Mjanja ni mtu wa namna gani kwenye biblia?(Mathayo 27:63)

Mjanja ni mtu wa namna gani kwenye biblia?(Mathayo 27:63)

Mjanja ni mtu anayetumia njia za kujifanya, ili kuwadanganya au kuwalaghai wengine. (Mtu mdanganyifu).

Makuhani walimwita Bwana wetu kwa jina hilo; walimfananisha na mtu mdanganyifu anayewalaghai watu kwa kujifanya kuwa anaweza kufufuka wakati hawezi, ili watu wamwamini pale wanafunzi wake watakapokuja kuiba maiti yake.

Mathayo 27:62 “Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato,

63 wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka.

64 Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza.

65 Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo.

66 Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi”.

Bwana hakuitwa jina hilo tu, kuna wakati walimwambia ana pepo, wengine wakamwambia amerukwa na akili”.

Hivyo hilo ni jambo la kawaida hata kwa mtakatifu kuzushiwa majina kama hayo. Lakini Bwana alishatupa taarifa hizo mapema, na hiyo ni kututhibitishia kuwa sisi ni wanafunzi wake kweli kweli, alisema;

Yohana 15:20 “Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.

Mathayo 10:25 “Yamtosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli, je! Si zaidi wale walio wa nyumbani mwake”?

Shalom.

Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Hazama ni nini katika biblia?(Ezekieli 16:12, Kutoka 24:47)

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Rangi ya kaharabu ni ipi kibiblia(Ezekieli 1:4,27,8:2)?

Bilauri ni nini kibiblia?(Ufunuo 21:11,22:1)

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments