NIFANYALO WEWE HUJUI SASA; LAKINI UTALIFAHAMU BAADAYE.

NIFANYALO WEWE HUJUI SASA; LAKINI UTALIFAHAMU BAADAYE.

Wakati ule ambao Bwana Yesu anawatawadha wanafunzi wake miguu, Petro alimuuliza Bwana swali la mshangao sana, lililoashiria kugoma kutawadhwa miguu na Bwana, kwasababu alitazamia kuwa wao ndio wangepaswa wamtawaze yeye miguu, na sio yeye awatawadhe wao, Lakini Bwana alimwambia maneno haya;

Yohana 13:7 “Yesu akajibu, akamwambia, Nifanyalo wewe hujui sasa; lakini utalifahamu baadaye”.

Nachotaka uone hapo  kuhusu  Bwana Yesu ni kuwa, si kila jambo analolifanya katika maisha yako sasa, au unaloliona akilitenda nje kwa wengine, ambalo hulielewi utalipatia majibu yake leo leo. Mengine amekusudia uyafahamu baadaye.

Yapo maisha Mungu anaweza kukupitisha wewe kama mkristo uliyeokoka  yakawa ni nje kabisa na matarajio yako, na ukijiangalia, huna kasoro yoyote na Mungu, lakini bado unajiuliza, kwanini mimi, mbona wenye dhambi hayawakuti kama yaliyonikutuma mimi..Kwanini matatizo haya yamenipata wakati huu, kwanini ugonjwa huu umenikuta mimi kama mtumishi wa Bwana, kwanini Mungu anaruhusu nichukiwe na ndugu zangu kwasababu ya ukristo wangu, kwanini Mungu mpaka sasa hanipi kazi, japokuwa nimekuwa nikimtumikia muda wote huu..

Maswali kama hayo alijiuliza Ayubu wakati ule alipokumbana na matatizo yasiyoeleweka chanzo chake ni nini.

Nataka nikuambie ukishajiona upo katika mazingira kama hayo, na ndani yako unashuhudiwa kabisa wewe ni mtoto wa Mungu, ni heri tu utulie, kwasababu si kila jambo utapata majibu yake leo leo, pengine ni ushuhuda Mungu anautengeneza ndani yako, ili uje kuwa msaada mkubwa sana kwa watu wengine baadaye, watakaopitia hali kama za kwako ili waimarike.

Au hata kama ikiwa ni kwa ajili yako, basi ujue lipo jambo bora Zaidi litakuja mbele yako, Hivyo usikata tamaa ya kuendelea kumtumikia  Mungu,. Yeye mwenyewe alisema..

Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.

Unaona kumbe lipo tumaini kwenye siku za mwisho, siku ambazo huwezi tena kufanya mabadiliko yoyote, siku ambazo huwezi tena kurekebisha chochote hapo ndipo tumaini linatokea.. Siku hizo zikifika utasema, ni heri wakati ule Mungu hakunipa kile, au ni heri wakati ule Mungu alinipitisha pale nione, au ni heri wakati ule Mungu hakunijibu maombi yale, leo hii ningeshakuwa nimepotea, au nimekufa, au nimepoteza kila kitu, au ningefanana na wale waliopata hasara ya nafsi zao.

Tunapaswa tusiwe watu wa kutafuta tafuta sababu za kila ugumu unaokuja mbele yetu mwisho wa siku tutakuwa ni watu wa kulaumu laumu, au kunung’unika nung’unika, si kila jambo utalipatia jawabu lake papo kwa papo, hivyo wewe ishi maisha yanayompendeza Mungu sikuzote, haijalishi mambo yatakuonyookea, au hayatakunyookea sasa.. Songa mbele na Bwana, kwasababu anajua mawazo anayokuwazia, kamwe hawezi kukuacha, utafahamu sababu za yeye kufanya hivyo mbeleni, lakini sasa mtazame Kristo.

Siku hizo ndio zile utasema ni heri nilichagua kumtafuta Mungu, faida yake leo hii nimeiona.

Vivyo hivyo yapo mambo mengi sana kama kanisa la Kristo, Bwana ametuficha leo, kuna maswali ambayo kwa namna ya kawaida hatuwezi kuwa na majibu yake sasa, lakini tutakuja kufahamu baadaye, aidha tukiwa hapa hapa duniani au tukishavuka ng’ambo.

1Wakorintho 13:12 “Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana”.

Kwahiyo, tuzidi kumtazama Bwana Yesu, tumpende, na tumwamini, kamwe hawezi kutuacha. Sifa, heshima na utufuku vina yeye milele na milele.

Amen.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

Nini maana ya “heri mtu asiyekaa barazani pa wenye mizaha?”

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

SWALI: Bwana Yesu Asifiwe Naombeni Ufafanuzi Je Maneno Haya Yana Maana Gani

1wakoritho15:18-19 “na Hapo Wao Nao Waliolala Katika Kristo Wamepotea , 19 “kama Katika Maisha Haya Tu Tumemtumaini Kristo, Sisi Tu Maskini Kuliko Watu Wote”


JIBU: Ni rahisi, kudhani mistari hiyo inathibitisha kuwa wale waliokufa katika Yesu Kristo wamepotea katika uwongo wa kiimani. Lakini mistari hiyo haimaanishi hivyo, ukianzia vifungu vya juu, na ukiendelea mpaka vile vya chini utalithibitisha hilo. Tusome..

1Wakorintho 15:12 “Basi, ikiwa Kristo anahubiriwa ya kwamba amefufuka katika wafu, mbona baadhi yenu husema kwamba hakuna kiyama ya wafu?

13 Lakini kama hakuna kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka;

14 tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure.

15 Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.

16 Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.

17 Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.

18 Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea.

19 Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.

20 Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.

Unaona, mistari hiyo inatuonyesha kuwa, wakati ule kulizuka kundi la Wakorintho ambao walianza kuamini kuwa hakuna kiyama ya wafu(yaani hakuna ufufuo wa wafu), Imani kama ile waliokuwa nayo masadukayo, kwamba mtu akifa amekufa, habari yake imeishia hapo. Isipokuwa tu tofauti yao na masadukayo ni kuwa masadukayo walikuwa hawamwamini Kristo, lakini hawa walikuwa wanamwamini, na tena walikuwa wanaamini kuwa alikufa akafufuka.

Sasa ndio hapo ukisoma mstari wa 13-18 utaona mtume Paulo anawauliza maswali, yanayokinzana na Imani yao, anawauliza kama hawamini kuwa kuna kiyama wa wafu, kwanini waamini kuwa Kristo alifufuka?. Na kama hakufufuka, basi Imani yao ni bure, hata hao waliolala katika Kristo wamepotea. Hawapaswi kuamini hata ufufuo wa Yesu.

Mpaka hapo utakuwa umeona kuwa, mstari huo wa 18 haumaanishi kuwa wale waliolala katika Kristo wamepotea.

Lakini mstari wa 19 anamalizia na kusema..

19 Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.

Neno maskini kama lilivyotumika hapo ni Zaidi ya kukosa fedha.. Yaani sisi tuliomwamini Kristo, kwasababu ya maamuzi yetu hayo ya kumwishia yeye, tutakuwa kama watu waliodharaulika, au watu waliotupwa chini kuliko watu wote ulimwenguni. Japo tu juu ya wote.

Swali ni je! Na wewe leo hii Unaogopa kuchekwa kwa ajili ya Yesu? Au kudharauliwa, au kutengwa, au kufukuzwa kazi kwa ajili yake? Mitume hawakujali hilo, kwanini wewe uogope?..Kumbuka kumwamini Yesu ni pamoja na kukubali shutma kwa ajili ya jina lake. Huko ndiko kujitwika msalaba wako alikokuzungumzia Bwana Yesu

Alisema.

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Lakini Zaidi ya yote alisema maneno haya kwa wale watakaoshinda….

Ufunuo 3:21 “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

VIKAANGUKA MACHONI PAKE VITU KAMA MAGAMBA.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

Rudi nyumbani

Print this post

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya huu mstari?

Wakorintho 3:17 “Basi ‘Bwana’ ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru”.


JIBU: Kauli hiyo kinyume chake ni kuwa, kama  Roho wa Bwana hayupo basi mahali hapo hapana uhuru wowote, kwa mujibu wa biblia.

Lakini ni uhuru wa aina gani Roho Mtakatifu analeta.

kibiblia Roho Mtakatifu alikuja kuleta Uhuru wa aina mbili.

  • Uhuru wa kutuondoa katika utumwa wa dhambi na mateso.

  • Uhuru wa kututoa katika utumwa wa sheria.

1). Tukianzana na uhuru wa kutuondoa katika utumwa wa dhambi;

Siku ile Bwana Yesu alipoanza huduma yake ya kuhubiri alisema maneno haya..

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Umeona hiyo ni kuonyesha kuwa Roho Mtakatifu aliposhuka juu ya watu wake na katika kanisa alikuwa na kazi ya kuwatoa watu katika vifungo vya dhambi na mateso ya  ibilisi, yaani waliokuwa wanasumbuliwa na mapepo, waliokuwa wanateswa na magonjwa, na hofu, na mauti, na shida  vyote hivyo vilikuja kuondolewa na Roho Mtakatifu mwenyewe,

na pia ukizidi kusoma tena katika Isaya 61:3-4 utaona unabii huo wa Roho Mtakatifu unaendelea kusema..

“…kuwafariji wote waliao; 3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe”.

Unaona anafanya pia kazi ya kuwatoa watu katika huzuni zao, kuwafariji,kuwapa mataji ya utukufu na sifa. huo ni Zaidi ya Uhuru, ambao hakuna mtu yeyote hapa duniani angeweza kuutoa.

2). Uhuru wa sheria;

Pia alikuja kutukomboa sisi tuliokuwa chini ya sharia, tutoke katika laana ya sheria..

Wagalatia 4:3 “Kadhalika na sisi, tulipokuwa watoto, tulikuwa tukitumikishwa na kawaida za kwanza za dunia.

4 Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria,

5 kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana.

6 Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.

7 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu”.

Roho Mtakatifu alikuja kututoa katika utumwa wa sheria, ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Yesu Kristo na sio kwa matendo yetu tena. Kwasababu hapo mwanzo tulijitahidi sana kumpendeza Mungu kwa kushika sheria, lakini sheria ilituzidi nguvu, kwasababu ya udhaifu wa miili yetu. Hivyo tangu enzi za agano la kale, hakuwahi kuonekana hata mmoja aliyeweza kumpendeza Mungu kwa matendo yake mwenyewe, haijalishi walijitahidi kiasi gani.

Hivyo ili Mungu kutuokoa,  alimtuma mwanawe Yesu Kristo duniani, ili yeye peke yake atende mema, pasipo kufanya dhambi yoyote, kisha Mungu amuhesabie haki yeye peke yake kwa matendo yake, na ndipo sasa sisi  tutakaomwamini Yesu baadaye tuhesabiwa haki kama vile yeye, kwa njia ya matendo yake na sio yetu..

Kwahiyo, ikiwa wewe umemwamini Yesu, na ukampokea Roho wake, basi ujue Mungu haangalii matendo yako, kama ndio kipimo cha yeye kukubali, bali anamwangalia mwana wake YESU KRISTO uliyemwamini, na hivyo unahesabiwa haki, kama vile hujawahi kumkosea Mungu, kwasababu VAZI la Yesu linakufunika mbele yako.

Huoni kama huo ni uhuru mkubwa sana? Unahesabiwa haki kwa kumwamini tu!  Lakini ikumbukwe kuwa hiyo haimaanishi kuwa tuendelee kutenda dhambi kisa tu hatuhesabiwi haki kwa matendo yetu, hapana, hata kwa namna ya kawaida, huwezi kwenda kupeleka mkono kwenye tundu la nyoka akung’ate kila saa, kisa tu dawa ya kutibu sumu ipo, hapana, vinginevyo utakuwa mwendawazimu, bali utachukua tahadhari kubwa sana, kwa kuzidi kukaa mbali na nyoka, kwasababu unajua sumu yake sikuzote ni kifo..

Na sisi vivyo hivyo maadamu tunahesabiwa haki kwa kumwamini Yesu Kristo ni jukumu letu sote, tukae mbali na dhambi, kwa kadiri tuwezavyo, katika utakatifu wote ili tupate kumzalia Mungu matunda. Na hiyo ndio ishara ya kuamini kwetu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa Roho Mtakatifu ametuletea uhuru mkubwa sana hapa duniani.  kiasi kwamba mtu yeyote atakayempokea, atakuwa HURU KWELI KWELI. Jambo ambalo watu wengi hawalifahamu, wakidhani kwa Mungu ni utumwa.

Swali ni je wewe umeshampokea ndani yako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Kumbuka Pasipo Roho Mtakatifu huwezi kwenda katika unyakuo, na haji ndani yako isipokuwa  kwanza umemwamini  Yesu Kristo, kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa na kuwa tayari kuyaacha mambo yako maovu uliyokuwa unayafanya huko nyuma. Na pili kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele, na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, Na hapo ndipo Mungu atakapokupa kipawa cha Roho Mtakatifu ndani yako bure.

Hivyo ikiwa utapenda kumkaribisha Yesu maishani mwako, basi tafuta mchungaji yoyote, au mtumishi yoyote aliyesimama katika Imani, akusaidie, au wasiliana nasi kwa namba hizi: +255693036618 / +255789001312

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Sitara ni nini katika biblia?

Sitara limetokana na neno “sitiri”, na kusitiri maana yake ni “kuficha kitu au jambo” hivyo kitu chochote kinachositiri kinaitwa “Sitara”. Nguo ni mfano wa Sitara, kwani inasitiri maungo yetu.. Kadhalika pazia linalowekwa mlangoni ni mfano wa Sitara, kwani linasitiri mambo yaliyopo ndani, au yanayoendelea ndani n.k

Kwamfano katika biblia tunaona, sehemu ile ambapo Sanduku la Agano lilikuwa linawekwa, paliwekwa pazia ambalo lilikuwa linatenganisha patakatifu, na patakatifu pa patakatifu, ili kulisitiri sanduku la agano lililokuwa ndani, sasa pazia lile lilikuwa linajulikana kama PAZIA LA SITARA.

Hesabu 4:5 “hapo watakapong’oa safari, Haruni ataingia ndani, na wanawe, nao watalishusha PAZIA LA SITARA, na kulifunika sanduku la ushahidi kwa hilo pazia;”

Pia unaweza kusoma juu ya pazia hilo katika Kutoka 35:12, Kutoka 39:34, Kutoka 40:21 na Kutoka 36:37.

Na katika wakati wetu huu, sitara yetu ni YESU KRISTO. Yeye pekee ndiye aliyechukua dhambi zetu, na kusitiri uovu wetu kupitia msalaba, maana yake pale tunapomwamini na kutubu, dhambi zetu zote zinasitirika mbele za Baba, na tunaonekana kama hatujawahi kutenda dhambi kabisa, yeye ndio kama vazi letu , kufahamu zaidi, ni kwa namna gani Yesu ni vazi letu (Sitara yetu) fungua hapa >> Mtakatifu ni nani?.

Pamoja na hayo, Yesu ni sitara yetu dhidi ya madhara yote yanayoletwa na yule adui yetu shetani, kama  vile shida, magonjwa na adha.

Zaburi 32:7 “Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso, Utanizungusha nyimbo za wokovu”.

Zaburi 119:114 “Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea”.

Hivyo ni Baraka kubwa kumfanya Bwana, sitara yetu…Lakini ni laana kubwa kumfanya shetani au wanadamu kuwa sitara yetu.

Yeremia 17:5 “Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana

6 Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

 7 Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.

  8 Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda”

Ukimkataa Bwana moyoni mwako, na kuikubali sayansi, hutaona mema yatakapotokea, utakuwa umelaaniwa biblia inasema hivyo.

Bwana atusaidie tuzidi kumfanya yeye SITARA YETU YA DAIMA. Ngome yetu, kimbilio letu, msaada wetu na jabali letu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

WAPE WATU WANGU RUHUSA ILI WAPATE KUNITUMIKIA.

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Rudi nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

Jina kuu la Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu ambalo ndio mwanga wa njia yetu na Taa iongozayo miguu yetu. (Zab.119:135).

Kitabu cha Filemoni ni waraka ulioandikwa na Mtume Paulo wakati akiwa gerezani, Kwa mtu mmoja anayejulikana kama Filemoni. (Ikumbukwe kuwa waraka ni kama barua tu), hivyo Mtume Paulo aliandika waraka huo/barua hiyo kwa Filemoni, na waraka huo kwa uongozo wa Roho, ukawekwa kwenye orodha ya vitabu vya biblia kwasababu una maonyo makubwa na mafunzo makubwa kwa wakristo. Na pia ni mojawapo ya vitabu vifupi katika agano jipya.

Sasa huyu Filemoni alikuwa ni nani?

Filemoni alikuwa ni mmoja wa watu waliompokea Yesu, kupitia injili iliyokuwa inahubiriwa na wakina Paulo katika mji wa Efeso, hivyo huyu Filemoni alikutana na injili hiyo na kumpokea Yesu, na kuanza kumtumikia kwa moyo wake wote, mpaka kufikia hatua ya kuwa askofu wa kanisa, ambalo lilikuwa linakusanyika nyumbani kwake mwenyewe (Filemon 1:2), huko Kolosai.Lakini pamoja na hayo, mtu huyu alikuwa ana uwezo na alikuwa anamiliki watumwa nyumbani kwake  (yaani wafanyakazi).

Na mmoja wa watumwa wake aliyekuwa anaitwa Onesimo, siku moja alitoroka kwake na kumwibia baadhi ya mali zake, na kukimbia nazo Rumi. Wakati akiwa njiani kuelekea Rumi, alikutana na Paulo akihubiri injili, na Maneno ya Mungu yakamgusa na kumfanya kutubu kwa dhati kabisa. Na alipotubu ndipo baadaye Paulo akajua alikuwa ni mtumwa wa Filemoni yule wa Efeso, mtenda kazi kazi katika shamba la Mungu. Na kwasababu Paulo amemhakiki Onesimo kuwa ni kweli katubu kwa dhati, na kageuka kuwa mkristo, na kaacha wizi na mambo yote mabaya, na zaidi ya yote alikuwa anataka kufuatana na Paulo katika injili kila anakokwenda na hata katika vifungo vyake.

Lakini Paulo hakuruhusu afuatane naye badala yake kwa kuongozwa na hekima ya Roho akaamua amsafirishe amrudishe kwanza kwa Bwana wake, lakini asimrudishe mikono mitupu bali ampeleke na waraka kutoka kwake, wa ushuhuda wake kwa Onesimo,  kwamba kijana wake si yule aliyemwacha, bali amebadilika na kuwa mtu mwingine, (kawa kiumbe kipya), na katika waraka huo pia kulikuwa na mambo machache ya kumshauri Filemoni juu ya Onesimo mtumwa wake….

Kwasababu kwa wakati huo, kulingana na sheria za kirumi, endapo mtumwa akimtoroka bwana wake, na akipatikana, sheria kwake ilikuwa ni kifo. Kwahiyo Paulo alilijua hilo na ndio maana akaazimu kumrudisha Onesimo kwa bwana wake pamoja na waraka.

Na katika waraka huo aligusia vipengele vikuu 3 vifuatavyo.

1. Kwanza aliomba ampokee kwasababu kashatubu na kubadilika..

Filemoni 1:9 “lakini, kwa ajili ya upendo nakusihi, kwa kuwa ni kama nilivyo, Paulo mzee, na sasa mfungwa wa Kristo Yesu pia.

10 Nakusihi kwa ajili ya mtoto wangu niliyemzaa katika vifungo vyangu, yaani, Onesimo;

11 ambaye zamani alikuwa hakufai, bali sasa akufaa sana, wewe na mimi pia;

12 niliyemtuma kwako, yeye mwenyewe, maana ni moyo wangu hasa”

2. Baada ya kumpokea asimfanye tena kama mtumwa, bali kama ndugu katika Kristo.

Filemoni 1:16 “ tokea sasa, si kama mtumwa, bali zaidi ya mtumwa, ndugu mpendwa; kwangu mimi sana, na kwako wewe zaidi sana, katika mwili na katika Bwana.”

3 Na pia kama alimdhulumu, basi Paulo atamrudishia na kulipa pale alipodhulumiwa,

Filemoni 1:17 “Basi kama ukiniona mimi kuwa mshirika nawe, mpokee huyu kama mimi mwenyewe.

18 Na kama amekudhulumu, au unamwia kitu, ukiandike hicho juu yangu.

19 Mimi Paulo nimeandika kwa mkono wangu mwenyewe, mimi nitalipa. Sikuambii kwamba nakuwia hata nafsi yako”

Filemoni 1:20 “Naam, ndugu yangu, nipate faida kwako katika Bwana; uniburudishe moyo wangu katika Kristo.

21 Kwa kuwa nakuamini kutii kwako ndiyo maana nimekuandikia, nikijua ya kuwa utafanya zaidi ya hayo nisemayo”.

Katika waraka huu, biblia inatufundisha jinsi ya kuishi na watumwa wetu, ambao kwasasa tunaweza kusema watu tuliowaajiri.  Na pia inatufundisha majukumu ya kila mtumishi wa Mungu (kwamba anapaswa awe mpatanishi).

Unaweza kuwa umeokoka na kumwamini Yesu, na nyumbani unaye mfanya kazi wa ndani, au mlinzi wa geti, au unafanya kazi katika ofisi na chini wako kuna watumishi umewaajiri,…kumbuka huyo mtumishi wako, au mfanyakazi wako anapookoka na kuwa na Imani kama yako, fahamu kuwa huyo kwako ni kama ndugu, hupaswi kumfanya kama mtumwa wako tena…Ndio anaweza kuendelea na kazi yake ya nyumbani, au ya kulinda lakini, mchukulie kama ni ndugu yako..maana yake, kazi anayoifanya iendane sana na mshahara wake, kiasi kwamba ajihisi kama vile analipwa bure, ukilinganisha na kazi anayoifanya…

Pia utu wake uendane sawa na kazi anayoifanya…Maana yake anapofanya kazi yako ajihisi kama na yeye ni sehemu ya ile kazi, kwa kupendwa, kusikilizwa, kupewa muda wa kupumzika,  na si ajihisi ni kama mnyama, au mtumwa Fulani anayetumikishwa ili mwisho wa siku tu alipwe mshahara, na pia wewe kama bwana wake unapaswa uwe mvumilivu na mtu wa kusamehe kama Filemoni.

Wakolosai 4:1 “Ninyi akina bwana, wapeni watumwa wenu yaliyo haki na ya adili, mkijua ya kuwa ninyi nanyi mna Bwana mbinguni”.

Na pia kama wewe ni mtumwa huna budi kuwa mnyenyekevu, na kuwa na busara na hekima. Kwasababu biblia inasema pia..

Wakolosai 3:22 “Ninyi watumwa, watiini hao ambao kwa mwili ni bwana zenu, katika mambo yote, si kwa utumwa wa macho, kama wajipendekezao kwa wanadamu, bali kwa unyofu wa moyo, mkimcha Bwana.”

Maana yake ni kwamba, ijapokuwa boss wako ni ndugu yako katika Kristo, hupaswi kumkosea heshima, wala kumdharau. Ukimvunjia heshima, au ukimdharau na kumfanya boss wako ahuzunike tayari umemkosea Mungu.

Pia katika kitabu hichi tunajifunza, majukumu yetu kama watumishi wa Mungu, kwamba tuwe wapatanishi, hapo tunamwona Mtume Paulo, baada ya kumbadilisha Onesimo kwa injili yake, hakumchukua na kuanza ziara za kutembea naye, ingawa Onesimo alikuwa tayari na alitamani sana awe anatembea na Paulo, lakini Paulo aliona si vyema kutembea naye katika utumishi, na ilihali bado ni mtumwa wa mtu mwingine, hivyo ni vizuri kwanza akarudi kwa bwana wake, na kupatana naye, na kama bwana wake kama atampa ruhusa basi ndipo arudi na kuzunguka na wakina Paulo katika kuhubiri. Lakini si hekima kumchukua na ilihali katoroka kwa bwana wake, isingeleta picha nzuri, Filemoni asikie kwamba yule mtu aliyemuibia na kutoroka yupo huko anatembea na Paulo katika kuhubiri.

Vivyo hivyo hata katika wakati huu, wapo watu wamewaibia maboss zao, na wametubu kwa dhati kabisa, lakini hawataki kwenda kupatana na waliowaibia…wanataka watubu tu kimoyo moyo, na zaidi ya yote wanapokelewa makanisani na hata katika huduma na kupewa nafasi ya kuhudumu. Pasipo kujua kuwa huko nje wameacha sifa gani.

Wapo wengine wamekutwa katika udunia, na wameisikia injili na kuamua kutubu, lakini hapo kabla walikuwa wameshawakimbia wake zao, au waume zao, au familia zao…sasa kabla ya kuwapokea watu kama hao katika utumishi, ni vizuri kwanza wakapatane na ndugu zao, na wake zao au waume zao…Huku sisi tuliowahubiria tukiwasaidia, kama Paulo alivyomsaidia Onesimo kurudi kwa bwana wake kwa waraka, ili watakapoingia katika utumishi wasilete picha mbaya kwa walio nje.

Hivyo kama mchungaji, au mtumishi yeyote wa Mungu, tunapaswa tuchunguze kwanza historia ya mtu, kabla ya kuanza naye kazi ya huduma, hata kama ametubu kwa dhati, hiyo pekee haitoshi, anapaswa atengeneze machache ya nyuma, ambayo ameyaharibu, ili isipatikane dosari yoyote katika injili atakayoihubiri, au watakaoihubiri wale waliomhubiria.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA DEMA NA MARKO?

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Jitunze mguu wako uendapo nyumbani kwa Mungu”?

SWALI: BWANA apewe sifa mtumishi wa Mungu! Nakusalimia katika jina la YESU KIRSTO. naomba unifafanulie Mhubili 5:1 Mtumishi maana huwa sipaelewi vizuri.. Inasema.

Mhubiri 5:1 “Jitunze mguu wako uendapo nyumbani kwa Mungu; Maana ni heri kukaribia ili usikie, Kuliko kutoa kafara ya wapumbavu; Ambao hawajui kuwa wafanya mabaya”.


JIBU: Amen, jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo litukuzwe daima.

Katika vifungu hivyo, biblia inatutahadharisha jinsi ambavyo tunapaswa tuwe pale tunapotaka kwenda nyumbani mwa Mungu (Kanisani) kumfanyia ibada/ huduma. Anasema ni heri ukaribie usikie, kuliko kutoa kafara za wapumbavu. Maana yake ni kuwa si kila jambo tunaweza kulifanya katika kanisa ilimradi tu,  kama tunavyoweza kufanya mahali pengine popote. Kumbuka huduma yoyote, au dua yoyote, unayoifanya au unayoipelekea kwa Mungu hiyo ni kafara.

Leo hii utaona, binti au kijana ni mzinzi, halafu bado akifika kanisani, anakuwa wa kwanza kwenda pale mbele kumwimbia Mungu kwaya, hizo ni kafara za wapumbavu. Au mtu hajaitwa na Mungu, haliishi hata Neno la Mungu lakini ni wa kwanza kwenda kufundisha kanisani kisa tu anajiona anakipaji fulani cha kuongea.Sasa hizo ni kafara za wapumbavu ambazo biblia inasema, kuwa wafanyao hayo hawajui kuwa wanatenda mabaya.. Wanafanya mambo ambayo yatawasababishia madhara wao wenyewe.

Vilevile, kuwa na maneno mengi mbele za Bwana, ambayo hayana maana, hizo nazo ni kafara za wapumbavu, kwamfano utamwona mwingine, akifika tu magotini, ni kumnung’unikia Mungu, na kulalamika mbele zake mwanzo mwisho, kama vile wana wa Israeli walivyokuwa wanafanya kule jangwani ambao mwisho wao tunajua  ulikuwa ni kuangamizwa tu badala ya kuponywa.. Hizo nazo ni kafara za wapumbavu na ndio maana mistari inayofuata inasema..

Mhubiri 5:1 “Jitunze mguu wako uendapo nyumbani kwa Mungu; Maana ni heri kukaribia ili usikie, Kuliko kutoa kafara ya wapumbavu; Ambao hawajui kuwa wafanya mabaya.

2 Usiseme maneno ya ujinga kwa kinywa chako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu yuko mbinguni, na wewe upo chini, Kwa hiyo maneno yako na yawe machache”.

Unaona? Maneno yako yawe machache..Ni heri utumie muda mwingi kushukuru, na kuomba kuliko kutoa manung’uniko, au kulaani.

Pia, kafara za wapumbavu ni pamoja na kumwekea Mungu nadhiri, bila kutafakari kwanza, kwamfano utakuta mwingine anaahidi, atamfanyia Mungu kitu fulani kwenye kanisa, halafu hatimizi alichokiahidi, angali zipo katika uwezo wa mikono yao, kama walivyofanya Anania na Safira, ambao mwisho wa siku walikufa , Ukiendelea kusoma mstari wa 4 pale unasema..

Mhubiri 5:4 “Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hawi radhi na wapumbavu; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.

5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe”.

Pia kutoa sadaka, ambayo imetoka katika shughuli haramu, kama za ukahaba au madawa ya kulevya, usizipeleke nyumbani kwa Bwana..

Kumbukumbu 23: 18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Unaona?.. Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kama bado hujafahamu ni nini ambacho Mungu anakihitaji kwanza kwako, pale unapofika nyumbani mwake, ni heri usifanye chochote kabisa, ukae usikilize tu, ufundishwe mapenzi ya Mungu kwanza, na ndipo baadaye uanze kumfanyia Mungu huduma kanisani. Kuliko kukurupuka kufanyia Mungu chochote kabla hajafahamu mapenzi yake ni nini kwako.

Tunapaswa tujue Mungu, anahitaji kwanza UTAKATIFU wa maisha yetu, ndipo hayo mengine tutakapoyatoa yawe na Baraka zaidi, hatumdanganyishii Mungu kwa kutumika kwetu wakati maisha yetu yapo mbali na wokovu. Alisema mwenyewe..

1Samweli 15:22 “…Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu”.

Hivyo tujitahidi tujue kwanza mapenzi ya Mungu nini.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kwanini Yesu alisema “Na wakisikia wasikie, wasielewe Wasije wakaongoka?”

SWALI: Katika Marko 4:12, Bwana Yesu anasema.. “  ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije wakaongoka, na kusamehewa”. Swali ni kwamba, kwanini Yesu alisema hivyo kuwa acha wasisikie na kuelewa ili wasije wakaongoka na kusamehewa…na wakati kusudi lake si anataka watu watubu ili wapate kusamehewa dhambi?.


Jibu: Ukianza kusoma kuanzia juu kidogo utaona, Bwana Yesu alikuwa ameutoa ule mfano wa mpanzi mbele ya mkutano mkubwa, na baada ya kuutoa, hakutoa tafsiri yake, kwamba zile mbegu zilimaanisha nini, na lile konde maana yake nini.. Badala yake aliacha tu kama fumbo… Sasa kundi kubwa la watu waliokuwa wanamfuata Yesu, wengi wao walikuwa wanafuata miujiza tu, na si kingine… Lakini ni kundi dogo sana lililokuwa linafuata kwenda kusikia ni nini Yesu anazungumza…Kwa kuelewa zaidi pitia hapa>> Kwa wale walio nje, yote hufanywa kwa mifano.

Kwahiyo hili kundi dogo ambalo lilikuwa linafuatilia kwa makini maneno ya Yesu, ndio lililokuwa linamfuata baadaye Yesu akiwa peke yake na kumuuliza maana ya ile mifano yote aliyokuwa anaitoa. Na ndipo Yesu anawafafanulia mifano ile.

Lakini wengine wengi waliosalia, ambao hawakuwa na haja ya maneno ya uzima ya Yesu, badala yake walikuwa wanafuata miujiza tu, hawakuwa na muda wa kutaka kujua tafsiri ya ile mifano. Kwahiyo ile mifano ilipokuwa inatolewa na Yesu kwao iliishia kuwa kama hadithi tu, na wengine walikuwa wanaishia kuitafsiri wanavyojua wao. Lakini wale wengine wenye hekima walikuwa wanamfuata Yesu baadaye akiwa peke yake na kumuuliza maana ya ile mifano..

Marko 4:8  “Nyingine zikaanguka penye udongo ulio mzuri, zikazaa matunda, zikimea na kukua, na kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.

9  Akasema, Aliye na masikio ya kusikilia, na asikie.

10  NAYE ALIPOKUWA PEKE YAKE, wale watu waliomzunguka, na wale Thenashara, walimwuliza habari za ile mifano.

11  Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, bali kwa wale walio nje yote hufanywa kwa mifano,

12  ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije wakaongoka, na kusamehewa”.

Sasa kwanini iwe hivyo?..kwanini Yesu asitoe mfano na tafsiri yake palepale??

Ni kwasababu siku zote Mungu hamlazimishi mtu kumfuata, wala hamlazimishi mtu kusikia maneno ya uzima. Bali Yule ambaye amefungua moyo wake kutafuta kumjua ndiye anayemfunulia zaidi.

Luka 19:26 “Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho”

Kwahiyo lile kundi ambalo halikutaka kutafuta kujua maana ya ile mifano, hiyo ndio kundi lililozibwa macho lisione (maana yake lilinyang’anywa hata kile kidogo lilichokipokea), kwamba lisikie tu mifano lakini lisielewe, kwasababu limekataa kutafuta ukweli.. Kwasababu wametangulia kuyafumba macho yao, na hivyo Mungu akaongeza upofu juu yao….Utaona biblia inalifafanu hilo vizuri katika..

Matendo 28:25 “Na walipokuwa hawapatani wao kwa wao, wakaenda zao, Paulo alipokwisha kusema neno hili moja, ya kwamba, Roho Mtakatifu alinena vema na baba zetu, kwa kinywa cha nabii Isaya,

26  akisema, Enenda kwa watu hawa, ukawaambie, Kusikia, mtasikia wala hamtafahamu; Na kuona, mtaona wala hamtatambua;

27  Kwa maana mioyo ya watu hawa imepumbaa, Na masikio yao ni mazito ya kusikia, Na macho yao WAMEYAFUMBA; Wasije wakaona kwa macho yao, Na kusikia kwa masikio yao, Na kufahamu kwa mioyo yao, Na kubadili nia zao, nikawaponya”

Mstari wa 27, hapo unasema… “na macho yao WAMEYAFUMBA”.. Maana yake hayajafumbwa na mtu, bali wameyafumba wao wenyewe, ili wasisikie… wakati Bwana Yesu anatoa ile mifano, hawakutaka kwenda kutafuta kuuliza maana yake. Hiyo waliyafumba macho yao… Na hiyo sasa Mungu akaitia uzito mioyo yao ili waendelee kukaa katika hali hiyo hiyo…kama neno lake linavyosema katika…

 2Wathesalonike 2:10 “…..na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

11  Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;

12  ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”.

Kwahiyo kinachotangulia kwanza ni Watu kuikataa kweli ndani ya mioyo yao, ndipo ile nguvu ya upotevu inaachiwa juu yao..

Hiyo ni tahadhari tu hata kwetu.

Kinyume na inavyodhaniwa na wengi kuwa neema ni kitu cha kuchezea, na kwamba unaweza kuchagua muda wowote wa kumgeukia Mungu, pasipo kujua kuwa kumgeukia Mungu ni neema, na kwamba saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubalika ni sasa, endapo mtu ataisikia injili ikihubiriwa kwake na kuipuuzia pasipo kuzidi kutafuta ukweli, ile neema inaondolewa juu yake na nguvu ya upotevu inakuja juu yake.

Hizi ni siku za mwisho tunazoishi, na muda umekimbia sana, Kristo yupo mlangoni..na atakuja kama mwivi, kulinyakua kanisa lake, je utakuwa wapi siku hiyo? Wewe ambaye hulitilii maanani neno lake leo?..wewe ambaye ukiambiwa mavazi unayovaa ni mavazi yasiyompendeza Mungu, unadhihaki, wewe ambaye unaipuuzia sauti inayokuonya utubu ndani ya moyo wako?..

Bwana anarudi.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

BWANA AYAGANGE NA MACHO YETU PIA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi nyumbani

Print this post

VAZI KUU AMBALO MUNGU AMETUANDALIA KILA MMOJA WETU.

Ukisoma kitabu cha Mwanzo, utaona mara baada ya Adamu na Hawa kuasi, kwa kula yale matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya,ambayo Mungu aliwakataza wasiyale, utaona pale kwa tendo lile hawakuona kwanza dhambi ndani yao, bali waliliona tatizo kwenye miili yao. Hawakujiona wamemkosea Mungu, bali walijiona wapo uchi, na ndio maana muda ule ule wakaanza harakati zao za kutafuta namna ya kwenda kujisitiri na sio kwenda kutubu,

Wakaenda  kujishonea matawi ya mtini, ili wajirudishe katika hali yao ya mwanzo, wajaribu kuisitiri ile aibu iliyowaingia, sasa unaweza kudhani walikuwa ni wajinga, hapana hawakuwa wajinga, walijua kabisa, nyenzo iliyowafanya wao waweze kumkaribia Mungu na kuzungumza naye ilikuwa ipo katika miili yao. Ndio maana wakakimbilia kwanza kwenda kushona majani,wajisiriti na sio kutubu dhambi zao.

Lakini tunaona hata baada ya kufanya vile, bado haikusaidia waliendelea kujiona wapo uchi, kuonyesha kuwa aibu ile ilipenya mpaka ndani kabisa ya mioyo yao. waligundua hata wakijisitiri kwa nguo za namna gani, bado miili yao imeshaingiwa na aibu kubwa isiyoneneka.

Mwanzo 3:7 “Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo.

8 Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu asiwaone.

9 Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi?

10 Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha”.

Ni kama tu wakati wa Samsoni, yeye alijua kabisa asili ya nguvu zake ipo katika nywele zake, lakini siku alipokatwa nywele na Delila, muda ule ule alikuwa dhaifu hata wafilisti walipokuja hakuweza tena kushindana nao,. Ndivyo ilivyokuwa kwa Adamu na Hawa, ujasiri wao wa kuongea na Mungu ulikuwa upo katika miili yao. Lakini walipoasi maagizo ya Mungu, waliona kasoro kubwa sana, ambayo hata majani na ngozi ambazo Mungu alikuja kuwafanyia baadaye ziwasiriti bado hazikufanikiwa kuiondoa ile aibu ya miili yao.

Sasa, aibu hii ya miili ipo hadi sasa, na ndio maana kwa miili yetu hii hatuwezi kumwona Mungu, au kuzungumza na Mungu. Haiwezekani, tatizo sio Mungu, tatizo ni aibu iliyo kwenye miili yetu, haiwezi kustahili utakatifu wa Mungu, sikuzote tutaukimbia tu.

Na ndio maana baada ya Mungu kulijua hilo, akamtuma mwanawe Yesu Kristo duniani, ili afe, kisha afufuke, kisha aende mbinguni kutuandalia VAZI  lake mwenyewe ambalo Kila mmoja wetu atakapolivaa hilo, basi aibu hiyo ya mwili ife, na kuanzia hapo amwone Mungu, na azungumze naye Uso kwa Uso kwa ujasiri wote, katika utakatifu hata Zaidi ya kile alichokuwa anakifanya Adamu kwa Mungu pale Edeni.

Na vazi hilo ni MIILI MIPYA itakayoshuka kutoka mbinguni. Hapo ndipo utajua ni kwanini siku tukienda katika unyakuo, hatutaacha miili yetu hapa chini ardhini, bali tutafufuliwa nayo kwanza, kisha tutavikwa hii miili mipya kama vile VAZI,. Na saa hiyo hiyo  aibu ya mwili itaondoka..hatutajiona tena tupo uchi, tutapata ujasiri mkubwa sana wa kumwona Mungu wetu, na kuzungumza naye, na kumfurahia milele. Biblia inasema..

2Wakorintho 5:1 “Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni.

2 Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni;

3 IKIWA TUKIISHA KUVIKWAHATU TAONEKANA TU UCHI.

4 Kwa sababu sisi tulio katika maskani hii twaugua, tukilemewa; si kwamba twataka kuvuliwa, bali kuvikwa, ili kitu kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima”.

Unaona? Biblia inasema. Tukishavikwa hiyo miili mipya hatutaonekana tena tu Uchi.

Tutamani sana tuifikie hiyo siku, kwasababu itakuwa ni siku ya furaha isiyokuwa na kifani, miili yetu itafanana na ya malaika, haitakuwa na kuumwa, au kufa, au kusinzia, au kuchoka, au kushikwa na udhaifu wowote. Kwasababu itakuwa ni miili ya kimbinguni, vazi la utukufu.

Swali sasa lipo kwako, je wakati huo ukifika utakuwa wapi? Ikiwa leo usiku parapanda italia utakuwa wapi ndugu yangu, kwasababu dalili zote za mwisho wa dunia Bwana Yesu alizozizungumza katika maandiko zimeshatia karibia zote, tunachongoja sasahivi ni UNYAKUO muda wowote. Embu jiulize utakuwa katika majuto makubwa kiasi gani utakaposikia wenzako baadhi wameondoka, wapo mbinguni wakimfurahia Mungu, halafu  wewe umebaki hapa duniani, ukijiandaa na dhiki kuu ya mpinga-Kristo na mapigo ya Mungu.

Ndugu yangu, usisubiri, mhubiri Fulani siku moja aje kukubembeleza umgeukie Muumba wako, hizi ni nyakati za wewe mwenyewe kutafakari ulipotoka, ulipo na unapoelekea, na kufanya uamuzi sahihi, kwa hali inavyoendelea sasa hivi duniani, hakuna anayejua kama kesho atakuwa hai. Hivyo tukilijua hilo ni wakati wetu wa kumkaribisha Kristo mioyoni mwetu kwa kumaanisha kabisa.Ili atupe wokovu na uzima wa milele.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kutahayari ni nini katika biblia?(2Timotheo 2:15)

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

SWALI: Samahani mtumishi kuna andiko linatoka kitabu cha Mhubiri 7:29 sijalielewa vizuri linamaanisha nini

Mhubiri 7:29  “Tazama, hili tu nimeliona; Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu, lakini wamebuni mavumbuzi mengi”.


JIBU: Mungu alipomuumba mwanadamu alimuumba katika ukamilifu wote, Adamu na Hawa walikuwa ni watu ambao hawakuwa na kasoro yoyote, si ya kimwili, si ya kiroho. Waliumbwa katika ukamilifu wa furaha,amani, upendo, maarifa  na kumcha Mungu.

Lakini ilifika wakati, hawakuridhika, na vile ambavyo Mungu alivyowaumba na kuwaweka, wakataka kuwa sawa na Mungu, wakabuni namna yao wenyewe ya kuishi, ya kutaka uhuru wao wenyewe. Na ndio hapo utaona wakashawishika kwenda kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, ambayo Mungu aliwaambia wasile, Ili wakipate wanachokitafuta. Lakini matokeo yake ni kuwa mpaka sasa mwanadamu hajakipata alichokitafuta tangu wakati ule, kinyume chake ndio matatizo yalizidi kuongezeka japokuwa anajibunia kila siku njia zake mwenyewe za kuishi.

Mpaka sasa mambo hayo yanaendelea, tunavyoona watu wakijibadilisha maumbile yao, kisa tu hayawavutii machoni pao. Na ndio hapo utaona, wanawake wanachubua ngozi zao, ili waonekane weupe, wengine wanapaka make-up ili waonekane wa kitofauti na wenye mvuto zaidi, wanaweka kucha za bandia, wanavaa wigi za wazungu.. Yote hayo ni mavumbuzi mengi watu wanaojibunia..na kibaya zaidi leo hii wameshafikia mpaka hatua ya kubadilisha maumbile yao kwa kufanyiwa upasuaji na kunyeshwa madawa makali.

Hawataki tena kuwa wao wa asili kama Mungu alivyowaumba ,wanataka wawe kama wanavyotaka wao. Sasa badala mavumbuzi yao yawasaidie, kinyume chake ndio yanawaletea madhara kama sio kuwapoteza kabisa.

Hivyo, tunapaswa tujue kuwa si mpango wa Mungu tujigeuze mionekano yetu, kwasababu Mungu alituumba kwa mfano wake na sura yake, alishatuumbia ukamilifu ndani yetu,.Jukumu letu sisi ni kumcha yeye, na kuisiliza sauti yake basi.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?

Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Ufunuo 12 inaelezea vita vya wakati upi?

Swali: Yale maelezo ya Ufunuo 12:7-12, yanaeleza vita vya wakati upi?, ile ya kwanza kabisa kabla ya sisi kuumbwa au kuna nyingine iliyotokea tena?


Zipo vita mbili kuu zinazowahusu shetani na Malaika watakatifu.

Vita ya kwanza: Ni ile iliyopiganwa mbinguni, zamani sana kabla ya wanadamu kuumbwa,  pale ambapo ibilisi (yaani shetani), alipoasi kwa kutamani kuwa kama Mungu, na hivyo akashindwa vita ile na kutupwa chini, na baada ya kushindwa vita hiyo akawa hana uwezo tena wala mamlaka ya kurudi katika nafasi yake mbinguni. (akaondolewa mbinguni). Lakini hiyo haikumfanya asifike kwenye enzi ya haki ya Mungu iliyopo mbinguni.

Hata katika maisha ya kawaida, mtu anapoasi katika ngazi Fulani kuu ya serikalini mfano Uwaziri, na hata kufikia kufukuzwa, na kuipoteza ile nafasi, hiyo haimfanyi asiwasilishe mashtaka yake mahakamani. Maana yake kama ana haki zake za msingi, anazozidai kule alipoondolewa, au anajambo la kupashitaki kule alipotoka, mahakama ya haki lazima imsikilize na kumpa haki yake kama anastahili. Kwasababu Mahakama ni moja ya muhimili wa serikali ambayo, haina upandeo fulani wa kuegemea wala kupendelea, ina uwezo hata wa kuishtaki serikali nzima ilimradi tu impatie mtu  mmoja haki yake, na mtu yeyote anauwezo wa kwenda mahamani kushitaki.

Na pia enzi ya Mungu (yaani mbinguni) pamegawanyika katika sehemu kuu mbili, ipo sehemu ambapo Malaika wapo, ambapo ndio kule shetani alipokuwepo kabla ya kuasi, na pia kuna mahali pa kiti cha Hukumu ya Mungu.

Sasa shetani aliondolewa katika nafasi yake huko mahali malaika walipo, huko hawezi kufika tena wala kurudi, lakini mahali pa hukumu ya Mungu, mbinguni bado ana uwezo wa kufika, na kupeleka hoja zake, na mashtaka yake. Na Mungu siku zote ni wa haki, huwa hana upendeleo, anayestahili kumpatia haki yake anampatia na asiyestahili  hampatii.

Sasa  vita ya kwanza ilimwondoa shetani katika nafasi yake ya ukuu kule mbinguni, lakini haikuishia hapo, ipo vita nyingine ya pili ambayo ilianza kuendelea tangu alipoondolewa mbinguni mpaka sasa, na hiyo si nyingine zaidi ya vita katika enzi ya hukumu ya Mungu, huko shetani anafika kila siku, kupeleka hoja zake na mashtaka yake dhidi yetu. Na siku zote inajulikana vita vya mtu aliyeshindwa huwa ni vikali mno na vinaumiza kichwa, kwasababu kila siku utasikia yupo mahakamani kushitaki hiki au kile, mara kakata rufaa n.k. Kwahiyo hata baada ya shetani kushindwa mbinguni, bado anaendeleza vita katika enzi ya hukumu ya Mungu, iliyopo mbinguni.

Ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kumpokea Yesu, na kuishi maisha ya ukamilifu na uangalifu, kwasababu adui  yetu shetani yupo kila siku kuchukua habari zetu na kuzifikisha mbele za Mungu, na kutushitaki.

Lakini tunapookoka na kuishi maisha ya uangalifu katika hii dunia, shetani anakosa hoja za kupeleka mbele za Mungu, na badala yake, malaika watakatifu wanapeleka mambo mazuri tunayoyafanya mbele za Mungu, ili tupewe thawabu. Kwasababu kama vile wanavyotumwa na Mungu kutulinda, vile vile wanachukua mambo yetu mazuri tunayoyafanya na kuyapeleka mbele za haki ya Mungu..

Mathayo 18: 10  “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”.

Na kamwe malaika watakatifu hawapeleki mashitaka yetu mabaya mbele za Mungu wetu..ni shetani peke yake ndio anafanya hivyo…

2Petro 2: 11 “Wenye ushupavu, wenye kujikinai, hawatetemeki wakiyatukana matukufu; ijapokuwa malaika ambao ni wakuu zaidi kwa uwezo na nguvu, hawaleti mashitaka mabaya juu yao mbele za Bwana

Kwahiyo kwasasa  kinachoendelea mbinguni, mahali pa haki ya Mungu, wanasimama malaika watakatifu kututetea na wakati huo huo anapita shetani kila mara kutushitaki.. Hiyo ndio vita inayoendelea sasa katika roho, (mapambano kati ya Mikaeli na malaika zake wakishindana na Yule joka na malaika zake), kuhusu mambo yetu sisi tuliomwamini Yesu, Malaika wanatutetea, shetani anatushitaki..(Kwa urefu juu ya hoja hizo fungua hapa >> Huduma ya Malaika watakatifu)

Na vita hivyo  vitahitimishwa na unyakuo,  wakati watakatifu watakapoondolewa duniani, shetani hatakuwa tena na mtu wa kumshitaki, wala hoja ya kwenda kupeleka mbele za Mungu, kuwashitaki wateule, kwasababu watakuwa wameshashinda na wapo mbinguni wakati huo, na hivyo atatolewa moja kwa moja katika hiyo enzi ya haki ya Mungu, na baada ya kuondolewa na kutupwa chini atakasirika kwasababu hatafika tena kumshtaki mtu yeyote wa Mungu, hivyo atashuka kwa hasira na kuanza kufikiri jambo lingine la kufanya..

Na jambo la kwanza litakalomjia ni kutafuta kufanya vita na vita na Taifa la Israeli, pamoja na wale wakristo vuguvugu walioachwa kwenye unyakuo, ambao watakataa kuipokea chapa yake. Hivyo atashuka chini  na kumwingia Yule mwana wa kuasi (Mpinga-Kristo) na kuonyesha rangi zake zote kwa ulimwengu mzima,  atawatesa watu kwa miaka mitatu na nusu (Miezi 42). Huo ndio ule wakati wa dhiki kuu.

kama tunavyosoma katika Ufunuo 12..

Ufunuo 12:7  “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

8  nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

9  Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

10  NIKASIKIA SAUTI KUU MBINGUNI, IKISEMA, SASA KUMEKUWA WOKOVU, NA NGUVU, NA UFALME WA MUNGU WETU, NA MAMLAKA YA KRISTO WAKE; KWA MAANA AMETUPWA CHINI MSHITAKI WA NDUGU ZETU, YEYE AWASHITAKIYE MBELE ZA MUNGU WETU, MCHANA NA USIKU.

11  Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

12  Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”

Hapo katika mstari wa 10, utaona Malaika mmoja anatangaza kwamba…“Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku”..Maana yake Yule anayewashitaki watakatifu hawezi tena kupanda kwenda kuwashitaki…kashashindwa, kwasababu wateule wameshamshinda kwa damu ya mwanakondoo, na wameenda kwenye unyakuo mbinguni..huko hawezi kuwashitaki tena awatoe huko..

Lakini “ole wa nchi na bahari”..maana yake ole wa waliobakia ambao hawakwenda mbinguni. Ibilisi anashuka kwao mwenye ghadhabu nyingi, na pia ole kwa Taifa la Israeli, ambalo ndio “Yule mwanamke mwenye mimba (Ufu.12:1)”.

Hivyo hiyo biblia inatutahadharisha, juu ya mambo yanayokuja. Ndugu sasa hivi  unafahamika kama ni mkristo lakini unazini kwa siri, unaiba, unaua, unacheza kamari, unavaa vibaya, unatukana, n.k..kumbuka shetani anayefikisha hayo kila siku mbele za haki ya Mungu, na kukushitaki. Na lengo lake ni ufe katika hizo dhambi ili uwe wake milele, au kama unyakuo utapita leo wewe ubaki, uingie katika dhiki kuu.

Dhiki kuu sio sehemu ya kutamani kuwepo, kama umeshindwa leo  kumkiri Yesu wakati neema ya Mungu bado  ipo, hutaweza siku ile katika dhiki kuu. Kama umeshindwa kuvumilia njaa ya siku moja katika kufunga ili uutafute uso wa Mungu hutaweza kuvumilia njaa ya miaka mitatu na nusu ya dhiki kuu. Kama leo hii kipindi cha amani unashindwa kujikana nafsi na kuchukua msalaba wako umfuate Yesu, kamwe hutaweza kufanya hivyo wakati wa dhiki kuu.

Hapo Yule malaika anasema… “Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; AMBAO HAWAKUPENDA MAISHA YAO HATA KUFA”.

Je leo hii unayapenda maisha yako kiasi kwamba, wokovu kwako ni jambo lililopitwa na wakati?, fashion za dunia,umaarufu, kusifiwa, kutukuzwa, kupendwa na kila mtu ndio mambo ya heshima kwako?…Hapo biblia inasema “ambao hawakupenda maisha yao hata kufa!!!”, ndio waliomshinda shetani!!.

Bwana Yesu pia alisema.. Yohana 12:25  “Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele”.

Kama bado hujampokea Kristo maishani, ni vizuri ukampokea leo, kwa kumwamini kwamba alikuja duniani akafa kwaajili ya dhambi zako, na akafufuka na kupaa mbinguni, na pia atarudi tena. Na kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kutozifanya tena, Na pia kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38, 8:16), naye atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu, atakayekuongoza na kukutia katika kweli yote ya kuyaelewa maandiko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

The King’s Highway — A Journey to God through Christ

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

Rudi nyumbani

Print this post