Category Archive Home

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

Toa sadaka isiyo na kasoro kwa bwana.


Jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe!. Karibu tena tujifunze biblia..Hatuna budi kufanya hivyo kila siku..maadamu tumepewa uhai.

Leo tutaendelea kujifunza umuhimu wa kumtolea Mungu kitu kilicho bora..kama hujapita somo lililotangulia lenye kichwa kinachosema “TUPENDE KUMTOLEA MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.”..Naomba ulipitie kwanza ili tuweze kwenda pamoja katika masomo haya yanayofuata.

Kuna umuhimu mkubwa sana kumtolea Mungu vitu vinavyotugharimu. Tusipende kutoa tu ilimradi tumetoa, kwasababu Mungu wetu ana hekima kuliko sisi na anaitazama mioyo yetu kwa undani sana. Mtu akija na kukupa wewe zawadi..na ile zawadi aliyokupa ukaja kugundua haikuwa imekusudiwa uipokee wewe..Ilikuwa ni ya mtu mwingine lakini kwasababu mtu huyo hakuwepo, na hakuna wa kumpa ukapewa wewe, hutaichukulia kwa moyo wa furaha sana kama kama ingekuwa imelengwa kwako moja kwa moja, Sasa ni kweli umepewa zawadi..jambo jema na la kushukuru, hata hicho umekipata, lakini zawadi ile ingekuwa na nguvu kwako kama ingekuwa wewe ndio mlengwa wa kwanza. Kama sisi wanadamu tuna hisia kama hizo..basi Mungu naye hapendezwi na sadaka za masalia.

Anapenda tumtolee kitu ambacho tulikuwa tumekipanga kumtolea yeye na si makombo, hapendi kuwekwa wa pili…Kumweka wa pili ni kumdharau…Haangalii wingi bali anaangalia ubora wa ile sadaka. Sadaka unayomtolea ina ubora kiasi gani..inaugusa moyo wake kiasi gani, umeigharimikia kiasi gani, hata kama ni sh.100 lakini haikuwa chenji ya kiatu ulichokwenda kununua..

Katika Agano la kale ambapo utoaji wa sadaka ulihusisha kafara za Wanyama…Wanyama ambao walitumika kwa kafara hizo kama ng’ombe, mbuzi, kondoo, njiwa n.k Mungu alitoa amri kwamba kamwe wasitolewe wakiwa na kilema, udhaifu, ugonjwa wala wenye lawama yoyote..

Ilikuwa kumtolea Mungu ng’ombe aliye na chongo ni dhambi, kumtolea mwanakondoo aliye mlemavu ni dhambi…kadhalika kumtolea ng’ombe mwenye kumbukumbu yoyote mbaya huko nyuma kama kuua mtu, au kuua ng’ombe mwenzake au kufanya jambo lolote baya ilikuwa ni dhambi kumtoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Mungu. Ng’ombe wa sadaka alikuwa ni lazima asiwe na hatia.

Walawi 22: 20 “Lakini mnyama ye yote aliye na kilema msimtoe; kwa kuwa hatakubaliwa kwa ajili yenu”

Kumbukumbu 17:1“Usimchinjie Bwana, Mungu wako, ng’ombe wala kondoo aliye na kilema, wala neno ovu lo lote; kwa kuwa hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”

Malaki 1:13 “Tena mwasema, Tazama, jambo hili linatuchokesha namna gani! Nanyi mmelidharau, asema Bwana wa majeshi; nanyi mmeleta kitu kilichopatikana kwa udhalimu, na kilema, na kilicho kigonjwa; ndivyo mnavyoleta sadaka; je! Niikubali hii mikononi mwenu? Asema Bwana.

14 Lakini na alaaniwe mtu mwenye kudanganya, ambaye katika kundi lake ana mume, akaweka nadhiri, ila amtolea Bwana kitu kilicho na kilema; kwa maana mimi ni Mfalme mkuu, asema Bwana wa majeshi, na jina langu latisha katika Mataifa”.

Katika agano la kale ilikuwa hairuhusiwi hata kwenda kununua ng’ombe wa mtu usiyemjua..kwasababu hujui huyo ng’ombe au kondoo alikuwa na kasoro gani huko nyuma..labda alishaua mtu utajuaje!..au alishapigana na mwenzake na kumuua utajuaje?..kwahiyo ilikuwa ni lazima mnyama aidha atoke kwenye zizi lako mwenyewe au kwa mtu unayemjua ambaye ni mwaminifu sana au anayeaminika na watu..Ili kuepuka kumtolea Mungu kitu chenye kasoro.

Umewahi kujiuliza ni kwanini siku ile Bwana Yesu alipoingia hekaluni alikuta watu wanauza njiwa, ng’ombe na mbuzi na hakukuta wanauza mashati, nguo, viatu au vyakula?.

Yohana 2:13 “Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu akakwea mpaka Yerusalemu.

14 Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng’ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi”

Unajua ni kwanini?..Ni kwasababu watu walikuwa wanatoka mbali..wengine mataifa ya mbali na hivyo wengi wanaona uvivu kutenga muda kwenda kutafuta ng’ombe asiye na lawama wala kilema wala kasoro yoyote…walikuwa wanaona ni jambo linalochukua muda sana na linalogharimu fedha nyingi mpaka umpate huyo mnyama wa viwango hivyo…na bado ni gharama kumsafirisha yule mnyama kutoka huko waliko mpaka hekaluni kwa makuhani ili atolewe kama sadaka ya kuteketezwa..

Sasa ili kulikwepa hilo wakawa wanatafuta njia mbadala ya kuwapata wale Wanyama mahali karibu na hekalu lilipo..sasa watu wa mataifa wakaona hiyo ni fursa..wakaanza kupeleka ng’ombe zao zilizonona kwenda kuziuza karibu na hekalu, wengine wakawa wanauza ng’ombe waliowaiba, wengine wanauza ng’ombe ambao wanamagonjwa ambayo hayajaanza kujidhihirisha bado…lengo lao wapate fedha..wengine mbuzi wanaowauza wamelala na wanadamu huko nyuma…nani anajali ilimradi tu wapate fedha..wapo radhi hata kudanganya kwamba mbuzi yule au kondoo huyu hana hatia kabisa alikuwa msafi na mpole tangu anazaliwa ili wamuuze tu wapate fedha na Kesho walete wengine..wetengeneze pesa nyingi..wakaikoleza biashara mpaka pakageuka kuwa soko na vibaka wakawemo humo humo ndani pengine hata na kamari zilichezeshwa humo.

Na kwasababu wayahudi wanaokuja pale wanaotoka mbali huko na huko hawapendi kujisumbua kutafuta kilicho bora mbele za Mungu…wanauziwa pale pale hakaluni Wanyama ambao ni machakizo kuwatoa mbele za Mungu, ambao hawajui hata wametoka wapi..…Wanatoka nyumbani bila chochote..wanafika hekaluni wananua mbuzi, wanawapa makuhani wanatolewa sadaka mbele za Mungu, wanarudi nyumbani..na kuamini kwamba wametoka kubarikiwa…kumbe wametoka KULAANIWA!..Wakidhani kwamba wametoka kumheshimu Mungu kumbe wametoka kumdharau..Ndio maana Bwana aliwafukuza wote wanaouza hao wanyama mule hekaluni..kwasababu yalikuwa ni machukizo yanayoendela mule..

Je na unaithamini sadaka yako unayomtolea Mungu kila siku?..je ina kasoro yoyote?..Kama umeipata kwa njia ya wizi usiende kumtolea Mungu hiyo tayari ina dosari kadhalika kama sadaka uliyoipata umeipata kwa njia ya ukahaba usimtolee,.. kama umeipata kwa njia ya kuuza bar, au sigara, au madawa ya kulevya au kamari, au ufisadi, au rushwa au wizi ni heri usimtolee Mungu…kama ni vimasalia salia ndio umepanga umtolee Mungu..usivitoe…Kwasababu Biblia inasema..

Mithali 15: 8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana..”

Ni masuala ya sadaka haya haya ndio yaliyoutoa uhai wa Anania na mkewe Safira…Anania kauza kiwanja kapanga kumtolea Mungu fedha yote aliyouzia kiwanja..lakini yeye akawa anakwenda kumtolea Mungu chenji huku fedha nyingine kaizuia..matokeo yake akafa yeye na mkewe..na hiyo ni agano jipya sio agano la kale.

Kwahiyo ukitaka kumtolea Mungu tafuta donge nono..ambalo huwezi kumwambia hata mtu kwasababu atakushangaa na kukuona wa ajabu..Unapomtolea Mungu mtolee kwa fedha iliyopatikana kihalali na kiwango cha juu ili sadaka yako isiwe na kasoro..Na njia nyingine bora ambayo Mungu atakuongoza umtolee yeye ambayo haitakuwa ni ya kumdharau..mtolee yeye ili ubarikiwe.

Bwana akubariki sana.

Shalom

Kama hujaokoka..Okoka sasahivi na kama hujabatizwa katafute ubatizo sahihi haraka sana..kwasababu mambo hayo mawili yanakwenda pamoja..

Mada Nyinginezo:

USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.

Tofauti katika ya zaka na sadaka ni ipi?

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

KIJITO CHA UTAKASO.

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

TUMAINI NI NINI?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE WAJUA?

  • Je Wajua kuwa Yesu ni Mungu bofya hapa kujua zaidi >> Yesu
  • Je Wajua kwamba dunia itateketezwa kwa moto na si kwa maji tena? >> Dunia
  • Je Wajua kuwa tunaishi katika kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia >> Laodikia
  • Je Wajua mtu ambaye hajaokoka hawezi kuingia mbinguni?
  • Je Wajua kuwa watu watakaonyakuliwa ni wachache? >> Wachache
  • Je Wajua roho ya mwenye haki ikifa inakwenda paradiso na si mbinguni? >> Roho ya mtakatifu.
  • Je Wajua kuwa Unyakuo utakuwa ni siri na ni wachache ndio watakaojua na hakutakuwa na maajali mabarabarani >> Unyakuo
  • Je Wajua kuwa Nusu ya kitabu cha Ufuno kimeshatimia?>> Ufunuo
  • Je Wajua kwamba mpaka sasa hakuna mtu yeyote aliyeko mbinguni zaidi ya Yesu? >> Mbinguni
  • Je Wajua kwamba mpinga-Kristo atakuwa ni mtu anayeshika biblia? >> Mpinga Kristo
  • Je Wajua kumlaani Adui yako ni dhambi? >> Adui
  • Je Wajua hakuna kiwanda chochote cha fedha kuzimu? >>Fedha kuzimu
  • Je Wajua kucheza karata ni dhambi? >> Kucheza karata
  • Je Wajua kipaimara si jambo la kimaandiko >> Kipaimara
  • Je Wajua kuwa Mwanamke hapaswi kuwa Mchungaji wala Shemasi >> Nafasi ya Mwanamke
  • Je Wajua kuwa kuna utawala wa miaka 1000 unaokuja huko mbele?>> Miaka 1000
  • Je Wajua kuwa Mariamu si malkia wa mbinguni >> Malkia

Mada Nyinginezo:

Je! mtu aliyeokoka anaruhusiwa kumiliki Lodge ambayo ina Bar ndani yake?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

JE KUJIUA NI DHAMBI?

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

KUOTA UMECHELEWA MAHALI FULANI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

Je! watoto wachanga wanaweza kuhukumiwa na kutupwa motoni.


Biblia inatuonyesha kuwa watoto wachanga wanaweza kushiriki adhabu za watu wengine waovu wakiwa hapa hapa duniani kama tu vile wanavyoweza kushiriki baraka za watu wema wakiwa hapa hapa duniani ..Lakini baada ya kifo biblia haisemi kama watoto wachanga watatupwa motoni au watakwenda mbinguni..

Ipo mifano kadha wa kadha katika biblia ya watoto kuadhibiwa kwa makosa ya wengine, kwa mfano tukisoma habari za Nuhu, Tunaweza kuona Nuhu aliambiwa aingie katika Safina yeye na familia yake tu ( jumla, watu 8)..Jiulize huko nje kulikuwa na Watoto wangapi wachanga, au wanawake wangapi waliotoka tu kujifungua muda mfupi kabla ya gharika kuanza,..Lakini ulipofika wakati wa Mungu kuuondoa uovu ulimwenguni kote, waliarithiwa na Watoto nao ambao kwa jicho letu la kibinadamu tunaweza kusema walikuwa hawana hatia yoyote..

Vivyo hivyo katika Sodoma na Gomora, walipona watu watatu (3) tu kati ya maelfu kama sio mamilioni ya Watu (ikiwemo na Watoto wadogo) waliokuwepo katika miji ile.

Utaona sehemu nyingi katika biblia, Mungu akitoa laana kwa mtu mwovu ambayo wakati mwingine  haiishii kwake tu, bali inakwenda kuwaarithi mpaka wazao wake wote. Soma (2Samweli 21:1-10, Yoshua 7:1-26,)

Daudi alipomwasi Mungu na kwenda kuzini na mke wa Uria, kilichotokea, ni Mungu kumpiga yule mtoto aliyemzaa kwa maradhi hadi mwisho wa siku akafa, hiyo yote ilikuwa ni kwasababu ya kosa la Daudi kuimwaga damu isiyo na hatia na kulala na mwanamke ambaye hakuwa mke wake.

Vilevile hata katika kipindi cha Yona kutumwa Ninawi, alipoambiwa awahubirie watu wale kuwa  zimebakia siku 40  tu mji ule uteketezwe wote…Bila shaka jambo lingejirudia lile lile, kisingesalia kitu, sio tu Watoto, bali pia mifugo ambayo haina hatia yoyote, lakini walipotubu Mungu akaurehemu mji ule..Na sikia Mungu alichomwambia Yona..

Yona 4:11 “na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi ya mia na ishirini elfu, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufugwa wengi sana”?

Unaona hao wasioweza kupambanua mkono wao wa kulia kutoka katika mkono wao wa kushoto wengi wao ni Watoto.

Hivyo dhambi ni mbaya sana, Na inatabia ya kuambukiza,,Na ndivyo itakavyokuja kuwa hata katika mwisho wa dunia..Siku Mungu atakapokuja kuteketeza kila kitu, Adhabu itawakuta wote…

Lakini kuhusu hukumu ya Watoto kwenda kutupwa katika ziwa la moto. Hilo hatulijui, lakini tunachojua ni  kuwa Mungu ni Mungu wa haki. Hawezi kumuhukumu mtu kwa kosa ambalo halijui. Watoto wachanga hawawezi kutofautisha kati ya jema na baya, kama ni hivyo basi hapo  tunaweza kusema hakuna hukumu ya adhabu juu yao..

Mithali 8:20 “Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu”.

Zaidi ya yote biblia inawachukulia Watoto wachanga kama mfano mzuri wa kuigwa kwa wale watakourithi ufalme wa mbinguni..

Mathayo 19:14  “Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao”

Unaona anasema tena. …

Mathayo 18:2  Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,

3  akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Unaona, tabia za Watoto  ni tabia zenye sifa njema mbinguni kwahiyo hapo tunaweza kupata picha kuwa Watoto ambao bado hawajajitambua, wanaweza kuwepo mbinguni wote, lakini pale wanapojitambua tu, kwamba wanaweza kutofautisha kati ya mabaya na mema haijalishi watakuwa katika umri gani iwe ni miaka 6 au 10, hao moja kwa moja watapanda hukumuni. Na kama wamestahili kuzimu watakwenda kuzimu,  kama wamestahili uzima watakwenda uzimani.

Kwasababu biblia inasema, siku ile ya hukumu watakuwepo wakubwa kwa wadogo ili wahukumiwe..

Ufunuo 20:12  “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao”

Hivyo kwa kuhitimisha. Upo uwezekano mkubwa  kwa Watoto wote wachanga wanaokufa kuwepo mbinguni. Japo suala la hukumu tunamwachia Mungu mwenyewe..hivyo Kikubwa tu tuwalee Watoto wetu katika njia iwapasayo, ili  atakapofikia umri ule wa kuweza kupambanua mema na mabaya basi wawe katika mstari mzuri wa kumtii Mungu ili hata ikitokea kwa bahati mbaya amefariki hapo katikati basi tuwe na uhakika wapo katika mikono ya Mungu.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Luka 14:15 “Basi aliposikia hayo mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye alimwambia, Heri yule atakayekula mkate katika ufalme wa Mungu”.

Enzi za biblia chakula kilichokuwa kinapewa heshima kubwa zaidi katika sherehe kilikuwa ni mkate uliookwa vizuri kwa upishi makini..Ni sawa na tuseme leo hii KEKI..Tunajua sherehe isiyokuwa na keki haijakamilika..miongoni mwa vyakula vyote vya kwenye sherehe keki huwa ndio inayopewa heshima kubwa kuliko zote na huwa inawekwa pale mbele kabisa, ili kuliwa na watu mahususi, Na sio na kila mtu tu aliyealikwa tu karamuni..bali wale walengwa tu..wengine wote watakula vyakula vingine vilivyoandaliwa kwa ajali yao..

Hivyo Keki huwa ndio inayofunua vyeo vya watu pale karamuni..Wale wanaopewa kipaumbele cha kwanza kuila ndio wanatambulika kuwa wale ni walengwa wa juu, au wenye kuheshimiwa ziadi, vivyo hivyo na wanao fuata na wanaofuata..

Sasa tukirudi katika mstari ule, tunapaswa tujiulize yule mtu aliona tukio gani mpaka ikamsukumwa kusema maneno kama yale “Heri yule atakayekula mkate katika ufalme wa Mungu”??..Tukisoma mistari ya juu kidogo tunaona alizungumza maneno yale baada ya kuona mfumo mzima wa karamu aliyokuwa amealikwa siku hiyo..Biblia inatuambia, Farisayo mmoja mkuu sana, aliyekuwa na cheo kikubwa, aliamua afanye karamu yake siku ya sabato, na alipofanya akawaalika ndugu zake tu, na watu wakubwa wakubwa tu, pengine mawaziri wa nchi, au wabunge wa nchi, na marafiki zake walio mtajiri na majirani zake wale wenye vyeo na fedha n.k. Na huko huko akamwalika huyu mtu na Bwana YESU pia..

Sherehe ile bila shaka ilikuwa ni ya kifahari sana, pengine walikuwa katika ukumbu uliopambwa sana. Sasa wakiwa huko baadhi ya watu walioalikwa wengine wakawa wanakimbilia viti vya mbeleni ili wawe wa kwanza kutambuliwa na kulishwa mkate au tuiite keki ya wakati huo..Utasema hilo tumelijuaje kuwa walikuwa wanakimbilia viti vya mbele?..Tumelijua hilo kwa maneno ya Bwana Yesu mwenyewe pale alipowaambia wale waliolikwa..

Luka 14:7 “Akawaambia mfano wale walioalikwa, alipoona jinsi walivyochagua viti vya mbele; akisema,

8 Ukialikwa na mtu arusini, usiketi katika kiti cha mbele; isiwe kwamba amealikwa mtu mwenye kustahiwa kuliko wewe,

9 akaja yule aliyewaalika wewe na yeye, na kukuambia, Mpishe huyu! Ndipo utakapoanza kwa haya kushika mahali pa nyuma.

10 Bali ukialikwa, nenda ukaketi mahali pa nyuma, ili ajapo yule aliyekualika akuambie, Rafiki yangu, njoo huku mbele zaidi; ndipo utakapokuwa na utukufu mbele ya wote walioketi pamoja nawe.

11 Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa”.

Unaona Vile vile utasema tumejuaje sherehe ile ilikuwa ni ya watu wakubwa tu..Tumelijua hilo kutoka katika kinywa chwa Bwana Yesu mwenyewe….

Luka 14:12 “Akamwambia na yule aliyemwalika, Ufanyapo chakula cha mchana au cha jioni, usiwaite rafiki zako, wala ndugu zako, wala jamaa zako, wala jirani zako wenye mali; wao wasije wakakualika wewe ukapata malipo.

13 Bali ufanyapo karamu waite maskini, vilema, viwete, vipofu,

14 nawe utakuwa heri, kwa kuwa hao hawana cha kukulipa; kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki”.

Sasa, kutokana na hali nzima ya mazingira yaliyokuwa yanaendelea pale, kila mtu anatamani angepewa heshima ya mbele, aketi katika viti vya mbeleni, awe wa kwanza kulishwa keki, kutambuliwa..Ndio sasa tunaona huyu mtu mmoja aliyealikwa anatokea na kumwambia Bwana ama! kweli! HERI HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU..

Alipiga hesabu akasema kama duniani mambo ndio hivi, itakuwaje mbinguni mtu kupewa heshima ya juu zaidi katika karamu ile ya mwana-kondoo?.. Kuwa wa kwanza kulishwa MKATE wa mbinguni..Kupewa heshima ya viti vya mbele..Kuketi karibu kabisa na Kristo, kuzungumza naye kama mgeni rasmi mwalikwa..Utajisikiaje siku hiyo, kwenye meza moja na Ibrahimu, na manabii na mitume wa Kristo, mnacheka na kufurahi na Kristo akiwa katikati yenu…Ukiangalia wengi mmealikwa lakini si wote mpo katika meza moja na Bwana..

Mathayo 8:11 “Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;

12 bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

Leo hii yeye akiwa hapa duniani ataachaje kusema.. Heri yule atakayekula mkate katika ufalme wa Mungu?..Hata mtu yeyote anayejua thamani ya sherehe, anaelewa ni raha gani unajisikia unapopewa heshima ya juu zaidi katikati ya waalikwa.

Ndugu yangu karamu ya mwana-kondoo ipo karibu sana.. SIku ile ambayo parapanda italia, na wafu kufufuka, wakiungana na wale ambao watakuwa hai wakati huo, wote kwa pamoja wataisikia sauti ya Bwana Yesu ikiwaita hapo juu..Siku hiyo ndipo watakapoacha ardhi, na moja kwa moja safari ya kuelekea katika malango ya mbinguni itaanza..Siku hiyo wale walionyakuliwa hawataamini kwa macho yao kama kweli ndio siku hiyo imefika..Lakini ndivyo ilivyo wataanza safari mpaka mbinguni huku mabilioni kwa mabilioni ya malaika yakiwalaki..

Na moja kwa moja watapelekwa katika ukumbi wa kimbinguni usioelezeka kwa uzuri wake, miili yao wakati huo itakuwa imebadilishwa, watakuwa kama malaika..wana mavazi mazuri meupe yanayong’aa kama jua, wataketishwa katika sehemu waliyoandaliwa karamuni..Watayaona yale makao waliokuwa wamekwenda kuandaliwa kwa zaidi ya miaka 2000, na YESU.. Watazimia mioyo kwa furaha, wataketi watakula na kunywa na Bwana divai mpya..Watamwona Mungu,..watafurahi milele na milele.

Mathayo 26:29 “Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu’’.

Lakini wakati huo huku chini, mambo yatakuwa tofauti wengine watakuwa wakilia na kusaga meno. Wakihangaika katika dhiki ya mpinga-kristo,.Wengine watakuwa wanajuta..

Ndugu dalili zote zimeshatimia, pengine sisi sote tutashuhudia tukio hili la kunyakuliwa kwa kanisa siku za hivi karibuni..Lakini swali linakuja Je! na wewe ni mmojawapo wa watakaonyakuliwa? Je! unaouhakika hata ukifa leo utakuwepo katikati ufufuo wa kwanza? Kama hujui basi ni ishara kuwa utabaki hapa duniani, ndugu umgeukie Mungu angali muda unao, Tubu dhambi zako kuwa maanisha kumuishia Mungu katika kipindi hichi kifupi cha kumalizia ili kama akirudi hapa katikati nawe uwe mmojawapo wa wale watakaokwenda naye.

Ufunuo 19:6 “Nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, na kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi yenye nguvu, ikisema, Haleluya; kwa kuwa Bwana Mungu wetu, Mwenyezi, amemiliki.

7 Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.

9 Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

Bwana akubariki.Tafadhali Share ujumbe huu na kwa wengine. Pia usiache kutembelea website yetu hii (www wingulamashahidi org) kwa mafundisho zaidi.

Maran Atha . Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

Yeshuruni ni nani katika biblia?

JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.

MKUU WA ANGA.

ANTIPA SHAHIDI WANGU, MWAMINIFU WANGU.

Tofuati kati ya Myahudi, Mwisraeli na Muebrania ni ipi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NAKUTAKIA HERI YA MWAKA MPYA!

Shalom. Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…

Ni kwa Neema za Bwana tumeuona tena mwaka huu mpya wa 2020. Si wote waliovuka lakini sisi tumevuka..Utukufu na heshima na shukrani zina yeye. Amina.

Nakutakia mafanikio katika huu mwaka ulioanza. Mafanikio ya roho yako..ambayo hayo yatazaa mafanikio mengine yote yaliyosalia..kama maandiko yanavyosema katika..

3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”.

Katika Mwanzo wa mwaka wana wa Israeli waliachiliwa kutoka katika nyumba ya utumwa, wakawa huru, Hivyo Bwana akuachilie nawe pia kutoka katika nyumba ya utumwa wa Ibilisi katika jina la Yesu Kristo. Kila aina ya mikakati na vifungo vya Ibilisi Bwana akaviweke mbali nawe katika mwaka huu wa 2020. Ulioanza. Kila kilichokuwa kigumu Bwana akakifanye kuwa kilaini.

Pale ulipokuwa huwezi kusonga mbele katika Imani kutokana na majaribu mazito ya Adui..Bwana akayazuie katika mwaka huu katika jina la Yesu Kristo.

Mwaka huu ukawe mwaka wa Bwana, na kila ufanyalo kwa ajili ya Bwana, na kwa ajili yako binafsi likafanikiwe na kustawi.

Nakumbuka mwaka Fulani nyuma..tulikuwa tunafanya kila siku jioni ibada ndogo nyumbani..Tulikusudia kupitia vitabu vyote vya biblia sura baada ya sura, kila siku sura moja..Sasa miezi michache kama miwili na nusu hivi nyuma kabla ya mwaka huo kuisha tulianza kujifunza kitabu cha Zaburi..ikawa kila siku tunasoma mlango mmoja…hivyo hivyo, kama kawaida kesho tunafuata mwingine..maana yake baada ya siku 30 tulikuwa tumeshasoma Sura 30 za kitabu hicho…

Hatukuacha hata siku moja..Wakati tunaendelea kila siku kukichambua kitabu hicho, hapo ni baada ya kumaliza baadhi ya vitabu vingine vya nyuma, sasa ilipofika tarehe 31 Disemba usiku tulikuwa tumefika sura ya 65 ya kitabu hicho cha Zaburi..Siku hiyo hatukusoma tukatenga siku hiyo iwe maalumu kwa kumsifu Mungu na kumshukuru na kumwimbia..Hivyo tukasema tutaisoma hiyo sura ya 65 kesho yake yaani tarehe 1.. Tulimwimbia Mungu na kumsifu kwa namna isiyo ya kawaida, Ilipofika terehe moja jioni, tukakusanyika tena tuendelee na kitabu chetu hicho ambacho siku hiyo tulikuwa tumefika mlango wa 65. Je! Unajua katika mlango huo ndani yake tulikutana na nini?

Tusome..

Zaburi 65:9 “Umeijilia nchi na kuisitawisha, Umeitajirisha sana; Mto wa Mungu umejaa maji; Wawaruzuku watu nafaka Maana ndiwe uitengenezaye ardhi.

10 Matuta yake wayajaza maji; Wapasawazisha palipoinuka, Wailainisha nchi kwa manyunyu; Waibariki mimea yake.

11 UMEUVIKA MWAKA TAJI YA WEMA WAKO; Mapito yako yadondoza unono”

Mstari huo wa 11 unaosema “Umeuvika mwaka taji ya wema wako”.. ndio ukawa neno la Mwaka wetu..

Ilitufariji sana…hatukujua kuwa sura hiyo ya 65, inazungumzia habari ya mwaka mpya…hivyo ukawa ndio uthibitisho Mungu kazungumza na sisi, na kutupa Neno la Mwaka….Tukafahamu kumbe, ibada zetu zote zilikuwa zinahesabiwa!..Kumbe kila sura ilikuwa inahesabiwa..na hivyo Mungu ameilengesha ile siku ya tarehe moja katika mlango ule.

Na mwaka huo ulikuwa ni mwaka wa wema kweli wa Mungu kwa wote tuliokuwepo pale..Bwana alitufanyia wema mwingi sana sana kupita kiasi..kulitimiza Neno lake hilo alilotuambia.

Hivyo leo hii neno hili pia liwe lako. Bwana akauvike mwaka wako “taji ya wema wake”. Ukaone maajabu ambayo hujawahi kuyaona katika Maisha yako. Bwana akaufanye mwaka wako huu uwe mwaka wa Pentekoste, mwaka wa kumzalia matunda, mwaka ya kuishi maisha yampendezayo mwaka wa furaha na mafanikio. Akakubariki kila unapoingia na kila unapotoka.

Lakini Pamoja na Baraka hizo zote, pia nakukumbusha mwaka huu walee wanao katika njia iliyobora Zaidi ya kumcha Mungu kuliko mwaka jana. Usimnyime mwanao mapigo pale panapostahili kwasababu biblia inasema hatakufa!. Na pia mwaka huu fanya bidii kupiga hatua moja mbele, usiwe mvivu wa kufunga, pale ikupasapo kufunga na kuomba.. Usikubali kiwango kile kile cha rohoni ulichokuwa nacho mwaka jana, uwe nacho tena mwaka huu..Zidisha kiwango chako cha usafi na utakatifu..Anza mwaka wako na Bwana, Mwaka huu hesabu matunda utakayomletea Bwana yawe ni mara 10 zaidi ya mwaka jana..Yaani kwa ufupi kila kitu ulichokizembea mwaka jana usikiruhusu kivuke mwaka huu..

Na kwa kufanya hivyo Mungu kama alivyosema katika Neno lake, atakujilia na kukustawisha na kukutajirisha sana, na kisha ATAUVIKA MWAKA WAKO TAJI YA WEMA WAKE.(Zaburi 65)..Ndivyo itakavyokuwa kwako kwa jina la YESU KRISTO.

Amen.

Heri ya mwaka mpya 2020.

Mada Nyinginezo:

NI NINI KINAKUPATA UNAPOIPUUZIA INJILI?

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

OKOA BADALA YA KUANGAMIZA!

SAA YA KIAMA.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NI NINI KINAKUPATA UNAPOIPUUZIA INJILI?

unapoipuuzia injili unayohubiriwa mwaka mzima, Ni nini kinakupata?


Siku zote kuna makundi mawili ya watu. Kundi la kwanza ni watu ambao wakishaisikia injili kidogo tu, na kuchomwa dhimira zao ndani saa hiyo hiyo wapo tayari kutii na kutubu na kugeuka, mfano wa kundi hili tunalona katika siku ile ya Pentekoste, Mtume Petro alipofungua kinywa chake na kuanza kuwahubiria wale watu waliokuwa wanawashangaa walipokuwa wananena kwa lugha nyingine. Tunaona kwa maneno machache tu ya Petro, wengi wao walikuwa tayari kutubu na kugeuka.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu’’.

Lakini kundi la pili: Ni lile ambalo hata lihubiriweje injili, hata lioneje miujiza mingi kiasi gani, hata livutwe kwa maneno ya rohoni mazuri namna gani, hata lihubiriwe kuanzia asubuhi hadi jioni, bado litafanya moyo yao kuwa mgumu tu. Mfano wa kundi hili tunaliona kwa mtume Paulo pale alipofika Rumi na kukutana na mkusanyiko mkubwa wa watu ambao walikuwa tayari kumsikia kuanzia asubuhi mpaka jioni tusome.

Matendo 28:23 “Wakiisha kuagana naye siku, wakamjia katika nyumba aliyokaa, watu wengi sana, akawaeleza kwa taratibu na kuushuhudia ufalme wa Mungu, akiwaonya mambo yake Yesu, kwa maneno ya sheria ya Musa na ya manabii, tangu asubuhi hata jioni.

24 Wengine waliamini yale yaliyonenwa, WENGINE HAWAKUYAAMINI”.

Hata sasa kuna watu wanahubiriwa injili tangu mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka, lakini hawataki kugeuka, japo wanaisikia injili ikihubiriwa mitaani kwao, wanaisikia ikihubiriwa kwenye maredio kila siku, wanasikia injili ikihubiriwa kwenye matelevisheni, lakini bado wanafanya mioyo yao kuwa migumu, wanasikia injili ikihubiriwa mitandaoni kama hivi sasa, kuanzia mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka lakini wanapuuzia tu,wanaona ni kama habari zisizokuwa na manufaa yoyote katika maisha yake….Lakini hawafahamu kuwa maisha yao yapo hatarini sana.

Ndugu Neema ya Kristo si “jua” kwamba itakuwepo wakati wote, Jua likizama leo kuna matumaini kesho yake tena kuchomoza lakini neema ya Kristo ikishakupita ndugu, ndio imekupita hivyo milele, hutasema siku moja nitamgeukia Mungu, kwasababu kumgeukia Mungu ni kitendo kinachochochewa na Roho Mtakatifu mwenyewe, na si kama mtu atakavyo maandiko yapo wazi yanasema hivyo, “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka;(Yohana 6:44)”..Sasa kama Roho wa kukuvuta kwa Mungu hayupo ndani yako, kwamwe hutakaa umfuate Mungu kwa mapenzi yako mwenyewe au kwa jitihada zako..Badala yake kama ulikuwa zamani unasikia kuchomwa unaposikia mahubiri safari hii husikii tena hiyo hali ndani yako..Kama ulikuwa una kiu ya kusikiliza habari za Mungu hiyo kiu inakatika ndani yako…Ukiona hivyo ile nguvu ya kukuvuta kwa Mungu imeshaondolewa kwako.

Na biblia utakiona kama kitabu cha kipuuzi tu kwako, utaishia kukisoa, au kutokiamini kabisa..Hata uhubiriweje injili utasema hawa walokole, wanamsubiria Yesu ambaye harudi wamechanganyikiwa, utasema hakuna unyakuo, utakuwa unajiona unajua kila kitu…Utakuwa huna tofauti na mpagani ambaye hajawahi kumjua Mungu kabisa..

Na kibaya zaidi utakapokuwa unafanya hivyo utakuwa na uhakika wa unachokisema, utajiamini kupita kiasi, wala hutasikia hukumu yoyote ndani yako, kwamba kitu unachokifanya sio sahihi, hilo jambo hutasikia kabisa kwasababu Roho wa Mungu alishaondoka ndani yako siku nyingi..leo hii Unapoona watu wa mataifa wanavyomtukana Mungu usidhani ni wajinga sana, au si watu wa kutafakari sana, si wajinga ni kwasababu Yule Roho wa kuwavuta kwa Mungu hayupo ndani yao, wanatafuta point katika kitu point katika biblia hawaioni, wanatafuta kitu kimoja angalau cha kuwashawishi kuhusu Yesu ili waamini hawakioni…

Na ndio maana wanakufa katika dhambi zao, hata kama umshuhudie vipi habari za kuzimu, Zaidi sana ataishi kukutukana tu. Hafanyi hivyo makusudi, ni kwasababu ni kweli ndani yake hakuna chochote kinachomshawishi au kinachompa kila sababu ya yeye kuamini..

Na ndivyo itakavyokuwa kwa mtu Yule anayeichezea neema anayohubiriwa kila siku.

Biblia inaeleza pia katika agano la kale, kwamba unapofika mwaka wa maachilio, yaani mwaka wa watumwa wote kuwekwa huru..Ni sharti mabwana zao wawaache huru, amruhusu kila mmoja arudi nyumbani kwake kama alichukuliwa kwao, au aende kwake kama alishakuwa na kwake. ..Lakini sasa kama ikitokea mtumwa Yule anaukataa uhuru aliopewa..Yaana kwa mapenzi yake mwenyewe anasema mimi sitaki kuondoka kwa bwana wangu nataka kuendelea kuwa mtumwa wake milele. Soma.(Kumbukumbu 15:17)

Basi Yule Bwana wake anachofanya ni kuchukua uma wa moto, na kumtoboa sikio lake.. Na ile inakuwa kama muhuri kuwa Yule mtumwa sasa atamtumikia Bwana wake milele..Kama vile lile shimo katika sikio linavyokaa milele, ndivyo hivyo na yeye atakavyokaa katika hali hiyo ya utumwa milele.

Na leo hii Mungu anatutangazia mwaka wa maachilio, kwa kupitia damu ya mwanawe mpendwa Yesu Kristo kwamba kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele. Lakini kama inatokea mwaka huu tuliopewa wa maachilio, tunauchezea, bado mguu mmoja upo nje mwingine ndani, bado tunaendelea kuutamani utumwa wa shetani ambao ametutumikisha kwa muda mrefu, na haujatupa faida yoyote, bado tunataka kuendelea kuishi katika maisha ya kwenda motoni..Basi tujue kuwa tumetaka hivyo kwa hiari yetu wenyewe.

Sasa kitu kinachofanyika hapo katika ulimwengu wa roho, Yule bwana wako, ambaye ni shetani anakuja na uma huo wa moto, na kuupitisha katika sikio lako la rohoni..Na hiyo inakuwa ishara kwamba wewe ni wake milele..Ukishafikia hatua hiyo basi ile neema ya Mungu unakuacha, wala Mungu hashughuliki tena na wewe. Unakuwa mtu wa tofauti na pale ulipokuwa mwanzo, unaishi kuwa mtoto wa shetani ukisubiria kufa uende kuzimu.

Tangu Januari mpaka Disemba hii unasikia injili, Mungu anakupa neema ya kuwa na pumzi ya kuishi, aone kama huu mwaka hautaisha unamgeukia yeye, lakini bado hufanyi hivyo, alikutazama miaka ya nyuma lakini bado ukawa vilevile, na tena unaenda kuingia mwaka mwingine mpya, na bado unataka kuendelea kuwa katika hali hiyo hiyo ya dhambi..Unadhani neema ya Kristo itazidi kukusubiria hivyo milele?..Ule Uma shetani ameshauandaa, anasubiria wakati wake ufike tu..Na moja ya hizi siku usipokuwa tayari kuchagua njia ya kuiendea, ibilisi atakuchagulia njia kwa nguvu.

Ndugu kitu cha kuthamini cha kwanza katika maisha yako ni hii neema, ambayo haipo kwa watu wote. Mpaka sasa Bado unaendelea kunywa pombe, bado unaendelea kuzini, bado unaendelea kwenda disko, bado unatazama pornography, bado unafanya masturbation na hali unajua kabisa ni dhambi.. bado unafanya biashara haramu, bado unakula rushwa, bado ni mchawi na mshirikina wa chinichini, bado unakwenda kwa waganga, bado unaendelea kuishi na huyo mtu ambaye hamjafunga ndoa, ambaye si mke wako wala mume wako..Na kibaya zaidi wakati huo huo bado unaisikia injili ya kristo na kuipuuzia.

Injili ya Kristo sio kiburudisho kama miziki ya dunia hii ambayo unaisikiliza unapotaka kupunguza mawazo..Biblia imesema kuwa “Mungu hadhihakiwi, apandacho mtu ndicho atakachovuna”

Yageuze maisha yako kwa Bwana..Na yeye yupo tayari kukubadilisha kama utataka kumpokea leo hii. Anachotaka kwako ni aumue kwa moyo wako wote kugeuka leo, na sio nusu nusu, kama bado hujafikia kiwango cha maamuzi hayo ni heri uendelee tu..Kwasababu Mungu hatakugeuza na kukufanya kuwa mtu mwingine kama utakuwa bado unayatamani maisha ya dhambi..

Lakini kama unasema leo hii nipo tayari kumgeukia Yesu Kristo na nataka kuanza mwaka wangu mpya nikiwa ndani ya wokovu. Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika hali ya utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI KWA MUDA MREFU, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU KWA KUTOKUITII SAUTI YAKO KWA KIPINDI CHOTE HICHO. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KWA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo. Ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo kuanzia dakika hii, unaanza kwenda disko kuanzia sasa, unaacha pombe, sigara, uasherati, wizi, na unawasamehe wote waliokukosea kutoka moyoni kabisa.

Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile baada ya hapo unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwabudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako(Sawa sawa na Matendo 2:38). Ubatizo ni agizo la msingi kwa mtu Yule aliyeokoka hivyo usilipuuzie, hata kidogo, wala usijikawiishe kupata ubatizo.

Zingatia hayo na Bwana atakuwa pamoja nawe. Vilevile Usiacha kutembelea Website hii https://wingulamashahidi.org mara kwa mara ili ujifunze maneno ya uzima yatakayokusaidia kukua kiroho katika wakati huu wa kumalizia.

Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

NUHU WA SASA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI NAYAWEZA MAMBO YOTE KATIKA YEYE ANITIAYE NGUVU?

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu..


Wafilipi 4:12 “Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.

13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.

Huu ni mstari unaohamasisha sana, hususani  tunapopitia katika hali Fulani ngumu, pale tunapoona hatuwezi kuvuka au kuendelea mbele katika kitu fulani, pale tunapoona bado hatua moja tu ya sisi kukata tamaa.. Lakini tunapousoma mstari huu unatupa nguvu ya kuendelea mbele.. Na kubakia kusema..

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu..

Lakini kama ukisoma vizuri mistari ya juu yake utaona mtume Paulo anazungumzia mambo aliyoyapitia huko nyuma, kuna wakati alipitia kufanikiwa sana, vilevile kuna wakati alipitia kuishiwa sana, akawa hana hata shilingi mfukoni mwake, au kama anayo basi ni kidogo sana ukilinganisha na mahitaji aliyokuwa nayo.Tunalithibitisha hilo, wakati Fulani Paulo akiwa   Rumi alimwagiza Timotheo na kumwambia siku atakapokwenda aende la lile joho lake aliloliacha kwa Karpo kabla ya wakati wa baridi kuanza.

2Timotheo 4:13 “Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi”.

Kulikuwa hakuna sababu ya Paulo kumwambia Timotheo ambebee joho lake asafiri nalo mamia kama sio maelfu kwa maelfu  ya kilometa na mzigo wa koti, Mtume Paulo angeweza tu kununua joho(koti) lingine kule kule kama angekuwa na fedha ya kutosha, lakini hiyo yote ni kwasababu wakati wa kupungukiwa ulimpitia, lakini hakuiacha imani na maneno yake yalikuwa ni haya.. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Paulo anasema tena nimefundishwa kushiba na kuona njaa.. Katika ziara zake za kuhubiri injili alipitia vipindi vigumu sana mahali ambapo hakukuwa na namna yoyote ya kupata chakula, tunaweza kuliona pia hilo wakati ule alipokuwa anasafirishwa pamoja na wafungwa wengine kuelekea Rumi..Wakiwa kule kilindi kwa muda mrefu waliishiwa na chakula, mpaka watu waakanza kuishiwa na nguvu..Lakini Mungu alimuuokoa yeye pamoja na wafungwa wale katika hali ile, wala hakutetereka katika imani yake..

Matendo 27:20 “Jua wala nyota hazikuonekana kwa muda wa siku nyingi, na tufani kuu ikatushika, basi tukakata tamaa ya kuokoka.

21 Na walipokuwa wamekaa wakati mwingi bila kula chakula, Paulo akasimama katikati yao, akasema, Wanaume, iliwapasa kunisikiliza mimi na kutokung’oa nanga huko Krete, na kupata madhara haya na hasara hii.”

Na ndio maana hata huku mbele anaoujasiri wa kusema..

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu..

Anasema tena, nimefundishwa kuwa na vingi na kupungukiwa. Kuna wakati alifika hakuwa na haja ya kitu chochote, mpaka akawa na kitu cha kuwagawia wengine, lakini pia kuna wakati ulifika wa kupungukiwa lakini katika hayo yote kimiujiza ujiza katika vipindi hivyo vyote, baridi , joto, mvua na mafuriko hakutikisika hata kidogo katika imani yake..Anasema:

2Wakorintho 11:26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;

27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi.

28 Baghairi ya mambo ya nje, yako yanijiayo kila siku, ndiyo maangalizi ya makanisa yote.

 Unaona, mtu kama huyu pamoja na kupitia taabu zote hizi, na bado hajaiacha imani ataachaje kusema..

“Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”?

Lakini nataka nikuambie mpaka mtu apokee uweza huu wa kuweza mambo yote..Si suala la kujiamulia tu mtu mwenyewe kwa bidii zake, au kujitamkia tu kwa kinywa chake..Unaweza ukajitamkia kuanzia januari mpaka Disemba kwamba “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”. Lakini ikija tufani kidogo tu  unaweza kwenda na maji.

 Kama wewe sio mkristo, ukweli ni kwamba huyawezi mambo yote..Kama unajiita mkristo halafu hujaokoka,  bado huyawezi mambo yote..Wala usijidanganye kusema hivyo,…Hutakaa uweze kushinda majaribu yote ya huu ulimwengu na bado ukadumu kwa Kristo kwa moto ule ule, hutakaa uweze kustahimili taabu zote na bado usifanye dhambi..Kwamwe hutakaa uweze..

Kumbuka mtume Paulo hasemi “Nayaweza mambo yote katika mimi au katika nguvu zangu”.. anasema, Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu..”Yeye anitiaye nguvu”..Hivyo ni lazima huyu akutiaye nguvu awe ndani yako ndio uwezo huo wa kuweza mambo yote ukujie.

Unajiuliza saa nyingine ni kwanini unajaribiwa na vishawishi vya uzinzi, halafu unazidiwa na tamaa unakwenda kufanya uzinzi, ni kwasababu huyo akutiaye nguvu za kuweza kushinda vishawishi hivyo hayupo ndani yako, kama angekuwepo usingekaa utamani kufanya jambo hilo..

Au ulitamani usitazame pornography, au usifanye punyeto lakini ukajitahidi siku mbili,tatu mbele. Mwezi ulipopita  ukazidiwa na tamaa ukaenda kurudia yale yale uliyokuwa unayafanya…Ni kwasababu gani? Ni kwasababu Yule ambaye angepaswa kukutia nguvu ya kuweza kushinda majaribu hayo milele hakuwepo ndani yako.

Au ulikuwa unaonyesha dalili ya kumpenda Mungu kweli, lakini ulipokutana na vita kutoka kwa ndugu au wazazi wako, au marafiki wako, wakakuzidi nguvu, ukayarudia yaleyale uliyokuwa unayafanya mwanzoni kwa kuogopa tu utatengwa au utachukiwa..Ni kwasababu gani ulishindwa kustahimili? Ni kwasababu Yule akutiaye nguvu hakuwa ndani yako.

Au ulikuwa ni mkristo mzuri tu, unashuhudia hata wengine habari njema..lakini labda ulipitia hali Fulani ngumu ya kiuchumi, ukayumba kidogo na hiyo ikakufanya uamue kuacha wokovu wako na kwenda kujichanganya na dunia..Ni kwanini ulishindwa kuendelea mbele na imani? ni kwasababu Yule akutiaye nguvu ulishamwacha zamani.

Au sio tu katika shida, bali pia hata katika mafanikio,..Pengine Mungu alipokufanikisha katika kitu Fulani, labda pengine alikupa kazi nzuri yenye mshahara mkubwa, au alikupa nyumba nzuri, au alikupeleka nchi za nje kuishi, au alikuponya ugonjwa wako, na matokeo yake umemsahau Mungu wako umeyarudia yale yale ya zamani..Na leo hii unajiuliza imekuwaje kuwaje nimechukuliwa kirahisi na fahari za ulimwengu huu.. Jibu ni kwamba Yule akutiaye nguvu amekuacha na ndio maana huyawezi mambo yote.. Katika hayo bado huwezi kudumu katika njia wa wokovu..Umepimwa katika mizani nawe umepunguka.

Lakini leo hii ukasema ninataka kuanza upya na Bwana, ninataka atembee na mimi, anipe uwezo wa kuyaweza mambo yote, katika milima awe na mimi kunitia nguvu, katika mabonde awe na mimi kunifariji, katikati ya maadui awe na mimi kama mchungaji wangu, katikati ya vilindi awe nahodha wangu, katikati ya raha awe furaha yangu nisimuache..katikati ya mafanikio awe tajiri wangu, katikati ya afya awe sifa yangu..katika chochote kile kiwe ni chema au kibaya, bado awe ni Bwana na mwokozi wa maisha yangu..

Nami niwe na ujasiri wa kusema.. “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu” Shetani haniwezi kwa wimbi lolote atakalolita mbele yangu.. Unahitaji uwezo huo sasa ukujie??

Kumbuka ili uweze kupokea nguvu hizo kutoka kwa Bwana, yeye anachotaka kwako tu ni MOYO wa TOBA unaotamani tu kugeuka na kuacha..Moyo uliomaanisha kweli kweli kuacha hivyo vitu..Watu wengi hawaoni matokeo yoyote au badiliko lolote katika maisha yao kwasababu tu, hawamaanishi kuviacha vitu walivyokuwa wanavifanya nyuma.

Mwingine ni mlevi, anataka Mungu ampe nguvu ya kuacha ulevi, lakini hayupo tayari kuacha ulevi wenyewe, mwingine anakula ugoro, mwingine anavuta sigara, mwingine madawa ya kulevya, mwingine punyeto, mwingine ukahaba, wote hawa wanataka Mungu awepe nguvu ya kuacha lakini wao wenyewe bado wanatamani kuendelea kufanya hivyo vitu..

Ukisema nataka niache, unatakiwa umuonyeshe Mungu unakichukia hicho kitu kweli kweli, na kwamba ndio sababu ya kukupeleka kuzimu..Mungu anataka watu wanaomaanisha na sio watu wanaojaribu..Na Mungu akishaona moyo wako kama huo ambao unaambata na vitendo basi moja kwa moja anakushushia nguvu ya ajabu ambayo hiyo itakufanya wewe uone yale uliyokuwa unayafanya nyuma ni takataka na uozo,..

Sisi tulikuwa ni wazinzi wa kupindukia, tulikuwa ni watazamaji wa pornography, tulikuwa ni walevi, tulikuwa ni watukanaji lakini uwezo huo uliposhushwa juu yetu KIU ya hayo mambo yote yalikatwa ghafla. Na muda  wote tulikuwa tunatamani tu kumjua Mungu..Na hadi sasa ni miaka mingi imepita hata chembe ya mambo kama hayo haipo ndani yetu.. haijalishi ni vishawishi vingapi vinakuja mbele yetu ..tunaoujasiri wa kusema..

“Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”

Tumejengwa juu mwamba imara usioweza kutikiswa kwa kitu chochote.

Hivyo kama Mungu alikuwa mwaminifu katika Neno lake kutufanyia sisi hivyo..Anao uwezo huo pia wa kukuanyia na wewe leo hii kama utakubali..

Kama upo tayari kufanya hivyo kumpa Bwana Maisha yako…

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo. Ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako sawasasawa na Matendo 2:38. Kumbuka ubatizo sahihi ni muhimu sana kwa mtu aliyeokoka hivyo usipuuzie agizo hilo la Bwana.

Zingatia hayo na Bwana atakuwa pamoja nawe. Vilevile Usiacha kutembelea Website hii  https://wingulamashahidi.org mara kwa mara ili ujifunze maneno ya uzima..

Ubarikiwe sana.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

ANTIPA SHAHIDI WANGU, MWAMINIFU WANGU.

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

Kwanini Musa alipewa mbao mbili za mawe na sio moja au zaidi

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mungu anaweza kuongea wakati yeye ni Roho?

Swali 1: Mungu anaweza kuongea wakati yeye ni Roho?..Roho inaweza kuelewa, kutambua, kuona bila ubongo?.. Swali 2: Adamu na Hawa walimwona Mungu?.. Swali 3: Na je! Mungu anazidi kujificha kwetu au kujidhihirisha kadiri muda unavyozidi kwenda?.


Swali 1: Mungu anaweza kuongea wakati yeye ni Roho?..

Jibu: Kabla ya kwenda kwa Mungu, tuanze kwanza kwa mtu.  Mtu anapozungumza, kuzungumza kwake kunaanzia rohoni..katika roho yake ndio anazungumza..Mwili ni kama kipazia sauti cha roho katika mazingira ya kidunia… Ili kuelewa vizuri tafakari mfano ufuatao.

Umechukua simu yako na ukampigia ndugu yako (video-call) ambaye yupo mkoa mwingine au nchi nyingine..mkawa mnazungumza huku mnaonana kabisa kupitia simu…ukawa unamwona yule ndugu yako kupitia simu ile na kuisikia sauti yake…Sasa yule ndugu yako aliyeko mkoa mwingine, je anaweza kusema pasipo simu wewe huwezi kuzungumza naye?..Jibu ni hapana…unaweza kuzungumza naye hata pasipo simu, endapo akisafiri akakufuata mahali ulipo au ukimfuata mahali alipo bado mnaweza kuzungumza tu tena vizuri sana Zaidi hata ya kutumia simu…

Sasa simu ni kiunganishi tu, ambacho ili kiweze kutuunganisha na watu walioko mbali nasi kinahitaji kiwe na chaji, kiwe na betri, kiwe na network, kiwe na spika, na kiwe na jicho la kamera ili kiweze kumrekodi yule aliyeko mbali.

Na miili yetu ndio hivyo hivyo, ni kama simu tu! Ili iweze kuziunganisha roho zetu na mazingira ya kimwili Inahitaji ubongo, inahitaji moyo unaosukuma damu, inahitaji, macho mawili kurekodi matukio ya nje na kuyatuma katika roho zetu, inahitaji pua kuchukua taarifa za mwili kuzipeleka rohoni, n.k

Lakini pia pasipo hii miili tunaweza kuongea, kutazama, kuzungumza tena vizuri sana pasipo hata kuwa na miili.. Kama vile ilivyomubashara Zaidi mtu kuzungumza uso kwa uso na mwenzake Zaidi kuliko kuzungumza naye kwenye simu. Tukitoka katika huu mwili bado tunauwezo wa kuona, kusikia, kuzungumza n.k Mwili si kitu cha lazima sana kama vile simu isivyokuwa ya lazima.

Kwahiyo mwili ni njia tu, lakini mambo yote yanaanzia katika utu wa ndani. Na kama sisi tupo hivyo basi Mungu uwezo wake ni mkubwa Zaidi na mpana sana..upeo wake ni mkuu Zaidi ya huo na anaweza kufanya zaidi ya hayo. Ndio maana utaona mara kadhaa sauti ilisikika kutoka mbinguni ikisema huyu ni mwanangu mpendwa wangu.

Swali 2: Adamu na Hawa walimwona Mungu?

Jibu: Biblia haijasema moja kwa moja walikuwa wanamwona kwa namna gani, lakini kulingana na habari ile ni wazi kuwa walikuwa wanamwona kabisa wazi.

Swali 3: Kadiri muda unavyozidi kwenda, Mungu anazidi kujificha kwetu au kujidhihirisha?

Jibu: Mungu yupo karibu na sisi siku zote…hana wakati ambao alishawahi kuwa karibu nasi sana kuliko wakati mwingine wowote, wala hana wana wakati ambao alijitenga nasi. kamwe yeye yupo pale pale.  Kinachotufanya sisi tumwona yupo mbali nasi au karibu nasi ni kiwango cha maovu yetu na utakatifu wetu.

Isaya 59: 1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”.

Yakobo 4: 8  “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.

Anatushauri haya..

Kumbukumbu 30: 11 “Kwa maana maagizo haya nikuagizayo leo, si mazito mno kwako, wala si mbali.

12 Si mbinguni, hata useme, Ni nani atakayetupandia mbinguni akatuletee, aje atuambie tusikie, tupate kuyafanya?

13 Wala si ng’ambo ya pili ya bahari, hata useme, Ni nani atakayetuvukia bahari, akatuletee, aje atuambie, tusikie, tupate kuyafanya?

14 Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya.

15 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya”

Ubarikiwe.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Tafadhali share na wengine.


Mada Nyinginezo:

WEWE SI MALI YAKO MWENYEWE!

HISTORIA YA ISRAELI.

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.

SAUTI NI SAUTI YA YAKOBO, LAKINI MIKONO NI YA ESAU.

JINSI YA KUJIWEKA KARIBU NA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UMUHIMU WA YESU KWETU.

Umuhimu wa Yesu kwetu, ni mkubwa sana kama tunavyousoma katika kitabu cha .Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;”

Shalom jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tena tujifunze Neno la Mungu, ambalo ndio taa ingozayo miguu yetu na mwanga wa njia zetu.(Zab 119:105).

Kama tulivyotangulia kujifunza, na kama wengi wetu tunavyojua kwamba mtu wa rohoni sio mtu mwenye uwezo wa kuwaona wachawi..kama inavyoaminika na wengi.. Wale watu wawili waliokuwa wanakwenda Emau, macho yao ya rohoni yalipofumbuliwa hawakuona wachawi, au majini yaliyokuwa yanawazunguka..Bali walimwona Yesu.(kasome Luka 24:13-33,)

Hivyo mtu wa rohoni ni Yule mwenye uwezo wa kumwona na kumtambua Yesu Kristo katika maandiko na katika maisha yake. Mtu aliyefunuliwa macho ya rohoni atamjua sana Mwana wa Mungu, Yesu Kristo Zaidi ya kitu kingine chochote,atajua dhumuni la yeye kuja duniani ni lipi, mamlaka aliyonayo nayo ni yapi, nafasi aliyonayo sasahivi ni ipi, na ni wapi kaandikwa katika maandiko, na umuhimu wa Yesu katikati ya wanadamu…Na mtu wa namna hiyo ataishia kumheshimu na kuwa mwangalifu na Maisha yake kuwa ya kipekee sana.

Ukishindwa kumwelewa Yesu Kristo, basi haijalishi unaona maono kiasi gani, au una elimu  ya dini kubwa kiasi gani, au unaelimu nyingine kubwa kiasi gani, au unaona wachawi kiasi gani, bado wewe ni mfu kiroho na macho yako ya rohoni yamefumbwa… Kiini cha kumwona na kumjua Mungu ni Yesu Kristo.

Wakolosai 2:9  “Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”

Na ndio maana Biblia inatuambia tena katika ”..

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;”

Hivyo tunahitaji kumahamu sana huyu MWANA WA MUNGU, mafundisho yetu, mawazo yetu, shule yetu wakati wote inapaswa ilenge katika huyu mtu mmoja Yesu Kristo..Ili tuwe watu wa rohoni. Na leo kwa neema za Mungu tutajifunza kidogo juu ya huyu mwana wa Mungu (Yesu Kristo).

Tofauti na wengi tudhaniavyo kwamba Yesu Kristo anahitaji sana sifa kutoka kwetu..pasipo kumjua yeye ni nani?..Lakini ukweli ni kwamba Yesu Kristo anahitaji kwanza tumjue ndipo sifa zetu ziwe na maana kwake.  Hata katika hali ya kawaida, huwezi kuzithamini pongezi au sifa za mtu ambaye hakujui, ametokea tu huko ghafla na amesikia tu jina lako mitaani..halafu anakuja na kuanza kukupongeza na kukusifia kidogo utakuwa na mashaka..jambo la kwanza utamwuliza..je unanijua?…Tofauti na kama ingekuwa ni ndugu yako, ni wazi kuwa pongezi hizo utazithamini kwasababu anakujua sana,  anajua ulipotoka, uliyopitia, ulipo sasa na unapokwenda…

Hivyo pongezi zake zitakuwa na maana sana kwako kuliko za hao wengine ambao hawakujui wala hamjuani..Utafahamu ni za kinafki tu.

Kwahiyo hata sifa zetu tunazomsifia Bwana kama hazijachanganyikana na maarifa yakutosha ya kumjua yeye kiundani..basi sifa zetu ni za kishabiki tu ambazo hazina nguvu yoyote kwa Mungu.

Sasa hebu kwa ufupi tumwangalie kdogo huyu mwana wa Mungu (yaani umuhimu wa Yesu kwetu wanadamu).

Mungu alipomwumba Adamu alimpa mamlaka yote ya duniani..ikiwemo kutawala kila kiumbe pamoja na kuitiisha nchi..Adamu na uzao wake akafanywa kuwa mtawala wa vitu vyote..Hata shetani alikuwa chini yake,..hakuna kiumbe chochote kingekuwa na mamlaka ya  kusogeza hata jani moja isipokuwa kwa mamlaka ya Adamu, mamlaka hiyo Adamu aliendelea kuwa nayo mpaka  siku Hawa alipodanganywa na nyoka na kula tuna na kumpa mumewe..na wote wawili walipoasi hiyo mamlaka yote waliyopewa wakamwuzia shetani. Hivyo shetani akawa mtawala wa ulimwengu..akitaka kumtupia mwanadamu ugonjwa anweza, hata akitaka kumwua anao uwezo huo. Akitaka kuleta tufani anaweza na mwanadamu yoyote asimzuie.

Na hata funguo za kuzimu pia alizichukuwa shetani. Habari yetu sisi wanadamu ikawa imeishia pale, tukawa tumejiharibia wenyewe..Tukawa kundi moja na malaika walioasi, ambao wanasubiriwa kutupwa katika lile ziwa la moto…Kukawa hakuna tena nafasi ya kusamehewa, njia ya uzima ikafungwa kama ilivyofungwa kwa malaika walioasi mbinguni..shetani hakuwa na nafasi ya kutubu wala kuokolewa…Na sisi tukawa ndio hivyo hivyo..Hivyo likawa limesalia jambo moja tu mbele yetu, kufutwa sisi sote…

Lakini kwa huruma za Mungu..akatengeneza njia ya wokovu kwa mwanadamu….kwamba mwanadamu aokolewe..yaani ni kama bahati tu!..shetani na mapepo yake hawakupata hiyo bahati ya nafasi ya pili kama tuliyopata sisi. Na kwasababu ni mwanadamu ndiye aliyejiharibia hamna budi kwa njia ya mwanadamu huyo huyo ukombozi utokee.

Hivyo Mungu akaanza uumbaji mwingine wa mtu mwingine, ambaye huyo atakuwa kama Adamu..ambaye atapewa mamlaka yote ya duniani, atawale kila kitu na kila kiumbe,na vitu vyote viwe chini yake, kama Adamu, mtu huyo Ataumbwa akiwa mkamilifu na bila dhambi kama alivyoumbwa Adamu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO..Huyu Yesu ni Adamu wa Pili….Ameumbwa kwa viganja vya Mungu kwa uweza wa Roho katika tumbo la Bikira. Huyu alikuwa ni mwanadamu kabisa, lakini kuna SIRI kubwa iliyokuwepo ndani yake…japokuwa alionekana kama mwanadamu lakini alikuwa ni Mungu mwenyewe aliyeuvaa mwili..(kasome 1Timotheo 3:16). Lakini hilo halikuwa la muhimu sana sisi kulijua ndio maana biblia ikaliita ni siri..

Hivyo wakati wa Yesu Kristo kama Adamu wa pili kuzaliwa, kulikuwepo na kizazi pia cha Adamu ambacho kilishaasi na hivyo kinapaswa kiondolewe kibaki kizazi cha Yesu Kristo tu!.. Sasa Yesu Kristo hakuwa na mke wa kimwili kama Adamu wa kwanza..wala hakuwa na watoto wa kimwili…Kwasababu hiyo basi ili sisi tusiangamie na hiyo ghadhabu ya Mungu itakayomwangwa juu ya uzao wote wa Adamu ulioasi akatutwaa sisi na kutufanya kuwa kama uzao wake, na ndugu zake wakike na wakiume..(akatu-adopt).

Ulishawahi kuona mtu ambaye ni tajiri sana hana watoto, anakwenda nchi ya mbali  kutafuta mayatima ambao maisha yao yapo hatarini na kuwaleta kwake na kuwafanya kuwa wanawe? (anawaa-adopt)..Ndio hicho hicho, Bwana Yesu alichokifanya kwetu…alitutwaa sisi ambao tayari tulikuwa tumeshatamkiwa hukumu na kutufanya kuwa wake..Hivyo kwa yeyote ambaye atatii na kumkubali na kujiunga naye atahesabiwa kuwa ni uzao wa Yesu Kristo,  naye pia atashiriki pamoja naye katika ufalme aliopewa na Mungu kwamba akatawale viumbe vyote, na kila kitu kilichopo duniani, na vitu vyote.

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.

Sasa kabla ya wakati wa kuondolewa uzao wote wa Adamu ulioasi haujafika,Bwana Yesu  anatuma kwanza mwaliko, kwamba popote pale wanadamu wote walipo walio wa uzao wa Adamu wa kwanza walioasi ambao wanapenda maisha, waje kwake naye atawapokea…kwamba wamwendee huyu Yesu Kristo aliyekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na duniani wapate uzima.

Na huyu Yesu alianza kutuma mwaliko huo tangu vizazi vyuma na hata sasa anatuma..kwamba ufalme wake kuanza kutawala dunia umekaribia..kwamba muda ni mchache tu tuliobakiwa nao wa sisi kuitikia wito wa kuingia ndani ya hiyo neema..Utafika wakati wa utawala wake kuanza ambapo kutakuwa hakuna tena nafasi ya mtu yoyote kuingia..Mlango wa neema utafungwa.

Luka 13:23 “Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,

24 Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu”.

Wakati huo huyu Yesu Kristo tunayemwona sasa ambaye anatusihi sasa hatakuwa hivi tunavyomwona leo..Atageuka na kuwa miale ya moto,na  Mungu atakihukumu kizazi chote cha Adamu kilichoasi na kumkataa mwanawe mpendwa…na kuwanusuru wale wote waliomkimbilia Mwanawe pekee Yesu Kristo.

Unaweza kuona jinsi hiyo neema ilivyo ya ajabu..Sisi kupata nafasi ya kufanyika Uzao wa Yesu Kristo?…Watu ambao tulikuwa tumewekwa kundi moja na malaika walioasi?..

1Petro 2:9 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema”.

Ndugu Bwana Yesu ndiye aliyekabidhiwa kila kitu sasa…Hajaanza kutawala kwa utukufu wake sasa wala kuushusha  ufalme wake, kwasabababu bado anataka watu watubu ili wasiangamia…lakini fahamu kuwa ufalme wake umekaribia sana…na siku atakapokuja mataifa yote waliomkataa wataomboleza na kulia….Kama ulikuwa unamfahamu tu Yesu Kristo kama “mwanadamu wa kawaida ambaye hana umuhimu sana”..leo futa hayo mawazo…Yule sio wa kawaida kabisa…kashakabidhiwa mambo yote na sasa hivi yupo mbinguni,  angekuwa ni wa kawaida angekuwa duniani sasahivi au kaburini…lakini yupo mbingu ya juu sasa, ambako hakuna aliyewahi kufika hata sasa,  anasubiri mtu wa mwisho kuingia ndani, mlango ufungwe ashuke kuja kutawala…

Mathayo 28.16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu.

17 Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka.

18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, NIMEPEWA MAMLAKA YOTE MBINGUNI NA DUNIANI”.

Je bado unamchukulia kama ulivyokuwa unamchukulia?..Je bado unaichezea neema yake hiyo?..na kuendelea kuupenda ulimwengu?..bado unaendelea kuwa mzinzi, mtukanaji, mlevi, washerati, mvaaji nusu uchi, muwekaji make-up, mvaaji suruali,mpakaji wanja, lipstick, mvaaji mawigi na maherini? bado mtazamaji picha chafu mitandaoni, mfanyaji masturbation na mhudhuriaji disko,mtoaji mimba, bado unaendelea kuishi na mwanamke/mwanamume ambaye hamjaoana n.k?..

Itakuwa ni vizuri kama utamgeukia leo..Yeye atakupokea, na wokovu ni leo na si kesho kwasababu hujui mwisho wako ni lini..Hivyo kama umeamua kuingia na kufanyika mwanawe..unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kijitenga binafsi kwa dakika chache peke yako..Kisha piga magoti na nyosha mikono yako juu kuonyesha kuwa umejishusha na umejitambua wewe ni mkosaji..

Halafu anza kutubu kwa kuyakiri makosa yako yote, na yeye atakusamehe..na ukishatubu kwa namna hiyo hakikisha unaacha yale mambo uliyokuwa unayafanya..unaacha uzinzi, unatupa makeup zote, unachoma nguo zote za kikahaba ulizokuwa unavaa, unaacha kwenda bar, unaacha pia kuvuta sigara na kujitenga na makundi yote yanayochochoe hivyo vitu.

Na ukishaacha vyote kwa namna hiyo, toba yako itakuwa thabiti..Hatua inayofuata katafute ubatizo kama hujabatizwa, ubatizo sahihi ni ule wa maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:3)Na Mungu atakupa uwezo wa ajabu wa kushinda hizo dhambi..haitakuwa ngumu kwako kuishi bila kuzifanya. Na Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia..Na kuzidi kukufundisha umuhimu wa Yesu katika maisha yako na ya watu wengine.

Kumbuka ufalme wake umekaribia..na yeye ajaye aja upesi na wala hatakawia.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:


Mada Nyinginezo:

MWANA WA MUNGU.

SIRI YA MUNGU.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

KWANINI MUNGU ALITUUMBA WANADAMU.

JE ADAMU ALIKUWA NA KITOVU?

JE ! BWANA YESU ALIKUJA DUNIANI KUAMUA NINI?

Rudi Nyumbani

Print this post

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

Tumtolee Mungu vitu vinavyotugharimu hata kuhatarisha maisha…2Samweli 23:15 Daudi akatamani, akasema, Laiti mtu angeninywesha maji ya kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango!

Shalom, Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Ni siku nyingine tumepewa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha tushiriki pamoja kujifunza maneno matakatifu ya Mungu.

Leo kwa ufupi tutaichunguza habari moja inayotoka katika  kitabu kile cha Samweli wa pili, sura ile ya 13, tunaona kuna wakati Daudi alipokuwa katikati ya vita vikali na wafilisti, wakati akiwa kule mafichoni katika pango moja lijulikanalo kama pango la Adulamu, alitamani maji ya Kisima kilichokuwa Bethlehemu Lakini wakati huo  mji wa Bethlehemu ambao ndio ulikuwa mji wa Daudi ulikuwa umezungukwa na wafilisti (Maadui zao), na ndipo walipokuwa wameweka kambi zao hapo.. Hivyo Daudi akiwa kule mabondeni biblia inatuambia alitamani sana maji ya kisima cha Bethelehemu kule maadui zake walipo, Hivyo watatu kati ya wale mashujaa wake 300 aliokuwa nayo waliposikia maneno yale ya Daudi, wao wenyewe kwa sirisiri  wakapanga mikakati ya kwenda kumletea Daudi maji ya kisima kile bila hata ya kumwambia..

Ndipo wakaanza safari kutoka katikati ya kambi ya Daudi, wakaondoka hivyo hivyo bila kujali wanakwenda kuingia katika kambi ya maadui zao, kwasababu ilikuwa ili kufikia Kisima hicho ni lazima upenye katikati ya wafilisti, lakini wao waliondoka hivyo hivyo, hatujui walitumia njama gani, lakini walidhubutu kuhatarisha Maisha yao, kwa hali na mali ili tu wafikie azimio lao, la kuchota maji yale ya Kisima kile na kumletea Daudi..

Halikuwa jambo rahisi ni sawasawa na wewe leo uone umewekewa simba 100 mbele yako, halafu nyuma yao kuna lulu unayopaswa ukaichukue, si jambo rahisi kibinadamu lakini hawa mashujaa watatu wa juu wa Daudi hawakujali hilo, walifanikiwa kweli kupenya katikati ya wale watu kisirisiri, na kuyachota maji yale ya Kisima cha Bethlehemu na kumletea Daudi…Lakini Daudi alipoona Maji yale, tunaona mwitikio wake ulikuwa ni kinyume na matazamio yao..tusome..

2 Samweli 23:13 “Tena, watatu miongoni mwa wale thelathini waliokuwa wakuu wakashuka, wakamwendea Daudi wakati wa mavuno mpaka pango la Adulamu, na kikosi cha Wafilisti walikuwa wamefanya kambi katika bonde la Warefai.

14 Naye Daudi wakati ule alikuwako ngomeni, na jeshi la Wafilisti wakati ule walikuwako Bethlehemu.

15 Daudi akatamani, akasema, Laiti mtu angeninywesha maji ya kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango!

16 Basi hao mashujaa watatu wakapenya jeshi la Wafilisti, wakateka maji kutoka kile kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango, wakayachukua, wakamletea Daudi; walakini yeye hakukubali kuyanywa, akayamimina mbele za Bwana.

17 Akasema, Hasha, Bwana, nisifanye hivi; je! Si damu hii ya watu hao waliohatirisha nafsi zao? Kwa hiyo hakukubali kuyanywa”.

“Hayo ndiyo waliyoyafanya wale mashujaa watatu”

Kama tunavyoona hapo, Daudi hakudhubutu kuyanywa maji yake.Kwa nje yalikuwa yanaonekana ni maji lakini kwa ndani Daudi aliyaona ni damu.. Na damu sikuzote huwa hainywewi, kwasababu damu inabeba uhai..Na uhai unazungumza..

Daudi aliona maji yale ni dhabihu tosha ambayo haistahili kutolewa kwake ili kwa Mungu tu peke yake. Na ndio maana alichokifanya ni kuyachukua yale maji na kwenda kuyamwaga mbele za Bwana.. kama vile damu imwagikayo kwa ajili ya dhabihu.

Hivyo tunaona badala maji yale kuenda tumboni mwa Daudi, yalikwenda moja kwa moja hadi katika madhabahu ya Mungu mbinguni..Na hivyo bila shaka kwa tendo lile si tu Mungu kuwarehemu wale watu kwa jicho la tofauti bali pia kuwapa ushindi dhidi ya maadui zao.

Habari hiyo inafunua nini katika agano  jipya tulilopo?

Daudi anamfunua Bwana wetu Yesu Kristo, kumbuka wale mashujaa wa Daudi walikithamini kiu cha Daudi hawakujali kuwa hata pale kulikuwa na maji mengi tu si angekunywa ya pale  kwanini atafute ya mbali, lakini wao hawakujali hilo..na hivyo wakawa tayari kuhatarisha Maisha yao kwa ajili tu ya kuishibisha kiu yake, Hivyo kwa tendo lile ikamfanya Daudi asiyanywe maji yale, bali kwenda kuyamwanga mbele za BWANA.

Kristo naye alipokuwa msalabani alisema ninaona KIU..Lakini wale askari hawakuithamini kiu yake..Vilevile hadi sasa Kristo anasema ninaona kiu, lakini wengi wetu tunaidharau kiu yake tunaona kama anataka kutuau huyu, kutufilisi, yeye si ana kila kitu iweje tena atuombe sisi maji, utasema ni wapi kwenye maandiko Yesu anasema nina kiu..ukisoma Mathayo 25 utaona  anawaambia wale watu aliowafananisha na mbuzi kuwa alikuwa na kiu lakini hawakumnyeshwa, vilevile na wale wengine ambao aliwafananisha na kondoo akiwaambia  nilikuwa nina kiu na mlininywesha..

Ni kweli tunamnywesha kila siku maji kwa matoleo yetu, lakini Je! Maji hayo tunaweza kuyageuza kuwa Damu?. Kiasi kwamba ashindwe kuyanywa na kuyamwaga mbele za Mungu mbinguni kama dhabihu?

Kristo anatazamia, tumtolee kilicho bora, bila kujali inatugharimu kiasi gani..bila kujali tutapoteza nini, au tunapata hasara kiasi gani baada ya hiki, na hiyo yote ni kwa faida yetu sisi wenyewe (anataka tumtolee Mungu vile vinavyotugharimu)….Na kwa kufanya hivyo..haitamfikia tena kama maji yakatayo kiu,.. bali sadaka yako itamfikia kama DAMU..kama uhai wako mwenyewe..

Ukiingia  gharama kubwa kumpa Kristo kitu Fulani  jambo ambalo mtu wa kawaida hawezi kufanya, ..mbinguni unahesabika ni kama umemwaga damu yako kwa ajili yake..Haijalishi hicho kitu ni kidogo kiasi gani, kinachojalisha ni gharama uliyoingia. Je ni kubwa kiasi gani..mbele za Mungu, Yule mwanamke aliyekuwa mjane, aliingia gharama kubwa kutoa kila alichonacho ingawa kwa nje ilikuwa ni senti mbili tu.

Mtu anayefanya hivyo  anapata thawabu kama tu aliyechinjwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu. Hivyo tumtolee Mungu vile vinavyotugharimu Zaidi. Ili tuvuke hata kiwango vya baraka tu za kimwilini bali mpaka zile za mashahidi wa Yesu.

Tumtolee Mungu wetu kwa wingi, naye atatujaza kwa vingi.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin

Mafundisho mengine:

Tafadhali Share ujumbe huu na kwa wengine.


Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/tofauti-katika-ya-zaka-na-sadaka-ni-ipi/

SADAKA YA MALIMBUKO.

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post