Category Archive Home

WATU WASIOJIZUIA.

Kutokujizuia ni kitendo cha kukosa uwezo wa kutawala kitu fulani kisitokee kisichopaswa kufanyika kwa wakati huo. Kwa mfano mtu anapokuwa mlevi wakati mwingine anajikuta amejisaidia pale pale, au kinywa chake kinaanza kuzungumza maneno yasiyokuwa na maana, pengine ataanza kutukana au kufoka..Huko ni kutojizuia..mambo ambayo mfano angekuwa na akili timamu, asingeweza kuyafanya hadharani.

Biblia inasema moja ya dalili kubwa itakayotuonyesha kuwa tunaishi katika siku za mwisho ni kuwepo kwa wimbi kubwa la watu wasioweza KUJIZUIA. Na kutojizuia kunakozungumziwa hapo sio kujizuia kutokutokwa na haja, hapana bali kutojizuia kutenda maovu hadharani mbele za watu, hivyo si watu wema wanaozungumziwa hapa bali wanazungumziwa wale walio waovu, ili kutofautisha uovu ule wa nyuma na huu wa siku za mwisho, kumbuka waovu wa zamani walikuwa na kitu kinachoitwa Kujizuia, lakini waovu wa siku za mwisho biblia inaweka wazi kuwa hicho kitu hakitaonekana ndani yao kabisa.

2 Timotheo 3:1-17

1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,

3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, WASIOJIZUIA, wakali, wasiopenda mema,

4 wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;

5 wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.

Ilikuwa zamani, mwanamke kahaba ni mtu wa kujificha, anafanya ukahaba wake kwa siri hata ni ngumu kumtambua, mavazi yake ya kikahaba alikuwa anayavaa usiku tu tena katika eneo la shughuli zake, nje ya hapo huwezi kumkuta, ilikuwa huwezi kumwona hadharani ovyo ovyo eti anazunguka na uwazi wake barabarani, haikuwahi kutokea hivyo wakati wowote. lakini angalia sasa, makahaba wanashindwa kujiuzia kufanya mambo yao, wanakosa ule uwezo wa kutawala tamaa zao, ile hofu ya watu kuwaona na kuwachukulia hivi au vile haipo tena ndani yao, wapo tayari kupiga picha za uchi, na kutengeneza video za zisizofaa ambazo hazistahili kabisa kuwepo, na kwa ujasiri kabisa wana zi-post katika mitandao, ili watu wote wawaone, na kibaya zaidi wanaofanya hivyo wengi wao ni watu wanaojulikana, ili kusudi kwamba uchafu wao uweze kuwafikia watu wengi zaidi kwa muda mfupi, hizi ndizo ishara madhubuti za siku za mwisho.

Sio kana kwamba hayo mambo yalikuwa hayafanyiki zamani, hapana yalifanyika kwani biblia inatuambia hakuna jambo jipya chini ya mbingu, lakini kwanini unaona kama siku hizi maovu yameongezeka zaidi ya zamani,? Jibu ni kwamba hayajaongezeka kwa kiwango kile unachofikiri bali kinachoendelea sasa ni kwamba wafanyao maovu wa sasa wamepoteza kile kitu kinachoitwa kujizuia ndani yao..Roho ya kutokujali lolote imewavaa, roho ya “fuata mambo yako”, roho ya “ishi maisha yako”..roho ya “kutokujali” ndio inayotawala maisha yao. Na ndio maana hushangai hata kuona watu wa karne hizi watu waki-tengeneza video wanazini na wanyama n.k..Si ajabu tena kwao, kudhihirisha aibu zao wazi. Inasikitisha sana!

Kutukana hadharani hakukuwepo zamani, lakini sasa viwango vya matusi vimekithiri, mabarabarani, kwenye nyimbo za kidunia, kwenye mitandao, si watu wazima si watoto wadogo, maneno yanayozungumzwa huwezi kuamini kama marika kama hayo yanaweza kutoa maneno magumu kama hayo katika vinywa vyao.

Mashoga na wasagaji, wanajitangaza hadharani, hawajali tena hata vyombo vya dola na huku wanajua kabisa kwamba Sheria za nchi haziruhusu vitendo hivyo na kwamba mtu anayefanya hivyo adhabu yake ni kali, wao hilo wanaliona kabisa hawalijali sembuse Mungu wasiyemwona?. KUTOJIZUIA.

Washirikina waendao kutafuta mali kwa waganga wa kienyeji, zamani walikuwa hawadhubutu kuiathiri jamii hadharani kama wafanyavyo sasa hivi, lakini angalia leo, mtu anafikia hatua hata ya kwenda kukata viungo vya watu wasio na hatia (ma-albino, na mtatiti ya mabinti wadogo) kwa tamaa tu za mali.

Kutokujizui, Biblia inasema pia hapo juu siku za mwisho watatokea watu WAKALI, Wasiopenda mema, ile dhambi inapata nguvu mpaka sasa hawezi kutulia ndani, inajidhihirisha nje bila kujali kitu chochote wala mtu yoyote..

Dalili nyingine inayozungumziwa hapo juu ni “KUSINGIZIA”..Tafsiri halisi iliyotumika hapo, kusingizia maana yake, ni “kumzunguzia mwingine vibaya”, au “kumsengenya mtu” kwa lugha nyepesi iliyozoelewa sasa Ni ‘’Umbea”. Kusengenya ni KIU mtu anakuwa nayo ya kutaka kupakua habari za maisha ya mtu mwingine kwa nia ya udadisi ili kupata huko mambo ya kumzungumzia yasiyopendeza mbele za Mungu..

Haya mambo zamani yalikuwepo lakini sio kwa kiwango cha uwazi kilichopo sasa, utakuta mtu anashindwa kujizuia kabisa, Anashindwa kufanya mambo yake mwenyewe, anashindwa kuwazungumzia watu kwa wema, anajikuta kutwa kuchwa ni kudadisi maisha ya watu wengine kwa ubaya. Sasa ukiona wimbi la watu wa namna hii linaongezeka basi fahamu kuwa tunaishi katika majira ya mwisho wa Dunia.

Ndugu yangu. Kama vile hilo andiko linavyosema “siku za mwisho kutakuwako na nyakati za HATARI ”. Fahamu kuwa nyakati zenyewe ndio hizi tunazoishi..Ikiwa utashindwa kujizuia mwenyewe na kuona kila kitu kufanya ni SAWA TU!…Zamani ulikuwa unaona aibu kuvaa vimini na kutembea navyo barabarani lakini sasa unaona hakuna shida yoyote! Ujue kuwa upo katika hatari kubwa sana..roho ya kutokujali imekuingia.

Ukiona zamani ulikuwa ukitukana unajisikia vibaya lakini sasa matusi yamekuwa ni sehemu ya maisha yako. Ujue kuwa ile roho ya kutokujali imekuvaa..Kama vile wale watu wa sodoma na gomora, jinsi walivyokuwa na tabia ya kutokujizuia hata kufikia hatua ya kutaka kulala na wageni wale (malaika wa Mungu) waliokuja yamkini kusitiri uovu wao,lakini wao wakashindwa kujizuia. Jambo gani lilitokea muda mfupi baada ya pale?. Kwanza kabla hata maangamizi hayajawafikia walipigwa upofu. Na upofu ule ni wa daima..Vivyo hivyo na kwa watu wasiojizuia sasa, Upofu unakuja, na upofu huo ni wa daima, ukishamkuta tu mtu, basi huyo mtu hata afanyeje ni wa kuangamizwa tu! hawezi kutubu tena, neema inakuwa haipo tena juu yake, hata ahubiriweje injili.

Zamani ulikuwa unajisikia vibaya kula rushwa, na kufanya utapeli lakini sasa yote yamekuwa sawa kwako, zamani uliogopa hata kusogelea msonge wa waganga wa kienyeji lakini siku hizi pamekuwa kama nyumbani kwako, namba za waganga na watabiri wa nyota zimejaa kwenye simu yako ya mkononi. Upo katika hatari kubwa sana.

Hujizuii mwili wako, unatembea nusu-uchi barabarani na ku-post picha chafu mitandaoni, humwogopi tena Mungu kama hapo zamani, unakuwa ni sababu ya watu wengi kumkosea Mungu, kwa kutazama vitu unavyovipost na mavazi unayoyavaa..Dada upo katika HATARI kubwa sana. Hukumu yako haitakuwa sawa na wale wengine..siku ile fahamu tu utapigwa sana, kama usipotubu, kwasababu uliijua kweli na bado ukaendelea kufanya kwa makusudi. Kuzimu ipo ni kitu halisi kabisa, mtu yeyote asikudanganye kuwa hakuna kuzimu, ipo kabisa.

Tukiyajua hayo, basi ni wajibu wetu kumrudia muumba wetu, kabla ya huu uharibifu mkubwa ambao utaikumba dunia nzima haujatukuta sisi.. Tubu dhambi zako sasa, ukabatizwe upate ondoleo la dhambi zako.

Mwenye sikio asikie Neno hili, ambalo Roho wa Mungu anatuonya watu wa kizazi hiki. Kwamba tujihadhari nacho.

Ubarikiwe.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

Print this post

JE! UMECHAGULIWA KABLA YA KUWEKWA MISINGI YA ULIMWENGU?

Shalom mtu wa Mungu, karibu tujifunze Maneno ya Mungu, kwa Neema zake, leo tutajifunza somo linalosema, Kuchaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya Ulimwengu.

Tunajua kuwa Mungu tunayemwabudu, yaani Yule aliyekuwa anaabudiwa na wana wa Israeli ambaye sasa tunamwabudu na sisi watu wa Mataifa, Mungu muumba wa Mbingu na nchi hana mwanzo wala hana mwisho, sentensi hiyo tu! Inatosha kutujulisha yeye ni Mkuu kiasi gani, yeye ni zaidi ya upeo wetu wa kufikiri. Kwasababu kitu kisichokuwa na mwanzo wala kisichokuwa na mwisho ni kitu cha namna gani hicho?.

Hivyo basi kama hana mwanzo wala hana mwisho ni dhahiri kuwa atakuwa na uwezo wa kufahamu mwanzo wa ulimwengu na mwisho wa Ulimwengu mzima, ndio maana katika Neno lake anatabiri yatakayotokea katika siku za mwisho maelfu ya miaka nyuma kabla hata ya hiyo siku kutokea…Anasema siku za mwisho kutatokea hiki na kile, anaendelea kusema, baada ya dunia kuisha kutakuja utawala wa miaka 1000, anaendelea kusema baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha kiti cheupe cha hukumu kitawekwa, ambapo wafu wote watafufuliwa na kuhukumiwa n.k n.k..Mambo hayo yote Bwana tayari anayajua.

Na kama anajua mwisho wa dunia katika mtiririko wote, ni dhahiri kuwa atakuwa anajua pia mwanzo na mwisho wa kila mwanadamu katika mtiririko wote…ikiwa na maana kuwa anajua ni yupi ataokolewa na yupi hataokolewa, ni yupi ataingia mbinguni na ni yupi hataingia mbinguni siku ya mwisho…Na kama anayajua hayo ni dhahiri kuwa ni yeye huyo huyo ndiye anayechagua ni yupi ataokolewa na yupi hataokolewa..Kwasababu Bwana Yesu mwenyewe alisema “Hakuna awezaye kuja kwangu asipovutwa na Baba yangu aliyenipeleka (Yohana 6:44)”. Kwahiyo ni Roho Mtakatifu ndiye anayemvuta mtu kwa MUNGU na sio mtu mwenyewe anayejipeleka kwa Mungu.

Kama Mungu yupo hivyo pengine utasema, kwanini aumbe wengine hivi wengine vile? Huo ni kama vile udhalimu Fulani hivi…Jibu la swali hilo, Mtume Paulo alilitoa kwa uweza wa Roho akasema.. Tusome:

Warumi 9:13 “Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.

14 Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha!

15  Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye.

16 Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.

17 Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote.

18 Basi, kama ni hivyo, atakaye kumrehemu humrehemu, na atakaye kumfanya mgumu humfanya mgumu.

19 Basi, utaniambia, Mbona angali akilaumu? Kwa maana ni nani ashindanaye na kusudi lake?

20 La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?.

21 Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?”.

Umeona hapo? Hakuna awezaye kushindana na kusudi la Mungu, anafanya yote kama atakavyo yeye… “HILO LINAOGOPESHA SANA.” Sisi wanadamu hatuwezi kumwuliza Mungu kwanini anafanya vile au kwanini anafanya hivi.. Ulishawahi kuaamka asubuhi na kuanza kumwuliza Mungu kwanini hakutuumba na mabawa, kama alivyowapa malaika? nasi tuwe tunaruka juu kama ndege?… Au kuku amwulize Mungu kwanini yeye kaumbwa kuku na wala si mtu? Ndivyo ilivyompendeza yeye tuwe hivi tulivyo…

Sasa swali linakuja nitajuaje kuwa mimi nimekusudiwa wokovu, na tena Nimechaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu?.

Jibu la swali hilo hatuwezi kulipata kwa kufunga na kuomba Mungu atufunulie, wala hutuwezi kulipata kwa kukisia tu! Wala hatuwezi tukasema kwa kukisia tu Kwamba mimi nitakuwa ni miongoni wa waliochaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Ili tujue kwamba sisi ni miongoni wa waliochaguliwa Jibu la swali hilo tutalipata katika BIBLIA TU!

Neno la Mungu linasema hivi katika kitabu cha.

Waefeso 1: 3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;

4 kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo.

5 Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake”.

Ukitafakari kwa makini mstari huo wa nne utagundua vigezo vya kuchaguliwa tangu asili ni vipi?…hapo anasema “kama alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu ILI TUWE WATAKATIFU, WATU WASIO NA HATIA MBELE ZAKE KATIKA PENDO”…Zingatia hili neno “ILI TUWE WATAKATIFU”…hii ikiwa na maana kuwa mtu aliyechaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu..alama yake ni UTAKATIFU. Kama Yesu Kristo alivyokuwa mtakatifu tunapaswa tufanane naye ndio tuwe na uhakika kwamba na sisi ni miongoni mwa lile kundi lililochaguliwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu..

Na kama tunavyojua UTAKATIFU chanzo chake ni ROHO MTAKATIFU kama jina lenyewe lilivyo..roho chafu matunda yake ni uchafu, roho ya uzinzi matunda yake ni uzinzi, kadhalika na Roho takatifu matunda yake ni utakatifu. Kwahiyo kwa ufupi mtu yeyote ambaye maisha yake ni ya UTAKATIFU katika Kristo Yesu, huyo mtu asilimia 100 amechaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Hakuna alama nyingine zaidi ya hiyo. Kwasababu anafanana na Yesu Kristo na kama maandiko yanavyosema pia katika kitabu cha waebrania.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao” 

Unaona hapo? Tiketi ya kumwona Mungu ni UTAKATIFU. Kwahiyo kwa hitimisho namna ya kujichunguza kama umechaguliwa tangu asili ni kujichunguza maisha yako je! Ni ya utakatifu? Au sio ya utakatifu, hapo ndipo utakapojijua wewe upo kundi gani na ndipo utakapoijua roho iliyopo ndani yako? Je ni roho chafu au ni roho mtakatifu?..je! maisha yako yanafanana na maisha ya Yesu Kristo au Yuda eskariote, maana maandiko yanasema.

Warumi 8: 29 “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.

30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita,hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza”.

Je! Na wewe ni mtakatifu kama mwana wa Mungu, Yesu alivyokuwa mtakatifu, umefananishwa na yeye?..au ni mla rushwa?, au ni msengenyaji?, au ni mzinzi, au Ni mwasherati? au ni mtazamaji wa pornography au mfanyaji masturbation? Au wewe ni msagaji? Na kahaba? Je! Ni mlawiti?, je! Ni mvaaji wa nguo fupi na suruali zinazokuonyesha maungo yako? je ni muuaji au mhudhuriaji kwa waganga na disko? Je! Ni mtukanaji. Kama hayo yote  unayafanya na bado unakwenda kanisani na kujiita mkristo na kujifariji kwamba upo katika mstari wa watakaoenda mbinguni..napenda nikuambie ndugu yangu “ichunguze hiyo roho iliyopo ndani yako” sio roho mtakatifu bali ni roho nyingine ya Yule adui, inayokuongoza kwenda katika ziwa la moto. Roho wa Mungu aletaye utakatifu ndani ya mtu huyo ndio MUHURI AU ALAMA ya kukutambulisha kwamba wewe ni umechaguliwa tangu asili au la! Kwamba wewe umekusudiwa wokovu au la! Maandiko yanasema hivyo. (Waefeso 4: 30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye MLITIWA MUHURI hata siku ya ukombozi”).

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU.”

Ndugu yangu, naamini na wewe ni mmoja wa waliochaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ndio maana Roho Mtakatifu aletaye utakatifu hajakuacha kabisa yupo nje! Anagonga mlango wa moyo wako anataka kuingia ndani yako AKUTIE MUHURI WA UTAKATIFU, ili uwe na tiketi ya kumwona Mungu.

Lakini kama huisikii sauti yake wala kwako haina maana basi wewe sio miongoni mwa walio wake..kama biblia inavyosema katika Warumi 8:9 “Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. LAKINI MTU AWAYE YOTE ASIPOKUWA NA ROHO WA KRISTO, HUYO SI WAKE.”.

Swali linarudi lile lile..Je! wewe ni miongoni mwa walio wake au wasio wake??..je! wewe ni miongoni mwa watakaoenda mbinguni au watakaoenda katika lile ziwa la moto? Je! Unaisikia sasa sauti ya Roho mtakatifu anayekutaka utubu na uwe mtakatifu au huisikii?.. Jibu unalo wewe.

Ikiwa unataka leo hii Roho Mtakatifu aingie ndani yako, uwe miongoni mwa waliochaguliwa kabla ya msingi wa ulimwengu, unachopaswa kufanya hapo ulipo, tenga sio chini ya dakika 10 au zaidi hapo ulipo Tubu! mwambie Bwana akusamehe maovu yako yote, mweleze yote usifiche hata moja maana yeye anakujua kuingia kwako na kutoka kwako?..na kisha baada ya kufanya hivyo dhamiria kuacha hayo maisha ya dhambi uliyokuwa unaishi..usiende kulewa tena, usiende kufanya uasherati tena, achana na kampani mbovu n.k Kisha hatua ya pili inayofuata Nenda katafute ubatizo sahihi wa kweli wa kimaandiko nao ni wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, ili kumbukumbu la dhambi zako zifutwe kabisa kabisa… na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukupa wewe nguvu na uwezo wa kushinda dhambi na kuishi maisha ya utakatifu.

Uwezo huo au nguvu hiyo haiji isipokuwa kwanza umedhamiria kuacha njia zako mbaya za nyuma, wengi wanasema wametubu na kukoka lakini bado mioyo yao ipo Misri, na ndio maana wanashindwa kuishinda dhambi kwasababu hiyo.. Ile nguvu ya Roho Mtakatifu haijashushwa ndani yao kutokanana na mioyo yao kutokuwa thabiti kwa yeye waliyemtubia dhambi zako.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja KWA JINA LAKE YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.”

Hivyo fanya hivyo leo na Bwana atakuangazia Nuru yake.Hapo ndipo utapata uhakika ya kuwa umechaguliwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Kesho si yako, hizi ni siku za mwisho.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine na Bwana azidi kukubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinaendana:

JE! WEWE NI MBEGU HALISI?

EPUKA MUHURI WA SHETANI

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.


Rudi Nyumbani

Print this post

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

(Ndoto ya Ndugu Yusufu, kutoka Tabora, mwaminio wa ujumbe wa Malaki 4:5)

Mbarikiwe sana ndugu zangu, Ndugu zangu naomba nisaidieni kupata tafsiri ya hii  hii njozi maana imenitatiza  sana:

Niliota kwamba BWANA YESU KRISTO amekuja duniani .lakini alipokuja aliwakuta watu baadhi wakiendeleea na shughuli zao (hawakujua kuwa amekuja) .na alipo fika alichukua watu baadhi akatoka nao kidogo nje ya kijiji kile (lakini kuna mtu mwingine alisema kwamba kuna kitu amesahau sehemu basi akaamua kukirudia hicho kitu ;huku wale wengine ambao BWANA YESU kawatoa nje ya kijiji wakiambatana nae)_..

Sasa tulipofika mwisho wa kijiji kile (pembezoni mwa kijiji ) BWANA YESU akasema anaanza kubagua Kondoo na mbuzi kwenye lile kundi alilotoka nalo kwenye kile kijiji .. .tulipokuwa katika kujiandaa ghafla nikaona Kondoo na mbuzi mbele yetu ..basi watu wakaanza kwenda kwenye Kondoo na wengine kwenye mbuzi..

Bwana alipomaliza kuwabagua .akaenda tena kwenye kondoo ndicho kilicho nishangaza AKAANZA TENA KUWABAGUA HAO KONDOO TENA. alikuwa ananyosha kidole mkono wa kulia wanakuja kwake.. Lakini walikuwa kama wanataka kugombaniana kwenda kwa Bwana. Kati ya lile kundi walitoka watu wachache sana wa kwenda na Bwana. Sasa baada ya kuwachagua Bwana akaenda kama kwenye kitu cha usafiri hivi.(sikukifahamu ) na alipofika akaingia kwanza na sisi tukafuata nyuma lakini kabla ya kuanza kuingia akafika yule aliye omba ruhusa kule mwanzo  afuate kitu sehemu akasema nae anasitahili awe na BWANA lakini Bwana hakumkubalia .. Yule ndugu alilia sana akisema nae anastahili kuingia kwenye ule usafiri.

Na nilipokuwa nawaangalia ndugu niliokuwa nao sikumwona hata mmoja ninaye fahamiana nae.( hata mama yangu sikumwona hata baba ,wadogo zangu,hata ndugu na dada zikumwona hata mmoja) .ndio nikaaanza kusikitika nikitaka kulia ghafla ikaja sauti ikiniambia kwamba (nilikuwa kama nafikiria ikisema HAKITAINGIA KILICHO KINYONGE .na tena ikasema kwamba WALIO CHAGULIWA KABLA YA KUWEKWA MISINGI YA ULIMWENGU.).

Ndipo nikasikia Bwana akisema akimwita ndugu fulani..nilisika akisema PETRO KUNA CHAKULA .NIKAMWONA BWANA KAMA ANAANDAA CHAKULA HIVI. (Lakini cha kushangaza haya yote yalikuwa yakifanyika chini duniani) Baada ya hapo nikaona Mwanga mkali mbinguni. Hapohapo nikaamka . Nini maana yake ya hii njozi MUNGU wa mbinguni awafunulie maana yake. Shalom.

Ni wazi kuwa Bwana amekuonyesha maono ya siku za mwisho..Na ndoto hiyo tutaichapisha ili na wengine pia wanufaike kwasababu ujumbe huo haukuhusu wewe mwenyewe bali pia unalihusu  kanisa la Kristo kwa ujumla, ambao ni sisi sote humo humo kwa ujumla. Kwanza kuwa upande wako unapaswa uamini kuwa bibi-arusi wa Kristo ni tofauti na Kanisa la Kristo kwa ujumla, mke ni tofauti na suria japo wote wanaweza  kuwa ni milki ya Bwana arusi .Maana yake ni kuwa wanaoitwa wakristo ni wengi lakini bibi-arusi wa Kristo ni wachache sana, na ndio hao peke yao watakaokwenda kwenye unyakuo, na kutokana na uchache wao dunia haitajua kitu kitakachokuwa kinaendelea.,

Tofauti na watu wengi  wanavyodhani kuwa unyakuo ukifika duniani kote kutakotekea machafuko ya kila namna, kila mtu atajua, ajali zitatokea mabarabarani, mamilioni ya watu watapotea, kana kwamba njia ya mbinguni ni njia nyepesi kuiingia kama shetani anavyowadanganya watu, biblia inasema kule hakitaingia kilicho kinyonge, na kama ingekuwa wengi Bwana asingesema Kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, Embu kaa chini ufikirie siku za Nuhu walipona watu wangapi kama sio watu nane(8) tu kati ya mabilioni ya watu waliokuwa ulimwenguni?, Bwana asingesema tena kuja kwake kutafanana na kama zilivyokuwa  siku za Lutu, siku zile walipona watu watatu (3) tu kati ya malaki ya watu waliokuwa katika miji ile…Ukisoma tena mahali pengine alisema “mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.(Mathayo 7:14)”..Yote hayo yanathibitisha kuwa mbinguni sio kurahisi kama watu wanavyokufikiri au wanavyofundishwa.. Unyakuo hautakuwa kwa mtu yeyote ambayo hajaonyesha nia ya kuuingia, sio kusema tu nimeokoka basi! Na kuendelea kuishi mtu anavyojisikia.

Na ndio maana hapo kwenye ndoto umeona kumbe hata katikati ya kondoo bado kulikuwa na mchujo..Hiyo inalingana na maandiko kabisa kama tukitazama mfano wa wale wanawali 10, (Katika Mathayo 25) ambao wote walikuwa ni wanawali (mabikira) safi, wote walikuwa wanamsubiria Bwana wao, isipokuwa katikati yao wengine walikuwa wenye busara na wengine wapumbavu. Wale wenye busara walichukua taa zao pamoja na mafuta ya ziada, lakini wale wapumbavu hawakubeba mafuta ya ziada katika vyombo vyao, na wakati ambao Bwana wao sasa anakuja ili awachukue taa zao zikawa zinaanza kuzima , Hivyo wale wapumbavu wakawaomba wenzao wawapunguzie kidogo, lakini wale wakasema hapana tukiwapa hayawezi kututosha sisi pamoja na nyie ni heri mshike njia mkanunue ya kwenu, na walipokwenda kununua, wakati wanarudi wakakuta tayari mlango umeshafungwa..Bwana akawaambia Amin, nawaambia, siwajui ninyi.

Unaona? Siku hizi ni siku za mwisho, na inasikitisha kuwa idadi kubwa ya watu wanaojiita ni wakristo sio wakristo kweli kweli, wanaitwa hivyo kwasababu tu wamezaliwa katika familia za kikristo, lakini ukiangalia mienendo yao, tabia zao, uvaaji wao, mazungumzo yao, yapo mbali kabisa na Ukristo, yaani ni wakristo-jina.

sasa hao ni ndio wale mbuzi uliowaona wakitengwa mbali na wale kondoo…Kadhalika wapo ambao kweli walianza vizuri na Bwana walisimama imara lakini ilifika wakati wakaanza kupoa mguu mmoja ukawa  nje, mwingine ndani, mwanzoni macho yao yalikuwa yakielekea mbinguni, wamejitenga mbali na dhambi, wamethibitika katika imani lakini ikafikia wakati wakaanza kupoa mfano wa wale wanawali wapumbavu ambao hawakuwa na mafuta ya ziada katika taa zao. Na mafuta ya ziada ni UHAI WA ROHO WA MUNGU NDANI YA MTU. Sasa wakaanza kumzimisha Roho wa Mungu ndani yao, huko nyuma walianza vizuri lakini kidogo kidogo, wakaanza kupoa, mambo ya ulimwengu huu yakaanza kuwasonga, lakini ukiwatazama huwezi kujua kuwa wanamizigo ya kando inayowavuta, ibadani wanahudhuria, watavaa mavazi ya kujisitiri, hata katika maombi utawakuta, wanafanana kabisa na wale wakristo waaminifu waliosimama imara mbele za Mungu kwa uaminifu wote isipokuwa wao ni vuguvugu tu,  sasa hao ndio wale kondoo uliowaona wakichambuliwa katikati ya kondoo…Walipaswa waende na wale wengine lakini  kwa upumbavu wao wamebaki..

Ndugu hatupaswi kupoa kwa namna yoyote, hizi ni nyakati za mwisho, kanisa hili tunaloishi, ndilo kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, Ndio lile la mwisho kati ya yale 7 yazungumziwayo katika kitabu cha Ufunuo 2&3, Israeli imeshakuwa taifa huru tena, Ni nini tunachokisubiria sasa kama sio UNYAKUO.

Na Bwana anasema Kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku za kuja kwake mwana wa Adamu,.Ikiwa utautazama upepo wa ulimwengu na kujifariji kwa mambo maovu yanayoendelea, ukidhani kuwa Bwana anatumia  ile kauli ya “wengi wape”. Utajikuta unaingia katika gharika ya dhiki kuu, wakati wengi wapo mbinguni kwenye karamu ya mwanakondoo. Ndugu Unyakuo hautakuwa wa wazi kama watu wanavyodhani, unyakuo utakuwa ni SIRI, Na watakaofahamu ni wale wanawali werevu, wachache sana. Lakini dunia nzima itakuwa buzy wakati huo kumfurahia mpinga-Kristo na utawala wake.

Uamuzi ni wako ndugu unayesoma ujumbe huu, Kristo anarudi, na wala hatakawia, atakusanya ngano ghalani mwake na magugu atayatupa katika moto usiozimika…Tubu dhambi sasa, ukabatizwe, na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, kwasababu hatuna wakati mwingi katika kizazi hichi.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

USHUHUDA WA RICKY:

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU


Rudi Nyumbani

Print this post

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

Luka 18:1 Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?.

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi;

Shalom! Mwana/binti wa Mungu, karibu tuyachunguze maandiko, natumaini leo utajifunza jambo jipya litakalotusaidia katika maisha yako ya maombi..Embu jaribu kufikiria mfano huu watoto wawili mapacha wamemfuata baba yao tajiri kwa faragha na kumwomba awapatie kitu..mmoja kamwambia baba nimeona suruali nzuri dukani naomba uninunulie, na mwingine akasema baba nimeona ndege kubwa inapita angani, naomba uninunulie na mimi niwe na ya kwangu niendeshe..We unadhani maombi ya nani yatakuwa ya kwanza kujibiwa kwa haraka zaidi ya mwingine?..Ni wazi kuwa aliyeomba nguo inawezaka isipite hata siku awe ameshatimiziwa haja yake..Lakini huyo mwingine japo aliomba na mwenzake katika muda mmoja, japo walisikiwa wote katika muda mmoja, japo baba yao aliwahidi wote kuwapa walivyoviomba, lakini majibu ya huyu wa pili, yanaweza yasije kwa wakati alioutarajia, inaweza kumgharimu mambo mengi sana, ikiwemo muda, na maisha.

Na hiyo ni kwasababu gani?. Ni kwasababu jambo aliloliomba lina uzito mkubwa zaidi kuliko la Yule mwingine. Sasa japo baba yake alikuwa anao uwezo wa kumnunulia ndege hata wiki ile ile, lakini alijua kuwa kwa utoto wake hawezi bado kuendesha ndege, hana maarifa ya kutosha kwa alichokiomba, ni sharti kwanza aende shule, akasome masomo magumu ya sayansi, na Jeografia, kisha akajaribiwe katika vituo vingi vya ndege ndogo, na ndio baadaye sana pengine hata baada ya miaka 20 baada ya kufudhu madarasa hayo ndipo baba yake amnunulie ndege yake mwenyewe, aliyomwomba. Hivyo jambo atakalohakikisha baba kwa wakati huo ni kumwezesha kwa kumpeleka katika shule zenye mafunzo hayo, na kumkazania awe chini ya waalimu wazuri, na kusoma vitabu vingi, n.k. ili aweze kufikia malengo yake.

Vivyo hivyo na sisi, Bwana YESU alituambia imetupasa tumwombe Mungu sikuzote wala tusikate tamaa..Ukiona hujapata majibu ya maombi yako leo, haimaanishi kuwa Mungu hajayasikia, au Mungu anapenda kukuona una msumbua sumbua, kila siku kumpigia magoti hapana, jua kuwa majibu ya maombi yanatofautiana kulingana na hitaji lililopelekwa kwa Mungu.

Mungu huwa anamakusudi yake kufanya hivyo, na ndio wakati mwingine utaona unamwomba Mungu akufanyie kitu Fulani, utashangaa hata hujamaliza kuomba jambo hilo lilishatendeka zamani, na wakati huo huo pengine umekuwa ukimwomba Mungu hitaji fulani kwa muda mrefu lakini bado hujaona matokeo yoyote..Fahamu kuwa hilo uliloliomba lina uzito mkubwa mbele za Mungu kuliko lile la kwanza, na hivyo kabla hujalipokea linahitaji maandalizi kwanza.

Pengine wewe ni mgonjwa, na umeshamwomba Bwana kwa muda sasa pengine miaka akuponye ugonjwa wako lakini huoni dalili yoyote ya huo ugonjwa kuondoka, na wakati huo huo ukitazama unaona wengine wanakuja na matatizo makubwa hata zaidi ya ulionanayo na wanapokea miujiza yao saa ile ile, na wewe unajiuliza mimi  nina makosa gani?..

Ndugu jambo hilo lisikufanye kujiona kuwa Mungu hakuoni, au anapenda uendelee kuteseka. Fahamu kuwa wote wawili alishawasikia wakati mmoja mlipo mwomba, na wote wawili alishaanza kuwajibu maombi yetu tangu wakati ule ule mlipomwomba…Isipokuwa Mungu anajua njia nzuri zaidi ya sisi kutupatia hitaji la ombi letu kuliko sisi tunavyofikiri, Hivyo ukiona hakuna matokeo yoyote leo wala kesho zidi kufurahi kwasababu ombi lako wewe limeonekana kuwa na faida kubwa zaidi mbeleni kuliko lile la mwingine, kwanza kwako mwenyewe, na pia katika ufalme wa Mungu.

Tunasoma kwenye biblia, wakati Fulani Lazaro, aliugua sana, pengine alikuwa na ugonjwa uliokuwa unamsumbua kwa muda mrefu, labda tuseme kwasasa kisukari na wakati huo huo biblia inatuambia alikuwa ni rafiki wa karibu sana na YESU, alitembea na Yesu sehemu nyingi, pamoja naye hata katika mikutano ya uponyaji alikuwa pamoja na Bwana, aliweza kushuhudia jinsi watu wengi walivyokuwa wanaponywa kimiujiza. Lakini yeye alikuwa bado na ugonjwa wake, mpaka ilipofikia wakati hali imekuwa mbaya sana sasa hawezi hata kutoka kitandani mwake,

Hivyo akapeleka watu kwa Bwana aje upesi kumwombea walau atoke kitandani..Lakini Bwana alipopata taarifa zile, hakwenda popote, jiulize ni kwanini Bwana hakuondoka haraka haraka na kwenda Huko kumwangalia rafiki yake kipenzi, badala yake akabaki pale pale siku nyingine mbili..

Tengeneza picha wale watu waliompelekea Yesu taarifa, wakati wanarudi njiani walikuwa wanawaza nini vichwani mwao?, pengine walisema, huyu alikuwa anampenda Lazaro kweli?, au alikuwa anaonyesha unafki tu!, haiwezekani rafiki yake yupo ICU mahutihuti, na yeye yupo buzy na watu wengine hata asiowajua, rafiki yake anaumwa tangu siku nyingi kwanini asimponye yeye kwanza.? Lakini Yesu alisubiri mpaka mauti ilipomkuta..Ndipo sasa akaondoka aende kumtembelea rafiki yake..Tunasoma.

Yohana 11.17 “Basi Yesu alipofika, alimkuta amekwisha kuwamo kaburini yapata siku nne.

18 Na Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu, kadiri ya maili mbili hivi;

19 na watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa habari ya ndugu yao.

20 Basi Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alikwenda kumlaki; na Mariamu alikuwa akikaa nyumbani.

21 Basi Martha akamwambia Yesu, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa.

22 Lakini hata sasa najua ya kuwa yo yote utakayomwomba Mungu, Mungu atakupa.

23 Yesu akamwambia, Ndugu yako atafufuka.

24 Martha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.

25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;

26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?

27 Akamwambia, Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.

28 Naye alipokwisha kusema hayo, alikwenda zake; akamwita umbu lake Mariamu faraghani, akisema, Mwalimu yupo anakuita.

29 Naye aliposikia, aliondoka upesi, akamwendea.

30 Na Yesu alikuwa hajafika ndani ya kijiji; lakini alikuwa akalipo pale pale alipomlaki Martha.

31 Basi wale Wayahudi waliokuwapo na Mariamu nyumbani, wakimfariji, walipomwona jinsi alivyoondoka upesi na kutoka, walimfuata; huku wakidhania ya kuwa anakwenda kaburini ili alie huko.

32 Basi Mariamu alipofika pale alipokuwapo Yesu, na kumwona, alianguka miguuni pake, akamwambia, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa.

33 Basi Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliofuatana naye wanalia, aliugua rohoni, akafadhaika roho yake,

34 akasema, Mmemweka wapi?Wakamwambia, Bwana, njoo utazame.

35 Yesu akalia machozi.

36 Basi Wayahudi wakasema, Angalieni jinsi alivyompenda.

37 Bali wengine wao wakasema, Je! Huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?

38 Basi Yesu, hali akiugua tena nafsini mwake, akafika kwenye kaburi. Nalo lilikuwa ni pango, na jiwe limewekwa juu yake.

39 Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.

40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?

41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia.

42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.

43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.

44 Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake”.

Unaona hapo? Hata baadhi ya makutano waanza kudhihaki wakisema aliweza kuwaponya wengine kwanini alishindwa kumzuia huyu asife?..Lakini habari yote tunaijua, ule muujiza uliotokea pale, baada ya Lazaro kufufuliwa, Israeli yote Ilimtazama Kristo kwa jicho lingine, mpaka watoto wadogo wakawa wanamwimbia mabarabarani wakisema Hosana! na Mafarisayo na Masadukayo kuona vile sasa Israeli yote inakwenda kumgeukia ndipo walipopanga shauri la kumwua sio tu Yesu peke yake bali pia Lazaro kwasababu kwa ushuhuda wake aliwafanya watu wengi wamgeukie Mungu..Embu fikiria Lazaro alikufa na ugonjwa wake usiotibika, lakini sasa anafufuka bila ugonjwa wowote..alikufa pasipo umaarufu, lakini sasa anafufuka na umaarufu mkubwa.

Sasa angalia njia za Mungu zilivyo za ajabu, hata leo hii sikiliza shuhuda ambazo zinawajenga watu kuwafanya hata wakate shauri kumgeukia Mungu, utagundua kuwa shuhuda zao sio zile zilizokuja kwa majibu ya haraka, haraka mwingine atakwambia madaktari walithibitisha kuwa mapigo ya moyo yamesimama kabisa, lakini baadaye akaja kuamka, na kuwa mzima, n.k.

Hivyo ndugu Bwana anaposema imetupasa kumwomba Mungu bila kukata tamaa, haimaanishi kuwa Mungu anatupuuzia kama Yule kadhi dhalimu alivyokuwa anafanya hapana, Bali ni kwamba ametusikia na hivyo anatuandalia ushuhuda ulio bora zaidi kwetu sisi na kwa ajili ya ufalme wake. Unachopaswa kufanya ni kuzidi kumshukuru yeye kila wakati na kukaa katika uwepo wake bila kukata tamaa, haijalishi hali yako itakuwa enaendelea kuwa mbaya kiasi gani, jua tu hakuna dhara lolote litakalokutokea..Endelea tu kukaa uweponi mwake maombi yako yalishasikiwa tangu siku ya kwanza ulipoomba, Hivyo hiyo hali unayopitia sasa ni matokeo ya yale maombi.

Tukiyafahamu hayo, embu turudi sasa kwenye kiini cha somo letu kinachosema.. NI JAMBO GANI BWANA ANATAMANI SANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?..

Kama tulivyoona kila hitaji tunalomwomba Mungu hatupaswi kulikatia tamaa, iwe ni afya, iwe ni mafanikio, au chochote kile chema..Lakini lipo jambo ambalo Mungu analitamani kila mmoja wetu aliombe hilo usiku na mchana, awe na haja ya hilo siku zote za maisha yake..Ni jambo ambalo Mungu analiona ni KUU kuliko hitaji lolote tunaloweza kumwomba Mungu, ni jambo ambalo mtu akilipata basi ni sawa na Yule mtoto aliyemwomba baba yake ndege zaidi ya aliyemwomba nguo.

Jambo hilo Yesu alilifunua katika maombi maneno yanayofanana na yale yale tuliyosoma hapo juu..tusome:

Luka 10: 5 Akawaambia, Ni nani kwenu aliye na rafiki, akamwendea usiku wa manane, na kumwambia, Rafiki yangu, nikopeshe mikate mitatu,

6 kwa sababu rafiki yangu amefika kwangu, atoka safarini, nami sina kitu cha kuweka mbele yake;

7 na yule wa ndani amjibu akisema, Usinitaabishe; mlango umekwisha fungwa, nasi tumelala kitandani mimi na watoto wangu; siwezi kuondoka nikupe?

8 Nawaambia ya kwamba, ijapokuwa haondoki ampe kwa kuwa ni rafiki yake, lakini kwa vile asivyoacha kumwomba, ataondoka na kumpa kadiri ya haja yake.

9 Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.

10 Kwa kuwa kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

11 Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?

12 Au akimwomba yai, atampa nge?

13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni HATAZIDI SANA KUWAPA ROHO MTAKATIFU HAO WAMWOMBAO?.

Unaona hapo? HATAZIDI SANA KUWAPA ROHO MTAKATIFU HAO WAMWOMBAO?.Kwanini hakusema MALI, au AFYA, bali Roho Mtakatifu?..Ndugu kumbuka hii dunia isingekuwa hivi ilivyo kama Roho wa Mungu asingetua juu yake na kufanya uumbaji upya..Hata mtu yeyote anayesema amemwamini Yesu, hakumwamini hivi hivi kama hakuvutwa na Roho wa Mungu kwake (Yohana 6:44).. Hata leo hii anayesema amesimama, au anamtumikia Mungu, hafanyi hayo yote kama sio Roho wa Mungu amekufanya uwe hivyo. Roho wa Mungu ndio kila kitu kwenye maisha yetu..Ndio muhuri wa Mungu (waefeso 4:30), na ndio maana biblia inasema wale wote wasio na Roho wa Mungu hao sio wake (Warumi 8:9)..haijalishi utakuwa mwema kiasi gani…

Roho Mtakatifu ni karama ya bure kabisa, mtu anampokea pale tu anapoitii sauti yake na kumkaribisha ndani yake..Hii inakuja pale mtu anapokusudia kabisa kwa weupe wa moyo wake kutoka moyoni KUTUBU dhambi zake na kuacha maisha yake ya kale, kisha akaenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zake kulingana na (Matendo 2:38). Basi kuanzia hapo mtu wa namna hiyo anakuwa ametiwa muhuri na Mungu kwa Roho wake mtakatifu..Lakini hiyo peke yake haitoshi,.Kumwamini tu, bila ya kumtamani ROHO MTAKATIFU katika maisha yako, hutafika mahali popote…Wengi wameishia hapo na ndio mwisho wa siku Roho Mtakatifu amezimika ndani yao.

Pindi tu unapompokea BWANA kuanzia huo wakati na kuendelea ni jukumu lako kumtamani Roho Mtakatifu awe pamoja nawe. Na ndio hapo linakuja hilo ombi kuu la Bwana, Akupe Roho mtakatifu, au kwa lugha rahisi tunaweza kusema AKUJAZE Roho Mtakatifu…Ulikuwa katika kipimo cha chini lakini sasa unataka AKUJAZE mpaka kwenye kipimo cha juu kabisa. Kumbuka Roho Mtakatifu sio kunena kwa lugha, ni jambo lingine, Na kwa jinsi utakavyozidi kuendelea kuomba bila kukata tamaa, basi ujue ndivyo unavyojijengea daraja zuri la Mungu kuyatawala maisha yako yote, na kuruhusu madarasa Fulani upitie kwa kukuandaa kwa kazi yake teule ya utumishi mwema..Kama tunavyoona ilivyokuwa kwa Yohana mbatizaji, ilivyokuwa kwa Bwana Yesu na ilivyokuwa kwa mitume wake..Wote walipokea Ujazo wa Roho Mtakatifu,lakini hiyo ilikuja kwa jinsi walivyotamani kipawa hicho tunaona baadaye walikuja kuvipokea, Roho mtakatifu aliposhuka juu yao na kuwatia mafuta ya utumishi, ndipo hapo Mungu alitembea nao kwa namna ya kipekee sana.

Hivyo ni maombi yangu, mimi na wewe kila siku na sisi tusikate tamaa kuomba Roho Mtakatifu..Leo unaweza usione matokeo yoyote, lakini jua tu ombi lako limesikiwa, na kama hujakata tamaa juu ya hilo unaendelea kulishikilia basi jua maisha unayopitia sasa ni maandalizi ya kazi ya huyo Roho atakayekuja juu yako baadaye.

Waefeso 5:17 “Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO;”

Ubarikiwe sana.

“Share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

UFUFUO WA UZIMA NA WA HUKUMU.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.


Rudi Nyumbani

Print this post

TUMEPEWA, SI KUMWAMINI TU KRISTO, ILA NA KUTESWA KWA AJILI YAKE;

Wafilipi 1:29 “Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake; ”.

Ni mstari ambao wengi wetu hatuupendi, wala hautufurahishi… na mwingine ni

1 Wakorintho 14:34 unaosema “Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.

35 Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.”

Pamoja na..

1 Timotheo 2:11 “Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.

12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.

13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.”,

Mistari hii kwa mtu ambaye hasomi kabisa biblia akisiisikia kwa mara ya kwanza anaweza akapinga kama vile haipo katika Biblia Takatifu. Ni mistari inayochokiwa na wengi, na huwa haihubiriwi mara kwa mara. Na hata ikihubiriwa inapindishwa pindishwa ikipakwa pakwa rangi, kuipotezea maana halisi ya mistari hiyo.

Lakini Mistari yote hii inapatikana katika Agano jipya na imevuviwa na Roho Mtakatifu, na kuthibitishwa na yeye mwenyewe kwa ajili ya afya ya Roho zetu, na kwa faida zetu. Ndio maana Roho Mtakatifu akaruhusu iwepo katika Biblia Takatifu katika vizazi vyote..Na kama Bwana Yesu anavyosema “Mbingu na Nchi zitapita lakini Maneno yangu hayatapita kamwe”…ndivyo maneno hayo yatakavyodumu siku zote. Na pia inasema maneno ya Mungu yamehakikiwa na ni safi kama fedha iliyosafishwa mara saba (Zaburi 12:6).

Leo kwa Neema za Bwana hatutajifunza hiyo Mistari miwili ya Mwisho bali tutajifunza huo wa Kwanza, unaozungumzia HABARI YA KUTESWA KWA AJILI YA KRISTO.

Ni muhimu kufahamu, chochote Mungu anachotaka tukifanye ni kwa faida yetu, ni kwasababu anatupenda na anataka tupate faida nyingi kwa kupitia hicho…Kwahiyo chochote kile kiwe kibaya au kizuri kitokacho kwa Mungu kinacholetwa juu yetu sisi tuliomwamini yeye, ni kwa ajili ya kutujenga sisi hana lengo la kututesa hata kidogo kwasababu yeye mwenyewe amesema hapendi kuwatesa wanadamu (Maombolezo 3:33.. Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha).

Hata mzazi mwenye upendo wa kweli kwa mwanawe, chochote kile akiletacho juu ya mtoto wake kiwe kizuri au kibaya..lengo lake sio kumharibu bali kumfundisha, na wala lengo lake sio kumhuzinisha, bali kumjenga..ndivyo ilivyo kwa Baba yetu wa mbinguni.

Kwahiyo maandiko yanasema, hatujapewa kumwamini tu!!…yaani ikiwa na maana hatujapewa kumwamini tu Bwana Yesu na kusali na kuomba, na kutenda mema na kuishia hapo! Hapana! Bali tumepewa pia kuteswa kwa ajili yake.

Hivyo Kwanini Bwana anataka tuendelee mbele hatua ya kuteswa kwa ajili yake?..ina maana hiyo ya kumwamini tu haitoshi?!!.. Jibu ni kwamba haitoshi ndio maana anataka tuendelee mbele.

Lengo la kufanya vile ni ili ATUFANANISHE NA YESU KRISTO, MWANA WAKE. Ili kwamba turithi kama Kristo alivyorithi, kwasababu yeye ili aweze kuzirithi mbingu za mbingu, kikombe cha mateso hakukiepuka…ingawa kuna wakati aliomba “Baba ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke”…Lakini Baba hakumwepushia lengo lilikuwa sio kumtesa bali ni kumpa sababu ya kupata zile mbingu za mbingu alizomwahidia kumpa sababu ya yeye kwanini awe juu ya malaika wote.

Na kama alimpitisha mwanawe mpendwa Yesu Kristo katika mateso yale, pia atawapitisha wanawe wengine wote katika njia ile ile, ili kwamba na sisi nasi tuwe tumestahili kuzirithi zile ahadi kubwa namna ile Yesu alizozirithi. Na yeye ni mwaminifu kama alivyokuwa na Bwana Yesu ndivyo atakavyokuwa na sisi wakati wa mateso..na atatupa ushindi kama alivyompa BWANA Yesu.

Ufunuo 3:21 “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.”

Unaona nafasi ya kuketi na Bwana katika kiti cha enzi, ni lazima tushinde kama yeye alivyoshinda.

Yeye alipigwa pasipo sababu, na sisi hatuna budi kupitia wakati mwingine kupigwa pasipo sababu, yeye alichukiwa bure biblia inasema hivyo (Yohana 15:24-25), na sisi hatuna budi wakati mwingine kupitia kuchukiwa Bure kwasababu ya Imani yetu au mienendo yetu inayompendeza Mungu, yeye aliishinda hasira pale alipotemewa mate bila kosa lolote, na sisi hatuna budi kushinda hasira na ghadhabu tutakapozalilishwa pasipo sababu yoyote.

Yeye walimsimamishia mashahidi wa uongo lakini alishinda kwa kujinyenyekeza kama kondoo apelekwaye machinjoni wala hakupaza sauti yake kushindana na mtu, Isaya 53: 7 “Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, HAKUFUNUA KINYWA CHAKE”. Na sisi tunatakiwa tushinde vile vile, kwa kufumba vinywa vyetu tunapoonewa, na kusingiziwa mambo mabaya na kusimamishiwa mashahidi wa uongo.

Yeye alishinda kwa kuwaombea msamaha wale waliomsulibisha katika hatua yake ya mwisho ya uhai wake, na sisi tunapaswa tushinde kwa kuwasamehe wale wote wanaotutesa au kutuonea, au kutuumiza hata katika hatua ya mwisho ya uhai wetu.

Hiyo ndio maana ya kuteswa kwa ajili ya Kristo na kila mkristo wa kweli lazima apitie, kwasababu hatuwezi kusema tunafanana na Kristo, wakati historia za maisha yetu hazifanani na historia ya maisha yake. Ndio maana Bwana Yesu alituambia… “mtu yoyote akitaka kumfuata, sharti kwanza ajikane nafsi yake na ajitwike msalaba wake kisha amfuate”…Na zaidi ya yote apige gharama kwanza kabla ya kumfuata…Kwasababu njia ya Kristo ni njia ya Msalaba, ambayo mwisho wake ni KALVARI. Lakini mwisho wake una matunda makubwa sana.

Na tukishinda kama yeye basi tutarithi kama yeye alivyorithi…kama Mtume Paulo anavyosema mahali fulani..

2 Timotheo 2.9 “Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi.

10 Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele.

11 Ni neno la kuaminiwa. Kwa maana, Kama tukifa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia;

12 Kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi;”

Lakini pia biblia imetuonya tusiteswe kwaajili ya matendo mabaya..hatupaswi kuteswa kwajili ni wezi, au watukanaji, au wasengenyaji, au wakorofi au waasherati, au wala rushwa au mafisadi, au wachokozi… na kusema tunateswa kwa ajili ya Kristo, Hapo tutakuwa hatuteswi kwa ajili ya Kristo bali kwa ajili ya shetani.

1 Petro 4:12 “Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.

13 Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.

15 Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.

16 Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.

17 Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?

18 Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?

19 Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu na wamwekee amana roho zao, katika kutenda mema, kama kwa Muumba mwaminifu”.

Bwana atujalie sote, kuyaelewa maandiko na kuyatendea kazi. Tutakapokutana na hayo basi tusizimie mioyo tukidhani kuwa Mungu hatupendi au tuna bahati mbaya..Kwani tukumbuke kuwa hata watakatifu waliotutangulia walipitia mambo kama hayo hayo, na hata sasa wengine wanaendelea kupitia.

Bwana akubariki sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

IMANI NI KAMA MOTO.

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?(MATHAYO 6:24)

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.


Rudi Nyumbani

Print this post

VITA DHIDI YA MAADUI

Shalom karibu tujifunze Neno la Mungu, Maandiko yanatuambia “kumcha Bwana ni chanzo cha Maarifa”… Maneno ya Yesu Kristo yanafaida kubwa katika maisha zaidi hata tunavyofikiri.  Kwa jinsi tunavyozidi kumcha Bwana maarifa yetu ndivyo yanavyozidi kuongezeka siku baada ya siku, mpaka tunapofikia kiwango kile cha Maarifa cha kumfahamu yeye anachotaka tukifikie sisi kama tunavyosoma katika Waefeso 4:13. 

Nilipita sehemu Fulani, nikapisha na dada mmoja aliyekuwa anaongea na mwenzake, walikuwa wanatembea kwa kasi kidogo lakini nilifanikiwa kusikia moja ya kauli zake  akisema “tumepewa mamlaka ya kukanyaga nge na nyoka…akaendelea kumwambia mwenzake “adui yako akija mbele yako usimsubirishe we mkanyage..kwa maana tumepewa mamlaka hayo ”…Akiwa na maana kuwa mtu akija mbele yako ambaye yupo kinyume chako mdhuru kabla yeye hajakudhuru biblia imeturuhusu kufanya hivyo, tena hakikisha unammaliza kweli kweli.

Niliposikia hivyo nilisikitika sana, nikasema Bwana atusaidie kweli kweli,

Ndugu yangu nataka nikwambie..katika Agano jipya hatuna adui yoyote ambaye ni Mwanadamu…Adui yetu ni Shetani na majeshi yake, kwa maana kupigana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, maandiko yanatuambia hivyo… Vita juu ya damu na nyama vilikuwa katika Agano la kale, ndio maana tunawaona watu kama wakina Daudi, Sulemani, Sauli na wengine wote ndio waliokuwa na maadui ambao ni wanadamu kwasababu, bado walikuwa hawalijui agano lililo bora zaidi. Kwa neema Mungu aliyowapa aliwaruhusu wawaone maadui zao kwa njia ya kibinadamu, lakini haikuwa hivyo tangu mwanzo. Tangu Edeni adui wa kwanza wa mwanadamu alikuwa ni shetani.

Kwahiyo baada ya dhambi Mungu aliruhusu tuishi katika vipengele pengele Fulani vya maisha ambavyo vingi havikuwa ni njia kamili au mpango kamili wa Mungu japo aliviruhusu, kwamfano aliruhusu talaka, aliruhusu ndoa za wake wengi. N.k

 Lakini ulipokuja utimilifu wote ulioletwa wa lile Neno lililofanyika mwili ambaye ni Bwana wetu Yesu Kristo, kwa Neema aliweka mambo yote kama yanavyopaswa yawe katika utimilifu wote..ndio maana Bwana aliwaambia “watu haikuwa hivyo tangu mwanzo”,..wao walikazana kumwambia Bwana mbona Musa alifanya hivi, alisema vile…lakini Kristo alizidi kuwaambia haikuwa hivyo tangu mwanzo..

Na leo jambo ni lile lile watu tunaweza kujiuliza mbona Daudi alikuwa na maadui na aliwaua na aliwalaani… na sisi tufanye hivyo hivyo, lakini Kristo anatuambia haikuwa hivyo tangu mwanzo…haikuwa hivyo tangu mwanzo kujilipiza kisasi, haikuwa hivyo tangu mwanzo kumlaani mwanadamu mwenzako (ambaye tunaona roho ya uadui ipo ndani yake)…Utauliza hayo maneno yanatoka wapi kwenye biblia?..soma

Luka 6:28 “wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.”

Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi”..

38 Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho,na jino kwa jino; Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume,mgeuzie na la pili” 

Hayo ni maneno ya Bwana Yesu mwenyewe..anasema “mmesikia imenenwa….”

Sasa swali wamesikia kutoka kwa nani? Jibu ni wamesikia kutoka Kwa mababa waliowatangulia ambao ndio hao wakina Musa, Daudi, Eliya na wengine wote…

Ndugu yangu unaposoma kitabu cha Zaburi, pasipo uongozo wa Roho Mtakatifu wa kujua nyakati Mungu alizokuwa anatembea kwa kila nyakati itakupoteza kwasababu ndani ya Zaburi hiyo hiyo kuna sehemu imehalalisha mvinyo, Ndani ya zaburi hiyo hiyo usipokuwa na msaada wa roho kuielewa unaweza ukajifunza chuki na visasi, ndani ya sheria za Musa na torati pasipo msaada wa roho unaweza kujifunza mauaji na kiburi…Na ndani ya hiyo hiyo biblia unaweza kujifunza uasherati kama wengi sasahivi wanavyoitumia kuhalalisha ndoa za mitara.

Sasa tukirudi kwenye suala la “Maadui zetu”…swali ni je! Maadui wetu ni wakina nani sasa?

Kumbuka Tangu mwanzo adui ni Ibilisi biblia inasema hivyo, yeye ndiye atushitakiaye mbele za Mungu mchana na usiku, na ni mfano wa simba angurumaye atafutaye mtu wa kummeza (1 Petro 5:8). Huyo ndio adui yetu wa kwanza na wa mwisho, hivyo kwa kutumia majeshi yake ya mapepo wabaya..ndio anafanya vita na sisi.

Anayatuma mapepo yake yanawaingia watu, kwahiyo Yule mtu anageuka kuwa ofisi ya shetani kwa kujua au pasipo kujua..ndio hapo unakuta mtu anakuchukia ghafla pasipo sababu, au anakutafutia hila, anaanza kukupiga vita, au kukutafutia madhara, au wivu au anafurahia kuanguka kwako!…au anatafuta namna ya wewe kuiacha imani, sasa chanzo sio Yule mtu, bali ni roho iliyoko ndani yake…roho iliyoko ndani yake ndio roho ya uadui.

Sasa sio jukumu letu sisi kupambana na Yule mtu, kama watu wa agano la kale walivyokuwa wanafanya bali ni jukumu letu kupambana na ile roho inayotenda kazi ndani yake,  Yule mtu yeye ni  kama ofisi tu!! Awe anajua au asiwe anajua.. Watu wa agano la kale kama wakina Daudi walikuwa wanapambana na watu kwasababu bado walikuwa hawajapewa neema ya kujua chanzo cha mambo yote ni wapi lakini sisi tumepewa….

Ndio hapo biblia inatuambia katika

Wafilipi 6:11 “ Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; BALI NI JUU YA FALME NA MAMLAKA, JUU YA WAKUU WA GIZA HILI, JUU YA MAJESHI YA PEPO WABAYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO”

Hapo Neno linatuambia “tuweze kuzipinga hila za shetani na sio mwanadamu”.

Sasa namna ya kuipiga na kuikanyaga hii roho ya adui iliyopo ndani ya ndugu zetu!! Namna ya kuitowesha kabisha, na kuiharibu tumepewa silaha madhubuti za kuiangusha, pasipo kuidhuru ile ofisi shetani anayoitumia, maana nia na madhumuni ni kuipiga ile roho na kuiacha ile ofisi huru iokoke ili itumiwe na Mungu kama ofisi ya Nuru. Haleluya!!, sasa silaha za kuipiga ile roho ndio hizi zifuatazo.

Waefeso 6:13 “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama..

1)   Basi simameni, hali mmejifunga KWELI VIUNONI– Hakikisha unaifahamu kweli yote ya biblia, unamfahamu Yesu Kristo katika ukweli wote,Maneno ya Mungu kama haya.

2)   Dirii ya Haki kifuani– Hakikisha unauelewa vizuri ufunuo wa kuhesabiwa haki kwa Imani, kwamba sio kwa matendo tunaokolewa bali kwa neema, sio kwa matendo tunaponywa bali kwa neema, si kwa matendo tunapata ulinzi kutoka kwa Mungu bali kwa neema, sio kwa matendo tunampendeza Mungu bali kwa Neema kupitia Yesu Kristo. Hiyo itakusaidia shetani anapoleta mashtaka yake ya kukuhukumu ndani ya moyo wako, au nje unakuwa na mafuta ya kutosha kumshinda hoja zake, na kutokupepeswa na maneno ya mwovu yanapokuja juu yako.

3)    kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani– Hii ni silaha ya tatu madhubuti kabisa ya kuiharibu ile roho ya uadui ndani ya mtu, hatua hii ni ile mtu anapochukua hatua ya kwenda kumhubiria INJILI Yule mtu ambaye roho ya uadui ipo ndani yake, na kumhubiria sio tu kwa maneno bali kwa kielelezo cha matendo, unakwenda kumhubiria habari njema za wokovu, una mwombea, unaonyesha upendo, akikuomba chakula unampa,akikuomba nguo mvike, na hiyo inapelekea  Ile roho iliyoko ndani yake inapungua nguvu kwa kasi sana, na kutengeneza njia ya ushindi wa vita.

4)   Ngao ya Imani –Imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo, kwa lolote lile shetani atakalolileta, una imani kuwa halitafanikiwa, na zaidi ya yote una Imani kuwa wewe ni mwana wa Mungu mrithi wa ahadi zake, na hakuna chochote kitakachokudhuru, hata jeshi la mapepo kiasi gani,hata waganga wote duniani wakiungana kupambana wewe hakuna jambo lolote litakalofanikiwa kwasababu upo chini ya damu. Na unaimani kuwa  lolote umwombalo Baba atakutendea

5)   Tena ipokeeni chapeo ya wokovu– Chepeo ni HELMET kwa kiingereza, kazi yake ni kulinda sehemu ya kichwa..Na sisi tunaposimama mbele ya Adui yetu shetani, silaha yetu nyingine ni tumaini la Wokovu tulionao, kwamba tumemwamini Yesu Kristo aliyetukomboa kwa damu yake, na kutuahidia ukombozi wa miili yetu, kwahiyo hakuna chochote kitakachoweza kututoa kwake kwa kupitia Roho wake Mtakatifu tumetiwa Muhuri mpaka siku ya ukombozi wetu (Waefeso 4:30). Na huko huko ndio unajifunza kusamehe. Kwasababu unajua na wewe ulisamehewa deni kubwa kushinda hilo la ndugu yako.

6)   Upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu– Hii ndio silaha ya mwisho na ya umuhimu kuliko zote.. ukilifahamu Neno la Mungu, hakuna elimu yoyote ya shetani itakayokupiga chenga, kwasababu shetani naye anayo injili yake ambayo inafanana sana na injili ya Kweli, ambayo kwake nayo ni kama UPANGA anayokatakata nayo watu, ndio ile aliyokuwa anataka kumkata nayo Bwana kule jangwani injili ya “imeandikwa”..

lakini Bwana alimshinda kwasababu Neno la Mungu lilikuwa limekaa ndani yake kuliko shetani. Upanga wa Kristo ulikuwa mkali kuliko wa shetani aliweza kumkata shetani kwa kumjua hila zake na njama zake na mawazo yake… Waebrania 4:12 “ Tena Neno la Mungu li hai tena lina nguvu tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake, tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo”.alimshinda kwa Neno.

Hizo ndizo silaha 6 Muhimu na pekee za kushindana na Adui yetu shetani. Sasa kumbuka katika vita adui yako na yeye kavaa kama wewe, na yeye ana kweli yake kiunoni, ana dirii yake kifuani, ana chepeo yake kichwani ana injili yake miguuni, na ana upanga wake mkononi amepewa na shetani. Hivyo Ndivyo alivyo shetani ana injiili yake ya uongo ana imani yake ya uongo, ana wokovu wake wa uongo, ana haki yake ya uongo…yote hayo ni kwaajili naye kujilinda,lakini kwasababu sisi tunavyo vya ukweli na vyenye nguvu kuliko vyake tunamshinda. Lakini kama hatuna hata kimoja cha ukweli atatukatakata na upanga wake na kutuweka chini.

Sasa tutajuaje kwamba tumeshinda vita? Tutajua tumeshinda vita vizuri kama tutakuwa tumefanikiwa kumleta Yule mtu kwa Kristo, au tumempandia mbegu ya Kristo ndani yake, Kwasababu Yule ni mtu wa Mungu, anayestahili wokovu kama wengine tu! Kama sisi,  naye pia Mungu hapendi kumwona anakwenda kwenye ziwa la moto, naye anasikia maumivu kama sisi, na anahisia zote kama sisi tulizonazo.

Lakini endapo tukikosa shabaha! Na kuanza kupambana na Yule mtu badala ya kupambana na roho iliyopo ndani yake, na kuanza kumrudishia ubaya, kuanza kumlaani, kuanza kumwombea afe…na kusema Bwana katupa mamlaka ya kukanyaga nge na nyoka kwahiyo tumkanyage yeye kweli kweli, hapo tutakuwa hatujashinda vita bali tumeshindwa vita!! Na kugeuka kuwa vyombo vya shetani.

Na unajua ni sisi tu wakristo ndio hatuna hekima katika ukristo wetu, lakini watu wa ulimwengu huu kama biblia inavyosema wana hekima katika mambo yao…Kwamfano serikali inapotangaza vita dhidi ya UMASKINI, MARADHI na UJINGA..Huwezi kuona inakwenda kupambana na wagonjwa hospitalini, huwezi kuona inaenda kuua wagonjwa na kusema tunapapambana vita dhidi ya maradhi, au huwezi kuona inakwenda kuwaua maskini wa nchi na kusema tunapambana vita dhidi ya umaskini, au huwezi kuona serikali inakwenda kuwaua au kuwafukuza watu wasio na elimu kwa kisingizio cha kupambana vita dhidi ya Ujinga, badala yake utaona itaenda kutafuta suluhisho na tiba kwa watu wake waondokane na umaskini, maradhi na kukosa elimu..Lakini sisi wakristo ndio namba moja kuuwa watu wenye magonjwa ya kiroho, umaskini wa kiroho na ujinga wa kiroho na kusema ni maadui zetu! Yaani Inaonyesha ni jinsi gani hatujielewi!!!

Wakati Fulani Bwana alipokuwa anakwenda Samaria kuhubiri, wenyeji wa mji ule walimkataa, ndipo wanafunzi wake wakamwambia tushushe moto kama Eliya uwaangamize..lakini Bwana hakufanya vile kwasababu alijua tatizo sio hao watu bali ni roho iliyo ndani yao..akawaambia wanafunzi wake Mwana wa Adamu hakuja kuangamiza roho bali kuokoa.

Luka 9: 52 “akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.

53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.

54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?

55 Akawageukia, akawakanya. [AKASEMA, HAMJUI NI ROHO YA NAMNA GANI MLIYO NAYO.]

56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”

Sasa kama Bwana hakufanya hivyo kwanini sisi tufanye hivyo?? Tutakuwa na roho gani ndani yetu??..bila shaka itakuwa ni roho ya Ibilisi!! Roho ya kuangamiza badala ya kuokoa…

Nataka nikuambie tu ndugu, nge wetu ni shetani na nyoka wetu ni shetani, hao ndio tuliopewa mamlaka ya kuwakanyaga..na hatuwakanyagi kwa maneno bali kwa hizo silaha 6 hapo juu!!..Maombi ya kuwatakia shari ndugu zako acha kuanzia leo, maombi ya kuwalaani wale wanaokuudhi acha kuanzia leo, muhubiri au mwalimu anayekufundisha hivyo anakufundisha uongo na anakuhubiria uongo!!

Tena wengine wanaaambiwa watu kabisa waandike majina ya maadui zao wayaweke kwenye maboksi wayaombee wafe!! HAYO NI MAFUNDISHO YA MASHETANI!!..Kwanini usiweke jina la adui yako kwenye boksi umwombee ampe Kristo maisha yake? Kuliko kumwombea afe!!.Fikiria ni mama yako anaombewa afe na mtu mwingine wewe utafurahia kitendo hicho?. Mambo yale tunayotaka tutendewe sisi ndio tutendee wengine Bwana alitufundisha hivyo.

Warumi 12:14 “Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.”

Ni maombi yangu kuwa Bwana atakujalia kuyaona hayo na zaidi ya hayo.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

KISASI NI JUU YA BWANA.

KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.

OKOA BADALA YA KUANGAMIZA!

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!


Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

Shalom! Karibu tujifunze Neno la Mungu,leo tutajifunza siri mojawapo ya kipekee iliyolala katika kitabu cha cha Ruthu. Kitabu hichi ni chepesi kukisoma, kwasababu ni kitabu kinachoelezea historia ya maisha ya watu zaidi kuliko unabii, hivyo nakushauri mahali ulipo chukua biblia yake ukipitie kwanza binafsi,kisha tuendelee ni kitabu chenye sura 4 fupi zinazoeleweka, hivyo ni vema ukafanya hivyo ili tuende pamoja.

Kitabu hichi kinaanzana na habari ya mtu anayeitwa Elimeleki, ambaye huyu alikuwa akiishi Israeli zamani kipindi cha Waamuzi, na biblia inatuambia siku njaa ilipokuja katika mji ule, Elimeleki alifunga safari kwenda nchi ya jirani kuishi huko yeye pamoja na mke wake aliyeitwa Naomi pamoja na wana wake wawili wa kiume..Lakini baada ya Muda kidogo mambo yalibadilika Elimeleki alikufa na kumwacha mke wake akiwa mjane na watoto wake wawili katika nchi ya ugenini..

Na Baadaye kidogo watoto wake wote wawili walibahatika kupata wake wazuri tu, lakini kwa bahati mbaya, nao pia walifariki wakiwa bado hawajapata watoto na wale wanawake, Hivyo yule mwanamke mjane Naomi hakufanikiwa kuambulia chochote, si mume, si watoto, wala si wajukuu, na hapa sasa ameshakuwa mzee sana hawezi kubeba mimba tena, hata angesema azae asingeweza tena kwani muda umeshakwenda amekaa ugenini zaidi ya miaka 10, hata hana wa kumsaidia tena, nguvu zake zimeisha kilichobakia ni kurudi tu katika nchi yake Israeli kwenda kumalizia siku zake za kuishi.

Kabla hatujaendelea mbele Embu jiulize, zamani zile za kipindi cha waamuzi kulikuwa na watu wengi mashujaa tu kama tunavyokisoma, kulikuwa na wajane wengi tu, kulikuwa na watu wengi wema tu, Hivyo habari zao zingeweza kuandikwa kama mojawapo ya kumbukumbuku nzuri kama funzo kwa ajili ya vizazi vya mbeleni, lakini ni kwanini habari za watu wengine hazijaandikwa isipokuwa za huyu mtu mmoja tu Elimeleki na familia yake ndizo zimenakiliwa hapa, na kuwekwa kama vitabu vitakatifu?..

Njia za Mungu sio njia zetu, Naomi hakufahamu kuwa japo maisha yake yalionekena kuwa ni ya bahati mbaya mbele za watu, maisha ya kusahauliwa, mtu ambaye sasa hana kumbukumbu tena, ambaye aliyekuwa amefanikiwa sana lakini sasa si kitu, hana mume,wala watoto,wala wajukuu, wala mali, wala chochote kile..hakujua kuwa kumbe Mungu alikuwa anaandika kwa kupitia maisha yake ufunuo mzito ambao ndio huo unakuja kutusaidia hata sisi watu ambao hatukustahili kupata neema za kumjua Kristo. Kwahiyo wakati mwingine maisha ya mtu yanaweza kubeba ufunuo Fulani wa Roho.

Lakini tukiendelea kusoma habari tunaona Naomi sasa anakusudia kurudi katika nchi yake mpweke,mwenye uchungu mwingi, na hapa tunaona anawaambia wale wakwe zake, ambao mwanzoni walikuwa wameolewa na watoto wake wawili kwamba kila mmoja sasa awe na amani kurudi kwa jamaa zake wakaolewe na kufanikiwa na kuishi maisha ya furaha siku zote za maisha yao.

Lakini tunaona wale wanawake wawili mwanzoni wote walikataa kumwacha Naomi peke yake, Lakini hilo halikumfanya Naomi aache kuwasihi wasifuatane naye, kwani hakutaka mtu yeyote abebe wake wowote kwa kulazimishwa, hivyo aliwabariki na kuwaomba warudi kwa jamaa zao wenyewe, lakini kama tunavyosoma habari, moyo wa Ruthu ulikuwa thabiti kuliko wa Orpa, Yeye Orpa baadaye alikubali kurudi kwa jamaa zake lakini Ruthu hakutaka kinyume chake alikuwa tayari kuambatana na Naomi popote aendapo kwa gharama zozote, alikubali kuchukuliana na gharama zote.

Tunasoma:

Ruthu 1: 11 “Naye Naomi akasema, Enyi wanangu, mrejee; kwani kufuatana na mimi? Je! Mimi ninao watoto wa kiume tena tumboni mwangu, hata wawe waume zenu?

12 Enyi wanangu, mrejee; nendeni zenu; kwa kuwa mimi ni mzee, siwezi kupata mume tena. Kama ningesema, Natumaini; kama ningepata mume hata usiku huu, na kuzaa watoto wa kiume;

13 je! Mngesubiri hata watakapokuwa watu wazima? Mngejizuia msiwe na waume? La, sivyo, wanangu; maana ni vigumu kwangu kuliko kwenu, kwa sababu mkono wa Bwana umetoka juu yangu.

14 Nao wakapaza sauti zao, wakalia tena, na Orpa akambusu mkwewe, lakini Ruthuu akaambatana naye.

15 Naye akasema, Tazama, shemeji yako amerejea kwa watu wake, na kwa mungu wake; basi urejee wewe umfuate shemeji yako.

16 Naye Ruthu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu;

17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe nami.

18 Basi alipomwona kuwa amekaza nia yake kufuatana naye, aliacha kusema naye”.

Sasa ukiendelea kusoma habari huko mbeleni utaona Ruthu alikubali kuondoka na Naomi katika umaskini wao, Ruthu asijue anapoelekea, asijue wakifika watapokelewa na nini, Ruthu akimtazama mwanamke yule kashakuwa mzee, na yeye bado ni binti kijana, ambaye anao uwezo wa kwenda kuolewa tena, ameacha vijana wazuri wenye mali katika nchi yake mwenyewe, pengine mabinti wenzake wanamkebehi wakimwambia hivi wewe umelogwa na kale kabibi?

Kwani katakupa nini? mwangalie mwenzako Orpa, aliona mbele kuwa huko hakuna tena uelekeo wa maisha, zaidi ni kuzeeshwa tu akili za wazee na kuwahudumia tu, na mwisho wa siku kuwa kama mjakazi wao..Isitoshe anakwenda mahali asipopajua, wala hajawahi kuwafahamu watu wa huko, pengine walimwambia Unakwenda kupotea tu huko na mwisho wa siku utajuta..Wewe bado binti mdogo hata bado hujazaa, unakwenda wapi?

Lakini Ruthu hakujali kuipoteza nafsi yake kuwa ni kitu cha maana sana, kuliko kujitenga na mama wa mume wake marehemu, hivyo aliendelea kufuatana naye tu katika taabu zote kama alivyoapa.

Kumbuka ni sheria iliyokuwa imetolewa na Mungu katika Israeli, kwamba mtu yeyote aliye myahudi asioe mwanamke ambaye si myahudi, kadhalika ni mwiko pia kwa mwanamke wa Kiyahudi kuolewa na mtu wa mataifa, Lakini hapa tunaona Naomi akirudi katika nchi yake mwenyewe akiwa amemwambulia mtu mmoja tu..

Pengine wale ndugu zake waliokuwa wamebaki Israeli walitazamia Elimeleki pamoja na Naomi watarudi na mali nyingi, kondoo, mbuzi, ngamia pamoja wa watoto wao na wajukuu wengi, na wajakazi wengi. Lakini hapa anaonekana Naomi peke yake, na binti mmoja wa kimataifa, na tena kibaya zaidi ni heri angekuwa kijakazi wake, lakini kumbe ni mke wa mtoto wake, jambo ambalo ni machukizo makubwa kwa Israeli.

Lakini kwa jinsi Ruthu tabia yake ilivyokuwa njema, na ya kupendeza watu wote, na kwa ukarimu wake wote aliomfanyia Naomi bibi yake,basi habari zake zikasikika katikati ya jamaa za Naomi. Na siku moja alipokuwa anakwenda kuokota masazo ya nafaka kwenye mashamba ya watu matajiri, aliingia katika shamba la mtu mmoja mkuu sana wa mji huo jina lake Boazi, ndipo Boazi akamwona na kuulizia habari zake, na kuambiwa kuwa huyu ni binti wa Naomi.

Wakati huo huo Boazi na Elimeleki mumewe Naomi walikuwa ni mtu na kaka yake. Hivyo ukiendelea kusoma habari hiyo mpaka mwisho kwa kuwa sasa hatuna nafasi ya kueleza habari yote, utaona kuwa mwisho wa siku Ruthu ambaye ni mwanamke wa kimataifa anakuja kuolewa na Boazi mtu mkuu wa Uzao wa kifalme, na ndiye kwa kupitia huyu Mfalme Daudi alitokea. Daudi ni kitukuu cha RUTHU.

Sasa kama tunavyojua mambo yote yanayotokea katika agano la kale ni kivuli cha mambo yanayoendelea katika agano jipya, habari yote ya Naomi na Ruthu, ni habari ya Kristo na bibi-arusi wake ambayo Mungu alikuwa anaichora kwa kupitia maisha ya hawa watu.

Kumbuka YESU Kristo alishuka kutoka mbinguni na utajiri mkubwa, kama Mfalme, aliyeacha enzi na mamlaka juu mbinguni, alikuja kwa watu wake Wayahudi, na hivyo alikaa nao, alikula nao,mfano tu wa Naomi jinsi alivyotoka Israeli na mumewe na watoto wake, na mali zao nyingi na kukaa katika nchi ya ugenini Moabu.

Lakini haikuwa vile kwa Naomi kama alivyotarajia, Mungu alimpiga na kumwacha pasipo kitu chochote na kubakia yeye tu alivyo. Picha kamili ya Bwana wetu Yesu kristo jinsi alivyopitia, ilimpasa yeye awe mfalme kwa wakati ule aliokuja ulimwenguni kwa mara ya kwanza lakini Mungu hakufanya hivyo kwa wakati ule, kinyume chake, alikataliwa, watu walimwona kuwa si kitu, walimtupa, walimtemea mate, walimpiga mijeledi, walizipiga kura nguo zake, walimsulibisha jaribu kufikiria mtu ambaye angepaswa awe mfalme lakini sasa anakuwa kituko kitu cha kuchekesha hana lolote tena..

Biblia inasema hivi juu yake: 

2 Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.

3 ALIDHARAULIWA NA KUKATALIWA NA WATU; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; NA KAMA MTU AMBAYE WATU HUMFICHA NYUSO ZAO, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.

4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.(Isaya 53)”….

8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; NA MAISHA YAKE NI NANI ATAKAYEISIMULIA? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.

9 Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.

10 Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake;

11 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.

12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, Na kuwaombea wakosaji…

Unaona biblia inasema maisha yake Bwana Yesu ni nani awezaye uyasimulia?..Jinsi yalivyoonekana kuwa ya ajabu mbele za watu waliomwona kama vile maisha ya Naomi. Lakini kumbe Mungu alifanyia vile Naomi kwa makusudi ili ampate RUTHU haleluya..

Angalia ni upendo mkuu namna gani huo, kumgharimu Mungu kwenda kuyaharibu maisha na raha ya mwingine, kwa ajili ya mtu mmoja asiyestahili kupata lolote asiyekuwepo hata katika mzao wa kiyahudi huko mbali katika nchi za wachawi na waabudu masanamu…Kwani hakukuwa na wanawake wazuri Israeli, wenye kumcha Mungu wakati ule, walikuwepo, lakini kwa jinsi Rehema za Mungu zilivyokuwa nyingi, alikwenda kumtafutia Boazi mke mwema katika nchi za mataifa mabovu, tena kwa kuyaharibu kwanza maisha ya Naomi kwa kunyang’anya kila kitu pamoja na watoto wake ili tu Ruthu apate mlango wa kumwendea BOAZI.

Ndugu yangu, mimi na wewe hatukustahili kuitwa bibi-arusi wa Kristo hata kidogo..Wayahudi walistahili heshima hiyo, kwani wao ndio waliochanguliwa na Mungu tangu awali, Lakini Mungu alituhurumia sisi zaidi, na kuja kutuchagua kututoa sisi katikati ya mataifa, Na zaidi ya yote hakuja kututwaa pasipo gharama, hapana bali alimtoa mwanawe wa pekee ambaye ndiye kama Naomi wetu, kuja kuteseka kupoteza kila kitu alichokuwa nacho, kupigwa, kutemewa mate kudharauliwa, kwa ajili yetu, na mwisho wa siku kufa, na kufufuka na alipofufuka alitaka sasa kurudi kwa Baba yake juu mbinguni, katika makao yake aliyotoka huko kama vile Naomi alivyotaka kurudi kwa watu wa jamaa zake.

Lakini sasa tendo la sisi kumfuata Kristo lipo mikononi mwetu, na si mikononi mwake,..Je! tutaamua kuanza naye safari ya kwenda kwa BOAZI wetu mbinguni? Au tutataka kuwa kama Orpa, kuona kuwa Naomi hana faida yoyote kwetu, Yesu Kristo hana chochote cha kutugawia, tukimfuata tutaendelea kuwa maskini, tukimfuata tutakuwa washamba, tukimfuata kampani zetu za Disco na vilabuni zitatuacha, tukimfuata vimini vyetu tutavitupa, tukimfuata, tutaonekana vibibi,. tukimfuata tutakwenda kupotea moja kwa moja na kuwa vichaa..

Ndugu fahamu kuwa huu wakati ambao Bwana ameshakulipia gharama zote, hatakuja tena kukulazimisha, bali kinyume chake atakupa uhuru wa kuchagua, je! utakuwa tayari kujitwika msalaba wako kumfuata kama Ruthu au kuendelea kubaki katika dunia kama Orpa. Ukitaka kubaki kama Orpa ni sawa lakini kumbuka BOAZI yupo Israeli anamsubiria yule aliyetayari kumtii NAOMI, na maagizo yake yote.

Hivyo huu ni wakati wako wa kupiga gharama, mambo ambayo Wayahudi wameyakosa japo walikuwa wanayatazamia tangu zamani yamepewa wewe, mfano tu wa wale wajakazi wa Boazi waliokuwa wanafanya kazi shambani mwake miaka yote, hata mmoja hakuna aliyekuja kuolewa na Boazi isipokuwa mgeni wa mbali wa Ruthu. Ni kwasababu gani?..Ni kwasababu NAOMI ndiye aliyekuwa na SIRI ya jinsi ya kumwingia BOAZI na siri hiyo alipewa Ruthu peke yako.

Na ndio maana Bwana alimaanisha kuwaambia makutana maneno haya..

Luka 9:23 “Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

24 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.

25 Kwa kuwa yamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, kama akijiangamiza, au kujipoteza mwenyewe?”.

Na alisema “Mimi ndimi njia na kweli na Uzima mtu hafiki kwa Baba ila kwa njia yake yeye

Je! leo hii utachukua uamuzi wa kumfata Kristo? kama vile Ruthu alivyojitoa kikamilifu mpaka kuwa tayari kuacha vyote alivyonavyo kwa ajili ya mkwe wake?.

Hizi ni siku za mwisho Tubu ukabatizwe, moja ya hizi siku bibi-arusi wa Kristo atanyakuliwa kwenda kwenye karamu iliyoandaliwa huko juu ya Mungu mwenyewe, watakaofika huko ndugu si kila mtu anayejiita ni mkristo halafu maisha yake yanaonyesha kabisa hajachukua msalaba wake kumfauta Kristo, mguu mmoja upo nje, mwingine ndani, watakaokwenda kwenye unyakuo ni wachache sana, ni kikundi kidogo sana mfano wa Ruthu pekee yake, wale walioamua kumfuata Kristo kikweli kweli pasipo kuangalia mbele wala nyuma, Nawe usiwe ni mmojawapo wa watakaokosa karamu hiyo. Ni heri upoteze kila kitu sasa kuliko kuikosa karamu ya mwana-kondoo.

Ubarikiwe sana

Print this post

“WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”

Kila mmoja wetu anapiga hatua, na hizi hatua tunapiga kuelekea mahali Fulani, ilikuwa juzi ikawa jana, na sasa imekuwa leo, na hiyo ipo bayana kabisa kuwa yapo mambo mazito mbele yetu yanayotusubiri , upo unyakuo mbele yetu, na kama unyakuo hatutaukuta basi kifo hatutakikwepa..Leo unaweza ukasema kesho kutwa nitafanya hivi au nitafanya vile, au mwakani nitakuwa nimeshafika mahali Fulani, lakini kumbuka hata aliyekufa jana naye sio kwamba alijua safari yake imefika, hapana na yeye pia aliiona mbele yake kuwa itakuwa hivi au vile n.k…

Mtume Paulo aliwaambia watakatifu waliokuwa Rumi maneno haya “wokovu wetu sasa upo karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini”..Unaona? Hii ikiwa na maana kuwa leo hii tupo karibu na unyakuo zaidi kuliko ilivyokuwa jana na juzi, kuliko ilivyokuwa enzi za mtume Paulo..Na kama ni hivyo basi inatupaswa sisi watu wa kizazi hiki tuwe makini kiasi gani?..Ni wazi kuwa inatupaswa tumtafute Mungu zaidi, tujishughulishe na mambo ya mbinguni kuliko wao, tuishi maisha ya kujichunga mara nyingi zaidi ya wao.

Je! Unafahamu kuwa kanisa tunaloishi ndilo kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, na kuwa baada ya hili kuisha hakutakuwa na kanisa lingine lolote? kulingana kitabu cha Ufunuo 2&3. Kanisa hili litamalizikia na unyakuo, na ndilo kanisa la 7, Tofauti lile la mitume walilokuwa wanaishi ambao lilikuwa ni kanisa la Kwanza lijulikanalo kama Efeso,

Unafahamu kuwa unyakuo utakuwa ni kwa siri sana, na si kila mtu atafahamu habari hiyo kama wengi wanavyodhani? Kwamba Kutakuwa na makelele barabarani, na maajali.? Ni kundi dogo sana litakaloondoka, kiasi kwamba ulimwengu hautajua lolote, isipokuwa kikundi kidogo sana.

Unafahamu kuwa Ile Roho ya Mpinga-Kristo tayari imeshaanza kufanya kazi, na hiyo haitendi kazi pengine popote nje ya Kiongozi mkuu wa kidini mwenye wafuasi wengi kuliko wote duniani huko Vatican Roma?

Unafahamu kuwa Injili hii unayohubiriwa moja ya hizi siku itasikika Israeli kwa nguvu na wayahudi wote wataamini, na tukio hilo ukilishuhudia basi ujue kuwa unyakuo ulishakuacha siku nyingi. Kwasababu Mungu alishaahidi kuwa atawarudia watu wake, wayahudi, na siku atakayowarudia unyakuo utakuwa umeshapita.

Kwani ule unabii waliotabiriwa juu yao kwamba watarudi katika nchi yao umeshatimia, jopo kubwa la wayahudi wamesharudi kwao, na wachache waliosalia wanarudi kwa kasi sana, wanachongojea ni kumwagiwa roho ya Neema tu.Wamwamini masihi wao waliomsulibisha. Na kisha wawe tayari kumpokea.

Takwimu zinaonyesha kuwa hakuna taifa ambalo injili ya Kristo Yesu haijahubiriwa mpaka sasa, kila mji na kila kijiji, Yesu Kristo kashatajwa,na kumbuka biblia inasema pindi tu habari njema za ufalme zitakapohubiriwa katika ulimwengu wote hapo ndipo ule mwisho utakapokuja..Unadhani ni kitu gani Mungu anasubiria sasa..

Biblia imesema mambo mengi sana juu ya yatakayotekea siku za mwisho hatuwezi kuyazungumza yote hapa, lakini moja ya dalili ya wazi kabisa ambayo hata wewe unaiona ni juu ya kutokea kwa manabii wengi wa uongo. Wimbi hili lilianza kulipuka mwanzoni mwa miaka ya 2000, lakini limekuja kukolea zaidi kuanzia kipindi cha miaka ya 2010, Hii inayoonyesha wazi ni jinsi ule mwisho unavyokuja kwa haraka sana kushinda sisi tunavyofikiri.

Ishara nyingine ni kuwa Maasi yataongeza..Leo hii tunashuhudia vitendo viovu, na vya kikatili kila mahali, mambo machafu kwenye mitandao, kila aina ya uozo upo wazi siku hizi hadharani, wala sio siri tena hata watoto wadogo hakuna kitu chochote wasichokijua kinachoendelea cha ulimwengu huu.

Biblia inasema wakati huu wa mwisho ukikaribia kufika ndipo wale watu wa kukufuru na kudhihaki watakapoongoza, wakisema iko wapi ile ahadi ya kuja kwake,.. mbona YESU harudi tumwone, miaka 2,000 imepita amekufa nini?, pamoja na hayo mithali kadha wa kadha za kejeli zimetungwa kwa watu wote wote wanaomtazamia Kristo kuja. Hata injili zenyewe zimegeuzwa sasa, hakuhubiriwi tena kuja kwa Kristo kama zamani, bali mafanikio ya kidunia. Injili shetani alizomhubiria Bwana za kumpa Milki zote za dunia endapo akimsujudia.

Na kwa bahati mbaya watu wanaangalia wakidhani kuwa siku hiyo ikikaribia kufika pengine duniani kutakuwa na vita na machafuko ya kila namna.Lakini biblia inatuambia kuwa wakati wasemapo AMANI! AMANI!, ndipo uharibifu unapokuja kwa ghafla..

1Wathesalonike 5:2 “Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.”

Na ndio maana mtume Paulo anasema:

Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa MAANA SASA WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI

12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.

13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.

14 Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake”.

Ndugu kwanini ujiweke katika hali ya hatari kama hii, leo ni siku nyingine, tumeukaribia mwisho kuliko jana, usiseme bado nipo, bado sijawa tayari, utajikuta unaangukia kifo au dhiki kuu gafla. Saa ya wokovu ni sasa,hiyo kesho hata Bwana kasema tusiisumbuke kwasababu hatujui yatakayozaliwa ndani ya siku moja. umekufikia ujumbe huu mahali ulipo, unadhani ni kwa bahati bahati tu. Jua kuwa Mungu anataka kusema na wewe ili ayabadilishe maisha yako.

Bwana anasema, laiti mwenye nyumba angelijua saa ambayo mwizi atakuja usiku basi angelikesha. Hata ingekuwa ni wewe ungefanya hivyo.Lakini kwasababu hutaki kuibiwa usiku na ndio maana kubla hujalala unahakikisha umeufunga vizuri mlango wako kwa makomeo, Sio kwasababu unapenda kujifungia hapana. Ni kwasababu unachukua tahadhari kwasababu hujui ni lini mwizi atakuja.

Halikadhalika mimi na wewe hatujui siku ya kuja kwa BWANA, kwahiyo ni wajibu wetu kukesha, kuamka usingizini, kuvua mambo yetu ya kale, kuanza maisha mapya na Mungu wetu katika kizazi hichi cha hatari tunachoishi. Lakini tunajua tu muda  umekwenda sana.

Ikiwa utataka kutubu kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako, basi Kristo atakupokea na kukuosha dhambi zako.Na ukishabatizwa katika ubatizo sahihi wa kimaandiko (yaani ubatizo wa kuzamishwa na kwa jina la YESU KRISTO), kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako(Matendo 2:38). Basi yeye mwenyewe atakutia muhuri kwa Roho wake Mtakatifu kuwa ni wake,(Waefeso 4:30) na kisha baada ya hapo utaishi katika tumaini ukijua kabisa hata leo hii mambo yakibadilika utakuwa katika upande salama Ikiwa utaendelea kudumu katika njia zake..

Pia na wewe ambaye tayari ni Mkristo kumbuka kuwa “WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”. Hivyo huu si wakati wa kulegea au kupoa,au kutazama mambo ya ulimwengu huu, bali huu ni wakati wa kuzidi kujitakasa kila iitwapo leo, maadamu tunaona siku inakaribia na kwamba muda wowote tunaweza kuitwa juu nyumbani kwa Baba. Biblia inasema “tuutimize wokovu wetu kwa kuogopa na kutetemeka Wafilipi 2:12

Ubarikiwe sana.Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA


Rudi Nyumbani

Print this post

NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!

Shalom karibu tujifunze Neno la Mungu! Katika biblia takatifu leo,tunajifunza kwa sehemu maisha ya Yesu Kristo, ambayo ni muhimu sana kwetu sisi, kwasababu ni tiba ya mambo mengi. Kama biblia inavyotuambi kwamba “inatupasa tumfahamu SANA mwana wa Mungu, hata kufikia cheo cha kimo cha utimilifu wake, ili tusiwe tena watoto wachanga wa kupelekwa na upepo huku na kule (Waefeso 4:14)”.

Tunasoma Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa akizunguka mahali na mahali, kuhubiri injili, kwa marika yote na kwa watu wa aina zote, matajiri kwa maskini, wasafi kwa wachafu, wakubwa kwa wadogo hakuchagua kundi fulani tu! bali alienenda kwa wote..Ikifutufundisha na sisi pia kwamba tunapopeleka injili hatupaswi kubagua kundi fulani… kuna watu hawapeleki injili kabisa kwa maskini, na kuna watu pia hawapeleki injili kabisa kwa matajiri, ..hilo Bwana yeye hakulifanya, kwasababu nia yake yeye ilikuwa sio kutafuta faida fulani bali kutafuta roho za watu.

Lakini tunasoma, alipokuwa anaingia kila mahali, kila mtu alikuwa anamdhania tofauti…alipoingia kwa maskini na wenye dhambi alionekana kama mlevi na mtu asiyekuwa na maana…alipoingia kwa matajiri alionekana anatafuta faida fulani labda fedha kutoka kwao…Lakini nia yake haikuwa kutafuta fedha bali kuwafanya watu watubu wamgeukie Mungu..

Mathayo 9:10-13 “Ikawa alipoketi nyumbani ale chakula, tazama, watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuja wakaketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake.

11 Mafarisayo walipoona, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?

12 Naye aliposikia, aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi.

13 Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.

Unaona hapo Bwana anasema “NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA;”…Nia ya kuingia kwa watoza ushuru ambao walikuwa ndio matajiri kwa wakati huo sio kutaka fedha au zawadi kutoka kwao, hapana bali kutaka rehema…

kwamba wajione kuwa ni wenye dhambi na hivyo watubu!!.

Wengi wetu tunadhani, Bwana ana haja sana na mali zetu tulizonazo…au ana huzuni sana na umaskini tulionao…Nataka nikuambie ndugu yangu, Bwana haji kwako ili kutaka fedha au kukupa fedha, Bwana anakuja kwako kwa ajili ya roho yako, hauzuniki kwasababu ya umaskini wako wa mwilini bali anahuzunika sana kwasababu ya umaskini wako wa rohoni, ahufurahii sana utajiri wako wa mwilini bali anaufurahia sana utajiri wako wa rohoni…

leo hii anazungumza na wewe hapa!! Ni sawa tu na amekutembelea nyumbani mwako, ANATAKA REHEMA NA WALA SI SADAKA…ndio maana alisisitiza na kusema “nendeni mkajifunze nini maana ya maneno haya”…..sentensi hiyo ina maana kuwa hawakumwelewa nia yake ya kuingia kwenye nyumba za maskini na matajiri…hivyo wanapaswa wakakae chini wakajifunze kwa utulivu, wamwombe na Mungu awafunulie, nia ya Kristo ni nini kuwaendea, vinginevyo wataishia kutokumwelewa maisha yao yote…….. Ndugu Kristo anataka utubu uache dhambi, umgeukie yeye ili akupe uzima wa Milele, hataki sadaka yako, Yeye kila kinatoka kwake,

Anataka roho yako kwasababu kuna hukumu mbeleni inakuja kwa watu wote wasiomcha Mungu, na yeye hapendi mtu yeyote apotee kama maandiko yanavyosema. Kaa chini ujifunze ujue anataka nini kwako.

Mfano mwingine tunaweza kujifunza ni wakati Bwana anaingia kwenye nyumba ya mwanamke mmoja anayeitwa Martha, Martha hakuwa Tajiri alikuwa ni mtu wa kawaida tu, na alikuwa na dada yake anayeitwa Miriamu ambaye alikuwa anaishi naye…Siku moja akasikia Bwana anataka kuja kumtembelea nyumbani kwake…Kama tunavyojua wanawake wataanza kuhangaika huku na kule mambo ya jikoni, mara kusafisha sebule, mara kufagia uwani, mara kupika mboga hii na ile, mara kutengeneza kachumbari n.k n.k unakuta shughuli zinakuwa ni nyingi mpaka wakati mgeni anafika zinakuwa bado hazijaisha…Ndivyo ilivyokuwa kwa Martha alikuwa na shughuli nyingi mpaka Bwana anafika bado zilikuwa hajazimaliza…Na mdogo wake Miriamu alipomwona Bwana kaingia akaacha kumsaidia dada yake kazi na kwenda kuketi miguuni pa Bwana akisikiliza maneno ya uzima, wakati huo Martha bado ana vishughuli shughuli vingi huko jikoni..

Pengine akawa anajaribu kumwonyesha Miriamu viishara fulani atoke pale sebuleni , ili aje akashughulike kule jikoni na wenzake..lakini yeye kakazana kumsikiliza Bwana na maneno yake. Martha akashindwa kujizuia akaanza kuzungumza na Bwana..tunasoma habari hiyo katika …

Luka 10: 38 “Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake.

39 Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake.

40 Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie.

41 Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi;

42 lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa”.

Unaona jibu la Bwana hapo??…wengi hata mimi ningeweza kusema Bwana angemkemea Miriamu kwa uvivu..lakini haikuwa hivyo kwa Bwana badala yake alimsifia mbele ya dada yake Martha…Neno ni lile lile.. “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA”… Bwana hatafuti chakula kizuri, wala maandalizi mazuri, wala sadaka za mtu, wala huduma ya mtu, wala hapendezwi sana na sifa za mtu anazompa zaidi ya Rehema, anataka Toba!! Anataka uzima wa rohoni wa mtu, Hicho ndio cha kwanza anachokihitaji!…kwa ufupi laiti Martha angeanza kwanza kwa kukaa chini na kumsikiliza maneno yake, ndipo baadaye ampikie yeye na wanafunzi wake ingekuwa sawa…lakini yeye alitanguliza huduma kabla mtoa huduma hajatoa huduma yake..na matokeo yake alimwambia “unahangaika na kujisumbua kwa mambo mengi na wakati linalohitajikwa kwa sasa ni limoja tu REHEMA!”..Kaa chini kwanza sikiliza maneno ya uzima na hayo mengine yatafuata baadaye.

Ndugu yangu jifunze ni kitu gani Kristo anataka kwako. Usihangaike, wala usihangaishwe na kutoa sadaka wakati maisha yako ni machafu, ni kupoteza muda tu!! Kristo hajaja kukitafuta hicho kwako, usijisumbue kuhakikisha hukosi kutoa fungu la kumi kila siku na hali ndani ya moyo wako kumejaa kutokusamehe, kumejaa usengenyaji,kumejaa rushwa, kumejaa uasherati, kumejaa ulevi, anasa, pornography, ndani ya moyo wako kumejaa kutokujisitiri, kumejaa masturbation, kumejaa ibada za sanamu na miungu, kumejaa safari za waganga, kumejaa wivu na mambo yote mabaya.. Usijaribu kumfanyie yeye huduma kabla yeye hajakufanyia huduma…utaishia kumhuzunisha badala ya kumfurahisha, anachotaka kwako kwanza ni moyo safi…hiyo ndiyo sadaka ya kwanza anayoikubali mbele zake, Ndio maana Bwana aliwakemea mafarisayo kwa mambo hayo hayo..

Mathayo 23:23 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache”.

24 Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia.

25 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi.

26 Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi”.

Usitafute kufunga siku nyingi, au miezi mingi…wakati ndani yako hujataka wala kukusudia kuacha dhambi (kusamehe wale wote waliokukosea na mambo mengine yote)..hiyo siyo saumu Bwana anayoitaka..swaumu Bwana anayoitaka ni hii…

Isaya 58: 3 “Husema, Mbona tumefunga, lakini huoni? Mbona tumejitaabisha nafsi zetu, lakini huangalii? Fahamuni, siku ya kufunga kwenu mnatafuta anasa zenu wenyewe, na kuwalemea wote watendao kazi kwenu.

4 Tazama, ninyi mwafunga mpate kushindana na kugombana, na kupiga kwa ngumi ya uovu. Hamfungi siku hii ya leo hata kuisikizisha sauti yenu juu.

5 Je! Kufunga namna hii ni saumu niliyoichagua mimi? Je! Ni siku ya mtu kujitaabisha nafsi yake? Ni kuinama kichwa kama unyasi, na kutanda nguo za magunia na majivu chini yake? Je! Utasema ni siku ya kufunga, na ya kukubaliwa na Bwana?

6 JE! SAUMU NILIYOICHAGUA, SIYO YA NAMNA HII? KUFUNGUA VIFUNGO VYA UOVU, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira?

7 Je! Siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako, na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? Umwonapo mtu aliye uchi, umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe?

8 Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa Bwana utakufuata nyuma ukulinde.

9 Ndipo utaita, na Bwana ataitika; utalia, naye atasema, Mimi hapa. Kama ukiiondoa nira; isiwepo kati yako, wala kunyosha kidole, wala kunena maovu;”

Ni maombi yangu Bwana atakujalia kuyafahamu hayo na zaidi ya hayo na kuyatendea kazi. Kama hujampa Bwana maisha yako kikweli kweli, mlango upo wazi lakini sio siku zote, njia ya mlango huo inazidi kuwa nyembamba kwa kadri siku zinavyozidi kwenda, njia hiyo inazidi kusongwa siku baada ya siku, jana ilikuwa rahisi kwako kuokolewa kuliko leo na itafika wakati njia itakuwa nyembamba mpaka hakutakuwa na nafasi tena ya kupita na mlango utafungwa..

Hivyo ni vyema unapoyasikia haya leo uzingatia kumrudia Mungu wako kwa kutubu na kumaanisha kuacha dhambi zako..na maisha ya kale uliyokuwa unaishi yasiyompendeza Mungu, na Bwana atakusamehe na kukukaribisha kwake. Na baada ya kutubu katafute ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38), huo ni muhimu sana, kila aliyeamini alizingatia kubatizwa. Na baada ya hapo Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu, atakayekusaidia kushinda dhambi na kukutia katika kweli yote ya kuyafahamu maandiko. Na kwa kufanya hivyo utakuwa na uhakika wa uzima wa Milele.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine na Bwana atakubariki!


Mada Zinazoendana:

UDHAIFU WA SADAKA!

SADAKA ILIYOKUBALIKA.

TOFAUTI KATIKA YA ZAKA NA SADAKA NI IPI?

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.


Rudi Nyumbani

Print this post

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

Zipo karama tofauti tofauti zilizogawanywa na Bwana katika kanisa, hizo tunazisoma katika kitabu cha 1 Wakoritho 12:4-12

4 “Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule.

5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.

6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.

8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule;

9 mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja;

10 na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;

11 lakini kazi hizizote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.

12 Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo.”

Vipawa vyote hivi Mungu hugawa kwa jinsi apendavyo yeye..hakuna mtu anayechagua awe hivi au vile, hicho huwa mtu anazaliwa nacho Mungu anakishusha juu yake yeye mwenyewe.

Na vipawa vimegawanyika katika sehemu mbili, mwilini na rohoni, vipawa vya mwilini vinapimwa katika … nguvu,ushupavu, wepesi,akili, uzuri, mbio, uwezo Fulani wa kipekee katika michezo au darasani, uchoraji, au uandishi, ubunifu, au uimbaji, wengine uongozi, wengine ualimu, n.K kuna maelfu ya vipawa hivi na kila mtu anacho cha kwake…na wakati mwingine sio lazima mtu akijue kipawa chake anaweza akawa anakifanya hata pasipo yeye kujijua…Pia wengine wamepewa viwili viwili, wengine kimoja wengine vitano..Mungu ndiye agawaye jinsi apendavyo..

Lakini leo hatuzungumzii vipawa hivyo vya mwilini tutazungumzia vipawa vya rohoni, kama tunavyosoma katika kitabu hicho cha 1 Wakorintho 12..Kumbuka vipawa vya rohoni pia mtu anakuwa anazaliwa navyo, kama tu vipawa vya mwilini, isipokuwa kama mtu hajampa Kristo maisha yake kipawa kile kinaweza kuzimwa na shetani au shetani akakitumia kwa manufaa yake mwenyewe.

Kwamfano mtu anaweza akawa amezaliwa na kipawa cha unabii, lakini kwa kuwa maisha yake ya utotoni hayakuwa ya kikristo au wazazi wake sio wakristo, au wamemweka wakfu katika madhabahu za miungu, sasa kwa kuwa shetani anakuwa na hati miliki naye asilimia 100, basi anakuwa na uwezo wa kuizima ile karama isifanye kazi yoyote…ndio hapo baadaye mtu akishakuja kumpa Kristo maisha yake na kubatizwa anajikuta anaanza kuona maono n.k ambayo hapo kwanza alikuwa hayaoni, sasa, hiyo karama sio kwamba aliipata baada ya kumpa Kristo maisha yake, hapana bali alikuwa nayo tangu alipozaliwa, isipokuwa shetani alikuwa ameizuia. Au pia shetani anaweza asiifukie bali anainyakua na kuitumia kupitisha maono yake ya uongo, mara nyingi watu wa namna hiyo wanaishia kuwa waganga wa kienyeji,wenye roho za utambuzi.

Mwingine unakuta amezaliwa na karama fulani ya uongozi, lakini kwasababu bado hajampa Kristo maisha yake, shetani anaweza akaifukia ile karama, au akaitumia kwa mambo yake, ndio hapo unakuta mtu anakuwa ni kiongozi wa vikundi haramu, au kiongozi wa mambo maovu…Na siku anakuja kumpa Kristo maisha yake kikamilifu anajikuta anachukia zile kazi mbovu na kutafuta uongozi katika kazi za Mungu, ndio hapo unakuta anaenda kuwa Mchungaji, au Shemasi n.k.

Na karama nyingine za rohoni ndio hivyo hivyo kama uimbaji, imani, uinjilisti, ualimu,uponyaji, lugha n.k. Ndio maana kuna umuhimu sana wa Mtu kumpa Yesu Kristo maisha yake na kuzingatia ubatizo sahihi ili Roho Mtakatifu apate nafasi ya kumsafisha maisha yake na kufufua kile kipawa alichokiweka ndani yake.

Sasa wapo wengi wanapenda kujua karama zao, utasikia mtu anakwambia nitaijuaje karama yangu?..mimi sijui karama yangu? Nimejaribu kumwomba Mungu anionyeshe hajanionyesha, nimefunga sana na kusali bado sijaijua n.k

Nitaka nikuambie ndugu, karama yako hutaijua kwa kuichunguza chunguza, wala Mungu hatakwambia una karama hii wala ile, ni mara chache sana Mungu mwenyewe ndio anamwambia mtu karama yako ni hii au ile, wengi wanajipachikia karama kwasababu tu wanaipenda ile karama, lakini karama ya rohoni Mungu anampa kila mtu kwa jinsi anavyotaka yeye sio kwa jinsi anavyotaka mtu. Toa kabisa kwenye akili yako hiyo karama unayodhania ni yako, kwasababu inawezekana ikawa sio yako.

Namna ya kuifahamu karama yako ni rahisi sana…Kwanza kanuni ni ile ile, kumpa Yesu Kristo maisha yako kikamilifu, ikiwa na maana kumwamini Bwana Yesu Kristo kwa ufunuo wa Roho kuwa ni Mwokozi wa Maisha yako,na kwamba alikufa na akafufuka na akapaa mbinguni, na pia anaweza kukuokoa na wewe na kukufanya kiumbe kimpya.

kisha baada ya hayo ni kufuata maagizo yake ya kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, upate ondoleo la dhambi zako na kuzingatia kuishi maisha matakatifu kuanzia huo wakati na kuendelea…Kwa kufanya hivyo utakuwa umeweza kujinasua kutoka kwenye nguvu za giza ambazo zilikuwa zimeshika karama Mungu aliyokuwa amekuwekea ndani yako.…kumbuka shetani hataki ujue karama uliyo nayo kwasababu anajua itamletea madhara makubwa sana katika ufalme wake wa giza..Kwahiyo kitu cha kwanza hatakutumia wachawi wakuloge hapana! Ondoa kabisa hiyo akilini. Bali atakutumia mapepo yatakayohakikisha wewe humpi Kristo maisha yako kikamilifu. Au yatakayo kufanya usisimame imara kwa Mungu. Mapepo YATAKAYOKUFANYA USIMWELEWE YESU KRISTO NI NANI ili yapate uhakika kuwa hutakaa uijue karama yako daima.

Pili baada ya kuzaliwa mara ya pili kwa kumpa Kristo maisha yako, bado usianze kujichunguza chunguza karama yako ni ipi…Subiri!! Usianze kusema aa labda mimi ni mchungaji, au mwalimu au nabii…usifanye hivyo hata kidogo!!! Unachotakiwa kufanya ni kwenda kujiunga na kikundi cha wakristo wenzako kanisani, au mahali unapoishi, au popote pale…kile roho anachokusukuma kukifanya pale kwenye lile kusanyiko pasipo kumwiga mtu mwingine, wala pasipo kusukumwa wala kushuritishwa kifanye hicho…na kama kinakupa amani, na endapo ukijaribu kukiacha kukifanya kinakukosesha raha..hicho hicho kifanye, msukumo huo usiuzimishe endelea nao huo huo…

Baada ya muda Fulani, labda mwezi, au mwaka, au miaka kadhaa Bwana mwenyewe atakufunulia…na atakufunulia kwa namna hii: utaanza kusikia watu wanaanza kukuita mchungaji, au wengine wataanza kukufata na kukuomba uwaongoze katika sala au katika uimbaji…au wengine wataanza kukwambia tunaomba utuombee ukiona watu wengi wanakufuata hata usiowajua wanakuomba uwaombee ni kwasababu hapo nyuma wamekuona kwa muda mrefu kila ukiombea watu wanapona..Hivyo kwa kupitia hao unajua Bwana kakupa karama ya UPONYAJI.

Wengine watakuja wakikuomba uwaongoze katika kuabudu na kusifu, utaona mara kwa mara wanakutaka wewe ufanye hivyo, ni kwasababu wameona kila unapowaongoza kwenye sifa na kuabudu uwepo wa kipekee unashuka juu yao, uponyaji unatokea, faraja zinatokea, na watu wanageuka maisha yao..kwahiyo kwa kupitia hao unajua Bwana kakupa karama ya UIMBAJI.

Wengine watakuja na kukuomba uwaulizie Neno kutoka kwa Bwana, ni kwasababu wamekuona muda mrefu unatoa unabii na unakuja kutimia,unaona maono mara kwa mara nayo ni ya kweli, kwahiyo wakajua lazima utakuwa ni nabii…hivyo kwa kupitia hao ndio utajua kuwa Bwana kakupa karama ya kinabii.

Wengine utaanza kuona wanaanza kukuita mwinjilisti..ni kwasababu wameona mazao mengi uliyoyaleta kwa Kristo katika kuhubiri kwako, tofauti na wengine, hata kama watahubiri kutwa kuchwa, hawawezi kulinganisha na uinjilishaji wako unaoweza kuwavuta watu haraka kwa Kristo. na kama ukiwachunguza utaona hawakuiti hivyo kama kwa kujipendekeza kwako au kwa kutaka kukupa sifa bali utaona ni kama kwa kumaanisha hivi.… kwahiyo hapo utaelewa kwamba Bwana alikuchagua kabla ya kuzaliwa uwe mwinjilisti wake kwa kazi yake maalumu, ya kuvuna roho za watu na kusafisha ghala la shetani.

Wengine watakuja na kukwambia tunaomba utufundishe, ni kwasababu hapo nyuma wamekuchunguza kwa muda mrefu wakajua ukiwafundisha wewe wanaelewa zaidi kuliko mwingine ndio maana wanakufuata uwafundishe, kwahiyo kwa kupitia hao unajua Bwana kakupa karama ya UFUNDISHAJI au UELEKEZAJI.

Wengine watakufuata na kukwambia tunaomba ushauri, utashangaa kila anayekufuata hataki kuombewa, wala kuwekewa mikono hata kama anatatizo kubwa kiasi gani, anataka tu umshauri, anataka tu kukusikiliza umweleze njia impasayo akitoka huyu anakuja mwingine..ujue kwamba wamekuchunguza kwa muda mrefu na kujua kwamba wewe una Hekima..Hivyo wamepata mahali panapostahili..kwahiyo kwa kupitia hao utagundua umepewa karama ya NENO LA HEKIMA. Kwaajili ya kuwajaza hekima watoto wa Mungu.

Wengine watakufuata, wengi tu hawataki kuombewa wanataka faraja tu, na wanakufuata wewe tu, hawaendi hata kwa wachungaji wala manabii, wanakutaka wewe tu, ujue ni kwasababu wameona Maneno ya faraja ndani yako…kwa kupitia hao utajua kuwa kakupa karama ya FARAJA ndani yako. Hivyo ile silaha ya Bwana katika kuwaganga wale waliovunjika mioyo imo ndani yako.

Na karama nyingine zote ndio hivyo hivyo, utazijua kutokana na ushuhuda wa watu, wanakushuhudia wewe ni nani? Mtu hawezi kwenda kwenye duka la madawa kununua unga wa ngano, au hawezi kwenda hardware kununua dawa ya meno kila duka na bidhaa za aina yake..wateja ndio watakaosema pale utapata hichi, na pale kile…Usitafute kujipachikia karama kwa kujitazama au kwa kutafuta sifa Fulani au kwa kuona kwasababu karama ile inapendwa na wengi ngoja na mimi nijipe. Huko ni kujikweza ambapo Bwana Yesu alisema ajikwezaye atashushwa na ajishushaye atakwezwa.

Kila mmoja Mungu kamuumba na upekee wake, sio lazima sauti yako ifanane na ya Yule, kuhubiri kwako kuwe sawa na kwa Yule, hata Mungu japo alituumba kwa mfano wake, lakini lakini alimpa kila mmoja sura yake tofauti japo wote ni wanadamu. Vivyo hivyo na katika karama zake, alimpa kila mmoja wetu karama tofauti na hata ikitokea wawili au watatu au mia wanakarama moja, basi biblia inasema upo utofauti wa utendaji kazi, utendaji kazi wa huyu hauwezi ukawa sawa na wa Yule kwamba kila kitu wafanane hapana ukiona hivyo basi ujue ipo roho ya ufuasi nyuma ya huyo mtu.

Na lengo la hizo karama za rohoni ni tofauti za zile za mwilini, karama za mwilini nyingi zina lengo la kumpatia mtu riziki au kumfanya aishi katika dunia hii, au kumpa Mungu utukufu, mtu anakuwa na kipaji cha kukimbia ili akimbiapo apate tuzo itakayokuwa kama ni sehemu yake ya kupatia kipato, lakini karama za rohoni hazipo kwa lengo hilo…karama zote za rohoni ni kwa kusudi la kulijenga kanisa, kuwafanya watakatifu wawe wakamilifu, na kuwahudumia roho zao, na zote zinakuwa na lengo moja la kuwasafisha watu na kuwatengeneza kwa ajili ya kwenda mbinguni.

Kwahiyo ukiona msukumo wowote ndani yako unakuja kwa lengo la kwenda kujipatika kipato! Hiyo siyo karama ya Roho Mtakatifu, achana nayo ni kutoka kwa Yule mwovu. Karama za Mungu ni kwaajili ya kuujenga mwili wa Kristo na kuwatengeneza watakatifu. Utauliza hilo tunalipata wapi katika maandiko..soma.

Waefeso 4.11 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;

12 KWA KUSUDI LA KUWAKAMILISHA WATAKATIFU, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;

13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu”

Na Karama ambayo shetani anapenda sana kuwanasa watu wengi ni karama ya kinabii na uimbaji.. Hizi karama mbili ndizo karama ambazo shetani anajua watu wengi wanazipenda, wengi wanapenda kuitwa nabii nabii na wengi wanapendwa kuitwa waimbaji maarufu…. Kwasababu wanapenda umaarufu pamoja na fedha..nataka nikuambie ndugu yangu, asilimia kubwa ya wanaoimba miziki inayoitwa ya injili na manabii…ni waimbaji wa uongo na manabii wa uongo..

Kwanini ni manabii wa uongo na waimbaji wa uongo?? Jibu lipo hapo juu kwenye waefeso 4:12…je! WANAWAKAMILISHA WATAKATIFU??...au wanawaharibu watakatifu kwa mavazi yao na mienendo yao, na mafundisho yao?? JE! WANATUFIKISHA KATIKA CHEO CHA KIMO CHA UKAMILIFU WA KRISTO??...au wanatupeleka katika cheo cha kimo cha kumfahamu shetani? Wanachoimba na wanachokiishi kinawafanya watu watubu, au kuwafundisha watu chuki?

Ni matumaini yangu kuwa Bwana atakujalia kuyafahamu haya na zaidi ya haya. Na hatimaye kuifanya kazi yake kwa uaminifu katika Karama sahihi aliyoiweka ndani yako.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post