Category Archive Uncategorized @sw-tz

Sera za Faragha (Privacy policy)

Ifuatayao ni Sera ya Faragha ya Tovuti/App ya Nuru ya Upendo (wingulamashahidi.org)

Tarehe ya Mwisho wa Marekebisho: [21/05/2025]

Tunapenda kukushukuru kwa kuchagua kutumia kituo cha Wingulamashahidi, jukwaa la injili ya YESU KRISTO, mafundisho ya Biblia, maombi, na jumbe za wokovu kupitia tovuti yetu na app yetu rasmi. Tunathamini faragha yako na tunajitahidi kuhakikisha taarifa zako zinalindwa kikamilifu.


1. Taarifa Tunazokusanya

Lengo la kukusanya taarifa zako ni kukuletea huduma ya kiroho iliyo bora zaidi. Na taarifa tuzikusanyazo ni:

  • Taarifa  Binafsi (kama utazijaza): ambazo ni Jina lako, barua pepe, namba yako ya simu.

  • Taarifa za Kiufundi: Aina ya kifaa unachotumia, anwani ya IP, aina ya kivinjari, lugha, na mfumo wa uendeshaji.

  • Taarifa za Matumizi: Maudhui unayoyasoma, au kupakua, au kushiriki. Hii inatusaidia kujua aina gani ya masomo yanayopendelewa zaidi na watu.


2. Jinsi Tunavyozitumia Taarifa hizo

Taarifa hizi zinahitajika kwa:

  • Kukurushia masomo mapya kwenye barua pepe yako.

  • Kuboresha muundo na mwonekano wa tovuti pamoja na app

  • Kujibu maswali yako, maombi ya maombi, au mawasiliano mengine ya kiroho..


3. Ulinzi na usalama wa Taarifa Zako

Hatua za kiusalama tunazizingatia  (kama SSL, uthibitisho wa watumiaji, na encryption) kuhakikisha taarifa zako hazidukuliwi na yoyote, wala kupotea, wala kutumiwa bila idhini ya mhusika. Pia tunazingatia kanuni za kimaadili kulingana na ukristo.


4. Ushirikishaji wa Taarifa

Hatutashiriki wala kuziuza, kusambaza, au kugawa taarifa zako binafsi kwa mtu mwingine yoyote bila idhini yako isipokuwa:

  • Kwa mujibu wa sheria au maelekezo ya mamlaka husika.

  • Kwa watoa huduma wanaotusaidia kutoa huduma hizi (mfano: huduma ya kutuma barua pepe), kwa masharti ya usiri.

  • Ikiwa kama utachagua kushiriki jumbe kwenye mitandao ya kijamii.


5. Watoto

Hatukusanyi taarifa za watoto walio chini ya miaka 12 bila idhini ya wazazi au walezi. Ikiwa mzazi ataona kuwa kuwa mtoto wake ametoa taarifa binafsi bila idhini yao, basi tunaomba awasiliane nasi ili tuchukue hatua za kuondoa taarifa hizo mara moja.


6. Haki Zako

Unayo haki ya:

  • Kufahamu ni taarifa gani tulizonazo kuhusu wewe.

  • Kuomba taarifa zako zifutwe au kurekebishwa inapohitajika.

  • Kujiondoa kwenye orodha ya wanaopokea pokea mafundisho kwa njia ya barua pepe au yoyote ile.

  • Kuhoji matumizi ya taarifa zako kwa ajili ya tafiti, chunguzi au matangazo (kama yatakuwepo).


7. Vidakuzi (Cookies)

Tovuti yetu hutumia cookies ili kuboresha matumizi yako. Unaweza kuchagua kuzima kama haitakuwa ni mapendekezo yako, lakini hii yaweza kuathiri usomaji wako wa tovuti.


8. Mabadiliko ya Sera ya Faragha

Patakapotokea mabadiliko ya Sera hizi, tutakujuza mabadiliko hayo kupitia tovuti z. Mabadiliko huanza kutumika mara moja baada ya kuchapishwa.


9. Mawasiliano

Kwa maswali kuhusiana na sera hizi za faragha, tafadhali wasiliana nasi kupitia:

Barua pepe: wingulamashahidi@gmail.com
Tovuti: https://wingulamashahidi.org


Mungu akubariki sana kwa kuwa sehemu ya huduma hii. Tunakuombea baraka za Bwana YESU ziende nawe

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Shalom

Print this post

Tafsiri ya Mithali 3:27 inayosema ‘Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao’

SWALI: Nini maana ya Mithali 3:27 ?

[27]Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda.


JIBU: Kuna mambo mawili yaliyogusiwa katika hicho kifungu..

  1. Usiwanyime watu mema yaliyo Haki yao.
  2. Lakini pia, ‘ikiwa katika uwezo wa mkono wako’.

1] Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao.

Hili ni agizo la Bwana kuwasaidia wengine. Lakini pia Bwana anataka tujue ni akina nani wenye haki hiyo ya kusaidiwa.

Kibiblia Makundi ambayo ni haki yao kusaidiwa.(wawapo na shida), ni matatu (3)

 i) Familia (yaani ndugu wa mwilini)

1 Timotheo 5:8

[8]Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

Wazazi wako, wadogo zako, watoto wako. Ni haki yao kuwasaidia, kwasababu ni damu moja na wewe. Usipotimiza wajibu huo unahesabika sawa na mtu aliyeikana imani. Hakikisha jicho lako haliwapiti ndugu zako, ni sehemu ya wajibu.

ii) Ndugu wa rohoni:

Wagalatia 6:10

[10]Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

Kanisa la kwanza lilitambua jukumu hili la kusaidiana, vivyo hivyo na sisi ikiwa mpendwa mwenzako yupo katika hali na uhitaji mkubwa hupaswi kufumba macho, bali msaidie, watumishi wa Mungu wanaojibidiisha kuhubiri kweli ya Mungu wanastahili kusaidiwa mahitaji yao. (Warumi Romans 12:13, Hebrews 13:16).

1Yohana 3:17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.

Hapa inalenga pia na wajane pia walio ndani ya kanisa wale walio wajane kwelikweli. (1Timotheo 5:3–5, 9–10)

iii) Maskini.

Wapo maskini wengi ulimwenguni, ambao wanashindwa kufikiwa na mahitaji yao ya msingi, wengine wanakuwa mabarabarani walemavu, wagonjwa, majirani maskini, wote hawa pia wanastahili kusaidiwa.

Wagalatia 2:10 ila neno moja tu walitutakia, tuwakumbuke maskini; nami neno lilo hilo nalikuwa na bidii kulifanya.

Hayo ndio makundi yenye haki ya kusaidiwa. Lakini wengine wanaweza kusaidiwa lakini sio haki yao,ikiwa na maana hata wasiposaidiwa hakuna shitaka lolote juu yako kwa Mungu.

2]  Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda:

Lakini Ukiendelea kusoma anagusia tena jambo la pili ambalo ni; “Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda”.

Akiwa na maana gani?

Mtume Paulo kwa uweza wa  Roho aliandika maneno haya;

2 Wakorintho 8:12-13

[12]Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo.  [13]Maana sisemi hayo, ili wengine wapate raha nanyi mpate dhiki;

Yaani kwa jinsi moyo wako unavyoguswa, tenda mema,  lakini pia kulingana na uwezo wako uliokirimiwa na Mungu,  ili upande mmoja usiuache na taabu au kupungukiwa kabisa. Kwamfano umepata rizki kipimo cha watoto wako tu, ukaenda kukichukua na kuwapa maskini huku familia yako ikabaki Kulala njaa.. hapo hujafanya busara kwasababu umehamisha Tatizo sehemu moja kupeleka kwingine, hujatatua tatizo.

Tenda mema, bila kusahau pia kipimo chako ulichopimiwa cha mema.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Masomo mengine:

Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe?

Print this post

Je tamaa ni dhambi kulingana na Yakobo 1:15?

Swali: “Halafu ile tama ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti, (Yakobo 1:15).. je kutamani sio dhambi?”


Jibu: Kwa asili kutamani sio dhambi! Bali kunaweza kuwa ni mwanzo wa dhambi.. ni sawa na “kuongea”..kuongea si dhambi lakini kunaweza kuwa chanzo cha dhambi, kutegemea ni nini unaongea..

Na vile vile “tamaa” kwaasili ..imeumbwa ndani ya Mtu, na hata ndani ya viumbe vyote, ambayo lengo lake ni kuhamasisha jambo fulani jema au baya lifanyike katika mwili wa mtu au maisha ya mtu.

Kwamfano hatuwezi kumtafuta MUNGU kama yeye mwenyewe hajaiweka hiyo tamaa ndani yetu..hatuwezi kuomba kama yeye hatatuwekea hiyo tamaa ndani yetu n.k

Vile vile katika masuala ya mwilini,  tusingependa kula wala kuhamasika kula chakula kama tusingewekewa ndani yetu tamaa ya chakula, ile tamaa iliyowekwa ndani inatuhamasisha kula chakula, na tunapokula miili yetu inapata faida, na kutimiza lengo la kuendelea kuishi.. Lakini tamaa hiyo inapozidi mipaka inazaa ulafi na ulevi ambao ni dhambi (Soma Luka 21:34, Warumi 13:13, Wagalatia 5:21, na 1Petro 4:3).

Vile vile pia mtu kawekewa tamaa ndani yake ya kimwili kwa jinsia tofauti na yake, tamaa hiyo Mungu kaiweka ndani ya mtu kwa kusudi maalumu na wakati maalumu, kwamba wakati utakapofika mtu aweze kukutana na mke/mume wake na kuzaa watoto, kutimiza Baraka  alizozisema katika Mwanzo 1:28

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi:”.

Lakini tamaa hiyo inapozidi na kuvuka mipaka kiasi kwamba inampelekea mtu kushindwa kujitawala ndipo anapoanguka katika zinaa na hata zinaaa ya jinsia moja na yake.

Kwahiyo tamaa yoyote ile iwe ya chakula, au ya mwili  kwaasili sio mbaya, ila inapozaa matunda mabaya ndipo inageuka kuwa dhambi..Na ndicho Biblia ilichokimaanisha hapo katika  Yakobo 1:15 kuwa “tamaa ikiisha kuchukua mimba inazaa dhambi”..maana yake katika uasili wake sio dhambi!.. ila inapochochewa kwa njia isiyopaswa ndipo inapozaa dhambi.

Unatazama picha chafu mitandaoni, au unaposoma makala zenye maudhui ya zinaa, au unaposhiriki mijadala yenye maudhui ya zinaa  hapo unaizalia matunda ile tamaa ya mwili ndani yako, na hiyo ni dhambi, kwasababu mwisho wa siku itakupelekea kufanya zinaa au kujichua, au mawazo yako muda wote kutawaliwa na zinaa jambo ambalo biblia imesema kuwa ni machukizo kwa Bwana, moyo uwazayo mabaya (Mithali 6:18).

Biblia inatufundisha kutoyachochea mapenzi..

Wimbo 2: 7 “Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.

Na tamaa nyingine zote ni hivyo hivyo, hatuna budi kuzitawala ili zisizae dhambi, maana mshahara wa dhambi ni Mauti… na tamaa zinazozaa dhambi zote zinatokana na dunia na si MUNGU..

1Yohana 2:16 kuwa tamaa  ya macho na tamaa ya mwili inatokana na dunia na si Mungu

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI NJIA GANI MTU AITUMIE AWEZE KUSHINDA TAMAA NA VISHAWISHI?

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

Roho ya kukata tamaa ni nini na inatendaje kazi?

Print this post

Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?

SWALI: Naomba kufahamu Warumi 7:25 ina maana gani?

Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.

JIBU: Katika sura yote ya saba, mtume Paulo, anaeleza kwa kina mapambano yaliyo ndani ya mwamini.  Kwamba nia yake kutoka ndani ni kuitii sheria ya Mungu, lakini mwili wake kwa nje ni kikwazo kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kabisa kutimiza maadhimio yake.

Warumi 7:19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu

Na ni kweli huo ndio uhalisia wa kila mtu. Na ndio maana mwishoni mwa sura hiyo anahitimisha kwa kueleza hali hiyo, Lakini katika vifungu hivyo, wengi wanatafsiri vibaya wakidhani  Paulo anatetea udhaifu wa mwili hapana.. Kinyume chake alianza kwanza kueleza uhalisia wa kibinadamu, ili atoe suluhisho halisi la namna ya kushinda, ambalo ndio tunalisoma katika sura inayofuata ya nane (8)

Ambapo sasa kwenye sura ya nane(8) inayofuata, anaeleza namna ambayo Kristo anatusaidia kuishinda hiyo hali, kwa sheria nyingine  mpya ya Roho ambayo anaiweka ndani yetu.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yake ni kuwa, Roho Mtakatifu, anatuweka huru katika huo utumwa wa mwili unaotupelekesha.

Inahitaji tu kutii, kwa kumfuata Roho Mtakatifu, kisha yeye mwenyewe atatupa nguvu ya kushinda mambo yote ya mwilini. Lakini sio kwa kutegemea  nguvu zetu tu wenyewe.

Warumi 8: 5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.

7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.

9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.

10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.

Hivyo ukiishi kwa kumtii Roho Mtakatifu, basi huwezi tumikishwa tena na  mwili,

Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

Hitimisho:

Warumi 7:25, Paulo analenga hasaa sababu ya sisi kushindwa kutimiza sheria ya Mungu, Ni kwasababu ipo sheria nyingine (ya dhambi iliyojificha ndani yetu) ambayo ni ngumu kutoka kwa namna ya kibinadamu, hivyo anataka hilo tulijue ili tufahamu kuwa kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuishinda, Lakini kwa Yesu Kristo atupaye Roho wake ndani yetu, tukienenda kwa kumtii huyo, basi sheria hiyo ya dhambi tutaishinda kabisa kabisa.

Ni wito wa kila mwamini kujifunza kutembea katika Roho.

Je! Unafahamu namna ya kutembea katika Roho kama sio. Basi tutumie ujumbe kwa namba uzionazo chini ya somo hili tukutumie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Print this post

SADAKA INAONDOA MADHARA YA MAUTI

Sadaka inayotolewa kwa mwongozo wa Neno la MUNGU ina matokeo makubwa sana kwa anayeitoa. Yapo madhara yanayoondoka kwa maombi tu peke yake, lakini yapo mengine yanahitaji sadaka pamoja na maombi.

Hebu turejee Biblia kidogo tujifunze jambo..

Wakati ambapo Nabii Samweli anataka kwenda kumpaka mafuta Daudi ili awe mfalme mahali pa Sauli..biblia inatuambia kuwa alipofikiri kwenda tu hofu ilimwingia..

Na hofu hiyo ni kwamba alimwogopa Mfalme Sauli, kwani alijua kabisa endapo Sauli akisikia mtu mwingine anaenda kupakwa mafuta ya kifalme kuchukua sehemu yake, wivu utamwingia na atataka kumwua nabii Samweli na yule atakayeenda kupakwa mafuta.

Sasa ili zoezi la Daudi kupakwa mafuta likamilike bila kuleta madhara yoyote kwa Nabii Samweli na Daudi anayeenda kupakwa mafuta ya kifalme, SADAKA ILIHUSIKA!.

Utauliza ilihusika vipi?…turejee maandiko…

1 Samweli 16:1 “BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.

2 Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi BWANA akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea BWANA dhabihu.

3 Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako”

Je umeiona nafasi ya sadaka katika kuyaokoa maisha ya Samweli na Daudi?.

Hapo MUNGU hakushindwa kumwambia nabii Samweli aende hivyo hivyo na kwamba atamlinda!…La! Hakufanya bali alimwambia aende na dhabihu..

Jambo hilo Bwana MUNGU wetu aliliruhusu pia ili tuelewe umuhimu dhabihu/sadaka.

Unapomtoleo MUNGU kwa ufunuo wa Neno, bila kushurutishwa na mtu wala uchungu, kuna mambo mengi katika ulimwengu wa roho yanafanyika, kama ni nira za mauti zinalegea na kama kuna vifungo vya dhambi pia vinaondoka.

Na kumbuka sadaka kwa BWANA inapelekwa kwa BWANA, maana yake mahali ambapo BWANA anatumikiwa (mfano kanisani au mahali panapofanyika kazi ya MUNGU ikiwemo mikitano ya injili)..hapo ndipo penye neema.

Usipeleke sadaka yako maalumu mahali pengine kama kwa marafiki, au watu au maskini wa barabarani…ni vizuri kufanya hivyo na kuna baraka zake lakini vya Bwana vinapaswa vipelekwe kwa Bwana ndivyo maandiko yanavyofundisha..

Tenga kiasi chako kungine peleka kwa maskini na wenye uhitaji, lakini hakikisha una sadaka yako maalumu kwa BWANA utakayopeleka aidha kanisani au mahali popote kazi ya MUNGU inapofanyika kwa usahihi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu,

Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.

Kibiblia, hekima, ni uwezo wa  kupambanua , kuhukumu na kufanya maamuzi yenye matokeo makamilifu ya Ki-Mungu duniani.

Kwamfano, biblia inatuambia kwa hekima Mungu aliziumba mbingu na nchi (Mithali 8:22-31)

Sulemani alimwomba Mungu hekima ya kuchunga na kufanya hukumu kwa watu wake Israeli, na Mungu akampa, Danieli alipewa hekima ya upambanuzi wa ndoto na maono yote ya siri,

Kwa ufupi hekima ya ki-Mungu ni zaidi ya maarifa, elimu, au akili, ni uwezo wa juu sana ambao unazidi upeo wa ki-binadamu.

Lakini inapatikanaje?

Kumbuka Biblia inaitaja hekima pia kuwa ni mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

1Wakorintho 1:24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.

Na kama Ndio hekima mwenyewe..Basi ndani yake matunda yote ya hekima yapo.

Wakolosaia 2:3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

Hivyo ili mtu kuiona hekima tafsiri yake ni kuwa anapaswa amwone YESU. Na kumwona Yesu ni kumpokea kama Bwana na mwokozi wa maisha yako (Warumi 10:9), pamoja na kumtii kutembea katika njia zake.

Yesu anapatikana wapi?

Katika mahubiri, Mahubiri yanapatikana wapi? Kila mahali, kwenye njia kuu, viwanja, kwenye mikutaniko ya watu, mastendi, masokoni, mitandaoni n.k.

Anapazaje sauti?

Anapaza sauti kupitia watumishi wake mbalimbali Aliowatuma kumuhubiri.

Hivyo, hilo andiko linalosema,

Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.

Unaweza kuelewa sasa analenga injili, inayohubiriwa kila mahali duniani kote. Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kusema hajawahi kuisikia injili, kwasababu kila mahali inahubiriwa kwa nguvu. Kuonyesha kuwa hekima haijajificha ipo sikuzote, bali ni watu ndio wanaikwepa.

Mtu yeyote anayemwamini Kristo basi tayari amefungua mlango wa ufahamu mkubwa sana unaoweza kufungua mambo yote katika hii dunia.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kati ya Exegesis na Eisegesis. Ni ipi namna  bora ya kutafsiri maandiko?

JIBU: Haya ni maneno ya kiyunani, yanayoeleza namna tofauti ya kutafsiri maandishi.

1) Eksejesisi (exegesis).

Ni namna ya kutafsiri maandiko kwa kuzingatia mtazamo wa awali uliokusudiwa na mwandishi, kwa kuzingatia muktadha, hali ya kihistoria, matamshi na matumizi ya lugha.

2) Eisojesisi ( Eisegesis).

Ni namna ya kutafsiri Maandiko kwa namna ya mtazamo wa mtu mwenyewe, kwa kulileta andiko liendane Na wazo lake binafsi,. Namna hii haitilii maanani sana kusudio La kwanza la mwandishi, bali lile aliaminilio kuwa ni sahihi Kwake. (Mfano wa hii ni ile namna ya kusema nimefunuliwa)

Kwa ufupi eksejesisi ni Kuliruhusu andiko lijitafsiri lenyewe huku Eisojesisi ni lilete andiko litafsiri ninachokitaka au kiamini.

Je ipi inakubaliwa na Mungu?

Ijapokuwa Eksejesisi,(tafsiri ya awali) ndio msingi hasaa wa kusimamia katika kuyaelewa maandiko lakini eisojesisi pia Mungu huitumia kusema na sisi katika nyakati Fulani.

La kuzingatia ni kwamba kabla hujaipokea namna nyingine.. Ifahamu kwanza asili ya kwanza ya andiko hilo, ilikuwa ni nini.

Kwamfano Bwana Yesu aliposema.

Mathayo 11:28

[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

Katika Eksejesisi hiyo mizigo inayozungumziwa hapo na Bwana Yesu sio umaskini, Mateso, madeni, familia, majukumu,n.k. hapana, bali mizigo ya dhambi. Ndicho Bwana Yesu alichomaanisha na kusudi la kwanza lililomfanya kuja duniani lilikuwa ni hilo kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi zake.

Lakini pia Bwana anaweza tumia andiko hilo kulenga na mizigo mingine, kwasababu ni ukweli usiopingika alisema pia tumtwike yeye fadhaa zetu zote.

1 Petro 5:7

[7]huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

Hivyo namna zote Mungu anaweza kutumia kutujenga. Kwasababu Neno lake ni pana na njia zake hazichunguziki, katika kuwajenga, kuwafariji na kuwaponya watu. Isipokuwa hatari inakuja mtu kukosa kulipambanua vizuri Neno na matokeo yake kutegemea zaidi mtazamo (alioupokea), na kuacha biblia yenyewe kujieleza.

Hii ndio Imekuwa chumbuko la mafundisho mengi ya uongo, na potofu, kwamfano mtu atasema chapa ya mnyama (ufunuo 13) Ni ugonjwa wa Korona (covid-19). Wakati si kweli.

Au mtu atasema Yesu alitengeneza matope kwa mate yake akampaka mtu machoni akaona,(Yohana 9:6-7) hivyo na sisi kufanya kwa namna hiyo si kosa. Kumbe lile lilikuwa ni “ingilio la Mungu” la wakati husika lakini sio agizo la kudumu. Kwani agizo la daima ni kutumia jina la Yesu kutenda/kuamuru jambo lolote.(Kol 3:17)

Hivyo ili kubaki katika upande sahihi ni vema ukajifunza eksejesisi, (kufahamu muktadha wa kimaandiko), na ndio pale esiojesisi inapokuja Basi unaeweza Kuligawanya vema Neno la Mungu. Bila kuleta uharibifu/ madhara yoyote, katika imani au kwa kile unachowafundisha wengine.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

What Are the Different Types of Psalms?

If you’ve ever spent time reading the Psalms, you’ve probably noticed how wide-ranging they are—some feel like joyful songs, others like raw cries for help. That’s because the Psalms were written in different styles and for different purposes. Over time, scholars and readers have grouped them into a few main types to help us better understand them. Here’s a more down-to-earth look at each one:

🌟 1. Psalms of Praise

These are the joyful, uplifting psalms that focus entirely on God—who He is, what He’s done, and why He deserves our worship. They usually invite people (or even all of creation) to praise God and then give reasons for doing so.

  • Think: Big-picture awe and wonder.
  • Examples: Psalm 100, Psalm 148
  • Typical line: “Make a joyful noise to the Lord!”

😔 2. Psalms of Lament

These are some of the most emotional psalms. The writer is usually going through something really hard—feeling abandoned, attacked, or just overwhelmed—and cries out to God for help. What’s beautiful is that most of these still end with hope or a promise to trust God no matter what.

  • Think: Honest prayers from a hurting heart.
  • Examples: Psalm 13, Psalm 22
  • Typical line: “How long, O Lord? Will You forget me forever?”

🙏 3. Psalms of Thanksgiving

These are the “thank you” psalms. They usually reflect on a time when the writer was in trouble, called out to God, and then experienced His rescue or provision. It’s a look back at God’s faithfulness.

  • Think: Testimony in song form.
  • Examples: Psalm 30, Psalm 107
  • Typical line: “You turned my mourning into dancing.”

📖 4. Wisdom Psalms

These psalms feel more like life advice than a song. They talk about right and wrong, wise and foolish choices, and what it looks like to live in a way that honors God. Some sound like they could come straight from Proverbs.

  • Think: Spiritual guidance, usually contrasting good vs. evil.
  • Examples: Psalm 1, Psalm 119
  • Typical line: “Blessed is the one who does not walk in the counsel of the wicked.”

👑 5. Royal Psalms

These focus on kingship—sometimes about the earthly king of Israel (like David), and sometimes pointing ahead to the Messiah. They remind us that God is King over everything and that He works through leaders to bring justice.

  • Think: Big picture of God’s rule and promises.
  • Examples: Psalm 2, Psalm 72
  • Typical line: “You are my Son; today I have begotten You.”

💢 6. Imprecatory Psalms

These are the tough ones. In these psalms, the writer asks God to deal harshly with enemies or bring justice to evildoers. They come from a place of deep pain or injustice—not out of personal revenge, but a plea for God to act righteously.

  • Think: “God, this isn’t fair—do something!”
  • Examples: Psalm 69, Psalm 137
  • Typical line: “Let their names be blotted out of the book of life.”

These categories aren’t rigid—many psalms overlap. A lament might turn into praise. A royal psalm might include thanksgiving. That’s part of what makes the Psalms so real and relatable: they reflect the full range of human emotion and experience in our relationship with God.

Print this post

Nini maana ya Selahamalekothi?

Ilikuwa ni desturi ya wayahudi kuyapa majina, maeneo yote ambayo walikutana na Mungu kipekee.

Kwamfano Yakobo alipokutana na Mungu mahali fulani palipoitwa Luzu, kwa kuona maono yale ya ngazi kushuka kutoka mbinguni, na malaika wanashuka na kukwea, hakuondoka hivi hivi bali alipaita mahali pale Betheli yaani ‘ nyumba ya Mungu’ (Mwanzo 28:10-22).

Sehemu nyingine Mungu alipowasaidia Israeli kuwapiga wafilisti kwa kishindo kikubwa, Samweli alilisimamisha jiwe na kuliita Eneb-ezeri akimaanisha ‘hata sasa Bwana ametusaidia’ na 1Samweli 7:12.

Hivyo pia tukisoma kisa cha Mfalme Sauli na Daudi, tunaona mara nyingi Daudi alipowindwa ili auawe alifanikiwa kumtoroka Sauli, lakini upo wakati ambao alihusuriwa pande zote, Daudi akawa hana namna isipokuwa kungojea tu kuuliwa palepale pangoni, sasa wakati ambapo Sauli amemkaribia sana Daudi. Taarifa za ghafla zilimfikia na kuambiwa kwamba wafilisti wamevamia Israeli, hivyo ikambidi aache kumfuatilia Daudi arudi Israeli kupambana na adui zake.

Sasa tendo hilo la wokovu halikumwacha Daudi awe vilevile kinyume chake, alipaita mahali pale Selahamalekothi

1 Samweli 23:26-28

[26]Sauli akaenda upande huu wa mlima, na Daudi na watu wake wakaenda upande huu wa mlima; naye Daudi akafanya haraka sana kwenda zake kwa hofu ya Sauli; kwa sababu Sauli na watu wake wakamzunguka Daudi na watu wake ili kuwakamata.

[27]Lakini akaja mjumbe kwa Sauli, kusema, Njoo upesi, kwa kuwa Wafilisti wameishambulia nchi.

[28]Basi Sauli akarudi kutoka kumwinda Daudi, akaenda kinyume cha Wafilisti; kwa hiyo wakapaita mahali pale, Selahamalekothi.

Selahamalekothi ni neno la kiebrania lenye maana ya MWAMBA WA KUTOROKEA.

Daudi na watu wake walipaita mahali pale hivyo kufuatana ba jinsi Mungu alivyowaepusha na mkono wa Sauli, kwa njia isiyodhaniwa/ kutegemewa hata kidogo.

Ni kwanini wayaite majina maeneo hayo?

Ni Ili kuendelea kukumbuka matendo makuu Mungu aliyowatendea wasizisahau wafidhili zake kabisa.

Je na sisi ni alama gani tunaacha mahali ambapo tunamwona Mungu ametutendea makuu. PENDA kuandika shuhuda zako, ili wakati ujao zikusaidie kukumbuka fadhili za Mungu umshukuru.

Kikawaida Mungu huwa anatufanyia maajabu mengi Sana kila siku, lakini tunakuwa wepesi kuyasahu, ni vema tujifunze kwa namna yoyote kutunza kumbukumbu, hata kama si kwa kuandika lakini kwa njia zozote zile, mfano wa mababa zetu hawa.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

SIKU YA HOFU YANGU NITAKUTUMAINI WEWE.

Print this post

Wanethini ni watu gani kwenye biblia?

Wanethini ni kundi la watu ambao walitumika katika hekalu, ambao sio asili ya wayahudi. Wanatajwa sana kwenye kitabu cha Nehemia na Ezra. Maana ya neno ‘Nethini’  kwa kiyahudi linamaanisha “waliotolewa”. Wakimaanisha watu waliotelewa kuwasaidia walawi katika shughuli za hekaluni.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowataja;

Ezra 8:20 na katika Wanethini, ambao Daudi, na wakuu, walikuwa wamewaweka kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini mia mbili na ishirini; wote wametajwa kwa majina yao.

Nehemia 7:73 Hivyo makuhani, na Walawi, na mabawabu, na waimbaji, na baadhi ya watu, na Wanethini, na Israeli wote, wakakaa mijini mwao. Hata ulipowadia mwezi wa saba, wana wa Israeli walikuwa wakikaa katika miji yao.

Soma pia, (Ezra  2:43, 2:58, 7:24)

Asili yao:

Biblia haituonyeshi moja kwa moja asili yao ni wapi, lakini wanazuoni wengi huamini walitokea katika chimbuko la wale wagibeoni waliowadanganya Israeli wakati ule mpaka wakafanya nao maagano, Ambao Yoshua aliwapa kazi ya kupasua kuni, na kuteka maji.

Yoshua 9:27 Siku iyo hiyo Yoshua akawafanya kuwa ni wenye kupasua kuni, na wenye kuteka maji, kwa ajili ya mkutano, na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana, hata siku hii ya leo, katika mahali hapo atakapopachagua

Mbali na hawa wagibeoni wengine wanaweza wakawa ni wageni au mateka., ambao baadaye wakaja kuwekwa kwenye utumishi wa hekaluni.

Kazi yao:

Wanethini hawakufanya kazi zozote za kikuhani, ikumbukwe kuwa ilikuwa ni kosa, mtu ambaye sio myahudi tena wa kabila la Lawi kufanya shughuli zozote za kihekalu, Hawa walikuwa wanafanya kazi za usaidizi ule wa nje, kama vile kutweka maji, kukusanya kuni, usafi, na kazi nyingine zilizohitaji msaada wa pembeni.,Ili kuwaruhusu walawi wasilemewe  wajikite zaidi katika kazi za hekaluni.

Maandiko yanaonyesha walikuwa na makao yao maalumu palipoitwa Ofeli kule Yerusalemu karibu na hekalu (Nehemia 3:26)

Hata Baadaya ya uhamisho wa Babeli, tunaona mabaki yaliyorudi Israeli kufanya shughuli za kihekalu, hawa wanethini pia walirejea

Kwa ufupi wanethini walikuwa ni la watu (wasio-wayahudi) waliowekwa kwa ajili ya kusaidia shughuli za hekaluni.

Kwanini Bwana aruhusu jambo hili?

Licha ya kwamba Mungu ameliita kanisa lake na amelitenga, limtumikie lenyewe katika shughuli zote za kimadhabahu. Lakini Bado Bwana anaweza kunyanyua watu wengine nje ya kanisa, kusaidia kanisa kusonga mbele. Mfano wa hawa ni Yule akida wa kirumi ambaye alilipenda taifa la Israeli na  kulijengea sinagogi (Luka 7:1-5). Hakuwa myahudi lakini aliwasaidia wayahudi.

Hata sasa wanethini wapo wengi, hawapaswi kuzuiliwa, endapo wanasaidia kanisa au kazi ya Mungu, kwasababu ni Bwana ndiye aliyewavuta.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post