavyosema ndio ukristo wao utakubalika mbele za Mungu, na sio kutahiriwa tu bali pia wazishike sheria nyingi zote, kama torati inavyosema vinginevyo Mungu hawatambui.

Na kweli baadhi ya wagalatia hao wakaanza kuishi kama wayahudi walivyoishi, wakaanza kuzishika sabato, kutahiriwa, kutawadha kabla ya kula, n.k. mambo ambayo hapo kabla walikuwa hawayafanyi na Kristo alikuwa pamoja nao.

Lakini mtume Paulo kujua hilo wameshageukie injili ya aina nyingine ndio akawaandikia huo waraka kwao, mpaka kufika hatua ya kuwauliza ni nani ALIYEWALOGA?.

Wagalatia 3:1 “Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?

2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na Imani”?

Walikuwa wanaenenda vizuri, wamepokea Roho Mtakatifu, iweje sasa, wanayarudia mafundisho manyonge ya awali ya wayahudi ya kuishi katika mwili tena? Msiguse, msishike, msionje..(Wagalatia 2:21). Jambo hilo lilimshtusha sana mtume Paulo.

Sasa mwishoni kabisa baada ya maonyo mengi, mtume Paulo ndio anahitimisha kwa kusema..

Wagalatia 6:11 “TAZAMENI NI KWA HERUFI GANI KUBWA nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe!

12 Wote watakao kuonekana ni wazuri kwa mambo ya mwili, ndio wanaowashurutisha kutahiriwa; makusudi wasiudhiwe kwa ajili ya msalaba wa Kristo, hilo tu.

Kusema hivyo, ni kuonyesha msisitizo wa waraka wake, wa maneno aliyoyasema kuwa yupo makini na alichokisema, na anamaanisha..na ndio maana waraka huo akauandika kwa maneno makubwa, tofauti na nyaraka zake nyingine, kuonyesha kuwa maagizo aliyowapa ni sahihi.

Ni kama leo hii tu, ukikutana na habari fulani halafu katikati ukakutana na sentensi imeandikwa kwa herufi kubwa, utafahamu kuwa mwandishi anawekea msisitizo hicho alichokisema, ndicho alichokifanya Paulo wakati ule, waraka ule aliundika katika herufi kubwa(au maneno makubwa), kuonyesha msisitizo wa alichokisema.

Leo hii natamani pia baadhi ya madhehebu kama vile sabato watambue waraka huu, kwasababu kulikuwa na sababu kubwa sana ya Paulo kuandika maneno hayo, kwasababu alijua kabisa mambo haya bado yanaweza kupuuziwa na baadhi ya waaminio, hata siku za mwishoni, Lakini cha kusikitisha ni kuwa wagalatia wengi bado wapo  leo hii  miongoni  mwa wakristo.

Kitendo cha kuichagua siku Fulani na kuifanya kuwa takatifu Zaidi ya nyingine na kusema hiyo ndio muhuri wa Mungu, wakati biblia inatuambia muhuri wa utakatifu wetu ni Roho Mtakatifu (Waefeso 4:30), tujue kuwa tumeshalogwa na injili nyingine ambayo sio ile tuliyoachiwa na mitume.

Kitendo cha kusema nyama Fulani ni najisi, kwamba tukiila hiyo, tunamkosea Mungu, tujue tayari tumeshachukuliwa na mafundisho ya injili nyingine.

Turudi kwenye misingi ya Neno bila kujali madhehebu yetu yanatufundisha nini. Hapo ndipo tutakapokuwa salama. Vinginevyo tutakuwa tumeshachukuliwa na roho zidanganyazo ambazo zilizotabiriwa kutokea siku za mwisho za kuwazuia watu wasile vyakula ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani soma (1Timotheo 4:1-5).

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “yamfaa afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, na kutoswa katika kilindi cha bahari?”

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

FAHAMU UWIANO MUNGU ANAOHITAJI KUUONA KWETU.

“Yodi” ni nini kama tunavyoisoma katika Mathayo 5:18?

Rudi nyumbani

Print this post

TABIA KUU TATU ZA WAHUBIRI WALIORUDI NYUMA NA KUMWACHA MUNGU.

Muhubiri/ Mtumishi yeyote aliyerudi nyuma na kusahau kusudi lake tayari anageuka kuwa nabii wa uongo, kumbuka pia, biblia inapotaja nabii wa uongo, haimaanishi tu mtu Yule mwenye karama ya kinabii, hapana! Bali neno hilo ni neno la kiujumla linaloweza kumaanisha aidha Mwalimu wa uongo, au mchungaji wa uongo, au mtume wa uongo, au muinjilisti wa uongo, au hata muimbaji wa uongo, wote hao ni manabii wa uongo kibiblia.

Leo tutajifunza tabia kuu tatu za wahubiri waliorudi nyuma. Ambapo tukizijua tabia hizo zitatusaidia kujihadhari na upotevu wao.

 1. Tabia ya kwanza, huwa hawahubiri na wala hawapendi kuhubiri kuwa hizi ni siku za Mwisho,

2. Tabia ya pili, wanashambulia watumishi wanaohubiri kuhusu siku za mwisho.

3. Tabia ya tatu, ni watu wa kupenda anasa, aidha kwa siri au kwa wazi.

Hizo ndio tabia kuu tatu za manabii, waalimu, wainjilisti, au wachungaji waliorudi nyuma na kugeuka kuwa wa uongo! ambapo kitambo sana walishaliacha kusudi la Mungu na kufuata mambo yao.

Sasa hebu tusome mfano ufuatao ambao Bwana Yesu aliutoa, kuhusu watumishi waliorudi nyuma.

Mathayo 24:44 “Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

45  Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46  Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47  Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

48  Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

49  akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;

50  bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51  atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Bwana alitoa mfano huo kwa wanafunzi wake tu!..na kwa makutano yote.. Akimaanisha kuwa unawahusu mitume tu! Na wote ambao wameitwa katika kuifanya kazi ya kulisha kondoo wa Mungu. Huu ni tofauti na ule mfano wa mpanzi, ambao Bwana aliwaambia watu wote, (yaani makutano pamoja na wanafunzi), lakini mfano huu aliwatenga wanafunzi wake na kuwaambia wao peke yao. Na katika mfano huo alilinganisha utumishi aliowapa wa kwenda kuhubiri na utumishi wa mtu aliyeajiri wafanyakazi katika nyumba yake. Ambapo hiyo nyumba inaonekana ni kubwa mfano wa kasri ambayo ina watu wengi (wageni pamoja na wenyeji) vile vile ina wafanyakazi wengi tofauti tofauti, wapo wapishi, wapo wanaofua nguo, wapo walinzi, wapo wanaofanya usafi n.k

Lakini katika huo mfano tunaona mwenye nyumba ni kama alisafiri, na akawaachia majukumu kila mfanyakazi, na hakuwaambia ni lini atarudi, Hivyo kila mfanyakazi kwa nafasi yake alipaswa afanye kwa uaminifu, kwasababu hajui ni lini Bwana wake atakuja. Lakini akatokea mtumwa mmoja miongoni mwao, ambaye kazi yake ilikuwa ni ya upishi, ambapo aliachiwa posho ya kutosha ya kununua chakula apikie watu wa ile nyumba wale kila siku washibe, lakini kinyume chake alipoona Bwana wake anachelewa, alikengeuka na kuanza kuwazuilia chakula watu wa pale nyumbani, lakini haikuishia hapo akaanza kuwapiga wajoli wake, Neno mjoli maana yake ni “mfanyakazi-mwenza”.. yaani mtu anayefanya kazi pamoja na wewe anaitwa “mjoli wako”.

Kwahiyo huyu mpishi akaanza kuwapiga wale wafanyakazi wengine, pengine wale waliokuwa walinzi, au wanaofanya usafi n.k. Na mpaka mtu afikie hatua ya kuwapiga wafanyakazi wenzake maana yake ni kwamba tayari kuna vitu wale wenzake wanafanya ambavyo hakubaliani navyo. Maana yake wenzake ni waaminifu katika kazi zao lakini yeye si mwaminifu ndio maana anagombana nao, na hata kufikia kuwapiga.

Maana yake ni nini mfano huo?

Ukiona mtumishi kasahau Ono la Msingi la kwamba BWANA WAKE ANARUDI SIKU YOYOTE, na kugeukia mambo mengine. Tambua kwamba hiyo ndio dalili ya kwanza ya Mtumishi aliyerudi nyuma.

> Ukiona hakubaliani na kwamba Kristo wakati wowote anarudi, badala yake anahubiri na kuishi maisha kana kwamba Kristo atarudi miaka elfu5 mbele…Jitenge naye! Kwasababu Kitambo sana kashaliacha kusudi lake, na hivyo atakupoteza.

> Ukiona hakukumbushi kwamba siku yoyote kuanzia muda huu parapanda italia, kimbia! Jiokoe nafsi yako.

> Ukiona anakuhubiria vitu vya kidunia tu!..njoo upate mke, njoo upate nyumba, gari, mali.. na wala hakwambii kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na dalili zote za kurudi kwake zimetimia.. Jiokoe nafsi yako ndugu!

2. Tabia ya pili: Ukiona anawapiga wajoli wake (yaani wale watumishi wanaosimamia kweli) jihadhari naye. Utauliza anawapigaje?..Anawapiga kwa kuwarushia maneno!!, na kuwadharau. Na ni kwanini anafanya hivyo?.. ni kwasababu ameona wamekuwa waaminifu katika nafasi zao na yeye kashatoka kwenye mstari kitambo, hivyo atakapoona wengine wanahubiri kwa nguvu kwamba Kristo yupo mlangoni, atakwenda kinyume nao kwa nguvu!.. kwasababu yeye bado anatamani udunia. Hiyo ni dalili ya pili.

> Hivyo ukiona anashambulia sana mahubiri au wahubiri wanaohubiri kuhusu kurudi kwa Yesu. Jihadhari na huyo mtumishi. Ukiona anakuambia Yesu harudi leo wala kesho, hivyo endelea na maisha yako kama kawaida, jiokoe nafsi yako!.

3. Na tabia ya tatu na ya mwisho: Ni watu wa kupenda anasa. Katika huo mfano utaona anasema “anaacha kwenda kugawa chakula, anakula na kunywa na walevi”

> Ukiona mhubiri anapenda kusifia sifia vitu vya kiulimwengu kama magari, nyumba, mavazi, umaarufu, mwonekano, hiyo ni dalili mojawapo ya kwamba ni mtu wa anasa. Anaweza asikiri kwa kinywa lakini maisha yake ya siri ni ya anasa. Na mahubiri yake yatakuwa ni ya kutukuza mambo hayo hayo tu!.. Atakuwa anafanya juu chini ili awe maarufu, ili awe na mali nyingi, atabadilisha mpaka mtindo wa mahubiri ilimradi tu akusanye fedha, na umaarufu kutoka kwa watu. Ukiona hiyo dalili, jihadhari kwasababu tayari kasharudi nyuma. Kashaliacha kusudi aliloitiwa.

Lakini Bwana alisema maneno haya..

Mathayo 24:50 “bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51  atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Hapo Bwana anaanza kwa kusema “atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua”. Ndugu hao manabii na watumishi wanaokuhubiria kuwa Kristo harudi, wala haji leo wala kesho!!.. Kristo kasema mwenyewe atakuja siku wasiyoidhania… wakati wanadhani ndio wakati wa kujiongezea mali, ghafla Kristo atatokea, na atawakata vipande viwili. Je! Wewe unayewategemea hao utakuwa wapi siku hiyo???. Geuka! Mtazame Kristo yupo mlangoni kurudi, achana na wahubiri hao waliorudi nyuma, hawana tumaini lolote, siku yao itakuja ghafla na Kristo atawahukumu.

Na tena anasema atawakata vipande viwili: Kwanini viwili na si kumi?..na kwasababu wanajifanya kutumika upande wa Bwana na wakati huo huo wanazitumikia tamaa zao (wanatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja), hivyo zamani, adhabu ya mtu anayekamatwa anatumikia falme mbili kwa wakati mmoja ilikuwa ni kukatwa vipande viwili, kwasababu ni mnafiki na msaliti. Hivyo na Bwana atawakata vipande viwili watumishi wote wanaotumikia tumbo na huku wanasimama kuhubiri, atawakata vipande viwili wahubiri wote wanaodharau ujio wake.

Ndugu hizi ni nyakati za mwisho, Yesu anarudi, kizazi tunachoishi ni kizazi cha hatari kuliko vyote, kwasababu dalili zote za kurudi kwake zimeshatimia, Ugonjwa uliosambaa sasa ujulikanao kama corona ni mojawapo ya Tauni zilizotabiriwa kutokea kipindi kifupi kabla ya kurudi kwa Yesu mara ya pili (Soma Luka 21:11), na zaidi ya yote, Israeli imeshakuwa Taifa, wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36  nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

37  Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia”

Kama hujampokea Yesu, wakati wako ndio sasa na si kesho, hapo ulipo piga magoti, kisha omba rehema kwa Bwana Yesu, naye atakusamehe..na pia acha maovu yote uliyokuwa unayafanya kwa vitendo, kama ulikuwa unatazama filamu za kidunia unaacha na kuzifuta kwenye kifaa chako, kama ulikuwa unazini na kufanya uasherati unaacha kwa vitendo, kama ni binti ulikuwa unavaa vibaya, ikiwemo nguo zinazobana na suruali, na kama ulikuwa unapaka wanja, na kuvaa wigi, hereni, na kujichubua,na mambo mengine yote yanayofanana na hayo ya kidunia unayaacha, na unabeba msalaba wako unamfuata Yesu. Na baada ya hapo, bila kukawia tafuta ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu, kwaajili ya ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38).

Na kama ukifanya hayo yote  kwa Imani, Roho Mtakatifu atakuthibitisha kwa kukupa amani, na furaha isiyoelezeka, na pia atakupa uwezo wa kuushinda ulimwengu, na atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Muhubiri/ Mtumishi yeyote aliyerudi nyuma na kusahau kusudi lake tayari anageuka kuwa nabii wa uongo, kumbuka pia, biblia inapotaja nabii wa uongo, haimaanishi tu mtu Yule mwenye karama ya kinabii, hapana! Bali neno hilo ni neno la kiujumla linaloweza kumaanisha aidha Mwalimu wa uongo, au mchungaji wa uongo, au mtume wa uongo, au muinjilisti wa uongo, au hata muimbaji wa uongo, wote hao ni manabii wa uongo kibiblia.

Leo tutajifunza tabia kuu tatu za wahubiri waliorudi nyuma. Ambapo tukizijua tabia hizo zitatusaidia kujihadhari na upotevu wao.

 1. Tabia ya kwanza, huwa hawahubiri na wala hawapendi kuhubiri kuwa hizi ni siku za Mwisho,

2. Tabia ya pili, wanashambulia watumishi wanaohubiri kuhusu siku za mwisho.

3. Tabia ya tatu, ni watu wa kupenda anasa, aidha kwa siri au kwa wazi.

Hizo ndio tabia kuu tatu za manabii, waalimu, wainjilisti, au wachungaji waliorudi nyuma na kugeuka kuwa wa uongo! ambapo kitambo sana walishaliacha kusudi la Mungu na kufuata mambo yao.

Sasa hebu tusome mfano ufuatao ambao Bwana Yesu aliutoa, kuhusu watumishi waliorudi nyuma.

Mathayo 24:44 “Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

45  Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46  Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47  Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

48  Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

49  akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;

50  bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51  atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Bwana alitoa mfano huo kwa wanafunzi wake tu!..na kwa makutano yote.. Akimaanisha kuwa unawahusu mitume tu! Na wote ambao wameitwa katika kuifanya kazi ya kulisha kondoo wa Mungu. Huu ni tofauti na ule mfano wa mpanzi, ambao Bwana aliwaambia watu wote, (yaani makutano pamoja na wanafunzi), lakini mfano huu aliwatenga wanafunzi wake na kuwaambia wao peke yao. Na katika mfano huo alilinganisha utumishi aliowapa wa kwenda kuhubiri na utumishi wa mtu aliyeajiri wafanyakazi katika nyumba yake. Ambapo hiyo nyumba inaonekana ni kubwa mfano wa kasri ambayo ina watu wengi (wageni pamoja na wenyeji) vile vile ina wafanyakazi wengi tofauti tofauti, wapo wapishi, wapo wanaofua nguo, wapo walinzi, wapo wanaofanya usafi n.k

Lakini katika huo mfano tunaona mwenye nyumba ni kama alisafiri, na akawaachia majukumu kila mfanyakazi, na hakuwaambia ni lini atarudi, Hivyo kila mfanyakazi kwa nafasi yake alipaswa afanye kwa uaminifu, kwasababu hajui ni lini Bwana wake atakuja. Lakini akatokea mtumwa mmoja miongoni mwao, ambaye kazi yake ilikuwa ni ya upishi, ambapo aliachiwa posho ya kutosha ya kununua chakula apikie watu wa ile nyumba wale kila siku washibe, lakini kinyume chake alipoona Bwana wake anachelewa, alikengeuka na kuanza kuwazuilia chakula watu wa pale nyumbani, lakini haikuishia hapo akaanza kuwapiga wajoli wake, Neno mjoli maana yake ni “mfanyakazi-mwenza”.. yaani mtu anayefanya kazi pamoja na wewe anaitwa “mjoli wako”.

Kwahiyo huyu mpishi akaanza kuwapiga wale wafanyakazi wengine, pengine wale waliokuwa walinzi, au wanaofanya usafi n.k. Na mpaka mtu afikie hatua ya kuwapiga wafanyakazi wenzake maana yake ni kwamba tayari kuna vitu wale wenzake wanafanya ambavyo hakubaliani navyo. Maana yake wenzake ni waaminifu katika kazi zao lakini yeye si mwaminifu ndio maana anagombana nao, na hata kufikia kuwapiga.

Maana yake ni nini mfano huo?

Ukiona mtumishi kasahau Ono la Msingi la kwamba BWANA WAKE ANARUDI SIKU YOYOTE, na kugeukia mambo mengine. Tambua kwamba hiyo ndio dalili ya kwanza ya Mtumishi aliyerudi nyuma.

> Ukiona hakubaliani na kwamba Kristo wakati wowote anarudi, badala yake anahubiri na kuishi maisha kana kwamba Kristo atarudi miaka elfu5 mbele…Jitenge naye! Kwasababu Kitambo sana kashaliacha kusudi lake, na hivyo atakupoteza.

> Ukiona hakukumbushi kwamba siku yoyote kuanzia muda huu parapanda italia, kimbia! Jiokoe nafsi yako.

> Ukiona anakuhubiria vitu vya kidunia tu!..njoo upate mke, njoo upate nyumba, gari, mali.. na wala hakwambii kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na dalili zote za kurudi kwake zimetimia.. Jiokoe nafsi yako ndugu!

2. Tabia ya pili: Ukiona anawapiga wajoli wake (yaani wale watumishi wanaosimamia kweli) jihadhari naye. Utauliza anawapigaje?..Anawapiga kwa kuwarushia maneno!!, na kuwadharau. Na ni kwanini anafanya hivyo?.. ni kwasababu ameona wamekuwa waaminifu katika nafasi zao na yeye kashatoka kwenye mstari kitambo, hivyo atakapoona wengine wanahubiri kwa nguvu kwamba Kristo yupo mlangoni, atakwenda kinyume nao kwa nguvu!.. kwasababu yeye bado anatamani udunia. Hiyo ni dalili ya pili.

> Hivyo ukiona anashambulia sana mahubiri au wahubiri wanaohubiri kuhusu kurudi kwa Yesu. Jihadhari na huyo mtumishi. Ukiona anakuambia Yesu harudi leo wala kesho, hivyo endelea na maisha yako kama kawaida, jiokoe nafsi yako!.

3. Na tabia ya tatu na ya mwisho: Ni watu wa kupenda anasa. Katika huo mfano utaona anasema “anaacha kwenda kugawa chakula, anakula na kunywa na walevi”

> Ukiona mhubiri anapenda kusifia sifia vitu vya kiulimwengu kama magari, nyumba, mavazi, umaarufu, mwonekano, hiyo ni dalili mojawapo ya kwamba ni mtu wa anasa. Anaweza asikiri kwa kinywa lakini maisha yake ya siri ni ya anasa. Na mahubiri yake yatakuwa ni ya kutukuza mambo hayo hayo tu!.. Atakuwa anafanya juu chini ili awe maarufu, ili awe na mali nyingi, atabadilisha mpaka mtindo wa mahubiri ilimradi tu akusanye fedha, na umaarufu kutoka kwa watu. Ukiona hiyo dalili, jihadhari kwasababu tayari kasharudi nyuma. Kashaliacha kusudi aliloitiwa.

Lakini Bwana alisema maneno haya..

Mathayo 24:50 “bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51  atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Hapo Bwana anaanza kwa kusema “atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua”. Ndugu hao manabii na watumishi wanaokuhubiria kuwa Kristo harudi, wala haji leo wala kesho!!.. Kristo kasema mwenyewe atakuja siku wasiyoidhania… wakati wanadhani ndio wakati wa kujiongezea mali, ghafla Kristo atatokea, na atawakata vipande viwili. Je! Wewe unayewategemea hao utakuwa wapi siku hiyo???. Geuka! Mtazame Kristo yupo mlangoni kurudi, achana na wahubiri hao waliorudi nyuma, hawana tumaini lolote, siku yao itakuja ghafla na Kristo atawahukumu.

Na tena anasema atawakata vipande viwili: Kwanini viwili na si kumi?..na kwasababu wanajifanya kutumika upande wa Bwana na wakati huo huo wanazitumikia tamaa zao (wanatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja), hivyo zamani, adhabu ya mtu anayekamatwa anatumikia falme mbili kwa wakati mmoja ilikuwa ni kukatwa vipande viwili, kwasababu ni mnafiki na msaliti. Hivyo na Bwana atawakata vipande viwili watumishi wote wanaotumikia tumbo na huku wanasimama kuhubiri, atawakata vipande viwili wahubiri wote wanaodharau ujio wake.

Ndugu hizi ni nyakati za mwisho, Yesu anarudi, kizazi tunachoishi ni kizazi cha hatari kuliko vyote, kwasababu dalili zote za kurudi kwake zimeshatimia, Ugonjwa uliosambaa sasa ujulikanao kama corona ni mojawapo ya Tauni zilizotabiriwa kutokea kipindi kifupi kabla ya kurudi kwa Yesu mara ya pili (Soma Luka 21:11), na zaidi ya yote, Israeli imeshakuwa Taifa, wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36  nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

37  Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia”

Kama hujampokea Yesu, wakati wako ndio sasa na si kesho, hapo ulipo piga magoti, kisha omba rehema kwa Bwana Yesu, naye atakusamehe..na pia acha maovu yote uliyokuwa unayafanya kwa vitendo, kama ulikuwa unatazama filamu za kidunia unaacha na kuzifuta kwenye kifaa chako, kama ulikuwa unazini na kufanya uasherati unaacha kwa vitendo, kama ni binti ulikuwa unavaa vibaya, ikiwemo nguo zinazobana na suruali, na kama ulikuwa unapaka wanja, na kuvaa wigi, hereni, na kujichubua,na mambo mengine yote yanayofanana na hayo ya kidunia unayaacha, na unabeba msalaba wako unamfuata Yesu. Na baada ya hapo, bila kukawia tafuta ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu, kwaajili ya ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38).

Na kama ukifanya hayo yote  kwa Imani, Roho Mtakatifu atakuthibitisha kwa kukupa amani, na furaha isiyoelezeka, na pia atakupa uwezo wa kuushinda ulimwengu, na atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Gidamu ni nini? Kwanini Yohana alisema hastahili kuzilegeza gidamu za Yesu?

SWALI: Kwanini Yohana alisema hastahili kulegeza gidamu ya viatu vya Yesu, gidamu ni nini?

Gidamu ni mikanda maalumu ya viatu,

Viatu vya zamani vilikuwa havina muonekano kama tulionao sasa hivi, ambao vingi vinatengenezwa kwa muundo wa kutumbukiza tu mguu,, vya zamani vilikuwa zinashikiliwa na mikanda maalumu, au kamba maalumu, ambazo zinazungushwa kwenye miguu, ili kuwezesha kiatu kisitoke, sasa hiyo mikanda ndio inayoitwa Gidamu. tazama picha juu..

Neno hilo utalipata kwenye vifungu hivi;

Marko 1:7 “Akahubiri akisema, Yuaja nyuma yangu aliye na nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuinama na kuilegeza gidamu ya viatu vyake.

8 Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu”.

Luka 3:16 “Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto”;

Mathayo 3.11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto”.

Tukirudi kwenye swali kwanini Yohana Mbatizaji alisema hastahili kulegeza gidamu ya viatu Yesu?

Zamani na hata sasa kazi ya kufunga na kufungua mikanda/kamba za viatu ni kazi zinazofanywa na watumwa wa chini sana,  Wanachofanya ni kumwandalia bwana wao viatu, kisha kumvisha, na baadaye kuwavua tena pindi watakaporudi kutoka katika mihangaiko yao, na kuvichukua viatu hivyo mpaka sehemu ya usafi na kuhakikisha  wanaviosha, vinakuwa maridadi, kisha wanarudi kuwavisha tena bwana zao, hiyo ndio inakuwa ni kazi yao muda wote, siku zote.

Kwa desturi wa wayahudi kazi kama hii haikufanywa na mtumwa wowote wa kiyahudi, kwasababu ni kazi nyonge, dhaifu na ya kudharaulika, ilikuwa inafanywa na wakaanani tu(Watu wa mataifa mengine waliokuwa wanaishi Israeli wakati ule).

Sasa Yohana kusema hastahili kulegeza hata gidamu ya viatu vya Yesu, ni kuonyesha kutostahili kwake, kuifanya hata ile kazi ndogo sana ya Yesu Kristo, kwasababu Kristo ni mkuu kupita kiasi. Hivyo hata ile kazi inayoonekana ni ya kudharaulika sana kwake ni kubwa sana, kiasi cha kumfanya ajione hastahili kuifanya. Huo ni unyenyekevu wa hali ya juu sana na hofu aliyokuwa nayo Yohana kwa ajili ya Bwana wake Yesu Kristo.

Na matokeo yake, hatushangai ni kwanini Bwana Yesu alimfanya kuwa mtangulizi wake, na zaidi ya yote akamshuhudia kuwa katika uzao wa wanawake hakuwahi kutokea mtu aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni kuliko yeye. Hiyo yote ni kwasababu aliithamini sana hata ule wito mdogo sana wa Bwana Yesu.

Je na sisi tunaweza kuwa kama Yohana mbatizaji?..Kama tutashindwa kupiga deki kanisa la Bwana, au kuosha choo,  tutawezaje, kufanywa watangulizi wake..Tutawezaje kuonyeshwa siri za ndani za ufalme wa mbinguni kama alivyoonyeshwa Yohana, kama tutazidharau hata zile kazi zake ndogo.

 Thamini Gidamu za Yesu!

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya lijamu na hatamu ni ipi kibiblia?

Mtu mwenye “kitango” ni mtu wa namna gani kibiblia?

UFUNUO: Mlango wa 1

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Israeli wote wataokolewa siku ya mwisho kulingana na Warumi 11:26?

Jibu: Tusome,

Warumi 11:25 “ Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”

Ni kweli upo unabii wa Israeli wote kuokolewa katika siku za mwisho, kuna kipindi ambacho injili itahamia katika Taifa la Israeli baada ya unyakuo kupita!..wakati huo kanisa la mataifa litakuwa limeshanyakuliwa, Ndipo injili itaanza kuhubiriwa tena katika Taifa la Israeli na wale manabii wawili tunaowasoma katika kitabu cha Ufunuo 11, watahubiri kama nyakati za Yohana Mbatizaji isipokuwa zama hizo itakuwa ni kwa ishara nyingi na miujiza mfano wa ile ya Musa na Eliya.

Na kupitia injili ya hao manabii wawili, waisraeli wengi watamkubali Yesu kama Masihi, kumbuka kwasasa wayahudi wengi (yaani waisraeli wengi), hawaamini kuwa Yesu Yule aliyekuja na kufa na kufufuka kuwa ndiye Masihi aliyetabiriwa na manabii zamani, wanaamini kuwa Masihi bado hajaja, na Yesu sio Masihi, hivyo wanamsubiria mwingine!!..Biblia inasema macho yao yamefumbwa wasimtambue Yesu kuwa ndiye Masihi, ili sisi watu wa mataifa tupate neema. (Warumi 11:30-31).

Sasa swali la Msingi hapo, ni je Israeli wote wataokolewa?..hata kama ni watenda maovu?..na je kitendo tu cha kuzaliwa  Muisraeli tayari umeshapewa tiketi ya kuurithi uzima  wa milele?.

Jibu ni La!… Sio wote watakaookolewa, kwasababu wapo waisraeli wasioamini kabisa hata kama Mungu yupo, wapo wachawi na manabii wa uongo katikati ya jamii za Israeli mfano wa akina Bar-Yesu (Matendo 13:6), hao hawataokolewa na wataenda katika ziwa la moto, kama hawatatubu!..

Sasa kwanini hapo biblia iseme ni  “Israeli wote”, na si baadhi!.. kama watakuwepo baadhi ambao hawataokolewa?, kwanini iseme wote?.. Ili kuelewa vyema tusome mstari ufuatao.

Warumi 9:6  “Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka. MAANA HAWAWI WOTE WAISRAELI WALIO WA UZAO WA ISRAELI.

7  Wala hawawi wote wana kwa kuwa wazao wa Ibrahimu, bali, Katika Isaka wazao wako wataitwa; ”

Unaona hapo?.. Sio Waisraeli wote ni waisraeli, ni sawa na kusema “Si wote wanaojiita au wanaojulikana kuwa ni wakristo ni wakristo”. Sasa hivi duniani kuna zaidi ya mabilioni ya wakristo. Lakini kiuhalisia “Wakristo wa kweli ni wachache”, ni wale wanaozishika amri za Mungu na kufanya mapenzi yake, hao wengine ni wakristo jina tu!. Kwahiyo kwenye biblia kungekuwa na mstari unaosema “wakristo wote wataokolewa” bila shaka, ingekuwa imemaanisha “wale wakristo wa kweli” na si wakristo jina!.. mtu anayejiita mkristo lakini mchawi, hawezi kuurithi uzima wa milele, mtu anayejiita mkristo lakini ni mzinzi vivyo hivyo!

Kadhalika biblia iliposema “Israeli wote wataokolewa” ilimaanisha wale “wale waisraeli kweli kweli” ambao wanakwenda katika sheria za Mungu bila kupinda panda. Hao ndio wote watakaookolewa. Mfano wa hao ni wakina Nathanieli katika Yohana 1:47 “Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, MWISRAELI KWELI KWELI, hamna hila ndani yake”

 Lakini wengine wasiompenda Mungu, maana yake ni waisraeli jina tu!, Lakini sio waisraeli hasa!!, hao hawataokolewa, Ndicho Mtume Paulo alichokuwa anakimaanisha hapo katika Warumi 9:6 kuwa “….HAWAWI WOTE WAISRAELI WALIO WA UZAO WA ISRAELI”.

Vivyo hivyo hawawi wote wakristo, walio wa uzao Kristo!!. Walio uzao wa Kristo ni wale waliozaliwa mara ya pili, hao ndio Wakristo, wengine ni wakristo jina tu!..

Je wewe ni Mkristo halisi au mkristo jina tu!.. Mkristo jina ni Yule anayekwenda kanisani lakini anafanya uzinzi kwa siri, ni yule mwenye jina la kikristo lakini ni mtu wa kidunia, mkristo jina ni Yule anayeupenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu, mkristo jina ni yule asiyechukua msalaba wake na kumfuata Yesu. Lakini mkristo kweli kweli ni Yule aliyeukataa ulimwengu, anayejitwika msalaba wake kila siku na kumfuata Yesu kwa gharama zozote.

Bwana atusaidie tuwe wakristo halisi!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

AINA TATU ZA WAKRISTO.

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

Rudi nyumbani

Print this post

Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Ayari ni mtu aliyekosa utu,  mchoyo  na asiyejali watu,  anayejipenda mwenyewe, na mwenye hasira nyingi na madanganyifu. Kwa ufupi ni mtu asiyependa watu kwa ujumla.

Mfano wa watu hawa katika biblia ni Nabali, ambaye pamoja na kwamba Daudi na wenzake walimfanyia wema mwingi, hakujali kuwastahi hata kwa maji au kwa chakula (1Samweli 25).. na mwingine ni yule Tajiri wa Lazaro ambaye aliishi hapa duniani katika maisha ya anasa na ya ubinafsi, akafa katika dhambi zake, akaenda kuzimu.(Luka 16)

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia;

Isaya 32:5 “Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, WALA AYARI HATASEMWA KWAMBA NI KARIMU.

6 Maana mpumbavu atanena yaliyo upumbavu, na moyo wake utafanya maovu, ili kutenda hila na kusema yasiyo kweli juu ya Bwana, ili kuziacha nafsi za watu wenye njaa hazina kitu, na kukikomesha kinywaji chake mwenye kiu.

7 Tena VYOMBO VYAKE AYARI NI VIBAYA; hutunga hila mbaya, ili kuwaangamiza wanyonge kwa maneno ya uongo, mtu mhitaji ajaposema maneno yenye haki.

8 Bali mwungwana huwaza mambo ya kiungwana, naye hushika sana mambo ya kiungwana”.

Kwa mfano katika habari hiyo, kama ukianzia  mistari ya juu mstari wa kwanza utapata picha kamili ni nini kilikuwa kinazungumziwa,  anasema..

Isaya 32:1 Tazama, mfalme atamiliki kwa haki, na wakuu watatawala kwa hukumu.

Huo ni unabii unaomzungumzia Kristo katika utawala wake wa amani utaokuja huko mbeleni, kwasababu yeye ndiye atakayemiliki kama mfalme, Na katika huo utawala wake, hakutakuwa na kupindisha haki, kama ilivyo sasahivi, kwa sasahivi fisadi ndio anaonekana mwerevu, Mtu mbinafsi, ndiye anayeonekana  ana akili. Wapumbavu ndio wanaopewa uongozi, mtoa rushwa ndiye anayeonekana  ni mkarimu, Ayari (mtu asiyependa watu) ndio anayehesheshimika na kuogopeka katika jamii n.k.

Lakini katika huo utawala wa Amani wa miaka 1000 wa Yesu Kristo hapa duniani, hilo jambo halitakuwepo,  anasema..

“Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, wala AYARI hatasemwa kwamba ni karimu”.

Hii ikiwa na maana kuwa watenda haki ndio watasifika katika haki yao, bali watendao uovu, watakutana na fimbo ya chuma ya Yesu Kristo, (Ufunuo 2:27).

Fahamu kuwa, kwa Mungu hakuna upendeleo, hata leo hii ikiwa utakufa katika hali yako ya dhambi, hakuna nafasi ya pili, kama umestahili mbingu, utakwenda mbinguni, kama umestahili Jehanum, utakwenda Jehanum, nafasi ya kutubu ipo leo, haipo baada ya kufa, hivyo mgeukie Yesu Kristo ayaokoe Maisha yako. Kwasababu hizi ni siku za mwisho.. Wakati ambao mtu kufanya dhambi ndio anasifiwa.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

Mafundisho

Rudi nyumbani

Print this post

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tuyatafakari maandiko pamoja.

Je Bwana Yesu ni Mfalme katika maisha yako?..Kama una tabia zifuatazo, hajawa bado Mfalme kwako, haijalishi utamkiri kiasi gani.

Kama unamtafuta kwaajili ya faida zako za kimwili, ikiwemo kupata mali, kupata mke, kupata mume, kupata kupata watoto, kupata umaarufu, na mambo mengine yote ya kimwilini , Tambua kuwa yeye si mfalme kwako, haijalishi utamtangaza kwa watu kuwa ni mfalme kwako, lakini yeye hakujui!!.

Utauliza tunasoma wapi katika maandiko?.. Hebu tukitafakari kisa kifuatacho kwa ufupi kisha tutapata majibu…

Yohana 6:10  “Yesu akasema, Waketisheni watu. Na mahali pale palikuwa na majani tele. Basi watu waume wakaketi, wapata elfu tano jumla yao.

.11  Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka.

12  Nao waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kisipotee cho chote.

13  Basi wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili, vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyowabakia wale waliokula.

14  Basi watu wale, walipoiona ishara aliyoifanya, walisema, Hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni.

15  Kisha YESU, HALI AKITAMBUA YA KUWA WALITAKA KUJA KUMSHIKA ILI WAMFANYE MFALME, AKAJITENGA, AKAENDA TENA MLIMANI YEYE PEKE YAKE”.

Hebu jiulize, kwani! Bwana Yesu, hataki au hapendi kuitwa Mfalme??.. Hata hivyo ndicho anachokitengeneza sasa, anatengeneza ufalme wake, na yeye ndiye atakuwa Mfalme wa wafalme. Lakini hapa tunaona anaukataa na kuukimbia ufalme??..Ni kwanini?..Jibu ni rahisi, ni kwasababu yeye hatengenezi wala hatafuti ufalme wa kidunia.

Yohana 18:33  “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?

34  Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?

35  Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?

36  Yesu akajibu, UFALME WANGU SIO WA ULIMWENGU HUU. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa”

Hiyo ndio sababu aliwakimbia wale makutano waliotaka kumfanya awe mfalme wao… Waliona wakimpata atawasaidia kujenga miji yao, atawasaidia kunyanyua uchumi wa nchi yao, atawasaidia kupata fedha nyingi, atawasaidia kutokomeza umasikini.  Lakini Yesu aliwakimbia… na walimtafuta kwa bidii na walipompata sehemu nyingine aliwaambia maneno yafuatayo..

Yohana 6:24  “Basi mkutano, walipoona ya kuwa Yesu hayuko huko wala wanafunzi wake, waliingia mashuani wenyewe, wakaenda Kapernaumu wakimtafuta Yesu.

25  Hata walipomwona ng’ambo ya bahari, walimwambia, Rabi, wewe umekuja lini hapa?

26  Yesu akawajibu, akasema, AMIN, AMIN, NAWAAMBIENI, NINYI MNANITAFUTA, SI KWA SABABU MLIONA ISHARA, BALI KWA SABABU MLIKULA ILE MIKATE MKASHIBA.

27  Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa muhuri na Baba, yaani, Mungu”.

Na jitihada zao zote za kumtafuta awe mfalme, hata hakuwa mfalme wao, Yesu aliwaepuka. Kilichowatokea wale ndicho kinachotutokea kanisa la sasa. Biblia inasema…

Waebrania 13:8  “YESU KRISTO NI YEYE YULE, JANA NA LEO NA HATA MILELE.

9  Msichukuliwe na mafundisho ya namna nyingine nyingine, na ya kigeni; maana ni vizuri moyo ufanywe imara kwa neema, wala si kwa vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida”.

 Ndugu Bwana Yesu hajabadilika kama watu wanavyombadilisha sasa, Ni yeye Yule, jana, na leo na hata milele!!!…maana yake tabia zako ni zile zile hazijabadilika, kama aliwakimbia wale makutano, waliotaka kumfanya mfalme wao, atatukimbia na sisi pia vile vile, kama tukimwendea kwa mtindo ule.

Kama Bwana Yesu atawakana siku ile watu waliotoa pepo kwa jina lake, na huku mioyo yao ipo mbali naye??..si zaidi wewe aliyekupa mali leo na bado ni mlevi?. Hao amewapa uwezo wa kutoa pepo lakini kawakana mwisho wa siku?..jiulize wewe uliyepewa nyumba na gari na tumbo lako kufunguliwa na bado unavaa kidunia, jiulize utasilimika vipi siku ile?, wewe uliyeponywa kimiujiza na bado hutaki kujikana nafsi yako na kumfuata Yesu, utasalimika vipi?, wewe uliyeponywa ugonjwa kimiujiza na bado hutaki kuuacha ulimwengu, jiulize utasalimikaje siku ile?..

Unadhani Bwana kukupa wewe mali, au mtoto, au kukuponya ugonjwa wako uliokuwa sugu, ndio kitu cha kwanza anachokitafuta kwako??..lengo la kukufanyia hayo ni ili tu ugeuke! Utubu na uwe mkamilifu kama yeye na si kwa lengo lingine. Ukitafsiri kwamba Bwana kakuponya ugonjwa wako kwasababu anapendezwa na wewe..fahamu kuwa umepotea!..Ukitafsiri kuwa Bwana kaifanikisha biashara yako kwasababu eti anataka uwe bilionea, fahamu kuwa umepotea!!.. Ameifanikisha hiyo biashara yako kusudi kwamba utubu na umrudie yeye, uwe mkamilifu. Lakini ukidhani kuwa ni kwasababu amependezwa na wewe, na moyoni ukijitumainisha kwamba ni mfalme wako, na Bwana wako, siku ile atakukana, pamoja na kwamba ni yeye ndiye aliyekufanikisha!!

Kama hujampokea Yesu maishani,  mlango wa neema bado upo wazi, ingawa hautakuwa hivyo siku zote. Huu ni wakati wako wa kumpokea Yesu, kwa kumwamini moyoni mwako, na kukiri kwa kinywa chako, na kuamua kwa dhati kuacha dhambi zote ulizokuwa unazifanya.. Unaziacha kwa vitendo, kama ulikuwa ni mlevi unavunja vikao na makundi yote ya ulevi, kama ulikuwa ni kahaba, unachoma nguo zote za kikahaba ulizokuwa unavaa ikiwemo suruali zote, na lipstick, wanja na mengineyo, kama ulikuwa unasikiliza miziki ya kidunia unaifuta yote katika simu yako, au popote pale ulipoihifadhi, kama ulikuwa ni shabiki wa mambo ya kidunia kama mipira, filamu, na mambo yanayofanana na hayo, unayaacha yote.

Na baada ya kufanya hivyo unatafuta ubatizo sahihi, kama bado hujabatizwa, kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji tele, na kwa jina la Yesu Kristo, na baada ya hapo Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, ambaye atakuongoza katika kuijua kweli yote ya maandiko, na kukusaidia kuushinda ulimwengu.

Bwana akubariki.

afadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post