USIISHI KWA NDOTO!

USIISHI KWA NDOTO!

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko. Leo tutajifunza mbinu nyingine ambayo adui shetani anaitumia kuwapunguzia watu kasi ya kumtafuta Mungu.

Ni wazi kuwa kila mtu ana kiu ya kusikia sauti ya Mungu katika maisha yake, na ana kiu ya kujua ni nini kinamzunguka, ni hatari gani iliyopo sasa na iliyopo mbele yake. Na kutokana na wengi kukosa kufahamu ni namna gani wanaweza kuisikia sauti ya Mungu, wameishia kujikita kuishi kwa ndoto wanazoota, wakiamini  kuwa kila ndoto wanayoota ni Mungu anazungumza nao.

Leo nataka nikuambie ndugu, ambaye pengine una kiu ya kutafuta kuisikia sauti ya Mungu katika maisha yako, nataka nikuambie sauti ya Mungu haipo katika ndoto unazoota kila siku, njia pekee ya kuisikia sauti ya Mungu si ndoto unazoota bali ni NENO LA MUNGU linalokaa ndani yako. Sauti ya Mungu ni Neno lake katika biblia na si ndoto!.

Si kila ndoto ni sauti ya Mungu kwako. Nyingi zinakuja kutokana na shughuli zako za kila siku na mambo yaliyoujaza moyo wako.

Kwa mfano kama maisha yako yamejaa kutazama filamu za kidunia, na kusikiliza miziki, basi ndoto zako zitajaa hayo mambo, kama moyo wako umeujaza kutukana na maisha ya anasa, na ndoto zako pia zitakuwa hivyo hivyo, kama maisha yako yamejaa kufanya shughuli nyingi kutwa kuchwa, basi na ndoto zako zitakuwa zinahusiana na hizo hizo shughuli unazozifanya..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;….”.

Sasa inapotokea mtu anaacha kulisoma Neno, na kuishi kwa ndoto zake, na kwamba kila anachoota anatafsiri kwamba ni ujumbe kutoka kwa Mungu, mtu wa namna hiyo ni rahisi sana kupotezwa na uongo wa shetani. Kwasababu ameacha kujua njia sahihi ya kuisikia sauti ya Mungu, na amekijita kwenye ndoto anazoota kila siku.

Sauti ya Mungu, ni Neno lake ndani ya biblia takatifu. Ukitaka kujua Mungu anataka kuzungumza nawe nini kwa wakati huu, au kwa wakati ujao, nenda kasome biblia, na utaisikia sauti ya Mungu kwa wakati huo..inakuambia nini, (Ni kweli Mungu anaweza kuzungumza na mtu kwa ndoto, lakini hiyo ni mara chache sana..ukilinganisha na jinsi anavyoweza kuzungumza na sisi kwa kupitia Neno lake).

Yusufu japokuwa alikuwa na kipawa hicho cha Mungu kuzungumza naye kwa ndoto, lakini biblia inarekodi mara tatu tu, katika maisha yake yote. Lakini leo utaona mtu kila ndoto anayoota kwake ni ujumbe kutoka kwa Mungu!!. Na huku kaisahau kabisa biblia, hafahamu chochote kuhusu maneno ya Mungu.

Ndugu, Kama unaishi kwa ndoto, (Na kwamba kila asubuhi unapoamka wewe ni kutafuta tafsiri ya ndoto yako kwa watumishi), fahamu kuwa upo mbali sana na sauti ya Mungu, na ndoto unazoota umepofushwa macho ukidhani kuwa Mungu anazungumza na wewe kila siku huko kwenye ndoto zako. Mifano wa sauti ya Mungu kwako na kwangu ni hii >>

Mathayo 5:21 “Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu.

22 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto”.

Mathayo 5:38 “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;

Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili”.

Na..

Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki”.

Hiyo ndio mifano ya sauti na maonyo ya Mungu kwetu, ambayo ipo moja kwa moja isiyo na mafumbo yoyote. Lakini tukizutumainia ndoto tunazoota kila siku, na kufikiri huo ndio mlango wa kwanza wa Mungu kuzungumza na sisi, tutakuwa tumepotea njia pakubwa sana.

Hivyo tusiishi kwa ndoto, bali kwa Neno la Mungu!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

Akawaambia Enendeni ulimwenguni mwote,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE.(Marko16:15.) Yesu Anamaanisha nini kusema MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE?

Rudi nyumbani

Print this post

SHETANI ANAPOKUINGIA, ANATIA MOYO MGENI NDANI YAKO.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya uzima, ambayo ndio chakula cha kweli kitupacho afya roho zetu.

Lipo jambo moja nataka tujifunze leo linalohusiana na utendaji kazi wa shetani pale anapopata nafasi ya kumwingia mtu. Katika biblia tunaona Yuda ndiye mtu wa kwanza aliyerekodiwa kwa uwazi kabisa kuingiliwa na shetani. Tunalisoma hilo katika

Luka 22:3 “Shetani akamwingia Yuda, aitwaye Iskariote, naye ni mmoja wa wale Thenashara.

4 Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao”.

Na matokeo ya yeye kuingiliwa kule na shetani ilipelekea kutiwa moyo mwingine na ibilisi ambao yeye mwenyewe hakuwa nao kabisa.. Na moyo wenyewe ulikuwa ni moyo wa kusaliti.

Yohana 13:1 “Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo.

2 Hata wakati wa chakula cha jioni; naye Ibilisi amekwisha kumtia Yuda, mwana wa Simoni Iskariote, moyo wa kumsaliti;”

Sasa moyo kama huu ukishaingia ndani yako, huwa haujali kitu kingine chochote, huwa haufikirii kwamba huyu ni ndugu yangu, au huyu ni mama yangu, au huyu ni jirani yangu, au huyu ni mwenye haki, au nani n.k. wenyewe kazi yake ni kuvuruga, kuharibu, kusaliti, kuchinja kama sio kuua kabisa. Kwasababu si moyo wa mwanadamu tena unaofanya kazi ndani ya mtu bali ni moyo wa ibilisi mwenyewe ule wa kuasi.

Ndicho kilichomtokea Yuda, alipoingiwa na moyo huo, hakujali kuwa Yesu alimpenda Upeo kama tulivyosoma hapo juu, mpaka akamfanya kuwa msiri wake, na kumpa tonge lake alilolipenda yeye peke yake.. Lakini kinyume chake ni kuwa alimwinulia kisigino chake, akaenda kumsaliti kwa maadui zake, tena mbele ya macho yake kwa kumbusu. Usifikiri ule ulikuwa ni moyo wa Yuda.. Haukuwa moyo wake hata kidogo,  na ndio maana baadaye shetani alipomwacha, alijuta sana na mwisho wa siku akaenda kujinyonga.

Zaburi 41:9 “Msiri wangu tena niliyemtumaini, Aliyekula chakula changu, Ameniinulia kisigino chake”

Moyo huu huu ndio utakaomwingia mpinga-Kristo siku ile ya mwisho, ambaye kazi yake itakuwa ni kuchinja tu wale wote ambao hawana ile chapa ya mnyama. Na baadaye itamtoka na kuyaendea mataifa ili kuleta vita duniani.

Ufunuo 16:13 “Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.

14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.

Leo hii unaona watu wanafanya mauaji makubwa ya kinyama, na kuchinja watu, au kuwatoa ndugu zao kafara usidhani ni mioyo yao inafanya hivyo. Hao ni watu ambao tayari walishamfungulia milango shetani tangu zamani ya kuwaingia, na matokeo yake shetani naye akawawekea mioyo mingine ndani yao, ambayo haijali utu tena, au haithamini kitu chochote, haijalishi itaonyeshwa upendo mkubwa kiasi gani.

Na kwa kawaida mwisho wa siku watu hawa huwa wanaishia katika majuto makubwa sana, pale ambapo wanajiona wameishia katika dhiki, au vifungo, au kukaribia kuuliwa, kutokana na makosa yao, wakati huo shetani ameshawaacha..ndipo wanaposhangaa ilikuwaje walijihusisha katika mambo kama hayo.

Mpaka mtu anafikia hatua ya kuzini zini ovyo hajali chochote, hajali huyu ni mke wa mtu, au mume wa mtu, hajali maradhi, hajali kuwa ni machukizo kwa Mungu, hata wakati mwingine anafanya hivyo na wanyama, au watu wa jinsia moja na yeye, huo ni moyo mwingine wa ibilisi umeshakwisha kuingia ndani yake. Na mwisho wa siku itakuwa ni majuto tu kwake.

Tukumbuke kuwa Yuda alikuwa ni mtume aliyechaguliwa na Yesu mwenyewe, lakini kwa uzembe wake, yalimkuta mambo kama yale, hiyo ni kutufundisha kuwa hata sisi tunaosema tumeokoka yanaweza kutukuta endapo tutakuwa ni watu wa kumpa ibilisi nafasi au upenyo ndani ya maisha yetu.

Tusidhani kuwa tukishafikia hatua hiyo itakuwa ni rahisi kumshinda ibilisi, hilo haliwezekani. Hivyo tuwe makini sana. Tukisema tumeokoka tumaanishe kweli kweli, Yuda alianza na tabia ndogo sana ya wizi, ambayo hakuna mtu aliyejua ingempelekea hata kusaliti na mwisho wa siku kujinyonga. Na sisi mambo madogo madogo tunayoyakumbatia hayo ndiyo yatakuwa upenyo wa ibilisi kutuingia na kuweka mioyo mingine ndani yetu.

Bwana atutie nguvu sote katika safari yetu hii ya wokovu.

Swali ni je, umemwamini Yesu? Je amekusafisha dhambi zako kwa damu yake?. Kama sivyo, unasubiri nini?  Una habari kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Na shetani naye analijua hilo na ndio maana anafanya kazi zake kwa bidii kukuingia mtu kama wewe mwenye mawazo mawili, kukutia moyo mwingine ndani yako, kwasababu anajua wakati alionao ni mchache?.

Ufunuo 12:12 “..Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”.

Huu ni wakati wa kuamka katika usingizi wa mauti, na kumgeukia Kristo, na kumaanisha kweli kumfuata yeye, hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha kuwa tayari kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ikiwa hukubatizwa hapo kabla. Na baada ya hapo Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, atakayekulinda na kukuongoza katika kweli yote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Mwenye hekima huvuta roho za watu”

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Nini maana ya ‘Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu’ ?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Mwenye hekima huvuta roho za watu”

SWALI: Biblia ina maana gani inaposema “Mwenye hekima huvuta roho za watu”?


JIBU: Tusome.

Mthali 11:30 “Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima; Na mwenye hekima huvuta roho za watu”

Zipo hekima nyingi, lakini hekima inayozungumziwa katika biblia ni hekima ya rohoni, ambayo ndiyo kuu kuliko hekima zote, ndio hekima aliyonayo Mungu mwenyewe. Sasa hapo aliposema mwenye hekima huvuta roho za watu, anamaanisha kuwa yeye anayewavuta watu kwa Mungu au watu wamjue Mungu, huyo anatambulika kama mtu mwenye hekima sana.

Hekima hii ilianza kuonekana kwa Bwana wetu Yesu Kristo, Kama tunavyojua yeye aliacha enzi na nguvu na mamlaka huko mbinguni akashuka hapa duniani kwa lengo moja tu,  na kuturejeshea sisi ule uhusiano tuliokuwa tumeupoteza na Mungu, na ndio maana akawa radhi kuhubiri injili na kama hiyo haitoshi kuutoa uhai wake kwa ajili yetu.

Vivyo hivyo na sisi pia, tukisema tumeokoka, ni lazima tuwavute na wengine kwa Mungu, ili na wao pia waokoke kama sisi, Hapo ndipo tutatambulika na mbingu  kuwa tuna hekima, lakini kama hatuonyesha bidii ya namna hiyo, haijalishi tutasema sisi ni wa rohoni kiasi gani, bado tutakuwa hatuna hekima, kwa mujibu wa maandiko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

MATESO YA KUZIMU.

Je kuna uthibitisho wowote wa kimaandiko kwamba kutakuwa na mateso baada ya kifo kwa wale watakaokufa katika dhambi?.

Jibu ni ndio.. Tusome,

Luka 16:22 “Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

23  Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, ALIPOKUWA KATIKA MATESO, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.

24  Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu NINATESWA KATIKA MOTO HUU.

25  Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe UNAUMIZWA.”

Watu wote ambao watamkataa Yesu katika maisha haya, watakapokufa wataenda kuzimu kwenye mateso, watu wote wanaoliharibu hekalu la Roho Mtakatifu (yaani miili yao) kwa kuvaa vimini, nguo za utupu,  zinazochora maungo yao, wanaopaka wanja, wanaopaka hina, wanaoweka kucha za bandia, na wigi ili wafanane na wanawake wa ulimwengu huu, biblia imesema, wote wataingia katika lile ziwa la moto.

Na biblia inazidi kusema kuwa kuzimu haishibi watu na wala haijai,.. ni kubwa kuliko hii dunia tunayoishi.

Mithali 27:20 “KUZIMU NA UHARIBIFU HAVISHIBI;….”.

Mithali 30:15 “……………Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!

 16 KUZIMU; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!“.

Kuzimu haishibi!!..Inapokea tu watu kila siku kila saa… Ipo nafasi kubwa mno kuzimu na watu wanaingia huko kila siku. Biblia haidanganyi.

Watu wote wanaofanya uasherati, na wanaopenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu, ikiwemo kutazama filamu za kidunia, na tamthilia za kidunia, wote wataenda katika ziwa la moto kama hawatatubu na kuacha njia zao mbaya, hiyo ni kulingana na Neno la Mungu.

Wote wanaocheza kamari, ikiwemo kubeti, na michezo yote ya bahati nasibu. Wakifa katika hiyo hali wataenda kuzimu.

Watu wote wanaoishi na wanawake/wanaume ambao si wake zao/waume zao, na wote wanaotazama picha za utupu katika mitandao, na wanaojichua, na walawiti wote.. hao wakifa sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la moto, hiyo ni kulinga na Neno la Mungu.

Na wote watakaoingia kuzimu, hakuna mlango wa kurudi tena au kutoka huko, wakiwa katika mateso huko kuzimu watatamani kutubu lakini itakuwa wameshachelewa, watalia lakini hakuna atakayesikia, mateso yao yatakuwa makali usiku na mchana, watakuwa tu katika hali ya majuto, wakijutia kiburi chao, uchafu wao waliokuwa wanaufanya kwa siri au kwa wazi, uasherati wao waliokuwa wanaufanya bila hofu, ulevi wao waliokuwa wanaufanya kila siku, anasa zao N.k

Kwa uchungu na mateso mengi wakiwa huko, watajigundua kuwa shetani alikuwa amewapofusha macho na hivyo watamchukia shetani kwa ukomo wa chuki, lakini watakuwa wameshachelewa, wangepaswa wafanye hivyo kabla hawajaingia huko.

Ndugu hakuna maombi yoyote yanayopanda kutoka kuzimu kwenda kwa Mungu, hakuna kilio chochote kinachotoka kuzimu na kwenda kwa Mungu, wala hakuna utukufu wowote wa Mungu unaotoka kuzimu, hivyo Mungu hasikii kilio cha watu wanaolia kuzimu, wala kelele zao hazimfikii,  wala sifa zao kwa Mungu, hakuna mtandao kati ya kuzimu na mbingu. Walioingia huko ndio wamesahaulika hivyo.

Isaya 38:18 “Kwa kuwa kuzimu hakuwezi kukusifu; mauti haiwezi kukuadhimisha; Wale washukao shimoni hawawezi kuitarajia kweli yako.  19 Aliye hai, naam, aliye hai, ndiye atakayekusifu..”

Zaburi 6:5 “Maana mautini hapana kumbukumbu lako; Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?”

Shetani kanyanyua mahubiri, yanayosema kuwa kuna tumaini baada ya kifo, yaani wale watu waliokufa katika dhambi  na kuingia kuzimu, wanaweza kutolewa kutoka katika hayo mateso na kuingia peponi, kwasababu Mungu anasikia mateso yao na maumivu yao huko.. USIDANGANYIKE!!. Hakuna nafasi ya pili baada ya kifo, wala hakuna mageuzi wala mashauri kuzimu!!.. Wala hatuwezi kumwombea mtu aliyeshuka kuzimu, wala kumshauri Mungu juu ya hao waliopo kuzimu.

Mhubiri 9:10 “ Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, HUKO KUZIMU UENDAKO WEWE”.

Kaka/Dada unayesoma huu ujumbe, Iepuke kuzimu! Kwasababu kuzimu ipo kweli, sio nadharia, ni kitu halisi kabisa.  Na mtu akishuka huko hatatoka tena milele, na ndilo lengo kubwa la shetani, hataki kwenda mwenyewe kwenye moto wa milele, anataka kwenda na wengi.

Hivyo tusiruhusu hilo, aende peke yake na mapepo yake… Leo hii unapoisikia hii sauti nenda kachome hivyo vimini, na nguo zote za kikahaba, ikiwemo suruali, tupa hayo mawigi na mahereni unayovaa (mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu).. usiangalie ni kundi kubwa kiasi gani linakiuka Neno la Mungu. Kuzimu utashuka peke yako, wala hutakuwa na jopo kubwa la watu, kama hutatubu. Wale funza wa kuzimu, ambao Bwana Yesu alisema hawafi watakutesa kule kuzimu usiku na mchana, na utalia wala sauti yako haitasikika popote, utakuwa peke yako, katikati ya giza nene, ukiungua tu, kwenye moto usiozimika.

Siku hiyo utasema heri ningesikia na kutubu, nisingekuwepo huku..lakini haitasaidia chochote.

Hivyo geuka leo na kutubu kwa vitendo, hiyo miziki unayoisikiliza ya kidunia  itakupeleka kuzimu, futa yote leo katika simu yako, na itoe katika nyumba yako, hizo filamu acha kuzitazama kuanzia muda huu, haijalishi zinapendwa na kusifiwa na wangapi. Kuanzia leo anza kumfuata Yesu kwa kumaanisha, na wala usiwe mshabiki wa Kristo, bali uwe mfuasi wake.

Kama umeamua kumfuata Yesu leo kwa kutubu, na kudhamiria kuacha vyote.. Bali uamuzi huo ni bora kuliko kitu kingine chochote ambacho ungeweza kukifanya, hivyo ili usirudi tena nyuma na uukulie wokovu, hakikisha unakishikilia kile ulicho nacho kwa bidii sana, kwa kusoma Neno la Mungu kwa bidii, na kutafuta kuzijua habari zake kwa bidii, mahali popote pale anapohubiriwa.

Na pia ili kuukamilisha wokovu wako, ni lazima ukabatizwe ubatizo sahihi kama bado hujabatizwa, Ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO, ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kulingana na Matendo 2:38, Matendo 8:16, na Matendo 19:5, kwaajili ya ondoleo la dhambi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Kuota upo nchi nyingine.

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

KUZIMU NI WAPI

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

Rudi nyumbani

Print this post

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu? (Luka 23:31)


JIBU: Tunaona sehemu mbalimbali katika biblia Bwana Yesu alijifananisha na MTI, utaona kuna mahali anasema mimi ni mzabibu wa kweli, mtu akikaa ndani yake huzaa sana.(Yohana 15:1-8), Sehemu nyingine katika kitabu cha Ufunuo Yesu anajulikana kama mti wa Uzima (Ufunuo 22:2).Akiwa na maana kuwa yeye ni kama mti ulio hai mbichi, utoao matunda,..wenye maneno ya uzima, wenye ishara na miujiza mingi ya wazi, aliyewaponya watu wote waliomwendea bila kushindwa na chochote. Aliyewaweka huru waliokuwa wanasumbuliwa na mateso, na mapepo, aliyekuwa na uwezo wa kuwasamehe watu dhambi zao, Mtu ambaye hakuwahi kuwa na doa lolote la dhambi hapa duniani, lakini hilo halikuwa na thamani machoni pao, badala yake walimdhihaki, na kumpiga na kumuua.

Mti mbichi ambao haukustahili kuchomwa moto, lakini waliuchoma moto.. vipi kuhusu miti mikavu isiyozaa,wakiiona si ndo wataifanyia zaidi. Pengine Hawataikata hata, bali wataichomea pale pale ilipo kama kuni angali imesimama,.

Na sisi ndio kama hiyo miti mikavu, ambao tumezaliwa katika dhambi, ambao hatuna ishara kama za Yesu, hatufanyi uponyaji mkuu kama wa Bwana Yesu, tunamkosea Mungu mara kwa mara, hatutoi maneno ya uzima yanayowaokoa watu muda wote, tunajikwaa kila wakati, tunategemea vipi ulimwengu utatupokea?. Tusidhani kuwa chochote tutakachojitahidi kukitenda kwa ajili ya Kristo kitakuwa ni kitu cha kupendwa sana na wao.

Yeye mwenyewe alisema..

Yohana 15:18 “Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.

19 Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.

20 Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu.

21 Lakini haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa kuwa hawamjui yeye aliyenipeleka”.

Kwahiyo  maneno hayo ni kuwa Bwana Yesu alikuwa anatoa tu angalizo, kwamba yatakapotutokea tusiogope au tusidhani kuwa sisi hatupendwi na Mungu au tumekosea sehemu fulani na ndio maana yametukuta kama hayo,  hapana badala yake tujue kuwa kama alivyoyapitia yeye ndivyo tutakavyoyapitia na sisi pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 22

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

VIKAANGUKA MACHONI PAKE VITU KAMA MAGAMBA.

Rudi nyumbani

Print this post

Adhama ni nini katika biblia?

Adhama ni neno lenye maana ya “Uzuri wa hali ya juu sana”. Na huu uzuri ni Bwana Yesu tu peke yake ndio anao, yeye ndiye mwenye adhama.

Zaburi 93: 1 “Bwana ametamalaki, amejivika adhama, Bwana amejivika, na kujikaza nguvu. Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;

2 Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani; Wewe ndiwe uliye tangu milele”

Mistari mingine michache inayozungumzia adhama ni kama ifuatayo..

Zaburi 96:6 “Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake”.

Zaburi 104:1 “ Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Umejivika heshima na adhama.

2 Umejivika nuru kama vazi; Umezitandika mbingu kama pazia;”

Isaya 33:21 “ Bali huko Bwana atakuwa pamoja nasi, mwenye adhama; mahali penye mito mipana na vijito, pasipopita mashua na makasia yake; wala hapana merikebu ya vita itakayopita hapo”.

2Wakorintho 4:7 “Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu”.

Mistari mingine iliyotaja neno hilo ni pamoja na 1Nyakati 16:27, Zaburi 21:5, Zaburi 113:3,  Zaburi 148:13 na Zaburi 29:4.

Hivyo Bwana Yesu, peke yake ndiye mwenye heshima yote na adhama yote, na wala hakuna mwingine.

Ufunuo 5:9 “Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

Nini maana ya..“wakiwazuia watu wasioe” (1Timotheo 4:1)

UTUKUFU NA HESHIMA.

Rudi nyumbani

Print this post

2Samweli 24:1-14,inasema ni jambo la kutisha kuangukia katika mkono wa Bwana je! inakinzana na Waebrania 10:31?.

SWALI: Katika 2Samweli 24:1-14, Hapo tunaona Daudi anasema, afadhali kuangukia katika mkono wa Bwana, lakini anapingana na Paulo katika Waebrania 10:31, anaposema ni jambo la kutisha mtu kuangukia katika mikono ya Mungu aliye hai.

Jibu: Shalom, ukisoma kwa makini utaona kuwa sio kwamba maandiko yanapingana, kwamfano

Tukijifunza hicho kisa cha Daudi kwanini aseme ni heri kuangukia katika mikono ya Mungu, ndipo tutaelewa vizuri.

Kama tunavyoijua habari, Daudi alifanya kosa na Mungu akamwekea mapigo matatu mbele yake achague moja; Taifa lake lipigwe na njaa miaka 7, au Taifa lake lipigwe na ugonjwa wa Tauni siku tatu, au yeye mwenyewe akimbizwe na maadui zake miezi 3.

Sasa katika hizo adhabu tatu alizoambiwa achague, mbili kati ya hizo ni mkono wa Mungu na moja ni mkono wa mwanadamu.. Kwamfano hiyo ya njaa miaka saba na Tauni siku tatu, ni mkono wa Bwana, lakini hiyo ya kukimbizwa na maadui zake miezi 3, ni mkono wa mwanadamu.

Hivyo Daudi kwa uzoefu alioupata katika maisha yake, kupitia kufukuzwa na Sauli nyika kwa nyika, alijifunza kuwa kuwindwa na mwanadamu ni kubaya sana kwasababu mwanadamu hana rehema wala huruma..atakutafuta usiku na mchana, na hata akikushika hatakuhurumia.. Lakini kwa Mungu zipo rehema, huwa anaghairi mabaya, hata kama kashayanena, huwa ana huruma.

Kwahiyo Daudi alipopewa adhabu hizo tatu achague moja, ndipo yeye akachagua kuangukia mikononi mwa Mungu, kwasababu kuna rehema, Maana yake aidha Taifa lake lipigwe na njaa miaka 7 au wapigwe na tauni siku 3, kwasababu pengine wakiwa katikati ya hiyo adhabu Mungu anaweza kuwahurumia na kuikatisha adhabu hiyo, lakini asiangukie mikononi mwa wanadamu wamfukuze na kumwinda, kwani huwa hawakati tamaa na hawanaga huruma.

Na kweli, alipochagua kuangukia mikononi mwa Mungu, Tunasoma Mungu aliwapiga kweli kwa Tauni, lakini tunasoma hazikumalizika  siku zote tatu, Mungu aliizuilia ile Tauni, kwasababu ni mwingi wa rehema.

Tusome kidogo,

2Samweli 24:13 “Basi Gadi akamwendea Daudi, akamweleza, akamwambia, Basi, miaka saba ya njaa ikujie katika nchi yako? Au miezi mitatu ukimbie mbele ya adui zako, huku wakikufuatia? Au siku tatu iwe tauni katika nchi yako? Fanya shauri sasa, ufikiri, ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma.

14 Naye Daudi akamwambia Gadi, Nimeingia katika mashaka sana; basi sasa na TUANGUKE KATIKA MKONO WA BWANA; kwa kuwa rehema zake ni nyingi; wala nisianguke katika mkono wa wanadamu.

15 Basi Bwana akawaletea Israeli tauni tangu asubuhi hata wakati ulioamriwa; nao wakafa watu toka Dani mpaka Beer-sheba sabini elfu.

16 LAKINI HUYO MALAIKA ALIPONYOSHA MKONO WAKE KUELEKEA YERUSALEMU ILI AUHARIBU, BWANA AKAGHAIRI KATIKA MABAYA, AKAMWAMBIA HUYO MALAIKA MWENYE KUWAHARIBU WATU, YATOSHA, SASA ULEGEZE MKONO WAKO. NAYE YULE MALAIKA WA BWANA ALIKUWAKO KARIBU NA KIWANJA CHA KUPURIA CHA ARAUNA, MYEBUSI”.

Umeona hapo?, Bwana kaghairi mabaya!!.. Lakini hiyo haizifanyi adhabu zake kuwa HERI, Hata kama ataghairi mabaya lakini tayari kashaadhibu wengi, (hapo wameshaanguka watu elfu sabini, pengine walikusudiwa kuanguka watu laki tatu), lakini pamoja na hayo watu elfu sabini si wachache..Ni wengi sana, ni heri Daudi angeangukia kwenye kukimbizwa miezi mitatu yeye peke yake kuliko kuruhusu vifo vya watu elfu sabini..

Hivyo suala bado lipo pale pale kwamba ni jambo la kutisha kuangukia kwenye mikono ya Mungu hata kama ana rehema nyingi, kwasababu ni kweli anaweza akaghairi mabaya, lakini tayari atakuwa ameshaadhibu na kuharibu pakubwa sana..(watu elfu sabi). Ndicho Mtume Paulo alichokisema katika kitabu cha Waebrania…

Waebrania 10:30 “Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.

31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai”.

Kwahiyo mistari hiyo haikinzani bali inakubaliana katika jambo moja…Na Daudi alipochagua kuangukia katika mikono ya Mungu, si kwasababu adhabu za Mungu ni ndogo, bali ni kwasababu zina rehema ndani yake, kulinganisha na zile za wanadamu. Lakini hukumu za Mungu zinatisha na za kuogopwa, na ni kubwa kuliko za wanadamu, kwaufupi si za kutamani kabisa, kama Mtume Paulo alivyosema.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

AINA TATU ZA WAKRISTO.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII?

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

Rudi nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

Kitabu cha Tito ni waraka ulioandikwa na Mtume Paulo, kwa mtu anayejulikana kama Tito. Tito alikuwa ni mmoja wa watu waliogeuzwa kumgeukia Kristo, kupitia injili ya Mtume Paulo. Na mtu huyu alikuwa ni mwenyeji wa mji ulioitwa Krete.

Krete ni kisiwa kilichopo kusini mwa nchi ya Ugiriki, zamani kilikuwa kinaitwa Krete na hata leo hii bado kinaitwa hivyo hivyo Krete.

Kwahiyo Mtume Paulo katika ziara zake za kuhubiri, alifika pia katika kisiwa hicho, na hatimaye huyu Tito akawa mmoja wa matunda yake katika Injili. Na kwa kuwa alikuwa na bidii Zaidi  kuliko wengine, akachaguliwa kwa uongozo wa Roho Mtakatifu kuwa mwangalizi wa makanisa ya huo miji.

Na Paulo na wenzake baada ya kuondoka katika huo mji, kwenda kwenye miji mingine kwajili ya kuhubiri injili, ilibidi amwandikie waraka Tito, na kumpa maagizo machache ya namna ya kulijenga kanisa, Na maagizo hayo yalikuwa yamegawanyika katika vipengele viwili. 1) Maagizo jinsi ya kuteua viongozi wa kanisa na 2) Maagizo kwa waumini wote wa kanisa.

 1. MAAGIZO JINSI YA KUTEUA VIONGOZI WA KANISA.

Uteuzi wa viongozi ulitegemea vigezo fulani vya kimaandiko, hivyo ilibidi Paulo amfundishe Tito vigezo vya maaskofu, wachungaji na wazee wa kanisa, wanavyopaswa wawe, ili kanisa lisije likaanguka kwa kukosa uongozi thabiti, kutokana na kuwa viongozi wasio na vigezo. Hivyo Paulo kwa uongozo wa Roho akamwandikia Tito waraka huo na baadhi ya mambo aliyomwambia ni kama yafuatayo..

Tito 1:4 “ Tito, mwanangu hasa katika imani tuishirikiyo. Neema na iwe kwako na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.

5 Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;

6 ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.

7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno ,kwa kuwa ni wakili wa MUNGU;asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake,asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu.

8 bali awe mkaribishaji, mpenda wema, mwenye kiasi, mwenye haki, mtakatifu, mwenye kudhibiti nafsi yake;

9 akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.

10 Kwa maana kuna wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, wadanganyaji, na hasa wale wa tohara, ambao yapasa wazibwe vinywa vyao.

11 Hao wanapindua watu wa nyumba nzima, wakifundisha yasiyowapasa kwa ajili ya mapato ya aibu”

 2. MAAGIZO KWA WAUMINI WOTE WA KANISA.

Na pamoja na hayo, Paulo alimpa maagizo ndugu Tito, Na maagizo hayo yalikuwa ni maonyo kwa waumini wote, wazee wakike kwa wa kiume, na vijana wa kike kwa wakiume, na watumwa.

Aliwaonya wazee wanawake wawe katika utakatifu, ili wawe vielelezo kwa wanawake vijana, kadhalika na watumwa wawatii Bwana zao.

Tito 2:1 “Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima;

2 ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika saburi.

3 Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema;

4 ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.

6 Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi;

7 katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu,

8 na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.

9 Watumwa na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wenye kujibu,

10 wasiwe waibaji; bali wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote.

11 Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa”.

Na pia Mtume Paulo, alimpa maagizo Tito, kuwa awakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye mamlaka..

Tito 3:1 “Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema;

2 wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote”.

Na mwisho, akamwambia maneno haya..

Tito 2: 15 “Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote”.

Katika waraka huu tunajifunza mambo kadhaa.

1. Kwanza tunajifunza kanisa la Kristo linaongozwa na maaskofu, wachungaji, walio na vigezo vya kimaandiko, kama tulivyovisoma hapo juu..

2. Na pia kila mshirika wa kanisa, ni lazima ajifunze kuishi maisha ya utakatifu, Kama ni mzee fahamu kuwa kuna vijana chini yako na watoto, ambao wanapaswa kujifunza kutoka kwako, wakikuona wewe mzee una mizaa je watajifunza nini kutoka kwako?..wakikuona wewe mzee unavaa vibaya watajifunza nini kutoka kwako?.

Vivyo hivyo kama wewe ni mtumwa, labda unafanya kazi katika shirika fulani, au na juu yako wapo wakubwa kuliko wewe, halafu wanakuona huna adabu, ni mwizi, na sio mnyenyekevu, je unawatengenezea picha gani kuhusu ukristo?

Na pia kinatufundisha sisi kama washirika wa mwili wa Kristo, kunyenyekea kwa wenye mamlaka. Haijalishi mwenye mamlaka ni nani, biblia imetuonya tuwaheshimu na kuwanyenyekea, unyeyekevu unaozungumziwa hapo sio kuwaabudu au kuwaogopa kiasi kwamba hata wakikuambia usimwabudu Mungu wako uwatii.. Hapana! Bali unyenyekevu unaozungumziwa hapo ni ule wa wewe kufuata na kutii maelekezo yao yote ambayo yanaelekeza kufanya mema, na kuwaheshimu kama unavyowaheshimu watu wengine wote.

Kwamfano mwenye mamlaka katika mji wako amesema  “siku fulani ni ya kufanya usafi” hapo huna budi kutii.

 3. Na jambo la mwisho tunaloweza kujifunza ni kukaripia, na kuonya kwa mamlaka yote watu wote wanaokwenda kinyume na Neno la Mungu ndani ya kanisa. Paulo alimwambia Tito akaripie, hivyo hata leo tuna jukumu hilo hilo, la kukaripia uzinzi na wazinzi waliopo kanisani, kukaripia walevi waliopo kanisani, kukaripia watukanaji na wavaaji vibaya kanisani, tena biblia imesema tufanye hivyo kwa mamlaka yote, bila hofu kwasababu si dhambi. Wengi wanaogopa kukaripia kwasababu wanahisi kwamba watakuwa wanawahukumu watu. Hapana!. Kuambiwa ukweli sio kuhukumiwa bali ni kuonywa. Na biblia na ukristo kwa ujumla, dhima yake kubwa ni maonyo! Hakuna kitu kingine, kama hutaki maonyo, basi ukristo haukufai.

Bwana atubariki.

Kama hujampokea Yesu, kama bado unavaa vimini, kama bado ni mlevi, mshirikina,  mwizi n.k fahamu kuwa ukifa leo unakwenda jehanamu. Hivyo ni bora ukampokea Yesu leo kwa kutubu, na kuacha kufanya dhambi, ili upate wokovu na msamaha wa dhambi.

Yesu Kristo yupo mlangoni kurudi !!!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

UFUNUO Mlango wa 2: Sehemu ya pili.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Tusome,

2Petro 3:8 “Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja”.

Kama ukiendelea mbele kidogo kusoma mstari wa 9, utaona Mtume Petro anajaribu kumwelezea Mungu kwamba huwa hakawii kuzitimiza ahadi zake kwetu sisi wanadamu.  

2Petro 3:8 “Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.

 9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba”.

Aliona kuna watu wengi wanaona kama Mungu huwa anachelewa sana kutimiza aliyoyasema.. Alisema atarudi, mbona harudi na imeshapita miaka mingi? N.k

Ndipo akazungumza maneno hayo, ambayo pia yalizungumzwa kwa sehemu na Mfalme Daudi katika Zaburi..

Zaburi 90:4 “Maana miaka elfu machoni pako Ni kama siku ya jana ikiisha kupita, Na kama kesha la usiku”.

Maana yake ni kwamba tunapodhania kwamba Miaka elfu ni kipindi kirefu sana, kwa Mungu kwake ni kama siku moja tu ya jana iliyoisha. Na kwanini Kristo hajarudi mpaka miaka hii, sababu imeshatolewa hapo juu, kwamba “hapendi mtu yoyote apotee, bali wote waifikilie toba”. Hivyo anatuvumilia ili watu wote tuingie katika neema ya wokovu, kabla ya ule mwisho kufika,  maana ule mwisho ukifika kama hatutakuwa ndani ya wokovu, hakutakuwa na nafasi ya pili.

Lakini pia kama tukifikiri Mungu kawahi sana, basi tusisahau kuwa siku moja kwa Mungu ni sawa na miaka elfu, maana yake, tunaishi nje ya muda, (muda umeenda sana), na ule mwisho upo karibu sana. Kristo yupo mlangoni..

Na ndio maana biblia inasema “saa ya wokovu ni sasa”.

2Wakorintho 6.2 “Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa”

Kadhalika katika mambo mengine ya kimaisha, tunapoona siku moja ni fupi sana kwetu Mungu kufanya jambo, tujue kuwa kwa Mungu ni kama miaka elfu, maana yake ahadi zake alizotuahidi anaweza kuzitimiza  ndani ya siku moja… Kwahiyo hatupaswi kumkosea Mungu Imani, hata kama tumeona siku inakaribia kuisha na hatujapata kile tunachokitafuta, tufahamu kuwa Mungu anaweza kufanya jambo kubwa ndani ya siku hiyo hiyo moja kabla haijaisha yote, kwasababu kwake yeye ni kama miaka elfu.

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

Jina la Mwokozi wetu Yesu, libarikiwe.

Mnadhiri ni mtu aliyejitenga na mambo fulani ili atimize nadhiri/Ahadi aliyoiweka kwa Mungu wake. Kwamfano katika agano la kale, kama mtu ameweka nadhiri fulani kwa Mungu, labda  ya kumtolea sadaka Fulani, na akatamka kwa kinywa chake mwenyewe mbele za Mungu, basi yalikuwepo maagizo Fulani ya kufanya ambayo yanaambatana na nadhiri hiyo aliyoiweka ili asije akaisahau nadhiri hiyo aliyoiweka.

Na agizo la kwanza kwa mtu aliyeweka nadhiri, ni kwamba hakupaswa kabisa kunywa divai wala kilevi cha aina yoyote ile.

Hesabu 6: 1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Nena na watu wa Israeli, uwaambie, Mtu mume au mtu mke atakapoweka nadhiri kubwa, nadhiri ya Mnadhiri, ili ajiweke wakfu kwa Bwana;

3 atajitenga na divai na vileo; hatakunywa siki ya divai, wala siki ya kileo, wala asinywe maji yo yote ya zabibu, wala asile zabibu, mbichi wala zilizokauka.

 4 Siku zote za kujitenga kwake asile kitu cho chote kilichoandaliwa kwa mzabibu, tangu kokwa hata maganda”.

Na kwanini Mungu akataze mtu asinywe kileo chochote, wakati wa nadhiri yake? . Ni kwasababu kileo kinamtoa mtu ufahamu, na kumfanya ajisahau, hata ajikute anazungumza maneno au anafanya vitendo ambavyo ni kinyume na ile nadhiri aliyomwekea Mungu, hivyo ikawa dhambi kubwa kwake. Maana yake ni kwamba mtu aliyemwekea Mungu nadhiri ni lazima awe katika akili yake timamu wakati wote, hapaswi hata dakika moja kujitoa nje ya ufahamu wake kwa kileo, au kwa kitu kingine chochote.

2. Sheria ya Mnadhiri (yaani mtu aliyeweka nadhiri) ilikuwa ni lazima, aziache nywele zake ziwe ndefu, (Hapaswi kuzikata kabisa).

Hesabu 6: 5 Siku zote za nadhiri yake ya kujitenga, wembe usimfikilie kichwani mwake; hata hizo siku zitakapotimia, ambazo alijiweka wakfu kwa Bwana, atakuwa mtakatifu, ataziacha nywele za kichwani mwake zikue ziwe ndefu”.

Siku zote nywele ni ishara ya uwepo wa Mungu juu yetu. Na nywele huwa ni nyingi kichwani, na zina tabia ya kukua, kila siku zinaongezeka kimo, Ndivyo rehema na Neema za Mungu zilivyo nyingi juu yetu, zinaongezeka kila kukicha.

Maombolezo 3: 22 “Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.

23 Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu”

Kwahiyo mnadhiri yeyote, ambaye alikuwa amemwekea Mungu nadhiri, hakukata nywele zake, mpaka siku ambayo atatimiza nadhiri hiyo ndipo ataruhusiwa kuzikata. (Matendo 18:18, matendo 21:23).

Sasa kama ukiendelea kusoma zaidi juu ya sheria hizo za mnadhiri, utaona kuwa pia mnadhiri yeyote pamoja na kutokukata nywele zake na kunywa kileo, alipaswa pia siku zote ajitenge na kila aina ya unajisi, maana yake alipaswa ajiweke katika hali ya utakatifu. Na kama akishindwa kutimiza vigezo hivyo nadhiri yake hiyo inakuwa ni batili na ni dhambi kwake.

Lakini pia kulikuwa na Baraka za kipekee kwa mtu aliyemwekea Mungu nadhiri, kipindi chote wakati yupo katika hiyo nadhiri na hata baada ya kuimaliza hiyo nadhiri. Na baraka hiyo ya kipekee ilikuwa ni kutembea na nguvu za Mungu, kwa namna isiyokuwa ya kawaida..Na nguvu hiyo kazi yake ni kumweka mtu mbali na maadui wa kiroho.

Sasa leo kwa msaada wa Bwana tutajifunza mtu mmoja katika maandiko, ambaye alikaa katika nadhiri za Mungu, na kuzifurahia nguvu za Mungu, mpaka siku alipojisahau na kutoka nje ya nadhiri na kupata madhara, na kupitia mtu huyo tutajua umuhimu wa kukaa katika nadhiri kwa Mungu wetu tulizomwekea.

Na mtu huyo ambaye tutajifunza habari zake  si mwingine zaidi ya Samsoni.

Biblia inasema Samsoni alikuwa Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yake.  Mungu mwenyewe ndiye aliyemfanya awe mnadhiri wake.

Na kama sheria ya Mnadhiri wa Mungu inavyosema, hakupaswa anywe divai, wala kileo kingine chochote, hivyo Samsoni hakunywa kileo chochote tangu akiwa tumboni mwa mama yake, ndio maana Mungu alimwambia mama yake asinywe divai wakati wa uja uzito wake, kadhalika kama mnadhiri wa Mungu hakupaswa kukatwa nywele zake, kulingana na maagizo Mungu aliyotoa katika torati kumhusu mnadhiri..

Waamuzi 13:3 “Malaika wa Bwana akamtokea yule mwanamke, akamwambia, Tazama, wewe sasa u tasa, huzai; lakini utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume.

4 Basi sasa, jihadhari, nakuomba, usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilicho najisi;

5 kwani tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume; na wembe usipite juu ya kichwa chake; maana mtoto huyo atakuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni; naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya Wafilisti”.

Umeona hapo?..ni kwanini Samsoni nywele zake hazikupaswa kukatwa.? Si kwasababu alikuwa ni mtu maalumu sana, bali ni kwasababu tayari alikuwa ni Mnadhiri, na sheria ya mnadhiri tangu wakati wa Musa ni kutokukata nywele, wala kunywa divai. Hivyo Samsoni hakupaswa kukata nywele zake wala kunywa kileo chochote maisha yake yote, ili nadhiri yake iwe na maana.

Sasa imezoeleka kufahamika kwamba, Samsoni nguvu zake zilikuwa katika nywele tu!..Lakini kiuhalisia ni kwamba hazikuwa katika nywele zake tu, bali hata katika kitu alichokuwa anakunywa… Ndio maana alionywa asinywe kileo chochote tangu akiwa tumboni…

Maana yake ni kwamba hata kama Delila asingejua siri ya nywele zake, lakini akajua siri ya kutokunywa kwake kileo, na hivyo akaenda kumtengenezea kileo na kumpa, bado nguvu za Samsoni  zingeisha mpaka atakapolevuka na kurudia akili yake, Kwasababu siri za nguvu za Samsoni, zilikuwa katika Neno la Mungu, ambalo linatoa maagizo juu ya mnadhiri, na neno hilo Mungu alilizungumza tangu wakati wa Torati ya Musa…

Hesabu 6: 1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Nena na watu wa Israeli, uwaambie, Mtu mume au mtu mke atakapoweka nadhiri kubwa, nadhiri ya Mnadhiri, ili ajiweke wakfu kwa Bwana;

3 atajitenga na divai na vileo; hatakunywa siki ya divai, wala siki ya kileo, wala asinywe maji yo yote ya zabibu, wala asile zabibu, mbichi wala zilizokauka.

 4 Siku zote za kujitenga kwake asile kitu cho chote kilichoandaliwa kwa mzabibu, tangu kokwa hata maganda

5 Siku zote za nadhiri yake ya kujitenga, wembe usimfikilie kichwani mwake; hata hizo siku zitakapotimia, ambazo alijiweka wakfu kwa Bwana, atakuwa mtakatifu, ataziacha nywele za kichwani mwake zikue ziwe ndefu”.

Kwahiyo kama mtu yupo katikati ya nadhiri halafu akakata nywele zake, anakuwa kashaharibu kila kitu…kadhalika kama yupo katikati ya nadhiri halafu akalewa na kilevi cha aina yoyote ile,  vile vile anakuwa kashaharibu kila kitu.. Kwahiyo Samsoni akiwa bado yupo katika nadhiri yake ambayo hiyo ilikuwa ni ya maisha, nywele zake  zilikatwa…na hivyo akawa amejiharibia mwenyewe.

Hiyo ilikuwa ni agano la kale, kwamba mtu akiweka nadhiri ni lazima aziache nywele zake zikue… na mtu akivunja maagizo hayo ya torati anakuwa amejiharibia mwenyewe.

Hali kadhali katika agano jipya, tunazo nadhiri; Zipo nadhiri ambazo sisi wenyewe tunaziweka…kwamfano zile za kuahidi kufanya jambo Fulani kwa Mungu, lakini zipo nadhiri ambazo sisi hatuamui kuziweka, bali Mungu mwenyewe ndiye anayeziweka katika maisha yetu, kama vile Samsoni.

 Samsoni hakumwekea Mungu nadhiri kwa kuamua yeye, isipokuwa Mungu mwenyewe ndiye aliyemwekea ile nadhiri tangu akiwa tumboni mwa mama yake,  yeye alijikuta tu tayari kazaliwa na ile nadhiri. Vivyo hivyo pia mtu anayezaliwa mara ya pili katika roho, tayari anakuwa na nadhiri ya Maisha,  ambayo hiyo ni Mungu anaiweka katika maisha yake, na inamfunga aishi katika sheria za Mungu, na wakati wote na ni lazima aishi kulingana na Neno la Mungu ili nguvu zake za rohoni zisipotee, wakati wote anapoishi hapa duniani.. Lakini kama akitoka nje ya neno la Mungu, na kuruhusu  adui shetani yake akate nywele zake za rohoni, kama alivyofanya kwa samsoni, atakuwa amejiweka katika hali ya hatari sana, ni heri hata asingezaliwa mara ya pili.

Sasa ifuatayo ni milango ambayo shetani anaitumia kuzikata nywele zetu za rohoni, na kututoa katika unadhiri mtakatifu.

1.Uzinzi na uasherati.

Unapofanya uzinzi au uasherati baada ya kuzaliwa mara ya pili,  au unapojihusisha na mahusiano yoyote ya kipepo, hapo tayari unakuwa umejiuza kwa shetani moja kwa moja.. Na hicho ndicho kilichomwangusha pia Samsoni…Biblia inasema katika Mithali 31:3 “Usiwape wanawake nguvu zako;…”.  Na inasema pia..

1Wakorintho 6:18  “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”.

Hapo inasema, ikimbieni sio ikemeeni…

Siku hizi ni fashion kila kijana kuwa na girlfriend, na binti kuwa na boyfriend, tena hayo yanafanyika kanisani, na kila mtu anajua..halafu huyo huyo analalamika siku hizi nguvu za kusali zimeisha, anasumbuliwa na mapepo, anaota ndoto mbaya, akisoma neno dakika mbili anasikia usingizi, anashindwa kujizuia kutenda dhambi, mambo yake hayaendi sawa n.k..Sasa hizo nguvu zitatoka wapi wakati tayari umeshampa shetani?…tayari shetani kashakata nywele zako, kwa uasherati wako huo, hiyo nguvu ya kuomba utatolea wapi?, hiyo nguvu ya kusoma neno utatolea wapi, hiyo nguvu ya kwenda kuhubiri utatolea wapi, hiyo nguvu ya kufunga utatolea wapi?, utakemea pepo gani litoke?..kwaufupi katika roho, shetani ameshakupofusha macho na anakusagisha ngano katika gereza lake kama alivyomfanya Samsoni. (Waamuzi 16:21).

2.Ibada za sanamu.

Huu ni mlango wa pili, shetani anaoutumia kututoa katika unadhiri mtakatifu. Kumbuka siku zote pale tunapozaliwa mara ya pili, hatupaswi kumwambudu mtu yeyote wala kitu chochote. Tunapomfanya mtu Fulani, achukue nafasi ya Mungu, au kitu Fulani tulichokitengeneza kwa mikono yetu kichukue nafasi ya Mungu..tayari tumemfungulia shetani mlango wa kutuondoa kwenye unadhiri wetu mtakatifu.

Na mambo mengine yote yaliyosalia yaliyo kinyume na Neno la Mungu, ni mlango wa adui kututoa kwenye unadhiri mtakatifu.

Sasa inawezekanana tayari shetani kashakutoa katika  unadhiri wako, ambao Bwana alikuwekea tangu siku ile ulipozaliwa mara ya pili, ndio maana ulikuwa unanguvu nyingi za rohoni, kuangusha ngome na mamlaka kwa jina la Yesu, hata adui akuzingire kiasi gani, hakukuweza, kama vile Samsoni, ulikuwa una nguvu za kusali na kusoma Neno, na kushinda dhambi.. Lakini ulimfungulia shetani mlango mahali Fulani na akaziondoa nguvu zako, na mpaka sasa huwezi tena kufanya yale uliyokuwa unafanya mwanzo.

Suluhisho ni moja, ni kuanguka chini na kujinyenyekeza kwa Mungu, kwa kutubu kama Samsoni alivyofanya, na kuachana na mambo yote yaliyo kinyume na Neno la Mungu, kama ulikuwa unaishi maisha ya uasherati unayaacha kwa vitendo, ikiwemo kukata mawasiliano na hao uliokuwa unafanya nao uashetari, kama ulikuwa unaabudu sanamu, unaacha na kutubu, kama udanganyifu wa mali ulikuwa umekushika, unapunguza muda wa kufanya shughuli na kuongeza muda wa kumtafuta Mungu n.k. Kama ukifanya hayo Mungu ni wa rehema, kama alivyomrehemu Samsoni, na kumrejeshea tena nguvu zake. Na wewe utarudia katika hali yako ya unadhiri mtakatifu,kama ule wakati ambapo majeshi ya adui yalikuwa hayawezi kusimama mbele yako.

Lakini kama bado unaupenda ulimwengu, fahamu kuwa upo gereza na macho yako yamepofushwa, na kama bado hujampokea Yesu kabisa maishani mwako, ni vyema ukampokea leo, maadamu anapatikana, itafika wakati utatamani siku moja ya mwana wa Adamu katika maisha yako usiione, kama ukiipuuzia sauti yake inayokuita leo.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NADHIRI.

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?

Fadhili ni nini? Nini maana ya “fadhili zake ni za milele” kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post