Shalom,
Bwana atusadie ili kila siku tuzidi kuujua uweza wa Mungu,
Kuna wakati Bwana Yesu aliwaambia viongozi wa dini na watu wote kuwa wanapotea kwasababu moja tu, nayo ni kwasababu hawayajui maandiko na uweza wa Mungu (Mt.22:29).
Nasi Bwana atusaidie tusipotee kwa kukosa kuujua uweza wake.
Na moja ya uweza wake ambao pengine hatuujui ni ule uwezo wa kumlipa mtu, kwa kazi asiyostahili, kwasababu tu katia mkono wake shambani mwake..
Embu tafakari ule mfano alioutoa Bwana juu ya yule mtu mwenye nyumba ambaye aliamka asubuhi ili akawaajiri watu wakafanye kazi shambani mwake, pengine saa 12 asubuhi akaenda akakutana na kundi la kwanza akapatana nalo kiasi Fulani cha fedha, biblia inasema akaenda tena saa tatu akukutana na kundi lingine limekaa tu sokoni halina kazi yoyote, nalo pia akaliambia nendeni shambani, akatoka tena sita na saa tisa, akawakuta wengine wapo hawana kazi, akawaambia nao hivyo hivyo nendeni,, na mwisho wa siku, jioni kabisa ile giza linakaribia kuingia akakutana na kundi lingine ambalo kutwa kuchwa limekaa tu, halina kazi yoyote, nalo pia akaliambia nendeni shambani, mkaangalie kazi ya kufanya,
Ni wazi kuwa hili kundi la mwisho halikukutana na kazi yoyote nzito ya kufanya kule shambani, pengine lilikuwa linakufunga funga tu viroba, viwili vitatu, kwani kazi yote ilishamalizwa na wale wengine ambao walikuwepo tangu asubuhi.
Sasa embu tengeneza picha kidogo kwenye kichwa chako, labda wale wa kwanza walipowaona wanakuja waliwacheka au kuwadharau, au kuwahurumia sana? Pengine wakanong’onezana wakisema kama sisi tutalipwa elfu hamsini hamsini, hawa watalipwa sh. Ngapi? kama sio elfu elfu, Lakini matazamio yao yalikuwa tofauti, wakati malipo yalipofika, Mwenye shamba akaja akawalipa wote, fedha sawa sawa, lakini wale wa kwanza wakamlalamikia mwenye shamba wakimwambia mbona umetulipa sawa na hawa, ambao hawajataabika kwa chochote? Lakini Bwana akawaambia maneno haya;
Mathayo 20:13 “Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari?
14 Chukua iliyo yako, uende zako; NAPENDA KUMPA HUYU WA MWISHO SAWA NA WEWE.
15 SI HALALI YANGU KUTUMIA VILIVYO VYANGU KAMA NIPENDAVYO? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema”?
Unaona? Ameamua kufanya hivyo kwasababu mali ni yake na sio ya yule aliyeajiriwa..Hivyo akitoa vingi au akitoa vichache, hilo ni lake, wewe hupungukiwi kwa chochote maadamu umelipwa kile ulichokubaliana naye. Bwana aliguswa kuona tu walau wamefanya kitu fulani katika shamba lake, haijalishi wamechelewa kiasi gani.
Hata leo hii, tunapaswa tuujue huu uweza wa Mungu, ili tusijione sisi ni wadhaifu kuliko watu mashuhuri waliomtumikia Mungu huko nyuma, au wanaomtumikia sasa, tusijione sisi hatuwezi kulipwa sawa na mitume, tusijione sisi hatuwezi kulipwa sawa na manabii,..Hilo wazo tulifute, Bwana alipatana na mitume wake kuwa katika ulimwengu ujao wataketi katika viti 12 wakihukumu makabila 12 ya Israeli,
Mathayo 19:27 “Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?
28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli”.
Hilo ni kweli kabisa lakini hata mimi na wewe Bwana anaweza kutuketisha pamoja nao, tukayahukumu mataifa, na mitume wasiwe na la kumlaumu Bwana. Kwasababu ni haki yake kutumia vilivyo vyake kama apendavyo. Alisema hivyo pia katika ufunuo..
Ufunuo 3:21 “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”
Hivyo ndugu yangu tusipotee kwa kutokujua uweza wa Mungu. Unaweza ukajiona umechelewa, pengine umeshakuwa mzee wa miaka 70, unajiuliza hata nikimtumikia Mungu nitakwenda kupata thawabu gani kule? Wewe itende tu kazi yake, maadamu upo shambani kwa sasa endelea kuifanya kwa uaminifu kwa huu muda mchache uliobakiwa nao..Kwasababu huujui uweza wa Mungu!..Thawabu zinatoka kwake na sio kwa mwanadamu, hivyo ukitumika kwa uaminifu, nani ajuaye utapata kilicho sawa na mitume.
Hata na sisi sote pia, kila mmoja wetu, ni kweli kuna mahali amezembea au amechelewa, kuingia shambani mwa Bwana. Amekuwa kama wale wa saa kumi na moja jioni. Sasa huu sio wakati wa kuanza kujilaumu, au kujiona hufai.. Kumbuka hata kama ungekuwa umebakisha wiki moja uondoke duniani, na umeokoka, tafuta kazi ya kufanya ya Bwana, usikae tu hivi hivi, jibidiishe, kwa lolote kwa chochote uhakikishe injili inasonga mbele. Kwasababu hata Bwana hakuwalipa watu ambao hawajafanya chochote.
Na suala la malipo muachie yeye. Ni haki yake kutumia vya kwake kama apendavyo,
Hivyo sisi tuliookoka, tuamke sasa tuanze kwa Bwana kwa hari nyingine mpya. Na wewe ambaye bado upo nje ya Kristo, mlango wa neema upo wazi, lakini hautakuwa hivi sikuzote, njoo kwa Yesu ayabadilishe maisha yako, njoo uokolewe, uoshwe dhambi zako, dunia hii inakwenda kuisha, tunaishi katika dakika za nyiongeza tu. Unyakuo wa kanisa upo karibu, jiulize ukifa leo katika dhambi utaenda kuwa mgeni wa nani huko uendako??
Hivyo tubu, na kama hujabatizwa ukabatizwe katika ubatizo sahihi kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako mapema kabisa, ikiwa utahitaji huduma hiyo unaweza kuwasiliana nasi,. Na baada ya hapo anza kuishi maisha yanayolingana na wokovu.
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho”.
Shalom.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Bwana Yesu alimaanisha nini aliposema; Mafarisayo Hupanua HIRIZI zao, na kuongeza MATAMVUA yao?
Njuga ni kengele ndogo ndogo zinazofungwa miguuni au mikononi, na wakati mwingine shingoni, wanavishwa watoto, au watu wanapotaka kucheza ngoma, au wanyama, kama vile ngamia, na farasi n.k..tazama picha
Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolitaja Neno hilo;
Isaya 3:16 “Bwana akasema tena, Kwa sababu binti za Sayuni wana kiburi, na kuenenda na shingo zilizonyoshwa, na macho ya kutamani, wakienenda kwa hatua za madaha, na kuliza njuga kwa miguu yao;
17 Basi, kwa hiyo, Bwana atawapiga binti za Sayuni kwa pele za utosini, na Bwana ataifunua aibu yao”.
Zekaria 14:20 “Siku hiyo katika njuga za farasi yataandikwa maneno haya, WATAKATIFU KWA Bwana; navyo vyombo vilivyomo ndani ya nyumba ya Bwana vitakuwa kama mabakuli yaliyoko mbele ya madhabahu”.
Kutoka 28:33 “Nawe katika pindo zake utatia makomamanga ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu, kuzunguka pindo zake kotekote; na njuga za dhahabu kati ya hayo makomamanga pande zote;
Kutoka 28:34 “njuga ya dhahabu na komamanga, njuga ya dhahabu na komamanga, katika pindo za joho kuizunguka pande zote. 35 Nayo itakuwa juu ya Haruni akitumika; na sauti ya hizo njuga itasikilikana hapo aingiapo ndani ya mahali patakatifu mbele ya Bwana na hapo atokapo nje, ili kwamba asife.
36 Nawe fanya bamba la dhahabu safi na kuchora juu yake, mfano wa machoro ya muhuri, MTAKATIFU KWA Bwana”.
Soma pia;
Kutoka 38:25-26, Isaya 3:18.
Maana yake rohoni ni ipi?
Njuga zinafanya kazi kuu mbili, ya kwanza ni zinafungwa ili mtu au mnyama asipotee, kwasababu kule anapotembea zile kengele zinalia kumtambulisha yupo wapi.
Na pili zinatumika kama zana za muziki, katika tamaduni nyingi watu wanaocheza ngoma walikuwa navaa njuga.
Vivyo hivyo kila mmoja wetu ni lazima awe amevishwa njuga za Bwana, ili tusipotee usoni pa Bwana, na pili ili kumwimbia Mungu sifa, za kweli.
Hivyo anakuwa amevikwa njuga hizi, pale anapojazwa Roho Mtakatifu. Swali ni je sisi tumejazwa Roho Mtakatifu?
Shalom.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tazama tafsiri ya maneno mengine ya ki-biblia chini.
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Je kuweka mapambo kama mikufu, vikuku na kutoboa pua ni dhambi?
Mjanja ni mtu anayetumia njia za kujifanya, ili kuwadanganya au kuwalaghai wengine. (Mtu mdanganyifu).
Makuhani walimwita Bwana wetu kwa jina hilo; walimfananisha na mtu mdanganyifu anayewalaghai watu kwa kujifanya kuwa anaweza kufufuka wakati hawezi, ili watu wamwamini pale wanafunzi wake watakapokuja kuiba maiti yake.
Mathayo 27:62 “Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato,
63 wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka.
64 Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza.
65 Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo.
66 Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi”.
Bwana hakuitwa jina hilo tu, kuna wakati walimwambia ana pepo, wengine wakamwambia amerukwa na akili”.
Hivyo hilo ni jambo la kawaida hata kwa mtakatifu kuzushiwa majina kama hayo. Lakini Bwana alishatupa taarifa hizo mapema, na hiyo ni kututhibitishia kuwa sisi ni wanafunzi wake kweli kweli, alisema;
Yohana 15:20 “Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.
Mathayo 10:25 “Yamtosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli, je! Si zaidi wale walio wa nyumbani mwake”?
Shalom.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Safari ya wana wa Israeli kutoka Misri, kuelekea Kaanani, ni ufunuo kamili wa safari yetu ya Kristo kutuokoa katika dhambi na kutuingiza katika Neema ya wokovu. Musa anafananishwa na Kristo.. Kama vile Musa alivyowaongoza wana wa Israeli kutoka Misri, kwa ishara na miujiza Mingi aliyokirimiwa na Mungu, ndivyo Kristo alivyodhihirishwa kwetu kutuokoa kutoka dhambini, kwa ishara na miujiza mikubwa kuliko ile ya Musa. Sasa ni kwa namna gani safari ile ya wana wa Israeli imefananishwa na safari yetu ya wokovu, unaweza kusoma binafsi kitabu cha 1Wakorintho 10:1-12.
Lakini kuna kipengele kimoja ningependa tukiangalie katika Wito huo wa kutolewa Misri kupelekwa Kaanani..na hicho tunakisoma katika mstari ufuatao..
Kutoka 8:1 “Bwana akamwambia Musa, Ingia kwa Farao, ukamwambie, Bwana asema hivi, Wape watu wangu ruhusa, ili WAPATE KUNITUMIKIA”
Tusome tena;
Kutoka 9:13 “Bwana akamwambia Musa, Ondoka asubuhi na mapema, ukasimame mbele ya Farao, umwambie, Bwana, Mungu wa Waebrania, asema, Wape watu wangu ruhusa WAENDE ILI WANITUMIKIE”.
Kupitia mistari hiyo nataka tuona sababu Nyingine ya Mungu kuwatoa wana wa Israeli kwenye utumwa wa Farao ni ipi.
Hapo tunasoma kwamba Bwana aliwatoa ili WAKAMTUMIKIE. Maana yake ni kwamba Wamefunguliwa kwenye utumwa mmoja na kupelekwa kwenye utumwa mwingine. Hawajafunguliwa na kisha kuwekwa huru tu, kutembea tembea huko la!. Bali walifunguliwa kutoka kumtumikia Farao na kupelekwa katika utumwa wa kumtumikia Mungu.
Pia tunasoma maneno hayo hayo katika…
Kutoka 10:3 “Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, na kumwambia, Bwana, Mungu wa Waebrania, asema hivi, Je! Utakataa hata lini kujinyenyekeza mbele zangu? Wape watu wangu ruhusa waende zao, ILI WANITUMIKIE”.
Ndugu, ni muhimu kulifahamu hili kwasababu pia lengo la Kristo kututoa dhambini ni hilo hilo la sisi kwenda kumtumikia yeye. Anatufungua ile nira ya Adui ambayo ni ngumu, na kutuvisha nira yake iliyo laini..
Ndio Bwana Yesu alisema katika Mathayo 11:28 kwamba “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”
SASA TUNAMTUMIKIA KWA NAMNA GANI?
Warumi 6:16 “Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki.
17 Lakini Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa mioyo yenu ile namna ya elimu ambayo mliwekwa chini yake;
18 na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki”
Unapowahubiria wengine Neno la Mungu, hapo tayari umefanyika kuwa mtumishi wa Mungu..Unakuwa unamtumikia Mungu, na Mungu atakuheshimu..Na kumtumikia Mungu sio tu kuwa mchungaji, au Mhubiri mkubwa, au Nabii au Mtume. Hapana…popote pale ambapo unaweza kufaa katika kulitangaza Neno..Katika nafasi hiyo, tayari unamtumikia Mungu. Hakunaga karama ya Mhubiri Mkubwa, au Nabii Mkuu, au Mchungaji mkuu, au Mwalimu mkuu…kama ni mhubiri ni mhubiri mbele za Kristo wote ni sawa, kama ni mwalimu ni mwalimu mbele za Kristo wote wanaheshimika sawa n.k. Aliye nabii mkuu ni Yesu mwenyewe, aliye Mwalimu Mkuu ni Yesu pekee, aliye Mtume Mkuu ni Yesu pekee..wengine wote haijalishi wingi wa wafuasi walionao…wote mbele ya Kristo wanafanana.
Hivyo kwa hitimisho ni muhimu kufahamu tumetolewa dhambini ili tukamtumikie Mungu na si tukajitumike wenyewe au tukautumikie ulimwengu. Ndio maana wana wa Israeli hatua ya kwanza baada ya kutolewa Misri, walipelekwa nyikani kupewa sheria na amri za Mungu..Na walipoingia kaanani Bwana aliwapa jukumu la kuwafundisha wana wao na vizazi vyao vilivyokuja juu ya sheria, amri na hukumu za Mungu. Na sisi wa sasa tunalo jukumu hilo hilo baada ya kuokoka.
Umeokoka, nenda kamtumikie Mungu..kwa kuwafundisha wengine uliyojifunza.
Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”
Maran atha!
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Bildi ni kitu cha kupimia kina cha maji,Mara nyingi huwa ni kamba ambayo wanaifungia kitu kizito kwenye moja ya ncha zake, kisha wanakishusha kitu hicho kwenye maji, aidha ya mto, au ya ziwa, au ya bahari. na moja kwa moja mpaka kwenye sakafu ya bahari. Kikishafika kule wanapima urefu wa kamba ile na hapo ndipo wanapojua bahari hiyo ina urefu wa kina gani.
Neno hilo utalipata, katika ile habari ya mtume Paulo alipokuwa akisafirishwa kama mfungwa kuelekea Rumi. Kama vile tunavyoijua habari, walipokuwa katikati ya safari yao bahari iliwachafukia sana, mpaka wakakata tamaa ya kuishi, wakakaa siku nyingi bila kuona jua wala nyota. Lakini kama baada ya siku 14 walifika mahali ambapo walihisi kama kuna nchi kavu mbele yao, hivyo ikabidi wajaribu habati yao kwa kupima kina cha maji sehemu mbili tofauti ili waone kama ni kweli kina ndio kinapungua au kinaongezeka..
Hapo ndipo wakatupa bildi hizo kwenye maji, walipotupa ya kwanza ikapima urefu wa “pima” 20, (Pima moja ni sawa na futi 6), hivyo urefu wa kwanza ulikuwa ni futi 120.
Wakaenda mbele kidogo wakatupa bildi nyingine tena, wakapata pima 15 ambazo ni sawasawa na futi 90. Hapo ndipo walipogundua kuwa kina cha bahari kinapungua na kwamba wapo karibu na nchi kavu. Ikawabidi watie nanga, wasisogee popote tena mpaka kukuche.
Matendo 27:27 “Hata usiku wa kumi na nne ulipofika, tulipokuwa tukichukuliwa huko na huko katika bahari ya Adria, kama usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia nchi kavu.
28 Wakatupa bildi wakapata pima ishirini, wakaendelea kidogo wakatupa bildi tena, wakapata pima kumi na tano.
29 Wakachelea tusije tukapwelewa mahali penye miamba, wakatupa nanga nne za tezi, wakaomba kuche.”.
Hata sisi wakristo kila mmoja rohoni anapaswa awe na bildi ya kuipima safari yake akiwa hapa duniani.
Ni lazima tupime mienendo yetu, kila wakati, je namna ya maisha tunayoishi leo na jana tofauti yake ni nini?. Ikiwa hali ya maisha tunayoishi leo ndio inatufanya tuende mbali zaidi na Mungu, tupoe kiroho kuliko ilivyokuwa hapo jana..Hapo tunapaswa tuchukue maamuzi ya haraka sana ya kubadili mfumo wa maisha yetu, ili tusiendelee mbele kwenye madhara zaidi. Tukapotea moja kwa moja.
Lakini kama tutaishi maisha ambayo kila siku yanatutupa mbali na Mungu na bado tunaona ni sawa tu, tunaruhusu yaendelee hivyo hivyo , tujue kuwa mwisho wetu utakuwa ni mbaya sana.
Swali ni je mara ya mwisho kuishusha bildi yako ni lini?
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Jina tukufu la Bwana wetu Yesu libarikiwe daima.
Karibu tuzidi kujifunza maneno ya uzima, kwasababu tupo katika nyakati za ukongoni kweli kweli, hivyo ni wajibu wetu kuzidi kujua mambo yahusuyo ukombozi wetu kwa umakini zaidi..
Neno letu la leo linatoka katika vifungu hivi;
Marko 9:30 “Wakatoka huko, WAKAPITA KATIKATI YA GALILAYA; NAYE HAKUTAKA MTU KUJUA.
31 KWA SABABU ALIKUWA AKIWAFUNDISHA WANAFUNZI WAKE, AKAWAAMBIA, Mwana wa Adamu yuaenda kutiwa katika mikono ya watu, nao watamwua; hata akiisha kuuawa, baada ya siku tatu atafufuka”.
Katika maneno hayo swali kuu unaweza ukajiuliza ni hili, ni kwanini Yesu hakutana watu wamwone , alipokuwa akipita Galilaya, ikumbukwe kuwa mji huo alishauendea mara nyingi na akafanya miujiza mingi kupita kiasi, lakini inafika wakati huu tena kwanini asijidhihirishe awahubirie na kuwaponya makutano kama kawaida badala yake, anaupita mji huo huo kimya kimya tena kwa siri kubwa.
Ukisoma hapo utaona biblia inatupa sababu ya yeye kufanya vile, inatuambia ni kwasababu alikuwa anataka kuwafundisha wanafunzi wake, hilo tu…Hiyo inatupa kuijua tabia nyingine ya Bwana Yesu ambayo pengine tulikuwa hatuijui. Hata sasa, wapo atakaowafundisha kwa wazi, na wapo atakaowafundisha akiwa sirini na mtu mwingine yeyote hatajua,.
Wakati wote makutano walifundishwa kwa wazi, lakini wale aliowaita, kisha baadaye wakawa wanafunzi wake, aliwavusha daraja lingine la rohoni, akawa anawafundisha mambo mengine tofauti kabisa na yale makutano aliyokuwa anawafundisha.
Na baadhi ya mambo yenyewe aliyowafundisha, kama tunavyosoma habari ni yale ambayo yatakwenda kutokea kipindi kifupi mbele yao, yaani juu ya kukamatwa kwa Yesu, mpaka kusulibiwa na kufufuka na kupaa. Walikuwa wanapewa siri za ukombozi wote wa mwanadamu kabla ya wakati wenyewe kufika..mambo ambayo makutano hawakuelezwa, wala kudokezewa hata kidogo.. Na waliambiwa mengine mengi zaidi ya hayo. Kwamfano hizi habari zote tunazozijua zihusuzo siku za mwisho, hawakuambiwa makutano, hapana bali hicho kilikuwa ni chakula walichopewa wanafunzi wake tu walipokuwa kule katika mlima wa mizeituni, (Mathayo 24, Marko 13, Luka 21:5).
Na ndio maana Bwana Yesu mahali pengine aliwaambia, niliyowaambia sirini, utafika wakati mtayasema hadharani, na ndio haya yanayotufaidia sisi..
Kwahiyo, hata sasa huu sio wakati wa kuzunguka huku na huko, kufurahia Yesu anaponya, Yesu anafufua, Yesu anabariki, hatupaswi kuwa kama makutano tu, waliomfuata Yesu, kwa ajili ya mikate na miujiza, na ishara, tunapaswa sasa tuingie gharama za kufanyika kuwa wanafunzi wake,(hicho ndicho anachokihitaji) kwasababu yapo mambo yahusuyo siri za Ufalme wa mbinguni, na Unyakuo tunapaswa tuyajue kwa wakati huu mfupi tuliobakiwa nao, na hatutayajua kama hatutakuwa wanafunzi kweli kweli wa Bwana Yesu.
Yesu ni yeye Yule jana na leo na hata milele, tusidhani alipojificha kwa wale, hawezi kujificha na kwetu pia..Hivyo tusipumbazwe na kitu chochote, kwa maana sisi tukizembea, wapo wengine wakati wetu huu huu wamekaa katika vyumba vya siri na Bwana Yesu wanafunuliwa mambo ambayo yanahusu wokovu wetu.
Tusikubali kuachwa nyuma na Yesu, tusikubali apite kwenye mitaa yetu, na kwenye makanisa yetu, na kwenye mikutano yetu kwa siri, Embu leo tujiachie na kufanyika kuwa wanafunzi wake kweli kweli.
Na tunafanya hivyo kwa kujitwika misalaba yetu, na kuuacha ulimwengu nyuma, na kumkaribisha ndani yetu, Na baada ya hapo, yeye mwenyewe atahusika, kutufundisha.
Tuzidi kukumbuka kuwa; Hii dunia ipo ukingoni sana, hatutashangaa hata unyakuo ukiwa ni usiku wa leo, kwasababu hakuna chochote ambacho hakijatimia, hivyo tukiyajua hayo hatutakuwa na muda tena wa kuichezea chezea neema ya wokovu. Yesu sio kama tunavyomfikiri, Sio kama tunavyomwaza vichwani mwetu, Yesu ni hekima ya Mungu na Nguvu ya Mungu yenyewe kama biblia inavyotuambia (1Wakorintho 1:24), tukifanyika kuwa wanafunzi wake kweli kweli, hatutabaki kama tulivyo.
Hivyo tuanze sasa kufanyika wanafunzi wa Bwana.
Maran Atha.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Ni vitu vipi hivyo viwili visivyoweza kubadilika? (Ebr 6:18)
Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?
Zaburi 9:10 “Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe, Maana Wewe, Bwana hukuwaacha wakutafutao”.
Shalom, tuzidi kujikumbusha kuwa..
Mungu anapenda sana watu wanaomtafuta, anapenda watu wanaoonyesha Nia ya dhati katika kumjua yeye, Mtu anayemtafuta Mungu kamwe Mungu hawezi kumuacha. Atakuwa naye bega kwa bega tu, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu, kwasababu ni ahadi yake kuwa hawaachi wamtafutao.
Mungu si kama sisi wanadamu, sisi ni rahisi kumuacha mtu mwenzetu ghafla tu, hususani pale tunapoona hana msaada wowote kwetu, au katuudhi kwa mara moja, lakini kwa Mungu hilo halipo, haangalii ulimuudhi mara ngapi huko nyuma, wala haangalii madhaifu yako, haangalii uchanga wako, au ujuaji wako, hivyo vyote sio vinavyomshawishi, hivyo hilo hata usilifikirie unapokusudia kumgeukia yeye, ikiwa leo hii utageuka na kusema naanza tena upya na Baba..Saa hiyo hiyo na yeye anaonyesha nia ya kuanza kupiga hatua na wewe,kama kwamba hakuna chochote kibaya ulichowahi kumtendea huko nyuma.
Shetani atakuambia Mungu hawezi kukusikia mtu kama wewe, atajifunuaje kwako, kumbuka dhambi ile uliyofanya zamani, au dhambi hii unayotenda sasahivi unadhani atakusamehe? Ukiona hivyo yapinge hayo mawazo anafanya hivyo ili kukuvunja tu moyo usiendelee au usiwaze kumtafuta Mungu..Lakini ahadi ya Mungu ni ile ile kuwa kamwe hawaachi hao wamtafutao.
Yohana 6:37 “Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe”.
Unaona? Mungu hawezi kuwaacha wale wote wanaomwendea yeye, hilo wazo halijawahi kuingia ndani yake, yaani kile kitendo tu cha kuamua na kusema namfuata Yesu, ujue ni tayari umeshapokelewa bila masharti yoyote, ni mlango ambao upo wazi wakati wote,kwa mtu yeyote haijalishi dini yake wala dhehebu lake, yaani ni jambo ambalo halina maswali maswali, au mashaka mashaka, ukimtafuta utajifunua kwako tu.
Sauti ya shetani inawadanganya wengi na kuwaambia, Mungu hawezi kujishughulisha na watu kama wao, bado huwajakidhi vigezo vya kusikiwa na Mungu, hawana upako wowote, wao ni takataka tu machoni pake, Ndugu hiyo sauti ikikuambia hivyo ijibu uiambie, ingekuwa mimi sina thamani yoyote machoni pake basi asingeniumba, lakini kama ameona vema kuniumba mimi mpaka nikawa hivi nilivyo mwanadamu kamili mwenye mfano wake na sura yake, na hakuniumba mende, au panya, au kononono basi mimi ni wa thamani nyingi machoni pake..
Hivyo ukishajipa moyo kwa namna hiyo halafu ukaanza kuutafuta uso wa Mungu wako, yeye mwenye atajifunua kwako, ni lazima afanye hivyo kwasababu anasema kamwe hawaachi wamtafutao, Mungu anafungwa na Neno lake, akisema hivi, amesema ni lazima atimize, sio kama sisi tulivyo.
Hivyo hatua ya kwanza kabisa inayothibitisha kuwa unamtafuta Mungu, ni kwa kutubu kwanza dhambi zako, kwa kumaanisha kabisa kuziacha, na pili kuwa tayari kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kimaandiko wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38) kama hukuwahi kubatizwa hapo kabla, na tatu ni kuanza kuzingatia kujifunza Neno la Mungu, na kuishi maisha yampendezayo Mungu na kufanya ushirika na kusali..
Ukizingatia hayo, nakutakia kila la heri katika kukutana na Mungu siku baada ya siku katika maisha yako yote hapa duniani, Kwasababu Bwana ni Mungu ambaye kamwe hawaachi wamtafutao.
Shalom.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”
Ni vitu vipi hivyo viwili visivyoweza kubadilika? (Ebr 6:18)
SWALI: Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati” (1 Wakorinto:15:56)?.
JIBU: Pale Adamu alipoasi katika bustani ya Edeni, alipewa mapigo mawili makubwa…la kwanza Ardhi imelaaniwa kwa ajili yake, la pili ATAKUFA. Maana yake ni kwamba, Matokeo ya ardhi kulaaniwa ndio yale Bwana Mungu aliyoyataja pale kwamba atakula kwa jasho, maana yake ni kwamba ataishi lakini katika hali ya kuishi huko atakuwa katika mateso ya kuhangaika siku zote za Maisha yake, hatapumzika!.
Lakini pigo la pili aliloambiwa kwamba Atakufa, biblia haijataja matokeo yake…Maana yake ni kwamba nalo pia sio zuri, maana yake ni kwamba katika kufa huko pia sio kwamba atakwenda kustarehe na kupumzika. Hapana!.. Baada ya kufa atakwenda sehemu ya wafu nako huko sio sehemu ya kwenda kupumzika, bali pia kuna kutaabika baada ya kifo, kwasababu kifo ni pigo!.
Hivyo kabla ya Bwana Yesu mtu yeyote awe mkamilifu au mwovu baada ya kufa alikuwa anashuka sehemu ya wafu ambayo haikuwa salama sana, bado anaendelea kuitumikia laana, na shetani alikuwa anao uwezo wa kufika mahali wafu walipo, na baadhi yao kuwafanya anavyotaka..Sasa ili kuelewa vizuri kasome Habari za Samweli, jinsi shetani alivyomtaabisha kwa kumpandisha kutoka kwa wafu (kasome 1Samweli 28:15). Hivyo mauti ilikuwa ni sehemu chungu, kwasababu shetani alikuwa na mamlaka nako.
Mpaka Bwana Yesu alipokuja na kwenda kuzitwaa funguo za mauti na kuzimu, Ndipo ukatokea wokovu kwa wale watakaokufa katika haki, kwa kuhamishwa na kuwekwa sehemu salama inayoitwa Paradiso. Huko watapumzika bila kufikiwa na adui shetani, (kwasababu funguo anazo Kristo na si shetani tena, hivyo shetani hawezi kuwafikia wala hajui walipo), watakaa huko wakingoja ufufuo wa kwenda mbinguni, siku ile parapanda ya mwisho itakapolia, ambapo watafufuliwa na kuvaa miili yao ya asili kwanza, kisha ya utukufu itavikwa juu ya ile ya asili (ili ule unaoharibika uvae kutokuharibika, na mauti imezwe na uzima 1Wakorintho 15:54) na kisha wataungana na watakatifu walio hai, wote wakiwa na miili yao ya utukufu isiyoweza kuharibika wala kufa na kwa Pamoja watakwenda mbinguni.
Lakini wafu waliokufa katika dhambi (yaani ambao hawajamwamini Yesu), wanapokufa hawaendi paradiso bali kuzimu sehemu ya mateso ya muda, wakingojea kusimamishwa siku ile katika kiti cha hukumu na kuhukumiwa kulingana na matendo yao, na kutupwa katika lile ziwa la moto Pamoja na shetani na malaiika zake.
Hivyo Mauti ina UCHUNGU kwa wale waliokufa nje ya Kristo, na kwa wale watakaokufa wakiwa hawajampokea Kristo. Kwasababu hata baada ya kufa wataendelea kuteseka.. Na uchungu huo unakuja ni kwasababu ya Maisha ya Dhambi waliyokuwa wanayaishi, hivyo baada ya kufa, watapata uchungu, Lakini kama wangeishi Maisha ya utakatifu ambayo yanakuja kwa kumpokea Bwana Yesu na kujazwa Roho Mtakatifu, basi wasingepata uchungu baada ya kifo, badala yake baada ya kifo wangepumzishwa mahali pa raha panapoitwa peponi/paradiso…sawasawa na andiko hili ….
“Ufunuo 14:12 Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.
13 Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA TANGU SASA. NAAM, ASEMA ROHO, WAPATE KUPUMZIKA BAADA YA TAABU ZAO; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”
Hiyo ndiyo sababu biblia inasema hapo katika 1Wakorintho 15:56 kuwa “UCHUNGU WA MAUTI NI DHAMBI”.. Maana yake tukifa katika dhambi, tutapata uchungu baada ya kifo.
Hapo ndipo utakapojua umuhimu wa Yesu Kristo upi?, na jinsi gani kama sio Baba kumleta ulimwenguni, shughuli yetu ilikuwa imekwisha!..tungekuwa hatuko salama hata baada ya kifo..Uchungu tungeendelea nao, baada ya kufa, na hiyo ingekuwa ni milele.
Kama utataka kujua mistari inayozungumzia Habari za Yesu kuzitwaa funguo za Mauti na kuzimu, na jinsi yeye mwenyewe alivyoshinda uchungu wa Mauti,.unaweza kusoma binafsi mistari ifuatayo.. (Matendo 2:23-27, Ufunuo 1:17-18, Warumi 14:8-9).
Sasa sehemu ya pili, inasema “NGUVU YA TORATI NI DHAMBI”..Maana yake ni Nini?
Ili tuelewe ni kwa namna gani, Torati au sheria ndiyo nguvu ya dhambi…Hebu tutafakari mifano ifuatayo..
Kama umewahi kuchunguza, mahali ambapo pamewekwa sheria kali, ndipo panapovuta umakini wa watu zaidi..Ukimwambia mtu usipite mahali hapa usiku, ndio kama umemtangazia apite..kwasababu kila siku atajiuliza kwanini yule anikataze nisipite pale usiku, kwani kuna nini…siku moja nitajaribu nipite kwa siri ili nijue ni nini kinaendelea pale. Umeona?..Hapo hiyo sheria uliyompa kwamba asipite mahali hapo usiku, tayari imemfungulia mlango wa kuivunja…Lakini kama usingemwambia hata asingehangaika kutafuta kupita mahali hapo usiku.
Vivyo hivyo, ukimwacha mtoto nyumbani na kumwambia ni marufuku kufungua kile chumba, ukikufungua ni utakuwa umefanya makosa!…Sasa kwa kumwambia vile ndio kama umemjulisha kuwa akatafute kukifungua hata kwa siri ili aangalie kuna nini ndani ambacho kinakatazwa kisiangaliwe, hivyo atajizuia siku ya kwanza, ya pili lakini siku moja atakuwa anajiuliza ni nini kipo kule, hivyo atatafuta hata kuchungulia tu.. “tayari kashaivunja ile sheria”.
Kadhalika sheria inaposema “Usizini” tayari imefungua mlango wa yule anayeambiwa usizini akazini…Ni hivyo hivyo na dhambi nyingine zozote..zinapata nguvu katika SHERIA au AMRI. Ndio maana Mtume Paulo kwa uongozo wa Roho alisema..
Warumi 7:8 “ Lakini dhambi ilipata nafasi kwa ile amri, ikafanya ndani yangu kila namna ya kutamani. KWA MAANA DHAMBI BILA SHERIA IMEKUFA.
9 Nami nalikuwa hai hapo kwanza bila sheria; ila ilipokuja ile amri, dhambi ilihuika, nami nikafa”.
Warumi 7: 5 “ Kwa maana tulipokuwa katika hali ya mwili, tamaa za dhambi, zilizokuwako kwa sababu ya torati, zilitenda kazi katika viungo vyetu hata mkaizalia mauti mazao”.
10 Nikaona ile amri iletayo uzima ya kuwa kwangu mimi ilileta mauti”.
Hiyo ndio sababu Neno la Mungu linasema hapo.. “Nguvu ya dhambi ni Torati”. Lakini Bwana Yesu alipokuja na kutoa uhai wake pale Kalvari, na kufufuka na kupaa mbinguni..alituachia ahadi ya Baba, ambayo ni Roho Mtakatifu.. Kwa huyo hatuishi kwa Sheria. Na hatuwi chini ya sheria..Huyo anatusaidia kushinda dhambi pasipo sheria…Maana yake ni kwamba sheria isema kwamba usizini, au isiseme bado Dhambi haina nguvu juu yetu. Hiyo ni nguvu ya kipekee sana na zawadi isiyoelezeka. Na hapa pia ndio utaona umuhimu wa Yesu Kristo. Kama sio kuja, ahadi hii tusingeipata…Ingekuwa kwa jinsi sheria zinavyoongezeka ndivyo na dhambi ingetulemea sana. Lakini wote waliompokea Kristo na kupokea Roho wake mtakatifu, wanapewa uwezo wa kipekee kushinda ndambi.
Hivyo kama hujampokea Kristo ndugu yangu..tumaini lako lipo kwa nani?..Unafikiri utaweza kushinda zinaa kwa nguvu zako?, unafikiri utaweza kuushinda ulevi? Au usengenyaji?..Hutaweza..na kwa jinsi utakavyozidi kujiwekea sheria kwamba sitafanya hivi au sitafanya vile, ndivyo unavyozidi kujimaliza..kwasababu nguvu ya dhambi ipo katika hizo sheria unazojiwekea…kwasababu utakapojiwekea sheria ya kwamba kesho sijakunywa pombe na humtaki Yesu, hiyo sheria uliyojiwekea utavumilia siku ya kwanza, pengine na ya pili.. lakini zitakapopita siku kadhaa utapata kiu ambayo hujawahi kuipata.. na utalewa mara mbili Zaidi ya ulivyokuwa unalewa. Kwasababu hiyo basi..mpokee Kristo leo, wokovu ni bure ili upate uwezo wa kushinda dhambi, na pia uepukane na UCHUNGU WA MAUTI.. ambao utawapata wale wote ambao hawajampokea Yesu baada ya kumaliza maisha haya. Baada ya kutubu, tafuta ubatizo sahihi ambao ni wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo, ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (Matendo 2:38, Matendo 8:16). Na Roho Mtakatifu atakutia muhuri..
Bwana akubariki.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Maran athan
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?
Kama ni msomaji wa biblia utakuwa umekatana na hili neno sehemu nyingi..
Shokoa ni kiswahili cha zamani chenye maana ya “Vibarua”. Hususani wale waliotekwa na kulazimishwa kufanya kazi kwa nguvu.
Kwamfano katika biblia tunamwona Mfalme Sulemani, aliwachukua watu Shokoa..
2Nyakati 2: 7 “Basi kwa habari ya watu wote waliosalia wa Wahiti, na wa Waamori, na wa Waperizi, na wa Wahivi, na wa Wayebusi, wasiokuwa wa Israeli;
8 wa watoto wao waliosalia baada yao katika nchi, ambao wana wa Israeli hawakuwakomesha, katika hao Sulemani akawatumikisha SHOKOA HATA LEO”
Mistari mingine inayozungumzia juu ya shokoa ni 1Wafalme 5:13 , Yoshua 17:13, Waamuzi 1:28, Waamuzi 1:30 n.k
Na hata leo adui yetu shetani anawachukua watu Shokoa, kwa kuwateka na kuwatumikisha kwa nguvu. Anawatumikisha kwa dhambi, magonjwa, tabu na hofu.Wote aliowateka hawana raha, wala furaha, wala amani..Wamejawa na mashaka na kukata tamaa.. Yote hayo yanawapata kwasababu wamechukuliwa mateka (Shokoa) na adui shetani.
Lakini habari njema ni kwamba..Yupo mmoja ALIYETIWA MAFUTA NA MUNGU KUKOMESHA UTEKA. Huyo akikuweka huru umekuwa huru kweli kweli.. hofu yote itaondoka, hofu ya kifo, shida, tabu na magonjwa anaiondoa..na kisha anakupa raha nafsini mwako. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.
Isaya 61: 1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, KUWATANGAZİA MATEKA UHURU WAO, NA HAO WALİOFUNGWA HABARİ ZA KUFUNGULİWA KWAO.
2 Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao”
Ukimpokea maishani mwako, Uteka shetani aliokuteka, itakuwa ni zamu yako kumteka yeye…atakaa chini ya miguu yako, na ukimwambia ondoka ataondoka kwa hofu nyingi.
Kama hujampokea na utamani kufanya hivyo fuatiliza sala hii ya mwongozo wa toba kwa kufungua hapa >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
Shalom.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maandiko. Yapo mambo kadhaa ya kujikumbusha pale tunapokuwa wakristo.
Ni lazima tujue kuwa Tunaposema tumeokoka, maana yake ni kuwa tunakuwa tumeingia katika maagano ya ndoa takatifu na Mungu wetu. Mungu anakuwa mume wetu (Yeremia 3:14), na sisi tunakuwa bibi-arusi wake katika roho. Sasa ipo tahadhari ambayo Mungu alishaitoa tangu zamani za kale kwa watu wake alioingia nao maagano, aliwaambia, Mimi ni Mungu mwenye WIVU. Soma Kutoka 20:4-6, utaliona hilo, na kwamba wivu wake ni mbaya na unaweza kwenda hata mpaka vizazi vine mbeleni, kama watu hawatamgeukia yeye. Na hiyo ni kwa kosa tu la kufanya ibada za sanamu.
Unaweza ukajiuliza Mungu muumba wa mbingu na nchi anakuwaje na wivu? Jibu ni kwamba wivu ni sehemu yake, kwasababu sisi wanadamu tuliumbwa kwa mfano wake, na sio yeye kwa mfano wetu, hivyo tabia ya kuwa na wivu katika mahusiano imetoka kwake na sio kwetu..
Na biblia inatuambia ukali wa wivu unazidi hata ule wa ghadhabu au hasira..Ni heri ukutane na mtu mwenye hasira umemuulia ndugu yake, kuliko kukutana na mtu mwenye wivu wa mpenzi wake.
Mithali 27:4 “Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu”.
Na ndio maana tunapaswa tuliweke hilo akilini sisi wakristo, kwasababu wivu wa Mungu ulio juu yetu sisi wa agano jipya ni mkali kuliko ule uliokuwa kipindi cha agano la lake.
Unajua ni kwanini?
Ni kwasababu ya ROHO MTAKATIFU, basi. Ni heri wale waliomtia Mungu wivu jangwani kwa kutengeneza ndama wa dhahabu, na kumwabudu kuliko sisi tunaomtia wivu Roho Mtakatifu leo hii. Pale tunaposema tunapoiacha njia ya wokovu na kwenda kusujudia sanamu tunazozoziita za watakatifu, au tunapokwenda kuzini, au kufanya uasherati, ni ishara kamili kuwa tunamtia wivu Roho Mtakatifu aliye ndani yetu.
1Wakorintho 10: 21 “Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani. 22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?”
Biblia inasema hivi;
Yakobo 4:4 “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.
5 AU MWADHANI YA KWAMBA MAANDIKO YASEMA BURE? HUYO ROHO AKAAYE NDANI YETU HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?
Kama tunavyosoma katika maandiko hayo, kwa lugha rahisi ni kuwa pale Roho Mtakatifu anapoingia ndani yetu, anatupenda upeo, yaani anatupenda sana kiasi kwamba anatuonea wivu mkali pale tunapoyahalifu maagizo ya Mungu kwa makusudi.
Na wivu huo unaweza kumfanya achukue uamuzi wowote mbaya juu yetu; Baadhi yetu anaruhusu hata tupitie magonjwa, wengine hata vifo visivyokuwa vya wakati, na sio shetani bali ni Mungu mwenyewe kasababisha.
Waefeso 4:30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi”.
Lakini Mungu wetu mara nyingi amekuwa ni wa rehema, anaipitishia ghadhabu yake mbali, akingojea mtu mmoja atubu amgeukie.
Hivyo kama wewe ni mmojawapo, ambaye ulikuwa umeokoka ukamuasi Mungu, ukamtia Roho Mtakatifu wivu mwingi kwa matendo yako, na kwamba ulistahili kuhukumiwa, lakini mpaka leo bado unaishi, ni kwa neema tu, hivyo kama upo tayari kugeuka kwa dhati, fahamu kuwa Mungu atakusamehe.
Kwahiyo unachopaswa kufanya ni wewe mwenyewe kufanya maamuzi ya kutubu, kwa kwenda sehemu yako ya siri, utubu mbele za Mungu, kisha, na baada ya hapo anza kuishi kama mkristo wa kweli, kwasababu Mungu ataanza kuyaangalia matendo yako kama kweli umebadilika, hivyo ukiwa umecha kweli kweli, basi ataiondoa hasira ya wivu wake juu yako, na kukuponya kama alikuwa tayari ameshaanza kukurarua.
Hivyo sikuzote kumbuka: Roho hututamani kiasi cha kutuonea wivu. Ni wajibu wetu kuishi kwa makini sana katika ukristo wetu.
Kama umeguswa kushare somo hili au mengine kama haya kwenye magroup ya whatsapp na penginepo, utafanya vyema kufanya hivyo, lakini tunaomba ufanye hivyo bila kubadilisha chochote wala kuondoa anwani ya wingulamashahidi na kuweka namba zako za simu ili kuzuia mkanganyiko. Kwasababu tumepokea malalamiko, kuna watu wasio kuwa na nia ya Kristo, kuchukua masomo na mwisho kuondoa namba au anwani yetu na kuweka namba zao, lengo lao ni kutaka sadaka kutoka kwa watu. (Wingu La Mashahidi hatujawahi kumpigia mtu simu na kumwomba sadaka). Hivyo chukua tahadhari!.
Bwana atubariki sote na kutuzidishia neema yake.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618
Mada Nyinginezo:
JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.
KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?
KWANINI MAISHA MAGUMU?
IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!
IMANI NI KUWA NA UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO.