Jibu: Kutakabari maana yake ni “kuwa na kiburi”…Na hicho kinaweza kuja kutokana na kujiamini sana, au kuwa na kitu fulani ambacho wengine hawana, na kujiona huhitaji kitu kingine chochote…Kutakabari huko kunazaa kujisifu au kujiona bora kuliko wengine, na kujiinua sana hata kudharau wengine au kumdharau Muumba.
Katika biblia tunaweza kuona mifano kadhaa ya watu waliotakabari..
Huyu alikuwa mtoto wa Mfalme Daudi, wakati Daudi alipokuwa mzee, alijiona yeye ni bora kuliko watoto wengine wote wa Daudi, hata pasipo kumshirikisha baba yake, akaenda kujitangaza kwa watu kuwa yeye ndiye mfalme, angali bado baba yake akiwa hai.
1Wafalme 1: 5 “Ndipo Adonia mwana wa Hagithi AKATAKABARI, akasema, Mimi nitakuwa mfalme. Akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, na watu hamsini wapige mbio mbele yake”.
Lakini tunaona badae hakupata hicho alichokuwa anakitafuta, na nafasi hiyo alipewa Sulemani.
Wana wa Israeli ilifika wakati walimwacha Mungu, na hata kufikia hatua ya kuwatukana na kuwadharau manabii wake, na kupelekea ghadhabu ya Mungu kumwagwa juu yao kwa kuuawa na baadhi yao kupelekwa Babeli utumwani.
2Nyakati 36:15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na KUYADHARAU MANENO YAKE, NA KUWACHEKA MANABİİ WAKE, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake”
Kutakabari huko kwa wana wa Israeli ndiko kukapelekea kuchukuliwa utumwani.
Nehemia 9: 29 “ukawashuhudia ili uwarudishe tena katika sheria yako; LAKINI WALITAKABARI, wasizisikilize amri zako, bali wakazihalifu hukumu zako, (ambazo mtu akizitenda ataishi katika hizo), nao wakayaondoa mabega yao, wakafanya shingo zao kuwa ngumu, wasitake kusikiliza”.
Yeremia 48: 29 “Tumesikia habari za kiburi cha Moabu; Ya kuwa ana kiburi kingi; Jeuri yake, na kiburi chake, na majivuno yake, Na jinsi ALIVYOTAKABARI moyoni mwake.
30 Najua ghadhabu yake, asema Bwana, ya kuwa si kitu; majisifu yake hayakutenda neno lo lote.
31 Kwa sababu hiyo nitampigia yowe Moabu, naam, nitapiga kelele kwa ajili ya Moabu yote; nitawaombolezea watu wa Kir-heresi”.
Na mfano wa wengine waliotakabari kupita kiasi ni Farao (soma Nehemia 9:10), Nebukadneza (Danieli 4:37) n.k
Madhara ya kutakabari.
Tukiwa watu wa kutakabari Tutaanguka kama walivyoanguka wana wa Israeli na wengine wote waliokuwa wakitakabari katika biblia..
Mithali 16: 18 “Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye KUTAKABARI hutangulia MAANGUKO”.
Bwana atusaidie tusiwe na roho ya kutakabari..bali tuwe wanyenyekevu kama Bwana wetu Yesu Kristo alivyokuwa..
Kama hujaokoka na ungependa kufanya hivyo leo..basi utakuwa umefanya uamuzi bora ambao hutaujutia maisha yako yote.. Fungua hapa kwa msaada wa sala ya Toba >> SALA YA TOBA
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?
Utauliza je! Shetani ana uwezo wa kuzuia majibu ya maombi?. Jibu ni ndio!.
Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa shetani kamwe hana uwezo wa kuzuia maombi kumfikia Mungu..Maombi yeyote yale mtu anayoomba, yanapanda juu kwa Mungu moja kwa moja..Lakini kitu pekee ambacho shetani anachoweza kufanya ni kuzuia majibu ya Maombi..
Tunaona jambo hili kipindi cha Nabii Danieli..
Danieli 10:12 “Ndipo akaniambia, Usiogope, Danielii; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi”
Mkuu wa Uajemi, biblia inayomzungumzia hapo, ni Pepo lililowekwa kuwa kuu juu ya ufalme wa Uajemi..Hivyo kazi zote za giza zilizokuwa zinaendelea katika Taifa hilo la uajemi zilikuwa zinaratibishwa na pepo hilo.
Lakini utasoma hapo, Tangu siku ile ya kwanza tu Danieli alipotia moyo wake ufahamu, (yaani maana yake alipoanza kufikiria mambo ya kuomba)..tayari mawazo hayo yalishamfikia Mungu kama maombi..Na tayari majibu yalishatolewa..lakini Malaika yule alipokuwa anarudisha majibu kwa Danieli alizuiliwa na pepo hilo la Uajemi.
Sasa hivyo ndio vita vinavyoendelea hata sasa.. Vita vya Malaika wanaotuhudumia dhidi ya majeshi ya mapepo..Na vita hivyo si vingine zaidi ya vile vya hoja!..
Maana yake ni kwamba..Bwana anapoachilia majibu ya wewe kupata jambo fulani..shetani anakimbilia kupeleka hoja za mashitaka dhidi yako.. Anamwambia Bwana huyu mtu hastahili kupokea hicho unachompa kwasababu ana tabia hii, hii na ile…jana tu katoka kuiba, juzi katoka kuzini na wala hajatubu…Na wewe neno lako linasema husikii maombi ya waovu!..iweje umsikie na kumpa huyo kitu hicho?..Na mashitaka mengine mengi, anayapeleka mbele za Mungu kuhusu wewe.. Sasa mashitaka hayo kama ni ya kweli, basi Mungu hana upendeleo, shetani anashinda dhidi yako…Hivyo malaika yule aliyepewa jukumu la kukuletea baraka zako, anakuwa hawezi kukufikishia kile ulichoomba kutokana na kwamba umeonekana hustahili kukipokea kile kitu, kutokana na mashitaka ya shetani..
Ndivyo biblia inavyosema..
1Petro 5: 8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa MSHITAKI WENU IBILISI, kama simba angurumaye, huzungukazunguka, akitafuta mtu ammeze”.
Hapo inasema “mshitaki wenu” na si “mshindani wenu”..Maana yake kazi yake kubwa ni kutushitaki.. Na pia biblia inazidi kutufundisha jambo hilo hilo katika…
Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, YEYE AWASHITAKIYE MBELE ZA MUNGU WETU, MCHANA NA USIKU ”
Hivyo ni muhimu kufahamu kila kitu KIOVU tunachokifanya ni POINT kubwa kwa shetani, kwa ajili ya kutuzuilia maombi yetu na baraka zetu siku za mbeleni.
Na sio tu mambo mabaya tunayofanya ni POINT kwa shetani, hata mazuri tunayofanya bado shetani hatachoka kutushitaki kupitia hayo hayo mazuri…ndicho kilichomtokea Danieli pamoja na Ayubu Mtumishi wa Mungu..
Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.
7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.
9 Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure?
10 Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.
11 Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.
12 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana”.
Unaona na hapo?..Ayubu anatenda mema lakini bado shetani hakuacha kumchochoe Mungu amuangamize..
Ayubu 2: 3 “Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, UJAPOKUWA ULINICHOCHEA JUU YAKE, ILI NIMWANGAMIZE PASIPOKUWA NA SABABU”.
Hapo Bwana alimletea Ayubu mabaya kwa uchochozi wa shetani ijapokuwa Ayubu alikuwa mkamilifu, hebu jiulize kwa mtu ambaye sio mkamilifu, mzinzi, mwasherati, msengenyaji, mtukanaji n.k ni Mashitaka mangapi mabaya yanapelekwa mbele za Mungu na shetani dhidi yake??..
Hivyo ni muhimu kufahamu hilo kwamba shetani anao uwezo wa kuzuia majibu ya maombi yetu kwa njia hiyo.
Hivyo suluhisho pekee ili maombi yetu yasizuiliwe ni KUWA WAKAMILIFU MBELE ZA MUNGU KAMA AYUBU… Ndio ni kweli, Bwana alisikiliza uchochezi wa shetani na kumletea Ayubu yale majaribu, lakini haimaanishi kwamba kila uchochozi shetani anaoupeleka sasa kwa Mungu dhidi yetu, basi Mungu atausikiliza kama alivyousikiliza wa Ayubu, kama tukiwa wakamilifu. La Mwingi anaukataa kwasababu ni wakamilifu mbele zake, na zaidi ya yote anatuletea baraka badala ya mabaya shetani anayotutakia.
Lakini tusipojitahidi kuwa wakamilifu, kwa kuzishika amri zake na kuliishi Neno lake, basi tufahamu kuwa majibu ya maombi yetu yatakuwa ni ndoto, na badala yake tunaweza kupata matatizo badala ya baraka, kwasababu shetani yupo kutushitaki…
NA NI UKAMILIFU UPI AMBAO UTATUSAIDIA KUPATA MAJIBU YA MAOMBI YETU.
2. Kwa kuwa waombaji (Yohana 14:13, 1 Wathesalonike 5:17, Luka 22:40).
Na mengine yanayohusiana na mambo hayo… Tukiyafanya hayo, basi tunao uhakika wa maombi ya majibu yetu kutufikia, bila kuzuiwa na mamlaka ya giza. Na pia kama tuna uhakika kwamba tunayafanya hayo, basi tuombe kwa ujasiri na Imani, pasipo mashaka…
Na pia kumbuka sio kila jibu la ombi linalokawia ni limezuiliwa na shetani.. Hapana!..Mengine hayajazuiliwa isipokuwa wakati wake wa majibu bado haujafika…Ukifika wakati jibu litakufikia tu!. Ni sawa na mwanafunzi anayemwomba Mungu awe daktari, hawezi kupata jibu la ombi hilo siku ile anayoomba, kashasikiwa maombi yake lakini hana budi kupitia madarasa fulani ambayo yatamjenga ili wakati utakapofika wa kupokea jibu la ombi lake, awe kashaandaliwa kielimu vya kutosha, ndio hapo inaweza kumchukia hata miaka 15 mbeleni, mpaka hicho alichomwomba Mungu kitimie (sasa huo ni mfano tu!).. Na maombi mengine ni hivyo hivyo, unaweza kumwomba Mungu leo, usikipate hicho kitu leo leo..kikaya kutokea baadaye sana, baada ya Mungu kukuaandaa vya kutosha. Hivyo ni muhimu kulijua pia hilo.
Bwana atubariki na kutusaidia.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
FAIDA ZA MAOMBI.
FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU
Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?
MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.
TUMEPEWA, SI KUMWAMINI TU KRISTO, ILA NA KUTESWA KWA AJILI YAKE;
Sala ya Uponyaji/Maombi ya uponyaji
Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo.
Kusudi lingine kuu tukiachilia mbali lile la wokovu wa roho zetu ambalo lilimfanya Bwana Yesu aache enzi na mamlaka na ukuu kule mbinguni ashuke duniani, lilikuwa ni kutuponya na miili yetu pia.
Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa”,
Mathayo 8: 17 “Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu”.
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu;..”
Ni Yesu peke yake, ndiye mwenye uwezo wa kuyaondoa magonjwa yetu yote moja kwa moja, hakuna mwingine anayeweza kufanya hivyo, na ndio maana tunamtumaini yeye. Na ni mapenzi yake kuwa sisi tuponywe(Soma Mathayo 8:2-3). Inawezekana wewe unayeusoma ujumbe huu, upo katika hali mbaya wakati huu, inawezekana upo mahutihuti hospitalini,au umekuwa ukisumbuliwa na huo ugonjwa kwa muda mrefu, umejaribu kwenda huko na kule bila kupata mafanikio yoyote, umepoteza fedha nyingi kwa ajili ya matibabu lakini hakuna matumaini yoyote. Pengine hata ulishahudhuria katika nyumba za maombi lakini bado hali yako ipo palepale, nataka nikuambie usivunjike moyo, hilo bado halimfanyi Yesu asikuponye ugonjwa wako.
Inawezekana unao ugonjwa wa siri, na unaogopa hata kuwaeleza watu, inawezekana umepata ugonjwa usioponyeka, Umepata Ukimwi, au Kansa, au Kisukari, n.k. Nataka nikuambie hayo yote si kitu kwa Bwana Yesu.
Kama Yesu alifanya muujiza wa kuuponya mwili wa mtu ambaye alikuwa ameshakufa kwa ugonjwa mbaya sana(Lazaro) na mwili wake ulikuwa tayari umeshaanza kutoa mafunza kaburini, lakini akauridisha na ukiwa mzima bila shida yoyote.. Si zaidi wewe ambaye bado hata hujafa, bado hata mwili wako hujaanza kutoa mafunza? Atakuponya.
Anachotaka kwako ni kuamini tu! Basi.
Na imani inakuja kwa kusikia, hicho ndicho chanzo cha Imani, (Warumi 10:17) Unapolisoma Neno lake, imani inajengeka, unasoma shuhuda mbalimbali za jinsi Bwana alivyowaponya watu katika maandiko ndipo imani yako kwake inavyojengeka, na kuwa kubwa zaidi,
Unaweza kufungua masomo haya, na shuhuda hizi mbili tatu, zitakusaidia kuiimarisha imani yako;
Zaburi 107:19 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao”.
Sala ya Uponyaji/Maombi ya uponyaji
Lipo kusudi la Mungu kukufikisha katika ukurasa huu kwa wakati huu; Kwa baada ya maombi haya mafupi ambayo tutakwenda kuomba pamoja amini kuwa kuna tendo linakwenda kutendeka ndani yako kuanzia huu wakati;
Tunapokwenda kuomba pamoja nataka mahali ulipo, weka mkono wako katika eneo la ugonjwa lilipo. Kisha zungumza maneno haya:
Bwana Yesu, wewe ni mponyaji wangu. Ulisema unalituma Neno lako ili uniponye(Zab 107:20).. Na pia ulisema Neno lako li hai tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga wowote ukatao kuwili (Waebr 4:12). Hivyo Bwana Yesu mponyaji wangu, naomba sasa ulitume Neno lako ndani ya mwili wangu likafanye uponyaji. Likaondoe magonjwa yote haya yanayonisumbua (yataje). Likakate kate kazi zote za ibilisi zilizopangwa ndani ya mwili wangu. Nikawe mzima kabisa sawasawa na maneno yako uliyosema katika Yeremia 30:17 ..kwamba utanirejesha afya yangu na kuniponya jeraha zangu. Naiita afya yangu sasa sawasawa na ahadi zako kwa jina la Yesu Kristo, nauita uzima wangu kwa jina la Yesu Kristo.
Asante Mungu wangu kwa upendo wako, na kwa uponyaji wako. Amen.
Basi ikiwa umeomba sala hiyo fupi: Hapo hapo na mimi nitakwenda kukuombea.
Ee Mungu baba, nakushukuru kwa mwanao huyu ambaye ameona msaada pekee, unatoka kwako na si kwa mtu mwingine yeyote. Baba nakuomba ikiwa ametenda dhambi iliyomstahili ugonjwa huo nakuomba Mungu wangu umsamehe, ikiwa amepata ugonjwa huo kwa nguvu za giza basi leo natangaza mwisho wake, kwa Jina la Yesu Kristo. Naomba kama mtumishi wako, umpe afya yake, ili akajue kuwa hakuna mwingine awazaye kutuokoa sisi isipokuwa wewe YEHOVA, na kwa kupitia ushuhuda huo akapate kwenda kulitangaza jina lako kuu kwa mataifa. Asante kwa uponyaji huo ambao tayari umeshaanza kuingia katika mwili wake. Amen.
Sasa kama nilivyosema, zidi kuamini kuwa tayari Kristo amekuponya. Lakini pia ikiwa bado hujaokoka, (Yaani bado hujampa Yesu Kristo maisha yako) Ni vema ukafanya hivyo sasa. Kwasababu hali nyingine haziwezi kuondoka ndani ya mtu, kama mtu mwenyewe hajaamua kukubaliana na Yule anayekwenda kumponya.
Kumbuka wokovu wa roho yako ni bora zaidi kuliko huo wa mwili wako. Ukiponywa mwili, halafu roho ikaangamia faida yake ni nini? Lakini vikiponywa vyote ni faida jumla jumla. Tukizingatia kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu yupo mlangoni kurudi. Hatuna muda tena kwa kuvumiliana na shetani nyakati hizi za hatari, Hivyo bila kuchelewa, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba ya kupewa maelekezo mengine >>>> SALA YA TOBA
Bwana akubariki sana.
Kama utahitaji maombezi zaidi, basi wasiliana nasi kwa namba hizi bure, +255 693036618/ +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Neno hilo italisoma katika ile habari ya Stefano alipokuwa anatumiwa na Mungu kufanya ishara na maajabu yasiyokuwa ya kawaida katika kanisa lake.
Lakini baadhi ya wayahudi wa masinagogi mbali mbali walipoliona hilo wakamchukua kuja kujadiliana naye, na baada ya kuona kuwa wameshindwa waliingiwa wivu na kufanya mambo ambayo huwezi kudhani dhehebu la dini linaweza kufanya. Sasa moja ya sinagogi hilo lilikuwa ndio hilo lililoitwa Sinagogi la Mahuru; kulikuwa na mengine pia tusome.
Matendo 6:8 Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.
9 Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa sinagogi la Mahuru, na la Wakirene, na la Waiskanderia, na la wale wa Kilikia na Asia, wakaondoka na kujadiliana na Stefano;
10 lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye.
11 Hata wakashawishi watu waliosema, Tumemsikia mtu huyu akinena maneno ya kumtukana Musa na Mungu.
12 Wakawataharakisha watu na wazee na waandishi, wakamwendea, wakamkamata, wakampeleka mbele ya baraza.
13 Wakasimamisha mashahidi wa uongo waliosema, Mtu huyu haachi kusema maneno ya kufuru juu ya mahali hapa patakatifu na juu ya torati;
Sasa ni kwanini liitwe kwa jina hilo?
Biblia haijaeleza chochote kuhusu chimbuko la sinagogi hilo mpaka wakajiita hivyo, lakini inaaminiwa na baadhi ya wanazuoni kuwa kulikuwa na kundi la wayahudi ambao walikuwa ni watumwa wa dola ya Ki-Rumi, Na baadaye wakafanywa kuwa huru, na ndipo hapo wakawa na sinagogi lao, wakaliita Sinagogi la mahuru. Yaani sinagogi la watu waliofanywa kuwa huru.
Hivyo hata kama chimbuko la jina hilo lingekuwa ni tofauti na hiyo, lakini bado jina lake ni nzuri, “Mahuru”. Lakini shida inakuja ni pale ambapo mioyo yao haiakisi jina hilo. Ni wazi kuwa watu hawa hawakuwekwa huru moyoni, kwasababu kama wangewekwa huru wasingekuwa na wivu, na wasingemzushia Stefano habari za uongo. Hiyo ni kuonyesha kuwa walikuwa ni watu walio mbali na wokovu kuliko hata watu wasiomjua Mungu kabisa.
Tunajifunza nini?
Hatushangai hata sasa kuona yapo makanisa mengi, na mikusanyiko mingi, yenye majina mazuri ya rohoni, yenye misalaba mingi, yenye kila aina ya mapambo mazuri ya rohoni. Lakini ndani yake wanazipinga nguvu za Roho Mtakatifu kama walivyompinga Stefano.
Biblia ilishatabiri katika kitabu cha 1Timotheo 3 kuwa katika nyakati za mwisho watatokea watu wengi wa namna hiyo
2Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.
2 Maana watu watakuwa……….
5 wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao”.
Unaona watakuwa wenye mfano wa utauwa lakini wanazikana Mungu za Mungu.
Huu si wakati wa kujivunia dhehebu au dini ndugu, ni wakati wa kujivunia Kristo ndani yako. Unaweza ukawa na dhehebu zuri kweli, kubwa kweli, lakini Mungu amelikataa, wewe litakufaidia nini? Tunapaswa tuutafute utakatifu kwa bidii kwasababu hatuwezi kumwona Mungu tusipokuwa nao(Waebr 12:14).
Tunapaswa tujichunge tusifanane na hawa wa sinagogi la mahuru ambao wana jina zuri lakini ni wapinga-Kristo ndani yao.
Bwana atusaidie.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)
Jina la Bwana wetu libarikiwe daima. Nakukaribisha katika kujifunza Maneno ya Mungu. Leo kwa ufupi tutatazama sehemu ya maisha ya Bwana wetu Yesu jinsi yalivyokuwa hapa duniani. Kama tunavyojua maisha yake ni ufunuo tosha wa kanisa la Kristo jinsi linavyopaswa liwe.
Tukisoma maandiko tunaona Bwana Yesu alitabiriwa kuwa atatokea katika uzao wa Daudi, na pia katika mji wake ujulikanao kama Bethlehemu (kasome Mika 5:1, na Mathayo 2:6), na kama tunavyojua ni kweli yalitimia kama yalivyotabiriwa, alizaliwa Bethlehemu ya Uyahudi. Lakini Yesu hakuishi katika mji huo wa Daudi (Bethlehemu) au katikati ya wazao wa Daudi, bali alikwenda kuishi katika mji mwingine mmoja mdogo huko Galilaya ulioitwa Nazareti, ulio mbali kabisa na mji wa Bethlehemu. Nazarethi uli
Mji huu ulikuwa kaskazini mwa Israeli, na ndio wa mwisho kabisa kimaendeleo kuliko miji yote iliyokuwa Israeli wakati ule, ni mji ambao haukuandikiwa unabii wowote katika biblia nzima, japo Mungu tayari alikuwa ameshautolea unabii wake kupitia vinywa vya manabii wake (Mathayo 2:23). Ni mji ambao haukuwa na watu wengi, mji ambao haukuwa machachari, mji uliosahaulika kabisa, wala hakuna mtu aliyetazamia kuwa mtu yeyote mkuu angeweza kutokea huko?
Na ndio maana utaona hata Filipo alipokuwa anamwelezea Nathanieli habari za masihi, Nathanieli alimwambia Je! Inawezekana kweli jambo jema kutokea Nazareti, Mji kama ule ambao hauna sifa yoyote nzuri, iweje Masihi atokee huko, maandiko yanatuambia masihi atatokea mji mtakatifu kule Bethelemu, Yuda, iweje utuletee habari ya kijiji hichi ambacho hata hakina sifa yoyote nzuri,
Yohana 1:46 “Nathanaeli akamwambia, Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone”.
Lakini hapo ndipo mahali sahihi ambapo Mungu alipachagua mwokozi wa ulimwengu aishi kwa miaka karibia 30. Karibia asilimia 90 ya maisha ya Bwana Yesu yalikuwa katika mji huu uliosahaulika, na ndio maana utaona kila mahali watu walikuwa wanamtambulisha kama Yesu wa Nazareti (Mathayo 26:11), Hiyo yote ni kwasababu maisha yake mengi aliyaishia huko. Na sio tu watu na mitume peke wao walimtambulisha kwa jina hilo, Pilato naye alimtambua kwa jina hilo, Mapepo nayo yalimtambua kwa jina hilo..
Marko 1:23 “Na mara palikuwapo ndani ya sinagogi lao mtu mwenye pepo mchafu; akapaza sauti,
24 akisema, Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je! Umekuja kutuangamiza”?
Hata yeye mwenyewe Bwana, alijitambulisha kwa jina la mji wake siku ile alipomtokea Sauli alipokuwa anakimbilia Dameski;
Matendo 22:6 “Ikawa nilipokuwa nikisafiri, nikikaribia Dameski, wakati wa adhuhuri, ghafula nuru kuu ilitoka mbinguni, ikanimulikia pande zote.
27 Nikaanguka nchi, nikasikia sauti ikiniambia, Sauli, Sauli, mbona unaniudhi?
8 Nikajibu, Wewe u nani, Bwana? Akaniambia, Mimi ni Yesu Mnazareti, ambaye wewe unaniudhi”.
Inawezekana na sisi tunamtambua Bwana Yesu kwa jina hilo, lakini tumekuwa hatujui ni kwanini tunamwita wa Nazareti, tunapaswa tujue ni kwanini iwe Nazareti na sio Bethlehemu, au Korazini, au Kapernaumu?
Mungu anataka na sisi, tujue mazingira yetu, sio sababu ya yeye kutotimiza ahadi zake juu yetu. Kuna wengine wanasema ni kwasababu nipo kijijini, laiti ningekuwa mjini ningefanya hiki au kile kwa ajili ya Mungu, hiyo isiwe sababu ndugu, mkumbuke Yesu, Yule Yesu wa Nazareti na sio Yesu wa Bethlehemu..upate kujifunza!.
Pengine utasema kwasababu nimezaliwa Afrika, ningezaliwa ulaya ningemfanyia Mungu makubwa, ndugu mkumbuke Yesu wa Nazareti.
Tusiwe na sababu zozote zile, Bwana wetu alizaliwa katika hori la kulishia ng’ombe, alikuwa maskini biblia inatuambia hivyo, aliishi katika mji usiokuwa na maendeleo yoyote. Lakini kutoka katika mji huo dunia nzima imejua kuwa yeye ni mwokozi Yule Yule aliyetabiriwa na manabii.
Hivyo na sisi katika mazingira yoyote tuliyopo, haijalishi ni mazuri au mabaya, haijalishi ni ya kisasa au ya kale, tanaweza kulikamilisha kusudi la Mungu kikamilifu, kama Mungu alivyokusudia, endapo tukiwa waaminifu kwake kama Mwokozi wetu alivyokuwa mwaminifu kwa Baba.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Katika kitabu cha Zaburi na Mithali Neno mpumbavu linatajwa sana, naomba kufahamu mpumbavu ni mtu wa namna gani kibiblia?
Biblia haielezi moja kwa moja maana ya mpumbavu, bali inaeleza tabia zinazoambatana na mtu mpumbavu, embu tupitie baadhi ya vifungu vinavyolizungumzia neno hilo na mwisho kabisa hivyo ndivyo vitakavyotusaidia kujua mpumbavu ni mtu wa nanma gani;
Zaburi 14:1 “Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema”.
Mithali 10:8 “Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka”.
Mithali 9:13 “Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu”.
Mithali 10:14 “Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa; Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu”.
Mithali 10:23 “Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo; Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima”.
Mithali 12:15 “Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri”.
Mithali 12:16 “Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu”.
Mithali 14:1 “Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe”.
Mithali 15:5 “Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara”.
Mithali 14:16 “Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu; Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai”.
Mithali 20:3 “Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana”.
Mithali 14:3 “Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi, Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi”.
Mithali 15:20 “Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mpumbavu humdharau mamaye”.
Hivi ni baadhi ya vifungu tu, lakini unaweza kuona mpumbavu ni mtu anayetajwa kuwa ana dharau, asiye na heshima, anayeropoka ropoka, asimcha Mungu, asiamini hata kama kuna Mungu, asiyetaka kurekebishwa, anayependa ugomvi, anayesambaza habari za uzushi n.k.
Na tabia zote hizi huwa zinafanya na mtu mwenye dhambi, kwasasa ni mtu ambaye hajakombolewa na Yesu.
Hivyo tafsiri hasaa ya Neno mpumbavu, ni mtu ambaye hajazaliwa mara pili.
Kwahiyo ikiwa wewe upo nje ya Kristo, haijalishi utakuwa msomi kiasi gani, au utakuwa tajiri kiasi gani, a utakuwa na ushawishi mwingi kiasi gani, wewe ni mpumbavu kibiblia, kwasababu hutakosa tabia mojawapo ya wapumbavu zinayozungumziwa katika biblia.
Ni Yesu pekee ndio mwenye uwezo wa kumgeuza mtu moyo wake na kumfanya kuwa mtu mwingine kabisa. Yeye mwenyewe alisema.. Wote wanaompokea anawapa UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu. (Yohana 1:12). Hii ikiwa na maana ukimkaribisha Yesu katika maisha yako, ni uhakika kuwa UWEZO huo utakuja ndani yako, wa kuweza kuzishinda tabia zote za wapumbavu, yaani kushinda ulevi, kushinda uzinzi, kushinda anasa, kushinda usengenyaji n.k..
Hivyo kwanini usimpe leo YESU maisha yako ayaokoe, na utoke kuwa mojawapo ya wapumbavu mpaka kuwa mwana wa Mungu mteule, mbarikiwa aliyeandaliwa kwa ajili ya kuurithi uzima wa milele? Ikiwa upo tayari leo kuokoka, basi fungua hapa kwa ajli ya kuongozwa sala ya Toba na kupata maelekezo mengine ya kiroho >>>>> SALA YA TOBA
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Hivi ni vifupisho vya nyakati.
K.K – Maana yake ni Kabla ya kuzaliwa Kristo Yesu. Kwa kiingereza (B.C – Before Christ)
Na
B.K - Maana yake ni Baada ya kuzaliwa kwake Kristo Yesu. Kwa kiingereza (A.D– Anno Domino- Katika mwaka wa Bwana )
Lakini mahali pengine wanatumia kifupi cha K.W.K kumaanisha K.K. na WK kumaanisha B.K. Husasani kwa watu ambao sio wakristo, au hawaamini habari za Yesu Kristo, Lakini maana ni ile ile moja.
K.W.K maana yake ni Kabla ya wakati wa kawaida. Kwa kiingereza (B.C.E – Before the common Era)
Na,
W.K Maana yake ni Wakati wa kawaida. Kwa kiingereza (C.E– Common Era)
Kwamfano unaweza kukutana na habari fulani ya historia kwa mfano inasema kitabu cha Danieli kiliandikwa mwaka 600 KK, au 600 KWK, Hiyo inamaanisha kuwa kiliandikwa miaka 600 kabla ya kuzaliwa kwa Kristo.
Au utakutana na habari inasema Hekalu la Yerusalemu lilibomolewa mwaka 70 BK, Au 70 WW. Maana yake ni hekalu lilibomolewa mwaka wa 70 baada ya Kristo kuzaliwa duniani.
Hivyo tunaposema huu ni mwaka fulani wa 2000 + haimaanishi tangu dunia iumbwe ni miaka elfu mbili imepita hapana, bali ni miaka 2000 baada ya kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Kabla ya hapo kulikuwa na miaka mingine mingi iliyopita, zaidi ya 4000, ambayo ndiyo inahesabika kama miaka kabla ya Kristo.
Bwana akubariki.
Je! Umeokoka? Je! Unahabari kuwa hatuna muda mrefu sana, mpaka unyakuo upite? Yote yaliyotabiriwa yameshatimia, na kwamba pengine kizazi chetu kitashuhudia tukio zima la mwisho wa dunia? Swali la kujiuliza je na sisi tumejiwekaje.
Ikiwa upo nje ya Kristo na unataka leo ayageuze maisha yako. Basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako. Fungua hapa kwa ajili ya Sala ya Toba na maelekezo mengine >>> SALA YA TOBA
Na Bwana akubariki sana.
Pia Tazama maana ya maneno mengine ya kibiblia chini.
Kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Hosana ni neno la kiyahudi lenye maana ya “OKOA”. Neno hili limeonekana mara ya kwanza kwenye biblia kipindi wakati Bwana Yesu anaingia Yerusalemu, ambapo wenyeji walimpokea kwa furaha, wakimwimbia na kumtukuza Mungu kwa shangwe nyingi..
Yohana 12: 12 “Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu;
13 wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, HOSANA! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli!”
Habari hiyo hiyo unaweza kuisoma tena katika Mathayo 21:9, Mathayo 21:15, na Marko 11:9-10.
Sasa swali la kujiuliza ni kwanini, Hao watu watumie hilo Neno “Hosana” na si Neno lingine lolote…labda “karibu Ee Masihi..karibu ee Masihi”..badala yake wanamkaribisha kwa kumwambia “Hosana” yaani “okoa..okoa”.
Ikumbukwe kuwa Wayahudi (yaani Waisraeli), wakati Bwana Yesu yupo duniani walikuwa wapo chini ya utawala wa kirumi.. Wakati huo dola ya kirumi ndiyo iliyokuwa inatawala dunia nzima chini ya Mfalme Kaisari aliyeko Rumi.
Kwahivyo wakati Kristo yupo duniani, Israeli ilikuwa ni koloni la hawa warumi, Ndio maana utaona pia waliomsulubisha Bwana ni askari wa kirumi. Hivyo waisraeli wote walikuwa wanalazimishwa kumpa Kodi Kaisari, na walikuwa wanamtumikia. Na kwasababu walikuwa wanayajua maandiko kwamba ipo siku Masihi (yaani Kristo), atakuja na kuwaokoa na utumwa wote na maadui zote..kama maandiko yanavyosema…katika Zekaria
Zekaria 14: 3 “Hapo ndipo atakapotokea Bwana, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita”.
Hivyo Wayahudi wote walikuwa wanaitazamia hiyo siku ambayo Masihi atakuja kuwaokoa kwa mkono mkuu. Na baadhi waliokuwa wamemwamini Yesu kama ndiye Masihi huyo kafika, hivyo wakabeba matawi ya mitende na kumshangilia na kumfurahia alipoingia Yerusalemu, huku wakimwimbia..Hosana… hosana..au okokoa…okoa!
Na wanafunzi wake pia walitazamia wakati huo ndio ulikuwa umefika au umekaribia wa wakovu, wakati wa Masihi kuwapigania na kuwarudishia ufalme..wasiwe tena koloni la Taifa lingine. Ndio maana utaona kipindi kifupi tu baada ya kufufuka kwake, walimwuliza hilo swali..
Matendo 1:6 “Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?
7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao”.
Hivyo ule haukuwa wakati wa Masihi kuwaokoa Israeli, dhidi ya utawala unaowatumikisha. Iliwapasa kwanza wakahubiri injili kwa watu wa mataifa yote kwanza, na injili itakapokwisha kuhubiriwa na watu kuokolewa, Ndipo huo wokovu mkuu kwa Israeli uje.
Hivyo utafika wakati ambapo Kristo atashuka kutoka mbinguni kwa nguvu nyingi, naye atawapigania Israeli na kuwaokoa, wakati huo injili itakuwa imeshamalizika kuhubiriwa kwa mataifa yote na unyakuo utakuwa umeshapita, na ndio utakuwa mwanzo wa utawala wa Miaka 1000 ya Yesu Kristo hapa duniani, ambapo utakuwa utawala wa Amani, na atatawala akiwa pale Yerusalemu, Israeli Pamoja na watakatifu wake aliowanyakua.
Je! Wakati huo utakuwepo Pamoja na Kristo katika utawala huo, au utakuwa jehanamu?. Maisha yako ndio jibu lako.
Kama hujaokoka Mlango wa Neema upo wazi sasa, ila hautakuwa hivyo siku zote..Ukimpokea leo Kristo, utafanyika kiumbe kipya na utakuwa na uhakika wa kuzirithi ahadi za Mungu walizoandaliwa wote wampendao.
Kama umeamua leo kumpa Kristo Maisha yako basi fuatilisha sala hii ya toba hapa >> SALA YA TOBA.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Watu wa mataifa mengine yote ya ulimwengu tofauti na Taifa la Israeli, ndio wanaojulikana kama “watu wa Mataifa”.
Mungu alipoanza mpango wake wa kurejesha uhusiano wake na mwanadamu ambao ulipotea tangu pale Edeni, alianza na Taifa moja tu lijulikanalo kama “Israeli”, Na Taifa hili lilianza na mtu mmoja ajulikanaye kama Ibrahimu, ambaye huyu Ibrahimu akamzaa Isaka,.Isaka akamzaa Yakobo, Yakobo akazaa Watoto 12, na kwa kupitia majina ya Watoto hao ndipo yakazaliwa majina ya makabila 12 ya Israeli. Na hao Watoto wakazaa wana, na hatimaye likawa jeshi kubwa la watu wengi wa jamii ya Israeli, na kuwa Taifa.
Sasa watu wengine wote tofauti na uzao huo wa Ibrahimu, ndio watu wa mataifa. Kwasababu duniani kulikuwa na watu wengine wengi wa jamii nyingi, walikuwepo waMisri (ambao ndio sasa nchi ya Misri), walikuwepo waashuri (Ambao kwasasa ni maeneo ya Syria), walikuwepo wakushi (ambao sasa ni maeneo ya huku Afrika)..walikuwepo Wakaldayo (ambao sasa ni maeneo ya Iraq), walikuwepo watu wa bara la Hindi (ambao sasa ndio India), walikuwepo watu wa Uajemi na Umedi ambao ndio kwasasa maeneo ya (Kuwait,Qatar, UEA{Dubai} na sehemu za magharibi ya Saudi Arabia), walikuwepo Warumi (ambao sasa ndio Italy), walikuwepo Wayunani (kwasasa ni Ugiriki) na mataifa mengine mengi (Yote hayo yalijulikana kama Mataifa).
Sasa Mungu amekuwa akitembea na Taifa la Israeli pekee Kwa miaka Zaidi ya 1,500, wakati huo wote Mungu hakushughulika na hayo mataifa mengi yote (haijalishi yalikuwa yameendelea kiasi gani au yalikuwa yana watu wazuri kiasi gani). Taifa lake teule na pekee lilikuwa ni moja tu ambalo ni Israeli, ndio maana utaona Amri 10, walipewa Israeli na si watu wa Mataifa mengine, na agano lote la kale inahusu Habari za wana wa Israeli mwenendo wao na Mungu wao.
Sasa sio kwamba Mungu alikuwa hana mpango kabisa na watu wa Mataifa!. La! Alikuwa ana mpango nao mkubwa sana. Lakini siku zote hakiwezi kuzaliwa cha pili, kabla ya kuzaliwa cha kwanza, hawezi kunyonya mtoto wa pili kabla hajanyonya wa kwanza, hawezi kukumbatiwa mtoto wa pili kabla ya wa kwanza. Hata mama anayejifungua Watoto, ni lazima azaliwe mtoto wa kwanza, ndipo afuate wa pili… Na yule wa kwanza atapendwa na kutunza kabla ya yule wa pili.
Kwahiyo Taifa la Israeli ni mzaliwa wa kwanza kwa Mungu, na watu wa mataifa ni mzaliwa wa pili..
Kutoka 4: 22 “Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu;
23 nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako”.
Hivyo ulipofika muda wa “mzaliwa wa pili kuzaliwa, (yaani wakati wa watu wa mataifa nao kukumbukwa na Mungu). Mungu alianza mpango wake huo kwa kumleta Mwanawe mpendwa Yesu Kristo, awe sababu ya wokovu kwa watu wote wa mataifa.
Kama kuku aliyeacha vifaranga vyake vya kwanza, kwa kuvidonoa na kuanza malezi mapya ya uzao wa pili, Ndicho alichokifanya Mungu kwa Israeli, Neema iliondoka kwao na kuhamia kwa watu wa mataifa (yaani mimi na wewe).
Warumi 11:25 “ Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili”.
Tangu wakati wa Bwana Yesu mpaka sasa, watu wa mataifa yote..tunaweza kumkaribia Mungu, na kuzirithi baraka zile zile za rohoni, kama walizokirimiwa Israeli.
Hiyo ndiyo SIRI YA MUNGU, ambayo ilifichwa kwa miaka mingi, ambayo hata wana wa Israeli wenyewe hawakujua kwamba ingefika siku moja, watu wa Mataifa nao watapata upendeleo kwa Mungu kama wao.
Paulo ambaye ni Muisraeli aliiandika siri hiyo kwa ufunuo wa Roho na kusema..
Waefeso 3:4 “Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo.
5 Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;
6 YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, NA WA MWILI MMOJA, NA WASHIRIKI PAMOJA NASI WA AHADI YAKE ILIYO KATIKA KRISTO YESU KWA NJIA YA INJILI”.
Hivyo tangu Bwana Yesu aondoke duniani, imepita Zaidi ya miaka 2,000 kipindi kirefu Zaidi ya kile Mungu alichotembea na wana wa Israeli peke yao.. Maana yake ni kuwa kipindi cha Neema kwetu sisi watu wa mataifa nacho kinaenda kufikia ukomo. Na kitafikia ukomo kwa unyakuo.
Unyakuo ukishapita mlango wa Neema unakuwa umefungwa kwa watu wa Mataifa. Mungu atawarudia tena watu wake Israeli kwa kipindi kifupi sana cha juma moja ambalo ni sawa na Miaka 7, baada ya hapo, hukumu ya mataifa itaanza na Utawala wa amani wa Yesu Kristo wa miaka elfu.
Je umempokea Kristo?..Upo ndani ya neema?. Kama bado upo nje, basi jua umechelewa sana..hivyo usiendelee kupoteza muda, ingia ndani ya neema uisalimishe roho yako. Yesu anakupenda na alikufa kwa ajili yako.
kumbuka pia, watu wote ambao hawajaokoka, katika agano letu jipya huitwa watu wa mataifa,
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Nabii Elisha alikuwa ana maana gani kulia na kusema”Gari la Israeli na wapanda farasi wake”?
Kuota upo nchi nyingine.
Kama tunavyojua ukisafiri mahali ambapo ni tofuati na makazi yako ya asili, utakutana na mabadiliko mengi sana, hususani pale unapovuka mipaka na kuingia katika nchi nyingine, si ajabu kukutana na hali ya hewa ya aina nyingine, kukutana na watu wa jamii nyingine, kukutana na lugha gheni, n.k..
Na hiyo itakufanya usijione upo huru sana kama ulivyokuwa katika nchi yako mwenyewe.Na wakati mwingine inaweza kukufanya ujione haupo sehemu salama sana, kwasababu sio nchi yako, na haujaizoea.
Wana wa Israeli walipokuwa wanachukuliwa utumwani kupelekwa Babeli, wakiwa njiani walilia sana, hata wale wakaldayo,walipowashurutisha wawaimbie nyimbo za nchini mwao walikataa, wakasema tutaimbaje wimbo wa Bwana nchi ya ugenini?
Zaburi 137:1 “Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2 Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu.
3 Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4 Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni”?
Kwasababu walijua kabisa wanakwenda katika nchi ambayo sio ya kwao, katika mazingira ambayo hawajayazoea. Kwenye tamaduni mpya,
Hivyo unapojiona kwenye ndoto upo katika nchi ya ugenini, unaishi huko, au unatembea, Yapo mambo mawili hapo ambayo Mungu anakuonyesha.
Jambo la kwanza; Ikiwa wewe umeokoka, (yaani umeokolewa na Bwana Yesu), Hapo ni Mungu anakuonyesha wazi jinsi itakavyokuwa pale utakapotoka katika hifadhi yake. Utakuwa kama mtumwa, hivyo, jiangalie na jithibitishe, zidi kukaa katika mapenzi ya Mungu na kama ulikuwa umeshaanza kupoa, basi mgueukie Mungu wako kwa moyo wako wote. Ili ubakie katika nchi yako ya wokovu aliyokukusudia.
Lakini ikiwa hujaokoka, ni Mungu anakuonyesha hali yako ilivyo leo hii, upo katika nchi ya ugenini, japo hustahili kuwepo huko. Maisha yako yapo ugenini, hivyo huwezi kuwa huru, huwezi kuwa na amani, haijalishi pataonekana ni pazuri namna gani, Wana wa Israeli walilia, walipokuwa wanaenda ugenini. Hivyo na wewe pia uliye dhambini, upo ugenini, pengine kampani unazotembea nazo sio ambazo Mungu amekukusudia utembee nazo, Mungu anakuhitaji wewe ukae na watakatifu wenzako uyatafakari maisha ya mbinguni. Pengine ulevi, anasa, wizi n.k., sivyo ambavyo vinakupasa mtu kama wewe, na hilo unalijua kabisa, lakini bado unashikama nalo.
Embu yatafakari maisha yako, Je! Tangu ulipokuwa katika maisha ya dhambi ni raha gani umeipata au faida gani umepata?. Kwanini usizingatie kurudi nyumbani, kama yule mwana mpotevu aliyekwenda kuponda mali katika nchi ya mbali, lakini baadaye akazingatia kurudi kwa baba yake..Kwanini na wewe usizingatie kurudi kwa Baba yako wa mbinguni leo umwombe msamaha baada ya kupotea kwa muda mrefu.?
Ukisoma biblia utamwona Kaini yule aliyemuua ndugu yake ndiye aliyekuwa mtu asiye na kikao duniani, kama vile mapepo. Je na wewe unataka uwe mtu asiye na makao yake maalumu?
Leo hii ukikubali kutubu dhambi zako, Yesu atakupokea na kukusamehe, haijalishi wewe ni wa dini gani au dhehebu gani. Atakupokea, na kukukaribisha kwake, na atakupa raha nafsini mwako. Hivyo Kama upo tayari kufanya hivyo leo, basi fungua hapa kwa ajili ya maelekezo ya sala ya Toba, na Bwana akubariki. >>> SALA YA TOBA
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312/
Pia kwa ushauri/ratiba za ibada/ maombezi.
Jiunge kwenye magroup yetu ya Whatsapp kwa masomo ya kila siku ya Neno la Mungu.
Jiunge na channel yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP
Mada Nyinginezo: