Title April 2020

Mahuru ndio nini?

SWALI: Mahuru ndio nini? Kama Bwana alivyosema katika Mathayo 17:26, Na ni jambo gani tunajifunza pale?


JIBU: Tusome;

Mathayo 17:25 “Naye alipoingia nyumbani, Yesu alitangulia kumwuliza, akisema, Waonaje, Simoni? Wafalme wa dunia hutwaa kodi ama ushuru kwa watu gani? Kwa wana wao au kwa wageni?

26 Naye aliposema, Kwa wageni, Yesu alimwambia, Basi, kama ni hivyo, WANA NI MAHURU.

27 Lakini tusije tukawakwaza, enenda baharini ukatupe ndoana, ukatwae samaki yule azukaye kwanza; na ukifumbua mdomo wake utaona shekeli ichukue hiyo ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako”.

Ukisoma mstari huo..Bwana alikuwa anazungumzia juu ya wale wanaostahili kulipishwa kodi kulingana na tamaduni za wakati huo…Kwamba kwa wakati huo watu wanaotoka mji mmoja kuingia mwingine ambao si wa kwao walikuwa wanatozwa ushuru…lakini wale wenyeji walipokuwa wanarudi kuingia kwao hawatozwi ushuru kwasababu wao ni wenyeji au wana wa huo mji…

Hivyo hapa Bwana alikuwa ametoka na wanafunzi wake kutoka mji mmoja kwenda mwingine ndani ya Mkoa wake mwenyewe ulioitwa Galilaya…lakini wakataka kumtoza nusu shekeli na ilihali yeye ni mwenyeji wa Mkoa ule na wala si mgeni (Galilaya ilikuwa inajumuisha majimbo ya Nazareti, Korazini, Kapernaumu, Tiberia, Naini, Magdala na mengine machache madogo madogo), na Galilaya yote ilikuwa chini ya Mfalme Herode wa kirumi. Hivyo yoyote aliyekuwa mzawa wa majimbo hayo alikuwa huru kwenda popote katikati ya hayo majimbo pasipo kutozwa ushuru wowote…

Ni sawa na sisi tulivyo na uhuru wa kusafiri mkoa wowote bila vizuizi.

Lakini hawa walipomwona Yesu waliingiwa na tamaa ingawa walijua kabisa ni mzawa, lakini waliingiwa na tamaa labda pengine walimwona anafuatwa na watu wengi wakadhani atakuwa na pesa nyingi hivyo wakawa wanatafuta sababu za kupata fedha kutoka kwake..

Sasa Bwana ndio anamwuliza Petro je wanaotozwa ushuru ni wageni au WANA ?(neno wana ni sawa na wenyeji)…Ndio Petro anamjibu kwamba ni Wageni ndio wanaopaswa kutozwa ushuru na si wenyeji…Ndipo Bwana akamwambia basi kama ni hivyo Wana au kwa lugha nyingine wenyeji ni MAHURU..yaani maana yake wazawa WAPO HURU…Hawapaswi kutozwa chochote kulingana na sheria ya nchi.

Lakini kwasababu Bwana ana hekima nyingi na siku zote anampendeza Mungu na wanadamu hakutaka kuwakwaza kwa vyovyote vile..ndio akamwambia Petro akavue na samaki atakayezuka wa kwanza mdomoni atakuta fedha aje kuilipa kwaajili yake na ya Petro.

Tunajifunza hapo na sisi…sio kila vita vya kupambana nayo…vingine mwachie Bwana akupiganie..Hebu jiulize hapa Petro angeanza kugoma..oo hapana hiyo sio haki, mnatuonea, mnatunyanyasa..sisi ni wenyeji n.k Bila shaka asingeuona ule muujiza Bwana alioufanya…Na kama ukichunguza pale hawakuwa hata na senti..ndio maana Bwana akamwambia Petro akavue…Sasa kwa utulivu wa Petro faida aliyoipata ya kuwa mtulivu na kumtii Bwana na kumwamini alipoenda kuvua ili aje kulipa ushuru ambao si halali yake kuulipa.. alipata faida mara mbili..

Faida ya kwanza aliyoipata ni kwenda kulilipa lile deni alilokuwa anadaiwa ambalo halikuwa halili kwake kulilipa…na faida ya pili na ya muhimu ni Yule samaki…pengine alikwenda kumuuza au kumtumia kwa kitoweo baada ya kumtoa ile sarafu mdomoni…

Vivyo hivyo wakati mwingine tunaweza kusingiziwa kesi au madeni ambayo si halali kwetu kuyalipa…usining’unike katika hali kama hiyo..umejaribu kuonyesha kwamba sio halali lakini hueleweki usianze kunung’unika na kulalamika mpaka kuonekana sasa huna imani na maana..mpaka watu wakaanza kushangaa kama kweli wewe ni mkristo au la!..kwa matusi hayo na manung’uniko hayo..

Wewe unachopaswa kukifanya nenda katafute namna ya kulipa deni lile au kuikabili kesi ile, hata kulipa kile chote wanachokushitaki..na huko huko njiani Mungu atakufanyia muujiza wa kuilipa ile na utapata cha ziada.

Hizo zilikuwa ni kanuni za Bwana wakati wote, nasi tupate kitu kidogo cha kujifunza hapo..

Luka 6: 29 “Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang’anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.

30 Mpe kila akuombaye, na akunyang’anyaye vitu vyako, usitake akurudishie”.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

MOJA YA HIZI SIKU TUTAONA MABADILIKO MAKUBWA SANA.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUMBUKA, VIVUKO VYA YORDANI VINAKUNGOJA MBELENI.

Ni jambo la kawaida, kuona tabia za watu zinabadilika hususani pale wanapoona wanakaribia kwenda kuangamizwa wote,..Utaona wengi wao wanajigeuza na kujifanya kama vile wao ni kama wale wengine, ili wafanikiwe kijipenyeza kisirisiri katikati yao wasalimishe roho zao..

Hiyo ilitokea wakati wa kipindi cha Esta, pale ambapo maadui wa Wayahudi walipokusudia kuwaua wayahudi wote kwa kibali cha mfalme Ahasuero, lakini kibao kilipowageukia na kuona mfalme ndio amewapa heshima mara dufu,na ziadi ya yote amewapa mamlaka ya kuwatafuta wale maadui zao wawaue, biblia inatuambia jamii kubwa ya watu wakajigeuza na wenyewe kujifanya ni wayahudi ..

Esta 8:16 “Ikawa nuru na furaha na shangwe na heshima kwa Wayahudi.

17 Na katika kila jimbo, na kila mji, po pote palipowasili amri ya mfalme na mbiu yake, Wayahudi wakapata furaha na shangwe, karamu na sikukuu. Hata wengi wa watu wa nchi wakajifanya Wayahudi, kwa kuwa hofu ya Wayahudi imewaangukia”.

Unaona hapo?..

Tunasoma tena habari nyingine, kuna wakati jamii mbili za wana wa Israeli zilipigana, ambazo ni Ni jamii ya watu wa Efraimu, na watu wa Gileadi… Sababu ya vita yenyewe ilikuwa ni wale watu wa Gileadi walikwenda kupigana na maadui zao, bila kuwashirikisha watu wa Efraimu kwenda kuwasaidia, hivyo watu wa Efraimu wakakasirika kuona uamuzi ule waliouchukua ndugu zao hivyo wakapanga vita wawapige na Wagileadi, Lakini mambo yalikuwa ni tofuati, kinyume chake wao ndio waliopigwa..

Sasa baada ya kuona wanazidiwa na hali ndio inakuwa mbaya, ikawabidi, watoroke watu wengi, wajaribu kuvuka kujichanganya na jamii ya wagileadi. Sasa ilikuwa ili kufika ng’ambo ni sharti uvuke mto wa Yordani..Lakini wao walidhani ni rahisi rahisi tu kama siku zote, unavuka tu na kuingia bila kuulizwa chochote..wengine wakadhani hata wakiulizwa wewe ni nani, je ni mwenyeji wa huku watasema tu ndio, halafu basi wataruhusiwa kuvuka..

Hawakujua kuwa wale wagileadi walipata taarifa juu ya njama zao, Hivyo walichokifanya ni kwenda kusimama pale kwenye vivuko vya Yordani, pale mpakani, na watu wote, waliochanganyikana nao walipofika wavuke wasijue kuwa huyu ni nani na huyu ni nani, walitumia njama moja ya kuwakamata waefraimu katikati ya wagileadi, waliwaambia watamke Neno “shibolethi” tusome..

Waamuzi 12:5 “Nao Wagileadi wakavishika vivuko vya Yordani kinyume cha hao Waefraimu; kisha ilikuwa, hapo watoro waliotoroka Efraimu mmojawapo aliposema Niache nivuke, hao watu wa Gileadi wakamwambia, Je! Wewe u Mwefraimu? Kwamba alisema, La;

6 ndipo wakamwambia, Haya, tamka sasa neno hili, Shibolethi; naye akasema, Sibolethi; kwa maana hakuweza kufanya midomo yake kutamka neno hilo sawasawa; ndipo wakamshika, na kumwua hapo penye vivuko vya Yordani; basi wakaanguka wakati huo watu arobaini na mbili elfu wa Efraimu”.

Unaona, walitumia kigezo cha Lugha, kuwashika, vinginevyo wasingewatambua kwa namna yoyote, kwasababu walijua lugha ya asili ni kitu kinachoshikamana na mtu kuliko kitu kingine chochote, walijua lugha ya asili inaweza kweli kuigwa lakini haiwezi kuigwa kwa ufasaha wake wote, haijalishi mgeni atajifunza kwa miaka mingapi, ile lugha ambayo hajazaliwa nayo hawezi kuiiga kwa ufasaha wote..Hata leo hii mzungu aishi uswahilini hata miaka 50 na akakijua Kiswahili chote, bado kuna vimelea vya lugha hatoweza kuvitamka ipasavyo kama Yule mzawa..

Sasa Biblia inatuambia agano la kale ni kivule cha mambo yatakayotokea katika kipindi cha agano jipya..Na habari hizo hazijaandikwa ili kutusisimua tu, hapana bali zina ujumbe mkubwa sana kwetu katika roho.

Inamaana kuwa utafika wakati mambo ya wokovu hayatakuwa kama yalivyo leo hii, kuna wakati wale waovu watatamani sana kwa nguvu kujiingiza katika ufalme, watajigueza kwa kila namna ili tu wapate nafasi, lakini safari hii, haitakuwa ni kwa njia rahisi kwa wanavyodhani, bali watakuwa na mtihani mkubwa wa kufanya..

Luka 16:16 “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.

Utapimwa wokovu wako, sio kwa kusema tu mimi nimeokoka, mimi nilibatizwa, mimi ninakwenda kanisani bali vitazingatiwa vigezo vya ndani zaidi, utaulizwa je! Huo wokovu unauzoefu nao kiasi gani, Je, ni wa kujifunza tu, au ulikuwa ni sehemu ya maisha yako tangu zamani..

Hili ndio lile kundi ambalo Bwana alilitolea mfano wake, wa mtu Yule aliyekutwa ndani ya harusi lakini hana vazi la harusi mpaka watu wakawa wanashangaa ameingiaje ingiaje mule ndani na wakati hana vazi la harusi..Kumbuka wakati huu kule nje kulikuwa kunaendelea machinjo.. Akatoroka akaingia ndani, lakini alionekana kwasababu hakuwa na vazi (hakuwa na kadi ya mwaliko tangu zamani) Kilichofuata ni kwamba alikamatwa na kufungwa na kwenda kutupwa nje..

Ndipo Bwana akamalizia kwa kusema maneno haya.. “Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache”. Soma (Mathayo 22:1-14)

Hivyo ndugu anza kuujenga uhusiano wako na Mungu kuanzia sasa, usisubiri wakati Fulani, kubali kuzaliwa mara ya pili leo uikulie wokovu ujifunze lugha ya kimbinguni, kama bado hujaokoka.. kwasababu unafika wakati hapo mbele hakutakuwa tena na mlango wa neema ya yule atakayetaka kuingia.. kwa maana hizi ni nyakati za mwisho jambo ambalo hakuna mtu asiyelijua hilo.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

 

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Rudi Nyumbani:

Print this post

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

Tunapotenda Mema ni kwa faida yetu na si ya Mungu..kadhalika tunapofanya maovu ni kwa hasara yetu sisi na si hasara ya Mungu. Kwa mfano mtu anayezini biblia inasema anatenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe anafanya jambo litakalomwangamiza yeye mwenyewe.. maana yake anakuwa hana tofauti na mtu anayejiua…

Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.33 Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika”

Kadhalika mtu anayeiba au anayeua, HAMKOMOI MUNGU..bali anafanya jambo ambalo litawaumiza wanadamu wenzake na hali kadhalika litakalomwaribu yeye mwenyewe baadaye. Na dhambi nyingine zote ni hivyo hivyo…zina madhara kwetu na si kwa Mungu…Vivyo hivyo tunapotenda mema, mema hayo tunapoyafanya si kwa faida ya Mungu bali kwa faida yetu sisi wenyewe..Bwana anapotuasa na kututaka tutende mema si kwaajili yake yeye, bali kwaajili yetu sisi..ni sawa na mtu anayekizuia kisu katika shingo ya mtu anayetaka kujiua..Ndivyo anavyofanya kwetu pale anapotuzuia tusifanye dhambi..ni kwa faida yetu si yake…endapo akituacha tu basi tutajimaliza na hakuna kitakachosalia…

Kwamfano Biblia inasema wapeni watu vitu nanyi mtapewa…(Luka 6:38) kipimo cha kujaa, na kushindiliwa hata kusukwa sukwa ndivyo watu watakavyowapa vifuani mwenu…kwamaana kipimo kile tupimacho ndicho tutakachopimiwa…Maana yake ni kwamba sio kwamba Mungu anatupa sheria ngumu ili yeye ajifurahishe moyo wake anapotuona tunamtii..hapana anafanya vile ili sisi tupate faida..yeye hatumwongezei chochote kwa wema wetu tunaoufanya…

Hivyo ukitenda mema na kuwapa watu vitu na wewe utapewa vitu siku moja kwa kiwango kile kile ulichowapa wengine…Kwahiyo mema ni kwa faida yetu sisi na si ya Mungu.

Kwahiyo Biblia inapotuonya tusizini, au tusifanye uasherati, au tusiibe, au tusiue, au tuwaheshimu wazazi wetu n.k ni kwafaida yetu ili tupate mema katika ulimwengu huu na ule unayokuja..Na si kwa sababu Mungu anapenda kutuangalia kama kwenye Tv huku duniani tukitenda mema, kwamba ndio chakula chake yeye..Ukifikiri/tukifikiri hivyo..tutakuwa bado hatujamwelewa huyu Mungu tunayemwabudu…

Soma maandiko haya:

Ayubu 35: 5 “Ziangalie mbingu ukaone; Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe.

6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?

7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?

8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu”.

Umeona? Unapovaa vimini na suruali na kuonywa usivae kikahaba ni kwa faida yako mwanamke….Unapoua kwa kutoa mimba ni kwa hasara yako wewe na yule uliyemuua, …Unapojiongezea maasi juu ya maasi na dhambi juu ya dhambi, humpunguzii kitu Mungu kwasababu yeye haishi kwa dhambi zetu wala kwa haki yetu…Hivyo dhambi zako unazojiongezea juu kila siku ni sawa unasikia njaa na kukata kiungo chako kimoja kimoja kila siku ili ukile upunguze njaa..(hapo unajimaliza mwenyewe).

Unasikia mahubiri kila kona, ni kwasababu Mungu anakupenda na anataka upate faida wewe na si yeye..anataka usipate hasara wewe na si yeye..

Hili neno “hizi ni siku za mwisho” pengine umeshalisikia sasa hii ni mara ya elfu, na limeshakuchosha…lakini kipindi si kirefu hutalisikia tena kwasababu siku zenyewe zitakuwa zimeshatimia…Kristo atachukua walio wake na kila mtu atavuna alichokipanda akiwa hapa duniani. Na watakatifu watanyakuliwa..na dhiki kuu itaanza na siku ya Bwana itashuka ulimwenguni, wakati huo disko unazohudhuria sasa hazitakuwepo tena, bar unazokwenda kulewea hazitakuwepo tena, madili haramu na rushwa unazokula sasa hazitakuwepo tena…viwanda vinavyotengeneza mavazi yako ya kikahaba havitakuwepo tena, hakutakuwa na kurudi nyumbani kulala kutandani, wala kuangalia tv, wala kuingia internet..siku hizo zitahitimisha mambo hayo yote..Na baada ya hayo ziwa la moto litafunguliwa shetani na malaika zake watatupwa kwanza kwa maana lilitengenezwa kwaajili yao.

Kisha wote walio nje ya Kristo watafuata. Walio nje ya Kristo sio wale unaowategemea kwamba ni watu wa dini fulani..bali hata wewe uliye vuguvugu umbaye mguu mmoja upo nje mwingine ndani…ambaye ni mlevi lakini bado una jina la kikristo, ni mwasherani na mtembeaji uchi barabarani lakini bado unasali..wewe ndio mfano wa watakaoachwa wakati huo, na hiyo ni kulingana na maandiko na si mapokeo au mafundisho ya mtu binafsi aliyejiamulia tu kuzungumza.

Siku ya kunyakuliwa leo imekaribia sana kuliko jana na juzi…mwaka huu tumeukaribia unyakuo sana kuliko miaka ya nyuma..Hivyo huu ndio wakati wa kuongeza umakini wetu kuliko vipindi vya nyuma.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UFANYE NINI KAMA MKRISTO WAKATI HUU WA JANGA LA CORONA?

Watu baadhi kutoka nchi mbalimbali wamenitumia ujumbe wanasema, mtumishi huku kwetu hali sio nzuri hatuwezi kwenda kanisani kama tulivyozoea, hatuwezi kufanya chochote isipokuwa tu ni kukaa nyumbani, na wala hakuna dalali ya jambo hilo kuisha hivi karibuni…Tufanye nini?

Shalom, ndugu,

Ipo Habari moja katika biblia tunapaswa tujue na  tujifunze kama wakristo katika wakati huu ambao dunia ipo katika taharuki kubwa, Tukisoma kitabu cha matendo ya Mitume, kuna wakati ambapo mitume wa Bwana walipitia kipindi fulani cha ukimya mkubwa sana, jambo ambalo liliwapasa wasifanye kitu kingine Zaidi ya kwenda kujifungia gorofani. Kwanini walilazimika kuwa vile, ni kwasababu ni kipindi ambacho, Sio  YESU tu peke yake ambaye walizoea kumwona na kutembea naye kila siku hakuwa nao, bali pia Roho Mtakatifu ambaye walisikia habari zake alikuwa bado hajashuka juu yao.. walikuwa katikati ya pengo, kama vile mayatima fulani..

Kitu pekee kilichowafanya wawezi kukivuka hicho kipindi kifupi cha ukimya, ilikuwa ni ile AHADI TU, waliopewa na Bwana Yesu siku ile aliyokuwa anapaa..

Hiyo ndio iliyokuwa salama yao kwa wakati huo waliokuwa wanapitia..Kumbuka hawakujua ahadi hiyo itatimia lini, lakini maaadamu wana Neno la Ahadi, basi hiyo iliwafanya wapate nguvu siku baada ya siku, wavumilie hicho kipindi cha mpito mbele yao wakitumai kuwa siku si nyingi itatimia, na AHADI yenyewe ilikuwa ni kungojea YERUSALEMU, mpaka wakatakapopokea kipawa cha Roho Mtakatifu..Basi.

Matendo 1:3 “wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.

4  Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu;

5  ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache”.

Hivyo baada ya ile siku ya 40, hawakumwona, wala hawakusikia chochote, wala hawakuoona uwepo wowote, wala hawakuwa na shughuli nyingine yoyote ya kuhubiri, au kushuhudia kama pale mwanzo, au kuzunguka huku na huko kuhubiri..Bali iliwagharimu kwenda kukaa tu sehemu moja..na zaidi ya yote biblia inasema nje kulikuwa na hofu ya wayahudi.

Lakini biblia inatuonyesha ahadi hiyo haikuchelewa, bali ndani ya siku 10 mbeleni ilitimia, ambayo ndio iliyokuwa siku ya Pentekoste, Roho Mtakatifu aliwashukia mitume wake kwa nguvu ya ajabu, na hapo ndipo Mungu akaleta uamsho mwingine tena ambao uliitikisa dunia nzima katika historia..

Sasa swali ni Je ndani ya kipindi kile cha mpito ambacho hakukuwa na sapoti yoyote ya kimbinguni mitume walikuwa wanafanya nini ndani, Je! walikuwa wamelala tu au wameacha wakovu wao sasa wafikirie mambo yao ya kale, au walikuwa wamekaa wanapiga tu story na kuzungumzia Maisha ya wengine, au wanaangalia movie, au wanachat whatasapp kila wakati au wanacheza magemu, au wanafanya nini??

Embu Tusome..

Matendo 1:10  “Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,

11  wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.

12  Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.

13  Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.

14  Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja KATIKA KUSALI, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake”.

Unaona, biblia inasema hapo walikuwa WAKIDUMU KWA MOYO MMOJA KATIKA KUSALI,..

Ndugu, wakati huu wa LOCKDOWN, na kuwa karantini kutokana na janga la Corona, nchi yoyote uliyopo. Wakati huu Wa kuzuiwa kufanya ibada, au kuzunguka huku na huko, wa kuzuiwa kwenda mtaani kuhubiri kama ulivyokuwa unafanya  hapo mwanzoni, wa kuzuiwa kuitishi mikutano ya injili, wa kuzuiwa kwenda kumwabudu Mungu kanisani, kwenda kwenye masomo ya biblia, kila baada ya siku mbili, sio wakati wako wa wewe kuwa na kisingizio cha kuacha kumtafuta Mungu, na kurudi nyuma kwenye ulimwengu ulipokuwepo, wa kurudi kuanza sasa kutokusoma biblia yako,..bali huu ndio unapaswa uufanye muda wakati wako wa kudumu katika KUSALI kwa bidii ukiingalia ahadi ya Mungu iliyo mbele yako, kwamba hivi karibuni atakwenda tena kutuachilia, lakini hatatuachilia hivi hivi, bali atatuachilia na UAMSHO MKUBWA WA ROHO ambao haujawahi kutokea..kama ilivyokuwa katika kipindi cha Pentekoste.

Hivyo huu sio wakati wa kuzimia mioyo,  wala sio wakati wa kuogopa maadamu tupo ndani ya Kristo, badala yake ndio tuongeze kutazama juu, tukiziangalia Ahadi za Bwana ndani ya kipindi hichi cha mpito, tukiongeza viwango vyetu vya kujisomea biblia nyumbani, na kusali sana tena Zaidi ya pale tulipokuwa mwanzoni, ikiwezekana kufunga, na kila wakati kumtafakari Mungu kweli kweli..

Sisi hatujapitia kipindi cha kuachwa na mbinguni kwa Muda kwa ilivyokuwa kwa mitume, lakini wao hawakuiacha Imani, badala yake walidumu katika kusali tena walipanda OROFANI, juu kabisa mahali ambapo hapana  usumbufu wa watu kuingia na kutoka, ili wamtuafakari Mungu vizuri na kusali..

Vivyo hivyo huu ni wakati wa wewe, kupanda OROFANI (mahali penye utulivu), Umtafute Mungu peke yako, kwasababu UAMSHO MKUU SANA, Unakwenda kuzuka duniani kote hivi karibuni. Kipindi cha nyuma pengine ulikuwa na visingizio vya kutokusali, kwamba upo bize kutafuta riziki na shughuli leo hii mazingira yanakulazimisha kukaa nyumbani, na tena kuna agizo limetolewa la kuomba, hivyo isiwe sababu ya wewe kuhukumiwa siku ile kwa kutokuomba sasahivi…Unayo sababu inayoeleweka kidunia ya wewe kutozurura zurura mtaani, basi kaa nyumbani kuomba…utajitetea vipi siku ile??..Utasema ulikosa muda? Utasema serikali ilikuzuia kuomba? Leo hii imekutangazia wewe kuomba?.. Utasema sikuomba kwasababu mazingira yalikuwa hayaruhusu?..jibu unalo.

Hivyo nakutia moyo wewe mkristo ambaye umeathiriwa na hali hii ya sasa duniani, Fahamu kuwa ni kipindi kifupi tu cha Siku 10 rohoni kinapita ambacho ni Mungu mwenyewe kakiruhusu..hivyo kuwa na akili, kujua nyakati na majira, ongeza viwango vyako vya utakatifu kama vile hukuwahi kuishi hivyo hapo kabla, ni wakati wa kutubu (kutubu maana yake ni kuacha yale uliyokuwa unayafanya yasiyo mpendeza Mungu) ili hiyo  PENTEKOSTE itakapokuja kwa watu wa Mungu duniani, uwe na wewe ni mmojawapo..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia na kujikumbusha mambo yale yale ambayo tumekwisha kujifunza huko nyuma kupitia sehemu mbalimbali..

Wengi wanajiuliza je ubatizo ni wa muhimu?..Jibu ni NDIO ni wa muhimu sana na si kidogo. Shetani hapendi wengi wajue siri iliyopo katika ubatizo sahihi kwasababu anajua madhara yake.

Wakati wana wa Israeli wanatoka Misri, Farao bado alikuwa anawafuatilia fuatilia..lakini walipovuka tu bahari ya shamu na majeshi ya Farao yote kuzama kwenye ile bahari ya shamu ndio ikawa mwisho wa Farao na majeshi yake kuwafuatilia wana wa Israeli.

Kutoka 14:26 “Bwana akamwambia Musa, Nyosha mkono wako juu ya bahari, ili maji yarudi tena juu ya Wamisri, juu ya magari yao, na juu ya farasi zao.

27 Musa akaunyosha mkono wake juu ya bahari, na kulipopambazuka, bahari ikarudi kwa nguvu zake; Wamisri wakakimbia mbele yake; na Bwana akawakukutia mbali hao Wamisri kati ya bahari.

28 Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja.

29 Lakini wana wa Israeli wakaenda katika nchi kavu katikati ya bahari; na hayo maji yalikuwa ni kuta upande wao wa kuume, na upande wao wa kushoto.

30 Ndivyo Bwana alivyowaokoa Israeli siku ile mikononi mwa Wamisri; Waisraeli wakawaona Wamisri ufuoni kwa bahari, wamekufa”.

Sasa siri ilikuwa ni nini mpaka Mwisho wa Farao ukawa kwenye hiyo bahari ya Shamu?..Jibu ni rahisi: Ni huo ubatizo wana wa Israeli waliobatizwa kwa kupita katikati ya bahari hiyo.

Utauliza je!..ina maana wana wa Israeli walibatizwa katika bahari ya Shamu?..Jibu ni ndio!..

1Wakorintho 10:1 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;

2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;”

Unaona hapo?..kitendo cha Wana wa Israeli kupitishwa katika yale maji ya Shamu, pasipo kupatikana na madhara ndiko kunakofananishwa na ubatizo. Hivyo ule ubatizo ndio uliohitimisha kazi ya shetani na majeshi yake kuwafuatilia, haijalishi kuwa tayari walishapewa ruhusu huko nyuma ya kuondoka.

Hali kadhalika, ubatizo sahihi wa maji mengi sasa unafanya kazi hiyo hiyo. Unapoingia katika yale maji na kubatizwa katika jina la Yesu na kutoka katika yale maji…wewe utatoka salama ukiwa na furaha, na amani lakini nyuma yako yale majeshi ya mapepo wabaya yaliyokuwa yanakufuatia yanakufa na maji huko nyuma.

Hivyo maji ni ishara ya wokovu kwako na maangamizi kwa shetani na majeshi yake. Ndio maana Bwana Yesu alisema katika Roho kwamba pepo amtokapo mtu hupitia mahali pasipo maji(maana yake mahali ambapo hapana maji) ili apumzike na akirudi na kukuta nyumba yake imefagiliwa anakwenda kuwachukua pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye, na hali ya mwisho ya Yule mtu inakuwa mbaya kuliko ya kwanza.

Maana yake ni kwamba pepo likimtoka mtu na Yule mtu kama hatachukua uamuzi wa kuukamilisha wokovu wake ikiwemo kubatizwa ubatizo sahihi wa kuzama mwili mzima kulingana na maandiko na kudumu katika usafi..Mtu huyo yupo hatarini kurudiwa na zile zile nguvu za giza zilizomwacha hapo kwanza. Hivyo ubatizo sahihi ni wa muhimu sana…Na ubatizo sio dini mpya bali ni maagizo ya  Bwana wetu Yesu…na kwa faida yetu kama ilivyokuwa kwa faida kwa wana wa Israeli wakati wanatoka Misri, kama sio yale maji Farao angeendelea kuwafuatilia daima.

Shetani na mapepo yake yataendelea kumfuata Yule mtu ambaye hajakamilisha wokovu wake…Na Bwana alishatuambia katika Neno lake, kwamba “aaminiye na kubatizwa ataokoka”..maana yake mambo hayo mawili yanakwenda pamoja, hayaachani, vinginevyo ni ngumu sana kuokoka na mkono wa Adui.

Kama unakumbuka kile kisa cha Yule mtu aliyekuwa na mapepo yaliyojitambulisha kama JESHI. Mtu Yule aliingiwa na mapepo, na mapepo yale yalipomtoka yaliwaingia nguruwe…Jinsi wale Nguruwe walivyokwenda kuangamia majini ni mfano wa Farao na majeshi yake yalivyozama majini…Kwahiyo unaweza kuona kuna uhusiano mkubwa sana wa maji na majeshi ya Adui. Hivyo ubatizo ni wa muhimu sana. Pale tu mtu anapoamini na kutubu anapaswa akabatizwe bila kuchelewa…

Itakuwa ni jambo la kushangaza, mtu utasema umeokoka, halafu miezi inapita, miaka inapita, bado hujabatizwa, unaishi kwa kanuni ipi ya wokovu?

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM

Rudi Nyumbani:

Print this post

MALAIKA WAPELELEZI WA HUKUMU WANAPITA SASA.

Kabla Mungu hajaleta maangamizi katika dunia, huwa anawatuma kwanza malaika zake wapelelezi kwenda kuhakiki hicho kilichomfikia kuwa ni kweli au La, na ikithibitika kuwa ni kweli basi hatua inayofuata saa hiyo hiyo  ni wale malaika kutekeleza hukumu ya Mungu juu ya watu hao au Mji huo. Kwananini anawaagiza malaika hawa kwanza kupeleleza, je ni kwasababu yeye mwenyewe hajui kiwango cha maasi na haki yaliyomo ulimwenguni?..jibu ni hapana!..anajua kila kitu pasipo hata kutegemea malaika zake, wala mwanadamu..lakini anafanya hivyo ili pawepo na mashahidi ya kile kinachoendelea…Kama biblia inavyosema “Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa.(2Wakorintho 13:1)”

Ndicho kilichotokea kipindi kifupi kabla ya miji ya Sodoma na Gomora kuangamizwa. Mungu aliwatuma malaika zake wawili, kwenda kuipeleleza miji ile, na kama tunavyoifahamu habari, malaika wale walipofika jioni ile, wakakutana na Lutu, Lutu naye akawalazimisha kuingia nyumbani kwake, mwanzoni walikataa, lakini baadaye wakafika, na walipofika tu kumbe huku nyuma, walikuwepo pia wapelelezi wengine wanawafuatilia malaika wale, na hao si wengine zaidi ya watu wa miji ile..

Hivyo sio malaika tu waliokuwa wanapeleleza, na wao pia walikuwa wanapelelezwa, jambo ambalo linaendelea sasa katika roho..

Sasa walipoona hatma yao ni wapi, kuwa ni ile nyumba ya Lutu, hawakufanya chochote, bali walisubiri mpaka usiku ulipoingia  ndipo wakakusanyika wote wakaizingira ile nyumba ya Lutu na kumwambia Lutu, awatoe hao watu  ili wapate kulala nao..Embu fikiria hali yao ilivyokuwa mbaya..Sasa kama ukichunguza pale utaona, wale malaika hawakuchukua hatua yoyote kwanza, ni kama walikuwa wanawasikiliza walichokuwa wanamueleza Lutu pale nje, na mashindano yao pale mlangoni..Na baadaye ilipoonekana Lutu anashindwa, wakawa wanakaribia kuuvunja mlango, ndipo wakanyanyuka wakamvuta Lutu ndani, kisha wakawapiga upofu wale watu waliokuwepo pale mlangoni..

Hiyo ilisababisha ripoti yao ya upelelezi iwe imekamilika, kwamba Sodoma kumeoza na wao ni mashahidi, kilichobakia kwao ni kumuhimiza Lutu kwa haraka aondoke Sodoma kwa sababu miji ile wanakwenda kuiteketeza. (Soma Mwanzo 19 yote)

Ndugu yangu, dalili kubwa inayotutambulisha kuwa tunaishi katika wakati wa upelelezi wa malaika hawa, Sio kuzuka kwa vitendo vya Ushoga na usagaji tu peke yake, hapana, kwani hivyo vilikuwepo tangu zamani..lakini ni kuzuka kwa vitendo vya Ushoga na Usagaji katika nyumba ya Mungu…Tunavyoona leo hii ushoga unafungishwa katika nyumba ya Mungu, basi tujue hiyo ni dalili mbaya, ni sawa na kutaka kuzini na malaika wa Mungu walio katika kanisa lake..

Malaika hao wameshapita na wameshaona kile ambacho kilitokea wakati wa sodoma na Gomora ndicho kinachotokea na sasa hivi, hivyo wanachokifanya sasa ni kuwapiga watu upofu kwa kasi sana, ili wasione mlango wa neema tena ambao wenyewe wanauvunjia heshima, na kinachobakia kwa watu hao  ni maangamizi tu..

Unapojiona wewe ni mtazamaji wa Pornography, ujue kuwa wewe ni kundi moja na hawa wanaoufanya  ushoga nyumbani mwa Mungu, isipokuwa wewe tu ni mfuasi wa nyuma, lakini adhabu yenu ni moja,,..na hivi sasa unapigwa upofu, ambao hutakaa uuone mlango wa neema kamwe kama hutatubu. Ukiona unazini, na kwako wewe zinaa ni kama kitu cha kawaida na huku unajiita ni mkristo bado, ujue upofu unaendelea sasahivi duniani, ukiona unajihusisha na mambo yote ya kizinzi (iwe ni kujichua, au ulawiti) ujue upo katika kundi hilo la kupigwa upofu na malaika hawa wapelelezi wa Bwana.

Wanapopita na kuangalia makundi mengi ya watu, leo hii yapo kwenye simu zao mikononi, kutwa kuchwa ku-download video za pornography na kutazama video hizo, na miziki ya kidunia..ujue kuwa hao watu wanapigwa upofu, na malaika hao waliotumwa na Mungu kuipepeleza dunia, kabla ya kwenda kuangamizwa dunia hii kwa moto siku hizi za mwisho.

Wakati huu ni wakati wa hatari nyingi, ikimbie dhambi, unaweza kuona inavutia leo machoni pako, na ndivyo ilivyo dhambi siku zote ni ya kuvutia lakini mwisho wake ni majuto ya milele. Mungu tayari ameshakikasirikia kizazi hiki, kinachoichezea madhabahu yake mpaka kufikia hatua ya kufanya mambo ya ajabu kama hayo madhabahuni pake..Utasema ni hao sio mimi, kumbuka kile kikundi kichache kilichokuwa kinacheza mlangoni mwa Lutu ndicho kilichouwashia moto mji mzima wa Sodoma na Gomora..ikasababisha hata wengine walio mbali wasiojua chochote ambao wanafanya mambo kama hayo mwisho wao kufika. Kwahiyo uovu unapoendelea katika nyumba ya Mungu ni jambo la kuomboleza kwa wote.

Hivyo na sisi Bwana atusaidie tusiwe wamoja wapo, bali tuchukue hatua ya kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kabisa kumgeukia yeye, katika huu wakati mfupi wa kumalizia kabla ya unyakuo kupita. Kwasababu tusidhani kuwa yaliyowakuta wale, hawayawezi kutukuta na sisi.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

USINIPITE MWOKOZI

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

JIRANI YANGU NI NANI?

Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA?.Mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?

DANIELI: Mlango wa 8

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mtume Paulo alimwabudu malaika aliyetembea naye?

SWALI: Je! Mtume Paulo alikuwa anamwabudu malaika wake aliyekuwa anatembea naye kama tunavyosoma katika Matendo 27:23?

JIBU: Tuusome huo mstari..

Matendo 27:23 “Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,”

Mstari huu ukisomwa kwa haraka haraka ni rahisi kutafsiri kwamba Mtume Paulo alimaanisha kusema kwamba anamwabudu Malaika wake..Lakini ukiurudia tena taratibu utaona kwamba hapo Mtume Paulo hakumaanisha kuwa anamwabudu Malaika bali ni Mungu..

Sasa tunaweza kuiweka vizuri sentensi hiyo kama ifuatavyo; “Kwa maana usiku wa leo Malaika wa Mungu alinijia”…..sasa swali ni Mungu yupi?…ndio anaendelea kusema…Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye…

Hivyo ukirudia kusoma kwa namna hiyo huo mstari utapata tafsiri kamili.

Hivyo Pamoja na hayo tunazidi kujifunza kwamba tunapaswa kuzidi kuyachunguza maandiko, ili tupate kulielewa Neno la Mungu kama yeye Mungu wetu anavyotaka tulielewe..kwasababu ipo mistari mingi na Habari nyingi katika maandiko matakatifu ambazo wakati mwingine ni ngumu kuzielewa lakini tunapokaa chini na kutaka kumwuliza Roho Mtakatifu yeye ni mwaminifu na atatufulia, kwasababu tusipopata tafsiri kamili kwa msaada wa Roho Mtakatifu shetani anaweza kuitumia mistari hiyo hiyo kutukosesha na kutuhalalisha uovu wake…kama alivyoitumia baadhi ya mistari kuwadanganya watu kuhalalisha ulevi, zinaa, ndoa za mitara na hata ameshautumia mstari huu kwa baadhi ya watu kuhalalisha ibada za kuabudu malaika na ibada za sanamu.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

Kwanini Musa alipewa mbao mbili za mawe na sio moja au zaidi

Rudi Nyumbani:

Print this post

BASI, JIANGALIENI MIOYO YENU ISIJE IKALEMEWA NA ULAFI, NA ULEVI.

Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;

35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima”

Shalom, Jina kuu la mwokozi wetu Yesu libarikiwe daima.

Wengi tunayafahamu maneno hayo ya Bwana, lakini hatujui ni ulevi na ulafi wa namna gani unaozungumziwa katika Habari hiyo mpaka siku hiyo iwajilie ghafla, kama mtego unasavyo..

Ili kupata picha embu tutazame mfano mmoja halisi kabisa wa kwenye biblia na jinsi walivyolemewa na ulafi na ulevi wa kipekee mpaka, mwisho wao ulipowakuta kwa ghafla..

Sasa kama tukisoma kile kitabu cha Danieli sura ya 5, tunamwona mfalme mmoja aliyejulikana kwa jina la Belshaza, huyu alikuwa ni mtoto wa Nebukadreza, kama wengi tunavyoifahamu Habari, ni mtu ambaye alibahatika kuona mambo yote ambayo Baba yake aliyoyapita na jinsi alivyoadhibiwa kutokana kiburi chake na ukatili wa kutesa watu wasiokuwa na hatia na wengine kuwatupa katika matanuru ya moto, kama sio kuwachinja, lakini baadaye Mungu alikikomesha kiburi chake, kwa kumng’oa katika ufalme wake, akawa anaishi misituni kama sokwe Fulani tu, mpaka miaka 7 ilipoisha, na pale alipogundua kuwa Mungu ndiye anayetawala dunia nzima, na kwamba yeye ndio anatakiwa aogopwe ndipo akatubu na kumgeukia Mungu na Mungu akamrehemu na akamrejeshea enzi yake kupita kiasi hata kuliko pale alipokuwepo mwanzo.

Sasa huyu mtoto wake aliyeitwa Belshaza, alikuwa anayaona hayo yote, na alikuwa ameshapata somo kamili ambalo haikumpasa yeye tena alipitie kwasababu babayake tayari ameshafanyika mfano..Kama tu vile sisi, watu wa kizazi hiki, tayari mifano mingi ilishatangulia mbele yetu huko nyuma, mfano ile ya watu wa Nuhu, na Watu wa sodoma na Gomora, jinsi walivyoangamizwa kwa maovu yao, lakini sasa tunaona na kuzipuuzia, na kuzichukulia tu kama Habari zilizopitwa na wakati kama tu huyu mtoto wa Nebukadreza.

Yeye alipuuzia yale yote ambayo Baba yake aliyotendewa na Mungu.. Na kibaya Zaidi akaamua kuchukua hatua nyingine mbaya kuliko zote, ambayo ndiyo iliyompelekea hata Mungu kumwangamiza kwa ghafla na kwa haraka sana..Na hicho ndicho wote tunachopaswa tujifunze leo hii.

Alichofanya ni kuchukua vile vyombo vya hekaluni, ambavyo baba yake alivichukua kutoka Yerusalemu, alipouteketeza mji na hekalu, na kuvihifadhi asivitumie kwa kitu chochote kwasababu vilikuwa ni vitakatifu, lakini yeye (huyu Belshaza), akawa mlevi, na mlafi wa kupindukia, akawa anafanya karamu, akaona kuwa haitoshi kunywea vyombo vyake mwenyewe, chupa zake za vilabu vyake, na kutumia visu vyake vya kifalme kuchinjia nyama zake, na hata sahani zake akaona hazitoshi kuzitumia kuwekea vyakula vyake haramu…

hivyo akaenda kwenye hazina ya baba yake, na kupekua pekua na kuvikuta vile vyombo vya hekaluni ambavyo vilikuwa vimefunga na kuhifadhiwa visitumike, yeye akavichukua vile vyombo vitakatifu vya Mungu, akaanza kuvinywea na kuvilia yeye Pamoja na wakuu wake, na makahaba wake..Unaweza kuona Ni uvunjifu wa heshima kiasi gani.?? Hayo ndio mambo yanayoendelea katika roho sasa hivi..

Na alipomaliza kufanya vile tu, saa hiyo hiyo kiganja cha mkono kikatokea, kikasogea mpaka ukutani mahali ambapo mwanga ulikuwa unapiga, akaona kikiandika maneno yale, MENE, MENE, TEKELI NA PERESI.. Kama tunavyoijua habari maneno yale yalikuwa ni Hukumu, kwamba mwisho wake umeshafika, ufalme wake ndio umeishia pale..

Sasa huyu Belshaza, utaona tena aliposikia vile badala atubu, ndio kwanza anafikiria kumpandisha Danieli cheo, na kumfanya awe mkuu, unajua ni kwanini?.. Ni kwasababu alidhani, jambo hilo haliwezekani kutokea kwake, na hata kama likiwezekana basi litakuwa ni jambo la baadaye sana, kwasababu mji wake wote ameshauzungushiwa kuta kubwa sana pande zote, ambazo juu yake wapo walinzi wamekaa wakiangalia malango yake usiku na mchana yenye askari waliobebea wenye sifa dunia nzima, (kwasababu kipindi hicho Babeli ndio iliyokuwa inatawala dunia nzima)..

Hivyo Habari hizo za Danieli hazikumwogopesha hata kidogo, akiangalia kuwa hayo mataifa ambayo ameambiwa yatakuja kuuchukua ufalme wake, yaani umedi na uajemi ni vitaifa vidogo, visivyokuwa na nguvu, hivyo akawa hana hofu tena..

Lakini ndivyo alivyojidanganya..Biblia inasema usiku ule ule, alivamiwa na kuuliwa, na ufalme wake kuchukuliwa kirahisi na Wamedi na Waajemi, ni jambo la ghafla sana..utajiuliza wale watu walitokea wapi asipate Habari siku zote..

Ili kufahamu ukirudi katika historia inasema, ule mji wa Babeli ulikuwa na mto mkubwa ambao ulikuwa unaingiza maji katika mji, sasa kwa namna ya kawaida, maji yanayoingia katika mji hayawezi kuwekewa kuta, hivyo pale pale kwenye maingilio ya mto ule ndipo hapo hapo Wamedi walipokuja kuingilia usiku ule, walichokifanya ni kuupindisha ule mto mbali sana hivyo maji yakapungua ndipo walipopatia nafasi ya kuuingia mji, na kuwaua watu wale kwa ghafla sana na haraka usiku ule..wakati walinzi wa mji wanaendelea kulinda mageti makubwa kule..kumbe huku kwa njia ya chini ya watu wameshaingia mjini na kuanza kuangamiza watu.

Hata leo, Kanisa la sasa limeshalemewa na ulafi na ULEVI WA ROHONI, ni heri ungekuwa ni ulevi wa kawaida, lakini ni ulevi unaotumia vyombo vya hekaluni mwa Bwana na hiyo ndiyo inayoleta ghadhabu.. Yaani watu wanapomchanganya MUNGU NA DUNIA..leo wapo kanisani, kesho disko, leo wanamwimbia Mungu, kesho shetani, leo wanashiriki meza ya Bwana, kesho wanakwenda kuzini, yaani hayo yamekuwa mambo ya kawaida kabisa, mtu kusema ameokoka, na huku, anakunywa pombe kisirisiri, anazini nje ya ndoa, anajichua, anatazama picha za ngono ni mambo ya kawaida, anakula rushwa, ana honga..

Huo ndio ulevi na ulafi Bwana Yesu aliokuwa anauzungumzia pale..

Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;

35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima”

Moja ya hizi siku, dunia nzima itaingia katika mtego huo, wakati watu wakiwa katika vilele vya amani, katika furaha, ndipo mambo yatakapobadilika kwa ghafla. Hivyo ndugu, huu ni wakati wa kutengeneza uhusiano binafsi na Mungu..Dunia hii imeshaandikiwa MENE, MENE, TEKELI na PERESI..Ukizidi kung’ang’ania kwenda nao, mwisho wa siku itakuchukua kama ilivyomchukua Belshaza, Leo hii tubu itii injili, uokolewa, Usafishwa Maisha yako, Na Bwana atakusaidia kwa yale yaliyobakia.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

RABI, UNAKAA WAPI?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

ANGALIA USIJE UKANG’OA NGANO KATIKATI YA MAGUGU.

MUNGU AKIKUPITA LEO, HAIMAANISHI KUWA HAJAKUCHAGUA.

HATA NA BARNABA PIA AKACHUKULIWA NA UNAFIKI WAO!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

Chukua tahadhari juu ya neema ya Mungu.


Hakuna ulinzi mkubwa ambao mwanadamu anaweza kuupata kama ulinzi wa kuwa ndani ya Yesu..Kama wengi wetu tunavyojua au tulivyosikia kwamba watu wote waliompokea Yesu Kristo uhai wao unakuwa umefichwa pamoja na Kristo.(Wakolosai 3:3). Kiasi kwamba tunalindwa dhidi ya nguvu za giza na mipango yote ya Ibilisi.

Wengi wetu tunaifurahia neema hii na kutamani kuingia ndani yake lakini hatujui kuwa ikichukiliwa isivyopaswa ina madhara makubwa kuliko kitu kingine chochote tunachoweza kukijua.

Neema ya Mungu inafananishwa na nyumba ya karamu, yenye mlango…Mathayo 7:13. Sasa kama tujuavyo nyumba yoyote ile ya muhimu kama Ikulu au ukumbi wa sherehe ya muhimu sana ina mlango na vile vile ina uzio…na mara nyingi kuta zake zinakuwa zimezungushiwa uzio mwingine ambao ni wa umeme..Na kama ni nyumba yenye umuhimu mkubwa zaidi ya hayo inakuwa na walinzi wanaotembea tembea wenye silaha kuizunguka, lengo ni kuzuia watu wa wasiruke ukuta na kuingia ndani…Na ikitokea mtu akijaribu kukiuka na kuusogelea ukuta kutaka kuruka aingie ndani ndipo anaweza akajikuta kapigwa risasi au kapigwa shoti ya umeme, na hivyo hata kuweza kujisababishia kifo…Lakini ulinzi huo haujawekwa kwaajili ya kuangamiza watu, bali kulinda usalama.

Na Neema ya Mungu ni hivyo hivyo…Ipo nguvu ya ziada iwalindao wale watu walioingia ndani ya Neema ya Kristo..Nguvu hiyo ndiyo inayotulinda dhidi ya nguvu zote za giza, dhidi ya shetani na majeshi yake (mapepo na wachawi) na kila mpango mwovu wa Ibilisi..Hivyo yoyote anayejaribu kuingia kutaka kuwaharibu watu wa Mungu walio chini ya neema ya Mungu basi atakuwa anajitafutia matatizo yeye mwenyewe..

Lakini jambo lingine la kuogopesha ni kwamba ikitokea mtu aliyeko ndani ambaye tayari kashaingia ndani ya jengo hilo, akatoka na kwenda kupanda ukuta na kurukia zile nyaya za umeme zilizouzunguka ukuta, yeye naye atajeruhiwa vile vile kama sio kufa kabisa. Maumivu yale yale atakayoyasikia Yule anayetaka kuruka ukuta na kuingia ndani ndio hayo hayo atayapata Yule anayetaka kuruka na kutoka nje.

Madhara atakayoyapata mchawi anayetaka kuwadhuru watu wa Mungu, ndio hayo hayo atakayoyapata mkristo anayeuacha wokovu na kuurudia ulimwengu. Mkristo ambaye ameshaonja kipawa cha Mungu na kuburudika na neema ya Mungu, na ghafla anarudia uasherati wake, anarudia wizi wake, anarudia matusi yake, anarudia mauaji yake, usagaji wake, utoaji mimba wake, mambo ambayo alikuwa ameshayaacha machafu anayarudia tena…akidhani kwamba mkono wa Mungu ni kinyume cha wale waliopo nje pasipo kujua hata waliopo ndani ambao wanataka kutoka vile vile mkono wa Mungu upo kinyume chao.

Wengi wetu hatupendi kusikia mambo kama haya kwasababu hatupendi kuumizwa mioyo, hatupendi kusikia habari mbaya, lakini fahamu kuwa tahadhari siku zote sio habari njema, lakini zina umuhimu sana katika maisha hususani katika siku za baadaye…hata vidonge tupewacho na wataalamu wa afya ambavyo vinatumika kwa tiba, bado vina tahadhari zake…lengo la tahadhari zile sio kuwatisha watumiaji wala kuwakatisha tamaa bali kuwanufaisha zaidi.

Vivyo hivyo Neema ya Kristo inayo tahadhari…Na ni lazima kila mtu aijue tahadhari hiyo, wahubiri wengi hawaifundishi kwasababu watakosa waumini, na wao bado wanatafuta waumini…Lakini sikia leo hii mtu wa Mungu tahadhari, ili baadaye tusije kujuta, na tahadhari hii haikuhusu wewe unayesoma tu, hapana hata mimi ninayeandika inanihusu. Biblia inasema..

Waebrania 10:26 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;

27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.

28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Kama umeamua kumfuata Yesu basi umfuate kweli kweli..usiusogelee kabisa ukuta wa Neema..uwe ndani au nje ni upanga ukatao kuwili..Neno la Mungu linasema usizini…hizo ni kuta!..neno linasema usiibe, usiue hizo ni kuta..ukipanda na kuzivuka nguvu ya Mungu utakumaliza..ambayo hiyo Mungu hakuiweka kwaajili ya kuua watu, bali kwaajili ya kuwalinda watu wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEGANDA

SWALI: Shalom, nimekuwa na shida usiku nakuwa kama nimeganda siwezi kusogeza mkono au mguu au kuongea lakini akili nakuwa bado ninayo huwa nakemea inachukua muda kidogo naachiwa nashindwa kujua tatizo ni nini naomba nisaidie.


JIBU: Ndoto yoyote ambayo inakuja, na unajikuta katika mazingira ya kupambana na hali Fulani na huku unatumia jina la Yesu, ambapo mwanzoni inaonekana kuleta upinzani Fulani lakini baadaye inakuja kuachia kwa jinsi unavyozidi kuendelea kukemea ni ndoto yenye ujumbe kutoka kwa Mungu..

Wengine wanaota wanashindana na wachawi, na wale wachawi mwanzoni ni kama wanataka kumshinda lakini baadaye anawashinda kwa jina la YESU, wengine wanaota wamekutana na roho za mapepo, halafu kila alipolitaja jina la Yesu sauti, haitoki, lakini kwa jinsi alivyokuwa anaendelea kulitaja mwisho wa siku sauti inatoka na anayashinda.. Mwingine hata sio mapepo bali hali fulani ya udhaifu, kama hiyo ya kwako, unajikuta umeganda huwezi kusogeza kiungo chako hata kimoja, kila unapojaribu unashindwa, unajikuta unahitaji msaada kwa kulitaja jina la Yesu, na unapofanya hivyo mwanzoni ni kama inashindakana lakini baadaye inaachia hali hiyo  inaisha ghafla..

Zote hizo ni ndoto zenye ujumbe mmoja,..Ambao ni Mungu tu anakuonyesha SILAHA pekee ambayo inayoweza kukupa ushindi dhidi ya adui yako shetani, na silaha hiyo tayari umeshaijua ambayo ni jina la YESU. Hivyo ni kuongeza bidii ili uwe na mamlaka kamili juu ya jina hilo kuu.. (Kumbuka mamlaka hayaji kwa kulitamka tu kama ulivyoona kwenye ndoto, bali yanakuja kwa kumwelewa Yesu Kristo katika Neno lake, ndipo kutamka kwako kuwe na nguvu).

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.

Unaona hakuna lolote litakalokushinda, ikiwa maneno ya Mungu yatakuwa ndani yako kwasababu utakuwa umepewa mamlaka kamili na Kristo mwenyewe ya kushinda mambo yote..

Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru’’.

Hivyo jitahidi kumjua Kristo zaidi, au ongeza  bidii, ili upokee mamlaka hayo kamili..Ndio ujumbe mkuu unaopewa hapo.

Vile vile sababu nyingine ya pembeni, ambayo unapaswa ujue katika ndoto kama hizo za kujikuta umeganda kitandani na huwezi kufanya chochote, ambapo wengine zinakuja katika uhalisia kabisa kana kwamba  sio ndoto, bali ni kitu halisi na wanajiona hawawezi kusogeza kiungo chao chochote kitandani, na anatamani hata mtu amsaidie kusogeza mkono wake  lakini hawezi kumwambia, na wengine wanasema amekufa lakini yeye anajiona bado ..Ni kwamba hapo Mungu anakuonyesha, hali halisi ya jinsi watu wanavyokufa, na  Kwamba yapo maisha baada ya kufa, sio kama wengine wanavyodhani, ukifa huelewi chochote, La, ukifa roho yako inaendelea kuishi inaondolewa katika mwili wako na kupelekwa mahali pengine..(Mhubiri 12)..

Hivyo siku ya kufa, kila mtu atajiona jinsi anavyotoka katika mwili wake na kwenda sehemu nyingine, na ataona pia wanaomzunguka jinsi anavyowaacha!.

Hivyo tunapaswa tujiulize , je! tumejiandaaje huko tuendako? Jibu lipo katika maisha ya kila mmoja jinsi anavyoishi.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

KUOTA NYOKA.

JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

WAKATI WA JIONI KUTAKUWAKO NA NURU.

Rudi Nyumbani:

Print this post