Title 2020

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Shalom, karibu tujifunze Biblia Neno la Mungu…

Roho Mtakatifu atusaidie leo tena katika kuyatafakari maneno yake.Kama tunavyojua kuwa matukio mengi ambayo yaliwahi kutokea nyakati za kale na kurekodiwa katika biblia…mengi ya matukio hayo ni unabii wa mambo yatakayokuja kutokea baadaye…Kwamfano tunaweza kuona tukio la kugharikishwa dunia wakati wa Nuhu..Bwana Yesu alisema katika siku za mwisho maovu yatakuwa kama yalivyokuwa katika siku za Nuhu..Na kwa namna ile ile gharika ilivyowajia kwa ghafla wakafa wote ndivyo itakavyokuwa katika siku za mwisho wakati watu wanasema kuna amani na salama ndipo hapo hapo uharibifu unapokuja kwa ghafla.

Kadhalika tunaweza kujifunza tukio mojawapo ambalo pia litatupa picha kujua ni nini kitatokea kipindi kifupi kabla kanisa la Kristo kunyakuliwa.

Siku chache kabla ya kuja kwa Bwana Yesu duniani yaani kabla ya kuzaliwa kwake…Shetani alikuwa ameshauona ule ujauzito wa Mariamu hivyo akaanza kutengeneza njia ya kumwondosha Bwana Yesu. Kabla ya kuzaliwa au kipindi kifupi tu baada ya kuzaliwa.

Ghafla tu wazo likamwingia Kaisari ambaye ndiye aliyekuwa mfalme wa dunia nzima…wazo likamwingia aandike orodha ya majina ya watu wote ulimwenguni…Kwa ufupi maana yake ni kwamba kila mtu anapaswa kwenda mjini kwao kuchukua namba ya utambulisho.

Ni wazi kuwa kuna mambo fulani fulani yalitokea duniani wakati huo mpaka yakahimiza sensa hiyo ifanyike..pengine ukusanyaji wa kodi ulikuwa mgumu hivyo ikahitajika kila mtu asajiliwe, au pengine walitaka kutathimini na kudhibiti kiwango cha watu wanaozaliwa duniani.. Au pengine kulitokea watu waovu ambao walikuwa wanavuruga amani, hivyo ili kuwadhibiti ilihitaji sensa kufanyika na kwa kupitia sensa hiyo kila mtu apate kitambulisho chake.

Ni kama leo matapeli wa mitandao wanavyoongezeka inalazimu serikai itoe tamko la kila mtu kusajili laini ya simu yake kwa alama za vidole, ili kuwadhibiti…na kuongeza usalama.

Sasa harakati kama hizi zilianza kipindi kabla hata ya kuzaliwa kwa Bwana Yesu lakini zilifikia kilele kipindi kifupi kabla ya kuzaliwa Bwana Yesu…Watu wote wakapokea namba.

Luka 2:1 ‘Siku zile amri ilitoka kwa Kaisari Augusto ya kwamba iandikwe orodha ya majina ya watu wote wa ulimwengu.

2 Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyoandikwa hapo Kirenio alipokuwa liwali wa Shamu.

3 Watu wote wakaenda kuandikwa, kila mtu mjini kwao.

4 Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa mbari na jamaa ya Daudi;

5 ili aandikwe pamoja na Mariamu mkewe, ambaye amemposa, naye ana mimba.

6 Ikawa, katika kukaa huko, siku zake za kuzaa zikatimia,

7 akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori ya kulia ng’ombe, kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni”.

Lakini kama wengi wetu tujuavyo…Ndani ya sensa ile kulikuwa na mpango wa Mungu wa Bwana Yesu kwenda kuzaliwa Bethlehemu ili maandiko yatimie…lakini pia kulikuwa na mpango wa Ibilisi mkubwa sana wa kumwangamiza BWANA YESU katika uchanga wake pamoja na mama yake na Baba yake. Alikuwa anasuka mpango wa kwenda kummaliza Bwana Yesu kule mjini kwake Bethlehemu..Ndio maana Herode alitoa tamko la kwenda kutafutwa Bwana Yesu lakini walipomkosa aliagiza watoto wote waliopo Bethlehemu wauawe…Jiulize kwanini si miji mingine yote duniani bali Bethlehemu tu!..shetani naye ana target..hapigi huko na huko ovyo ovyo tu..

Mathayo 2:11 “Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.

12 Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.

13 Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.

14 Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;

15 akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu.

16 Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi.

Utajiuliza pia kwanini Bwana Yesu alisema, ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo ?(Mathayo 24:19), Alisema hivyo akifananisha jinsi wanawake wale walivyoshikwa na uchungu wakati wa kuja kwake mara ya kwanza, ndivyo itakavyokuwa katika siku za kuja kwake hata mara ya pili, embu fikiria jinsi watoto wale, walivyokuwa wakichinjwa kama kuku mbele yao, wapendwa wako wanauawa kikatili,..Ni uchungu kiasi gani Na ndivyo itakavyokuwa katika siku za mwisho..

Mathayo 2:17 “Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema,

18 Sauti ilisikiwa Rama, Kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, Asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako”.

Sasa kile kipindi kikikaribia kufikia dalili za watu kuingizwa katika kumbukumbu za mpinga kristo zitaanza…Mpinga-Kristo ataagiza watu wote kwenda kusajiliwa katika mfumo mpya wa kipinga-Kristo ambao huo utahusisha chips, kadi, vitambulisho vipya n.k..Kama vile Kaisari alivyotoa tamko kuandikwa orodha ya majina ya watu wote duniani ..(Na ndani yake kutakuwa na alama ya 666) Kila mtu atakwenda katika mji wake au makazi yake ya kudumu aliyopo kuhakiki taarifa zake kama vile Kaisari alivyotoa agizo la watu wote kwenda kuhesabiwa mjini kwao.

Wakati zoezi hilo lipo mbioni kutendeka hapo katikati unyakuo utatokea… Bwana atakuja mawinguni na kuwachukua walio wake na kuwaepusha na hiyo chapa..kama tu vile Yesu alipotokea duniani, alivyoondoshwa yeye pamoja na Mariamu na Yusufu kutoka Bethlehemu kukimbilia Misri mbali na ghadhabu ya Herode na Kaisari. Na kusababisha wale waliosalia walichinjwa kama kuku..

Mathayo 2:12 “Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.

Vivyo hivyo wakristo watakaokosa unyakuo, ambao watabaki na kuikataa ile chapa watateswa na mpinga-Kristo kwa dhiki ambayo haijawahi kuwepo tangu kuumbwa ulimwengu. Na Kama tu vile wakati dhiki inaendelea Bethlehemu, inaendelea Yesu pamoja na wazazi wake walikuwepo Misri, Vivyo hivyo wakati dhiki kuu inaendelea, Yesu pamoja na watakatifu wake watakuwa mbinguni.

Je wewe ni familia ya Bwana Yesu Kristo ambaye siku ile utaepushwa na dhiki siku ile na kwenda mbinguni? Kama Mariamu mamaye Yesu na Yusufu walivyoepushwa?…Utauliza nitakuwaje Baba au Mama wa Yesu mimi, na hapo hapo niwe mtoto wa Yesu?

Jibu la swali hilo lipo hapa.

Mathayo 12.46 “Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye.

47 Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe.

48 Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani?

49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu!

50 Kwa maana ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu”.

Je unafanya mapenzi ya Bwana Yesu? Au mapenzi ya shetani…mfano wa mapenzi ya shetani ni haya ulevi, uasherati, uzinzi, ufiraji, ulawiti,utoaji mimba, kujichua, kutazama picha za ngono mitandaoni, uabuduji sanamu, wizi, ulaji rushwa, usengenyaji n.k Biblia imetabiri watu wa namna hii hawataikwepa dhiki kuu…labda wawe wamekufa kabla ya hiyo siku kufika..lakini pia hata huko walipo hawapo sehemu salama…Hivyo suluhisho ni kukubali kubadili mtindo wa maisha yetu.

Kama hujaokoka okoka leo usisubiri kesho..Huwa Adui shetani akishaona umeujua ukweli kama huu unaousoma leo na akishaona unashawishika kumgeukia Kristo, anaweza hata akakusababishia kifo cha ghafla ili tu ufe ukiwa hujaokoka…hivyo usipuuzie habari njema za Yesu zinapoletwa mbele yako ambazo hutozwi hata senti kuzisikiliza unapewa bure kabisa…Jiulize ukifa leo utakuwa wapi? Jibu unalo matumaini yangu ni utamgeukia Kristo leo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MTINI, WENYE MAJANI.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

MPINGA-KRISTO

Mungu anasema hatagharikisha dunia na maji tena,.Kwanini watu wanasema dunia itaangamizwa?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?

SWALI: Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati naye pia alialikwa?. Inamaana wale wengine walipewa mavazi siku ile ya kuingia karamuni?


Tusome:

Mathayo 22:1  “Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema,

2  Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.

3  Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.

4  Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.

5  Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;

6  nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.

7  Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.

8  Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.

9  Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.

10  Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.

11  Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.

12  Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.

13  Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

14  Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache”


SWALI; Je! Inamaana kuwa wale wengine walipewa mavazi siku ile ya kuingia karamuni?

JIBU; Ndio wote waliolikwa pale walipewa vazi la arusi, kulikuwa na utaratibu walioupitia kwanza kabla ya kuingia kule harusini, kila aliyefika pale alihakikiwa kwanza na alipoonekana amekidhi vigezo ndipo akapewa vazi lile la Harusi, lakini yule mwingine alidhani ni kuingia tu, na yeye akajichanganya katikati ya kundi kinyemelewa..Na mwisho wa siku atakambulikana kwa mavazi yake yaliyotofauti na wengine….

Ndio makundi mawili yaliyopo katika kanisa la Kristo leo hii…wote wanasema yanasema nimeokoka nitakwenda mbinguni!! Lakini lipo linalotii na kufuata maagizo yote Kristo aliyoliekezeka..lakini lipo lingine linadhani maadamu tayari limeshakuwa mshirika wa kanisa basi hiyo inatosha, maadamu linatoa zaka, basi inatosha, maadamu linaimba kwaya inatosha, hakuna haja ya kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, hakuna haja ya kuishi maisha matakatifu, hakuna haja ya kuomba, hakuna haja ya kujikana nafsi na kumfuata Kristo, hakuna haja ya kuhakiki ni nini kimpendezacho Bwana, na ni kipi hakimpendezi, lenyewe halina mzigo wowote na dhambi, linachopenda ni kuhubiriwa mafanikio tu, na kubarikiwa, lakini likigusiwa habari za toba halipendi.

Kufanya uzinzi ni kitu cha kawaida kwao, kuvaa nguo za nusu uchi si jambo ajabu pia, kuvaa suruali (wanawake) linaona ni sawa, kunywa pombe ni sawa, kwenda disko ni sawa, kukaa kwenye kampani za kidunia hakuna shida yoyote..

Sasa hawa katika ulimwengu wa roho, ni kweli waliitwa na Bwana lakini hawakuteuliwa…kwasababu hawakuwa tayari kulitwaa vazi jeupe la harusi ambalo ndio kama tiketi ya kuingia mbinguni.

Na ndio maana maandiko yanasema

Ufunuo 19:7  “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8  Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.

9  Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

Unaona?, hiyo kitani nzuri, ing’arayo safi ya kuingia karamuni ni matendo ya haki ya watakatifu…Hivyo na sisi hatutaingia mbinguni kwenye karamu ya mwanakondoo kama matendo yetu hayatakuwa ya haki hata kama tutajiita tumeokoka vipi… Haijalishi Bwana Yesu alitutokea, au tuliona maono, au tulitubu mwanzoni na Mungu akasikia toba yetu, kama hatutajizoeza kuishi maisha matakatifu biblia inasema hatutaweza kumwona Mungu pasipo huo (Waebrania 12:14)

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

Naomba kujua watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

Kuna hukumu za aina ngapi?

Ule mfano wa wanawali 10 (Mathayo 25), wale watano hawakuwa na mafuta ya ziada katika chupa zao je yale mafuta ya ziada yanawakilisha nini?

KILA MTU ATATOA HABARI ZAKE MWENYEWE.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

JUMA LA 70 LA DANIELI

MPINGA-KRISTO

MKUU WA ANGA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

Shalom, Karibu tujifunze Neno la Mungu. Lipo swali ambalo tunaweza tukajiuliza siku ya leo, ni kwanini miujiza yote ile mikubwa namna ile Mungu alimtumia musa kuifanya na si mtu mwingine?…Licha ya kuwa ulikuwa ni mpango wa Mungu kuwaokoa wana wa Israeli kwa mkono hodari lakini pamoja na hayo ipo siri nyingine ambayo tunaweza kujifunza kwa Musa ambayo tukiijua na sisi basi Mungu atafanya kazi na sisi katika viwango vingine vya juu zaidi…

Mwanzoni kabisa wa huduma ya Musa, tunaona Mungu hakujidhihirisha kwake kwa njia ya wazi, ikiwa na maana kuwa hakumwona malaika, wala nabii, wala hakusikia sauti yoyote ikimwambia Njoo! Musa nataka nikutume., alichoona tu ni muujiza, kama na sisi tunavyoona leo hii miujiza ya wazi.. na hiyo ndio inayotupa uthibitisho kuwa wito wa Musa hakuwa wa kipekee sana kama wengi wetu tunavyodhani..

Kama unadhani kuona kijiti kinaungua halafu hakiteketei ni muujiza mkubwa zaidi ya unayoona leo hii roho za wafu zinafufuliwa kwa jina la Yesu kutoka mautini, jifirie mara mbili tena…

Lakini biblia inatuonyesha tabia ambayo Musa alikuwa nayo, pindi alipouona muujiza ule tu, hakupita kando, badala yake, moyo wake uliguswa sana, akasema muujiza huu hautanipita mpaka nijue maana yake ni nini, na ni nani aliyeweza kufanya maajabu makubwa kama haya..Ndipo Musa akasogea karibu..Embu jaribu kutengeneza picha akiwa pale akikitazama ki-mti kile cha kijani, kwa butwaa, akikiangalia mara mbili mbili, pengine anajiuliza kichwani, huyu aliyeweza kufanya hivi bila shaka atakuwa ni mkuu sana kwa maajabu na uweza, laiti ningemjua ningemng’ang’ania nisingemwacha….

Sasa wakati akiwa anafikiria hivyo na anataka kukaribia karibu zaidi ili azidi kuchunguza anachokiona ni macho yake au la! saa hiyo hiyo Mungu akaanza kuzungumza naye na kumwambia Musa,usikaribie mahali hapa, maana unaposimama ni nchi takatifu…..Tusome..

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.

2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea.

3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.”.

Kama tunavyojua sote baada ya hapo, ni nini kilitokea katika huduma ya Musa..Mungu alimtumia kwa ishara na miujiza isiyokuwa ya kawaida kwa kipindi chote..

Lakini tujiulize, Ni kwanini Mungu hakuzungumza naye moja kwa moja tangu mwanzoni na kumpa huduma ile kubwa, mpaka akaruhusu kwanza ageuke?

Ni kwasababu Mungu alikuwa anapima kujali kwake kwanza..Na ndio maana akatanguliza kwanza ule muujiza mdogo wa kijiti kuteketea, ili aone kama Musa atauthamini kwa kutaka kujua maana yake au La! ..Na laiti kama Musa asingeuthamini, na kupita zake kuendelea na mambo yake ya uchungaji kamwe Mungu asingekuwa na habari na Musa..maisha yangeendelea kama kawaida tu, kama vile hakuna chochote kilichotokea.

Mungu huwa anawaza na kusema, ikiwa muujiza mdogo kama huu hauthamini, atauthamini vipi nikija kumpasulia habari huko mbeleni, atathamini vipi siku nikijifunua kwake kama nguzo ya moto huko mbeleni?, atathamini vipi wakati nawashushia mana kutoka mbinguni? Atathamini vipi siku nikiyowatolea maji mwambani?.

Lakini Musa alithamini madogo yale, na Ndio maana Mungu alimtumia Musa katika makubwa pia.

Hata sisi ni kwanini Mungu hasemi na sisi au hatembei na sisi katika viwango vingine? Ni kwasababu hatuithamini miujiza ile midogo anayoipitisha mbele yetu sasa.. Tunaona ni kawaida tu..Musa hakuona kawaida….Kama Musa leo hii angeona wafu wanafufuliwa, tujiulize angemshangaa Mungu kwa viwango gani?..Je! yale Mungu anayotutendea ambayo tunaona kabisa ni miujiza mikubwa, Je yanatutafakarisha usiku na mchana, na kutufanya tumshangae Mungu na kumshukuru daima mpaka kumpa Mungu aone sababu ya kutufanyia na makubwa zaidi ya hayo? Je! yale tunayoona wengine wanatendewa na Mungu, na tunaona kabisa ule ni muujiza, Yule kaponywa, Yule kafunguliwa, Yule kaokolewa, Je hayo yanatuingia mioyoni mwetu kiasi cha kwamba yanatugeuza na kutufanya tumshangae Mungu kwa kipindi kirefu au tunayapuuzia tu?

Nataka nikuambie tukiyathamini hayo tunayoona leo hii kama madogo, na kuyatafakari sana, na kumsifu Mungu kwa ajili ya hayo, tuwe na uhakika kuwa tutafungua milango ya kuoiona miujiza mikubwa isiyokuwa ya kawaida katika Maisha yetu, au katika huduma zetu. Kama Mungu alimtumia Musa anaweza kututumia na sisi pia kudhihirisha utukufu wake kwa wasio mjua.

Lakini leo tukiyapuuzia, tujue kuwa hatutafika popote,..Tuthamini haya madogo tunayoyaona kwanza, na ndipo hayo makubwa mengine Mungu atuzidishie..tujifunze kwa mababa hawa waliotutangulia tufanikiwe..

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312


Mada Nyinginezo:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

“Ninyi ni chumvi ya dunia” Andiko hilo lina maana gani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

ITAFAKARI SIKU YA HUKUMU.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…Sio vibaya tukajikumbusha mambo ambayo tulishawahi kujifunza huko nyuma au kufundishwa..Bwana katika agano la kale aliwazuia wana wa Israeli kula wanyama ambao hawacheui…kucheua kama ilivyotafsiriwa kwenye biblia maana yake sio kutoa hewa mdomoni inayotoka tumboni..au kutapika…Hapana..kucheua ni tabia Wanyama wanayokuwa nayo ambapo baada ya kula nyasi huwa wanahifadhi chakula kile katika matumbo yao na kisha baadaye wanauwezo wa kukirudisha chakula kile na kukitafuna tena na kisha kukimeza kikiwa kimesagika vyema zaidi…Sasa mnyama kama nguruwe alikuwa hacheui, hivyo ni najisi…Ikifunua tabia ya aina ya watu fulani..ambao Hawana tabia ya kukumbuka mambo waliyojifunza nyuma, wala hawana tabia ya kurudia kutafakari tena na tena..wakila wamekula, hawana muda wa kukirudia tena kukitafakari, kukitafuna tena kile chakula…Na hiyo inawafanya wanakuwa warahisi kusahau mema yote na mazuri yote ambayo Mungu alishawhi kuwafanyia huko nyuma.

Lakini tukijifunza kujikumbusha mambo tuliyojifunza huko nyuma, na kurudia kuyatafakari tena na tena tunajiweka katika nafasi nzuri ya kumshinda yule mwovu, na hivyo katika roho sisi tunaonekana ni viumbe ambavyo si najisi mbele za Mungu.

Hivyo tujikumbushe kidogo kuhusu hukumu. Tuitafakari kidogo hukumu ya Bwana Yesu itusaidie kujua hukumu yetu itakuwaje huko mbeleni baada ya Maisha haya.

Kama tunavyojua Bwana alishtakiwa na Wayahudi (yaani wa-Israeli) lakini alisulubiwa na warumi (Yaani watu wa Mataifa). Kwahiyo jamii zote mbili: Wayahudi na sisi watu wa Mataifa) tuna hatia juu ya Damu ya Yesu. Ndio maana ukombozi na msamaha unatuhusu sote. Kwasababu wote tumetenda dhambi..

Warumi 3:23 “ kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu”..

Na kama Bwana Yesu alisimamishwa mbele ya kiti cha hukumu alivyokuwa hapa duniani…Na akahukumiwa mbele ya watu wote (wayahudi na watu wa mataifa), na akatoa hesabu ya mambo yote.

Yohana 19:13 “Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha”.

Vivyo hivyo siku ile ya hukumu watu wa mataifa yote duniani nao pia watasimama mbele zake yeye katika kiti cheupe cha hukumu. Na kila mmoja atatoa hesabu ya mambo yake aliyoyafanya alipokuwa hapa duniani.

Kwahiyo ufanyalo leo kumbuka kwamba siku moja litaletwa hukumuni..

Mhubiri 12:13 “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya”.

Na zaidi tena Biblia  inasema..

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.

12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.

13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.

15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.”

Kama Bwana Yesu na ukamilifu wake wote alisimama mbele ya kiti cha Hukumu cha Herode…Sisi ni nani tuikwepe hukumu inayokuja?..Tujitahidi siku ile tusiwepo katika kundi la watu watakaohukumiwa mauti ya milele katika ziwa la moto..bali watakaohukumiwa kwa kupewa thawabu katika kuushinda ulimwengu.

Mathayo 25:19 “Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.

20 Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida.

21 Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.

22 Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida.

23 Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.

24 Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;

25 basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako.

26 Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;

27 basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.

28 Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi”.

Tukikumbuka pia hakuna nafasi ya pili baada ya kifo..Mtu kaandikiwa kufa mara moja tu, na baada ya kifo ni hukumu kasome (Waebrania 9:27). Hakuna maombi yoyote yanayoweza kumwamisha mtu kutoka katika moto wa kuzimu na kumwingiza katika paradiso…Ukifa katika dhambi ndio tayari umepotea milele..Biblia inasema mti uangukiapo huko huko utalala (Mhubiri 11:3)…maana yake ukifa na kwenda kuzimu ndio huko huko utakuwepo milele.

Je umesimama katika Imani?..Unauhakika Kristo akija leo utakwenda naye. Bwana akusaidie, na Bwana atusaidie sote katika Jina la Yesu Kristo.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312


Mada Nyinginezo:

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.

HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.

HISTORIA YA ISRAELI.

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

Mambo 5 ambayo kila mkristo anapaswa kufahamu.


NJIA IMESONGA.

Kuvuka ng’ambo si kurahisi kama inavyodhaniwa na wengi.

Mathayo 7:13  “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

14  Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache”..

Hivyo usivunjike moyo, unapojikuta upo peke yako katika safari ya wokovu, kikubwa tu ni kukazana na Bwana, na kuhakikisha hurudi nyuma, kwasababu Bwana ameahidi kuwa pamoja na wewe safarini hadi mwisho.

MAJARIBU NI LAZIMA YAJE:

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Usirudi nyuma unapokutana na utelezi safarini, mambo kama magonjwa, misiba, kupungukiwa, kuuudhiwa kwa ajili ya wokovu, kutukanwa, kupoteza n.k…utakutana nayo.Lakini Jipe moyo kama Bwana alivyosema..Kwasababu pamoja na hayo ameahidi kutuwekea na mlango wa kutokea, hivyo hayatadumu milele.

MAISHA NI MAFUPI.

Yakobo 4:13  “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida;

14  walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka”.

Tukilijua hilo pia basi tutautumia muda wetu vizuri kwa Bwana, kwasababu hatujui ni muda gani tuliobakiwa nao hapa duniani. Hivyo hatutaishi kwa kujisahau mpaka kupitiwa na mambo mengine tukasahau kuwa tupo ukingoni mwa safari.

HUKUMU INAKUJA.

Warumi 14:12  “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.

Tukijua kuwa utafika wakati ambao kila mkristo atasimama mbele ya kiti cha enzi cha Kristo na kueleza ni jinsi gani alivyoitumia talanta yake…Hiyo inatuhimiza, kila siku tuishi maisha ya kujitathimini , na vilevile kuitenda kazi yake kwa uaminifu wote na kwa bidii, ili tusiwe miongoni mwa  lile kundi la watumwa walegevu”.

UMILELE UPO.

Danieli 12:2 “Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele”.

Kuna kuishi maisha yasiyo na mwisho huko mbeleni. Fikiria unakwenda kuwa nani?  Tukilijua hilo, basi itatufanya tuwekeze kwa bidii kule ili thawabu zetu ziwe nyingi, tuwe matajiri katika ufalme wa Mungu, kwasabaabu utajiri wa kule utakuwa ni wa kudumu milele, lakini tusipowekeza chochote, mambo yatakuwa ni kinyume chake, tutakwenda kuwa watu wa kawaida milele, au tusifike kabisa…

Mimi na wewe tupige mbio tuumalize mwendo salama…

Shalom.

Mada Nyinginezo:

KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

NGUVU YA MSAMAHA

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAJINI WAZURI WAPO?

Majini ni nini? Je kuna majini wazuri?, je pete za majini ni zipi? na namba za majini ni zipi?..Je kuna njia yoyote ya kupata utajiri wa haraka?

JIBU: Kwanza ni vizuri kufahamu majini ni nini?…Majini ni jina lingine la roho zilizoasi mbinguni, ambazo zilitupwa chini duniani pamoja na lusifa ambaye ndiye alikuwa kiongozi wao.

Majini jina lingine yanaitwa mapepo..wakati wakiwa mbinguni lusifa ambaye ndiye shetani aliwadanganya wasimame kinyume cha Mungu na kutaka kuwa kama Mungu…Lakini walishindwa vita vile na Malaika walio upande wa Mungu na kuishiwa kutupwa chini duniani.

Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye”

Kazi ya majini haya baada ya kutupwa duniani ni kwenda kinyume na kusudi la Mungu juu ya mwanadamu. Hivyo yanapambana usiku na mchana kuhakikisha kusudi la Mungu juu ya mwanadamu halifanikiwi. Majini haya au kwa lugha nyingine mapepo hayataki mwanadamu hata mmoja afike mbinguni. Hivyo yanatumia ujuzi wao na akili zao zote kuhakikisha yanatimiza malengo yao.

Kumbuka walioposhindwa vita mbinguni (kama tunavyosoma katika kitabu cha Ufunuo 12) hawakunyang’anywa na Mungu nguvu walizokuwa nazo wala ujuzi..walifukuzwa wakiwa na nguvu walizopewa na Mungu kadhalika na fahamu zao…Hivyo wanazo mpaka sasa nguvu… Ingawa sisi tuliookoka tumepewa nguvu zilizo kuu zaidi zao kupitia damu ya Yesu Kristo.

JE KUNA MAJINI WAZURI?

Majini wote ni wabaya hakuna jini hata mmoja aliye mzuri. Shetani aliye mkuu wa majini hayo anatumia nguvu kubwa kuwadanganya watu kwamba kuna majini wazuri..lengo lake ni ili watu wajishughulishe kuzitafuta roho hizo na kujishikamanisha nazo. Na kwa pamoja wafanye kazi ya kuziangusha roho nyingine.

JE PETE ZA MAJINI NI ZIPI?

Majini yanaweza kumwingia mtu yoyote kwa kupitia njia yoyote ile ambayo ipo kinyume na mapenzi ya Mungu sio pete tu!..Majini/mapepo yanaweza kumwingia mtu kwa kupitia mawigi ya kichwani, kwa kupita vipodozi, wanja, kwa kujichora tattoo,kwa kufanya ibada za sanamu na pia njia kuu ni kwa kupita kufanya uasherati na mtu ambaye si mke wako au mume wako na pia kwa kuangalia picha za ngono. Pete inaweza kuwa ni njia ya mwisho kabisa ya kuingiza majini ndani ya mtu.

Mtu anapokwenda kwa mganga au anapojiunga na kikundi fulani cha kichawi kama freemason na vingine anaweza kukabidhiwa pete, mkufu, picha au chochote kile…vitu hivyo ni mlango pia wa kuingiza roho za majini ndani ya mtu.

JE NAMBA ZA MAJINI NI ZIPI?

Maelfu ya watu wasio na ufahamu wanazunguka mitandaoni kutafuta namba za majini..Majini ni roho! hayawezi kuwa na namba za simu za mkononi. Mawakala wao ambao ni waganga wa kienyeji na wachawi ndio wenye namba za simu lakini si mapepo. Hayo ni maroho yanafanya kazi katika ulimwengu wa roho…

JE KUNA NJIA YOYOTE YA KUPATA UTAJIRI WA HARAKA KUPITIA MAJINI?

Uongo mkubwa shetani anaowadanganya wengi ni kwamba kwake kuna fedha za bure na za haraka!..Nataka nikuambie ndugu hicho kitu hakipo..lengo la shetani ni kukupeleka tu kuzimu hakuna lingine.

Njia ifuatayo ndiyo anayoitumia shetani kuwapatia watu mali kwa njia ya majini.

1.Anatumia mtu jini/pepo..Lile pepo linaweza kuwa la aina yoyote ile, aidha zinaa, ulevi, wizi, uuaji n.k Sasa lile jini, tuchukue mfano la zinaa linapomwingia mtu..au mtu anapokwenda kwa waganga kutafuta mali anapewa pete..Na ile pete ndani yake imebeba mojawapo ya hilo jini..labda tuseme la zinaa..Mtu anapoivaa lile pepo la zinaa linamwingia..yule mtu akitoka pale anakuwa mwasherati kupita kawaida…kama ni mwanamke anakuwa ni kahaba kupita kawaida…na hivyo linamsukuma kwenda kufanya kazi ya ukahaba. Na kwa kupitia hiyo kazi ya ukahaba ndipo anapopata fedha.. Lakini si kwamba anakaa tu na kisha fedha zinaingia.

Kadhalika na wizi, ni hivyo hivyo..pepo la wizi linamwingia na linakwenda kumfanya kuwa mwizi hodari..na kwa wizi ule anapata mali zisizohalali.

Na hivyo hivyo mauaji..Pepo linamwingia mtu na kumfanya aone kuua sio shida tena na kwa kupitia mauaji yale anapata kazi nyingi za ujambazi na hivyo kupata fedha kwa kazi hiyo.

Kwahiyo hakuna fedha za bure kwa shetani..Anakupa jini/pepo na jini hilo linakwenda kukutumikisha kupata hizo mali. Na hautakaa tu baada ya kuipokea hiyo pete..kwamba fedha zidondoke.

Hata wale wanaofanya uchawi ujulikanao kama chuma ulete..Nao pia wanavalishwa pepo hilo ambalo linawafanya wateseke kwa hali na mali kufanya uchawi huo..gharama wanazotumia kufanya uchawi huo ni mkubwa kuliko hata faida wanazozipata huko.

Hivyo kuyatafuta majini au kujishughulisha nao ni kujitesa na ni kwenda kinyume na mpango wa Mungu…Kufanya kazi na majini/mapepo ni kuwa Adui wa Mungu rasmi asilimia 100. Na kujitengenezea daraja zuri la kuwa miongoni mwa watakaoteswa sana katika ziwa la moto baada ya hukumu.

Na madhara ya kuwa na majini ni mauti..Majambazi wote kama Neema ya Kristo haitawapitia wanaishia kupigwa risasi, makahaba wote kama Neema ya Kristo haitawafikia wanaishia kufa kwa magonjwa…vivyo hivyo wezi wanaishia kuchomwa moto..Mafisadi wanaishia kufungwa..wachawi wanaishia kufa kifo cha ghafla n.k

Sasa kwanini kudanganyika na uwongo wa shetani kwamba kwake kuna fedha za bure?..Kwamba ni kuvaa pete tu, ni kuchinja mbuzi tu!..shetani anakuambia ni kuvaa pete tu lakini hakuambii ukahaba atakaokwenda kukutumikisha nao.

Hivyo kama Kama hujampa Kristo maisha yako. Mgeukie Leo..usitafute mali wala msaada kwa shetani na wala hakuna majini wazuri watakaokusaidia kupunguza ugumu wa maisha..shetani yeye kashaasi, anachokisubiria tu ni kutupwa katika ziwa la moto..na anataka kwenda na wengi..hivyo anatumia uongo wa kila namna kujaribu kuvuta watu kwake..tumwache aende yeye peke yake sisi tumgeukie Kristo tumaini la utukufu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

NDUGU,TUOMBEENI.

Ukiangalia ujenzi wa kwanza wa hekalu na ule wa pili utaona kuna utofauti fulani, Kwanza ule wa kwanza uliojengwa na mfalme Sulemani, ulikuwa ni wa utajiri mwingi, ambao ulikuwa tayari umeshakusanywa na Daudi baba yake Sulemani huko nyuma, pili ulikuwa ni wa amani, na utulivu, kiasi kwamba hata siku ile unapokamilika hakukusikika kelele wala sauti ya nyundo (1Wafalme 6:7).. Lakini ujenzi wa hekalu la pili ambalo lilibomolewa na mfalme Nebukadneza, ulikuwa ni wa shida sana, ulikuwa ni wenye vikwanzo vingi sana, vilevile uliozungukwa na maadui wengi, ili kukwamishwa tu Hekalu lile lisijengwe.

Ni kawaida ya shetani huwa akishajua jambo fulani au ujenzi fulani unafanyika, ambao utaleta madhara makubwa katika ufalme wake huko mbeleni, au utakuwa na utukufu mkubwa Zaidi wa Mungu ni lazima alete vipingamizi vingi..Na ndivyo ilivyokuwa katika ujenzi huu, Mungu aliwaambia wayahudi kuwa utukufu wa nyumba hiyo ya pili utakuwa ni mkuu kuliko ule wa nyumba ya kwanza (Hagai 2:9). Hivyo shetani kulijua hilo akanyanyua vipingamizi vingi sana.

Na miaka kadhaa tu kabla ujenzi huo haujaanza Mungu alishamwonyesha Danieli jinsi utakavyokuwa wa shida na mgumu.

Danieli 9:25 ‘Basi ujue na kufahamu, ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, KATIKA NYAKATI ZA TAABU’.

Hivyo Zeruababeli na Yoshua walipooanza kuijenga nyumba, mwanzoni tu wakakumbana na mikono ya maadui zao, wakawatisha wasiijenge, mpaka wakaenda kuomba kibali kutoka kwa mfalme, kazi hiyo isiendelee, mpaka baada ya miaka mingi kupita Mungu anawanyanyua tena mioyo yao na kuwaambia waanze kazi wasiogope.,Ndipo Mungu akawa pamoja nao na kuimaliza.

Lakini baada tena muda mrefu kupita hapo tayari hekalu limeshakamilika, shetani hakupumzika alilivamia tena hekalu, na kuharibu kuta zake, hapo ndipo tunaona Mungu akimnyanyua mtu mwingine aliyeitwa Nehemia, ili kuzisimamisha tena kuta za mji na kulikarabati hekalu, lakini mambo hayakuwa maraisi kama ilivyokuwa.

Maadui waliwalemea wakina Nehemia, ukipata nafasi pitia mwenyewe kitabu cha Nehemia usome jinsi walivyopata tabu..Mpaka ikafikia wakati sasa, kila mjenzi anabidi ajifunze na ujuzi mwingine wa ziada..Kwamba sio tu kujenga, bali pia kulinda..Kila mjenzi alilazimika kubeba silaha zake mgongoni, na wakati huo huo alikuwa anajenga..ili kwamba ikitokea tu maadui zao wamewavamia wakati wowote, basi wawezi kupambana nao. Na wengine walikuwa wakipokezana..wakati wanajenga wengine wanalinda.

Nehemia 4:16 “Ikawa tokea wakati huo, nusu ya watumishi wangu walitumika katika kazi hiyo, na nusu yao wakaishika mikuki, na ngao, na pinde, na darii; na maakida walikuwa nyuma ya nyumba yote ya Yuda.

17 Watu wale walioujenga ukuta, na wale waliochukua mizigo, walijitweka wenyewe, kila mtu alifanya kazi kwa mkono mmoja, na kwa mkono wake wa pili alishika silaha yake;

18 nao wajenzi, kila mtu alikuwa na upanga wake, umefungwa ubavuni mwake, ndivyo alivyojenga. Na yeye aliyepiga baragumu alikuwa karibu na mimi.

19 Nikawaambia wakuu, na mashehe na watu wengine; Kazi hii ni nyingi, tena kubwa, nasi tumetawanyika juu ya ukuta, kila mtu mbali na mwenzake;

20 basi mahali po pote mtakaposikia sauti ya baragumu, enendeni huko, mkatujie; Mungu wetu atatupigania.

21 Hivyo tukajitia kAtika kazi hiyo; na nusu yao waliishika mikuki, tangu alfajiri hata nyota zikatokea.

22 Kadhalika, wakati ule ule, nikawaambia watu, Kila mtu na akae ndani ya Yerusalemu pamoja na mtumishi wake, wapate kuwa walinzi wetu wakati wa usiku, na kufanya kazi wakati wa mchana.

23 Basi mimi, na ndugu zangu, na watumishi wangu, na watu wa ulinzi walionifuata, hatukuvua nguo zetu hata mmoja; kila mtu alikwenda kuteka maji akichukua silaha yake.

VIPI KUHUSU HEKALU LA SASA?

Sasa hilo lilikuwa ni hekalu la kimwili linapitia changamoto hizo, vipi kuhusu hekalu la Mungu la rohoni..ambalo ni kanisa lake? (2Wakorintho 6:16)..Tukisema kanisa hatumaanishi jengo hapana bali tunamaanisha waliomwamini Kristo..maana hiyo ndiyo tafsiri yake.. Shetani ataleta mapambano na Zaidi ya mapambano.. Kanisa la Mungu halisimami kirahisi rahisi kama wengi wanavyodhani, shetani hawezi kutulia kuangalia tu watu wanaokoka wanamfuata Kristo, wanapata uzima wa milele na asilete vipingamizi vingi..

Na hapo ndipo tunapolazimika kuvaa silaha zote za Injili kama tunavyozisoma katika Waefeso 6 ili tuweze kumpinga adui..Na silaha mojawapo ni MAOMBI.

Waefeso 6:18 ‘kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

19 pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;

20 ambayo kwa ajili yake mimi ni mjumbe katika minyororo; hata nipate ujasiri katika huyo kunena jinsi inipasavyo kunena’.

Unaona, mstari wa 19 na 20 Mtume Paulo hakuona aibu kuomba aombewe..Vivyo hivyo na watumishi wote wa Mungu hata sasa tunahitaji maombi yako ili kazi ya Mungu isikwamishwe na hila zote za shetani. Hata sisi tunaoandika masomo haya mitandaoni tunaomba maombi yenu sana..kwasababu ni vipingamizi vingi sana tunakumbana navyo..wakati mwingine shetani anaharibu vifaa tunavyotumia kuandika masomo haya, inatugharimu tutumie hivyo hivyo tu kwa shida…Wakati mwingine unapomaliza tu kuandaa na kutaka ku-post ibilisi anaharibu network nzima lakini kwa upande wa masomo tu, inaweza kukuchua hata masaa 2 au zaidi ku-post somo moja tu, lakini cha ajabu wakati huo huo network iko vizuri unapofungua kurasa nyingine, wakati mwingine unapanga ufanye hichi au kile cha kiMungu lakini kinanyanyuka hiki au kile kukukwamisha..Na changamoto nyingine nyingi tu ambazo huwezi kutaja moja moja hapa..Hivyo kwa nje mambo yanaweza kuonekana yapo vizuri lakini nyuma kuna vita vingi sana vinaendelea..

Hivyo maombi yako, yana mchango mkubwa sana kwetu na kwa wengine, na kwa ajili ya injili ya Mungu isonge mbele..Sisi wenyewe hatuwezi, hivyo tuombeane sote..Adui yetu shetani anapoona watu wengi wanamgeukia Mungu hawezi kutulia.

Hakuna silaha nyingine tutakayoweza kumshinda shetani Zaidi ya maombi.

1Wathesalonike 5:25 “Ndugu, tuombeeni”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

KAMA MHUBIRI NI WOKOVU UPI UNAUPELEKA KWA WATU?

UFUNUO: Mlango wa 11

DANIELI: Mlango wa 9

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

HATA NA BARNABA PIA AKACHUKULIWA NA UNAFIKI WAO!!

JE KUJIUA NI DHAMBI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! WEWE NI MWAKILISHI MWEMA?

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…

Tunasoma Bwana wetu Yesu Kristo alipoanza huduma yake alianza peke yake…lakini akiwa katikati ya huduma hiyo, kama wengi wetu tunavyojua aliwatafuta wanafunzi ambao hao baada ya yeye kuondoka wataiendeleza kazi aliyokuwa anaifanya yeye. Aliona kuwa mavuno ni mengi na yeye peke yake hatoshi inahitajika jeshi kubwa. Hivyo aliwatafuta wanafunzi wengi sana…idadi yao haijulikani lakini ni wengi…Miongoni mwa hao wanafunzi wengi aliokuwa nao akawatenga mitume 12..Kwaajili ya madarasa maalumu…Kuna mambo ambayo mitume 12 walikuwa wanaambiwa na Bwana ambayo wanafunzi wengine walikuwa hawaambiwi..

Lakini ilifika kipindi Mitume wakapelekwa mazoezini kama vile wanafunzi wa vyuoni wanavyopelekwa field leo..Bwana aliwatuma wazunguke kila mahali, watoe pepo wafufue wafu n.k…lakini na hiyo Bwana aliona haitoshi pia akawaagiza tena wanafunzi wengine 70 waende wakafanye kazi zile zile za Mitume 12..

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na KILA MAHALI ALIPOKUSUDIA KWENDA MWENYEWE.

2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake”.

Sasa nataka tuone huo mstari unaosema “wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe”.

Kuna mahali ambapo Kristo anakusudia kwenda mwenyewe lakini anatutuma sisi tuende kwa niaba yake….Kumbuka hatuendi mahali sisi tunapotaka kwenda bali yeye alipokuwa anataka kwenda mwenyewe…Ikiwa na maana kuwa tunakwenda kutimiza kusudi, na malengo ya mtu mwingine…Na sio malengo yetu. Sisi ni mawakili tu..Ni sawa Raisi amtume mtu fulani amwakilishe kwenye sherehe fulani aliyoalikwa kwenye Taifa lingine…Yule aliyetumwa ni mwakilishi tu…anapeleka pongezi, au shukrani au maombi kwa niaba ya yule aliyemtuma…hana la kuongeza wala la kupunguza kutoka kwenye nafsi yake mwenyewe.

Kadhalika tunapokuwa wakristo sisi ni wa wakilishi wa Yesu Kristo mahali tunapotumwa…Hatuna hati miliki ya injili, hivyo tunapaswa tuseme kile anachotaka sisi tukiseme..tunapaswa tufikie malengo yale anayotaka yeye afikie…Kwa ufupi tufanye kazi ile ile ambayo angekuwa yeye yupo hapo angeifanya.

Lakini tunapokuwa wakristo halafu hatuifanyi kama anavyotaka yeye…maana yake sisi ni waasi. Mtu asiyekuwakilisha vyema kama ulivyomwambia akuwakilishe maana yake huyo mtu tayari kashakuwa adui yako. Unakwenda na kuwahubiria watu injili ambayo Yesu Kristo hakuihubiri ni kujitafutia laana badala ya baraka..Biblia inasema hivyo katika..

Wagalatia 1:6 “Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine.

7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.

8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe.

9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe”.

Bwana Yesu alihubiri toba na ubatizo lakini wewe unasema hayo sio ya msingi..hapo unajitafutia laana…Bwana Yesu alihubiri kwamba tusishindane na mtu mwovu, tuwaombee wale wanaotuudhi, na tuwapende adui zetu..wewe unahubiri mlaani adui yako na mchukie anayekuchukia..Bwana Yesu alifundisha kwamba tusilale usingizi bali tukeshe katika roho nasi tuwe kama watu wanaomngojea yeye..Wewe unahubiria watu na kuwawekea mazingira ya kuzidi kuzama katika ulimwengu,..Bwana Yesu alihubiri mtu amwachaye mkewe na kwenda kuoa mwingine azini..wewe unafungisha ndoa za watu waliowaacha waume wao au wake zao, Bwana Yesu alifundisha kutawadhana miguu ni jukumu la Kila mwamini, lakini wewe unafundisha ule ulikuwa ni mfano tu wa rohoni n.k.

Je hayo unayoyahubiri Kristo angekuwa yupo hapo angewahubiria watu hayo unayoyahubiri wewe?..angewavumilia watu wanaowaacha wake zao na kwenda kuoa wengine?…angekuwa anafanya fanya mizaha unayofanya fanya leo madhabahuni au unapotumika? comedy..je angewahubiria watu waje kupokea magari na majumba na huku wanaangamia kwa uasherati wao na anasa zao?…

Je wewe ni mwakilishi mwema?..Bwana atusaidie tuwe wawakilishi wema kila siku katika kazi yake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255789001312

Mada Nyinginezo:

HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

CHAPA YA MNYAMA

Rudi Nyumbani:

Print this post

MUNGU AKIKUPITA LEO, HAIMAANISHI KUWA HAJAKUCHAGUA.

Shalom, Jina la Mfalme mkuu Yesu Kristo libarikiwe.

Nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko, Kama vile Paulo alivyomwambia Timotheo “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma..”(1Timotheo 4:13)..Nasi pia tunapaswa tuonyeshe bidii hiyo hiyo katika kusoma Neno la Mungu kwasababu kila siku yapo mambo mapya Mungu anahitaji tuyaone.

Hivyo, leo tutajifunza juu ya mtume mmoja wa kipekee kidogo anayeitwa Mathiya. Mtume huyu hatumsomi mahali pengine popote katika vitabu vya injili isipokuwa katika kitabu cha Matendo ya mitume. Mtume Huyu hakuwa miongoni mwa wale 12, lakini baadaye tunakuja kusoma alihesabiwa kuwa ni mmojawapo wa wale 12 kama wengi wetu tunavyojua, Na siri ya yeye kuhesabiwa kuwa mmojawapo wale mitume 12 wa Bwana, imeandikwa pale katika biblia, embu tusome:

Matendo 1:15 “Siku zile akasimama Petro kati ya hao ndugu (jumla ya majina ilipata mia na ishirini), akasema,

16 Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu;

17 kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii.

18 (Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka.

19 Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.)

20 Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo;

21 Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu,

22 kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.

23 Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya.

24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

25 ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.

26 Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja”.

Unaona huo mstari wa 21 na 22, unatuambia Mathiya ni mtu aliyefuatana na mitume wa Bwana tangu siku za mwanzoni kabisa mwa huduma ya Yesu, mpaka siku ile ambayo Ananyakuliwa mbinguni. Japo kulikuwa na mabonde mengi na hatari nyingi za kuuliwa na wayahudi, lakini huyu Mathiya hakuacha kuongozana na Bwana pamoja na mitume wake, japo kuna wakati wanafunzi wengi walijitenga na Kristo na kurudi nyuma kutokana na mafundisho yake ambayo hawakuyaelewa, lakini huyu Mathiya hakurudi nyuma…Mahali ambapo wanafunzi wake waliacha kila kitu na kumfuata Yesu, Mathiya naye alifanya hivyo japo Kristo hakumuhesabia kama mmoja wa mitume wake 12.

Embu tengeneza picha siku ile Bwana YESU ametoka kusali ndio anakwenda kuwateua mitume wake 12 wa kufuatana naye, katikati ya wanafunzi wengi aliokuwa nao,..Kumbuka Huyu Mathiya naye alikuwa pale, na akamwona Bwana anampita hana habari naye anawafuata wanafunzi wengine..Ingekuwa ni wewe upo hapo ingekuwa ni rahisi kuvunjika moyo. Lakini yeye kutokuchaguliwa hakukumfanya ajione hastahili kuwa mwanafunzi wake, au asifuatane na Bwana..

Lakini hakujua kuwa kwa kujitoa kule, na kumpenda Bwana kule, kumbe tayari siku nyingi ameshaandikiwa kuwa atakuwa miongoni mwa wale mitume 12.. Lakini mpaka Bwana anaondoka hajawahi kumwambia jambo hilo.. Hilo linakuja kuthibitika kwa vinywa vya mitume wake, wakisapotiwa na maandiko haya..

Zaburi 109:8 “Siku zake na ziwe chache, Usimamizi wake na atwae mtu mwingine”.

Usimamizi wa Yuda ambaye alitiwa mafuta na Yesu mwenyewe, ambaye aliheshimiwa na Yesu, ambaye alikula meza moja na Yesu, hapa inachukuliwa na Mathiya.

Hata leo hii, huhiitaji Bwana akutokee kama ilivyokuwa kwa mitume, ili kukuthibitisha wewe unaweza kuwa ni mteule wake, huhitaji Bwana akupe maono Fulani ndio umtumikie, huhitaji upitie shule Fulani ya biblia ndio upate uthibitisho kuwa Mungu yupo na wewe..Bwana anachohitaji kwako ni uaminifu wako kwake, tangu siku ile ulipoitikia wito wa kuokoka, ili wakati wake ukifika akunyanyue kama Mathiya..

Bwana alikuwa na wanafunzi wengi sana, lakini si wote walidumu naye wakati wote, walikuwa wanakuja na kuondoka, wanakuja na kuondoka, lakini waliodumu kuanzia mwanzo hadi mwisho ni wawili tu yaani Mathiya na Yule mwingine aliyeitwa Yusufu kati ya mamia ya wanafunzi waliokuwa wanamfuata.. Kama tu vile Yoshua na Kalebu walivyoingia nchi ya ahadi wao tu kati ya mamilioni ya watu waliotoka Misri.

Na Mathiya kumbukumbu lake halitafutika milele.. Tunaposoma kitabu cha Ufunuo juu ya ule mji Mtakatifu Yerusalemu mpya ushukao kutoka mbinguni wenye misingi 12 na malango 12..Na katika misingi ile pameandikwa majina 12 ya wale mitume 12 wa Yesu, (Ufunuo 21:14) ..Sasa jina mojawapo ni la huyu Mathiya.

Lakini safari yake haikuibukia juu juu tu yaani siku ile ya kura, bali ilianzia mbali, tangu wakati wa Yohana mbatizaji..Vivyo hivyo na sisi, tumtii Kristo sasa, tuyatii maagizo yake yote anayotuelekeza hata kama hatutaona tofauti yoyote nje leo hii, lakini mwisho wa siku ataonyesha tofauti yetu tusipozimia mioyo.. Tukiokoka tusiishi kama watu ambao Mungu hawatambui, tujue kuwa siku moja ya wokovu wetu inathamani kubwa sana mbele za Mungu.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.

JINSI BWANA ALIVYOWACHAGUA MITUME WAKE.

TIMAZI NI NINI

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

YONA: Mlango wa 4

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

Shalom. Karibu tujifunze Biblia, ambalo ndio Neno la Mungu, Mwanga wa njia yetu na Taa iongozayo miguu yetu.

Biblia inasema…Mungu anawaangazia jua lake waovu na wema…(Mathayo 5:45), na anawanyeshea mvua yake wenye haki na wasio haki..Maana yake ni kwamba…Riziki Mungu anawapa watu wote…Hata mchawi akienda kupanda mbegu zake shambani kwake…Mungu atazinyeshea mvua na zitaota.

Sasa msingi wa Neno hili la “Yeye anawaangazia jua lake waovu na wema na kuwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki” ndio utakaotupa picha kamili kuelewa kwamba baraka yoyote, au upendeleo wowote tunaopokea kutoka kwa Mungu sio uthibitisho namba moja wa kuonyesha kwamba tupo sawa na Mungu au hatupo sawa na Mungu…Kwasababu kumbe baraka hizo hizo zinaweza kuwapata wote waovu na wema kwa pamoja…Ndio maana unaona leo hii hata waovu wanafanikiwa sana.

Sasa sio kwamba tuwe waovu ndio tuwe tumepata tiketi ya kubarikiwa…Hapana!..Biblia inasema..katika Zaburi 92:7 “Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele”. Kwahiyo tusitafute kuwa waovu ili tufanikiwe.

Kadhalika Miaka ya watenda mabaya itafupishwa. Mtu mwovu atalifurahia jua kwa kitambo, ataifurahia neema kwa kitambo, ataufurahia wema wa Mungu kwa kitambo…lakini kifo kitamjia kwa ghafla.

Hivyo usifurahie kupata mafanikio fulani au baraka fulani, au kupata fursa fulani mbele yako baada ya kumwomba Mungu, na huku ndani ya moyo wako umemwacha Mungu ukayatafsiri mafanikio yale kama ni uthibitisho wa Mungu kupendezwa na wewe….kamwe usifanye hivyo!..kumbuka neno hili kuwa “Mungu anawanyeshea mvua waovu na wema”. Kwahiyo hata ukiwa mwovu hiyo haimzuii Mungu kukupa chakula.

Kadhalika usitafsiri majibu Mungu aliyokupa ya uponyaji..kwamba ulikuwa na ugonjwa fulani au tatizo fulani na ukamwomba Mungu naye akakuponya na wakati huo huo bado ni mlevi, mwasherati, kwamba uponyaji ulioupokea ni kwasababu Mungu amependezwa na wewe

Katika biblia kuna Mfalme mmoja ambaye alirasimisha ibada za sanamu katika Taifa la Israeli, mfalme huyo alikuwa anaitwa Yeroboamu…alitengeneza sanamu mbili za ndama akaziweka moja kaskazini mwa Israeli nyingine kusini, akawaambia Israeli wote kwamba sanamu hizo ndiyo miungu iliyowatoa wao Misri, hivyo wasiende Yerusalemu kuabudu bali wapande kwenda kuzisujudia sanamu hizo. Hivyo akawageuza mamilioni ya Wana wa Israeli mioyo na kuwafanya kuwa nusu-wachawi kwa muda mrefu kwa jinsi walivyokwenda kuziabudu sanamu hizo za ndama huko alikoziweka…

Na siku ya kuzivumbua sanamu hizo..alitengeneza madhababu juu yake na kutoa kafara…wakati anatoa kafara…akatokea nabii mmoja aliyetumwa na Mungu akatabiri mbele ya ile madhabahu kwamba siku inakuja ambayo itabomolewa na makuhani watakaohudumu katika hiyo madhabahu watachinjwa juu yake..Na huyu Mfalme alipomwona yule Nabii akanyosha mkono wake kutoa amri ya kukamatwa..Wakati anamnyooshea tu mkono wake…Ule mkono biblia unasema ukakatika …

Sasa maana yakukatika sio kwamba ulinyofoka na kuanguka chini hapana…bali maana yake ulikufa ule mkono…na ukakauka ukawa kama mkono wa maiti iliyokauka…ulikauka ukawa kama kijiti kikavu…ukawa hauna hisia hata kidogo..kama mkono uliopata kiharusi…Mfalme kuona vile akamwomba yule Nabii amwombee rehema kwa Mungu wake ili mkono wake urudi…na alipoombewa akapokea uponyaji wake siku hiyo hiyo na akaendelea na shughuli zake za kichawi…wala hakugeuka kubadilika..Na ndio Mfalme aliyefanya maovu kuliko wafalme wote waliowahi kutokea Israeli…yeye pamoja na mfalme Ahabu mumewe Yezebeli. Kasome 1Wafalme 12 na 13.

Sasa unaweza kuona huyu Mfalme alikuwa ni nusu-mchawi lakini katika uovu wake alimwomba Mungu amponye na Mungu akasikia na kumponya…na baada ya kuponywa aliendelea na Maisha yake ya ouvu…kwasababu alitaka tu apate uponyaji ili aweze kuendelea na maisha yake ya dhambi kama kawaida…… Sasa uponyaji alioupokea haukuwa uthibitisho wa kuwa Mungu amependezwa na yeye…Ni rehema za Mungu tu kwasababu yeye anawanyeshea mvua wenye haki na wasio haki…Lakini haimaanishi kuwa anapendezwa na wasio haki…Ndio maana huyu Mfalme Bwana alikuja kumwambia atakufa.

1Wafalme 14:10 “tazama, kwa hiyo mimi nitaleta mabaya juu ya nyumba yake Yeroboamu, nami nitamkatia Yeroboamu kila mwanamume, aliyefungwa na aliyeachwa katika Israeli, nami kuondoa nitawaondoa waliobaki wa nyumba yake Yeroboamu, kama mtu aondoavyo mavi, hata itakapokwisha pia”

Hiyo ndiyo imekuwa kawaida ya Mungu wetu…yeye huwanyeshea mvua waovu na wema…huwapa uponyaji makahaba na wasio makahaba endapo watamlilia, huwapa mali waovu na wasio waovu, huwanyanyua wenye haki na wasio haki..Hivyo kamwe usitumie kipimo cha wema wa Mungu juu yako kutafsiri uwepo wa Mungu katika Maisha yako…Hivyo ni vitu viwili tofauti.

Watakuwepo watu waliobarikiwa na mali kuzimu, watakuwepo watu walioponywa magonjwa yao na kuwa wazima kuzimu, watakuwepo watu kuzimu ambao waliofanyiwa mambo mengi mazuri na Mungu wakiwa duniani tena wakiwa ni waovu. Na wenye shuhuda nyingi tu, jinsi Mungu alivyowapigania katika mambo yao. N.k.

Uwepo wa Mungu juu ya Maisha yako unapimwa kwa maisha ya utakatifu unayoishi…Usifurahi umeponywa na huku bado unaendelea kuvaa vimini, Usifurahie unapata riziki kimiujiza na huku unakula rushwa, ukafikiri Bwana anapendezwa na wewe, usifurahie umetoka tu kuzini na mtu ambaye si mume wako, halafu kesho ukapata promosheni ya kupandishwa cheo kazini..ukadhani baraka hizo ni uthibitisho wa Mungu kupendezwa na wewe.

usifurahie uliombewa ukapona kansa na huku bado umemwacha mke wako au mume wako na unadhani Mungu yupo na wewe!..Usifurahie ulifunga siku kadhaa ukamwomba Mungu akupe nyumba na kweli akakupa na huku bado Maisha yako hutaki kujitakasa ukahitimisha kwa muujiza ule Mungu anapendezwa sana na wewe ndio maana akakuponya, au akakupa hiki au kile…kumbuka yeye anawanyeshea mvua waovu na wema…hivyo sio jambo kubwa sana yeye kukupa uponyaji wake angali ukiwa bado na ukahaba wako…Lakini usipotubu…Neno lake lipo pale pale..waasherati na wafiraji, na wezi, na waabudu sanamu, na wachawi, sehemu yao ni katika lile ziwa la Moto.

1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? MSIDANGANYIKE; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Bwana akubariki sana…ikiwa hujamkabidhi Yesu Kristo Maisha yako..fanya hivyo leo angali tunao bado huu muda mchache…

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

Biblia ni nini?

SAYUNI ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post