Shushani ngomeni ni sehemu gani kwasasa?
Mji wa shushani/Susa kwasasa upo eneo linaloitwa Shush katika nchi ya Iran.
kabla wamedi na waajemi kuiangusha Babaeli, Shushani ulikuwa ni mji mkuu wa Elamu, ambao tunaona Danieli akiuzungumzia katika.
Danieli 8:1 “Katika mwaka wa tatu wa kumiliki kwake mfalme Belshaza maono yalinitokea mimi, naam, mimi Danieli, baada ya hayo yaliyonitokea hapo kwanza.
2 Nami naliona katika maono; ilitukia, nilipoona, nalikuwako huko Shushani ngomeni, katika wilaya ya Elamu; nikaona katika maono, nami nalikuwa karibu na mto Ulai”.
Lakini baada ya wamedi na waajemi kuuchukua ufalme, mji huu ulikuja kugeuzwa kuwa mji wa kifalme wa wafalme wa Uajemi na Umedi.
Katika biblia tunaona Esta aliishi sehemu kubwa ya umalkia wake katika mji huu wa kifalme Shushani.
Esta 1:1 Zamani za Ahasuero; naye huyu Ahasuero alimiliki toka Bara Hindi mpaka Kushi, juu ya majimbo mia na ishirini na saba;
2 siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;
Unaweza kusoma pia, (Esta 2:3,5,8 Esta 3:15, Esta 4:8,16, Esta 8:14, Esta 9:6,11,12,13.)
Vilevile Nehemia naye alipokuwa mnyweshaji wa mfalme wa kiajemi alikuwa katika mji huu, huu wa Shushani..
Nehemia 1:1 “Habari za Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa katika mwezi wa Kisleu, mwaka wa ishirini, nilipokuwapo Shushani ngomeni,
2 Hanani, mmoja wa ndugu zangu, akanijia, yeye na watu wengine waliotoka Yuda; nami nikawauliza habari za Wayahudi waliopona, hao watu wa uhamisho waliosalia; na habari za Yerusalemu”.
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia ya mara kwa mara kwa njia ya whatsapp au email yako, basi tutumie ujumbe kwa kupitia namba hii: +255 789001312
Mada Nyinginezo:
MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?
Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?
Israeli ipo bara gani?
UNYAKUO.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Safari ya kwenda mbinguni ni safari isiyo na siku ya kupumzika. Kama vile moyo unavyodunda bila kusimama kwa miaka na miaka…Ndivyo safari ya Mbinguni ilivyo.. Ni mwendelezo kila kukicha, tukilala, tukiamka tupo safarini.
Hivyo ni lazima kulikumbuka hilo. Na safari ya kwenda mbinguni ni ngumu kuliko ya kwenda kuzimu. Hata katika hali ya kawaida, kupanda juu ni kugumu kuliko kushuka… Ukitaka kushuka kilima unaweza kujiachia tu ukaserereka mpaka ukafika chini, pasipo kutumia nguvu yoyote.
Lakini upandapo kilima huwezi kujiachia, ni lazima kupambana na kutumia nguvu nyingi ili kufika juu. Na safari ya kwenda mbinguni ipo hivyo hivyo. Kila hatua ni ya kujishika usianguke. Kwasababu ipo nguvu itakayotuvuta chini tusipojishika vizuri.
1Wakorintho 10:12 “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.
Hivyo ni lazima tujiangalia sana! kwasababu kubomoa ni rahisi kuliko kujenga, mahali tunapoishi, mahali tunapofanyia kazi, mazingira tunayoishi n.k Ni lazima kuhakikisha hayaharibu imani yetu na wala hayakwamishi safari yetu ya kwenda mbinguni.
Mbingu ipo! na Kristo Mwana wa Mungu anarudi!.
Bwana akubariki.
Mada Nyinginezo:
IPELEKE SADAKA YAKO MAHALI SAHIHI,ILI UBARIKIWE.
Je! Shetani alitolea wapi uovu?
UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.
FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.
NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Neno la Mungu ambalo ndio taa ya miguu yetu na mwana uiongozayo njia yetu (Zab.119:105).
Katika safari ya Imani usisahau kamwe kuifanya kazi ya Mungu kwa bidii, kuhakikisha Habari ya ufalme inamfikia kila mtu. Lakini lililo kubwa Zaidi ni kuhakikisha wewe Pamoja na nyumba yako mnaokolewa, wewe Pamoja na Watoto wako, mume wako, mke wako na Watoto wako na wote unaoishi nao wanaokolewa. Utasema hiyo inawezekana hata kama hawataki kabisa kusikia Habari za Mungu?..Jibu ni ndio inawezekana.
Kama umewahi kusoma Habari za Rahabu, utakuwa unaelewa…alipopewa nafasi ya kuokoka yeye peke yake binafsi, hakuona ni vyema kuokoka mwenyewe bali aliiokoa na familia yake yote..
Yoshua 2:12 “Basi sasa, nawasihi, niapieni kwa Bwana, kwa kuwa nimewatendea ihisani, ya kwamba ninyi nanyi mtaitendea ihisani NYUMBA YA BABA YANGU; tena nipeni alama ya uaminifu
13 ya kwamba mtawaponya hai baba yangu na mama yangu, na ndugu zangu wanaume na wanawake, na vitu vyote walivyo navyo, na kutuokoa roho zetu na kufa.
14 Wale wanaume wakamwambia, Uhai wetu badala ya uhai wenu, ikiwa hamwitangazi habari ya shughuli yetu hii; kisha itakuwa, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutakutendea kwa ihisani na uaminifu”
Kama umewahi kusoma pia Habari za Lutu utakuwa unajua kuwa kabla ya maangamizi kushuka, aliondoka na mke wake na Watoto wake wawili, na baadhi ya ndugu zake pia aliwahubiria.
Na hata wakati wa Gharika..Nuhu hakuona vyema kuokoka yeye peke yake lakini biblia inasema Safina ile aliyoitengeneza ilikuwa pia ni kwaajili ya Watoto wake.
Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.
7 Kwa imani Nuhu akiisha kuonywa na Mungu katika habari za mambo yasiyoonekana bado, kwa jinsi alivyomcha Mungu, ALIUNDA SAFINA, APATE KUOKOA NYUMBA YAKE. Na hivyo akauhukumu makosa ulimwengu, akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa Imani”.
Umeona hapo? Anasema aliiunda ili apate kuiokoa familia yake, kwahiyo lengo la Safina halikuwa kumwokoa Nuhu tu, Mungu angeweza kumwokoa Nuhu kwa njia nyingine bila hata hiyo Safina, lakini kwasababu Nuhu alikuwa na familia na pia kulikuwa na Wanyama, Ndipo Mungu akatengeneza njia hiyo ya wokovu kwa kupita Safina.
Na kama umegundua kitu ni kwamba Mungu hakuitengeneza yeye ile Safina bali alimwambia Nuhu aitengeneze, kwasababu aliyekuwa ameonekana mwenye haki mbele za Mungu ni Nuhu peke yake, (Mwanzo 6:8) hao mwengine hawakustahili, hawakumpendeza Mungu kabisa katika njia zao, ndio maana utaona Hamu kipindi kifupi tu baada ya kutoka kwenye Safina aliutazama uchi wa Baba yake kwa makusudi, na wala hata hakusikia kitu kikimhukumu ndani yake kwa alichokifanya. (Sasa unaweza kujiuliza imekuwaje mtu kama huyo hakuangamia kwenye gharika Pamoja na waovu wengine). Jibu ni kwasababu ya Baba yao…hivyo gharama za kuwaokoa watoto wake na mke wake zilikuwa ni za Nuhu..
Hivyo Nuhu ilimbidi afanye kazi kubwa ya kutengeneza Safina ile kwa miaka mingi sana, ili tu familia yake ipone na baadhi ya wanyama.
Kadhalika utasoma pia Musa, alikuwa ni mtu wa namna hiyo hiyo, kwani ulipofika wakati wana wa Israeli jangwani walipomkasirisha Mungu kiasi cha Mungu kutaka kuwaangamiza wote, Musa alisimama kuwatetea mbele za Mungu kwa bidii.
Kutoka 22:7 “Bwana akamwambia Musa, Haya! Shuka; kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao,
8 wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu, wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.
9 Tena Bwana akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu.
10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
11 Musa akamsihi sana Bwana, Mungu wake, na kusema, Bwana, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.
13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.
14 Na Bwana akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake”
Mifano ipo mingi sana, hatuwezi kuandika yote hapa, lakini kwa hiyo michache unaweza kuelewa kuwa sisi tuliobahatika neema ya wokovu, tunalo jukumu la kusimama kwaajili ya nyumba zetu. Bwana amekupa neema wewe mmoja, ili wengine wote katika nyumba yako waokolewe. Ni jukumu lako na si la Mungu, kupambana kwa bidii ili waingie ndani ya mlango huu wa Neema, kama Musa alivyopambana, kama Nuhu alivyopambana, kama Lutu alivyopamba na kama Rahabu alivyopambana. Na hiyo inakuja kwa kuwaombea kwa bidii na si kuwahukumu, inakuja kwa kuhubiria wanao kwa bidii sana Habari za wokovu, kwa kumhubiria mkeo au mumeo na kumwombea..huku wewe mwenyewe ukionyesha kumpendeza Mungu na kutokuiga wala kufanya matendo kama yao.
Kwa kufanya hivyo ipo neema ya wokovu ambayo itamwagika kwa watu wa nyumbani kwako pia, nao pia mwishoni wataokolewa kama wewe. Hivyo hupaswi/hatupaswi kufurahia wokovu ukiwa kwetu tu!.. tunapaswa tufurahie ukiwa kwa wengine pia.
Mwisho kabisa. Bwana anakaribia kurudi, mambo yote ya ulimwengu yatabatilishwa, na mlango wa neema utafungwa Bwana Yesu alisema wengi watatamani kuingia siku hiyo wasiweze. Hivyo kama hujampokea Yesu na unasoma jumbe hizi kila siku, au jumbe nyingine zinazofanana na hizi, basi siku ile hutasema hukusikia, nakushauri yakabadhi Maisha yako kwa Yesu, yeye ndiye Njia, kweli na Uzima..hakuna namna utaweza kuiona mbingu kama unakataa Habari za uzima sasa.
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
HATUTAACHA KUJIFUNZA NENO KILA INAPOITWA LEO.
Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?
USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.
Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?
HUYU SI YULE SEREMALA, MWANA WA MARIAMU?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2
Ikabodi maana yake ni “Utukufu umeondoka”
Hili ni jina ambalo alipewa mtoto wa Finehasi na mke wake siku alipokuwa anajifungua, na hiyo ni baada ya kusikia Mume wake amekufa katika vita, pamoja sanduku la agano kuchukuliwa na wafilisti na yeye vilevile anakaribia kufa ndipo akaona jina sahihi linalompasa huyo mtoto ni IKABODI, akiwa na maana kuwa utukufu wa Mungu umeondoka katika Israeli.
1Samweli 4:19 “Tena mkwewe, mkewe huyo Finehasi, alikuwa mja-mzito, karibu na kuzaa; basi, aliposikia habari ya kutwaliwa sanduku la Mungu, na ya kwamba mkwewe na mumewe wamekufa, akajiinamisha, akazaa; maana utungu wake ulimfikilia.
20 Hata alipokuwa katika kufa, wale wanawake waliohudhuria karibu naye wakamwambia, Usiogope; kwa maana umezaa mtoto mwanamume. Walakini hakujibu, wala hakumtazama.
21 Akamwita mtoto, IKABODI, akisema, Huo utukufu umeondoka katika Israeli; kwa sababu sanduku la Mungu lilikuwa limetwaliwa, na kwa sababu ya mkwewe na mumewe.
22 Naam, akasema, Huo utukufu umeondoka katika Israeli; maana sanduku la Mungu limetwaliwa”.
Lakini hiyo yote ni kwasababu ya Makosa ya Eli kuhani mkuu kutowazuia watoto wake (Hofni na Finehasi) kuinajisi madhabahu ya Mungu, kwa kulala na wale wanawake waliokuwa wanahudumu mbele ya hema ya Bwana. Japokuwa walionywa sana lakini hawakusikia, ndipo Mungu akamwambia Eli kwa kinywa cha Samweli kuwa atafanya jambo ambalo wakisikia, masikio yao wote yatawasha..Na jambo lenyewe ndio hilo la Sanduku la Mungu kuibwa na maadui jambo ambalo halijawahi kutokea katika historia ya taifa la Israeli.
Hata sasa, utukufu wa Mungu unaweza kuondoka katika kanisa Fulani(Ikabodi), ikiwa wahudumu au watumishi wa madhabahuni hiyo ya Mungu watainajisi nyumba ya Mungu kwa kufanya dhambi za makusudi, mfano wa hawa watoto wa Eli.
Vilevile utukufu wa Mungu unaweza kuondoka(Ikabodi), kwa mtu binafsi, ikiwa ataonywa mara nyingi asisikie. Ikiwa na wewe unaonywa mara nyingi auche dhambi, uache uzinzi, uache anasa, utubu umgeukie Kristo lakini husikii, upo wakati huo utukufu wa Mungu utaondoka ndani yako moja kwa moja, na siku ukiondoka basi habari yako imeishia hapo hapo kamwe hutakaa uiamini injili tena.
Hivyo ikiwa upo bado nje ya Kristo tubu dhambi zako ukabatizwe. Na Bwana atakuponya.
Kama upo tayari kufanya hivyo, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo ya biblia kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?
USISUBIRI MPAKA MUNGU AKUAMBIE, NDIO UFANYE!
CHA KUTUMAINI SINA lyrics
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
EPUKA MUHURI WA SHETANI
Shalom.
Marko 8:23-26 Inatuambia Yesu alipokutana na Yule kipofu kule Bethsaida, Hakumponya palepale kama ilivyokuwa desturi yake ya kuponya watu wote wanaomfuata, bali biblia inatuambia alimchukua kwa kumshika mkono na kuanza kumtoa kwanza nje ya kijiji.
“22 Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.
23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu?
24 Akatazama juu, akasema, Naona watu kama miti, inakwenda.
25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.
26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie”.
Jaribu kutengeneza picha, wewe ni kipofu, unapelekwa kwa daktari kwa ajili ya kupewa dawa uondoke, badala ya kukutibu anakuchukua anaondoka na wewe, bila maelekezo yoyote, na kibaya zaidi afadhali angekuwa anakupeleka hospitali nyingine badala yake anakupeleka mahali ambapo hata husikii tena sauti za watu, nje kabisa ya mji, ni rahisi kudhani huyu mtu hana nia nzuri na mimi.. Lakini tunaona huyu kipofu alitii, japokuwa hajui ni wapi anapelekwa, pengine alitembezwa na Yesu kilometa kadhaa, mpaka wanafikia mahali ambapo hamna makazi ya watu, ni mashamba tu, hata wale watu waliompeleka kwake walishamwacha, amebaki yeye tu na Yesu, na pengine na wanafunzi wake tu.
Akiwa sasa hana tumaini lolote, haelewi ni kitu gani kinaendelea hapo ndipo Yesu anamwekea mikono yake, na kumponya..Lakini utajiuliza tena, ni kwanini biblia inatuaeleza aliponywa mara ya kwanza na ya pili?..Ni kwasababu kuna jambo Yesu alitaka tujue kuhusu upofu wa Yule mtu..Ukiyatafakari vizuri maneno yake utagundua kuwa mtu Yule hakuwa kipofu tangu alipozaliwa, bali aliupata upofu wake wakati Fulani katika maisha yake. Kwasababu kama angekuwa ni kipofu wa kuzaliwa asingesema naona watu kama miti inakwenda..Mtu aliyezaliwa kipofu hawezi kutofautisha mti na mtu.
Hivyo upofu wake hakuzaliwa nao, aliupata sehemu Fulani, na huko si kwingine zaidi ya kule kijijini alipokuwepo. Na ndio maana utaona Bwana Yesu alimpomaliza kumponya akamwambia..Hata kijijini usiingie.
Hichi ndicho kinachoendelea sasahivi rohoni, ulimwengu huu umewapofusha watu wengi rohoni, masumbufu ya ulimwengu huu, anasa, mambo ya kidunia, hawaoni tena kuwa hizi ni siku za mwisho, hawaoni tena kuwa unyakuo upo karibu, hawaoni tena kuwa dunia hii imeshaoza, haijalishi watasikia injili ngumu kiasi gani bado wataona ni kawaida tu..
2Wakorintho 4:3 “Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea;
4 AMBAO NDANI YAO MUNGU WA DUNIA HII AMEPOFUSHA FIKIRA ZAO WASIOAMINI, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.
Lakini kama tunavyosoma hapo, mtu akitaka Yesu amfumbue macho, hakuna njia ya mkato vigezo ni sharti Yesu akuchukue nje ya kijiji..Ni lazima kwanza katika upofu wako ukubali Yesu akutoe katika ulimwengu, ni sharti ukubali kujitenga na anasa, lazima ukubali kuacha fashion na kuvaa mavazi ya kikahaba, ni lazima ukubali kuachana na marafiki wabaya, na mambo yote yasiyompendeza Mungu, yaani kwa ufupi ukubali kuipoteza nafsi yako kwenye mambo ya kidunia, na hapo ndipo Bwana YESU atakapokufumbua macho yako, na kuona mambo yote ya rohoni WAZI WAZI,
Kumwona shetani jinsi anavyofanya kazi katikati ya watu wa ulimwengu huu, kuona jinsi unyakuo ulivyo karibu, kuona jinsi ulivyokuwa hatarini kuelekea kuzimu.. Hapo ndipo utajijua kweli ulikuwa kipofu, lakini sasa hivi upo kwenye ulimwengu huwezi kujiona kwasababu tayari umepofushwa macho.
Ndugu pengine hii ni mara yako ya elfu kulisikia hili Neno kuwa hizi ni siku za mwisho, Hata kama Unyakuo hautakukuta, basi ujue hata siku zako za kuishi hapa duniani si nyingi, hujui kesho utaamkia wapi? Wanaokufa na kushuka kuzimu idadi yao haihesabiki, ukifa leo katika upofu ulio nao, hakuna tumaini tena la uzima baada ya hapo.
Kama wewe ni mkristo na unajua kuwa hili ndio kanisa la mwisho la 7 lijulikanalo kama Laodikia (Ufu.3:14) na kwamba hakutakuwa na kanisa lingine baada ya hili (Ufu.10:7), halafu bado huyathamini maisha yako ya rohoni, hiyo ni dalili kubwa kuwa umepofushwa macho na ulimwengu huu.
Huu ni wakati ambao tayari magugu na ngano vimeshajitenga, wale walio hapo katikati (yaani vuguvugu), upande wao ni wa shetani, kwasababu Bwana Yesu alishasema atawatapika..Ni heri utemwe, kuliko kutapikwa, matapishi hata kuyaangalia huwezi, sembuse kuliwa tena?.Usisibiri utapikwe, Tubu mtafute Bwana Yesu hichi kipindi cha kumalizia.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je udhaifu au ulemavu wangu unaweza kuzuia watu kumwamini Yesu?
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.
Lipo swali moja muhimu sana linaloulizwa na wengi?..Je kama mimi nina tatizo fulani labla la kuona, au kusikia, au nina ulemavu fulani ambao unaonekana kabisa…Je hali kama hiyo nikienda kuhubiri/kushuhudia watu wataokoka kweli?..Si wataniuliza mbona huyo Mungu hajakuponya wewe kwanza atawezaje kutuponya sisi?.
Hii ni mojawapo ya silaha ya shetani anayoitumia kuhakikisha injili haihubiriwi!…Na silaha nyingine anayoitumia ni sauti inayosema “umemkufuru Roho Mtakatifu”..ukisikia sauti yoyote unakuambia hayo maneno mawili kwamba “huwezi kuhubiri kutokana na udhaifu wako” au “umeshamkufuru Roho Mtakatifu”.. Basi jua moja kwa moja hizo ni sauti za Adui shetani, hivyo zipuuzie!.
Sasa kabla ya kuendelea mbele ni vizuri tukafahamu mambo machache yafuatayo.
Kwanza Aliyepewa jukumu la kuhubiria wanadamu injili, ni Mwanadamu huyo huyo na si malaika. Hakuna mahali popote Mungu amewahi kumtuma malaika akahubiri injili. Na hakuna mwanadamu aliyeumbwa na Mungu asiye na kasoro kabisa!..Hata yule mhubiri maarufu na mashuhuri unayemfahamu na kumsikia anayo mapungufu yasiyohesabika. Kwahiyo Mungu anajua kabisa wanadamu wote wanayo mapungufu lakini akawapa hivyo hivyo jukumu la kubeba maneno yake na kuwasambazia wengine wasiyo nayo. Hivyo angekuwa anaangalia udhaifu kama ndio kigezo cha mtu kwenda kulihubiri neno lake, hakuna mwanadamu angestahili kuwa mhubiri…pengine Mungu angewatumia malaika wake walio watakatifu huko mbinguni na wala si wanadamu.
Kwahiyo kumbe kasoro zetu hazihusiani na sisi kukidhi vigezo vya kuhubiri Neno la Mungu!..maana yake ni kwamba uwe mrefu, uwe mfupi, uwe unajua kuongea au hujui kuongea vizuri, uwe na kigugumizi, uwe mzungu, uwe mwafrika, uwe albino, uwe kiziwi, uwe kipofu, uwe huna miguu, uwe huna mikono, uwe maskini, uwe tajiri, uwe hujui kusoma, uwe mtu mdogo kabisa katika jamii, uwe mtu mkubwa.. uwe yoyote yule uwazaye kuwa, maadamu unaitwa MWANADAMU!. Basi umeshafuzu kuwa na uwezo wa kulibeba Neno la Mungu na kuwapelekea wengine.
Kigezo cha kwanza cha wewe kuweza kuwapelekea wengine NENO la Mungu ni wewe kwanza uwe na hilo Neno la Mungu ndani yako. Hicho ndio kigezo cha kwanza na cha Muhimu, kwasababu hata katika hali ya kawaida, hakuna mwalimu anaweza kumfundisha mwanafunzi maarifa ambayo yeye mwenyewe hana!. Hivyo ni lazima Neno la Kristo likae ndani yako, na hiyo inakuja kwa kumpokea Mwokozi Yesu Kristo na kulisoma Neno lake na KULIISHI HILO NENO!.
Baada ya hapo! Unaweza kuhubiri Injili kwa mtu yeyote yule.. Usisubiri Uone maono, au utokewe na Yesu au Malaika.. Wengi wanaisubiri hii hatua na hawaifikii..Wanatamani wasikie sauti KWANZA ikiwaambia nenda kahubiri!.. “Ndugu usiisubirie hiyo sauti “ hutakaa uisikie milele..Ni kwanini hutakaa uisikie?..Ni kwasababu tayari alishasema katika neno lake… “ENENDENI MKAWAFANYE MATAIFA YOTE KUWA WANAFUNZI..(Mathayo 28:28)”. Usisubiri sauti nyingine..hutaisikia!!
Sasa Swali lingine…Ni nini kinachomgeuza Mtu kama sio Ukamilifu wetu wa kuongea na kusikia vizuri?
Tusome mstari ufuatao kisha tutajua..
Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”
Hapo anasema “NENO LA MUNGU” Sio maneno yaliyopangiliwa vizuri, wala sio midomo yetu inayoweza kuumba maneno mwanana, wala sio rangi za nyuso zetu, wala sio masikio yetu yanayosikia vizuri maneno tunayoulizwa na wale tunaowahubiria, wala macho yetu yanayotazama vyema watu tunaowahubiria wala ufupi wetu, wala urefu wetu, wala elimu yetu…Bali NENO LA MUNGU!..Hilo ndio lenye nguvu…linapotajwa na mwanadamu yeyote ambaye kalishika…basi linapenya mpaka ndani ya ule moyo wa anayelisikia..linamchana chana na kumgawanya moyo wake…linapenya na kumfunulia yule anayelisikia mambo yake ya siri anayoyafanya atoke katika hali yake ya kawaida. Wakati wewe unafikiri anasikiliza kigugumizi chako, au anazitafakari kasoro zako… kumbe mwenzio Roho Mtakatifu anateta naye huko, anaugulia ndani kwa ndani..
2Wakoritho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo”
Kwahiyo usikubali kusikiliza uongo wa shetani ambao unakukatisha tamaa kwenda kuhubiri injili..Kama husikii vizuri, wewe hubiri hivyo hivyo, yule unayemhubiria akikuuliza swali sogea karibu msikilize tena na tena, ukiona bado humsikiI, wewe endelea mbele..usianze kuutafakari udhaifu wako…kwasababu hata yeye wakati huo atakuwa hautafakari udhaifu wako!… na pia hatakuchukia ila lile Neno utakalomwambia hata kama ni moja tayari ni Nguvu ya Mungu..na ni mbegu..
Tatizo kubwa la wengi ni kufikiri kwamba Injili ni maneno mengi… jambo ambalo sio kweli!…Mtu anayehubiri maneno mengi basi ni kaongozwa na Roho kufanya hivyo…Lakini Neno moja tu la MUNGU!..Linatosha kubadilisha moyo mgumu wa jiwe na kuwa mlaini.. Kwa neno moja tu la Mungu na iwe Nuru!..ndio iliumba jua hili ambalo mpaka leo tunalo vizazi na vizazi.. Hivyo usitafute sana ujuzi wala utaalamu katika kwenda kulitangaza Neno la Mungu…Wewe Tafuta Roho Mtakatifu. Kisha itumie karama yako Mungu aliyokupa.
Mwanamke mmoja mashuhuri anayeitwa Fanny Crosby alizaliwa akiwa mzima lakini baada ya wiki mbili akawa kipofu, aliishi duniani katika hali hiyo hiyo ya upofu kwa muda wa miaka 95, lakini hakuacha kutafuta mahali ambapo angemtumikia Mungu licha ya kuwa alikuwa kipofu, alifanikiwa kuandika nyimbo zaidi ya 8,000, katika kipindi hicho cha karne ya 19, akajulikana kwa jina la malkia wa nyimbo za injili, na mwimbaji kipofu, moja ya tenzi mbili muhimu ambazo mpaka leo hii unazijua na kuziimba “Usinipite Mwokozi” na “Ndio dhamana Yesu wangu” pengine ulikuwa hujui ziliimbwa na huyu mama kipofu, na kwa kupitia uimbaji wake, na kuwahubiria wengine alifanikiwa kuwavuta watu wengi kwa Kristo.
Hivyo na sisi, kila mmoja wetu amesimame na kile Mungu alichokiweka ndani yake kuhakikisha injili inawafikia wengi.
Bwana akubariki.
www wingulamshahidi org
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
USINIPITE MWOKOZI Lyrics
REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.
MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU
Mto Frati upo nchi gani, na Umuhimu wake katika biblia ni upi, kwanini utajwe sana?
Mto Frati ni moja ya mito mikubwa na mirefu iliyopo Mashariki ya kati, Mto mwingine ukiwa ni Hidekeli (Tigris), mto huu unaanzia Uturuki na kutoka hapo unakatiza katika nchi ya Syria na Iraq na kwenda kumwaga maji yake katika Ghuba ya uajemi.
Tazama picha.
Mto Frati na Mto Hidekeli (Tigris) ni moja ya mito minne ambayo inatajawa kwenye biblia ilikuwa inatoa maji katika bustani ya Edeni.
Mwanzo 2:10 “Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne.
11 Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu;
12 na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham. 13 Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi.
14 Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati”.
Lakini kingine cha kushangaza juu ya mto Frati ni kuwa umetajwa pia kitabu cha Ufunuo, Kama tu vile Babeli ilivyotajwa tangu kwenye kitabu cha Mwanzo hadi Ufunuo. Kuonyesha kuwa kama vile ilivyo Babeli ya mwilini, hivyo hivyo pia ipo Babeli ya rohoni (Ufunuo 17 & 18). Halikadhalika na kwa mto Frati, sio tu ule unaouna pale Mashariki ya kati, hapana bali pia rohoni upo, na siku moja utakauka, na ukishakauka basi dunia itaingia katika vita kuu ya Tatu ya dunia
Ufunuo 9:14 ikimwambia yule malaika wa sita aliyekuwa na baragumu, Wafungue nao malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Frati.
15 Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue theluthi ya wanadamu.
16 Na hesabu ya majeshi ya wapanda farasi ilikuwa elfu ishirini mara elfu kumi; nilisikia hesabu yao.
17 Hiyo ndivyo nilivyowaona hao farasi katika maono yangu, nao waliokaa juu yao, wana dirii kifuani, kama za moto, na za samawi, na za kiberiti; na vichwa vya farasi hao ni kama vichwa vya simba, na katika vinywa vyao hutoka moto na moshi na kiberiti.
18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo matatu hayo, kwa moto huo na moshi huo na kiberiti hicho, yaliyotoka katika vinywa vyao.
19 Kwa maana nguvu za hao farasi ni katika vinywa vyao, na katika mikia yao; maana mikia yao ni mfano wa nyoka, ina vichwa, nao wanadhuru kwa hivyo”.
Unaona?. Watu wengi hawajui kuwa kipindi hicho kimekaribia sana,. Lakini kabla hilo halijatokea, kutatungulia kwanza Tukio la UNYAKUO, (kufahamu vizuri unyakuo utakuwaje kuwaje, tazama, masomo yaliyoorodheshwa chini).
Dalili zote zinaonyesha kizazi chetu kitaweza kushuhudia mambo hayo yote. Swali la kujiuliza Je! na wewe umejiwake tayari kwa tukio la kurudi kwa pili kwa Yesu Kristo? Je! Maisha yako yanauhakisi wokovu? Kama sivyo basi jitathimini sasa kwasababu ni kipindi kifupi cha neema tulichobakiwa nacho, Dunia hii inapumbaza kweli na wengi hawalijui hilo, Yesu atakuja kama mwivi usiku.
Hivyo kama upo tayari kumpa Yesu leo maisha yako, hilo jambo la muhimu sana, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo ya Neno la Mungu kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Tazama chini vichwa vingine vya masomo.
Mada Nyinginezo:
MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?
MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?
UFUNUO: Mlango wa 9.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
MAONO YA NABII AMOSI.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Mto Yordani uko nchi gani kwa sasa duniani?
Mto Yordani upo katika eneo la Mashariki ya kati, ni mto ambao unasimama kama mpaka wa mataifa mbalimbali, Ikiwemo Lebanoni, Syria, Israeli, na Yordani.
Ni kama vile ziwa Tanganyika lilivyo simama kama mpaka wa nchi 4, Congo, Burundi, Tanzania, na Zambia ndivyo ilivyo hata na kwa mto Yordani,
Nchi ya Yordani, unayoisikia leo hii pale mashariki ya kati, imechukua jina lake kutoka katika mto huu.
Mto huu chanzo chake ni kwenye chemchemi kadhaa zinazotiririka kutoka katika mlima Hermoni ulio mpakani mwa Lebanoni na Syria.Kisha kutoka hapo unateremsha maji yake mpaka Israeli kwenye bahari ya Galilaya/Tiberia/Genesareti. Na kutoka hapo unaibukia upande wa pili na kuendelea na safari yake moja kwa moja mpaka bahari ya Chumvi.
Tazama picha chini.
Mto huu, umekuwa kitovu katika historia ya Israeli kuanzia agano la kale mpaka agano jipya. Yoshua aliusimamisha mto huu na wana wa Israeli wakavuka kuelekea Yeriko.
Vilevile mto huu huu katika agano jipya ndio makutano mengi yalikuwa yanavuka kumwendea Yesu ili waponywe.(Mathayo 19:1-2), Na ni mto ambao Yesu mwenyewe alibatiziwa.
Kuonyesha kuwa ili nawe upate wokovu na ushindi dhidi ya maadui zako,na ili uponywe nafsi yako, ni lazima Uvuke Yordani yako ya Rohoni..Ili ukakutane na Yesu ng’ambo ya pili huna budi kuvuka Yordani, Na Unavukaje Yordani? Ni kwa kubatizwa, kama Yesu alivyobatizwa kwenye mto ule.
Hivyo na wewe sharti ukishamwamini Yesu moja kwa moja ukabatizwe, mahali popote penye maji tele kama ishara ya kuwa umeokoka kweli kweli. Na kuwa unakwenda kuwashinda maadui zako.
Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.
Wengi wanapuuzia maagizo haya ya msingi, wanadhani kuamini tu inatosha, Ndugu kubatizwa ni tendo lenye maana kubwa sana kwako rohoni, aliyetupa maagizo hayo hakuwa amekosa cha kutuagiza bali alijua umuhimu wake.
Swali Nji wewe umebatizwa ipasavyo? Kama sivyo basi kafanye hivyo.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda masomo yetu yawe yanakufikia njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Israeli ipo bara gani?
Wafilisti ni watu gani.
MJUMBE WA AGANO.
Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?
Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako ya rohoni?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
UNYAKUO.
Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako rohoni?
Mlima Sinai, au kwa jina lingine unajulikana kama Mlima Horebu, upo katika Rasi ya Sinai, Nchi ya Misri..Tazama katika picha.
Mlima huu, ni mlima ambao Mungu aliutumia kuwapa wana wa Israeli Torati na zile Amri 10. Ni mlima ambao wana wa Israeli waliutazama kwa muda mrefu kama mlima ambao unamtambulisha Mungu yupoje pale anapotaka kuzungumza na watu wake. Kufuatana na mstari huu;
Kutoka 19:16 “Ikawa siku ya tatu, wakati wa asubuhi, palikuwa na ngurumo na umeme, na wingu zito juu ya mlima, na sauti ya baragumu iliyolia sana. Watu wote waliokuwa kituoni wakatetemeka.
17 Musa akawatoa hao watu katika kituo, akawaleta ili waonane na Mungu; wakasimama pande za chini za kile kilima. 18 Mlima wa Sinai wote pia ukatoa moshi, kwa sababu Bwana alishuka katika moto; na ule moshi wake ukapanda juu kama moshi wa tanuu, mlima wote ukatetemeka sana.
19 Na hapo sauti ya baragumu ilipozidi kulia sana, Musa akanena, naye Mungu akamwitikia kwa sauti.
20 Bwana akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; Bwana akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu”.
Unaona, wana wa Israeli walijiundia picha kuwa siku zote Mungu akishuka mahali kuzungumza na mtu/watu ni lazima kuwe na moto, na matetemeko, na upepo mkali n.k. .
Eliya naye alidhani vivyo hivyo, wakati mmoja alipokuwa anamkimbia Yezebeli, alienda kwenye mlima huu wa Musa, mlima Sinai (Horebu) kwa ajili ya kukutana na Mungu, Na yeye akidhani kuwa ili Mungu ashuke mahali Fulani ni lazima uwepo moto, na matetemeko ya ardhi. Lakini siku hiyo alipokwenda kwenye mlima huo ndio alijua ukweli wote wa Mungu.
Ni kweli kama ilivyo ada, Mungu alijifunua kwake kama alivyojifunua kwa Musa na Wana wa Israeli kwa radi, mingurumo n.k. Lakini Eliya aligundua mbona bado simwona MUNGU?
1Wafalme 19:8 “Akainuka, akala, akanywa, akaenda katika nguvu za chakula hicho siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu, mlima wa Mungu.
9 Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya?
10 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.
11 Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;
12 na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.
13 Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi yake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango. Na tazama, sauti ikamjia, kusema, Unafanya nini hapa, Eliya”?
Unaona Eliya alipoisia tu ile sauti ya utulivu na upole. Hapo ndipo alipousikia uwepo wa Mungu ukibubujika ndani yake akajua sasa Mungu ameshuka kuzungumza na mimi.. Hapo ndipo alipofahamu kuwa Mungu hakai katika milima, hakai katika tufani, hakai katika upepo wa kisulisuli, bali katika utulivu na upole.
Vivyo hivyo na wewe leo hii unahitaji kumwona Mungu, unahitaji kukutana na Mungu katika Sinai, yako..Basi jifunze kujinyenyekeza mbele zake, kaa katika utulivu mkubwa wa Roho, huku ukijifunza kanuni za Mungu katika maandiko, na hakika atajifunua kwako zaidi hata ya alivyojifunua kwa wana wa Israeli. Mungu ni mnyenyekevu na hivyo anajifunua kwa wanyenyekevu kwake, wanaolitii Neno lake.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Israeli ipo bara gani?
Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)
SAYUNI ni nini?
Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?
Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?
SWALI: Neno “Korbani” linalozungumziwa katika Marko 7:11 lina maana gani?
JIBU: Ili tupate picha nzuri ya Neno hilo embu tusome sehemu zote mbili zinazozungumzia jambo hilo hilo moja.
Mathayo 15 :1-6
1 “Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema,
2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula.
3 Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.
5 Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu,
6 basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu”.
Marko 7:8-13
“8 Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.
9 Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.
10 Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe.
11 Bali ninyi husema, Mtu akimwambia babaye au mamaye, NI KORBANI, yaani, wakfu, kitu changu cho chote kikupasacho kufaidiwa nacho, huwa basi;
12 wala hammruhusu baada ya hayo kumtendea neno babaye au mamaye;
13 huku mkilitangua neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyopokeana; tena mwafanya mambo mengi yaliyo sawasawa na hayo.
Kama tunavyosoma hapo, biblia imeshatoa tafsiri ya hilo Neno Korbani mbele kidogo kuwa linaamanisha WAKFU.
Kitu chochote kilichowekwa wakfu ina maana kuwa hakitumiwi kwa mtumizi mengine yoyote isipokuwa kwa Mungu tu. Sasa katika habari hiyo, utaona Bwana Yesu alikuwa anawelenga sana sana Mafarisayo na waandishi kwa unafki wao kwa kujifanya kuwa wanaishika torati yote, wakati yapo mambo mengine mengi ya torati walikuwa wanayakaidi.
Na ndio hapo Bwana Yesu akawatolea mfano mmojawapo, ambao ulihusu kuwaheshimu wazazi, kama mojawapo ya amri ambazo Mungu alizitoa zishikwe na watu wote. Na biblia iliposema kuwaheshimu wazazi, ilikuwa sio tu kuwaonyeshea heshima na utiifu, hapana ilikuwa ni zaidi ya hapo ikiwemo kuwahudumia kifedha, hususani wakiwa wazee.
Sasa hawa waandishi walikuwa wanayapindisha hayo maagizo, kwa kuwashurutisha watu, kuepuka majukumu yao ya kuwahudumia wazazi wao, kinyume chake walikuwa wanawaambia hayo wanayoyapata kwa ajili ya wazazi wanaweza tu kuyafanya kuwa wakfu(Korbani) mbele za Mungu, na ikawa ni sawa tu na kama wamewahudumia wazazi wao, isiwe dhambi mbele za Mungu.
Hivyo kama mtu alikuwa ametenga fedha yake kiasi kwa ajili ya matumizi ya baba yake au mama yake kule kijijini, basi walihimiziwa walizete Hekaluni kwa ajili ya Mungu kama wakfu..
Na mzazi akimuuliza, mbona huniletei matumizi, basi Yule kijana atasema, fedha hii au nafaka hii niliyoivuna ni wakfu kwa Mungu.
Hivyo watu wengi wakawa wanawaacha wazazi wao katika hali ya shida na umaskini wa hali ya juu. Jambo ambalo Mungu hakuliagiza.
Ndipo Yesu anawakemea hawa waandishi kwa kuyapindua maagizo ya Mungu, ya kutotimiza majukumu yao ya kuwahudumia wazazi kwa kanuni zao walizojitungia.
Nini tunajifunza?
Kumbuka biblia haifundishi watu wakimbie majukumu yao ya kifamilia kwa wazazi wao hususani pale wanapokuwa wazee kwa kisingizio kuwa wanamtolea Mungu.. Biblia inasema usipowahudumia watu wa nyumbani kwako, wewe ni kuliko hata mtu asiyeamini(1Timotheo 5:8).. Lakini pia biblia haifundishi kuwa watu waache kumtolea Mungu kwa kisingizio kuwa wanayo majukumu mengi ya kifamilia.
Lazima ujue kila utoaji una sehemu yake, na Baraka zake. Watu wa nyumbani kwako wana sehemu yao, maskini wana sehemu yao, na Mungu pia anayosehemu yake..Usipojua hilo utakuwa nawe pia unatangua torati kwa kufuata mawazo yako mwenyewe uliyojitungia. Kwasababu wapo watu wengi leo hii, wameacha kupeleka fedha zao kanisani, au kwenye huduma za Mungu, wanasema sitoi sadaka yangu, na ukiwauliza ni kwanini?, wanasema mbona hatuoni zikienda kuwahudumia maskini na wajane kama ilivyokuwa katika kanisa la kwanza la mitume…Lakini mtu huyo huyo hajui kuwa watakatifu wa kanisa la kwanza sio kama hawa wa sasahivi, wale walikuwa wapo tayari kuuza mashamba yao na viwanja vyao na kuleta kwa Mungu, hivyo kwa namna ya kawaida nishati ya kutosha ni lazima iwepo nyumbani kwa Mungu hata kuwahudumia mpaka wajane.
Lakini kama wewe unampelekea Mungu shilingi, wakati hiyo fedha hata gharama za umeme kanisani hazijitoshelezi, unapata wapi ujasiri wa kutaka kujua mfuko wa kanisa unatumikaje?? Fikiria tu. Je wewe unaweza kuuza shamba lako kule kijijini, umletee Mungu?
Bwana atusaidie,.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?
WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.
MIJI YA MAKIMBILIO.
JE KUVAA PETE NI DHAMBI?
MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.
YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.
Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?