Si jambo la kawaida mwanadamu kula Udongo!.. Hivyo inapotokea mtu anakula udongo kupitiliza, basi hilo laweza kuwa tatizo la kiroho zaidi ya kuwa tatizo la kisayansi..
Ndio zipo tafiti chache zinazoonesha kuwa mwanamke anapokuwa mja mzito anaweza kuwa na hamu ya kula udongo, na pia mtu aliyepungukiwa na madini Fulani mwilini anaweza kula udongo..
Tafiti hizi zaweza kuwa kweli kwa sehemu, lakini inapotokea Mtu chakula chake kinageuka kuwa udongo, na wengine hata baada ya kumaliza kubeba ujauzito bado wanaendelea kula udongo, na hata kwenda kununua basi hilo ni tatizo la kiroho Zaidi.
Kwasababu maandiko yanasema anayekula mavumbi/udongo ni nyoka tu peke yake.
Mwanzo 3:14 “Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, NA MAVUMBI UTAKULA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKO”
Hivyo kama unaona unalo tatizo la kula udongo kwa kiwango cha kushindwa kujizuia, basi ipo roho inayokutumikisha katika hilo, kama tu vile roho ya kujichua, hivyo suluhisho kwanza ni kumkaribisha BWANA YESU katika maisha yako, kwa kutubu na kumaanisha kuacha dhambi, kisha kutafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU, na baada ya hapo hiyo roho itaondoka yenyewe na utarudi kuwa mtu wa kawaida.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TATIZO LA VISIGINO KUUMA KIBIBLIA
JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?
TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.
Jibu: Turejee.
Isaya 1:31 “Na mtu hodari atakuwa kama MAKUMBI, na kazi yake kama cheche ya moto; nao watawaka pamoja, wala hapana atakayewazima”.
“Makumbi” ni malighafi yoyote inayotumika katika kuanza au kuchochea moto, mfano; mbao, vijiti au nyasi kavu.
Katika kitabu hiko cha Isaya, biblia imemtaja mtu hodari kwamba siku hizo atakuwa si kitu bali kama tu vijiti vishikavyo moto na kuteketea.
Isaya 1:28 “Lakini kuharibika kwao wakosao nao wenye dhambi kutatokea wakati mmoja, nao wamwachao Bwana watateketezwa.
29 Kwa maana watatahayarika kwa sababu ya mialoni mliyoitamani, nanyi mtaaibishwa kwa sababu ya bustani mlizozichagua.
30 Maana mtakuwa kama mwaloni ambao majani yake yakauka, na kama bustani isiyo na maji.
31 Na mtu hodari ATAKUWA KAMA MAKUMBI, na kazi yake kama cheche ya moto; nao watawaka pamoja, wala hapana atakayewazima”.
Bwana hata sasa atusaidie tusimwache, bali tuzishike amri zake na maagizo yake ili tusiteketee kwa moto wake.
Yeremia 5:11 “Maana nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamenitenda kwa hiana sana, asema Bwana.
12 Wamemkataa Bwana, na kusema, Si yeye; wala hayatatupata mabaya; wala hatutaona upanga wala njaa;
13 na manabii watakuwa upepo, wala neno lake halimo ndani yao; basi ndivyo watakavyotendwa.
14 Kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wa majeshi, asema hivi, Kwa sababu mnasema neno hili, tazama, nitafanya maneno yangu katika KINYWA CHAKO KUWA MOTO, NA WATU HAWA KUWA KUNI, NAO MOTO UTAWALA”
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JIBU: Baada ya Yesu kukutana na wale wenye ukoma kumi, na kuwaagiza waende kujionyesha kwa makuhani
biblia inatuonyesha walipokea uponyaji wote wakiwa bado wapo njiani, lakini tunaona yule mkoma mmoja hakuendelea na safari yake. Palepale ilimbidi ahairishe kwanza safari yake Na kuja kumshukuru Yesu, na ndipo pengine aendelee na safari yake ya kuelekea kwa makuhani.
Luka 17:14-19
[14]Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
[15]Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;
[16]akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
[17]Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?
[18]Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?
[19]Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.
Kwanini afanye vile ni kwasababu aliona umuhimu wa kumshukuru Yesu Kristo kwanza zaidi ya wahudumu wake.
Jambo lolote Mungu analotaka kututendea kupitia wahudumu wake..Tujue kuwa Shukrani zetu za kwanza zinapaswa zimrudie yeye.
Amina.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14
Rudi Nyumbani
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Je Bwana YESU alipanda mlimani na wanafunzi wake baada ya siku ngapi?..ni Sita au Nane?, Kwa maana katika Mathayo 17:1 na Marko 9:2 panaonyesha ni baada ya siku sita (6) lakini tukisoma Luka 9:28 panaonyesha ni siku ni nane (8) Je ukweli ni upi?.
Jibu: Turejee mistari hiyo..
Mathayo 17:1 “Na baada ya SIKU SITA Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani”
Hapa ni kweli tunasoma “Siku sita” na Marko 9:2 tunasoma vile vile ni siku sita (6).
Tusome tena Luka 9:28..
Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata SIKU NANE, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba”.
Hapa tunasoma ni siku nane (8) na si sita tena, swali ni je! Biblia inajichanganya?, au mwandishi mmoja amekosea?
Jibu ni La! Biblia haijichanganyi na wala hakuna mwandishi aliyekosea, wote wapo sawa na maneno yote ni hakika, kwasababu biblia ni kitabu kilichohakikiwa na Roho Mtakatifu mwenyewe na hakina makossa (Mithali 30:5).
Sasa kama ni hivyo kwanini panaonekana kuna tofauti ya siku?..
Mwandishi wa kitabu cha Luka alionyesha jumla ya siku walizokaa mlimani, na Mwandishi wa kitabu cha Mathayo na Marko wakaonyesha siku walizoondoka katika makazi yao na kuelekea mlimani.
Sasa ni kwamba baada ya Bwana kuwaambia wanafunzi wake kuwa wapo ambao hawataonja mauti hata watakapoona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu, zilipita siku sita akawachukua wanafunzi wake baadhi (ambao ni Petro, Yohana na Yakobo) akapanda nao mlimani.
Na biblia haijaeleza katika hizo siku sita kabla ya kupanda mlimani walikuwa wanafanya nini au walikuwa wapi, pengine waliachana kidogo, au walikuwa katika huduma zilizowatenga kwa muda siku sita, mpaka ilipofika siku hiyo ya kupanda mlimani….hiyo yote haijaeleza lakini inasema tu baada ya siku sita alipanda nao mlimani, na ndicho Mwandishi Mathayo na Marko walichokieleza.
Lakini sasa Luka yeye hakulenga kuelezea siku waliyopanda mlimani, kwamba ni baada ya siku sita za yale maneno, bali yeye alisema “YAPATA SIKU NANE”… Hilo Neno “Yapata” ni neno la ujumla, likielezea Muda wa safari Nzima, kuwa ni SIKU NANE (8), Maana yake baada ya siku sita walipanda mlimani sawasawa na Mwandishi Mathayo na Marko na kule mlimani walikaa siku mbili (2), na kufanya jumla ya siku kuwa nane, ndicho mwandishi alichokilenga. (kwahiyo muda waliokaa mlimani ni siku mbili, lakini walipanda baada ya siku sita).
Kwahiyo biblia haijajichanganya hapo, bali ni uelewa wetu ndio unaojichanganya.
Je umempokea BWANA YESU?.. Na je unajua kuwa dalili zote zinaonyesha kuwa kizazi tulichopo ni cha mwisho?..Je umejiandaaje? Taa yako inawaka?
Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;
36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na
Je bado unaendelea na maisha ya dhambi?, bado unakunywa pombe?, bado unazini, bado unajichua, bado unavaa kidunia?
Muda umeisha, msikilize Roho Mtakatifu, na usizisikilize roho zidanganyazo.
1Timotheo 4:1“Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani”
Maran tha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TABIA SITA (6) ZA WANAFUNZI WA YESU.
KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?
Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?
Ayubu 38:1
[1]Ndipo BWANA akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,
JIBU: Tukumbuke kuwa Mungu ana njia nyingi za kuzungumza na watu. Na kila njia huwa na maana fulani nyuma yake.
Utakumbuka Alipokutana na Musa alizungumza naye katika kijiti kinachoungua lakini hakiteketei..Kuwafundisha wana wa Israeli kuwa atakuwa pamoja nao hata katika moto wa majaribu lakini hawatateketea kabisa..
Kwamfano akina Shedraki, Meshaki na Abednego, walipojaribiwa kwa kutupwa tanuruni, hawakuungua au Danieli kwenye tundu la simba, hakupatwa na dhara lolote kwasababu walimtumaini Mungu.
Kutufundisha kuwa hata sasa, na sisi tuliomwamini Kristo, hakuna jaribu la aina yoyote linaloweza kutufanya sisi tuangamie na kupotea mbali na uso wa Mungu. Kwasababu yeye yupo nasi sikuzote.
Halikadhalika tunaona na hapa pia anamtokea Ayubu katika upepo wa kisulisuli..
Kisulisuli hutafsirika kama aina nyingine ya janga, mfano tu wa gharika au tetemeko. Kazi ya kisulisuli huwa ni kuzomba vitu dhaifu labda makapi, au vitu ambavyo havina msingi imara…
Isaya 40:24
[24]Naam, hawakupandwa; hawakutiwa katika ardhi kama mbegu; naam, shina lao halikutia mizizi katika ardhi; tena awapuzia tu, wakanyauka, upepo wa kisulisuli wawaondoa kama mabua makavu.
Hivyo Mungu kutumia njia hii, ni kumwonyesha Ayubu kwamba hata katika zomba-zomba za kiroho yeye yupo huko na watu wake.
Vitu vyote vya Ayubu vilizombwa, Kuanzia mali, watoto,.mifugo, hadi mke wake kwasababu ya udhaifu wa imani akazombwa na hila za shetani. Wao wakidhani kuwa Mungu amewaacha kumbe alikuwa nao daima. Tufahamu kuwa dhoruba, tufani, giza, au mwanga..vyote kwake ni sawasawa.
Lakini pia kuna wakati Mungu anazungumza katika utulivu. Utakumbuka tena habari ya Eliya wakati ule anamfuata Mungu kule mlima Horebu, akitarajia Mungu aseme naye katika fujo. Lakini hakumwona Mungu, katika matetemeko wala moto, bali katika sauti ndogo ya utulivu.
Kuonyesha kuwa Mungu husema nasi pia katika utulivu.
1 Wafalme 19:11-12
[11]Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za BWANA. Na tazama, BWANA akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za BWANA; lakini BWANA hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini BWANA hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;
[12]na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini BWANA hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.
Hivyo ikiwa umeokoka na umesimama imara na Bwana ni vizuri kufahamu kuwa nyakati zote, Mungu yupo nasi. Ni kawaida watu wakishapitia changamoto fulani hufikiri kuwa Mungu hayupo nao, kumbe sivyo nyakati zote nm ziwe za majaribu, za visulisuli, za mafuriko n.k. Tunapaswa tumwone yeye,.kwasababu yupo pamoja na sisi.
Kwasababu ndiye msaada wetu.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani