Category Archive Wahubiri (Watumishi)

KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?

Kutokuihubiri injili, madhara yake ni yapi?


Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..Karibu tujifunze Biblia mtu wa Mungu…Leo tutajifunza mambo machache muhimu yahusuyo majukumu yetu ya kuihubiri Injili.

Injili maana yake ni “Habari njema”..Habari yoyote au ujumbe wowote unaoupeleka kwa mtu au watu ulio mwema huo tayari ni injili…Zipo Injili za aina nyingi duniani lakini ipo injili moja tu ya wokovu..Au kwa lugha nyingine inaitwa “Injili ya Msalaba”…Injili ya Msalaba inamhusu Yesu Kristo mwana wa Mungu aliyetumwa kuichukua dhambi ya ulimwengu..Hiyo inahusu wokovu wa mwanadamu ambaye alipotea dhambi. Na Kumbuka wanadamu wote walipotea dhambini hivyo injili hii inamuhusu kila mmoja wetu.

Sasa Baada ya Bwana Yesu kuondoka ilikuwa ni sharti injili ihubiriwe ulimwenguni kote kwa kila kiumbe, na kwamba kila mwanadamu lazima aisikie injili hiyo ya wokovu…Na kwa hiari yake mwenyewe achague UZIMA au MAUTI. Kwasababu hiyo basi akawaagiza mitume wake akawaambia..

Marko 13.9-10

Marko 13.9 “Nanyi jihadharini nafsi zenu; maana watawapeleka ninyi mabarazani; na katika masinagogi mtapigwa; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao.

10 NA SHARTI INJILI IHUBIRIWE KWANZA KATIKA MATAIFA YOTE”.

Hapo anasema ni SHARTI!..Maana yake ni lazima injili ifike kila mahali..Kwa uzima na kifo, hata ikigharimu uhai ni lazima injili iwafikie watu..Hivyo hilo ni jukumu tulilopewa watu wote tuliompokea Kristo..Ni lazima tuihubiri Injili…Na siku zote Mungu anatumia watu kuhubiri Injili, kawachagua watu kusimama madhabahuni kumwakilisha…kamwe hatumii wanyama, wala malaika, wala kiumbe kingine chochote kamchagua mwanadamu tu!!..

Sasa kuna hatari kubwa sana ya kutokuihubiri injili…Kuna hatari kubwa sana ya kutokuitumia karama Mungu aliyokupa katika kuwahubiria wengine..Bwana amekuokoa wewe, ili na wewe ukawe msaada kwa wengine…hajatuokoa ili tu tufurahi sisi wenyewe..Kama tunavyojua wengi wetu hatujampokea Yesu kwa kutokewa na yeye…wengi wetu tumesikia injili ikihubiriwa mahali fulani na mtu Fulani wa Mungu ndipo kwa kupitia hayo mahubiri tukaokoka… Kutokuihubiri injili ni kosa kwa mtu anayeitwa mkristo.

Injili ni kuambukiza:

Kadhalika huo ndio utaratibu wa Mungu, Ni lazima tuisikie kutoka kwa mtu fulani wa Mungu…na hivyo na sisi pia lazima tuwahubirie wengine ambao nao watasikia kutoka kwetu, ni kama mnyororo huyu anamzaa huyu katika imani, huyo anamzaa Yule na kuendelea..

Sasa kama umeokolewa na hutaki kuzaa wengine…kuna hatari kubwa sana…Tukirudi kwenye biblia tunamsoma Nabii mmoja aliyeitwa EZEKIELI..Huyu alikuwa ni nabii wa Mungu wa kweli kabisa., ambaye alikuwa miongoni mwa watu wachache waliochukuliwa kwenda Babeli…wakati yupo huko Mungu mwenyewe alimtokea akamwonyesha maono akiwa ameketi katika kiti chake cha Enzi huku maserafi na makerubi wakiwa wamemzunguka pande zote..akasikia sauti ya Mungu mwenyewe..Na Mungu akamtuma aende kuwaambia wana wa Israeli maovu yao na maasi yao na mambo yatakayokuja kuwatokea huko mbeleni wasipotubu.

Lakini yeye alipotoka pale baada ya kuona maono hayo…akaenda kukaa kimya, hakuwaambia watu chochote… sio kwamba alikuwa na dharau hapana! Hakumdharau Mungu…lakini alikuwa anaogopa kuwaambia(Alikuwa na hofu)….alikuwa na uchungu kweli na hasira moyoni, kwa maovu yaliyokuwa yanafanyika katikati ya watu wake lakini alikuwa anajifikiria fikiria namna ya kuwaambia..…akakaa siku saba hawaambii hao watu maono aliyoonyeshwa na Mungu…Baada ya siku saba maono yakamjia tena na kumwonya kwa anachokifanya cha kutowaambia watu maneno ya Mungu..Mungu akamwonya vikali kwa tabia hiyo..

Tusome..

Ezekieli 3:15 “Ndipo nikawafikia watu waliohamishwa, huko Tel-abibu, waliokuwa wakikaa karibu na mto Kebari, nikafika huko walikokuwa wakikaa; nikaketi huko miongoni mwao muda wa siku saba, katika hali ya ushangao mwingi.

16 Hata ikawa, mwisho wa siku saba, neno la Bwana likanijia, kusema,

17 Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.

18 Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.

19 Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako”.

Umeona?..Ezekieli baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa Bwana kwamba “damu ya mtu itakuwa juu yake endapo hatamwambia maneno aliyoambiwa amwambie”..Ndipo akaelewa hakuna suala la mizaha tena kwenye kupeleka ujumbe wa Mungu kwa watu…Tangu wakati huo chochote alichoonyeshwa aliwafikishia wahusika kama kilivyo…Kwasababu alijua atadaiwa damu!. Hakuishi maisha ya kutokuihubiri injili tena.

Ndugu..Kama Bwana anakuonyesha maono ya kuwaonya watu juu ya dhambi zao na wewe huwaambii jifunze kwa Ezekieli hapo juu, kama unafahamu Neno na uwaambii wengine kuna hatari…Ni afadhali uwaambie wakatae kwa mapenzi yao wenyewe wewe utakuwa umenawa mikono..kuliko kutowaambia kabisa…mtu huyo akitoka na kwa bahati mbaya akagongwa na gari na kufa, unadhani wewe utakuwa katika hali gani?.

Kama umefahamu kuwa wazinzi na waasherati watakwenda kuzimu wasipotubu, na wewe mwenyewe sio mwasherati kwanini usiwaambie?…Mwambie ili aokoke, suala la kumbadilisha sio juu yako…wewe kazi yako ni kuhubiri tu injili…Lakini pia kama na wewe binafsi unafanya mambo hayo hayo wanayowafanya hao basi hapo usiwahubirie kwasababu wewe mwenyewe unahitaji wokovu..Na kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzake..biblia inasema hivyo.

Anza kuchukua hatua:

Hivyo kama ulikuwa uhubiri..anza leo!..Kama ulikuwa unaogopa kuwaambia watu juu ya habari ya siku za mwisho anza kuwaambia..Ezekieli aliogopa kuliko wewe lakini aliposikia suala la damu ya hao watu itatakwa juu yake, aligueka mara moja na wewe hivyo hivyo geuka leo..Na Bwana atakusaidia. Ipo hatari kubwa sana ya kutokuihubiri injili

Na kama hujaokoka kabisa..Tubu leo, mlango wa Neema bado upo wazi.. ila hautakuwa hivi siku zote..Umesoma hapo juu kitu gani kitamtokea mtu Yule atakayekufa katika dhambi zake huku ameonywa na amekataa…

Tusome tena…

Eze.3:19 “Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye , wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako”.

Na wewe leo umesikia injili usipotaka kutubu utakufa katika dhambi zako na madhara ya kufa na dhambi ni ziwa la moto.

kwahiyo pale ulipo mwombe Bwana msamaha, tubia uasherati wako kama ni mwasherati, ulevi wako,uongo wako, rushwa zako, usengenyaji wako,wizi wako, matusi yako… kisha katafute Ubatizo sahihi kama hujabatizwa na Roho Mtakatifu atakutakasa na kukufanya kuwa mkamilifu kama yeye alivyo mkamilifu…

Marko 1:15 “akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili”.

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Shalom.

Mada Nyinginezo:

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

 

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

UPAKO NI NINI?

Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

Rudi Nyumbani:

Print this post

HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.

Shalom! Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima!

Karibu tujifunze Biblia, kwa Neema Bwana aliyotupa.

Biblia inasema katika Wagalatia 1:7b

“…. lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.

8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe.

9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe”.

Maneno hayo aliyazungumza Mtume Paulo kwa Uweza wa Roho, na Roho Mtakatifu mwenyewe akayatia Muhuri yafae kwaajili ya kutuonya na kututahadharisha sisi watu wa vizazi vyote. Ni maneno ambayo huwezi kuamini kama yapo kwenye Biblia Takatifu hususani katika agano jipya, lakini yapo!

Kuna hatari kubwa sana ya kuigeuza Injili ya Yesu Kristo kwa makusudi..ili tu mtu upendwe, au upate wafuasi wengi, au ujulikane…Kufundisha Injili nyingine tofauti na hiyo iliyohubiriwa na Mitume ndio “kuongeza Neno la Mungu” kunakozungumziwa katika biblia….ambapo Biblia imesema mtu wa namna hiyo ataongezewa mapigo katika siku ile.

Ufunuo 22: 18 “Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki”.

Biblia inaposema wazi kuwa waasherati na waabudu sanamu pamoja na walevi watakwenda kwenye ziwa la moto, na wewe unasema “si kweli acha kuhukumu”..unaposema biblia imeruhusu pombe!! hapo ni sawa na unahubiri Injili nyingine tofauti na ile Iliyohubiriwa na hivyo “Umelaaniwa”

1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”

Biblia inaposema wazi katika Agano jipya kwamba Wanawake wavae mavazi ya kujisitiri, si kwa kusuka nywele!..

1Timotheo 2: 9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”.

Wewe unasema “Mungu haangalii mavazi anaangalia roho” sentensi ambayo haipo kwenye Biblia nzima…uliisikia kutoka kwa mtu fulani asiyefahamu maandiko nawe ukai-copy bila kuchunguza imetoka wapi!…..fahamu kuwa unahubiri Injili nyingine ambayo haipo kwenye Biblia…Na hakuna mtu yoyote anakuhukumu hapo..bali biblia yenyewe ndio inayokuhukumu kwamba UMELAANIWA!

Biblia inaposema katika Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”. Wewe unasema kuwa ubatizo haujalishi sana! Si lazima ubatizwe, Hapo unahubiri Injili ya Laana!

Pengine ulikuwa hujui kwamba hizo injili ni za laana! Na ulikuwa unazihubiri, Lakini leo umejua..Tubu mlipize shetani kwa uongo aliokudanganya kwa muda mrefu! Tubu nenda kachome vimini vyote ulivyokuwa unavaa,(na nguo zote zinazochora maungo yako) na kamwe usihubiri Injili hiyo uliyokuwa unaihubiri ya Laana kwamba Mungu haangalii mavazi…Ulikuwa unasuka nywele!, kafumue ziweke katika hali yake ya asilia Mungu alizokuumbia, ulikuwa unavaa mawigi, na kupaka lipstick pamoja na mapambopambo ya kidunia..jirudishe katika hali yako ya asili..Umesoma haya kwa macho yako! Hutasema siku ile hujaambiwa, wala hukusikia, au haujafafanuliwa vizuri!..

Ukikubali maonyo na kugeuka ni vizuri! Utakuwa umeisalimisha roho yako, lakini ukikataa pia ni vizuri, kwasababu Injili sio kitu cha kulazimishwa……isipokuwa hakikisha kama unajipamba jipambe kikweli kweli, Kama unavaa vimini tafuta vile vikali kabisa, kama unasuka, suka mitindo yote na ya kila namna…unapaka poda, uwanja, weka mwingi wa kutosha unavaa wigi tafuta za kila mtindo….usiwe nusu nusu, ili siku ile katika ziwa la moto usije ukajuta kwanini hukujipamba sana, utakapoona ulijipamba kidogo tu na bado umetupwa katika ziwa la moto!…usije ukajuta kwanini ulikuwa una nguo moja tu! Kimini ambacho ulikuwa unakivaa mara moja tu kwa mwezi katika tukio maalumu…na nguo nyingine ndefu za kujisitiri ulikuwa unazivaa kila siku na bado umetupwa kwenye ziwa la Moto!

Kama umechagua kwenda kuzimu usikubali kinguo kimoja tu kikupeleke kule! Tafuta madebe ya vimini na suruali zile zinazobana kabisa, pamoja na maboksi ya lipstick yatumie… kwasababu Bwana Yesu alisema mwenyewe katika Ufunuo.

Ufunuo 22:10 “ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho”.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Maran atha!

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NGUVU YA UPOTEVU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU.

LAANA YA YERIKO.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA.

INJILI YA MILELE.

JE! KUBET NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia inasema askofu anapaswa awe mume wa mke mmoja! Je! Wale wasiooa kwa ajili ya injili hawawezi kuwa maaskofu?

1 Timotheo 3:1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja,..” 


JIBU: swali zuri, na pia wengi wanachanganyikiwa kuhusu hilo, wakidhani kuwa mtu yeyote anayeitwa askofu ni lazima aoe…lakini unapaswa uelewe kuwa hapo Mtume Paulo alisema hivyo kwa mantiki ipi?, hakuwalenga wale ambao hawajaoa bado hapana, bali aliwalenga wale ambao wanao wake zaidi ya mmoja..kwamba hao ndio hawapaswi kuwa maaskofu, kwasababu ni lazima waonyeshe kielelezo kwanza wao wenyewe katika nyumba zao na ndio waje kuchunga wa nje, sasa kama mtu alikuwa na wake 6 kabla hajaamini na akaingia kwenye ukristo na ukristo unasema mtu anapaswa awe na mke mmoja, sasa unadhani wale atakaowachunga yeye kama askofu atakuwa anacho kielelezo gani? 

Na ndio maana haipaswi mtu yeyote anayeitwa askofu au mchungaji awe na mke zaidi ya mmoja…Lakini haikumaanisha pale kwamba ni lazima kila anayetaka kuwa askofu awe na mke, huo ni uelewa hafifu wa maandiko. Kumbuka mtume Paulo naye hakuwa na mke, lakini alikuwa mwangalizi wa makanisa yote, Kristo naye hakuwa na mke lakini yeye ndiye Askofu wa maaskofu. Hivyo hapo maneno hayo yaliwalenga wale ambao tayari wanao mke zaidi ya mmoja. 

1Wakoritho 7:32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.

34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe

Ubarikiwe.

Maran atha


Mada zinazoendana:

MATOWASHI NI WAKINA NANI?

JE! NI VIBAYA KUTAJA HUDUMA KWA KUJIPA CHEO? MFANO MIGHTY PROPHET, CHIEF APOSTLE N.K.?

NITAMJUAJE NABII WA UONGO?

MLINZI, NI HABARI GANI ZA USIKU?

BIDII YA MFALME YOSIA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KAMA MHUBIRI NI WOKOVU UPI UNAUPELEKA KWA WATU?

Mithali 20:14 “Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi; Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.”

Ni wazi kabisa kwa jinsi tunavyozidi kuwa hapa duniani kuna mambo ambayo hayakwepeki, mfano kama hatutakuwa wauzaji, basi tutakuwa wanunuzi wa vitu fulani, Mungu karuhusu iwe hivyo ili kutufundisha sisi kwa nadharia mambo yanayoendelea rohoni, na kama tunavyofahamu siku zote ile lugha ya biashara, muuzaji atataka kupandisha thamani ya ile bidhaa yake juu kidogo kwa kiwango ambacho si chake, ili kusudi kwamba ikitokea mnunuzi ataitaka bidhaa ile kwa gharama ya chini kidogo, basi asimpoteze mteja wake atampunguzia mpaka kwenye kiwango cha thamani halisi aliyokusudia kuiuza hapo mwanzo, Na hivyo yule mteja atakapoona amepunguziwa bei basi hiyo itamfanya aridhike na kununua bidhaa ile, pasipo kujua kuwa kile alichokitoa ndio thamani halisi ya bidhaa ile.

Hali kadhalika na mnunuzi naye, anataka kwenda kwa muuzaji tayari kichwani ameshajipanga kuwa atakapofika kwa muuzaji ni lazima ashushe kidogo thamani ya kile kitu, hata kama anajua thamani yake inaweza ikawa ni ile ile iliyowekwa na muuzaji, lakini ni lazima afanye hivyo, hiyo ni ili tu aipate ile bidhaa kwa bei ya unafuu kidogo, na mwisho wa siku anaipata, hivyo hayo ni mambo ya kawaida kabisa na yapo siku zote masokoni…Ili biashara ifanyike ni lazima kuwe na mapambano ya bei.

 

Vile vile na Sisi (mimi na wewe) kama wahubiri tunafanya biashara, na biashara tunayoifanya ni ya kuuza Wokovu kwa watu wenye dhambi, ili tumpatie Kristo faida za watu, ikiwa tutauweka sokoni wokovu wetu katika thamani ya chini, basi tujue kuwa wale watakaovutiwa na kuja kuununua watautaka kuunua kwa thamani ya chini zaidi ya hiyo unayouza, haiwezekani waupokee kwa mara ya kwanza kwa gharama zile zile unazozitaka wewe, kwa viwango vile vile unavyovitaka wewe,..ni hatua kwa hatua..

Sasa injili zetu na mafundisho yetu, yakiwa ni manyonge, mtu unamvuta kwa Kristo leo, halafu unamwambia kuvaa suruali ni sawa, kuweka makucha ya bandia mfano wa mnyama kenge ni sawa, kuimba miziki ya kidunia ni sawa wala hakuna shida yoyote, hatukemei dhambi, hatumuhubirii mtu utakatifu, ambao pasipo huo tunajua kabisa hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao biblia inasema hivyo katika (Waebrania 12:14) muda wote sisi tunamfundisha mafundisho ya jinsi ya kufanikiwa hapa duniani, huku tunapuuzia mafanikio ya Roho yake ambayo ni kwa kumjua Kristo na wokovu wake kamili..anachokifamu tu tangu siku ile tumemvuta kwa Kristo ni “pokea kwa jina la YESU”, Anafahamu tu shuhuda za kichawi zaidi kuliko shuhuda za Yesu, hajui hata baada ya kifo ni nini kinafuata, hajui unyakuo ni kitu gani, hajua maandiko, yeye tunachomuhubiria tu ni kwamba “watapigana nawe lakini hawatashinda”…..

Ni kweli kabisa hapo tumefanikiwa kuwavuta, ni sawa na tunawaudhia bidhaa zetu za wokovu tulizopewa na Kristo, lakini tunategemea vipi watu kama hao wataununua kwa gharama ile ile unayoitazamia wewe, kwamba wawe watakatifu kama wewe au kuliko wewe, hilo haliwezekani kinyume chake wataupokea wokovu wako kwa thamani ya chini kidogo, na ndio hapo utakuta japo ulimleta mtu kwa Kristo lakini maisha yake yapo mbali na Kristo, utasikia ni mzinzi, ni mlevi, utasema mbona nilimhubiria mimi akaokoka?..Ndio ulimhubiria lakini ulimpa viwango hafifu vya wokovu, na hivyo kama ilivyo desturi ya mnunuzi si jambo la kushangaza kuinunua bidhaa yako kwa kiwango cha chini kidogo, na matokeo yake ndio akawa kama alivyo, mtukanaji, mzinzi, mvaaji vimini barabarani, msengenyaji, anajulikana mtaani kwa utapeli, n.k…

Ndugu, biblia inasema kazi ya kila mtu itapimwa, usifurahie watu wengi kukimbilia bidhaa zako, zilizo hafifu za bei ya chini, (mfano wa bidhaa za kichina) zinazotengenezwa na majani tu, ambazo hata jua haziwezi kustahimili, ni kweli utaziuza nyingi kwa wakati mmoja lakini faida yake itakuja kidogo, tofauti na mtu Yule anayefanya biashara ya DHAHABU, atapata mteja mara moja kwa mwezi lakini faida yake ni mara 1000 ya zaidi ya Yule wa mchicha.

1Wakorintho 3: 11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.

12 Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedhaau mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.

13 Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.

14 Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu.

15 Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto”.

Unaona hapo?..Tunapaswa tujitathimini ni wokovu upi tunawapelekea wenye dhambi, ili siku ile tusije tukajikuta wote tunaangukia katika hasara na majuto, na kazi zetu na taabu zetu zikaonekana kuwa ni bure…Tuupe wokovu thamani yake, tuwafundishe watu UTAKATIFU na NENO la Mungu, na TOBA! tusiwafiche juu ya hukumu inayokuja, tuwaambie ukweli njia inayokwenda UZIMANI ni nyembamba nayo imesonga nao wanayoiona ni wachache, na inayoenda mautini NI PANA, tuwaambie kulingana na maandiko wanawake kuvaa vimini, suruali, mapambo, ni dhambi na vinapeleka wengi kuzimu. Ni kweli mambo kama hayo hayapendwi lakini mnunuzi atakayekuja kuununua wokovu wa namna hiyo..Atakuwa ni wa uhakika, na ndio hao biblia inasema mbingu nzima na malaika juu mbinguni wanawafurahia wakitubu..Lakini sio wokovu tu mwepesi ambao huo kila mtu anasema anao lakini roho yake ipo mbali ni Kristo.Hatupaswi kuhubiri vile watu wanavyovitaka, bali kile Kristo anachokitaka, hilo ndio jukumu letu.

Naamini, utakuwa umeongeza kitu katika vile ulivyojaliwa kuvijua, Bwana akubariki na atuongezee Neema yako sote tuzidi kumjua yeye. 

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

 


Mada Zinazoendana:

LILE TUMAINI LILILO NDANI YETU LINAPOULIZIWA.

BEI YA UFALME WA MBINGUNI:

LULU YA THAMANI.

MAMA WA MAKAHABA


Rudi Nyumbani

Print this post