Swali: Katika Mathayo 27:31-32 tunasoma kuwa Simoni Mkirene alimsaidia Bwana kuubeba msalaba wakati anaelekea mahali pa kusulibishwa, lakini tukirudi katika Yohana 19:17-18 tunasoma kuwa hakusaidiwa na mtu badala yake aliubeba mwenyewe mpaka Golgotha, je mwandishi yupi yupo sahihi?.
Jibu: Turejee mistari hiyo..
Mathayo 27:31 “Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake.
33 Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa”
Hapa ni kweli Simoni Mkirene alimsaidia Bwana kuubeba msalaba..
Lakini hebu tusome tena Yohana 19:17-18..
Yohana 19:16 “Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe; nao wakampokea Yesu.
17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha.
18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati”.
Hapa inaonyesha ni kama hakusaidiwa na mtu mpaka alipofika Golgotha..
Je kwa mantiki hiyo biblia inajichanganya?…
Jibu ni La! Biblia ni kitabu kisicho na makosa wala mkanganyiko mahali popote, isipokuwa fahamu zetu na pambanuzi zetu ndizo zinazojichanganya.
Sasa tukirejea katika habari hizo mbili, ni kwamba Mwandishi wa kitabu cha Yohana (ambaye ni Yohana mwenyewe) alijaribu kueleza safari ya Bwana kwenda Golgotha kwa ujumla, bila kuhusisha matukio madogo madogo yaliyokuwa yanatokea njiani.
Kwamfano utaona yeye kasema tu Bwana alijichukulia msalaba wake mpaka Golgotha, pasipo kutaja matukio kama ya kutemewa mate njiani, au wale wanawake kumlilia na Bwana kuwajibu kwamba wajililie nafsi zao na watoto wao (Luka 13:26-28).. Sasa matukio kama haya Yohana hajayataja lakini haimaanishi kuwa amesema hayapo, la! Bali ni kwamba kafupisha tu habari.. hata wewe/mimi tunaweza kuelezea jambo kwa urefu au ufupi kutegemea na mapenzi yetu.
Lakini sasa tukirudi kwa Mathayo yeye kataja safari ya Bwana kwa urefu kidogo, akihusisha matukio madogo madogo yaliyokuwa yanaendelea njiani katika safari yake..na mojawapo ya tukio ndio hilo la Simoni Mkirene aliyekuwa anatokea shamba na akashurutishwa kuubeba msalaba wa Bwana YESU.
Na utaona pia ijapokuwa Mathayo alirekodi tukio la Simoni Mkirene kumsaidia Bwana msalaba, lakini pia hakutaja tukio la wanawake waliomlilia Bwana njiani, ambapo tukio hilo linakuja kutajwa na mwandishi mwingine wa kitabu kingine ambaye ni Luka..
Luka 23:26 “Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.
27 Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.
28 Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.
29 Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha”.
Umeona kwahiyo habari ya Bwana YESU kujichukulia msalaba mpaka Golgotha kama ilivyoandikwa na Yohana haipingani na ile iliyoandikwa na Luka, Mathayo au Marko.. kinachotofautisha habari hizo ni kwamba moja imeandikwa kwa urefu nyingine kwa ufupi.
Je umempokea YESU, je umeubeba msalaba wako na kumfuata?.. Je unajua ni kwanini Simoni Mkirene aliruhusiwa kubeba msalaba nyuma ya YESU?.. ni ufunuo kuwa tukitaka kumfuata YESU ni lazima tubebe msalaba tumfuate YESU nyuma.
Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.
35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MANENO SABA YA YESU MSALABANI.
YESU MNAZARETI, ANWANI YA MSALABA.
MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.
Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?
SWALI: Biblia inasema maziwa ni kwa watoto wachanga, lakini chakula kigumu ni cha watu wazima. Mfano wa chakula hichi kigumu ni kipi?
Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya
JIBU:
Kabla ya kufahamu hicho chakula kigumu, ni vema kujua kwanza maziwa ni yapi.
Hivyo ukiendelea kusoma vifungu vinavyofuata anasema..
Waebrania 6:1 Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, 2 na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele. 3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia.
Sasa hayo mafundisho ya kwanza ya Kristo ndio maziwa. Yaani Mafundisho ya toba, imani kwa Mungu, ubatizo, kuwekewa mikono, kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele ni mafundisho ya watoto wachanga..kiroho hujulikana kama maziwa..
Kimsingi mtoto akiendelea kunywa maziwa tu peke yake daima, kitakachotokea baadaye ni kudumaa kama sio kufa kabisa, hivyo itafika wakati tu atahitaji chakula kingine ili aendelee kuishi. Vivyo hivyo na sisi, vipo vyakula ambavyo tunapaswa tule, kwa jinsi tunavyoendelea kukua kiroho.
Vifuavyo ndio vyakula vigumu vya kiroho vya watu wazima:
Mathayo 5:44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu jambo hilo linaenda kinyume na asili ya mwanadamu, linafunua asili ya ndani kabisa ya Kristo, ambayo si rahisi mtu aliyemchanga kiroho, kuielewa, au kulipokea nyakati za mwanzoni, yaani kumwombea na kumpenda Yule ambaye anaiwinda roho yake au aliyemjeruhi, ..
Wafilipi 1:29 Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu mwamini mchanga, mara nyingi atapenda kuambiwa maneno ya faraja, baraka, na mafanikio, awapo kwa Kristo, lakini mkristo aliyekomaa, anayaona mapenzi ya Mungu pia hata katika majaribu na kuyashangalia.
1Wathesalonike 3:3 mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo
Soma pia 1Petro 1:6-8, 4:13, Wakolosai 1:24, Luka 6:22-23
Waebrania 5:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya
Mkristo aliyekomaa kiroho, anafundishwa na Mungu kutambua na kugawanya vema mambo yote, kujua vilivyo najisi na visivyo najisi, mafundisho ya kweli na yale ya uongo, anafundishwa, busara, ujuzi na hekima hata katika kuhubiri injili kwa makundi yote, bila kuanguka na kunajisika, kwasababu amepewa roho ya upambanuzi ambayo huja kwa kuzoeshwa na Mungu kwa kipindi Fulani cha muda kupitia Neno lake.
1Wakorintho 9:20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.
21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. 22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
Soma pia, 1Wakorintho 8:6-13, Yohana 2:1-12, Mathayo 11:19.
Kwanini ni chakula kigumu? Kwasababu mtu ambaye ni mchanga kiroho, akijihusisha katika viwango hivyo, hupotea na kunajisika kama sio kupotea kabisa. Ndicho kilichowatokea Adamu na Hawa kuuvamia mtu wa ujuzi wa mema na mabaya nje ya ratiba ya Mungu, matokeo yake wakayavuna mabaya, wala sio mema.
Katika wokovu ipo fimbo ya Mungu; Mzazi yoyote huwa hatoi zawadi tu, sikuzote, hacheki na mwanawe siku zote, lakini pia kuna wakati fimbo hutumika, Vivyo hivyo Mungu ni Baba yetu, huadhibu, pale tunapokosea..
Waebrania 12:11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.
Kwanini ni kigumu? Kukubali marekebisho kwa kuadhibiwa kama sehemu ya kutengenezwa na Mungu, si jambo rahisi mtu kulikubali mkristo ambaye hajakomaa. Yeye atakachojua tu, kuwa Mungu ni upendo.
Luka 9:23 Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.
Kwanini ni chakula kigumu? Aliye mchanga kiroho kukubali kukataa mapenzi , kuingia gharama kuacha vyote na kuyakubali ya Mungu tu, si jambo rahisi kwa mwanafunzi wa ngazi ya chini.
Wafilipi 2:3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba
Kwanini ni chakula kigumu?.
Mkristo mchanga kiroho, si rahisi kuangalia mambo ya wengine, mfano wa Kristo, si rahisi kujinyenyekeza na kukubali kutembea kama mtumwa ili kuwatumikia wengine.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Kama mwamini mpya ni lazima ufahamu kuwa kanisa sio jengo, bali kanisa ni watu wa Mungu waliookolewa na kuwekwa pamoja ili kumwabudu Mungu, na kuhudumiana.
1 Wakorintho 12:27
[27]Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
Kama vile viungo vinavyoshirikiana, vivyo hivyo na wewe huna budi kuwa na ushirika wote wa kanisa, sio kuwa mtembeleaji. Kila mwamini ni kiungo Katika mwili huo.
Waefeso 5:25-27
25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;
Kristo anataka ujue kuwa unapookoka, unakuwa katika kifungo chake, mfano tu wa mwanamke aliye katika ndoa. Bwana mmoja, mwili mmoja, huku akimtii yeye katika yote. Vivyo hivyo na wewe, tangu huu wakati uliokoka ni wajibu wako, kumtumikia Kristo tu, na kumtii katika yote atakayokuagiza ndani ya kanisa.
Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu”.
Kama mwanafamilia unakuwa na haki ya kupokea na kurithi ahadi zote ambazo Mungu alizoahidi kwa watu wake, kwasababu wewe tayari umeshafanywa kuwa mwana wake.
1Wakorintho 3:16 -17
16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.
Kwamba ukishaokoka, wewe na waamini wenzako mnaitwa nyumba ya Mungu, hivyo ni wajibu wako kuifanya nyumba hiyo safi sikuzote kwa kuishi maisha ya utakatifu, kwasababu Mungu haishi mahali pachafu, bali pasafi. Wewe ni nyumba ya Mungu, iheshimu nyumba yake.
Kwa kupitia mafundisho, mahubiri, madara ya uanafunzi, uyapatayo ndani ya kanisa, pamoja na madhihirisho mbalimbali ya karama za Mungu, utajikuta unajengeka kwa haraka sana na Matokeo yake utajengwa na kukua kiroho, tofauti Na kama ungekuwa peke yako. (Waefeso 4: 11-13)
Mahali Bora pa kumwabudu, na kumsifu Mungu kwa uhuru na nguvu, ni Pale uwapo katika mkusanyiko. Daudi alisema;
Zaburi 95:6
[6]Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.
Kanisa lina misingi ya maombi na Maombezi. Bwana Yesu alisema;
Yakobo 5:16
[16]Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
Huwezi kusaidika pale unapoishiwa na nguvu, kama huna jamii ya watu nyuma yako kukushika mkono kimaombi au kihali usimame. Kanisa la kwanza, lilipokusanyika, lilisaidiana katika mahitaji, lakini pia lilitatua migogoro, mbalimbali iliyozuka katikati yao. Hivyo mtu anayekosa kanisa, ukweli ni kwamba anaishi kama yatima wa kiroho.
Kanisa Ni kama karakana ya Mungu inayowaandaa watu, kuwa watendakazi. Ni mahali ambapo utatambua Karama yako. Kisha kuitumia hiyo kuwahudumia wengine na kuipeleka mbele kazi ya Mungu.
Matendo 2:41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali
Mengi kwa jinsi uwezavyo..
Biblia inatuambia tuonyana kila inapoitwa leo (yaani kila siku).
Waebrania 3:13 Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi. 14 Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho;
Pamoja na hilo, atakatifu wa zamani, ukiachilia mbali makusanyiko ya katikati ya wiki, ilikuwa ni lazima siku ya kwanza ya juma wote wakusanyike. (1Wakorintho 16:2). Yaani kila jumapili ilikuwa ni siku ya Bwana.
Kanisa ni kama Shule kwa mwanafunzi. Tunajua Shule kama Shule sio elimu. Bali shule hutoa elimu. Kwasababu ndani yake wapo waalimu, zipo nidhamu, wapo wanafunzi wenzako , yapo majaribio, Vipo vitabu n.k. ambavyo vinakusaidia Kufaulu vizuri katika masomo yako.
Halikadhalika wewe kama mwamini mpya, ni lazima uwe na kanisa. Mwamvuli wako, ujengwe ukue, uandaliwe. Kanisa ni chombo maalumu alichokiunda Mungu, siku ile ya pentekoste ili watu wake wamwone yeye.
Zingatia sio kila mkusanyiko unaosema ni wa-kikisto ni kweli ni kanisa la Mungu. Kwasababu manabii, na wapinga-Kristo wapo sasa duniani.
> Epuka mikusanyiko isiyo mfanya YESU KRISTO kama ndio msingi, na wokovu wa mahali hapo.
> Epuka mikusanyiko isiyokurejeza katika maisha haki na utakatifu.
> Epuka mikusanyiko isiyokukumbusha juu ya hatma ya maisha yajayo, yaani kuzimu na mbinguni
> Epuka mikusanyiko isiyoamini katika utendaji kazi wa karama za Roho Mtakatifu.
Omba, kwanza, kisha fanya maamuzi.
Ikiwa bado hujawa na uhakika wa pa kukusanyika. Basi wasiliana na sisi tukusaidie mahali sahihi pa kukusanyika..
Vifungu hivi visitoke akilini mwako:
Waebrania 10:25
[25]wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Mhubiri 4:9-10
[9]Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
[10]Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
Zaburi 122:1
[1]Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa BWANA.
WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA
WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU
KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.
KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Maisha Mapya ya wokovu yanasukumwa na maombi. Kama Neno ni chakula, basi maombi ni maji. Vilevile huwezi tenganisha maisha ya wokovu na uombaji.
Ni tendo la kuongea na Mungu, lakini pia kumsikia. Maombi sio maneno matupu tu, au utaratibu wa kidini, bali ni mahusiano halisi kati ya sisi na Mungu.
Yeremia 33:3
[3]Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.
Maandiko hayatoi ukomo wa maombi. Zaidi sana yanasisitiza tuombe kila wakati na bila kukoma.
1Wathesalonike 5:17 ombeni bila kukoma;
Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
Hivyo Maombi ni tendo endelevu la wakati wote.
Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Luka 3:21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu
zilifunuka
Mathayo 17:20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]
Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Zipo aina mbalimbali za maombi, ili kufahamu kwa kina bofya hapa >> KUNA AINA NGAPI ZA MAOMBI?
Ramani kuu ya maombi tulishafundishwa na Bwana Yesu Kristo. Ambayo ndio ile Sala, ijulikanayo kama “Sala ya Bwana”. Hivyo kufahamu namna ya kuiomba fungua hapa >>>> Namna bora ya kuiomba sala ya Bwana
Miongozo mingine itakayokusaidia kutanua upeo wako wa uombaji kwa lengo la ukuaji wa kiroho Bofya hapa >>> MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.
Haya ni mafundisho, mengine yatakayokusaidia kujua kwa undani kuhusu maombi;
Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?
MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.
JINSI YA KUVURUGA MIPANGO YA MUNGU.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Kama tulivyotangulia kuona kuwa kusoma Neno kunazidisha Ujazo wa Roho Mtakatifu Ndani Yetu..lakini pia ndio Chakula kikuu cha Roho zetu. Bila NENO ni sawa na mwili bila chakula, huawezi kuishi.
Mathayo 4:4
[4]Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
> Kusoma biblia ndiko kunakoweza kukukuza kiroho, (1Petro 2:2,),
> Pia ndipo unapoweza kufanywa upya ufahamu wako (Warumi 12:12).
> Lakini pia Ndani ya biblia kuna unabii wa maisha yako, kuna faraja, Kuna maonyo, kuna mashauri na miongozo (Zaburi 119:105).
Hivyo hakuna Namna mtu atayatenganisha maisha ya wokovu na usomaji Neno.
Sasa unapotaka kuanza kusoma unapaswa ufahamu Kuna usomaji wa aina mbili kuu.
Aina hizi mbili Ni muhimu kuendana nazo. Kuijua biblia yote ni jambo la msingi, kwasababu ili Kuelewa muktadha wa biblia ni lazima kwanza kuzielewa habari mbalimbali zilizo katika biblia.
Hivyo ni lazima Uwe na nidhamu ya kusoma kila siku. Na kama ukifanya Hivyo kwa kusoma sura 6-7 kwa siku, basi ndani ya miezi sita (6), utakuwa umeimaliza biblia yote. Ukimaliza kuisoma rudia tena na tena.
Lakini kusoma kwa muktadha ni kusoma kwa mnyumbuliko, kunahitaji pia mkufunzi Wa kukusaidia kuelewa. Pamoja na utafakariji sana wa Neno, na kwenda taratibu taratibu ili Roho Mtakatifu Akusaidie kuelewa.
1) Hakikisha unakuwa na biblia yako, wewe kama mwanafunzi mpya wa Kristo, yenye agano la kale na lile jipya. Biblia yenye vitabu 66
2) Tenga Muda wa utulivu wa kujisomea kila siku. Ni vema ukawa na mahali pako pa utulivu, ili kuweza kusoma kwa umakini zaidi.
3) Kuwa na daftari Na kalamu, ili Kuandika kila unachojifunza, kwa kumbukumbu zako za baadaye.
4) Omba kwanza kila unapoanza kujisomea biblia ili Mungu Akupe uelewa.
5) Mwisho Hakikisha unakitendea kazi kila unachokisoma.
Kujisomea na wengine pia ni jambo jema la ziada. Uwezavyo kupata rafiki ambaye anapenda biblia, basi kutana naye mara kwa mara, utafakari Naye maandiko. Epuka kampani za watu wasio- na kiu ya Mungu wakati wako huu, tumia muda wako mwingi katika kumtafakari Mungu, ili ukue kiroho kwa haraka, mtoto mchanga huwa ananyonya hata mara saba kwa siku. Kwasababu mwili wake upo katika kukua unahitaji maziwa wakati wote. Vivyo hivyo na wewe hakikisha una muda wa kutosha wa kusoma biblia kila siku.
Vifungu hivi unaweza ukavikariri viwe Kama nanga ya maisha yako ya usomaji Neno.
Zaburi 119:11
[11]Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
Waebrania 4:12
[12]Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
Yoshua 1:8
[8]Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.
Bwana akubariki.
Haya ni mafundisho yanayoweza kukusaidia kupata mwongozo wa usomaji biblia mzuri.
MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.
Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?
CHAMBUZI ZA VITABU VYA AGANO JIPYA.
NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.
Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Ahadi ya Roho Mtakatifu ni ya kila mwamini. (Matendo 2:39). Ni msaidizi ambaye Mungu alitupa ili kutuwezesha kuishi maisha ya wokovu kwa viwango vya ki-Mungu hapa duniani.
Hivyo siku ile ulipomkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako. Tayari ulipokea Roho Mtakatifu siku hiyo hiyo.
Isipokuwa Huwezi ukahisi chochote ndani, bali kwa jinsi unavyoendelea kutii kwa kumfuata Bwana utaziona tu kazi zake ndani yako.
Na hizi ndio kazi zake kuu azifanyazo Roho Mtakatifu anapokaa ndani ya mtu;
Yohana 16:13
[13]Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
Yohana 14:26
[26]Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana
hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
Hivyo humfanya aendelee kuishi maisha ya utakatifu (Yohana 16:8)
Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu
1Wakorintho 12:7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo
Roho yeye yule;
9 mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule
mmoja;
10 na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho;
mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;
11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake
kama apendavyo yeye
Matendo 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi
wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Hivyo faida zote hizi hudhihirika ndani ya mtu kwa wingi , hutegemea jinsi mtu huyo anavyompa Roho Mtakatifu nafasi ndani yake. Ndio maana ni vema wewe kama mwamini mpya ujue mambo haya ili usije ukajikuta unamzimisha Roho Mtakatifu ndani yako. Ukawa unaisha maisha ya kama mtu ambaye hajaokoka.
Moja ya agizo la Bwana Yesu kwetu sisi, ni kwamba “tujikane nafsi”. Kujikana maana yake ni kuyatakataa matakwa yetu wenyewe ya mwilini na kukubali yale ya Mungu tu. Ulikuwa mlevi unakuwa tayari kukaa mbali na ulevi, ulikuwa ni kahaba unauaga ukahaba wako. n.k.
Kuwekewa mikono kunanyanyua mafuta Ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu kwa namna nyingine. Na matokeo yake ni kuwa unaambukizwa pia neema.. Katika maandiko tunaona wapo watu kadha wa kadha waliojazwa Roho kwa namna hii. (Matendo 8:17, Matendo 19:6 , 2 Timotheo 1:6 )
Kiwango cha chini ambacho Bwana alituagiza ni SAA moja. Zaidi Pia katika maombi yako mwambie Bwana nijalie kuomba kwa Roho ( kwa kunena kwa lugha) ikiwa bado kipawa hichi hakijakushukia, Ni muhimu pia.
Zingatia: Katika uombaji wako,jifunze kutoa sauti, pia jiachie mbele zake. Huwezi kunena kwa lugha moyoni.. ni lazima kinywa kihusike hivyo Jifunze kuomba huku kinywa chako kikitoa maneno kabisa. Hiyo ni nidhamu nzuri katika hatua za ujazwaji Roho.
Tunajazwa Roho Kwa kuitambua sauti yake inatuagiza nini. Na sauti yake ni biblia. mahali Pekee penye uwepo wote wa Mungu ni kwenye Neno lake.
Hivyo zingatia sana hilo. Mkristo ambaye hasomi NENO, kamwe hatakaa aweze kumsikia wala kumwelewa Roho Mtakatifu.
Ukizingatia hayo basi, utaona uzuri wa Roho Mtakatifu ndani yako.
Mafundisho ya ziada kuhusu Roho Mtakatifu
YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.
NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.
Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?
NAMNA YA KUNENA KWA LUGHA MPYA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Ubatizo ni agizo la Bwana katika hatua za awali za wokovu. Wapo watu wanaosema Ubatizo hauna maana, ndugu usijaribu kufanya hivyo, unaweza usiwe na maana kwako, lakini unaomaana kwa yule aliyekupa hayo maagizo.
Mathayo 28:19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Ikiwa yeye hakuwa na dhambi wala kasoro yoyote alibatizwa, kwanini sisi tusibatizwe?
Mathayo 3:13 Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.
Ubatizo ni ishara ya nje ya kile ulichokiamini, kuwa umekufa kwa habari ya dhambi, kisha ukafufuka katika upya na Kristo.
Warumi 6:3-4
[3]Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
[4]Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.
Ni yule aliyeamini, yaani kuupokea ujumbe wa injili kwa geuko(toba).
Matendo 2:41
Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa;…
Haraka sana, tangu siku ile alipoamini. Ubatizo sio mpaka umekomaa kiroho au kimafundisho, hapana, bali ulipopokea tu wokovu, wakati huo huo unastahili ubatizo.
Matendo ya Mitume 2:38
[38]Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Ni ule wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23, Matendo 8:36-38 ),
Na kwa jina la Yesu Kristo.(Ambalo ndio Jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu) [Mathayo 28:19, matendo 8:16, 10:48, 19:5]
Ndio, ili kufuata mkondo sahihi wa kimaandiko, huna budi kubatizwa tena.
Kwakuwa umeokoka, na bado hujapata huduma hiyo basi waweza tafuta Kanisa la kiroho, ambalo linaamini katika ubatizo wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ili utimize agizo hilo.
Lakini ikiwa utapenda kusaidiwa na sisi. Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo:
+255693036618 / +255789001312
Bwana akubariki.
Mistari ya kusimamia kila ukumbukapo tendo la ubatizo.
Wakolosai 2:12 Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu.
Wagalatia 3:27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.
Bwana akubariki.
Kwa mafundisho zaidi kuhusu ubatizo
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Dini ni mfumo au utaratibu wa kumwabudu Mungu. Kwamfano ukienda mahali ukaona watu wamekusanyika na kukubaliana kuabudu kitu Fulani, ni lazima utaona tu utaratibu, au mwongozo au miiko wamejiwekea ya kuifuata na kuishika, ili ibada yao iwe na matokeo. Sasa huo utaratibu ndio unaitwa dini.
Hata imani yetu ndani ya Kristo, inasukumwa na dini. Hatumwabudu tu Mungu kama tunavyotaka bali Mungu aliweka utaratibu na njia ya kuifuata.
Lakini Dhehebu, ni “aina ya dini”. Ambayo huzalika ndani ya imani ile ile moja. Kwamfano utaona wakristo imani yao ni moja kwa Kristo Yesu, na msingi wa kuegemea ni biblia ile ile moja takatifu. Lakini ndani yao kuna michipuko mingi tofauti tofauti ya kitaratibu na ufanyaji ibada, kulingana na walivyoielewa biblia. Ndio hapo utaona wengine wanajiita wapentekesto, wengine wakatoliki, wengine wasabato, n.k. Sasa hii yote ni michupuko, ambayo mengine inakaribiana sana na uhalisia, na mengine inakwenda mbali na kweli ya Mungu.
Lakini cha kumshukuru Mungu ni kuwa biblia imeshaeleza asili ya dini ya kweli inapaswa iweje….
Yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. 27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Kwamba ni lazima itakuwa ya kimatendo zaidi. Yaani utafunzwa utakatifu, na kujitoa.
Hapana, kwasababu Yesu hakuja kuleta dhehebu jipya duniani. Kwani alipokuja alikuta tayari yapo madhehebu mengi yamesha-zaliwa kama tu ilivyo sasa, mfano Mafarisayo, na masadukayo. Lakini hakuwahi kutetea lolote kati yao. Bali alisisitiza watu kumwamini yeye, kama ndio njia ya kweli na uzima mtu asipofanya hivyo hawezi kumwona Baba (Yohana 14:6).
Ikiwa na maana haijalishi una dhehebu zuri kiasi gani. Ukikosa shabaha ya Ukristo, bado mbinguni huendi. Waamini wengi wanashikilia zaidi dini, jambo ambalo ni jema, lakini dini ni kisaidizi cha imani. Sio imani yenyewe, ni sawa na shule na elimu, tunaweza kusema shule ni kisaidizi cha elimu, lakini sio elimu yenyewe.
Hivyo ni busara kuchukua tahadhari ya dhehebu unalotaka kumwabudia Mungu, kwasababu ukweli ni kwamba madhehebu mengine hayana ubora wa kumfanya mtu awe mkristo kamili.
Kwamfano dhehebu lisilo, patana na imani katika Kristo Yesu tu, au lisilofundisha utakatifu, au lisilo amini juu ya vipawa vya Roho Mtakatifu, au linalochanganya ibada ya Mungu na sanamu, bali linasisitiza mambo ya mwilini tu, hilo halikujengi, bali linakupoteza.
Lifananishe kwanza na biblia yako, huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ndio ufanye maamuzi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?
Haya ndio mambo ambayo baada ya kuokoka, wokovu hufanya juu ya maisha ya mtu
Yohana 3:3
[3]Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
Maana yake ni kwamba pindi tu unapookoka, ni lazima ufahamu si kwamba unarekebisha yale maisha yako ya kale, na kuwa mtu mwema hapana bali unakuwa mtu mwingine kabisa. Kama mtoto mchana aliyekuja duniani, katika mazingira mapya kabisa.
Kwasababu ukristo sio nembo, au kikundi, au mtindo fulani au aina fulani ya dini hapana bali ni ulimwengu mwingine kabisa ambao mtu anaanza kuuishi.
2 Wakorintho 5:17
[17]Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.
Wakolosai 1:13
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
Maana yake ni kuwa tunakuwa tayari kutoka chini ya utawala wote wa shetani, yaani kufuatisha mambo Ya kidunia, na anasa, wizi, tunaacha, Kama tulikuwa na vikoba vya kiganga, hirizi, mazindiko Yote hayo tunayaondoa, na kuanza kumtumikia Kristo, mfalme mpya.
Wafilipi 2:12-13
[12]Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
[13]Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Maana yake ni lazima Tujue wokovu ni mwendelezo ijapokuwa tunaokolewa pindi tu tunapookoka, lakini hatuupokei tu, na kusema tayari imekwisha hapana bali unapaswa udumu Moyoni mwetu, na kuhakikisha kila siku tunaweka umakini kwa kuuzalia matunda, kwa kufanya bidii kuishi maisha yampendezayo Mungu.
Hivyo kwa ufupi wokovu sio tu, kipawa cha Mungu Kwetu, lakini pia kukubali maisha mapya, mfalme mpya, na njia mpya.
Maana yake ni nini?
Tangu siku hii ya leo wewe uliyookoka hakikisha unayaweka kando mambo yote ya kale ambayo ulikuwa unayafanya yasiyompendeza Mungu, kwasababu hiyo ndio TOBA pekee, kama ulikuwa mzinzi acha mara moja, ulikuwa mlevi, ulikuwa mwizi, ulikuwa mlanguzi acha, kama alivyofanya Zakayo alipokutana na Kristo. Kisha endelea kuishi maisha ya utakaso kila siku, ili Wokovu wako uzidi kuwa thabiti.
Bofya hapa kurudi kwenye mwongozo mkuu wa mafundisho ya mwongofu mpya. >>
Nini kinafuata? bofya hapa. >>>
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.