Category Archive Home

Makao ambayo Yesu alikwenda kutuandalia ni yapi?

SWALI: Yesu alimaanisha nini kusema ninakwenda kuwaandalia makao? Ni makao yapi hayo alikwenda kutuandalia.


JIBU: Tusome,

Yohana 14 :1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.

3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”.

Makao ni mahali ambao mtu ataweza kutulia na kuendesha aidha maisha yake au kufanya shughuli zake kama alivyokusudia yeye mwenyewe kwa utulivu.. Mtu asiyekuwa na makao yoyote, (yaani haishi kwenye nyumba, au kibanda) utagundua kuwa maisha yake ni ya kutanga tanga leo utamwona huku kesho kule, leo utamsikia yupo mji huu, kesho ule..hiyo yote ni kwasababu hana mahali pa kutulia. Anakuwa kama mgeni duniani.

Sasa ndivyo ilivyo pia katika roho, Mungu alipomuumba mwanadamu, alikuwa ni roho kamili, lakini sasa alipokusudia mwanadamu huyu aishi hapa duniani, alimuundia na makao yake maalumu (yaani Nyumba ya roho yake) ambayo ndio mwili,. Sasa mwili huo unamsaidia, aweze kuishi, kutulia, na kuipumzisha roho yake akiwa hapa duniani.

Na ndio maana mwili unaitwa nyumba ya roho. Lakini pia kuna roho nyingine ambazo zipo hapa duniani, ambazo hazikuumbiwa makao,(yaani miili), na roho hizo ni mapepo, ambayo Mungu aliyatupa dunia baada ya kuasi zamani sana miaka mingi kabla ya mwanadamu kuumbwa.

Sasa hizi roho kwasababu hazina miili ya kutulia, huwa zinazurura zurura hapa duniani bila kazi yoyote, hivyo zinachofanya ni kufanya bidii zote, kutafuta makao, na ndio hapo zinawaingia wanadamu ambao wapo nje ya wokovu. Zikishawaingia mule ndio zinapata pumziko. Lakini zikiwa nje, hakuna raha yoyote, na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.

44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.

45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”.

Umeona hiyo ndio kazi yao..kwasababu hawana maskani (Nyumba /Miili), hivyo huwa wanafanya juu chini, wakimwingia mtu wasitoke na kwenda kuzurura zurura tu.

Kwahiyo, tunaweza kuona hapo, mwanadamu anazo maskani mbili Na zote hizo ni nguzo muhimu za kumsaidia kuishi hapa duniani.

Maskani ya kwanza ni mwili wake mwenyewe, ambao Mungu kamwekea roho yake ndani yake. Na maskani ya pili ni nyumba/kibanda, ambayo anaweza kutulia ndani yake na kuishi na kuendeleza maisha yake.

Vivyo hivyo na huko mbinguni.

Tutakapofika kule zipo maskani za aina mbili, maskani ya kwanza, itakuwa ni hiyo miili ya kimbinguni, na maskani ya pili, itakuwa ni makao, kama makao, miji na majumba ya sisi kuishi.

Sasa Bwana Yesu aliposema anakwenda kutuandalia makao, alimaanisha yote, makao ya roho zetu, na makao ya hiyo miiili tutakayoipokea huko mbinguni.

Kumbuka miili hiyo haitakuwa kama hii inayoona uharibifu, iliyotengenezwa kwa udongo, hapana bali miili hiyo imeundwa na Mungu mwenyewe, Isiyougua, isiyozeeka, isiyosikia njaa, isiyo sinzia, isiyochoka.. Bwana Yesu alirahisisha akasema tutafanana na malaika, Kama vile tunavyowaona malaika na sisi ndio tutakuwa hivyo.

2 Wakorintho 5 :1 “Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni.

2 Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni;

3 ikiwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tu uchi.

4 Kwa sababu sisi tulio katika maskani hii twaugua, tukilemewa; si kwamba twataka kuvuliwa, bali kuvikwa, ili kitu kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima:.

Umeona, hivyo, siku ile ya unyakuo, ndipo tutapokea miili hiyo mipya ya kimbinguni, lakini ni sharti kwanza turudishwe kwenye miili yetu hii ya udhaifu, kisha ivaliwe na ile mipya, ndio tuende mbinguni. unaweza kujiuliza ni kwanini Mungu afanye vile, anafanya hivyo ili kutimiza maandiko yake kuwa hata nywele za vichwa vyetu zimehesabiwa, hakuna hata kimoja kitakachopotea (Mathayo 10:30).

1Wakorintho 5:51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

53 Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.

54 Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda”.

Pengine leo hii unaoudhaifu Fulani katika mwili wako, lakini ukifika kule, hutauona huo udhaifu.  Hivyo tukaze mwendo tuyafikilie hayo tuliyoandaliwa. Na hiyo Yerusalemu mpya wa kimbinguni, ambayo itakushuka kutoka kwa Mungu mwenyewe. Miji mizuri yenye kuvutia na kupendeza. Mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Hayo ndiyo makao ambayo Bwana Yesu alikwenda kutuandalia sisi kwa miaka 2000 sasa.

Bwana atutie nguvu.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

Mafundisho

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia ilimaanisha nini watu wasitoe vizazi vyao kwa Moleki?

Moleki ni nani? Na Kwanini Mungu alikataza watu kutoa vizazi vyao na kuwapa Moleki?

Walawi 20: 1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Tena uwaambie wana wa Israeli, Mtu awaye yote miongoni mwa wana wa Israeli, au miongoni mwa wageni waketio katika Israeli, atakayetoa katika kizazi chake na kumpa Moleki, sharti atauawa; wenyeji wa nchi watampiga kwa mawe.


Moleki ni mungu aliyeabudiwa katika nchi ya kaanani na nchi za kando kando, kama vile Amoni, mungu  huyu alikuwa tofauti na miungu mingine ya kipagani, kama vile Baali, kwani huyu, alihitaji kafara za watu ili kuwapa watu mahitaji yao. Walichokuwa wanakifanya ni kuwapitisha watoto wao katika moto na kuwatoa kafara.

Jambo ambalo Mungu aliwaonya na kuwakataza sana, wana wa Israeli tangu wakiwa jangwani, kabla hawajaiingia hiyo nchi ya ahadi kwamba watakapofika wasijihusishe na miungu hiyo ya uongo kwa namna yoyote ile, kwani Mungu alijua watu wake watakutana nayo.

Utalisoma hilo tena katika..

Walawi 18:21 “Nawe usitoe kizazi chako cho chote na kuwapisha kwa Moleki, wala usilinajisi jina la Mungu wako; mimi ndimi Bwana”.

Lakini pamoja na hayo, wana wa Israeli waliyakaidi maagizo ya Mungu wakaanza kuiga taratibu hizo za kishirikina za kuwatoa watoto wao kafara. Jambo hilo tunaweza kuona lilianzana  kwanza na mfalme Sulemani, ambaye ndiye aliyekuwa wa kwanza kabisa kumjengea madhabahu  mungu huyo katika Israeli, na hivyo ikawa chukizo kubwa sana. Na hiyo ndio ilikuwa sababu ya Mungu, kumshusha viwango mfalme Sulemani.

1Wafalme 11:7 “Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni”.

Mambo hayo waliendelea kufanyika Israeli kwa kipindi kirefu, wengine wakidhani kuwa ni Mungu kaagiza, au kwamba Mungu ndio anavutiwa na kafara hiyo kuliko ya mbuzi na kondoo. Lakini hawakujua kuwa ni mambo ambayo yalikuwa ni machukizo makubwa sana kwa Mungu.

Yeremia 32:35 “Tena walijenga mahali palipoinuka kwa Baali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwapitisha wana wao na binti zao katika moto kwa ajili ya Moleki, jambo nisilowaagiza; wala halikuingia moyoni mwangu kwamba walitende chukizo hilo; wapate kumkosesha Yuda”.

Ni nini Bwana anataka tujifunze kwa watu hawa?

Kuchanganya desturi za miungu ya kipagani na ibada za Mungu muumba wa mbingu na nchi, ni mambo ambayo yanaendelea hata sasa hivi katika agano jipya.

Kwamfano kitendo cha kuweka sanamu za watakatifu walitaongulia, na kuabudu kupitia hizo, kufuatana na desturi zao, ambazo hazipo katika maandiko, ni machukizo makubwa sana. Kusali Rozari, ni machukizo kwa Mungu, vilevile kudhani kuwa wapo wapatanishi wengi kati ya Mungu na wanadamu, na Yesu ni mmojawapo tu ya wapatanishi hao,hayo ni makufuru mbele za Mungu. Kwani biblia inasema mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ni mmoja tu, naye ni Yesu Kristo hakuna mpatanishi mwingine.

Hivyo ni lazima tuwe makini sana na tunachokiabudu, kwasababu hapo ndipo wivu wa Mungu unapolala. Tukijifanya hatuoni, tujue kuwa Mungu hatauvumilia upumbavu wetu, kama alivyofanya kwa wana wa Israeli. Kwasababu yeye mwenyewe ametuita tumwabudu katika Roho na Kweli na si katika ujinga na upagani.

Jina la Bwana libarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe,  Nakukaribisha katika kujifunza elimu ya ufalme wa mbinguni. Kumbuka kila habari katika biblia inayo ujumbe fulani nyuma yake. Hakuna habari isiyo na maana.

Leo kwa ufupi tutatazama habari ya mwamuzi mmoja aliyeitwa, Ehudi. Sasa wakati tunakwenda kutafakari habari zake naomba ufahamu kuwa Lengo la somo hili, ni kuamsha ile karama iliyo ndani yako ili  itende kazi..

Kuna wakati wana wa Israeli walimkosea sana Mungu, hivyo Mungu akawaweka chini mkono wa adui yao aliyeitwa Elgoni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka 18. Lakini walipomlilia Mungu, Mungu akawasikia  na kuwatumia huyu mwamuzi aliyeitwa Ehudi.

Biblia inatuambia Ehudi alikuwa ni mtu anayetumia SHOTO. Sasa biblia mpaka iandike habari kama hizo za mkono mtu anaotumia, inamaana kuwa lipo jambo la kujifunza. Ukisoma habari yenyewe pale utaona walimchukua huyu na kumpeleka kwa huyo mfalme wa Moabu ili awasilishe tunu zao ambazo walikuwa wanazipeleka kwa huyo mfalme mara kwa mara.

Sasa siku alipoenda, aliundaa upanga mrefu, kisha akauficha kwenye paja lake la kulia. Na alipofika mbele ya askari wake akazitoa zawadi hizo mbele yao..Lakini alipomalizia, hakuondoka bali aliomba aongee na mfalme faragha, kana kwamba kuna ujumbe amepewa na wakuu wa Israeli utokao kwa Mungu, amwambie, hivyo haipasi kila mtu asikie.

Ndipo mfalme akamchukua peke yake katika ukumbi wake, akawaondoa askari wake, akafunga milango. Sasa biblia inatuambia huyu Elgoni alikuwa ni mtu mkubwa sana, mwenye mraba minne, kiasi kwamba ili kumdondosha mtu kama huyo ilihitaji watu wengi, na sio mmoja tena wenye nguvu.

Lakini Mungu alilijua hilo,  na ndio maana akawatumia mtu kama Ehudi anayetumia shoto na si kilia ili kumdondosha huyo.

Kama tunavyosoma habari, aliutoa ule upanga wake, na kwa nguvu aliuzamisha kwenye Tumbo lake, ambalo pengine lilikuwa limefunikwa kwa nguo nzito, lakini upanga  ule ulipita kwa jinsi zile nguvu zilivyokuwa nyingi, kisha ukaenda kushikamana na mafuta ya tumboni na kutokea upande wa pili.. Lakini ni heri tu ungeingia upanga peke yake, biblia inasema, mpaka ule upini wa upanga ulizama ndani kabisa, usionekane. Jambo ambalo si rahisi hata kidogo kwa mtu kuuzamisha upini kwenye tumbo. Inahitaji presha kubwa sana ya kusukuma, ambayo kwa nguvu za kawaida za kibinadamu haiwezekani.

Waamuzi 3:21 “Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake;

22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma”.

Unaona, ukisoma tena, utaona tena hata katika vita zamani, wana wa Israeli waliwachagua mashujaa wanaotumia shoto, kwasababu aliweka uwezo mkubwa sana wa shabaha ndani yao.

Waamuzi 20:15 “Hao wana wa Benyamini walihesabiwa siku ile kutoka hiyo miji, watu waume ishirini na sita elfu waliotumia upanga, zaidi ya hao waliokaa Gibea, ambao walihesabiwa watu wateule mia saba.

16 Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose”.

Tukiyafahamu haya turudi sasa katika kiini cha ujumbe wetu wa leo, kwasababu lengo sio kueleza umahiri wa watu wanaotumia shoto au kulia, hapana. Bali ni kutufundisha sisi mambo ya rohoni yahusuyo wokovu wetu.

Kumbuka mkono huu wa kushoto huwa haupewi heshima, wala hauwezi kutumiwa sehemu zote, hauwezi kutumia kulia chakula, au kumpia mtu mkono, n.k. Lakini uwezo na nguvu Mungu alioupa unazidi hata ule wa kulia.

Hiyo ni kuonyesha pia, Mwili wa Kristo unao viungo vingi, vingine Mungu amevikusidia kabisa vipewe  heshima, lakini vingine Mungu amevikusudia pia visiwe na heshima yoyote, lakini vimepewa nguvu na ufasaha wa hali ya juu.

1Wakorintho 12:23 “Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana.

24 Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;

25 ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe”

Umeona? Ni lazima tufahamu si kila mtu atakuwa mchungaji, si kila mtu atakuwa mtume, si kila mtu atakuwa nabii, si kila mtu atakuwa mwalimu, zipo karama nyingi nzito na zenye nguvu  ambazo watu wanazo lakini wamezizimisha ndani yao kwasababu  wanachofikiria tu ni kuwa pale watakapokuwa wakristo basi ni kwenda kuwa wachungaji, au mitume au watu fulani maarufu wanaojulikana.

Na ndio maana karama nyingi za kipekee kama za miujiza, uponyaji, karama za ufasiri wa lugha, karama za faraja, za kukirimu n.k. hazionekani au zimekufa kabisa katika kanisa, kwasababu hatuziangalii hizo sote tunataka tukawe mitume, wachungaji na manabii.

Ukiona lipo jambo linaamka ndani yako kwa ajili ya Mungu, ambalo pengine lipo tofauti na wengine na unaona kabisa  linakupa furaha kulifanya, usilizimishe, lifanye hilo kwa bidii kwasababu huo ndio mwanzo wa kuijua karama yako. Na Mungu ameiweka hiyo ndani yako ili ilisaidie kanisa kwa sehemu kubwa sana. Fanya kile kitu kinachougua ndani yako sana.. Kama ni kumtolea Mungu, basi mtolee sana, kama ni kufundisha basi fundisha sana, kama ni kufanya uinjilisti ufanye huo kwa bidii, kama Mungu anakuonyesha mambo ya rohoni, yachochee hayo ili yakawe faida kwa mwili wote wa Kristo.

Kumbuka hakuna kiungo kisichokuwa na kazi  kanisani, maadamu umeokoka na umejazwa Roho, umuhimu wake ni lazima utaonekana tu. Lakini kazi ya kiungo ni ngumu kuonekana kama kitakuwa chenyewe chenyewe, hivyo kaa na watakatifu wengine, ndipo hapo utajua kwa urahisi karama yako ni ipi. Karama nyingine haziwezi kufanya kazi kama zitakaa zenyewe nyumbani,

Jitahidi ujue nafasi yako ni ipi ili umtumikie Mungu katika hiyo. Kwasababu kila mmoja wetu anatarajiwa na Bwana amzalie matunda.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

USINIE MAKUU.

Neno “Via” linamaanisha nini katika biblia?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Mchokoo ni nini katika maandiko? (Matendo 26:14)

Rudi nyumbani

Print this post

Kama Musa aliandika vitabu vya torati, Je! kifo chake alikiandikaje mule?

SWALI: Ukisoma kitabu cha kumbukumbu la torati sura ya 34 unaona Musa anakufa na kitabu kinaendelea kuandika mpaka kifo chake, je huoni kuwa ni makosa kusema vitabu vitano vya kwanza vya Biblia vimeandikwa na Musa? maana mtu hawezi kuelezea kifo chake kuwa amekufa lini na kuzikwa lini?asante.


JIBU: Kuhusu uandishi wa Musa juu ya kifo chake, pia hilo linawezekana, kumbuka Musa alikuwa ni mtu ambaye alikuwa karibu sana na Mungu, hivyo Mungu kumfunulia mambo yajayo sio jambo la kushangaza sana, kama aliweza kumfunulia mambo yaliyopita, tangu Adamu, na mambo yote yaliyotendeka pale Edeni, mpaka Nuhu na Gharika yake, mpaka sodoma na Gomora, angeshindwaje kumfunulia kifo chake na kukiandika?

Lakini pia, inawezekana, waandishi wengine walimalizia kitabu hicho kwenye ile sura ya  34, kama vile Yoshua, ambaye alikuwa  karibu sana na Musa, au Eleazari, ambaye alikuwa mtoto wa Haruni,mkuu wa kabila la lawi, mwingine ni  Samweli, au Ezra.

Hivyo Kwa vyovyote vile, tunapaswa tujue biblia ni kitabu kilichovuviwa na Roho Mtakatifu, na hivyo yapo matukio ambayo waandishi wake tunaweza tusiwajue moja kwa moja kwasababu lengo la kitabu kile sio kuwaeleza wao, bali ni ule ujumbe uliopo ndani yake.

Hivyo cha muhimu ni Bwana azidi kutupa macho ya kuyaelewa yote yaliyoandikwa ndani yake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe. Naomba ya nifafanulie juu ya “kujikana mwenyewe” na “kujitwika msalaba” wako inamaanisha nifanye nini hasaa?


JIBU: Tusome..

Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.

35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.

36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?

37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake”?

Kujikana ni kukataa mapenzi yako na kukubali kufuata yale ya Mungu, haijalishi yatakuwa hayakupendezi au hayakufai kwa wakati huo namna gani.

Pale ambapo, Mungu anataka ufanye hivi, na wewe unaona nafsi yako haitaki kukifanya, kwasababu moja au nyingine. sasa kule kutii cha Mungu na kukataa cha kwako huko ndiko kujikana nafsi.

Kwamfano Mungu anaposema wanawake wavae mavazi ya kujisitiri,(1Timotheo 2:9) na wewe ni mvaaji mzuri wa nguo zinazochora maungo na zile za kiume, sasa unapokubali kutii yale ya Mungu, ukaanza kuvaa magauni, bila kujali nafsi yako inakuambia utakuwa mshamba, au watu watakuambia hupendezi, huko ndiko kujikana nafsi.

Au pale Mungu anapokuambia, kiungo chako kimoja kikikukosea kikate, kuliko mwili mzima kutupwa jehanamu, na kama tunavyojua kiungo ni kitu kinachojishikamanisha na wewe. Na vitu vinavyojishikamanisha na maisha yetu ni vingi, vingine vizuri, vingine vibaya, sasa pale ambapo, pengine  marafiki ulionao wanakukosesha, na kuchukua uamuzi wa kukata nao mazoea, na kuanza kutafuta marafiki wenye malengo na kimbingu na wewe, hapo ndipo umejikana nafsi.

Unapoacha, miziki ya kidunia, au kukesha kwenye muvi na kuchati  kwenye mambo yasiyokuwa na maana, na kuutumia muda huo kumtafakari Mungu, au kumtafuta yeye, huko ndiko kujikana nafsi Bwana Yesu anakokuzungumzia.

Pia Kujitwika msalaba, ni ishara ya kukubali dhiki kwa ajili ya Kristo. Kumbuka msalaba ni kitu ambacho Yesu alikibeba na kwenda kusulubishwa kwa hicho. Sio kitu ambacho alikwenda kukilalia. Ni sawa na mtu leo hii akuambie jivike mabomu yako, uende sehemu ya kujilipua.

Hivyo na sisi ili tuwe wanafunzi wa Kristo kweli, hatuna budi pia kukubali mashutumu na wakati mwingine kupitia dhiki kwa ajili ya jina lake. Hapo ndipo tutakuwa tumeonyesha tumeibeba misalaba yetu kweli kweli. Alama ya misumari yetu.

Biblia inasema..

2Timotheo 3:12 “Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa”.

Wafilipi 1:29 “Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;”

Na pia Bwana Yesu alisema..

Yohana 15:20 “Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.

Hiyo ndio maana ya kujikana nafasi na kujitwika msalaba wako.

Bwana atujalie tuwe na moyo huo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

ESTA: Mlango wa 4

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Rudi nyumbani

Print this post

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

Mungu anayo agenda, na usipojua agenda ya Mungu katika siku hizi za mwisho ni ngumu sana kuiona ile ng’ambo, Leo hii tunaishi maisha ya juu juu tu kwasababu hatujamjua YESU ni nani na tabia zake ni zipi kulingana na majira ya wakati.

Tunapenda kumjua tu katika ule upande wake mmoja, wa upole na unyenyekevu (Mathayo 11:29)..Lakini hatujui ule upande mwingine ambao anasema yeye ni MKEMEAJI, na MKANAJI, na MFUKUZAJI na MUUAJI WA WAOVU. Ikiwa leo hii hatutamwamini, halafu tukafa, au siku ile ya mwisho ikatukuta tupo katika njia zetu wenyewe, tujue kuwa tabia tutakazoziona kwake kipindi hicho zitatustaajabisha sana, tena sana.

Kanisa hili la mwisho tunaloishi linaloitwa Laodikia, ndio kanisa pekee kati ya yale saba, ambalo Bwana amelikemea vikali, kwa tabia zake, za kuwa vuguvugu.. Hii ikiwa na maana kuwa mimi na wewe kama tupo katika uvuguvugu huu uliopo sasa hivi duniani tujue kuwa tupo katika Hasira ya Kristo, ya kwenda kutapikwa.

Uvuguvugu wa kusema mimi nimeokoka, lakini maisha yako hayauhakisi wokovu ule wa kimaandiko, ndio tabia ya kanisa hili la mwisho ilivyo, mamilioni ya wakristo ndio hivyo walivyo leo hii. Jambo ambalo halikuwepo miaka ya zamani, ambayo watu hawakumchanganya Mungu na uovu, waliookoka walijulikana, waliokuwa waovu walijulikana. Hakukuwa na mtu aliyeshiriki meza ya Bwana na wakati huo huo ni mzinzi au mlevi, mtu anakwenda ibadani, halafu kesho pia anakwenda disco, hayakuwepo hayo. Waovu walijitenga, na watakatifu waliookolewa walijitenga, Lakini leo hii ni kawaida sana, kusikia hata mmiliki bar anasema ameokoka.

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

3.16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi NAWAKEMEA, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami”.

Lakini pia hakemei tu peke yake, kuna siku atasimama KUWAKANA na kuwaonea aibu watu wengi sana, mbele ya Baba yake, na mbele ya  maelfu ya malaika zake huko mbinguni. Ikiwa leo hii unamwonea Kristo aibu unaogopa kuitwa mlokole, unaogopa kuvaa vizuri mavazi ya kujisitiri kisa utaitwa mshamba, unaona aibu kumtumikia Mungu wako, siku ile utakuonea aibu na wewe kweli kweli, hata hatapeleka jicho lake kukangalia.. wakati wengine akiwapongeza na kuwasifia.wewe utakuwa kama mtu baki tu.

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Halikadhalika na kumkana vivyo hivyo, naye pia atakukana siku ile.

Kama hilo halitoshi Bwana Yesu pia anasema, atawafukuza watu wengi sana, siku ile, sio wachache, bali wengi sana. Na watakaofukuzwa sio watu wasiomjua Kristo bali, ni sisi sisi tuliopo kanisani, tunaolitumia jina lake kutenda miujiza lakini hatutaki kuishi maisha yampendezayo yeye. Tunapenda maisha ya uvuguvugu.

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Biblia bado inatuonyesha siku ile atakapotokea mawinguni atawaua wanadamu wengi sana watakaokuwa wameipokea ile chapa ya mnyama na kufanya vita naye..

Ufunuo 19:13 “Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana”.

Unaweza kuona jinsi mwonekano wa Bwana utakavyokuwa wa tofauti sana wakati ule?. Ndio hapo utakapojua ni kwanini biblia inasema mataifa watamwombolezea, kwasababu hatakuja tena na sura ya upole kama wengi wetu tunavyodhani, bali atakuja na jina jipya la kifalme, la kuteka na kutawala, la kutiisha lenye nguvu nyingi. Sio tena la kuokoa mtu.

Lakini kwa upande wa pili, kwa wale waliomtii, waliokubali kutembea katika njia zake, anasema atawakiri, na kuona fahari kwa ajili yao mbele za Mungu na za malaika wake, vilevile atawapa mamlaka ya kutawala pamoja naye kama wafalme, Na atawafuta machozi watakatifu wake wote.

Hivyo ndugu, leo hii Kristo bado kaketi kama mwana-kondoo, aliyechinjwa, mpole, mnyenyekevu, aokoaye, anakuvuta kwa upole mwingi kwake, ili usiopote katika aungamivu wa ulimwengu. Angalia wakati huu umebakia mchache sana, kabla ya yeye kwenda kubadilisha ofisi yake. Kwanini usitubu umrudie muumba wako?

 Damu yake bado ipo kukuokoa, na kukusamehe kabisa, mkaribishe leo kwenye moyo wako, akupe uwezo mpya wa kuushindwa huu ulimwengu. Pengine ulishamwamini au kumpokea lakini umekuwa mkristo vuguvugu mkristo jin, jambo ambalo ndio halitaki kabisa, amelikemea, hivyo toka kwenye huo uvuguvugu wako, toka katika udhehebu, mfuate Yesu kweli kweli, ondoa vizuizi vyote vinavyokufanya usiwe safi mbele za Mungu.  Na yeye mwenyewe atakutengeneza na kukufanya uwe tayari kwa ajili ya kwenda kwenye unyakuo ambao upo karibuni kutokea.

Natumai sote tutaanzana kuuonyesha mabadiliko mapya. Kabla ya mabadiliko yake hayajajidhihirisha kwetu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

UFUNUO: Mlango wa 2 part 3

UFUNUO: Mlango wa 14

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

UFUNUO: Mlango wa 19

Rudi nyumbani

Print this post

Neno Maganjo linamaanisha nini katika biblia?

Maganjo ni kitu kilichoharibiwa, kwa mfano jengo likiharibiwa labda tuseme kwa  kombora, lile gofu linalobakia ndio maganjo. Au mji unapochomwa moto, yale masalia salia ya mji, ndio maganjo.

Mungu amekuwa akitumia Neno hili kuonyesha jinsi adhabu yake itakavyokuwa kwa wasiomcha yeye.

Hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utaweza kukutana na Neno hilo;

Walawi 26:30 “Nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, na kuziangusha sanamu zenu za jua, nami nitaitupa mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu; na roho yangu itawachukia.

31 NAMI NITAIFANYA MIJI YENU IWE MAGANJO, na mahali penu patakatifu nitapatia ukiwa; wala sitasikia harufu ya manukato yenu yapendezayo.

32 Nami nitaitia hiyo nchi ukiwa; na adui zenu watakaokaa huko wataistaajabia”.

Ezekieli 6:14 “Nami nitanyosha mkono wangu juu yao, na kuifanya nchi kuwa MAGANJO, tena ukiwa mbaya kuliko jangwa upande wa Dibla, katika makao yao yote; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana”.

Yeremia 51:42 “Bahari imefika juu ya Babeli, Umefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.

43 Miji yake imekuwa MAGANJO; Nchi ya ukame, na jangwa; Nchi asimokaa mtu ye yote, Wala hapiti mwanadamu huko”.

Yeremia 4:7 “Simba ametoka katika kichaka chake, ndiye aangamizaye mataifa; ameanza kushika njia, ametoka katika mahali pake; ili aifanye nchi yako kuwa ukiwa, miji yako ifanywe MAGANJO, asibaki mwenyeji ndani yake. 8 Kwa sababu hiyo jifungeni nguo za magunia; ombolezeni na kulia kwa uchungu; kwa maana hasira kali ya Bwana haikugeuka na kutuacha”.

Som pia Ezekieli 12:20, 29:12, Amosi 9:14

Hata sasa, huu ulimwengu, utakwenda kufanywa maganjo kipindi si kirefu, haijalishi umejengwa vizuri kiasi gani, haijalishi umeshafikia hatua ya kuwa ustaarabu mzuri namna gani,..Bwana Yesu alisema kuwa hakuna jiwe litakalosalia juu ya jiwe. Kila kitu unachokiona leo hii kitateketezwa, siku ile ya Bwana itakapofika. Kila kitu kitafumuliwa, moto utaisafisha kweli kweli hii dunia, kama vile gharika ilivyoisafisha dunia ya kwanza wakati ule wa Nuhu.

Soma.

2Petro 3:10 “Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,

12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka”?

Swali ni je! Mimi na wewe tumeekeza wapi maisha yetu?  Je ni duniani au mbinguni?..Kumbuka duniani ni tunapita, yapo maisha ya milele huko mbeleni yanatungojea.. Ni wajibu wetu kutambua lililo la muhimu kwanza, ambalo ni wokovu wetu, Lengo la Mungu kuifanya hii dunia kuwa maganjo si kwamba ni mbaya hapana, bali sisi ndio tumeifanya kuwa mbaya kwa dhambi zetu, na hivyo ni lazima iteketezwe tu.

Hivyo sisi sote tusiwe washirika wa hiyo ghadhabu ya Mungu. Kumbuka Unyakuo upo mlangoni. Na haya mambo hatutashangaa kuyaona yakitimia hata kwenye kizazi chetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

KWA WALE WALIO NJE “YOTE” HUFANYWA KWA MIFANO.

UFUNUO: Mlango wa 14

Sodoma ipo nchi gani?

Rudi nyumbani

Print this post

KWA WALE WALIO NJE “YOTE” HUFANYWA KWA MIFANO.

Nakusalimu katika jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo, ambaye yeye peke yake ndiye Mungu, aliyeshuka katika mwili wa kibinadamu kutukomboa sisi.

Yapo mambo ambayo hatuwezi kudhania kama Bwana Yesu angeyafanya alipokuwa hapa duniani.. Japo alikuja kweli kutuokoa, lakini hakuufanya wokovu kuwa mrahisi kiivyo kama wengi tunavyodhani.

Yesu havutiwi na wingi wa watu  wanaokuja  kumsikiliza, au wanaosema wanamfuata, hilo halimshawishi hata kidogo kutoa siri zake zote za wokovu. Wakati ule kulikuwa na umati mkubwa wa watu, ambao walikuwa wakimfuata kila mahali,  wengine mpaka wanakanyagana, sasa unaweza kudhani Bwana angetumia fursa ile, kuwapa siri za Mungu wazi wazi.. Lakini biblia inatuambia hilo hakulifanya, badala yake alizungumza nao kwa mifano (yaani mafumbo). Na kama unavyojua mafumbo huwa hayampi tu majibu ya moja kwa moja, ikiwa na maana kuwa mtu anaweza akatoka hapo asipate jibu la wazo lako kama hatofikiria sana, au kutaka kuambiwa maana yake.. Unaweza kujiuliza kwanini afanye vile?

Bwana Yesu hataki kuwaokoa watu wasiomaanisha kweli kuutaka wokovu ndani ya mioyo yao. Haokoi wasikilizaji tu, bali watu wanaotaka kuelewa nini maana ya wokovu na wokovu huo unapatikanaje ndani ya mioyo yao. Na ndio maana alizungumza nao kwanza kwa mafumbo, na baadaye akawaambia wanafunzi wake kauli hii .”kwa wale walio nje, YOTE hufanywa kwa mifano”..Unaona? Hakusema “machache” hapana, bali YOTE.. Ikiwa na maana hakuna kufananuliwa chochote, ikiwa upo mbali na Kristo. Habari za Kristo zitakuwa mafumbo tu kwako, haijalishi wewe unamfuata kwenye mikutano yake, au unahudhuria semina zake nyingi kiasi gani.

Watu wengi waliomfuata Kristo walikuwa ni watembeleaji tu, wengine walimtafuta kwa ajili miujiza, wengine kama wapelelezi, wengine wasikilizaji tu wa kupoteza muda ili uende, wengine ni kuutazama mwonekano wake upoje, anavaaje,n.k…Hayo tu, hawana cha ziada..Wachache sana ndio waliokuwa wanatafuta kumjua yeye kwa kile alichokileta duniani, na ndio hao ambao baada ya mafundisho kuisha, walijiona nafsini mwao hakuna chochote walichokipata, zaidi ya stori stori tu, hakuna lolote lililowajengwa rohoni, ndipo wakamfuata akiwa peke yake, katika utulivu wakamwomba awafunulie siri za mifano ile… Hao ndio Yesu alikuwa amewakusudia wokovu.

Marko 4:10 “Naye alipokuwa peke yake, wale watu waliomzunguka, na wale Thenashara, walimwuliza habari za ile mifano.

11 Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, BALI KWA WALE WALIO NJE YOTE HUFANYWA KWA MIFANO,

12 ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije wakaongoka, na kusamehewa”

Leo hii, upo umati mkubwa sana katika kanisa, upo umati mkubwa sana wanaosema wanamtafuta Mungu kila mahali,.Wakidhani Yesu anavutiwa na kumtembelea kwao.

Hilo halipo, ikiwa mtu mwenyewe binafsi hataki kumtafuta Kristo akiwa peke yake, amsaidie, hataki kuonyesha bidii yake kwa Kristo kujifunza na kumtafakari, kukitendea kazi kile alichokisikia, asahau kuupokea wokovu wake halisi wa  kweli kweli.

Na ndio maana leo hii, utaona wokovu hauna nguvu yoyote ndani ya mioyo ya baadhi ya watu, mtu atasema ameokoka, lakini uzinzi unamshinda, ulevi unamshinda. Amekaa miaka mingi katika kanisa lakini hajui hata kama kuna jambo linaloitwa Unyakuo, hajui kama hili kanisa tunaloishi ndio kanisa la mwisho, lijulikanalo kama LAODIKIA kulingana na maandiko (Ufunuo 3), na kwamba hakutakuwa na kanisa lingine zaidi ya hili, hajui mpango wa Mungu kwa kanisa lake kwa wakati huu tunaoishi ni nini? Lakini atasema anamjua Kristo, na amemwona. Hajui kuwa hata watu wa kipindi kile walimwona Yesu, wakala naye, wakasikia sauti yake, wakaona miujiza yake mingi, lakini aliowafunulia siri za ufalme wa mbinguni ni wachache sana. Wale waliokwenda kutendea kazi kile walichokisikia.

Ndugu Bwana Yesu anawaokoa watu waliomaanisha kweli kweli, sio wasikilizaji tu, wasio na bidii yoyote, miaka nenda rudi, ni wasikilizaji tu wa mahubiri, makanisani,  mitandaoni, n.k.,  huwajishughulishi  kwa lolote kumtafuta Yesu binafsi, wakidhani kuwa Yesu amewafunulia tayari siri zake.

Huu wakati sio wa  kuwa vuguvugu, ni wakati wa kujitwika msalaba wako na kumfuata YESU. Kumbuka alisema..

Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.

25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.

26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake”?

Vinginevyo, tukiwa watu wasiomaanisha, kama wale makutano, tujue kuwa YOTE, ya Yesu, tutayasikia tu kama mifano.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

UFUNUO: Mlango wa 14

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA DEMA NA MARKO?

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

JIBU: Tusome,

Mithali 10:10 “Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka”.

Kukonyeza ni ishara inayojulikana  kama ya undanganyifu au ya kupoteza uaminifu. Ni jambo la kawaida tumekuwa tukiliona hata katika maisha ya kawaida, kwa mfano, labda mteja, mmoja amekwenda kununua bidhaa Fulani kwa muuzaji sokoni, Sasa ikatokea, ghafla muuzaji mwingine akakatiza anauza bidhaa kama ile ile, Ni kawaida ya mnunuzi  kutaka kuulizia bei halisi ya hiyo bidhaa kwa muuzaji mwingine, Sasa kama kweli yule muuzaji wa kwanza aliambiwa bei halali ,hatoonyesha chochote, lakini kama alitaka kumuuzia kwa bei ya juu Zaidi kuliko ilivyo kawaida, yule muuzaji wa kwanza atatumia ishara Fulani, aidha kumkonyeza muuzaji mwenzake, ili akae kimya..Asimwambie bei halali.

Sasa hiyo ni dalili ya kukosa uaminifu.

Mfano mwingine, utakuta labda mtu na familia yake wamealikwa kwenye sherehe fulani, na kule kwenye sherehe pengine baba wa familia hiyo akakutana na wanawake wengine wazuri, akawatamani, sasa njia ambayo anaweza kutumia kuwasiliana nao, kirahisi ili pengine baadaye wakutane, ni kwa kumkonyeza,..Huo ni mfano tu.

Umeona  kitendo hicho  kimetumika kama  ishara ya udanganyifu.

Biblia inasema..

Mithali 6:12 “Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu; Huenda njiani mwenye kinywa cha upotofu.

13 HUKONYEZA KWA MACHO, hunena kwa miguu, Huwaashiria watu kwa vidole vyake”

Na kukonyeza kwa siku hizi kumezidi hata kule kunakojulikana kwa kutumia jicho, zipo ishara nyingi za kukonyeza inategemea na mahali husika. Wakati mwingine hata lugha Fulani inaweza kutumika kukonyeza.

Sasa biblia inasema watu wa namna hiyo huleta masikitizo. Na masikitizo hayo huja kote kote, kwake, pamoja na kwa yule aliyemkonyeza. Ikiwa na maana mwisho wake hauwi mzuri sikuzote. Ni uchungu na majuto.

Biblia inatuonya tusiwe watu wa hila, za kutumia ishara za udanganyifu kuleta madhara, au uharibifu kwa wengine.

Hilo ni kosa.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Mfalme Ahazia alianza kutawala akiwa na umri gani?

SWALI: tukisoma  2Mambo ya Nyakati 22:2.Inasema Hivi..

“Ahazia alikuwa na umri wa miaka AROBAINI NA MIWILI ALIPOANZA KUTAWALA; akatawala mwaka mmoja huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Athalia binti Omri”.

NA tena Tukisoma  2Wafalme 8:26 inasema Hivi..

“;Ahazia alikuwa na umri wa miaka ISHIRINI NA MIWILI ALIPOANZA KUTAWALA; akatawala mwaka mmoja huko Yerusalemu. Na jina la mamaye aliitwa Athalia binti Omri mfalme wa Israeli”.

>>Hapa sijaelewa Kwenye Hizi Habari Kwa maana Kwenye 2Nyakati unasema Ahazia alianza kutawala akiwa na miaka 42 ila Kwenye 2Wafalme Inasema Ahazia alianza kutawala Akiwa na miaka 22..Naona Hii mistari Kama Inajipinga Yenyewe.

Umri hasaa wa Ahazia alipoanza kutawala ni upi?


JIBU: Vifungu hivyo vinaonekana kama vinajipinga, aidha kimojawapo kimekosewa au vyote, wengine wanasema ni hitilafu katika uchapishaji wa maandiko ya kale. Lakini kama ingekuwa ni hitilafu kwenye  uchapishaji, ni wazi kuwa tangu zamani Wayahudi wangeshaliona hilo na kulirekebisha, kwasababu wale wapo makini sana katika uandishi wao, hususani katika mambo matukufu ya Mungu,  lakini maandiko hayo yalikuwepo hivyo hivyo kwa maelfu ya miaka mbeleni. Na hawakuona hitilafu yoyote.

Lakini swali ni je, Ahazia alianza kutawala akiwa na umri wa miaka mingapi?

Ukweli ni kwamba alianza kutawala akiwa na miaka 22, kwasababu kama angekuwa ameanza kutawala akiwa na miaka 42, maandiko yangekuwa yamekosewa kwasababu utawala wa baba yake uliisha akiwa na umri wa miaka 40  (Soma 2Wafalme 8:17, 2Nyakati 21:20) . Hivyo, kama  Ahazi angekuwa ameanza kutawala akiwa na umri wa miaka 42 basi angekuwa amemzidi baba yake kwa umri wa miaka 2 zaidi jambo ambalo haliwezekani kabisa.

Lakini ni kwanini, sehemu nyingine ionyeshe alianza kutawala akiwa na miaka 22, na sehemu nyingine miaka 42?

Zipo thathimini nyingi, lakini tukitazama historia fupi  ya baba yake huyu Ahazia itatupa mwanga kidogo wa kuelekewa kwenye jibu letu. Baba yake huyu Ahazia aliitwa, Yehoramu. Yehoramu alikuwa ni mtawala mbaya sana mwenye uchu wa madaraka na ubinafsi, kwani hata Baba yake (Yehoshafati) alipokufa, licha ya kwamba aliwaachia mali nyingi yeye pamoja na ndugu zake, lakini pamoja na hayo alikwenda kuwaua wote, ili yeye avimiliki vyote.

Tendo hilo la kumwaga damu zisizokuwa na hatia za kuwaua ndugu zako, lilimuhuzunisha sana Mungu, ndipo Mungu akamlaani kwa kumpiga  na ugonjwa huo usiokuwa na tiba wa kutokwa na utumbo.

Hivyo, hilo lilimfanya asiweze, kutawala vema katika hali ile ya kuugua..akawa kama mtu wa kukaa ndani tu aliyetengwa.

Sasa kumbuka na biblia haieleze kama alikufa kwanza ndipo mtoto wake, akachukua ufalme, hapana, inasema, alianza kutawala akiwa na miaka32, kisha akatawala miaka 8 tu. Lakini haisemi kwamba alikufa, hapana, kwahiyo pengine aliendelea kuishi, kwa kipindi kingine mbele akiwa kama mfalme asiyekuwa na kazi yoyote.

Hiyo ikapelekea wenyewe wa Yerusalemu kumfanya mwanawe kuwa mfalme, hivyo Ahazia akawa mfalme akiwa na umri wa miaka 22, lakini hakuwa mfalme kamili kabisa,kwasababu baba yake alikuwa bado hajafa. Ndipo alipokuja kufa huko mbeleni, Ahazia tayari alikuwa ameshafikisha umri wa miaka 42, ndipo wakamfanya kuwa mfalme kamili wa Yerusalemu. Akatawala miaka mmoja tu. Ambao ulianza kuhesabiwa katika umri wake wa 42

Hivyo biblia  inaposema alianza kutawala akiwa na miaka 22 katika kitabu cha Wafalme, na miaka 42 katika kitabu cha Mambo ya Nyakati, biblia haijipingi, ni pengine tumekosa historia ya kutosha ya matukio yote ndani ya biblia ndio maana tunaona kama baadhi ya vifungu vimekosewa, lakini ukweli ni kwamba maandiko matakatifu hakuna mahali yalipokosewa..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Je! Ni ipi tarehe sahihi Evil-merodaki alimtoa Yekonia gerezani?

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

Biblia ilimaanisha nini iliposema “Mwanamke atamlinda mwanamume” Yeremia 31:22?

KURUDI ISRAELI KWASASA NI KUGUMU, SIO KAMA KULE MWANZONI.

Maseyidi 12 wa Ishmaeli, ni wakina nani?.2)Taa ya Mungu ambayo ilikuwa haijazima wakati wa Eli ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post