Title November 2021

Kwanini kabla ya Kristo, miaka ilikuwa inahesabiwa kwa kurudi nyuma?

Nyakati zote kabla na hata baada ya Kristo miaka inahesabiwa kwa kwenda mbele, hakuna wakati wowote au kipindi chochote miaka ilihesabiwa kwa kurudi nyuma.

Litakuwa ni jambo lisilo la kiakili kama miaka itahesabiwa kwa kurudi nyuma..yaani kwa mfano leo ni mwaka 2021 halafu mwakani iwe mwaka 2020 badala ya 2022.

Sasa kama ni hivyo tunaweza kujiuliza ni kwanini, miaka ya nyuma inaonekana kama inahesabika kwa kurudi nyuma?.

Ili tuelewe vizuri hilo hebu tujifunze katika huu mfano mdogo.

Tuseme mwaka 2019 kulitokea janga kubwa la dunia la Korona lililobadilisha mfumo mzima wa maisha ya walimwengu.

Na kisha mtu mmoja akataka kurejea  tukio fulani lililotokea mwaka2015 ambapo kulitokea janga la kimbunga,na akasema.. “miaka 4 kabla ya Korona kuzuka duniani, kulitokea kimbunga kikubwa kikaharibu miundo mbinu”.

Na mwingine labda akataka kurejea tukio lililotokea mwaka 1978, wakati Tanganyika inapigana na Idd Amini wa Uganda, badala ya kusema mwaka 1978 kulitokea vita, akasema miaka 41, kabla ya janga la korona (41Kk) kulitokea vita kati ya Tanganyika na Uganda, vilivyogharimu uhai wa watu wengi.

Vile vile mtu mwingine labda akataka kurejea vita vya pili vya dunia vilivyotokea mwaka 1945, hivyo badala ya kutaja huo mwaka 1945 akasema, miaka 74 kabla ya Korona,(74kk) ilitokea vita kubwa sana ya dunia iliyogharimu maisha ya watu wengi..

Tuseme na mwingine akataka kurejeatukio la ajali lililotokea mwaka 2021, hivyo badala ya kusema mwaka 2021 kulitokea ajali mbaya sana, akasema miaka miwili baada ya Korona kuzuka duniani(2Bk), kulitokea ajali mbaya sana. N.k hiyo ni mifano tu.

Sasa kwa kusema hivyo haimaanishi, kwamba kuanzia mwaka huo wa 2019 janga la Korona lilipotokea kushuka chini, miaka ilikuwa inahesabiwa kwa kurudi nyuma.

La! Miaka ilikuwa inahesabiwa kwa kupanda, lakini kwasababu kulitokea tukio kubwa na maarufu mwaka 2019 ikabidi kalenda ibadilike, matukio yote ya nyuma yatajwe kwa kurejea tukio fulani kubwa lililowahi kutokea.

Kadhalika Kuzaliwa kwa MKUU WA UZIMA, NA MWANZILISHI WA MAMBO YOTE, YESU KRISTO. Ni lazima dunia itetemeke, tarehe haziwezi kubaki vile vile, majira hayawezi kubaki vile vile, kadhalika na kuzimu haiwezi kubaki vile vile. Ni lazima mabadiliko makubwa yaambatane na kuzaliwa kwake, kwasababu kitu alichokileta ulimwenguni ni kikubwa, Damu yake iliyomwagika pale Kalvari, imeleta mageuzi makubwa katika ulimwengu wa mwili na roho.

Maandiko yanasema..Kristo alikuja kuutangaza MWAKA WA BWANA uliokubaliwa (Isaya 61:1-2). Hivyo haiwezekani “aje autangaze mwaka wa Bwana” halafu tarehe zibaki vile vile. Ni lazima tu matukio yote ya kabla au baada yarejee kuzaliwa kwake.

Isaya 61:1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema….

2 Kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao”.

Bwana Yesu amekuwa Jiwe kuu la pembeni, Jiwe la kurejea..Korona imetikisa dunia lakini bado haijaweza kubadilisha majira, wapo wanadamu waliokuwa maarufu lakini hawajabadili majira, wamekuja na kupita, ni mkuu wa Uzima (Yesu), pekee yake ndiye ambaye mpaka leo, alama yake ipo katika kila mwanzo wa barua, mwanzo wa siku, na miezi na Miaka. Kuonesha kwamba yupo hai mpaka sasa hivi, na hakuna aliyemzidi,  leo hii hakuna mahali utakwenda usilisikie jina la Yesu likitajwa.

Na kama jinsi yeye alivyokuwa nguzo ya kurejewa, atabaki kuwa hivyo hivyo milele.

Je! Umemwamini leo?.. Umetubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha?, umebatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu upate ondoleo la dhambi zako?. Kama bado ni vyema ukafanya hivyo leo, maadamu mlango wa neema upo wazi, siku utakapofungwa kutakuwa hakuna nafasi tena ya kutubu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

USITAZAME NYUMA!

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Rudi nyumbani

Print this post

Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

Mithali 25: 20 “Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito, Ni kama yeye avuaye nguo wakati wa baridi; Ni kama siki juu ya magadi”.

Anaposema amwimbiaye nyimbo..anamaanisha nyimbo za furaha, au za shangwe kumwimbia mtu mwenye moyo mzito, kwa kudhania kuwa ndio zitatuliza uchungu wake, kumbe kinyume chake, ndio zinamwongezea masikitiko moyoni mwake.

Sulemani kwa hekima ya ki-Mungu aliliona hilo, kwamba, ni vema kuendana na hisia za mtu, kwamfano, kuna watu wapo katika uchungu mzito sana mioyoni mwao, pengine labda wa kufiwa  na mume/mke wake, au mzazi wake, au ndugu yake wa karibu sana, na wewe kwa mawazo yako ukaona ili kuwatuliza ni kwenda kuwachekesha, chekesha, au kuwaburudisha kwa nyimbo za furaha,..Ujue kuwa hapo hautatui tatizo. Ni lazima ujue hali ya mtu wakati huo, yupo katika uchungu wa namna gani.

Biblia inasema..

Warumi 12:15 “Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao”.

Lakini kama unaonyesha kufurahi pamoja na hao walioa, ukidhani ndio kiashiria cha kuwachangamsha..Ni rahisi kuwasha moto mwingine,

Kwasababu mtu Yule anaweza kudhani hujathamini hata kile anachokipitia, na matokeo yake atachukia badala ya kupona,..Ni ndio hapo anasema sawa na kumvua mtu nguo zake wakati wa baridi kali, ni nini kinatokea? Ni mateso zaidi kama sio kifo.

Kwahiyo tuwe na hekima ya kujua ni dawa ipi tunaitumia kumponya mtu aliyevunjika moyo. Ikiwa kweli anahitaji, furaja za nyimbo tutumie hizo, lakini kama yupo katika uchungu mwingi sana wa moyo, tuendane na hisia zake, hiyo ndio dawa pekee ya kuwaponya watu kama hao.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:

Rudi nyumbani

Print this post

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Lengo la Mungu kuwapa watu amri ya kuitunza sabato lilikuwa ni tofauti na lilivyochukuliwa au kutafsiriwa.Tuchukue mfano wa kawaida wa kimaisha…

Kikawaida, kila mtu ni lazima katika siku moja anao muda wa kulala (kupumzika), ili mwili wake uwe katika ustawi bora, hakuna mtu asiyelala kabisa.Hivyo ni sawa na kusema usingizi umeumbwa kwa ajili yetu sisi, ili tupate kuwa na afya bora na sio sisi tumeumbwa tuutumikie usingizi.
Kwa mantiki hiyo basi, ingawa tuna sheria ya kulala kila siku, lakini hatuna sheria ya muda wa kulala au wakati wa kulala.

Wengine watalala kuanzia saa 3 usiku na kuamka saa 11 alfajiri ili kuwahi shughuli zao..hivyo wakawa wamelala masaa 8.

Wengine wataanza kulala kuanzia saa 6 usiku na kuamka saa 2 asubuhi na wakawa wamelala masaa yaleyale 8..wengine hawatalala kabisa usiku bali watalala mchana..

Hao wote wametimiza sheria ya kulala,ilitowekwa na Mungu, hakuna hata mmoja aliyeivunja..isipokuwa kila mtu kaitimiza kwa wakati wake aliouona unafaa.

Hivyo muda wa kulala haujalishi kinachojalisha ni masaa na matokeo baada ya kulala..kwamba wote mtalala na miili itakuwa imepumzika..Na usipolala mwili wenyewe utakutumia taarifa ya deni la usingizi, hivyo hilo deni utalilipa tu, na taarifa hiyo sio Mungu anayekutumia bali ni mwili ndio unaokutumia.

Lakini sasa inapotokea kwamba ni amri kwamba kila saa 3 usiku mpaka saa 11 asubuhi watu wote wawe vitandani wamelala, hapo tutakuwa tunauabudu usingizi, tutakuwa ni watumwa wa usingizi, na tutakuwa wajinga na maana ya kulala itakuwa imepotea kabisa.

Kwasababu kuna wakati itakubidi uwahi kulala ili uwahi kuamka, kuna kipindi utachelewa kulala kutokana na dharura za kimaisha na hivyo utajikuta unachelewa kuamka pia, kuna wakati utaugua utakuwa kitandani muda wote, au usiwe unapata usingizi kabisa..Hivyo usingizi upo lakini ni sisi ndio tunaouendesha na sio wenyewe unatuendesha sisi..Hatuwi watumwa wa usingizi!

Na Sabato ni hivyo hivyo..

Maandiko yanasema Sabato ilifanyika kwaajili yetu na sio sisi kwaajili ya sabato.

Marko 2:27 “Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato”

Mungu aliiweka sabato ili tupumzike tupate muda wa kumtafakari yeye, na kutengeneza mambo yetu ya kiroho katika wiki inatofuata mbele yetu, kama vile usingizi ulivyowekwa kwamba tupumzike ili miili yetu istawi, ipate nafasi ya kujitengeneza upya kwaajili ya kuiendea siku inayofuata.
Hivyo ni kweli tumepewa amri ya kuishika sabato, lakini hiyo hatuishiki kwa kanuni fulani maalumu, kwamba ni lazima iwe ni kila jumamosi, kiasi kwamba mtu ukiabudu siku tofauti na hiyo ni kosa!…au kwamba ni lazima iwe kila jumapili kiasi kwamba mtu akiabudi jumamosi ni kosa, hapo tutakuwa hatujaelewa maana ya Sabato!.

Hivyo siku ya Bwana ni chaguzi wetu, kwamba siku ipi ni bora kwetu, kama ni jumamosi, au jumapili, au jumatatu, au jumanne au siku nyingine yeyote maadamu, katika hiyo tutaifanya siku nzima iwe takatifu kwa Bwana.

Kulingana na mfumo wa kalenda ya nchi yetu, siku ambazo hazina masumbufu ni jumamosi na jumapili, hizo ni siku ambazo ni nzuri kuzifanya kuwa za Bwana, lakini pia sio amri, hata jumanne ni siku iliyokubalika, hata jumatano, lakini shida ya siku hizo ni kwamba zina masimbufu mengi ya kimaisha, hivyo ni ngumu kuzitakasa.

Mataifa ya kiarabu, siku ya ijumaa ndio siku isiyo na masumbufu kwao, kama vile ilivyo jumapili na jumamosi kwetu, kwao ni ijumaa…hivyo siku kama hiyo kulingana na kalenda za mataifa hayo ni vizuri kuifanya siku ya Bwana iwe Ijumaa kuliko jumapili au jumamosi kwasababu, siku ya jumapili ni sheria watu wao kwenda makazini kama kawaida tofauti na huku kwetu.

Ni jambo la aibu mkristo kushindania siku ya kuabudu.
Utakuta mtu hafahamu kitu kingine chochote zaidi ya kushabikia jumamosi au jumapili. Mtu kama huyo anakuwa hana tofauti na mtu anayeshabikia muda wa kulala.

Bwana atupe macho ya kuyaona haya, na tutokane na upofu huo, ambao unaufanya ukristo usieleweke kwa watu waliopo nje.

1 Wakorintho 14:40 “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Rudi nyumbani

Print this post

Ratli/ Ratili ni nini katika biblia?

Ratili ni kipimo cha uzito kilichotumika enzi za kale..chenye uzito sawa na Gramu 500 hivi. Karibia na nusu kilo.

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia..

Yohana 19:39

[39]Akaenda Nikodemo naye, (yule aliyemwendea usiku hapo kwanza), akaleta machanganyiko ya manemane na uudi, yapata ratli mia.

Pia..

Yohana 12:3

[3]Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu.

Unaweza kupata picha Mariamu alibeba manukato yaliyokuwa na uzito wa karibia nusu kilo..na yote akammwagia Bwana Yesu..manukato ambayo ingetosha tu kuchukua kidogo na kumpaka lakini yeye aliyamimina kwake kama maji.

Kwasasa mafuta hayo kwa wingi wake ni thamani isiyo pungua milioni 6 kwa fedha za kitanzania..kufunua ni jinsi gani Mariamu alimthaminisha Yesu kuliko mtu mwingine yeyote au mfalme yeyote duniani..

Si ajabu kwanini matendo ya watu kama hawa tunayasoma hadi leo katika maandiko..Ni kutufundisha kuwa na sisi pia tukitoa vitu vyetu vya thamani nyingi sana kwa ajili ya Mungu..

Mungu naye ni lazima arudishe fadhila kwetu kwa kutupa kumbukumbu la daima..ndivyo alivyofanya kwa yule mwanamke pale watu walipomng’unikia kwa upotevu wote ule..Bwana alisema..

Marko 14:8-9

[8]Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu marhamu kwa ajili ya maziko.

[9]Amin, nawaambia, Kila ihubiriwapo Injili katika ulimwengu wote, na hili alilotenda huyu litatajwa kwa kumbukumbu lake.

Swali ni je na sisi tunaweza kumthamini Bwana kwa namna hiyo? Bwana atupe macho hayo.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Panda/ Sauti ya panda ni nini kibiblia?(Danieli 3:5)

Kinubi ni nini katika biblia? (1Samweli 16:16, 23)

Rudi nyumbani

Print this post

Mtima ni nini kibiblia?.

“Mtima” ni neno linalowakilisha aidha “nafsi ya mtu” au “roho ya mtu”

Hivyo mtu anayeugua rohoni, ni sawa na kusema “anaugua katika mtima wake”.. kadhalika mtu aliyeumizwa nafsini mwake ni sawa na kusema “kaumizwa katika mtima wake”..hivyo ni neno linalotumika kuwakilisha aidha Roho au Nafsi ya mtu.

Katika biblia neno hilo limeonekana mara kadhaa..

Ayubu 19:27 “Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu”.

Maombolezo 1:20 “Angalia, Ee Bwana; maana mimi ni katika dhiki; Mtima wangu umetaabika; Moyo wangu umegeuka ndani yangu; Maana nimeasi vibaya sana; Huko nje upanga hufisha watu; Nyumbani mna kama mauti”.

Yeremia 4:19 “Mtima wangu, mtima wangu! Naumwa katika moyo wangu wa ndani; moyo wangu umefadhaika ndani yangu; siwezi kunyamaza; kwa sababu umesikia, Ee nafsi yangu, sauti ya tarumbeta, mshindo wa vita”.

Mistari mingine inayotaja neno hilo ni pamoja na Zaburi 26:2, Mithali 20:30, na Zaburi 139:13.

Kila mwanadamu anao “Mtima” kwasababu ndio utu wa ndani. Na mitima yetu (yaani nafsi zetu na Roho zetu) zinapaswa ziwe safi siku zote.. Na Mungu anazitakasa nafsi zetu kwa sisi kwanza kujitenga na kila ubaya kama maandiko yanavyosema..

1Wathesalonike 5:22 “Jitengeni na ubaya wa kila namna”.

23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi NAFSI ZENU na ROHO ZENU na MIILI YENU mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo”.

Je! Umejitenga na kila ubaya?..umejitenga na Ulevi?, uzinzi? Ushirikina?, uvaaji mbaya? Utukanaji?, wizi, ushabiki wa mambo ya kidunia?.. Kama bado hujajitenga na hayo yote, na huku unaomba kwamba Mungu akusafishe roho yako, au akupe amani katika nafsi yako, au aponye majeraha yako ya ndani, au akulinde na nguvu za giza..tambua kuwa unapoteza muda wako. Sharti kwanza ni wewe kujitenge na kila ubaya ili umfungulie Mungu mlango wa kukusafisha.

Lakini kama hutaki kujitenga na ubaya wote huo, bado unaukumbatia hakuna utakaso wowote utakaoupata kutoka kwa Mungu, kama bado unaishi na huyu unayemwita boyfriend, au girlfriend, tambua kuwa roho yako bado imefungwa, kama bado unashiriki mazungumzo machafu na hizo kampani za rafiki ulio nao, unajifungia mlango wa utakaso, kama bado unayo miziki ya kidunia na filamu za kidunia katika simu yako unafunga milango ya utakaso wako.

Maandiko yanasema “Tujitenge na ubaya wa kila namna” na sio “tuuombee Ubaya”.. Utakuta mtu anakwenda kutafuta kuombewa aache uzinzi, na huku hajajitenga na vichocheo vyote vya uzinzi. Mtu wa namna hii ataomba na kuombewa, na hakuna chochote atakachopokea, kwasababu hajajua kanuni ya kupokea Utakaso.

Utakaso unaanza kwanza kwa sisi “kujitenga na ule uovu”..Ndipo Roho Mtakatifu anatuongezea nguvu za sisi kuushinda uovu.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu”,(Mwanzo 1:26)?

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

UMEDI NA UAJEMI ZILITAWALAJE?

Katika biblia tunaona kama Umedi na Uajemi zikitajwa kwa pamoja, kana kwamba ni Taifa moja, ingawa ni falme mbili tofauti, sasa zilitawalaje?

Umedi na Uajemi Ni utawala mmoja ulioundwa na Falme mbili tofauti, Ili kuelewa vizuri tuchukue mfano wa Taifa la Tanzania, Taifa la Tanzania limeundwa na mataifa mawili, Zanzibar na Tanganyika, Na yalipoungana ndio ikawa Tanzania, Kwahiyo badala ya kusema Tanzania, tunaweza kusema ni Taifa la Tanganyika na Zanzibar. Na ukitazama utaona unapofika wakati uchaguzi wa uRaisi, Raisi anayechaguliwa kuiongoza nchi yote anaweza kutoka upande wowote ule kati ya pande hizo mbili. Utaona leo anaweza kutokea Tanganyika, awamu ijayo akatokea Zanzibar.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Ufalme wa Umedi na Uajemi. Zilikuwa ni falme mbili zilizoungana na kuwa ufalme mmoja. Lakini wafalme waliokuwa wanatawala, walikuwa wanapokezana, awamu hii mfalme anaweza kutokea Umedi, awamu ijayo akatokea Uajemi. Kama vile Raisi wa Tanzania, leo anaweza kutokea Bara, awamu ijayo akatokea Zanzibar.

Ndio maana utaona baada tu ya Ufalme wa Babeli kuanguka, ufalme uliochukua hatamu ni Dario, wa Umedi, huyu ndiye aliyemwangusha Nebukadneza, lakini bado hakuwapa ruhusa Israeli warudi nchini kwao, Israeli waliendelea kukaa mateka. Ingawa huyu Dario, alimheshimu sana Danieli, hata kumweka Danieli kuwa mkuu wa Maliwali wa ufalme wake wote.

Danieli 6:30 “Usiku uo huo Belshaza, mfalme wa Wakaldayo, akauawa.

31 Na Dario, Mmedi, akaupokea ufalme, naye umri wake alikuwa na miaka sitini na miwili”.

Danieli 7:1 “Ilimpendeza Dario kuweka juu ya ufalme maliwali mia na ishirini, wawe juu ya ufalme wote;

2 na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danielii alikuwa mmoja wao; ili maliwali hawa watoe hesabu kwao, mfalme asipate hasara.

3 Basi Danielii huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote”.

Lakini ulipofika utawala wa Koreshi miaka michache baadaye ambaye alikuwa ni Muajemi ndipo Israeli walipofunguliwa kutoka katika utumwa, na kupewa ruhusa kurudi nchini kwao, kuutengeneza mji wao na Hekalu la Mungu lililobomolewa na Mfalme Nebukadneza.

2Nyakati 36:22 “Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,

23 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi; Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu, ulioko Yuda. Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee”.

Hivyo utawala huu wa Umedi na Uajemi, ndio Mungu alioutumia kuwapa raha Israeli, kwani ndio uliowaweka Israeli huru, na kuwapa ruhusa ya kwenda kuijenga nchi yao, ingawa ni kwa vipindi vya tabu, lakini hatimaye kazi ya ujenzi ilikamilika katika utawala huu kabla ya kuingia utawala wa UYUNANI, ambao uliusumbua sana Israeli.

Pia katikati ya utawala huu wa Umedi na Uajemi, ndipo Malkia Esta alitokea.

Esta 1:1 “Zamani za Ahasuero; naye huyu Ahasuero alimiliki toka Bara Hindi mpaka Kushi, juu ya majimbo mia na ishirini na saba;

2 siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;

3 mwaka wa tatu wa kumiliki kwake, ikawa aliwafanyia karamu maakida wake wote na majumbe wake; WAKUU WA UAJEMI NA UMEDI, watu wenye cheo na maakida wa majimbo, wakihudhuria mbele zake”.

Lakini pamoja na kwamba ulikuwa ni ufalme uliotawala dunia, na uliowanufaisha Israeli kwa sehemu kubwa, hata kufikia wakati binti wa kiisraeli, (yaani Esta) kuwa Malkia wa dunia, lakini bado ufalme huo ulikuja kuanguka, kuonyesha kuwa Falme zote zitaanguka haijalishi ni Nzuri au Mbaya. Lakini ufalme wa Mmoja tu Yesu Kristo ndio utakaodumu milele. Sawasawa na maono aliyoyaona Nebukadreza.

Nebukadreza aliona jiwe lililochongwa pasipo kazi ya mikono, ikizipiga zile falme tano zilizotawala, (yaani Babeli, Umeni na Uajemi, Uyunani, na Rumi), na kuziangusha zote, na kisha jiwe hilo kuwa milima mikubwa iliyoijaza dunia yote. Na ufunuo wa jiwe hilo ni utawala wa Yesu Kristo, ambao ndio utazivunja falme hizo zote na utasambaa duniani kote.

Siku si nyingi parapanda ya mwisho italia, na wafu watafufuliwa na kwenda mbinguni, na hukumu ya mataifa waliosalia duniani itaanza, mataifa yataanguka yote na dunia itatikiswa, kabla ya kuanza utawala wa Mfalme Yesu Kristo, wa miaka elfu, ambao utasambaa ulimwenguni kote. Utakuwa ni utawala wa Amani kabla ya kuingia katika umilele katika mbingu mpya na nchi mpya.

Je utakuwa wapi siku hiyo? Utawala wa Farao ulipita, utawala wa Nebukadneza ulipita, utawala wa Malkia Esta ulipita, na tawala nyingine zote zilipita!, unadhani ni nini ambacho hakitapita kilichosalia katika huu ulimwengu?.. Vyote vitapita lakini Maneno ya Yesu Kristo hayatapita kamwe, alisema atarudi! Atarudi tu!, haijalishi dunia itasemaje!.. na atakuja kama mwivi.

Mathayo 24:35 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?

YEZEBELI ALIKUWA NANI

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

Rudi nyumbani

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)

Jina la Bwana YESU Kristo libarikiwe, karibu katika mwendelezo wa uchambuzi wa vitabu vya biblia, Tumekwisha kuvitazama vitabu kadhaa nyuma, na leo kwa neema za Bwana tutapiga hatua moja mbele, kukitazama kitabu cha Isaya.

Kabla ya kuendelea mbele,  ni muhimu kufahamu kuwa huu ni ufupisho tu!, na sio utimilifu wenyewe! hivyo kila mtu analo jukumu la kukisoma kitabu hichi cha Isaya kabla na baada ya kusoma ufupisho huu. Na vile vile, kama hujapitia uchambuzi wa vitabu vilivyotangulia, ni vizuri uupitie kwanza ili tuweze kwenda pamoja katika vitabu hivi vya mbeleni.

Kama hujapata uchambuzi huo basi unaweza kufungua hapa >>> Vitabu vya Biblia: Sehemu ya kwanza (www.wingulamashahidi.org) au unaweza ukatujuza kupitia inbox kwa namba zilizopo mwisho wa somo ili tuweze kukutumia.

Mwandishi wa kitabu cha Isaya ni Nabii Isaya mwenyewe, kitabu cha Isaya kina sura 66 sawasawa kabisa na jumla ya vitabu vyote vya biblia, ambavyo ni 66.

Tofauti na vitabu vingine vya kinabii kama Hosea, Zekaria, Hagai, Obadia, Yona, Habakuki, Malaki na vingine baadhi, ambavyo vimebeba Nabii za kipindi fulani tu au za jamii ya watu fulani tu!, labda kuhusu Mwisho wa dunia, au kuchukuliwa kwa Israeli kwenda Babeli, au hukumu ya Taifa fulani litubu!, vinakuwa havijabeba, au vinabeba kwa sehemu ndogo sana..

Lakini kitabu cha Isaya  ni kitabu ambacho kimebeba UNABII wa mambo karibia yote kwa mapana na marefu.

Kitabu cha Isaya, kina unabii kuanzia Israeli kuchukuliwa Mateka na kupelekwa Babeli, vile vile kina unabii wa kurejeshwa kwao, kina unabii wa kuanguka kwa Babeli, na hukumu ya Babeli, kina unabii wa kujengwa tena hekalu lililobomolewa, kadhalika kina unabii kuanguka na kunyanyuka kwa Mataifa mengine nje ya Israeli, vile vile kina unabii wa UJIO WA MASIHI, (Hakuna kitabu kingine chochote kilichotabiri kwa kina jinsi Masihi atakavyokuwa na tabia zake kama kitabu hiki, tutakuja kuliona hilo vizuri mbele kidogo)..

Kitabu cha Isaya pia kimetabiri Siku ya Ghadhabu ya Mungu, ambayo itakuja  baada ya Unyakuo wa kanisa kupita!, kimetabiri mpaka kipindi cha utawala wa miaka 1000,wakati ambao Kristo atatawala na watakatifu wake kwa miaka elfu akiwa hapa duniani, na mambo mengine mengi.

Leo tutazitazama nabii hizi chache, Lakini kabla ya kwenda kuzitazama.. Ni vyema pia kufahamu jambo lingine la muhimu, kwamba Kitabu cha Isaya hakijaandikwa kwa muda wa siku moja, au mwezi, au mwaka mmoja. Hapana!.

Kitabu cha Isaya kimeandikwa kwa kipindi cha Miaka 58 kuanzia mwaka (739KK-681KK)

Kwa kadiri Isaya alivyokuwa anapewa maono ndivyo alivyokuwa anaandika, na sio kila siku alikuwa anapewa maono, wakati mwingine ilipita kipindi kirefu hata zaidi ya mwaka, pasipo kupokea unabii wowote wa kuandika.. Hivyo Sura zote 66 za kitabu hicho, ni mfululizo wa Maono aliyoyaona Isaya, katika kipindi chote cha Maisha yake, tangu alipoanza kuona maono mpaka alipokufa (yaani miaka 58).

Ndio maana utaona maono ya kitabu hicho ni kama yamechanganyikana..Ni kwasababu hakupewa kipindi kimoja.. Leo anaweza kupewa Ono linalomhusu Masia, akaliandika katika Sura moja, mwezi ujao au mwaka ujao akapewa linalohusu kuanguka kwa Babeli akaliandika chini katika sura ya pili, baada ya miaka miwili tena anapewa ono linalomhusu Masia tena (Yesu Kristo), tofauti na lile la kwanza, akaliandika katika sura ya 3, baada ya miezi kadhaa anapewa unabii tena kuhusu Utawala wa miaka elfu n.k Kwahiyo ni unabii juu ya unabii, kwa vipindi tofauti tofauti.

MAISHA YA ISAYA.

Isaya alikuwa ni Mwana wa mtu aliyeitwa Amozi, biblia haijaleza huyu Amozi, baba yake Isaya alikuwa ni mtu wa namna gani, lakini ni wazi kuwa alikuwa ni mtu maarufu, aliyekuwa anajulikana). maana ya jina Isaya ni “Bwana ni Wokovu”..(Isaya alianza kuona maono ya Mungu baada ya kifo cha mfalme Uzia (Isaya 6:1), Na ni nabii aliyetokea mapema kabla ya wakina Yeremia, Danieli, Ezekieli, Yona na wengine wengi..

Biblia haijaeleza kwa undani sana maisha ya Isaya, lakini maandiko yanasema alioa Nabii Mke na kuzaa nae watoto (Isaya 8:3), Na mwanamke huyo aliyemwoa, alimwoa kwa agizo la Bwana, kwasababu Mungu aliyafanya maisha yake kuwa ishara kwa Israeli, kama vile alivyoyafanya ya Hosea na Ezekieli.

Ni kawaida ya Mungu kuyafanya maisha ya watumishi wake kuwa Ishara kwa dunia, Kwamfano utaona Nabii Ezekieli kuna mahali aliagizwa na Mungu ale kinyesi, lengo ni kufikisha ujumbe fulani kwa watu fulani, kadhalika kuna mahali Nabii Hosea aliambiwa na Mungu akaoe mwanamke wa uzinzi, na kuzaa naye watoto ili kufikisha ujumbe fulani kwa watu fulani. Vile vile Nabii huyu  Isaya Mungu aliyachagua maisha yake kuyafanya ishara kama hawa wengine, ili kufikisha ujumbe fulani. Kwamfano utaona kuna mahali Nabii Isaya, aliambiwa na Mungu, atembee uchi..

Isaya 20:2 “wakati huo Bwana alinena kwa kinywa cha Isaya, mwana wa Amozi, akisema, Haya, uvue nguo ya magunia viunoni mwako, na viatu vyako miguuni mwako.

3 Naye akafanya hivyo akaenda uchi, miguu yake haina viatu. Bwana akasema, Kama vile mtumishi wangu Isaya anavyokwenda uchi, hana viatu, awe ishara na ajabu kwa muda wa miaka mitatu juu ya Misri na juu ya Kushi;

4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawachukua uchi, wafungwa wa Misri, na watu wa Kushi waliohamishwa, watoto kwa wazee, hawana viatu, matako yao wazi, Misri iaibishwe.

5 Nao watafadhaika, na kuona haya kwa ajili ya Kushi, matumaini yao, na Misri, utukufu wao”.

Kwa maelezo marefu kwanini Isaya aliagizwa atembee uchi unaweza kufungua hapa >>Kwanini Isaya aliagizwa atembee uchi?, (www.wingulamashahidi.org) Au ukatujuza kwa njia ya inbox, tukutumie somo kamili .

Kwahiyo Maisha ya Isaya, mbali na kutoa Unabii, Mungu aliyatumia maisha yake pia kama Ishara, kulingana na historia, Nabii Isaya alikufa kifo cha kukatwa na Msumeno sawasawa na Waebrania 11:37.

NABII ZA ISAYA.

Nabii za Isaya zimegawanyika katika vipengele vitano, 1) Unabii juu ya Yuda na Israeli kabla ya Uamisho wa Babeli, 2) Unabii juu ya Israeli baada ya Uamisho 3) Unabii wa kuja kwa Masihi, mara ya kwanza na mara ya pili  4) Unabii wa kuanguka kwa mataifa  5) Unabii wa hukumu ya Mungu na Utawala wa miaka Elfu .

Tutaziangalia Nabii hizi kwa uchache moja baada ya nyingine.

 1. Unabii wa Yuda na Israeli kabla ya Uamisho wa Babeli.

Nabii Isaya alitokea miaka miaka karibia 155 kabla ya Uamisho wa Babeli, Na Israeli pamoja na Yuda ilikuwa tayari imeshafanya machukizo makubwa mbele za Bwana, hivyo Nabii Isaya alianza kutabiri kuanguka kwa Yerusalemu miaka 155 kabla ya maangamizi hayo kutokea. (kuonyesha ni jinsi gani Mungu alivyo na huruma, jinsi anavyotoa kipindi kirefu cha watu kutubu, na kugeuka), lakini tunaona hawakutubu na siku ilipofikia uharibifu uliwajia ghafla na wote wakapelekwa utumwani.

Ufunuo 22: 4 “Kwa sababu hiyo nasema, Geuza uso wako usinitazame, nipate kulia kwa uchungu; usijishughulishe kunifariji, kwa ajili ya kuharibika kwake binti ya watu wangu.

5 Kwa maana siku ya kutaabika, siku ya kukanyagwa, siku ya fujo inakuja, itokayo kwa Bwana, Bwana wa majeshi, katika bonde la Maono; inabomoa kuta; na kuililia milima”.

Huo ni unabii wa kuharibiwa kwa Yuda, na Mfalme Nebukadreza.

 2. Unabii wa Israeli baada ya kuhamishwa.

Pamoja na Isaya kutabiri kuanguka kwa Yerusalemu, lakini pia alitabiri wayahudi kurejeshwa tena Yerusalemu kutoka Babeli, aliabiri atatokea mfalme anayeitwa Koreshi, atakayewaweka huru wayahudi, na kuwapa ruhusa warejee nchini mwao wakiwa huru..

Isaya 44:26 “nilithibitishaye neno la mtumishi wangu, na kuyafikiliza mashauri ya wajumbe wangu; niuambiaye Yerusalemu, Utakaliwa na watu, nayo miji ya Yuda, Itajengwa, nami nitapainua mahali pake palipobomoka;

27 niviambiaye vilindi, Kauka, nami nitaikausha mito yako;

28 nimwambiaye Koreshi, Mchungaji wangu, naye atayatenda mapenzi yangu; hata ataunena Yerusalemu, Utajengwa; na hilo hekalu, Msingi wako utawekwa”.

Unaweza kusoma tena juu ya Unabii huo wa Koreshi katika Isaya 45:1-2

 3. Unabii wa kuja kwa Masihi.

Baada ya Nabii Isaya kuonyeshwa kurejeshwa kwa Wayahudi kutoka utumwani, na kustarehe katika nchi yao, Mungu aliendelea kumwonyesha maono ya kuja kwa Masihi yaani Yesu, alimwonyesha tangu kuzaliwa kwake jinsi kutakavyokuwa kwamba, atazaliwa na Bikira(Isaya 7:14), Na jinsi atakavyopitia mateso na kufa, kwaajili ya dhambi zetu, kama vile mwanakondoo apelekwaye machinjoni.

Isaya 53:1 “Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?

2 Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.

3 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.

4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

6 Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.

7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.

8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu”.

Hakuna mahali pengine popote katika biblia palipotabiri Bwana kuzaliwa na Bikira isipokuwa hapa katika Isaya tu,  wala hakuna kitabu kingine chochote kilichoelezea mateso ya Bwana Yesu kwa mapana namna hii kama hichi kitabu cha Isaya.

Nabii Isaya hakuishia tu kufunuliwa hayo juu ya Masihi, bali alifunuliwa mpaka utawala wake wa kifalme ambao utakuja baada ya hasira ya Bwana kupita, yaani utawala wa miaka elfu moja. (tutakuja kuuona  vizuri mbele kidogo), Lakini kwa habari za unabii wa ujio wa Masihi na tabia zake, unaweza pia kuzisoma katika mistari hii>>Isaya 11:1-2, Isaya 61, na Isaya 9:6.

 4. Unabii wa kuanguka kwa Mataifa.

Sehemu hii ya unabii ndio iliyochukua nafasi kubwa katika kitabu cha Isaya. Bwana Mungu alimwonyesha Isaya, Nabii juu ya Mataifa yote ambayo kwa namna moja au nyingine yalihusiana na taifa la Israeli, kuanzia Misri, Babeli, Ashuru, Moabu, Filisti, Tiro, Kushi, Edomu na mengine machache.

Mataifa hayo Bwana Mungu alitabiri kuanguka kwao, kwasababu na yenyewe yalifanya mabaya kama Israeli tu!, Kwamfano Taifa la Babeli liliwatesa Israeli watu wa Mungu, ijapokuwa aliliruhusu hilo kwa lengo la kuwaadhibu Israeli, lakini bado Babeli ilikuwa na hatia juu ya hilo, kadhalika Babeli ndio ilikuwa kitovu cha machukizo yote ya ulimwengu kipindi hicho. (Kumbuka katika siku hizi za mwisho pia kuna Babeli nyingine ya kiroho, ambayo inawachukua watu utumwani na vile vile Mungu kaitabiria hukumu, kama alivyoitabiria Babeli hii, kama utapenda kujua Babeli hiyo unaweza kufungua hapa  >>> Babeli ya rohoni au ukatutumia ujumbe inbox, tukutumie somo kamili). Hivyo Mungu aliyaadhibu na kutabiri kuanguka kwao.

Tutapitia mataifa machache, na mengine tutayasoma kwa nafasi zetu..

Taifa la Babeli.

Isaya 14: 4 “utatunga mithali hii juu ya mfalme wa Babeli, na kusema, Jinsi alivyokoma mwenye kuonea; Jinsi ulivyokoma mji ule wenye jeuri!

5 Bwana amelivunja gongo la wabaya, Fimbo ya enzi yao wenye kutawala.

6 Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu”.

Soma tena..

Isaya 47:1 “Haya, shuka, keti mavumbini, Ewe bikira, binti Babeli; Keti chini pasipo kiti cha enzi, Ewe binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.

2 Twaa mawe ya kusagia, usage unga; Vua utaji wako, ondoa mavazi yako, Funua mguu wako, pita katika mito ya maji.

3 Uchi wako utafunuliwa, Naam, aibu yako itaonekana. Nitalipa kisasi; simkubali mtu ye yote.

4 Mkombozi wetu, Bwana wa majeshi ndilo jina lake, Mtakatifu wa Israeli.

5 Kaa kimya, ingia gizani, Ee binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena Malkia wa falme.

6 Nalikuwa nimekasirika na watu wangu, naliutia unajisi urithi wangu, nikawatia mkononi mwako; wewe hukuwatendea rehema; uliwatia wazee nira yako, nayo nzito sana.

7 Ukasema, Mimi nitakuwa bibi milele; hata hukuyatia hayo moyoni mwako, wala hukukumbuka mwisho wa mambo hayo.

8 Sasa, basi, sikia haya, wewe upendaye anasa, ukaaye na kujiona salama, wewe usemaye moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi; sitaketi mfano wa mjane, wala sitajua kufiwa na watoto”

Pia unaweza kusoma Isaya 13, inazungumzia unabii huo huo wa kuanguka kwa Babeli.

Misri.

Misri ni taifa lililowatesa Israeli, kipindi kabla hawajaingia nchi ya Ahadi, Taifa hili limekuwa adui kwa Israeli mara kadhaa, na pia limekuwa kitovu cha maasi mengi duniani, hata baada ya Israeli kuingia nchi ya kaanani. Bwana alilitabiria pia kuanguka kwake katika mistari hii >> Isaya 19:1-5

Ashuru.

Taifa Ashuru ni taifa lililowachukua pia Israeli utumwani, nalo pia Bwana alilitabiria kuanguka.. Hukumu ya taifa hilo unaweza kuisoma kupitia mistari hii >> Isaya 10:5, Isaya 14:25-27.

Ufilisti

Filisti ni mji uliokuwa unawatesa Israeli mara nyingi, na uliokuwa unaabudu miungu kwa kiwango kikubwa, Unabii kwa kuanguka kwake unaweza kuusoma kupitia mistari hii >> Isaya 142:8-38.

Moabu

Moabu ni Taifa lililokuwa adui wa Israeli kwa kipindi chote, ndilo taifa lililomwajiri Balaamu awalaani Israeli walipokuwa wanaiendea nchi yao ya Ahadi..Bwana alilitabiria kuanguka kwake kupitia nabii Isaya, katika mistari hii >> Isaya 15:1-5

Tiro

Tiro ni mji uliokuwa karibu na Sidoni, katika nchi ya Lebanoni, huku ndiko Yezebeli alipotokea na ndipo kulipokuwa kitovu cha ibada za mungu baali. Ulikuwa ni mji wa kibiashara, na wafanya biashara na ulikuwa umejaa udhalimu. Bwana aliutabiria kuanguka kwake katika mistari hii >> Isaya 23:1-6

Mataifa mengine madogo madogo kama Edomu, Kushi, Dameski na mengine yanayohusiana na miji hiyo, Bwana aliitabiria kuanguka kwao kupitia mistari hii>>(Isaya 63:1-6, Isaya 34:1-10, Isaya 17:1-6, na Isaya 18:1-3).

 5. Unabii wa hukumu ya Mungu na Utawala wa miaka Elfu .

Pamoja na Isaya kupewa unabii wa Kuanguka kwa Mataifa, alionyeshwa pia mwisho wa dunia, yaani hukumu ya ulimwengu mzima, wakati Ghadhabu ya Mungu itakapomwagwa duniani kutokana na maasi na maovu ya ulimwengu, na vile vile akaonyeshwa utawala wa amani wa Bwana Yesu wa miaka elfu moja duniani na mbingu mpya na nchi mpya.

Siku ya Ghadhabu ya Bwana na hasira yake.

Isaya 24:1 “Tazama, Bwana ameifanya dunia kuwa tupu, aifanya ukiwa, aipindua, na kuwatawanya wakaao ndani yake.

2 Na itakuwa kama ilivyo hali ya watu, ndivyo itakavyokuwa hali ya kuhani; kama ilivyo hali ya mtumwa, ndivyo itakavyokuwa hali ya bwana wake; kama ilivyo hali ya mjakazi, ndivyo itakavyokuwa hali ya bibi yake; kama ilivyo hali yake anunuaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake auzaye; kama ilivyo hali yake akopeshaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake akopaye; kama ilivyo hali yake atwaaye faida, ndivyo itakavyokuwa hali yake ampaye faida.

3 Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana Bwana amenena neno hilo.

4 Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika.

5 Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele.

6 Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu”.

Utawala wa amani wa miaka elfu na wa mbingu mpya na nchi mpya.

Isaya 65:17 “Maana, tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.

18 Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.

19 Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.

20 Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.

21 Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake.

22 Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.

23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na Bwana, na watoto wao pamoja nao.

24 Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.

25 Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng’ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema Bwana”.

Ni nini tunajifunza katika kitabu hichi cha Isaya?

Tunajifunza kuwa maneno ya Mungu hayapiti kamwe!. Alitabiri habari za kuanguka kwa Yerusalemu, zikatimia kama zilivyo, alitabiri habari za kuzaliwa Masihi kupitia bikira, na zikatimia kama zilivyo, na ametabiri kuanguka kwa mataifa pamoja na siku ya kisasi cha Bwana, vile vile zitatimia kama zilivyo.

Hizi ni siku za mwisho, siku ya hasira ya Bwana imekaribia, unyakuo wa kanisa utakapopita tu!, kitakachokuwa kimebaki ni dhiki kuu na hiyo siku ya hasira ya Bwana!, Jua litatiwa giza, maji yote yatakuwa damu, milima na visiwa vitahama, na Bwana atawahukumu wanadamu wote wanaotenda maasi, na mwisho wao utakuwa katika lile ziwa la moto. Lakini watakatifu, yaani wote waliooshwa kwa damu ya mwanakondoo, watairithi hiyo mbingu mpya na nchi mpya.

Je mimi na wewe tutakuwa wapi siku hiyo?

Bwana akubariki.

Usikose mwendelezo wa vitabu vinavyofuata.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

MNARA WA BABELI

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NANI ATAKAYEWAPA ILIYO YENU WENYEWE?

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.

Ulishawahi kuutafakari kwa ukaribu huu mstari ambao Bwana Yesu aliusema katika..

Luka 16:12 “Na kama hamkuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?

Kauli hii ni kinyume na sisi tunavyoweza kuitafsiri. Kwa kawaida, ni sharti kwanza mtu atazame uaminifu wa kile cha kwako kwanza, ndipo ashawishike kukuongezea kilicho cha kwake. Ukienda kukopa Benki ni sharti waangalie mipango/ mikakati yako na matumizi yako kwa kile ambacho tayari umeshaanza kukifanya, ndipo wakupe mkopo wa kuongezea biashara yako.

Vinginevyo ukienda hoe hae, huna malengo au mipango, ni wazi kuwa hutaambulia chochote, kwasababu wanahofia kama tu hicho cha kwako kidogo kimekushinda kukitazama, ukiongezewa kikubwa utawezaje?

Kama cha kwako mwenyewe haukijali, utajali vipi vya wengine?. Kama unajiibia mwenyewe ofisini kwako, utayahurumiaje mashirika ya wengine uliyopewa uyasimamie..

Lakini kwa Mungu ni tofauti, ili akupe kitu chako mwenyewe, ni sharti kwanza ukijali cha mtu mwingine. Ni sharti kwanza uonyeshe uaminifu kile cha mwingine ulichowekewa dhamana.

Unataka Mungu akupe uchungaji wako, Atakuangalia Je ulishawahi kuwajali kondoo wa Mungu, katika hilo kanisa ulilowekwa chini yake sasa? Ulishawahi kuwahudumia kwa upendo kabisa na kuwajali kama Mungu anavyotaka, Kama hukuweza basi ni ngumu sana Mungu kukupa cha kwako.

Mtu anamwomba Mungu ampe watoto wa kulea, lakini watoto wa familia nyingine hawajali, wala hata hana mpango nao kisa tu hajawazaa yeye.. Mungu akishaona hivyo, anasema, hata akikupa wa kwako hutaweza kuwalea, ni heri tu ubaki hivyo hivyo ..

Leo watu wengi wanamwomba Mungu awape ofisi zao wenyewe, Je, pale ulipowekwa kama muajiriwa unatumika kwa uaminifu?.

Unataka Mungu akupe nyumba yako mwenyewe, Je! Umekuwa mwaminifu katika hiyo nyumba ya mwingine Mungu aliyokuweka chini yake? Unaijali, unaitunza, unaipa thamani kama vile ni ya kwako?

Chochote tunachokitaka kwa Mungu, tujue kuwa atatujaribu kwanza kwa kutuletea hicho hicho kutoka kwa wengine,aupime uaminifu wetu. Mungu alimpima Yusufu katika nyumba ya Potifa kama je! Atakuwa mwaminifu? Na alipouona uaminifu wake, ndipo akampa cha kwake, akawa waziri mkuu kule Misri.

Hata katika ufalme wa Mungu, hatutapewa miji yetu wenyewe tuimiliki kule kwenye mbingu mpya na nchi mpya kama hatutakuwa waaminifu hapa duniani, kwa utumishi Mungu aliotuwekea chini yake katika kanisa lake.

Ikiwa tunalegea legea, au tunavipuuzia vya Mungu, au tunafanya mambo ya aibu, tusahau kule kupewa chochote na Mungu wetu ili tumiliki.

Tafakari tena habari hii..

Luka 19:12 “Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.

13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.

14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.

15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.

16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.

17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.

18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.

19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.

20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.

21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.

22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;

23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?

24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.

25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.

26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho”.

Hivyo tuwe waaminifu, mahali popote Mungu alipotuweka. Kwasababu hiyo ndio itakayofungua milango ya kuwepa vya kwetu wenyewe.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KUWA MWAMINIFU KWA MANENO YAKO MWENYEWE,

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

Rudi nyumbani

Print this post

LITURJIA NI NINI? NA JE IPO KIMAANDIKO?.

Liturjia/Litrujia ni mwongozo wa jinsi ya kufanya ibada unaotumiwa na makanisa mengi.

Ibada inaundwa na vitu vikuu vitano, ambavyo ni Maombi, Neno, Matoleo, Sifa, na Meza ya Bwana. Vitu hivi vitano ndivyo vinavyoiunda ibada.

Kwahiyo ukiwapo mwongozo wowote wa jinsi ya kuviendesha vitu hivi, na mwongozo huo ukawekwa kwenye kitabu maalumu..Mwongozo huo ndio unaojulikana na wengi kama Liturjia.

Kikawaida hakuna kanisa lisilo na mwongozo, na ni jambo la kimaandiko makanisa yawe na mwongizo fulani, ili mambo yote yafanyike kwa uzuri na utaratibu..

1 Wakorintho 14:40 “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu”.

Kanisa lisilo na utaratibu, ni rahisi kushambuliwa na shetani na kuvurugwa.

Lakini sasa mwongozo huu unatakiwa ufanyika kwa kipimo fulani, sio uzidi mipaka hata kuchukua nafasi ya Roho Mtakatifu.

Mwongozo wa kanisa unapovuka mipaka, hata kuchukua nafasi ya Roho Mtakatifu ndani ya kanisa, mwongozo huo unageuka na kuwa sumu ya kuliharibu kanisa kiroho.

Kwamfano, kanisa linapoweka ratiba ya masomo na mahubiri ya mwaka mzima, na kuyaweka kwenye kitabu maalumu..kwamba jumapili hii, litasomwa Neno kutoka kitabu fulani, jumatano ni kutoka kitabu fulani, sura namba fulani, na mstari namba fulani..Hivyo kunakuwa hakuna ruhusa ya kufundisha jambo lingine lolote nje na utararibu huo (Liturjia hiyo).

Mfumo kama huo (Liturjia/Litrujia) unamzuia Roho Mtakatifu, na kumzimisha asifanye kazi ndani ya kanisa, na hivyo kudhoofisha nguvu ya kanisa..

Kwasababu hata Roho Mtakatifu akitaka kusema jambo lingine jipya kupitia mhubiri huyo, tayari kuna mfumo unaolizuia hilo unaosema, fundisha tu kilichopo kwenye liturjia.

Roho mtakatifu akitaka kuwafungua watu kwa njia ya maombezi, kunakuwa tayari kuna mfumo uliowekwa unaolizuia hilo, mtu akitaka kutoa unabii upo mfumo tayari unaomzuia, ambao unasema ni kusoma Neno tu, Roho akishuka na kuwaongoza watu kunena kwa lugha na kufasiri, kunakuwa na mfumo unaozuia hilo n.k.

Na maandiko yanasema..tusimzimishe Roho..

1 Wathesalonike 5:19 “Msimzimishe Roho”.

Sasa mfumo kama huo (au Litrujia hiyo), ni mpango wa adui.

Makanisa mengi sasa, hususani yale yanayojulikana sana ndio yamemzimisha Roho Mtakatifu kwa sehemu kubwa sana kupitia hizo Liturjia. Unakuta Kanisa kwa nje linapendeza, lina vutia, linawashirika wengi, lakini ndani halina Roho Mtakatifu..bali miomgozo ya wanadamu, na kanuni za kibinadamu.

Roho Mtakatifu ndio uhai wa kanisa, mtu yeyote au kanisa lolote likikosa Roho Mtakatifu hilo sio kanisa la Mungu tena, bali la wanadamu (Warumi 8:9).

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba, Liturjia ni nini?.. ni mifumo ya wanadamu ya jinsi ya kufanya ibada, na katika zama hizi, Litrujia zote zimezidi kimo cha Kristo na hata kuchukua nafasi za Roho Mtakatifu.

Hivyo hatuna budi kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu na si Liturjia zetu zilizomzimisha Roho Mtakatifu.

Utaratibu bora ni ule wa kupanga muda wa ibada, siku za kukusanyika, utaratibu wa matoleo, ratiba za wakati wa maombi, na kujifunza biblia..(Na hata huo pia unaweza kugeuzwa kulingana na wakati na wakati, jinsi Roho atakavyo liongoza kanisa).

Na usiofaa ndio huo wa kupanga nini cha kufundisha cha mwaka mzima, na kukiweka kwenye kitabu… kamwe hatuwezi kumpangia Roho Mtakatifu nini cha kusema cha mwaka mzima, yeye anatoa ufunuo siku kwa siku, kwa jinsi atakavyo yeye..na sio sisi tumpangie cha kusema kupitia liturjia zetu, huo ni mpango wa adui wa kuliharibu kanisa.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

Nini maana ya kuabudu?

Rudi nyumbani

Print this post

Furaha ni nini?

Furaha kwa tafsiri ya kawaida, ni muhemko chanya wa kihisia unaotakana na aidha kuridhishwa na jambo fulani au kupata kitu fulani.

Kwa mfano katika biblia Wale mamajusi walipoina tena ile nyota  ya Bwana kule Bethelehemu, walifurahi.

Mathayo 2:10 “Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno”.

Utaona pia wale waliokwenda kaburini kwa Yesu,Na kukuta ameshafufuka, Biblia inasema walifurahi sana.

Mathayo 28:8 “Wakaondoka upesi kutoka kaburini, kwa hofu na furaha nyingi, wakaenda mbio kuwapasha wanafunzi wake habari”.

Hata mbinguni malaika wanapoona mtu mmoja ametubu dhambi, huwa wanafurahi pia.

Luka 15:10 “Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye”.

Kwahiyo utaona hapo furaha tunayoijua,  huwa inazaliwa kutokana  na kupatikana kwa kitu fulani kilichokuwa kinatarajiwa au jambo fulani.

Lakini furaha halisi ya ki-Mungu.  Ni furaha inayozidi mipaka, , hata katika shida furaha hii ipo. Ni furaha ambayo huwezi kuielezea kwa upatikanaji tu, kama furaha nyingine, inazidi mipaka hiyo.. Kwa kifupi ni kuwa haiathiriwi na hali au mazingira.

Na furaha yenyewe inaletwa na KRISTO YESU mwenyewe.

Ikiwa na maana mtu anayempokea Kristo, kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. Mungu anakuwa na jukumu la kumininia furaha hii kwa Roho Mtakatifu atakayempokea kipindi hicho.

Warumi 15:13 “Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu”.

1Nyakati 16:27 “Heshima na adhama ziko mbele zake; Nguvu na furaha zipo mahali pake”.

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.

Luka 2:10 “Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;

11 maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana”.

Yokobo 1:2 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;

3 mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”

1Petro 4:13 “Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe”.

Kwa muda wako pitia vifungu hivi

1Petro 1:8, Yohana 17:13

Na wewe ikiwa ni mmojawapo wa wale wanaotaka kuonja FURAHA hii ya Ki-Mungu ambayo si watu wote wanaweza kuonjeshwa utakuwa umefanya uamuzi wa busara sana. Kwasababu ni kwake tu peke yake ndipo Furaha inapopatikana, hakuna mwingine, Bwana anasema hivi;

Zaburi 5: 11 “Nao wote wanaokukimbilia watafurahi; Watapiga daima kelele za furaha. Kwa kuwa Wewe unawahifadhi, Walipendao jina lako watakufurahia”.

Zaburi 51:12 “Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi.

Unaona? Basi fungua leo moyo wako, Kristo aingie ndani yako, kukusamehe, na kukuwekea furaha idumuyo. Ikiwa Upo tayari leo kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.

Bwana akubariki.

Wafilipi 4:4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

Unyenyekevu ni nini?

Gombo ni nini?

Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.

Rudi nyumbani

Print this post