WALIYATWAA MAVAZI YAKE, WAKAFANYA MAFUNGU MANNE,

WALIYATWAA MAVAZI YAKE, WAKAFANYA MAFUNGU MANNE,

Yohana 19:23 “Nao askari walipomsulibisha Yesu, waliyatwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu.

24 Basi wakaambiana, Tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani. Ili litimie andiko lile linenalo, Waligawanya nguo zangu, Na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari”.

Ulishawahi kujiuliza ni kwanini biblia haijakaa kimya kuhusiana na mavazi ya Yesu pale Goligotha, na jinsi yalivyopigiwa kura? Mpaka kufikia hatua ya kugawanywa katika mafungu manne (4) kwa wale askari wanne waliokuwa pale msalabani.? Na lile moja la 5 ambalo ni kanzu yake kupigiwa kura?. Haikuandikwa kutengeneza stori tu, kwamba Yesu alikuwa na mavazi matano, bali kulikuwa na maana nzito nyuma yake.

Hiyo ni kuonyesha kuwa hakubakiwa na nguo hata moja muda ule alipotundikwa  pale msalabani. Alisulibiwa akiwa uchi kabisa wa mnyama. Ni jambo ambalo haliwezekani kwamba nguo nyingine zipigiwe kura, na kugawanya, halafu nyingine abakiwe nazo kutundikiwa msalabani, Maandiko hayatuonyeshi hivyo. Kile tunachokiona kwenye misalaba ya kuchonga au kwenye muvi  kwamba Bwana Yesu alisulibiwa akiwa na kipande cha nguo cha kumsitiri, si kweli. Ukweli ni kwamba alisulibiwa akiwa uchi kabisa wa mnyama. Hata hivyo wakati ule wa Rumi wahalifu wote waliouliwa kwa kusulibiwa ilikuwa ni lazima wasulibiwe uchi, ili kwamba sio tu wafe kwa mateso bali pia wafe kwa aibu.

Je! ulishawahi kutafakari kwa utulivu kwanini Kristo aruhusu hayo yote yampitie, wakati alikuwa na uwezo kabisa wa kuyaepuka? Unadhani hakikuwa kitendo cha aibu kile? Kilikuwa ni kitendo kikubwa sana cha aibu, ambacho ninauhakika hata wewe ungekuwepo wakati ule usingedhubutu hata kumwangalia pale msalabani akiwa katika hali ile. Lakini yeye hakuona aibu, kuwekwa uchi, ilimradi tu mimi na wewe tu tuokoke. Huko ni kujitoa kulikopitiliza.

Hakunionea haya mimi, vilevile hakukuonea haya wewe, kinyume chake biblia inatuambia aliidharau aibu,

Waebrania 12:2 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba NA KUIDHARAU AIBU, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu”.

Unaona, ukitafakari hilo vizuri, ndugu yangu, hutaona sababu ya wewe kumwonea aibu Bwana wako, katika dunia hii mbovu. Hutaona aibu kuitwa mshamba, kwa ajili yake, hutaona sababu  kuogopa kuitangaza injili yake.

Paulo alisema..

Warumi 1:16 “Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia”.

Alimwambia pia Timotheo maneno hayo hayo;

2Timotheo 1:8a “Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, ..;”

Huu si wakati wa kufikiria Fulani atanionaje, au marafiki watanichukuliaje, au majirani watanizungumziaje ikiwa nitampa Kristo Maisha yangu. Kumbuka Yesu hakukuonea haya wewe, aliposulibiwa uchi mbele ya kadamnasi, mbele ya maelfu ya watu waliokuwa pale Goligota, kwanini wewe umwonee haya yeye wakati hujafikia hata hatua ya kutembezwa uchi barabarani kwa ajili yake?.

Ukimkataa leo wakati utafika atakukataa na wewe.

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Tengeneza picha unasimama mbele ya mamilioni kwa mamilioni ya malaika, halafu Kristo anakuonea aibu mbele yao, utajisikiaje? Hali Fulani mbaya,

Hivyo chukua msalaba wako ujitwike umfate Kristo. Hizi ni siku za mwisho, yupo mlangoni kurudi. Kama bado hujatubu basi huu ndio wakati wako, mwamini yeye ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako na yeye mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu atakayekuongoza katika kweli yote.

Ikiwa utahitaji kuokoka, basi wasiliana nasi kwa namba hizi hapo chini, Nasi tutakusaidia katika hilo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

VAZI KUU AMBALO MUNGU AMETUANDALIA KILA MMOJA WETU.

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

Kutahayari ni nini katika biblia?(2Timotheo 2:15)

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

Nguo za magunia katika biblia ni zipi?

Rudi nyumbani

Print this post

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

Yapo mambo mengi Bwana Yesu aliyoyafanya ambayo katika akili za kawaida, ni ngumu kuaminika. Yapo mengi lakini leo tulitazame moja kuu, ambalo hakuna mwanadamu yeyote wala kiumbe chochote kinachoweza kufanya. Na jambo hilo si lingine zaidi ya  UWEZO WA KUUTOA UHAI WAKE NA KUURUDISHA.

Umewahi kujiuliza mtu anawezaje wezaje kuutoa uhai wake yeye mwenyewe na kujirudishia??..Ni kama vile hilo jambo haliwezekani ee?..Lakini liliwezekana kwa Jemedari, Mkuu wa Uzima, Yesu.. Hebu tusome mistari ifuatayo ili tuelewe vizuri….(Zingatia vipengele vilivyoanishwa kwa herufu kubwa)

Yohana 10:15  “kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami NAUTOA UHAI WANGU KWA AJILI YA KONDOO.

16  Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.

17  Ndiposa Baba anipenda, KWA SABABU NAUTOA UHAI WANGU ILI NIUTWAE TENA.

18  HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE. NAMI NINAO UWEZA WA KUUTOA, NINAO NA UWEZA WA KUUTWAA TENA. AGIZO HILO NALILIPOKEA KWA BABA YANGU.

19  Kukaingia tena matengano kati ya Wayahudi, kwa ajili ya maneno hayo.

20  Wengi wao wakasema, Ana pepo huyu, tena ana wazimu; mbona mnamsikiliza?.

21  Wengine wakasema, Maneno hayo siyo ya mtu mwenye pepo. Je! Pepo aweza kuwafumbua macho vipofu?”

Hapo Bwana Yesu anasema “Hakuna mtu autoaye uhai wake bali anautoa mwenyewe”.. Utauliza vipi pale msalabani, sio wale watu walimuua??.. Nataka nikuambie kuwa hawakumuua, biblia inasema “yeye mwenyewe aliitoa roho yake (Mathayo 27:50  “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake”)

Ndio maana baadaye wale askari  walipotaka kwenda kuivunja miguu yake wakamkuta kashakufa..kwasababu kikawaida adhabu ya kutundikwa msalabani inamchukua mtu hata siku 4 ndipo afe..Maana lengo la wao kumsulubisha mtu msalabani sio afe tu!, bali afe kifo cha mateso, kama ingekuwa lengo ni kumuua tu, wangemkata kata na mapanga afe!… Kwahiyo waliposhangaa Bwana Yesu kafa mapema vile pale msalabani, iliwaogopesha na kuwashtusha sana, kuwa Yule ni mtu wa namna gani..Mpaka Pilato naye alishtuka!!.

Marko 15:43  “akaenda Yusufu, mtu wa Arimathaya, mstahiki, mtu wa baraza ya mashauri, naye mwenyewe anautazamia ufalme wa Mungu; akafanya ujasiri, akaingia mbele ya Pilato akauomba mwili wake Yesu.

44  LAKINI PILATO AKASTAAJABU, KWAMBA AMEKWISHA KUFA. akamwita yule akida, akamwuliza KWAMBA AMEKUFA KITAMBO”

Umeona jinsi Bwana Yesu alivyokuwa wa kipekee???. Hakuwa mtu wa kawaida Yule, bali alikuwa ni “Mungu katika Mwili wa kibinadamu”, kwasababu katika hali ya kawaida hakuna mwanadamu anayeweza kuamua kuutoa uhai wake. Unakaa tu na kuamua, kuiondoa roho yako??..hilo jambo haliwezekani kibinadamu.

Na kumbuka ipo tofauti kati ya “kuutoa uhai wake” na “kujiua”. Bwana Yesu hakujiua!, maana yake ingempasa afanye jambo la kujidhuru,  lakini yeye hakufanya hivyo, bali aliutoa uhai wake… Maana yake kama angeamua asiutoe uhai wake angeweza pia kukaa pale msalabani daima, wangempiga na kumtesa lakini asingekufa na wangeshangaa kwanini hafi.. Hiyo ni kwasababu Nguvu za Mauti na Uhai tayari zilikuwa mikononi mwake.

Na hajaishia hapo, anaendelea kusema “Ana uwezo wa kuutoa uhai wake na kuutwa tena”. Maana yake ana uwezo wa KUJIFUFUA PIA!!. Na agizo hilo alipokea kutoka kwa baba. Yaani agizo la kuutoa uhai wake na kuurudisha. Baba alimwambia afanye hivyo.. “sasa sio kosa kusema Bwana Yesu, alifufuliwa na Baba, ni sahihi kabisa kwasababu nguvu zote zinatoka juu, na ili utukufu wote apokee yeye, ni sahihi kusema Baba alimfufua, lakini kiuhalisia ni kwamba Baba alimpa maagizo na uwezo wa kujifufua mwenyewe.”

SASA NINI LENGO LA KUUTOA UHAI WAKE NA KUJIRUDISHIA??

Lengo la Bwana Yesu kuutoa uhai wake na kujirudishia sio kutuonyesha sisi kuwa yeye ni mtaalamu au mtu wa miujiza! Hapana, bali kulikuwa na maana kubwa sana kiroho, kwanini autoe uhai wake na kujirudishia.

Ili tuelewe vizuri hebu tafakari mfano ufuatao.

Umenunua simu na haiwezi kuingia internet, wenye mtandao wakakwambia wanakutumia settings za internet, zikubali na baada ya HAPO ZIMA SIMU YAKO NA KUIWASHA TENA, ili ziweze kufanya kazi. Sasa lengo la wao kukuambia uzime simu yako na kuiwasha baada ya kupokea hizo settings, si kwasababu hawapendi simu yako iwe imewaka muda wote, hapana!.. Lengo la wao kukuambia ufanye vile ni kwasababu zile settings ili ziweze kufanya kazi ni lazima program zote kwenye simu ziache kufanya kazi kwa muda ili hizo mpya zinapoingia zipate nafasi, na unapowasha simu unakuta tayari zile settings za internet zimeanza kufanya kazi kwenye simu yako, na unajikuta unaweza kuingia internet.  Lakini usipofanya hivyo (usipozima simu yako na kuiwasha), utabaki nazo tu ndani ya simu yako na hazitakusaidia chochote.

Na kama umegundua simu yenye uwezo mkubwa kidogo ina uchaguzi wa kujiwasha na kujizima yenyewe yaani “restart button”, kiasi kwamba ukibonyesha hiyo “restart” simu inajizima yenyewe na kujiwasha, pasipo wewe kuizima wala kuiwasha.

Na Bwana Yesu, ni hivyo hivyo baada ya kupokea maagizo ya uzima wa milele, kwamba injili lazima ihubiriwe ulimwenguni kote, Ilikuwa ni lazima “afe na kufufuka”. Kulikuwa hakuna namna..vinginevyo ukombozi usingeenea kila mahali.. Ni kama tu zile settings za internet, zisipofanya kazi katika simu haiwezekani kujiunganisha na ulimwengu wote. Na zinaingia kwa kuizima simu na kuiwasha tena.

Hiyo ndio sababu ya Bwana Yesu kuuondoa  uhai wake yeye mwenyewe na kuurudisha tena. Haleluya!!. Kwa lugha ya kueleweka ni kama ali-restart uhai wake. Alisema maneno yafuatayo..

Yohana 12: 24  “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi”.

Umeona kwahiyo Bwana Yesu ilimpasa afe, na kufufuka kwa faida yetu sisi, hususani sisi watu wa Mataifa.. Ndio maana hapo alisema “anao kondoo wa zizi lingine” maana yake ni sisi watu wa Mataifa…kondoo wa zizi lake ni wayahudi. Hivyo ili atupate na sisi watu wa mataifa ilimpasa atoe uhai wake na kuutwaa tena..

Yohana 10:15  “kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami NAUTOA UHAI WANGU KWA AJILI YA KONDOO.

16  Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja”

Je umemwamini Yesu?.. Je unamheshimu yeye ambaye aliutoa uhai wake ili kuja kukupata wewe kondoo wa mbali uliyepotea??.  Je umemthamini kwa kutii maagizo yake ya msingi, ya kutubu dhambi zako, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu, pamoja na kupokea kipawa cha Roho wake Mtakatifu juu yako?. Kama bado ni vyema ukafanya hivyo maadamu bado unayo nafasi…

Kumbuka hii ni neema ya kipekee sana tuliyopewa…haitadumu milele..

Waebrania 10:28  “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29  Mwaonaje? HAIKUMPASA ADHABU ILIYO KUBWA ZAIDI MTU YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, NA KUIHESABU DAMU YA AGANO ALIYOTAKASWA KWAYO KUWA NI KITU OVYO, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Na pia…

Waebrania 2:3  “sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia;

4  Mungu naye akishuhudu pamoja nao kwa ishara na ajabu na nguvu za namna nyingi, na kwa magawanyo ya Roho Mtakatifu, kama alivyopenda mwenyewe”

Neema ni ipo, lakini haitadumu milele, tukiipuuzia… Bwana anatuita wote tuingie zizini mwake, ni heri tukaingia, lakini tukiipuzia na kuidharau neema, siku moja mlango utafungwa na hautafunguliwa tena..

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin


Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

WAKAMWACHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

Rudi nyumbani

Print this post

Zile Rangi saba za Upinde wa Mvua zinawakilisha nini?

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia, maneno ya Mungu wetu aliye juu..kwasababu maneno yake ndio Mwanga wa njia yetu ya kuelekea mbinguni, na Taa iongozayo miguu yetu.(Zab.119:105)

Je umewahi kujiuliza kwanini bendera nyingi zinakuwa ni kitambaa chenye rangi mbali mbali, na kila rangi inakuwa na maana fulani?. Utaona mataifa mengi bendera zao zinakuwa  na mistari tu ya rangi tatu au nne au tano. Na kama ukifuatilia utagundua zile rangi si urembo, bali zimebeba maana fulani kwa hilo Taifa.

Kwamfano bendera ya Taifa la Tanzania ina rangi 4, Nyeusi, Njano, kijani na Bluu. Rangi nyeusi inawakilisha wenyeji wa Taifa hilo (ni watu wenye ngozi nyeusi), rangi ya njano inawakilisha maliasili zote zilizopo ndani ya Taifa hilo, rangi ya kijani inawakilisha mimea na uoto wa asili wote pamoja na mazao ya nchi.. na rangi ya bluu inawakilisha Maji yote ikiwemo bahari, mito na maziwa. Hivyo kama ukiweza kuzisoma rangi hizo tayari utakuwa umeshalielewa Taifa la Tanzania, ni taifa la namna gani hata kabla ya kufika.

Kadhalika na Bwana Mungu wetu anayo bendera yake ambayo inawakilisha tabia zake. Na bendera yake hiyo aliiwasilisha kwetu baada tu ya ile gharika ya wakati wa Nuhu. Na hiyo si nyingine zaidi ya Ule Upinde wa Mvua wenye rangi saba. Kikawaida Bendera zetu zinakuwa ni kitambaa tu kilichochorwa mistari ya rangi, na tunaipandisha inakuwa inapepea angani,  lakini bendera ya Bwana haijachorwa katika kitambaa bali katika anga juu sana, na imechorwa kwa mistari ya rangi saba.

upinde wa mvua

Bendera hiyo Ndiyo inayomwelezea Mungu ni nani kwetu..

Sasa kabla ya kuendelea mbele ni vizuri tukazijua tabia kuu mbili za Mungu, ambazo hizo ndio msingi wa somo letu.. Biblia inasema Mungu ni MWINGI WA HASIRA (Nahumu 1:2) na vile vile biblia inasema Mungu ni MWINGI WA HURUMA.(Kutoka 34:6, Zaburi 145:8, Yoeli 2:13, Yona 4:2). Hizo ndio tabia kuu mbili za Mungu wetu. Ana hasira nyingi sana, vile vile ana huruma nyingi sana. Lakini pamoja na kwamba ni mwingi wa hasira, biblia imesema si mwepesi wa hasira, maana yake si rahisi akasirike kwa haraka.

Hivyo tukirudi katika mifano ya maisha ya kawaida..Mtu anavyozidi kuwa na hasira ndivyo ndani mwake kunavyozidi kuwaka, maana yake ni kwamba ni kama kuna moto unachochowa ndani yake na anazidi kuwa mwekundu, ikiwemo unyama huko huko.. Ndio maana watu weupe wakikasirika ni rahisi kuona hata ngozi za nyuso zao zimebadilika na kuwa nyekundu.. Hivyo rangi nyekundu inawakilisha hasira au ghadhabu..

Lakini vile vile, mtu huyo huyo hasira yake inapoanza kupoa utaona ule wekundu unaondoka na anarudia rangi yake. Ule wekundu unaanza kufifia kidogo kidogo mpaka, unaisha kabisa…

Vile vile Katika mifano mingine ya maisha ya kawaida pia kitu cha moto sana kinawakilishwa na rangi nyekundu, lakini kitu cha baridi kinawakilishwa na rangi ya bluu.. maana yake rangi ya bluu ni rangi ya utulivu uliozidi sana, ni rangi ya upole, ni rangi ya kulipooza jambo la moto!, ni rangi ya kutuliza ghadhabu kwa ufupi ni rangi ya rehema…na ni kinyume kabisa cha rangi ya Nyekundu.

maji ya moto

Kwa mifano hiyo tutakuwa tumeshaanza kuelewa kwanini uwepo upinde angani unaoanza na  Rangi nyekundu, na kisha zifuate rangi nyingine mpaka itokee rangi ya mwisho ya bluu..Utaona kwa jinsi zile rangi zinavyozidi kusogea mbele ile nyekundu inafifia na kuwa rangi ya chungwa (Orange), na kisha njano na kisha kijani… Maana yake hapo, Hasira ya Mungu inapungua kutoka juu kushuka chini, mpaka kufikia kusamehe kabisa..na kutoa neema (Ndio rangi ya kijani iliyopo katikati)..

Na inavyozidi kuendelea utaona Neema ya Mungu inazidi kuwa nyingi na hata kuelekea kwenye rangi ile ya blue ambayo inawakilisha utulivu wa Mungu wa hali ya juu, na Neema isiyo na kikomo..kiasi kwamba Rehema zake ni nyingi mno na hata kuipooza na kuizima ghadhabu yote..Hivyo rangi  inavyozidi kukolea kuwa bluu ndivyo  neema zake zinavyozidi kuwa nyingi….Ndio maana hata anga lina rangi ya bluu, kuonyesha wingi wa huruma zake kuliko hasira zake.

Hivyo zile rangi saba zinawakilisha ghadhabu ya Mungu jinsi inavyosogea na kubadilika  kuwa Rehema zake…Ndio maana Baada ya Nuhu kutoka kwenye gharika, Mungu aliirehemu dunia ambayo alikuwa ameighadhibikia kwa ghadhabu kubwa, na kuahidi kutoiangamiza tena kwa maji. Hapo ni hasira zake zimesogea kutoka kwenye nyekundu kwenda kwenye blue.

Ni Mungu tu pekee ndio ana tabia hiyo, hakuna kiumbe kingine duniani, au mbinguni ambacho kina wingi wa hasira na hapo hapo kina wingi wa huruma.

Ndio maana alisema katika..

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30  kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”

Haijalishi Umemwudhi Bwana kiasi gani leo, kumbuka huruma ni nyingi, yupo tayari kukusamehe kabisa endapo utamgeukia yeye kwa moyo wako wote na kudhamiria kuacha dhambi. Unachopaswa kufanya ni kutubu mbele zake kwa moyo wa unyenyekevu kabisa na kisha kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu, na kupokea Roho Mtakatifu. Naye atafuta dhambi zako zote, na kukufanya kuwa mtakatifu kana kwamba hujawahi kumkosea kabisa katika maisha yako. Na wala ghadhabu yake haitakuwa juu yako hata kidogo.

Lakini ukipuuzia rehema zake hizo ambazo zinapatikana bure, na kuzidi kuisogelea ghadhabu yake, fahamu kuwa yeye bado hajabadilika, bado ni mwingi wa hasira… alisema…katika Nahumu 1: 2 “Bwana ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; Bwana hujilipiza kisasi, NAYE NI MWINGI WA HASIRA; Bwana hujilipiza kisasi juu ya adui zake, huwawekea adui zake akiba ya hasira”

Ni jambo baya sana kuangukia kwenye hasira ya Mungu, ni heri ukatubu leo na kumwamini..

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin


Mada Nyinginezo:

MUNGU HAONI SHIDA KUMUHAKIKISHIA MWOVU ULINZI.

Fadhili ni nini? Nini maana ya “fadhili zake ni za milele” kibiblia?

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

TAFUTA KUWA NA AMANI NA WATU WOTE.

NIKUPE WEWE URITHI WA BABA ZANGU?

Rudi nyumbani

Print this post

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Neno hili utalikuta sehemu nyingi sana katika biblia,  kwa mfano hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakutana na neno hilo;

Ayubu 13:28 “Nijapokuwa ni kama kitu kilichooza, kinachosinyaa, Mfano wa nguo iliyoliwa na nondo.

Isaya 50: 9 “Tazama, Bwana MUNGU atanisaidia; ni nani atakayenihukumu kuwa mkosa? Tazama hao wote watachakaa kama vazi; nondo atawala”.

Mathayo 6:19 “Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba;

20 bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi;

21 kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako”.

Yakobo 5:1 “Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.

2 Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo”.

Soma pia Ayubu 4:19, Zaburi 39:11, Isaya 51: 8, Hosea 5:12

Nondo ni wadudu, jamii ya vipepeo, unaweza kuwaona kwenye picha juu. Wadudu hawa, huwa wakishafikia hatua ya kutaga mayai, tabia yao ni kwenda kwenye nyumba za watu, na kutaga maeneo ambayo yana nguo, au sehemu zenye asili ya vitu vya pamba pamba au manyoya kama vile kwenye makapeti, n.k. lengo likuwa ni siku vifaranga watakapototolewa wapate chakula, na chakula chao ndio hizo nguo.

Kwa kawaida wakishafikia hatua ya vipepeo hawana uharibifu wowote, lakini wakiwa bado ni “lava” ndio wanatafuna nguo, na vitu vyote vyenye jamii ya hiyo vilivyopo ndani.

Natumai hata na wewe ulishawahi kuwaona, tazama picha  chini, hao wanaoonekana kama vimbegu vya maboga ndio lava wenyewe.

lava wa nondo

Ndio hapo unashangaa suti yako nzuri uliyoiacha kabatini, umeinunua kwa bei ghali unaikuta na matobo tobo, unadhani ni mende, hujui kuwa ni kazi ya hawa wadudu.

nguo iliyoliwa na nondo

Sasa kibiblia wadudu  hawa walikuwa wanawakilisha uharibifu, wa aina yoyote. Na ndio maana Bwana Yesu alisema;

“Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba”; ..Akiwa na maana kuwa haijalishi ni vitu vilaini au vigumu, kama ni vya chuma, vitaliwa na kutu,  vikiwa ni laini kama nguo bado vitaliwa na nondo. Hiyo ni kuonyesha kuwa hakuna hazina yoyote inayodumu ikiwa haikuwekezwa mbinguni.

Ni ajabu sana, kumwona Mkristo anayo mabilioni ya pesa kwenye account zake za benki, ukimuuliza zote hizo ni za nini atakuambia najiwekea akiba ya baadaye na watoto wangu. Wakati huo huo hajawahi kufikiria hata kumfanyia Mungu kitu. Hajui kuwa mali zina mbawa, kama biblia inavyosema. (Mithali 23:5)

Kunaweza tokea anguko kubwa la uchumi na fedha isiwe na thamani tena, kunaweza tokea wizi, na hazina zako zote zikachukuliwa na wengine, kunaweza tokea matatizo Fulani ya ghafla na hicho ulichojilimbikizia kwa miaka mingi ukakitumia chote kutatua matatizo hayo, au pengine unaweza ukafa na usifaidi chochote katika hicho ulichojikusanyia wakaja kula wengine, na hao wengine biblia inasema hujui kama watakuwa na hekima au wapumbavu, wakazitapanya kizembe, na hazina yako ikawa ni bure..

Lakini mtu anayejiwekea hazina kwa Mungu, Mtu kama huyo hazina yake ni lazima idumu milele. Kwanza itamwongezea ulinzi wa kiroho na kimwili akiwa hapa hapa duniani, pili itaandikwa mbinguni, na siku ile Bwana atakapomlipa kila mtu kulingana na kazi yake ,basi  na yeye pia atapokea thawabu idumuyo milele.

Jiulize ndugu, nguvu zako zote unazipeleka wapi? Au unamwandalia NONDO azile? Kama utashindwa leo hii kuifanya kazi ya madhabahuni, basi hakikisha kuwa nguvu zako unazozitaabikia huko usiku na mchana, unazielekeza kwa Mungu wako, ili Mungu awe na sababu ya kukukumbuka siku ile, aone kuwa hukwenda kutaabika bure, bali kwa ajili yake.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin

 

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini ndugu wanaokaa pamoja wawe kama mafuta ya Haruni?

SWALI: Naomba ufananuzi wa mstari huu, ni kwanini ndugu wanaokaa pamoja wafananishwe kama na mafuta mazuri yashukayo ndevuni mwa Haruni?

Zaburi 133:1 “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja.

2 Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake”.


JIBU: Tunapaswa tujiulize ni kwanini awe ni Haruni na sio mtu mwingine kama vile Daudi, au Samweli au Eliya?. Haruni alikuwa ni kuhani mkuu. Na ukuhani wake ulikuwa na matokeo pale alipotiwa mafuta na Mungu (Kutoka 30:30, Walawi 8:12).

Hivyo kitendo cha ndugu kukaa pamoja katika Kristo, tena kwa umoja, wakinia mamoja, kwa upendo wote.. Rohoni kitendo hicho kinachukua umbile la kuhani mkuu anayetiwa mafuta mengi sana ambayo hayaishii tu kwenye kichwa au ndevu zake, bali yanatiririka kabisa mpaka kwenye pindo za mavazi yake.

Na kama tunavyojua leo hii, kuhani mkuu tunaye mmoja tu, ambaye ndiye Bwana wetu Yesu Kristo. Hivyo tunapokaa pamoja kwa umoja sisi kama kanisa la Kristo, msingi wetu ukiwa ni Biblia, basi rohoni tunachukua lile umbile la Kristo alipokuwa anatiwa mafuta na Mungu hapa duniani.  Biblia inasema mafuta aliyotiwa yalikuwa ni mengi kuliko  kuhani au mtakatifu yoyote aliyewahi kuishi hapa duniani.

Waebrania 1:8 “Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.

9 Umependa haki, umechukia maasi; KWA HIYO MUNGU, MUNGU WAKO, AMEKUTIA MAFUTA, MAFUTA YA SHANGWE KUPITA WENZIO.

Unaona, Na matokeo ya mafuta yale, ilikuwa si kingine zaidi ya kuwamulikia watu injili ya kweli, kutenda miujiza, kufungua, kukomboa, kuponya n.k.

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Ipo siri kubwa sana katika hilo. Leo hii hatuuoni uhai wa Kristo ndani ya kanisa, kwasababu moja tu, hatuna upendo, wala hatunii mamoja, kila mtu anafikiria mambo yake mwenyewe, na sio ya Kristo. Bwana atusaidie tuufikie umoja wa imani, kama lilivyokuwa katika kanisa la kwanza la mitume. Ambalo kwa kupitia kanuni hiyo waliweza kuupindua ulimwengu kwa kipindi kifupi sana. Kwasababu Mafuta ya Kristo yaliyokuwa yanamiminika katikati yao, yalikuwa ni yale yenyewe kabisa. kwa ule umoja tu na mshikamano waliokuwa nao.

Fikiria ni watu ambao walifikia hatua ya kusema, vitu walivyonavyo sio mali zao binafsi bali za shirika. Je na sisi tunaweza kufikia huko?

Bwana atusaidie sana.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin

Mada Nyinginezo:

UPAKO NI NINI?

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

Kwanini Kuhani wa Mungu Eli alikufa kwa kuvunjika shingo?

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Rudi nyumbani

Print this post

MILANGO YA KUZIMU.

Milango ni wingi wa neno “mlango”..( Malango na Milango), ni neno moja. Katika biblia tunasoma Neno hilo likitajwa na Bwana Yesu..

Mathayo 16:18 “ Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; WALA MILANGO YA KUZIMU HAITALISHINDA.

19  Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”.

Tunasoma Mamlaka hayo alipewa Mtume Petro,  na Mitume wengine pia walipewa mamlaka kama hayo (soma Yohana 20:23).

Sasa Mlango maana yake ni maingilio ya mahali, Vitu au watu wanaingia ndani ya nyumba au ndani ya mji kupitia milango yake, hakuna namna wanaweza kupitia kwingine.

Kwahiyo Kristo aliposema atalijenga kanisa ambalo milango ya kuzimu haitalishinda, Maana yake ni kwamba kanisa Bwana Yesu atakalolijenga, litakuwa na nguvu dhidi ya Milango yote ya kuzimu.

Sasa Milango ya kuzimu ni ipi?

Milango ya kuzimu ni mambo yote ambayo yanayompa mtu tiketi ya moja kwa moja kuingia kuzimu. Ifuatayo ni baadhi tu!

1Wakorintho 6:9  “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? MSIDANGANYIKE; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”

Kwahiyo Ibada za sanamu: Ni lango la kuzimu…Uasherani: ni lango la kuzimu!. Mtu anayefanya uasherati kajifungulia mlango wa kwenda kuzimu, Uuaji ni lango la kuzimu, Wizi ni lango la kuzimu, Anasa ni lango la kuzimu, Ulevi ni lango la kuzimu. Na mengine mengi yanayofanana na hayo!.. ndio maana Bwana Yesu kaitaja kama “Milango”..maana yake ipo mingi… Maana yake hata ukitenda mojawapo kati ya hayo bado utaingia kuzimu tu! Hata kama hutafanya hayo mengine yaliyosalia.. Ukiwa mzinzi tu, hata kama huibi, au sio mlevi, tayari utaenda kuzimu tu!..Kwasababu uzinzi, ni moja wapo ya lango la kuzimu..utafika kule kule tu, alipo mlevi na muuaji. Kwasababu kuzimu ina milango mingi.

Yakobo 2:10  “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.

11  Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria”.

Kwahiyo Kanisa Bwana atakalolitengeneza Maana yake litakuwa ni Kanisa Takatifu lisilo na kunyanzi wala hila, Kanisa ambalo litaliendea LANGO MOJA TU LA MBINGUNI (Yaani Yesu), na wala halivutwi na Malango ya kuzimu!. Kanisa la namna hiyo ndio Bwana aliahidi kulijenga.

Na alianza kulijenga siku ile ya Pentekoste, Roho Mtakatifu aliposhuka juu  ya watu wake, akawajaza Roho Mtakatifu, na kuwapa nguvu za kushinda milango yote ya kuzimu.

Roho Mtakatifu ndio Muhuri wa Mungu, anaposhuka juu ya mtu, anaondoa ile kiu yote ya kufanya dhambi, kiasi kwamba dunia inamshangaa mtu huyo anawezaje kuishi bila kufanya zinaa katika kizazi hiki, anawezaje kuishi bila kuvuta sigara wala kunywa pombe, na hata hatumii nguvu kujizuia, anawezaje kuishi bila kutukana, bila kuiba, anawezaje kuishi maisha ya ustaarabu kiasi hicho, anawezaje kuwa na amani na huku hana kitu mfukoni, anawezaje kuwa na amani na huku kila mtu yupo kinyume naye, anawezaje kuishi bila kumkana huyo Yesu, anawezaje kuishi bila kuvutwa na anasa na starehe za dunia?..n.k pasipo kujua kuwa ipo nguvu waliyopewa ya kuishinda MILANGO YA KUZIMU.

Je na wewe unayo hiyo nguvu?. Au malango ya kuzimu yana nguvu juu yako?.

Kwa ufunuo Petro aliopewa ndio Bwana aliosema atalijenga kanisa lake juu yake, na  milango ya kuzimu haitalishinda…na ufunuo huo si mwingine zaidi ya YESU NDIYE MWANA WA MUNGU.

Mathayo 16:15  “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16  Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

17  Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18  Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”

Hivyo ukitaka milango ya kuzimu uishinde, njia ni moja tu, nayo ni KUMWAMINI YESU KUWA NDIYE MWANA WA MUNGU, Huo ndio Msingi, ambao kanisa la Mungu linajengwa juu yake. Ukitafuta msingi mwingine kamwe hutaweza kupata nguvu ya kuishinda milango ya kuzimu.

Na kumwamini Yesu, ni kutubu kwa kudhamiria kuacha kabisa dhambi zote, na baada ya hapo ubatizo, na mwisho kupokea Roho Mtakatifu, kama muhuri wa Mungu, ambaye huyo ndio ukamilifu wa kazi ya Mungu juu ya Mtu, ndiye anayetoa nguvu za kuyashinda malango ya kuzimu.

Kumbuka biblia inasema kuzimu haishibi..(Mithali 30:16), wanaoshuka huko ni wengi kila siku.Na ina milango mingi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin


Mada Nyinginezo:

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

LANGO LIMEBADILIKA.

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

Print this post

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe mtumishi wa Mungu, samahani naomba kuuliza swali kwenye 2Wafalme 8:7-15. Kwanini Elisha alimwambia Hazaeli amwambie mfalme kuwa atapona na wakati Bwana alimuonyesha Elisha kuwa mfalme atakufa. Je! Ni kwanini Elisha alisema hivyo?. Je! Ni kweli alidanganya? Na ni kwanini alifanya hivyo?


JIBU: Tusome vifungu vyenyewe kwa faida ya wengine pia..

2Wafalme 8:7 “Kisha, Elisha akaenda Dameski; na Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, alikuwa hawezi; akaambiwa ya kwamba, Yule mtu wa Mungu amefika hapa.

7 Kisha, Elisha akaenda Dameski; na Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, alikuwa hawezi; akaambiwa ya kwamba, Yule mtu wa Mungu amefika hapa.

8 Mfalme akamwambia Hazaeli, Chukua zawadi mkononi mwako, ukaende ili kumlaki yule mtu wa Mungu, ukamwulize Bwana kwa kinywa chake, kusema, Je! Nitapona ugonjwa huu?

9 Basi Hazaeli akaenda kumlaki, akachukua zawadi mkononi mwake, za kila kitu chema kilichopatikana Dameski, kiasi cha mizigo ya ngamia arobaini, akaenda, akasimama mbele yake akasema, Mwana wako Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, amenituma kwako, kusema, Je nitapona ugonjwa huu?

10 Elisha akamwambia, Enenda, ukamwambie, BILA SHAKA UTAPONA; LAKINI BWANA AMENIONYESHA YA KWAMBA BILA SHAKA ATAKUFA.

11 Akamkazia macho hata akatahayari; na yule mtu wa Mungu akalia machozi.

12 Hazaeli akasema, Bwana wangu analilia nini? Akajibu, Kwa sababu nayajua mabaya utakayowatenda wana wa Israeli; utazichoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, utawaseta-seta watoto wao wachanga na wanawake wao wenye mimba utawapasua.

13 Hazaeli akasema, Lakini mimi mtumwa wako ni nani, mimi niliye mbwa tu, hata nifanye jambo hili kubwa? Elisha akajibu, Bwana amenionyesha ya kwamba wewe utakuwa mfalme juu ya Shamu.

14 Ndipo akamwacha Elisha, akarudi kwa bwana wake; naye akamwambia, Elisha alikuambiaje? Akajibu, Aliniambia ya kuwa bila shaka utapona.

15 Ikawa siku ya pili yake, akatwaa tandiko la kitanda, akalichovya katika maji, akalitandaza juu ya uso wake, hata akafa. Na Hazaeli akatawala badala yake”.

Ukingalia hapo, Elisha hakumdanganya Ben-hadadi kuhusiana na ugonjwa wake. Asingeweza kufanya vile kwani Ben-hadadi hakwenda kwa shari wala kwa dharau, bali alikwenda kwa unyenyekevu mwingi mpaka kuchukua uamuzi wa kubeba na sadaka zake kwa mtumishi wa Mungu. Kwahiyo Elisha kama mtumishi wa Mungu asingewezeka kufanya jambo kama hilo

Hivyo Elisha alipomwambia kuwa atapona, lakini bila shaka kuwa atakufa.. alikuwa anazungumza mambo mawili tofauti, jambo la kwanza ni kuwa kuhusiana na ugonjwa wake aliouulizia kuwa utamletea mauti,  Elisha alimwambia kuwa huo hautamletea mauti, bali atapona, lakini mauti yake itakuja kwasababu nyingine kabisa.

Na ndio maana utaona hapo baada ya siku mbili, biblia inasema alitwaa tandiko la kitanda, (blanketi). Kisha akalichovya kwenye maji, akalitandaza juu ya uso wake akafa. Kwa kawaida ukichukua hata shuka tu jepesi, akafunikwa uso, kisha maji yakamwagwa juu yake, huwezi pata pumzi, utakufa tu. Ndivyo ilivyokuwa kwa Ben-hadadi. Aliuawa kwa kifo kingine kabisa lakini sio cha ugonjwa wake.

Hatujui ni nini kilimpelekea mpaka akafanya vile, pengine labda alipokea taarifa mbaya kutoka kwa maadui zake za kuvamiwa, au alifanyiwa hila na watumishi wake, ikiwemo huyu Hazaeli, hatajui, lakini utaona kifo kilikuja kwa njia nyingine kabisa ya kujinyonga kwa kukosa pumzi na sio kwa ugonjwa.

Hivyo, jambo ambalo tunaweza kujifunza ni kuwa, Mungu anaweza kusema na wewe, juu ya habari ya uzima wako, au mafanikio yako, au amani yako. Lakini wakati huo huo anaweza kuzungumza juu ya kifo chako.

Kwamfano unaweza muuliza Mungu, Je! Nikifanya biashara fulani, nitafanikiwa na kupata faida? Akakujibu ndio utafanikiwa na kuwa tajiri sana mpaka kumiliki mashirika 20 . Lakini kwasababu ulimuuliza juu ya biashara yako tu, hukumuuliza juu ya hatma ya maisha yako ya milele. Unashangaa, baada ya mwezi mmoja unakufa.

Tunapaswa tuwe na hekima ya kutaka kujua pande zote, kama Daudi ambaye alimwomba Mungu, amjalie pia kujua hesabu ya miaka yake hapa duniani. Ili aishi maisha ya kumcha Mungu…

Zaburi 39:4 “Bwana, unijulishe mwisho wangu, Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani; Nijue jinsi nilivyo dhaifu”.

Inasikitisha kuona kuwa watu wanathamini sana mambo ya mwilini, lakini ya rohoni wanayatupalia nyuma. Kana kwamba huko watakapokwenda yatafuatana nao.  Ukiwaeleza habari za mbinguni na kuzimu, wanakupuuzia, wao wanapoona Mungu anapozungumza nao juu ya mafanikio yao, ndio wanadhani wamefika. Kumbe hawajui, hapa duniani ni tuna pita tu.

Mtafute Mungu ndugu yangu.. Vya duniani vinapita!

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?

JIBU: Watu wengi wanajaribu kutoa  tofauti katika  maneno hayo mawili, lakini ukweli ni kwamba yanamaanisha jambo lile lile moja, ufalme wa mbinguni ndio ufalme wa Mungu.

Na ndio maana kuna mahali Bwana Yesu  alisema maneno haya kwa wanafunzi wake;

Mathayo 19:23 “Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika UFALME WA MBINGUNI.

24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika UFALME WA MUNGU”.

Ukichunguza hapo utaona Bwana Yesu alikuwa anamaanisha kitu kimoja katika hayo maneno mawili, ufalme wa Mungu na ule wa mbinguni..Hivyo unapokutana na mwandishi mmoja anatumia sana neno ufalme wa mbinguni, na mwingine ufalme wa Mungu, usichanganyikiwe ujue wanamaanisha kitu kilekile kimoja.

Ni sawa na ule mfano wa “kuapa” ambao Bwana Yesu aliwaambia mafarisayo, wao walidhani kama ukiapa kwa mbingu sio kosa, bali ukiapa kwa yeye akatiye juu ya kiti cha enzi mbinguni ndio kosa…Wakijaribu kutofautisha kati ya Makao ya Mungu na Mungu mwenyewe.. Lakini Yesu aliwaita viongozi vipofu kwasababu  hawakujua kuwa ukishaitaja mbingu, tayari moja kwa moja umeshamtaja na Yule akaaye ndani yake .  Soma..

Mathayo 23:16 “Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga.

17 Wapumbavu ninyi na vipofu; maana ni ipi iliyo kubwa, ile dhahabu, au lile hekalu liitakasalo dhahabu?

18 Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga.

19 Vipofu ninyi; maana ni ipi iliyo kubwa, ile sadaka, au ile madhabahu iitakasayo sadaka?

20 Basi yeye aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hiyo, na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.

21 Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo, na kwa yeye akaaye ndani yake.

22 Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa yeye aketiye juu yake”.

Vivyo hivyo unaposema Ufalme wa Mbinguni, unapaswa ufahamu kuwa unautaja Ufalme wa Mungu mwenyewe anayeishi huko. Jambo ni lile lile hakuna tofauti yoyote.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

DANIELI: Mlango wa 11

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

UFUNUO: Mlango wa 11

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kwanini tunambariki Mungu? Je! Mungu huwa anabarikiwa?

SWALI: Tafadhali naomba ufafanuzi wa jambo hili, kibiblia tunaambiwa kwamba mkubwa atambariki mdogo. Sasa kuna baadhi ya wakristo waliookoka wanapokuwa katika maombi, wamezoea kusema “Nakubariki Mungu wa mbingu kwa wema wako.”. Je ni sahihi kumwambia Mungu wetu hivyo?


JIBU: Neno kubariki linamaana Zaidi ya ile ya kumuombea mtu mafanikio, ambayo tumeizoea,  kwamba mkubwa anambariki mdogo, lengo  likiwa ni ili aje kupokea mema kutoka kwa Mungu baadaye.

Bali Neno kubariki kibiblia linamaanisha pia ya kutukuza, au kuheshimisha jambo,kitu au jina. kwamba limestahili kupokea sifa zote njema..

Hivyo mkristo anaposema nalibariki jina la Bwana. Hana maana kuwa analiombea mafanikio kana kwamba linategemea baraka kutoka kwake ili lifanikiwe pasipo hizo haliwezi kufanikiwa, hapana.

Bali linamaana  ya juu Zaidi, yaani “analipa heshima zake zote kwamba limestahili heri”

Katika biblia utaona Ayubu alilibariki jina la Mungu wakati ule alipokuwa anapitia matatizo, alisema maneno hayo…

Ayubu 1:21 “akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; JINA LA BWANA NA LIBARIKIWE”.

Unaona? vilevile malaika mbinguni, usiku na mchana wanalibariki jina lake.

Ufunuo 5:11 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,

12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu NA BARAKA”.

13 Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, BARAKA NA HESHIMA na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele.

Soma pia.. Ufunuo 7:12.

Hivyo, na sisi tunapolibariki jina la Bwana, ni kwamba tunaonyesha kuwa tunathamini haki  yote na uzima, na amani, na furaha,  na upendo, unaotoka katika jina hilo. Ni lugha nzuri Zaidi tuliyonayo  ya kumtukuza Bwana , na hakuna shida yoyote kusema hivyo.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Mafundisho

UFUNUO: Mlango wa 7 & 11

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

SWALI: Mstari huu unamaanisha nini?

Waefeso 3:14 “Kwa hiyo nampigia Baba magoti,

15 ambaye kwa jina lake UBABA WOTE WA MBINGUNI NA WA DUNIANI UNAITWA”,


JIBU: Mungu ni Baba wa kila kitu, Baba wa vilivyo mbinguni, na vilevile  Baba wa vilivyo duniani. Na kama tunavyojua jukumu la Baba ni kuhakikisha anaihudumia familia yake vizuri, anaitunza, anailisha, anaivisha, anaiburudisha, vivyo hivyo Mungu wetu ni Baba wa viumbe vyake vyote, vilivyo juu mbinguni (yaani malaika zake wote), na vilivyo chini duniani (Wanadamu wote). Anavihudumia na kuvitosheleza vyote kulingana na mahitaji yao. Kwasababu yeye ndiye aliyeumba kila kitu, Na ndiye mpaji wa wote.

Wakolosai 1:16 “Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake”.

Na ndio maana mtume Paulo anasema Anampigia magoti yeye, kwasababu uweza wake wa ubaba haupo tu, hapa duniani, bali pia upo kule mbinguni. Na utaendelea kuwa hivyo milele na milele. Hivyo Baba kama huyo ndiye anayestahili kupigiwa magoti.

Wafilipi 2:9 “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

Na sisi pia tuliookoka tunapaswa tukumbuke kuwa tunaye BABA MKUU juu mbinguni. Na kwamba anaowezo wa kututimizia mahitaji yetu yote ya mwilini na rohoni. Lakini ni sharti kwanza tujue kuenenda katika kanuni zake, ili afanyike kwetu Baba kweli kweli. Na kanuni yenyewe ni ile ile, ya kuutafuta kwanza ufalme wake na haki yake, ndipo hayo mengine atatuzidishia kirahisi.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 6:26 “Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao? 27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa”.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Mbari ni nini kibiblia?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

Rudi nyumbani

Print this post