Mara nyingi Mungu wetu akitaka kutupa ujumbe, au kumpa mtu ujumbe huwa anazungumza na sisi kwa mifano, au kwa ishara, na mifano hiyo inatusaidia kuzielewa vizuri hisia zake kwetu au kwa kitu fulani..…Kwamfano utaona Daudi alipowaacha wanawake waliokuwa wengi katika nchi yake na kwenda kumchukua mke wa Uria, utaona kabla Bwana hajampa ile adhabu alimpa mfano kwanza ambao ulimsaidia kuelewa kwa undani hisia ya Mungu juu yake kwa kile alichokifanya.
Hebu tusome kidogo,
2 Samweli 12:1 “Ndipo Bwana akamtuma Nathani aende kwa Daudi. Naye akamwendea, akamwambia, Palikuwa na watu wawili katika mji mmoja; mmoja wao alikuwa tajiri, wa pili maskini.
2 Yule tajiri alikuwa na kondoo na ng’ombe wengi sana;
3 bali yule maskini hakuwa na kitu, ila mwana kondoo mmoja, mdogo, ambaye amemnunua na kumlea; naye akakua pamoja naye, na pamoja na wanawe; hula sehemu ya posho lake, na kukinywea kikombe chake, na kulala kifuani mwake, akawa kwake kama binti.
4 Hata msafiri mmoja akamfikilia yule tajiri, naye akaacha kutwaa mmoja wa kondoo zake mwenyewe au mmoja wa ng’ombe zake mwenyewe, ili kumwandalia yule msafiri aliyemfikilia, bali alimnyang’anya yule maskini mwana-kondoo wake, akamwandalia yule mtu aliyemfikilia.
5 Ndipo hasira ya Daudi ikawaka sana juu ya mtu yule; akamwambia Nathani, Aishivyo Bwana, mtu huyo aliyetenda jambo hili, hakika yake astahili kufa;
6 naye atamrudishia yule mwana-kondoo mara nne, kwa sababu ametenda neno hili, na kwa sababu hakuwa na huruma.
7 Basi Nathani akamwambia Daudi, Wewe ndiwe mtu huyo. Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nalikutia mafuta, uwe mfalme juu ya Israeli, nikakuokoa na mkono wa Sauli;
8 nami nikakupa nyumba ya bwana wako, na wake za bwana wako kifuani mwako; nikakupa nyumba ya Israeli na ya Yuda; na kama hayo yangalikuwa machache, ningalikuongezea mambo kadha wa kadha.
9 Kwa nini umelidharau neno la Bwana, na kufanya yaliyo mabaya machoni pake? Umempiga Uria, Mhiti, kwa upanga, nawe umemtwaa mkewe awe mke wako, nawe umemwua huyo kwa upanga wa wana wa Amoni.
10 Basi, sasa upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa sababu umenidharau, ukamtwaa mkewe Uria, Mhiti, kuwa mke wako.
11 Bwana asema hivi, Angalia, nitakuondokeshea uovu katika nyumba yako, nami nitawatwaa wake zako mbele ya macho yako, na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako mbele ya jua hili.
12 Maana wewe ulifanya jambo lile kwa siri; bali mimi nitalifanya jambo hili mbele ya Israeli wote na mbele ya jua”.
Na sehemu nyingine nyingi katika biblia, agano la kale na agano jipya utaona Mungu anazungumza kwa mifano kufikisha ujumbe wake au hisia zake kwa watu wake.
Lakini pia Mungu wetu anatumia mifano kutuonyesha hisia zake pindi tunapotubu na kumgeukia yeye… Wengi wetu hatujui ni jinsi gani Mungu anavyohisi juu yetu, na anavyotuhurumia, hususani pale tunapoghairi maovu yetu na mabaya yetu na kugeukia haki, wengi tunadhani Mungu huwa hasamehi, na anakumbuka kumbuka makosa yetu mara kwa mara…Hebu chukua muda tafakari ule mfano wa mwana mpotevu, Bwana alioutoa katika Luka 15:11-32, utaona jinsi gani Huruma za Mungu jinsi zilivyo kuu kwetu pindi tunapotubu na kuacha maovu.
“Luka 15:20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena.
22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;
23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;
24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.”
Vilevile Sio mifano tu, hata katika ishara Mungu anazungumza na watu wake, kasome kitabu cha Ezekieli mlango wa 4 na wa 5 na Isaya 20:3.
Sasa hebu tuitazame ishara ya mwisho ambao tutazidi kufahamu hisia ya Mungu juu yetu pindi tunapogeuka na kutubu.
Kama wewe ni msomi wa biblia utakuwa unaijua vizuri habari ile ya Nabii Yona, jinsi alivyoikimbia sauti ya Mungu na mwishowe kujikuta yupo katika tumbo la nyangumi siku tatu, na baadaye kulazimika kuitii sauti ya Mungu na kwenda kuwahubiria watu wa Ninawi..Na alipowahubiria biblia inasema walitubu na kuacha njia zao mbaya..Na kwa tendo lile Mungu aliwasamehe na kughairi kuwaangamiza…Lakini kitendo kile cha Mungu kuwasamehe hakikumpendeza Nabii Yona, kwani alitafakari mateso aliyoyapitia yote na shida zote zile mpaka za kukaa tumboni mwa samaki siku tatu, na mwishowe Mungu hafanyi chochote?..yeye alitamani watu wauawe…Lakini hisia za Mungu hazikuwa hizo..yeye aliwahurumia watu wake, lakini Yona hakujua ukubwa wa huruma na hisia za Mungu juu ya watu wa Ninawi mpaka Mungu alipozungumza naye tena kwa ishara nyingine ya Mtango.
Kwani alipokuwa amekaa kwa mbali autazame mji ukiangamizwa, Mungu aliuotesha mtango ambao uliota ndani ya siku moja, ukawa na matawi yenye uvuli, na kwasababu jua lilikuwa kali na Yona alikuwa na hasira na uchungu.. alipouona ule mtango akaenda kukaa chini yake, apate kivuli, na pengine pia ale matango mawili matatu asahahu shida zake, na alipozidiwa na burudani za mtango ule siku nzima, akasahau habari za Ninawi na kuangamizwa kwake.
Lakini biblia inasema siku ya pili yake alivyoamka mambo yalibadilika, ule mtango uliliwa na buu na jua ukaupiga ukakauka, Yona kuona vile akakasirika tena..Hasira yake ikarudi kama mwanzo..kwanini mtango umekauka ambao ndio uliokuwa unamfanya asahau shida zake na apunguze hasira zake.
Kwa tukio hilo Mungu akampa somo Yona…kama vile ule mtango ulivyomfanya asahau shida zake na hasira zake kwa uvuli tu wa matawi yake, pengine na kwa matunda yake yaliyouzaa ndani ya siku moja, na ukamfanya pia auhurumie ule mtango..(Yona 4)
Ni hivyo hivyo watu wa Ninawi kwa kutubu kwao ni kama mtango ulioota juu ya kichwa cha Mungu, ambapo hapo kwanza Mungu aliwakasirikia watu wa Ninawi kwa maovu yao, lakini walipotubu na kuacha njia zao mbaya ni kama mtango ulioota juu ya kichwa cha Mungu, ukampa utulivu ndani ya moyo wake, na kumfanya asahau na kughairi mabaya aliyopanga kuwaletea watu wa Ninawi.
Hivyo kila siku tunapoghairi mabaya yetu, ndipo matawi yetu mbele za Mungu wetu yanavyoongezeka, na tunapozidi na kuzidi kuwa wasafi na hata kufikia hatua ya kuzaa matunda ndipo tunapomfanya Mungu wetu aburudike na kusahau mabaya yetu yote…Lakini tunapozidisha uovu, ni tunayapunguza wenyewe matawi yetu na hivyo dhambi zetu zinafika kwake na kumghadhibisha…
Hivyo Mungu wetu anatupenda na kutuhurumia…kuna uhusiano mkubwa sana wa matendo yetu na hisia za Mungu wetu..hivyo tujitahidi kuupendeza moyo wake ndipo tutakapata mema…kila siku tujisafishe, kama tulikuwa tumeacha matusi lakini bado vitabia vidogo vidogo vya ugomvi, vinatutawala tuvisafishe na hivyo..ndivyo tunavyozidi kujiepusha na hasira ya Mungu.
Mungu wetu anatupenda, Mungu wetu anatuhurumia na bado tunayo nafasi kubwa kwake.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.
Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?
Shalom.
Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”.
Biblia inatuambia biblia inatumia Neno “majeshi” ikimaanisha ni mengi na pia yapo makundi makundi, na inatumia pia neno “wabaya”.Ikimaanisha wanafanya kazi mbaya..
Sasa kabla ya kufahamu ni kwa namna gani yanafanya kazi, ni vizuri kwanza kujua Malaika watakatifu huwa wanafanya kazi gani kwa wanadamu. Kwasababu mapepo hapo kabla ya kuasi walikuwa ni malaika,hivyo baada ya kulaaniwa ndipo yakawa mapepo, na baadhi yao yakatupwa duniani, mengine yakapelekwa kwenye vifungo vya giza (2Petro 2:4),..Sasa haya yaliyopo duniani, hayafanyi kazi nyingine, Zaidi ya kuzitazama zile kazi za malaika watakatifu na kwenda kinyume nazo basi..
Ni mara chache sana mapepo yakitaka kumshambulia mtu, yanakwenda moja moja, huwa yanakwenda kama jeshi, yakisaidiana, kwasababu mbinu hiyo yaliwaiga malaika watakatifu..
Soma Habari za Elisha jinsi yule mtumishi wake, alivyofunguliwa macho na kuona majeshi ya malaika watakatifu yamewazunguka..
Utagundua pia na mapepo nayo yanafanya hivyo hivyo, utaona yule mtu aliyekuwa kule mlimani, uchi, Bwana alipoyaulizwa jina lao, yakasema, Legioni, maana yake tupo wengi (jeshi).
Hivyo ni vizuri kujua kazi ya malaika watakatifu duniani..Nao kazi yao kuu ni hii..KUWAHUDUMIA WATAKATIFU.
Hivyo, mapepo sikuzote ni kunyume na malaika..
Sasa kazi kuu ya malaika watakatifu duniani kama tulivyosema, si nyingine Zaidi ya KUWAHUDUMIA WATAKATIFU..Soma..
Waebrania 1:13 “ Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako?
14 Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?”
Unaweza kuona hapo malaika watakatifu hawajaagizwa kuwahudumia kila mtu tu duniani, isipokuwa wale watakatifu..kumbuka huduma, ni utumishi, malaika hawawatumikii watu waovu, bali watakatifu tu..
Sasa mapepo haya, kwasababu lengo lao sikuzote ni kwenda kinyume na malaika wa Mungu, nao pia wanafanya kazi ya kihuduma ya kuwaharibu watakatifu..na si watu wengine waovu kwasababu hao tayari walishapotea zamani..Mtu mwovu hashambuliwi na mapepo bali anatumiwa na mapepo kufanya kazi zao.
Hivyo ukiokoka leo, majeshi ya mapepo wabaya yanaanza huduma ya kutafuta njia ya kukuangusha uache wokovu. Hiyo ndiyo agenda yao ya kwanza…Hivyo ni vizuri ukajua namna ya kuyadhibiti, ili wokovu wao uwe na matunda na udumu.
Mambo ya kufanya unapooka ni lazima uwe mtu wa.
1) KUSALI: Bwana anasema..
Mathayo 2:41 “Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”. Hakuna namna unaweza kuzidhibiti/kuyashinda hizo roho kama si mtu wa maombi…
2) KUJIEPUSHA NA UOVU: Maovu, yanauficha uso wa Mungu, Hivyo inapelekea pia na malaika wa Bwana kuondoka, matokeo yake ulinzi wa Mungu unaondoka juu yako, na mapepo yanachukua nafasi ya kukuangusha.(Isaya 59:1-2 )
3) KUJIFUNZA NENO: Neno la Mungu likikaa kwa wingi ndani yako unakuwa na maarifa ya kutosha ya kumshinda ibilisi (Wakolosai 3:16). Kumbuka Kristo alimshinda shetani kwasababu Neno la Mungu lilikuwa kwa wingi ndani yake.
4) KUFANYA USHIRIKA NA WENGINE: Kukutanika na wengine, kanisani, kwenye vikundi vya maombi, kwasababu ukiwa peke yako upo hatarini shetani kukupindua lakini mkiwa wengi, ni ngumu ibilisi kukupata..(Waebrania 10:25).
Mhubiri 4:11 “Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?
12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi”.
Hayo ni mambo makuu yatakayokusaidia kujikinga na majeshi haya, na kuyakaribisha majeshi ya Malaika wa Mungu yatembee nawe.
Kumbuka shetani Pamoja na malaika zake( yaani mapepo), wanafahamu kuwa muda wao ni mchache sana. Hivyo wanaongeza bidii katika kufanya kazi ya kuwaangusha watakatifu.
Sasa endapo mtu asipojibidiisha, na kukaa kuendelea na Maisha ya kawaida ya siku zote, baada ya kuokoka , ni ngumu mtu huyo kushindana na hayo majeshi ya mapepo, Utarudi tu nyuma kama sio kuucha wokovu kabisa.
Hivyo tuongeze bidii, na kuzingatia hivyo vigezo.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kuna nguvu katika mzaliwa wa pili.
Shalom, jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe,
Biblia inasema Israeli ni Mzaliwa wa kwanza wa Mungu..
Kutoka 4: 22 “Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni MWANANGU MIMI, MZALIWA WA KWANZA WANGU;
23 nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako”.
Kama kuna mzaliwa wa kwanza maana yake kuna mzaliwa wa pili..Na kama vile mzaliwa wa kwanza hapo biblia imelitaja ni Taifa la Israeli..maana yake mzaliwa wa pili ni mataifa mengine yaliyosalia…Na hiyo ni sababu Taifa la Israeli ndio limekuwa la kwanza kushiriki Baraka za Mungu kabla ya sisi watu wa mataifa…Sababu pekee ndio hiyo, kwamba lenyewe ndio mzaliwa wa kwanza, kumjua Mungu.
Itakuwa ni ajabu watoto wa mwisho katika familia wanakuja juu na kuanza kumlaumu mzazi wao kwanini kaka yao amekuwa wa kwanza kunyonya kabla yao?, na kwanini wamerithi nguo za kaka yao na viatu vyake, lakini kaka yao hakurithi vyao? N.k Ukiona mtoto ananung’unika kwa ajili ya hayo basi kuna uwezekano akili yake haijakomaa vizuri…kwasababu kama ingekuwa imekomaa vizuri ingekuwa ni rahisi sana kujua ni kwanini kaka yake kamtangulia kwa kila kitu….angejua ni kwasababu kaka yake ndio kazaliwa wa kwanza na kisha yeye ndio akafuata…hiyo ndio sababu ya kipekee na hakuna nyingine.
Halikadhalika leo hii tutauliza ni kwanini Mungu aliwachagua kwanza Israeli na kuwapa upendeleo ?..Jibu ndio hilo hapo juu la Kutoka 4:22 kwamba Israeli ni MZALIWA WA KWANZA. Hivyo hana budi kunyonya baraka za Mungu kabla yetu, hana budi kuvivaa viatu vipya, na sisi watu wa mataifa tutakapozaliwa baadaye tutavirithi vile vile viatu..Ndio maana tunatumia kitabu cha biblia agano la kale ambalo limejaa Maisha ya Wana wa Israeli tu ili kujifunzia njia za Mungu.
Lakini ipo siri nyingine kubwa juu yetu sisi watu wa mataifa, ambao hatukuchaguliwa kuwa wazao wa kwanza. Na siri hiyo ipo katika msalaba.
Kwa kupitia Yesu Kristo, sisi watu wa mataifa, wakati wetu ulipofika wa kuzaliwa tulipata baraka mara dufu Zaidi ya wana wa Israeli. Bwana Yesu alitufanya sisi ambao hapo kwanza tulionekana kuwa sio warithi,..akatufanya kuwa warithi..Kwasababu urithi siku zote ulimhusu mzaliwa wa kwanza tu.
Waefeso 2:12 “kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani.
13 Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo.
14 Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga”.
Umeona ni Neema ya namna gani hiyo?..Mimi na wewe hatukustahili kuitwa warithi, waliostahili kuitwa warithi ni jamii ya Wana wa Israeli peke yao, kwasababu wao ndio wazaliwa wa kwanza, lakini sasa sisi watu wa mataifa ni warithi kupitia msalaba wa Yesu Kristo…
Yakobo ulipofika wakati wa kuwabariki wana wa Yusufu, ambapo alitakiwa mkono wa kuume auweke juu ya mzaliwa wa kwanza na ule wa kushoto juu ya mzaliwa wa pili, kinyume chake mikono yake aliipishanisha kama ishara ya msalaba na ule wa kushoto akauweka juu mzaliwa wa kwanza na wa kuume juu ya mzaliwa wa pili(Mwanzo 48:8-17). Siri hiyo ni kubwa sana.
Tendo hilo lilikuwa ni ufunuo wa msalaba, kupitia msalaba Baba yetu wa mbinguni alitubariki sisi tuliokuwa wa uzao wa pili, baraka ambazo zingestahili kupokewa kwa mzao wa kwanza yaani wana wa Israeli. Ni neema kubwa sana tuliyopewa, ambayo hatupaswi kuipuuza hata kidogo..
Je bado unaupuuza msalaba?..je bado upo bize kutafuta fursa za fedha kuliko kutafuta kujua siri zilizopo katika msalaba?..Kumbuka urithi ambao wana wa Mungu wameahidiwa ni mbingu mpya na nchi mpya…Katika mbingu hiyo na nchi hiyo, hakuna kuumwa, hakuna kuteseka, hakuna dhiki, hakuna njaa..hakuna mwanzo wa siku wala mwisho..Milele na milele Watoto wa Mungu watang’aa na kuishi bila tabu wala dhiki, wala majuto..kwa ufupi biblia inasema kuna mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia tuliyoandaliwa.
Ni maombi yangu kuwa injili ya msalaba haitakuwa upuuzi kwetu..Kabla Biblia inavyosema katika..1Wakorintho 1:18 “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu”.
Kama hujaokolewa leo ni siku yako..huu sio wakati wa kutanga tanga na kushabikia udhehebu au udini uliokuwa nao..Kumpa Yesu Maisha yako sio dini mpya wala dhehebu jipya..ni Neno la Mungu..Hii neema ya msalaba tuliyoipokea ya kufanyika warithi haitadumu milele, ipo siku itaisha, na Neema hii inatufundisha kuukataa ubaya…maana yake ni kwamba ukiwa mwasherati, mzinzi, mwizi, mlevi, mtukanaji, mtoaji mimba, msagaji na mambo mengine yote yanayofanana na hayo yasiyompendeza Mungu, bado hujaingia katika neema hii, hivyo unahitaji kuingia katika Neema hii..
Kama upo tayari kufanya hivyo leo..basi uamuzi unaoufanya ni wa busara, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kujitenga dakika kadhaa peke yako na kuomba rehema mbele za Mungu kwa yote uliyoyafanya yasiyompendeza yeye…na dhamiria kutoyafanya tena kwa vitendo, tubia kwa dhati kabisa uasherati wako na usiufanye tena, usagaji wako, utoaji mimba uliokuwa unatenda, ukahaba, uvaaji nusu uchi kikahaba, wizi, utukanaji na mambo mengine yote ya siri..Na Bwana atakusamehe kwasababu yeye ni mwenye huruma na mwingi wa rehema, endapo umedhamiria kweli kwa dhati kuacha hayo matendo maovu uliyokuwa unayafanya.
Baada ya hapo, usikawie haraka sana katafute ubatizo sahihi kama hujabatizwa…kipengele hichi ni cha muhimu sana..Ingekuwa ni mimi mwanadamu natoa maagizo ya kupokea wokovu ningekiruka labda pengine kisingekuwa na maana sana kwangu, lakini sivyo kwa Mungu, kitendo hichi cha ubatizo kina maana sana kwake..hivyo akaagiza kwamba kila aaminiye ni lazima akabatizwe, hata mimi linalihusu agizo hili, hata mchungaji yoyote yule, hata Paulo lilimhusu, zaidi sana Bwana wetu yeye mwenyewe alikuwa kielelezo alikwenda kubatizwa..Hivyo hatupaswi kupuuza hata kidogo, nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu Kristo, ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, ikiwa kweli umemaanisha kutubu na kumwishia Kristo, ukiona jambo hilo ni mizigo kwako, ni wazi kuwa bado hujatubu kwa kumaanisha..Lakini ukizingatia hilo Bwana atakupokea kabisa na Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia.
Na hapo utakuwa umekamilisha wokovu wako na kuzaliwa mara ya pili kulingana na maandiko.Kumbuka tunaishi katika siku za mwisho na majuto makuu yanakaribia kuja ulimwenguni kote kwa wale wote watakaomkataa Kristo. Bwana atusaidie mimi na wewe tusiwe miongoni mwao. Hizi ni nyakati za mwisho kweli kweli, wala si mzaha..
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kuna watu wawili ambao tunaweza kujifunza leo katika ile safari ya Bwana Yesu kuelekea Yeriko, Biblia inatuambia kulikuwa na mkutano mkubwa wa watu waliokuwa wakimfuata, kumbuka wote hao kila mmoja alikuwa anatamani Yesu amuhudumie binafsi, walikuwa ni watu wenye matatizo mbalimbali, wengine matatizo ya familia zao, wengine biashara, wengine magonjwa, wengine walimfuata kwa lengo tu la kumwona Yesu n.k.
Sasa katikati ya umati mkubwa wote huo wa watu, waliokuwa wanataka kuhudumiwa, Bwana alikutana na watu wawili wa kipekee..
Mtu wa kwanza:
Alikuwa ni Yule maskini kipofu..tusome habari yake:
Luka 18:35 “Ikawa alipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya njia, akiomba sadaka;
36 na alipowasikia makutano wakipita, aliuliza, Kuna nini?
37 Wakamwambia, Yesu wa Nazareti anapita.
38 Akapiga kelele, akisema, Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.
39 Basi wale waliotangulia wakamkemea ili anyamaze; lakini yeye alizidi sana kupaza sauti, Ee Mwana wa Daudi, unirehemu.
40 Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia, alimwuliza,
41 Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona.
42 Yesu akamwambia, Upewe kuona; imani yako imekuponya.
43 Mara hiyo akapata kuona, akamfuata, huku akimtukuza Mungu. Na watu wote walipoona hayo walimsifu Mungu”.
TAFAKARI: Huyu alikuwa ni kipofu, haoni, wala hakuwa na namna yoyote ile ya kumfikia Kristo ili ahudumiwe, lakini alikuwa wa kwanza kuhudumiwa na kumwona Kristo kwa karibu kuliko watu wote waliokuwa wanamfuata YESU tangu mbali, watu wenye macho, na wenye miguu, na wenye masikio, hata mmoja hakumteka YESU.
Mtu wa PILI:
Alikuwa ni Zakayo; Huyu alikuwa ni tajiri, lakini alifahamu utajiri wake usingemsaidia kumwona Yesu, licha tu ya kumkaribia..Na alipojaribu kupitia kutumia nguvu, walau kupiga vikumbo ili amwone tu Yesu, bado ilishindwa kutokana na ufupi wake.. Hivyo kwa namna ya kawaida kama kukata tamaa angepaswa awe ameshakataa tamaa siku nyingi..lakini turudie kusoma tena..
Luka 19:1 “Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.
2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.
3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.
4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.
5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako.
6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha”.
Kama tunavyosoma, alikwenda mbele akapanda juu ya mkuyu. Na Yesu alipopita alikuwa wa kwanza kumwona, na kumwita, akawashinda hata watu wengi ambao walikuwa warefu, wenye mbavu, wepesi..
Jambo gani tunaweza kujifunza:
Watu wengi tunafikiri madhaifu yetu ndio kikwazo cha sisi kutomkaribia Mungu, au kutokuwa watumishi wa Mungu..Tunaishia kusema, Ahh! Yule si ni kwasababu amezaliwa katika familia ya kikristo, au Yule si ni kwasababu anayo pesa ya kutosha kuendesha huduma, au Yule si ni kwasababu anayo miguu miwili ya kuhubiri injili..Au Yule si ni kwasababu ni kijana, au mtu mzima n.k.
Tunavisingizio vingi lakini hatujui, watu wanaonekana haiwezekani kumfikia Yesu kwa madhaifu yao,ndio wanaokuwa wa kwanza kufaidika na yeye, kama hawatakata tamaa katika kumtafuta kwa bidii katika hali zao hizo hizo.
Utashangaa siku moja Bwana anamfanya kuwa mchungaji, au mwinjilisti, wa jamii kubwa ya watu ambao tangu zamani walikuwa wanajiita ni wakristo.. lakini yeye hakuwa hata na dalili za kuwa mkristo, katokea katika jamii wa waabudu miti, au wachawi.
Hivyo katika hali uliyonayo ambayo pengine inakufanya ujione ni kikwazo cha wewe kumfikia Mungu, hupaswi kuvunjika moyo endelea kupaza sauti kwa Bwana, panda kabisa juu ya mkuyu mtafute Bwana kwa bidii, usiwaangalie waliokutangulia katika imani, wewe fanya kwa nafasi yako. Utashangaa tu wakati utafika utakuwa wa kwanza kuhudumiwa na Kristo, zaidi ya hao unaodhani wanamjua Mungu tangu zamani.
Sasa mambo hayo hayawezekani kama hujaokoka. Hivyo kama upo nje ya Kristo, huu ndio wakati wako wa kumkaribisha mwokozi moyoni mwako, Hivyo tubu kwa kumaanisha dhambi zako, kisha ukabatizwe, kisha Bwana atakupa Roho Mtakatifu, na kuanzia huo wakati na kuendelea, Kristo ataelekeza macho yake kukutazama wewe kwanza.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Bwana Yesu alimaanisha nini aliposema; Mafarisayo Hupanua HIRIZI zao, na kuongeza MATAMVUA yao?
Shalom, Jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Neno la Mungu..Ni muhimu kila mmoja wetu kuzaliwa mara ya pili na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, na kazi ya Roho Mtakatifu ni kutufanya sisi kuwa watakatifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyo mtakatifu..(1Petro 1:16).
Na kazi nyingine ya Roho Mtakatifu juu yetu ni kututumia sisi kuwavuta wengine kwa Kristo, na anaposhuka juu ya mtu anampa kipawa au karama…Karama hiyo ndiyo inayomtofautisha yeye na watu wengine..Haiwezekani watu wawili wakawa wanafanana asilimia mia..wanaweza kukaribiana huduma au karama lakini wasifanane asilimia mia. Hivyo ni muhimu sana kutojilinganisha na mwingine, wala kutotamani kuwa kama mwingine..
Kwamfano hebu tuichunguze karama ya kinabii kwa kujifunza juu ya manabii wa Bwana waliowahi kupita katika agano la kale….Tujifunze juu ya hawa manabii watatu MUSA, DANIELI na ISAYA.
Hawa watatu walikuwa ni manabii wa Bwana…na biblia inawaita wote ni manabii lakini kama ukichunguza kwa makini utaona kila mmoja alikuwa ni nabii kwa namna yake.
Tukianza na Musa, huyu hakuwa anaona maono ya siku za Mwisho, hakuwa anaona mambo yatakayokuja kutokea katika siku za mwisho kama vile siku ya Bwana, au hukumu ya mwisho wa dunia, hukumu ya wanadamu n.k Lakini Roho wa Mungu ajimtia mafuta mahususi kumfunulia torati, sheria ya Mungu, sheria za makuhani, na kumfahamisha yale yaliyotokea zamani..na alimtia mafuta kuwa kiongozi wa Taifa teule la Mungu, kuwatoa utumwani Misri na kuwapeleka nchi ya ahadi kaanani.
Lakini tukimtazama Nabii Danieli, huyu hakuwa anatembea na Mungu kama Musa…Musa alikuwa anaonana na Mungu uso kwa uso lakini Danieli hakuwa hivyo… Mungu alikuwa anamwonyesha Danieli mambo yatakayokuja kutokea siku za mwisho, kama kunyanyuka kwa mpinga Kristo, kunyanyuka kwa falme zitakazokuja kutawala dunia, kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu na kujengwa kwa hekalu..mambo ambayo Musa pamoja na uhusiano wake wote na Mungu hakuonyeshwa.
Hali kadhalika tukirudi kwa Nabii Isaya…Huyu naye hakuwa kama Musa wala Danieli…Huyu Bwana Mungu alimwonyesha zaidi mambo yajayo ambayo yatatokea baada ya mwisho wa dunia, alionyeshwa mambo yatakayotokea wakati wa utawala wa miaka 1000, alionyeshwa zaidi unabii kuhusu Ujio wa Bwana Yesu na kuzaliwa kwake kwa uwazi zaidi kuliko manabii wengine wowote..Kabla ya Nabii Isaya hakukuwa na nabii yoyote aliyejua kuwa Masihi atazaliwa na bikiri, au Bwana Yesu atasulubiwa na kuchinjwa kama mwana kondoo, wala hakuna aliyejua kwamba Masihi atapigwa kwaajili ya dhambi zetu hata Nabii Musa hakuwa analijua hilo..japokuwa alikuwa anauuona uso wa Mungu.
Hatuna muda wa kutosha wa kumwangalia Nabii Yohana Mbatizaji jinsi Roho Mtakatifu alivyomtumia tofauti na manabii wengine wote, hatujamtazama Nabii Ezekieli na Hosea jinsi Mungu alivyowatumia kama ishara..hawa walikuwa wanaambiwa waoe wake wa kizinzi, wengine wale kinyesi, wengine walala upande mmoja kwa siku nyingi..Hatujamtazama Eliya na Elisha jinsi Mungu alivyowatumia kitofauti na manabii wengine.
Eliya hakutoa unabii wowote kuhusu ujio wa Masihi, wala mwisho wa dunia lakini alitabiri mambo yaliyokuwa yanatokea papo kwa hapo..na zaidi ya yote kwa ishara na maajabu mengi..
Sasa manabii wote tuliowatazama hapo juu Biblia inawaita MANABII WA BWANA…Lakini wote hawakuwa wanafanana…Na ndio hivyo hivyo kwa Wachungaji, wainjilisti, waalimu, mitume, waimbaji, wenye karama ya Imani, wenye karama za masaidiano, wenye karama za neno la hekima na maarifa n.k… Wote hawafanani.
1Wakorintho 12:4 “Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule.
5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.
6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana”.
Hivyo tunajifunza ni muhimu kukaa kila mtu katika nafasi yake..kwasababu kamwe hatuwezi kufanana..Katika karama moja kuna utendaji kazi hata elfu moja tofauti tofauti…
Sasa tatizo linakuja ni mtu kutamani kuwa kama mwingine, …Unapotamani kuwa kama mwingine vilevile, ni uthibitisho tosha wa kuiua karama iliyopo ndani yako, Kwasababu kamwe hatuwezi kufanana..hata wale mapacha wanaofanana sana ukizidi kuwachunguza utaona wanao tofauti..na unavyozidi kukaa nao ndio kabisa utaona wanatofautiana sana…hiyo ikionyesha kwamba katika nafasi zetu sisi wanadamu Mungu hajawahi kutuumba tukafanana asilimia mia kama vile sisimizi wanavyofanana..
Hivyo karama Mungu aliyoiweka ndani yako ni ya kipekee tofauti na ya mwingine, na Roho ameiweka ndani yako kwa makusudi yake ya kuwavuta wengine kwake. Hivyo tembea katika kile Mungu alichokiweka ndani yako.
Bwana atusaidie sana kuzifahamu na kuzithibitisha karama zetu ili tusimzimishe Roho ndani yetu…
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Maran atha!
Mada Nyinginezo:
Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?
Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
JIBU: Tusome
2Wakorintho 12:7 “Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi.
8 Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke.
9 Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu.”
Kumekuwa na mtazamo mingi juu ya mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo, wengine wanabaki kudhani ni mwiba halisi kabisa uliwekwa ubavuni mwake, kwamba kila anapojaribu kujivuna basi unamtoboa..wengine wanasema ni kumbukumbu ya yale mambo mabaya aliyoyafanya kule nyuma hivyo Mungu alikuwa anamletea yale mawazo yanamsononesha na hivyo yanageuka kuwa kama mwiba kwake na anaacha kujivuna.
Lakini, katika hayo yote, tukiutazama tena kwa ukaribu ule mstari wa 7, unasema Mungu alimwekea mwiba katika mwili wake “Mjumbe wa shetani”..Hilo Neno mjumbe, ni Neno linalomaanisha mtu na sio mawazo fulani au kitu fulani. Hata katika akili ya kawaida mwiba wa kijiti una uhusiano gani na kujisifu?..Hivyo hapo Paulo hakuzungumzia kijiti cha mwiba au ugonjwa fulani katika mwili wake bali alikuwa anamzungumzia mtu fulani, ambaye ndiy aliyekuwa kama mwiba kwake…
Sasa swali lingine utauliza mbona kasema ni katika mwili na sio katika roho?..Jibu ni kwamba Neno mwili linaweza kumaanisha maisha ya mtu au watu…Hebu soma mistari ifuatayo Bwana aliyokuwa anawaambia wana wa Israeli tutazidi kuelewa..
Hesabu 33: 55 “Lakini kama hamtaki kuwafukuza wenyeji wa nchi watoke mbele yenu; ndipo hao ambao mtakaowasaza watakuwa kama sindano machoni mwenu, na kama miiba ubavuni mwenu, nao watawasumbua katika hiyo nchi ambayo mwakaa.
56 Kisha itakuwa, kama nilivyoazimia kuwatenda wao, ndivyo nitakavyowatenda ninyi”.
Waamuzi 2: 3 “Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu”.
Umeona hapo?..maisha ya mtu yanaweza kufananishwa na mwili, na mtu anayekusumbua na kukutesa katika maisha yako anaweza kufananishwa na mwiba mwilini mwako…
Lakini tukirudi kwa Mtume Paulo, huyu mtu ambaye alikuwa ni mwiba kwake alikuwa ni nani?
Tukisoma.. 2Timotheo 4:14 inasema..
“Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake.
15 Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.”.
Biblia haijatoa habari zake ndefu juu ya huyu Iskanda, mfua shaba. Lakini inatueleza alikuwa kikwazo kikubwa sana wa Paulo, katika maisha yake na katika huduma yake.. Hajiatumia neno “Ubaya ” tu bali imetumia neno “Ubaya mwingi”.Kuashiria ni matendo mengi mabaya huyu Iskanda alimwonyesha Paulo.
Pengine, alikuwa anamzungia Paulo kwa ubaya tu wakati wote, alikuwa anazungumzia mapungufu yake tu, jinsi alivyokuwa muuaji huko nyuma (akiwaua na kuwatesa wakristo), akimshuhudia na maneno mengine ya uongo mbele za watu waliokuwa wanamwamini Paulo..Na hiyo ikawa inamfanya Yule Paulo ambaye anasifika kwa mafunuo mengi, na miujiza mingi, na huduma kubwa, kuonekana kuwa sio kitu katikati ya baadhi ya watu waliokuwa wanamwamini.
Hilo si ajabu kuliona hata leo unaweza kuliona kwa viongozi wengi wa nchi, Mungu anawanyanyulia wapinzani kama mwiba kwao, ili wazungumze mabaya yao tu, au mapungufu yao, haijalishi kiongozi huyo atakuwa amefanya mambo mangapi mazuri ya kimaendeleo kiasi gani. Mungu anaruhusu hayo ili kiongozi huyo asijivune kupita kiasi.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Paulo kwa huyu Iskanda mfua shaba alikuwa mwiba mkubwa kwake, mpaka akamwomba Mungu amwondolee (amwue),
Soma:
1Timotheo 1:20 “Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu”.
lakini Mungu alimwambia Neema yake yamtosha..Hivyo aliendelea kubakia nao, mpaka wakati wake ulipokwisha.
Vivyo hivyo na sisi, tukiwa watu wa kujivuna, kujiona sisi ni kitu Fulani, kisa tumepiga hatua kuliko wengine, au tuna kitu kikubwa kuliko wengine. Tukumbuke kuwa Bwana anaweza kutunyanyulia miiba, kututweza..
Shalom.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?
IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.
FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.
JE! TUNAPASWA KUUAMINI UNABII WA SYLVIA BROWNE?
Je kuweka mapambo kama mikufu, vikuku na kutoboa pua ni dhambi?
Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?
JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?
Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?
Jambo linalotupa wengi kiburi ni kufikiri kwamba miili hii tuliyonayo ni mali yetu wenyewe..Lakini kama mtu ukitenga muda na kutafakari kwa kina utakuja kugundua kuwa mwili ulionao hauna mamlaka nao asilimia mia, na hivyo huo ni uthibitisho kwamba si mali yako kabisa..
Kama mwili ungekuwa ni mali yako ungekuwa na uwezo wa kujichagulia kimo, au rangi au jinsia…ungekuwa pia na uwezo wa kuyazuia mapigo ya moyo yasidunde pindi unapotaka, au ungekuwa na uwezo wa kuzuia damu isizunguke mwilini au mwili usitoe jasho wakati wa joto linapozidi kuwa kali. Lakini kama mojawapo ya mambo hayo huwezi basi ni uthibitisho kwamba huo mwili ni mali ya mtu mwingine ambaye wewe humjui. Kwa ujumla sio milki yako binafsi…Kama biblia inavyosema..
1Wakorintho 6:19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE”
Kwasababu hiyo basi ndio maana ni lazima tuishi chini ya amri za mwenye miili hii…akisema miili hii haipaswi kufanywa kituo cha dhambi..basi tunatii kwasababu sio mali yetu..akisema hatupaswi kuitumia kwa zinaa, au ulevi, au uasherati basi ni lazima tutii kwasababu sio ya kwetu ni yake yeye. Sisi ni wageni waalikwa au wapangaji tu ndani ya hii miili yake..Hatuna uhuru asilimia 100 wa kuiweka tunavyotaka sisi. Akisema hatupaswi kuivisha mavazi yapasayo jinsia nyingine, hatupaswi kuhoji kwanini au kwasababu gani.
Sasa hebu tujifunze Zaidi juu Mmiliki wa hii miili tuliyonayo.
Kuna wakati Bwana wetu Yesu aliulizwa swali lifuatalo na Mafarisayo…
Mathayo 22:17 “Basi utuambie, Waonaje? Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo?
18 Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?
19 Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari.
20 Akawaambia, NI YA NANI SANAMU HII, NA ANWANI HII?
21 Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, NA MUNGU YALIYO YA MUNGU”
Ukisoma mstari huo wa 20 utaona Bwana anawauliza maswali mawili..1).Ni ya nani sanamu hii? Maana yake ile sura juu ya ile sarafu ni sura ya nani?…2).Na ni ya nani anwani hii?. Na wote wakajibu ni ya Kaisari..na yeye Bwana akawaambia vya Kaisari mpeni Kaisari na vya Mungu mpeni Mungu..
Sasa swali linakuja, vya Mungu ni vipi hapo?…Ndio vinaweza kuwa navyo pia ni fedha, (kama sadaka, zaka au malimbuko)..lakini hebu leo tuingie ndani Zaidi kujifunza vilivyo vya Mungu ni vipi.
Turudi kusoma kitabu cha Mwanzo..
Mwanzo 1: 26 “Mungu akasema, Na tumfanye MTU KWA MFANO WETU, KWA SURA YETU; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.
Mpaka hapo utakuwa umeona vya Mungu ni vipi?…Miili yetu ndio vya Mungu tunavyopaswa tumpe..kwasababu miili yetu ndio imebeba SURA na MFANO wa Mungu…Kwahiyo kama Bwana alivyowaambia watu wampe kodi Kaisari kwasababu tu sarafu ile imebeba sura yake na anwani yake..zaidi sana tunapaswa tumpe Kristo miili yetu kwasababu imebeba sura na mfano wa Mungu..
Kwahiyo tunapaswa tujipime kila siku je hii miili yetu tunaiweka jinsi Mungu anavyotaka?…Je tunaiweka katika utakatifu, je tunaishughulisha katika kufunga na kuomba na kuifikisha kwenye nyumba za Ibada?..Kama hufanyi hivyo, kila ukifika muda wa kuomba unasema umechoka!..ukifika muda wa kufunga unasema unaumwa, ikifika siku ya kwenda kwenye ibada unasema unapumzika…Kumbuka utatoa hesabu siku ile kwa mwenye huo mwili.
Kama unautumia mwili huo kuufanyia uzinzi, au uasherati…jitafakari sana, kama unafikiri ni mali yako hiyo anza kujitafakari tena upya, kama unafikiri una uhuru wa kuitembeza bila mavazi au kuichubua, au kuiweka kila aina ya matangazo anza kujitafakari tena upya, kama unafikiri ni ya kupokea mimba na kutoa tu jinsi utakavyo hilo nalo lifikirie…
Bwana atusaidie daima..
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu”,(Mwanzo 1:26)?
JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.
CHAPA YA MNYAMA
Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
CHUKIZO LA UHARIBIFU
KAMA TUNATAKA KUWA ASKARI WA BWANA, NI LAZIMA TUJUE VIGEZO.
Kwanini kabila la Dani limeondolewa kwenye Ufunuo 7?
Jina la Bwana Yesu libarikiwe ndugu yangu..Karibu tuyatafakari kwa pamoja maneno ya uzima,
Biblia inasema..
Isaya 29:15 “Ole wao wanaojitahidi kumficha Bwana mashauri yao, na matendo yao yamo gizani, nao husema, Ni nani atuonaye? Nani atujuaye?.
Mungu hapa anatupa onyo sisi tunaodhani kuwa kwa nguvu zetu wenyewe tunajitosheleza kuyaendesha maisha yetu,..tunasema hakuna haja ya Mungu kuingilia mipango yetu..hatuhitaji kumwomba Mungu, kwani yeye ni nani mbona hatumwoni akituongozea kitu chochote, Sasa ya nini kumuhusisha katika mambo yetu., Tunaweza tusiseme hivyo kwa midomo lakini moyoni mwetu tunawaza hivyo,..
Leo ninataka kwenda kuoa/kuoelewa ya nini nimwombe Mungu kuhusu mchumba mwema, wacha nikatafute tu anayevutia machoni pangu..Leo ninataka kufungua biashara mpya wacha nifanye tu yoyote nipendayo hata kama si halali ya nini kumshirikisha Mungu, leo nimepataka kazi nzuri ya nini kupelekea sadaka ya shukrani kanisani kwa aliyonitendea..Leo ninapokea mshahara mzuri, ninapata faida kubwa, ya nini kutoa fungu la kumi kwa kila mapato yangu, tendo hilo linaniongezea nini mimi?..Ya nini kuwapelekea wale wachungaji wapiga-dili wanaowaza kula sadaka zetu tu kila siku?…
Ukiamka asubuhi unachowaza, ni mipango yako tu, unasema hakuna Mungu,..,.Lakini unajua kabisa ukiumwa leo karibu na kufa utataka msaada kutoka kwa Mungu, unajua kabisa ukifa leo katika dhambi hujui utajikuta upande upi, unajua kabisa, upo mashakani kwa hofu za magonjwa, ajali, vifo vya ghafla n.k lakini bado kwako wewe habari za Mungu ni kama habari wa wajinga..za watu waliokataa tamaa za maisha, watu maskini, watu wasiokuwa na elimu, watu wavivu wa kufikiri..walioathiriwa na dini za wazungu,..Hivyo ndivyo unavyoyachukulia masuala ya imani.
Ndugu, Bwana anasema Ole,.. kumbuka sisi wanadamu ni mvuke tu ndugu, tushushe viburi vyetu dunia hii sio yetu, hata pumzi tulizonazo si zetu, ni kama tu tumekopeshwa na muhusika. Sasa kwanini uishi tu kama utakavyo?
Yakobo 4:13 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida;
14 walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka.
15 Badala ya kusema, Bwana akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi.
16 Lakini sasa mwajisifu katika majivuno yenu; kujisifu kote kwa namna hii ni kubaya”.
Tunapoishi maisha ya kama vile Mungu kwetu ni mtu-baki, hana umuhimu wowote, tujue kabisa tupo hatarini. Pale unapokutana na maneno ya Mungu halafu unatoa maneno ya mzaha,mzaha tu,au kejeli ni ujasiri gani unaokusukuma ufanye hivyo?
Unapokutana na Neno la Uzima, halafu unatukana, ni faida gani unapata, unaposhindana na sauti ya Mungu, hujui unajiharibu mwenyewe…Ayubu 40:2 “Je! Mwenye hoja atashindana na Mwenyezi? Mwenye kujadiliana na Mungu, na ajibu yeye”.
Kwasababu unaona Mungu amekaa kimya hafanyi chochote, ndio unajiamulia kuishi maisha unayotaka wewe,maisha yako yapo gizani, unaendelea kufanya dhambi kwa sirisiri ..Mungu amekuacha pasipo kujijua ndugu…Zaburi 81:12 “Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao”
Mithali 1:29 “Kwa kuwa walichukia maarifa, Wala hawakuchagua kumcha Bwana.
30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote.
31 Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.
32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”
Ndugu, hata sisi tulikuwa hivyo tu lakini siku tulipoona haya maisha ni tambara bovu, tulimpokea Kristo na sasa tumeokolewa tunamtumaini na kumtegemea yeye, na mashauri yetu yote yapo kwake.
Na wewe leo, badilisha aina ya maisha unayoishi, mguekie Kristo, au kama ulikuwa ndani ya Kristo na umemsahau Muumba wako kwa kiwango hicho, ni wakati sasa wa kujinyenyekeza na kumkabidhi njia zako zote na mashauri yako yote,
Mithali 16:3 “Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika”.
Hizi ni nyakati za kumalizia, tupo ukingoni kabisa wa muda, Kristo yupo mlangoni kurudi..Mguekie Yesu Mkuu wa uzima ayatawale maisha yako..Usimfiche mashauri yako, usimfiche chochote, hakikisha kila jambo lililo mbele yako Mungu ndio mshauri wako wa kwanza, hakikisha hufanyi chochote bila Bwana kuwa kiongozi wako.
Yeremia 17:7 “Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.
8 Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda”.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
CHUKIZO LA UHARIBIFU
VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA
IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!
USIJITAFUTIE KULAMBWA NA MBWA KWA DHAMBI YA KUTAMANI.
JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.
MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?
Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?
SWALI: Mstari huu una maana gani?…
Mithali 26:4 “Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Usije ukafanana naye.
5 Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Asije akawa mwenye hekima machoni pake”.
JIBU: Katika huo mstari hilo neno “sawasawa” jinsi lilivyojirudia mara mbili..ndilo linalochanganya..lakini tukitafakari kwa kina tutagundua kuwa hilo Neno halijichanganyi, lipo sawasawa.
Sasa kabla ya kuendelea mbele hebu tujifunze mtu mpumbavu ni mtu wa namna gani,
Mpumbavu ni mtu asiyeweza kupambanua mambo vizuri hususani ya ki-Mungu. Mtu ambaye bado anafuata mambo ya ulimwengu au ambaye haamini kuhusu Mungu ni mpumbavu kulingana na biblia, kwasababu bado hajaweza kupambanua vizuri elimu ya maisha, ambayo ni kumjua muumba wake, na kuepukana na uovu….Hiyo ndiyo elimu ya kwanza ambayo kila mwanadamu anapaswa awe nayo..kwasababu hata wanyama na ndege kwa sehemu fulani wanayo. Wanajua kuwa kuna muumba..
Zaburi 14:1 “Mpumbavu amesema moyoni Hakuna Mungu”..
Na neno “upumbavu au mpumbavu” kama linavyotumika kwenye biblia sio tusi….bali ni hali mtu aliyonayo ya kushindwa “kupambanua mambo” kama tulivyotangulia kujifunza.
Sasa mtu asiyemjua Kristo anapokutana na wewe unayemjua Kristo na kukutukana matusi, na wewe unapomjibu kwa kurudisha matusi…hapo wewe na yeye hamna tofauti..wote wawili mmefanana na ni wapumbavu…hiyo ndio maana biblia inasema usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake ili usije ukafanana naye.
Lakini kama amekutukana…na wewe uliye ndani ya Kristo, ukatambua Yule mtu tatizo lake ni dhambi ndani ya moyo wake, na hivyo kulingana na biblia ni mpumbavu, na anamhitaji Yesu ili upumbavu wake uondoke…na hivyo kwa hekima ukaanza kumjibu kwa na kumuelekeza njia iliyo sahihi kwa upole na utaratibu..hapo atakapoona wewe umemzidi hekima, hujamrudishia tusi kama yeye alivyokutukana, yeye atajiona hana hekima..na hivyo atachomwa dhamira yake na kushawishika kugeuka kuacha njia yake mbaya.
Au pale mpumbavu anapotoa maneno ya kukulaani, lakini wewe ukambariki hapo ni sawa na umemjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,
Ambapo kwa tendo hicho kitamfanya ajione hana hekima machoni pake mwenyewe.
Ubarikiwe.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAP
Mada Nyinginezo:
FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.
Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?
MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.
UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.
Hapa ana maana gani kusema hivi? ” Usiseme moyoni mwako,Ni nani atakayepanda kwenda Mbinguni? (yaani ni kumleta Kristo chini), “au,Ni nani Atakayeshuka kwenda Kuzimu? (yaani, ni kumleta Kristo juu,kutoka kwa wafu.). {Warumi10:6-7.}
Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?
Paulo alimwambia Timotheo atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lake, Je! tunaruhusiwa na sisi pia kutumia pombe?
USIINGIE MKATABA NA DHAMBI.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Lipo tukio ambalo, wengi wetu tunalijua lihusulo yule kijana aliyepagawa na mapepo, ambapo tunaona baba yake alimchukua na kumpeleka kwa mitume wa Yesu, lakini walishindwa kulitoa lile pepo, lakini baadaye kidogo walipomwona Bwana anashuka milimani, baba yake yule kijana alimkimbilia Bwana, na kumwambia nisaidie mwanangu, nilimleta kwa wanafunzi wako lakini hawakuweza kumtoa..
Ndipo Bwana Yesu akawaambia wamlete kwake, sasa alipofika tu kwake, mambo yalikuwa nje ya matarajio ya watu wengi waliokuwepo mahali pale.. Embu tusome tena Pamoja Habari hiyo kwa utaratibu, lipo jambo jipya naamini tutalipata mwisho wa Habari hiyo.
Marko 9:17 “Mtu mmoja katika mkutano akamjibu, Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo bubu;
18 na kila ampagaapo, humbwaga chini, naye hutoka povu na kusaga meno na kukonda; nikasema na wanafunzi wako wamtoe pepo, wasiweze.
19 Akawajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, nikae nanyi hata lini? Nichukuliane nanyi hata lini? Mleteni kwangu.
20 Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa, akitokwa na povu.
21 Akamwuliza babaye, Amepatwa na haya tangu lini? Akasema, Tangu utoto.
22 Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia.
23 Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.
24 Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
25 Naye Yesu akiona ya kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi, mimi nakuamuru, mtoke huyu, wala usimwingie tena.
26 Akalia, AKAMTIA KIFAFA SANA, akamtoka; naye AKAWA KAMA AMEKUFA; hata wengi wakasema, Amekufa.
27 Lakini Yesu akamshika mkono akamwinua naye akasimama”
Kama tunavyoona ule mstari wa 26 anasema, pepo yule akalia, halafu akamtia kifafa sana, Neno “sana” sio kitendo cha kawaida, ukitaka kujua si kitendo cha kawaida utaona kwa mahangaiko yake mtoto yule na kelele zake kuliwasababisha mpaka watu waliokuwa mbali wasogee karibu, wakisema kuna nini pale? Wakawa wanakuja kwa kasi..wengine walidhani pengine mtu anaungua moto, au kapewa sumu,..pengine baba yake yule kijana akafikiri mbona sasa hali hii ndio imekuwa mbaya Zaidi kuliko mwanzo..wale watu wengine wakafikiri na wao, afadhali alivyokuwa mwanzo, huyu mtu ndio kaharibu kabisa mambo, hali yake imekithiri zaidi..
Tengeneza picha, Na kibaya Zaidi ni kitendo kilichofuata cha yule kijana kutulia baada ya muda mfupi, akawa hapepesi midomo tena kama mtu mwenye kifafa anavyofanya siku zote, wala macho, wala haonekani kama anapumua, alikuwa kimya.. Unadhani jambo gani lingefuata kwa wale watu waliokuwa pale..Ni wazi kama tunavyosoma Habari walisema..Kijana AMESHAKUFA huyu..
wengine pengine wakakimbia saa hiyo hiyo wakisema hii ishakuwa kesi sasa, wengine pengine walianza kudondosha machozi..n.k.
Lakini ule upande wa pili Je! Bwana Yesu muda wote huo alikuwa anafanya nini?
Jibu ni alikuwa anaangalia uponyaji wa Mungu unavyofanya kazi ndani ya yule kijana.. alitulia kimya mpaka pale alipoona kazi ya Mungu imekamilika ndani ya yule kijana,…. Na ghafla tu wakati watu wanaendelea kufikiria tufanye nini?, Wanamwona Bwana anakwenda kumshika kijana mkono na kumnyanyua..
Alivyonyanyuka hakunyanyuka kama mgonjwa mwenye maruwe ruwe, hakunyanyuka kwa kuyumba yumba kama mtu ambaye hajapona vizuri, bali alinyanyuka kama vile mtu aliyeamka usingizini, asubuhi, akiwa fresh, akiona tabasamu zuri la Kristo likiyatazama macho yake.. Kijana akijiona mwepesi, mtulivu, kama vile sio yeye, na tangu huo wakati akawa mzima kabisa..
Sasa ni kwanini Kristo achague, njia kama ile kumponya yule kijana? Na sio zile zilizozoeleka kwamba anafika tu anamgusa mtu na saa hiyo hiyo anapona bila mateso yoyote wala mahangaiko kama yale..
Ni kuonyesha kuwa Kristo anavyowaponya watu wengine Roho zao kwa namna hiyo hiyo pasipo wao kujijua.. Kuna wakati mtu atamwomba Mungu niponye roho yangu..Niponye shida zangu, niponye vifungo vyangu, niponye magonjwa yangu.. Lakini baada ya kuomba vile mambo ndio yanakuwa tofauti, hali ndio inakuwa mbaya Zaidi kinyume na matarajio yake,.. mwingine ni mgonjwa, ugonjwa wake unaonekana kama ndio unazidi, mwingine ana mapepo, maroho hayo ndio yanaonekana kama yanazidi..wala usiogope maadamu ulishamwomba Kristo juu ya uponyaji wako, ujue kuwa hayo maroho yameshakutana na Kristo mwenyewe, hivyo ndio yanavyoungua ndani yako kwa Neno lake..na wakati si mwingi yatatoweka moja kwa moja.
Huo ugonjwa unaokusumbua muda mrefu, umemwomba Kristo akuponye, ameshakusikia na ameshakuponya, lakini hizo dalili za ugonjwa zinazoonekana kama zinazidi, zisikutishe, wakati utafika utaondoka kabisa..usiogope maneno au hisia za wanaokuzunguka, wamekukatia tamaa kiasi gani Kumbuka yule kijana alifikia hatua ya kuonekana amekufa kabisa..hana tumaini tena, lakini ghafla alishikwa mkono na kunyanyuliwa juu na Kristo..Ni nani anayeweza kufa mbele ya Kristo?..yeye ndiye UFUFUO NA UZIMA!
Hivyo na wewe maadamu umemkabidhi Kristo shida yako ujue kuwa hutakufa nayo..Utakufa na nyingi lakini sio hiyo, unachopaswa kufanya ni kuamini Tu.. Basi hicho tu, amini kuwa Kristo amekusikia na atameshakuponya…Lakini hakikisha upo ndani ya Kristo kwanza.
Vilevile katika roho, ukimwomba Kristo akuvushe katika daraja lingine, usishangae kuonekana na watu umekufa kabisa kiuelekeo machoni pa watu..Hiyo ni kawaida..Hivyo uwe tayari kwa hilo pia..kwasababu ni sharti aondoe yote yasiyofaa ndani yako, na ndipo alete mapya ndani yako, kwa Kristo ni lazima upoteze ndipo upate, usipokuwa tayari kufanya hivyo, ni huwezi kuvushwa hatua nyingine..Kwahiyo hilo nalo uwe nalo tayari.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAP
Mada Nyinginezo:
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..
Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MPINGA-KRISTO
USIMWOGOPE YEZEBELI.