Kwanini yesu kristo ni wa muhimu kwetu?
Moja ya majukumu tuliyonayo ni “Kumfahamu sana Yesu Kristo”..Hili ni moja ya jukumu kubwa sana tulilonalo kwasababu ndio msingi wa ukombozi wetu..Tusipomfahamu Yesu kwa mapana na marefu basi ni ngumu kujua nafasi zetu pamoja na Neema tuliyopewa…Na matokeo ya kutomwelewa Yesu ni kuishia kuidharau neema na kupotea.
Sasa jukumu la kumjua Yesu, sio kujua sura yake alikuwa ni mzuri kiasi gani, au alikuwa na rangi gani, au alikuwa na nywele za namna gani, au alikuwa anapenda kula nini?..Hapana hilo sio jukumu tulilopewa la kumfahamu kwa namna hiyo..Jukumu tulilopewa ni KUIFAHAMU VIZURI ILE NAFASI ALIYONAYO. Tukishaifahamu ile nafasi basi tutamjua Mungu sana. Na mpaka sasa hakuna aliyefikia kikomo cha kuijua hiyo nafasi yote..bali kwa siku zinavyozidi kwenda tunazidi kuilewa na ndivyo tunavyozidi kumpenda Mungu na kumheshimu.
Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”
Leo tujikumbushe ni kwa namna gani kifo cha Yesu kilivyokuwa na umuhimu kwetu sisi tuliokuwa tumepotea kwenye dhambi.
Katika Biblia tunasoma muda mfupi kabla ya Bwana Yesu kupandishwa msalabani..Pilato aliwafungulia mfungwa mmoja ambaye alikuwa ni mkatili katika mji ule..Na huyo si mwingine Zaidi ya BARABA.
Huyu Baraba alikuwa na Kesi ya mauaji ya watu kadhaa hapo mjini, na alikuwa ni mkatili..Biblia inamwita “mfungwa mashuhuri” (Mathayo 27:16). Watu wote walimshuhudia kuwa alikuwa ni mkatili, hivyo walikuwa hawamhitaji hata kidogo, hivyo alikamatwa na warumi na kutiwa gerezani akisubiria hukumu yake ipite..Na bila shaka angeuawa kifo cha kikatili kuliko mtu mwingine yoyote yule, kwasababu kila mtu alikuwa amemkinai. Na alivyokuwa kule gerezani kila mtu pamoja na yeye mwenyewe alikuwa anajua ndiye anayestahili adhabu kubwa kuliko wote. Kulikuwa hakuna uwezekano wa kupona hata kidogo…Lakini kama wasemavyo watu “hata mnyororo ulio imara sana, lazima utakuwa na sehemu yake dhaifu”..Hata kama sehemu inaonekana hakuna njia basi Mungu anaweza kufanya njia.
Baraba akiwa mule gerezani labda moyo wake ukaanza kumchoma na kujihisi alifanya makosa, aliua wale watu pasipo hatia, akitazama pembeni anajua kuna mtu aliua tu mtu mmoja na alihukumiwa kukatwa kichwa yeye akijiangalia kashaangusha watu kadhaa huko nyuma hukumu yake itakuwaje?…
Siku moja tu asubuhi alishangaa anaitwa nje, atoke gerezani..na alipotoka akijua anakwenda kuuawa na pengine wafungwa wote wakajua anakwenda kumalizwa kwa hasira nyingi..ghafla anatoka nje anaona watu wengi wanamshangilia nje, wanafurahi kufunguliwa kwake..anaona wanampigia mpaka vigelegele, Baraba afunguliwe! Baraba afunguliwe!… kwa pembeni anamwona Pilato anamwambia kuanzia leo upo huru kama watu wengine, rudi nyumbani kwako kafurahi na mke wako na Watoto wako, upo huru..Wakati anashangaa jambo hilo linawezekanaje labda walikosea wanamaanisha Baraba mwingine…. kwa pembeni kidogo anaona mtu amewekwa taji la miiba kichwani kakaa kimya sana, mpole kama mwanakondoo anayekaribia kuchinjwa….Pilato anamwambia Yule kabeba hukumu yako…Yule atakufa kwa niaba yako…Ni wazi bila shaka alishangaa kidogo..
Naamini Maisha yake yalianza kubadilika kuanzia pale na kuendelea…Kwasababu alijua chanzo cha uzima wake na uhuru wake ni nini?..kwamba kama si Yesu kuwa vile alivyokuwa, kufanyiwa yale aliyofanyiwa, kama sio Yesu kukataliwa yeye angekufa…kwasababu kama Yesu angekubaliwa basi yeye asingepona…Hivyo kwa kupingwa na kupigwa kbbwake Yesu yeye amepona!.
Je mtu wa namna hiyo atarudia tena kuua?, atamkebehi YESU?, Ataudharau msalaba? Atajisifu?…Na je mfano akiudharau msalaba na kutoka pale na kuendelea na mauaji yake unahisi ni nini kitampata mbele za Mungu na watu?
Hiyo ndiyo nafasi ya Yesu kwetu ilivyo… Baraba ni mfano wa mimi na wewe…Sasa ni kwa namna gani Bwana Yesu anachukua dhambi zetu?..Sio kwa kubeba kifurushi na kukiweka mabegani kwake…Hapana ilimgharimu Maisha yake…ilimgharimu kukataliwa, kupingwa, kutemewa mate, kutukanwa, kudhihakiwa..Kwajinsi alivyodhihakiwa sana na kutukanwa sana ndipo thamani ya Baraba kule gerezani ilivyokuwa inazidi kupanda. Hadhi ya Bwana Yesu ilishuka ili yetu ipande.
Wakati Baraba yupo kule gerezani alikuwa hajui kama Kristo anatukanwa huko nje kwaajili yake.
Ndugu yangu…Msalaba sio jambo la kupuuzia au kuchezea hata kidogo…Mambo yote mema unayoyapata leo hii ni kwasababu ya Yesu Kristo, kama sio yeye dunia ingeshaisha siku nyingi…Mungu angeshaimaliza dunia kwa laana kitambo sana…Maisha yangeshaisha miaka mingi sana iliyopita huko nyuma.
Watu wengi hawajui kuwa wanapiganiwa na Mungu pasipo hata wao kumwomba Mungu, wengi hawajui hata katika uasherati wao ni Mungu ndiye anayewapa riziki pasipo hata wao kumwomba, na hawajui ni hiyo neema, ni kwasababu ya YESU KRISTO. Kama sio Yesu kuteseka miaka 2020 iliyopita hakuna mwasherati ambaye mpaka leo angekuwa anaishi..Wote tulistahili kufa.
Lakini Neema hii unaichezea..unadhani ni haki yako kuishi na usherati wako, uwizi wako, ufisadi wako, ulevi wako, uuaji wako, utukanaji wako, usagaji wako, ulawiti wako, uchafu wako n.k Hii Neema ipo siku itaisha na siku hiyo ndipo utakapojua kuwa Hii neema ilikuwa ni ya thamani kiasi gani.
Hii Neema itakapoondolewa, itaondoka na kanisa..watakatifu wataondolewa ulimwenguni, dhiki kuu itaanza, mpingakristo atanyanyuka, ataua wengi na baadaye maji ya bahari na visima na mito yote itageuzwa kuwa damu, utatokea ugonjwa wa majipu ulio hatari kuliko huu uliozuka sasa unaoitwa CORONA. Utasambaa duniani kote hakuna mtu atakayesalimika kwa wale watakaoachwa kwenye unyakuo, wakati huo hakutakuwa na mtu wa kukwambia utubu dhambi zako.
Siku hizo hakutakuwa na masinema tena watu wanayokwenda kuangalia michezo , hakutakuwa na mipira watu wanayokwenda kuangalia, barabara zitakuwa wazi, kila mtu atakuwa peke yake peke yake akiugulia mapigo hayo..Unaona leo ugonjwa huu wa Corona leo ulivyosababisha mabarabara kufungwa, mashule kufungwa, hakuna mtu kwenda kazini kwenye mataifa yaliyoathirika, kila mtu kajifungia ndani..siku hizo itakuwa mara 100 ya hiyo, hata mnyama wako wa kufugwa hutamsogelea, kutakuwa hakuna kutembea mabarabarani..kila mtu anashiriki mapigo hayo kivyakevyake.
Katikati ya gonjwa hilo la ajabu litakalolipuka la majipu…mvua zitaacha kunyesha, jua litashushwa chini, kutakuwa hakuna kitu chochote kilicho kijani kitakachoonekana, mvua ya mawe itashuka, sio ya mawe ya barafu..mawe kama mawe, makubwa kama talanta, kutatokea matetemeko na milipuko ya volcano duniani kote, na baada ya siku za maunguzo ya jua kupita….jua litakuja kuondolewa kutakuwa na giza la ajabu kuliko lile lililotokea kipindi cha Farao, nyota hazitakuwepo, mwezi utaonekana kuwa mwekundu kama damu kwa kipindi kirefu, mambo hayo yote yanakuja ndani ya wakati mmoja..na mambo mengine mengi ya ajabu yatakuwepo, mambo haya sio hadithi za kutunga kasome Ufunuo 16 yote, utaona, na kama unyakuo utakupita basi utayashuhudia hayo yote.
Waebrania 10:25 “wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia. 26 Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi; 27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao. 28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu. 29 MWAONAJE? HAIKUMPASA ADHABU ILIYO KUBWA ZAIDI MTU YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, NA KUIHESABU DAMU YA AGANO ALIYOTAKASWA KWAYO KUWA NI KITU OVYO, na kumfanyia jeuri Roho wa neema? 30 Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake. 31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.”
Waebrania 10:25 “wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
26 Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;
27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.
28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.
29 MWAONAJE? HAIKUMPASA ADHABU ILIYO KUBWA ZAIDI MTU YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, NA KUIHESABU DAMU YA AGANO ALIYOTAKASWA KWAYO KUWA NI KITU OVYO, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?
30 Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.
31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.”
Kama hujageuka na kutubu mlango wa Neema leo upo wazi…Ni heri usitumie muda ku-comment na ku-like badala yake ukatubu kama hujatubu. Usisome tu kama hadithi ya kukufurahisha, bali ujumbe huu ukawe sababu ya mageuzi kwako..
Na maana ya kutubu ni “kugeuka”..maana yake unadhamiria kuyaacha yale uliyokuwa unayafanya yasiyompendeza Mungu, na unakwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi na kupokea Roho Mtakatifu. Mambo hayo unayafanya kwa moyo wako wote.
Bwana akubariki sana. Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa > WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
RABI, UNAKAA WAPI?
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
YULE JOKA WA ZAMANI.
HAPANA HATA MMOJA ATAKAYEIONJA KARAMU YANGU.
UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.
Rudi Nyumbani:
Print this post
SWALI: Samahani mtumishi naomba ufafanuzi wa kauli hii ya Bwana Yesu aliimanisha nini? “KWA NINI KUNIITA MWEMA? HAKUNA ALIYE MWEMA ILA MMOJA, NDIYE MUNGU.” Hapa nashindwa kuelewa alivyomjibu kwani alikosea wapi maana hata mimi leo hii najua Yesu ni mwema na alikuwa mwema!! Nisaidie kunifafanulia. Amina.
JIBU: Tusome habari yenyewe..
Marko 10:17 “Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamwuliza, MWALIMU MWEMA, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele? 18 Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu. 19 Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye, Waheshimu baba yako na mama yako. 20 Akamwambia, Mwalimu, haya yote nimeyashika tangu utoto wangu. 21 Yesu akamkazia macho, akampenda, akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. 22 Walakini yeye akakunja uso kwa neno hilo, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi. 23 Yesu akatazama kotekote, akawaambia wanafunzi wake, Jinsi itakavyokuwa shida wenye mali kuingia katika ufalme wa Mungu!.
Marko 10:17 “Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamwuliza, MWALIMU MWEMA, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele?
18 Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.
19 Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye, Waheshimu baba yako na mama yako.
20 Akamwambia, Mwalimu, haya yote nimeyashika tangu utoto wangu.
21 Yesu akamkazia macho, akampenda, akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.
22 Walakini yeye akakunja uso kwa neno hilo, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Yesu akatazama kotekote, akawaambia wanafunzi wake, Jinsi itakavyokuwa shida wenye mali kuingia katika ufalme wa Mungu!.
Wengi wanatumia vipengele hivi (hususani wale wasio wakristo), Kuthibitisha kuwa Yesu hakuwa Mungu, kwasababu hapa alikana kabisa kuwa yeye hakuwa mwema ila Mungu peke yake,…Lakini ukisoma kwa utulivu na ukimwomba Roho Mtakatifu akufumbue macho, utagundua kuwa Bwana Yesu hakukana kuwa yeye sio Mwema..Hakusema umekosea badili kauli yako!..Lakini alimuuliza swali tu!..Kwanini unaniita mimi mwema?..Kuuliza swali sio kukana….alitaka kupata mawazo yake, ni nini aliona ndani yake mpaka yeye amwite vile mwema…
Ni sawa na leo hii ukutane na mtu Fulani mkubwa ukamkimbilia na kumpigia magoti na kumwambia muheshimiwa, maagizo yoyote utakayonipa mimi nitayafanya..Na yeye akakuuliza ni kwanini unaniita mimi muheshimiwa?..anayeheshimiwa ni lazima awe kiongozi na mwenye mamlaka, Na hivyo utakuwa radhi, kutii chochote atakaachokuambia kukifanya kulingana na kauli yako… Na ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu alipomwambia yule kijana, hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu, yaani yeyote uliyemwona kuwa ni mwema basi ujue huyo ni Mungu..
Hivyo Unaongea na huyo aliye mwema ambaye ni Mungu.. Kama unadhani Kristo alikuwa anapinga yeye kuitwa mwema..Soma tena, (Yohana 10:11) utaona anajiita mimi ndimi mchungaji mwema…Sasa ikiwa alikuwa anajipinga vile basi asingejiita na hapa pia mchungaji mwema..Na pia kasome Yohana 14:8-10 utaona Uungu wa Bwana Yesu. Lakini utaona alimuuliza kijana yule vile, ili kumjengea mazingira ya kukishika kila ambacho atakachokwenda kumwambia mbele, kwa kigezo kile kile cha kumtambua kuwa yeye ni mwema kama Mungu…
Ndipo pale alipomwambia, umezishika amri akasema, nimezishika zote, lakini Bwana Yesu akaona kuwa hajazishika zote, imesalia moja, tena ile ya kwanza ya kumpenda Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote,kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote..Ndipo akamwambia umepungukiwa na moja, nenda akauze vyote ulivyo navyo, na kuwapa maskini, kisha njoo amfuate..
Lakini Yule kijana aliposikia habari za mali zake zinagusiwa akaondoka amekunja uso wake, kwasababu alipenda mali zake kuliko kumpenda Mungu.. Jaribu kufikiria kama angemtii Kristo, kama alivyomtambua kuwa yeye ni mwema kama Mungu na kuyafuata yote aliyoambiwa ..Leo hii yule angekuwa wapi?..
Bila shaka angekuwa ni mtume wa 13, Lakini alipenda mali zake kuliko kumpenda Mungu. Hata leo hii, tukimjua Kristo kama Mungu, pale anapotuambia tumpende yeye kwa nguvu zetu zote, pale anapotuambia tuache mambo Fulani ya kidunia, hatuna budi kuacha mara moja vinginevyo tutakuwa ni wanafki..
Bwana akubariki.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?
Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?
KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.
Ufisadi una maanisha nini katika biblia?
USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.
1Wathesalonike 5:18 “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu. 19 MSIMZIMISHE ROHO;”
Roho Mtakatifu anafananishwa na moto…Wakati ule wa Pentekoste Roho aliposhuka juu ya wale watu..alishuka mfano wa ndimi za moto…Hakushuka kama ndimi tu, bali kama ndimi za moto.. Maana yake ni kwamba Roho Mtakatifu anafananishwa na moto kwa tabia zake.
Sasa maana ya ndimi za moto ni nini?…Maana yake ni katika vinywa vyao zilitoka lugha zenye kuchoma kazi zote za Adui…Ndio maana muda mfupi tu baada ya tukio lile, wale mitume waliposimama na kuwashuhudia watu, walichomwa mioyo yao kwa namna isiyokuwa ya kawaida, na siku hiyo hiyo wakatubu watu elfu tatu na kubatizwa.
Matendo 2:1 “Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. 2 Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. 3 Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. 4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka. Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. 6 Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. 7 Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? 8 Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo?”
Matendo 2:1 “Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.
2 Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.
3 Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.
4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu.
6 Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7 Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya?
8 Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo?”
Tukienda mpaka mstari wa 37 unasema..
“37 Walipoyasikia haya WAKACHOMWA MIOYO YAO, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. 40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. 41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka WATU WAPATA ELFU TATU.”.
“37 Walipoyasikia haya WAKACHOMWA MIOYO YAO, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.
40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.
41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka WATU WAPATA ELFU TATU.”.
Unaona? Hapo walichomwa mioyo yao?..sasa kilichowachoma ni nini…ni maneno ya moto yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vya wale mitume walipokuwa wanawahubiria, siku zote walikuwa wanaishi na wakina Petro lakini maneno yao yalikuwa hayawachomi, lakini siku hii ya Pentekoste baada ya kupokea ndimi za moto..Maneno yao yakawa na uwezo wa kuchoma nia za Adui shetani ndani ya mioyo ya watu na kuwafanya waitii Injili. Hiyo yote ni kutokana na Roho waliyempokea na si kingine.
Hali kadhalika ndimi hizi hizi za moto walizozipokea Mitume ambazo kwa maneno yale machache tu siku ile waliweza kuwavuta watu wengi kwa Kristo takribani elfu 3…Ndio moto huo huo ambao wakiomba kitu kwa Mungu wa mbingu na nchi Mungu anawasikia na kuwajibu haraka zaidi kuliko wangekuwa hawana roho..Kwasababu ndimi hizo hizo zinaingia mpaka kwenye moyo wa Mungu na kwenda kumshawishi Mungu kwa kuugua kusikoweza kutamkwa na hivyo kupokea majibu kwa haraka sana..(Kumbuka neno ndimi ni wingi wa neno ULIMI, na ulimi ni neno linalowakilisha Lugha/usemi)..
Hivyo Usemi uliovuviwa Roho Mtakatifu unakuwa ni usemi wa moto. Kwahiyo mtu yeyote mwenye Roho Mtakatifu anapoomba iwe kwa kunena kwa lugha au isiwe kwa kunena kwa lugha, ule usemi wake mbele za Mungu unakuwa kama ni moto..unapenya mpaka kwenye vilindi vya moyo wa Mungu na kumshawishi kwa namna isiyoelezeka..hiyo ndiyo maana ya lile neno linalosema “Roho hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa (Warumi 8:26)”.
Maana yake ni kwamba tunapoomba tukiwa na Roho Mtakatifu lugha zetu hizi mbele za Mungu haziendi kama za watu wengine wa kawaida bali zinakwenda zikiwa zimejazwa nguvu mara nyingi zaidi za kuushawishi moyo wa Mungu kuliko tunavyoweza kuelezea..Kama tu vile mtu mwenye Roho Mtakatifu anavyohubiri, hatatumia nguvu nyingi kumshawishi Yule mtu aokoke..bali yale maneno yake yatakwenda kama moto wa Roho kuugua ndani ya Yule mtu kwa namna isiyoweza kutamka, na hatimaye Yule mtu kukata shauri kuokoka.
Lakini sasa huyu Roho Mtakatifu anaweza kuzimishwa..na ndio biblia inatuambia hapo.. “Msimzimishe Roho”..Maana yake ule moto wa Roho ndani ya mtu unazima. Maneno yake yanakuwa hayana nguvu tena ya kumbadilisha mtu, wala yanakuwa hayana nguvu tena kuushawishi moyo wa Mungu kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Mtu anapofikia hali kama hii ambapo “Roho kashazima ndani yake”…atalazimisha kutumia nguvu zake za kimwili na hekima yake ya kibinadamu na kila mbinu kumshawishi mtu amgeukie Mungu na atashindwa..
1Wakorintho 2:4 “Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu, 5 ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu”.
1Wakorintho 2:4 “Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,
5 ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu”.
Hali kadhalika maombi yake siku zote yatakuwa sio ya kuushawishi moyo wa Mungu..
Sasa ni mambo gani yanayomzimisha Roho ndani ya Mtu?
Jambo la kwanza ni kuudharau msalaba na kumfanyia Jeuri Roho Mtakatifu kwa kulidharau Neno lake…Neno lake linaposema hivi, na ndani ya moyo wako Roho Mtakatifu anakushuhudia kabisa kwamba jambo hili kulifanya sio sawa,..lakini wewe unalipuuzia, unadharau au unaonyesha jeuri mbele yake unafanya yale yasiyompendeza..hapo ule moto ambao pengine ulikuwa umeshaanza kuwaka ndani yako unazima ghafla.
Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, NA KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?”
2.Pili unapompinga Roho Mtakatifu kwa matendo yako..Kumpinga maana yake hukubaliani na kile anachokisema..Kwamfano biblia inasema.. “Waefeso 5.18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”..Na wewe unasema maana yake sio hiyo bali ni nyingine, na huku unaendelea kujihalalishia ulevi..hapo unampinga Roho Mtakatifu..Au biblia inaposema..
“1Timotheo 2:9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani; 10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.”…
“1Timotheo 2:9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.”…
Na wewe unasema maana yake sio hiyo bali ni nyingine..hapo unapingana na Roho Mtakatifu na hivyo upo hatarini kumzimisha Roho.
Matendo 7:51 “Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo”.
Ili tufanikiwe katika kila kitu hapa duniani, tunamhitaji Roho Mtakatifu..Huyo ni kama moto, akizimika ndani yetu hakuna chochote tutakachoweza kufanya..hata maombi yetu yatakuwa ni bure mbele za Mungu..Na kama tayari kashazima ndani yetu suluhisho la kuurudisha ule moto wake ni kutubu na kuanza kumtii Roho Mtakatifu, na kutompinga wala kulidharau Neno lake.
Kama hujampa Yesu Kristo maisha yako basi mpe leo, ulitii Neno lake wala usiudharau msalaba kwani ni kwa faida yako, tubu leo kwa kumaanisha kuziacha dhambi zote ulizokuwa unazifanya, na nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa na kwa jina la YESU, na Roho Mtakatifu atashuka juu yako kama moto.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?
MAFUNDISHO YA MASHETANI
KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?
SIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, BALI MAFARAKANO.
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.
SWALI: Naomba kufahamu,Yale maneno yanayookana juu ya msalaba wa Bwana Yesu (I.N.R.I) yana maana gani, Nimekuwa nikiyaona kwenye picha za msalaba lakini siyaoni mahali popote kwenye biblia?.
JIBU: Tukisoma kitabu cha Yohana sura ya 19 mstari wa 19-20 inasema..
“Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.
20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani”.
Kama tunavyosoma,. Pale juu ya msalaba wa Bwana Yesu, Pilato alingongelea kibao ambacho kilikuwa kinamwelezea kuwa yeye ni nani,.. Sasa maneno hayo YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI kwa Kilatino (au, Kirumi) yanasomeka hivi…”Iesus Nazarenus Rex Iudaeorum.” Na kifupi chake ndio hiyo I.N.R.I…
Sasa madhehebu mengi hususani, Katoliki, Anglikana na Lutheran, wanapenda kutumia Ufipisho huo wa lugha ya kilatino (kirumi), kiyawakilisha yale maneno yaliyoandikwa juu ya msalaba wa Yesu.
Lakini Ukweli ni kwamba juu ya msalaba, hayakuandikwa maneno yale katika ufupisho wowote, bali yaliandikwa vile vile kama yalivyokuwa tena kwa lugha zote tatu, ili kila mtu aliyepita aweze kuyasoma, na ndio maana wale Mafarisayo wakamwambia Pilato. Usiandike, kuwa huyu ni Mfalme wa Wayahudi; bali andika kuwa yeye ndio anajiita, mfalme wa Wayahudi…Unaona ikiashiria kwamba maandishi yale yalikuwa yanasomeka kabisa na sio kwamba yameandikwa kwa kifupisho fulani.
Lakini pamoja na hayo yote, kujua au kutokuja msalaba ulikuwaje, kwamba ulikuwa ni mrefu sana, au ni mfupi sana, au ulikuwa ni wa alama ya kujumlisha, au ni wa nguzo iliyosimama, au kwamba maandishi yake yaliandikwa kwa wino wa bluu au wa njano, Hayo yote hayachangii chochote katika wokovu wetu?? Kwasababu hata katika Neno hilo hilo YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI, ukisoma injili nyingine utaona linasema tu MFALME WA WAYAHUDI(Marko 15:26), na sehemu nyingine linasema HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI(Luka 23:38)..Unaona sasa ukiyatafsiri hayo katika lugha ya kilatino (kirumi) utaona ni tofauti kabisa na hiyo yenye kifupisho cha INRI.
Sasa Hiyo yote ni kutufundisha kuwa tunachopaswa kujua ni kwamba Kristo alisulibiwa juu ya mti, na kwamba kusulibiwa kwake kumeleta ondoleo la dhambi la maisha yetu. Hicho ndicho kiini cha msalaba, na kwamba yoyote amwaminiye Yesu Kristo atapata ondoleo la dhambi zake na ukombozi wa Maisha yake, Hivyo tusiitazame misalaba sana, na kuipa heshima mpaka sasa imeshawafanya wengine wafikie hatua ya kuiabudu na kuisujudia..jambo ambalo ni machukizo makubwa mbele za Mungu.
Ubarikiwe.
Tafadhali share na wengine.
Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga
UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.
Yeremia 33:3 (NIITE NAMI NITAKUITIKIA)
INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?
KWANINI NAYAWEZA MAMBO YOTE KATIKA YEYE ANITIAYE NGUVU?
WhatsApp
Shalom, Nini kinachokufanya umfuate Yesu au uende kanisani?..Je moyo wako ni mnyofu mbele za Mungu?
Katika biblia, Agano jipya tunamsoma Mchawi mmoja aliyeitwa Simoni, ambaye alikuwa akifanya uchawi, na kuwadanganya watu, mpaka watu wakaamini kuwa anatumiwa na Mungu kufanya ishara zile, na alijigamba kuwa yeye ni Mtu Mkubwa (wa Mungu)...mpaka mji wote ukadanganyika na kumwamini. Lakini huyu Simoni aliposikia injili aliamini na akabatizwa…Lakini Nia yake ya ndani haikuwa kugeuka na kuacha dhambi zake za uchawi bali kuongeza nguvu zake za kichawi..Yaani maana yake alimwamini Yesu, ili apate kuongeza nguvu za kufanya miujiza na si kwasababu anautaka wokovu.
Ndugu mpendwa kigezo cha mtu kumkiri Yesu au kubatizwa sio tiketi pekee ya kukubaliwa na Bwana Yesu. Linahitajika jambo lingine na ziada, nalo ni “badiliko la kweli la ndani”.
Huyu Simoni mara ya kwanza alikuwa ni mchawi ambaye alijifanya ni mtumishi wa Mungu, lakini baadaye alipoona ukristo umeingia mahali pale akaona sasa ameshapata vazi jipya la kufunika kazi yake hiyo ya uchawi.
Hebu soma kwa makini habari ifuatayo usiruke kipengele hata kimoja…
Matendo 8:9 “Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa. 10 Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu. 11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake. 12 Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake. 13 Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka 14 Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana; 15 ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu; 16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu. 17 Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu. 18 Hata Simoni alipoona ya kuwa watu wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya mitume, akataka kuwapa fedha akisema, 19 Nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakayemweka mikono yangu, apokee Roho Mtakatifu. 20 Lakini Petro akamwambia, Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali. 21 Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa MOYO WAKO SI MNYOFU MBELE ZA MUNGU. 22 Basi, tubia uovu wako huu, ukamwombe Bwana, ili kama yamkini, usamehewe fikira hii ya moyo wako. 23 Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu”
Matendo 8:9 “Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.
10 Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.
11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.
12 Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake.
13 Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka
14 Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;
15 ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;
16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.
17 Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
18 Hata Simoni alipoona ya kuwa watu wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya mitume, akataka kuwapa fedha akisema,
19 Nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakayemweka mikono yangu, apokee Roho Mtakatifu.
20 Lakini Petro akamwambia, Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.
21 Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa MOYO WAKO SI MNYOFU MBELE ZA MUNGU.
22 Basi, tubia uovu wako huu, ukamwombe Bwana, ili kama yamkini, usamehewe fikira hii ya moyo wako.
23 Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu”
Sasa watu wa namna hii wapo wengi katika kanisa. Hususani katika hizi siku za mwisho, ambapo kwa asili ni waganga wa kienyeji, wengine ni wachawi wana mapepo ya utambuzi na bado wanazipenda kazi zao za kuagua, zinawapatia faida nyingi..hivyo wanapouona ukristo wa kweli unahubiriwa wanaona kama ni vazi jipya na hivyo wanakwenda kubatizwa na kusimama mimbarani kuendelea na uaguzi wao, wengine sio wachawi lakini ni wanasiasa tu ambao wanaona wakifanya siasi kwa vazi la uanasiasa hawafikii kirahisi malengo yao, hivyo wanajigeuza na kuwa wakristo ili waendeleze siasa zao katika madhabahu ya Mungu.
Na sio tu kwenye eneo zima la utumishi, bali hata walio waumini, wapo wengine wengine wanakwenda tu kanisani kwasababu wanashida ya wachumba kwasababu wameambiwa wachumba wazuri watawapata kanisani, lakini mioyoni mwao hawana habari na Kristo. Wanakubali kubatizwa kuwasababu wamesikia kwa kufanya hivyo mambo yao ya kimaisha yataenda sawa, kama tu huyu Simoni mchawi.
Wengine wanakwenda tu kwasababu ni siku nyingi hawajaenda kanisani, hivyo wanataka angalau waende mara moja moja kwa mwezi au mwaka, lakini ndani ya mioyo yao hawana nia na Mungu wala hawana mpango wa kubadilisha mtindo wa Maisha yao na kufanyika kiumbe kipya kwasababu mioyo yao sio minyoofu mbele za Mungu.
Wengine wanakwenda kwa nia tu ya kuonyesha mavazi yao, kila wanaponunua vazi jipya, wanawaza ni wapi watakwenda kujionyesha?..wanagundua ni kanisani..Hivyo kanisa ni kama kioo chao,…wengine wanapenda tu kukusanyika kwenye jumuiya ya watu wengi hawapendi kukaa wenyewe wenyewe, wanapenda kwenda kusikiliza vichekesho na kupata burudani za nyimbo za kwaya..wengine wanapenda kufanyiwa uaguzi, akipitia vita kidogo, au hasara kidogo katika Maisha yake anakwenda kumtafuta mbaya wake kwa waganga wa kienyeji..sasa akipata kanisa ambalo linatoa huduma kama hizo ndipo anapokita mizizi hapo lakini yeye hana mpango na kumwondoa Adui mkubwa wa dhambi katika Maisha yake.
Sasa kundi lote hili ndio linalojumuisha “Manabii na Makristo wa uongo watakaotokea siku za mwisho”…Wengi wanafikiri Manabii wa uongo ni wale tu wanaosimama pale madhabahuni na kujiita manabii…hapana sio hao tu, hata wachungaji wasio na nia ya Kristo biblia inawaita manabii wa uongo, hata waalimu wanaopotosha biblia inawapa jina moja hilo hilo ambalo ni manabii wa uongo, hata waimbaji walio kinyume na Neno la Mung una wanaopotosha watu wa nyimbo zao na mavazi yao na Maisha yao..jina lao ni hilo hilo “manabii wa uongo au makristo wa uongo”..
Hali kadhalika hata Waumini ambao wanakwenda kanisani kwa nia ambayo sio ya Kristo mioyoni mwao jina lao ni hilo hilo “manabii wa uongo na makristo wa uongo” kwasababu wanawadanganya watu wa nje na waumini wenzao walio waaminifu kwamba wameokoka kumbe ndani hawana nia ya Kristo. Hivyo manabii wa uongo ni jina la ujumla..kuwafunua wale wote ambao wanajifanya wana uhusiano na Imani ya Kikristo na kumbe ndani yao ni maadui wa Msalaba.
Je na wewe upo kwenye kundi gani?..la makristo wa uongo au wa kweli?..Kama unakwenda kanisani kwasababu ya kutafuta majumba, mke au mali…wewe sio nabii wa uongo???…Je uasherati umeuacha?, je matusi umeyaacha, rushwa umeziacha, wizi umeuacha?, usengenyaji umeuacha?, kuishi na mwanamke/mwanamume ambaye humjafunga ndoa bado unaendelea kuishi naye?, ..kama bado hujaacha hayo yote kwanini unajiita mkristo?..huoni kama wewe utakuwa ni mkristo wa uongo?..uliyetabiriwa kutokea siku za mwisho?, ambao mtawadanganya wengi?..
Unatoa fedha nyingi kanisani ili upokee baraka kwenye kazi yako haramu ya uuzaji wa pombe..wewe una tofauti gani na huyu Simoni mchawi ambaye anataka kuwapa fedha wakina Petro ili na yeye awe na uwezo wa kuwawekea watu mikono washukiwe na nguvu za Mungu..Lakini wakina Petro walimwambia..
“20 Lakini Petro akamwambia, Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali. 21 Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa MOYO WAKO SI MNYOFU MBELE ZA MUNGU.”
“20 Lakini Petro akamwambia, Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.
21 Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa MOYO WAKO SI MNYOFU MBELE ZA MUNGU.”
Lakini pamoja na hayo, pengine ulifanya hayo yote pasipo kujua…ulikuwa unakwenda kanisani nusu uchi kwasababu hukupata kufahamu kuwa unafanya dhambi, ulikuwa unafanya biashara haramu na huku unakwenda kutafa baraka kwa kazi hiyo kanisani kwasababu ulikuwa hujui. Kristo anakupenda na bado unauwezo wa kutengeneza upya na kuwa kipenzi cha Mungu..Unachopaswa kufanya ni kutubu tu!..Toba ni kila mtu anatubu, haijalishi ni mchungaji, mwalimu, au Nabii..wote tunatubu..na Mungu anapendezwa na mtu mwenye kunyenyekea..
Hivyo tubia mambo hayo yote kama ulikuwa unayafanya..na kisha usiyafanye tena..Baada ya kutubu na kudhamiria kuanza Maisha mapya na Kristo, nenda katafute ubatizo sahihi mahali popote ili upate kukamilisha wokovu wako, kumbuka ubatizo ni muhimu, na ni lazima uwe wa Maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38).
Na moyo wako utakuwa mnyofu mbele za Bwana na utafanyika kuwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu, na Roho Mtakatifu mwenyewe atakuongoza kufanya yaliyosalia.
YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.
ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!
KIJITO CHA UTAKASO.
USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.
Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?
MSHAHARA WA DHAMBI:
WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.
MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.
Maombi(uombaji) ni nyenzo namba moja ya kumfikisha mtu uweponi mwa Mungu kwa haraka sana. Na kama tunavyofahamu sikuzote mtu yeyote aliyepo mbele za uso wa Yehova mwenyewe, uwezekano wa yeye kujibiwa mahitaji yake yote upo. Hivyo shetani kwa kulijua hilo hataki, mtu wakati wowote mtu afike huko hivyo anachofanya ni kumletea tu saikolojia za kipepo ili zimfanye asidhubutu kutaka kwenda kusali wakati wowote.
Na baadhi ya saikolojia hizo ni hizi:
Siku zote Kabla ya mtu hajafikiria tu kwenda kuomba, mawazo ya kwanza yanayomjia kichwani pake ni “nimechoka”..Ataanza kufikiria Nimekuwa kazini siku nzima, sijapata muda wa kupumzika, hata kidogo, hapa nilipo usingizi wenyewe umenikamata, najisikia homa homa, hivyo wacha leo nipumzike nitaomba siku nyingine..
Mwingine atasema nimefanya kazi ya Mungu siku nzima, tangu asubuhi hadi jioni hata sasa bado wapo watu wananitegemea nikawafundishe, nina mialiko mingi ya mikutano hivyo wiki hii nimechoka wacha nisiende kusali..
Lakini Bwana wetu Yesu Kristo yeye alikuwa anachoka kuliko hata sisi kwa utumishi mgumu kwa kuzunguka huko na kule, Utaona upo wakati baada ya kuwahubiriwa makutanao siku nzima mpaka imeshafika jioni badala awaage aende akapumzike kidogo, kinyume chake aliwalazimisha mitume wake watangulie mashuani, yeye akabaki nyuma kwenda kusali mlimani, alikaa kule masaa mengi, akisali, sio kwamba hakuwa amechoka hapana. Lakini alijua umuhimu wa maombi.
Mathayo 14:22 “Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano. 23 Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. 24 Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho. 25 Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.”
Mathayo 14:22 “Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.
23 Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake.
24 Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho.
25 Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.”
Sisi pia, kwanini Neno “Nimechoka” linataka kuchukua nafasi ya maombi yetu?.Kwamwe tusikiendekeze hicho kigezo cha nimechoka kuchukua nafasi yetu ya maombi.
2. Sina Muda wa kuomba:
Neno lingine shetani analoliwekwa kwenye vichwa vya watu ni hili “sina muda wa kuomba”..kwani nimetingwa na mambo mengi, na shughuli nyingi nipo bize sana…Nimekutana na Watu wengi wakiniambia maneno haya, wanasema wanashindwa kwenda ibadani au kuomba kwasababu ya kukosa muda….Wapo pia watumishi wa Mungu wanaosema mimi nipo bize sana na huduma hivyo sina muda wa kuomba binafsi muda mrefu, ninamialiko mingi ya semina, sehemu mbali mbali..
Lakini nataka nikuambie pia tunaye Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ndiye kielelezo cha utumishi wetu, yeye alikuwa bize kuliko hata sisi, muda mwingine makutano walikuwa wanamsonga, muda wote wanataka awafundishe lakini biblia inatuambia..alijieupua, akaenda kutafuta mahali pa utulivu akaomba huko..
Luka 5:15 “Lakini habari zake zikazidi kuenea, wakakutanika makutano mengi wamsikilize na kuponywa magonjwa yao. 16 Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba”.
Luka 5:15 “Lakini habari zake zikazidi kuenea, wakakutanika makutano mengi wamsikilize na kuponywa magonjwa yao.
16 Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba”.
Alifanya vile kwasababu alijua hata ile huduma aliyokuwa anaifanya ilihitaji maombi ili iweze kusimama, ni jambo la kushangaza kama tutasema sisi ni watumishi wa Mungu halafu tunakosa muda wa kuomba…Nasi pia tujiepue tupate muda wa kuomba binafsi.
Jambo lingine ni hili shetani analileta kichwani,.. mbona ninaweza kuyamudu tu Maisha yangu bila maombi?..Ni kweli utayamuda Maisha yako ya kidunia, lakini sio Maisha yako ya wokovu.
Utamudu kwenda disko, utamudu kuendelea kuwa mlevi, utamudu kuiba, utamudu kuwa mwasherati na utamudu kuwa bize na kazi zako kuliko hata hata kumtafuta Mungu na mambo mengine yanayofanana na hayo utayamudu kwasababu hayo yote hayahitaji maombi.
Lakini ukisema umeokoka halafu sio mwombaji, basi ujue hutaweza kuyashinda majaribu ya aina yoyote ile, Bwana Yesu mwenyewe alisema..Kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni..Unadhani alikuwa anatania, unadhani shetani ataufurahia wokovu wako, ustarehe tu, halafu mwisho wa siku uende mbinguni?. Atakutafuta tu na kama wewe sio mwombaji basi huwezi kuchomoka,..na ndio maana taamaa za mwili unashindwa kuzitawala, kwasababu huombi, unashindwa kuwa na kiasi kwasababu muda wa maombi huna, hauuhisi uwepo wa Mungu maishani mwako, kwasababu wewe sio mwombaji..
Yakobo 4:1 “Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu? 2 Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa HAMWOMBI!” Maombi ni Mafuta ya wokovu, kama vile gari lisivyoweza kwenda bila Petrol vivyo hivyo, wokovu wako hauwezi kupiga hatua yoyote bila kuwa maombi..
Yakobo 4:1 “Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?
2 Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa HAMWOMBI!”
Maombi ni Mafuta ya wokovu, kama vile gari lisivyoweza kwenda bila Petrol vivyo hivyo, wokovu wako hauwezi kupiga hatua yoyote bila kuwa maombi..
Saikolojia nyingine ya ki-shetani ni hii ya kudhani kuwa maombi yako hayawezi kujibiwa. Unaona kama ukiomba utapoteza muda bure,.Nataka nikuambie, Maombi yote yanasikiwa ikiwa utaomba sawasawa na mapenzi yake, lakini sio jambo la kufanya siku moja halafu basi Kesho unaendelea na mambo yako mengine, maombi ni sehemu ya Maisha ya mkristo ni mwendelezo, majibu ya maombi mengine yanakuja kwa kuomba tena na tena, leo, Kesho, Kesho kutwa n.k…lakini katika kuomba huko Bwana Yesu ametupa uhakika kuwa Ombi lolote la namna hiyo mwisho wa siku ni lazima lijibiwe tu..haliwezi kuachwa..
Luka 18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa”. Mathayo 7:7 “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; 8 kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa”.
Luka 18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa”.
Mathayo 7:7 “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; 8 kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa”.
Mwisho, nataka nikuambie Wapo watu wanadhani wanaweza kuvumbua njia nyingine ya kuwasiliana na Mungu kirahisi au watapata suluhisho la matatizo yao Zaidi ya maombi..Fahamu kuwa Bwana wetu Yesu ameshatusaidia kufanya utafiti, sasa usitafute utafiti mwingine wa kwako wewe au wa kwangu mimi mbali na ule aliouthibitisha Yesu wa maombi..Yeye alikuwa hana dhambi hata moja, alikuwa ni mtakatifu sana, lakini katika utakatifu wake wote huo hakutupilia mbali suala la maombi alilifanya kama nyenzo ya yeye kufikia malengo yake, alifanya maombi kuwa sehemu ya Maisha yake..
Na wakati mwingine alikuwa anaomba kwa jasho na machozi mengi, na hata damu ilimtoka, akisihi mpaka akawa anasikilizwa…
Vinginevyo asingepokea kitu, Je mimi na wewe ambao si wakamilifu kama Bwana Yesu tunapaswaje?..tunaona raha gani kuishi Maisha ya kutokuomba halafu tunajiita bado ni wakristo..?
Waebrania 5:7 “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu”;
Hivyo tusitafute njia ya mkato..Kama tunataka tumwone Mungu akitembea katika Maisha yetu kwa ukaribu Zaidi na sisi, huu ndio wakati wa kuanza upya tena kwa nguvu za Maombi. Bwana alituambia walau saa moja kwa siku..Hivyo tujitahidi, tupambane, tushindane, tusiruhusu uongo wa shetani utuvurugie uombaji wetu, tusiruhusu, kukosa muda kutuvurugia ratiba yetu, tusiruhusu kutegemea nguvu zetu na akili zetu kutuharibia uombaji wetu..
Tuombe, tuombe, tuombe..
https://wingulamashahidi.org/mafundisho-ya-ndoa/
LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.
AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!
UJIO WA BWANA YESU.
JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?
AMEFUFUKA KWELI KWELI.
Unajua ni kitu gani kilikuwa kinaendelea siku chache kabla ya Nuhu kuingia Safinani?…Mungu alimwambia Nuhu ingia wewe na mke wako na watoto wako na wanyama wote ndani ya safina..
Sasa kitendo tu cha Nuhu kuingia mule , muda huo huo Mungu aliufunga mlango. Lakini cha kushangaza zaidi ni kuwa tendo la kufunga mlango halikumaanisha kuwa mvua itaanza kunyesha siku hiyo hiyo, hapana tunasoma mvua haikunyesha siku ile ile, bali ilisubiri muda wa siku saba, ndipo baadaye gharika ikashuka.. Mwanzo 7:13-17
Jambo tunaweza kuona hapo ni kuwa mlango wa wokovu ulikuwa umeshafungwa siku kadhaa nyuma kabla ya siku yenyewe ya maangamizi kufika..Pengine baadhi ya watu kuona jinsi mlango ule ulivyofungwa kwa namna isiyokuwa ya kawaida, walighahiri mawazo yao, wakamfuata Nuhu, wakamgongea mlango, wakimwambia Nuhu tufungulie tumegundua ni kweli hii dunia inakwenda kuangamizwa yote hivi karibuni hivyo na sisi tunataka kuzisalimisha roho zetu, tunakusihi utufungulie na sisi tuingie ndani…
Jibu la Nuhu, lilikuwa ni nini?, Mimi sikuufunga mlango, ni Mungu ndiye aliyeufunga na sijui katumia njia gani kuufunga kwasababu sioni hata komeo, wala kufuli pembeni, ni kama vile tumesakafiwa humu ndani, nitawasalidieje ndugu zangu..Ombeni, kwa Mungu labda atawasikia na kuwafungulia huu mlango kwasababu siku yenyewe ya maangamizi naona bado haijafika..
Pengine wale watu wachache waliokuwa pale nje, wakaanza kumlilia Mungu kwa machozi sana ili wafunguliwe mlango lakini hakukuwa na aliyejibu.. wengine walidhihaki na kuona Nuhu ndo kaamua kabisa kujisakafia ndani afie kule,..lakini wale wachache pengine wakaendelea kumsihi Nuhu kutafuta njia ya kuingia safinani.. Siku tano kabla ya gharika, wakaongezeka na wengine tena, nao pia wakawa wanamwambia Nuhu tufungulie ndugu zako, kwa maana kutokana na hali hii tunaoiona inavyoendelea sasa hivi, hii dunia siku chache sana inakwendwa kuangamizwa tufungulie Nuhu, tumetubu na ndio maana tumekuja kabla ya maangamizi yenyewe kufika tunakuomba utufungulie….Lakini Nuhu jibu lake lilikuwa ni lile lile sikuufunga mlango mimi..
Siku tatu kabla gharika, watu bado wanabisha hodi tu, wanatafuta upenyo mdogo lakini hawaoni, siku mbili kabla ya gharika, wanazidi kumsumbua Nuhu labda atafute kiupenyo cha mlango kwa huko ndani uvunje tuingie, lakini biblia inatuambia safina ile ilipigwa lami nje na ndani, hivyo hakukuwa na uwezekano wa kuivunja kiurahisi…
Mpaka ilipotimia siku ile ya gharika yenyewe kushuka,walikuwepo wengi sana pale nje ya safina wakimlilia Mungu, na kubisha hodi kwa bidii sana..lakini walikuwa tayari wameshachelewa..
Ndugu Biblia inatuambia wazi kama ilivyokuwa wote wakaangamia…hakuna aliyesalimika….Sasa biblia inatuambia kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu ndivyo itakavyokuja kuwa katika siku za kuja kwake mwana wa Adamu..Bwana Yesu alisema wazi kabisa..
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze. 25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako; 26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu. 27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu. 28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.
27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.
Wengi tunadhani mambo hayo yatayokea baada ya kufa, jibu la ni La!, Hayo mambo yatakuwa ni hapa hapa duniani kipindi kifupi kabla ya unyakuo kupita…kuna watu watatamani sana waingizwe katika orodha ya watakaonyakuliwa lakini itakuwa ni ngumu tena..
Fahamu kuwa kitendo cha unyakuo sio kitendo cha kuotea tu, kwamba tunaishi ilimradi tu,halafu siku ile ikifika tutatoweka tu kwa bahati, hapana, Unyakuo unao HATUA zake..Na wale watakaonyakuliwa watajijua kabisa…jambo ambalo hawatajua ni siku yenyewe ya kuondoka, lakini watapewa uhakika huo wa kuondoka wakiwa bado wapo hapa hapa duniani kama vile ilivyokuwa kwa Eliya..
Sasa uhakika huo watautolea wapi?
Ukisoma kitabu cha ufunuo sura ya 10 yote utaona yapo mambo ambayo Yohana alionyeshwa akiwa katika kile kisiwa cha Patmo yahusuyo sauti za zile ngurumo saba, ambapo alipotaka kuziandika aliambiwa asubiri kwanza asiandike….Sasa hizo ni siri ambazo Mungu amezitunza kwa ajili ya bibi-arusi wake anayejiwekwa tayari leo hii kwa unyakuo.. Siri hizo hazijaandikwa mahali popote kwenye biblia..Lakini wakati huo utakapofika, Mungu atazihubiri duniani…Na hizo ndizo zitakazomvuta bibi-arusi ndani ya safina tayari kwa unyakuo siku yoyote..
Sasa wale ambao sio bibi-arusi wa Kristo,watakaposikia hizo jumbe zinahubiriwa, ndipo na wao watakaposhtuka ahaa!! Kwa mambo haya, ndio tunajua sasa unyakuo kweli ni siku yoyote..Hapo ndipo na wao watakapoanza shamra shamra za kumtafuta Mungu kwa kumaanisha, ndipo watakapoanza kubisha na kugonga kwa nguvu, wakitamani nao wahesabiwe..Siku hizo wataitafuta hiyo neema kwa bidii zote lakini hawataipata…
kwasababu mwana wa Adamu ameshasimama na kuufunga mlango…
Hao ndio wale wanawali wapumbavu, waliokwenda kutafuta mafuta na waliporudi wakakuta mlango umeshafunga..Ndivyo itavyokuja kuwa siku za hivi karibuni..(Soma Mathayo 25:1-12)
Nataka nikuambie ukishasikia tu ujumbe mwingine wa tofauti unapita duniani kote kwa nguvu nyingi za Mungu na udhihirisho mwingi, na kusikia mambo mageni masikioni mwako, yahusuyo safari ya kwenda nyumbani kwa Baba, kama bado wewe ni mkristo vuguvugu, basi ujue habari yako imeshakwisha mlango wa neema umekwisha fungwa..Ni heri kama utakuwa umesimama katika utakatifu na imani kwasababu hapo ndipo utakapopata uhakika wa kuondoka kwako hivi karibuni..Lakini kama wewe ni vuguvugu kwasababu hapa hatuzungumzii wale ambao ni baridi kwasababu wao hawataelewa chochote kitakachokuwa kinaendelea, tunamzungumzia wewe ambaye ni vuguvugu, habari yako siku hiyo itakuwa imekwisha..
Wewe ndio itakaoshuhudia wenzako wakienda mbinguni,..Utakuwa umelala na mume wako ambaye kila siku unamwona anajibidiisha kumtafuta Mungu na wewe utajikuta umeachwa, utakuwa unazungumza na mke wako na ghafla ataondoka, mwanao atakuwa amekwenda shule siku hiyo utashangaa harudi…Na ndio maana biblia inatuasa, TUJIWEKE TAYARI, kwa maana hatujui ni siku gani ajapo Bwana ..Hii dunia haina muda mrefu, Unyakuo si jambo la kulichukulia juu juu tu, ukiukosa ule, hali itakayokuwa inaendelea hapa duniani haielezeki, Bwana Yesu anavyosema utalia na kusaga meno alimaanisha kweli hivyo kwamba kusema hivyo kuwa kutakuwa na maombolezo ya ajabu kwa wale ambao watakuokosa unyakuo.
Bwana atutie nguvu katika safari yetu.
Maran Atha.
MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.
Shalom. Jina kuu la Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe.
Karibu tujifunze biblia.
Mathayo 3:5 “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani; 6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao. 7 Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? 8 Basi zaeni matunda yapasayo toba; 9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto. 10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”
Mathayo 3:5 “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;
6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao.
7 Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?
8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;
9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.
10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”
Soma tena mstari wa 7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? ”
Tunaweza kuiweka vizuri hiyo sentensi kwa namna hii “Enyi wazao wa nyoka ni nani aliyewadanganya(maana yake ni nani aliyewaonya) kwamba mtaiepuka hukumu inayokuja kwa njia hiyo mnayoitaka nyie?”..Njia gani?…Njia hiyo ya kuja kutaka kubatizwa na huku bado hamtaki kuacha dhambi zenu…Ni nani aliyewahubiria kuwa mtaikwepa hukumu kwa namna hiyo?…Maana yake mnafikiri kuwa kwa kuja kubatizwa tu hiyo inatosha kuikwepa hukumu itakayokuja….Mnajidanganya!…ZAENI MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!…Maana yake ni kwamba baada ya kutubu ishini kulingana na kutubu kwenu..Kama ulikuwa ni mwasherati, tubu na UACHE UASHERATI! Usiufanye tena, kama ulikuwa na kiburi tu na uache kuwa mwenye kiburi tena, kama ulikuwa mlevi unatubu na kuachana na ulevi wako, n.k..Huu ubatizo hautakuwa na msaada wowote kwenu kama mtakuja tu kubatizwa na huku bado hamjaacha matendo yenu mabaya. Huo ndio ujumbe Yohana Mbatizaji alikuwa anataka kuwapa wale Mafarisayo na Masadukayo.
Mafarisayo walisikia injili ya Yohana, wakaogopa, lakini wakasema aah ngoja tukabatizwe na sisi ili pengine tutaokoka huko mbeleni, lakini mioyoni mwao walikuwa hawana mpango wa kubadilika haka kidogo,..Walitaka kuugeuza ubatizo wa Yohana kama dini tu!..kama ni Liturujia mpya tu ya kufuata, kama katekisimo tu!..lakini walikuwa hawajui lengo kuu la ule ubatizo ni nini.. Lengo lake kuu lilikuwa ni kutubu na KUACHA DHAMBI!..sio kwenda kulowekwa kwenye maji na kurudi kuendelea na Maisha yako ya dhambi kama kawaida, na jina lako liwe limeshaandikwa mbinguni. Sio hivyo kabisa.
Vivyo hivyo na leo, ubatizo sio dini, na wala sio lebo ya kwamba Mungu anataka watu waliobatizwa ndio wawe wamepata tiketi ya kuingia mbinguni haijalishi wanaishije, yeye anataka tu watu wabatizwe.. hapana! Mungu anataka watu waliotubu na KUACHA DHAMBI. Hao ndio mbele za Mungu ubatizo wao una maana lakini kama mtu hujatubu kwa KUACHA DHAMBI, mtu huyo anamdhihaki Mungu.
Ukimuuliza mtu je umeokoka anakujibu, mimi nimebatizwa!..ukimuuliza tena je una uhakika wa kwenda mbinguni anakujibu ndio nilishabatizwa. Ubatizo hauna uhusiano wowote na kwenda mbinguni kama hujatubu kwa kuacha dhambi..Ndicho mafarisayo walichokuwa wanaenda kufanya kwa Yohana.
Umesema tu umetubu lakini bado unaendelea kuvuta sigara, bado unaendelea na uasherati, unaendelea na ulevi na ulawiti na usagaji, na pornography, halafu unasema umebatizwa au unakwenda KUTAFUTA UBATIZO, Ukidhani ndio unampendeza Mungu, na kwamba ndio utakwenda mbinguni..nataka nikuambie hapo unakwenda kujitafutia tu Laana badala ya Baraka.
Kutubu maana yake ni kugeuka na kuacha kile ulichokuwa unakifanya, na sio kusema tu mdomoni nimeacha na ilihali Maisha yako bado yapo vile vile. Ikiwa haupo tayari kuokoka, basi ni heri usiugize wokovu, wala usijiite hivyo, kwasababu ndivyo unavyomtia Mungu wivu kwa mienendo yako.
Watu wa Ninawi Mungu aliwasamehe kwasababu Aliona matendo yao kwamba wamegueka, wameacha mambo maovu waliyokuwa wanayafanya, hiyo ndiyo ikawafanya Waepukane na hukumu ile ambayo ilikuwa inawajia, na Mungu hakuona midomo yao kwamba wametubu kwa midomo ndipo awasamehe, hapana! bali matendo yao ndiyo yaliyosababisha wao kusamehewa.
Yona 3:10 “Mungu akaona MATENDO YAO, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”
Hali kadhalika, usifanyike kuwa mzao wa nyoka, kwa kutafuta kutimiza maagizo ya Mungu na huku moyoni huna mpango wa kutenda mapenzi yake. Hizo ni tabia za Nyoka kibiblia. Mafarisayo wanamwendea Yohana kubatizwa na huku mioyoni mwao ni wale wale watu wenye viburi, wanaopenda utukufu, wenye wivu, wenye chuki, …maana japokuwa walikuwa wanamwendea Yohana kubatizwa lakini mioyoni mwao walikuwa wanamchukia n.k
Kama umeamua kumfuata Yesu leo, basi kubali pia kubeba na msalaba wako, kabla ya kwenda kubatizwa piga gharama kabisa kwamba unakwenda kuacha dhambi moja kwa moja, kwamba dunia ndio umeipa mgongo hivyo, msalaba mbele, ulimwengu umeuacha nyuma..Na kwa kufanya hivyo ndipo utaona nguvu za Mungu katika Maisha yako zikikusaidia na kukuongoza na ndivyo Mungu atakavyokukaribia Zaidi na kukupenda. Na kukubariki.
MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!
JE! UMEFANYIKA KUWA MWANAFUNZI WA BWANA?
HISTORIA YA ISRAELI.
INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.
AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.
Nyimbo za Injili ni zipi?, waimbaji wanapaswa waitendeje huduma hiyo?..
Shalom. Karibu tuongeze maarifa kuhusu Neno la Mungu..Tukilijua Neno la Mungu vyema, tutayajua mapenzi ya Mungu na hivyo tutaishi kulingana na yeye anavyopenda na tutabarikiwa.
Moja ya karama ya muhimu sana katika Mwili wa Kristo ni karama ya uimbaji. Sasa ni wazi kuwa mtu yoyote anaweza kuimba, awe mwanamume au mwanamke..Lakini yupo ambaye akiimba nyimbo au akiimbisha basi kunaambatana na nguvu fulani za kipekee za Roho Mtakatifu. Sasa nguvu hizo sio za kuwafanya watu waanguke au walie..Hapana bali nguvu hizo ni zile zinazomfanya mtu apate badiliko fulani la rohoni, ageuke kutoka kuwa mwenye dhambi mpaka kuwa mtakatifu.
Mwimbaji huyu anapoimba au anapoimbisha, basi Roho yule yule anayeshuka juu ya watu wakati Mchungaji anahubiri ndio huyo huyo anayeshuka juu ya watu wakati anaimbisha.
Sasa huduma ya uimbaji sio huduma ya kutafuta fedha, kama vile huduma nyingine yoyote katika mwili wa Kristo isivyo ya lengo la kutafuta fedha wala umaarufu. Mchungaji au Mwalimu anapohubiri katika kanisa lake, na anapoalikwa mahali pengine au Taifa lingine kwenda kuihubiri Injili, hapaswi kwenda kule kwa lengo la kutafuta fedha. Biblia inasema tumepewa bure tutoe bure..Hivyo atakwenda kule alikoalikwa na atahubiri bure..Ndio wale waliomwalika watamgharimia nauli, pamoja na malazi na makazi kwa huo wakati, lakini hapaswi kwenda kwa lengo la kutafuta malipo/mshahara. Kama waliomwalika watakuwa na moyo mwingine na kusema hatutapenda mtumishi huyu aondoke mikono mitupu, hivyo kwa kuguswa kwao wakampatia chochote kile iwe fedha, au mali..hapo sio dhambi kupokea..lakini Mchungaji, au mwalimu au mtu yoyote yule hapaswi kuomba chochote, wala kuonyesha dalili ya kuwa mhitaji.
Mungu anajua kuwahudumia watu wake, haihitaji yeye kusaidiwa, hivyo aliposema…”Tumepewa bure tutoe bure alimaanisha kabisa”..kwamba kwa namna yoyote ile atawafungulia watumishi wake mlango wa kula na kunywa hata njia hiyo.
Vivyo hivyo na uimbaji wa nyimbo za injili. Mtu yeyote aliyepewa karama hiyo hapaswi kuwa kama wasanii wa nyimbo za ulimwengu ambao wapo kwa lengo la kutafuta fedha kwa sanaa zao hizo. Mtu mwenye karama ya uimbaji atafanya kazi ya Mungu bure pasipo malipo..akifika mahali kaalikwa kwenda kuongoza nyimbo za kumsifu Mungu na kumwabudu, hapaswi kutazamia malipo kwa namna yoyote ile. Anapaswa afanye kazi yake ya uimbaji kwa uaminifu kama ya mchungaji aliyealikwa…aimbe nyimbo za injili na kuhakikisha neema ya Mungu imeshuka juu ya watu, hiyo ndio inapaswa iwe furaha yake ya kwanza, na lengo lake kuu la kwenda pale.
Hali kadhalika hapaswi kubadilika kimavazi na kufanana na wasanii wa kidunia..Kazi ya Mungu sio ya kuonyesha uanamitindo…kwamba leo umevaa hiki, kesho unavaa kile, ili watu wakuone jinsi unavyojua kuvaa…Vaa nguo za heshima, kama ni mwanamke vaa gauni refu haijalishi ni la gharama au sio la gharama, lakini lazima liwe la kujisitiri, hupaswi kwenda kufanya huduma huku umevaa suruali, huku mgongo upo wazi, huku umejichubua uso, huku umeweka make up mfano wa Mwanamke Yezebeli wa kwenye biblia..hali kadhalika mwanaume hupaswi kwenda kufanya huduma huku umenyoa kidunia, huku umevaa nguo za kubana, huku umejipamba mpaka unakaribia kufanana na wanawake.
Ukifanya hivyo na kwenda kufanya huduma na mambo hayo machafu utakuwa bado hujaelewa nini maana ya kumtumikia Mungu, utakuwa unamdharau Mungu na madhabahu yake, na utakapoambiwa ukweli utaona kama unaonewa WIVU, hakuna wivu hapo unaoonewa, ni kwa faida yako binafsi..Unakwenda kuzitafutia laana badala ya baraka ndugu…..Unapoacha kusimama katika Neno la Mungu na kujilinganisha na wasanii wa kidunia, ni sawa na mchungaji aliyeacha majukumu yake madhabahuni na kujilinganisha na wanasiasa waliopo bungeni.
Ndugu yangu, uliyejaliwa karama ya uimbaji..Utumie kwa utukufu wa Mungu, kama wachungaji ambao wamealikwa kutembea dunia yote kuhubiri hawabweteki na kwanini wewe unabweteka na kujiharibia huduma yako kwa kuwaiga hao wasanii wa kidunia au hata baadhi ya wanaojiita wasanii wa injili ambao hawajaelewa maana ya kumtumikia Mungu?
Sasa utauliza je! Sitakiwi kabisa kwenda kurekodi nyimbo zangu studio?
Hapana unapaswa ukazirekodi kabisa tena kwa bidii nyingi, kwa uongozo thabiti wa Roho Mtakatifu, ili injili ienee kwa wengi, na kuwa msaada na baraka kwa wengi..Lakini katika hiyo usiigeuze kuwa ndio sehemu ya kupatia fedha na utajiri. Weka bei ya bidhaa hiyo ambayo inalingana na gharama ulizoingia, na faida kidogo kwaajili ya msingi wa kazi zitakazofuata kama hizo na si kwaajili ya kupata fedha, wala kwaajili ya kujiandaa kuwa msanii maarufu. Na hupaswi kukasirika unaposikia watu wanabarikiwa kwa nyimbo ulizoimba, au wanaziimba nyimbo zilizotungwa na wewe pasipo kukutaja wewe wala kukupa malipo…Hupaswi kukasirika, zaidi ya yote unapaswa ufurahi kwasababu injili ya Kristo inakwenda mbele.
Kwasababu hata wachungaji ndio hivyo hivyo, wanapotengeneza kitabu..na mafunuo waliyoyapata na kuyaandika ndani ya kile kitabu yatakwenda kufundishwa huko na huko, kila mahali na hata kumrudia yeye mwenyewe…na wala hawasemi wala kuchukia kwamba ule ufunuo ni wa kwao na kwamba wana hati miliki nao, mtu mwingine hapaswi kuhubiri bila idhini yao. Kama yupo Mtumishi wa namna hiyo, basi huyo naye bado hajaelewa nini maana ya kuwa mtumishi, kwasababu injili ya Kristo haihubiriwi kwa hati miliki. Lakini kama hujawahi kuona kwanini wewe muimbaji uchukie na kukwazika kuona mtu anaimba nyimbo uliyoiimba wewe bila hata kukutaja au kukutambua?.
Ukiona unasikia huo wivu basi fahamu kuwa bado kuna kasoro ndani yako, upo kutafuta umaarufu na faida kupitia kazi ya Mungu, na haupo kwa lengo la kuisambaza injili. Huna tofauti na Yuda Iskariote.
Hivyo zingatia hayo machache mtu wa Mungu, na Bwana atakusaidia, kama una huduma yoyote ndani yako ya kuhudumu kwa nyimbo za injili, tenga muda uilinganishe na huduma nyingine katika mwili wa Kristo jinsi zinavyofanya kazi, ili upate hekima na ufahamu jinsi ya kuitenda kazi ya Mungu katika shamba lake.
Bwaan akubariki.
NYIMBO ZA WOKOVU
NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?
KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?
Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.
MATUMIZI YA DIVAI.
JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?
KITABU CHA UZIMA
Ukisoma ule waraka wa pili ambao Paulo alimwandikia Timotheo kuanzia ile sura ya tatu mstari wa 1-9, utaona jinsi Paulo alivyoanza kumweleza Timotheo juu ya mambo yatakayotokea siku za mwisho..Lakini alianza kwa kumwambia neno hili “siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari”.. Jiulize ni kwa nini alimwambia hivyo?. Alimwambia hivyo kwasababu aliona jinsi wimbi kubwa la watu wenye mfano wa utauwa (wanaonekana kama ni watu wa Mungu), lakini wakizikana nguvu zake, watakavyonyanyuka na kuwapoteza wengi.
Hao watu hawakuwepo wakati mwingine wowote isipokuwa tu watatokea katika siku za mwisho, yaani watu wanaoonekana ni watumishi wa Mungu, wanaoonekana wanawaongoza watu katika njia za kweli, lakini kumbe nyuma ya mgongo wanazikana nguvu za Mungu..
Sasa hizi nguvu za Mungu ni zipi?..
Biblia inatueleza “Neno la msalaba” ndio nguvu ya Mungu..
1Wakorintho 1:18 “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu”.
Sehemu nyingine inaiita injili kama “uweza wa Mungu (POWER)” Warumi 1:16.
Unaona Injili inayolenga ukombozi wa msalaba, inayowafanya watu wautazame msalabani, watubu dhambi , wakapate msamaha na ondoleo la dhambi zao, hapo ndipo nguvu za Mungu zilipo..
Hakuna mahali popote biblia inasema nguvu za Mungu zipo katika mali, au biashara na majumba..Hayo hayawezi kumfanya mtu apate uzima wa milele…Sasa watu wa namna hii ndio watanyanyuka sana katikati ya kanisa la Mungu, ambao watakuwa wanajifanya ni wanatangaza habari za wokovu, kumbe wanahubiri mambo yao mengine, hawana habari na injili ya toba, wala hata haiwavutii, wala hawajali kwamba mtu wanayemchunga na kuchukua sadaka zake anaweza kufa leo na kwenda kuzimu kutokana na dhambi zake, hilo hawalijali wao wapo radhi kuwasisitizia tu mafanikio ya miili yao, lakini si roho zao.
Wengine wapo radhi, kuwakaririsha mapokeo ya dini zao, ili watu wawe tu wa kidini, wajue litrujia, wasome rozari, na sala zote za marehemu, lakini hao hao watu ukiwauliza je umeokoka, watakauambia mimi si mlokole, ukiwauliza, Je! Unajua kuwa kuna kitu kinachoitwa Unyakuo, watakauambia..sijui unazungumzia kitu gani!!..Sasa embu fikiria mtu wa namna hiyo mbinguni atakwendaje?..Lakini hayo yote ni kiongozi wake hajawahi kumwambia hayo mambo, ni kiongozi ambaye anao mfano wa utauwa lakini anazikana nguvu za Mungu..
Sasa Paulo aliwafananisha watu hawa na Yane na Yambre ambao walinyanyuka wakati wa Musa..Jinsi walivyokuwa wanapingana naye..
2Timotheo 3:8 “Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani. 9 Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa Dhahiri”.
2Timotheo 3:8 “Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.
9 Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa Dhahiri”.
Sasa kama uwafahamu Yane na Yambre ni wakina nani…
Walikuwa ni wale wachawi wa Farao ambao Musa alipokuwa anafanya miujiza na wao walikuwa wanafanya ili tu kumpinga Musa.
Unaona? Jambo pekee ambalo lilikuwa linawatofautisha hawa wachawi wawili (Yane na Yambre) na Musa, halikuwa miujiza..hapana, hata wao kwa sehemu fulani walipewa kufanya miujiza, jambo pekee lililowatofautisha na Musa, ni UJUMBE waliobeba.. Musa alikuja na ishara lakini alikuwa na Ujumbe nyuma ya ishara zile..Nao ndio huu “Bwana asema hivi! Waache watu wangu huru,waende kunitumikia”..Lakini Yane na Yambre hawakuwa na ujumbe wowote isipokuwa kupinga tu, na kuwaburudisha na kuwatumainisha wamisri kwa miujiza yao,..Ni wana-mazingaombwe tu!..Mtu anayefanya mazingaumbwe siku zote hana ujumbe wowote kwa mazingaombwe yake, anafanya tu kuburudisha watu, na wala wakati mwingine anaweza asiongee kuanzia anaanza mazingaombwe yake mpaka anamaliza. Na wakina Yane walikuwa hivyo hivyo.
Musa alikuwa na ujumbe wa ukombozi, wa kuwatangazia watu uhuru watoke katika utumwa mgumu wa Farao, Ambao kwa sasa sisi tuliookolewa tunafananishwa na wana wa Israeli pale tunapomwamini Kristo, tunaokolewa kutoka katika utumwa wa dhambi wa Ibilisi.
Sasa ukiona, mtu anakujia na miujiza na ishara hizi au zile, lakini hana ujumbe wowote wa kukutoa Misri (kukutoa kwenye utumwa wa dhambi), Basi ujue kuwa unaongozwa na Yane na Yambre(wana mazingaombwe), watumishi wa shetani.. Haijalishi watashika biblia, haijilishi watakuombea upone kiasi gani, Yane na Yambre waliweza kuyafanya hayo yote, haijalishi watafanya miujiza mingi vipi, kama hawana ujumbe wa kukurudisha msalabani upate ukombozi wa roho yako, Ujue hao ni Yane na Yambre tu wanakuongoza…
Ndio hao sasa mtume Paulo anaowazungumzia kuwa “wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake”…..Hizi ndio nyakati zenyewe za hatari zinazozungumziwa hapo. Mahali popote unapoongozwa embu jipime nafsi yako, je tangu umekuwa hapo ni kitu gani kimeongezeka katika Maisha yako ya rohoni kwa ujumla, Je! Mahusiano yako na Mungu yameongezeka au yapo pale pale?, Kama sivyo basi ujue upo chini ya Yane na Yambre wa siku za mwisho.
Na kibaya Zaidi kama hujui, watu waliochangia kuufanya moyo wa Farao kuwa mgumu ni hawa wachawi wawili..Kama sio wao basi pengine Farao angeshatubu zamani..(Ingawa ni Mungu mwenyewe ndiye aliyeruhsu). Vivyo hivyo leo hutaki kumgeukia Kristo na kutaka kutubu dhambi zako na kutafuta utakatifu kwasababu tayari wapo akina Yane na Yambre wanaokupumbaza na miujiza, ukikumbushwa habari ya utakatifu na kwenda mbinguni, unasema nabii wetu/kiongozi wetu wa kidini mbona hajawahi kutufundisha hayo, na miujiza mbona inafanyika mingi tu..
Ndugu siku ukifa na kujikuta upo kuzimu, hutakuwa na la kujitetea, kwasababu biblia inatuambia..mtu akifa matendo yake yanafuatana naye (Ufunuo 14:13)..Haisema majumba yake, au magari yake, au bishara yake, au dhehebu lake, inasema matendo yake..Sasa kama nabii wako au mchungaji wako, anakutumaisha na mambo ya ulimwengu huu na wewe unaona raha, nataka nikuambie siku ile vyote pamoja na mali zako, pamoja na huyo kiongozi wako wa imani, aliyekuwa anakufundisha kujiwekea hazina duniani badala ya mbinguni, wote watakuaga pale makaburini, utakuwa umebakia wewe mwenyewe, utashangaa ni matendo yako tu yapo na wewe..hayo ndiyo yatakayoeleza hatma yako ni nini..
kwasababu biblia imeshatuonya jinsi ya kuendana na watu wa namna hii, hivyo ni wajibu wako wewe binafsi kutumia akili, kwa kuutafuta uhusiano wako binafsi na Mungu wako…Kuupima wokovu wako kama upo sawasawa au la, na kama haupo! Basi ndio ufanye bidii kumtafuta Kristo kwa moyo wako wote na kwa nguvu zako zote, katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, maadamu muda unao..
2Wakorintho 13:5 “Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa”
Usisubiri ufe ndipo ujue kuwa ulikuwa kwenye njia isiyo sahihi, amka usingizi, anza kuyatengeneza Maisha yako.
Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza”.
Maran atha!
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
HUDUMA YA (ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI).
HATUTAACHA KUJIFUNZA NENO KILA INAPOITWA LEO.
Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?
HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.