Title 2020

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Ndoto ni eneo ambalo watu wengi wanadanganywa na kupotoshwa na hiyo yote ni kutokana na kukosa maarifa ya kutosha. Wapo watu wengi mitandaoni, wanaowaeleza watu tafsiri za ndoto mbalimbali zao na mwisho wanaambatanisha na dawa zao za kibiashara wakiwadanganya watu kuwa hizo zitaleta suluhisho la matatizo yao.

Wengi wa hao watu kama si wafanyabiashara basi ni waganga wa kienyeji na hawana lolote la kukusaidia zaidi ya kukuongezea matatizo. Kumbuka Ndoto si tatizo la kimwili hivyo hakuna tiba yoyote ya kimwili kama vile dawa ya kunywa au ya kumeza itakayoweza kuleta suluhisho la ndoto zako.

Kwa ufupi Zipo ndoto za aina tatu, 

  1. Zinazotokana na Mungu:
  2. Zinazotokana na shetani
  3. Zinazotokana na mtu mwenyewe.

Ndoto zinazotokana na Mungu zinachukua sehemu ndogo sana ya ndoto zote mtu anazoota kila siku naweza kusema hata asilimia 5 tu ya ndoto zote ulizowahi kuota,..

Vivyo hivyo na za shetani nazo hazina asilimia kubwa ya ndoto unazoziota mara kwa mara.

Lakini ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe hizi ndizo zinazochukua sehemu kubwa ya ulimwengu wa ndoto za wanadamu. Na hapa ndipo watu wengi wanapokosa shabaha, wakidhani kila ndoto tu wanayoiota ni lazima iwe na tafsiri, au ni lazima iwe imebeba ujumbe maalum.

Sasa hizo aina mbili za kwanza, (yaani ndoto za Mungu, na za Shetani) huwa zinabeba maana kubwa sana rohoni, ili kufahamu jinsi ya kuweza kuzitambua aina hizi za ndoto  fungua hapa..>>> Tofauti kati ya ndoto za Mungu na Shetani

Leo hii nitajikita kukuorodheshea baadhi ya ndoto ambazo watu wengi wanaota na hawajui nyingi kati ya hizo zinatokana na mwili wenyewe..

Ukiota Hizi  uzipuuzie, wala usihangaike kutafuta maana zake, kwasabu hizi huwa zinakuja aidha kutokana na shughuli nyingi..

  • Kwamfano wewe ni mkulima, hivyo kila siku kuota upo shambani unalima, au unaota pembejeo au mazao, hilo ni jambo la kawaida…

Soma..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;..”

  • Au kama akili yako muda wako wote kutwa kuchwa ilikuwa unafikiria masomo tu, basi jua kuota unafanya mitihani litakuwa  ni jambo la kawaida,
  • Vilevile ndoto za namna hii zinakuja kutokana na mabadiliko ya mwili. Kama ulilala una njaa, basi tarajia usiku kuota unakula kula hushibi, kama ulikunywa maji mengi na hivyo kibofu kimejaa, tarajia usiku kuota unakojoa kojoa mkojo hauishi, n.k.

Isaya 29: 8  “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni”.

Hivyo watu wengi wanaota ndoto nyingi za namna hiyo, na nyingine ubongo unazitengeneza wenyewe. Kwamfano utakuta mtu anatafuta kufahamu Tafsiri za ndoto mbalimbali kama hizi:

  1. Kunyonyesha mtoto: Wanaoota ndoto hizi asilimia kubwa ni wanawake, kwasababu wao ndio akili yao sehemu kubwa ilishajengeka katika mazingira ya kuwa na Watoto hata kama hajazaa..Hivyo kuota unanyonyesha haliwezi kuwa ni jambo la ajabu
  2. Vivyo hivyo kuota mbwa:
  3. kuota  panya,
  4. Wengine wanatafuta kujua ndoto za magari zinamaanisha nini: Magari tunakutana nayo kila siku barabarani.
  5. ukiota unaswali, .
  6. Maana ya ndoto nyevu,
  7. kuota una nywele ndefu,
  8. ndoto ya kufua nguo,
  9. tafsiri ya ndoto ya harusi.
  10. kuota unavua samaki, na za  kuogelea,
  11. Kuota umegeuza nguo
  12. Ndoto za kuogelea
  13. Kuota ajali
  14. Kuota umeua mtu
  15. Kuota upinde wa mvua
  16. Ndoto za meli
  17. Kuota unanyeshewa na mvua
  18. Maana ya ndoto za kuolewa
  19. Unachuma matunda
  20. Unakunywa pombe
  21. Umevaa nguo nyeupe, 
  22. Ndoto za mayai
  23. Ndoto ya Nyama
  24. Ndoto za asubuhi
  25. Kuota unaoga
  26. Kuota Wanyama, kama mbuzi, sungura, kinyonga, kobe, ngamia, tembo, mamba, kiboko, nyani, paka, mbwa, ng’ombe.N.k. Zote hizi zipuuzie tu. Hazina maana yoyote kwako.
  27. Kuota wadudu kama sisimizi, siafu, konokono, mchwa, mbu, nge, mjusi, mende,tandu
  28. Kuota mapacha.
  29. Kuota jirani, ndugu yako,
  30. Kuota unakula mkaa.
  31. Kuota unatapika.
  32. Watu wanavuna.
  33. Ndoto za kutembea peku.
  34. Unafagia, Unalia,
  35. Kumuota raisi, waziri mkuu, makamu wa raisi, mbunge. Hawa kila siku unawaona kwenye Tv, au unawasikia kwenye Radio, ni lazima utawaota tu usiku siku moja.
  36. Ndoto Juu ya mpenzi wako.
  37. Kuota kabati.
  38. Unafua nguo,
  39. Unaosha vyombo, Maiti,
  40. Kuota jeneza
  41. Ukiota karanga, vitunguu, nyanya, pilau, sherehe,
  42. Kuota Unauza duka

Nakadhalika, Nakadhalika..zipo nyingi, nyingine unazijua wewe mwenyewe, hatuwezi kuziorodhesha zote hapa.. Lakini zote hizo hazina umuhimu wa kutafuta kujua maana zake. Kwasababu ukienda kwa mtindo huo utachanganyikiwa mwilini na rohoni.

Kikubwa ni kufahamu kuwa njia Kuu  ambayo Mungu aliichagua kuzungumza na wanadamu ni kupitia Neno lake (Biblia tu)

Ikiwa wewe ni mwenye dhambi nataka nikuambie hizi ni nyakati za mwisho, Mafundisho mengi ya uongo, na ya mashetani yamezagaa kila mahali, Usipotaka kusimama, shetani ni lazima akuzombe kwenye aina ya mafundisho hayo ya mashetani na kukupa tafsiri ya kila ndoto unayoiota….

Tubu mgeukie Mungu wako, dalili zote zinathibitisha hilo kuwa tunaishi katika siku za mwisho. Maisha yako yapo hatarini sana, kwani hujui siku yako ya kuondoka ni lini, na hata kama hutaondoka leo au kesho, lakini UNYAKUO upo karibuni sana.. Yesu yupo mlangoni kuja kuwachukua wateule wake.

Kutoa shanga za wanawake maarufu kama vile pendanti, http://www.swisswatch.is/ best replica watches chokers na. Nunua vito vya thamani katika aina mbalimbali za metali na vito ili kuendana na tukio lolote.

Angalia hali halisi ya ulimwengu ulivyo sasa halafu niambie ni dalili ipi Yesu aliyosema kuhusu siku za mwisho haijatimia, angalia magonjwa ya mlipuko, angalia tetesi za vita, angalia matetemeko, angalia kuongozeka kwa maasi duniani,..yote hayo yalitabiriwa.

Huu si wakati wa kuangalia mambo mengine Zaidi ya wokovu wako. Nani ajuaye leo hii Mungu kakupitisha kwenye ukurasa huu ni ili Akuokoe? Kwasababu anaompango mkubwa na wewe maishani mwako?

Hivyo kama wewe ni mwislamu usiogope kumkabidhi YESU Maisha yako leo, fungua tu moyo wako mruhusu atende kazi, nawe utaona badiliko la ajabu atakalolileta ndani yako.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithibitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwabudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Bofya chini kwa kujiunga na magroup yetu ya Whatsapp, kwa  mafundisho ya kila siku.

Mada nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

MIJI YA MAKIMBILIO.

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKATI WA JUA KALI NDIO WAKATI WA KAZI:

Hebu tuchukue muda kidogo kuisoma habari ifuatayo naamini tutajifunza kitu,

1Samweli 11: 1 “Ikawa, kama baada ya mwezi mmoja, Nahashi, Mwamoni ,akakwea na kupanga marago juu ya Yabesh-gileadi;na watu wote wa Yabeshi wakamwambia Nahashi, Fanya mapatano nasi,na sisi tutakutumikia.

2 Huyo Nahashi, Mwamoni, akawaambia, Kwa sharti hii mimi nitapatana nanyi, kila mtu ang’olewe jicho la kuume; na kwa jambo hilo nitawashutumu Waisraeli wote pia.

3 Basi wazee wa Yabeshi wakamjibu, Tuachie siku saba, ili tutume wajumbe waende mipakani mwote mwa Israeli; kisha, ikiwa hakuna atakayetuokoa, tutakutokea.

4 Hivyo wajumbe wakafika Gibea ya Sauli, wakasema maneno hayo masikioni mwa watu; na watu wote wakainua sauti zao wakalia.

5 Na tazama, Sauli akaja akifuata ng’ombe kutoka kondeni; naye Sauli akauliza, Watu hawa wana nini, hata wakalia? Wakamwambia maneno ya watu wale wa Yabeshi.

6 Na roho ya MUNGU IKAMJILIA SAULI KWA NGUVU, hapo alipoyasikia maneno yale, na hasira yake ikawaka sana.

7 Naye akatwaa jozi ya ng’ombe, akawakata-kata vipande, kisha akavipeleka vile vipande mipakani mwote mwa Israeli kwa mikono ya wajumbe, kusema, Ye yote asiyetoka nyuma ya Sauli na Samweli, ng’ombe zake watatendwa vivi hivi. Basi utisho wa Bwana ukawaangukia wale watu, wakatoka kama mtu mmoja.

8 Naye akawahesabu huko Bezeki; Waisraeli walikuwa mia tatu elfu, na Wayuda thelathini elfu.

9 Nao wakawaambia hao wajumbe waliokuja, Waambieni watu wa Yabesh-gileadi, Kesho, WAKATI WA JUA KALI, mtapata wokovu. Basi wale wajumbe wakaenda, wakawaarifu watu wa Yabeshi; nao walifurahiwa.

10 Kwa hiyo watu wa Yabeshi walisema, Kesho tutawatokea, nanyi mtatufanyia yote myaonayo kuwa ni mema.

11 Ikawa, kesho yake, Sauli akawapanga watu katika vikosi vitatu; nao wakaingia katikati ya marago kwenye zamu ya asubuhi, wakawapiga Waamoni hata WAKATI WA JUA KALI; kisha ikawa wale waliosalia wakatawanyika, hata wasiachwe wawili wao pamoja”.

Biblia inasema taa ya mwili ni jicho, maana yake mtu akitolewa macho anakuwa kipofu, giza linaingia katika mwili wake wote, hebu fanya utafiti wa kufunga macho yako uone utakachokiona…bila shaka ni giza tupu…

Mathayo 6:22 “Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.

23 Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo!”

Kwahiyo kwa tukio hilo hapo juu, kuna wakati Mfalme wa Moabu alitaka kuingia katika ardhi ya Israeli inayoitwa Yabeshi, na alipoingia kwasababu ya wingi wa majeshi yake akawatishia Israeli vikali, nao wakaogopa, wakanyenyekea chini yake wakamwambia fanya mapatano nasi (maana yake kama unataka kitu chochote kutoka kwetu hata kama ni kodi tutakupatia)..lakini Yule mfalme kwa kiburi akasema hatataka kitu chochote bali kumng’oa kila mtu wa mji huo wa Yabeshi jicho la kuume…Na lengo la kuwaambia hivyo ni ile awaaibishe na pia aliingize giza katika mji ule, kwasababu alijua jicho la mtu ndio mwangaza wake..mtu hakuna chochote anaweza kufanya.

Jambo hilo liliwahuzunisha watu wa Yabeshi, mpaka kufikia hatua ya kwenda kuomba msaada wa ndugu zao waisraeli walio kwenye majimbo mengine, na wakati huo Israeli walikuwa wameshajitakia mfalme, na walimteua Sauli…lakini kila mtu alikuwa anamdharau Sauli kwa kuwa walimwona kama ni kijana laini asiye na uwezo wa kutawala wala wa vita. Lakini biblia inasema ROHO YA MUNGU ilimjia Sauli kwa nguvu na kumpa moyo wa ujasiri na ushujaa, na kutoka kwenda kuwapiga wamoabu na kuwaangamiza wote kabisa…Lakini jambo pekee ni kwamba hawakuwapiga wakati wa jioni, au wakati wa asubuhi, bali waliwapiga wakati wa JUA KALI linaloangaza…Kuashiria kuwa wao sio WANA WA USIKU bali wa Mchana.. Na kamwe Nuru ya macho yao haiwezi kuzimwa…wala giza haliwezi kuingia kwao.  Hivyo kwa imani waliwaua wakati wa jua kali..

Kama tujuavyo wakati wa jua kali, ndipo watu wanazimia nguvu, ndio wakati watu wanachoka haraka, ndio wakati ambao mwili unapungukiwa maji….Lakini kwa majeshi ya Bwana, hicho ni kinyume chake…wakati wa mchana ndio wakati wa kushinda na kupambana…

Wakati wa mchana(jua kali) ndio wakati wa kuingia vitani, wakati wa mchana ndio wakati wa kwenda kuyavamia majeshi ya adui, wakati wa mchana ndio wakati wa kwenda kuteka nyara, ndio wakati wa kumnyang’anya shetani mateka, wakati wa jua kali ndio wakati wa kuhubiri injili..

Bwana Yesu alisema…

Yohana 9:4 “Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi

5 Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”.

Wakati huu wa jua kali ndio wakati adui yetu kukosa nguvu, ndio wakati anaoungua, ndio wakati ambao anakimbilia kivulini na mafichoni…hivyo ndio wakati wa kumfuata huko kwa vishindo kama Sauli alivyofanya, na kumwangusha na kumnyang’anya mateka sio wakati wa sisi kulitafuta giza au kivuli kama wao.. “Na Yesu ndio Nuru yetu, ndio jua letu..na sisi ni wana wa Nuru, jua lake halituchomi wala halituumizi wala halituchoshi, wala halitumalizi maji mwilini”..linawadhoofisha maadui zetu lakini si sisi.

Isaya 18:4 “Maanaa Bwana ameniambia hivi, Mimi nitatulia, na kuangalia katika makazi yangu, kama wakati wa mwangaza mweupe wa JUA KALI, mfano wa wingu la umande katika hari ya mavuno”.

Ifanye kazi ya Mungu wakati huu wa Neema, wakati huu wa jua kali…usiku unakuja ambao hutaweza…wakati adui atakuwa na nguvu…na wakati huo ni kipindi cha dhiki kuu…wakati ambao neema ya Yesu itafungwa…huo ndio wakati wa mamlaka ya nguvu za giza kutenda kazi..kutatokea dhiki isiyo ya kawaida!. Yule joka atakapopata nguvu…..Bwana atuepushe na hiyo dhiki, ili wakati huo utakapofika utukute tuwe tumeshanyakuliwa na watakatifu wengine kwenda mbinguni kwa baba na tumeshaimaliza kazi yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

USIHUZUNIKE.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

Nuhu alipataje ujuzi wa kuwatambua wanyama wale wote na kuwaweka ndani ya Safina?

JE! UMEFUNDISHWA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

Shalom,

Jina la mwokozi wetu, Mfalme wa Wafalme na Bwana wa mabwana, Yesu Kristo libarikiwe daima. Ni siku nyingine tena hivyo Nakukaribisha tuyatafakari pamoja maandiko.

Neno linasema..

Warumi 10:1 “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.

 2  Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa”.

Kama tunavyoweza kuona hapo kuwa “Juhudi” tu peke yake hazitoshi, kama hatuna maarifa ya kutosha ya kumwabudu Mungu, tutakuwa tunafanya kazi bure.. Na hapa ndipo kundi kubwa la sisi wanadamu tunaposhindwa kumfikia Mungu, tunaishia kuona kama vile Mungu hayupo na sisi japokuwa tunajibidiisha kwake..

Leo tutayatazama makundi mawili  ya watu wa namna hii katika biblia ambao kweli yana bidii kwa ajili ya Mungu lakini sio katika maarifa:

Kundi la kwanza ni lile la watu walio ndani ya Imani ya Kikristo.

Na Kundi la Pili ni lile lililo nje Ya Imani ya Kikristo, lakini linadai kuwa linamtafuta Mungu wa kweli na linampenda.

Tutayatazama yote mawili kibiblia, na ikiwa mimi au wewe, au sote  tunaangukia kwenye mojawapo ya makundi hayo basi tujithamini mapema na kugeuka haraka sana kabla ya kupotea kwetu.

Tukianzana na hili kundi la kwanza ambalo ni la wale walio ndani ya Kristo…

Sasa Katika biblia Kuna mtu anaitwa Martha. Huyu Siku moja alimkaribisha Bwana Yesu kwake. Lakini yeye hakujua Kristo anataka nini, badala yake akawa anajitaabisha na mambo mengine yasiyo na maana sana machoni pa Bwana, mara anakwenda kuosha vyombo, mara anakwenda jikoni kuandaa chakula, mara anachota  maji kwenye majagi kwa ajili ya wageni,  mara anafanya hiki mara kile,..Na kibaya zaidi kilichokuwa kinamkasirisha ni pale anapomwona mdogo wake, Miriamu hajisumbui kwa lolote ameketi tu pale miguuni pake akimsikiliza Bwana..

Martha kuona vile akidhani ni utomvu wa nidhani, akamsemelea kwa Bwana ili aondoke pale..Lakini Bwana akasema..

Luka 10:41 “…. Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi;

42  lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa”.

Sasa huyu ni mfano wa watu ambao wanaobidii kweli kwa ajili ya Mungu lakini si katika maarifa..Wanadhani Mungu anapendezwa na taabu zao na masumbufu yao na huku maagizo ya msingi ya rohoni wanayaacha yawapite..

Leo hii lipo kundi la wakristo, ambao, hawana muda wa kuyatafakari maneno ya uzima ya Kristo, hawana muda wa kusali, hawana muda wa kumwomba Roho Mtakatifu awafundishe mapenzi ya YESU, hawana hata muda wa kuutafuta ubatizo sahihi, lakini kwenye kwaya wapo na wana bidii sana, kwenye ujenzi wa kanisa wapo, na wanajitoa kwa bidii, kwenye michango yote wapo haiwapiti, wako tayari kufanya hiki au kile kwa ajili tu ya Mungu hawaachi, wanajitoa kweli hata usafi wa kanisa ni wenye bidii sana, lakini tukirudi kwenye bible-study tu, huwaoni,..

Ni kweli wanachokifanya si kibaya, wanajuhudi kwa ajili ya Mungu lakini si katika maarifa kama vile Martha..Hivyo mbele za Mungu wanaonekana hawajafanya chochote haijalishi bidii yao ni kubwa kiasi gani. Kwasababu mambo ya msingi wameyaacha. Kwasababu ni heri usiwe unaimba kwaya, ni heri ukawa hufanyi mambo mengine lakini Neno la Mungu unalishika kwa bidii na unalisoma sana na kulichunguza, na umebatizwa, na umepokea Roho Mtakatifu, unaweza ukakosa kitu cha kuchangia lakini ukawa ni mtu wa kusali sana, ukawa ni mtu ambaye haiwezi kupita siku hujajifunza biblia na kuisoma peke yako pasipo kusubiria mtu fulani akuelezee, huku ukimtegemea Roho Mtakatifu akufundishe n.k.

Kundi la Pili: Ni la watu ambao si wakristo, lakini wapo ulimwenguni kote wanadai kuwa wanamuheshimu Mungu.. Na wengi wao ni kweli wanao nia nzuri, na wanaweza wakawa na juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu kuliko hata wewe, lakini mwisho wake, watu wa namna hii, huwa ndio wanakwenda mbali kabisa na mpango wa Mungu, na wakati mwingine wanaiharibu kabisa kazi yake.. Na hiyo yote ni kutokana na kukosa maarifa ya kumwabudia Mungu.

Mfano wa watu hawa ni Mtume Paulo mwenyewe. Yeye kabla ya kumpokea Kristo alikuwa ni mtu mwenye bidii kwa Mungu kweli, lakini kwasababu alikosa maarifa matokeo yake akawa anawaua mpaka wakristo akidhani anamtolea Mungu sadaka (Wafilipi 3:6-7)..Na wayahudi wengine wote ndio walikuwa vivyo hivyo kama yeye.

Wengine walio katika kundi hili ni waislamu..Sio wote unaowaona wanawachinja watu kule Syria na Iraq na Somalia ukadhani hawampendi Mungu..hapana, wengine wanafanya vile kwasababu wanadhani ndio wanamuheshimu Mungu, kama mtume Paulo, kumbe juhudi zao si katika maarifa na hivyo inawafanya wazidi kupotea Zaidi na kwenda kinyume na Mungu, na hata kuwa adui wa Mungu kabisa..Kama vile Neno linavyosema..

Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa..”

Lakini maarifa sahihi yanapatikana wapi?

Ndugu, ni kwanini tunasisitiza sana YESU, YESU, YESU,? Nikwasababu maarifa yote na hekima yote zinapatikana kwake tu (Wakolosai 2:3). Huyo tu, ukimpata, au ukimjua katika usahihi wote, basi ujue kuwa utamwabudu Mungu katika maarifa na sio katika ujinga.

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”

Na Yesu yupo wapi? Jibu ni kuwa Yupo katika NENO lake(biblia)..Hivyo kama wewe ni muislamu au upo katika dini nyingine yoyote, mgeukie Yesu sasa, mwamini yeye, ayaongoze Maisha yako. umwabudu Mungu katika maarifa anayoyataka, ili akufurahie..kwasababu anasema..

Yohana 14:6  “…Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”… Hakuna njia nyingine ya kumfikia Baba isipokuwa kwa kupitia Yesu.

Vilevile na wewe kama ni mkristo lakini bado unasua sua, unaishi kidini dini tu,..kwaya kwako ni muhimu kuliko kulisoma Neno, kutoa sadaka nyingi kwako ni muhimu kuliko kuutafuta ubatizo sahihi na Roho Mtakatifu, Huu ni wakati wako wa kujihurumia, na kugeuka na kuanza kumwabudu yeye katika Roho na Kweli, kwa kujifunza mapenzi yake katika Neno lake (biblia).

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MTANGO WA YONA.

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTAPATAJE RAHA NAFSINI?

Mathayo 11: 28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”

Kama ukiutafakari huo mfano Bwana Yesu alioutoa….utagundua kwamba aliwafananisha watu aliowaona mbele yao na punda wa kubeba mizigo ambao Bwana wao hao punda kawafunga NIRA shingoni na kuwabebesha mizigo waivute huko nyuma. Na kitu kingine Bwana Yesu alichokiona kwa hao punda ni kwamba wamefunga NIRA shingoni ambayo ni ngumu sana, pengine inachubua ngozi ya shingo sana…na sio hicho tu, aliona pia mzigo wanaobebeshwa na Bwana wao ni mkubwa sana, kuliko uwezo wao…Na lililobaya kuliko yote, ambalo naamini ndilo lililomfanya azungumze ni “tabia ya bwana wa hao punda”…kwani alikuwa ni mkali sana na sio mnyenyekevu…pengine alikuwa anawatandika viboko, na alikuwa anawaendesha kwa ukali, na awapi pumziko ni kazi tu mwanzo mwisho..

Hivyo Bwana Yesu kuona vile akawahurumia….akasema maneno yafuatayo..

“Njooni kwangu ninyi nyote(maana yake mwacheni huyo Bwana wetu mje kwangu mimi) msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha…..zingatia hilo neno “nitawapumzisha”..maana yake huko walipokuwepo walikuwa hawapumzishwi, lakini hapa wanaahidiwa Pumziko…Lakini hajaishia hapo tu anaendelea kusema…jitieni nira yangu mjifunze kwangu (maana yake vueni hiyo nira ngumu ya Bwana wenu mvae ya kwangu)..na pia mjifunze kwangu (maana yake mchukue mafunzo yangu ya namna ya kufanya kazi hizo za mizigo)…kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo (sio kama huyo Bwana wenu ambaye anawatumikisha kwa ukali na hana unyenyekevu)..Na Bwana Yesu anamalizia kwa kusema NANYI MTAPATA RAHA NAFSINI MWENU.

Hebu tafakari hilo tukio…Ni sawa na wewe unafanya kazi mahali Fulani ambapo boss wako anakupa mshahara mdogo sana, halafu anakufanyisha kazi nyingi kuliko hata uwezo wako, halafu pamoja na hayo yote, anakuwa mkali kwako na kukunyanyasa…Na kisha anatokea mtu mwingine anakuhurumia anakwambia njoo fanya kazi kwangu, nitakupa mshahara mzuri, nitakupa kazi za wastani, kwakuwa mshahara wangu mimi ni mzuri na kazi zangu si nyingi…na zaidi ya yote mimi ni mpole na mnyenyekevu…nawe utapata raha maishani mwako?…Je utakataa kwenda???..Bila shaka utaondoka kwa miguu yote miwili pasipo kutazama nyuma..

Na ndivyo hivyo hivyo tunapokuwa dhambini…Biblia inasema atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi…maana yake kila ambaye hajampokea Yesu anakuwa chini ya utumwa wa shetani penda asipende…na shetani ni bwana anayetesa, asiye mnyenyekevu, mkali, na nira yake ni ngumu na mzigo wake ni mzito kwa ufupi ni muuaji, yupo kwa maslahi yake akutumie wewe kupata watu wengi wa kuwapeleka jehanamu na mwisho wa siku akumalizie na wewe…

Lakini Bwana Yesu anatokea leo mbele yako na kukwambia mwanangu…utumwa uliotumikishwa na shetani..unatosha, vua hiyo nira, tua huo mzigo…njoo kwangu UTAPATA RAHA NAFSINI..Je hutaki raha??

Hivyo kama hujampokea Kristo leo..huu ndio wakati wa kutua mzigo wako Kalvari…hupendi raha?..kama hupendi sawa unaweza kuendelea kubaki kwenye dhambi…lakini kama unataka raha nafsini mwako..sio wakati wakuichezea hiyo fursa..vua leo hivyo vimini, tupa hizo hereni, hizo lipstick zitupe, hizo suruali ulizokuwa unazivaa acha kuzivaa kuanzia leo…sigara na pombe ulizokuwa unakunywa, uasherati uliokuwa unaufanya wote uweke chini ni mzigo mzito…mfuate Yesu leo..na hakuna haja ya kuhadithiwa wala kusimuliwa baada ya kuviacha hivyo vyote..utaona mwenyewe raha itakayoingia ndani yako…utaona kama ulikuwa umechukuliwa msukule sasa umerudia akili yako timamu…utakuwa huru kuliko maelezo, wala hutatamani kumrudia shetani tena..utajilaumu kwanini hukumgeukia Kristo tangu zamani. Hata sisi tulikuwa hivyo, lakini raha hii tumeionja tukaona ni kweli.

Shetani atakuonea wivu baada ya kumkimbia, atakutishia hivi na vile, lakini usiogope utakuwa chini ya Bwana ambaye si mkali kama shetani wala si mkorofi maisha yako yote…

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

AMEFUFUKA KWELI KWELI.

JE WAKRISTO TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA VALENTINE’S DAY?

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Tukishaokoka tu hatujiishii tu kwenye kujitenga na dhambi, kama vile kuzini, kuvaa nguo za uchi uchi, kuiba, kula rushwa, kutoa mimba, n.k..Sio tu hapo bali pia tunapaswa tuishi maisha ya kujizuia na mambo mengine mengi… Yapo mambo mengi ambayo tunaweza kuyafanya lakini hatujui kuwa yanaweza kuzisonga imani zetu na wakati mwingine tushindwe kuzaa matunda..

Kwamfano rafiki yako wa kidunia anaweza kukwambia naomba nisindikize kwenye birthday ya rafiki yangu, jambo hilo linaweza lisiwe ni dhambi, lakini kabla ya kufikiria kufanya hivyo jiulize?, Je! Ni faida gani na hasara gani utapata kwenye shughuli kama hizo?..Faida inaweza ikawa ni kula na kucheka, lakini tusijidanganye, hasara rohoni zitakuwa ni nyingi kuliko faida? Ukitoka pale ndio utajua.

Au Kuna tamthilia fulani kwenye Tv, halafu unasema haina shida, ni burudani, lakini ukweli ni kwamba, akili yako yote itahamia kule, kitu kitakachokupa furaha ni pale unapoikumbuka ile tamthilia ilipoishia..Na hivyo unakuwa mtumwa wa hiyo.

Au Unaunga urafiki na kila mtu wa mtaani kwako, hata wale waovu, wewe kila mtu tu ni rafiki Kwanini usichague kuishi nao kama majirani, wa kusalimia na kujuliana hali, mpaka ijiingize ndani muwe marafiki, mkutane kila siku mjadili mambo mengine ambayo hata sio ya maana?.

Una magroup kama 50 ya kuchat whatsapp, kuanzia ya shule ya chekechea, mpaka chuo, magroup mpaka ya marafiki wa mtaani, mpaka ya michezo na ya vichekesho vya kila namna..Hayo yote yanakusaidia nini, rohoni? Lakini group la kujifunza biblia unalo moja tu..Akili yako inaposongwa na mambo mengi inaisonga ile mbegu ya Mungu iliyopandwa au inayopandwa ndani yako isikue (sawa na ule mfano Bwana Yesu alioutoa wa mbegu zilizopandwa kwenye miiba, ambazo zilisongwa na shughuli na hazikuzaa)

Kabla ya kwenda kuzurura huku na huko vijiweni ulishawahi kujiuliza kuna umuhimu gani wa kwenda huko?

Tukiishi maisha ya namna hiyo ya kutojizuia biblia inatuambia.. hatutaipokea tuzo kamwe tuliyowekewa mbele yetu.

1Wakorintho 9:24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

25 Na kila ashindanaye katika michezo HUJIZUIA KATIKA YOTE; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika”.

Unaona Mtume Paulo anaendelea kusema…

“26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Si kila kitu cha kuvutia tunapaswa tukijaribu, ni lazima tujifunze kujizuia, kama vile wanamichezo, na kuchagua vipi vya kuchukua na vipi vya kuacha.. ili kusudi kwamba tupate muda mwingi wa kutumia kumtafakari Mungu, na kusali, na kufanya ibada..Vinginevyo wakati wote tutaona ratiba imesonga, muda ni kidogo wa kujihusisha na mambo ya msingi ya wokovu wetu.

Ndio hapo Utashangaa unapojaribu kwenda mlimani au sehemu yako faragha kusali mara marafiki wanakupigia simu, wanakuuliza upo wapi, tunataka tuje? Mara muda wa tamthilia umefika unawaza umalize ibada haraka haraka uende ukaangalie(mawazo yako yote yapo kule), mara unafungua whatsap ili ukaangalie ni nini kinaendelea huko, na kwenye lile group lako moja la Neno ulilojiunga, hapo hapo message kama 200 zinaingia kutoka magroup mengine tofauti tofauti, yanakuvutia usome hizo message jiulize utapata wapi muda wa kulitafakari vizuri Neno la Mungu?.

Hivyo muda wako utakuwa ni wasongwa songwa tu hivyo daima.

Chagua marafiki tu wachache wa karibu, hao wengine kama wanaulazima wabakie kuwa marafiki wa mbali ambao hawawezi kujishikamanisha na wewe muda mwingi..Pia Acha kufuatilia movie na thamthilia za Kikorea na nyinginezo kwenye TV, ziache zipite,dunia hii inapita ndugu (na hayo ma-movie na matamthilia karibia yote yana maudhui ya kipepo, kuyafuatilia ni kujiongezea idadi ya mapepo tu maishani mwako.)… Left magroup yote yasiyo na maana, bakiwa na yale ya kujifunza Neno la Mungu,.na ya familia…Group la watu wa shule ya msingi ulilosoma miaka 10 au 20 huko nyuma linakusaidia nini kwasasa?..labda lingekuwa na maana kwako kama ungekuwa huna jukumu lingine la kuutafuta uso wa Mungu, lakini kwasababu umepewa jukumu lingine na mamlaka iliyo juu…hilo group la shule ya msingi ondoka, kwasababu linakuchukulia muda wako na ilihali huo muda ungeutumia kusoma biblia…Mbona kabla ya hii mitandao ulikuwa unaweza kuishi na ulikuwa na furaha tu..kwanini sasahivi ushindwe?

Futa mazoea na baadhi ya watu unaoishi nao mtaani, abakie kuwa jirani mwema kwako basi, lakini kuingiliana maisha futa uhusiano huo, sio lazima ujiunge vijiweni mwao..wala usiogope kwamba siku ukipata matatizo hawatakusaidia…(Bwana ndiye ngome yetu na kimbilio letu hatuna hofu na wanadamu, Waebrania 13:6), tunapomtii Mungu na yeye anakuwa upande wetu na si upande wa Adui.

Na baada ya kufanya hayo…utakuwa umeuokoa muda mwingi sana sasa utumie huo muda wako ulioupata, kuomba, kusoma biblia, kujifunza Neno la Mungu kwa bidii, kufanya ibada, nakuambia ukijijenga utamaduni huo licha tu ya kuwa utapata amani Fulani moyoni lakini pia utamwona Mungu maishani mwako kwa namna isiyokuwa ya kawaida. Atajifunua kwako.. Matokeo yake Utakuwa kiroho kwa haraka sana na kwa kasi, mpaka kumzalia Mungu matunda ndani ya kipindi kifupi sana..Lakini tukiyaendekeza maisha ya kutojizuia, miezi, itaenda, miaka itaenda, tutakuwa wale wale wachanga, ambao ni rahisi kuchukuliwa tena na ibilisi.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

KWANINI USIICHAGUE TUZO ISIYOHARIBIKA?

NI NANI ALIYEWALOGA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

RAFIKI WA KWELI NI YUPI?

Rafiki wa kweli ni mmoja tu naye ni YESU..Leo tutatazama ni kwanini!.

Ni rahisi kujitoa kwa ndugu yako wa damu, kujitoa kwa mali na hali….hata wakati mwingine kujitoa hata uhai kwaajili ya ndugu yako wa damu, hilo linawezekana pia…Ndio, wengi wapo radhi wafe ili watoto wao waishi, wapo radhi wao wapitie shida nyingi na dhiki lakini wadogo zao, au wazazi wao wasipitie hizo dhiki. hilo kundi la watu lipo, tena idadi yake ni kubwa sana…

Lakini kuwapata watu ambao wanaweza kuutoa uhai wao kwaajili ya “rafiki zao”, ni wachache sana, kama sio hawapo kabisa..

Kwanini ni ngumu?..kwasababu Ndugu ni bora mara nyingi kuliko rafiki, Baba ni bora kuliko rafiki, mtoto ni bora kuliko jirani rafiki, mama ni bora kuliko rafiki n.k..kwasababu rafiki haaminiki leo anaweza kuwa rafiki yako mzuri kesho akawa adui yako tena mbaya sana…Sifa hiyo ya rafiki ndiyo inayoficha thamani ya urafiki usiwe na nguvu kuliko cha ndugu wa damu.

Lakini endapo akitokea mtu ambaye atakuwa tayari kuutoa uhai kwake kwaajili ya rafiki zake…Yaani yeye yupo tayari kufa ili tu rafiki zake wasife!…bila shaka huyo mtu atakuwa ni wakipekee sana..Kwasababu japokuwa anaujua unafiki wa marafiki lakini yupo tayari kuutoa uhai wake hivyo hivyo, hata kama anajua hao marafiki wanaweza kuja kumsaliti au kumkana baadaye.. Hakika huyo atakuwa zaidi ya rafiki…Upendo wake utakuwa umepita upendo wa ndugu..

Na huyo si mwingine zaidi ya Yesu..ambaye alikubali kuutoa uhai wake kwa sisi rafiki zake, ambao ni vigeugeu..Ndio!..alijua Petro atakwenda kumkana masaa machache tu mbeleni lakini alikubali kuutoa uhai wake kwaajili yake hivyo hivyo…Alijua Yuda anakwenda kumsaliti masaa machache tu mbele lakini alimwita rafiki..(kasome Mathayo 26:48-50).

Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.

15 Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu”.

Je bado tu hujamwona rafiki wa kweli?..Yeye mwenyewe anasema HAKUNA ALIYE NA UPENDO MWINGI KULIKO HUU, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake…(Kuutoa kwa Ndugu ni rahisi lakini si rafiki).

Mimi siwezi kuwa rafiki yako wa kweli, wala yule rafiki yako wa karibu sana hawezi kuwa rafiki yako kwa kiwango hicho cha kufikia kuutoa uhai wake kwaajili yako…Je! huyo rafiki yako ukijua kwamba kesho atakusaliti ufe, je utaendelea kumpenda leo?..bado utaendelea kumwita rafiki??…

Au je rafiki yako akijua kwamba kesho utamrusha ataendelea kukuita leo rafiki? Si atakuchukia na kukuita mnafiki..je! yupo tayari kufa kwa ajili yako?..kama haweza basi sio rafiki wa kweli..ni rafiki tu! Lakini si rafiki wa kweli.

Rafiki wa kweli yupo mmoja tu…ambaye hata sasa japokuwa upo mbali naye bado anakupenda, na alishakufa kwaajili yako..

Mithali 18:24 “…. Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu”.

Hivyo msogelee huyu rafiki aitwaye YESU, yeye si mnafiki, haweki kinyongo, wala hasitisiti..amekupenda amekupenda!!..hana kusitasita..Na anamaanisha kuhitaji kuyaokoa Maisha yako.

Usimdharau, Mpe maisha yako leo kama hujampa…na utapata mema, na siku ya mwisho atakufufua na atatufufua wote tuliomwamini na kumpokea…Maana alisema mahali atakapokuwepo ndipo na sisi tutakapokuwepo.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

JIRANI YANGU NI NANI?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UZAO WA NYOKA.

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

BASI, JIANGALIENI MIOYO YENU ISIJE IKALEMEWA NA ULAFI, NA ULEVI.

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MIJI YA MAKIMBILIO.

Wana wa Israeli walipoingia katika nchi ya Ahadi, Na kuigawanya ile nchi, Makabila yote yalipewa Urithi wa ardhi isipokuwa kabila la Lawi, Wao waliganywa katikati ya makabila mengine yote 11 yaliyosalia..  Kati ya makabila hayo ilitengwa miji 48, sehemu tofauti tofauti kwa ajili ya Wana hawa wa Lawi.

Lakini kati ya miji hiyo 48, Ilitengwa miji 6 maalumu, ambayo iliitwa “miji ya makimbilio”…Miji hiyo haikuwa sehemu moja bali  ilikuwa imezagaa karibia  taifa zima. Miji hiyo ilitengwa mahususi kwa ajili ya wale watu ambao walifanya makosa ya uuaji yasiyokuwa ya makusudi, kwa wageni wa wenyeji..(Soma Hesabu 35:1-8)

Ikumbukwe kuwa katika torati ya Musa, ilikuwa ni kosa linalostahili kifo, ikiwa utamua mtu mwenzako, (Kutoka 21:14), hata moja ya zile amri 10 ilikataza tendo hilo.. Sasa mtu yeyote ambaye alipatikana na kosa la mauaji, ilikuwa ni lazima auawe kulingana na sheria au,auawe na mlipiza kisasi.

Lakini pamoja na hayo yapo makosa ambayo yalijulikana sio ya makusudi kwamfano, wakati mwingine labda wanakata magogo maporini na kwa bahati mbaya shoka likamponyoka mmojawao na kwenda kumpiga mtu mwingine ikampelekea mauti, sasa kosa kama hilo ni la bahati mbaya, kwasababu huyo hakukusudia kuua ni bahati mbaya tu (Soma Kumbukumbu 19:5)..Hivyo sheria inaweza isimuhukumu lakini “mlipiza kisasi” labda ndugu yake yule aliyeuliwa anaweza akalipiza kisasi kwa tendo hilo na isiwe ni dhambi. Sasa mtu kama huyu nusura yake ili apone..Ilikuwa ni sharti akimbilie kwenye mojawapo wa miji hiyo sita iliyotengwa.

Miji hiyo iliwekwa karibu na miji yote, kiasi kwamba mkimbizi, atatumia mwendo wa siku moja tu au chini ya hapo, kuufikia mmojawapo wa miji hiyo.. Vitabu vya kihistoria vya kiyahudi vinasema  njia za kuelekea miji hiyo zilikuwa ni pana, zilizochongwa vizuri, bila mabonde, au miinuko yoyote, ili kumsaidia mtu huyo afikie miji hiyo kwa haraka bila kipingamizi chochote, na pembeleni kunakuwa na kibao kimeandikwa ‘Miklat’ yaani “Makimbilio”

Sasa anapofika malangoni mwa miji hiyo, anakutana na wazee wa mji pale,(Ambao ni walawi). Anawaeleza tatizo lake, (kwamba ameua pasipo kukusudia), ndipo wale wazee wanampa hifadhi. Na wale washitaki wake watakapokuja na kuwaomba wazee  wamtoe wamuue wale wazee hawatawaruhusu..kulingana na torati.

Mtu huyo ataendelea kubaki huko mjini mpaka kuhani mkuu atakapokufa (kasome Yoshua 20:6) ndipo atakapokuwa huru kurudi katika nchi yake mwenyewe. Lakini akiondoka ndani ya mji ule kabla ya kuhani mkuu kufa, wale walipiza kisasi wakimwona wakamvizia na kumuua, wale watu waliomuua hawatashitakiwa kwa mauaji yale.(watakuwa hawana hatia kwa watakachokifanya)..Kwahiyo huyo mtu hataruhusiwa hata kwenda kuwasalimia ndugu zake nje ya mji, wala kwenda kununua chochote, wala kutalii..atabaki humohumo…mpaka kuhani mkuu atakapokufa ndio atakuwa huru kutoka.

Yoshua 20:1 “Kisha Bwana akanena na Yoshua, na kumwambia,

2 Nena wewe na wana wa Israeli, uwaambie, Haya, toeni hiyo miji ya makimbilio, ambayo niliwaambia habari zake kwa mkono wa Musa;

3 ili kwamba mwenye kuua mtu, aliyemwua mtu awaye yote pasipo kukusudia, na pasipo kujua, apate kukimbilia kuko; nayo itakuwa ni mahali pa kukimbilia kwenu, kumkimbia huyo ajilipizaye kisasi cha damu.

4 Naye ataikimbilia miji hiyo mmojawapo, naye atasimama hapo penye maingilio ya lango la huo mji, kisha atanena neno lake masikioni mwa wazee wa mji; nao watamtia kwao ndani ya mji, na kumpa mahali, ili apate kukaa kati yao.

Hivyo ndivyo watu waliofanya makosa ya uuaji usio wa makusudi walivyonusuka Israeli..

Je! Habari hiyo inafunua nini katika agano jipya?

Sisi tumepata neema iliyo kubwa zaidi ya hao, sio tu wanaofanya dhambi za bahati mbaya ndio wanaopata neema ya wokovu kama hao .Hapana, bali sasa hivi ni wote waliofanya dhambi..ziwe za bahati mbaya au makusudi, Mungu ametupa MJI WA KUKIMBILIA, nao ndio  huo “kuwa ndani ya KRISTO”..

Haijalishi umeua watu wengi kiasi gani kwa makusudi, umetoa mimba nyingi namna gani, umeloga watu wengi vipi, umezini nje ya ndoa mara nyingi kiasi gani, umejibadilisha maumbile yako, umekuwa shoga, umekuwa msagaji, anaiba, unatapeli.. Mambo ambayo unajua kabisa unastahili ziwa la moto leo hii, unastahili kuuliwa na Mungu, unastahili hukumu wakati huu..

Lakini Bwana anakupa nafasi nyingine, ambayo itakuwa ni salama yako..Nayo ni msalabani.

Hakuna sehemu nyingine yoyote utakayoweza kuepuka hukumu isipokuwa kwa Yesu ndugu yangu. Hizo dhambi zako huwezi kuzificha ili usihukumiwe, kama leo hii hutayasalimisha maisha yako kwa Bwana Yesu.

Nje yake, ni HUKUMU tu  wala hakuna kingine..Ukifa leo katika hali uliyopo, fahamu kuwa hakuna msamaha milele, Vilevile ukiendelea kuishi katika maisha hayo ya dhambi fahamu kuwa ibilisi mshitaki wako anakuwinda usiku na mchana akuangamize.. Anakupangia mipango mingi kwasababu anajua unastahili hukumu kwa hizo dhambi zako nyingi..Hawezi kukuacha kukufuatilia maadamu anakuona bado upo nje ya Kristo. Biblia inasema shetani ni mshtaki…maana yake anafananishwa na huyo mlipiza kisasi Habari zake tulizozisoma hapo juu.

Kimbilia kwa YESU, ndiye Kuhani mkuu leo..

Vilevile na wewe ambaye upo tayari ndani ya wokovu, baki huko huko usifikirie hata kidogo kurudi kwenye ulimwengu..Kama vile tunaona wale ambao walitoroka kabla kuhani mkuu hajafa, walijiweka wenyewe hatarini kuuliwa na walipiza kisasi wao..Nawe pia usijaribu kufanya hivyo, dhambi ulizomfanyia Mungu huko nyuma zinatosha,.Usitoke nje ya mji wa Yesu wa makimbilio.

Na katika Habari hiyo makuhani wakuu walikuwa wanakufa ndipo mtu yule aliyeua bila kukusudia awe huru kurudi kwenye mji wake wa zamani…Lakini sasa hivi kuhani mkuu wetu YESU HAFI MILELE!!…Yupo…na maadamu yupo hai, hatupaswi kutoka nje ya uzio wake tusije tukafa.

Na kitu kingine cha kipekee ni kwamba….Ndani ya hiyo miji sita ya makimbilio…ilikuwa ni miji ya raha, haikuwa ni miji ya shida, kwasababu ilikuwa ni miji makuhani wa Bwana wanaishi..hivyo hakukukauka chakula, zaka zote na baraka zote wana wa Israeli walizokuwa wanamtolea Mungu, za mashambani na katika shughuli zao zote walikuwa wanazipeleka kwenye hii miji..Hivyo ilikuwa ni miji ya baraka, neema na rehema…aliyekimbilia kule aliishi Maisha yake yote bila shida!..kwani ni miji iliyobarikiwa, mtu huyo hawezi kamwe kupungukiwa na chochote kile iwe mavazi, chakula wala mahitaji mengine yoyote..lakini pia ilikuwa ni miji mitakatifu sio ya anasa, kwasababu ndio watumishi wa Mungu (makuhani wa Bwana) walikuwa wanakaa huko.

Kadhalika na leo ndani ya milki ya Yesu ambaye ndie Kuhani mkuu wetu, ni mji mtakatifu, wote wanaomkimbilia yeye wanakaa salama, wanatunzwa na kuhifadhiwa Maisha yao yote. Huoni hizo ni baraka za ajabu?

Ikiwa hujatubu na leo upo tayari kumkabidhi Kristo maisha yako kwa Bwana. Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

JE KUJIUA NI DHAMBI?

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.

Bwana Yesu sehemu nyingi aliifananisha baadhi ya mifumo ya maisha yetu na ufalme wa mbinguni…Kwamfano utaona alisema ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta lulu nzuri; naye alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua (Mathayo 13:45).

Maana yake ni kwamba injili au Neno la Mungu pia limeandikwa katikati ya maisha yetu…

Yupo mtu mmoja aliufananisha ufalme wa mbinguni na sayari iliyo mbali sana….ambayo kwa mbali inaonekana ndogo sana kama nyota…lakini isogelewapo na kukaribiwa zaidi ni kubwa mno yenye uwezo wa kubeba viumbe vyote vya ulimwengu….Au kama ndege iliyo mbali sana angali, ambapo tukiwa huku chini tunaweza kuiona ni ndogo sana kuliko kalamu…lakini ishukapo chini ni kubwa yenye uwezo wa kubeba watu wengi na mizigo yao..

Hali kadhalika ufalme wa mbinguni unaonekana ni mdogo sana ukiwa mbali na mtu au watu…lakini ushukapo chini au ukaribiwapo ni mkubwa san ana wenye uwezo wa kubeba watu wengi na mizigo yao.. Hiyo yote ni mifano ya maisha ambayo imebeba injili ya Mungu ndani yake.

Upo mfano mwingine wa kimaisha ambao tunaweza kuutafakari kwa pamoja….ambao huo utaweza kutusaidia kumjua Mungu zaidi na ulinzi wake kwetu…

Hebu tafakari zile hifadhi za taifa kule porini, ndani yake kuna wanyama wengi, wanaishi…lakini wote wanalindwa na mamlaka kuu ya serikali pasipo wao kujijua, ushwari wa wao kuishi bila kuuawa na majangili inatokana na kazi ngumu askari wanazozifanya usiku na mchana kuzizunguka hifadhi hizo…ipo mipaka ambayo wananchi hawaruhusiwi kuisogelea kabisa licha ya kuiingia.

Na watoto wa Mungu wanakuwa wapo kwenye hifadhi ya Mungu…wanalindwa na serikali ya mbinguni…Malaika wanahakikisha kwamba hakuna pepo lolote linaloingia ndani ya mipaka hiyo na kuwadhuru…tunaweza tusiwaone malaika kwa macho siku zote za maisha yetu, lakini wapo wanatulinda..

Lakini kama tunavyojua mnyama yoyote akitoka nje ya ile hifadhi, usalama wake unapotea kwasababu huko nje majangili wapo na maadui wengi…hali kadhalika wanyama wanaoishi katikati ya wanadamu kifo chao hakithaminiki…mbwa wa kawaida halindwi na akifa anaonekana kama uchafu tu…lakini mbwa mwitu mmoja akifa ni hasara kubwa kwa Taifa. Wana thamani kubwa sana kwa taifa..na hakuna nchi inaweka nembo yake ya taifa mnyama wa kufugwa, utaona mara nyingi ni wanyama waliopo kwenye hifadhi za Taifa.

Hivyo na sisi tukitaka tusiishi maisha ya mashaka, maisha ambayo hayana usumbufu, yaliyokusudiwa kuishi mwanadamu…maisha ya ulinzi, maisha ya kuthaminika na mamlaka ya mbinguni, hatuna budi kuingia ndani ya “hifadhi ya Mungu (yaani ya mbinguni)”…Malaika kazi yao ni kuwahudumia tu wateule wa Mungu kasome waebrania 1:14, hakuna askari wa hifadhi anashughulika na mbwa wa kufuga (sehemu yao ni ndogo sana)…lakini wanakesha kwa wanyama wa hifadhini…Na malaika wa Mungu ni hivyo hivyo, wanakesha kuwalinda na kuwahudumia watakatifu.

Hakuna malaika anayetumwa kwenda kumlinda mwasherati asife, hakuna malaika anayetumwa kwenda kumlinda muuaji asikamatwe, au mtukanaji asiwindwe na wachawi n.k

Kwahiyo tunapokaa chini ya hifadhi ya Kristo ndio tunajipandisha thamani..Na hifadhi ya Mungu inazungukwa na mipaka ya Neno la Mungu…unapomwamini Yesu Kristo na kutubu dhambi zote na kubatizwa tayari unakuwa chini ya mamlaka ya mbinguni…shetani hawezi kukusogelea tena….na unapozidi kutoikaribia na kutoivuka ile mipaka ndivyo unavyozidi kuwa salama…Neno la Mungu linasema usiibe, usizini, usiue, usile rushwa n.k. Hiyo ndiyo mipaka.

Kama hujamwamini Yesu unasubiri nini?..mlango wa neema upo wazi, lakini hautakuwa hivyo siku zote…Tubu leo mgeukie Yesu, hizi ni siku za mwisho, na Yesu anakaribia kurudi. Fanya bidii ili uingie katika hifadhi ya Mungu.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

Tofauti kati ya kuungama na kutubu ni ipi?

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Rudi Nyumbani:

Print this post

BIBLIA TAKATIFU.

Biblia takatifu ni kitabu kilichobeba maneno ya Mungu katika mfumo wa maandishi..Kitabu hichi kimebeba taarifa muhimu zote zinazomhusu mwanadamu…biolojia ya mwili wake, mwanzo na mwisho wa milki yake..Biblia takatifu ndio kitabu pekee kinachompa mwanadamu kalenda yake ya miaka inayokuja mbele yake.

Biblia ni kitabu kitakatifu…ndio maana inaitwa “biblia takatifu”… sasa sio karatasi yaliyokiandikia ndio matakatifu, au wino uliotumika kuandikia ndio mtakatifu wala jalada lililotumika…hapana, bali kilicho kitakatifu ni maneno yaliyoandikwa mule ndani.. Kwahiyo kitabu hicho kikitumika kwa akili ya damu na nyama..ya kuamini kwamba makaratasi yale na wino ndio matakatifu hakina manufaa yoyote kwa mwanadamu.

Tukiitumia biblia na kuiweka kifuani mwetu tukiamini kuwa itaondoa matatizo yetu hatutanufaika na chochote, tukiichukua biblia na kwenda kutolea nayo pepo hatutanufaika chochote, tukiichukua biblia na kuiweka kichwani usiku kama mto ili wachawi au mambo mabaya yasitupate hatutaambulia chochote. Ni sawa na mgonjwa anayeumwa kichwa na kuichukua dawa ya panadol na kuiweka kifuani, au kichwani kama mto akiamini itamtibu ugonjwa wake.

Au ni sawa na mtu anayechukua kitabu cha upishi (kinachoelezea hatua ya upishi)..na kukipeleka hicho kitabu jikoni mbele ya masufuria na majiko kimpikie…Unaona kitabu hakiwezi kupika haijalishi kimehakikiwa na mtaala wa nchi, na kupewa daraja la kwanza. Ili kitabu hicho kiwe na manufaa ni sharti aliyenacho akisome, ile elimu iingie kichwani mwake, kwa ile elimu ndipo aitumie kupika.

Vivyo hivyo na biblia takatifu ili iwe na manufaa kwetu, ni lazima tuyasome yale yaliyoandikwa mule ndani, tupate elimu ya kutosha..ndipo ile elimu tuitumie katika kumpendeza Mungu, kumshinda adui, kupata Baraka na mafanikio.

Biblia takatifu ni kitabu cha maarifa, hekima, na mashauri. Hakuna kitabu chochote chenye mashauri bora na hekima zilizo kuu kuliko biblia.

Kwamfano hebu itafakari hii hekima..

Luka 12:23 “Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.

24 Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana ghala wala uchaga, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!

25 Na yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

26 Basi, ikiwa hamwezi hata neno lililo dogo, kwa nini kujisumbua kwa ajili ya yale mengine?

27 Yatafakarini maua jinsi yameavyo; hayatendi kazi wala hayasokoti; nami nawaambia ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

28 Basi, ikiwa Mungu huvika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatawatendea ninyi zaidi, enyi wa imani haba?”

Biblia takatifu ndio katiba ya wanadamu. Kwa kutumia katiba mtu anaweza kuhukumiwa na anaweza kupatiwa haki yake. Na kama vile jinsi ilivyo kwamba hakuna mtu aliye juu ya katiba ya nchi..Hata Raisi wa nchi hawezi kuivunja katiba…kadhalika Biblia ni katiba ya wanadamu..hakuna mwanadamu yoyote wala malaika anayeweza kuvuka mipaka ya maneno yaliyoandikwa ndani ya kitabu hicho (yaani biblia takatifu)..Zaidi ya yote hata Mungu mwenyewe hawezi kulivunja Neno lake…Kwamfano alisema hataiangamiza tena dunia kwa maji…haiwezekani hata siku moja akalivunja hilo neno na kuiangamiza dunia kwa gharika…Naam dunia itaadhibiwa kwa kitu kingine kama maandiko yanavyosema katika kitabu cha Petro lakini si kwa maji tena…Na hiyo ni kwasababu analishika Neno lake alilolisema.

Alisema pia yoyote amwaminiye mwanawe mpendwa YESU KRISTO, Ataokoka na hukumu ya milele, na asiyemwamini atahukumiwa…Hilo Neno hawezi kamwe kulibadilisha kwamba..baadaye ageuke na kusema “hapana wote watakaomwamini hawatapata uzima wa milele” wala hawezi kulitangua neno lake alilosema kwamba “wote wasiomwamini watahukumiwa”..Neno lake litabaki palepale..mbingu na nchi zitapita lakini maneno yake yatabaki yale yale.

Biblia takatifu ni maneno ya Mungu yenye ujumbe pia wa maonyo na ahadi. Hakuna kitabu kingine chochote chenye ahadi, kitabu cha fizikia hakina ahadi yoyote, kitabu cha saikolojia hakina ahadi yoyote ndani yake, kitabu cha hisabati hakina ahadi yoyote ile, lakini biblia takatifu imejaa ahadi zilizo thabiti mpaka za vizazi vijavyo vya watoto wetu, mifugo yetu, mali zetu na hata maisha ya ulimwengu ujao.

Bwana atusaidie kulishika Neno lake na kuliheshimu, kwa faida yetu wenyewe hapa duniani na kwa maisha yanayokuja baada ya haya.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

KITABU CHA UZIMA

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

Shalom,

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima. Karibu tena tujifunze maneno ya uzima wa milele.

Yohana 1:35-39 inasema..

“Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake. 36 Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!

37 Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

38 Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?

39 Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI”.

Unaweza ukajiuliza kulikuwa na umuhimu gani kwenye Habari hii kutoa muda ambao Yesu aligeuka na kuzungumza na wale wanafunzi wawili..?Ambao muda wenyewe ulikuwa ni saa kumi?..Ulishawahi kujiuliza umuhimu wa huo muda kuwekwa pale?. Wakati mwingi tunaweza kuona ni kawaida tu lakini, kila jambo lina sababu yake,.

Tukiitafakari tangu juu Habari hiyo utaona wanafunzi hao ambao mmojawapo alikuwa ni Andrea, walipoonyeshwa tu Yesu na Yohana mbatizaji , mara moja waliacha kumsikiliza Yohana na kuanza kumfuata Bwana kwa nyuma tena kimya kimya…

Hawakusubiri apotelee mbali kwasababu kumbuka wakati huo Yesu alikuwa anakatiza njiani, pengine alikuwa anatembea kwa mwendo wa kasi kidogo hatujui, lakini hawakumwacha apotee mbele ya macho yao.. waliendelea kumfuatilia hivyo hivyo mpaka wajue anapokaa, japo biblia haijaandika ni kwa muda gani waliutumia kumfuatilia , pengine jambo hilo lilianza majira ya asubuhi labda kwenye saa nne nne hivi , au saa 6, au saa 7 hatujui.. Lakini walimfuatilia kwa muda tu.

Hawakujua kuwa Bwana alishagundua kuwa kuna watu wawili wanamfuatailia kwa nyuma tangu mbali..wao hawakuligundua hilo, walidhani Bwana bado hajui chochote..

Ghafla tu majira fulani yalipofika kwenye saa kumi alasiri wakashangaa Bwana amewageukia, na kuwauliza.. ,

Mnatafuta nini? Pengine kwa hofu kidogo hawakuwa na cha kusema.. wakajibu Rabi unakaa wapi?.. Ndipo Bwana akawachukua na kwenda kuwaonyesha anapokaa, wakakaa naye siku ile yote..

Hiyo ilikuwa ni saa kumi alasiri Kabla jua halijazama walimpata Yesu.

Ndugu mpendwa,

Biblia inatuhimiza kuwa tutafute nasi tutaona kwasababu kila atafutaye ataona..

Leo hii unaweza ukawa unamtafuta Kristo, unaonyesha bidii kujifunza Neno lake, unafuata nyendo zake, nakwambia haijalishi itakugharimu muda mrefu kiasi gani kumtafuta, lakini ni uhakika kuwa kabla jua lako halijazama utamwona Kristo. Kristo hawezi kuruhusu mpaka giza liingie bado upo tu katika hali hiyo hiyo ya kumtafuta yeye. Hayupo hivyo..alisema kila atafutaye ni lazima apate.

Siku moja moja atajidhihirisha kwako, atajifunua kwako, kwa namna ambayo hakuifanya hapo mwanzo.

Watu wengi leo hii wamekata tamaa, kumtafuta Bwana, kisa miezi imepita, miaka kadhaa imepita, hawaoni Mungu akichua hatua yoyote maishani mwao? Hawajui kuwa, Bwana alishaona bidii yako ya kumtafuta Kristo tangu zamani, Lakini muda wako wa saa kumi ulikuwa haujafika..

Mtazame, Simeoni, yeye alikuwa ni mtu mwenye haki, lakini Mungu alimwambia kabla hujafa, utamwona Masihi.. Kati ya mabilioni ya watu waliokuwa duniani wakati ule, yeye ni mmoja kati ya watu wachache sana waliomtambua Kristo kuzaliwa kwake(Luka 2:25).

Hakuna mtu anayemtafuta Mungu, Mungu akamwacha, asijifunue kwake.

Lakini Saa kumi yako itafika tu, siku fulani, wakati fulani, majira fulani..Atakugeukia, na kujifunua kwako kwa namna isiyo ya kawaida, Na atakufahamisha mengi sana.

Usikate tamaa.

Luka 11:9 “Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; TAFUTENI, NANYI MTAONA; bisheni, nanyi mtafunguliwa.

10 Kwa kuwa kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

11 Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?

12 Au akimwomba yai, atampa nge?

13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni HATAZIDI SANA KUWAPA ROHO MTAKATIFU HAO WAMWOMBAO?”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

MTANGO WA YONA.

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

KUWA WEWE.

Rudi Nyumbani:

Print this post