Kama kichwa cha waraka Huu kinavyosema… “Waraka wa pili wa Paulo Mtume kwa Wakorintho”
Kutuonyesha kuwa Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hichi..
Tunaweza kukigawanya katika sehemu kuu tatu (3)
1) Utendaji kazi wa Mungu, na wajibu wa watakatifu katika huduma na maisha yao ( sura ya 1-7)
2) Utoaji bora kwa mkristo.(Sura ya 8-9)
3) Utetezi wa huduma ya Paulo (10-13)
1) Utendaji kazi wa Mungu, na wajibu wa watakatifu katika huduma na maisha yao ( sura ya 1-7)
Katika sura hizi, Mtume anagusia maeneo kadha wa kadha, kama ifuatavyo.
i) Faraja ya Mungu
Paulo anatoa shukrani zake kwa jinsi Mungu anavyoweza kuwafariji watu wake katikati na dhiki na majaribu mazito. Akimtaja Mungu kama ni ndio mtoa faraja yote, katika dhiki zetu. (1-3-7)
2 Wakorintho 1:3-4
[3]Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote;
[4]atufarijiye katika dhiki zetu zote ili nasi tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote, kwa faraja hizo, tunazofarijiwa na Mungu.
ii) Nafasi ya kutubu.
Sehemu inayofuata Paulo anaeleza sababu ya kutofika Korintho haraka, kama ilivyodhaniwa. Ni ili asilete tena huzuni zaidi kama akiwakuta bado hawajakamilika. Na hiyo ni kutokana na kuwa hawakuwa na mabadiliko ya haraka kwa agizo lake la kwanza, hivyo hakutaka afanye ziara ya ghafla bali wayatengeneze kwanza wao wenyewe ili ziara yake kwao, safari hii iwe ya raha na sio ya hukumu.(1:23-2:4)
iii) Wajibu wa kusamehe. (2:5-11)
Paulo anawahimiza wakorintho kusamehe kwa wale watu wanaoleta huzuni ndani ya kanisa, Hususani waliomnenea vibaya utume wake. Anahimiza kuliko kusimamia adhabu ziwapasazo ambazo wana haki kweli ya kuzipokea. Kinyume chake wawasamehe ili wawapate tena wasipotee kabisa katika huzuni zao.
IV) Utukufu wa agano jipya.(sura ya 3-5)
Paulo Anaeleza jinsi gani, agano jipya utukufu wake ulivyo mbali na ule wa agano la kale. Kwasababu utukufu wa agano jipya umekuja Katika Roho atoaye uhuru.
Paulo anaeleza kwasababu hiyo hatupaswi kulegea kwa kuenenda kwa hila au kulichanganya Neno la Mungu na uongo. Au kwa kutohubiri injili. Bali kufanya yote bila kujali utu wetu wa nje kuchakaa. Tukijua kuwa ule wa ndani unafanywa upya siku baada ya siku na kwamba ipo siku tutasimama mbele ya kiti hukumu kutoa Hesabu ya mambo yetu yote tuliyoyatenda katika mwili.
Paulo anaeleza kwamba kama Kristo alivyopewa huduma ya upatanisho sisi pia tumepewa Neno Hilo hilo ndani yetu. Kuupatanisha ulimwengu na Mungu kupitia Yesu Kristo. Akionyesha kuwa ni wajibu wetu sote kuhubiri injili.
V) Maisha ya ukamilifu (sura ya 6-7)
Paulo anawasihi Wakoritho waikunjue mioyo yao na waishi maisha ya ukamilifu na ya uangalifu wasiwe kwazo la namna yoyote ili utumishi wao usije laumiwa siku ile ya Bwana
Lakini pia anawapa onyo wasiwe na ushirika na wasioamini.
Pamoja na hilo katika sura ya saba, Paulo anaeleza furaha yake kwa Wakorintho Kwa kuitii toba..kufuatana na waraka aliowaandikia hapo kabla wa huzuni ( Ambao haupo miongoni mwa nyaraka hizi zilizo kwenye biblia). Ambapo walipousoma walitubu na kugeuka, kwelikweli. Kuonyesha utii wa toba. Ambao unapaswa uonekane ndani ya makanisa hata sasa.
2) Utoaji bora kwa mkristo.(8-9)
Katika sura ya 8-9
Paulo anahimiza michango kwa ajili ya watakatifu walio Yerusalemu, Akitolea mfano watakatifu wa Makedonia jinsi walivyoweza kutoa kwa ukarimu hata katika umaskini wao, vivyo hivyo na wao anawahimiza wawe na moyo huo huo. Akiwaonyesha jinsi Bwana wetu Yesu alivyotupa kielelezo cha kukubali kuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.
2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
Kwasababu utumishi wa namna hiyo sio tu unawapata watakatifu rizki lakini pia huleta matunda ya shukrani kwa Mungu.
2 Wakorintho 9:12
[12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu;
3) Utetezi wa huduma yake (Paulo). Sura ya 10-13
Katika sura hizi Paulo anaitetea Huduma yake dhidi ya watu wengine wanaojitukuza mbele za watu, kana kwamba ni mtume wa kweli kumbe ni mitume wa uongo, ambao huwashawishi watu kwa majivuno ya nje na ukali, lakini si ya kazi.
2 Wakorintho 11:20
[20]Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.
Hivyo Paulo anawaeleza kwa upana uthabiti wa huduma yake, tangu asili ya kabila lake, mateso aliyopitia, akionyesha mpaka kusimama vile, hakukutokea hivi hivi tu, bali katika masumbufu mengi, anawaeleza pia maono aliyoyafikia mpaka kunyakuliwa mbingu ya tatu, hiyo yote ni kuwaonyesha wakorintho kama wanataka kuamini kwa watu wanaojisifia basi yeye anawazidi wao, lakini hatumii njia hiyo, bali ya udhaifu ili asihesabiwe zaidi ya vile watu wavionavyo Kwake.
Salamu za mwisho.
Anahimiza wakoritho wanie Mamoja, watimilike na wafarijike.
Hivyo kwa ufupi mambo haya makuu tunaweza kuyapata katika waraka huu;
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.
Rudi Nyumbani
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.
JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..
NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza
Kitabu hichi ni moja ya nyaraka zilizondikwa na mtume Paulo katika agano jipya,
Waraka huu amegusia mambo mengi, hasahasa katika eneo la marekebisho na maonyo. Unagusia nidhani na taratibu za kikristo zinazopaswa zifuatwe ndani ya kanisa, unazungumzia pia eneo la uhalisia wa ufufuo wa wafu katika siku ya mwisho pamoja eneo la upendo.
Na huu ndio uchambuzi wake katika maeneo mama;
Paulo anatoa onyo juu ya migawanyo ambayo ilianza kutokea ndani ya kanisa iliyozaa wivu na fitina, ambayo ilisababishwa kwa baadhi ya watu kujiwekea matabaka kwa kujivunia viongozi kwa kusema mimi ni wa Paulo, mimi ni wa Apolo, mimi ni wa Kefa. Akiwatahadharisha na kuwasihi kwa kuwaeleza kwamba wao ni wahudumu tu katika nafasi mbalimbali, bali mkuzaji ni Kristo. Na hivyo hawapaswi kujivunia wao, bali Kristo
Kristo ni hekima ya Mungu na nguvu ya Mungu.(1:18- 2:16)
Eneo la pili Paulo anatoa ufahamu hasaa juu ya hekima anayoitambua Mungu, akionyesha kuwa hekima ya ulimwengu huu, kwa Mungu ni upuzi, bali hekima ya Mungu ameificha ndani ya Kristo Yesu, na hivyo amewachagua watu wadhaifu na wanyonge kuwadhihirishia hiyo. Akionyesha kuwa mtu asitegemee sana kumwona Mungu katika mambo yanayodhaniwa kuwa ni makuu, bali katika Kristo Yesu.
1 Wakorintho 1:24
[24]bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.
Katika eneo hili Paulo anastaajabishwa kwa kuzuka kwa zinaa mbaya ambayo haionekani hata kwa mataifa yaani mtu na mzazi wake kuzini,. Akiwaagiza kutoa hukumu juu ya watu kama hao, hata kwa kuwakabidhi shetani (lengo ni waponyeke)
Kwasababu wakiachwa mwisho wao huwa ni kulichafua kanisa, (kulitia unajisi),
Vilevile tunaona Paulo akitoa agizo kuwa kanisa halipaswi kuchangamana na wazinzi.
Akisisitiza kuwa mtakatifu sio tu awe amehesabiwa haki bali pia awe ameoshwa na kutakaswa na udhalimu wote.
Anawaagiza pia watakatifu hawapaswi kupeleka mashtaka yao kwa watu wa kimataifa, bali kanisa ni zaidi ya mahakama ambayo watakatifu wanapaswa watatulie migogoro yao hapo.
Paulo anaeleza kwa upana, taratibu ya kindoa, katika eneo la haki zao za ndani na kuachana, na wito wa utowashi(useja). Katika eneo la haki, anasisitiza kuwa kila mwanandoa anapaswa atambue kuwa hana haki juu ya mwili wake mwenyewe, bali mwenzake, lakini pia katika kuachana, anaeleza ikiwa mwanandoa mmoja haamini, Yule aliyeamini hapaswi kumwachwa mwenzake, ikiwa bado anataka kuendelea kuishi naye. Lakini pia anatoa pendekezo lake Mtu akitaka kumtumikia Mungu kwa wepesi zaidi bila kuvutwa na mambo ya mwilini na dhiki za kiulimwengu. Basi akikaa bila kuoa/kuolewa afanya vema zaidi.
Anaeleza jinsi gani mkristo anapaswa kukabiliana na dhamiri yake na ile ya wengine,katika maamuzi ayafanyayo kwa ujuzi wake, akigusia eneo la vyakula (hususani vile vilivyotolewa sadaka kwa sanamu), kwamba hivyo havituhudhurishi mbele za Mungu, lakini tukila pia tuangalie wengine wanaathirikaje. Tusije tukawakwaza kwa ujuzi wetu. Paulo anaeleza ili tuweze kufikia hapo yatupaswa kuyafanya yote katika upendo.
1 Wakorintho 8:11-13
[11]Na yule aliye dhaifu aangamizwa kwa ujuzi wako, naye ni ndugu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.
[12]Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo.
[13]Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu.
Lakini pia anaeleza haki waliyonayo mitume, kwamba wanaouwezo wa kula katika fungu la kanisa, lakini hawakutumia ujuzi wao wote, ili waweze kuifikisha injili kiwepesi kwa watu bila kuwazuilia na wengine.
Paulo anatoa utaratibu wa ki-Mungu wa namna ya kuhudumu, kufuatana na hali ya kijinsia. Kwamba kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha mwanamume ni Kristo na kichwa cha Kristo ni Mungu. Hivyo mwanawake anapaswa wafunikwe vichwa awapo ibadani, ili kuonyesha kichwa chake(mumewe) kinamilikiwa na Kristo. Na kwamba wanawake wanapaswa watii uongozi (1Wakorintho 14:34-40)
Paulo anaeleza pia nidhani katika kushiriki meza ya Bwana, kwamba inapaswa ifanywe katika ufahamu na utaratibu sahihi wa rohoni, vinginevyo itapelekea hukumu badala ya baraka
Paulo anazungumzia kwa undani karama mbalimbali ambazo Mungu ameziweka katika kanisa na kwamba zinapaswa ziwe kwa lengo la kufaidiana na kujengana. Lakini anaeleza kipawa kilicho bora zaidi ya karama zote, nacho ni upendo, ambacho anakieleza kwa urefu katika sura inayofuata ya 13, kwamba hichi kimezidi vyote.
1 Wakorintho 13:1-8
[1]Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
[2]Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
[3]Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
[4]Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
[5]haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
[6]haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
[7]huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
[8]Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
Katika eneo hili Paulo anahimiza fundisho la kufufuliwa kwa wafu, akionyesha jinsi lilivyo umuhimu katika imani ya kikristo, na hiyo ni kutokana na baadhi ya watu waliozuka ndani ya kanisa kufundisha fundisho la kisadukayo kwamba hakuna ufufuo wa wafu.
Akieleza jinsi Bwana atakavyokuja kwamba siku ya kurudi kwake parapanda italia na wote kwa pamoja (tulio hai na waliokufa) tutaipokea miili mipya ya utukufu itokayo mbinguni.
Katika sehemu hii ya mwisho Paulo anawaagiza juu ya utaratibu wa changizo kwa ajili ya watakatifu, kwamba vifanyike kila siku ya kwanza ya juma wakutanikapo, anawaagiza pia wakeshe, wawe hodari, na mambo yao yote yatendeke katika upendo.
Kwa hitimisho ni kuwa waraka huu unalenga hasa marekebisho, juu ya mambo mengi yaliyokuwa yanatendeka kwasababu ya ujinga, upumbavu, na dhambi ndani ya kanisa la Kristo. Na Ukweli ni kwamba mambo kama haya haya ni rahisi kuonekana hata katika kanisa la leo. Waraka huu tuusomapo yatupasa tuutazame kwa jicho la kikakanisa je! makosa kama ya wakorintho yapo katikati yetu, kama ni ndio basi tujirekebishe haraka sana.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Kichwa cha waraka huu kinasema. “ Waraka wa pili wa Paulo mtume kwa Wathesalonike”
Kutuonyesha kuwa Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu, kwa kanisa hili la Thesalonike.
Lakini pamoja na hilo tunaona Waraka huu wa pili kama ulivyo ule wa kwanza anawataja pia Timotheo na silwano(Sila), kama waandishi wenza.
Aliundika akiwa Korintho, sawasawa na taarifa tunazozipata katika kitabu cha Matendo 18,.
Maudhui makuu ya waraka huu yalikuwa ni matatu(3), nayo ni;
Kwa maelezo mafupi tuyaangazie maeneo hayo matatu.
> Paulo anawatia moyo watakatifu kwa uthabiti wa imani yao ambayo imesimama sikuzote hata ilipopitia kwenye dhiki nyingi na adha.
2 Wathesalonike 1:4
[4]Hata na sisi wenyewe twaona fahari juu yenu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya saburi yenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na dhiki mnazostahimili.
> Lakini pia anawaeleza hatma ya watu wanaowaletea adha, kwamba Mungu ni wa haki, na atawalipiza kisasi hao wanaowatesa. Kwa kuwaadhibu kwa maangamizi ya milele.(1:8-9)
2 Wathesalonike 1:6
[6]Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi;
> Lakini anaeleza ahadi ya raha ambayo Mungu amewawekea waamini huko mbeleni watesekao kwa ajili yake.
2 Wathesalonike 1:7
[7]na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake
Anarekebisha upotofu uliozuka juu ya siku ya Bwana,kama kweli tayari imeshakuwapo au la, hivyo katika sura hii ya pili, anawaonya kwa kuwaambia siku hiyo haiji kabla ya ule ukengeufu kwanza kuja, na yule mwana wa kuasi, mwana wa uharibifu (mpinga-kristo) kufunuliwa.
2 Wathesalonike 2:1-3
[1]Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake,
[2]kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo.
[3]Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;
Akiwa na maana kuwa kabla ya Kristo kurudi mara ya pili, ukengeufu wa kiroho mkubwa sana utatokea, na yule mpiga-kristo kujidhihirisha na kujulikana kwa kazi zake.
Ambazo zitakuwa ni kama ifuatavyo;
> Kujiinua juu ya kila kitu kiitwacho Mungu, akijifanya yeye ndio kama Mungu.
2 Wathesalonike 2:4
[4]yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.
> Atakuwa na utendaji kazi wa shetani ndani yake, kwa kufanya maajabu ya uongo ili kuwadanganya wote waliomkataa Mungu katika fahamu zao.(2:9-12)
> Lakini mwisho wake utakuwa ni kuangamizwa na Yesu.(2:8)
Paulo anaendelea kusema kwasasa hawezi kutenda kazi kwasababu yupo azuiaye, mpaka atakapoondolewa.
2 Wathesalonike 2:6-7
[6]Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
[7]Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
Na huyo si mwingine zaidi ya Roho Mtakatifu. Lakini kumbuka Sio kwamba ataondolewa lakini mifumo yake inayozuia utendaji kazi wa mpinga-Kristo itafikia mwisho..Kwamfano kanisa kunyakuliwa, na mifumo ya kiutawala iliyoruhusiwa na Mungu maalumu kudhibiti kazi zake, kuachwa kutumiwa na Mungu, na malaika wanaohuduma duniani kwa ajili ya usalama wa watakatifu, kuondolewa..
Vitu kama hivi vitakapoondolewa basi mpinga-Kristo atapata uhuru wote kutendakazi kwa jinsi apendavyo.
Paulo anawasisitiza watakatifu juu ya kuiombea huduma, ili injili ya Kristo itukuzwe, lakini pia aweze kuepushwa na watu wabaya.
Pamoja na hilo anatoa tahadhari kuhusu uvivu, akiwasisitiza wafanye kazi kwa mikono yao, pengine kwasababu ya ufahamu usio sahihi waliokuwa nao hapo mwanzo, kwamba mwisho tayari umekwisha fika.
Pia anawatia moyo watakatifu wasikate tamaa katika kutenda mema. Huku akiwahiza wadumu katika mapokeo yao tu waliyowaachia, na si mengineyo.
mwisho anamaliza na salamu pamoja na baraka kwa kanisa.
Kwa ufupi tuusomapo waraka huu Bwana anataka tuendelee kuthibiti katika imani,.haijalishi ni dhiki za namna gani tutazipitia.
Lakini pia tuwe na ufahamu sahihi juu ya siku za mwisho. Kwasababu tatizo hili lipo hata sasa, baadhi ya watu wakiamini kuwa siku ya Bwana imeshakuja. Lakini kama tulivyojuzwa hapo, haiwezi fika kabla, mpinga-Kristo kudhihirishwa na hilo litakuwa wazi kabisa duniani kote.
Na mwisho ni wajibu wetu kuombea huduma, na wanaojitaabisha kuhubiri injili ili walindwe na watu wabaya. Je unamwombea mchungaji wako?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa kwanza.
Rudi Nyumbani
Maandiko yanasema Makwazo hayana budi kuja (Luka 17:1)
Unapofanyiwa jambo baya na Mtu wako wa karibu au wa Mbali, huwa ni ngumu kusahau…
Kama umeshaokoka na ni mtu uliye mwepesi kusamehe na kusahau, basi Bwana amekutengeneza kwelikweli na umetengenezekeka, Lakini kama ndani yako kuna UGUMU wa kusamehe, fahamu kuwa hilo ni tatizo ambalo unapaswa ulitafutie ufumbuzi haraka sana, mwanzoni mwa mwaka.
Umeumizwa na Ndugu, umeumizwa na Mpendwa mwenzako, umeumizwa na Rafiki, umeumizwa na Mke, Umeumizwa na Mume, umeumizwa na watoto, mchungaji, mshirika wako, mkufunzuki wako au mtu mwingine yeyote, leo itoe hiyo sumu..
Fanya jambo hili moja ili ushinde hali hiyo ya kutokusamehe na hatimaye uachilie msamaha.
UTAFAKARI MSAMAHA WA YESU.
Tafakari ni mambo mangapi mabaya uliyoyafanya au unayoyafanya kwa MUNGU, unaweza ukawa hujawahi kumfanyia mtu ubaya, lakini vipi MUNGU?.. Je hujawahi kumfanyia ubaya kabisa?..huna dhambi kabisa??, huna kasoro kabisa??.. Hilo ni jambo lisilowezekana. (2Nyakati 6:36)
Tafakari tu mawazo yako kwa siku yanavyo vuka na kuwa machafu, na MUNGU anakutazama tu!, tafakari ni vipindi vingapi umewaka hasira moyoni na Mungu anakutazama tu, tafakari ni mangapi amekusamehe, na ni mangapi unayohitaji ukusamehe.
Hayo yote uliyoyafanya na unayoyafanya Mungu anayatazama tu, na yupo tayari kukusamehe, au huenda ameshakusamehe, sasa kama wewe umesamehewa mengi hivyo bure kabisa, vipi na wewe kwanini usimsamehe yule aliyekokosea mwaka jana, au mwezi jana, au siku ya jana??.
Wakati mwingine si lazima yeye akuombe msamaha, Wewe samehe tu hata kama hajaja kukuomba msamaha, maana hata BWANA aliwasamehe wale wasiomwomba msamaha..
Luka 23:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.
35 Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake.”
Wengine watakukosea na daima wataendelea kujiona wapo sawa, na wengine wataendelea kukukosea tu!.. Lakini kanuni ni ile ile KUSAMEHE..
Hivyo kwa kuutafakari mambo ya maisha yako, na kasoro zako mbele za MUNGU, Huwezi kukosa sababu za wewe kutosamehe.
Kwa kumalizia hebu tafakari kwa undani maandiko yafuatayo…
Mathayo 18:21 “Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?
22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.
24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.
25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.
26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.
27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.
28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.
29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.
30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.
31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka”.
Kumbe tusipokuwa na TAFAKARI ya kutosha kwa msamaha BWANA aliotupa, yaweza kuwa sababu ya sisi pia kutosamehewa!. Lakini kama tukifakari kwamba na sisi tumeshafanya mengi mabaya, ambayo hayakustahili msamaha basi na sisi pia tutasamehe.
Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.
21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.
22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.
Mwombe Bwana katika mwanzo wa mwaka huu akuumbie “Moyo wa kusamehe”.. Ni yeye ndiye anayetoa huo moyo, ikiwa tutamwomba, kwa kumaanisha kabisa, Hivyo jifungie chumbani kwako, au tafuta sehemu yoyote yenye utulivu na mwambie Bwana.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TAFAKARI SANA KABLA YA KUAMUA HATIMA YAKO.
Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.
Kitabu hichi kama kinavyojitambulisha katika mwanzo wake ‘Waraka wa kwanza wa Paulo mtume kwa Wathesalonike’.
Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu. Aliuandika akiwa Korintho. Tumelijua hilo kufuatana na ujio wa Timotheo kutoka Makedonia na kumpa ripoti nzuri ya maendeleo yao ya kiroho, kuanzia eneo la imani, upendo na tumaini, ambazo tunazisoma katika kitabu cha Matendo ya mitume sura ya 18.
Kwasababu ya ugumu wa kuwafikia uliochangiwa na shetani, Akasukumwa kuandika nyaraka hizi mbili kwa watakatifu hawa, kuwajenga katika maeneo kadha wa kadha, ambazo zilipishana kwa miezi kadhaa tu.
Kitabu hichi kina sura tano (5)
Maudhui kuu ya waraka huu ni matatu(3)
Tuyaangalie hayo maeneo matatu kwa ufupisho;
Paulo anaanza kwa kuwashuhudia kwa maneno mengi dhiki alizozipata katika kuieneza injili kwao, na jinsi alivyoweza kustahimili, Na kwamba wao pia wanapopitia dhiki za namna mbalimbali kutoka kwa watu wa taifa lao, wasivunjike moyo na kuiacha imani. Wajue kuwa dhiki pia wamewekewa watakatifu.
1 Wathesalonike 2:14
[14]Maana ninyi, ndugu, mlikuwa wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyo katika Uyahudi, katika Kristo Yesu; kwa kuwa mlipata mateso yale yale kwa watu wa taifa lenu wenyewe, waliyoyapata na hao kwa Wayahudi;
[15]ambao walimwua Bwana Yesu, na hao manabii, na kutuudhi sisi; wala hawampendezi Mungu, wala hawapatani na watu wo wote;
1 Wathesalonike 3:3
[3]mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.
Paulo anagusia maeneo mengi kuanzia upendo hadi utakatifu kwamba wana wajibu wa kuongezeka katika hivyo ili wasionekane katika lawama katika siku ile ya kuja Bwana wetu Yesu Kristo kutoka mbinguni.
1 Wathesalonike 3:12-13
[12]Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;
[13]apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.
> Anagusia pia katika eneo la kudhibiti miili yetu katika utakatifu na heshima na sio katika tamaa mbaya(4:1-5),
> Halikadhalika wakristo kuonyesha mwenendo wa adabu kwa walio nje, kwa kutenda shughuli zetu wenyewe ili tusiwe na uhitaji wa vitu vyao (4:11-12)
> Pia kama watakatifu ni mwiko kulipana baya kwa baya (5:15),
> Tunapaswa sikuzote tudumu katika kuomba, kufurahi, kushukuru kwa kila jambo, tusimzimishe Roho, tusipuuzie unabii, tujitenge na ubaya wa kila namna.(5:16-23)
> Lakini Paulo anahimiza mwenendo wetu unapaswa uende mpaka kwa wale wanaotusimamia na kutuchunga kwamba tuwastahi.
1 Wathesalonike 5:12-13
[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni;
[13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.
> Na katika yote ni wajibu wetu sote kufarijiana na kuonyana na kuvumiliana na kutiana nguvu(5:14-15)
Paulo anawafiriji kwa kuwaambia wafu waliolala katika Kristo, siku ya mwisho wataamshwa wote..wasidhani kuwa hawatawaona wapendwa wao waliotangulia.
1 Wathesalonike 4:13-16
[13]Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
[14]Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.
[15]Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
Sambamba na hilo, anawafumbua macho juu ya nyakati na majira ya kurudi kwa Yesu kwamba hakutakuwa na taarifa zozote au viashiria vyovyote kwa watu wa dunia. Bali itawajilia kwa ghafla tena katika nyakati ambazo wanasema kuna amani na shwari.
Hivyo anawatahadharisha watakatifu nao kuwa macho wakati wote.
1 Wathesalonike 5:1-11
[1]Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
[2]Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
[3]Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
[4]Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.
[5]Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.
[6]Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
[7]Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.
[8]Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.
[9]Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo;
[10]ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala.
[11]Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.
Hivyo kwa ufupi ni kuwa waraka huu. Unawataka wakristo kuthibitika katika imani, haijalishi ni changamoto gani za kimaisha au ugumu gani watakutana nao kwa wapinga-kristo, Wanapaswa waendelee kusimama hivyo hivyo mpaka mwisho katika Kristo Yesu.
Lakini pia wajue Bwana anarudi, na atakuja ghafla, Hivyo yawapasa wawe watu wa mchana sikuzote wasilale usingizi kwa kuhakikisha wanaishi maisha ya utakatifu, na adabu, ili atakaporudi Bwana wasiwe na lawama yoyote.
Bwana akubariki.
Je! Umeokoka? Kama ni la, fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya wokovu. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha wafilipi
Kama pale mwanzo kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo mtume kwa wafilipi”.
Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hiki. Ni moja ya nyaraka ambazo Paulo aliziandika akiwa kama mfungwa, aidha kule Rumi.
Maudhui makuu ya waraka huu mfupi wenye sura nne(4) yalikuwa ni kuwatia moyo watakatifu na kuwahimiza waiendeleze furaha ya Mungu ndani yao,bila kukwamishwa na dhiki za aina yoyote, lakini pia sehemu ya pili ni kuwataka wapige hatua katika mwenendo wao ndani ya injili waliyoipokea.
Tukianza na hiyo sehemu ya kwanza:
Paulo anahimiza watakatifu kufurahi katika dhiki zote, ikizingatiwa kuwa Kanisa hili lilishuhudia vifungo na mapigo mengi ya Paulo. Kama tunavyosoma kwenye Matendo 16:16-40, Kule ambapo Paulo na Sila walipigwa sana na kutupwa gerezani, biblia inatuambia kulikuwa ni huku Filipi. Lakini hata katika waraka huu bado anashuhudia kuwa dhiki zake, zimekuwa wazi kwa maaskari, na watu wote wa huko (1:12-13).
Hivyo Paulo alijua watu wa Filipi huwenda wakawa na huzuni nyingi juu yake, au juu ya injili, kutokana na dhiki nyingi walizoziona kupitia yeye.
Lakini hapa anawaeleza kuwa yeye anafuraha sikuzote katika Kristo.
> Anaendelea kueleza furaha yake haiathiriwi na watu wanaomzushia fitna ili apitie mateso, maadamu anayeathirika ni yeye si Kristo. Basi bado anafurahi..(1:17-18)
> Anasema hata akihukumiwa kifo kwa ajili ya watakatifu, bado furaha yake itazidi zaidi wala haiwezi kuathiriwa..
Wafilipi 2:17-18
[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.
[18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
Hivyo anawahimiza pia na wafilipi wafurahi kama yeye, wala wasione huzuni kwasababu ya dhiki hizi, kwasababu tumewekewa kuwa sehemu yetu katika ushuhuda wa injili.
Wafilipi 1:29
[29]Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Hizi ni sehemu nyingine kadha wa kadha Paulo akihimiza jambo hilo hilo,
Wafilipi 3:1
[1]Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana.
Wafilipi 4:4
[4]Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
Sehemu ya Pili:
Katika sehemu ya pili Paulo anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaipasa injili waliyopokea. Na hiyo ni ili wasiwe na ila na lawama,na udanganyifu. Kuonyesha kuwa injili, inayo na taratibu zake..Sio kuamini tu na kusema nimeokoka…bali pia kutii agizo lake.
Wafilipi 1:27
[27]Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, ili, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;
Anaendelea kusema watakatifu wana wajibu wa kunia mamoja, kutenda mambo yote bila majivuno,wala manung’uniko, wala mashindano, wanapaswa kutenda yote bila ubinafsi bali na ya wengine..
Anasisitiza watakatifu wanapaswa wawe wanyenyekevu, wenye nia ya Kristo..ambaye yeye hapo mwanzo alikuwa kama Mungu lakini alijishusha kwa kukubali kuachia nafasi yake, akawa kama mtumwa, akajinyenyekeza mpaka mauti ya msalaba,lakini Mungu akamkweza zaidi ya vitu vyote..Na sisi tulioipokea injili tunapaswa tuwe na nia hiyo hiyo ya unyenyekevu.(2:1-16)
Anasisitiza zaidi Wakristo wanapaswa wawe wapole, pia wawe waombaji na wenye shukrani.(4:5)
Halikadhalika ni wajibu wetu sote kuutumiza wokovu tulioupokea kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu ndiye Mungu atendaye kazi ndani yetu.(2:12-13)
Pamoja na hayo Watakatifu wana wajibu pia wa kuyahakiki mambo yote yaliyo mazuri na kuyaiga, (2:1-2)
Wafilipi 4:8
[8]Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
Lakini pia anawatahadharisha kujiepusha na wahubiri wa uongo akianzana na wayahudi (watu wa tohara), ambao wanahubiri wokovu kwa njia ya torati zaidi ya ile tuipatayo ndani ya Kristo Yesu kwa njia ya imani. (3:1–16,)
Pamoja watumishi ambao fundisho lao ni la mambo ya duniani tu, na sio yale ya kumwelekeza mtu mbinguni (3:17-21).
Mwisho, Paulo anatoa salamu zake, na shukrani kwa huduma ya utoaji kanisa hilo lililomfanyia, na linaloendelea kumfanyia.
Hivyo kwa hitimisho, waraka huu maudhui kuu ni kuwafariji watakatifu wafurahi katika mambo yote, tukizingatia tunda la Roho ni furaha. Yesu alisema tufurahi na kushangalia pale tunapoudhiwa, kwa ajili ya jina lake. Hivyo, hakuna eneo lolote furaha ya Mungu ndani yetu ,inastahili kukatishwa. Tupitiapo magonjwa kama Epafrodito(2:25-30), shida, njaa, tumefundishwa kuyaweza yote ndani ya Kristo(4:12-3). Hivyo furaha yetu haiwezi kuathiriwa..Ilinde furaha yako.
Lakini anahimiza mwenendo upasao injili. Kwamba huo utaweza kufanikiwa pale tunapokubali kuwa na nia kama ile ya Kristo, ya unyenyekevu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.
Kama kitabu kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo Mtume kwa Waefeso”. Paulo ndiye aliyeuandika waraka huu.
Aliuandika akiwa kama mfungwa kule Rumi.
Waraka huu una sura sita(6), ambazo tunaweza kuzigawanya katika makundi mama mawili.
1) kundi la kwanza ni Sura ya 1-3,
Sura hizi zinaeleza asili ya Imani yetu iliyo katika Kristo Yesu jinsi ilivyo ya kipekee kwa nguvu na mamlaka, na ubora, na uweza na ukuu, na utajiri, na utukufu usiopimika, kwa akili za kibinadamu.(1:20-23).
2) Lakini kundi la pili ni Sura 4-6
Inaeleza juu ya mwenendo wetu, jinsi unavyopaswa uwe katika imani tuliyoipokea. Kwasababu ni vitu vinavyokwenda sambamba, haviwezi kutenganishwa, katika fundisho la ukristo.
Kwa ufupi; Katika Kundi la kwanza Yafuatayo ni mambo mama ambayo mwandishi ameyazungumzia juu ya mambo tunayoyapata ndani ya mwokozi wetu Yesu Kristo.
Haya ni mambo ya muhimu sana, ambayo tunapaswa tuyafahamu juu ya Kristo tuliyempokea ndani yetu. Kulingana na mwandishi tukiyajua hayo itatufanya tusiwe watoto wachanga, wa kuchukuliwa na kila upepo wa elimu ya uongo, kwa hila za watu, na ujanja, na njia za udanganyifu (4:14).
Lakini katika kundi la pili ambalo ni sura ya 4-6;
Tunaelezwa wajibu wetu kimwenendo, baada ya kumwamini Kristo, jinsi unavyopaswa uwe, kwamba hatupaswi kuenenda kama mataifa waenendavyo, bali kinyume chake tukue mpaka kuufikia utimilifu wake.
Ambayo hiyo huja Kwa njia ya kuhudumiana kwa karama mbalimbali sisi kwa sisi katika kifungo cha umoja, kama kanisa la Kristo. (4:16)
Anaeleza pia yampasa kila mmoja binafsi auvue ule utu wa kale wa dhambi, na kuuvaa mpya mpya wa utakatifu na haki (4:20-24),
kwa kuuvua uongo, pia tusiruhusu hasira zitutawale, tusiwe wezi, vinywa vyetu visitoe maneno mabaya na matusi, tuwe wafadhili sisi kwa sisi, tusimzimishe Roho, upendo wetu udumu, uasherati usitajwe, wala aibu, wala ubishi.
Kwasababu watendao kama haya kulingana na Mungu hawana urithi katika ufalme wa Mungu.
Waefeso 5:5
[5]Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.
Halikadhalika Mwandishi anatoa pia agizo juu ya matendo ya giza kwamba tuyaonapo tuyakemee, vilevile tujiepushe walevi, bali tujazwe Roho wakati wote, kwa kumfanyia Mungu ibada.
Waefeso 5:18-20
[18]Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;
[19]mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;
[20]na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
Mwandishi anazidi kugusia mienendo yetu mpaka katika ngazi za kifamilia na kikazi.
kwamba wake wanapaswa wawatii waume zao, vilevile waume wawapende wake zao. Watoto wawaheshimu wazazi wao, na wazazi wasiwachokoze watoto wao, Watumwa wawatii bwana zao, na mabwana wasiwatishe watumwa wao.(5:22-6:9)
Anagusia pia eneo la vita vyetu. Kwamba rohoni tupo vitani dhidi ya adui yetu shetani na mapepo yake, yenye kazi ya kuwapofusha watu macho, lakini pia kurusha mishale ya moto kutuangamiza. Hivyo tunapashwa tuvae silaha zote za Mungu, ili tuweze kusimama. (6:10-20). Anaorodhesha silaha hizo. ambazo zinakamilishwa kwa sala na maombi ya daima.
Na mwisho anatoa salamu zake kwa watakatifu, akiwaambia pia habari zake nyingine watakazisikia kwa Tikiko, aliyempeleka kwao.
Kwa ufupisho.
Kitabu hichi kinatupa ufahamu kuhusu ubora wa imani tuliyoipokea lakini pia wajibu wetu baada ya hapo, kwasababu tusipothamini na kulegea adui yetu shetani na majeshi yake yatashambulia imani yetu na hatimaye, tukayakosa tuliyohakikishiwa.
Ukishaamini tembea katika utakatifu. Ukiwa unapiga hatua kila siku kwenda mbali na dhambi, basi fahamu kuwa ukombozi wako ni hakika. Kwasababu msalaba una nguvu ya kukusaidia madhaifu yako.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)
Rudi Nyumbani