Category Archive Home

KWAKUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU:

Nehemia 8:10 “Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU”.

Hapa anaposema “Furaha ya Bwana ni Nguvu zetu” hamaanishi “kufurahi kwa Bwana ndio Nguvu zetu”, hapana bali anamaanisha “Furaha yetu sisi katika Bwana ndiyo Nguvu yetu”.. Maana yake tunapofurahi tukiwa ndani ya MUNGU hiyo ni Nguvu kwetu..

Neno la Mungu linasema katika 1Wathesalonike 5:16 na Wafilipi 4:4 kuwa tufurahi siku zote katika Bwana..

Wafilipi 4:4 “Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini”

Furaha ya Bwana inapokuwa ndani yetu, ndivyo tunazidi kupata NGUVU za mambo yote.. Sasa tunaivutaje Furaha ya MUNGU ndani yetu?..Kwa mambo haya sita (06), furaha ya Mungu itaingia ndani yetu.

    1. KUOKOKA

Mwimbaji mmoja wa Tenzi no. 22, (wimbo; Kale nilitembea) alisema hivi katika ubeti mmoja …

“ Hicho ndicho chanzo cha kufurahi kwangu, hapo ndipo mzigo uliponitulia…

usifiwe msalaba, lisifiwe kaburi linalozidi yote, asifiwe Mwokozi”.

Akimaanisha Msalaba ndio chanzo cha kwanza cha Furaha yake, na hiyo ni kweli kabisa.. Mtu aliyemkimbilia YESU huyo kafungua mlango wa kwanza wa mkondo wa Furaha katika maisha.. kwasababu yeye mwenyewe alisema tukienda kwake atatupumzisha na mizigo tuliyotwikwa na shetani na tutapata raha.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”

   2. MAOMBI.

Huu ni ufunguo wa pili wa  Furaha ya kiMungu.. Bwana YESU alisema tuombe ili furaha yetu iwe timilifu..

Yohana 16:23 “Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.

24 Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu”.

Unapokuwa mwombaji wa mara kwa mara, ukiwa binafsi au katika kikundi cha maombi, kamwe huwezi kupungukiwa Furaha, kwani maombi yanaumba Furaha ya kiMungu yenyewe ndani ya mtu.

    3. KULIISHI NENO LA MUNGU.

Huu ni ufunguo wa tatu wa Furaha ya Mungu:  Tunapolitenda Neno la Mungu/amri za Mungu moja kwa moja Furaha ya Bwana inaumbika ndani yetu, ambayo ndio chanzo cha nguvu yetu.

Yohana 5:10 “Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.

11 Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na FURAHA YENU ITIMIZWE”.

      4. KUIFANYA KAZI YA MUNGU.

Huu ni ufunguo wa Nne wa Furaha ya kiMungu ndani.. Unapojishughulisha na kazi yoyote ya Mungu, iwe kuhubiri mitaani, au kufanya huduma kanisani, au kumtolea Mungu sadaka, au shughuli nyingine yoyote ile ya kikanisa au nje ya kanisa inayohusu ufalme wa Mbinguni, hiko ni chanzo kikubwa sana cha Furaha ya kiungu, ambacho ndicho chanzo cha Nguvu za MUNGU.

Watu wenye kumtumikia Mungu kwa nguvu zao au mali zao wamejaa furaha siku zote.. hata kama watapitia vipindi vya huzuni, lakini kwa kipindi kifupi sana Furaha yao inarejea na wanakuwa na nguvu nyingi za rohoni, wanapotazama matunda ya kazi yao katika Mungu furaha yao inaongezeka.

2Wathesalonike 2:19 “Maana tumaini letu, au furaha yetu, au taji ya kujionea fahari, ni nini? Je! Si ninyi, mbele za Bwana wetu Yesu, wakati wa kuja kwake?

20 Maana ninyi ndinyi utukufu wetu, NA FURAHA YETU”.

     5. KUMSIFU MUNGU.

Huu ni ufunguo wa tano wa Furaha ya kiMungu, tunapomsifu Mungu katika Roho na Kweli, Furaha ya kiMungu inaumbika ndani yetu.. na matokeo ya Furaha hiyo ni Nguvu ya Mungu..

Zaburi 43:4 “Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu”.

Msifu Mungu kwa vitu unavyoviona, msifu Mungu kwa uumbaji wake, msifu kwa upendo wake, msifu kwa miujiza yake n.k

    6. KUSOMA NENO LA MUNGU.

Hiki ni chanzo sita cha Furaha Mungu, Mtu anayesoma Neno la Mungu maisha yake yatatawaliwa na Furaha tu siku zote..

Yeremia 15:16 “Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na MANENO YAKO yalikuwa ni FURAHA KWANGU, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi”.

Ukiwa na Furaha ya Mungu utakuwa na Nguvu ya Kuendelea mbele katika mambo yote, utakuwa na nguvu ya kuomba, utakuwa na nguvu za kusubiri, utakuwa na nguvu ya kuinua wengine nk n.k.

Anza leo kuitafuta Furaha ya Mungu kwani hiyo ndio Nguvu yako, na kama tayari ipo ndani yako basi zidi kuipalilia kwa kufanya mambo hayo sita na mengine yanayofanana na hayo.

Mungu akubariki.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

UTAPATAJE RAHA NAFSINI?

MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.

MSINGI WA NYUMBA YA MUNGU, NI JINA LA MUNGU.

Print this post

Nipo Tayari Kubatizwa.

Ubatizo ni agizo la Bwana katika hatua za awali za wokovu. Wapo watu wanaosema Ubatizo hauna maana, ndugu usijaribu kufanya hivyo, unaweza usiwe na maana kwako, lakini unaomaana kwa yule aliyekupa hayo maagizo.

Kwanini tunabatizwa?

  • Ni agizo la Bwana.

Mathayo 28:19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

  • Tunafuata kielelezo chake yeye mwenyewe:

Ikiwa yeye hakuwa na dhambi wala kasoro yoyote alibatizwa, kwanini sisi tusibatizwe?

Mathayo 3:13 Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.

  • Ni ishara ya nje ya kazi iliyotendeka ndani

Ubatizo ni ishara ya nje ya kile ulichokiamini, kuwa umekufa kwa habari ya dhambi, kisha ukafufuka katika upya na  Kristo.

Warumi 6:3-4

[3]Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

[4]Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Ni nani anayepaswa kubatizwa.

Ni yule aliyeamini, yaani kuupokea ujumbe wa injili kwa geuko(toba).

Matendo 2:41

Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa;…

Ni wakati gani anapaswa abatizwe?

Haraka sana, tangu siku ile alipoamini. Ubatizo sio mpaka  umekomaa kiroho au kimafundisho, hapana, bali ulipopokea tu wokovu, wakati huo huo unastahili ubatizo.

Matendo ya Mitume 2:38

[38]Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Ubatizo sahihi ni upi?

Ni ule wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23, Matendo 8:36-38 ),

Na kwa jina la Yesu Kristo.(Ambalo ndio Jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu) [Mathayo 28:19, matendo 8:16, 10:48, 19:5]

Ikiwa Sikubatizwa kwa kuzamishwa katika maji mengi, au nilibatizwa nikiwa mtoto mchanga yanipasa nibatizwe tena?

Ndio, ili kufuata mkondo sahihi wa kimaandiko, huna budi kubatizwa tena.

Msaada wa ubatizo:

Kwakuwa umeokoka, na bado hujapata huduma hiyo basi waweza tafuta Kanisa la kiroho, ambalo linaamini katika ubatizo wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ili utimize agizo hilo.

Lakini ikiwa utapenda kusaidiwa na sisi. Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo:

+255693036618 / +255789001312

Bwana akubariki.

Mistari ya kusimamia kila ukumbukapo tendo la ubatizo.

Wakolosai 2:12 Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu.

Wagalatia 3:27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.

Bwana akubariki.

Kwa mafundisho zaidi kuhusu ubatizo

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Tofauti kati ya dhehebu na dini ni ipi?

Dini ni mfumo au utaratibu wa kumwabudu Mungu. Kwamfano ukienda mahali ukaona watu wamekusanyika na kukubaliana kuabudu kitu Fulani, ni lazima utaona tu utaratibu, au mwongozo au miiko wamejiwekea ya kuifuata na kuishika, ili ibada yao iwe na matokeo. Sasa huo utaratibu ndio unaitwa dini.

Hata imani yetu ndani ya Kristo, inasukumwa na dini. Hatumwabudu tu Mungu kama tunavyotaka bali Mungu aliweka utaratibu na njia ya kuifuata.

Lakini Dhehebu, ni “aina ya dini”. Ambayo huzalika ndani ya imani ile ile moja. Kwamfano utaona wakristo imani yao ni moja kwa Kristo Yesu, na msingi wa kuegemea ni biblia ile ile moja takatifu. Lakini ndani yao kuna michipuko mingi tofauti tofauti ya kitaratibu na ufanyaji ibada, kulingana na walivyoielewa biblia. Ndio hapo utaona wengine wanajiita wapentekesto, wengine wakatoliki, wengine wasabato, n.k. Sasa hii yote ni michupuko, ambayo mengine inakaribiana sana na uhalisia, na mengine inakwenda mbali na kweli ya Mungu.

Lakini cha kumshukuru Mungu ni kuwa biblia imeshaeleza asili ya dini ya kweli inapaswa iweje….

Yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. 27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.

Kwamba ni lazima itakuwa ya kimatendo zaidi. Yaani utafunzwa utakatifu, na kujitoa.

Swali lingine je! Dhehebu linampeleka mtu mbinguni?

Hapana, kwasababu Yesu hakuja kuleta dhehebu jipya duniani. Kwani alipokuja alikuta tayari yapo madhehebu mengi yamesha-zaliwa kama tu ilivyo sasa, mfano Mafarisayo, na masadukayo. Lakini hakuwahi kutetea lolote kati yao. Bali alisisitiza watu kumwamini yeye, kama ndio njia ya kweli na uzima mtu asipofanya hivyo hawezi  kumwona Baba (Yohana 14:6).

Ikiwa na maana haijalishi una dhehebu zuri kiasi gani. Ukikosa shabaha ya Ukristo, bado mbinguni huendi. Waamini wengi wanashikilia zaidi dini, jambo ambalo ni jema, lakini dini ni kisaidizi cha imani. Sio imani yenyewe, ni sawa na shule na elimu, tunaweza kusema shule ni kisaidizi cha elimu, lakini sio elimu yenyewe.

Hivyo ni busara kuchukua tahadhari ya dhehebu unalotaka kumwabudia Mungu, kwasababu ukweli ni kwamba madhehebu mengine hayana ubora wa kumfanya mtu awe mkristo kamili.

Kwamfano dhehebu lisilo, patana na imani katika Kristo Yesu tu, au lisilofundisha utakatifu, au lisilo amini juu ya vipawa vya Roho Mtakatifu, au linalochanganya ibada ya Mungu na sanamu, bali linasisitiza mambo ya mwilini tu, hilo halikujengi, bali linakupoteza.

Lifananishe  kwanza na biblia yako, huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ndio ufanye maamuzi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE NI YESU YUPI UNAYE? WA KIDINI AU WA UFUNUO!

Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?

Print this post

Kwanini MUNGU aangamize watoto kwenye gharika ya Nuhu?

Swali: Tunajua watoto wachanga hawana dhambi sasa kwanini ile gharika ya Nuhu ilizomba mpaka vichnga?..kwanini Mungu aangamize mpaka watoto wasio na hatia?..napata utata na gharika ile ya Nuhu, na kwenye ile miji ya Sodoma na Gomora je na watoto nao walifanya dhambi ya kustahili kuchomwa na kugharikishwa vile?


Jibu: Ni kweli Biblia inaonyesha ile gharika iliua wote wenye roho ya uhai puani, ikiwemo watoto wachanga na wanyama… na waliosalia ni watu nane tu! Kati ya Dunia iliyokuwa imejaa mabilioni ya watu.

Mwanzo 7:22 “kila kitu chenye pumzi ya roho ya uhai puani mwake kikafa, kila kilichokuwako katika nchi kavu”

Sasa kwanini Mungu aangamize hadi watoto wadogo, na ilihali tunajua kuwa watoto hawana dhambi.

Jibu la swali hili ni kwamba, “mtu anaweza kubeba adhabu ya dhambi ya mwingine lakini asibebe ile dhambi” ili tuelewe vizuri tutafakari huu mfano.. “Mama mjamzito kafanya kosa likamsababishia kifo, ni wazi kuwa na mtoto aliyeko tumboni naye atakufa” kwahiyo adhabu wameshiriki wawili lakini aliyefanya kosa ni mmoja.

Ni hivyo hivyo kipindi cha gharika na kipindi cha Sodoma na Gomora, Watoto walibeba adhabu za wazazi wao ingawa si dhambi!..(wao hawakufanya dhambi yoyote), lakini kutokana na maasi kuwa mengi ikawasababisha nao kushirikishwa katika adhabu hiyo, lakini hiyo haimaanishi kuwa hawataokolewa siku ya mwisho.. huwenda watakaokolewa katika ufufuo wa mwisho kwasababu Mungu ni Mungu wa haki hawezi kumhukumu mtu asiye na kosa.

Lakini kwa wengine (watu wazima) waliosalia ambao ndio waliowasababisha watoto wao kuangamizwa na maovu yao, hao biblia imesema kuwa ipo hukumu nyingine itawapata ya kuhukumiwa kwa mara nyingine na kutupwa katika lile ziwa la moto.

Mathayo 10:15 “Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.

Hapo anasema itakuwa rahisi Sodoma na Gomora kustahimili, maana yake ipo adhabu nyingine kwa watu wa Sodoma na Gomora zaidi ya hiyo iliyowapata ya kuteketezwa kwa moto kutoka mbinguni..

Ndio maana Biblia inasema tumwogope yeye awezaye kuuua mwili, na akiisha kuua mwili (kwa moto au maji au kitu kingine) bado anauwezo wa kushughulika na roho tena na kuihukumu katika ziwa la Moto.

Luka 12:5 “Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana uweza wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo”

Watu wa Sodoma na Gomora, pamoja na watu wa gharika ya Nuhu waliuawa katika mwili, lakini bado tena ipo adhabu nyingine inakuja juu yao, jambo linalotisha sana..

Kwahiyo jambo kuu la kujifunza ni kuwa adhabu inaweza kurithiwa au kushirikishwa na mwingine hata pasipo kufanya kosa, na kinyume chake ni kweli Baraka zinaweza kurithiwa hata pasipo mwingine kufanya mema.. Mzazi unaweza kuwa chanzo cha Baraka au matatizo kwa mtoto wako.

Fahamu kuwa Kama utakuwa mwovu kupindukia basi fahamu pia watoto wako hawatakuwa salama kwa uovu wako, ndicho kilichomtokea Mfalme Daudi baada ya kwenda kulala na mke wa Uria, Biblia inasema mtoto aliyezaliwa alikufa, ijapokuwa mtoto hakufanya kosa lolote… lakini alilazimika kubeba adhabu ya baba yake.

Vile vile kuna mambo mema unaweza kuyafanya yakawa akiba njema kwa watoto wako, au watu wanaokuzunguka wakati wa sasa au wa baadaye.. Kwahiyo ni lazima kumcha Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je gharika ya Nuhu iliangamiza hadi samaki wa baharini na nyangumi?.

JE! NI CHEMCHEMI IPI INATOKA NDANI YAKO, YA MITO AU YA KISIMA?

USIPINDUE MAMBO

Je! Adamu na Hawa walizikiwa wapi?

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Print this post

USIGEUZE JIWE KUWA MKATE.

Je unaujua uhusiano wa JIWE na MKATE kibiblia?.. Hebu leo tujifunze…

Mathayo 7:8 “ kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, MWANAWE AKIMWOMBA MKATE, ATAMPA JIWE?”

Ni hakika, hakuna mzazi yoyote mwenye akili timamu, ambaye mtoto wake akimwomba MKATE atampa JIWE. Hayupo mzazi wa namna hiyo, wala wanyama hawawezi kufanya mambo ya mfano huo wa watoto wao.

Lakini tunaona wakati fulani shetani alijaribu kumchonganisha Bwana YESU na Baba yake wa mbinguni kwa kumwambia, AGEUZE JIWE LIWE MKATE, kana kwamba Baba wa mbinguni alikuwa amemwekea yale mawe kule jangwani kuwa chakula chake (uvunjifu mkubwa wa heshima)!

Luka 4:2 “akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.

3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, LIAMBIE JIWE HILI LIWE MKATE”.

Hili lilikuwa ni jaribu kubwa la shetani kwa Bwana YESU kutaka kumwingizia roho ya kumwona Baba wa mbinguni kama ni mkatili, ambaye anampa mwanae mawe badala ya mkate kupindi cha njaa, na hivyo adui sasa anamfundisha ayageuze yale mawe kuwa mkate.

Na adui alijua kuwa endapo KRISTO angefanya vile (kwaasababu huo uwezo wa kugeuza jiwe kuwa mkate alikuwa nao) angempokonya uhusiano wake mwema aliokuwa nao na Baba yake, na tangu ule wakati angejua Baba anatoa mawe kwa watoto wake badala ya mkate.

Lakini Kristo kwasababu alikuwa amejaa Roho Mtakatifu aliyajua mafumbo yote ya shetani, hivyo hakudanganyika,  na ndio maana hapo baadae katika Mathayo 7:9 akawaambia wanafunzi wake kuwa Baba mwema hawezi kumpa mtoto wake JIWE badala ya MKATE, sasa kwanini alisema vile?..kwasababu alishakutana na jaribu la namna hiyo hiyo jangwani.

Hali kadhalika unapopitia hali Fulani ya majaribu, usianze kutanga tanga na kuruhusu hofu, na kuona kama kila kitu kilichoko mbele yako hata kisicho na uhai ni fursa kutoka kwa MUNGU, sio kila kitu ni fursa kwako wakati wa majaribu!…vingi ni mitego ya ibilisi kwasababu anajua upo katika hali ya uhitaji wa hali ya juuu….hiyo ndiyo kawaida ya shetani.. alitaka pia kumwaminisha Bwana YESU kuwa yale mawe ni fursa ya kuondoa njaa yake.

Si kila kazi inayokuja mbele yako wakati wa vipindi vigumu ni fursa kutoka kwa MUNGU, kazi nyingine ni za Ibilisi (ni mawe). Mungu hawezi kukupa hayo kama riziki, ziache zipite!.. kazi za Bar ni mawe!, kazi ya Saloni za kiduni ni mawe!, kazi inayohusisha rushwa ni jiwe!, kazi inayohusisha kuuza utu wako ni jiwe!, kazi inayohusisha kuabudu miungu mingine ni jiwe!.. usizigeuze MAWE hayo kuwa MKATE!, hata kama una njaa ya kukaribia kufa!..ziache zipite, si majibu kutoka kwa MUNGU, bali ni majaribu kutoka kwa shetani, kwani huwezi kumwomba Baba wa mbinguni MKATE akakupa JIWE.

Huwezi kumwomba akupe kazi nzuri halafu akakuletea kazi ya kujiuza mwili wako!.. huyo sio MUNGU, bali ni ibilisi…Njaa yako, udhaifu wako, changamoto zako ambazo ni za muda tu!, zisikufanye ukaharibu mahusiano yako na MUNGU moja kwa moja.

Je tayari umeshampokea YESU?.. Kama bado fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho, na YESU amekaribia kurudi, na dunia inaenda kuisha, ni heri leo ukayasalimisha maisha yako kwake, ili usamehewe dhambi zako na jina lako liandikwe kwenye kitabu cha Uzima cha Mwanakondoo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Je ni kweli Bwana YESU hajui siku ya kuja kwake? (Mathayo 24:36)

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI.

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

Print this post

Tafsiri ya Mithali 3:27 inayosema ‘Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao’

SWALI: Nini maana ya Mithali 3:27 ?

[27]Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda.


JIBU: Kuna mambo mawili yaliyogusiwa katika hicho kifungu..

  1. Usiwanyime watu mema yaliyo Haki yao.
  2. Lakini pia, ‘ikiwa katika uwezo wa mkono wako’.

1] Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao.

Hili ni agizo la Bwana kuwasaidia wengine. Lakini pia Bwana anataka tujue ni akina nani wenye haki hiyo ya kusaidiwa.

Kibiblia Makundi ambayo ni haki yao kusaidiwa.(wawapo na shida), ni matatu (3)

 i) Familia (yaani ndugu wa mwilini)

1 Timotheo 5:8

[8]Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

Wazazi wako, wadogo zako, watoto wako. Ni haki yao kuwasaidia, kwasababu ni damu moja na wewe. Usipotimiza wajibu huo unahesabika sawa na mtu aliyeikana imani. Hakikisha jicho lako haliwapiti ndugu zako, ni sehemu ya wajibu.

ii) Ndugu wa rohoni:

Wagalatia 6:10

[10]Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

Kanisa la kwanza lilitambua jukumu hili la kusaidiana, vivyo hivyo na sisi ikiwa mpendwa mwenzako yupo katika hali na uhitaji mkubwa hupaswi kufumba macho, bali msaidie, watumishi wa Mungu wanaojibidiisha kuhubiri kweli ya Mungu wanastahili kusaidiwa mahitaji yao. (Warumi Romans 12:13, Hebrews 13:16).

1Yohana 3:17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.

Hapa inalenga pia na wajane pia walio ndani ya kanisa wale walio wajane kwelikweli. (1Timotheo 5:3–5, 9–10)

iii) Maskini.

Wapo maskini wengi ulimwenguni, ambao wanashindwa kufikiwa na mahitaji yao ya msingi, wengine wanakuwa mabarabarani walemavu, wagonjwa, majirani maskini, wote hawa pia wanastahili kusaidiwa.

Wagalatia 2:10 ila neno moja tu walitutakia, tuwakumbuke maskini; nami neno lilo hilo nalikuwa na bidii kulifanya.

Hayo ndio makundi yenye haki ya kusaidiwa. Lakini wengine wanaweza kusaidiwa lakini sio haki yao,ikiwa na maana hata wasiposaidiwa hakuna shitaka lolote juu yako kwa Mungu.

2]  Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda:

Lakini Ukiendelea kusoma anagusia tena jambo la pili ambalo ni; “Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda”.

Akiwa na maana gani?

Mtume Paulo kwa uweza wa  Roho aliandika maneno haya;

2 Wakorintho 8:12-13

[12]Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo.  [13]Maana sisemi hayo, ili wengine wapate raha nanyi mpate dhiki;

Yaani kwa jinsi moyo wako unavyoguswa, tenda mema,  lakini pia kulingana na uwezo wako uliokirimiwa na Mungu,  ili upande mmoja usiuache na taabu au kupungukiwa kabisa. Kwamfano umepata rizki kipimo cha watoto wako tu, ukaenda kukichukua na kuwapa maskini huku familia yako ikabaki Kulala njaa.. hapo hujafanya busara kwasababu umehamisha Tatizo sehemu moja kupeleka kwingine, hujatatua tatizo.

Tenda mema, bila kusahau pia kipimo chako ulichopimiwa cha mema.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Masomo mengine:

Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe?

Print this post

Ipi tofauti ya Falme, Mamlaka na Wakuu wa giza (Waefeso 6:12)

Jibu: Turejee..

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya FALME na MAMLAKA, juu ya WAKUU WA GIZA HILI, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”.

Hapa kuna vitu vinne, vilivyogawanyika katika sehemu mbili.. Kundi la kwanza ni “FALME na MAMLAKA” na kundi la pili ni “WAKUU WA GIZA na JESHI LA MAPEPO” jumla mambo manne (4)

Sasa hebu tuanze na kundi la kwanza la FALME na MAMLAKA.

Mwandishi (ambaye ni Paulo, Mtume wa Bwana YESU) alitumia mfumo wa Tawala za dunia, kutoa picha ya tawala za ufalme wa giza.

Katika Dunia tunajua kunakuwa na Falme za wanadamu… Kwamfano kuna Falme za kiafrika, falme za kiarabu, Falme za kiasia n.k,

Sasa kwa vizazi vyetu nyakati hizi mfano wa Falme ni hizi SERIKALI tulizonazo (ambapo kila nchi inayo serikali yake), lakini zamani za kale Falme zilibaki kuitwa falme..Kwamfano kwenye Biblia utaona kulikuwa na Ufalme wa Umedi na Uajemi, Ufalme wa Babeli, Ufalme wa Uyunani, Ufalme wa Rumi n.k.. Hizi zote zilikuwa ni falme na ziliongozwa na Wafalme.. kwahiyo katika ulimwengu kulikuwepo na Falme Nyingi, zenye wafalme wengi, lakini dunia ni moja.

Tusogee mbele zaidi..

Chini ya kila Falme (au serikali) kunakuwa na Mamlaka, kwamfano katika Serikali ya nchi ya Tanzania, kuna Mamlaka mbalimbali, kuna Mamlaka ya mapato (TRA), Mamlaka ya Maji safi na maji taka, Mamlaka ya mawasiliano, Mamlala ya Hali ya hewa, Mamlaka ya Elimu, Mamlaka ya bandari n.k, hivi vyote ni viungo vya Serikali kwaajili ya kuwahudumu walio chini ya Serikali/Ufalme.

Kwahiyo tunaweza kurahisisha kwa kusema mfano huu, “Vyanzo vya maji vyote vilivyopo katika UFALME wa Tanzania vipo chini ya MAMLAKA ya maji ya maji ya nchi hiyo”… au Ukusanyaji wa kodi za wananchi katika Ufalme/serikali ya Tanzania upo chini ya MAMLAKA ya Ukusanyaji mapato (TRA)….Au jukumu la Ulinzi wa raia na mali zao la Ufalme wa Tanzania lipo chini ya Mamlaka ya ulinzi na usalama kupitia chombo chake maalumu kiitwacho Polisi….Umeona huo muunganiko wa Ufalme na Mamlaka?.

Na kawaida kila Mamlaka inayo Wakuu wake na jeshi.. Ndio hapo utasikia “Mkuu wa mamlaka ya mapato” au Mkuu wa mamlaka ya mawasiliano,  na jeshi zima la mamlaka hiyo ni wafanya kazi wote waliopo chini ya mamlaka hiyo..

Na katika ULIMWENGU wa giza ni hivyo hivyo, kuna FALME na pia kuna MAMLAKA mbalimbali… Zipo mamlaka za uuaji na utekaji (mfano wa hizo ni zile zilizoruhusiwa kumkamata Bwana YESU (Soma Luka 22:53),

zipo mamlaka za uharibifu wa ndoa, zipo mamlaka za uharibifu wa huduma, zipo mamlaka za uharibifu wa familia, kazi n.k n.k,

Na kila mamlaka ya giza inayo Mkuu wake/Kiongozi ambaye ni Pepo (hao Ndio wanaoitwa wakuu wa giza)..  Hapa ndipo tunapofika katika kundi la Pili la WAKUU WA GIZA na MAJESHI YA MAPEPO.

Sasa kama kuna kiongozi au mkuu, ni wazi kuwa kuna Jeshi chini yake, (hakuna kiongozi/mkuu asiye  na jeshi la watu chini yake la kuliongoza)

hivyo mapepo yote yaliyosalia yanayofanya kazi chini ya Wakuu wa giza ndio wanatengeneza kundi la majeshi ya mapepo wabaya.

Kwahiyo Biblia inaposema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama bali juu ya FALME NA MAMLAKA NA WAKUU WA GIZA NA MAJESHI YA PEPO WABAYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, imemaanisha kuwa tunapambana na wakuu wa giza (Wakuu wa mapepo) na majeshi yao ambayo yanatumia Mamlaka na Ufalme wa giza kupambana nasi.

Kwahiyo ufalme wa giza, imesimama katika ngazi zake, kuonyesha kuwa vita vyetu si virahisi kama tunavyovichukulia, kupambana na falme si kazi ndogo! Inahitaji msuli wa kutosha wa kiroho, maana yake ni lazima mtu uwe umesimama kwelikweli, umezama kweli kweli kwenye ufalme wenye nguvu kuliko huo wa giza.

Na hakuna ufalme mwingine wenye nguvu kuuzidi ufalme wa giza, zaidi ya UFALME WA MBINGUNI, ambao Mkuu wa Ufalme huo ni YESU KRISTO (Mwamba Mgumu). Huyo ndiye mwenye nguvu za kuuvunja nguvu zote za falme za giza, na hana namba mbili yake!..

Je unaye YESU moyoni na maishani?.. Kama hujaokoka fahamu kuwa upo chini ya ufalme wa giza na mamlaka za giza hata kama ni tajiri, au una afya au una mafanikio mengine yote, bado upo chini ya utawala wa giza, wanaweza kukufanya chochote kwa wakati wowote, na wanaweza kukutumia vyovyote watakavyo, Mgeukie YESU leo na uhame kutoka katika huo ufalme wa giza.

Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;

14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.

16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.

17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.

18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mkristo anaweza akawa na mapepo?

Je! tunaweza kuwaamuru Malaika kama tunavyoyaamuru mapepo?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.

Print this post

Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?

SWALI: Naomba kufahamu Warumi 7:25 ina maana gani?

Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.

JIBU: Katika sura yote ya saba, mtume Paulo, anaeleza kwa kina mapambano yaliyo ndani ya mwamini.  Kwamba nia yake kutoka ndani ni kuitii sheria ya Mungu, lakini mwili wake kwa nje ni kikwazo kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kabisa kutimiza maadhimio yake.

Warumi 7:19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu

Na ni kweli huo ndio uhalisia wa kila mtu. Na ndio maana mwishoni mwa sura hiyo anahitimisha kwa kueleza hali hiyo, Lakini katika vifungu hivyo, wengi wanatafsiri vibaya wakidhani  Paulo anatetea udhaifu wa mwili hapana.. Kinyume chake alianza kwanza kueleza uhalisia wa kibinadamu, ili atoe suluhisho halisi la namna ya kushinda, ambalo ndio tunalisoma katika sura inayofuata ya nane (8)

Ambapo sasa kwenye sura ya nane(8) inayofuata, anaeleza namna ambayo Kristo anatusaidia kuishinda hiyo hali, kwa sheria nyingine  mpya ya Roho ambayo anaiweka ndani yetu.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yake ni kuwa, Roho Mtakatifu, anatuweka huru katika huo utumwa wa mwili unaotupelekesha.

Inahitaji tu kutii, kwa kumfuata Roho Mtakatifu, kisha yeye mwenyewe atatupa nguvu ya kushinda mambo yote ya mwilini. Lakini sio kwa kutegemea  nguvu zetu tu wenyewe.

Warumi 8: 5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.

7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.

9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.

10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.

Hivyo ukiishi kwa kumtii Roho Mtakatifu, basi huwezi tumikishwa tena na  mwili,

Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

Hitimisho:

Warumi 7:25, Paulo analenga hasaa sababu ya sisi kushindwa kutimiza sheria ya Mungu, Ni kwasababu ipo sheria nyingine (ya dhambi iliyojificha ndani yetu) ambayo ni ngumu kutoka kwa namna ya kibinadamu, hivyo anataka hilo tulijue ili tufahamu kuwa kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuishinda, Lakini kwa Yesu Kristo atupaye Roho wake ndani yetu, tukienenda kwa kumtii huyo, basi sheria hiyo ya dhambi tutaishinda kabisa kabisa.

Ni wito wa kila mwamini kujifunza kutembea katika Roho.

Je! Unafahamu namna ya kutembea katika Roho kama sio. Basi tutumie ujumbe kwa namba uzionazo chini ya somo hili tukutumie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Print this post

Kwanini Nyaraka za Paulo kwa makanisa tuzifanye kuwa nyaraka zetu leo?

Swali: Nyaraka za Paulo tunaona ni barua kwenda kwa makanisa yaliyokuwepo wakati huo, kama Korintho, Efeso, Kolosai na Galatia na nyingine kwenda kwa watu waliokuwepo wakati huo, kama Timotheo, Tito na Filemoni sasa iweje nyaraka hizo zituhusu na sisi na hata ziwe ni neno la MUNGU?, na kuzitumia hizo kufundishia sasa?


Jibu: Swali zuri lakini ili tuweze kupata majibu yaliyojitosheleza, hetu tutafakari mifano ya kawaida iliyopo,

Alikuwepo mwanasayansi mmoja  wa kijerumani maarufu ambaye sasa ni marehemu ajulikanaye kama Albert Einstein (Mgunduzi wa kanuni ya kutengeneza bomu la Nyuklia), huyu wakati wa vita vya pili vya dunia alimwandikia waraka Raisi wa Marekani aitwaye Roosevelt, kwamba atengeneze silaha ya Nyuklia, kabla Adolf Hitler hajaitengeneza, na katika waraka huo alimpa pia hiyo fomula/kanuni ya kutengeneza silaha hiyo. (Waraka huo uliandikwa mwaka Agosti 2,1939).

Na matokeo ya waraka huo ni Raisi Roosevelt kuunda bomu la Nyuklia, na kwenda kulifanyia majaribio katika miji miwili ya nchi ya Japani (Mji wa Heroshima na Nagasaki).

Lakini ajabu ni kwamba baada ya wakati huo, sehemu za waraka huo zilizobeba kanuni za utengenezaji wa nyuklia zilivuja na kufikia mataifa mengine, na mataifa hayo kama Urusi hayakulaza damu bali nayo pia yakaunda mabomu ya nyuklia yenye kanuni ile ile, zilizokuwepo ndani ya ule waraka.

Na cha ajabu zaidi ni kwamba miaka mingine mingi mbele mataifa mengine kama Ufaransa, Pakistani,India, na mengine machache yakaichukua kanuni hiyo hiyo ya kuunda bomu la Nyuklia na kutengeneza mabomu yao,

Na cha kushangaza zaidi na zaidi ni kwamba mataifa mengine mengi leo yanafanya jitihada kuunda mabomu yao kupita kanuni ile ile ya mwanasayansi huyo Albert Einstein aliyetokea miaka mingi huko nyuma kupitia waraka wake aliomwandikia Raisi wa Marekani.

Sasa swali la kujiuliza, ni hili; kulikuwa kuna haja gani ya Mataifa kama Urusi, Ufaransa, na mengineyo kufuatilia waraka Einstein aliomwandikia Raisi Roosevelt na hata kuzitumia kanuni/fomula alizoziandika ndani yake kutengeneza mabomu yao??..

Tulitegemea waraka wa Einstein kwenda kwa Raisi huyo, uishe matumizi baada ya kusomwa na kutumika na Raisi huyo wa Marekani, lakini ajabu ni kwamba mpaka sasa una matokeo katika ulimwengu wetu, ingawa uliandikwa miaka mingi iliyopita.

Kwahiyo Utaona kwamba sababu pekee ya mataifa mpaka leo hii kuitumia kanuni ya mwanasayansi huyo aliyetokea miaka mingi huko nyuma ni kwasababu alichokigundua Albert Einstein ni kitu cha Kweli chenye manufaa na tija si tu kwa wakati wake tu, au Taifa lake tu bali hata kwa mataifa mengine na kwa vizazi vingi vijavyo.

Na ni hivyo hivyo Nyaraka za Mtume Paulo na za Mitume wengine… kwa jicho la nje zitaonekana kama zimeandikwa kwaajili ya makanisa yale ya wakati ule, au kwaajili ya watu wa wakati ule, lakini kwa jicho la rohoni ni ujumbe kwetu zaidi hata ya watu wa wakati ule.

Kwasababu yaliyoandikwa katika nyaraka za Mitume wa kwenye Biblia ni maneno ya kweli yanayoishi katika vizazi vyote, na tena kwa jinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo yanavyohitajika zaidi kwasababu yaliyokuwa yanatendeka zamani, sasa hivi yamezidi mara nyingi sana.

Vita vya kiroho walivyokuwa wanapigana watu wa kanisa la Korintho, Galatia, na mengineyo nyakati hizo ndizo tunazopambana sasa, tena wakati huu zimezidi zaidi, kwahiyo tunahitaji fomula na kanuni za wanasayansi wetu wa kiroho (Mitume na manabii wa kwenye Biblia) kutengeneza silaha zetu za kiroho sasa, na kupambana hivi vita mpaka tushinde.

Lakini tukibaki na kusema zile nyaraka zilikuwa ni za wakorintho tu peke yao na wagalatia tu peke yao, na kwamba sisi hazituhusu tutamalizwa vizuri na shetani, ni sawa na Taifa la Urusi liseme ule waraka wa Einstein aliomwandikia Raisi wa Marekani, kuhusu utengenezaji wa Nyuklia uliwahusu Wamarekani peke yao, wangekuwa na akili hiyo, leo wangeisha, au wangetawaliwa!.

Na sisi ni lazima tuiamini Biblia, kuwa ni Neno la MUNGU linaloishi kwa nyakati zote na vizazi vyote, hakuna wakati litaisha matumizi, au litapitwa na wakati, Mafunuo yaliyokuwemo ndani ya Biblia yana nguvu na Uwezo, kwani waliofunuliwa wamefunuliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu na si kwa akili zao.

Mwisho; Je umempokea YESU kwelikweli au kidini?.. kama maisha unayoishi ni ya uvuguvugu bado hunaye YESU, unamhitaji YESU aingie maishani mwako, unahitaji kujikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata YESU, Fanya mageuzi na acha kuishi maisha ya uvuguvugu, kwani tunaishi nyakati za hatari na muda umeenda sana, na parapanda inalia muda wowote, na mambo yote yatapita.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Print this post

SADAKA INAONDOA MADHARA YA MAUTI

Sadaka inayotolewa kwa mwongozo wa Neno la MUNGU ina matokeo makubwa sana kwa anayeitoa. Yapo madhara yanayoondoka kwa maombi tu peke yake, lakini yapo mengine yanahitaji sadaka pamoja na maombi.

Hebu turejee Biblia kidogo tujifunze jambo..

Wakati ambapo Nabii Samweli anataka kwenda kumpaka mafuta Daudi ili awe mfalme mahali pa Sauli..biblia inatuambia kuwa alipofikiri kwenda tu hofu ilimwingia..

Na hofu hiyo ni kwamba alimwogopa Mfalme Sauli, kwani alijua kabisa endapo Sauli akisikia mtu mwingine anaenda kupakwa mafuta ya kifalme kuchukua sehemu yake, wivu utamwingia na atataka kumwua nabii Samweli na yule atakayeenda kupakwa mafuta.

Sasa ili zoezi la Daudi kupakwa mafuta likamilike bila kuleta madhara yoyote kwa Nabii Samweli na Daudi anayeenda kupakwa mafuta ya kifalme, SADAKA ILIHUSIKA!.

Utauliza ilihusika vipi?…turejee maandiko…

1 Samweli 16:1 “BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.

2 Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi BWANA akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea BWANA dhabihu.

3 Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako”

Je umeiona nafasi ya sadaka katika kuyaokoa maisha ya Samweli na Daudi?.

Hapo MUNGU hakushindwa kumwambia nabii Samweli aende hivyo hivyo na kwamba atamlinda!…La! Hakufanya bali alimwambia aende na dhabihu..

Jambo hilo Bwana MUNGU wetu aliliruhusu pia ili tuelewe umuhimu dhabihu/sadaka.

Unapomtoleo MUNGU kwa ufunuo wa Neno, bila kushurutishwa na mtu wala uchungu, kuna mambo mengi katika ulimwengu wa roho yanafanyika, kama ni nira za mauti zinalegea na kama kuna vifungo vya dhambi pia vinaondoka.

Na kumbuka sadaka kwa BWANA inapelekwa kwa BWANA, maana yake mahali ambapo BWANA anatumikiwa (mfano kanisani au mahali panapofanyika kazi ya MUNGU ikiwemo mikitano ya injili)..hapo ndipo penye neema.

Usipeleke sadaka yako maalumu mahali pengine kama kwa marafiki, au watu au maskini wa barabarani…ni vizuri kufanya hivyo na kuna baraka zake lakini vya Bwana vinapaswa vipelekwe kwa Bwana ndivyo maandiko yanavyofundisha..

Tenga kiasi chako kungine peleka kwa maskini na wenye uhitaji, lakini hakikisha una sadaka yako maalumu kwa BWANA utakayopeleka aidha kanisani au mahali popote kazi ya MUNGU inapofanyika kwa usahihi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post