Category Archive Home

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

Biblia inatuambia katika 2Timotheo 3:1 kwamba siku za mwisho kutakuwa na NYAKATI ZA HATARI SANA, na kama ni nyakati za Hatari tunapaswa tuchukue tahadhari kubwa zaidi kuliko hata za watakatifu waliokuwa wanaishi nyakati za kale kabla yetu, kwasababu biblia pia inasema shetani angali akijua kuwa muda wake ni mchache anafanya juu chini awaangushe wengi kwa njia yoyote ile. Mkristo ni kuwa makini huu sio wakati wa kuamini kila “roho” inayodai kuwa ni ya Mungu, biblia imetuonya na kutuambia,

1Timotheo 4:1 “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani”

Sasa mambo ya duniani yanatufundisha nini?, kwamba tunajua hakuna mtu yeyote asiyependa kununua kitu kilicho katika uhalisia wake (original), na kama kitu hicho kitasifika kweli kuwa ni original basi hakitakosa kuwa na feki yake baada ya muda fulani,

Lakini utakuta kwa mwanzo kilipoanza kutolewa masokoni labda tuseme ni simu utaona kuwa karibia simu hizo zote zilikuwa ni original, lakini kwa jinsi siku zilivyokuwa zinazidi kwenda, kidogo kidogo utashangaa kuona feki chache zipo humo humo zikifanana kabisa na zile original, na kwa jinsi siku zitakavyozidi kuendelea kwenda, hata zile original huwa zinazidiwa na feki sokoni, Feki zinakuwa ni nyingi, na matokeo yake huuzwa kwa bei rahisi, na hizo ndio watu hupenda kuzikimbilia kwasababu ni bei nafuu..Lakini baadaye wanajikuta wanaangukia katika majuto pale wanapogundua kuwa hazidumu, halafu bado hazikidhi mahitaji yale ambayo aliyoyatarajia kuyaona kutoka katika hizo simu..

Na ndio hapo inampelekea mtu kuhangaika kutoka kwa fundi huyu hadi fundi yule,na kutumia gharama kubwa zaidi hata ya ile aliyoinunulia, akiona tatizo bado lipo anachukia kabisa kuwa na simu na kujuta ni kwanini alinunua simu na mwisho wa siku kuitupa..tatizo sio AINA YA ILE SIMU bali tatizo ni U-FEKI wa simu.

Kadhalika katika ukristo hakuna kitu ambacho shetani hajafanikiwa kukiundia feki chake, biblia inasema, anao wachungaji wa uongo (Yer 23:1), anao mitume wa uongo (2Kor 11:3), anao waalimu wa uongo, watumishi wa uongo na manabii wa uongo (2Petro 2:1). Kama vile tu Bwana alivyokuwa na watumishi wake wanaomtumikia, Sasa shetani kuwa na watumishi wa uongo tu haitoshi ni vema pia kujua hao watumishi wanamtumikia nani, au wanamtangaza nani, au wanamuhubiri nani?.

Kama vile tu mitume, wainjilisti, waalimu, na manabii wa Bwana walikuwa wanafanya kazi moja ya kumtangaza YESU KRISTO ili watu wote wamwamini yeye, kadhalika hawa nao wanafanya kazi moja ya kumtangaza “yesu” wao ambaye siye yule YESU tunayemwambudu wa kwenye maandiko, na wanafanya hivyo ili watu tu wamwamini huyo waangamie siku za mwisho.

Biblia ilishaweka wazi kabisa, kuwa yupo “yesu” mwingine, yupo “roho” nyingine, kadhalika ipo nayo “injili nyingine” ambayo sio ile Bwana aliyoitoa kupitia mitume wake watakatifu tangu mwanzo, soma

2Wakorintho 11:4 “Maana yeye ajaye akihubiri YESU MWINGINE ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea ROHO NYINGINE msiyoipokea, au INJILI NYINGINE msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!”

Unaona hapo? Kazi ya hawa watumishi wa uongo ni kumtangaza yesu mwingine anayoonekana kama ni YESU halisi, na roho mwingine anayeonekana kama ni ROHO wa Mungu halisi ya Mungu na Injili nyingine ineyoonekana kama ni injili halisi ya Mungu lakini kumbe ni yesu-FEKI, roho-FEKI, na injili-FEKI. Lakini tunajua kitu feki kwa mwonekano wa nje! ni ngumu kugundua kwasababu vyote vitaonekana kuwa ni sawa lakini utendaji kazi wake, na udumuji wake ndio vitakavyowatenganisha..wote watalijata jina la YESU katika shughuli zao za ibada, watatolea mapepo na kutabiri n.k..

Na ndio maana Bwana alisema mtawatambua kwa MATUNDA YAO, hicho tu!.

Mathayo 7.15-23 “ Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa MATUNDA YAO. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?

17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.

20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.

21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Ndugu kumbuka ili uwe na uhakika YESU uliyempokea katika maisha yako, ni HALISI, ni lazima ujiulize, JE! UNAUHAKIKA UMEOKOLEWA NA KUSAFISHWA DHAMBI ZAKO KWA DAMU YAKE?, Kiasi kwamba hata ukifa sasa bila shaka yoyote utakwenda mbinguni moja kwa moja?. Kwasababu kumbuka kiini cha Kristo kuja duniani mpaka kufikia hatua ya kuitoa nafsi yake sio wewe kuwa bilionea hapana bali ni suala la UKOMBOZI, je! wewe tangu umfahamu YESU, alishawahi kuyabalisha maisha yako, na kupata uhakika wa wokovu ndani ya nafsi yako?. Jana yako inatofauti na leo yako? Kama sivyo basi! Ujue ulimpokea YESU mwingine ambaye siye aliyehubiriwa na mitume.

Kadhalika unasema unaye ROHO MTAKATIFU, je! huyo Roho aliyeko ndani yako anakufanya kuwa MTAKATIFU kama jina lake lilivyo?, na Je! anakuongoza katika kuijua kweli yote kama maandiko yanavyosema (Yohana 16:13)?, na Je! anakushuhudia kila siku katika maisha yako kuwa wewe ni mwana wa Mungu?(Warumi 8:16). Kama sio basi ufahamu kuwa ulipokea roho nyingine ambayo sio ROHO MTAKATIFU. Kadhalika ulihubiriwa injili nyingine ambayo sio injili iliyohubiriwa na watumishi wa Mungu hao mitume (yaani biblia).

Na ndio maana hauwezi kudumu katika IMANI, ni kwasababu gani? Ni kwasababu hukumpokea Kristo HALISI katika maisha yako, leo unasimama kesho unaanguka, Huyo ni yesu mwingine ulimpokea asiyeweza kukupa wokovu wa uhakika katika maisha yako. Dhambi inakutawala, unashindwa kuitawala dhambi na bado unasema umeokoka, unashidwa KUJILINDA hapo ndugu hujaokoka, biblia inasema wote waliozaliwa na Mungu hawatendi dhambi, ikiwa na maana kuwa dhambi haiwatawali 1Yohana 5.18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu HUJILINDA, wala yule mwovu hamgusi.”

Na ndio sababu huwezi kudumu katika imani kwasababu ni yesu-feki ulimpokea ukidhani ni BWANA YESU KRISTO. Kumbuka kazi ya Mungu haiwezi kuwa na kasoro, Kristo akimwokoa mtu kamwokoa kweli kweli wala habahatishi kwasababu msalaba una nguvu kuliko kitu chochote kilichowahi kusikika chini ya jua hili.

Ulikuwa hivyo ni kwasababu ulikuwa radhi kusikiliza injili isiyo ya gharama,(unayoweza kuipata sokoni muda wowote), ile ambayo manabii wa uongo wanayoifundisha kwamba unaweza ukawa ni mkristo bado pia ukawa ni wa kidunia, unaweza ukawa mkristo bado usijikane nafsi yako usiishe kama mitume walivyoishi kujikana nafsi zao, bado uwe unaishi maisha kama mfano wa watu wa ulimwengu huu na huku umeokoka, ukristo usioweza kuachana anasa, ukristo ambao unaruhusu mwanamke kuvaa suruali na vimini, pamoja na mawigi, na Kupaka lipsticks na wanja, ukristo unaosema Mungu siku zote ni wa rehema, hawezi kuwaangamiza watu wake aliwaumba hivyo ishi tu atakurehemu kwa neema zake maadamu umemkiri kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako inatosha.

Injili ambayo haina muda kusisitiza mtu kuishi maisha ya kujilinda roho yako kila siku, bali unasisitiza kila siku kuulinda mfuko wako. Ukristo unatoa tu mafundisho ya mafanikio ya kidunia na kupuuzia mafanikio ya kimbinguni..

Hizo zote ni INJILI nyingine zisizoweza kumwokoa mwanadamu, na zinatumia jina la “yesu” mwingine linalofanana na BWANA YESU KRISTO kuwatumainisha watu wajione kuwa wapo salama kumbe Kristo hawatambui!, Kinachowatambulisha kwamba wao sio WA-KRISTO ni matunda yanaonekana ndani ya maisha ya watu wanaowahubiria.

Ndugu shetani ni wa HILA tangu mwanzo, alimdanganya ADAMU na kufanikiwa. hashindwi kutundanganya sisi na kufanikiwa kama hatutathamini roho zetu. Tusijipe matumaini ya bure kwamba tumeokoka na huku maisha yetu hayauhakisi wokovu. Ukristo halisi sio rahisi kuupata kama vile kitu original kisivyo rahisi kukipata, Ukristo wa YESU KRISTO MWOKOZI wa ulimwengu una gharama zake.

Ikiwa umekubali kweli ayaokoe maisha yako dhamiria kweli kweli kutoka moyoni, kwamba upo tayari kumwishia yeye, kwa gharama zozote zile atakazokuambia, na yeye akishaona hiyo nia yako na utayari wako basi moja kwa moja ATAKUPA UWEZO WA KUFANYIKA MTOTO WA MUNGU (Yohana 1:12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;).

Sasa UWEZO huo wa kufanyika mtoto wa Mungu hauji kwa kila mtu tu ambaye anasema kampokea YESU bure bure, hapana bali unakuja kwa wale tu! waliodhamiria kwa dhati ndani ya mioyo yao kuanzia huo wakati na kwendelea kumwishia BWANA kwa gharama zozote zile, hapo ndipo yule Roho Mtakatifu sasa anaushusha huo uwezo, na hapo ndipo utakapoweza kuishinda dhambi na kudumu katika Imani ya YESU KRISTO BWANA wetu.

Ni maombi yangu kuwa ikiwa tunatamani kweli tuponywe roho zetu, basi tumtafute YESU HALISI, bila kukwepa vigezo vyote vitakavyoambatana na kumfuata yeye. Vinginevyo tutajikuta tumeangukia katika matumaini ya uongo ya manabii na watumishi wengi wa uongo ambao hawana huruma na hatma ya maisha ya mtu bali mambo ya ulimwengu huu tu, na katika siku ile tukajikuta tunaanza kumwambia Bwana mbona nilinena kwa lugha?, mbona niliongozwa sala ya toba?, mbona nilibatizwa? mbona nilikuona wewe kwenye maono? Na yeye atakwambia “Sikukujua kamwe; ondoka kwangu, wewe utendaye maovu”!!.

Ni hali gani utajisikia siku hiyo ukingundua kuwa ulimpokea yesu mwingine ambaye siye yeye HALISI?. Hizi ni nyakati za mwisho za HATARI mtafute YESU KRISTO wa kwenye Biblia, ambaye hasa lengo lake la kwanza ni kuigeuza roho yako kukupa uzima wa milele, na si kitu kingine.SIMAMA IMARA! BWANA ATAKUIMARISHA.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.

UTHABITI WA AGANO LA MUNGU KWA MKRISTO.

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO

BWANA ALIPOSEMA “SIKUJA KUTANGUA TORATI BALI KUITIMILIZA” ALIKUWA ANAMAANISHA NINI?

KATIKA 1YOHANA 5:6-9, (A) NI KWA NAMNA GANI YESU ALIKUJA KWA MAJI NA DAMU?


Rudi Nyumbani

Print this post

MAISHA YETU NI MILKI YA YESU KRISTO.

Kanisa linafananishwa na mwanamke, Bwana ndio kapenda kulifananisha kanisa lake na mwanamke, akifunua kwamba kama vile mwanaume ampendavyo mkewe ndivyo Kristo anavyolipenda kanisa lake. Na kama ijulikanavyo huwa kuna hatua zinafuatwa kabla ya mwanamume kumtwaa mwanamke awe mkewe, na moja ya hatua muhimu sana inakuwa ni MAHARI. Mahari kazi yake ni kumwongezea ujasiri mwanamume kwamba hakumpata mke wake kirahisi, amemgharimia. Na baada ya kulipa mahari ,ni ndoa kufungwa,hapo Yule mwanamke anahama kwao na kuhamia kwa mume wake, na zaidi ya yote jina lake la ukoo linabadilika, Jina la ukoo linabadilika kuonyesha kwamba kuanzia huo wakati na kuendelea yeye sio milki ya ukoo wa wazazi wake tena, bali anakuwa milki ya ukoo mwingine wa mume wake.

Sasa Bwana aliruhusu huo utamaduni uendelee kuwepo mpaka leo katikati ya wanadamu, ili kuufanya wokovu ueleweke kirahisi kwetu, kwa kulinganisha namna mwanamke anavyotwaliwa kutoka kwa wazazi wake, mpaka anapotolewa mahari, mpaka anapokuwa mke halali wa mwanaume tutapata picha namna kanisa la Kristo navyo lilivyotawaliwa kutoka katika dunia.

Hatua ya kwanza Kristo anawahubiria watu wake watoke katika ulimwengu kwa ishara na miujiza mingi, kama vile mwanamume amshawishivyo mwanamke katika hatua za awali, kisha baada ya hapo Bwana Yesu ni kulipia mahari, na Mahari anayolipa ni damu yake aliyoimwaga pale Golgotha ambapo alitoa nafsi yake kama fidia kwa mkewe (YAANI KANISA), Gharama hii aliyoingia ilimfanya yeye awe na uhalali wa kulimiliki kanisa asilimia 100%.

Na hatua ya mwisho ni mtu kubadilishwa jina na kupewa jina jipya la mumewe, kama vile jina la mwanamke la ukoo linavyobadilika na kuhamia moja kwa moja kwa mumewe. Sasa mwanamke au mwanamume asipopitia hatua zote hizo ndoa yake inakuwa sio halali.

Sasa mimi na wewe, ili kwamba tuweze kuwa wake halali wa Bwana wetu Yesu Kristo, sharti ni lazima tukubali kumwamini na kumgeukia yeye na kuacha wazazi wetu waliotuzaa, yaani kuuacha ulimwengu na mambo yake yote, sharti lazima tumtii kwa kutubu na kumaanisha kabisa kuacha dhambi na maisha ya nyuma ya anasa na kufanyika viumbe vipya.

Kisha hatua inayofuata baada ya kumkubali Yesu moyoni mwetu, Ni Bwana Yesu mwenyewe kutusafisha kwa maji na kwa damu kwa gharama aliyoingia pale Golgotha, Na ndio maana pale Golgotha wale askari wa kirumi walipomchoma mkuki ubavuni, kulitoka maji na damu, ambayo ile ni kama ishara ya mahari kwetu, kwamba tunasafishwa kwa maji na damu.

1 Yohana 5: 6 Huyu ndiye aliyekuja KWA MAJI NA DAMU, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu. Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli”.

Hatua hii inamfanya mtu kuwa mke halali aliyetwaliwa kwa gharama, Bwana anakusafisha dhambi zako zote, na kukuweka kuwa huru na dhambi. Na Neno lake ndio maji yanayotusafisha na Neno lake linasema…

Matendo 2: 37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Unaona hapo? namna mke halali wa Yesu Kristo anavyoandaliwa?…sio kwa kujiunga na dhehebu au kanisa bali ni kwa KUTUBU, Na KUBATIZWA KATIKA JINA LA YESU KRISTO, na kupokea kipawa cha Roho. Na kuanzia huo wakati jina lako linabadilika, na kuitwa Mkristo au wa-Yesu Kristo. Kwasababu umebatizwa kwa hilo jina, na Huwezi kuwa mkristo kama hujapitia hizo hatua.

Huwezi kuitwa wa Yesu Kristo kama haujabatizwa kwa hilo jina, sehemu zote kwenye maandiko watakatifu walibatizwa kwa hilo jina, yaani jina la Yesu, ukisoma mistari ifuatayo utaona jambo hilo {Matendo 2:38. Matendo 8:12, Matendo 8:16, Matendo 10:48 na Matendo 19:5}

Kwahiyo kama tu mwanamke aliyeolewa,anakuwa hawezi kujiamulia tu mambo, kwamba anaweza akalala popote atakapo, au akafanya chochote atakacho juu ya mwili wake, bali anakuwa ameingia kama kwenye kifungo Fulani, ambacho hakimpi uhuru wa kuwa na mahusiano ya karibu na kila mtu. Vivyo hivyo na kwa mkristo aliyempa Bwana maisha yake kwa kutubu na, na kubatizwa kwa jina lake Yesu Kristo, anakuwa ni milki halali ya Yesu Kristo, hana ruhusa ya kujiamulia mambo tu, au kufanya chochote anachojisikia akiwa katikati ya mahusiano yake yeye na Bwana.. Na ndio maana Biblia inasema katika

1 Wakoritho 6: 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE;

20 maana MLINUNULIWA KWA THAMANI. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.

Unaona hapo, biblia inasema “SISI SI MALI YETU WENYEWE” ikiwa na maana kwamba ni “sisi tuliozaliwa mara ya pili ni milki ya mtu mwingine” na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO, hivyo hatuwezi kujiamulia chochote katika miili yetu, au katika aina ya maisha tunayotaka tuishi, Kwasababu yeye (Yesu Kristo) alitununua kwa thamani, nyingi maandiko yanasema hivyo.

Kwahiyo Bwana anao uhalali wa kutufanya chochote endapo tukijihusisha na mambo yoyote katika maisha yetu au katika miili yetu yatakayomtia wivu, au kumuudhi au kumhuzunisha. Kama biblia inavyosema katika..

1 Wakoritho 3: 16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

17 KAMA MTU AKILIHARIBU HEKALU LA MUNGU, MUNGU ATAMHARIBU MTU HUYO. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi”.

Sasa tukiliharibu hekalu la Mungu yaani miili yetu, Bwana naye atatuharibu, kwahiyo tunapokuwa wakristo sio suala la kujichagulia maisha hapana ni suala la kuchaguliwa maisha na yeye aliyetutolea mahari sisi, Wivu wa Bwana unakuwa kwa wale aliwatolea mahari yaani wale aliowasafisha dhambi zao kwa damu yake, Maovu makubwa yanayomchukiza sio ya watu waliomkataa, hapana bali ni yale ya watu walio wake na bado wanafanya dhambi,(wanakuwa vuguvugu) katika maisha ya kawaida hakuna mwanamume yeyote aonaye wivu akiona mwanamke mwingine asiye wake anafanya uasherati, lakini ataona wivu zaidi endapo akimwona mke wake aliyemtolea mahari na kumwoa anamsaliti na kufanya uasherati. Na ndio maana Bwana baada ya kuwatoa wana wa Israeli Misri aliwapatia amri 10 wao tu! Hakuwapa zile amri kumi watu wote wa ulimwengu mzima, au watu wa Misri. Kwanini? Ni kwasababu Misri hakuwa mke wake halali bali Israeli.

Dada/kaka unayesoma ujumbe huu, kama kweli umeamua kumfuata Bwana na umepita hizo hatua tatu, yaani KUTUBU, na KUBATIZWA KATIKA JINA LA YESU na kupokea ROHO MTAKATIFU. Na bado unajiamulia maisha, nakushauri usifanye hivyo tena, badilisha mtazamo wako, usiwe kama mwanamke mpumbavu aliyeingia kwenye ndoa na asijue mikataba na makubaliano ya hiyo ndoa, kama umeamua kuwa mkristo mwili wako ni hekalu ya Roho Mtakatifu, usilichore tattoo, usifanye uasherati, usiunyweshe pombe, wala usiuvutishe sigara, usiuvalishe nusu uchi, wala usiuvalishe mavazi yasilolipasa ya jinsia nyingine, wala usiufanye mwili usiwe katika hali yake ya asili. Kwasababu mwili huo sio milki yako mwenyewe ni Milki ya mtu mwingine ambaye anaweza kukufanya lolote endapo ukiuharibu na hautapata mtetezi.

Zipo faida leo ukidumu katika uaminifu wako kama bibi-arusi wa Kristo, asiye na hila wala mawaa, kwasababu biblia kama inavyosema katika mbingu mpya na nchi mpya Uje mji mtakatifu wa Mungu yaani YERUSALEMU mpya ushukao kutoka mbinguni ndio bibi-arusi wa Kristo(Ufunuo 21), Mungu atakaa ndani yake, Na katika huo (ambao ndio sisi) Mungu ndio atafanya maskani kumbuka hatafanya maskani kwa kila mtu tu atakayekuwepo huko hapana, bali kwa bibi-arusi tu.. Hivyo tukaze mwendo kama bibi-arusi wa kweli wa Kristo.

Ubarikiwe.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine, na Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

UNAFANYA NINI HAPO?

BWANA ALIMAANISHA NINI KWENYE MSTARI HUU MARKO 2:21″ HAKUNA MTU ASHONAYE KIRAKA CHA NGUO MPYA KATIKA VAZI KUKUU;?

ULE MFANO WA WANAWALI 10 (MATHAYO 25), WALE WATANO HAWAKUWA NA MAFUTA YA ZIADA KATIKA CHUPA ZAO JE YALE MAFUTA YA ZIADA YANAWAKILISHA NINI?


Rudi Nyumbani

Print this post

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Bwana Mungu wetu kaumba vitu vyote vya mwilini, kufunua vitu vya rohoni, aliumba milima, kufundisha kuwa kuna milima ya rohoni, aliumba maji kuonyesha kwamba kuna maji ya rohoni, aliruhusu mauti iwepo kufunua kwamba kuna mauti ya kiroho,aliruhusu vyakula viwepo ili kufunua kwamba kuna vyakula vya rohoni, kwasababu mwanadamu ameumbwa katika pande mbili, rohoni na mwilini. Na ndio maana alisema kwenye Neno lake Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu (Mathayo 4:4)”.

Hivyo kama kuna mauti ya mwilini, ni wazi kuwa ipo pia mauti ya rohoni. Na kama vile, mauti ya mwilini ilivyo na nguvu leo, kiasi kwamba kila nafsi lazime ipitie, vivyo hivyo mauti ya rohoni ina nguvu ile ile ambayo inalazimisha kila kiumbe kife kwa namna ya roho. Na hii mauti ya rohoni iliingia pale Edeni, Adamu na Hawa walipoasi. Na kama tunavyojua leo hii hakuna dawa ya kifo cha mwilini, Kifo ni kifo tu! Vivyo hivyo na dawa ya Kifo cha rohoni haikuwepo mpaka njia ya mti wa uzima YESU KRISTO ALIPOFUNULIWA. Ndio tiba ya kifo ikapatikana vinginevyo hakungekuwa na uzima wa milele kwa kiumbe chochote kile.

Kwahiyo mara nyingi Bwana anapenda kutufundisha kwa kutumia mifano ya mwilini, kufunua vitu vya rohoni, kwamfano tunamwona yule mwanamke msamaria siku moja alipokwenda kisimani kuteka maji akakutana na Bwana, na Bwana akamwomba maji, na yule mwanamke alipotaka kuanza maandalizi ya kumpatia maji kutoka katika kisima kile, kwa kumuuliza baadhi ya maswali,Bwana alimkatisha palepale na kumwambia… “ kama ungaliijua KARAMA YA MUNGU, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, UNGALIMWOMBA YEYE, NAYE ANGALIKUPA MAJI YALIYO HAI (Yohana 4:10)”

Na palepale yule mwanamke alidhani Bwana anazungumzia habari za maji yale ya mwilini ya kwenye kwenye visima, akafurahi akatamani apewe yale maji. Tunaweza kuona mistari hiyo tuone jambo..

“11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai.

12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?

13 YESU AKAJIBU, AKAMWAMBIA, KILA ANYWAYE MAJI HAYA ATAONA KIU TENA;

14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi HATAONA KIU MILELE; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, YAKIBUBUJIKIA UZIMA WA MILELE.

15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka”

Unaona hapo, Bwana anazidi kumtoa yule mwanamke Msamaria kwenye mawazo ya maji ya mwilini na kumpeleka kwenye mawazo ya maji ya rohoni, lakini bado alikuwa hajamwelewa. Alijaribu kutumia mfano wa maji ya mwilini ili kumwonyesha umuhimu wa maji ya rohoni lakini bado hakumwelewa vizuri mpaka baadaye kidogo. Alijaribu kumfunulia KARAMA YA MUNGU lakini bado ilimuwia ngumu kumuelewa kwa wakati ule kwasababu ya mapokeo ya kibinadamu aliyokuwa nayo. Bwana alichotaka kwa yule mwanamke ni KUTUBU, NA KUACHA DHAMBI ALIZOKUWA ANAZIFANYA, NA KUMGEUKIA MUNGU kwa moyo wake wote! Na kuishi maisha mapya yanayompendeza Mungu Hicho tu! ndio Bwana alichokuwa anatafuta kwa yule mwanamke. Hiyo ndiyo KARAMA YA MUNGU aliyokuwa anataka kumpa yule mwanamke…ili asife kwa kukosa maji ya uzima akaukosa uzima wa milele..Na ndio maana biblia inasema katika..

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; BALI KARAMA YA MUNGU ni UZIMA WA MILELE katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Na baada ya Bwana kumfunulia siri ya moyo wake kwamba anao waume watano na yule aliyenaye sasa si wake, ndipo alipotambua kwamba yeye ni mwenye dhambi, na kwamba Bwana alikuwa hazungumzii maji ya mwilini bali ya roho yake, yatakayompa uzima wa milele.

Tunaweza tukajifunza tena mfano mwingine katika maandiko wa Mtu aliyeielewa haraka KARAMA YA MUNGU pasipo Bwana kutumia nguvu nyingi kumfafanulia, na huyu si mwingine zaidi ya Petro. Wakati Fulani Bwana alimwendea Petro kwa mara ya kwanza kama alivyomwendea yule mwanamke Msamaria, akamkuta anaosha nyavu, kwasababu wamefanya kazi ya kuchosha usiku mzima bila kupata kitu, Na Petro alipomwona Bwana alidhani ni muhubiri tu wa kawaida, mwalimu wa torati kama walimu wengine, hivyo kwa heshima yake akaona bora amtii tu, Tunasoma hayo katika..

Luka 5: 4 “Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.

5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.

6 Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika;

7 wakawapungia mikono washirika wao waliokuwa katika chombo cha pili, waje kuwasaidia; wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili, hata vikataka kuzama.

8 Simoni Petro alipoona hayo, alianguka magotini pa Yesu, akisema, ONDOKA KWANGU, KWA KUWA MIMI NI MTU MWENYE DHAMBI, BWANA.

9 Maana alishikwa na ushangao, yeye na wote waliokuwa pamoja naye, kwa sababu ya wingi wa samaki walioupata”;

Unaweza ukaona hapo, Petro baada ya kuiona ile ishara ya kupata samaki wengi namna ile, akatambua KARAMA YA MUNGU nyuma ya ile ishara, akatambua kuwa mtu aliyesimama mbele yake ni MKUU WA UZIMA, na yeye ni mtakatifu na hachangamani na uchafu, akaogopa akamwangukia chini akamwambia “ONDOKA KWANGU, KWA KUWA MIMI NI MTU MWENYE DHAMBI, BWANA” alitambua Bwana Yesu hakuja kumpa yeye VIKAPU VYA SAMAKI, hakumfanyia ile ishara ili kumfanya yeye kuwa milionea, bali aliifanya ile ishara ili kumwonyesha Petro kwamba yeye ni mwenye dhambi kiasi gani na kwamba anahitaji UZIMA WA MILELE. Bwana hakumfanyia ile ishara Petro kwasababu anavutiwa sana na ile kazi aliyokuwa anaifanya ya kuvua samaki, hapana alimfanyia Petro ile ishara kwasababu aliona dhambi ndani ya Petro na hakutaka Petro apotee, Na Petro alilitambua hilo akatubu mbele zake.

Na jambo hili hili linaendelea leo, Bwana Yesu anakutembelea kwenye mambo yako unayoyafanya, labda shughuli Fulani ya kujipatia kipato, au labda elimu, au mali, au afya…Inatokea umepitia au ulipitia hali Fulani ulikuwa unaugua sana na Bwana akakuponya kimiujiza, na ndani ya moyo wako ukashuhudiwa kuwa ungestahili kufa lakini umepona… Sasa huu si wakati wa kuanza kutazama mambo ya mwilini, kwamba sasa umepata afya ndio wakati wa kusaka fedha kwa nguvu uwe tajiri kwasababu Mungu kakunyanyua tena, au ukadhani kwamba Bwana alikuponya kwasababu alikuhurumia sana ulipokuwa unateseka na maumivu ya magonjwa yako,

Nataka nikwambie ndugu Bwana hakukuhurumia kwasababu ulikuwa unateseka na maumivu ya ugonjwa bali alikuhurumia akakuponya kwasababu alikuhurumia usije ukafa na dhambi ulizo nazo ndani yako na ukaingia kwenye lile ziwa la moto hivyo ni muhimu sana kuielewa KARAMA YA MUNGU juu maisha yako? Bwana alikuponya kimiujiza ili UKATUBU, ukaache uasherati, ukaache anasa, ukaache usengenyaji, ukaaache rushwa,ukaache kuishi na mume au mke ambaye hamjafunga ndoa, ukaache kuiba, ukaache pombe, alikuponya magonjwa ya zinaa ili ukaache uasherati na uzinzi n.k

Bwana hakukufanikisha kwenye kazi yako ya kujipatia kipato, kwasababu anataka sadaka au fungu la kumi kutoka kwako, au kwasababu alikuhurumia sana ulikuwa maskini kwa muda mrefu na ulikuwa unateseka hapana!! Bwana alikufanikisha kwenye shughuli zako kwasababu anaona maisha yako kuna sehemu pengine hayajakamilika mbele zake, anakufanyia ishara kubwa namna hiyo kama alivyomfanyia Petro, anataka UANGUKE CHINI utambue kwamba, Jicho la Mungu linakutazama kuliko unavyodhani, mambo yako na dhambi zako za siri anayoana kuliko unavyofikiri, ziko wazi mbele zake, anataka uone kwamba MTAKATIFU WA WATAKATIFU AMEKUSOGELEA, Anataka uone kwamba hatua moja mbele yako kasimama mtu asiyechangamana na dhambi. Na anataka akupatie uzima wa milele!

Biblia inasema mtu asipozaliwa mara ya pili hawezi kuuona ufalme wa mbinguni, (Yohana 3:3). HIYO NDIYO KARAMA YA MUNGU KWAKO.

Bwana Azidi kukubariki sana, Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KARAMA ILIYO KUU.

MOYO ULIOELEKEA KWA MUNGU.

MTUME PAULO ALIKUWA NA MAANA GANI KUSEMA NIKAKUFA KILA SIKU??

MBONA MUNGU ANARUHUSU WATU WAPATE SHIDA, ILHALI ANA UWEZO WA KUTUEPUSHA?


Rudi Nyumbani

Print this post

UMEPATA UHAKIKA WA KUTOKUINGIA HUKUMUNI KATIKA SIKU ILE?

Jaribu kufikiria dikteta Adolf Hitler wa ujerumani Yule aliyesababisha vita ya pili ya dunia, na kuhusika kwa mauaji ya mamilioni ya raia wasiokuwa na hatia ulimwenguni kote, mfano leo hii angekuwa hai, unadhani hatma ya maisha yake ingekuwa ni nini?, watu wa ulimwengu mzima wangetaka Yule mtu apewe adhabu gani?, Ni wazi kuwa kila mtu angetoa maoni ya adhabu yake ya kipekee ya mateso yasiyokuwa ya kawaida ambayo walau yangeweza kulipiza kisasi cha yale mabaya yote aliyowafanyia watu wasiokuwa na hatia, wale watu aliowachoma katika matanuru ya gesi na kuwaua kwa vifo vya kikatili na mateso na kusababisha vita ya pili ya dunia. Yeye naye angepewa adhabu mojawapo ya hizo watu wangeridhika kumuona analipa deni la alichokipanda.

Lakini pia jaribu kufikiria mfano amekamatwa na kwenda kuhifadhiwa mahali Fulani pa siri, kisha ukasikia baada ya siku chache kaachiwa huru, sasa ni raia wa kawaida kama raia mwingine ambaye hajafanya kosa lolote, na cha kushangaza zaidi sio tu kutokupewa adhabu yoyote bali hata MAHAKAMANI penyewe mahali ambapo ni pa haki hajapandishwa kushitakiwa. Badala yake kaachiwa yupo huru na anaendelea na maisha yake ya kawaida…

Kwa namna ya kawaida hilo ni jambo lisilokaa liwezekane, lakini kwa Mungu limewezekana..

Bwana Yesu anasema.. Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; WALA HAINGII HUKUMUNI, BALI AMEPITA KUTOKA MAUTINI KUINGIA UZIMANI”.

Ndugu yangu mimi na wewe nafsi zetu zinatushuhudia kabisa sio wakamilifu kwa asilimia zote, na kama sio wakamilifu mbele za Mungu amri ni moja tu, ni lazima tukahukumiwe adhabu kwa kutokukamilika mbele zake, Na biblia ipo wazi juu ya hilo, Lakini ashukuruwe Kristo alisema amwaminiye yeye, yuna uzima wa milele, WALA HAINGII HUKUMUNI, BALI AMEPITA KUTOKA MAUTINI KUINGIA UZIMANI.

Ikiwa na maana kuwa siku ile Kristo atakaposimama kuyahukumu mataifa yote ulimwenguni katika kile kiti chake cheupe cha enzi wale wote waliomwamini yeye hawatakuwepo hapo, badala yake wao ndio watakaosimama na Kristo kuyahukumu mataifa yote.Tunasoma..

Ufunuo 20.11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.

12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.

13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.

15 Na iwapon mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.

Unaona hapo? Leo hii wewe ni mlevi,mtazamaji wa pornography, mfanyaji wa mustarbation, msengenyaji, mwizi, mzinzi, maisha yako hayana matumaini, unaishi kwa hofu, kila siku unahisi kuhukumiwa ndani ya nafsi yako, kuwa njia unayoiendea ni ya mauti, na unafahamu kabisa kuwa hata ukifa leo utahukumiwa tu na kwenda katika ziwa la moto, kwanini unaendelea kuyahatarisha maisha yako, kwa kuishi maisha ya namna hiyo ya kutokujali?, kwanini unaipuuzia neema hii ya kipekee ya kuvukishwa toka mautini mpaka uzimani? Neema ya kutokuingizwa hukumuni? Bwana anasema NJOO! KWANGU unywe maji ukate hiyo kiu..Lakini bado upo vuguvugu, unadhani kwa matendo yako utaweza kusimama mbele zake siku ile? hii neema haitadumu milele..Ni neema ambayo mwanadamu yoyote asingestahili kupewa.

Ni maombi yangu, tusitamani KUSIMAMA MBELE YA KITI CHEUPE CHA HUKUMU CHA MUNGU siku ile kwasababu tukishajikuta tu tumesimama pale, habari yetu imekwisha hatutakuwa na cha kujitetea, kwa njia yoyote makosa ni lazima tu yaonekana ndani yetu. Na baada ya hapo ni safari ya moja kwa moja kwenda katika lile ziwa la moto.

Tuipishe hukumu ya Mungu hakuna anayependa kupandishwa mahakamani hata  katika mahakama za kibinadamu tu hakuna anayenda kufikishwa kule, itakuwaje siku ile kukutana uso kwa uso wa Mungu mwenyewe katika mahakama? Ni jambo la kutisha sana, tusitamani tuwepo.

Tubu sasa maadamu muda upo, salimisha maisha yako kwa Kristo leo, kesho haipo, kabatizwe katika ubatizo sahihi baada ya kuamini kwako kama haujafanya hivyo haraka iwezekanavyo ili upate ondoleo la dhambi zako, na ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa kwenye maji mengi na uwe ni kwa jina la YESU KRISTO ubatizo mwingine nje ya huo ni batili, Kisha Bwana atakupa Roho wake mtakatifu na hapo utakuwa UMESHAZALIWA MARA YA PILI..Na kama hizo hatua hazijakamilika ndani yako, hapo bado hujazaliwa mara ya pili. Bado hujavuka toka mautini kwenda uzimani, bado hujaikwepa hukumu…

Fanya bidii kumtafuta YESU siku hizi ni za hatari.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu, 

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!

UPUMBAVU WA MUNGU.

JE! NI HALALI KWA MTU WA MUNGU KUTUMIA NJIA ZA UZAZI WA MPANGO?

JE! NI DHAMBI KWA MKRISTO KWENDA HOSPITALI AU KUTUMIA MITI SHAMBA ANAPOUGUA?


Rudi Nyumbani

Print this post

MTETEZI WAKO NI NANI?

Mwinjilisti mmoja maarufu wa Marekani aliyeitwa Danny Martin, katika jitihada zake nyingi za kumtumikia Mungu siku moja usiku alijiona kwenye ndoto kwamba amekufa,na huko upande wa pili alijikuta yupo safarini kuelekea mbinguni, kwa mbali aliyaona malango makubwa sana, lakini alipokaribia mahali pale alisikia mtu mmoja akimwambia “Ni nani huyu anakaribia hapa?” Kwa ujasiri akajibu ni “mimi Martin Muhubiri wa Injili” lakini wale watu wakamwambia kabla hujaingia ndani subiri kwanza hapo mlangoni tuliangalie jina lako kama lipo kwenye KITABU au la!

Hivyo walipoangalia na kulikosa wakasema “Jina lako halimo huku”…Lakini Danny akasema “Haiwezekani jina langu kukosekana humo mimi ni mtumishi wa Mungu” wale watu wakamwambia hiyo haijalishi ulikuwa nani duniani ukishafika hapa kama jina lako halipo huku, hatuna cha kukusaidia huwezi kuingia ndani ya malango haya ya mbinguni.

Ndipo Danny akawaomba wale watu wamsaidie afanye nini? Lakini wale watu wakamwambia sisi hatuwezi kukusaidia labda kama unataka kukata rufaa kwa Mungu mwenyewe katika kile KITI CHAKE CHEUPE CHA ENZI . 

Ndipo Danny akasema sina namna inanipasa nifanye hivyo. Basi wakamruhusu kuelekea mahali kilipo kiti cheupe cha Enzi cha Mungu, juu sana. (Anaeleza Danny) kwa jinsi nilivyokuwa ninazidi kuelekea juu ndivyo mwanga mkali ulivyokuwa unazidi sana, nilikuwa ninakwenda kwa haraka lakini ilinibidi nipunguze mwendo na baada ya muda kidogo nikasimama kabisa. Ndipo nikasikia sauti ikisema ni nani huyu anayekikaribia kiti changu cha hukumu cha haki?..Ndipo nikasema ni mimi Danny, mwinjilisti wa Kimarekani niliyevuna roho nyingi sana za watu kwako, lakini nilipofika getini wale walinzi walinizuia nisiingie.

Ndipo ile sauti ikamwambia “Vema mimi ninapenda haki”..”Mimi ninazo AMRI”..Je! Danny katika maisha yako yote hujawahi kusema uongo? . Danny anaelezea akisema “nilidhani mimi nimekuwa mtu mwaminifu siku zote lakini nilipofika mbele ya ule uwepo wa ajabu wa Mungu nilijiona kuwa kumbe sikuwa hivyo”..Ndipo nikasema …”Hapana Bwana nimekuwa nikisema uongo”…Akaniuliza tena…Danny ulishawahi kuiba?…Danny anasema: hapo nyuma nilidhani kuwa mimi ni mwaminifu sana lakini mbele zake siku hiyo niliona mapungufu mengi sana ndani yangu..Ndipo nikamwambia “Ndio Bwana nilishawahi kuiba”…

Akaniuliza tena, Danny ulishawahi kutenda dhambi?..Nikamjibu Ndio Bwana..

Akaniuliza..ulishawahi kufanya hivi, ulishawahi kufanya vile?…..Nikasema Ndio Bwana nilishafanya..

Danny anazidi kuelezea ( wakati huo nilisikia kama mifupa yangu inachomoka kwenye maungio yangu, nikitazamia tu kusikia lile neno Bwana alilolisema katika Mathayo 25: Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;))..

Lakini muda huo wakati nayatazamia hayo yafuate nyuma yangu nilisikia sauti nzuri ya unyenyekevu na ya kupendeza,ikizungumza na nilipogeuka nikaona sura nzuri ya tabasamu ambayo sikuwahi kuiona hapo kabla katika maisha yangu..Akasema:

Baba ni kweli Danny kwa bidii zake alijitahidi kufanya kilicho kizuri japo alishindwa, lakini kipo alichokifanya alipokuwa duniani, yeye alitia juhudi zote kusimama kwa ajili yangu Hivyo mimi nami nipo hapa kusimama kwa ajili yake.

Ndugu yangu Je! Bwana hakusema? Katika Luka 9: 9.23 Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

24 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.

25 Kwa kuwa yamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, kama akijiangamiza, au kujipoteza mwenyewe?

26 KWA SABABU KILA ATAKAYENIONEA “HAYA” MIMI NA MANENO YANGU, MWANA WA ADAMU ATAMWONEA HAYA MTU HUYO, ATAKAPOKUJA KATIKA UTUKUFU WAKE NA WA BABA NA WA MALAIKA WATAKATIFU.

Ipo siku ambayo Bwana atatukiri mbele za Baba yake, pia ipo siku ambayo Bwana atatukana mbele za Mungu.

Leo hii tunamwoneaje Kristo HAYA?. Ni pale tunapokataa kujikana nafsi zetu kwa Kristo kila siku, pale tunapoambiwa tutubu tukaoshwe dhambi zetu sasa wakati muda angali bado upo lakini sisi tunaona kama siku tukiwa hivyo watu watatuona kama washamba, pale unapoona siku ukiwa mkristo, pombe hutakunywa tena, pale unapoona siku ukiwa mkristo disco hutakwenda tena, unapoona siku ukiwa mkristo uasherati hutafanya tena, pale unapoona siku ukiwa mkristo kampani zako mbovu hutaongozana nazo tena, unakataa kufanya hivyo sasa kwasababu unaupenda ulimwengu kuliko Mungu…Hapo ni sawa na kumwonea HAYA Kristo na maneno yake. Biblia inasema katika

1 Yohana 2 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.”

Ndugu kama ukifa leo hii utaenda kuwa mgeni wa nani huko? Ni nani atakayesimama huko kukutetea mbele ya kile kiti cheupe cha hukumu cha Mungu?. Bwana anasema KWA SABABU KILA ATAKAYENIONEA “HAYA” MIMI NA MANENO YANGU, MWANA WA ADAMU ATAMWONEA HAYA MTU HUYO, ATAKAPOKUJA KATIKA UTUKUFU WAKE NA WA BABA NA WA MALAIKA WATAKATIFU.

Unakataa kuchukua msalaba wako sasa umfuate Kristo, kwasababu unajua ukristo hauhitaji mwanamke anayevaa nguo zinazochora maungo, na suruali, unajua mwanamke wa kikristo havai mapambo ya kikahaba na kiasherati, unaogopa utaonekana wa kale, hivyo unaona ni bora uwe vuguvugu, huko ni kumwonea HAYA KRISTO. Ni kweli leo utafanikiwa kukwepa hayo kwa kitambo sasa lakini siku ile ambayo utasimama kwa nafsi yako, mahali ambapo utahitaji mtetezi utakosa, utagundua kuwa ulivyoipenda nafsi yako wakati ulipokuwa duniani ndivyo ulivyokuwa unaipoteza, na siku hiyo ndiyo utagundua kuwa Bwana hakudanganya alivyosema “”Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.

Ndugu yangu maisha haya yanapita, unatafuta mali kupita kiasi unamsahau Mungu muumba wako, unapendezwa na mambo ya ulimwenguni hata muda na Mungu wako huna, kuna siku itafika utamuhitaji sana Kristo awe mtetezi wako lakini yeye atasimama kando asikujibu lolote kwasababu hataona la kukujibu, Badala yake atakukana na kusema sikujui wewe. Utajisikiaje siku hiyo?, mbele ya mahakama ya haki ya Mungu?

Hizi ni nyakati za hatari biblia ilizozisema, ni heri ujisalimishe kwake, kwa hii miaka sabini themanini uliyopewa hapa duniani kuliko ukawe na majuto ya milele baada ya kufa. Isikie sauti ya YESU KRISTO leo na usiyaonee haya maneno yake. Anza maisha yako upya uchukue msalaba wako sasa umfuate, uwe radhi kuipoteza nafsi yako kwa ajili yake ili uwe na uhakika siku zinazokuja kwamba utaipata kuliko kuipata sasa kwa anasa na raha za kitambo za dunia kisha siku ile uipoteze milele.

Tubu dhambi zako muda huu, na ikiwa bado hujabatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele katika JINA LA YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako,(kulingana na matendo 2:38,8:16, 10:48 na 19:5 na Mathayo 28:19) fanya bidii ufanye hivyo, naye Mungu aliyemwaminifu atakugawia kipawa cha Roho Mtakatifu. Ili uwe na uhakika wa kuzaliwa mara ya pili.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali wape ujumbe huu na wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE

LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI

BWANA YESU ALIMAANISHA NINI PALE ALIPOSEMA “MKONO WAKO UKIKUKOSESHA UKATE?

TOFAUTI KATIKA YA ZAKA NA SADAKA NI IPI?


Rudi Nyumbani

Print this post

BADO KITAMBO KIDOGO HAMNIONI

Bwana Yesu alisema, ilimpasa yeye aondoke ili Roho Mtakatifu aje, hata hivyo Roho Mtakatifu sio kitu kingine tofauti na Yesu, bali ni yeye yeye Bwana Yesu katika mfumo wa Roho,

Kwamfano Mchawi anapotaka kukiloga kikundi cha watu Fulani au kijiji, hawezi kufanya uchawi wake kwa namna ya kimwili bali atakiendea kijiji kile au watu wale kwa namna ya Roho isiyoweza kuonekana kwa macho na kuleta madhara makubwa sana katika kile kijiji. Atakuwa ana uwezo wa kudhuru watu hata 100 kwa mda mfupi kuliko kuwa katika mwili. Sasa ni Yule Yule mchawi ila anatenda kazi katika namna ya roho.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, ili kwamba ajipatie matokeo makubwa zaidi ilimpasa aondoke katika namna ya kimwili, ili aje tena katika namna ya roho ili alete matokeo makubwa zaidi katika ulimwengu.

Na ndio maana Bwana Yesu kabla ya kuondoka aliwaambia wanafunzi wake, kwamba bado kitambo hawamwoni na tena bado kidogo watamwona tena, akimaanisha kuwa muda mfupi baadaye atakwenda kusulibiwa na atachukuliwa juu mbinguni nao hawatamwona tena, lakini baada ya kusulibiwa na kupaa muda mfupi baadaye watamwona tena (atakuja kwao) kwa namna ya Roho katika siku ile ya Pentekoste..

Tunasoma ;

Yohana 16:12 “Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa.

13 Lakini yeye atakapokuja, HUYO ROHO WA KWELI, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.

15 Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari.

16 BADO KITAMBO KIDOGO NANYI HAMNIONI; NA TENA BADO KITAMBO KIDOGO NANYI MTANIONA.

17 Basi baadhi ya wanafunzi wake wakasemezana, Neno gani hilo asemalo, BADO KITAMBO KIDOGO NANYI HAMNIONI, NA TENA BADO KITAMBO KIDOGO NANYI MTANIONA? NA HILO, KWA SABABU NAENDA ZANGU KWA BABA?

18 Basi walisema, Neno gani hilo asemalo; hilo, Bado kitambo kidogo? Hatujui asemalo.

19 Yesu alifahamu ya kwamba wanataka kumwuliza, akawaambia, Ndilo hilo mnaloulizana, ya kuwa nalisema, BADO KITAMBO KIDOGO NANYI HAMNIONI, NA TENA BADO KITAMBO KIDOGO NANYI MTANIONA?”

Kwahiyo ili Bwana Yesu aweze kuhudumia mamilioni ya watu waliopo duniani asingeweza kubaki katika ile hali ya mwili, ilimpasa aje kwa namna ya Roho, ili aweze kuwaganga moyo wengi waliovunjika moyo, ili aweze kuwafundisha watu wengi wa ulimwengu mzima, ili aweze kuwatembelea majumbani mwao, mtu mmoja mmoja, lakini katika ile hali ya mwili aliyokuwepo ingekuwa ni ngumu, ingechukua mamilioni ya miaka kutimiza kusudi lake, hivyo ilimpasa abadili njia ya kuwafikia wanadamu, kwa sababu hiyo basi akawaambia wanafunzi wake bado kitambo kidogo nanyi hamnioni na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona, na kweli siku ile Bwana Yesu alipoondoka wanafunzi wake walihuzunika sana, wakajihisi kuwa mayatima, wakajifungia ndani kwa hofu ya wayahudi, mioyo yao ilikuwa mizito kwasababu Bwana ameondoka, lakini tunasoma katika siku ile ya Pentekoste Roho Mtakatifu alipowashukia mioyo yao ilihuishwa tena, wakapata ujasiri wa hali ya juu, wakamwona Kristo tena, wakamuhisi wapo karibu naye kuliko hata hapo kabla walipokuwa naye. Walipokea nguvu ya ajabu, Huyo alikuwa ni Yule Yule Kristo katika Roho. Na baada ya hapo ndio tunaona injili ikaenda duniani kote.

Injili ilianza kuenea kwa kasi duniani kote nguvu sana, kwasababu Kristo hatendi kazi tena katika mwili mmoja bali katika Roho, hivyo matokeo yake yanakuwa ni makubwa zaidi, ni Kristo Yule Yule hajabadilika lakini sasa hatumii tena njia ile aliyokuwa anaitumia, bali anatumia njia iliyobora zaidi kuufikishia ulimwengu wokovu.

Ni sawa na mtu aliyekuwa anatangaza biashara yake kwa mabango barabarani kwenye hari za jua kali, lakini baadaye akabadilisha mbinu na kuanza kutumia mitandao kutangaza matangazo yake ili kupata matokeo makubwa zaidi, sasa huyo mtu hajabadilika ni yeye Yule Yule isipokuwa tu amebadilisha njia ya kuwafikia watu. Badala ya yeye kwenda kugonga nyumba moja moja kutangaza biashara yake, ambapo pengine kwa siku angewafikia watu 100 tu! sasa anatumia mitandao ya kijamii ambapo kwa siku anaweza kuwafikia hata watu laki moja na zaidi, pasipo hata yeye kuwepo maeneo yao. Kwa kupitia mitandao anakuwa anatimiza kusudi lile lile kama tu angetumia miguu yake..tena zaidi ya yote anapata matokeo bora zaidi.

Kadhalika Bwana Yesu alisema.. “Walipo wawili au watatu wamekusanyika kwa jina langu, MIMI NIPO PAPO HAPO KATIKATI YAO”

Unaona hapo? Hayupo kwa namna ya kimwili lakini yupo kwa namna ya Roho, kwahiyo kama wakikusanyika wawili au watatu kwa jina lake, hasemi uongo ni kweli yupo katakati yao, sawa tu na kama angekuwepo kwa namna ya kimwili.

Kaka/ Dada unayesoma ujumbe huu, ni muhimu kujua kwamba Kristo yupo leo anatembea ulimwenguni, anafanya kazi zile zile, isipokuwa tu haonekani kwa macho, ni Kristo Yule Yule aliyekuwa anatembea na wakina Petro, ni Yule Yule aliyekuwa anagonga kwenye jumba za watu, na kwenye miji ili aingie aihubiri injili. Na wale waliomkubali aliwapa uzima wa Milele na wale waliomkataa aliwaacha na kwenda kwa wengine, Na leo ndio Yule Yule anagonga katika mioyo ya watu kwa namna ya Roho akitaka aingie ayabadilishe maisha ya watu na kuwaletea wokovu. Aliwaambia wanafunzi wake maneno haya wakati anawatuma kwenda kuhubiri injili…

Luka 10:10 “Na mji wo wote mtakaouingia, NAO HAWAWAKARIBISHI, TOKENI HUMO, nanyi mkipita katika njia zake semeni,

11 HATA MAVUMBI YA MJI WENU YALIYOGANDAMANA NA MIGUU YETU TUNAYAKUNG’UTA JUU YENU. Lakini jueni hili, ya kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia.

12 Nawaambia ya kwamba SIKU ILE ITAKUWA RAHISI ZAIDI SODOMA KUISTAHIMILI ADHABU YAKE KULIKO MJI HUO”.

Umeona ndugu?, hakuna nafasi ya pili kama ukimkataa Kristo kwa makusudi sasa, unapohubiriwa injili yake kwa Roho wake, anaondoka na kwenda kwa mwingine? Na kwako inabakia kuwa hukumu. Biblia inasema waasherati wote, wasengenyaji, walafi, walawiti, walevi,wachafu,watukanaji, wala rushwa, waabudu, sanamu sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti, HAIDANGANYI!! Ni kweli itakuwa hivyo, mtu yeyote anayekuambia kwamba walevi wataokolewa anakudanganya, yeyote anayekuambia kwamba wanaopaka wanja na lipstiki na kuvaa wigi na suruali na herein wataokolewa kwamba Mungu haangalii Roho anaangalia mwili, nataka nikuambia jambo hili moja Roho Mtakatifu anasema sehemu yao itakuwa ni KATIKA LILE ZIWA LA MOTO!!. Anayekuambia kwamba kuwa kuishi na mwanamume au mwanamke ambaye hamjafunga ndoa au ambaye ameachana na mke/mume wake sio dhambi, anakudanganya Yesu Kristo anazungumza na wewe leo kwa namna ya Roho, kwamba “AMWACHAYE MKE WAKE NA KUOA MWINGINE AZINI, NAYE ALIYEMUOA YULE ALIYEACHWA AZINI” Mtii Yesu Kristo leo na maneno yake, Usiusikilize uongo wa shetani ambao baadaye utakufanya ujute milele.

Bwana alisema..UFUNUO 3: 20 “TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI, NABISHA; MTU AKIISIKIA SAUTI YANGU, NA KUUFUNGUA MLANGO, NITAINGIA KWAKE, NAMI NITAKULA PAMOJA NAYE, NA YEYE PAMOJA NAME”.

Tubu leo kama hujafanya hivyo, mpe Bwana maisha yako ayabadilishe, kabla hajaacha kugonga ndani ya moyo wako na kuhamia kwa mwingine, ukishatubu fanya hima ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa Jina la Yesu Kristo, kwa ajili ya ondoleo la dhambi, uwe na uhakika wa wokovu wako na BWANA mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake, ndipo utakapokuwa na uhakika wa kuzaliwa mara ya pili.

Bwana akubariki.

Print this post

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA

Luka 12:35 “VIUNO VYENU na viwe vimefungwa, na TAA ZENU ziwe zinawaka;

36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia.

38 Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao.”

Tunaweza kujiuliza ni Kwanini ni VIUNO na ni kwanini ni TAA..Katika mfano huu tunaona kulikuwa na mtu mmoja aliyekuwa na watumwa wake wanaomtumikia sikuzote nyumbani kwake, lakini ilitokea siku moja alipokea kadi ya mwaliko wa harusi mahali Fulani. Na kama tunavyofahamu sikuzote harusi nyingi huwa zinafanyika usiku. Na kama ni usiku basi itamgharimu kuchelewa kidogo kurudi nyumbani Kwasababu Harusi itatarajiwa iishe usiku sana. Na yeye akiangalia anao watumwa nyumbani kwake ambao pengine mkataba alioingia nao wa kufanya kazi mwisho unapaswa uwe ni saa moja jioni. Na baada ya hapo watumwa hao wanakuwa huru kwenda kumpumzia au kufanya shughuli zao binafsi.

Lakini hapa limetokea jambo ambalo linamgharimu Bwana wao kuchelewa, hivyo inamlazimu kuwasihi wamsubirie wasilale mpaka atakaporudi kutoka Harusini ili waje kumfungulia pindi tu atakapogonga malango ya nyumba … Unajua Kwa hali ya kawaida, wapo watumwa wengine watasema, huyu bwana amevunja mkataba tulioingia naye hivyo sisi hatutaweza kumngojea mpaka muda huo, kwanza katufanyisha kazi mchana kutwa tena na bado hapa anataka tukeshe mpaka usiku wa manane, atatupa fedha ya ziada? Wengine watasema sisi tutamngojea lisaa limoja au mawili na asipoonekana tutalala.

Lakini wengine wakarimu watasema hapana tusifanye hivyo bwana wetu huwa hana desturi ya kutufanyia hivi sikuzote, imekuwa ni dharura tu,na ni leo tu kesho haitakuwa hivi, hivyo tuvumilie kwa siku hii moja tumngojee bwana wetu asije akalala nje! Kwenye hatari nyingi.

Hivyo ni wazi kuwa wapo watakaokataa na watakaokubali. Lakini habari hiyo inaendelea kutuambia nini?

“37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo ATAWAKUTA WANAKESHA. Amin, nawaambieni, ATAJIFUNGA NA KUWAKARIBISHA CHAKULANI, ATAKUJA na KUWAHUDUMIA.”

Unaona hapo mfano huo unaturudisha pia kuitafakari habari ya wana wa Israeli siku ile ambayo Mungu aliona vema kuwatoa utumwani baada ya kukaa miaka 430 katika hali ya mateso, Kwa kuwa hatuna muda wa kuelezea matukio yote lakini tunafahamu siku ile ya mwisho ya wao kukaa katika nchi ya Misri Mungu aliwapa maagizo, na ikumbukwe kuwa hawakutoka nchi ya Misri MCHANA, hapana bali ilikuwa ni USIKU wa manane kwasababu ndio uliokuwa mpango wa Mungu watoke usiku.

Lakini kabla ya kutoka kwao Mungu aliwapa maagizo na maagizo na mojawapo ya maagizo hayo ilikuwa ni KUFUNGWA MKANDA VIUNONI na KUVALIWA kwa VIATU. Tunafahamu mtu akienda kulala ni lazima azilege nguo zake, atoe mikanda kisha azime taa na alale. Lakini kama nguo zako bado zimebanwa na mkanda pamoja na viatu ni wazi kuwa mtu huyo yupo katika mazingira ya kutoka muda wowote.

Lakini wana wa Israeli hawakujua uzito wa wao kuambiwa hivyo, mpaka tunavyosoma pale Farao na wamisri wote wakiwafukuza wenyewe kutoka Misri pamoja na zawadi nyingi usiku ule ule, hapo ndipo walipotambua kuwa kumbe! KUVAA KULE NDIO ILIKUWA NI KUONDOKA! Wengine waliwaza mbona! imekuwa Ghafla ghafla tu, hili jambo si lingesubiria walau asubuhi tu, tuanze kuweka vitu vyetu vizuri, tuwaage majirani zetu, tuwafuate wadeni wetu watulipe kwanza?, tukavune ngano zetu tupate chakula cha kusafiria? Nk. Lakini mbona jambo hili Mungu kaliharakisha mapema hivi?….Tunasoma usiku ule ule safari ilianza (Kutoka 12), lakini jaribu kifikiria kama mwisraeli mmoja asingetiii yale maagizo na kwenda kuamua kujifungia ndani kwake na kuvua nguo zake na kulala, unadhani atakapoamka ni jambo gani atakutana nalo?, WENZAKE HAWAPO!!. Na ndivyo itakavyokuwa katika siku hizi za mwisho Bwana alisema.

“VIUNO VYENU na viwe vimefungwa, na TAA ZENU ziwe zinawaka;

36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka ARUSINI, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia.

38 Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao.”

Unaona hapo, laiti kama hawa watumwa wote wangekuwa tayari kumngojea bwana wao mpaka atakaporudi kutoka arusini ili wamfungulie, kwa fadhila Bwana wao asingewaambia laleni mpumzike, hapana badala yake kwa kuwa VIUNO VYAO VIMESHAFUNGWA ikiashiria utayari wao wa kuondoka.

Moja kwa moja yeye mwenyewe atawakaribisha katika karamu yake aliyokwenda kuiandaa baada ya kutoka arusini, na kuwahudumia kwa kila kitu ambacho wangekihitaji, usiku ule ule wangeondoka pale nyumbani na kwenda mahali pengine kabisa kula raha ya daima. Kadhalika wao nao wangestaajabia kwanini Bwana wetu asingesubiri walau asubuhi ifike tuoge, tuvae vizuri tuwaambie na wenzetu kisha ndio tuende kwa pamoja huko kwenye hiyo karamu aliyotuandalia…kwanini kachukua maamuzi ya haraka haraka usiku huu?.. Lakini hivyo ndivyo ilivyompendeza Bwana wao.

Ndugu siku ya kuondoka kwa wana wa Mungu hapa duniani hakutakuwa kwa kukutazamia kama wengi wanavyodhani. Utakuwa ni wakati usiofaa kwa wengi hata katikati ya watumishi wake waaminifu.

Bwana alipotupa maagizo kwamba TUKESHE, TAA ZETU ZIWE ZINAWAKA na VIUNO VYETU VIWE VIMEFUNGWA. Alijua kabisa itakuwa ni wakati wa usiku wa manane ndio muda utakuwa wa kurudi kwake . Na sasa ndio tupo hicho kipindi ambapo dunia ipo katika kilele cha giza kuu kuliko hata vizazi vyote vya nyuma vilivyotutangulia. Maovu yameongezeka kuliko hata kipindi cha Sodoma, ushoga unahalalishwa hata mahali patakatifu. Hizo ndio dalili madhubuti kuonyesha kwamba tupo katika giza nene la usiku wa manane.

Lakini kumbuka pia Bwana wetu yupo karibu kurudi kutoka katika arusi ya faragha aliyoalikwa na BABA yake mbinguni. Na watakaokwenda naye ni wale tu ambao TAA zao zinawaka na VIUNO vyao vimefungwa, yaani wale ambao kila siku macho yao yapo mbinguni. Biblia inasema “jifungeni KWELI kiunoni” na kweli ni NENO LA MUNGU (Waefeso 6:14). Hivyo wale wote wataokadumu katika msingi ya Neno la Mungu wakielekeza macho yao mbinguni bila kujali mambo yanayopita ya ulimwengu, kadhalika pia wale ambao TAA zao zinawaka, kumbuka ili taa iwake inahitaji mafuta, na mafuta ni ROHO MTAKATIFU, Hivyo wale ambao waliotajazwa Roho na kila wakati wanaufanya uteule wao na wito wao imara bila kumzimisha Roho wa Mungu ndani yao, hao ndio siku ile BWANA atakapogonga watamsikia na kuingia kwenye Karamu aliyoiandaa yeye mwenyewe. Na pia ili taa iwake lazima kuwe na giza, taa haiwezi kuwashwa wakati wa mchana, hivyo wakati huu ambapo dunia imejaa matendo ya giza, ndio wakati wa kuzifanya taa zetu ziwake.

Lakini wengine wote waliosalia, wapendao matendo ya giza hawatajua lolote, itakapopambazuka tu ndipo watakapogundua kuwa wenzao hawapo, na ndiko kutakako kuwa na kilio na kusaga meno. Katika dhiki kuu, na katika siku ile ya BWANA.

Ni kwanini leo maisha yako yasiuhakisi wokovu?, Ni kwanini bado upo usingizini?. Na uzingizi hauna nguvu mchana,JE! Unao huhakika hata Bwana akija leo, utakuwa mwepesi kumsikia akigonga mlango wa moyo wako?, Mambo ya ulimwengu huu yanakusonga?, Unawatazama wanadamu? Hao watakusaidia nini endapo umesikia unyakuo umekupita, ? na wewe umebaki? ujana wako, mali zako na nguvu zako zitakuwa msaada gani kwako katika siku hiyo?

BWANA ANASEMA..

Waefeso 5:14 “……AMKA, WEWE USINZIAYE, UFUFUKE KATIKA WAFU, Na Kristo atakuangaza.

15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 MKIUKOMBOA WAKATI KWA MAANA ZAMANI HIZI NI ZA UOVU.”

Kama haujatubu ndugu fanya hivyo sasa, huu si wakati wa kuishi maisha ya kubahatisha, UKOMBOE WAKATI! nenda ukabatizwe katika ubatizo ulio sahihi wa maji mengi katika jina la YESU KRISTO haraka baada ya kutubu dhambi zako ili upate ondoleo la dhambi (Matendo 2:38) …Kumbuka kuzaliwa mara ya pili ni kutubu, kubatizwa na kupokea kipawa cha Roho, na kuishi maisha matakatifu katika Kristo, na si vinginevyo. Ikiwa bado hujapitia hatua hizo zote hapo bado hujazaliwa mara ya pili. Na Bwana alisema mtu wa namna hiyo hawezi kuuona ufalme wa mbinguni (Yohana 3:5).

Fanya bidii utubu na Bwana atakuangazia neema yake.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine, Na Bwana atakubariki

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KAMA MWIZI USIKU WA MANANE:

BEI YA UFALME WA MBINGUNI:

JE! UMECHAGULIWA TANGU ASILI?

ZILE TUNU (DHAHABU, UVUMBA NA MANEMANE) MAMAJUSI WALIZOZITOA KWA BWANA (MATHAYO 2) . ZILIWAKILISHA NINI?

SAYUNI NI NINI?


Rudi Nyumbani

Print this post

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

Mathayo 5: 13 “NINYI NI CHUMVI YA DUNIA; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.

14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.

15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.

16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.”

Bwana Yesu aliwafananisha watakatifu waliopo duniani na CHUMVI,. Tunafahamu sifa ya chumvi, ni kiungo kisicholika chenyewe kama chenyewe, bali ni lazima kwanza kichanganywe na kitu kingine kama chakula ili kilete ladha, kadhalika chumvi huwa haitengenezwi na mchanganyiko mwingine wowote isipokuwa ni chumvi kama chumvi tu, ikichanganya na vingine inakuwa tena si chumvi bali ni kitu kingine.

Vivyo hivyo mkristo yeyote aliyekolewa, kwa kuzaliwa mara ya pili, mbele za Mungu ni kama chumvi katika ulimwengu. Anapoamua kuacha dhambi na maisha mabovu aliyokuwa anaishi huko nyuma, mbinguni yeye anaonekana kama chumvi safi katikati ya ulimwengu. Lakini chumvi tunafahamu inaharibika pale tu inapojichanganya na kitu kingine au inapomwagika. Kwa mfano chumvi ikiingia mchanga ni wazi kuwa hakuna mtu atakayeweza kutenganisha punje moja moja kutoka katika huo mchanga, badala yake itakuwa ni ya kutupwa tu, hata kama ilinunuliwa kwa thamani kubwa kiasi gani, haifai tena.

Na ndivyo ilivyo kwetu, tunapokuwa wakristo tunapaswa tuwe makini sana, tunapaswa tujilinde sana, tunapokaa katikati ya ulimwengu, kwasababu biblia inasema tunakuwa kama Nuru katikati yao, Kwa mienendo yetu na matendo yetu. Lakini sasa matendo yetu yakiwa mabovu ni sawasawa na chumvi iliyoharibika. Tunapotazamwa na dunia tuwe na mienendo inayostahili na bora kuliko yao halafu tunaonekana ni walevi, watukanaji, waasherati, wasengenyaji, watoaji wa maneno ya mizaha, wagomvi, fitna, wivu, na chuki, tunakosa nidhamu katika jamii, je! Tutatiwa nini hata tukolee?. Kilichobaki ni kutupwa tu nje! Na kukanyagwa na watu. Hatua hiyo ni sawa na ile hatua ya kutapikwa, kwasababu unakuwa vuguvugu na si baridi wala si moto,..Ni chumvi iliyoingia mchanga.

Biblia imesema katika 1Wakorintho 10: 12 “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”. Unaona hapo? Ukristo ni wakutunzwa sana kuliko kitu kingine chochote, kwasababu ukristo wako ukishaharibika tu mara moja unakuwa haufai tena kwasababu maandiko ndivyo yanavyosema.

Wafilipi 2:11”… .UTIMIZENI WOKOVU WENU WENYEWE KWA KUOGOPA NA KUTETEMEKA

13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu,”

Tunapaswa tujilinde kila siku, kila mahali, kama tumekusudia kweli kwa kumaanisha kuacha mambo ya ulimwengu na kufanyika kuwa chumvi safi, tudumu katika hali hiyo hiyo, tusiitie chumvi uchafu, kwasababu chumvi si kama maharage ambayo yakianguka yanaweza yakaokoteka na kuosheka….Kwasababu biblia inasema sisi watakatifu IMANI tumekabidhiwa MARA MOJA TU (Yuda 1:3). Ikiwa na maana kuwa ukristo si wa kwenda na kurudi, kwenda na kurudi tu kama tunavyotaka..

2Petro 2: 20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, HALI YAO YA MWISHO IMEKUWA MBAYA KULIKO ILE YA KWANZA.

21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, KULIKO KUIJUA, KISHA KUIACHA ILE AMRI TAKATIFU WALIYOPEWA.

22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, MBWA AMEYARUDIA MATAPIKO YAKE MWENYEWE, NA NGURUWE ALIYEOSHWA AMERUDI KUGAA-GAA MATOPENI ”.

Hivyo kama wewe ni mkristo ambaye ulishaokolewa na hujasimama imara huu ni wakati wa kufanya hivyo maadamu mlango wa neema bado haujafungwa, unayo nafasi ya kuwa moto,unayo sasa nafasi ya kufanyika CHUMVI, Unachopaswa kufanya ni kuanza maisha yako ya ukristo upya na kuamua kujikana nafsi yako kila siku kwa Bwana, na kukaa mbali na vishawishi vyote vya dunia ambavyo vitakufanya ukristo wako uwe vuguvugu, marafiki, disco, anasa, uvaaji mbaya, fashion,ulevi, usengenyaji, pornography, kujihusisha na ku-chat na kupost vitu visivyofaa katika mitandao, n.k. vifanye kuwa ni adui yako, na Bwana mwenyewe atakuongezea nguvu ya kuvishinda.

Kama wewe hujazaliwa mara ya pili ni afadhali ukafanya hivyo sasa. Na kuzaliwa mara ya pili maana yake ni kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi zako, kisha kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi, katika JINA LA YESU KRISTO. Na Bwana atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu. Kumbuka Bwana Yesu alisema mtu asipozaliwa mara ya pili [yaani kwa maji na kwa Roho] hawezi kuuona ufalme wa mbinguni. Ni maombi yangu ufanye hivyo sasa.

Waebrania 2: 3 “SISI JE! TUTAPATAJE KUPONA, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia;”

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

Print this post

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Wengi wetu tunafahamu kitu gani kilitokea kabla ya Edeni, kwamba ibilisi/ shetani, alimwasi Mungu na kuondolewa katika nafasi yake aliyokuwapo, biblia inasema alikuwa ni Kerubi aliyetiwa mafuta, na alinyanyuliwa juu ya Mlima wa Mungu, yaani juu ya malaika wengine wote, alikuwa ni mzuri na mkamilifu katika njia zake zote na alikuwa na hekima nyingi sana, mpaka siku ile uovu ulipoonekana ndani yake, Sasa kulingana na wingi wa sifa alizokuwa nazo, na wingi wa heshima uliomzunguka tunafahamu moyo wake ulinyanyuka akatamani kuwa kama Mungu.(ukisoma Ezekieli 28:11-18, Isaya 14:12 utaona jambo hilo.)

Sasa ni nani aliyemdanganya shetani?

Jibu ni kwamba hakuna aliyemdanganya shetani, bali alijidanganya yeye mwenyewe, pale alipoona amenyanyuliwa na Mungu, hivyo alitamani awe Zaidi ya pale alipo, HILO TU! alionywa lakini alikataa, mpaka alipotolewa katika ile nafasi na kufukuzwa katika yale makao ya nuru ya utukufu aliyokuwepo, na baada ya kufukuzwa Bwana Mungu hakumuua mpaka majira yatakapofika, wala hakumnyanganya HEKIMA, na UZURI aliokuwa nao, wala hakumnyanganya NGUVU alizokuwa nazo, alichomuondolea ni ile nafasi aliyokuwa nayo mbinguni ya utukufu wa Mungu, hivyo baada ya hapo kwa kujua muda wake ni mfupi akaanza kuujenga ufalme wake na wale malaika walioasi pamoja naye, kwa hekima aliyokuwa nayo na kwa nguvu alizokuwa nazo,

Ni sawa tu na mkuu wa majeshi aliyeasi na kuondolewa katika nafasi yake ya ukuu wa majeshi, na kuamua kuondoka na wafuasi wake wengi kwenda msituni, kuanzisha kikundi cha uasi, sasa huyo mwanajeshi aliyeasi atakua amepoteza nafasi yake katika nchi lakini sio uzoefu wake, au ujuzi wake, au akili zake, ndivyo ilivyo kwa shetani baada ya kuasi hakuondolewa ujuzi wake, wala uwezo wake wa kufanya mambo,wala akili yake. Wengi wanafikiri kuwa siku shetani alipolaaniwa alibadilika na kuwa kitu cha ajabu sana na cha kutisha chenye mapembe na sura mbaya kisichoweza kufikiri, hapana, bali aliondolewa utukufu ule wa Mungu ndani yake. Na tunafahamu kitu chochote kikiondolewa utukufu wa Mungu, basi kinakuwa ni kama mfu tu katika roho.

Sasa baada ya Bwana Mungu kuanza uumbaji wa mwanadamu wa kwanza (Adamu), tayari shetani alikuwa ameshatengeneza ufalme wake ulioasi, unaojulikana kama ufalme wa giza. Na huu Ufalme wake una kazi moja tu, “kuenda kinyume na kila kitu ufalme wa Mungu unachokifanya”. Ukiamini kuwa upo wakati utasimama wenyewe na kutawala kila kitu.

Kwahiyo baada ya Adamu kuumbwa, Shetani kwa hekima yake alijua Mungu kamweka mwanadamu katika nafasi ya juu sana, kama alivyokuwa yeye, hivyo njia pekee aliyojua anaweza kuuimarisha ufalme wake ni kumwangusha mwanadamu kwa kumletea mawazo kama aliyokuwa nayo yeye hapo kwanza, “mawazo ya kujiinua kutaka kuwa kama Mungu”. Alijua kabisa njia pekee Bwana Mungu anayochukizwa nayo kwake ni KUJIINUA, Hivyo akamletea sasa mawazo kama yale yale kupitia nyoka, Tunasoma.

Mwanzo 3: 1 “Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;

3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.

4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, NANYI MTAKUWA KAMA MUNGU, mkijua mema na mabaya”.

Unaweza ukaona hapo, shetani kitu alichoona kinaweza kikawavutia sana ili waasi ni hili neno WATAKUWA KAMA MUNGU. Jambo ambalo hata yeye mwenyewe hakuweza kulifikia kuwa kama Mungu, badala yake lilimshusha chini kutoka katika nafasi yake ya ukuu mpaka kuwa pepo. Na tunaona Adamu na Hawa nao baada ya kula tunda, badala ya kuwa kama Mungu kama walivyoahidiwa na shetani, wakapoteza ile nafasi yao kama shetani alivyopoteza ya kwake, wakafukuzwa nao vile vile kutoka katika Edeni bustani ya Mungu aliyokuwa amewaumbia wao. Unaona? Shetani aliwafundisha wasiridhike na nafasi waliyokuwa nayo pale Edeni, aliwafundisha wanaweza kuwa Zaidi ya pale.

Sasa shetani na yeye hajabadilika; mbinu aliyoitumia kuwaangusha malaika wenzake walioasi naye, na aliyotumia kuwaangusha wanadamu wa kwanza Adamu na Hawa, anaitumia hata leo kuwaangusha wanadamu, kuhakikisha anawatoa katika nafasi zao, na hatumii njia nyingine Zaidi ya kuwaletea watu “roho ya kujiinua (KIBURI)” Anajua kiburi ndicho kilichomshusha yeye chini, na ndio hicho hicho anawapachikia watu ili washushwe chini kutoka katika nafasi zao. Na kama ilivyo kawaida yake, shetani analilenga kanisa kwanza Zaidi ya watu wa ulimwengu huu, hivyo anafanya juu chini kuipachika hii roho ndani ya kanisa,

Inatokea wananyanyuka watu wachache [ambao shetani anawatumia pasipo wao kujua ] ndani ya kanisa wanaoanza kumsifia labda mchungaji, au mwalimu, au askofu, utasikia wataanza kumwambia “unajua wewe askofu huwa ukizungumza tu, mimi huwa nakuona unakuwa kama malaika”..unajua wewe mchungaji ni wakipekee sana, yaani una karama zote, yaani tumezunguka kote hakuna mfano wako, yaani wewe ni shujaa na wakipekee sana, wewe ni kiboko yao,n.k. sasa kwa sifa zote hizo ni rahisi yule mtu wa Mungu kujiona yeye kweli ni bora kuliko wengine, pasipo kujua kuwa ni roho ya shetani inataka kumpeleka mahali fulani, ananyanyuka moyo na yeye kuanza kuamini kwamba ni bora kuliko wengine, na mwisho wa siku anajikuta ameshajiinua kupita kawaida.

Na mbinu nyingine shetani anayopenda kuitumia pasipo watu wengi kujua, ni mapepo, anapenda kutumia mapepo kuwapandikizia watu wengi kiburi, kwamfano inatokea mtu kaenda kumuombea mtu mwingine na yule mtu akalipuka mapepo, na yale mapepo, yakaanza kumsifia, “wewe ni mtu hatari sana, tunakuogopa, yaaani unatuunguza na unatutesa sana tangu siku nyingi, yataendelea kumwambia sisi tumetoka jupita tumewajaribu, wachungaji wengi tumewashinda ni wewe peke yako ndio unayetutesa”..na yataendelea kumwambia hadithi nyingi za uongo ambazo zote maudhui yake ni kumnyanyua yule mtumishi, na yule mtumishi pasipo kujua kwamba zile roho ni kongwe tangu Edeni na zinajua namna ya kumwangusha mwanadamu, atadhani kuwa zinamwambia ukweli, atadhani kuwa yeye kweli ndiye wa kipekee kuliko watu wote duniani, pasipo kujua kwamba “shetani ni mwongo tangu zamani na yeye ni baba wa uongo” maandiko yanasema hivyo. Sasa yule mtumishi atatoka pale na kuamini kuwa hakuna kama yeye na pasipo kujua kuwa amepandikiziwa roho ya kiburi tayari, atakwenda huku na huko kujisifu kuwa hakuna kama yeye.

Biblia inasema “inasema ajishushaye atakwezwa naye ajikwezaye atashushwa”

Ndugu/dada: mali, uzuri, cheo, ukubwa, umaarufu, utakatifu, utumishi,uchungaji, karama, kipaji, kipawa au chochote kile kisikupe kiburi, na kujiona kuwa unastahili heshima ya kipekee Zaidi kuliko wengine, visikufanye ujione kuwa baada ya Mungu mbinguni unafuata wewe. Hiyo ni roho halisi ya shetani kabisa aliyoiachia kuwaangusha watu. Ilimwangusha shetani na ndiyo hiyo hiyo anayotumia kuziangusha nyota nyingi za mbinguni leo (yaani watakatifu).

Biblia inasema katika 1Wakoritho 10: 12 “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”. Unyenyekevu ndiyo silaha pekee ya kuishinda roho ya kiburi ya shetani. Kama biblia inavyosema katika..

1 Petro 5: 5“..Naam, ninyi nyote JIFUNGENI UNYENYEKEVU, mpate kuhudumiana; kwa sababu MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI, lakini HUWAPA WANYENYEKEVU NEEMA.

6 Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;

7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

8 Mwe na kiasi na kukesha; KWA KUWA MSHITAKI WENU IBILISI, KAMA SIMBA ANGURUMAYE, HUZUNGUKA-ZUNGUKA, AKITAFUTA MTU AMMEZE. ”

Je! Ni kiburi cha uzima kimekutawala mpaka unaona kuwa hata wokovu si kitu cha maana sana kwako?, Hebu tubu leo uoshwe dhambi zako, na kubatizwa katika ubatizo uliosahihi wa maji tele katika Jina la YESU, ili Bwana akupe ondoleo la dhambi zako. Ukae mbali na hila za ibilisi na mitego yake yote katika kizazi hichi.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Print this post

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

Ukiitafakari hii neema tuliyopewa sisi watu wa mataifa ambao hapo mwanzo tulikuwa ni watu wasio na Mungu duniani ni kubwa sana, kiasi kwamba Mungu tangu zamani aliwaficha watu wake wengi, hata manabii wake waliomcha yeye katika Israeli, hawakuweza kuielewa neema hiyo, Mungu aliiweka katika SIRI kubwa sana, ambayo aliitunza mpaka wakati ulipofika wa kufunuliwa kwake, na siri yenyewe Mtume Paulo aliisema katika

Waefeso 3:3 ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu;

3 ya kwamba KWA KUFUNULIWA NALIJULISHWA SIRI HIYO, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.

4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu KATIKA SIRI YAKE KRISTO.

5 SIRI HIYO HAWAKUJULISHWA WANADAMU KATIKA VIZAZI VINGINE; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

6 YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, NA WA MWILI MMOJA, NA WASHIRIKI PAMOJA NASI WA AHADI YAKE ILIYO KATIKA KRISTO YESU KWA NJIA YA INJILI;.

Unaona hapo siri yenyewe ni kuwa kumbe hata sisi mataifa ni warithi wa ahadi za Ibrahimu kama wayahudi, katika Kristo. Watu ambao hapo mwanzo tulikuwa tunaonekana kama mbwa kwa wayahudi na ndivyo tulivyokuwa. Lakini Mungu alivyo wa upendo,alituingiza sisi kwa nguvu kupitia Yesu Kristo nasi tuwe warithi sawasawa na wao.

Hivyo ndugu kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utagundua kuwa tangu kipindi cha wana wa Israeli walipokuwa Babeli , Mungu alimfunulia mtumishi wake Danieli muda wa siku zilizobakia mpaka dunia kuisha, ukisoma Danieli 9 utaona kuwa Nabii Danieli aliambiwa muda wa MAJUMA 70 umewekwa kwa watu wake (yaani Waisraeli), mpaka kila kitu kitakapokamilika. Na kumbuka juma moja ni sawa na miaka 7 kibiblia, hivyo ukipiga hesabu utaona jumla yake ni miaka 490 [70×7=490] tu, tangu ule wakati walipotoka Babeli mpaka ulimwengu kuisha.

Lakini ukisoma pale utaona hayo majuma 70 yaligawanywa katika vipindi vitatu, yaani majuma 7 ya kwanza, halafu na majumba 62, kisha juma 1 la mwisho , kukamilisha majuma yote 70. Hatuna muda wa kueleza kwa urefu juu ya migawanyiko hiyo lakini biblia inasema lile juma la 69 litaishia na masihi (YESU KRISTO) kusulibiwa.

Danieli 9: 26 “Na baada ya yale majuma sitini na mawili, MASIHI ATAKATILIWA MBALI, naye atakuwa hana kitu; na watu wa mkuu atakayekuja watauangamiza mji, na patakatifu; na mwisho wake utakuwa pamoja na gharika, na hata mwisho ule vita vitakuwapo; ukiwa umekwisha kukusudiwa.”

Kisha linakuwa limebakia juma moja, ambalo ni sawa na miaka 7 tu ili kila kitu kiwe kimeisha.

Lakini juma hili la mwisho ukichunguza halikuendelea mara baada ya Kristo kusulibiwa, kwasababu kama lingeendelea basi mwisho ulipaswa uwe umeshafika miaka 7 tu mara baada ya kifo cha BWANA YESU, Lakini sasa tunaona imepitia takribani miaka 2000 na mwisho bado haujaja. Jambo ambalo halikuwahi kuonekana katika unabii wowote katika agano la kale. Jambo ambalo manabii wa Mungu hawakuliona wala kufunuliwa.

Na ndio maana hatupaswi kuacha kushukuru neema ya Kristo, kwasababu wokovu huu tunauona sasa ulipaswa uwe kwa WAYAHUDI tu peke yao watu wa Mungu. Jaribu kutengeneza picha kama mwisho ungefika ule wakati Kristo anaondoka duniani sisi wengine leo hii tungekuwa wapi?,Maana hata mitume wa Kristo walitazamia mwisho ungefika baada ya Bwana Yesu kufufuka..

Matendo 1:6 “ Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, JE! BWANA, WAKATI HUU NDIPO UNAPOWARUDISHIA ISRAELI UFALME?

7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.

8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, AKAINULIWA, WINGU LIKAMPOKEA KUTOKA MACHONI PAO.”

Kama Bwana asingesema hayo,sisi watu wa mataifa tungekuwa waabudu mizimu, na masanamu, tungekufa na baada ya kufa moja kwa moja ni kuzimu, lakini ashukuruwe Mungu neema ile haikutupita ambayo ililetwa na BWANA WETU YESU KRISTO, ambaye katika ule wakati wa kusulibiwa kwake aliusitisha muda wa WAISRAELI kwanza, usiishe ili atukomboe sisi watu wa mataifa, kwa neema yake, Alituhurumia sisi kwa kulitenga lile juma moja kwanza lililosalia mpaka dunia kuisha, ili hapo katikati atukomboe sisi watu wa mataifa. Na ndio hii miaka 2000 sasahivi tuliyopo ya hii neema. Kwamba kwa kipindi cha miaka takribani 2000 tuingie ndani ya safina sisi watu wa mataifa.

Lakini ndugu fahamu pia hii neema haitadumu milele, tupo ukingoni sana na leo hii tutaona ni jinsi gani ilivyokaribu kuondoka kushinda hata sisi tunavyofikiri, na ikiondoka Mungu anamalizia lile juma 1 moja la mwisho lililobakia (yaani miaka 7) kwa wayahudi WATEULE wake tu!! kisha mwisho wa dunia unawasili. Ndugu ukilijua hilo hutafanya mchezo na wokovu wako sasa.

Mungu aliwapiga upofu makusudi wayahudi(Waisraeli) wasiupokee wokovu tangu wakati ule Kristo kusulibiwa ili sisi tuupate, kwasababu kama wangeupokea wokovu wa KRISTO wakati ule basi dunia ingekuwa imeshakwisha. Mungu aliwajeruhi wayahudi kwa ajili yetu, na ndio maana unaona sasa hivi wengi wao hawamwamini Yesu kama ndiye yule masiya waliokuwa wanamtazamia.. Ni kwasababu gani?, ni kwasababu Mungu alipiga mwenyewe upofu ili tu sisi tuokoke, Mungu aliwatia mwenyewe jeraha sio kwasababu wao walikuwa na dhambi nyingi kushinda sisi hapana, kinyume chake sisi ndio tuliokuwa na dhambi nyingi kuliko wao, lakini Mungu alifanya vile kutuhurumia sisi (yaani mimi na wewe) tufikilie wokovu. Soma kitabu cha Warumi sura ya 11 yote utaona jambo hilo.

Lakini pamoja na hayo tunasoma miaka mingi iliyopita Mungu aliwaahidi kuwarudia watu wake wateule wayahudi, baada ya kipindi fulani mbele, na kuwaimarisha tena. Na Ndio sasa tunasoma katika kitabu cha Hosea, yeye anasema:

HOSEA 6:1 Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.

2 BAADA YA SIKU MBILI ATATUFUFUA; SIKU YA TATU ATATUINUA, NASI TUTAISHI MBELE ZAKE.

3 Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi.

Umeyaelewa maneno hayo?, Huo unabii unawahusu wayahudi tu! {yaani waisraeli}, Hosea anasema njoni tumrudie Bwana, akiwaambia wayahudi wenzake katika Roho, baada ya SIKU MBILI atatufufua na siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.

Kama ukisoma biblia katika kitabu cha 2Petro 3:8 utafahamu kuwa kwa Mungu SIKU MOJA NI SAWA NA MIAKA 1000, Hivyo hapo utaona kuwa unabii unaweza ukatafsiriwa hivi “Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu. baada ya miaka 2000 atatufua na mwaka wa 3000 atatuinua”.

Ndugu tangu Kristo kuondoka hadi sasa, miaka 2000 inakaribia kuisha, na miaka ya hivi karibuni tutaanza wa 3000, na huo mwaka wa 3000 utakuwa ni milenia ya ule utawala wa miaka 1000 wa Yesu Kristo duniani (Ufunuo 20:4). Sasa kama hapo anavyosema atatufufa, atafunga jeraha zetu na kutuponya, hiyo inamaanisha kuwa huo ndio utakuwa ule wakati wa wayahudi kurudiwa na Mungu wao, kumaliza lile juma moja la mwisho lililokuwa limesalia (yaani miaka 7) ili dunia kuisha. Utakuwa ni wakati wa Israeli kurudishiwa ufalme kama walivyomuuliza Bwana siku ile kabla ya kupaa kwake.

Ndugu neema ikishalirudia Taifa la Israeli, unyakuo wa kanisa utakuwa umeshapita, kitakachokuwa kimebakia katika mataifa yote ulimwenguni ni MAJUTO NA MAOMBOLEZO, fikiri Bwana ametuhurumia kwa kipindi kirefu hichi chote ili mtu tu yeyote asiangamie lakini bado unaichekezea hii neema iliyopo kwa kitambo tu. Bwana aliposema kutakuwa na kilio na kusaga meno, alimaanisha kweli wala hakutudanganya. Miaka 2000 hii inaisha, Taifa la Israeli linazidi kunyanyuka siku baada ya siku, ule mwisho unakaribia, je! Umejiwekaje tayari sasa?. Kwanini bado unaichezea hii neema ya msalaba ambayo sisi hatukistahili kuipata?. Utajibu nini siku ile?. Au utajitetea vipi?.

Waebrania 2: 3 “SISI JE! TUTAPATAJE KUPONA, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? AMBAO KWANZA ULINENWA NA BWANA, KISHA UKATHIBITIKA KWETU NA WALE WALIOSIKIA;”

Hizi ni saa za majeruhi kama hujakamilishwa katika wokovu fanya bidi sana, utubu, ubatizwe katika ubatizo sahihi wa maji tele na katika Jina la Yesu Kristo, upate ondoleo la dhambi zako, kisha udumu katika ushirika wa Kristo na mafundisho ya biblia angali siku ile inakaribia.

Kwasababu moja ya hizi siku dunia itakuwa imekwisha kabisa.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu, na Mungu atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

JE! DAMU INA UMUHIMU WOWOTE KATIKA MAISHA??

ZIFAHAMU NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE SABA.

JE! MTU ANAPOFUNGA KWA MUDA WA SAA 24,ANAPASWA KUNYWA MAJI AU KITU CHOCHOTE?

JE! NI SAHIHI KUMUITA MARIA MAMA WA MUNGU?


Rudi Nyumbani

Print this post