Category Archive Uncategorized @sw-tz

Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?

SWALI: Je! Yesu ni Mungu? Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?


JIBU: Yesu alikuwa ni Mungu katika mwili (1Timotheo 3:16)…lakini hakuja kutafuta kuabudiwa wala kusujudiwa!…Mpaka Mungu amevaa mwili na kuja ulimwenguni, maana yake hajaja kutafuta kuabudiwa, kama angekuwa amekuja kutafuta utukufu wake basi, kulikuwa hakuna haja ya kuuvaa mwili na kushuka duniani, naamini Mbingu ilikuwa inamtosha…. hivyo ni lazima atakuwa amekuja kwa kusudi lingine na si la kutafuta utukufu. Hapo ndipo wengi wa wasio wakristo wanaposhindwa kuelewa, na baadhi ya walio wakristo.

Unapoona askari wa kuongoza barabarani (Traffic man), kaondoka barabarani na kaenda nyumbani kubadilisha nguo zake hizo nyeupe…na akavaa nguo za kiraia na kuingia mtaani basi ni dhahiri kuwa huko mtaani alikokwenda hajakwenda kutafuta kuongoza magari bali kaenda kutafuta mambo yake mengine ya kawaida..labda anaenda hospitalini au sokoni au kusalimia ndugu na marafiki, au kufuatilia mambo yake mengine ambayo ni tofauti na ya kikazi….. (ni kweli bado atabaki kuwa askari, lakini yupo nje ya ofisi yake), hivyo hataweza kuyatumia yale mamlaka aliyonayo ya kuongoza magari,…na akiwa barabarani na nguo zake za kiraia, hata watu wanaweza wasimtambue kama ni askari, atakuwa kama raia wengine tu, na magari atakuwa anayakwepa tu kama raia wengine, na atazingatia sheria zote za barabarani kama raia wengine…

Na Bwana Yesu ni hivyo hivyo…alipokuwa mbinguni alikuwa ni Mungu, anayestahili kuabudiwa na kuheshimiwa…aliposhuka duniani alikivua kile cheo cha Kiungu…na kuwa kama mwanadamu (kwa lengo la kuja kumkomboa mwanadamu na si kuabudiwa kama Mungu)..na baada ya kumaliza akarudi mbinguni alikotoka katika cheo chake.

Hivyo akiwa kama mwanadamu alikuwa hana budi aishi kama wanadamu wengine, hana budi awe mtu wa ibada kama watu wengine, hana budi ale, anywe, alale, achoke, apitie yote mwanadamu wa kawaida anayopitia na hata ikiwezekana afe…ili tu kusudi lake lililomleta duniani litimie la kumkomboa mwanadamu…lakini alikuwa bado ni Mungu.

Wafilipi 2: 5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa YUNA NAMNA YA MUNGU, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali ALIJIFANYA kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

Umeona hapo mstari wa 7?..unasema “ALIJIFANYA”..kama unakielewa Kiswahili vizuri utakuwa unajua maana ya “KUJIFANYA”..Maana yake ni kama kujigeuza/kuigiza kuwa kitu Fulani na kumbe sio…kwa lengo la kutimiza kusudi Fulani tu!…Hivyo Bwana Yesu aliyejifanya kuwa hana utukufu…ili ashuke aje kutukomboa na kutuonyesha njia jinsi mwanadamu kamili anayemcha Mungu anapaswe awe.

Hivyo kufa kwa Bwana Yesu, hakumfanyi yeye asiwe Mungu..na pia muujiza mkubwa duniani na mbinguni sio kutokufa!!… Huo ni muujiza mdogo sana…..“miujiza mkubwa ni uwezo wa mtu kuutoa uhai wake na kisha kujirudishia ule uhai”..Huo ndio muujiza mkubwa kuliko yote!..na uwezo huo alikuwa nao Yesu pekee yake.

Yohana 10:17 “Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.

18 HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE. NAMI NINAO UWEZA WA KUUTOA, NINAO NA UWEZA WA KUUTWAA TENA. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu”.

Sasa utauliza ni wapi, Yesu aliutoa uhai wake mwenyewe?…kasome Luka 23:46-47. Bwana Yesu aliutoa uhai wake mwenyewe! Hakuna mtu aliyemsaidia kuutoa..hata Pilato alishangaa imekuwaje amewahi kufa kiasi kile (Marko 15:44). Na aliurudisha uhai wake mwenyewe baada ya siku tatu (kule kaburini hakuna mtu aliyeenda kumfufua au kumwombea afufuke).

Alijirudishia uhai wake mwenyewe!..Nadhani huo ni muujiza mkubwa sana.. Je wewe unaweza kufanya hivyo????

Hata mfano nikikuwekea watu wawili mbele yako mmoja hawezi kuukata mguu wake na mwingine anao uwezo wa kuukata na kuurudisha….nikakwambia kati ya hao wawili ni yupi hapo wa kuogopwa zaidi??..Bila shaka utaniambia “Yule mwenye uwezo wa kuukata mguu wake na kisha kujirudisha tena ndiye wa kuogopwa zaidi kuliko huyo mwingine”.

Kwahiyo kuupima uungu wa Bwana Yesu na kifo chake ni hoja dhaifu!!..miungu ya kipagani ndio isiyo na uwezo wa kufanya hayo..lakini Mungu wa mbingu na nchi (YESU KRISTO) anaweza kufanya mambo yote. Mpaka sasa katika historia hajatokea nabii yoyote wala mtume yeyote aliyofanya miujiza kama aliyofanya Bwana Yesu, sasa kwanini asiwe Mungu?. Na siku moja atarudi na kila jicho litamwona na kila goti litapigwa, na kila kinywa kitakiri…Wengi itakuwa ni jambo la kushtukiza sana kwao, kwasababu hawataamini kwamba kweli ndiye!..kwasababu walidanganyika wakiwa duniani kwamba hatarudi.

Lakini anatupenda na wala hataki mtu yoyote apotee bali wote tuifikie toba, ili tuokoke na tuje kutawala naye milele.

Bwana atubariki tuzidi kumjua yeye!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

Katika biblia Neno “Mshenzi” linatajwa.Kwanini liwekwe?

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Agano jipya ni nini?

Agano jipya ni nini?


Tukitamka neno “agano jipya”  tunathibitisha kuwa lilishawahi kuwepo agano la zamani (La kale) hapo kabla.

Hivyo ili kufahamu agano jipya ni nini, ni vizuri kwanza ukapata msingi wa agano la Kale, lilikuwaje.

Kama tunavyojua Biblia imeundwa na maagano makuu wawili, yaani jipya na la kale.

  1. Agano la Kale:

Sasa msingi wa agano la kale ulitoka kwa mtu mmoja aliyeitwa Ibrahimu. Mungu alipomuita hakumuita ilimradi tu, bali aliingia agano naye akamwambia atambariki na kumfanya kuwa baba wa mataifa mengi, ikiwa tu atakuwa mkamilifu na atakwenda  katika njia zake..Tusome.

Mwanzo 17:1 “Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. 

2 Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana. 

3 Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema, 

4 Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi, 

5 wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi. 

6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako. 

7 Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako. 

8 Nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao. 

9 Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada. yako. 

10 Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa. 

11 Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi”.

Unaona, Jinsi Mungu alivyokuwa mwaminifu, baadaye Mungu akaja kumtimizia kweli agano aliliomuahidia, kwa jinsi uzao wake ulivyokuwa unaongezeka duniani kwa kasi, Lakini wakati huo wote uzao wake ulikuwa haumjui Mungu vizuri, ulikuwa bado haujajua kanuni za agano hilo ambalo Mungu aliloingia na Ibrahimu baba yao linavyopaswa liwe..

Ndio hapo wakiwa kule jangwani sasa Mungu anamtumia Musa kusema nao na kuwapa sheria na amri za kuzishika ili wafanikiwe..

Sheria hizo ndizo zilizoandikwa katika vitabu vya Torati: yaani

  • Mwanzo
  • Kutoka
  • Hesabu
  • Mambo ya Walawi
  • Kumbukumbu la Torati.

Hivyo vitabu hivyo vitano vilikamilisha Sheria yote ya Agano hilo ambalo Mungu aliingia na Ibrahimu.

Lakini hiyo peke yake haikuwa inatosha wana wa Israeli kumfahamu Mungu katika ukamilifu wote, Hivyo ilipasa  Mungu azungumze nao mara kwa mara kupitia watu mbalimbali wakamilifu na manabii wake.. Mfano tunamwona mtu kama Ayubu, Esta, Ruthu, kwa kupitia maisha ya hawa Mungu aliwafundisha wana wa Israeli jinsi ya kuishi katika njia zake. Vilevile akawa anasema nao mara kwa mara kupitia manabii wake wengi na waamuzi na mfano Samweli, Isaya, Yeremia, Danieli, Yona,Malaki N.k.

Hivyo kwa kupitia hao pia, na vitabu vyao walivyoviandika, iliwasaidia wana wa Israeli walishike na kulikumbuka agano ambalo aliingia nao zamani.

Kwahiyo tunapovisoma vitabu 39 vya Agano la Kale,.. tunafahamu kuwa ni jumuisho la sheria zote na kanuni zote za Mungu kwa wale alioingia nao agano kupitia Ibrahimu.

Sasa mpaka hapo umeshapata msingi wa Agano la kale kwa ufupi lilipoanzia..


      2.  Tukirudi kwenye agano jipya..

Hilo ni agano lingine lili bora zaidi kuliko lile la Ibrahimu.,

Hili nalo  Mungu aliingia katika agano na mtu mmoja tu, kama vile alivyoingia na Ibrahimu.. Na mtu huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

Ibrahimu alipewa tu uzao wake wa kimwili, lakini huyu alipewa uzao wa wote wenye mwili wakimwamini tu kwa kuzaliwa mara ya pili.

Na ndio maana kuna umuhimu wa kila mmoja wetu kuzaliwa mara ya pili ili tufanyike kuwa uzao wake. yeye mwenyewe alisema..

Yohana 3:3  “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”.

Na kubatizwa kwetu ndio ishara ya tohara yenyewe ya rohoni kama ilivyokuwa kwa Ibrahimu na watoto wake wote walipotahiriwa kwa kutolewa magovi. Vivyo hivyo na sisi tunapaswa tukabatizwe kama ishara ya kutahiriwa mioyo yetu.

Lakini tukishazaliwa mara ya pili, hilo tu peke yake haitoshi, ni sharti pia tujue kanuni, na amri Mungu anazozitaka za agano hili ili tuweze kudumu ndani yake. Kama Uzao wa Ibrahimu ulivyopewa.

Hapo ndipo vitabu vya Injili ya Yesu Kristo, na vile  vya mitume, viliandikwa kwa ajili yetu ili sisi sote tutakapovisoma na kuvishika basi tuweze kudumu na kuimarika katika hilo agano jipya la Damu ya Yesu Kristo.

Ndipo hapo tunakutana na vitabu 27 vya agano jipya.

Hivyo kwa kwa hitimisho fupi.. Agano jipya ni agano Mungu aliloingia na Yesu pamoja na uzao wake wote. Ambao mimi na wewe tunahesabiwa katika uzao huo  kwa kumwamini Yesu na kubatizwa.

Tukifanikiwa kufanya hivyo basi na baraka zote, Mungu alizomuahidia Yesu Kristo, na sisi sote pia tunazishiriki na kuzirithi, ikiwemo uzima wa milele.

Bwana akubariki.

Je! Na wewe upo ndani ya agano jipya? Kama bado basi fanya hima ukaribishe Yesu leo ndani ya maisha yako akuokoe ufanyike uzao wa kifalme. Kumbuka hii ni neema ambayo sisi watu wa mataifa hatukustahili, hivyo uiichezee hata kidogo..

1Petro 2:9  “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; 10  ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema”.

Haleluya.

Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

UTIMILIFU WA TORATI.

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

KUTAHIRIWA KIBIBLIA

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UPENDO WA MUNGU.

Upendo wa Mungu ni upi?


Kwanza kabla ya kufahamu upendo wa Mungu upoje, ni muhimu kufahamu aina za upendo. Zipo aina kuu tatu za upendo.

  1. Aina ya kwanza ni Upendo unaotokana na hisia, ujulikanao kama EROS. Huu ndio upendo wa mke na mume, katika biblia tunaweza kuona Sulemani akiueleza kwa mapana na marefu katika kitabu cha Wimbo ulio Bora.

Wimbo ulio bora 1:13 “Mpendwa wangu ni kama mfuko wa manemane Ukilazwa usiku maziwani mwangu. 

14 Mpendwa wangu ni kama kishada cha hina, Katika mizabibu huko Engedi. 

15 Tazama, u mzuri, mpenzi wangu, U mzuri, macho yako ni kama ya hua.  16 Tazama, u mzuri, mpendwa wangu, Wapendeza, na kitanda chetu ni majani; 

17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, Na viguzo vyetu ni miberoshi.”

  1. Upendo wa pili ni ule unaozuka kutokana na mahusiano mtu mmoja alio nao kwa mwingine, almaarufu kama PHILEO,. Huu unaweza ukawa upendo wa mtu na ndugu yake, mchezaji mwenzake, mfanyakazi mwenzake, mwanafunzi mwenzake, mkristo mwenzako, n.k. ni upendo ambao kama hakuna kitu cha kuwaunganisha pamoja, au faida fulani kupatikana, hauwezi kuzaliwa.

Upendo wa namna hii sio upendo mkamilifu sana (ikiwa na maana haujafikia viwango vile vyenyewe),  mkristo, kwasababu hata wenye dhambi wanaweza kuwa nao, Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5.46  “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47  Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48  Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

  1. Upendo wa tatu ndio mkuu kuliko yote unajuliana kama AGAPE (UPENDO WA KI-MUNGU).

Huu ndio Upendo ambao Yesu alikuwa anaulenga kila mahali, Ni upendo usiokuwa na masharti, Unampenda mtu bila ya kuwa na sababu yoyote ya kukufanya umpende, haijalishi awe nawe anakupenda au hakupendi, anakuchikia au hakuchukii,  anakusema vibaya au hakusemi vibaya..Unapenda bila masharti, aina hii ya upendo ndio aliokuwa nao Yesu.

Biblia imeziorodhesha tabia za Upendo huo wa ki-Mungu katika kitabu cha Wakoritho wa kwanza. Tusome.

 1Wakoritho 13:4  “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5  haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6  haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7  huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8  Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika”.

Hivyo mpaka hapo sasa umeshauelewa huu upendo wa Mungu ni upi? Ni upendo usiojali wewe ni nani na ndio maana biblia ilisema..

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Hivyo kama wewe ni mwenye dhambi ujue kuwa Mungu anakupenda na ndio maana anataka kukuokoa usiende kuzimu na dhambi zako, haijalishi ulimkosea kiasi gani, leo hii yupo tayari kukusamehe na kukupa uzima wa milele, Hivyo usikiapo ujumbe huu, usiufanye moyo wako kuwa mgumu bali, mgeukie yeye na akusemehe dhambi zako.

Hizi ni siku za mwisho ukifa na dhambi zako hakika utakwenda kuzimu.

Shalom.

Upendo wa Mungu, ni wa kipekee sana.

Mada Nyinginezo:

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

UNYAKUO.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

Print this post

SIKU ZA MWISHO WA DUNIA.

Siku za mwisho wa dunia zitakuwaje?


Ukweli ni kwamba dalili zote zinaonyesha kuwa tunaishi katika siku hizo.

Shetani anawapufusha watu wengi macho wasilione hilo, ili waendelee kujiburudisha katika mambo maovu ya ulimwengu huu ili siku hiyo iwajilie kwa ghafla kama ilivyowajiliwa watu wa Sodoma na Gomora, na watu wa Nuhu.

Kabla ya hii dunia kuisha kuna mambo kadha wa kadha ambayo yatatangulia.

  • Kwa ufupi tukio la kwanza ambalo ni kuu tunalolingojea sasa hivi ni tukio la UNYAKUO.

Ikiwa bado hujafahamu Unyakuo ni nini, na litawahusu nani na nani bofya hapa ili ufahamu >> UNYAKUO.

Sasa ikitokea mfano Yesu amerudi leo, na ameshanyakua watakatifu wake, basi dunia hii itakuwa imebakiwa na muda mfupi sana usiozidi miaka 7 tu mpaka iishe, Hiyo ni kulingana na unabii wa Danieli (Soma Danieli 9:24-27). Ili kufahamu vema bofya hapa >> DANIELI: Mlango wa 9

  • Sasa ndani ya hicho kipindi cha miaka saba Mpinga-Kristo atanyanyuka ili kuleta dhiki kuu kwa wale ambao watakuwa wamebaki hapa duniani hawakwenda katika unyakuo. Yeye ndiye atakayelisimamisha chukizo la uharibifu..Kwa maelezo marefu fungua hapa kufahamu Zaidi >> CHUKIZO LA UHARIBIFU
  • Sasa mpinga-Kristo akishamaliza kazi yake, kutakuwa na mapigo mengine ya Mungu ya vitasa saba, mahususi kwa ajili ya kuwaadhibu wale wote watakaokuwa hai ulimwenguni kwa wakati huo bofya hapa ili kujua urefu wa mapigo hayo. >> SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!
  • Kisha baada ya hapo  itafuata Hukumu ya Mungu kwa mataifa. Na hapo ndipo Mungu atakapotenga mbuzi na kondoo.. Kondoo atawaweka mkono wake wa kuume, na mbuzi atawaweka mkono wake wa kushoto.

Siku za mwisho wa dunia.

  • Na baada ya hapo utaanza utawala wa Amani wa miaka 1000 duniani wa Yesu Kristo(Hiyo ni baada ya dunia na waovu wote kusafishwa). Bofya hapa >> UTAWALA WA MIAKA 1000.
  • Na mwisho wa ule utawala wa miaka 1000 shetani atafunguliwa kwa muda tena kuwajaribu watu watakaokuwepo ulimwengu wakati huo..Hapo ndipo atakapokamatwa na kutupwa katika lile ziwa la moto.
  • Kisha kitakachofuata ni hukumu ya kiti cheupe cha enzi cha mwana-kondoo. Hapo ndipo mataifa yote yatapokusanyika yahukumiwe.
  • Na kila kitu kikishakwisha, Ile Yerusalemu mpya itashuka kutoka mbinguni. Na ndipo maskani ya Mungu itakuwa Pamoja na wanadamu. Na watu wataishi na Mungu milele na milele na milele isiyokuwa na mwisho. >> UFUNUO: Mlango wa 21

Hakutakuwa na machozi tena wala vilio, wala misiba, wala huzuni,wala magonjwa wala majaribu. Bali tutaishi na Mungu wetu katika furaha isiyokuwa na kifani milele na milele, kipindi hicho ndicho tutakachojua nini maana ya Maisha..kwasasa umilele wote huo tutakaishi na Mungu tutayajua mengi sana.

Ni jukumu letu mimi na wewe, kukaza mwendo kipindi hichi, ili tuhakikishe kuwa Unyakuo hautupiti.

Kufahamu zaidi juu ya siku za mwisho wa dunia, angalia mada nyinginezo chini..

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAONO YA NABII AMOSI.

BONDE LA KUKATA MANENO.

MPINGA-KRISTO

MIHURI SABA

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Lewiathani ni nani?

Lewiathani ni nani?


Zaburi 104: 25 “Bahari iko kule, kubwa na upana, Ndimo mlimo viendavyo visivyohesabika, Viumbe hai vidogo kwa vikubwa.

26 Ndimo zipitamo merikebu, Ndimo alimo LEWIATHANI ULIYEMWUMBA ACHEZE HUMO.

27 Hao wote wanakungoja Wewe, Uwape chakula chao kwa wakati wake”

Vipo viumbe vingi vilivyopo ambavyo havijagunduliwa bado, na pia vipo baadhi ambavyo vilipotea wakati wa gharaka…tafiti zinaonyesha kuna idadi kubwa sana ya viumbe vinavyopotea kila siku duniani, inakadiriwa kuwa kati ya aina 200-2,000 ya viumbe vinapotea kila mwaka ulimwenguni ambayo ni idadi kubwa sana, na vipo pia ambavyo vinagunduliwa, ambavyo vilikuwa havijawahi kufahamika.

Sasa kama biblia inavyosema hapo juu kuna nyoka baharini aitwaye “lewiathani”..Huyo nyoka ni kweli yupo…Ni aina ya nyoka tu ambao pengine wanaweza kuwa wakubwa zaidi kuliko nyoka wa kawaida kama chatu au anakonda na wenye uwezo mkubwa, lakini wamo humo baharini, na Wanasayansi bado hawajawaona, lakini labda watakuja kuwaona au walishatoweka zamani kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi…lakini watu walioishi zamani waliwajua nyoka hao kiundani.

Lakini hilo sio la muhimu sana, kufahamu kama wapo au la!…na wala si suala la kuweka hofu, kwamba kitakuwa ni kiumbe cha kutisha sana na cha kuogopeka…Kwasababu viumbe vyote vilivyoumbwa na Mwenyezi Mungu vimewekwa chini ya Mwanadamu, avitiishe na kuvitawala, hakuna kiumbe chochote kilichomzidi mwanadamu kwa uweza na nguvu…Hivyo hata vikiwa na umbo kubwa na la kutisha kiasi gani, bado havitakuwa na akili kama mwanadamu, na vitakuwa chini ya mwanadamu tu!…haijalishi vitakuwa vimesifiwa kiasi gani katika biblia, bado havitakuwa na utashi wala akili ya kumzidi mwanadamu..

Kwamfano utaona katika biblia wanyama wengine wakisifiwa sana (Ayubu 40:16-24, na Ayubu 41:12-34), lakini bado haviwezi kulinganishwa na mtu.

Na huyu Nyoka anayeitwa LEWIATHANI ni hivyo hivyo..ni mnyama tu kama wanyama wengine, haijalishi atasifiwa kiasi gani lakini bado atakuwa ni mnyama tu atakayekuwa chini ya mwanadamu.

Ayubu 3:7 “Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe.

8 Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani”.

Sasa kwanini biblia imtaje huyu Lewiathani?.

Biblia mara nyingi inatumia Wanyama kuwafananisha na watu…kwamfano utaona shetani anatambulika kama JOKA (Ufu.12), kutokana na mnyama wa kwanza kukaribisha dhambi ulimwenguni kuwa “nyoka”..hali kadhalika Bwana wetu Yesu anafahamika kama “mwanakondoo” kutokana na tabia ya upole wa kondoo n.k

Hivyo pia Lewiathani kama nyoka aishie baharini tabia zake zimefananishwa na tabia za mpinga-Kristo ambaye siku za Mwisho Bwana atamwua.

Isaya 27:1 “Katika siku hiyo Bwana, kwa upanga wake ulio mkali, ulio mkubwa, ulio na nguvu, atamwadhibu lewiathani, nyoka yule mwepesi, na lewiathani, nyoka yule mwenye kuzonga-zonga; naye atamwua yule joka aliye baharini”.

Tunasoma pia katika…

2Wathesalonike 2:7 “Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;

9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;

10 na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa”.

Siku za mwisho Bwana atamharibu mpinga-kristo na wafuasi wake wote…Bwana atusaidie kutuepusha na roho ya MpingaKristo ambayo inatenda kazi sasa.

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

https://wingulamashahidi.org/2019/08/30/maswali-na-majibu-2/

Nini maana ya ‘Usimwekee mtu mikono kwa haraka’?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNACHEZA MPIRA.

Kuota unacheza mpira kuna maanisha nini kiroho?


Ndoto za namna hii kuwa zinakuja kutoka katika makundi mawili,

Kundi la kwanza ni kutokana na shughuli za kila siku.

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;..”.

Kwamfano kuota unacheza mpira, asilimia kubwa ya ndoto hii huotwa na wanaume. Na hiyo ni kutokana na kwamba aidha mtu huyo kwa sasa anajishughulisha na mchezo wa mipira, au huko yumba alishawahi kucheza mpira, aisha shuleni au mitaani n.k..

Sasa ukiota ndoto ya namna hii mara kwa mara, basi huna haja ya kuwa na wasiwasi kwani ni ndoto tu, ambayo imekuja kutoka na shughuli za kila siku, Na hiyo inakuwa haina maana yoyote rohoni.

Kundi la Pili, ni kutokana na Mungu.

Lakini pia, ndoto kama hiyo inaweza kuja kwa namna ya kipekee sana, yaani kwa uzito usiokuwa wa kawaida, pengine ulikuwa unashindana sana kucheza, timu yako imezidiwa sana, au mmewazidi wale wengine sana, au wewe unacheza vizuri au vibaya kuliko wengine.. Kiasi kwamba ulipoamka  imekukaa sana akilini tofauti na ndoto ambazo ndoto ambazo unaotaga kila siku.

Basi ukiona hivyo lipo jambo Mungu anakukumbusha.

Kumbuka hapa dunia tupo katika mashindano, Na kila mmoja ni kama mchezaji, Na Lengo la mchezaji sikuzote ni kushinda tu, na sio kushindwa, ili mwisho wa siku akapokee medali ya dhahabu au kombe.

Biblia inasema..

1Wakoritho 9.24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

25 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.

26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Unaona, wewe kwa upande wako ulijiona unashiriki katika mchezo aina ya mpira, wengine wanaota wakikimbia riadha, wengine wakiogelea n.k.

Hivyo kuota unacheza mpira ni Mungu anakukumbusha kuwa upo kwenye mashindano ndugu. Sijui kwa upande wako maisha yako yapoje, kwasababu watu wengine Mungu anazungumza nao hata mara mbili au mara tatu, ili tu waelewe sauti ya Mungu..Lakini hawasikii. Soma hapa..

Ayubu 33:14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao”,

Hivyo kama wewe ni mmojawapo na bado upo nje ya Kristo, ni heri ukajitathamini vizuri tena. Kwasababu Yesu anao mpango mkubwa na wewe katika maisha yako haijalishi wewe ni muislamu na nani. Unachopaswa kufanya ni kumgeukia tu yeye uanze kushindana mashindano ambayo alikukusudia wewe ushindane ya kwenda mbinguni.. Kwasababu lipo taji bora alilokuandalia.

Si bahati mbaya ukutane na ujumbe huu. Hivyo usipuuzie, Mungu anakupenda, na anataka kukuokoa.

Ubarikiwe.

Fuatilia vichwa vingine vya masomo vilivyoainishwa chini ikiwa utahitaji kumjua Kristo zaidi.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Je ushabiki wa mpira ni dhambi?

USIYADHARAU MARUDIA YA BWANA.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA NYOKA.

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Sala ya Toba na Rehema.

Ni jambo jema kutafuta sala ya toba na rehema, angali muda upo.

Inawezekana umemkosea Mungu sana, na leo unatamani kujua kama ipo njia ya kumrudia yeye tena, inawezekana, umeua, au umetoka nje ya ndoa, au umetoa mimba, umemtukana Mungu, umeiba, umeenda kwa waganga, umewavunjia heshima wazazi wako, umeaudhi watu wengine n.k.

Inawezekana pia wewe ni mmojawapo wa ambao wameona kuendelea kuishi Maisha bila Mungu ni kupotea tu, na umeamua sasa uutafute uso wake. Basi kama wewe ni mmojawapo, uamuzi ulioufikiria ni mzuri sana, Na yapo makusudi makubwa sana Mungu kukufikisha mahali hapa,

Bwana Yesu alisema..

Yohana 6:37  “Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe”.

Kama leo umeamua kudhamiria kweli kutubu dhambi zako, basi ni ahadi yake kuwa hatakutupa nje kamwe! Kuanzia huu wakati na kuendelea utaona maajabu makubwa sana katika Maisha yako kama ilivyokuwa hata kwetu.

Kinachohitajika ni wewe tu, kumaanisha kabisa kutoka katika moyo wako kwamba kuanzia leo, wewe na dhambi basi! Ulimwengu nyuma Yesu mbele, hilo tu, pekee linatosha wewe kuupokea wokovu wa Bwana..Anataka kukusamehe lakini ni mpaka pale wewe utakapojutia na kusema mimi ninauaga ulimwengu kwa miguu yote miwili.

Wengi wanadhani ni sala Fulani tu, ndio inayompa mtu wokovu, hapana, nitakuonyesha sehemu kwenye biblia mwanamke mmoja mwenye dhambi nyingi (kahaba) kwa kujutia tu makosa yake, mpaka kulia machozi mengi sana mbele za Yesu..Hilo peke yake lilitosha kwa Yesu kuuona moyo wake uliomaanisha kutubu  na saa ile ile Yesu akamwambia, UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO. Soma (Luka 7:36-48), utathibitisha hilo.

Hivyo hata na wewe leo ukitia Nia kweli kweli, basi sala fupi nitakayokuambia uiombe  hapo mbele kidogo, italeta mabadiliko makubwa sana katika Maisha yako ya rohoni. Kwasababu moja kwa moja Kristo anakwenda kuingia ndani  yako kukubadilisha, na kuanzia huu wakati na kuendelea ataendelea kuwa na wewe kukusaidia kushinda na baadhi ya yale mambo ambayo ulikuwa huwezi.

Hivyo kama upo tayari kutubu leo dhambi zako, basi

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Sasa unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Yesu mwokozi yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Pia unaweza kuihifadhi tovuti yetu hii , katika kumbukumbu zako (www.wingulamashahidi.org), ili wakati mwingine ikusaidie, kwani yapo mafundisho mengi Zaidi ya 1000  na maswali mengi ya biblia yaliyojibiwa, ambayo unaweza ukajifunza na kuimarika kiroho sana, ukiwa hata hapo hapo nyumbani kwako kwenye simu yako.

Ubarikiwe sana

Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

YESU MPONYAJI.

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

UMEFUMBULIWA MACHO YAKO YA KIROHO?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

MKATAE SHETANI NA MAWAZO YAKE YA KIBINADAMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

Ndio yupo samaki ajulikanaye kama nguva, kwa lugha ya kiingereza anaitwa Sea cow, kwa maelezo yake marefu juu ya mwonekano wake na jinsi anavyozaa, na kuishi baharini msome Wikipedia kwa link hii>> https://sw.wikipedia.org/wiki/Nguva

Lakini huyu samaki nguva sio kama wale watu wanaomaanisha kwamba anakiwili wili cha mwanadamu na mkia wa samaki (samaki mtu).. Katika uumbaji wa Mungu hakuna kiumbe kama hicho, wala huwezi kukikuta katika bahari yoyote duniani.

Viumbe hawa walianza kuzungumziwa tangu zamani kwenye hadithi za kimila za mataifa mbali mbali,huko Asia na Ulaya lakini katika maisha halisi hawapo, wengine wanasema samaki hao wanaweza wakaongea kama mwanadamu, lakini hilo jambo ni batili.

Katika Biblia kiumbe kama huyu hajatajwa, aliyetajwa ambaye kidogo aliweza kumkaribia mwanadamu ni NYOKA peke yake, Na hiyo ilikuwa ni kabla hajalaaniwa(Mwanzo 3:1)..Yeye ndiye aliyekuwa mwerevu kuliko wanyama wote mwituni, aliweza kuongea kama mtu, na alikuwa anatembea kwa miguu, lakini alipolaaniwa ndio akawa nyoka huyu ambaye tunayomwona sasa, anatembea kwa matumbo, hata akili yoyote.

Kwahiyo baada ya hapo hakukuwa na kiumbe mwingine yeyote aliyemkaribia mwanadamu.

Lakini pia ni vizuri kufahamu, mambo mengi sana ya ki-pepo, yanahushishwa na hivi viumbe vya kudhaniwa wasio halisi.. kwamfano Dragoni, joka lenye vichwa saba litoalo moto mdomoni, ni mungu wa jamii Fulani huko Asia, hususani China, ambaye kiuhalisia nyoka huyo hayupo duniani, fuatilia tena tembo mwenye mikono mingi huko India, samaki mtu, n.k.

Hivyo kuwa makini na elimu kama hizo, ni rahisi kushawishiwa kuwa viumbe kama hao wapo, na kupewa maelekezo jinsi ya kuwaona au kukutana nao, kumbe hujui ndivyo unavyoingizwa katika elimu za mashetani na mwisho wa siku unazama kabisa huko, unadhani umefanikiwa kuwaona kumbe ni mapepo yaliyojigeuza kwa mfano wa hivyo viumbe visivyo halisi..

Hizi ni siku za mwisho za hatari biblia inasema..

1 Timotheo 4 :1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;”

Unaona? Mafundisho ya mashetani yamezaa kila kona..Na kama husomi biblia yako, basi upo hatarini kuchukuliwa nayo moja kwa moja..Je! Umempa Yesu maisha yako? Kama sivyo unasubiri nini, huoni kama upo hatarini? Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho. Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwake, na yeye ni mwaminifu atakuokoa na kukusamehe makosa yako yote, haijalishi ulifanya dhambi kiasi gani.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

 

MAFUNDISHO YA MASHETANI

NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI.

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

PARAPANDA ITALIA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

PARAPANDA ITALIA.

Siku moja inapopita, ndivyo tunavyoikaribia ile siku kuu ya kwenda mbinguni, siku ile ya Parapanda kulia, ambapo watakatifu wote duniani wataisikia, hakika itasikiwa na wao tu, na sio kila mtu duniani kama wengi wetu tunavyodhani…Watu wenye dhambi wakati huo hawataisikia parapanda hiyo hata chembe..

Siku hiyo pengine itakuwa ni asubuhi kwa upande wetu, au jioni au  usiku wa manane ukiwa umelala.. Kama wewe ni mtakatifu utasikia sauti nzuri ya shangwe, ikiambatana na parapanda ya Mungu, na wale wafu waliokufa katika Kristo, wao nao pia wataisikia kutoka kule makaburini, na kufufuka na kuanza kutembea duniani, na wewe utawaona, halafu ghafla, tutaliona jeshi kubwa la malaika likitokea, likiambatana na Bwana, na wakati huo huo ghafla tutaona miili yetu ikibadilishwa kutoka katika miili hii ya unyonge ya mauti na kuwa miili ya utukufu, wakati hilo likuwa linaendelea katika kipindi kifupi sana cha kufumba na kufumbua tutajikuta mawinguni na Bwana YESU, huo ndio wakati tutaenda naye kule mbinguni kula naye ile karamu ya mwana kondoo aliyokwenda kutuandalia miaka 2000 iliyopita.

Unaweza kudhani jambo hilo ni bado sana, lakini nataka nikuambie mimi na wewe tunaishi katika yale majira ya kuja kwa Bwana mara ya pili. Dalili zote zinaonyesha, Angalia milipuko ya magonjwa mfano wa Tauni (Corona) yaliyotabiriwa na Bwana Yesu yakitokea ulimwenguni (Luka 21:11)..Hiyo ni dalili ya kwamba tupo ukingoni mwa wakati kuliko tunavyoweza kudhani, angalia tena kuchipuka kwa taifa la Israeli, yaani mtini, ndio kunathibitisha kabisa wakati wa majira ya mataifa(yaani mimi na wewe) upo ukingoni.

Jambo ambalo wakristo wengi hatufahamu, ni pale tunapodhani Mungu ana ile kauli ya “wengi wape”..Yaani, kwasababu ulimwengu huu uliojawa na uovu na waovu wengi Mungu hawezi kuuangamiza au kunyakua wale wachache walio waaminifu kwake..

Yesu alisema kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, na kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, jiulize, waliookoka katika siku za Nuhu walikuwa ni wangapi kama sio 7 tu katika ya mabilioni ya watu waliokuwa ulimwenguni, vilevile waliookoka katika siku za Lutu walikuwa wangapi kama sio watatu katika ya Malaki ya watu waliokuwa katika miji ile ya Sodoma na Gomora,

Ukitazama tena kwa ukaribu utaona aliye nyakuliwa alikuwa  ni mtu mmoja tu (HENOKO) kati ya watu wote waliokuwa wanaishi kipindi chote kabla ya gharika, kwasababu ni yeye tu peke yake ndiye aliyempendeza Mungu.

Vivyo hivyo katika wakati huu watakaonyakuliwa ni wale tu watakaompendeza Mungu, hao ndio peke yao watakaosikia Parapanda ya Mungu ikilia kutoka mawinguni, hata kama watakuwa ni watu 100 katika ulimwengu mzima, hao tu ndio watakoenda, wengine wote waliosalia hawatajua chochote, watashangaa tu mbona kundi dogo la watu wachache sana halipo duniani..

Wengine watadhani, wameibiwa tu, wengine watadhani wametoroka, n.k. Lakini ulimwengu hautaelewa chochote kwasababu litakuwa ni kundi dogo sana, kumbe hawajui wenzao siku nyingi tayari wapo mbinguni wakila karamu ya mwana kondoo, lakini huku chini kitakachokuwa kinaendelea ni dhiki kuu ya mpinga Kristo. Na baada ya hapo ni maangamizo.

1Wathesalonike 4:16  “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17  Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.

18  Basi, farijianeni kwa maneno hayo.”

Ndugu yangu jiulize, Yesu akirudi leo utakuwa katika upande upi? Na injili zote hizi ulizosikia utajitetea vipi siku ile kusema hujaambiwa? Ishara zote hizi za siku za mwisho utajitetea vipi siku ile mbele za Mungu? Mungu ni mwingi wa rehema lakini pia ana ghadhabu nyingi.

Ili kufahamu vizuri ni jinsi gani tunaishi katika siku za mwisho angalia MADA nyingine, mwisho kabisa wa somo hili, uone ni wakati gani huu tunaishi..

Kama hujaokoka, basi huu ndio wakati wako wa kuyatengeneza mambo yako na Kristo, ili kusudi kwamba hata ikitokea paraparanda italia leo usiku basi uwe na uhakika kuwa na wewe utakwenda kumlaki mawinguni. Unachopaswa kufanya ni kukusudia tu kumkaribisha Yesu maishani mwako, kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, na kuwa tayari kuyaanza Maisha mapya  ya wokovu.

Kama utamaanisha kufanya hivyo ni ahadi yake kuwa atakuja ndani yako na wewe kuanzia huo wakati utaanza kuona badiliko kubwa ndani yako, hivyo kama upo tayari kufanya hivyo sasa,

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tazama mada nyingine chini zinazoeleza Habari za kurudi kwa Kristo duniani..

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAONO YA NABII AMOSI.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

RAFIKI MWEMA.

Rafiki mwema ni nani?


Uzuri ni kwamba kila mmoja wetu alishawahi kuwa na rafiki au marafiki katika maisha yake.. Kama ulishawahi kuwa na marafiki wengi utagundua kuwa wengine walikuwa marafiki zako kwasababu mliendana tu tabia hivyo tu,, na  wengine walikuwa marafiki kutokana na maslahi Fulani au mazingira Fulani au fursa Fulani, labda shuleni,  au kwenye biashara au kazini, au katika mambo ya kiimani n.k…

Kati ya hao wapo ambao ni wa kudumu yaani mnaweza kupotezana hata kwa muda mrefu lakini urafiki wenu ukadumu palepale, au mazingira Fulani yakatokea aidha ya kutofautiana kipato lakini bado urafiki wenu ukaendelea kudumu,  na wapo ambao ni wa muda tu, kukitokea kutengana kidogo, au mazingira Fulani kubadilika basi urafiki huo unakufa hapo hapo..

Lakini kwa vyovyote vile katika makundi yote hayo swali ni je utawezaje kumtambua rafiki mwema?

Jibu ni rahisi rafiki mwema, ni Yule ambaye atauweza kuutoa uhai wake ili wewe upone. Kwamfano, rafiki  yako asikie wewe umelazwa figo zako zote mbili zimekufa upo hoi kitandani mahuti huti, ili uishi ni lazima figo zote mbili zipatikane kutoka kwa watu wengine ili upachikwe wewe uendelee kuishi, Halafu wakati huo huo anatokea rafiki yako, ambaye hana hata undugu na wewe, mlikutana tu mkaendana tabia, mkashirikiana pamoja..

Na sasa anakuambia rafiki yangu, mimi leo hii nimeamua kuzitoa figo zangu zote mbili, ili wewe upone, Unaweza ukajiuliza huyu mtu anawaza nini? Akitoa figo zake sisi yeye atakufa, na itakuwa hasara tu ile ile..Ukizingatia yeye bado anayo malengo yake mengi ya maisha, mimi ninafaida gani kwake? Pengine unamkatalia Lakini yeye bado anakusisitiza kuwa anakwenda kutoa figo zake zote mbili afe ili wewe upone.. Na kweli anakwenda kufanya hivyo. Anatolewa unapewa wewe na yeye muda huo huo anakufa.. Je! Mtu kama huyo si zaidi ya rafiki mwema kwako?

Ukweli ni kwamba Katika ulimwengu mzima hakuna mtu anayeweza kufanya hivyo..

Lakini habari njema ni kwamba yupo ambaye aliweza kufanya hivyo kwa ajili yangu na wewe ili tupone..Na mtu huyo si mwingine zaidi ya YESU, alisema mwenye hivi…

Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo”.

Upendo huu ni zaidi ya upendo wa ndugu, Ndugu yako hawezi kuifikia hatua hii, ya kufa ili wewe uokoke, lakini Kristo alikufa ili mimi na wewe tupate uzima wa milele..

Na ndio maana maandiko yanasema..

Mithali 18: 24 Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.

Sasa huyu rafiki aambatanaye kuliko ndugu, ndio YESU KRISTO mwenyewe..

Hivyo ukimkaribisha huyu maishani mwako, ni uhakika kuwa utakuwa salama, na hutakuwa na wasiwasi kwamba utapotea tena baada ya hapo, kwasababu yeye tayari alishalipa gharama za upotevu wako kabla hata hujazaliwa. Kwahiyo kama ukimfanya leo kuwa rafiki yako, basi atakuwa rafiki yako kweli kweli, na mema yote utayaona..

Lakini ule mtari wa 14 anasema..

“Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.”

Unaona?  Ili na wewe Yesu awe rafiki yako ni sharti utii anayokuamuru.. Kama ulikuwa ni mwenye dhambi unatubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, kisha unakwenda kubatizwa katika maji mengi kama alivyotupa  maagizo katika Mathayo 28:19, Na baada ya hapo atakutia muhuri kwa Roho wake Mtakatifu atayemwachilia ndani yako wakati huo huo. Na hapo ndipo utakuwa na uhakika kuwa sasa umeshafanyika kuwa rafiki yake.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

YESU MPONYAJI.

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

HATA NA BARNABA PIA AKACHUKULIWA NA UNAFIKI WAO!!

Rudi Nyumbani:

Print this post