Title 2020

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

Biblia inasema kila jambo na majira yake (Mhubiri 3)…maana yake ni kwamba hata mti una majira yake ya kuzaa matunda…sio kila wakati, tutakwenda kukuta maembe katika mti wa muembe…Inahitajika uwe ni msimu wa maembe ndipo mti uzae…Haijalishi huo mti utaumwagilia maji kiasi gani, au utauwekea mbolea kiasi gani…Kama sio msimu wake wa kuzaa hautazaa….Hiyo yote ni kwasababu gani?..Ni kwasababu kila jambo lina majira yake.

Vivyo hivyo katika roho, tangu Bwana wetu Mkuu Yesu Kristo, apae juu mbinguni kwenda kutuandalia makao..majira yalibadilika…kabla ya hapo hakukuwa na mlango wowote wa sisi kumzalia Mungu matunda anayoyataka…ikiwa na maana waliokuwa na fursa ya kumjua Mungu kwa undani na kunufaika sana walikuwa ni manabii wa Mungu wachache waliochaguliwa..na si watu wote, Roho Mtakatifu alikuwa anashuka juu ya watu wa Mungu wachache aliowachagua…kasome vizuri habari ile ya Musa katika..

Hesabu 11:24 “Musa akatoka, akawaambia watu maneno ya Bwana; akawakutanisha watu sabini miongoni mwa wazee wa watu, akawaweka kuizunguka Hema.

25 Ndipo Bwana akashuka ndani ya wingu, akanena naye, akatwaa sehemu ya roho iliyokuwa juu ya Musa, akaitia juu ya wale wazee sabini; ikawa, roho hiyo ilipowashukia, wakatabiri, lakini hawakufanya hivyo tena.

26 Lakini watu wawili walisalia kambini, jina la mmoja aliitwa Eldadi, na jina la wa pili aliitwa Medadi; na roho ile ikawashukia; nao walikuwa miongoni mwao walioandikwa, lakini walikuwa hawakutoka kwenda hemani; nao wakatabiri kambini.

27 Mtu mmoja kijana akapiga mbio, akaenda akamwambia Musa, akasema, Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.

28 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa tangu ujana wake, akajibu akasema, Ee bwana wangu Musa, uwakataze.

29 Musa akamwambia, Je! Umekuwa na wivu kwa ajili yangu; INGEKUWA HERI KAMA WATU WOTE WA BWANA WANGEKUWA MANABII NA KAMA BWANA ANGEWATIA ROHO YAKE.

30 Kisha Musa akaenda akaingia kambini, yeye na wale wazee wa Israeli”.

Umeona hapo mstari wa 29?.. Musa anasema ingekuwa heri kama watu wote wa Bwana, Bwana angewatia roho yake…Ikiwa na maana kuwa ni wachache tu waliochaguliwa kwa Neema ndio waliokuwa wananufaika na kipawa cha Roho Mtakatifu. Wengine wote walitamani lakini hawakukipata. Kwanini?..ni kwasababu haukuwa wakati wala majira ya kitu hicho, kushuka kwa watu wote.

Lakini Bwana Mungu wetu, ambaye ni alitabiri kwamba utafika wakati Roho huyu atamwagwa kwa wote wenye mwili…huo utakuwa ni msimu wa kuzaa matunda…Kwahiyo watakaozaliwa msimu huo watakuwa na bahati sana..Na wakati huo si mwingine zaidi ya tangu ule wakati Bwana wetu alipopaa mbinguni mpaka wakati huu wa sasa tunaouishi sisi.. Bwana alisema…

Yoeli 2:27 “Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe.

28 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono”

Hii ni neema ya ajabu sana, ambayo hatupaswi tuipuuzie…Huu ndio wakati uliokubalika wa Bwana kutumwagia kipawa chake cha Roho Mtakatifu pasipo ubaguzi…Ndio maana biblia inasema katika…

2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati ULIOKUBALIKA NDIYO SASA; tazama siku ya wokovu ni sasa)”

Ndugu huu ndio wakati uliokubalika…biblia inasema watu wa zamani walikitamani hichi kipindi tunachoishi sisi…wafalme walikitamani, wakuu walitamani waonje kipawa cha Roho Mtakatifu, waliomba na kusubiri, lakini walikufa bila kuifikia hii saa tuliyopo sasa..Lakini sisi ndio tupo hiyo saa, ambayo yule Roho aliyeshuka juu ya Musa, ndiye huyo huyo ambaye tunamiminiwa sisi wengine ambao hata hatustahili…Ni neema ya namna gani?..Tukose kila kitu lakini tusimkose Roho Mtakatifu kwasababu huyo ndiye Muhuri wa Mungu (Waefeso 4:30)..

Je umempokea huyu Roho Mtakatifu?..kama bado fahamu kuwa anapatikana bure kwa yeyote ambaye atamuhitaji, lakini hatumuhitaji kwa mdomo bali kwa vitendo..maana yake ni hii: Ili ashuke juu yako ni lazima utubu kwa kumaanisha kuacha dhambi kweli kweli…kwasababu yeye ni Roho Takatifu ya Mungu, na hivyo haichangamani na uchafu wa aina yoyote,

kwahiyo unatubu kwa dhati kabisa na kwa vitendo..kama ulikuwa unaiba unaacha wizi na kuwarudishia uliowaibia mali zao kama bado unazimiliki, kama ulikuwa unajiuza, unaacha na kufuta namba za wote uliokuwa unajishughulisha nao katika kazi hiyo, kama ulikuwa unafanya uchafu wowote ule kama kujichua, unatazama picha chafu, ulikuwa mfiraji, msagaji, mlaji rushwa, muuaji n.k unaviacha vyote hivyo…kisha unakwenda kwa Yesu, na kumwomba rehema…Na Bwana wetu mwenye huruma akiona umegeuka kwa vitendo namna hiyo…tayari Yule Roho wake Mtakatifu atakuwa ameshakukaribia sana, utaanza kuona ni kama vile ulikuwa unatembea na kuchoka na ghafla nguvu mpya imekuingia…

Na kukamilisha muhuri huo wa Roho Mtakatifu ndani yako, nenda katafute ubatizo sahihi haraka sana, na ubatizo sahihi kulingana na maandiko ni ule wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO…Kumbuka jina la Bwana Yesu ndio Jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu…Hakuna jina lingine tulilopewa sisi wanadamu litupasalo kuokolewa kwalo isipokuwa jina la Yesu.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

USIMWOGOPE YEZEBELI.

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

JIRANI YANGU NI NANI?

KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.

MPINGA-KRISTO

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Kristo hakuitwa Imanueli badala yake akaitwa Yesu?

SWALI: Unabii uliotolewa na Isaya kumuhusu Kristo unasema angekuja kuitwa Imanueli (Isaya 7:14), lakini badala yake tunaona alikuja kuitwa Yesu? Ni kwanini?


JIBU: Tukisoma pale katika Mathayo 1:19-23 Inasema..

Mathayo 1:19 “Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.

20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.

22 Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema,

23 Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; NAO WATAMWITA JINA LAKE IMANUELI; YAANI, MUNGU PAMOJA NASI”.

Jiulize ni kwanini biblia haijaishia tu pale kwenye jina Imanueli, badala yake ikamalizia kuandika mpaka tafsiri yake, yaani “Mungu Pamoja nasi”?..Ni Kwasababu msisitizo upo hapo kwenye hiyo tafsiri na sio jina tu..

Ukiangalia tena utaona Malaika anasema “Nao watamwita” Ikimaanisha “sisi” ndio tutakaomwita yeye kuwa ni Mungu ambaye yupo Pamoja nasi..Lakini yeye jina lake hasaa sio hilo bali ni YESU ..ambayo tafsiri yake ni (YEHOVA-MWOKOZI).

Jambo hilo limekuja kutimia kama lilivyo kwasababu sisi ndio tunaojua Yesu kwetu sisi si mwokozi tu, bali ni Zaidi ya mwokozi,..Ni Mungu kwetu, aliyeutwaa mwili akaishi Pamoja nasi..Kama maandiko yanavyosema..

Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu”…..

14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.”

“Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”(Wakolosai 2:9) .

“tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;(Tito 2:13)

Hivyo tunao ujasiri wote wa kusema kuwa YESU ni MUNGU WETU..

Yaani IMANUELI.

Haleluya. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

nini maana ya haya maneno aliyosema Bwana ; Tuliwapiga filimbi wala hamkucheza; Tuliomboleza wala hamkulia?

 

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

BWANA HUWAJUA HAO WAMKIMBILIAO.

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

Je! kuna ubaya wowote kuwaombea ndugu zetu waliokufa katika dhambi, Mungu awakumbuke katika ufalme wa mbinguni?.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hakuna mtu anenaye katika Roho,kusema Yesu amelaaniwa

SWALI: Mstari huu una maana gani?

1 wakorinto 12:3 “Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

JIBU: Maana yake ni kwamba hakuna mtu aliyejazwa Roho Mtakatifu anayeweza kusema Yesu amelaaniwa, hilo haliwezekani kwasababu mpaka ameshaingia ndani katika Roho hawezi kumwona Yesu kwa namna hiyo….Na vile vile hakuna mtu ambaye hajajazwa Roho Mtakatifu anayeweza kusema Yesu ni Bwana…Ni lazima yeye naye awe katika Roho Mtakatifu kwanza ndio awe na ufunuo huo wa kusema Yesu Ni Bwana,

Vinginevyo atakuwa anatamka kwa mdomo tu, kwamba Yesu ni mwokozi wangu, au Yesu ni Bwana wangu, au Yesu ni njia lakini isiwe imetoka ndani ya moyo wake…akawa anasema kishabiki tu!..au kidini tu au kwa kuiga tu!…wakati ndani ya moyo wake hajapata ufunuo kamili au hajamwelewa Yesu kabisa!…ambao ufunuo huo wa kumwelewa Yesu, unatoka kwa Roho Mtakatifu mwenyewe. Ndio maana hapo anasema pasipo Roho Mtakatifu mtu hawezi kusema Yesu ni Bwana, kutoka ndani ya vilindi vya moyo wake!!…

Na sio hilo tu!…Pia mtu ambaye hana Roho Mtakatifu biblia inasema huyo sio wa Mungu..

Warumi 8:9 “…Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.”

Kwanini sio wake?…Kwasababu huwezi kusema unamjua Mungu wakati kile kinachokufanya wewe umjue yeye hakipo ndani yako….(na hicho kinachotufanya tumjue yeye, na kutufunulia maandiko ni Roho Mtakatifu)…Kamwe hatuwezi sisi kumjua Mungu wala kumwelewa wala kumfuata yeye kwa nguvu zetu, tunamhitaji Roho Mtakatifu huyo ndiye anayetuvuta na kutusogeza kwa Mungu na kutufunulia Yesu ni nani..(Yohana 6:44, Yohana 15:16).

Hivyo ni muhimu sana kuwa na Roho Mtakatifu kwasababu huyo ndio MUHURI wa Mungu kwa mtu, Kama vile alama ya mnyama ilivyo(666), vivyo hivyo alama ya Mungu au muhuri wa Mungu ni Roho Mtakatifu ndani ya mtu (soma Waefeso 1:13, Waefeso 4:30 na 2Wakorintho 1:22).

Maran atha!

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?

Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

سؤال: ماذا كانت الشوكة في لحم بولس؟

سؤال: ماذا كانت الشوكة في لحم بولس؟

الجواب: دعنا نقرأ ،

2 كورنثوس 12: 7 “لئلا يرفعني فوق القياس من خلال وفرة الوحي ، أعطيت لي شوكة في الجسد ، رسول الشيطان ليعطفني ، لئلا أرفع من فوق القياس.

8 من اجل هذا طلبت من الرب ثلاث مرات ليخرج عني.

9 فقال لي تكفيك نعمتي لان قوتي في الضعف تكمل. لذلك ، بكل سرور ، سأفضل المجد في عيوبي ، حتى تتوقف قوة المسيح علي “

كان هناك الكثير من التكهنات حول الشوكة في جسد بول ، لا يزال البعض يعتقد أنها كانت شوكة حقيقية موضوعة على جانبه ، أنه في كل مرة يحاول التباهي بها فإنه يخترقها.

يقول آخرون أنها ذكرى للأشياء السيئة التي فعلها في الماضي ، لذلك كان الله يجلب له الأفكار التي كانت تحركه ، والتي اتضح أنها شوكة له وتوقف عن التفاخر / التفاخر.

ولكن ، في كل هذا ، إذا نظرنا عن كثب إلى الآية 7 ، فإنها تقول أن الله كان لديه شوكة في جسده “رسول الشيطان”.

تلك الكلمة ، “رسول” ، هي كلمة تعني شخصًا وليس فكرة أو فكرة أو شيء ما. حتى بالمعنى السليم ، ما علاقة شجيرة الشوك بالتفاخر؟

لذلك لم يكن بول يتحدث عن شجيرة شوكة أو بعض الأمراض في جسده ، لكنه كان يتحدث عن شخص كان مثل شوكة له.

الآن سؤال آخر ستطرحه هو لماذا يقول أنه في الجسد وليس في الروح؟

الجواب هو أن كلمة الجسد يمكن أن تعني حياة شخص أو شعب …

دعونا نقرأ الآيات التالية التي قالها الرب لبني إسرائيل وسوف نفهم المزيد.

Numbers 33:55 ولكن ان لم تطردوا سكان الارض من امامكم. فيكون ان الذين تركتهم يبقون في عينيك وشوك في جانبكم ويغشونكم في الارض التي تسكنون فيها.

56 علاوة على ذلك ، سأفعل بك ، كما ظننت أن أفعل بهم “.

Judges 2: 3 3 لذلك قلت ايضا لا اطردهم من امامك. بل يكونون كجواهر في جنبكم وتكون آلهتهم فخا لكم.

هل رأيت أن؟ .. يمكن مقارنة حياة المرء بجسد ، ويمكن تشبيه الشخص الذي يزعجك ويعذبك في حياتك بشوكة في جسمك.

ولكن إذا عدنا إلى الرسول بولس ، فمن كان هذا الشوكة؟

عندما نقرأ .. 2 تيموثاوس 4:14 تقول ..

“الإسكندر النحاسي جعلني شرًا كثيرًا: يكافئه الرب حسب أعماله:

15 منهم تكون ايضا. لأنه صمد كثيرا في كلماتنا “

لم يقدم الكتاب المقدس الكثير من المعلومات عن هذا الإسكندر ، وهو صانع نحاسي. لكنه يخبرنا أنه كان أكبر عقبة لبولس في حياته وخدمته. لم يستخدم كلمة “شرير” فحسب ، بل استخدم أيضًا كلمة “شرير كثير” ، لإظهار أن العديد من الأعمال الشريرة التي أظهرها الإسكندر لبولس.

ربما كان يسيء تمثيل بولس طوال الوقت ، كان يتحدث فقط عن أوجه القصور الخاصة به ، وكيف كان قاتلاً في الماضي (قتل واضطهاد المسيحيين) ، يشهد تصريحات كاذبة أمام الناس الذين آمنوا بولس.

وهذا جعل بول ، الذي اشتهر بالكثير من الوحي ، والكثير من المعجزات ، والخدامات العظيمة ، يبدو أنه لا يوجد في وسط بعض الذين آمنوا به.

ليس من غير المعتاد رؤيتها اليوم ، يمكنك رؤيتها للعديد من قادة العالم ، الله يرفع خصومهم كشوكة لهم ، للتحدث فقط عن شرهم ، أو عيوبهم ، بغض النظر عن عدد الأشياء الجيدة التي قام بها القائد. سمح الله بذلك حتى لا يتفاخر القائد كثيراً.

كان هذا هو الحال مع بولس بالنسبة للإسكندر الحداثي البرونزي. كان شوكة عظيمة ، حتى توسل الله أن يأخذه ، (ليقتل)

اقرأ ، ١ تيموثاوس ١: ٢٠ “منهم هميناوس والاسكندر. الذي سلمته للشيطان ، لكي لا يتعلموا التجديف “

لكن الله أخبره أن نعمته كانت كافية. لذلك بقي معها حتى وقته قد انتهى.

وبالمثل ، إذا كنا متغطرسين ، فإننا نعتقد أننا شيء ما ، فقد قمنا بشيء أفضل من الآخرين ، أو لدينا شيء أكبر من الآخرين.

لنتذكر أن الرب يستطيع أن يرفع لنا الشوك.

شالوم مران عطا!

يرجى مشاركة هذه الأخبار الجيدة مع الآخرين ، وكذلك إذا كنت ترغب في أن نرسل إليك هذه الدروس عبر بريدك الإلكتروني أو WhatsApp أرسل لنا رسالة في مربع التعليق أدناه أو اتصل عل+255 789001312(tanzania country code)


من أين حصل قايين على زوجته؟

ما هو كتاب الحياة؟

من هو الجشورون في الكتاب المقدس؟

التنين القديم

Print this post

Tofauti kati ya kuungama na kutubu ni ipi?

Kuungama kunakwenda sambamba na kutubu.

Kuungama ni kitendo cha kukiri, au kukubali makosa yako kuwa wewe ni mwenye dhambi au ulikosa na hivyo unahitaji kusamehewa.

Mathayo 3:5 “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;
6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao”.

Matendo 19:17 “Habari hii ikajulikana na Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawaingia wote, na jina la Bwana Yesu likatukuzwa.
18 Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao”.

1Yohana 1:8 “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.
9 Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Lakini kutubu ni kitendo chenyewe cha kujutia  yale uliyoyaungama tayari (yaani makosa yako)..Ili usamehewe. Na hii inaambatana na kukusidia kuyaacha kivitendo yale uliyokuwa unayafanya kwa kuomba msamaha .

Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona”.

Mathayo 21:28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.

29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.

30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.

31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Basi Yesu akawaambia, Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu.

32 Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini, nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.”

Na ndio maana mtu hawezi kusema nimetubu kama hajaungama dhambi zake, Yaani hajakubali kuwa amekosa mbele za Mungu, kwamba yeye ni mwenye dhambi na hivyo anahitaji rehema.

Mithali 28:13 “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema”.

Hivyo kutubu kunaambatana na kuungama, kama ukienda mbele za Mungu halafu huoni kosa lako nini, basi hapo hakuna toba yoyote.

Ubarikiwe.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

 

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

Rudi Nyumbani:

Print this post

KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.

Kanisa la Kristo limefananishwa na mwili wa binadamu. Kama vile mwili ulivyo na viungo mbalimbali, mfano mikono, miguu, macho, masikio, mdomo n.k. vikiongozwa na kitu kimoja cha muhimu kiitwacho kichwa. Vivyo hivyo na kanisa la Kristo. Biblia inasema sisi tu viungo mbalimbali na kichwa chetu ni Kristo.

Sasa kama vile katika mwili tunajua hakuna kiungo hata kimoja kisichokuwa na shughuli yoyote vivyo hivyo sisi kama viungo hakuna hata mmoja anayesema ameokoka akawa hana shughuli yoyote ya  kufanya katika mwili wa Kristo. Tena sifa nyingine ya viungo ni  kwamba vyote huwa vina vinashirikiana kwa umoja usiokuwa wa kawaida.

Waefeso 4:16 “Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo”.

Umeona huwezi kusema umeokoka, miezi inapita, miaka inapita, hakionekani chochote unachokichangia katika mwili wa Kristo,..Ukiona hivyo basi ujue ulishakufa kutoka katika mwili wa Kristo, na hivyo ulishakatwa na kutupwa nje siku nyingi. Hutambuliki, ukijiona ni wa kuhubiriwa tu daima, lakini wewe hakionekani chochote unachomfanyia Kristo,ni lazima ujitathimini tena mara mbili wokovu wako.

Tabia ya viungo vilivyo hai vya Kristo ni hizi.

1.Kwanza kiungo kinakuwa kinalihudumia kanisa la Kristo kwa mali zake: Ni jukumu la kila mkristo kumtolea Mungu ili kazi ya injili izidi kuenda mbele, na hii sio tu kwamba inawahusu wanaopelekewa injili tu, bali pia kwa Yule anayeipeleka injili, yeye pia anao wajibu wa kumtolea Mungu, sehemu ya alivyo navyo kwa kadiri alivyokirimiwa neema.. Kwasababu jukumu hilo ni la kila kiungo.

2. Pili ni wajibu wa kila kiungo kuliombea kanisa: Maombi ni sehemu ya maisha ya mkristo yoyote, ni lazima aliombe kanisa lote la Mungu kwa ujumla duniani kote, Si rahisi kukutana viungo vyote kwa wakati mmoja, lakini maombi yanawakutanisha katika roho..Hata viungo katika mwili si vyote vinavyokutana, lakini vinajuana, na kusaidiana kwa kuchukuliana udhaifu, vivyo hivyo na sisi, kuliombea kanisa la Kristo ni wajibu wetu kila siku kama wakristo. Macho hayawezi kujiosha yenyewe ni lazima mikono iisaidie, na kadhalika hata mkono mmoja unauhitaji mkono mwingine..

3. Tatu; Kiungo ni lazima kifanye kazi ya kupeleka habari njema kwa wengine: Jukumu ambalo tulipewa wote na Bwana wetu ambaye ni Kichwa, ni kwamba tuenende ulimwenguni mwote, tukawafanye mataifa kuwa wanafunzi (Mathayo 28:19).. Hivyo kila mmoja wetu kwa jinsi alivyopewa karama, anayowajibu wa kuifanya kazi ya kuwahubiria wengine kwa jinsi awezavyo. Ikiwa ni muhubiri, unawajibu wa kuhubiri kwa bidii, ikiwa ni mwinjilisti, mwalimu, mtume, nabii, mwimbaji, mwandishi, n.k. Unafanya vyote kwa bidii, na katika Roho na kweli..Na hiyo inathibitisha kuwa wewe ni kiungo kilicho hai.

Hizo ni ndizo dalili zinazothibitisha uhai wa viungo vya Kristo.  Lakini ni kwanini watu wengi wanaosema ni wakristo wamekosa vigezo hivyo  vitatu kwa pamoja?

Ni kwasababu hawataki kukaa ndani ya Kristo kumtii yeye, ambaye ndiye anayewajalia watu uhai huo. Ndugu usipokitii kichwa, kamwe huwezi kufanya lolote mwilini. Bwana Yesu mwenyewe alisema.

Yohana 15:4 “Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

15 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

6 Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea”.

Umeona,..Ukiwa hutakubali kumaanisha kuyasalimisha maisha yako moja kwa moja kwa Kristo, yaani kukataa maisha ya mguu mmoja ndani mwingine nje, kamwe hutaweza kuwa kiungo hai, hata iweje. Wewe utakuwa ni sawa na tawi lililokatwa linangojea tu kutupwa motoni. Na pia kumbuka huwezi kuwa na karama zote, hata viungo vya mwili vinatufundisha, lakini utakuwa na karama yako ya kipekee ambayo itakuwa ya muhimu katika kanisa la Kristo.

Huu ni wakati wa wewe, kufanyika kiungo hai Kristo..Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi tubu makosa yako, mrudie Kristo, nenda kabatizwe kama ulikuwa hujabatizwa ipasavyo hapo kabla, kwa ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele sawasawa na (Yohana 3:23 na Matendo 2;38). Kisha kuanzia huo wakati anza kuishi maisha yanayouhakisi wokovu.

Na kuanzia huo wakati  wewe mwenyewe utaona tu, Kristo anavyoanza kukutumia kwa ile karama atakayoishusha ndani yako..Na wewe pia utakuwa kiungo chenye kazi yake maalimu ndani ya mwili wa Kristo. Siku ile ya mwisho kikisubiriwa kupewa heshima yake ya kipekee.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Biblia inasema..

Ufunuo 14:14 “Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe, na juu ya wingu hilo ameketi mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji ya dhahabu juu ya kichwa chake, na katika mkono wake mundu mkali.

15 Na malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu yeye aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.

16 Na yeye aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu wake juu ya nchi, nchi ikavunwa”.

Ndugu saa ya mavuno, ipo karibu sana..tena Sanaa.. Utauliza tunajuaje kuwa ipo karibu? Tunajua kutokana na jinsi tunavyoona magugu na ngano yanavyojitenga kwa kasi katika kanisa la Mungu, na katika dunia kwa ujumla. Baadhi ambao walikuwa wanasema huyo Yesu mbona hahukumu dunia, nataka niwaambie wapo kwenye uwezekano mkubwa sana wa kukumbana na hukumu hiyo wakiwa bado hai, kama hawatageuka..

Hawajui kuwa Siri ya Mungu ya kutowahukumu waovu tangu zamani, imejificha ndani ya ule mfano wa magugu na ngano ambao Bwana Yesu aliutoa kwa makutano, embu tusome kidogo..

Mathayo 13:24 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.

27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?

28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?

29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.

30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Na tafsiri yake ilikuwa ni hii..

37 Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu;

38 lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu;

39 yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika.

40 Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.

41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,

42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Hakuyang’oa magugu, kwasababu magugu yakiwa machanga ni ngumu kuyatambua, yanafanana sana na ngano.

Vivyo hivyo Zamani ilikuwa ni ngumu sana kuwatambua watu ambao ni mashoga katika kanisa la Kristo, Lakini leo hii tunawaona tena wana vyama vyao na viongozi wao katika hayo wanayoyaita makanisa yao. Zamani, ilikuwa ngumu kuona mtu anayejiita mkristo halafu ni mzinzi, lakini leo hii utawaona tena kwa mavazi yao ya kikahaba , utaona waasherati wazi wazi katika nyumba ya Mungu, na wengine wanajiita wachungaji na manabii…Wahuni ilikuwa ni ngumu kuwajua ndani ya kanisa, lakini leo utawaona wazi wazi..n.k

Mambo hayo kama ukifuatilia historia utaona Kuanzia karne ya 19 kushuka chini, hayakuwepo kabisa,..Vilevile dunia nzima ilikuwa inaamini walau kuna kitu kinachoitwa Mungu..Lakini leo hii, utaona wimbi kubwa la watu ulimwenguni lisiloamini Mungu kabisa..Hiyo ni ishara kuwa ngano na magugu tayari yameshajitenga, na kukomaa..Ulikuwa huwezi kuona mkristo anajihusisha na miziki ya kidunia, lakini leo hii utawaona kwa staili za uimbaji wao..

Utajiuliza ujasiri wote huo wameutolea wapi?.. Sio ujasiri, bali ni magugu yamekomaa sasa, yanajitofautisha na ngano halisi za Mungu. Haziwezi kuishi Maisha matakatifu kwasababu zenyewe hazikuwa ngano tangu awali, mwanzoni zilijifanya tu kama wakristo ili zipate hifadhi ya mvua ya neema, lakini sasa zimeshakua hazihitaji tena kujificha..

Na hiyo ndio inayokwenda kupelekea wavunaji (malaika) wa Bwana, waje kuuvuna ulimwengu huu wakati sio mwingi.

Wawafunge matita matita, kabla ya kwenda kuwateketeza kwenye lile ziwa la moto. Na hiyo inakuja pale mtu anapohubiriwa njia ya kweli lakini anashupaza shingo yake, wale malaika wanachofanya ni kumtia muhuri, ambayo ndio Kamba yenyewe. Sasa Hilo likishakutokea basi mtu huyo ni ngumu kumgeukia Mungu, ataendelea kuwa hivyo hivyo mkaidi, mpaka mwisho…

anachosubiria ni hukumu tu ya mwisho. (Na hiyo ni kulingana na maandiko na sio kumhukumu Mtu). Wokovu hauna uvuguvugu..

Hichi si kipindi tena cha kuishi Maisha ya kutokujali, si wakati wa kufurahia maovu kanisani, si wakati wa kuiga kila staili ya Maisha inayozuka ulimwenguni, si wakati wa kupokea kila aina ya elimu za uongo zinazohubiriwa na manabii wa uongo, Huu si wakati wa kushikilia dini, Bali Ni wakati wa kuujenga uhusiano wako wewe na Mungu. Kabla ya nyakati za hatari hazijafika..

Kumbuka..Yule malaika alimbiwa..

Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.

Kipindi chenyewe ndio hichi.. Je! Unasubiria uwekwe kwenye kundi la magugu? Kama sivyo basi yasalimishe Maisha yako kwa Kristo na yeye atakuponya. Kimbilia msalabani upate wokovu wa kweli, ambao sasa unapatikana bure, utafika wakati hautapatikana kabisa.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

SWALI: Je ni sahihi kualikwa kwenye karamu za watu wasio wakristo (mfano waislamu kwenye sikukuu zao za eid au futari) na kula nao ni dhambi?


JIBU: Swali hili jibu lake lipo katika kitabu cha 1Wakorintho 8, Mtume Paulo kwa uweza wa Roho alifafanua jambo hili, akasema chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu (Maana yake hakitusogezi mbele za Mungu)..tukila hatuonekani watakatifu mbele za Mungu na wala tusipokula hatujipunguzii kitu kutoka kwa Mungu…(1Wakorintho 8:8).

Tunajua Mungu ni mmoja na ndiye aliyeumba vitu vyote, Naye ni Yehova, sababu hiyo basi hakuna mchele wowote ulioumbwa na shetani, wala muhogo ulioumbwa na mungu fulani mwenye jina fulani aliyeko Asia, wala hakuna pilipili iliyoumbwa na mungu fulani aliyopo mashariki ya kati tofauti na Yehova, n.k. vyote hivyo vinatoka kwake.

Hiyo ikiwa na maana kwamba chakula chochote kilichopikwa kwa mimea au viungo vyovyote vinavyopatikana katika dunia tunayoiishi vimetengenezwa na Mungu mmoja na ni halali kuliwa. Ukipita njiani na kukuta mpera na una njaa usiogope kula! Hakuna chochote kitakachokupata, ukitumiwa zawadi ya chakula fulani na baada ya kumshukuru Mungu kile kwa Imani, utakuwa hujafanya kosa lolote mbele za Mungu.

Ukifika mahali umekaribishwa chakula usianze kuuliza uliza kimetoka wapi, au kimepitia wapi au kimetengenezwa na nini…wewe baada ya kumshukuru Mungu kula!, lakini wenyewe wakikwambia chakula hichi ni wakfu kwaajili ya miungu yetu hapo usile kwasababu ukila utawafanya na wao waamini kwamba miungu yao ipo sawa…na kama kuna mkristo aliyemchanga kiroho karibu yako akikuona umekula chakula hicho atashawishika kuamini kwamba ni sahihi kuabudu hiyo miungu na hivyo utamsababisha aanguke kitu ambacho hakimpendezi Mungu mtu yoyote apotee..Kwahiyo kwaajili ya dhamira za hao watu ili wasitie muhuri ibada hizo, hapo tu ndio biblia imetukataza tusile…

Na kuna tofauti ya “chakula cha sherehe” na “chakula cha sadaka”…Chakula kinachopikwa kwenye sherehe ya mtu asiyeamini sio chakula kinachotolewa sadaka, hata Bwana alialikwa mara nyingi na watu wenye dhambi na wasioamini na alikula …chakula kinachotolewa sadaka ni kwa mfano unakuta labda kuna msiba umetokea, na wahusika wananjinja kuku fulani maalumu wa kimatambiko na damu yake imemwagwa sehemu fulani na nyama ya yule kuku inapaswa iliwe na watu fulani maalumu..sasa nyama ya yule kuku aliyefanyiwa matambiko ndio mfano wa chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, hicho ndio tunapaswa kuwa nacho makini…Lakini pilau iliyopikwa au chakula kingine chochote kilichopikwa kwenye huo msiba kisichohusisha matambiko sio chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu….Na sherehe ni hivyo hivyo.

1Wakorintho 10:25 “Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri; 26 maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo.

27 Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.

28 Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.

29 Nasema, dhamiri, lakini si yako, bali ya yule mwingine. Maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?

30 Ikiwa mimi natumia sehemu yangu kwa shukrani, kwa nini nitukanwe, kwa ajili ya kitu nikishukuriacho?

31 Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.

32 Msiwakoseshe Wayahudi wala Wayunani wala kanisa la Mungu,

33 vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa.”

Kwahiyo ikiwa ni ndugu yako au jirani yako (labda ni muislamu au mhindu ), na amekualika kwake au kwenye sherehe yao na amekuandalia chakula kwajinsi anavyojua yeye…kula bila kuhojihoji hufanyi dhambi kwa Mungu….isipokuwa tu amekupa chakula kilichotolewa sadaka na amekueleza

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

 

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

Kwanini Bwana aliongea na Abramu baada ya kutengeana na Lutu?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

RABI, UNAKAA WAPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

Habari ya uumbaji ina mafunzo mengi sana. Biblia inatuambia Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke kwa mfano wake(Mwanzo 1:27). Lakini katika siku sita za uumbaji, Tunaona kulikuwa na uumbaji mmoja muhimu ulikosekana., Embu tengeneza picha mpaka Mungu anastarehe siku ya saba, mwanamke hakuwepo,..Ni kama vile Mungu alijifanya amemsahau hivi..Lakini kulikuwa na sababu kubwa mno ya yeye kufanya hivyo.

Alimwacha Adamu awepo peke yake duniani kwa kipindi fulani kirefu, aone uumbaji wake wote, aushangae huo, aseme ama kweli Mungu ameumba..kila kitu kweli ni kizuri, tazama jua, tazama, nyota, tazama twiga, tazama nyangumi, tazama hiki tazama kile, vyote ni vikamilifu, vimejitosheleza kweli kweli, sihitaji kingine…

Lakini hakujua kuwa Mungu alikuwa hajaukamilisha uumbaji wake bado (hiyo siri alikuwa nayo mwenyewe), ameihifadhi mpaka wakati mtimilifu utakapofika.

Sasa baada ya Mungu kumuacha Adamu kwa kipindi chote hicho kirefu, pengine miezi, miaka inapita aendelee kufikiria hivyo hivyo kuwa kila kitu ndio tayari, mpango wote umekamilika, Mungu kamaliza uumbaji wake, , shughuli zinaendelea kama kawaida bustanini.. Lakini wakati ulipofika wa Mungu kuikamilisha kazi yake alishuka bustanini tena kama muumbaji yule yule wa zamani..

Tungeweza kudhani labda angeshuka ardhini amtoe mwanadamu mwingine kwenye udongo mwekundu, lakini mambo yalikuwa ni tofuati, alimkabili Adamu moja kwa moja..Na mara moja Akamletea usingizi mzito sana. Wakati Adamu akiwa ndotoni, mkono wa Mungu ulianza kupita sehemu ya ubavu wake, pengine mfano wa kisu kikali(hatujui), tunachojua ni kuwa aliundoa ubavu wake mmoja, jaribu kutengeneza picha operasheni iliyokuwa inafanyika pale ni ya namna gani..Si ajabu hata Mungu alimletea usingizi mzito..

Hatushangai hata madaktari wa leo wameiga mbinu hiyo ya Mungu ya kufanya operasheni, yaani kumpiga kwanza mtu nusu-kaputi ili apotelee usingizini kabla ya kumfanyia matibabu makubwa..Wanafanya hivyo Si kwamba hawapendi mtu aone operasheni ile hapana, kwanza ni ili kuepuka usumbufu, chukulia mfano ikiwa mtu yule ataona tumbo linakatwa na utumbo unatolewa nje au anaona kichwa chake kinapasuliwa, anaweza asikubali, au akaogopa kupitiliza na mwisho wa siku akasababisha operesheni isiende vizuri au hata kifo kabisa..Na ndivyo ilivyokuwa kwa Mungu..Alikuwa anamfanyia Adamu operasheni yenye umakini sana, ya kuumba kitu bora kuliko vyote alivyovifanya ndani ya siku zile 6.. Hivyo ikamgharimu atafute njia itakayomfanya awe na utulivu, na ndio akatumia njia ya usingizi mzito, kwasababu kinachokwenda kuumbwa ni bora sana.

Sasa Mungu alipomaliza kuutoa ubavu wake mmoja, akarudishia nyama eneo lile, ndipo akauchukua ule ubavu akamuumbia Hawa. Na kazi ilipomalizika, bwana Adamu akazinduka usingizini, kujitazama anajiona kama vile mwili umepungua, na kuangalia pembeni anamwona mgeni, ambaye si wa pale bustanini. Na kumtazama vizuri anaona hafanani na swala, hafanani ni mbuzi bali anafanana na yeye, anazungumza kama yeye, anaumbile linalokaribia kufanana na la kwake.. Hapo ndipo alipogundua kuwa ni ile sehemu ya mwili wake ameumbwa yule mtu.

Na Adamu alipomwangalia tena hakuona wa kulinganishwa naye katikati ya uumbaji wote ambao Mungu alishawahi kufanya.

Sasa Ni jambo gani Mungu alikuwa anamwonyesha Adamu?

Alikuwa anamwonyesha kuwa uumbaji wake bora unatoka ndani ya mtu, na si penginepo.. Hakuna mwanaume asiyejua katika uumbaji wote wa Mungu hakuna hata kimoja kinachoweza kufananishwa na mwanamke.

Vivyo hivyo somo hilo Mungu hakumfundisha Adamu tu peke yake,..Bali na Hawa pia, pale alipomwekea uwezo wa kubeba mimba, ambapo aliruhusu kiumbe kikae ndani ya tumbo lake kwa miezi 9, lakini baada ya ya hapo, ghafla anatokea tena mwanamume..

Na vivyo hivyo hakuna mwanamke asiyejua kuwa katika uumbaji wote wa Mungu, hakuna kilichoumbwa bora kama mwanamume…Lakini mwanamume huyo anatoka katika tumbo lake na sio mbinguni au ardhini tena. Na kwa kupitia mzunguko huo huo duni leo imejaa watu.

Mambo hayo hayo yanaendelea rohoni hata sasa, Uumbaji mkamilifu wa Mungu unatimia ndani ya Maisha ya wanadamu..ikiwa tu tutamruhusu aifanye kazi yake mwenyewe ndani yetu bila kusumbuliwa..Mungu anataka kufanya makubwa kupitia sisi, kuliko angefanya yeye mwenyewe. Lakini ni sisi hatuwi watulivu kufanyiwa operasheni.

Tunashindana na Mungu, kwa mambo mengi maovu,anapotuambia tuache Maisha ya dhambi, hatuwi tayari kufanya hivyo, tunapoambiwa tusivae nguo zisizompa Mungu utukufu hatuwi tayari, tunapoambiwa tuombe, hatutaki, tunapoambiwa tuikimbie zinaa sisi tunairidhia, biblia inapotuonya tuache hiki au kile hatutaki kutii, tunachosema ni Mungu haangalii mwili anaangalia mavazi, tunapoambiwa tujitenge na mambo ya ulimwengu, tunamwona kama anatunyima uhuru wetu, kila siku tunashindana na mkono wake.. na wakati huo huo tunataka Mungu aumbe mambo makubwa maishani mwetu..Ataumbaje katika hali hiyo ya masumbufu?

Mungu anahitaji utulivu wa roho, tukiukosa huo tusitazamie uumbaji wowote. Tusitazamie Mungu kufanya miujiza maishani mwetu. Ikiwa wewe ni mwenye dhambi, huu ni wakati wako sasa wa kumrudia Mungu, Anza kujenga uhusiano wako vizuri na Mungu, ndipo Mungu naye achukue nafasi ya kuumba mambo mazuri ndani yako.

Tubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, na pia nenda kabatizwe kulingana na matendo 2:38, na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu atakayekuongoza na kukutia katika kweli yote na kukupa utulivu wa roho.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

 

MJUMBE WA AGANO.

Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

KUWA WEWE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

Jibu la swali hili linahitaji umakini mkubwa kwasababu lisipoeleweka vizuri ni rahisi kusema biblia ina ubaguzi wa kijinsia au biblia haimaanishi hivyo inavyomaanisha.

Hebu tusome mistari michache ifuatayo..

1Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.

4 Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake.

5 Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa.

6 Maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe.

7 Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.

8 Maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke katika mwanamume.

9 Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.

10 Kwa hiyo imempasa mwanamke awe na DALILI YA KUMILIKIWA KICHWANI, kwa ajili ya malaika”.

Katika mistari hii Mtume Paulo aliandika kwa uongozo wa Roho Mtakatifu ili kufikisha ujumbe kwa kanisa lote la Mungu kwa wote watakaosoma waraka huo, na waraka huo haukuwahusu wakorintho tu kama wengi wanavyotafsiri..bali ililihusu kanisa la Kristo kwa ujumla, ikiwemo na sisi watu wa nyakati hizi za mwisho.

Sasa kama ukisoma mistari hiyo utaona, Imejikita sana katika Eneo la KICHWA…Na imezungumzia vichwa vitatu…1) kichwa cha Kristo, 2) Kichwa cha Mwanamume 3) Kichwa cha mwanamke…

Tukianza na kichwa cha Kwanza, ambacho ni cha Kristo, biblia imekitaja kuwa ni Mungu mwenyewe…maana yake aliyekuwa na mamlaka juu ya Kristo ni Mungu peke yake, ambaye ndiye Baba yake..

Na pili kichwa cha Mwanamume ni Kristo..maana yake ni kwamba..Kristo ndiye mwenye mamlaka juu ya kila mwanamume…

Na tatu kichwa cha kila mwanamke ni mwanamume…Maana yake ni kwamba mwenye mamlaka juu ya mwanamke ni mwanamume…Na mamlaka hayo mwanamume alipewa na Mungu pale Edeni (Mwanzo 3:16)

Sasa kwasababu mwanamume ndiye kichwa cha Mwanamke…basi mwanamke ni lazima aonyeshe dalili au ishara ya kumilikiwa katika kichwa chake…na ishara hiyo sio nyingine zaidi ya kufunika kichwa…Ni kama vile ulivyo utaratibu wa mwanamke kuvishwa shela linalofunika mpaka kichwa wakati wa harusi au anapovishwa pete, ni kuonyesha ishara ya kumilikiwa na mwingine…Ndivyo hivyo hivyo kila mwanamke anapaswa afunike kichwa anapokuwa kanisani kuonyesha ishara ya unyenyekevu, na ya kumilikiwa na wanaume ambao ndio vichwa vyao.

Sasa wengi wakisikia hili neno kutawaliwa/kumilikiwa wanachukia na linawakwaza!..wanadhani wameambiwa waabudu wanaume, (kumbuka anayestahili kuabudiwa ni Bwana wetu mmoja tu Yesu Kristo)!..Lakini katikati yetu wanadamu Mungu katuweka chini ya milki ya watu wengine, ili kufikisha ujumbe Fulani wa rohoni. Kwamfano Mtoto yoyote yule awe wa kiume au wakike anapokuwa mdogo anakuwa yupo chini ya milki ya wazazi wake, kwa faida yake huyo mtoto…Sasa mtoto akichukia kumilikiwa na wazazi wake atakuwa ni mgonjwa, kwasababu Mungu akitaka kumlisha au kumbariki ni lazima atumie wazazi wake/walezi wake kumbariki huyo mtoto. Na ndio hivyo hivyo, katika roho wanawake wote ni milki ya wanaume, ndivyo Mungu alivyopenda iwe hivyo, hakuna awezaye kubadilisha, na hiyo pia ni kwa faida ya wanawake..

Mwanamke yoyote anayekataa kutawaliwa au kumilikiwa na mwanamume akidhani atakuwa anamwabudu, anajimaliza mwenyewe!…ukitaka mambo yako yaende sawa kubali kumilikiwa, lakini ukitaka laana kataa kumilikiwa!…Vivyo hivyo unapokuwa kanisani mwanamke ukitaka ufaidike na ibada yako FUNIKA KICHWA CHAKO!, kama ishara ya kumilikiwa!…na tena biblia hapo kwenye mstari wa 10 inasema wazi kabisa kwamba “kwaajili ya malaika funika kichwa chako”….Maana yake ni kwamba malaika wa Bwana wanaopita kanisani kwaajili ya kuwahudumia watakatifu kulingana na Waebrania 1:14, wanapopita na kukuta kichwa chako kipo wazi, na tena umeweka wigi, au rasta hawawezi kukuhudumia…

Na ndio kazi ya shetani kuyafanya yale mambo madogo yaonekane sio maana sana, ili watu wasipate Baraka kutoka kwa Mungu..

Funika kichwa mwanamke wa kikristo uwapo ibadani, hilo ni Neno la Mungu na lipo katika agano jipya na si la kale, Usilidharau Neno la Mungu kwa kiburi cha kupandikiziwa na shetani, usikubali shetani akichezee kichwa chako..kumbuka ndio utukufu wako upo hapo, biblia inasema hivyo.

Kama maneno haya unafikiri ni ya uongo, hebu fanya utafiti siku moja, kisafishe kichwa chako, vaa vizuri, funika kichwa chako kwa kitambaa/kilemba, halafu nenda kanisani..utaona utofauti wa siku hiyo na siku nyingine, ndipo utakapojua kuwa Neno la Mungu sio uwongo…Utaona hata maneno yanayotoka katika kichwa chako yanakuwa na nguvu na uweza, hata uombaji wako utakuwa tofauti,,utatembea na jeshi la malaika wa mbinguni. Vilevile jambo hilo linaambatana na kujisitiri, ukiwa ni mwanamke wa kuvaa ovyo ovyo tu kila mahali, kamwe hutakaa uuone utukufu wa Mungu haijalishi utasema wewe umeokoka kiasi gani.

Hilo ni Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

NI NANI ALIYEWALOGA?

USIMZIMISHE ROHO.

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post