Category Archive Home

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

Urimu na thumimu ni nini?


Katika Agano la kale Mungu alikuwa akitumia njia kuu tatu aidha kuwasilisha  ujumbe au leta majibu au kuthibitisha jambo..Njia ya kwanza ni manabii, njia ya pili ni ndoto, na njia ya tatu ni Urimu na thumimu.

Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha 1Samweli 28:4  pale ambapo Mfalme Sauli alipokwenda kuuliza kwa Bwana kuhusu vita iliyokuwa inamkabili mbele yake dhidi ya wafilisti, Kama watashinda au La, lakini Bwana hakumjibu kwa njia yoyote kati ya hizo tatu..

1Samweli 28:4 “Nao Wafilisti wakakusanyika, wakaenda kufanya kambi huko Shunemu; naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote, nao wakapiga hema katika Gilboa. 

5 Basi alipowaona hao majeshi ya Wafilisti, huyo Sauli akaogopa, na moyo wake ukatetemeka sana. 

6 Lakini Sauli alipouliza kwa Bwana, Bwana hakumjibu, wala kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa manabii”.

URIMU NA THUMIMU maana yake nini nini?

Urimu maana yake ni “Mianga” Na Thumimu “mikamilifu”..Haya Ni mawe 12 ya aina tofauti tofauti yaliyokuwa yamegundishwa katika ki-mfuko kidogo kilichokuwa kinakaa katika kifua cha kuhani mkuu. Hivyo ikiwa kuna jambo watu wanahitaji kupata uhakika kutoka kwa Bwana basi Mawe haya yalikuwa yanatoa mwanga Fulani unaoakisiana, kuthibitisha jambo hilo, Na hivyo kama jambo hilo sio sawa basi hayakutoa mwanga wowote. Urimu na Thimumu ilikuwa inatoa jibu la mwisho japo si mara zote ilikuwa inatumika.

Kwa mara ya kwanza urimu na thumimu inaonekana katika kitabu cha Kutoka 28:29-30

29 Na Haruni atayachukua majina ya wana wa Israeli katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu juu ya moyo wake, hapo atakapoingia ndani ya mahali patakatifu, kuwa ukumbusho mbele ya Bwana daima. 

30 Nawe utie hizo Urimu na Thumimu katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu; nazo zitakuwa juu ya moyo wa Haruni, hapo atakapoingia ndani mbele ya Bwana; na Haruni atachukua hukumu ya hao wana wa Israeli juu ya moyo wake mbele ya Bwana daima.

Soma tena..

Walawi 8:6 Basi Musa akawaleta Haruni na wanawe, akawaosha kwa maji. 

7 Kisha akamvika Haruni ile kanzu, na kumfunga mshipi, na kumvika joho, na kumvika naivera, na kumfunga huo mshipi wa kazi ya mstadi wa naivera na kumfunga naivera kwa huo mshipi. 

8 Kisha akamtia kile kifuko cha kifuani; akatia hizo Urimu na Thumimu katika hicho kifuko cha kifuani. 

9 Akamvika na kile kilemba kichwani mwake; na juu ya kilemba, upande wa mbele, akakitia kile kipande cha dhahabu, hiyo taji takatifu; kama Bwana alivyomwagiza Musa.

Ukipata tena nafasi Soma  Kumbukumbu 33:8, Hesabu 27:21..

Tunaona tena, wakati mfalme Sauli alipopishana na mwanawe kuhusu kuvunjwa viapo ambavyo alivyoweka, alitaka Mungu ahukumu katikati yao ni nani mwenye makosa, Hivyo alitumia Urimu na Thumimu kuomba uthibitisho huo.

1Samweli 14:41 “Kwa hiyo Sauli akamwambia Bwana, Mungu wa Israeli, [Kwani usimjibu mtumishi wako leo? Ikiwa dhambi i ndani yangu, au ndani yake Yonathani mwanangu, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, utoe Urimu; bali ukisema hivi, Dhambi i katika watu wako Israeli,] utoe Thumimu ,Basi Yonathani na Sauli wakatwaliwa,lakini watu wakapona”.

JE! URIMU NA THUMIMU iliendelea kudumu muda wote?

Wakati wana wa Israeli wanachukuliwa tena utumwani Babeli, na hekalu la Mungu kubomolewa, ndio ilikuwa mwisho wa kutumika kwa urimu na thumimu. Hata waliporudi na kujenga upya nyumba ya Bwana, kitendo hicho hakikuonekana kikitendekea tena katikati ya makuhani.

KATIKA AGANO JIPYA URIMU NA THUMUMI NI NINI?

Kama vile ilivyokuwa katika agano la kale, ili kuthitisha jambo ilikuwa ni lazima mawe yale yatoe mwangaza Fulani wa tofuati, vivyo hivyo katika agano jipya Urimu na thumimu yetu ni BIBLIA TAKATIFU. Kila Neno, kila ndoto au kila unabii, kabla haujapokelewa au kuaminiwa ni lazima kwanza uletwe kwenye biblia ambayo ndio Urimu na Thumimu yetu..Na unabii huo au ndoto hiyo kama haipatani na maandiko basi tunapaswa tuukate ufunuo huo haijalishi utaonekana unao uhalisia mkubwa kiasi gani.

Katika nyakati hizi za mwisho shetani anabuni njama mpya za kuwadanganya watu kila siku kwa kivuli cha Neno Ufunuo..Kila mmoja anasema nimefunuliwa..hata jambo ambalo linaonekana linakiuka misingi ya Imani ya kikristo mtu anasema amefunuliwa.. Ni kweli tunayahitaji mafunuo ili tuyaelewe maandiko, lakini kila ufunuo  ili ukubalike ni lazima upatane na Urimu na Thumimu yetu ambayo ni biblia.

Upotashaji uliopo.

Lakini utajiuliza mbona, nabii yule alipokutabiria hivi au vile ni kweli vilitokea kama vilivyo na leo  hii kakupa tena maagizo mengine uachane na mume wako au mke wako ukaoane na mwingine..Nataka nikuambie kama Neno la Mungu likiwa halijakaa vizuri ndani yako unaweza kumsikiliza ukadhani kuwa ni maagizo ya Mungu, ukamwacha mke wako ukaenda kuoa mwingine au kuoelewa na mwingine, kisa tu nabii kasema, na kisa tu alishakutabiria kipindi cha nyuma na jambo Fulani likawa ni kweli..

Lakini wewe kwa kukosa ufahamu wa kimaandiko, hujui kuwa unakwenda kuishi katika uzinzi, umeshachukuliwa na maji, kwasababu biblia inasema mtu amwachae mke wake na kwenda kuoelewa na mwingine azini..

Marko 10:11  “Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;

12  na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini”.

Ndugu yangu embu soma maandiko haya upate picha halisi ya kitu  ninachokuambia..

KUMBU: MLANGO 13

1 Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, 

2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; 

3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote. 

4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye. 

5 Na yule nabii, au yule mwotaji wa ndoto, na auawe, kwa kuwa amesema yaliyopotoka juu ya Bwana, Mungu wenu, aliyewatoa katika nchi ya Misri, akakukomboa katika nyumba ya utumwa, apate yule mtu kukupotoa katika njia aliyokuamuru Bwana, Mungu wako, uiendee. Ndivyo utakavyouondoa uovu utoke katikati yako. 

Unaona? Tunapaswa kabla ya kupokea Neno lolote au unabii wowote, tuutazame je unakubaliwa na Urimu na thumimu yetu (yaani biblia) au La. Tukizingatia hayo tutakuwa tumejiweka katika nafasi nzuri ya kuzishinda kirahisi hila za shetani katika nyakati hizi za mwisho ambazo anazileta kupitia   manabii wake na walimu wake wa uongo, katika siku hizi za mwisho. Mfano tena mtu anaweza akaja akakwambia kata mti huu au ule, unasababisha vifo vya wababa katika familia au ngo’a ua hili au lile, linatunza majini, au usifuge paka, au njiwa wanatumiwa na wachawi n.k. .

Mafundisho ya uongo.

Yote hayo ni mafundisho au mafunuo yaliyotoka kuzimu ambayo hayana msingi wowote wa kimaandiko, Zaidi tu yanawafanya watu waishi Maisha ya woga na wasiwasi wakidhani kuwa vitu vya nje vinaweza kuathiri Maisha yao rohoni, na kusahau kuwa asili ya laana zote zipo rohoni pale mtu anapokuwa mbali na muumba wake, anapotenda dhambi ndipo anapokumbana na laana. Na mafunuo mengine mengi ya namna hiyo..

Leo hii umeshaijua urimu na thumimu yako(BIBLIA), Hivyo jambo lolote linapokujia lipime kwanza na maandiko.

Je! Umeokoka? Je unafahamu kuwa tunaishi katika kizazi ambacho dalili zote zinaonyesha kuwa tutashuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa YESU KRISTO?. Je! Una habari kuwa hili ndio kanisa la saba na la  mwisho lijulikanalo kama LAODIKIA tunaloishi(Ufunuo 3), na baada ya hili hakutakuwa na kanisa lingine mbeleni. Je! Unataarifa kuwa Israeli imeshachipuka, na hii neema siku si nyingine itarudi kwao na ikisharudi kule, upande wetu mlango wa neema utakuwa umeshafungwa?

Unaona tupo katika hatari kubwa kiasi gani..Unasubiri nini usiokoke..Usimpe Kristo Maisha yako.. Huu ulimwengu umekupa faida gani tangu uanze kutaabika nao, Lakini Kristo anakuahidi amani idumuyo isitoshe anakupa na uzima wa milele juu.. Hakuna mwanadamu yoyote anaweza kukuahidia mambo mazuri kama hayo.

Yeye mwenyewe anasema..

Mathayo 11:28  “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30  kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”

Unaona? Amekuahidi mizigo yako yote ataitua, yeye hasemi uongo, ukiwa utakuwa tayari tu kumpokea muda huo huo anaanza kufanya kazi ndani yako ya kukugeuza..Hivyo usifanya moyo wako kuwa mgumu, chukua uamuzi huo sasa..

Kama upo tayari kufanya hivyo kumpa Bwana Maisha yako…

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Zingatia hayo na Bwana atakuwa pamoja nawe. Vilevile Usiacha kutembelea Website hii  https://wingulamashahidi.org mara kwa mara ili ujifunze maneno ya uzima..

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Zile tunu (Dhahabu, uvumba na manemane) Mamajusi walizozitoa kwa Bwana (Mathayo 2) . ziliwakilisha nini?

Je! sisi ni wafalme na makuhani kwa namna gani?

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

Usipokuwa mwaminifu sasa, nafasi yako itachukuliwa na mtu mwingine.


Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Mkuu wa Uzima libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia Neno la Mungu..Taa iongozayo miguu yetu na mwanga wa njia zetu.

Leo tutajifunza madhara ya kutokuwa mwaminifu katika kazi ya Mungu… Kuna tofauti ya utendaji kazi kati ya mtu na mtu…Mtu anatenda kazi ya Mungu kulingana na karama aliyopewa. Hivyo kama mtu kapewa karama Fulani halafu karama ile haitumii au anaitumia isivyopaswa basi kuna madhara makubwa sana…Na moja ya dhara hilo ni nafasi yake kunyang’anywa na kupewa mwingine.

Na kitu cha kuogopesha ambacho watu wengi hawakifahamu ni kwamba Mungu kamwe hamnyang’anyi mtu karama…bali anamnyang’anya ile huduma…Yaani ile Neema ambayo Mungu angetembea naye kwa karama aliyompa..Neema hiyo anapewa mwingine ambaye atazaa Zaidi lakini yule mtu ataendelea kukaa na karama yake ile ile lakini hatatumika katika viwango ambavyo Mungu alikuwa amemkusudia atumike. Kama alikuwa na karama ya kinabii..ataendelea kuona maono..Lakini lile kusudi kuu ambalo Mungu alilikusudia kumtumia kwa karama ile linahamishiwa kwa mtu mwingine.

Katika Biblia tunamwona mtu mmoja aliyeitwa SAULI ambaye alipakwa mafuta na Mungu mwenyewe, na Roho wa Mungu akamshukia juu yake kwa nguvu ile awe mtawala juu ya Israeli. Lakini pamoja na kuwa alitiwa mafuta na Mungu mwenyewe na Mungu alimnyanyua kutoka chini, na kupewa uweza na nguvu nyingi..lakini mtu yule hakuitumia vyema nafasi yake, aliacha kumheshimu Mungu na kumtii…Mungu akimwambia afanye hivi..yeye anafanya vile..na kile asichopaswa kukifanya ndicho alichokuwa anakifanya, na alikuwa anafanya vile kwa makusudi. Jambo ambalo lilimhuzunisha Mungu na kufikia hatua ya kuondoa nafasi yake na kumpa mtu mwingine.

1Samweli 15:24 “Ndipo Sauli akamwambia Samweli, Nimefanya dhambi; maana nimeihalifu amri ya Bwana, pia na maneno yako; kwa sababu naliwaogopa wale watu, nikaitii sauti yao.

25 Basi sasa, nakuomba, unisamehe dhambi yangu; rudi pamoja nami, nipate kumwabudu Bwana.

26 Samweli akasema, Sitarudi pamoja nawe; kwa sababu umelikataa neno la Bwana, Bwana naye amekukataa wewe, usiwe mfalme wa Israeli.

27 Naye Samweli alipogeuka, aende zake, Sauli akaushika upindo wa vazi lake, nalo likararuka.

28 Basi Samweli akamwambia, Leo Bwana amekurarulia ufalme wa Israeli, naye amempa jirani yako, aliye mwema kuliko wewe.

29 Tena Yeye aliye Nguvu za Israeli hatanena uongo, wala hataona majuto; maana siye mwanadamu, hata ajute”.

Wakati Sauli anaidharau hiyo nafasi aliyowekwa..Tayari Mungu alikuwa ameshamwandaa Daudi kuichukua nafasi yake.

Sulemani naye baada ya kutumika kwa muda mrefu..ilifika kipindi akakengeuka na kuitumikia miungu migeni jambo ambalo ni kinyume na maagizo ya Mungu..Nafasi yake naye ikachukuliwa na mtumishi wake.

1Wafalme 11:11 “Kwa hiyo Bwana akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo, wala hukuyashika maagano yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako”.

Na ipo mifano mingine mingi katika biblia..lakini wa mwisho tunausoma ni wa Yuda aliyekuwa mwanafunzi wa Yesu. Huyu naye alipewa nafasi katika huduma ya Kristo..lakini aliichezea na kuidharau nafasi ile..na mwishowe kufungua mlango wa roho ya shetani kumwingia ili kumsaliti Bwana..Na siku zote kazi ya Mungu haipwayi..

Wala hakuna mtu maalum kwa Mungu..ukikataa kumtumikia Mungu sasa..basi Mungu anao watu wengi, nafasi yako inachukuliwa na mtu mwingine…Yeye hana mtu mmoja tu au watu Fulani kadhaa anaowategemea kwamba wakikosekana hao basi kazi yake haiendi mbele. Nataka nikuambie hata Paulo angeukataa wito wa Mungu angenyanyuka mtu mwingine kuifanya kazi kama ile ile ya Paulo kwa wakati ule ule..Lakini Paulo na wengine wamekuwa vile walivyo kwasababu waliutii utumishi wa Mungu na kuuheshimu.

Matendo 1:15 “Siku zile akasimama Petro kati ya hao ndugu (jumla ya majina ilipata mia na ishirini), akasema,

16 Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu;

17 kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii.

18 (Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka………20 Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo;

21 Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu,

22 kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.

23 Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya.

24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

25 ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. 26 Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.”

Umeona?..Mungu hakufanya kazi ya hasara…kumbe wakati Yuda anaanza kufikiria kumsaliti Bwana..Tayari Mungu alikuwa ameshaandaa mtu wa kuichukua nafasi yake tangu wakati ule ule…Huyu Mathiya alikuwa na Yesu tangu ubatizo wa Yohana mpaka kupaa kwake…alikuwa ameshawekwa tayari kuichukua nafasi ya Yuda.

Hata sisi leo hii, wapo watu waliowekwa tayari kuzichukua nafasi zetu, tangu siku ile tulipookoka..Tunapozichezea hizi nafasi tulizopewa sasa katika kumtumikia Mungu, katika kuhubiri injili, katika kuihudumia Injili..Siku inafika kinara kitaondolewa na kupewa mwingine ambaye tayari alikuwa ameshaandaliwa.

Mifano hiyo tuliyojifunza ni ya kwenye biblia..lakini tunaweza kujifunza mfano mwingine katika mtu wa nyakati zetu..Na huyu si mwingine ya Mhubiri wa Mungu mashuhuri Reinhard Bonnke…ambaye wengi wetu tunamfahamu, ambaye wiki kadhaa nyuma tulisikia habari za kufariki kwake. Huyu mwanzoni mwa huduma yake kabla hajaingia kwenye kazi ya kuwavuna mamilioni ya watu kwa Kristo, alikuwa anasua sua kidogo. Mungu anamwita kufanya kazi ya kupeleka injili kwa mataifa ya Afrika ili mamilioni waokolewe..lakini yeye akawa anakawia kawia na kujishauri shauri kana kwamba yeye ni mtu maalumu sana.

Wakati bado yupo anajifikiria fikiria, siku moja alisikia sauti inamwambia “nafasi hiyo nimekupa kwasababu kuna mwingine alipewa akaikataa, na wewe ukiikataa atapewa mtu mwingine”. Baada ya kusikia hivyo aliogopa sana..Ndipo akaamua kwa gharama zote kuifanya kazi ya Mungu ili nafasi yake isichukuliwe na mwingine..Na matokeo ya kutii kwake ndiyo tunayoyaona leo,..Mungu alimtumia kuvuna mamilioni ya watu Afrika waliokuwa wanakwenda kuzimu.

Hivyo na sisi tunajifunza..Kamwe tusijione ni watu maalum mbele za Mungu. Kamwe tusijidhanie ni sisi tu ndio Mungu anao..Mungu anao watu wake wengi, ambao wapo tayari kwa utumishi wake..Eliya Mtishbi kuna kipindi alikwenda kusimama mbele za Mungu na kumwambia.. “Ni mimi tu peke yangu nimebaki nabii wako” ..lakini Mungu alimwambiaje?

Warumi 11: 3 “Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu.

4 Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali”.

Leo hii unajiona una kipawa cha kuimba..Wewe ukiimba watu wanatubu, lakini unavaa vimini, unapiga make-up, unavaa nusu uchi, ni mwasherati kwa sirisiri..umeonywa mara kadhaa lakini hutaki kusikia…Nataka nikuambie kamwe usijifikirie upo peke yako..Nafasi yako atapewa mtu mwingine.

Wewe ni Mchungaji, au Mwalimu, au Nabii au Mtume au Mhubiri…lakini chini kwa chini ni mwasherati, chini kwa chini ni unalivuruga kundi, chini kwa chini ni mtu wa kupenda anasa na mapato ya udhalimu, chini kwa chini ni mzinzi..unadhani Mungu hakuoni..Utamficha mwanadamu lakini si Mungu…Nafasi yako itachukuliwa na mwingine na pengine hata imeshachukuliwa hujui tu!..Unaweza ukawa bado unaendelea kuota ndoto, unaendelea kuona maono, unaendelea kuimba vizuri hiyo siyo hoja!…

Hata Sulemani aliponyang’anywa ufalme wake hakuondolewa kila kitu alibakishiwa hekima yake…hata Sauli aliponyang’anywa ufalme wake hakupokonywa siku hiyo hiyo alikufa akiwa mfalme, lakini kumbe tayari utukufu wa Mungu ulikuwa umeshamwondokea…Hata Yuda nia ya kumsaliti ilipoingia ndani yake Bwana hakumfukuza aliendelea kutembea naye lakini, utukufu ulikuwa tayari umeshamwondoka na siku ya mwisho alipasuka matumbo.

Hivyo sikia maonyo ya Mungu leo mtu wa Mungu, na Bwana azidi kutusaidia tudumu katika Neema yake kithabiti. Tukikumbuka kuwa muda tuliona nao ni mchache..Kristo yu malangoni kurudi.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.

UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI

MPINGA-KRISTO

UNYAKUO.

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?

Unamalizaje mwaka wako?.Unamtukazaje Mungu katika sikukuu hizi na mwisho wa mwaka wako?


Ilikuwa ni Disemba 24, 1964, jaribio la kwanza la wanasayansi la kusafiri kutoka katika obiti (muhimili) wa dunia na kuelekea katika obiti ya mwezi..Ni jaribio ambalo lilikuwa ni la kwanza na la hatari sana, kiasi kwamba ingetokea tu injini moja ya chombo cha wana anga hao kufeli basi watu hao ndio wangepotea milele katika anga za mbali..

Tukio hilo la kuondoka kwao lilishuhudiwa na dunia nzima siku hiyo, watu wakiwa na shauku ya kuona ni nini kitatokea, katika ziara hiyo ya masafa ya mbali ya anga, vyombo vyote vya habari vilikuwa wazi na televisheni zote wakizungumzia safari hiyo ambayo ilichukua takribani siku tatu kuifikia orbit ya mwezi,..Sasa wana anga hao wakiwa tayari wameshaingia katika obiti ya mwezi wakijiandaa kuizunguka mara 10 Wakiwa kule angani kuchukua picha za matukio kitendo cha kuishuhudia “Dunia kunyanyuka”..Sio “Mwezi kunyanyuka” kama tulivyozea huku kuona mwezi ukinyanyuka kutoka mashariki mpaka kufika angani..Wao walifika hatua hiyo ya kushuhudia na kuchukua video ambayo ipo mitandaoni hadi leo jinsi dunia inavyoonekana kwa mbali ikinyanyuka kutoka katika pembe za mwezi hadi juu kama vile mwezi unavyonyanyuka kutoka katika pembe za dunia..

Lakini sasa wana anga wale 3, wakiwa wanajiandaa kutoa ripoti hiyo..Walikatisha matangazo yao..wakiwa sasa kule kule angani wakaiambia Dunia maneno haya..

Nukuu.

“Wakati tunakaribia kushuhudia tukio hili kuu, timu yetu ya Apollo 8 tunao ujumbe tunataka tuwaambie watu wote mlio katika dunia.. Na ujumbe wenyewe ndio huu..

1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.

5 Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.

6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.

7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo. 8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.

9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.

10 Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.”

Walipomaliza kuisoma mistari hiyo ya kitabu cha Mwanzo 1:1-10 wote watatu, walifunga biblia zao kwa kusema maneno haya:

“Sisi kama timu ya Apollo 8, tunamalizia kwa kuwaambia muwe na usiku mwema, wenye amani, na Heri ya krisimasi, Mungu awabariki wote, wote mlio katika dunia nzuri.”

Mwisho wa Nukuu.

Ikiwa utapenda kusikia audio hiyo basi bofya link hii.>>

Maneno hayo yaliugusa moyo wa ulimwengu mzima kwa wakati ule.. Na kuwafanya watu wengi, wajifikirie mara mbili juu ya Maisha yao ya rohoni, ikiwa wanasayansi wanaukiri utukufu wa Mungu wakiwa maelfu ya kilometa mbali na dunia..Inatupasaje sisi?..

Watu wale waliporudi salama duniani, Habari zao zikavuma sana, ndio waliowekwa kuwa watu wa mwaka kipindi hicho..

Kama hiyo haitoshi mwaka mmoja baadaye..timu nyingine ya wanasayansi wa anga (Astronauts) iliyojulikana kama Apollo 11,nayo ya watu watatu, ilifunga safari nyingine tena, lakini awamu hii sio kama ile ya kwanza ya kuuzunguka mwezi, bali hii ilikuwa ni kutua kabisa mwezini kwa mara ya kwanza..

Safari ilianza July 20, 1969 na ilipofikia July 21 walikuwa wameshafika katika uso wa mwezi..muda mchache tu baada ya kutua, mmojawapo kati ya wale watatu aliitoa divai yake na mkate wake, aliyoichua kutoka kanisani mwao..akamwomba kamanda wake wasitishe matangazo yote kwa muda, jambo lisilo la kawaida aliashiriki meza ya Bwana akiwa kule mwezini..Na alipomaliza aliomba wasikilizaji wake wote duniani wasikilize anachowaambia..

Akausoma mstari huu kwa nguvu dunia nzima ikiwa inasikia..

Yohana 15:5 “Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote”.

Akafunga biblia yake..wakaendelea na shughuli za kule mwenzi Na Walipomaliza shughuli zao baada ya masaa kadhaa, wakawasha chombo chao, wakaondoka..Sasa akiwa wanauacha mwezi, huku wakiangalia magimba ya ajabu Mungu aliyoyaumba angani..huyu mwanaanga aliyeitwa Buzz Aldrin.

Akaifungua tena biblia yake, akasema ninao ujumbe bado kwa dunia yote…huku mamilioni ya watu duniani wakiwasikiliza akasoma tena mstari huu..

Zaburi 8:3 “Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha;

4 Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie”

Haleluya!!..Kama ilivyo ada maneno hayo yaliigusa mioyo ya watu wengi duniani..wakisema ikiwa watu hawa wanafanikiwa katika mambo makubwa kama haya, Lakini bado hawaachi kuitangaza mauti ya Kristo, na utukufu wa Mungu..Inatupasaje sisi ambao hatujafika popote?

Kama ulikuwa hujui hawa ndio waliokuwa wanadamu wa kwanza na wa mwisho kutua mwezini..Lakini katika mafanikio yao hawakuacha kumtukuza Mungu..hawakuacha kuyatimiza maagizo Kristo aliyowapa kama wakristo pasipo kujali hali na mazingira..

Embu tujiulize Watu kama hawa Mungu ataachaje kuwafikisha mbali ikiwa wanaiadhimisha Krisimasi yao kwa kuutangaza utukufu wa Mungu, wanafunga mwaka kwa kuubariki uumbaji wa Mungu..

Hata wakiwa mwezini mahali ambapo hapana oxyjeni, kusikoweza kuishi kiumbe chochote mkristo huyu haachi kuishiriki meza ya Bwana, wanaithamini damu ya Emanueli iliyomwagika pale Kalvari kwa ajili yao miaka 2000 iliyopita..Na sisi Je tutapate kupona tusipouthamini wokovu mkuu namna hii..

Wewe na mimi hatujawahi kufika mwezini, hatujawahi kuona hata mambo makubwa na ya kustaajabisha, wala hatuna elimu ya juu na utajiri wa kuwafikia watu hawa na taifa lao, ambao kimsingi ndio wangepaswa wawe wakwanza kusema hakuna Mungu lakini kinyume chake katika mafanikio yao ndio wanaokuwa wa kwanza kumuhubiri Kristo..

biblia inatuambia…

Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu..”

Na wewe Je! Bado unafikiria kuumaliza mwaka wako bar, au guest? Au Disko? Au Casino? Au kwenye kumbi za starehe?…Kumbuka hawa ndio watakaotuhukumu siku ile.. Ni heri ukaufunga mwaka wako kwa Bwana na kusema kuanzia leo nimeamua kumfuata Kristo kwa moyo wangu wote.

Ukifanya hivyo kwa kumaanisha kabisa, atakupokea, ameahidi hivyo katika Neno lake kuwa yeyote aendaye kwake hatamtupa nje kamwe..(Yohana 6:37).Na yeye si mwongo mwongo kama sisi.

Unasubiri Nini tubu leo dhambi zako kabla ya kuingia mwaka huu mpya..Ukabatizwe katika ubatizo wa kimaandiko wa kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako, kisha Bwana akupe kipawa cha Roho wake Mtakatifu kukulinda na kukuongoza hadi siku ile ya mwisho wa Maisha yako kama unyakuo utakuwa haujapita..Usisieme mimi ni wa dini hii, au ile hivyo siwezi kuwa mkristo, wala usiseme mimi dhehebu langu ni hili, hivyo siwezi kuokoka..Wokovu ni mlango wa wazi kwa watu wote..na wokovu ni wa lazima! Kama tunapenda maisha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Shalom.

Mada Nyinginezo:

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

SAA YA KIAMA.

CHAPA YA MNYAMA

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.

Shalom.Karibu tujifunze Biblia..Neno la Mungu linasema katika 1Timotheo 6:20 “ Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo”.

Moja ya vitu vinavyobomoa Imani au vinavyomharibu mtu au vinavyoharibu huduma ni mashindano ya dini. Aina yoyote ya mashindano ya dini yanaasisiwa na shetani mwenyewe.

Na chanzo kikubwa cha mashindano ya dini ni Ujuzi wa mambo Fulani. Inapotokea mtu anafahamu kitu Fulani ambacho anahisi mwingine hajakifahamu au anahisi mwingine hafanyi kama inavyostahili….Mtu huyu Ule ujuzi unaweza kumletea kiburi na ni rahisi kuzaa majivuno na mwishowe mashindano..

Biblia inasema hivyo katika 1Wakorintho 8:1 “… Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga”.

Baadhi ya mashindano hayo ambayo yametengenezwa na shetani mwenyewe katika hizi siku za mwisho ni haya.

  • Mashindano kati ya uislamu na ukristo.
  • Mashindano ya Yesu ni Mungu au si Mungu
  • Mashindano ya kushindania siku ya kuabudu kama ni jumapili, au jumamosi
  • Mashindano ya kula nyama ya nguruwe n.k
  • Mashindano ya dhehebu la kweli la kuabudu.

Yapo mengi lakini hayo ndiyo yanayoshika nafasi za juu..Utakuta watu wanabishana tangu asubuhi mpaka jioni kila mmoja akitaka kumthibitishia mwenzake kwamba yupo sahihi na kwamba yeye anajua Zaidi.

Sasa kama ukichunguza mwisho wa mabishano hayo ni magombano au kutukanana au kudhihakiana au kuwekeana vinyongo au kupigana au Kuumizana au kuaibishana… Na mabishano hayo huwa hayaishagi..utaona yametulia tu kidogo baada ya masaa kadhaa au hata siku kadhaa yanaanza tena..kila mmoja kaenda kukusanya point zake mpya huko alikokwenda..na anarudi kwenye uwanja wa mapambano upya!..na mashindano yanaanza tena.

Kamwe hutaona katika hayo mazungumzo pamoja na point zao zote wanazozitoa na kukosoana..hutaona hata mtu akitubu, hutaona mtu akigeuka na kusema asante Bwana kwa kunifumbua macho!..hutaona mtu akitoka na moyo wa furaha na upendo na uchangamfu!.. Sasa ikiwa kama matunda ya Roho hayapatikani katikati ya hayo mazungumzo unategemea vipi yawe mazungumzo ya ki-Mungu?..Ni wazi kuwa ni mazungumzo ya kishetani…kwasababu mazungumzo ya kishetani ndiyo yanayozaa hasira, vinyongo, chuki, wivu, matusi, dhihaka, kuaibishana n.k

Biblia imetuonya sehemu kadha wa kadha juu ya mashindano ya dini..kwamba tuyaepuke..

2Timotheo 2:14 “Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao”.

Sasa swali linakuja… kama je! Unafahamu jambo ambalo unaamini ni sahihi na unataka kumshirikisha mtu asiyelijua na unapoanza tu kumshirikisha anaanza kushindana na wewe..katika hali hiyo unafanyaje?.

Jibu: Unapokutana na mtu ambaye unapomweleza ukweli hataki kusikia, jambo la kwanza yeye ni kupinga na kutaka kuleta mashindano..katika hali kama hiyo wewe unayemhubiria unahitaji kuwa na hekima..Hapo unapaswa ujishushe uwe mpole…Hakuna mtu asiyempenda mtu mpole au anayejishusha!..Unaanza kumweleza kwa upole na kwa utaratibu…Yule mtu akiona upole wako na utaratibu wako, akiona amekutupia tusi umenyamaza hujamrudishia..amekulaani umetulia kimya…hawezi kuendelea kukutukana wala kukupazia sauti, anapoona hakuna muitikio upande wa pili..hivyo atatulia na kukusikiliza..na moyoni atajua kuwa wewe hujaja kushindana naye bali umekuja kumfundisha..hivyo atakuheshimu, hata kama hatakubaliana na wewe katika baadhi ya points lakini hatashindana na wewe!…

Sasa taratibu ataanza kukusikiliza na Roho wa Mungu atamshuhudia ndani yake kwamba unayoyasema ni kweli…hata kama hatayakiri hapo mbele yako lakini baadaye atakapokwenda kutafakari atagundua kuwa ni kweli.

Lakini pale tu unapokutana naye na kuanza kujionyesha kwamba wewe unajua Zaidi yake, na anapotoa maneno ya kutukana unachokiamini na wewe unatukana anachokiamini, anapokurushia mshale na wewe unajibu mapigo kwa kutumia mistari..hapo tayari utakuwa umeshawasha moto wa mashindano na kamwe hamtafikia suluhu..ataishia kusema wewe ni mbishi na hujui lolote, hata kama unachozungumza kina ukweli kiasi gani.

1Petro 3:15 “Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu”.

Mungu hawezi kamwe kuwepo mahali penye machafuko kama Neno lake linavyosema katika..1 Wakorintho 14: 33 “Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu”. Hivyo katika kuhubiri au kushuhudia au kumshirikisha mtu jambo Fulani ni lazima pawepo na hali ya utulivu ndipo Roho Mtakatifu aweze kuwepo katikati yetu kutuhudumia.

Na Zaidi ya hayo, wapo watu ambao wamepandikizwa na shetani mwenyewe katika kumharibu mtu wa Mungu ambaye amesimama katika Imani ili aonekane ni mwovu..Na watu hao ni watu wa kuanzisha ubishi, ambao kazi yao kubwa ni kwenda kumchochea mtu aliyesimama abishane au agombane ili watu wengine wanaomzunguka wamwone kuwa si kitu, ni mtakatifu feki!..na waishie kutomsikiliza tena…Watu wa namna hiyo watakuja tu na kuanzisha mada na kukutaja wakitaka mchango wako..lakini lengo lao ukiwasoma si kutaka kujifunza bali kubishana na wewe…Watu kama hao wameanzisha mada na umejaribu kuwajibu kwa upole na hawaonyeshi kuelewa hao biblia imeturuhusu tuwakatae…Tusizungumze nao, wakituhoji ni ruksa kutowajibu….Wengi wa hao wametumwa na shetani kabisa kufanya hiyo kazi.

Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana”

Hivyo mijadala ya mashindano tujiepushe nayo, mijadala ya kushindania mistari ya biblia tujiepushe nayo na mijadala ya kila aina ambayo mwisho wake ni ugomvi na makelele tujiepushe nayo vilevile…

2Timotheo 2:23 “Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi.

24 Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu;

25 akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli;

26 wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake”

Bwana atusaidie katika kulitimiza na hilo pia..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UFUNUO: Mlango wa 1

DANIELI: Mlango wa 1

ESTA: Mlango wa 1 & 2

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini biblia inasema mtu wa rohoni huyatambua yote?

SWALI: Mstari huu una maana gani? 1Wakorintho 2:15 “Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu”?


JIBU: Ukianza kusoma kuanzia ile mstari wa kwanza utaona mtume Paulo, akieleza vizuri maana halisi ya kuwa mtu wa rohoni.. mtu wa rohoni sio mtu anayeona wachawi, au anayeota ndoto, au anayeona maono, mtu anaweza akawa na vipawa hivyo vyote lakini bado asiwe ni mtu wa rohoni.

Kulingana na mistari hiyo mtu wa rohoni ni mtu aliye na ufahamu wa kuzitambua siri za Mungu kwa Roho Mtakatifu. Na siri kuu ya Mungu ipo katika kumjua Yesu Kristo, ambayo biblia inasema kama watawala wa dunia hii wangeijua , wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu;(1Wakorintho 2:8)..

Unaona, wangejua kuwa suluhisho la mambo yote lipo kwa Yule, maarifa yote na siri zote walizokuwa wanazitafuta kwa miaka na miaka zipo kwa Yule, wasingemsulibisha…biblia inaeleza kabisa..Lakini walifumbwa macho yasione, hivyo wakabakia kuyatambua mambo ya mwilini tu.

Yohana 12:37 “Walakini ajapokuwa amefanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, hawakumwamini;

38 ili litimie lile neno la nabii Isaya alilolisema, Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu; Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?

39 Ndiyo sababu wao hawakuweza kusadiki; kwa maana Isaya alisema tena,

40 Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakafahamu kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya.

41 Maneno hayo aliyasema Isaya, kwa kuwa aliuona utukufu wake, akataja habari zake”.

Hivyo ukiona wewe kila siku unamjua Kristo katika viwango vingine, basi ujue kuwa wewe ni mtu wa rohoni mwenye viwango vya hali ya juu..Ukiona kila usomapo Biblia unaziona habari za Yesu, kila ukitazama vitu vya asili unaiona injili ya Yesu, kila Ukitazama Maisha ni kama unayasikia maneno ya Yesu yanazungumza na wewe masikioni yanakuonya kila unalotaka kulifanya unatamani liwe linalompendeza Yesu… hapo wewe ni mtu wa rohoni…Na sio ukisoma biblia unaona wachawi, au ukisali unaona wachawi hapo bado hujawa mtu wa rohoni.

Na ndipo hapo biblia inasema.. mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu.. Utakuwa na uwezo wa kuyatambua mambo yote, na siri zote za Mungu wanadamu wasizozijua…hakuna jambo lolote litakuwa ni jipya machoni pako na zaidi ya yote bado utakuwa hautambuliwi na yeyote.. Yaana maana yake, hakuna mwanadamu yeyote mwenye tabia ya asili atakayeweza kukutambua, akikuangalia ataishia tu kuona vya nje, watasema umerukwa na akili kama vile Paulo alivyoambiwa, wengine watasema una mapepo, kama vile Yohana Mbatizaji alivyoambiwa..Wengine watakauambia umelogwa..

Ni kwasababu ufahamu wao umeishia hapo kwenye mambo ya nje, hawawezi kuona zaidi ya hapo..furaha na tumaini lililopo ndani yako..Hawajui kuwa ndani yako ni Roho Mtakatifu anakufundisha, lakini wewe utakuwa na ufahamu wa kuelewa yao yote. Utagundua kuwa wanavyokufikiria wewe sivyo ulivyo.

Hivyo upo umuhimu wa kumpa Kristo maisha yako, kama hujampa au kama ulishampa hapo kabla na ukapoa ni wakati wa kuweka mambo yako sawa..Ili Roho wa Mungu awe na nafasi ya kukufunulia yale usiyoyajua kuhusu Bwana Yesu Kristo.

Ubarikiwe.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye namba hizi: +255789001312/ +255693036618

  

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

TUTAMKARIBIA MUNGU KWA IDADI YA MVI ZETU ROHONI.

Rudi Nyumbani

Print this post

KUOTA UNAFANYA TENDO LA NDOA.

Kuota unafanya tendo la ndoa au kuota unafanya mapenzi na mtu usiyemjua maana yake ni nini?


Awali ya yote tunapaswa kufahamu kuwa Ndoto yoyote ya zinaa, haitokani na Mungu..Ni aidha inatokana na mtu mwenyewe au shetani. Leo tutaangazia makundi mawili ya watu wanaoota ndoto za namna hii:

Kundi la kwanza ni: Kwa mtu ambaye hajaokoka:

Biblia inasema..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;…”

Hii ikiwa na maana kuwa, yale mambo au vile vitu tulivyokuwa tunavifanya au kuvifikiria mchana kutwa mara nyingi huwa ndio hivyo hivyo tunaviota tukiwa tumelala..

Hata kama hatutaviota vilevile kama vilivyo lakini tutaota mambo yanayoendana na matukio tuliyokuwa tunayafanya katika mazingira yanayotuzunguka..Kwamfano kama wewe wiki nzima ulikuwa unashinda mashambani tu kulima na kupalilia shamba lako..Uwezekano wa wewe kuota upo shambani unafanya shughuli kama hizo ni mkubwa sana..Kama wewe ulikuwa shuleni mwaka mzima bwenini uwezekano wa kuendelea kuota ndoto upo shuleni ni mkubwa..

Vivyo hivyo kama wewe ni mlevi unayeshinda bar kila siku usiku uwezekano wa kuota ndoto za upo bar unakunywa pombe na marafiki zako ni mkubwa..Haiwezekani mtu ambaye hajawahi kuenda bar au kunywa pombe Maisha yake yote akaota anakunywa pombe bar na akalewa. Vivyo hivyo hata katika zinaa, kama Maisha yako yote, na wakati wako wote unawaza uzinzi kichwani, unatazama picha chafu mitandaoni, na video za pornography, unafanya mustarbation, unaangalia muvi za mapenzi, unasiliza nyimbo za kidunia za kizinzi, maneno unayozungumza kila mara ni ya usherati tu, jinsi ya kumpata binti yule au kaka yule..Nataka nikuambie kila siku usiku kuota unafanya tendo la ndoa au unafanya mapenzi na mtu usiyemjua au unayemjua itakuwa ni jambo la kawaida kwako.

Kwasababu Maisha yako yote yapo katika uzinzi..Shughuli kubwa iliyo katika ubongo wako ni zinaa..

Vilevile yapo mapepo ya namna hii mahususi kutoka kuzimu yanawavaa watu ambao hawajaokoka ili kuchochea hii hali ndani yao. Ndio hapo utamwona mtu ndoto kama hizi zinakuwa ni sehemu ya Maisha yake, anajikuta mara kwa mara anafanya mapenzi na mtu asiyemjua, leo,Kesho, anapumzika wiki moja hali ile ile inajirudia tena na tena, ukiona hivyo ujue lipo pepo limeshakuvaa.

Unahitaji kugeuzwa Maisha yako.

Kundi la Pili: Kwa mtu aliyeokoka.

Lakini kama wewe upo ndani ya Kristo.

Mambo mawili yanaweza yakawa yanahusika.

La Kwanza. Ni ishara ya kuwa kuna mahali unapoa,.Umepunguza kiwango chako cha nguvu za rohoni, kuna mahali unapadokoa au baadhi ya mambo kidunia yanakuchukua..Hivyo hapo unapaswa uongeze bidii yako kwa Mungu, ongoza kiwango chako cha maombi, tumia muda mrefu kusoma biblia kuliko kufuatilia mambo yasiyokuwa na maana. Simama imara katika Imani yako. Kabla hujalala jijengee utaratibu kwa kuomba. Na hiyo hali haitajirudia tena.

Lakini kama wewe umeokoka na bado unauhakika umesimama imara katika Imani, na ndoto kama hiyo imekujia bila kutazamia, na ishara kuwa ulikuwa hufurahii ni kwamba hata katika hiyo ndoto ulikuwa unaonyesha upinzani,kukataa hicho kitendo, au kujiuliza inakuaje kuaje nipo katika hali hii na mimi nimeokoka.. basi hali kama hiyo ikikujia Ikimee mara moja kwa jina la YESU, kisha mwambie shetani huwezi kunijaribu kwa kishawishi chochote..Na ndoto kama hizo hutaziota tena..

Jambo ambalo watu wengi hawafahamu ni kuwa zinaa, kuiondoa ndani ya mtu inahitaji muujiza, na anayeweza kuikata kiu hiyo ni YESU KRISTO peke yake, haijalishi wewe ni mkristo au wewe ni muislamu au hauna dini ..Ni Yesu pekee ndio anayeweza kukubadilisha na kukufanya uishi Maisha yaliyo  mbali na zinaa.

Dhambi hii, inawashinda wengi, na ndio dhambi inayoongoza kuwapeleka watu kuzimu.  Isitoshe biblia inasema, Kama vile ilivyokuwa katika siku za Sodoma na Gomora ndivyo itakavyokuwa siku za kuja kwake mwana wa Adamu. Kumbuka siku za Sodoma na Gomora, kulikuwa na uzinzi wa kiwango vya hali ya juu kama vilivyopo sasa, kulikuwa kuna mashoga na wasagaji waliokuwa wanajidhirisha waziwazi kama ilivyo sasa.. Na hiyo ndio ikiwa sababu ya miji ile kuteketezwa..Lakini cha kuogopesha Zaidi ni kwamba, kati ya maelfu kama sio mamilioni ya watu waliokuwa katika miji ile, ni watu watatu tu ndio walionusurika..wengine wote waliteketea kwa moto..

Luka 17:28  “Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;

29  lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.

30  Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu”

Soma tena kwa makini mstari huu:

Yuda1:7  “Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.

8  Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu”.

Unaona? Vivyo hivyo na jambo kubwa Zaidi litakalofanya ulimwengu huu uteketezwe siku ambazo si nyingi, ni dhambi ya zinaa, vilevile watakaonusurika watakuwa ni wachache sana. Mungu huwa hana wengi wape,.Leo hii unaweza kusema mbona kila mtu yupo hivi au yupo vile..Lakini nataka nikuambie  hata kama dunia nzima imeamua kuasi Mungu akimuona mtu mmoja tu, inatosha yeye kuangamiza..

Hivyo ikiwa wewe ni mwenye dhambi, haijalishi dini yako, au dhehebu lako.Yesu anawaokoa watu wote, na bado anaendelea kuokoa ikiwa mtu atakuwa tayari kutaka kuokolewa naye, kwasababu neema yake kaiachia kwa watu wote. Ikiwa leo hii unataka kusema Maisha ya uzinzi basi, nataka YESU anasaidie niishinde dhambi hii na nyingine zote…Ukiwa unamaanisha kweli kufanya hivyo..Basi leo hii hapo ulipo anaweza kukuokoa na kukugeuza na kukufanya kuwa mtoto wake.

Ikiwa upo tayari kubadilishwa leo Maisha yako na Yesu..Basi fahamu kuwa yeye yupo hapo pembeni yako kukusaidia, unachopaswa kufanya ni kufungua tu moyo wako..Uhitaji unione mimi, au usikie sauti yangu..Suala la wokovu ni Zaidi ya upeo wa fikra za kibinadamu. Leo hii YESU atayageuza Maisha yako, na atafanya muujiza mkubwa ndani yako kwa namna ambayo hujawahi kuidhania.

Hata na yale mengine mbali na uzinzi, labda ulevi, matusi, wizi yote atayaua ndani yako ikiwa tu utakuwa tayari kumpokea Leo. Yesu yupo hai, yupo tayari kwa mtu yeyote kumsaidia wakati wowote bure.. hivyo bila kukawia kawia hapo ulipo chukua muda jitenge eneo la utulivu. Kama upo ndani tafuta chumba ujitenge peke yako, kisha piga magoti..Ukiwa hapo chini umepiga magoti sema sala hii kwa sauti..

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU WA KUSHINDA DHAMBI, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA, NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KWA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani Mungu amekusikia ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa matendo, hapo ulipo ikiwa ulikuwa na picha chafu katika siku yako, anza kwa kuzifuta, ikiwa ulikuwa unayafanya  mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Kuanzia leo hii utaanza kuona badiliko kubwa ndani yako. Jambo lingine unalohitaji kufanya ni kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na katika kujifunza biblia ili uukulie wokovu.

Hata kama wewe ulikuwa ni muislamu, tafuta kanisa lililokaribu na wewe la kiroho, waeleze uamuzi wako uliouchukua, kisha wao watakuelekeza hatua inayofuata au kama utahitaji msaada wa kanisa kwa eneo lako basi wasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312.. Ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Yazingatie hayo. Na Bwana atakuwa pamoja na wewe katika kila hatua ya Maisha yako. Na ndoto zote hizo za Kuota unafanya tendo la ndoa au kuota unafanya mapenzi na mtu usiyemjua, zitaisha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:


Bwana akubariki.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Pia zidi kutembelea website yetu hii, kwa mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

Nitajuaje kama ndoto ni ya Mungu au ya Shetani?

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

Kuota unafanya Mtihani.

Kuota unakimbizwa.

MKUU WA ANGA.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NDOA NI NINI?

Ndoa ni nini? Je ndoa za kibinadamu ni zipi na ndoa ya kimbinguni ni ipi?


karibu tujifunze masomo ya ndoa na elimu ya ndoa na mafunzo ya ndoa kwa mapana.

Ndoa ni muunganiko wa kimwili kwa namna ya roho kati ya watu wawili wa jinsia mbili tofauti.  Kuna aina mbili za Ndoa. Zipo ndoa za kibinadamu na ndoa ya kimbinguni.

Ndoa za kibinadamu zinahusisha Mume mmoja na mke mmoja…Lakini Ndoa ya kimbinguni inahusisha Mume mmoja (Aitwaye Yesu Kristo) na mke wake mmoja aitwaye Kanisa.

Ndoa za kibinadamu.

Kama tulivyotangulia kusema hapo juu..Ndoa hii ni muunganiko wa kimwili baina ya watu wawili wa jinsia mbili tofauti. Ndoa ya kwanza ilifungishwa na Mungu mwenyewe pale Edeni…baada ya Adamu kukabidhiwa Hawa aliyetoka ubavuni mwake. Na ilihusisha Mume mmoja na mke mmoja…Hakuumbwa Adamu mmoja na wakina Hawa wengi…au Hawa mmoja na wakina Adamu wengi. Kama ingekuwa ni hivyo basi Ndoa ya mume mmoja na wake wengi ingekuwa halali..au ya mke mmoja waume wengi.

Mathayo 19:3 “Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?

4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe”.

Na kuna tofauti kati ya ndoa na harusi..Ndoa ndio kama tulivyoizungumza hapo juu kwamba ni muunganiko wa kimwili watu wawili wa jinsia mbili tofauti.  Lakini harusi ni sherehe au karamu inayofanywa baada ya ndoa kufungwa.

Sasa kuna maswali machache yafuatayo ya kujiuliza: Maswali haya yanalenga kwa urefu juu  ya masomo ya ndoa na mafunzo ya ndoa/Elimu ya ndoa

  • Je ni lazima kuoa au kuolewa?

Biblia haijaweka sharti la kwamba kila mtu ni lazima aoe au aolewe. Zaidi ya yote ni vizuri mtu kutokuoa kabisa au kutokuolewa kwa ajili ya kuifanya kazi ya Mungu. Biblia inasema hivyo katika..

1 Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.

34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe.

35 Nasema hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine”

Kuna faida kubwa ya kutokuoa au kutokuolewa kwaajili ya kuifanya kazi ya Mungu..lakini kama sio kwasababu hiyo ni heri kuoa au kuolewa. Kwasababu Ndoa ina faida kubwa sana, na ina baraka na heshima.  Mtu aliyefunga ndoa takatifu. Kuna Baraka za kipekee na Neema kutoka kwa Mungu anazipokea zaidi ya yule ambaye hajaoa au hajaolewa. Hivyo ni vizuri kuoa au kuolewa..(hususani Unapozidi kuelewa upana juu ya ndoa ni nini na majukumu yako baada ya ndoa hiyo utabarikiwa sana kuliko kawaida )

lakini pia ni vizuri kutooa au kutokuolewa kwaajili ya ufalme wa mbinguni.

Maswali mengine ya muhimu ya kujiuliza kuhusu elimu ya ndoa/mafunzo ya ndoa ni kama yafuatayo.

  • Nitampataje Mwenza wa Maisha?: Jibu la Swali hili utalipata mwisho kabisa wa somo hili. au bofya hapa >> Mwenza wa Maisha
  • Je ni ruhusa kutoa Talaka baada ya kufunga ndoa?: Jibu la Swali hili pia utalipata mwishoni mwa somo hili au bofya link hii >> Talaka
  • Je ni Lazima kutoa mahari kabla ya kufunga ndoa?, Na je pia ndoa ni lazima ifungiwe kanisani?: Jibu la swali hili pia utalipata mwishoni kabisa mwa somo hili kwenye link za mapendekezo au bofya hapa kujua >> Mahari
  • Je Ndoa ya Yesu Kristo ikoje? Kwa mapana zaidi?: Jibu la Swali hili pia unaweza kulipata katika link za mapendekezo mwishoni mwa somo hili, Au bofya hapa kusoma >> Ndoa ya Kristo

Kama utakuwa umeyafuatilia hayo masomo ya ndoa hapo juu na kuzifungua link hizo kwa umakini utakuwa umeelewa kwa sehemu kubwa ndoa ni nini?.  Hivyo kama umedhamiria kuoa au kuolewa..Basi kumbuka jambo moja na la muhimu kuwa “Ndoa inapaswa iheshimiwe na watu wote.”. Sio iheshimiwe na wewe tu na mpenzi wako peke yenu!.. Hapana bali watu wote..Ikiwa na maana kuwa ukifanya jambo lolote litakaloifanya ndoa yenu isiwe na heshima, watu wakaidharau…Hiyo tayari ni dhambi! mbele za Mungu.

Waebrania 13:4 “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu”.

Ukishaoa au kuolewa huo sio wakati wa kutanga tanga huku na huko kuzungumza zungumza habari za ndoa yenu..huko ni kuiondolea heshima ndoa yenu! na ni dhambi..Ukishaoa sio wakati wa kuudhiana mpaka kutupiana maneno au kupigana hadi watu wa nje wanawaona..huko ni kuivunjia heshima ndoa…ambapo ni dhambi! n.k

Ukishaoa sio wakati wa kukaa kwenye vibaraza vya mizaha, na vijiweni kuzungumza kama mtu ambaye hajaoa au hajaolewa, na wala si wakati wa kuvaa kama kahaba, au mhuni huko ni kuivunjia heshima ndoa ambako ni dhambi na kujitafutia laana. Ni lazima ufahamu ndoa ni nini!

Kama hujafahamu Agano lililopo katika ndoa ni heri ukasubiri kwanza, kuliko kukurupuka na kuoa au kuolewa na kisha kuiharibu ndoa na kuangukia Hukumu.

Yapo mengi ya kuzungumzia juu ya ndoa ni nini, lakini hapa hatuwezi kuyaandika yote, naomba ufungua link hizo nilizokupatia hapo juu au hizi hapa chini, yapo maelezo marefu na ya kutosha kuhusu ELIMU YA NDOA.

Bwana akubariki sana.

Na kama hujampa Yesu Kristo maisha yako.. Nakushauri ufanye hivyo sasa. Mahusiano ya kwanza ya kutafuta kabla ya kuoa au kuolewa ni mahusiano yetu sisi binafsi na Yesu Kristo. Huyo ndiye tumaini la wokovu wetu na mwokozi wa kila mwenye mwili. Na biblia inasema pia itatufaidia nini tuupate ulimwengu mzima na tupate hasara ya nafsi zetu..

Hivyo kila kitu kitapita…hata baada ya kifo hakutakuwa na kuoa wala kuolewa..Ni mambo mengine yatafuata. Hivyo ni muhimu sana kwanza kutafuta uhusiano binafsi na Yesu Kristo kabla ya mambo yote..Na huo tunaupata kwa kumwamini, na kutubu dhambi zetu zote kwa kukudhamiria kutozifanya tena..Na kubatizwa..na Roho Mtakatifu atatuongoza katika kweli yote.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Maranatha!

Mafundisho mengine:


Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI AU KUTOA TALAKA?

Je Mahari ina ulazima wowote?

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MADHABAHU NI NINI?

Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. Pamoja na maswali mengi ya biblia yaliyojibiwa..kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/FAyJLXo8guQ0iZ0JzQKbXg

Madhabahu ni nini?..Je madhabahu ya kuvukiza uvumba ni nini?..je hata sasa watu wanatengeneza madhabahu za kutolea dhabihu?…madhabahu ya kwanza kutengenezwa ni ipi?

Madhabahu ni mahali ambapo sadaka zinatolewa.. Katika Agano la Kale, Bwana Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wamtolee sadaka…Zilikuwepo sadaka za aina mbali mbali kama vile sadaka za dhambi, sadaka za shukrani na nyinginezo.

Lakini sadaka yoyote iliyokuwa inatolewa kama ni sadaka kuteketezwa, Ilikuwa ni lazima madhabahu itengenezwe. Kwa lugha rahisi na ambayo inaweza kueleweka ni kwamba baada ya mnyama yule aliyewekwa tayari kwaajili ya sadaka kuchinjwa..aliwekwa juu ya kuni zilizopangwa vizuri zilizo juu ya mawe…hivyo madhabahu ilitengenezwa kwa mawe na kuni..Ni sehemu maalumu ya kumchomea yule mnyama mpaka eteketee kabisa..

Madhabahu ya kwanza ilitengenezwa na Habili ambaye alimtolea Bwana sadaka ya kuteketezwa juu yake. Na Mungu aliiitakabali zaidi ya Kaini ndugu yake.

Katika Biblia tunasoma pia Nuhu alimjengea Bwana madhabahu baada ya kutoka kwenye safina.(Soma Mwanzo 8:20)

Na pia Ibrahimu alimtengenezea Mungu madhabahu mara kadha wa kadha alipotaka kumtolea Mungu sadaka…Ndio maana tunaona hata wakati ule alipojaribiwa na Mungu amtoe Isaka mwanawe..tunaona alitengeneza madhabahu.

This image has an empty alt attribute; its file name is Abraham-to-Sacrifice-Isaac-2.jpg

Na wengine wote kama akina Yakobo, Eliya, na Musa walipotaka kumtolea Mungu sadaka walitengeneza madhabahu..Na kulikuwa na maagizo maalumu ya namna ya kutengeneza madhabahu kama Mungu anavyotaka…ilikuwa sio ruhusa kutengeneza madhabahu kama za wapagani..kulikuwa na maagizo maalumu ya namna ya kuitengeneza ambapo hatuwezi kuyaangalia yote lakini mojawapo ilikuwa ni hili…

Kumbukumbu  27:5 “Na huko umjengee madhabahu Bwana, Mungu wako, madhabahu ya mawe, usitumie chombo cha chuma juu yake.

6 Jenga hiyo madhabahu ya Bwana, Mungu wako, kwa mawe yasiyochongwa; ukamtolee Bwana, Mungu wako, sadaka za kuteketezwa juu yake;”

Kulikuwepo pia kuna aina nyingine ya madhabahu iliyojulikana kama madhabau ya kuvukizia uvumba (Soma kutoka 30:27). Hii ilitumika kwaajili ya kuchomea uvumba mtakatifu ndani hema ya Mungu au Nyumba ya Mungu ..Madhabahu hii haikutengenezwa kwa mawe na kuni kama ile madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa..Hii ilikuwa ndogo na ilikuwa ni kama jiko hivi…Tazama picha chini.

madhabahu ya kuvukizia uvumba

Lakini katika Agano jipya hatuna tena hizo Madhabahu zenye mfano huo..

Madhabahu yetu kwa sasa ni mioyo yetu…Tunapomkubali Yesu Kristo na kuingia moyoni mwetu…Na anapotusafisha na kutupa Roho wake mtakatifu hapo ndipo madhabahu yetu inapokamilika katika viwango Mungu anavyovitaka..Na kuanzia huo wakati shughuli zotezote za kiibada, ikiwemo sadaka, maombi, dua, sala, utukufu, shukrani ndipo vinakubalika mbele za Mungu.

Zaburi 51:16 “Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa, Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.

17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau”

Lakini kama mtu hajasafishwa maisha yake kwa damu ya Yesu basi madhabahu ya moyo wake inakuwa ni chafu na hivyo hawezi kumpendeza Mungu kwa chochote kile.

Mbali na hilo, upo pia utaratibu wa kuiita mimbari ya kanisa kuwa ni madhabahu..Kiuhalisia ile sio madhabahu..Lakini pia si dhambi kuiita madhabahu na kuiheshimu. Kwasababu ni mahali ambapo Neno la Mungu (chakula cha Roho zetu linahubiriwa na tunapeleka matoleo yetu pale)..Na pia chochote kitakachofanyika pale kinyume na Neno la Mungu au kisichokuwa na utukufu wa Mungu, Ni dhambi na hivyo ni kujitafutia laana badala ya baraka..Na kumbuka pia sehemu ya mimbari ya kanisa (ambayo inajulikana kama madhabahu)..haipaswi kupambwa pambwa na mishumaa, au sanamu mpaka kufikia hatua watu wanakwenda kuvisujudia na kuviangukia na kuviogopa…Hiyo ni ibada za sanamu na ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Mimbari inapaswa iwe ni sehemu ya kawaida tu…

Lakini madhabahu halisi ni mioyo yetu..Na hatupaswi kuweka msisitizo mkubwa wa kuiheshimu madhabahu ya kanisa na huku madhabahu halisi ya mioyo yetu imechafuka. Biblia inasema..

Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima”

Utakuta mtu anaiogopa madhabahu ya kanisa na kuiheshimu..Lakini kuiheshimu madhabahu halisi ya moyo wake ambapo ndipo mahali Mungu yupo karibu sana na yeye haiheshimu..Atamwabudu Mungu huku moyoni mwake ni muuaji, mwasherati, mwenye chuki na kinyongo na kutokusamehe.

Bwana atusaidie kufanya madhabahu za mioyo yetu kuwa safi..ili maombi yetu, sala zetu, dua zetu pamoja na sadaka zetu zipate kibali mbele za Mungu wetu.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Ubarikiwe sana.

+255693036618/ +255789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

Usilale usingizi wakati wa kumngojea Bwana.


Luka 12: 35  “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka; 

36  nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara. 

37  Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia. 

38  Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao. 

39  Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa. 

40  Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.”

Tusome mstari mwingine tena unaofanana na huo…

Marko 13:35 “Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba, kwamba ni jioni, au kwamba ni usiku wa manane, au awikapo jimbi, au asubuhi; 

36  asije akawasili ghafula akawakuta mmelala. 

37  Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni”.

Hapa tunaona tukio la Mtu mmoja ambaye tajiri…ambaye ana nyumba yake yenye wafanyakazi wengi..na kila mfanyakazi ana majukumu yake kama tunavyojua…wapo wa wakutengeneza chakula, wakufanya usafi, wapo wa kulisha mifugo, wapo wakuhakikisha usalama, n.k Kila mmoja ana majukumu yake.

Lakini tunaona alitoka siku moja na kwenda arusini..akawaambia watumwa wake wakeshe!..hakuwaambia kwamba atarudi siku hiyo hiyo…lakini aliwaaambia tu atarudi siku yoyote…Hivyo akawaambia muda wowote wawe tayari..siku atakayokuja kama ni jioni, au asubuhi au usiku wa manane awakute wakiwa katika shughuli zao kama kawaida..waohusika na usalama basi wawe wa kwanza kumfungulia mlango atakapofika n.k

Akawasisitiza sana wawe macho muda wote kwasababu hawajui siku wala saa atakapokuja. Sasa endapo angekuja baada ya siku mbili mida ya saa 8 usiku akawakuta wamelala unadhani angejisikiaje?..Ni wazi kuwa angeudhika sana na kuwafukuza kazi wote..

Mfano huo huo unalinganishwa na kurudi kwake Bwana Yesu mara ya pili. Kumbuka mtu yoyote aliyeokoka kwa dhati ni mtumishi wa Yesu Kristo..Ni lazima kuna kitu Fulani ambacho amepewa na Kristo kwaajili ya kuundeleza ufalme…Na kitu hicho ni karama aliyopewa…Na karama hiyo Bwana Yesu anataka iendelee kufanya kazi muda wote mpaka siku atakayokuja.. Lakini akija na kukuta Karama aliyokupa imekufa haifanyi kazi…Na sio tu haifanyi kazi bali pia wewe mwenyewe umelala usingizi (yaani umechukuliwa na ulimwengu)..Basi kuna hatari ya kutupwa katika ziwa la moto.

Hivyo tukumbuke kila siku kwamba tupo kazini..na hivyo tuwe waaminifu na majukumu yetu tuliyokabidhiwa na Bwana.

usilale usingizi..Kwasababu Biblia inasema katika;

Waebrani 10:37  “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada nyinginezo;

BIRIKA LA SILOAMU.

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA

MAUTI YA PILI NI NINI?

BONDE LA KUKATA MANENO.

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

USISIKILIZE DHIHAKA ZA SHETANI, ZITAKUKWAMISHA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

HAPANA HATA MMOJA ATAKAYEIONJA KARAMU YANGU.

“Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”


Tukisoma Luka 14 kuanzia mstari wa 16-24. Tunaona Bwana Yesu akitoa mfano wa mtu mmoja aliyefanya karamu kubwa sana. Na siku ilipofika ya sherehe muda wa chakula akatuma mtumwa wake kwenda kuwaita wale waliolikwa waje karamuni lakini mwitikio wao siku hiyo ulikuwa ni tofauti, badala ya kuja kila mmoja akaanza kutoa udhuru mmoja akasema mimi nimenunua shamba ni sharti niende kulitazama nisije nikawa nimeuziwa bonde, hivyo nisamehe, mwingine akasema nimenunua ng’ombe hivyo ni sharti niende kiwajaribu nisije nikawa nimeuziwa vilema na wagonjwa, mwingine akasema nimeoa nitakwenda honey-moon siwezi kuja nisamehe..

Lakini yule mtu alikasirika sana..Ukisoma pale kwa makini utagundua kuwa hakukasirika kwa waliokuwa wamepanga kuyafanya, hapana lakini alikasirika kwa wao kupuuzia mwaliko wake. Kwasababu udhuru zao hawakuzitoa mwanzoni kabisa walipoalikwa kabla hata sherehe kuanza, Bali walisubiria wazitoe siku ambayo kila kitu kipo tayari,.. mahali ambapo mwenye kualika hawezi kuahirisha na kufanya wakati mwingine ambapo wote watakuwa free. Hiyo ni kuonyesha kuwa walikuwa hawataki kabisa kuhudhuria sherehe ya yule aliyewaalika tangu mwanzo, na ndio maana wakazihifadhi sababu zao wasizitoe tangu siku nyingi na kuzitoa siku ile ya sherehe yenyewe, walijifanya kama wamepatwa na emergency hivi kumbe mambo hayo walikuwa wanayatambua tangu mwanzo..

Lakini sasa tunaona mwisho wa mfano ule, Bwana YESU anasema maneno haya:

Luka 14:24 “Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.

Hapa ndipo kiini cha somo kilipo..

Kwanini aseme tena hivyo “wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu.”

Kulikuwa kuna maana gani ya kusema hivyo wakati tayari walishaikataa tangu mwanzo?..Embu jaribu kufikiria mtu amekualika unakataa halafu anakuapia hutaonja sherehe yake…Si unaweza kumwona kama ni Mwenda wazimu?. Lakini ukiwa na akili utajiuliza maswali Fulani kichwani kwako kwanini aniambie vile??

Kipindi Fulani nyuma, kuna Rafiki yangu ambaye alipomaliza masomo yake alikwenda katika mafunzo ya jeshi kwa matumaini kuwa akimaliza aajiriwe kule, lakini kwa bahati mbaya walikaa kule muda mrefu, sana, wakisubiria ajira kwa muda mrefu lakini hazikutoka..Mpaka wakati wa mafunzo ulipoisha sasa wanalazimika kila mmoja arudi nyumbani kwao, ni kama vile alikata tamaa akiangalia ameshapoteza miaka kadhaa kule jeshini na leo hii anaambiwa arudi nyumbani!!..

Lakini wakiwa huko nyumbani, tamko linatolewa na raisi kuwa kuna mgodi mahali Fulani unahitaji ujenzi wa kuzungushwa ukuta mgodi wote, na wanaohitajika kwa shughuli hiyo ni walewale vijana waliokuwa katika mafunzo ya jeshi, lakini kwa sharti kuwa hakuna malipo, wala posho bali ni kitendo tu cha kujitolea..hivyo anayetaka kwenda na aende, na asiyetaka vilevile ni sawa.

Wengi wao waliposikia hivyo hawakutaka hata kufuatilia habari hizo, wengine walidhihaki, wakagoma, wakaona kama ni mambo yaleyale, kwenda kupoteza muda halafu mwisho wa siku hautazamwi unarudishwa nyumbani kukaa.Lakini huyu Rafiki yangu na wenzake wachache sana, wakaamua tu kwenda kujitolea kufanya kazi hiyo, wakitumaini pengine labda wataangaliwa wakishamaliza ujenzi huo, lakini walifanya kazi ile kwa shida ananiadithia, kwasababu ilikuwa ni ngumu na walipewa kipindi kifupi sana cha kuimaliza..

Wakafanikiwa kuimaliza, kisha wakapewa kila mmoja cheti, wakitumaini wataitwa walau jeshini, lakini wakaambiwa asanteni kwa msaada wenu rudini nyumbani..Basi wakarudi nyumbani, muda ukapita wale wengine wakaanza kuwacheka, na kuwakejeli, lakini sasa baada ya ujenzi ule kukamilika na serikali kuona imefanikiwa kukusanya mapato mengi kwa kipindi kifupi kwasababu ya ujenzi wa ukuta ule,.kukomweshwa kwa vya utoroshaji madini. Ndipo raisi akakumbuka Je! Wale watu waliojengwa ule ukuta wamefanyiwa fadhila gani?..Akatoa tamko la siku 2 wale vijana wote waliojenga ukuta ule wafike makao makuu ya polisi wakiwa na vyeti vyao mkononi wapokee ajira zao za kujiunga na Jeshi.

Sasa wale wengine ambao walikataa kujitolea waliposikia hivyo, matumbo yalijaa moto, wakaanza kuhangaika huku na huko wengine wanatafuta namna ya kufoji vyeti vile, wengine wakatafuta namna ya kutoa rushwa, wengine siku ile ile na wao pia walifunga safari wakiungana na wale wenzao kwa ajili ya udahili, wakitumainia kuwa na wao pia watapata rehema ya kuruhusiwa kujiunga na wenzao..Lakini pamoja na kwamba safari zao kuwa ndefu, kutoka kila mkoa nchini.. waliishia kufukuzwa tu getini pale..wengine wakaanza kulia na kulaumu, wakiona wale ambao walikuwa wanawacheka sasa sio wenzao tena..Wenzano wanapata ajira wao wanarudi nyumbani..Wengine wakawa wanajuta ni kwanini walikataa mwaliko ule wa kuujenga ukuta wa mgodi..waliokuwa wanawaambia nyimbo za mizaha leo hii wao ndio wanalia..

Na ndivyo itakavyokuwa katika karamu ya mwana-kondoo. Leo hii wengi wanaalikwa mamilioni kwa mamilioni takribani karibu kila mtu duniani anaalikwa ili tu kuingia katika karamu ile ya mwana-kondoo, lakini wanaouitikia mwaliko huo ni wachache sana, tena sana, pengine hao ambao hawaitikii wana sababu zao za msingi sana za kusimamia..wengine wanasema wokovu hauna faida, wengine wanasema unanifanya niwe maskini, wengine wanasema, nilichonacho sasa kinanipa faida kuliko hicho ninachokitazamia kuja huko mbeleni..Wengine wanasema siwezi kuacha biashara yangu hii haramu, ni sharti nitafute fedha kwanza kisha Mungu uzeeni, nikishastaafu…Wengine wanasema nimeujaribu wokovu huo kwa muda mrefu na sijaona faida yake hivyo sitaki kuusikia…Wote hawa wanaosababu zao, na pengine ni sababu za msingi sana..

Lakini nataka nikuambie, leo hii hutaki, lakini siku moja kibao kitakugeukia wewe.. utatamani hicho ulichokikataa lakini utakuwa tayari umeshachelewa?. Ni kwasababu gani utamani kukipata tena hicho ulichokikataa? Ni kwasababu utaona mambo yaliyo kinyume na matarajio yako.

Wale waliopewa mwaliko na kuanza kutoa udhuru wa kununua ng’ombe wengine shamba wengine wameoa..waliidharau ile karamu na Zaidi ya yote walijua hata wakienda kwenye ile karamu watagharimika gharama nyingine za kutoa zawadi..Lakini kinyume chake pengine yule Bwana arusi aliwaalika kwenye karamu yake aliwaalika kwenda kuwapa zawadi waalikwa wake na si kupokea zawadi..Utajisikiaje unaikataa harusi ambayo ulidhani unakwenda kutoa zawadi kumbe ndio unakwenda kupewa zawadi?..Unaona wenzako waliokwenda wanapewa majumba, mashamba, magari, mang’ombe n.k … utatatami kwenda kujiunga lakini utashindwa..?

Ndivyo itakavyokuwa siku watakatifu watakapokwenda mbinguni…Wewe uliyeudharau mwaliko leo..Utaona kwa mbali uzuri ambao Mungu amewaandalia watu wake, milele, utaona hiyo miili mipya waliyoandaliwa wateule wa Mungu milele jinsi ilivyo mizuri yenye utukufu mwingi, na wewe huna, utaona hiyo miji mizuri na majumba mazuri walioandaliwa watakatifu na wewe utakuwa huna chochote, utaona mambo ambayo hata wale walioitikia mwaliko, hawajawahi kuyaona, wala kuyasikia, wala kuyategemea..Siku hiyo utajuta utasema ni kwanini sikuitikia mwito ule wa karamu ya mwanakondoo..

Utafanya bidii kweli uingie lakini hutaweza..Ndio hili Neno litakapotimia juu yako..

Luka 14:24 “Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu: yangu”.

Ndugu Parapanda ipo karibuni kulia, UNYAKUO ni tendo tunalolitazamia sasahivi mbele yetu,..Ukiendelea kuutazama huu ulimwengu ambao haukuahidii kitu chochote baada ya kufa, utapata hasara ya nafsi yako mwenyewe. Ushauri wangu ni kuwa Chukua hatua tubu dhambi zako mgeukie Kristo, maadamu wakati wa kuitikia wito mwaliko unao, kabla siku za hatari hazijakukuta..

Ufunuo 19:9 “Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

Rudi Nyumbani:

 

Print this post