Title February 2022

Walakini ataokolewa kwa uzazi wake.

SWALI: Biblia inaposema mwanamke ataokolewa kwa uzazi wake, inamaanisha nini?

1Timotheo 2:14 “Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.

15 Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi”.


JIBU: Tofauti na inavyotafsiriwa na watu wengi, kwamba andiko hilo linamaanisha kuwa mwanamke yeyote ambaye atakuwa na watoto wa kulea, basi mwisho wa siku ataokolewa kwa kutimiza tu kusudi hilo.  Mtazamo ambao sio sahihi na unakinzana na maandiko, Kwasababu kama kila mwanamke angekuwa anaokolewa kwa namna hiyo, hata wanawake wachawi nao wangeokolewa kwasababu na wao pia wanao watoto wa kulea.

Lakini biblia ilimaanisha nini kuandika hivyo? 

Mtume Paulo aliandika maneno hayo, kuonyesha jinsi gani huduma ya mwanamke ambaye ana watoto jinsi ilivyo na nguvu hata kusababishia wokovu kwake mwenyewe IKIWA atawalea watoto wake katika misingi ya imani, upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi kama ilivyoainishwa hapo..Na sio kwa kuzaa tu basi.

Kwasababu atakuwa ameifanya huduma ya kuokoa kizazi kingine.. Tengeneza picha kama wanawake wote ulimwenguni wangekuwa wanatimiza wajibu wao huu wa kuwalea watoto wao katika misingi ya imani, leo hii, kusingekuwa na haja ya kuhubiri injili kwasababu watoto wote wangekuwa tayari wanamjua Mungu. Lakini injili imekuwa ngumu kwa kizazi cha sasa kwasababu jambo la kwanza mzazi analolithamini kwa mtoto wake ni elimu tu, Mungu ni ziada, mtoto akifaulu darasani ndio furaha yake kubwa, wakati hajui hata mstari mmoja wa biblia. Hajui hata pambio moja la kumsifu Mungu. Mzazi haoni aibu hata mtoto wake anakuwa hadi mtu mzima hajui biblia ina vitabu vingapi.

Kwahiyo hapo mtume Paulo alikuwa anaonyesha nguvu iliyopo katika mwanamke kulea watoto wake vema, ambayo mwisho wa siku itampelekea hata na wokovu wake mwenyewe. Kwamfano Mungu akiona mtoto Yule ambaye alilelewa katika misingi kama Samweli, amekuwa sababu ya wokovu kwa Israeli, unategemea vipi Mungu amwache mama aliyemlea?. Ni sawa tu na yule anayewavuta watu kwa Kristo, ambao biblia inasema kitendo hicho kina nguvu ya kuokoa roho ya mhubiri na kufunika wingi wa dhambi zake.

Yakobo 5:20 “jueni ya kuwa yeye amrejezaye mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na kufunika wingi wa dhambi”.

Kwahiyo ikiwa wewe ni mwanamke na Mungu kakujalia watoto ujue jukumu lako la kwanza, la injili ni kwa watoto wako, hakikisha hao wanakuwa katika misingi ya kumcha Mungu, wafundishe, na pale wanapokosea Mungu kakupa ruhusu ya kuwaadhibu, lengo ni kuwaweka katika mstari wa kumcha Bwana, na sio kuwatesa. Ukifanya hivyo matokeo yake utakuja kuyaona baada ya haya maisha hapa duniani.

Tito 2:4 “ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

Tusome,

Kutoka 3:5 “Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.

Viatu Musa alivyoambiwa avivue ni vya mwilini kabisa!, na si vya rohoni. Na tunasoma si tu Musa peke yake bali hata Yoshua kuna mahali alifika akaambiwa avue viatu vyake (Yoshua 5:15).

Katika agano la kale Usafi mbele za Mungu ulithibitishwa kwa vitu vya nje!…kama kuoga, kunawa, kutawadha, kuvua n.k! Kwamfano watu walikuwa hawali chakula kabla hawajanawa mpaka kwenye viwiko..Mtu yeyote aliyekula bila kunawa alionekana ni mchafu (najisi), mbele za Mungu na wanadamu.

Marko 7:2 “wakaona wengine katika wanafunzi wake wakila vyakula kwa mikono najisi, yaani, isiyonawiwa.

3 Kwa maana Mafarisayo na Wayahudi wote wasiponawa mikono mpaka kiwiko, hawali, wakishika mapokeo ya wazee wao

4 tena wakitoka sokoni, wasipotawadha, hawali; na yako mambo mengine waliyopokea kuyashika, kama kuosha vikombe, na midumu, na vyombo vya shaba.”.

Ndivyo Mungu alivyotembea na watu wa agano la kale. (Usafi ulithibitika kwa vitu vya nje). Ndio maana tunaona hata hapo Musa alipokutana na Mungu alimwambia avue viatu vyake, kadhalika wakati Fulani Mungu alipotaka kukutana na wana wa Israeli na kusema nao katika mlima huo huo, aliwaambia  wafue nguo zao wawe safi (Kutoka 19:10).

Sasa kwanini Musa aambiwe avue viatu na si kitu kingine?.. Viatu ni vazi linalokanyaga uchafu wa kila aina njiani, kiatu hicho hicho hapa kinakanyaga taka, mbele kidogo kinakanyaga mavumbi..mbele tena kidogo kinakanyaga kinyesi cha mtu au mnyama.. hivyo si kitu kisafi!. Ndio maana Musa akaambiwa avue viatu vyake.

Lakini je! Hiyo ni sheria hata sasa?, kwamba tukitaka kwenda kwenye nyumba za ibada kukutana na Mungu ni lazima tuvue viatu vyetu, au tuoge au tutawadhe ili tusiwe najisi mbele za Mungu?

Jibu ni la!, Usafi wa nje, hautosogezi karibu na Mungu. Kutokuoga na kuingia kwenye nyumba ya ibada hakutufanyi tukataliwe na Mungu, vile vile kuingia katika nyumba ya Mungu na viatu mguuni hakutufanyi tuwe najisi.

Bwana Yesu alisema…

Mathayo 15:16 “Yesu akasema, Hata sasa ninyi nanyi mngali hamna akili?

17 Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?

18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19 Kwa maana MOYONI HUTOKA MAWAZO MABAYA, UUAJI, UZINZI, UASHERATI; WIVI, USHUHUDA WA UONGO, NA MATUKANO;

20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; LAKINI KULA KABLA HAJANAWA MIKONO HAKUMTII MTU UNAJISI”.

Lakini hiyo haitupi amri ya kuwa wachafu wakati wote!, kwamba tuifanye nyumba ya Mungu jalala!..au tusiwe watu wa kuoga, au tusiwe watu wa kunawa mikono kabla ya kula!. Tuna wajibu wa kuwa wasafi kwa kadri tuwezavyo!..na kuifanya nyumba ya Mungu kuwa safi wakati wote, kama viatu vina matope ni vizuri kuvisafisha nje kabla ya kuingia navyo ndani kwenye nyumba ya ibada (Hiyo inahitaji tu akili za kawaida, kupambanua!).. lakini sio kulifanya jambo hilo ndio msingi wa kumkaribia Mungu. La! Hatumkaribii Mungu kwa hayo mambo.

Hivyo tunapaswa tuvue viatu vya roho zetu, na si vya mwilini, viatu vyetu vya rohoni ndivyo vinavyobeba uchafu wa kila aina haya maisha!, ambao ndio huo Bwana alioutaja.. Uongo, mawazo mabaya, uasherati, uzinzi, wizi na mengine yote yanayofanana na hayo,

Je! Umempokea Yesu?, umeoshwa dhambi zako kwa damu?, viatu vya moyo wako umevivua?

Bwana Yesu yu karibu!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Gidamu ni nini? Kwanini Yohana alisema hastahili kuzilegeza gidamu za Yesu?

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI UNAJISI UNAVYOMGHARIMU MTU.

Bwana wetu Yesu Kristo atukuzwa. Ni siku nyingine tena tumepewa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha tujifunze Neno la Mungu, maadamu siku yenyewe inakaribia.

Kama vile “Utakatifu na utakaso” vinavyokwenda Pamoja, vivyo hivyo, “Dhambi na Unajisi” ni vitu vinavyokwenda bega kwa bega.

Tofauti na Dhambi na unajisi ni ipi?

Dhambi ni kitendo mtu anachofanya kinyume na Mungu, na huwa inaambatana na kuvunja sheria, au maagizo yake. Kama vile kuzini, kuua, kuabudu sanamu n.k.

Lakini unajisi ni kitendo mtu anachokifanya kinyume na yeye mwenyewe, ambacho mwisho wa siku kinampelekea, Mungu kujitenga naye au kumuacha kwa muda Fulani.

Mtu mwenye dhambi unajisi hauna nguvu kwake bali dhambi tu, ..Lakini mtu aliyeokoka vyote vina madhara kwake, yaani dhambi na unajisi.

Ni sawa na doa jeusi lililopo katika shati, jeupe, doa hilo lingekuwa katika shati jeusi, shati hilo lingeendelea kuvalika kwasababu doa halionekani, lakini likiwa katika shati jeupe hata kama litakuwa safi vipi, doa lile tayari limeshaharibu kila kitu. Sasa huo ndio unajisi. Ambao mtu mchafu, hauna madhara yoyote kwake, lakini kwa msafi ni pigo kubwa.

Sasa kabla kufahamu Zaidi, embu tuangalie kwa agano la kale baadhi ya unajisi ulikuwa katika mambo gani.

Zamani, ilikuwa ukila au ukishika mzoga wa wadudu, au Wanyama ambao ni najisi, adhabu yake ilikuwa na wewe unakuwa najisi, kwa muda wa siku nzima..

Walawi 11:23 “Lakini vyote vitambaavyo vyenye mabawa, vilivyo na miguu minne, ni machukizo kwenu.

24 Nanyi mtakuwa najisi kwa wanyama hao; kila atakayegusa mzoga wao atakuwa ni najisi hata jioni;

Soma pia Walawi 11:29-32

Halikadhalika, kulikuwa na unajisi, wa kujifungua, ikiwa mwanamke atajifungua tu, kile kitendo cha kutokwa damu, tayari ni unajisi ambao  unakugharimu siku saba, Pamoja na hayo, unajisi huo ulimgharimu siku nyingine tena 33, au 66 ikiwa ni mtoto wa kiume.. Kufanya jumla ya siku 40 kwa wa kiume, na siku 80 kwa wakike.

Unajisi huu ulikuwa pia katika kugusa maiti, au kutokwa na uchafu mwilini Soma(Walawi 15:16-20). Ulikuwa unakuwa najisi kwa muda wa siku 7, baada ya kujitakasa.

Sasa nachotaka uone ni kuwa, makosa kama haya aliyafanya mtu juu yake mwenyewe, ambayo hata huwezi kuyaona katika zile amri 10, lakini Mungu aliyatazama sana.

Katika agano la kale, wapo ambao walikuwa wanajitahidi kutotenda dhambi, yaani hawazini, hawaabudu sanamu, hawaibi, wanazitunza sabato n.k.

Lakini walikuwa wanakoseshwa na vitu vidogo tu kama hivyo vya unajisi, Na hivyo vikawa vinatia doa ukamilifu wao. Na matokeo yake, wakawa hawaruhusiwi kuingia hemani kwa Mungu, au katika mkusanyiko wowote wa watakatifu kwa kipindi Fulani, kulingana na aina ya unajisi wenyewe.. kama ni siku moja, au wiki, au miezi..

JE! Katika agano jipya unajisi upoje?

Unajisi wa sasa sio kama ule wa zamani, wa kushika, au kuionja, au kutokwa na vitu mwilini hapana.. Unajisi wa sasa wa mtu upo moyoni, Bwana Yesu alisema hivi;

Mathayo 15:17 “Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?

18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;

20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi”.

Kama tunavyosoma, hapo, yale mambo ambayo yanakutoka moyoni, kama vile tamaa, uzinzi, uasherati, n.k. Sasa kumbuka hasemi kufanya uzinzi, au uasherati, bali kukutoka..yaani mawazo ya uzinzi au ya uasherati, hayo ndiyo yanayokutia wewe unajisi, kama mtakatifu.

Unaweza kweli ukawa huzini na wanawake, lakini kuruhusu tu tamaa ndani yako, tayari umeshajitia unajisi, unaonekana kama vile tayari umezini sawasawa na maneno ya Bwana Yesu (Mathayo 5:28).

Na matokeo yake, inaweza kukuchukua kipindi Fulani kirefu, usiuone uwepo wa Mungu maishani mwako, kwasababu ya unajisi tu kama huo.

Pengine, unawasengenya wengine, unatukana, una chuki na wengine, kiburi, kijicho n.k.(Soma Marko 7:17-23) mambo kama hayo yanaweza kukufanya uikose furaha ya wokovu kwa kipindi kirefu sana, hata baada ya kutubu kwako.

Hivyo unajisi ni wakujiepusha nao sana wewe kama mtakatifu wa Mungu, unaweza ukawa hauuji lakini kitendo tu cha kumchukia ndugu yako, tayari ni sawa na muuji. Umeshajitia unajisi.

Ili uendelee kubaki katika uwepo wa Mungu wakati wowote, uulinde sana moyo wako.

Bwana atusaidie sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

JIEPUSHE NA UNAJISI.

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

SHINA LA UCHUNGU, LISICHIPUKE NDANI YETU.

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibu tuyatafakari maneno ya uzima, ambayo pekee ndio yanayoweza kutufanya sisi tuwe huru kweli kweli hapa duniani( Yohana 8:32).

Leo tutajifunza, kanuni mojawapo ya kibiblia ambayo itatusaidia sisi kuweza kupokea jumbe, au mafunuo, au maarifa sahihi kutoka kwa Mungu, Imenisaidia mimi, naamini pia itakusaidia na wewe.

Kanuni ya sisi kuzungumza na Mungu, ni tofauti na ya kwake kuzungumza na sisi. Sisi tukitaka kuwasiliana naye tunachofanya ni moja kwa moja kwenda katika uwepo wake, na kupiga magoti na kupelekea haja zetu kwake, Na tukishamaliza tutanyanyuka na kuondoka na kwenda katika shughuli zetu.

Lakini Mungu, hana utaratibu huo wa kuzungumza na wewe papo kwa papo, kwa wewe ufanyavyo. Na hiyo imewafanya watu wengi wakate tamaa, pale wanapoona hakuna mwitikio wowote, kutoka upande wa pili wa Mungu.

Lakini leo tutajifunza kanuni ambayo muhimu sana kuizingatia ikiwa wewe unataka kumsikia Mungu, au kupokea mafunuo sahihi kutoka kwake.

NA KANUNI YENYEWE NI “UTULIVU”

Sauti ya Mungu ya kweli ipo katika utulivu, na si mahali pengine, Eliya alikuwa ni nabii ambaye Bwana anazungumza naye na kumpa taarifa nyingi, lakini hakuwahi kuisikia sauti ya Mungu vizuri, hadi siku ile alipokuwa katika utulivu, na ndio maana utaona akaufunika uso wake, alipomsikia (kuonyesha kuwa amemwona Mungu, hivyo hastahili hata kuzungumza naye). Lakini mara nyingine zote huko nyuma hakuwahi kuufunika uso wake. Utajiuliza ni kwanini? Ni kwasababu Mungu hakuwa karibu naye kama alivyomwona siku hiyo, alipokaa katika utulivu (1Wafalme 19:9-13).

Elisha alipotaka kupokea taarifa sahihi, na maagizo kutoka kwa Bwana juu ya nini yafanye yale mataifa matatu yaliyotaka kuangamizwa na taifa la Moabu,..hakukurupuka tu na kuzungumza na Bwana, bali alitaka kwanza kukaa katika utulivu, akamwita mpiga kinanda,aimbe naye nyimbo za kumsifu Mungu, ndipo taarifa sahihi zikamshukia baadaye.

2Wafalme 3:14 “Elisha akasema, Kama Bwana wa majeshi aishivyo, ambaye nimesimama mbele zake, kama singemwangalia uso wake Yehoshafati mfalme wa Yuda, singekutazama, wala kuonana nawe.

15 Ila sasa niletee mpiga kinanda. Ikawa, mpiga kinanda alipokipiga, mkono wa Bwana ukamjia juu yake.

16 Akasema, Bwana asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. 17 Kwa kuwa Bwana asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu.

18 Na jambo hili ni jepesi machoni pa Bwana; pia atawatia Wamoabi mikononi mwenu”.

Vilevile Mungu alipotaka kuzungumza na Musa, ili kumpa zile mbao mbili za amri na sheria yake, alimwita mlimani, , lakini utaona Musa hakwenda moja kwa moja tu,hadi kileleni bali ilimbidi asubirie chini kwa muda wa siku sita (6). Ndipo siku ya saba akasikia sauti ya Mungu ikimwita apande mlimani.

Kutoka 24:15 “Musa akapanda mlimani, lile wingu likaufunikiza mlima.

16 Na huo utukufu wa Bwana ukakaa juu ya mlima wa Sinai; lile wingu likaufunikiza siku sita; na siku ya saba akamwita Musa toka kati ya lile wingu.

17 Na kuonekana kwake ule utukufu wa Bwana kulikuwa kama moto uteketezao, juu ya mlima machoni pa wana wa Israeli.

18 Musa akaingia ndani ya lile wingu, akapanda mlimani; Musa akawa humo katika ule mlima siku arobaini, mchana na usiku”.

Kwa mifano hiyo michache ni kutuonyesha na sisi kuwa, tukitaka tumsikie Bwana, hatuna budi kuwa katika utulivu rohoni, kwamfano unapokwenda kuomba, usiishie kuzungumza tu maneno yako halafu basi unaondoka, mpe Bwana nafasi, kaa chini imba, baadaye tafakari uweza wa Mungu, soma biblia, tafakari tena, kisha rudia tena kuomba.. kwa jinsi unavyokaa sana katika uwepo wa Mungu, ndivyo unavyompa nafasi Mungu ya kushuka na kukuhudumia.

Ghafla tu utaona wingu linakushukia roho, na hapo hapo unapokea ufunuo au maarifa, au taarifa Fulani ambazo hukuwahi kuziwaza au kuzifikiri, hapo ujue tayari ni Mungu huyo, au utapokea amani Fulani, au ufumbuzi Fulani, au agizo Fulani, hapo ujue Mungu anazungumza na wewe. Lakini inahitaji utulivu wa kitambo kidogo, wakati mwingine hata masaa kadhaa. Ni kweli yapo majira utaomba tu na kuondoka, lakini yapo majira ni lazima ujiwekee muda kwa Mungu, apate nafasi ya kusema na wewe.

Vilevile, yafanya Maisha yako, yawe katika utulivu, ukiwa ni mtu wa kukesha tu mitandaoni, kuchat chat kwenye magroup, au muda wote kutazama tazama, tv au tamthilia, au muvi, miziki au michezo michezo, au kuzurura zurura, leo party hii, kesho ile.. Fahamu kuwa mambo kama hayo ni adui mkubwa sana wa Mungu kuzungumza na wewe, haijalishi utakuwa ni mwombaji kiasi gani, hutakuwa unaona mwitikio wowote kutoka kwa Mungu. Hiyo ni kwasababu haupo katika utulivu.

Kuwa mtulivu maishani, tumia muda wako, kusikiliza nyimbo za sifa kama Elisha alivyokuwa anafanya, tumia weekend zako kwenda mikesha kuomba, soma sana biblia, punguza marafiki ambao ni maadui wa Imani yako, zungumza sana Habari za Kristo, katika mazungumzo hayo utaona ufunuo unaingia ndani yake, kwasababu Kristo kashaungana nawe katika kinywa chako kama ilivyokuwa kwa wale watu wawili wa Emau (Luka 24:13)

Ukizingatia hivyo. Utamsikia, kama sio kupokea mafunuo mengi kutoka kwake, daima jiweke katika utulivu.

Bwana akubariki.

Sote tunatamani Mungu azungumze nasi, lakini tumekuwa na wasiwasi, tukadhani kuwa Mungu yupo mbali sana, na anasema tu na watumishi wakubwa, au manabii, hawezi kusema na wewe. Ukweli ni kwamba, Karama ya mtu, sio kigezo cha Mungu kuzungumza naye, haijalishi atasikia sauti, au maono, au ndoto nyingi kiasi gani. Mungu anaweza kuzungumza na kila mtu, kulingana na njia yake mwenyewe aliyotaka azungumze naye.

Japokuwa Eliya alikuwa karibu sana na Mungu, na kupokea maono mengi, na taarifa nyingi kutoka kwa Yehova, lakini hakuwahi kumsikia Mungu mwenyewe, na ndio maana hakuwahi kuufunika uso wake, maana yake hakusitiri uovu wake, alipokuwa anaongea na Mungu hadi siku ile alipokaa katika utulivu na ndio akamsikia Bwana kwa mara nyingine.,

1Wafalme 19:9 “Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya?

10 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.

11 Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;

12 na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.

13 Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi yake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango. Na tazama, sauti ikamjia, kusema, Unafanya nini hapa, Eliya?”

SAUTI YA MUNGU IPO KATIKA UTULIVU.

Jambo ambalo, wakristo wa sasa tunalikwepa sana,

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

USIISHI KWA NDOTO!

TEGEMEA MUNGU KUZUNGUMZA NAWE KATIKA MAMBO MADOGO

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya vifungeni viuno vya Nia zenu? (1Petro 1:13).

Tusome,

1Petro 1:13 “Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.

14 Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu”.

Popote panapozungumziwa “kujifunga viuno” katika biblia panamaanisha “kuwa na utayari”. Kama ni msomaji mzuri wa biblia utakumbuka kipindi wana wa Israeli wanatolewa Misri na Mungu, ile siku ya  kwanza, wakiwa wanamla Yule pasaka, Bwana Mungu aliwaambia wamle huku wamevaa viatu vyao miguuni, na kujifunga mikanda viunoni (maana yake wawe katika mazingira ya kuondoka)..sio wawe katika mazingira ya kulala baada ya kula, bali mazingira ya kuondoka baada ya kula.

Kutoka 12:10 ‘Wala msisaze kitu chake cho chote hata asubuhi, bali kitu kitakachosalia hata asubuhi mtakichoma kwa moto.

11 Tena mtamla hivi; MTAKUWA MMEFUNGWA VIUNO VYENU, mmevaa viatu vyenu miguuni, na fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka; ni pasaka ya Bwana”.

Kwahiyo “kujifunga viuno” kunamaanisha “kujiweka tayari”. Hivyo tunaposema “tujifunge viuno vya akili zetu” tutakuwa tunamaanisha “tuwe tayari kiakili”.. Vile vile tunaposema “tujifunge viuno vya roho zetu, wakati wa kumngojea Bwana”..tutakuwa tumemaanisha “tujiweke tayari katika roho zetu katika kumngoja Bwana” kama Bwana alivyosema katika Luka 12:35..

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia”.

Vile vile tunaposema “tujifunge viuno vya Nia zetu” maana yake ni “tuwe/tujiweke tayari Nia zetu” Kwa jambo fulani linalofuata.

Kwahiyo huo mstari wa 1Petro 1:13 badala ya kusema “vifungeni viuno vya Nia zenu”…tunaweza kuuweka hivi “Kwa hiyo kuwenu tayari katika Nia zenu; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo”.

Je! Na sisi  viuno vyetu vimefungwa?…tupo tayari katika Nia zetu?, Tupo tayari kwenda mbinguni?..Tupo tayari kuihubiri injili?, tupo tayari kumtumikia Mungu kwa mioyo yetu yote na nguvu zetu zote?

2Timotheo 4:1 “Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;

2 lihubiri neno, UWE TAYARI, WAKATI UKUFAAO NA WAKATI USIOKUFAA, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.

Hizi ni siku za Mwisho na Kristo anarudi siku yoyote, na atakaporudi alisema atarudi na ujira wake..

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.

Je ni sahihi kuweka walinzi kulinda mali zetu?

Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).

CHAMBO ILIYO BORA.

Rudi nyumbani

Print this post

USIPUNGUZE KUTUMBUIZA!

Unaweza kujiuliza je! Sisi tumeitiwa kutumbiza?.. Jibu ni Ndio! sisi tumeitiwa kutumbuiza lakini si kwenye majukwaa ya dansi au anasa. Bali mbele za Malaika na wanadamu kupitia Maisha yetu ya usafi na utakatifu!.

1Wakorintho 4:9 “Maana nadhani ya kuwa Mungu ametutoa sisi mitume mwisho, kama watu waliohukumiwa wauawe; kwa sababu TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; kwa malaika na wanadamu”.

Maana yake Maisha yetu ni kama tamthilia inayotazamwa!, ambayo baada ya kuisha itatolewa hukumu kama ni nzuri au mbaya!.

Kutumbuiza ni kitendo cha kuonesha ujuzi wako na kipaji chako mbele ya watu wanaokuzunguka kwa lengo la kupata fedha!,

Wanaoimba na kucheza dansi kwenye majukwaa wanatumbuiza!, wanaoruka sarakasi kwenye majukwaa  huku wanaimba wanakuwa wanatumbuiza, wanaocheza na nyoka mbele za umati wanakuwa wanatumbuiza! N.k

Leo napenda tuangalie kibiblia hii namna ya kutumbuiza kwa kutumia nyoka.

Kipindi cha Nyuma kidogo!, na hata sasa katika nchi baadhi, kuna mchezo wa kutafuta nyoka wenye sumu kali (kama Kobra), na kisha kujifunza kuwapumbaza kwa nyimbo na sauti za filimbi, na kwenda nao kufanya maonyesho kwenye matamasha kwa lengo la kupata fedha!, Watu walipowaona watu hao wanauwezo wa kusimama mbele ya Nyoka  wenye sumu bila kudhuriwa, waliburudika na kuwapa fedha nyingi kuliko hata wale waliokuwa wanaruka sarakasi au kuimba tu peke yake!, kwasababu ni jambo ambalo lilikuwa si la kawaida!.

Lakini pamja na hayo ulikuwa ni mchezo wa hatari sana, kwani endapo ikitokea ajali yule Nyoka akamwuma yule Mtumbuizaji, basi mchezo ndio umeishia pale pale na hakuna fedha yoyote atakayopata huyo mtumbuizaji!, Hivyo ilihitaji umakini mkubwa..

Sulemani kwa hekima alisema..

Mhubiri 10:11 “NYOKA AKIUMA ASIJATUMBUIZWA, BASI HAKUNA FAIDA YA MTUMBUIZI”.

Hii ni hekima ya kidunia tu ambayo Sulemani aliitoa kwa kutazama Maisha ya watumbuizaji!. Lakini hakuisema tu hiyo hekima kutufurahisha!, la!, bali hekima hiyo ina funzo kubwa sana kwetu wakristo ndio maana ipo kwenye biblia!, ingekuwa haina funzo lolote isingewekwa kwenye biblia.

Na sisi wakristo ni watumbuizaji!, Na Nyoka ni adui yetu shetani!..ambaye anasimama kutupinga siku zote!, akitafuta kutudhuru siku zote katika Maisha yetu ya hapa duniani, Na mbingu inatutazama tutaumalizaje mchezo wetu!, jinsi gani tutampumbaza shetani mpaka mwisho, ili tupokee Tuzo bora!.

Endapo tukisimama mpaka mwisho wa muda wetu bila kuangushwa na shetani aliyeko mbele yetu basi tutapokea tuzo kubwa sana mbinguni, lakini tukiumwa na shetani kama maandiko yasemavyo hapo juu.. “Nyoka akiuma asijatumbuizwa, Basi hakuna faida ya mtumbuizi”.

Hatuna faida yeyote tutakayoipata endapo tukiruhusu shetani atuangushe.

Sasa tunampumbazaje shetani?

Zamani hawa watu waliokuwa wanawapumbaza nyoka!, walitumia sauti za filimbi, walikuwa wanazipuliza filimbi zile kwa ustadi, na walikuwa hawapotezi umakini katika hilo, walijua kwa kupoteza umakini kidogo tu!, wale nyoka akili zao zinawarudia na kuwadhuru!..Sasa zile filimbi hazikuwa zinawaburudisha wale nyoka hata washindwe kuwauma..la!, bali zilikuwa zinawachanganya!..zinawafanya wale nyoka, wakose sababu ya kuwauma!..kwani nyoka ili amuume mtu, ni lazima apate shabaha ya utulivu katika akili yake, sasa zile sauti za filimbi zilikuwa zinawakosesha shabaha, hivyo wanakuwa wanababaika na kusubiri wakati zitakapotulia..

Sasa wakati zile sauti zinawapumbaza wale nyoka, wakati huo huo zinawafurahisha watazamaji..

Na sisi wakristo ili shetani ashindwe juu ya Maisha yetu!, hatuna budi muda wote tupulize filimbi zetu za kiroho, huku tukimkabili adui yetu shetani. Na wakati filimbi hizo zinampumbaza shetani na majeshi yake, wakati huo huo zitakuwa zinaifurahisha mbingu.

Sasa Filimbi hizo za kiroho ni zipi?

Zifuatazo ni filimbi za kiroho.

1/Utakatifu

3/Maombi

4/Kusoma Neno

2/Ushuhudiaji

Tukizipuliza filimbi hizi Nne!, basi shetani atakuwa hana nguvu zozote kwetu, atakuwa kama ZUZU!, mpaka tunamaliza safari yetu hapa duniani!.

Na faida kubwa ya kumfanya shetani zuzu hapa duniani ni Thawabu kubwa kule mbinguni, na heshima kubwa!..kwasababu yeye aliyekuwa anajiona ni kitu!, amekuwa takataka mbele yetu!.

Bwana atusaidie tusiyapunguze mambo hayo..Maana tukipunguza utakatifu, Maombi, Kusoma Neno, na Ushuhudiaji basi tunamrejeshea shetani shabaha yake!, na akituangusha basi anguko letu linakuwa kubwa na hatutakuwa na thawabu yoyote baada ya Maisha haya.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.

KUOTA NYOKA.

Rudi nyumbani

Print this post

Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.

SWALI: Biblia inamaana gani kusema Yesu atawachunga kwa fimbo ya chuma..kwanini iwe ya chuma?

 Ufunuo wa Yohana 19:15
[15]Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

JIBU: Fimbo ya mchungaji sikuzote ni fimbo ya mti…ambayo ukichapwa haiwezi kukuletea madhara makubwa sana, zaidi ya maumivu tu mwilini..

Lakini tengeneza picha unapigwa kwa chuma iliyoundwa kwa mfumo wa fimbo..kama vile nondo ngumu..unategemea ni nini kitatokea hapo katika mwili? Sio kusikia tu maumivu lakini pia kuharibika kwa baadhi ya viungo kama vile misuli na mifupa kuvinjika kutatokea. Na kama ukipigwa sehemu mbaya kama vile kichwani..moja kwa moja ni mauti. Kwasababu anayekupiga hana lengo la kukuadhibu bali kukuharibu.

Ndivyo inavyomuonyesha Bwana Yesu, atakapokuja kuwa katika ule utawala wa miaka 1000 hapa duniani.

Kama vile tunavyosoma katika maandiko kuwa yeye ni mchungaji mwema (Yohana 10:14-16)..Ikiwa anamaanisha kuwa Leo hii anatuchunga kondoo wake kwa fimbo ya mti, na ndio maana anapotuadhibu hatuangamii kabisa kwasababu sisi ni kondoo anayetupenda na kututakia mema, anafanya hivyo kwa lengo la kitufanya tu tusitoke katika njia adui akatuangamiza.

Lakini atakapokuja na kutawala kama mfalme wa wafalme biblia inatuambia Amani itatawala duniani kote…kiasi kwamba waovu watakuwepo lakini kwa ule utiisho wake tu, hakuna dhambi yoyote itakayochukua nafasi, kwani adhabu zitakuwa kali kwa watu watakaojaribu kuipindisha amani.

Kwasababu wakati huo atakuwa hachungi kondoo tena kwasababu watakuwa wameshaokolewa, bali atashughulika na mbwa mwitu, hao ndio watapigwa kwa fimbo hiyo kali.

Isaya 65:20
[20]Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.

Hiyo ndio fimbo ya chuma..uovu wala waovu hawatavumilika kwa namna yoyote ile..Vilevile kushindwa kutekeleza maagizo ya ufalme wa Bwana Yesu utakumbana tu na fimbo hiyo ya chuma. Soma (Zekaria 14:17-20).

Kumbuka Jambo hilo atalitekeleza Kristo pamoja na watakatifu wake, wale ambao waliushinda huu ulimwengu wakaenda naye katika unyakuo.

Ufunuo wa Yohana 2:26-27
[26]Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,
[27]naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu.

Hivyo ni vizuri ukafahamu kuwa Kristo anazo fimbo mbili…Ni heri sasa ukubali kuchungwa naye kwa fimbo ya miti…wakati utafika kabla hata ya utawala wenyewe kuanza…fimbo hiyo ya chuma ataipitisha kwa ulimwengu mzima, kwa yale mapigo atakayoyashusha humu ulimwengu ili kuwaangamiza wote..

Si jambo la kulitamani hata kidogo. Ni heri umpe Kristo maisha yako leo hii ayaokoe, akupe uzima wa milele. Hizi ni nyakati za mwisho. Unyakuo upo mlangoni.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata somo lote la utawala wa miaka 1000 wa Yesu Kristo utakavyokuwa..nitumie ujumbe inbox kwa namba hii +255693036618..nikupe somo lake.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi nyumbani

Print this post

UMUHIMU WA KUBATIZWA.

Ubatizo ni agizo la msingi sana, si la kulipuuzia hata kidogo!, na kwasababu shetani anajua ni agizo la msingi basi atatufuta kila njia watu wasibatizwe kabisa, au wabatizwe isivyopaswa na mioyoni waendelee kuamini kuwa tayari wameshabatizwa.

Faida za ubatizo zipo nyingi sana, lakini leo tutajifunza faida moja kuu ya ubatizo. Ambapo baada ya kuijua hiyo, basi sisi wenyewe tutafanya maamuzi tukabatizwe au tusibatizwe!.

Na faida yenyewe ni KUOKOLEWA NA GHADHABU YA MUNGU JUU YA MAADUI ZETU NA MAADUI WA BWANA.

Mungu alipotaka kumwokoa Nuhu, ilimbidi aigharikishe dunia yote na yeye Nuhu akiwa ndani yake!, lakini siri ni kwamba maji yaliwaua maadui zake Nuhu na maadui za Bwana huko nje!, lakini yakamwacha Nuhu salama.

Kwaufupi tendo hilo biblia inalifananisha na Ubatizo kwa Nuhu.

Ndio maana maandiko yanasema…

1Petro 3:20 “watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji.

21 MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO, UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo”.

Hivyo ubatizo wa Nuhu na nyumba yake, ulikuwa ni kwa lengo la kuuondoa Uovu uliokuwa unamzunguka.

Kadhalika wakati Mungu alipotaka kuliharibu jeshi la Farao moja kwa moja lisiwasumbue Israeli tena, hakutumia ugonjwa wa Tauni, wala hakushusha moto, bali alikwenda kuligharikisha katika bahari ya Shamu, na ndio ikawa mwisho wa waMisri kuwafuatilia wana wa Israeli. (Tendo hilo pia linafananishwa na ubatizo wa wana wa Israeli).

1Wakorintho 10:1 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;

2 WOTE WAKABATIZWA WAWE WA MUSA KATIKA WINGU NA KATIKA BAHARI”

Sasa gharika iliua maadui wote wa Bwana na kumwacha Nuhu mwenyewe salama, vile vile Bahari ya Shamu iliwaua maadui wote wa Bwana na kuwaacha Israeli salama. Vivyo hivyo Ubatizo wa maji mengi leo unawaua maadui wote wa Bwana juu ya mtu, wanaotufuatilia na kutuacha sisi salama.

Unapozamishwa katika maji mengi na kuibuka juu, hapo ni sawa na umepita katika ile bahari ya Shamu yenye maji mengi na kwasababu upo ndani ya kuta zinazozuia maji (yaani upo ndani ya Yesu) unakuwa unatoka salama bila kufa, lakini maadui zako ambao ni (madhaifu ya yule adui, tabu, mapepo, shida, na mambo mengine yote kutoka kwa yule adui), hayatatoka salama kwenye hayo maji. Yatakuwa ndio mwisho wao, kama majeshi ya Farao yalivyogharikishwa, kwasababu yale maji si kwa lengo la kukuangamiza wewe, bali kuyaangamiza majeshi yote ya adui.

Nuhu alipita katikati ya maji mengi lakini yale maji hayakumuua, bali yaliwaangamiza wale watu waliokuwa wanamdhihaki, waliokuwa wamtesa kutokana na Imani yake, pengine waliokuwa wanamfunga, waliokuwa wanamfanyia dhuluma n.k.

Na maji ya ubatizo si kwa lengo la kukudhuru wewe, bali kukuokoa na kuyaharibu majeshi ya Adui ambayo yakibaki yatakuletea madhara katika safari yako.

Ndio maana maandiko yanasema..

1Petro 3:21 “MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO, UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI…”

Je! na wewe unataka majeshi ya Adui yasiendelee kukufuata, baada ya kumpokea Kristo!, tafuta ubatizo wa maji mengi na kwa Jina la Yesu, (Au kama ulibatizwa isivyo sahihi kwa kunyunyiziwa au kwa jina lingine lisilo la Yesu, basi rekebisha ubatizo huo kama wale watu wa Efeso katika Matendo 19:1-5)

Na ni kwanini ubatizo ni kwa jina la YESU na si kwa jina lingine?, ni kwasababu maandiko yanasema wakati ule  wa nawa Israeli wanavuka Shamu “WOTE WAKABATIZWA WAWE WA MUSA KATIKA WINGU NA KATIKA BAHARI”. Na Musa wetu sasahivi watu wa agano jipya ni BWANA YESU, ambaye anatutoa sisi kutoka Misri ya kiroho na kutupeleka Kaanani(mbinguni), na anatuagiza kila mmoja wetu tubatizwe kwa jina lake ili tuwe wake, ndio maana tunabatizwa kwa jina la Bwana Yesu kila mmoja (soma Matendo 2:38, Matendo 8:16, Matendo 10:48 na Matendo 19:5).

Zipo faida nyingi sana za ubatizo, hii ni mojawapo tu, tenga muda tafuta kuzijua zote!, kwamaana ni muhimu sana kuzijua.

Kama bado hujaabatizwa tafuta kanisa ukabatizwe, au hapo hapo kanisa ulipo ulizia ubatizo (lakini hakikisha ni ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu)!, Fanya hivyo haraka iwezekanavyo,

Na ubatizo ni bure!, na wala hauhitaji madarasa ya kupitia. Yule Mkushi aliyebatizwa na Mtume Filipo, hakupitishwa kwenye darasa lolote, pale alipoamini tu!, tayari alikidhi vigezo vyote vya kubatizwa, na akabatizwa!

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?

Je ni lazima kupitia mafundisho ya muda mrefu kabla ya kubatizwa?

NUNUA MAJI YA UZIMA.

FUMBO ZA SHETANI.

Rudi nyumbani

Print this post

VIJANA NA MAHUSIANO.

Karibu katika darasa fupi, linalohusu vijana na mahusiano.

Yapo maswali kadhaa ya kujifunza kwa kijana kabla ya kuanza mahusiano ya aina yoyote ile, na mambo yenyewe ni haya;

1. Je ni wakati gani ulio sahihi wa kuanza mahusiano?

 2. Je ni mtu gani sahihi wa kujiingiza naye katika mahusiano?

 3. Je mambo gani ninapaswa niyafanye na yapi sipaswi kuyafanya ninapoingia katika uhusiano?

Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa darasa hili linawahusu/linawafaa zaidi vijana wa kiume na wa kike ambao tayari wameshaokoka!, yaani wametubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu na wanaitazamia mbingu mpya na nchi mpya. Kama bado hujampokea Bwana Yesu basi mafunzo haya yanaweza yasikusaidie, hivyo ni vyema kwanza ukampokea Bwana Yesu (ukaokoka), na ndipo mambo mengine yafuate baadaye.

Mahusiano yamegawanyika katika sehemu kuu (2),  Yapo Mahusiano kabla ya Ndoa, na Mahusiano baada ya Ndoa. Mahusiano kabla ya ndoa, yanaitwa Uchumba ambayo tutajikita sana kujifunza juu ya haya katika siku ya leo.


  1. Ni wakati gani ulio sahihi wa kuanza mahusiano Kwa kijana wa kiume:

Kama wewe ni kijana wa kiume na umeokoka, wakati sahihi wa kuanza mahusiano ni wakati ambao tayari unajitegemea mwenyewe. Maana yake una sehemu yako mwenyewe ya kuishi na una kipato chako mwenyewe, haumtegemei mzazi au ndugu!, kwasababu hatua ya uchumba ndio hatua ya awali kabla ya kuoa, na huwezi kuoa ukiwa bado hata wewe mwenyewe huwezi kujitunza, utamtuzaje huyo mke anayekuja?.

Kwasababu hiyo basi si wakati sahihi wa kuanza mahusiano yoyote ukiwa bado ni Mwanafunzi,  au ukiwa bado upo kwa wazazi wako, au ukiwa huna shughuli yoyote ya kukuingizia kipato!.

Ni umri gani sahihi wa kuanza Mahusiano, kwa kijana wa kiume?

Hapa inategemea na umri ulioanza kujitegemea mwenyewe, katika zama hizi vijana wengi wa kiume kuanzia miaka 25 na zaidi ndio wanaanza kujitegemeana hiyo ni kutokana na mifumo ya Elimu. Mtu atamaliza shule akiwa na zaidi ya miaka 20, na kujikuta kuanza kufanya kazi za mikono akiwa na zaidi ya miaka hata 25, wakati huo unaweza kuwa wakati sahihi wa kuanza uchumba.

Wapo wengine wanawahi kuanza kujitegemea wenyewe kabla ya umri huo!, hao wanaweza kuwahi kuanza mahusiano..lakini mahusiano ya mapema ni hatari sana, kwasababu akili ya kijana bado haijakomaa vizuri katika kujua mambo mengi ya kimaisha na wengi wanaingia huko kutokana na tamaa za kimwili tu!,.. Hivyo Ni vizuri kijana wa kiume akaanza mahusiano zaidi ya miaka 25.


Kwa kijana wa kike:

Wakati sahihi wa kuanza mahusiano kwa kijana wa kike, si wakati upo shule, bali wakati ambao umemaliza shule,

Vile vile umri sahihi wa kuanza mahusiano ni miaka 20 na zaidi!.. Zamani kidogo ilikuwa ni mapema, lakini zama hizi, shule zimewafanya watu wachelewe kuanza maisha yao kujitegemea. Lakini vijana wengi wa kike walio chini ya miaka 20 sasa wanaojiingiza kwenye mahusiano ya uchumba wengi wanaongozwa na tamaa tu!, aidha kwa kujua au kwa kutokujua. Na wengi wa hao wakifikisha miaka 30, akili zao zinapofika hatua ya kupevuka wanajigundua kuwa walikuwa wanafanya vitu vya kitoto na vya kipumbavu.


 2. Je ni mtu gani sahihi wa kujiingiza naye katika mahusiano?

Kwa kijana wa kiume:

Mtu sahihi wa kuanza naye mahusiano sio yule uliyeoneshwa na Nabii, au Mchungaji, au uliyechaguliwa na mtu. Kamwe usianze mahusiano na mtu yeyote ambaye umesaidiwa kuchaguliwa. Uchaguzi utachagua wewe!, Yule Bwana aliyekuchagulia atakuja kwako na wewe utajikuta unampenda, anakidhi vigezo vyako!..Hivyo ndivyo Bwana anavyowapa watu wenza wao na sio kuchaguliwa na mchungaji au Nabii, au kuoteshwa ndoto.

Vile  vile usianze mahusiano na msichana/ mwanamke yeyote ambaye yeye ndiye anayekuomba au kukulazimisha umwoe!.

Kwa kijana wa kike:

Kwa kijana wa kike mtu sahihi wa kuanza naye mahusiano si mwanafunzi,  haijalishi anaonesha kukupenda kiasi gani, bado sio mtu sahihi, hapa sizungumzii wale watu ambao ni wafanyakazi lakini wanajiongezea elimu ya juu (hili tayari ni kundi la watu wazima wanaojitambua), wanafunzi tunaowazungumzia hapa ni wale wa sekondari, na wale waliotoka sekondari na moja kwa moja chuo.


 4. Je mambo gani napaswa niyafanye na yapi sipaswi kuyafanya ninapoanza mahusiano?

Fanya mambo yafuatayo unapoanza mahusiano.

Kwa kijana wa kiume!

Mfahamu huyo mtu kwanza, na kama ameokoka anza naye urafiki kama wa dada na kaka tu Kama hajaokoka au si mtu wa imani moja nawe!, mhubirie kwanza aokoke, akimkubali Bwana Yesu, atakukubali na wewe, akimkataa Bwana Yesu hawezi kukukubali na wewe!. Usimwahidi kwamba utamwoa endapo akiokoka maana kwa kufanya hivyo atakukubali ilimradi tu aolewe na wewe!, hivyo mvute kwa Kristo kama unavyowavuta wengine wote.

Akikubali kumtii Kristo na kumpata Roho Mtakatifu ambaye umempokea wewe, na hata kushiriki kanisa moja nawe, hapo unaweza kuanza naye urafiki kama wa kaka na dada tu!, wa kuheshimiana, wakati huo unaweza kuongeza kumjali zaidi kuliko wengine wote wanaomzunguka, kwa kufanya hivyo atakuwa ameshaanza kujua kuwa unamjali, na hivyo atakupenda na hapo ni rahisi kuendelea na hatua nyingine.

Kwa kijana wa kike!

Kwasababu ni mwanaume ndiye anayemchagua mwanamke!, kijana wa kike hupaswi kujiweka au kujitangaza kwamba unatafuta mchumba.. Kaa katika hali yako ya asili, umri usikuogopeshe wala kukutatanisha, wapo wanaoolewa hata na miaka 60, na wanakuwa na furaha, hivyo usijitafutishe mchumba.. usijipendekeze sana kwa vijana wa kiume!, bali dumu katika usafi wa Rohoni na wa Mwilini, jiweke katika mazingira ya usafi na ya upole!, Bwana atakuletea mtu sahihi ambaye atakuheshimu, kwa wakati sahihi. (www wingulamashahidi org).

Hali kadhalika utakayemwona anakuja kwako kuwa naye makini, kwasababu Matunda mazuri si mtu tu anayeyapenda bali hata nyani, na ndege na popo na bundi wanayapenda!, (maana yake hata watu waovu wanawapenda wanawake wanaojiheshimu na watakatifu), hivyo kuwa makini, Kama hajaokoka mkaribishe kanisani, na jitahidi usimhubirie wewe, kwamaana ni rahisi kukubali kuokoka ili akupate!, bali mwunganishe na mchungaji wa kiume kanisani, au na mtu yeyote aliyesimama pale kanisani, kama akimsikiliza huyo na kumkubali Kristo, ni rahisi kuwa mtu sahihi Bwana aliyekukusudia, lakini kama hataki kujihusisha na mchungaji au mtu yeyote kanisani, jitenge naye, usitazame uzuri wake au fedha zake, ni pando la adui, anakutafuta kwa faida zake tu!

Mambo yafuatayo usiyafanye unapokuwa katika Mahusiano ya uchumba!


Kwa kijana wa kiume/kike.

1/ Usikutane kimwili na huyo uliyeanza naye mahusiano, wala msishikane wala kubusiana, (Kujaliana tayari ni ujumbe tosha kwamba kila mmoja anampenda mwenzie, na sio kufanya hayo mambo)

2/ Usimtembelee huyo kijana/binti nyumbani kwake akiwa peke yake, tafuta mwenzako muwe wawili ndipo umtembelee, hiyo itaongeza heshima yenu na vile vile shetani hatapata nafasi. Vile vile tafuta masomo mazuri yanayohusu mahusiano, yaliyofundishwa na watumishi wa Mungu wa kweli, mshirikishe mwenzio asikilize mafundisho hayo, au asome, au ahudhurie semina ili aanze kujiandaa na kuwa mume au mke.

Baada ya kuhakiki kuwa huyu mwenzangu ananifaa kimaisha na vile vile ananifaa kiroho, vile vile amekukubali uwe mwenza wake, basi hatua ya ndoa inaweza kufuata. Mambo yafuatayo yatakufaa baada ya mwenzako kukubali kufunga ndoa naye.

 1. Tangaza kwa wazazi: Kumbuka unapoenda kutangaza isiwe ni jambo la kushtusha kwa wazazi wako au walezi, ni vizuri wawe wanamjua huyu mwenza wako hata kabla ya hapo, ili wawe na amani naye.

2. Baada ya kutangaza kwa wazazi, Ndoa inapaswa utangazwe kanisani. Baada ya kanisa kujua na kupewa taratibu zote za ndoa, Mahari zitapangwa (Ni lazima kijana wa kiume ulipe mahari, ikiwa kubwa sana omba upunguziwe au kopa mahali ulipe), ni kinyume na maandiko kijana wa kiume kutolipa mahari, Kristo aliingia Gharama kutukomboa sisi (ndio damu yake) ambayo inafananishwa na mahari kwetu sisi bibiarusi wake, kwahiyo ni lazima kijana ulipe mahari.

3. Baada ya Mahari na ndoa kutangazwa na kufungwa, kanisani. Hapo Mmekuwa Bwana arusi na Bibi-Arusi, mnaweza kufanya mambo yote yanayowahusu wana-ndoa. Hampaswi kuishi kama wachumba tena.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

MAMA, TAZAMA, MWANAO.

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi nyumbani

Print this post

SHINA LA UCHUNGU, LISICHIPUKE NDANI YETU.

Biblia inasema;

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;

15 mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo”.

Mistari hiyo kwa namna nyingine tunaweza kusema; Tukikosa amani, na watu wote, tukikosa utakatifu pia basi tutapungukiwa na neema ya Mungu, na matokeo yake ni kuwa shina la uchungu litachipuka ndani, na kuwasababishia watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.

Ni kweli mstari huu unalenga watakatifu wa Mungu..

Tukikosa, mambo hayo mawili, yaani Amani na watu wote, na Utakatifu, kuna uwezekano mkubwa sana wa hili shina la uchungu kuchipuka ndani yetu.

Jiulize kama wewe ni Mtakatifu je, una amani na watu wote? Ikiwa na maana una amani na watakatifu wenzako na watu wengine wa nje?..Ni jambo la kujitahidi sana, hata kama ni gumu ni lazima ujitahidi kama biblia inavyosema, kwasababu ukiukosa tu huo, matokeo yake ni kuwa  UCHUNGU uchungu utaanza kuchipuka ndani yako.

Kibiblia Uchungu, ni hali ambayo inakuwa na  mchanganyiko wa hasira, kinyongo, wivu, chuki, ghadhabu, na maumivu kwa mtu mwingine.

Na biblia inatuonyesha huwa linaanza kama mbegu, mpaka baadaye linachupuka na kuota mizizi mpaka kuwa shina nene. Na likishafikia hatua hiyo ya kuwa shina, kuliondoa ndani yako ni ngumu sana, litakusumbua kwa muda mrefu kweli, kwasababu tayari limeshakita mizizi kwenye moyo wako.

Hili shina limewasumbua sana wapendwa, hivyo tujitahidi sana tusilipe nafasi mioyoni mwetu..

Mfano mmojawapo katika biblia wa mtu aliyesumbuliwa na shina hili ni Mfalme Sauli.

Lilimwanza pale alipomwacha Mungu, na Mungu kuuhamisha ufalme wake kwenda kwa Daudi. Utaona alipojua hilo alianza  kumchukia Daudi kidogo kidogo, badala akatae ile hali, akaendelea kumchukia Daudi kwa kila kitu mpaka baadaye akaonyesha kwa nje sasa yale yaliyokuwa ndani ya moyo wake, akaanza kuweka mikakati ya kumwinda na kumfukuza maporini na majeshi yake ili amuue, bila sababu yoyote. Ikawa ni ngumu tena, kulishinda lile shina la uchungu lililokuwa ndani yake.

Hata alipojaribu kutubu mara ya kwanza na ya pili juu ya jambo hilo la kumwinda Daudi bado alishindwa, kwasababu shina hilo limeshakita mizizi mkubwa ndani yake (1Samweli 24).

Hivyo na sisi, tumeonywa, tujitahidi sana, tena sana tuwe na amani na kila mtu, ni jukumu la kila mtakatifu, kila mshirika, kila mtumishi, si mchungaji, si nabii, si mtume, wote,  jukumu hili ni letu, kuwa na amani na watu wote, tusiruhusu chuki, hasira, vinyongo, na wapendwa wenzetu, au ubaya wowote, vilevile na watu wa nje wa kidunia, tusigombane nao.

Kama wewe ni mchungaji, hakikisha huna neno la mshirika yoyote, au mchungaji mwenza, kama wewe ni mtendakazi kanisani, ondoa uadui wa siri na mtendakazi mwenzako, hata kama hakupendezi, jitahidi kwa upande wako uwe na amani na kila mtu kanisani.

Hiyo itatufanya tuwe mahali salama. Tuliepuke hili shina baya la adui mioyoni mwetu.

Yakobo 3:14 “Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli.

15 Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani.

16 Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya.

17 Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki”.

Waefeso 4:26 “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;

27 wala msimpe Ibilisi nafasi”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

KIFAHAMU KIGEZO  CHA KUSAMEHEWA NA MUNGU.

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

Rudi nyumbani

Print this post