JIBU: Tukiweza kulijibu na swali hili “Ikiwa sisi tunakula ili tuishi, Je! Mungu naye anakula nini ili aishi?”…Basi tutaweza pia kulijibu hilo linaloulizwa kirahisi.
Awali ya yote ni vizuri kufahamu kuwa wazo lolote ambalo linakuja katika vichwa vyetu fahamu kuwa lilishawahi kuumbwa hapo kabla, Hivyo wakati ulipofika na kuwekwa katika kichwa chako au changu, ndipo tukaliwaza, vinginevyo tusingekaa tuwe na wazo kama hilo vichwani mwetu kama hili la “Mungu aliumbwa na nani” kama halikuwahi kubuniwa na aliyetuumba.. hakuna wazo linalozuka lenyewe tu hewani, labda wewe ndio uwe wa kwanza kuligundua, ni kama kumputa tulizonazo kila kitu kilichomo ndani yake, kiliwekwa na mtu kwanza (installed)
Hivyo mpaka hapo ulipofikia kuwaza tu Mungu aliumbwa na nani, fahamu kuwa ni yeye mwenyewe alilibuni hilo wazo kisha akaliweka kwa makusudi katika ufahamu wako,..Hivyo usifikiri kuwa umegundua wazo la kumnasa Mungu, kama hilo la Mungu aliumbwa na nani,..nataka kwanza uondoe hilo akilini. Na aliamua kufanya hivyo ili wakati wake wa kufikirika ukifika ujiulize weee!!, uumize kichwa weee! kisha ukose majibu! … Wazo hilo alipenda tu ukose majibu yake, kama vile yale mengine alivyopenda upate majibu yake.
Jibu rahisi ni kuwa Mungu hatuwezi kumpima katika “wazo la kuumba au kuumbwa”..kwasababu hayo mawazo ya kuumba au kuumba aliyabuni yeye, hivyo hayawezi kuwa sehemu ya maisha yake..yeye, ni zaidi ya upeo wa fikra zetu.
Jaribu kuwazia mfano huu, unaohusiana na vitu tulivyoviumba sisi wanadamu ambavyo ni vya elektroniki…Sasa kisa tu tumeviundia mfumo wa kutegemea umeme katika kujiendesha pale vinapoishiwa nguvu tunavichaji betri zako katika umeme.. Na kwamba visipochajiwa ni lazima tu vizime au vife kabisa, Simu zetu zinasema hivyo hivyo, saa zetu hivyo hivyo , komputa zetu, na tochi zetu zinasema hivyo hivyo n.k..Halafu siku moja sasa eti na vyenyewe vinaungana na kutuuliza sisi tulioviumba maswali, vinasema Je! betri zenu ziko wapi, na mnachajiwa wapi? kwasababu hakuna maisha nje ya umeme?
Unaona lakini sisi je tunaishi kwa betri au umeme?…jibu ni la, maisha yetu yanaendeshwa na kitu kingine tofauti na wanachokifikiria, bali mambo hayo ya umeme tumeviumbia vifaa vyetu vya elektroniki ili viishi kwayo..zaidi ya hapo haviwezi kujua jambo lingine linalotuhusu sisi..
Vivyo hivyo na sisi kwa kuwa tumezungukwa na mazingira ya “kuumba na kuumbwa”,kila kitu tunaona ni lazima kiwe na chanzo chake ….Basi na sisi tunahitimisha na kusema Je Mungu naye kaumbwa na nani?..
Jibu linalojitosheleza ndio hilo..Mungu hayupo katika viwango vya kibinadamu ni zaidi ya upeo wa fahamu zetu..hatuwezi kumpima katika mambo ya uumbaji.. ni sawa na leo uulize mwanga una ladha gani, au rangi ina harufu gani..na ndio maana tunapotoa jibu la mkato kuwa Mungu hajaumbwa basi ujue ni kwasababu hizo tunazozisema hapo juu….Mungu ni Zaidi ya upeo wa fikra na kwamba hatuwezi kumweka katika hilo kundi la uumbaji.
Ubarikiwe.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?
Je! Mungu anasababisha ajali, kwamfano ajali ya kivuko cha MV Nyerere kuzama?
Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?
Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?
Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?
KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?
SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.
Ipo mifano mingi katika biblia ya watu ambao, walijaribu kumgeuza Mungu kama mganga wa kienyeji na mwisho wao ukawa mbaya sana. Siku zote watu wanaokwenda kwa waganga utagundua wengi wao hawafahamiani hata na hao waganga wanaowaendea, wala hawana uhusiano nao wowote.
Wakifika pale wanaeleza tu matatizo yao, kisha mganga anawatamizia haja zao, kisha wanakwenda zao..Sasa jambo kama hilo usijaribu kulifanya kwa Mungu ni hatari mno.
Wana wa Israeli kuna wakati Fulani walikuwa wanajaribu kufanya hivyo hivyo, unakuta mtu kamwacha Mungu zamani, ndani yake kuna vinyago, hashiki torati ya Mugu, lakini pale anapokumbwa tu na matatizo fulani labda anaumwa, au anataka kufanya jambo Fulani ndipo anataka kwenda kumuuliza Mungu kwa kupitia nabii wake..Sasa karibu wote waliokuwa wanafanya hivyo Mungu alikuwa anawaua bila huruma.
Kama huyo nabii ni nabii wa kweli wa Mungu aliyesimama. Mungu atamwambia moja kwa moja kuwa atakufa. Ndicho pia kilichomkuta Yeroboamu na mkewe walipokwenda kuuliza habari za uzima wa mtoto wao kwa nabii Ahiya, walitabiriwa mabaya na vifo soma (1Wafalme14).
Lakini kama nabii huyo ni nabii wa uongo au vuguvugu..Mungu anachofanya ni anamdanganya Yule nabii aliyemwendea, Na Mungu anajua kabisa kwasababu unamwamini nabii Yule kwamba chochote atakachokuambia utafanya, kumbe huo ndio unakuwa mtego wa kwenda kukuangamiza wewe, Mfano huo tunaouna kwa mfalme Ahabu, pale alipotaka kwenda kupigana vita na mfalme wa Shamu, na biblia inasema Mungu akawadanganya wale manabii 400 wote wakamtabiria ushindi kumbe ndio ulikuwa unakwenda kuwa mwisho wake.. Mungu atakuahikishia hata kwa nabii zaidi ya mmoja unachokifanya ni sahihi, kumbe ni uongo ujue kabisa amekusudia kukuua soma (1Wafalme 22:1-39)..Ndicho kilichomkuta Balaamu, ilikuwa ni nusu afe, punda ndiye aliyemuokoa japokuwa ni Mungu ndiye aliyemwambia aende (Hesabu 22:1-34)..Wote hawa ni mfano wa watu waliojaribu kumgeuza Mungu mganga wa kienyeji kwamba wao wapewe tu haja za mioyo yao, mengine zaidi ya hayo hawataki..
Angalia jambo aliloambiwa Ezekieli na Mungu..
Ezekieli 14:1 Ndipo baadhi ya wazee wa Israeli wakanijia, wakaketi mbele yangu.
2 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
3 Mwanadamu, watu hawa wametwaa vinyago vyao na kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni laiki yangu niulizwe na wao katika neno lo lote?
4 Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake;
5 ili niwakamate nyumba ya Israeli kwa mioyo yao wenyewe, kwa sababu wamefarakana nami kwa vinyago vyao……
7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe;
8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
9 Na nabii akidanganyika, na kusema neno, mimi, Bwana, nimemdanganya nabii yule, nami nitaunyosha mkono wangu juu yake, na kumwangamiza, asiwe kati ya watu wangu Israeli.
10 Nao watauchukua uovu wao; uovu wa nabii utakuwa sawasawa na uovu wake yule amwendeaye aulize neno;
Unaona hapo mstari wa 9? Anasema mimi Bwana nimemdanganya nabii Yule.. Kama ulikuwa unahitaji kupona, pengine nabii Yule atakupa maagizo Fulani ambayo ni kweli ameyapokea kutoka kwa Mungu, labda tuseme atakuambia Mungu kaniambia, funga siku tatu, kisha kula chakula kisichokuwa na chumvi tu, baada ya hapo utakuwa mzima..Kumbe jambo hilo ndio linakwenda kukuangamiza kabisa.. Na Mungu anafanya hivyo kwasababu umemdharau yeye kwa kumgeuza kuwa kama mganga wa kienyeji, angali ulikuwa unajua kabisa ndani ya moyo wako kuna dhambi umekataa toba, na utakatifu halafu unamwendea yeye akupe haja ya moyo wako wa dhambi..
Hata leo hii, Mungu anawaangamiza watu wengi kwa namna hiyo pasipo wao kujijua.. Wakati Mungu anawapigia kelele kila siku watubu, waache dhambi, watoe vinyago ndani ya mioyo yao, hawataki kusikia wala kuzingatia maagizo hayo, wanadhani Mungu anafurahishwa nao, wanadhani Mungu ni wa neema siku zote badala yake wakiwa bado ni walevi, wala rushwa, wazinzi, waabudu sanamu, washirikina, watazamaji pornography, wasagaji wanamwendea Mungu, kwa kupitia mtu anayejiita nabii, au mtume, au mchungaji, amwombee au amtatulie matatizo yake pengine ya kiafya, au ya kiuchumi, au ya kifamilia…Wahudumiwe tu kisha waondoke wakaendelee na maisha yao ya kawaida ya kila siku..
Ndugu kama ni wewe mmojawapo usijaribu kufanya hivyo tena,..Kwasababu UTAKUFA.. nenda kawatafuta waganga wa kienyeji itakuwa ni salama kwako, lakini sio Mungu kama unamwendea Mungu halafu hutaki kuacha dhambi.. Nakuambia ukweli UTAKUFA NDUGU…
Utaishia kudanganywa tu,..tena na Mungu mwenyewe, unakimbilia mafuta ya upako, unausahau mafuta ya roho yako (Roho Mtakatifu) ambayo yanaokoa roho yako, unakimbilia maji, unasahau maji ya uzima ambayo yanaokoa roho yako.. Timiza kwanza agizo la msingi ambalo ni wokovu na utakatifu..Ndipo Mungu akupe neema ya kutatuliwa na hayo mengine.
Vinginevyo utakufa, hata kama sio kwa njia hiyo, itakuwa kwa nyingine.
Au wewe ni mlevi, mzinzi, mwendaji disko, mlaji rushwa, halafu unakwenda kanisa kila siku, kunakufaidia nini sasa? na kibaya zaidi unashiriki na meza ya Bwana kabisa..Huko ni kujitafutia kifo ndugu. Break! ya kwanza kwa Mungu ni utakatifu (Waebrania 14:12),Mungu hapambwi kwa sadaka, au kwenda kwako kanisani, anachohitaji kwako ni Utakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Nje ya hapo wewe ni adui wa Mungu.
Hiyo ni tahadhari kwako, wewe..Umekwisha sikia, Mungu hadhihakiwa, apandacho Mtu ndicho atakachokuna maandiko yanasema hivyo.
Maran Atha.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MPINGA-KRISTO
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
TAZAMA KRISTO YUPO HAPA,AU YUKO KULE MSISADIKI.
JUMA LA 70 LA DANIELI
DANIELI: Mlango wa 1
Katika Biblia kuna mahali panasema… “Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo (Wagalatia 6:2)”.
Lakini Biblia hiyo hiyo mbele kidogo katika mstari wa 6 inasema “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe (Wagalatia 6: 5)”.
Ni rahisi kuona kama biblia inajichanganya lakini sio kweli, biblia sikuzote ipo sawa,.Isipokuwa tu Mungu anahitaji tupate msaada wake katika kuyatafakari maandiko yake.
Biblia iliposema kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe…Ilikuwa inalenga juu ya matendo ya mtu..Kwamba kila mtu matendo yake yatamfuata mpaka siku ile ya hukumu..Na hayo anakuwa ni kama ameyabeba…atayabeba yeye peke yake na atasimama nayo mbele ya kiti cha Hukumu siku ile akiwa peke yake. Hivyo matendo ya mtu yanafananishwa na FURUSHI!.
Kadhalika Biblia iliposema tuchukuliane mizigo ilimaanisha tusaidiane sisi kwa sisi..Maana yake tukiwa na nguvu tunapaswa tuwasaidie wale wasio na nguvu..Ili tuwe wenye haki mbele za Mungu..na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeitimiza sheria ya Kristo ambayo ni UPENDO.(Yohana 13:34, 1Yohana 3:17-18).
Katika siku hizi za mwisho Biblia imetabiri kwamba upendo wa wengi utapoa!…Upendo wa watu kumpenda Mungu utapoa, kadhalika na upendo wa watu kupendana wao kwa wao utapoa. Na hivyo kuifanya dunia kuikosa hii sheria ya Kristo ambayo ni UPENDO.
Na biblia imetuasa kuwa kuna upendo wa Ulimi na upendo wa tendo.
1Yohana 3: 17 “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?
18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli”
Kwahiyo kama tumeokoka ni lazima tuitimize hiyo sheria ya Kristo. Tupendane kama matendo kama yeye alivyotupenda sisi. Sio tu kumuombea au kumuhurumia bali pia kutenda.
Na pendo hilo pia ni pamoja na KUCHUKULIANA MIZIGO.
Unaposikia mpendwa mwenzako ana tatizo hili au lile na unajua kabisa yupo katika shida ambayo hawezi kuzungumza..Usisubiri yeye akuambie wewe chukua hatua ya kwenda kumsaidia tatizo lake. Ukiona ndugu yako ni mgonjwa pamoja na kumwombea chukua hatua ya kwenda kumtazama, kumfariji na hata kumhudumia. Usiangalia wewe ulipokuwa na matatizo alikuja kukutafuta au la!..kuwa kama kipofu kwa mabaya uliyofanyiwa na uwe mkumbukaji wa mazuri aliyowahi kukufanyia…
Wengi wetu hatujui kuwa Neema ya Mungu juu ya Maisha yetu inaongezeka juu yetu siku baada ya siku, na pia inaweza ikapungua juu yetu endapo tukiipuuzia…Unapomsaidia mtu hususani mkristo mwenzako..na ukamsaidia kwa moyo kabisa…
Kuna Neema fulani inakuwa inaongezeka juu yako kiasi kwamba utakavyokuja tena kumsaidia mwingine hutasikia uzito kama ulivyosikia kwa yule wa kwanza…na hivyo hivyo watatu utakuwa mwepesi Zaidi…na kwajinsi unavyoendelea hivyo hivyo ile Neema ya utakatifu inaongezeka juu yako mpaka unafikia hatua kusaidia mtu kwako si jambo kubwa wala kukuwazisha kichwa, linakuwa linatoka lenyewe kama vile pumzi…Na Neema hiyo ya utakatifu inavyoongezeka juu yako inaambatana na Milango mikubwa sana ya Baraka…Kwasababu unakuwa umeshaaminiwa na Mungu sana…
Kwasababu Bwana anajua hata akishusha kwako kiasi fulani cha mali, asilimia 90 ya ile itakwenda kuwasaidia watu wake walioko katika shida..walioko katika uhitaji, anajua kiasi kikubwa cha ile fedha au mali itaenda katika kuiendeleza kazi ya yake…hivyo yule mtu anakuwa kama Bomba la Mungu la kupitishia baraka kwa watu wake…Hivyo na lenyewe haliwezi likakauka maji. Lakini mtu anayejizuia kuchukua mizigo ya wengine mtu huyo anakuwa kama ni bomba lililofungwa…Bomba lililofungwa haliwezi kupokea maji kutoka kwenye chanzo kadhalika haliwezi kujaza ndoo za maji zilizopo chini yake kwenye foleni..lakini lililofunguliwa kwa jinsi linavyotoa ndivyo linavyopokea.
Tenga muda nenda kajaribu kuwatafuta watu waliojizoeza kusaidia watu sana kiasi kwamba hata kutoa chochote kwao si shida..tenga muda wahoji waulize kama walishawahi kupungukiwa..watakupa shuhuda za ajabu sana…
Hivyo hatuna budi leo kujikumbusha jambo hili..ili tuzidi kuielewa Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo inavyofanya kazi.
Warumi 15:1 “Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wao wasio na nguvu, wala haitupasi kujipendeza wenyewe.
2 Kila mtu miongoni mwetu na ampendeze jirani yake, apate wema, akajengwe.
3 Kwa maana Kristo naye hakujipendeza mwenyewe; bali kama ilivyoandikwa, Malaumu yao waliokulaumu wewe yalinipata mimi”.
Kuwahubiria pia wengine habari za Mungu ni kuwachukulia mizigo yao…Bwana akikupa kitu na kile kitu hutaki kuwashirikisha wengine ukidhani kwamba watajua Zaidi kuliko wewe, au hawatakutaja wewe uliyewashirikisha hapo unajifungia mwenyewe bomba lako la neema. Mungu hawezi kukupa jambo jipya kama lile la zamani hujalitoa..Toa lile la zamani katika hazina yako washirikishe wengine bure! Ili Uweze kupokea lingine lakini ukiwa na moyo wa uchoyo na wivu na hutaki kutoa hazina Mungu aliyoiweka ndani yako kwa muda mrefu, ukisema ufunuo huu ni wangu tu…kamwe usitegemee kubarikiwa kwa vyovyote vile..
Bwana Yesu alisema katika Mathayo 13:52 “Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale”.
Hivyo jizoeze kuwashirikisha wengine habari za Uzima..Umepata kitu fulani ambacho kimekusaidia wewe na umeona kuna wengine kama wewe wengi kinaweza kuwasaidia…huo ndio wakati wa KUWACHUKULIA MIZIGO YAO!..Na watakutaja mbele za Mungu katika maombi yao kwamba uliwasaidia na Mungu atakukumbuka na wewe na kukubariki.
Unaona mpendwa mwenzako anafanya kitu fulani cha kujiendeleza na anahangaika mno na wewe una ujuzi wa kutosha wa namna ya kumsaidia, usingoje akutafute, wala usimwonee wivu..wewe huo ndio wakati wa kumchukulia MZIGO!..Kama umekutana na nafasi za kazi na unaona pengine zitamfaa mtakatifu mwenzako Msaidie hata kama hapo alipo tayari kaendelea kuliko wewe. Wewe timiza wajibu wako kwasababu yupo Mungu juu anayetazama..Na mambo mengine yote ya kimaisha na ya ki-roho…SHERIA YA KRISTO NI ILE ILE UPENDO!! Na KUCHULULIANA MIZIGO.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?
USIMPE NGUVU SHETANI.
INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.
IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.
KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.
TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
Uvumilivu wa mungu ulipokuwa ukingoja, siku za nuhu
Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe. Nakukaribisha tulitafakari Neno la Mungu, ambalo ndio pekee lenye uwezo wa kuokoa roho za watu.
Ndugu yangu nataka ufahamu kuwa kuzimu inafananishwa na GEREZA kubwa sana lenye Malango na makomeo yake..Soma (Isaya 38:10 na Ayubu 17:6) utalithibitisha hilo..Haisemi mlango au komeo tu kana kwamba ni mmoja mmoja, hapana Bali ma-lango, ma-komeo, Hii ikiwa na maana kuna kifungo, na magereza mengi tofauti tofauti kulingana na aina ya dhambi za watu. Kama ukifa leo katika dhambi basi lipo lango lako uliloandaliwa na watu wa aina yako katika gereza lenu. Na huko sio kukaa tu, hapana kuna shida na mateso ya hali ya juu sana..Wote wanakaa huko wakisubiria siku ile ya hukumu wahukumiwe kisha ndio watupwe katika lile ziwa la moto.
Na gereza la juu kabisa ni lile la shetani na malaika zake, ambalo kwasasa wapo baadhi yao huko wamefungwa wakingojea kutupwa kwenye lile ziwa la moto siku ile ya mwisho itakapofika, japo wapo wengine baadhi yao duniani wakizunguka, ndio hawa wanaoiharibu dunia..
2Petro 2:4 “Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu”;
Lakini leo nataka tujifunze jambo moja, ambalo pengine huwa tunalipitia kila siku lakini hatulielewi.. Na jambo lenyewe ni lile la Bwana Yesu kushuka kuzimu, na kuwaendea roho waliokaa kifungoni..Embu tusome..
1Petro 3:18 “Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,
19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;
20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji”.
Utaona hapo, tukio lililofuata baada ya Kristo kufa msalabani lilikuwa ni kushuka kuzimu, na kwenda kuzitembelea hizi roho zilizokuwa vifungoni, lakini biblia haiwataji wafungwa wote, bali inatuonyesha watu Fulani tu, katika gereza Fulani mahususi, ambalo Bwana Yesu alikwenda kuwahubiria… Na hao si wengine Zaidi ya watu wa kipindi cha Nuhu..Sio kwamba hakuenda kwa wengine lakini kulikuwa na sababu kwa nini walilengwa watu wale…kwasababu na sisi ndio tunaofananishwa na kundi hilo..
Sasa huko kuhubiri kunakozungumizwa sio kwenda kuhubiriwa labda watubu au wageuke, hapana, kuhubiri kupo kwa aina nyingi, kutangaziwa hukumu nayo ni moja ya mahubiri, alikwenda kuwatangazia hukumu yao, ni kwanini wao wanastahili adhabu kubwa kuliko wote..
Na dhambi yao ilikuwa si nyingine Zaidi ya kupuuzia “Uvumilivu wa Mungu” uliokuwa ukilia juu yao siku baada ya siku..
Walipokuwa wanajua kabisa ni kweli dunia inakwenda kuangamizwa lakini wanafanya makusudi kushupaza shingo zao, wakiiona Safina ikijengwa, kwa muda wa miaka yote hiyo, walipokuwa wakihubiriwa na Nuhu kwa muda mrefu sana wa miaka 120 watubu waache dhambi zao lakini wanakataa..Wakimsikia Nuhu akiwaambia Mungu anawapenda, hataki hata mmoja aangamie, lakini wao wanaenda kinyume chake, wanaishi Maisha ya uovu, wanazini makusudi, walewa makusudi, wanafanya uchawi na ushirikina..wanasema huyo Mungu anayesema ataangamiza dunia mbona hatumwoni akiangamiza, kashakufa, wewe Nuhu acha ukichaa, wewe ni mvivu, hutaki kujishughulisha wewe unawaza tu mbinguni, na Maisha mwilini utaishije sasa, umaskini wa akili na ulimbukeni wa kifikra?..
Lakini siku ilipofika uvumilivu wa Mungu uliposema Basiii…Hakusalia hata mmoja..na wote moja kwa moja wakapelekwa katika gereza lao moja mahususi, lililokuwa limetengwa kwa ajili ya watu wa namna hiyo wanaostahili hukumu ya juu Zaidi..Na ndipo huko Kristo alipowafuata kuzimu..
Biblia inatuambia kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu ndivyo itakavyokuwa siku za kuja kwake mwana wa Adamu, Siku za Nuhu watu walipuuzia wokovu, japokuwa walielezwa kuwa dunia inakwenda kuteketezwa lakini walitukana..Ndivyo ilivyo leo hii, dalili zote za kuja kwa Kristo zimeshatimia katika karne hii ya 20 na 21,..Na mojawapo ya dalili ya juu kabisa ni kutokea na kuongezeka kwa kasi kwa manabii wa Uongo na makristo wa uongo..mambo ambayo ukimuuliza hata mtu aliyekufa mwaka 90’, atakwambia jambo hilo hatujawahi kuliona wala kulisikia kama limeshawahi kutokea katika historia..Lakini sisi leo hii tunalishuhudia kwa macho yetu, lakini badala watu watubu wamgeukie Mungu, ndio kwanza wanatoa maneno ya kudhihaki…huyo Yesu mpaka leo miaka 2000 imepita hajaja amekufa..,mizaha, jina la Kristo linatajwa kiholela holela mpaka kwenye comedy …. wanaudharau uvumilivu wa Mungu…
Moja ya siku hizi, hii dunia itafika mwisho.. Na kibaya Zaidi tumeambiwa mwisho huo utakuja kwa ghafla sana. Hakuna mtu atayetazamia kama kweli huo ndio wakati wenyewe..kwasababu biblia inatuambia utakuja wakati wa amani..sio wakati wa vita..leo hii tunaishi katika hicho kipindi.. Na kama ikitokea umekufa katika hali ya dhambi, ukijua kuwa kila siku umekuwa ukikutana na mahubiri na injili zinazokuhubiria ugeuke lakini hutaki..basi ujue gereza lako litakuwa ni lile la hali ya juu Zaidi kuliko lile la watu wa Nuhu na lile la watu wa sodoma na Gomora.
Mathayo 11:20 “Ndipo akaanza kuikemea miji ile ambamo ndani yake ilifanyika miujiza yake iliyo mingi, kwa sababu haikutubu.
21 Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.
22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi. 23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.
24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.
Ukiona kwanini dunia mpaka dakika hii haijateketezwa, ujue kuwa sio kwamba Mungu anafurahia ulawiti wako, au uzinzi wako, au ulevi wako, au uvaaji vimini vyako, ni kwasababu uvumilivu wake unakungoja utubu, ili usiingie katika adhabu kuu ya siku ile.
Kama bado unasua sua, au upo vuguvugu ni wakati sasa wa kuanza kuyatengeneza mambo yako sawa na Mungu wako..Usijivunie dini au dhehebu,..wakati tuliopo ni wakati wa kuutafuta uhusiano wako binafsi na Mungu wako. Jiulize je! Ikiwa unyakuo utapita leo nitakuwa na uhakika wa kwenda na Bwana..Je! nikifa leo nitakuwa na uhakika wa kwenda mbinguni, au kwenye haya magereza ya milele nikiteseka huko usiku na mchana..
Watu wa kizazi chetu hichi ni watu ambao tumewekewa thawabu kubwa Zaidi kama tukishinda(Ufunuo 3:21)..Lakini pia tuzimbea na kuichezea neema tumeahidiwa adhabu iliyo kubwa zaidi kuliko wote waliotutangulia.. Hivyo uamuzi ni wetu sisi, Uzima au Mauti. Lakini sisi tunaopenda Maisha tutachagua uzima ambao unaletwa na Yesu Kristo tu peke yake,kwa kumwamini yeye na kujitwika misalaba yetu kila siku na kumfuata.
uvumilivu wa Mungu ni upendo kwetu.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Maran Atha.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?
Kuna ufufuo wa aina ngapi?
WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.
MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.
KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.
Shalom..Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…
Karibu tujifunze biblia…
Katika biblia kama wengi wetu tujuavyo…Kuwa maisha yanahubiri Injili, kadhalika vitu vya asili vinahubiri Injili…maana yake Mtu akijaliwa hekima mno kwa kuvisoma tu vitu vya asili anaweza kupata ufunuo mkubwa sana wa vitu vya ufalme wa Mbinguni..
Tukimwangalia kama Bwana wetu Yesu Kristo, kila mahali alikuwa anasema ufalme wa mbinguni umefanana na hiki au kile…Utaona kuna sehemu anasema
“ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu. Mathayo 13:24-26”..
Sehemu nyingine anasema Ufalme wa mbinguni umefanana na mpanzi aliyetoka kwenda kupanda mbegu zake, nyingine ziliangukia njiani ndege wakazila, nyingine kwenye miamba, nyingine kwenye miiba na nyingine kwenye udongo mzuri.. Maana yake ni kwamba kumbe hata katika ulimaji na upandaji kuna injili ya Kristo mule.. kwamba inahitajika hekima kiuvumbua.
Hata jinsi wezi wanavyovunja usiku na kuiba..kuna injili ndani yake…(Bwana Yesu alilifananisha tukio la kuja kwake na tukio la wizi usiku wa manane wakati tulalapo)…Hata katika mafisadi kuna injili ndani yake (kasome Luka 16:1-12)..Hivyo inahitajika hekima ya kiMungu kuivumbua bila kuiga mabaya hao.
Vivyo hivyo ukirudi katika miti kuna injili(Mathayo 13:31-32), katika ndege kuna injili (kasome Mathayo 6:26)..katika mapishi kuna injili (kasome Mathayo 13:33)..katika kufanya biashara kuna injili (Mathayo 13:45)…katika wavuvi kuna injili (kasome Mathayo 13:47)….katika kutafuta Ajira kuna injili pia (soma Mathayo 20:1-10).
Kadhalika katika kuoa na kuolewa na kualikwa katika harusi kuna injili (kasome Mathayo 22:1-13)..
Kwahiyo utaona karibia kila kitu kinahubiri Injili…Hakuna kitu hata kimoja kisichohubiri Injili…Inahitajika tu hekima kupata fundisho au funzo la kiMungu katika kila kitu.. Na ndio maaana mtu kama Sulemani Mungu alimpa hekima nyingi ya kufahamu kanuni za ki-Mungu duniani kwasababu alitazama karibu kila kitu kwa jicho la kumwona Mungu ndani yake, ndipo Hekima ikaingia ndani yake..
1Wafalme 4:32 “Naye akanena mifano elfu tatu, na nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano.
33 Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata hisopo umeao ukutani; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki.
34 Wakaja wa mataifa yote ili waisikie hekima ya Sulemani, toka wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamepata habari za hekima yake”.
Hivyo huu sio wakati wa kulala tena bali wakati wa kumwomba Roho Mtakatifu atufungue macho ya rohoni tuweze kuielewa injili inayojihubiri yenyewe katika kila kitu na kuifanyia kazi…Tukiwatazama ndege na wanyama hatuoni wanyama mashoga wala wasagaji hiyo ni injili ikitufundisha kuwa usagaji na ushoga si mpango wa Mungu..ni machukizo mbele za Bwana Yesu.
Tv tulizonazo, internet pamoja na simu zinatuhubiria Injili…Leo hii tukio dogo tu likitokea katika kijiji Fulani ndani sana kwa kupitia simu za mkononi..ndani ya dakika chache sana litaweza kuwa limeshamfikia hata Raisi wa nchi…ikifunua kuwa hata mtu chochote anachokifanya akiwa hapa duniani ndani ya muda mfupi sana kitakuwa kimeshamfikia Mungu wa mbingu na nchi..
Mahakama zinahubiri Injili..kama mtu akikutwa na kosa ambalo linamfanya asiendelee kukaa katika jamii yake tuchukue mfano labda kaua…cha kwanza atakamatwa na mapolisi, na kupelekwa mahabusu, kabla ya kuhukumiwa kisha atapandishwa kizimbani mahakamani kusomewa hukumu yake na baada ya hapo magereza..atakaa huko bila kurudia maisha yake ya asili kwa kipindi cha chote cha maisha yake..
Na hukumu ya Mungu mwenyezi ndio ipo hivyo hivyo…
Leo hii mtu akifanya dhambi hata zikamfikia Mungu, na alishaonywa na hataki kutubu anaendelea tu kufanya kwa makusudi…mtu Yule atakufa katika dhambi zake..hapo ni sawa na amekamatwa, na moja kwa moja atapelekwa jehanamu/kuzimu kafungwa huko…ambapo ni mfano wa mahabusu(magereza ya kitambo)…atakaa huko kwa kipindi Fulani akingoja siku atakayopandishwa mbele ya kiti cheupe cha Hukumu cha Mungu mwenyezi..ambapo atahukumiwa kulingana na matendo yake na kasha kutupwa katika lile ziwa la moto ambalo linafananishwa na magereza ya milele katika mazingira ya dunia yetu.
Mambo yote tukiyatafakari kwa jicho hilo..hatutaendelea kuuchukulia wokovu wetu kama ni jambo si la kuchezea bali tutauheshimu na kuushikilia sana kwa maana ni kitu cha thamani tulichopewa. Hizi ni nyakati za mwisho.
Bwana atusaidie sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA
Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?
LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.
Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?
JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.
UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
UBATILI.
Kulingana na kanisa Katoliki Sakramenti Ni ishara ya wazi ionekanayo, ya neema isiyoonekana, iliyofanywa na Yesu Kristo mwenyewe, itumike kutuletea au kutuongezea neema mioyoni mwetu.
Yaani kwa lugha nyepesi ni ishara za nje zionekanazo zilizobeba neema ya wokovu, zilizofanywa kwanza na Bwana Yesu, ambazo tukizifanya na sisi zitatuongezea neema moyoni mwetu ya kumkaribia Mungu Zaidi.
“Kulingana na kanisa Katoliki SAKRAMENTI hizi zipo saba (7), Nazo ni:
Kwamba kila mtu anayekuja katika ukristo ni sharti aupokee ubatizo, haijalishi ni Watoto wachanga, au vijana,au watu wazima, hawana budu kuupokea ubatizo. Ni ishara ya nje ya kuingizwa katika imani ya kikristo. Hii ni sakramenti ya kwanza.
Kipaimara ni Neno lenye maana ya “uthibitisho”. Kulingana na imani ya kikatoliki, ubatizo peke yake hautoshi, unahitaji kukamilishwa na tendo lingine la kipaimara kwa kuwekewa mikono. Hivyo Siku ambayo mtu huyo anapokea kipaimara hicho huwa anapakwa mafuta ya kunukia kwenye paji la uso wake yajulikanayo kama KRISMA, kama ishara ya kutiwa muhuri kuwa mtu huyo ni milki halali ya Bwana, kufuatana na andiko hili (Yohana 6:27). Hii ndiyo sakramenti ya pili.
Kushiriki meza ya Bwana. Kuula mwili wa Bwana na damu yake.. (1Wakorintho 11:23-25). Kama vile Bwana Yesu alivyowaagiza wanafunzi wake wafanye vile kwa ukumbusho wake.
Hii ni ibada maalumu kwa ajili ya wagonjwa kama ilivyofanywa na mitume kwa agizo la Yakobo (Yakobo 5:14) ..Mathayo 10:1, Marko 6:3…Hii nayo ni moja ya sakramenti ya Bwana.
Inahusisha kuungama dhambi, na hii ni lazima uende mbele za Padri na kuzikiri dhambi zako mbele zake, na yeye atakuombea na dhambi zako zitaondolewa kama agizo ambalo Kristo aliwapa mitume wake..(Yohana 20:23).
Uteuzi wa Vyeo katika kanisa..kama vile ukasisi, ushemasi, na uaskofu.Kama vile jinsi Bwana Yesu alivyowachagua mitume wake,.Na vivyo hivyo uteuzi katika kanisa ufanyike katika kuliongoza kundi, hiyo inafuatana na kuteuliwa na kuwekewa mikono na askofu wa jimbo.
Ndoa ya wakristo ni sakramenti ya Yesu na kanisa lake. Ufunuo 21;9..Kama vile Kristo alivyoona na kanisa lake, vivyo hivyo ndoa inafunua sakramenti hiyo.
Lakini Je! Maagizo haya yote ni ya kibiblia na Je ni lazima kila mkristo ayafuate ili apokelewa na Mungu?..
Ukweli ni kwamba agizo la ubatizo ni agizo la msingi katika Imani, lakini ubatizo unakuja kwa mtu aliyetambua kwanza kuwa yeye ni mwenye dhambi na hivyo anahitaji KUOKOLEWA. Hapo ndipo anapotubu na kwenda kubatizwa kwa hiari yake mwenyewe. Lakini mtoto mchanga hajatambua bado jema na baya, wala yeye mwenyewe hajitambui hivyo ubatizo kwake hauna maana.. wao wanawekewa tu mkono, kama wakfu kwa Bwana. Lakini sio kubatizwa.. Hivyo suala la ubatizo kwa vichanga ni batili.
Kwahiyo ubatizo sahihi ni ule wa kujimbua kwanza, wewe ni mwenye dhambi na kwamba unahitaji kuokolewa, vile vile ni sharti uwe wa maji tele sawasawa na Yohana 3:23, Na uwe kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na maandiko haya (Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5), ubatizo mwingine nje ya hapo ni batili kulingana na biblia, hivyo kama ulibatizwa tofauti na hapo unahitaji kwenda kubatizwa tena.
Vilevile Watoto wachanga ni kweli wanapaswa wawekewe mikono kama mbaraka kutoka kwa Bwana. Sawasawa na Bwana Yesu alivyofanya (Mathayo 19:14-15)..Lakini sio kwenda kupitia mafundisho Fulani ya mapokeo kwanza mwaka mzima na ndipo baadaye aje kuwekewa mikono na askofu au Padre..Agizo hilo halipo kwenye maandiko.
Halikadhalika, utumizi wa mafuta kwa ajili ya kuombea wagonjwa si jambo la kuliundia kanuni..kwasababu sio mafuta yanayomponya mtu bali kinachoweza kumponya mtu ni damu ya Yesu tu peke yake. Kwasababu biblia imetuambia..yoyote tufanyayo tufanye yote kwa jina la YESU Kristo. (Matendo 4:12)
Na mwisho kabisa, kuwekewa mikono kwa ajili ya utumishi na waliokutangulia kwenye Imani ni jambo jema lakini pasipo hilo haimaanishi kuwa huwezi kutumika katika kuifanya kazi ya Mungu sawasawa na wale wengine. Ikumbukwe kuwa mitume 12 walichanguliwa kweli na Bwana Yesu Kristo, wakaishi naye, wakala naye, wakapewa agizo naye.Lakini biblia inatuambia Mtume Paulo alitenda kazi Zaidi ya hao wote, na yeye hakuwa miongoni mwa wale 12, wala hakuwahi kutembea na Yesu duniani,.
Utume wetu unathibitishwa na Roho Mtakatifu ndani yetu. Ni vema kumtafuta Roho Mtakatifu, kuliko kutafuta vyeo. Kwasababu yeye ndiye anayewatia nguvu wateule wake katika kumtumikia. Hata wewe Bwana anaweza kukufanya kuwa mtumishi wake, endapo tu utatii na kuwa mwaminifu kwa kila anachokulekeza kukifanya.
Hivyo ndugu, toka katika kamba za udini, na kamba za mapokeo, ambazo nyingi ya hizi zinakufunga usiomwone Mungu katika utimilifu anaotaka. Rudi kwenye Neno. Penda kujifunza kusoma biblia peke yako huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie. Penda pia kujifunza sehemu mbalimbali, na Roho Mtakatifu atakusaidia kuchagua kilicho sahihi na kutupa kisichosahihi, kwasababu ndiyo kazi yake hiyo Yesu aliyosema amemtuma duniani kwayo..(Yohana 16:13)
Je! Unajua kuwa tunaishi katika kanisa la mwisho la saba lijulikanalo kama LAODIKIA, na UNYAKUO upo karibu..Siku yoyote wateule watotoweka na kwenda mbinguni kwa BABA..? Kama hujafanya hivyo ni heri ukamgeukia Mungu wako sasa, kwasababu muda tuliobakiwa nao ni mchache kabla PARAPANDA haijalia. Kama upo tayari kutubu dhambi zako leo na kusema nataka leo hii Bwana Yesu aanze kutembea na mimi maishani mwangu..
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya Kipaimara?..Na je! Ni jambo la kimaandiko?
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
UNYAKUO.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?
JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
SWALI: Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe, kwanini asingeyatoa tu na kuyaacha yaende sehemu nyingine mbali na wale nguruwe, kwani kufanya vile si ni kama aliharibu biashara au mali za wengine?
JIBU: Kulikuwa na sababu kuu mbili kwanini lile tukio litendeke vile:Sababu ya kwanza ni kwasababu yale mapepo yenyewe yalimwomba Bwana yawaingie wale nguruwe..Na sababu ya pili ambayo ndio kuu, ni ili Mungu atengeneze ushuhuda wenye nguvu zaidi utakaoweza kuwavuta wanadamu wengi watubu kirahisi.
Kumbuka kuwa pale awali, Yesu alipoliuliza lile pepo jina lako ni nani..lilijibu na kusema jina langu ni LEGIONI kwasababu tupo wengi..Na Legioni kwa zamani lilikuwa ni jeshi lenye askari si chini ya 82,000..Hivyo piga hesabu mapepo yaliyokuwa ndani ya Yule mtu hayakupungua idadi hiyo, jaribu kufiria jambo hiyo si rahisi kuamini na wengi kama lingewezekana mtu kuwa na idadi kubwa ya mapepo namna hiyo .
Hivyo Yesu kuona vile, kuwa wameomba jambo ambalo litaufanya ushuhuda uwe na nguvu zaidi, na kwamba kwa kupitia huo utawahakikishia kuwa mapepo kweli yapo, na kwamba yanaweza kumuingia mtu kwa wingi wa idadi ile, na kwamba yanaweza kumvaa mtu na kumfanya afanye vitu ambavyo yeye mwenyewe hajataka kuvifanya ikiwemo hata kujiua..Ndio akaruhusu yawaingie wale nguruwe ambao walikuwa 2,000,.Ambayo kwa hesabu za haraka haraka nguruwe mmoja aliingiwa na mapepo si chini ya 40,..aliruhusu hivyo ili watu waone kwa macho yao, kwamba mapepo yapo na jinsi mapepo yakimwingia mtu yanavyomfanya na yanapompelekea mwishoni..MAUTINI..Kwahiyo kwa tukio lile ndipo tulipofahamu kuwa mapepo sio nadharia bali ni vitu halisi kabisa…
Hivyo wale wachungaji walivyoshuhudia kitendo kile tu, waliondoka na kwenda kuhubiri mashambani na na vijijini matendo makuu waliyoyaona kwa macho yao, ndipo wale watu waliohubiriwa na wachungaji pia wakaja kushuhudia kwa macho yao..kuona wale nguruwe wakielea ziwani wote wamekufa, na mtu Yule ni mzima kabisa wataachaje kuamini?…Kwasababu hakuna mtu mwenye nguvu ya kwenda kukamata nguruwe 2000 na kuwazamisha baharini..ni lazima kuna nguvu nyingine ya zida imehusika hapo.
Vile vile na Yule mtu aliyekuwa kichaa alipokwenda kuhubiri na kutoa ushuhuda ule mzito sio ajabu biblia inatuambia alipoenda kuhubiri huko Dekapoli watu wote WALISTAAJABIA, walichokistaajabia ni nini kama sio huu ushuhuda wa nguruwe kuingiliwa na mapepo?. Na hapo pia bila shaka wengi walitubu kwa kupitia ule. (Soma Marko 5:12-20)..Kama vile ulivyokuwa ushuhuda wa Nabii Yona…watu waliposikia jinsi alivyokaa tumboni mwa samaki siku tatu bila kufa..wakaamini na kutubu kwa ishara ile.
Hivyo hata leo hii, Kristo anaweza kuruhusu mtu apate hasara Fulani ili uwe ushuhuda wa kuwaponya watu wengine. Shetani alimwomba Mungu ampige Ayubu, kama tu haya mapepo yalivyoomba ruhusa Bwana Yesu kuiharibu mifugo ya wengine..Lakini kwa kupitia maisha ya Ayubu sisi leo hii tunaponyeka. Hivyo si kila adhabu ambayo hukustahili inapokupata, ikufanya umchukie Mungu, mengine ni kwa utukufu wa Mungu, zaidi zidi tu kusonga mbele maadamu wewe bado ni mwana wa MUNGU.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Kurudi Nyuma kiimani maana yake nini?..Nitapokeaje nguvu ya kushinda dhambi?
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lizidi kubarikiwa..Karibu tujifunze maandiko.
Swali la kujiuliza leo ni nini maana ya kurudi nyuma…Mtu mmoja ukikutana naye na ukapata bahati ya kumwuliza je umeokoka?..Atakuambia ndio niliokoka ila nimerudi nyuma…Ukizidi kumwuliza je umerudi nyuma kwa namna gani atakwambia…Tamaa za kimwili zilinizidia hivyo nikajikuta ninarudi nyuma na kuangikia katika uasherati
Kama jambo hili unalipitia na wewe ndugu yangu wa thamani nataka leo hii nikuambie kuwa hukurudi nyuma…bali ulikuwa hujaokoka kabisa!…hivyo unapaswa uokoke. Leo nitakuambia mtu aliyerudi nyuma anakuwaje..
Mtu ambaye amempokea Yesu Kristo kikamilifu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake, na kudhamiria kabisa kuuacha ulimwengu kwa vitendo, na kubeba msalaba wake na kumfuata Yesu na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi…Mtu wa namna hiyo anakuwa tayari ameshaokoka..Na katika ulimwengu wa roho..anakuwa amekufa kwa habari ya dhambi, na yu hai kwa habari ya haki na anakuwa amehama kutoka mautini kuingia uzimani, na kuyavua matendo yote ya giza. Huyo anakuwa yupo chini ya mikono salama ya Yesu mwenyewe…Bwana Yesu anampa nguvu ya ajabu ya kushinda dhambi na ulimwengu kwa kutiwa muhuri na Roho Mtakatifu…Mtu huyo shetani hawezi tena kwa namna yoyote kumnyakua kutoka mikononi mwa Mungu…Uhai wake unakuwa unafichwa pamoja na Kristo.
Wakolosai 3:3 “Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu”.
Mtu huyo anakirimiwa uwezo wa ajabu wa kushinda dhambi..kiasi kwamba kutenda dhambi kwake ni uchaguzi..sio kitu kinachomlazimu kama vile pumzi…Shetani anapomletea vishawishi vya kufanya uasherati ni kama mtu anayepitisha viatu barabarani …hivyo ni uamuzi wa Yule mnunuzi aidha anunue au asinunue…vilevile na Yule muuzaji anakuwa hana uwezo wa kumlazimisha anunue au akivae(ni jambo la uchaguzi), halihusishi kulazimisha…Ndivyo shetani anavyokuwa mbele ya mtu aliyeokoka kikamilifu.
Lakini kwa mtu ambaye hajaokoka dhambi kwake ni sheria, sio jambo la kuchagua, ni lazima afanye, atake asitake..anakuwa mtumwa wa ile dhambi, anakuwa na wakati mwingine na uwezo wa kujizuia kwa kipindi Fulani lakini baada ya muda mfupi anairudia ile dhambi kwa kishindo..… shetani anapomletea ushawishi wa kutenda dhambi kuna nguvu ya ajabu inamsukuma kuifanya ile dhambi hata kama hapendi, na kisha anakwenda kuifanya…
Ndio maana unasikia mtu anakwambia yaani nashindwa kuitawala tamaaa yangu najikuta nafanya hiki au kile, nashindwa kuacha kufanya uasherati, nashindwa kuacha kujichua, nashindwa kuacha kuangali picha chafu za ngono, nashindwa kuacha kunywa pombe, nashindwa kuacha kuvuta sigara, nashindwa kuacha kusikiliza miziki ya kidunia n.k…. Sasa huyo ni mtu ambaye hayupo ndani ya Kristo..
Na hali hiyo ya kushindwa kuishinda dhambi inatokana na mtu mwenyewe hajaamua kumfuata Kristo kwa kujikana nafsi, anatamani kuokoka na huku bado anatamani kuendelea kuishi na girlfriend wake/boyfriend wake, anatamani kuokoka lakini bado anazipenda movie zake na tamthilia zake na miziki yake, anakuwa hayupo tayari kuviacha kwa vitendo…hivyo ule uwezo wa kushinda haushuki ndani yake.
Sasa kwa mtu ambaye kashaokoka kikamilifu na uwezo huo wa kushinda dhambi umeshuka ndani yake…kuna uwezekano wa kupitia vipindi Fulani vidogo vidogo vya kurudi nyuma..Kurudi kwake nyuma hakutakuwa kuvuka kabisa mstari na kurudia ulimwengu hata kufikia viwango vya kurudi kufanya uasherati au kurudi kutoa mimba, au kurudi kunywa pombe au kuvuta sigara…hapana..bali kurudi kwake nyuma kunakuwa ni aidha kupunguza kiwango chake cha kusali kidogo..pengine alikuwa anasali masaa kadhaa lakini sasa kajikuta kapunguza anasali muda mfupi …alikuwa ana upendo sana, anajigundua upendo wake umepungua kidogo…alikuwa anasaidia watu lakini kajikuta kapunguza…alikuwa anajituma kuhubiria wengine lakini kajikuta kapunguza…na sio kaacha kabisa hapana! Bali kapunguza….Mtu wa namna hiyo ndio KARUDI NYUMA KIIMANI!..Na si mtu karudi kwenye uasherati, karudi kwenye ulevi, karudi kwenye anasa ndio karudi nyuma…Huyo hajarudi nyuma bali alikuwa hapo kwanza hajaokoka kabisa!..hivyo anapaswa aokoke.
Na kama imetokea mtu kashaokoka kabisa na nguvu ile ya kushinda dhambi ilishashuka juu yake…kiasi kwamba dhambi mbele yake ikija ni chaguo…na si kiamrisho…kiasi kwamba alishaacha uasherati na kulikuwa hakuna nguvu yoyote ya kumchukua katika dhambi hiyo, alikuwa ameushinda ulimwengu kiasi kwamba uuaji kwake ilikuwa ni kitu ambacho asingeweza kukifanya kwa namna yoyote ile…Mtu wa namna hiyo akaamua kwa idhini yake kuchagua kurudi kwenye dhambi…Basi biblia imesema wazi kuwa mtu wa Namna hiyo amemsulubisha Kristo mara ya pili hivyo ile neema ya kuvutwa tena kurudi kutubu..inaondolewa kabisa…kamwe hatasikia tena nguvu ya kutubu na hivyo ataendelea kuwa mbaya hivyo hivyo mpaka mauti…Kwasababu nguvu inayotuvuta kwa Mungu na kutushikilia ndiyo inayoitwa Neema, sasa mtu aliyeipokea hiyo neema na kwa idhini yake anayarudia matapishi huyo haiwezekani kutubu…Sio kwamba siku moja atataka kutubu asisamehewe!..Hapana…bali ile hali ya kutaka kutubu inaondolewa ndani yake kiasi kwamba hatatamani hata kutubu tena. Anakuwa kama watu ambao hawataki kusikia injili kabisa.
2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.
21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.
22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni”.
Na tena inasema katika Waebrania..
Waebrania 6:4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,
5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri”.
Hivyo kama umeokoka kikamilifu, na unaona kuna nguvu ya kushinda dhambi ndani yako..Usigeuke kurudi nyuma ndugu yangu…usirudie uasherati wala uzinzi wala ulevi, wala utoaji mimba usiichezee hiyo Neema uliyopewa (Nguvu ya kushinda dhambi ni ya kuithamini sana kuliko kitu kingine, maana ndiyo Neema yenyewe hiyo)…Usipoithamini kutakuwa hakuna nafasi ya pili wewe au mimi kurudia utakatifu tena…Ndicho kilichomkuta shetani. Aliichezea neema na hivyo akajiharibia mwenyewe…
Kadhalika kama ulikuwa unadhani kwamba kwa kufanya kwako uasherati ni kwamba ulirudi nyuma baada ya kuokoka!…Na leo unataka kutubu!..Basi Neema ya kukuvuta kwa Kristo bali inalia moyoni mwako… Hivyo Leo fahamu kuwa hukurudi nyuma bali ulikuwa hujaokoka kabisa!!..Na kama leo hii unataka kutubu na kusema unataka kuokoka kabisa na kuacha dhambi na ulimwengu..Ukidhamiria kutoka moyoni kwa vitendo kwamba kuanzia leo na si kesho unaacha kutazama yale matamthilia ya kihindi na ya kifilipino unayoyatazama yenye maudhui ya kipepo, unaacha kuvaa vimini na unakwenda kuvipiga moto vyote sasa hivi, unaacha kuvaa suruali haijalishi una gauni moja tu, unaacha kupaka wanja, hereni, kuvaa wigi, kujichubua, unaacha kusikiliza miziki ya kidunia na unaifuta yote hata kwenye simu yako..na kuanzia leo ukisema ninaamua kumfuata Yesu kwa gharama zozote na kwamba upo radhi hata kuchukiwa, kutengwa, kuonekana mjinga na kujikana nafsi kwa viwango vyote na kwenda kubatizwa ubatizo sahihi…hapo ndipo utaona uweza wa Mungu juu ya maisha yako wa kushinda dhambi, utakapopokea uwezo wa kushinda Uasherati, ulevi, anasa, na vitu vyote vya kidunia kirahisi havitakuendesha na kukufanya ufanye jambo usilotaka wewe kulifanya.
Idadi kubwa ya watu wanaojiita wakristo hawajapokea uweza huo ndio maana wao kushinda dhambi ni ngumu…Bado hawajamuonja Kristo..Kumuonja Kristo maana yake ni kuonja huo uwezo ndani yako..Na pasipo huo uwezo kushuka ndani yako..kamwe huwezi kuishinda dhambi..kila siku utasema umeokoka, na kila siku utaongozwa sala ya Toba..lakini baada ya siku mbili tatu utarudia mambo yote ya kale…Fomula pekee ya kuipokea huo uwezo ni hiyo hapo juu…Amua kujikana nafsi kwa kuacha vitu vyote kwa vitendo.
Bwana akubariki sana.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Naomba watu wote tusome hii…
Hakuna mtu asiyejua kuwa shetani, naye hujigeuza na kuwa mfano wa malaika wa Nuru (2Wakorintho 11:14)? Lakini tunapaswa tujiulize lengo la yeye kujibadilisha vile ni nini? Utagundua kuwa Hana lengo lingine zaidi ya kuuchafua utakatifu wa malaika ili na wao pia waonekane kuwa ni waovu. Vivyo hivyo na watumishi wake nao wanafanya kazi hiyo hiyo .. Ili mwisho wa siku tuhitimishe kuwa wote ni wabaya, wote ndio wale wale wapotoshaji.
Embu jaribu kuufikia tena vizuri ule mfano Bwana Yesu aliousema..
Mathayo 13:24 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu”.
Umeelewa hapo? Ni kwanini magugu yaliachwa yaendelee kuwepo shambani hadi wakati wa Mavuno? Unadhani mwenye shamba alikuwa anapenda kuyaona yakiendelea kustawi shambani muda wote huo?, jibu ni la! lakini ilimpasa atumie hekima kwasababu alijua kama akitaka tu kuyashughulika kuyafyeka atajikuta anazing’oa na ngano ndani yake na mwisho wa siku atapata hasara kubwa ya kazi yake aliyoitaabikia..
Kwasababu wanasema wakati magugu yakiwa machanga, huwa yanatabia ya kushikamana sana na ngano, vilevile yanafanana mno kiasi kwamba kutofautisha gugu katikati ya ngano ni kazi sana..Hivyo ukijaribu kung’oa tu gugu moja, pembeni yake unaweza kuta zilikuwa ngano 6 zimejishikamanisha nayo, na mwisho wa siku ni hasara…Hivyo si kazi rahisi kama unavyofikiria, mahali pekee ambao utaweza kuziona na kuzing’oa bila kuathiri ngani ni wakati wa mavuno tu, kwasababu maumbile yako yanajitofautisha kabisa na ngano..
Ndugu yangu, tusiwe wepesi wa kutoa hukumu ya moja kwa moja kuwa makanisa yote ya kiroho, yanapotosha, makanisa madogo madogo ambayo hajasajiliwa yote ni feki, wachungaji wote ambao wanawaombea watu shida zao ni bandia, watu wote wanaokesha makanisani na kumwomba Mungu usiku na mchana ni wajinga, hawana akili, wote wanaomlilia Mungu ni wapumbavu, masikini waliokosa uelekeo wa maisha, wenye stress za maisha, wavivu na wasiojituma, wamekata tamaa, hawapendi kufanya kazi, wanapenda vya bure..
Ikiwa ni wapumbavu, wewe unataka wafanye nini ili wawe na hekima? Unataka waache kumlilia Mungu wao wakaililie pesa? Hiyo ndiyo iliyowaleta duniani?…Unataka Watumishi waache kuhudumu madhabahuni wote waondoke na wewe waende ofisi kutafuta pesa, ni nani basi atakayekaa kukuletea wewe injili,? Hata elimu yako inakufundisha kitu kinachoitwa Opportunity cost, ili uweze kufanya jambo moja kikamilifu ni lazima uache kufanya lingine..Huwezi kushika mawili kwa wakati mmoja..Na wengi wanaosema mambo kama hayo asilimia kubwa ni wale ambao hata Kristo hajaumbika vizuri ndani yao, wala hawayajua maandiko yanaagiza nini kuhusu mambo ya ibada..Si wote wanaomlilia Mungu hawajasoma kama wewe unavyofikiri, si wote wanaomtafuta Mungu, ni maskini kama wewe unavyodhani, si wote wanaokesha kuomba hawajui kuwa kuna kufanya kazi..
Tusitumie vigezo vya watu wachache wanaotumiwa na shetani kuliharibu kanisa la Mungu na kuhitimisha na wengine wote hawafai.. Wanaotumia mafuta ya upako, chumvi,sabuni, balbu, maji, wanaohubiri habari za mafanikio wakati wote, wanasahau toba ya msamaha, hao wote ndio mapando ya shetani yaliyowekwa ili kuwafanya watumishi wengine wote waonekane kuwa ni wa uongo…
Embu fumba kinywa chako, ishia tu kukemea, kukaripia na kuhubiri lakini usishiriki katika kuchua hatua yoyote ya nguvu, ili kutokomeza hilo suala na kuyaita makanisa yote ya kiroho ni (vibanda-Imani), na kutaka yote yafungiwe, au yawekwe masharti katika kuabudu.. wewe mwachie Mungu, yeye ndio atakayeshughulika nao, na yeye ndiye atakayewapukutisha mmoja baada ya mwingine, hiyo sio kazi yako rafiki.
Lakini ukijiona wewe una hekima zaidi ya Mungu..Angalia kuna roho ya mpinga-kristo inakunyemelea nyuma yako. Na Siku utakapoimpa ibilisi nguvu ya kutosha basi ujue kuwa wakati utafika hutaweza kuuza wala kununua wala kufanya jambo lolote kama hutakuwa na ile chapa ya mnyama…ambayo chumbuko lake litakuwa katika mambo kama hayo hayo ya ibada za sharti..
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
CHAPA YA MNYAMA
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
JE! WEWE NI MBEGU HALISI YA KRISTO?
TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?
DANIELI: Mlango wa 12.
MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.
Kulingana na historia ya Taifa la Israeli, tangu zamani wakiwa jangwani walikuwa wanamwabudu Mungu kwa kumtolea Dhabihu za aina mbalimbali mbele ya ile hema ya kukutania kama Musa alivyoagaizwa na Mungu kufanya, Na hema hii ilikuwa ni ya kuhama hama sio rasmi. Lakini mara baada ya kuingia katika nchi yao ya ahadi, Mfalme Daudi baada ya kuona kuwa Mungu hana eneo rasmi la kuliweka jina lake, eneo ambalo watu wa makabila yote ya Israeli yatakusanyika kumtolea Mungu kafara, akaazimia ndani ya moyo wake kumjengea Mungu nyumba.. Hivyo Mungu akasikia matamanio yake, na kuyaridhia lakini kwa masharti kuwa mwanawe ndiye atakayemjengea Nyumba hiyo.
Hivyo mwanawe Sulemani akaja kumjengea Mungu Nyumba kwa mafanikio yote, ambayo Mungu aliitukuza na kuliweka jina lake huko katika mji wa Yerusalemu..Na Nyumba hiyo ndiyo iliyoitwa HEKALU. Hivyo Hekalu hili lilikuwa ni moja tu, watu wote walipanda kwenda kumtolea Mungu kafara zao mbele ya hekalu hili lililokuwepo Yerusalemu.
2 Nyakati 7:1 “Basi Sulemani alipokwisha maombi hayo, moto ukashuka kutoka mbinguni, ukateketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu; utukufu wa Bwana ukaijaza nyumba.
2 Wala makuhani hawakuweza kuingia nyumbani mwa Bwana, kwa kuwa utukufu wa Bwana umeijaza nyumba ya Bwana.
3 Wakatazama wana wa Israeli wote, uliposhuka ule moto, utukufu wa Bwana ulipokuwapo juu ya nyumba; wakasujudu kifulifuli hata nchi sakafuni, wakaabudu, wakamshukuru Bwana, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele”
Lakini mara baada ya wana wa Israeli kuchukuliwa tena utumwani Babeli, na nyumba ya Mungu kubomolewa, kukawa hakuna tena sehemu ya kwenda kumfanyia Mungu ibada na kutoa sadaka za kuteketezwa, Hivyo waliporudi tena Yerusalemu kutoka Babeli, iliwalazimu kuwa na makusanyiko madogo madogo kwa ajili ya kujifunzia torati, na kusoma Zaburi pamoja na Kufanya dua. Hayo ndio yaliyoitwa masinagogi, Na Huko ndipo madhehebu ya mafarisayo na Masadukayo yalipozaliwa. Na yaliendelea kusambaa karibu sehemu kubwa ya dunia.
Muda rasmi haujulikana yalianza hasaa wakati gani..Lakini ni kipindi cha kati ya kuchukuliwa babeli hadi kipindi cha karibu na kuja kwa Bwana Yesu Kristo.
Na ndio maana Biblia inarekodi Bwana Yesu alikuwa pia akizunguka katika masinagogi yao akihubiri.
Marko 1:38 “ Akawaambia, Twendeni mahali pengine, mpaka vijiji vilivyo karibu, nipate kuhubiri huko nako; maana kwa hiyo nalitokea.
39 Akaenda akihubiri katika masinagogi yao, katika nchi yote ya Galilaya, na kutoa pepo”
Unaona soma pia (Luka 4:16-21)
Kulingana na tafsiri ya kibiblia kanisa maana yake ni “walioitwa”..Wale walio mwamini Yesu Kristo, wakiwa wamekusanyika wawili au watatu kwa jina lake, tayari hilo ni kanisa. Japokuwa Neno hilo limezoeleka na wengi kama jengo linalotumiwa na wakristo kuabudia..
Hivyo kwa kuhitimisha hekalu lilikuwa ni moja, ambalo lilijengwa na Mfalme Sulemani, lakaja kubomolewa na Mfalme Nebukadneza wa Babeli, likaja kujengwa tena na Zerubabeli na kubomolewa na Warumi mwaka 70 W.K, Na litakuja kujengwa tena pale Jerusalemu katika siku za mwisho.. Lakini masinagogi yalikuwa mengi, ambayo tunaweza kuyaita makanisa ya wayahudi yakifundisha dini za kiyahudi.. Na makanisa ambayo leo hii tunayaona ni Makanisa ya kikristo yakifundisha imani ya YESU KRISTO..Hiyo ndio tofauti yao.
Shalom.
[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=4AC-rH1ndvo[/embedyt]
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)
Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?
Tofuati kati ya Myahudi, Mwisraeli na Muebrania ni ipi?
Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?
Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?
TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!
Tofauti katika ya zaka na sadaka ni ipi?